Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Septemba 22


Sakata la viwanja Kibaha, Waziri Mkuu atoa onyo kali

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bw. Evarist Ndikilo atoe wiki mbili kwa wakuu wa taasisi za umma na za binafsi wajieleze ni lini wataendeleza viwanja vya ofisi walivyopewa mjini Kibaha.

Ametoa agizo hilo jana Septemba 21, 2016 wakati akizindua Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania (2015 – 2020) na Mradi wa Maboresho ya Mahakama ya Tanzania, Kibaha, mkoani Pwani.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Mkuu wa Mkoa huo kwamba kuna taasisi za umma na za binafsi ambazo zimepewa viwanja vya kujenga Ofisi kwa zaidi ya miaka mitatu lakini zimeshindwa kuviendeleza hadi sasa wakati kuna watu bado wana shida ya kupatiwa viwanja.

“Kibaha ni kimbilio la mkoa wa Dar es Salaam, kule kumejaa na hapa kuna nafasi kwa hiyo hawa ambao hawajaendeleza waandikie barua leo hii hii na uwape wiki mbili waeleze ni lini watakuwa tayari kuanza kazi hiyo.”– Majaliwa

Taasisi hizo zilizotanjwa na Waziri Mkuu ni Hazina ndogo yenye viwanja viwili ambapo kiwanja kimoja chenye namba 232 kimeendelezwa lakini kiwanja kingine chenye namba 221 bado hakijaendelezwa.

 Taasisi nyingine na viwanja vyao kwenye mabano ni Chuo Kikuu Huria (kitalu na. 228), Njuweni Institute (kitalu na. 229), TANESCO (kitalu na. 218), TRA (kitalu na. 233) na SF Group (kitalu na. 225). Vingine ni vya Benki ya CRDB na TAKUKURU ambavyo hakutaja namba za vitalu vyake.

Majaliwa alisema kuwa anajua kuna watu wa Serikali watasema hawana bajeti, lakini Bunge la bajeti linaanza Aprili mwakani. Kwa hiyo, wajipange kwenye bajeti ijayo, ili ifikapo Julai mosi, 2018 hawajafanya kitu, wachukuliwe hatua.

“Tuchukue viwanja vyetu tuwape wengine, na hawa wanaosuasua, tuwaache ili watakapokuwa tayari waombe upya na tutawapa wakati mwingine,” Majaliwa.

Waziri Mkuu pia alimtaka Ndikilo awawekee deadline ya kujieleza katika barua hizo.

Kauli ya Rais Magufuli kufuatia vifo vya watu 13 vilivyosababishwa na ajali ya basi la Super Shem

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. John Mongella kufuatia vifo vya watu 13 vilivyosababishwa na ajali ya barabarani iliyotokana na basi la abiria la Kampuni ya Super Shem kuligonga basi dogo la abiria (Daladala) katika kijiji cha Mwamaya kilichopo katika Kata ya Hungumalwa, Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza.

Ajali hiyo imetokea  tarehe 21 Septemba, 2016 Majira ya saa 12:15 Asubuhi baada ya basi hilo dogo lililokuwa likitoka Kijiji cha Shirima kwenda Nyegezi Mjini Mwanza kuingia ghafla barabara kuu na kisha kugongwa na basi la Kampuni ya Super Shem lililokuwa likitoka Mkoani Mbeya kwenda Mwanza.

Katika ajali hiyo watu wote 13 waliopoteza maisha na majeruhi 15 waliolazwa hospitali walikuwa abiria wa basi dogo lililogongwa.

Rais Magufuli ameelezea kupokea taarifa za ajali hiyo kwa mshituko mkubwa hasa ikizingatiwa kuwa imetokea ikiwa ni siku moja tu tangu Watanzania wengine 12 wapoteze maisha katika ajali ya basi la Kampuni ya New Force iliyotokea katika kijiji cha Lilombwi, Kata ya Kifanya, Tarafa ya Igominyi Mkoani Njombe.

“Nimesikitishwa sana na vifo vingine vya watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali huko Mwanza, nakuomba Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. John Mongella unifikishie salamu za pole kwa familia zote zilizopoteza ndugu, jamaa na marafiki katika ajali hii.

“Nawaombea wote waliotangulia mbele za haki wapumzishwe mahali pema na pia wote walioguswa na msiba wawe na moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi kigumu cha majonzi ya kuondokewa na jamaa zao” Amesisitiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia amewaombea majeruhi wote wa ajali hii wapone haraka  ili waungane na familia zao na kuendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
21 Septemba, 2016

Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kupima Madereva Walevi

$
0
0
Wakala ya Mkemia Mkuu wa Serikali imekusudia kuendesha kampeni maalum ya kupima matumizi ya vilevi kwa madereva wanaosafirisha abiria na mizigo ikiwa ni hatua ya kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani nchini.

Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mkemia Mkuu wa Serikali Profesa  Samwel Manyele alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili kwa wadau wa kemikali juu ya matumizi salama ya kemikali nchini.

Profesa Manyele alisema utaratibu wa kuwapima madereva hao utaanza hivi karibuni na utawezesha kupunguza tatizo la ajali barabarani na kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kutoa ushirikiano katika zoezi hilo.

“Madereva wote wanaosafirisha mizigo na abiria watatakiwa kupita kwenye kipimo ambacho kitaonyesha kama madereva hao wanatumia vilevi, hali hiyo itasaidia kutatua tatizo la ajali za barabarani nchini”, alisema Manyele.

Profesa  Manyele alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kutoa uwezo na uelewa kwa wahusika  hasa wasimamizi wa shughuli za kemikali na matumizi salama juu ya kukabiliana na matukio au ajali za kemikali pale yanapotokea.

Vilio Vyatawala JNIA Baada ya Madereva 10 Waliokuwa Wametekwa DRC Kuwasili Nchini

$
0
0

Vilio vya furaha kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki, vimetawala katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam jana, baada ya kuwasili kwa madereva 10 wa Tanzania waliotekwa na kunusurika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Madereva hao waliwasili katika uwanja huo saa 9 alasiri, wakitoka Kigali, Rwanda kwa ndege ya Shirika la Ndege la Rwanda na kukutana na familia zao kwa mara ya kwanza baada ya kuokolewa.

Wakiwa uwanja wa ndege, walizungumza na waandishi wa habari na kueleza namna walivyotekwa na waasi waliovalia sare za jeshi zisizofanana na walivyosafirishwa zaidi ya kilometa 50 porini usiku na mchana, wakitembea kwa magoti na kupoteza tumaini la kupona huku baadhi wakifanikiwa kutoroka na wengine kuokolewa.

Kabla ya kuwasili kwa madereva hao, ndugu hao walikusanyika uwanjani hapo wakiwa na shauku ya kukutana na madereva hao ambao Septemba 14, mwaka huu, walikumbwa na kadhia ya kutekwa na kundi la wanamgambo huku magari waliyokuwa nayo yakichomwa moto na hatma yao kutojulikana.

Hata hivyo, kutokana na juhudi za Serikali ya DRC na Tanzania, madereva hao walifanikiwa kuokolewa na kupatiwa matibabu ambapo jana walirejea nchini rasmi.

Baada ya madereva hao kumaliza kuzungumza na waandishi wa habari, walitoka nje kwenda kuonana na ndugu zao waliokuwa wamekusanywa pembeni, lakini walipowaona tu walishindwa kujizuia na kuwakimbilia madereva hao ambao nao waliwakimbilia huku wakilia na kutamka maneno ya kumshukuru Mungu kwa kuonana tena.

Baadhi ya familia ziliambatana na watoto wa madereva hao, ambao katika hali ya kutia simanzi baada ya kuwaona wazazi wao, waliangua kilio kwa sauti huku wakiwaita baba zao na kuwakumbatia kwa furaha.

Madereva waliookolewa kutoka Tanzania na waliowasili jana ni Kumbuka Selemani, Hussein Mohammed, Bakari Nassoro, Issa Omary, Amdani Zarafi, Adam James, Mbwana Said, Ali Juma, Athuman Fadhil na Amis Mshana.

Familia za madereva zazungumza 
Mke wa dereva Ali Juma, Jamila Ali, alisema anamshukuru Mungu kwa kuonana tena na mumewe, jambo ambalo hakulitarajia kwani baada ya kupewa taarifa za kutekwa kwake, walikata tamaa ya kumuona tena. Pia alizishukuru Serikali zote mbili kwa juhudi za haraka, walizochukua baada ya kupata taarifa ya kutekwa kwa mumewe na wenzake.

“Mimi nilipata taarifa kutoka kwa mwanangu mkubwa aliyenisihi nimpigie simu baba yake, lakini baada ya kupiga simu ilikuwa ikipokewa na kuwekwa pembeni bila mtu kuongea, lakini nilisikia watu wakiongea kwa lugha ya kifaransa mpaka nikamaliza vocha yangu ya Sh 10,000,” alisema.

Alisema wakati akipiga simu hiyo, alikuwa hafahamu chochote kuhusu kutekwa kwa mumewe, ila baadaye alisikia kwenye taarifa ya habari, ndipo alipotambua kuwa na mumewe yupo miongoni mwa madereva waliotekwa kutokana na kampuni iliyotajwa ambao ni Simba Logistics.

Mariam Ayoub ambaye ni mke wa Mbwana Said, alisema anamshukuru Mungu baada ya mumewe kurejea salama na kwamba siku ya jana ni ya furaha kwake na familia yake. 

Alisema tangu apate taarifa za kutekwa kwa mumewe kupitia taarifa ya habari hakuweza kula, wala kulala usingizi huku akiwa na mtoto mdogo wa mwaka mmoja na nusu.

 “Leo nina furaha kubwa wala siwezi kuelezea zaidi,” alisema huku akilia.

Naye dada wa Bakari Nassoro, Halima Juma ambaye alikuwa akielezea furaha ya kuonana na ndugu huku akilia, alisema familia yake ilishakata tamaa ya kumuona tena ndugu yao huyo kutokana na simulizi za kutisha, walizokuwa wakihadithiwa kuhusu waasi wa DRC. 

Baada ya kuonana na familia zao, madereva hao walipiga picha ya kumbukumbu na kisha kuondoka uwanjani hapo kila dereva na familia yake.

Madereva wasimulia
Awali wakati akisimulia kama sinema juu ya kilichowapata wakati wakitekwa, Kumbuka Selemani, alisema siku hiyo ya Septemba 14, mwaka huu katika eneo la Namoya Jimbo la Kivu Kusini mwa nchi ya DRC, madereva hao walitoka kushusha mzigo wa saruji kilometa 12 kutoka eneo walilotekewa.

Alisema mara baada ya kushusha mzigo huo wakati wakirejea, walikuwa wakiongozana na magari mengine ya kampuni hiyo ya Simba Logistics yeye akiwa dereva wa gari namba nane.

Alisema wakati akikaribia eneo la Kivu, ghafla alisimamishwa na mtu aliyekuwa amebeba silaha nzito huku amevaa mavazi ya jeshi yasiyoeleweka, kwa maana ya kuchanganywa na kumtaka ashuke kwenye gari hilo na amkabidhi kila kitu, ikiwemo hati yake ya kusafiria na kadi ya gari.

“Wakati nimeshashuka niko chini namkabidhi vitu vyangu, mara lilitokea gari la tisa ambalo baada ya kumuona yule mwanajeshi, lilisimama na kuanza kugeuza kwa maana ya kukimbia. Ndipo yule askari akaachana na mimi akaanza kulirushia risasi lile gari lililokuwa linaendelea kugeuza,” alisimulia.

Alisema risasi zile kwa bahati zilipiga kwenye kioo cha pembeni cha lori lingine la 10 lililokuwa linalokuja ambalo nalo baada ya kuona hali ile liligeuza.“Mimi nilipoona ameelekeza mawazo yake kwenye yale magari nikapata upenyo na kukimbilia porini.”

Alisema aliingia msituni na kuanza kutembea umbali mrefu akitafuta kujiokoa hadi alipoona kikosi kingine cha polisi ambacho alilazimika kukichunguza kwanza ili kujua kama ni wale watekaji au askari halali wa nchi hiyo.

Alisema alibaini kuwa ni askari halali kutokana na mavazi yao kuwa ya kawaida ya kipolisi bila kuchanganywa ndipo alipojitokeza na kujisalimisha kwa kunyoosha mikono juu. Askari wale walimchukua na kumhoji na kisha kumpatia huduma za kawaida ikiwemo chakula.

“Wakati najiandaa kupanda pikipiki kwenda kula nikashangaa namuona na mwenzangu (Mshana) ambaye naye alitoroka nikaunganishwa naye,” alisema.

Kwa upande wake Mshana, alisema naye alisimamishwa na kuamriwa ashuke kwenye gari na kukabidhi kila kitu ikiwemo hati yake ya kusafiria na simu. Aliunganishwa na wenzake aliowakuta tayari wametekwa na kuongozwa kuelekea porini huku wakiwa wamefungwa mikono.

Alisema katika msafara huo, mmoja wa askari alitangulia mbele na wengine walifuatia nyuma na kuongozwa kwenye pori zito ambalo wakati mwingine walilazimika kutembea kwa magoti kwani haikuwezekana kutembea huku umesimama.

“Tulipotembea kama kilometa 13 ikabidi nimwambie mwenzangu (Athuman Fadhil) kwamba tutafute njia ya kujiokoa. Hata hivyo alinijibu kwamba kuwa yeye hawezi kwa kuwa amevaa nguo inayomtambulisha zaidi endapo akitoroka itajulikana na wenzetu watapata shida,” alisema.

Alisema walitembea mbele kidogo ndipo alipobaini umbali kidogo kati yake na askari ambapo pembeni yake kulikuwa na kinjia cha kujipenyeza ndipo alipoamua kutambaa kwa magoti na kujipenyeza kwenye kinjia hicho na kufanikiwa kujificha bila kuonekana.

Alisema mara baada ya wenzake kupita alianza safari kwenye pori hilo bila kujua anakokwenda mpaka alipofanikiwa kukutana na kikosi cha Polisi ambacho kilimchukua na kumpeleka sehemu salama.

Athuman Fadhili ambaye alitekwa hadi kuokolewa na majeshi ya DRC, alisema baada ya mwenzake kutoroka alipata matumaini kuwa atasaidia kuwaletea msaada hivyo waliendelea na safari kama kilometa 30 zaidi kwenye msitu huo mnene.

Alisema katika safari hiyo ya mateso ya siku mbili walitembea usiku na mchana huku wakichanwachanwa na miba, walifika kwenye eneo la kijiji ambacho hata hivyo kilikuwa na nyumba chache, wakaamriwa watembee kwa kutambaa ili wasionekane na wanakijiji hao.

Baada ya kilometa tano kutoka kwenye hicho kijiji walifika kwenye makazi ya muda ya watekaji hao na kukutana na mkubwa wao aliyejitambulisha kama Shehe Hassan aliyeamuru wapewe maji na kuanza kuwahoji majina yao kupitia hati zao za kusafiria na kutaka kujua kuhusu familia zao.

Walibeba mizigo ya waasi 
Alisema wakiwa katika eneo hilo, mmoja wa viongozi wa watekaji hao aliyekuwa akizungumza kwa simu na bosi wao mwingine alitoa taarifa kuwa majeshi ya DRC yanawafuatilia hivyo wanatakiwa kujihadhari.

Baada ya mahojiano hayo walipewa chakula na maji na kisha giza lilipoingia walitafutiwa eneo la kulala ambalo ni hema lililowekewa turubai. Alisema majira ya saa sita au saa saba usiku huku mvua kubwa ikiwa inanyesha, waliamshwa na kutakiwa kuendelea na safari kwa kuwa hali ya usalama katika eneo hilo ni tata kutokana na majeshi ya DRC kuzidi kuwakaribia.

“Tulikuwa tumechoka sana kutokana na kubeba mizigo yetu na yao safari nzima lakini tulilazimika kutembea tu. Ilifikia mahali tulitamani kupigwa hata risasi ili tupumzike na kuondokana na mateso tuliyokuwa tunayapata,” alisema Fadhili.

Walitaka dola 4,000 kutoka kwa Dewji 
Alisema wakati wakiendelea kutembea, viongozi wa watekaji hao waliendelea kuwasiliana njia nzima na bosi wa Simba Logistics, Azim Dewji na kumpa saa 24 awe ametoa dola za Marekani 4,000 kwa kila dereva ili waachiwe huru.

“Lakini baadaye wao wenyewe wakaanza kubishana juu ya namna ya kuzipata fedha hizo kutokana na hali halisi ya msitu huo. Wakaambizana fedha hizo zipelekwe kupitia helikopta ya kampuni walikoshushia mzigo wa saruji na madereva hao wapepee bendera kuonesha wako salama na fedha hizo zidondoshwe,” alifafanua.

Alisema walitembea tena umbali kidogo ndipo waliposimama na kupewa chakula aina ya ugali wa mhogo uliokuwa umejaa michanga pamoja na mboga za majani wasiyoyajua na kulazimika kula tu kwa kuwa walikuwa na njaa.

Fadhil alisema waliendelea kubaki katika eneo hilo kwa muda, ndipo watekaji hao walipomtuma kijana wao akanunua unga mjini, baada ya muda alirejea akiwa anatweta na kuwataarifu kwa taharuki kuwa majeshi ya DRC yamekaribia eneo hilo.

Madereva wagawanywa kwa waasi
Kutokana na taharuki ya viongozi hao, kila mtekaji alipewa madereva wawili mpaka watatu awaongoze na kuanza kukimbia huku watekaji hao wakiwa wametangulia mbele.

“Walionesha kuchanganyikiwa kwa kweli wakaanza kutufokea huku wametushikia mitutu ya bunduki na kila kundi likaenda upande wake. Kwa kuwa wao ndio waliotangulia, tukaanza kutoroka mmoja mmoja mpaka kwenye kundi letu tukabaki wawili mimi na Issa,” alisema.

Alisema baada ya kubakia wawili wakaamua pia na wao watoroke kwani hali ilikuwa tete hivyo wakajitosa msituni na kuanza kukimbia hadi waliposikia sauti za maaskari wa DRC zikiwaita.

“Tulisikia wakituita kwa lafudhi yao ya kikongo, watanzania kuya (kuja) watanzania kuya (kuja) jitokezeni sisi ni jeshi la DRC tumewaokoa. Sikuamini masikio yangu tulijitokeza na kupewa msaada haraka,” alisema.

Dewji, Serikali ya Tanzania na Congo wazungumza 
Kwa upande wake, Dewji alilishukuru jeshi la DRC na Serikali ya Tanzania kwa kuwa naye bega kwa bega katika harakati za kuwaokoa madereva hao na kubainisha kuwa katika tukio hilo, magari ya kampuni yake ya Simba manne yalichomwa moto na hivyo kupata hasara ya Sh milioni 600.

Alisema alikuwa akiwasiliana na waasi hao kila mara wakimtaka atoe fedha hizo ambazo alikuwa tayari kuzitoa lakini alionywa na jeshi la DRC kuwa endapo atazitoa atawajengea tabia ya utekaji zaidi wanajeshi hao.

Aidha, Dewji alisema Serikali ya DRC imemuahidi kuwa itaendelea kuweka usalama kwa wafanyabiashara wa malori nchini humo na kumhakikishia ulinzi wa doria kila kampuni hiyo itakaposafirisha mizigo yake nchini.

 “Hiki kilichotokea ni bahati mbaya, tutaendelea na biashara lakini kwa tahadhari. Biashara yangu inagusa watu wengi si kampuni yangu pekee endapo nitasitisha wengi wataathirika,” alisisitiza.

Balozi wa DRC nchini, Jean Piorre Mutamba, alisema tukio hilo limemshtua na kumpa wakati mgumu, hasa ikizingatiwa kuwa ni balozi mpya aliyewasili nchini hivi karibuni, hivyo alitumia fikra zake zote ili kuhakikisha madereva hao wanaokolewa. 

Aliwataka madereva hao kuhakikisha wanawasiliana na ubalozi wa DRC kabla ya kuanza safari ili kuwawekea mazingira ya usalama zaidi na kuwafuatilia.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Susan Kolimba, aliwahakikishia madereva hao kwamba tukio hilo ni la bahati mbaya na kwamba Serikali ya Tanzania itaendelea kuwalinda wananchi wake wanaofanya kazi nje ya nchi.

“DRC ni nchi rafiki na tumekuwa tukifanya nao kazi nyingi. Nina imani tukio hili haliwezi kuvunja uhusiano wetu kwani serikali zote mbili zimefanya jitihada kubwa za kuwaokoa madereva hao,” alisisitiza.

Gavana wa Benki Kuu (BoT) Benno Ndulu, na Msajili wa Hazina Kizimbani Leo

$
0
0

Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemtaka Gavana wa Benki Kuu (BoT) Benno Ndulu, na Mwendeshaji wa benki ya FBME, Lawrence Mafuru, wafike mahakamani kujieleza jinsi watakavyotekeleza amri iliyoitaka BoT kulipa Sh bilioni 92.

Maofisa hao wanatakiwa kuieleza mahakama watakavyoilipa kampuni ya Coast Textiles Ltd fedha hizo na kama watashindwa kufanya hivyo, watafungwa jela kama wafungwa wa kesi ya madai.

Utekelezaji wa amri hiyo unatokana na uamuzi wa shauri namba 129 la mwaka 2009, ulioiamuru benki ya FBME kuilipa kampuni ya Coast Textiles Ltd fedha hizo baada ya kukamata kiwanda chake na kukiuza kwa kampuni ya Five Star Investment ltd.

Uuzwaji wa kiwanda hicho ulitokana na mgogoro wa ulipaji mkopo ambao kampuni ya Coast iliuchukua katika benki hiyo.

BoT inahusishwa kwenye shauri hilo kutokana na kuchukua uendeshaji wa benki ya FBME baada ya benki hiyo kuhusishwa na utakatishaji fedha nchini Cyprus.

Maofisa hao walitakiwa kufika mahakamani hapo Septemba 16 mwaka huu kwa ajili ya kueleza jinsi watakavyotekeleza amri hiyo, lakini hawakufika kwa kuwa wamewasilisha maombi ya kusimamisha shauri hilo ambayo yamepangwa kusikilizwa leo mbele ya Jaji Ama Munisi.

Katika kesi ya msingi iliyofunguliwa na kampuni ya Coast, mahakama iliamuru FBME iilipe kampuni hiyo Sh bilioni 21.2 na riba ya asilimia 21 kwa mwaka tangu Juni 28, 2001 hadi hukumu ilipotolewa, Julai 27, 2015.

Baada ya uamuzi huo, walalamikaji walipeleka maombi ya utekelezwaji wa hukumu hiyo, ambayo ukijumlisha na riba ni sawa na Sh bilioni 92.2.

Kutokana na maombi hayo, mahakama ilimuelekeza Gavana wa BoT kukamata akaunti mbili zinazomilikiwa na benki ya FBME, hata hivyo BoT iliwasilisha maombi ya kuchunguzwa kwa umiliki halali wa akaunti zinazoshikiliwa na kuiomba mahakama isitishe amri hiyo kwa kuwa BoT siyo miongoni mwa walalamikiwa kwenye shauri la msingi.

BoT iliingilia kati suala hilo, kwa kuwa kwa sasa ndiyo inayosimamia uendeshwaji wa benki ya FBME kwa ajili ya kulinda amana za wateja baada ya benki hiyo kuhusishwa na utakatishaji fedha.

Baada ya kusikiliza maombi hayo, mahakama iliondoa amri hiyo na kuamuru benki hiyo ilipe fedha, hata hivyo walalamikaji waliwasilisha maombi mengine ya kukazia hukumu katika Mahakama Kuu.

Katika maombi hayo Msajili wa Mahakama Kuu, Projest Kahyoza alitoa siku saba kwa maofisa hao kufika mahakamani kujieleza jinsi watakavyolipa fedha hizo na wakishindwa watafungwa jela kama wafungwa wa madai.

Tundu Lissu Aponea Chupuchupu Dhamana Yake Kufutwa

$
0
0
Hofu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kumfutia dhamana Tundu Lissu ambaye ni mtuhumiwa wa kesi ya uchochezi, imetoweka baada ya mahakama hiyo kukubaliana na utetezi wa  wadhamini wake kuwa, Lissu yupo Ujerumani kwa matibabu.

Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki, alishindwa kuhudhuria mahakamani siku ya juzi na hivyo wadhamini wake kutakiwa kufika mahakamani jana kujieleza, kwanini mtuhumiwa huyo asifutiwe dhamana. 

Kesi ya uchochezi inayomkabili Lissu ni kesi Na. 208 katika gazeti la MAWIO akiwa ni mtuhumiwa namba nne sambamba na Jabir Idrissa, Simon Mkina, na Ismail Merhaboob.

Jabir ni mwandishi mwandamizi wa MAWIO, Mkina ni mhariri wa gazeti hilo na Merhaboob ni meneja wa kampuni ya uchapishaji magazeti inayojulikana kwa jina la Flint.
Jana, wadhamini wa Lissu Ibrahim Ahmed na Robert Katula walisimama mbele ya Hakimu Thomas Simba anayesimamia kesi hiyo, na kusema kuwa Lissu hakutokea  mahakamani kwa sababu amesafiri nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, upande wa mashitaka ukiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Mutalemwa Kisheruji uliiomba mahakama kuzuia hati ya kusafiria ya mshitakiwa Lissu pamoja na kumuwekea sharti la kuiomba mahakama kibali cha kusafiria endapo atarudia tena kosa hilo kutokana kwamba hakufuata sheria kwa sababu alitakiwa kutoa taarifa mapema kabla ya siku ya shtaka kusikilizwa.

Lakini Hoja hiyo ilipingwa na Wakili wa upande wa utetezi Peter Kibatala na kuiomba mahakama kutenga siku nyingine ambapo alimuahidi hakimu kuwa kosa hilo halitajirudia tena na siku husika ya kusikilizwa shitaka mshatikiwa atakuja mahakamani.

Baada ya kusikiliza maombi ya pande zote mbili, Hakimu Simba alitoa onyo kali kwa mshitakiwa na kuwaambia wadhamini wa Lissu kuwa, endapo siku nyingi mshitakiwa huyo hatakuja mahakamani, wadhamini watalipa dhamana.

Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba, 4, 2016 baada ya mawakili wa pande zote mbili kuiridhia tarehe hiyo iwe siku ya kusikilizwa shtaka hilo.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 53 & 54 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0

Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

Ilioishia....
Nikanyanyuka na  kukifunga kibegi changu, nikatizama kwenye kioo cha computer yake, iliyopo juu ya meza yake, kilicho gawanyika katika vipande sita vya picha za video za kamera za ulinzi na kuona gari aina ya rangerover ikisimama kwa kasi  nje ya benki na wakashuka wasichana watano walio valia mavazi meusi huku wakiwa na bunduki mikonini mwao.Wakanza kuwashambulia askari huku walili wakiingia ndani ya benki na kuanza kuwashambulia askari na kuwaamrisha watu wote kulala chini.Nikamuona wakimuamrisha bwana turma kuingia kwenye chumba ambacho ndicho wanahifadhia pesa.

Endelea....
Japo ninaroho kidogo ya kikatili, ila kwa jinsi risasi zinavyo ngurumishwa nje na majambazi hawa, sikuthubutu hata kujaribu kutoka ndani ya chumba.Bastola yangu nikaishika vizuri kwa umakini huku macho yangu yakitazama kwenye kioo cha computer iliyopo juu ya meza.Nikawashuhudia wasichana wawili wakimuamrisha bwana turma kuingia ndani ya chumba ambacho ni chakuhifadhia pesa.Wakaendela kuingiza pesa kwenye mifuko yao, nikamuona msichana mwengine akiingia akiwa na bunduki.Sikusikia kitu anacho kizungumza.Nikaanza kusangaa baada yakuwaona watu wakivuliwa nguo na kupangwa mstari katika mlango wa kutokea nje
“wanataka kufanya nini hawa?”

Nilijiuliza swali ambalo jibu lake nikalipata  baada ya kuona watu wakitolewa nje wakiwa uchi pasipo kuwa na nguo hata moja kwenye miili yao.Wasichana wakajichanganya kwenye kundi kubwa la watu wanaotoka wakiwa, wanakimbia.Nikaitumia nafasi hiyo na mimi kutoka ndani ya chumba huku kibeki changu nikiwa nimekifunga vizuri na kukishika kwenye mkono wangu wa kushoto huku mkono wangu wa kulia nikiwa nimeishika bastola yangu.Nikajichanganya kwenye watu na kukimbilia lilipo gari letu,nikamkuta dorecy akiwa amejiinamia kwenye gari, nikafungua mlango wa gari na kuingia ndani

“eddy vipi huko?”
“tuondoke, sikwema huku”
Nikawasha gari na kuliingiza barabarani kwa kasi ya hali ya juu,
“eddy tunaelekea wapi?”
Dorecy aliniuliza huku akinitazama kwa macho makali, sikulijibu swali lake zaidi ya kuongeza mwendo kasi wa gari langu.Nikafika maeneo ya mataa na kukuta msongamano wa magari mengi yakiwa katika foleni
“shiitii”

Nilizungumza huku nikiitizama gari ndogo ya polisi inayokuja nyuma yangu kwa kasi, wakionekana kunifwatilia mimi.Kutokana nyuma yangu hakuna gari, nikairudisha nyuma gari yangu, na kuingia barabara ya pili inayopitwa na watembea kwa miguu, kazi yangu ikawa ni kupiga honi, huku nikiwa makini katika uendeshaji wangu.Watu wengi wakawa na kazi ya kulikwepa gari langu huku wengine wakijirusha kwenye mitaro kuepuka kifo
“eddy angalia mbelee”

Dorecy alizungumza kwa sauti kubwa, kwani kuku gari la abiria linakuja mbele yetu kwa mwendo wa kasi, kwa haraka sana nikakunja kushoto na kuzibaniza pikipiki za waendesha bodaboda zililozo pangwa barabarani wakisubiria wateja, kwa kupitia kioo cha pembeni, nikalishuhudia gari la abiria lilipoteza muelekeo na kuyakuma magari mengine na kusababisha ajali mbaya.Kwa ukubwa wa gari yangu haikuwa shida sana kuzikanyaga pikipiki mbili zilizopo mbele yangu.

Nikapata kiupenyo cha kuingia barabarani na cakumshukuru mungu, hakuna magari ya foleni ambayo yanaweza kunizuia kuendelea na safari yangu, huku nikiwaacha waendesha pikipiki wakitoa matusi mengi juu yangu
Kwa mbali nikaliona gari, walilokuja nalo majambazi likichanja mbuga barabara ya kuelekea mkoani

“wale ndio majambazi walio piga tukio benki”
Nilizungumza huku nililiinyooshea kidole gari la majambazi aina ya rangerover.
“mmmmm”
Dorecy aliguna, huku akinitazama machoni.Nikazidi kukanyaga mafuta na kuzidi kulisogelea majambazi, ambalo nalo linakwenda kwa mwendo wa kasi sana.

“eddy kuwa makini, wasije wakatushambulia”
“powa”
Sikuona gari yoyote ya polisi inayokuja nyuma yetu, nikazidi kulifukuzia gari la majambazi na gafla likakunja na kuingia porini
“eddy nyoosha tuu, tusiwafate”
“powa”
Nikaachana na gari la majambazi na kuelekea zangu barabara inayokwenda mikoa ya tanga na arusha.Kwa mbali nikawaona askari usalama barabarani wakiwa wamesimama.

“eddy punguza mwendo”
“huoni kama tutakamatwa?”
“nitazungumza nao mimi”
“dorecy”
“fanya hivyo, la sivyo itakuwa ni tatizo kubwa”
“powa”

Nikapunguza mwendo wa gari, na askari mmoja akatusimamisha, nikalisimamisha gari langu pembeni na askari huyo akaanza kuja kwa mwendo wa umakini, huku akilitazama gari langu.Nikaishika bastola yangu kwa umakini, ila dorecy akaushika mkono wangu wa kushoto ulio shika bastola

“tulia”
Dorecy alinizuia kufanya ambacho ninahaji kukifanya, kwa ishara askari akaniomba nifungua kioo cha gari upande nilio kaa mimi, nikatii kama alivyo hitaji mimi kufanya
“habari yako afande”
Jamaa alianza kunisalimia, nikaachia tabasamu pana ambalo muda wowote ninaweza kulibadilisha
“salama tuu, kaka”

“mbona gari yako, mbele kidogo imebonyea?”
“ahaaa kuna, mjinga alinibamiza kwenye mataa kule”
“ahaaa, munaelekea wapi?”
“nakwenda, tanga mara moja kuna kazi hapo tumeagizwa na rpc”
“kuna, gari tunaiwinda ya majambazi wamepiga tulio benki, ndio tupo tupo hapa, tunaisubiria”
“ipoje hiyo gari?”
Polisi akaniwasha simu yake na kunionyesha picha cha gari hilo

“nimetumiwa whatsap hii picha”
Dorecy akaitazama picha ya gari ambalo, tulikuwa tumeongozana nalo
“hii gari tumeongozana nayo”
Dorecy aliropoka na kunifanya nimgeukie na kumtazama kwa macho makali yaliyo jaa mshangao ndani yake
“imengia wapi?”
Dorecy akaanza kumuelekeza askari gari sehemu ilipo ingia, askari akawajulisha wezake na sisi tukaondoka.

“dorecy umefanya nini?”
“kwani tatizo lipo wapi?”
“sio tatizo lipo wapi, wewe inakuwaje unawachomesha watu wa watu katika ishu zao”
“sio ishu zao, kumbuka hata mimi ni askari”
“hata kama”
“sio hata kama, wewe hukuona ni watu wangapi walio uliwa nje ya benki”

“ila sijapenda hiyo tabia sawa”
“eddy, kumbuka hata wewe ni muhalifu”
“so”(sasa)
Nilimjibu dorecy kwa kifupi, huku nikiwa nimekasirika sana
“sihitaji hicho kibesi chako”
“unasemaje wewe?”
“sihitaji hicho kibesi chako cha kijinga, nitakubadilikia sasa hivi, umenielewa?”


Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Askari tisa JWTZ kizimbani kwa mauaji

$
0
0

ASKARI tisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ),   wamefikishwa mahakamani wakituhumiwa kwa mauaji ya mkazi mmoja wa Kata ya Chemchem Manispaa ya Tabora.

Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi,  Samson Kabigi, alisoma mashtaka dhidi ya watuhumiwa hao mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Tabora,  Agatha Chigulu.

Alidai kuwa askari hao wote  wa Kikosi cha 823 Msange, walitenda kosa hilo Septemba 10, mwaka huu.

Inadaiwa kuwa askari hao waliwashambulia wananchi   mjini Tabora  baada ya mkesha wa Fiesta.

Askari hao   ni  MT 109535 Koplo Msafiri Kitwima (26) na MT 92697 Private Thobias Salum (30) wakazi wa  Kata ya Chem Chem, MT 114612 Private Shomary Hemed  (24), MT 114685 Private Yusuph Muluthary (25) na MT 114110 Private Rajab Mbasa (24).

Wengine ni MT 114142 Private Selestine Machemba (24), MT 114125 Private Said Rashid (27), MT 114118 Private Rogasian Shayo (24)  na  MT 114684 Private Yustin Mwingira (24), ambao wote ni wakazi wa Kikosi cha 823 Msange.

Mwendesha Mashtaka Kabigi, alidai washtakiwa wote kwa pamoja Septemba 10, mwaka huu saa 9.00 mchana walimuua Omary Shaban.

Washtakiwa   hawakutakiwa kujibu chochote   kwa vile  shauri lao litasikilizwa na Mahakama Kuu.  Walirudishwa makabusu  hadi Oktoba 5, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 11 & 12

$
0
0

 MWANDISHI:EDDAZARIA G.MSULWA


ILIPOISHIA....
Anna akamuomba Rahab kuipokea simu hiyo
“Haloo”
“Dokta Will hapa nazungumza”
“Dokta vipi, mbona umetupiga na simu ya mezani?”
“Hilo halina tatizo sana, kikubwa nataka kuwaambi kuweni makini kwani kuna wanajeshi wametumwa kuja kuukagua huo msitu munapo ishi”
“Lini?”
“Unauliza lini? Wanakuja sasa hivi na wapo njia na hii taarifa nimepewa na kiongozi wao”

ENDELEA....
“Sawa nimekupata dokta”
“Cha kufanya ni kufunga handaki na nendeni mbali na lilipo”
“Hapa tulipo, ndio tulikuwa tunatoka, tunakwenda kuv......”
Fetty akamziba mdomo Rahab kabla hajaimalizia sentensi yake
“Mnakwenda wapi?”
“Kununua nguo za kuvaa”
“Sawa”
Rahab akakata simu

“Unajua wewe mtoto ni mwehu” Fetty alizungumza huku amemtolea macho Rahab
“Uwehu wangu upo wapi?”
“Unataka kumwambia kuwa tunataka kwenda kuvamia, hujui mazugumzo yote yanasikiwa kwenye mitandao ya simu”
“Ahaa, nilipitiwa”
“Sio kupitiwa, uacha hilo domo lako kubwa”
“Jamani hebu acheni kurumbana, ehee tuambie kuna ishu gani?”

“Anasema kuwa kuna wanajeshi wanakuja kuukagua huu msitu, na wapo njiani”
“Ahaaaa sasa inakuwaje?” Anna alizungumza
“Dokta amesema tufunge handaki na kuondoka, twende mbali na hapa”
“Mpango umeshakufaa huu” Halima alizungumza
“Sasa, mbona Ni shidaaaa” Agnes alizungumza huku akikaa kwenye kiti

“Jamani, tusiakate tamaa, kikubwa ni kuamua lile tunalo lihitaji” Fetty alizungumza
“Sawa, tunaamua je akili na maarifa yetu yanafikiria kile tunnacho taka kukifanya au tunaamua tuu, mwisho wa siku tufaye madudu ambayo yatatucost kwenye maisha yetu” Agnes alizungumza

“Nyinyi mbona waoga sana, kama maji tumeyavulia nguo tunapaswa kuyaoga” Rahab alizungumza
“Wewe acha misemo yako iliyopitwa na wakati, maji ukiyavulia nguo, ukiona yanazingua si unavaa na kuondoka.Kwani ni lazima kuoga” Anna alizungumza.

“Sikieni,dili limesha kufa kwa maana hapa kila mmoja anazungumza lake.Wapo wanao taka kufanya na wanao kataa.Sasa tuwafikirie hawa nguruwe wanao kuja huku”
 Fetty alizungumza huku akiwatazama wezake, hakuna aliye zungumza zaidi ya kufikiria cha kuzungumza.

“Watu wanasema, mwanaume hakimbii nyumba yake, bali anapambana kuhakikisha analinda mali zake na familia yake.Sisi sasa hivi ni sawa sawa na wanaume.Hapa ndio kwetu, hapa ndio tunapo ishi kwa amani.Hakuna aliyekuwa na kwake zaidi ya kutegemea maisha ya kuliwa na wanaume na kumnufaisha mwehu mmoja” Fetty alizungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo na msimamo

“Tunatakiwa kupambana, tunatakiwa kujilinda, Hatupaswi kukimbia makazi yetu.Kikubwa ni kuanyanyuka na kwenda kupambana na hao wanao jaribu kupambana na sisi.Hatuna uchaguzi mwingine.Simama lady’s”

Fetty alizungumza na kuwaamsha wezake walio kaa,wakazunguka duara moja na mikono yao ya kulia wakaikutanisha pamoja, huku wakiwa wamekunja ngumi.

“Tunatoka watano, tunarudi watano”  Agnes alizungumza
“KWA UMOJA TUNAWEZA”
Walizungumza kwa pamoja, kiasha wakaachiana, Kila mmoja akahakikisha silaha take ipo sawa
“Jamani ninapendekeza, tuvae vinasa sauti kwa ajili ya kuwasiliana kwa pamoja” Agnes alizungumza
“Hapo umenena wangu”

Anna alizungumza, akafungua kabati ambalo wameweka vinasa sauti, kila mmoja akachukua cha kwake na kukiweka kwenye masikio.Kila mmoja akahakikisha kinasa sauti chake kinafanya kazi

“Mnanisikia?” Halima alizungumza
“Ndio dada Halima” Rahab alijibu
“Fetty si ulivue hili jimwili” Agens alizungumza
“Nitapambana nalo hivyo hivyo”
“Mmmmm, haya big mama”

Wakacheka kwa pamoja na kutoka ndani ya pango,kila mmoja akaende njia yake huku wakiwa wameuzingira msitu wao.Kila mmoja akakaa kwenye nafasi ambayo angeweza kuona uingiaji wa wanajeshi hao waliotumwa kuja kufanya uchunguzi kwenye msitu.Kila mmoja akawa na hamu ya kutumia silaha yake, ambayo ameijaza risasi za kutosha.Masaa yakazidi kukatika pasipo kuona dalili yoyote ya majambazi kutokea kwenye msitu walio kuwepo.

“Jamani, mbona kimya? Agnes aliwauliza kupitia kinasa sauti chake
“Jua ndio linazama hivi” Rahbu alijibu
“Tuvuteni subira, kwa maana inaweza nao wamepanga kuvamia usiku” Fetty alizungumza
“Ahaa, jamani mimi njaa inaniuma” Anna alizungumza
“Wezako tunazungumza la maana wewe unazungumzia njaa hapa” Rahab alijibu

“Kwani kusema njaa, ndio nimekosea jamani?”
“Hujakosea ila ngoja tukamilishe hii kazi kwanza”
“Jamani kila mmoja awe makini kwenye pozi lake tunaumizana masikio” Halima alizungumza
“Powa bwana” Anna alizungumza
Masaa, yakazidi kukatika, hapakuwa na dalili yoyote ya mwanajeshi kutokea katika msitu wao.Hadi inatimu mida ya saa saa tano usiku hali ikaendela kuwa ya ukimya.

”Nimevumilia nimeshindwa, kama ni kuja waje tuu, Mimi ninakwenda kula jamani”
Anna alizungumza huku akisimama
“Hata mimi jamani” Rahab alizungumza
“Wewe si ulisema, tunazungumza ya maana subiri hao jamaa zako”
“Rahab na Anna tuachieni kelele” Agnes alizungumza
“Powa”

Anna akaanza safari ya kurudi lilipo handaki lao, hakuchukua muda sana akafanikiwa kufika kwenye handaki.Mazingira ya handaki akayakuta kama walivyo yaacha.Akafungua mfuniko wa handaki ambao ni wachuma na kushuka chini, huku bunduki yake ikiwa mkononi.Akawasha taa zote na kujirusha kwenye moja ya sofa huku akiwa amejichokea sana, Simu ya mezani ikamstua na taratibu akanyanyuka na kuifwata sehemu ilipo na akaipokea
“Hallo”
“Dokta Wille nazungumza”
 “Eheee”

Majina ya waliofariki katika ajali iliyohusisha basi la Super Shem na Hiace jijini Mwanza

$
0
0

WATU 13 wamefariki dunia katika ajali iliyohusisha basi la Super Shem lenye namba za usajili T 874 CWE lililokuwa likitokea Mbeya kuelekea Mwanza na Hiace yenye namba T 368 CWQ iliyokuwa ikitoka Jijini Mwanza kuelekea Wilaya ya Kwimba.

Katika ajali hiyo mfanyabaishara ndogo ndogo maarufu machinga, Peter Tobari, aliokoa maisha ya abiria zaidi ya 30 na kumsaidia dereva wa basi la Super Shem ambaye alikuwa amekandamizwa miguu na basi hilo baada ya kugongana na Hiace.

Ajali hiyo imetokea siku mbili baada ya ile ya basi la Kampuni ya New force iliyotokea mkoani Njombe  ikihusisha basi lenye namba T 429 DEU lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Songea mkoani Ruvuma, ambapo watu 12 walifariki dunia na wengine 28 kujeruhiwa vibaya. Katika ajali ya Mwanza, gari dogo aina ya Hiace liligongana uso kwa uso na basi la Super Shem na kusababisha vifo hivyo na wengine 10 kujeruhi.

Ajali hiyo imetokea umbali wa mita 200 kutoka kituo kidogo cha mabasi cha Hungumalwa njia panda ya Shelui na Mwamashimba katika Kijiji cha Mwamaya wilayani Kwimba mkoani Mwanza. Ilielezwa katika tukio hilo, dereva wa Hiace aliingia barabara kuu ya Mwanza-Shinyanga bila kuchukua hadhari na hivyo kukutana na basi hilo.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema baada ya ajali hiyo watu 10 walikufa papo hapo na wengine 11 kujeruhiwa, ambapo mmoja alifariki dunia akiwa njiani akipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba na wawili walifariki dunia wakati wakipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa matibabu zaidi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba, Dk. Bethod Nchemba, akizungumzia ajali hiyo alisema walipokea  majeruhi 10  wakiwemo wanaume na wanawake watano ambapo mmmoja alikuwa na hali mbaya  na alifariki akiwa mapokezi wakati akiendelea kupewa huduma.

Aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Monica Shija, Christina Costantine, Theresia Majenga wote wakiwa wakazi wa Kijiji cha Gulumwa wilayani Kwimba, Lwinzi Kope mkazi wa Kijiji cha Chaselwe, Mabula Magi wa Rukwa, Isaya Deogratius mkazi wa Mbande, Moses Kamel wa Kijiji cha Bupamwadomu, George Ndila mkazi wa Sangu, Kondakta wa hiace aliyefahamika kwa jina moja la Poni pamoja na mtu mmoja mwanaume, mama mmoja na mtoto ambao hawajafahamika wote wakiwa ni abira wa Hiace.

Alisema  majeruhi watatu wanaendelea vizuri na matibabu katika hospitali hiyo na miili tisa kati ya 11 imeshatambuliwa isipokuwa mwili wa mama mmoja na mtoto anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 5 na majeruhi sita wamelazimika kuhamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi.

Polisi waruhusu mikutano ya ndani ya vyama vya siasa

$
0
0

Jeshi la polisi nchini limeondoa marufuku ya mikutano ya ndani kwa vyama vya siasa kwa madai kwamba limeridhishwa na hali ya kiusalama iliyopo nchini.

Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Marijani   Mssanzya ametangaza kuondoa zuio hilo leo na kusema kuwa makatazo mengine ya mikutano ya vyama hivyo yako pale pale.

Mssanzya amesema mikutano ya hadhara na maandamano bado hairuhusiwi lakini wabunge wanaruhusiwa kufanya mikutano yao katika majimbo yao kwa mujibu wa katiba. 

"Maandamano na mikutano ya hadhara imezuiliwa hadi tathmini pana zaidi ya hali ya usalama itakapofanyika," amesema Mssanzya

ACT- Wazalendo Wafuta Kongamano la Kidemokrasia Walilokuwa Wamepanga Kulifanya Kesho Kutwa........Sasa Kufanyika Oktoba 8

$
0
0

1. Katika kikao chake cha tarehe 05 Septemba 2016, pamoja na mambo mengine, Kamati Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo iliazimia kuwa Chama kifanye Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia (National Democratic Congress) tarehe 24 Septemba 2016 jijini Dar es Salaam.

2. Tangu kutangazwa kwa umma kuhusu mipango ya kufanyika kwa mkutano huu, wanachama wetu wengi na wananchi kwa ujumla, wakiwemo baadhi kutoka mikoani wameonesha nia ya kushiriki. Ili kuwapa fursa viongozi, wanachama na wananchi kushiriki kwenye mkutano huu, Chama kimesogeza mbele tarehe ya kufanyika kwake hadi tarehe 08 Octoba 2016.

3. Wanachama na wananchi ambao wangependa kushiriki kwenye mkutano huu watume majina yao na majimbo wanayotoka kwa namba 0653619906/0717047574. Ili kutoa muda wa kutengeneza vitambulisho vya washiriki, siku ya mwisho ya kupokea majina ya washiriki ni tarehe 01 Oktoba 2016.

4. Ikumbukwe kuwa mbali na kujadili masuala mbalimbali ya nchi na bara la Afrika, Mkutano wa Kidemokrasia ndiyo fursa pekee ya kikatiba ambapo mwanachama/mwananchi wa kawaida anayeshiriki anapata fursa ya kuwahoji ana kwa ana viongozi wa kitaifa wa ACT Wazalendo juu ya masuala mbalimbali ya Chama.

Ado Shaibu
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma
Imetolewa leo tarehe 22 Septemba 2016.

Bodi ya Uhuru Media Group inayosimamia vyombo vya habari vya CCM Yajiuzulu

$
0
0

Bodi ya Uhuru Media Group inayosimamia vyombo vya habari vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambavyo ni Uhuru Publications Limited (UPL) wachapishaji wa Gazeti la Uhuru, Mzalendo na Burudani pamoja na Peoples’ Media Communication Limited (PMCL) inayoendesha kituo cha redio Uhuru imejiuzulu kupitia barua ya Mwenyekiti wa Bodi hiyo Al-haj Adam O. Kimbisa.

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli amepokea barua ya kujiuzulu kwa bodi hiyo leo tarehe 22 Septemba 2016 ambayo nakala yake imenakiliwa kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana. Barua hiyo inaeleza kuwa Mwenyekiti pamoja na wajumbe wote wa Bodi hiyo wameamua kwa hiyari yao kujiuzulu nafasi zao.

Bodi ya Uhuru Media Group ndiyo iliyokuwa na majukumu ya kusimamia, kuzielekeza na kuzishauri Menejimenti ya Makampuni hayo na kubuni mbinu na mikakati ya kuongeza ufanisi katika uendeshaji wa vyombo vya habari vya Chama.

Imetolewa na:-

CHRISTOPHER OLE SENDEKA (MNEC)
MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
Tarehe 22/09/2016.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Balozi Wa Urusi Na Jamhuri Ya Korea Hapa Nchini .....Azungumzia Ujenzi wa Daraja la Salender

$
0
0
Ujenzi wa Daraja la Salender litakalounganisha eneo la Coco Beach na eneo Agha Khan kupitia baharini Jijini Dar es Salaam unatarajiwa kuanza Mwezi Juni Mwakani baada ya Serikali ya Tanzania kukamilisha mchakato wa upatikanaji wa fedha za ujenzi kutoka benki ya Exim ya Korea.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema hayo leo tarehe 22 Septemba, 2016 muda mfupi baada ya kufanya Mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini Mhe. Song Geum-Young, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amesema ujenzi wa daraja hilo litakalokuwa na urefu wa kilometa 7 zikiwemo kilometa 1.4 zitakazopita baharini, unatarajiwa kukamilika mwaka 2020 na daraja hilo litasaidia kupunguza adha ya msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam.

"Mchakato wa kulijenga hili daraja la Salender unaendelea vizuri kwa sababu hivi sasa kampuni ya Kikorea ambayo inafanya usanifu ipo kwenye hatua za mwisho na zabuni zinategemewa kutangazwa mwezi wa tatu Mwaka kesho na zitakwenda haraka, kwa hiyo mambo yakienda vizuri ujenzi unaweza kuanza mwezi wa sita, bahati nzuri fedha zote zipo na zimeshatolewa na Benki ya Exim ya Korea" Amesema Rais Magufuli.

Aidha, Dkt. Magufuli amemshukuru Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa juhudi alizozifanya zilizowezesha kujengwa kwa hospitali ya Mloganzila  kwa ufadhili wa Jamhuri ya Korea na kwamba hospitali hiyo itakuwa ya kisasa zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Amesema ujenzi wa Hospitali hiyo unatarajiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu na kwamba tayari Madaktari na Wataalamu takribani 100 waliopata mafunzo nchini Korea na wenye ujuzi wa namna ya kutumia teknolojia inayowekwa kwenye hospitali hiyo wapo hapa nchini.

Rais Magufuli ambaye ameelezea nia ya Serikali ya Tanzania kufungua ofisi za Ubalozi Mjini Seoul nchini Korea ameongeza kuwa Serikali yake imedhamiria kuendeleza na kuimarisha uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya nchi hizi kwa lengo la kuwaletea manufaa wananchi ikiwemo kutumia teknolojia na ujuzi wa nchi ya Korea katika ujenzi wa Meli.

Kwa upande wake, Balozi wa Korea hapa nchini Mhe. Song Geum-Young ametoa salamu za pole kufuatia maafa ya tetemeko la Ardhi yaliyotokea Mkoani Kagera na mikoa jirani, na ameahidi kuwa Korea itatuma timu ya wataalamu kuja kuona namna ya kusaidia.

Balozi Song Geum-Young pia amemhakikishia Rais Magufuli kuwa Korea itaendeleza na kuimarisha uhusiano wake na Tanzania na kwamba itatoa ushirikiano wa kutosha kufanikisha miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa hapa nchini ikiwemo ujenzi wa Daraja la Salender, Meli, Hospitali ya Mloganzila na mingineyo.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Balozi wa Urusi hapa nchini Mhe. Yuri Popov ambapo viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa kihistoria baina ya nchi hizo huku wakitilia mkazo katika kukuza biashara na uwekezaji.

Pamoja na hayo Balozi Yuri Popov amepongeza na kuelezea kufurahishwa na hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli katika kuimarisha uchumi huku akibainisha kuwa kwa hatua hizi anaamini ajenda ya kujenga uchumi wa viwanda itafanikiwa.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amepokea taarifa ya hali ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na katika mazungumzo yake na Mkemia Mkuu wa Serikali Prof. Samwel Manyele, amemtaka kuendelea kuimarisha utendaji kazi wa maabara hiyo ili kuongeza ufanisi wa majukumu yake ambayo ni kufanyia uchunguzi vielelezo vya makosa ya Jinai na usimamizi wa sheria za udhibiti wa kemikali na udhibiti wa vinasaba vya binadamu (DNA).

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

22 Septemba, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kumkaribisha  Balozi wa Urusi hapa nchini Yuri Popov aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkemia Mkuu wa Serikali Profesa Samwel Manyele Ikulu jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU.

List Ya Vyuo Vilivyotoa Selection Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Vyuo Vikuu Mbalimbali 2016/2017

Orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na UDOM mwaka wa masomo 2016/2017

$
0
0
Kupata majina ya wanafunzi walichaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma ngazi ya Stashada, katika mwaka wa masomo 2016/2017, <<Bonyeza hapa>>

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 23

Rais Magufuli ateua viongozi wa juu wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL)

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images