Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wananchi Watakiwa Kuwa Wavumilivu Wakati Serikali Inachukua Hatua Maafa Ya Tetemeko La Ardhi Bukoba

$
0
0
Beatrice Lyimo na Eleuteri Mangi- MAELEZO Dodoma.

Wananchi wameaswa kuwa wavumilivu na kuendelea kushirikiana na Serikali wakati jitihada mbalimbali zikiendelea kuchukuliwa katika kukabiliana na athari za tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera hivi karibuni.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) George Simbachawene alipokuwa akitoa kauli ya Serikali bungeni kuhusu Maafa yaliyosababishwa na tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera siku ya jumamosi tarehe 10/09/2016.
 
Waziri Simbachawene amesema kuwa hadi leo tarehe 13/9/2016 idadi ya vifo vilivyosababishwa na tetemeko hilo katika Mkoa wa Kagera ni 17, ambapo majeruhi waliolazwa katika hospitali mbalimbali zilizoko Mkoani humo ni 169, majeruhi waliotibiwa na kuruhusiwa ni 83, nyumba za makazi zilizoanguka ni 840, nyumba za makazi zenye nyufa ni 1,264 pamoja na taasisi zilizoanguka na kupata nyufa ni 44.
 
Aidha, Waziri Simbachawene amesema kuwa mpaka sasa Serikali imechukua hatua za kuwaokoa watu na kuwapeleka hospitali kwa ajili ya matibabu na kuwapatia makazi ya muda baadhi ya wananchi ambao nyumba zao zimeathirika.
 
Pia Serikali inaendelea kutibu majeruhi bure na wenye Bima za Afya kutumia bima zao na kuongeza nguvu ya madaktari bingwa 15 kutoka mkoa ya Mwanza ili kuweza kutoa huduma ya haraka kwa wahanga hao.
 
Vilevile Waziri Simbachawene amesema kuwa Serikali imeelekeza wanajiolojia kuwatoa hofu wananchi kwa kutoa maelekezo ya kisayansi kuhusu hali hiyo na kuendelea kufanya tahimini ya athari zilizosababishwa na tetemeko hilo.
 
Hata hivyo Waziri Simbachawene amesema kuwa serikali imezifunga shule za sekondari Ihungo na Nyakato zilizopo mkoani humo kutokana na athari za tetemeko iliyopelekea kuharibika kwa miundombinu ikiwemo madarasa, vyoo, mabweni na maabara, wakati serikali ikiendelea na taratibu za kushughulikia tatizo hilo.
 
Waziri Simbachawene ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuhakikisha kuwa hatua za dharura zinachukuliwa kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuhakikisha ili kuwasaidia wahanga.
 
Mbali na hayo Mbunge wa Mlalo Mhe. Rashid Shangazi ametoa hoja juu ya wabunge kuchangia posho yao ya siku moja ili iweze kuwasaidia wahanga wa tetemeko hilo lililokadiriwa kuwa na ukubwa wa kiwango cha 5.7 katika vipimo vya Richter ambapo wabunge waliunga mkono hoja hiyo na kuridhia kuchangia kusaidia maafa hayo.
 
Aidha, Mbunge wa Muleba, Prof. Anna Tibaijuka ameishukuru Serikali kuwepo kwenye eneo la tukio mkoani Bukoba hatua ambayo imewapa faraja wanakagera na kutoa wito kwa wabunge na watu wenye mapenzi mema kuzidi kuwafariji wahanga hao.
 
Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Charles Tizeba amesema kuwa Serikali itafanya tathmini ya kina na ya kitaalamu ili kuepuka wale ambao wanatumia maafa hayo katika kujinufaisha.
 
Akishukuru kwa niaba ya Serikali Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amewashukuru wadau wote kwa kujitokeza na kushirikiana na Serikali katika kutatua changamoto na kuwahakikishia wabunge kuwa mchango wao utawafika walengwa na kuongeza kuwa jambo hilo limepelekea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusitisha safari yake nchini Zambia ili kuweza kusimamia suala hilo.
 
Aidha, Waziri Lukuvi amesema kuwa Serikali inauchungu mkubwa juu ya maafa hayo, hivyo amewataka wadau mbalimbali kujitokeza kusaidiana na Serikali ili kuweza kuwasaidia wahanga hao  na kuwapa pole waathirika wa tetemeko hilo na kuwaombea marehemu wapumnzike kwa amani. 

Polisi akikamata haulizi itikadi ya mtu - Mwigulu

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba amesema Jeshi la Polisi nchini linafanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu na linapomkamata mtu halimuulizi itikadi ya chama chake.
 
Waziri Mwigulu ameyasema hayo leo bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) kutoka Mwanza Susan Masele aliyetaka kupata kauli ya serikali juu ya askari polisi ambao wanawabambikizia kesi wafuasi wa UKAWA kwa kuwapa kesi za uchochezi.

“Jeshi la polisi linapowakamata watu, haliwaulizi itikadi zao, na linapowafikisha mahakamani haliwaulizi kadi za vyama vyao bali huangalia kosa ambalo limefanyika” Amesema Waziri Mwigulu.

Aidha waziri amesema kuwa wananchi wanaweza kupeleka malalamiko yao kuhusu Jeshi la Polisi katika vyombo vinavyoshughulikia sheria au katika makao makuu ya jeshi kwa kuwa kuna kitengo kinachoshuhulikia malalamiko ya wananchi.

Sambamba na hayo Waziri Mwigulu ameweka bayana kwamba askari ambao hukutwa na mashtaka ya kuwabambikizia wananchi kesi au mambo mengine na yakibainika kuwa ni ya kweli huadhibiwa na kulingana na sheria.

Selection Za Vyuo Vikuu Kwa Walioomba Kujiunga na Vyuo Mbalimbali Mwaka Huu Zimetoka

$
0
0


Selection za TCU kwa walioomba kujiunga na vyuo mbalimbali kwa mwaka wa masomo 2016/2017  zimetoka.

==> Bofya hapa  kuangalia  <<Selection Status >> 

NB:  Tumia index number yako na password





Namba ya akaunti ya kuwachangia walioathiriwa na tetemeko la ardhi Kagera

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Septemba 14

Wanafunzi Wacharaza Viboko Walimu Wao ........Mmoja Ang'olewa Meno Matano, Mwingine Ngeu Kichwani

$
0
0
Waziri wa Elimu, Prof Joyce Ndalichako

Wawanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Usevya wilayani Mlele Mkoa wa Katavi, wanadaiwa kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko walimu wao wawili miongoni mwao akiwemo Makamu Mkuu wa Shule hiyo, Makonda Ng’oka “Membele'‘ (34) ambaye ameng’olewa meno matano kwa kipigo hicho.

Walimu hao wawili wamedai kuwa hawako tayari kuendelea kufundisha katika shule hiyo huku wakisisitiza kuwa ni fedheha kwao kucharazwa viboko na wanafunzi wao wenyewe ambapo Mwalimu Gabriel Kambona aliachwa na ngeu kichwani.

Mei mwaka huu, Ng’oka “Membele” alifikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake akidaiwa kutenda kosa hilo kati ya Novemba 2015 na Aprili mwaka huu.

Ilisemekana kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Makamu Mkuu huyo wa shule hiyo kulifuatia wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo kumkataa na kutishia kuandamana kupinga vitendo vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.

Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo amekuwa akiwalawiti baadhi yao ikiwa ni adhabu mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni hapo.

Hata hivyo, baada ya kutopatikana ushahidi wa kumtia hatiani Ng’oka, Julai 27, mwaka huu Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda ilimwachia huru.

Mwalimu Ng’oka aliripoti kwenye kituo chake cha kazi shuleni Usevya Agosti Mosi mwaka huu ambako kurejea kwake shuleni hapo kunadaiwa kuamsha hasira kwa baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita wakidai hawapo tayari kumwona mwalimu huyo na familia yake shuleni hapo.

Akizungumza na wanahabari jana mjini hapa, Ng’oka alidai kuwa hayuko tayari kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo akihofia usalama wake na kutokana na kipigo alichokipata cha kushambuliwa na baadhi ya wanafunzi wake wa kidato cha tano na cha sita wakati akiwa nyumbani kwake na familia yake.

 Akisimulia mkasa huo, alisema Agosti 12, mwaka huu usiku alikuwa nyumbani kwake shuleni hapo pamoja na familia yake pamoja na mwalimu mwenzake, Gabriel Kambona aliyekuwa amemtembelea.

“Ghafla, saa mbili usiku nikiwa maliwatoni nikioga lilitokea kundi la wanafunzi wa kidato cha tano na sita wakiwa na silaha za jadi kama vile fimbo, marungu, mawe na matofali na kuanza kuishambulia familia yangu pamoja na mwalimu Kambona,” alieleza na kuongeza kuwa alilazimika ‘kuchomoka’ bafuni baada ya kusikia mayowe yaliyokuwa yakipigwa na familia yake wakiomba msaada. Alipofika sebuleni alishuhudia wanafunzi hao wakiishambulia familia yake kwa kuwacharaza viboko.

“Ndipo walinigeukia na kuanza kunishambulia kwa kunipiga kwa marungu na fimbo hadi nikapoteza fahamu nilizinduka nikiwa nimelazwa kwenye Kituo cha Afya Usevya na kubaini kuwa nimepoteza meno yangu matano huku nikiwa nimejeruhiwa vibaya kichwani. Baadaye nilihamishiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ambako nililazwa wiki moja na nusu kwa matibabu na sasa nimepewa rufaa niende Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar kwa matibabu zaidi,” alieleza.

Alidai kuwa uhasama baina yake na wanafunzi hao umedumu kwa muda mrefu, lakini anashangaa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya Mlele umeshindwa kumpangia kituo kingine cha kazi na kuchukua hatua yoyote kwa wanafunzi hao licha ya kupeleka majina yao kwa kuwa anawafahamu wote waliohusika.

Mwalimu Kambona alidai kuwa hayuko tayari kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwamba kitendo cha kupigwa na wanafunzi wake kimemfedhehesha.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo, walimu wa shule hiyo waliketi baada ya kutokea kwa tukio hilo, na walifikia maamuzi kuwa wanafunzi wote waliobainika kushiriki kuwashambulia walimu wao wasimamishwe shule akidai kuwa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya Mlele ulipinga.

“Nimeandika barua ya kuomba uhamisho kwani nia aibu kwangu kuendelea kufundisha wanafunzi ambao wamenishambulia na kunitoa ngeo kichwani ….. siku hiyo ya tukio niliibiwa simu mbili za kiganjani lakini jana nimefanikiwa kuikamata simu moja kwa mwanafunzi wa kidato cha tano anayeitwa , Alex Maiko Makona na tayari amemfikisha katika Kituo cha Polisi cha Usevya,” alidai.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Katavi, Gregori Mshota alisema tayari chama chake kimeanza kuwasiliana na uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na uongozi wa Wilaya ya Mlele ili kuhakikisha mwalimu huyo anakuwa salama.

Ofisa Elimu wa Mkoa wa Katavi, Ernest Hinju alidai kuwa suala hilo lipo ofisini kwake na wameanza kulitafutia ufumbuzi. “Jambo hili linahitaji ushirikishwaji wa vyombo mbalimbali ikiwemo Bodi ya Shule ya Sekondari ya Usevya,” alieleza.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa katika ziara mkoani Katavi mwezi uliopita, mke wa mwalimu Ng’oka alitinga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini Maji Moto akiwa na bango lenye malalamiko ya kutishiwa usalama wa maisha wa familia yake, na Waziri Mkuu alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa kushughulikia malalamiko hayo.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Apokea Zaidi Ya Sh. Bil. 1.4 Kwa Ajili Ya Maafa Ya Tetemeko La Kagera

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea michango wa zaidi ya sh. bilioni 1.4 kutoka kwa mabalozi wa nchi za nje nchini Tanzania na Jumuia ya Wafanyabiashara wa Kitanzania kwa ajili ya kusaidia wananchi waliothirika na tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera.

Tetemeko hilo lilitokea Jumamosi, 10 Septemba, 2016 na kusababisha vifo vya watu 17 hadi leo na wengine 253 kujeruhiwa. Pia limesababisha maelfu ya wananchi kukosa makazi baada ya nyumba 840 kuanguka na nyingine 1,264 zikipata nyufa yakiwemo majengo 44 ya taasisi mbalimbali za umma.

Akizungumza katika hafla ya uchangishaji fedha kwa ajili ya kusaidia wahanga hao jana Jumanne, 13 Septemba, 2016 Waziri Mkuu aliwashukuru kwa michango yao ya fedha na vifaa vya ujenzi ikiwemo mifuko 2,800 ya saruji. Amesema tetemeko hilo ni kubwa na halijawahi kutokea nchini.

Alisema tetemeko hilo limesababisha Serikali kuzifunga shule zake mbili za sekondari za Nyakato na Ihungo kati ya nne zilizoathirika vibaya na tetemeko hilo.

“Serikali itajitahidi kuhakikisha inarejesha miundombini iliyoharibiwa na tetemeko hilo katika kipindi kifupi ili wanafunzi na wananchi wengine waweze kuendelea na shughuli zao za kawaida,” alisema.

Waziri Mkuu alisema katika kuhakikisha suala hilo linashughulikiwa haraka tayari Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Muhagama yuko mkoani Kagera akiongoza kitengo cha maafa kufanya thamnili kujua athari zilizosababishwa na tetemeko hilo.

Mawaziri wengine walioko mkoani Kagera wakiendelea kufanya tathmini hiyo ni pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako.

Alisema Kamati ya Maafa ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Kamati ya Maafa ya mkoa wa Kagera imefungua akaunti maalumu katika benki ya CRDB kwa ajili ya kupokea michango kutoka kwa watu mbalimbali. Namba za akaunti hiyo ya Kamati ya Maafa ya Kagera ni CRDB 0152225617300.

Pia Waziri Mkuu aliwapongeza na kuwashukuru waheshimiwa Wabunge kwa kuamua kutoa posho zao za kikao cha jana kwa ajili ya kuchangia wahanga wa tetemeko hilo na kuwaomba wananchi wengine kujitokeza na kutoa michango yao.

Wakati huo huo viongozi wa makampuni ya mafuta ya GBP, Oil Com na Moil wameahidi kujenga shule mbili za Nyakato na Ihungo ambazo sehemu kubwa ya miundombinu yake imeharibika vibaya. Shule hizo zitajengwa katika kipindi cha siku 30.

Hafla hiyo iliyoongozwa na Waziri Mkuu ilihudhuriwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi, Dk. Aziz Mlima.

Wakurugenzi Wapya 13 Waapishwa.....Watakiwa kufuatilia maagizo ya viongozi

$
0
0
Wakurugenzi wapya 13 wa halmashauri wameapa kulinda maadili na kukabidhiwa majukumu ya kufuatilia maagizo ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, kwenye maeneo yao na kutoa mrejesho wa hatua za utekelezaji wake. 

Kiapo hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Angela Kairuki aliyewataka kutilia mkazo ufuatiliaji wa maagizo na kupambana na tatizo la watumishi hewa ambao idadi yao imefikia 17,102 waliogundulika katika kipindi cha kuanzia Machi mpaka sasa. 

Wakurugenzi hao walioteuliwa hivi karibuni na Rais, John Magufuli waliapishwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene katika ukumbi wa Tamisemi mjini Dodoma.

 Akizungumza mara baada ya kiapo hicho, waziri Kairuki aliwataka wakurugenzi hao kutekeleza matamko yote yanayotolewa na viongozi wa ngazi za juu serikalini, kwa kutoa mrejesho wa utekelezaji wake. 

Kairuki aliwataka kufanya kazi kwa bidii ili wawatumikie wananchi wanaowaongoza. 

Alisema katika ziara nyingi alizozifanya, amekuta wakurugenzi hawafuatilii matamko yanayotolewa na viongozi wa ngazi za juu serikalini katika maeneo yao. 

“Hata kwa wale ambao wanayafuatilia huwa hawatoi mrejesho wa hatua zilizofikiwa katika kutekeleza matamko hayo, hivyo ninawaomba mkayatekeleze maagizo na kurudisha mrejesho kwa kiwango kinachotakiwa,” alisema Kairuki. 

Pia, aliwataka wakurugenzi hao kwenda kusimamia fedha za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali hadi senti ya mwisho, ili kuhakikisha inatekelezwa kwa asilimia 100. 

Alisema kuna baadhi ya miradi ya maendeleo, inatekelezwa kwa fedha za Serikali na wakati huo huo inatumia fedha za wafadhili. 

Waziri Kairuki aliwataka wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa miradi yote inayotumia fedha za Serikali inasimamiwa ipasavyo. 

“Utakuta mradi mmoja unafadhiliwa na pia unatumia fedha za Serikali, kwa hiyo wafadhili wakija kukagua wanaonyeshwa jengo likiwa limekamilika na Serikali nayo ikija kukagua inaonyeshwa jengo hilohilo. Nataka mkasimamie fedha zote za Serikali kwenye mamlaka zenu,” alisema Kairuki. 

 Alisema kuna baadhi ya maeneo ambako fedha za Tasaf (mpango wa kunusuru kaya maskini), zimetumika kujengea maabara na kununulia madawati kinyume na malengo yaliyokusudiwa. 

Pia, aliwataka kuhakikisha kuwa hatua kali za kinidhamu zinachukuliwa kwa wakati kwa watumishi waliosimamishwa kazi katika kipindi cha miezi sita na si zaidi ya hapo. 

Alisema mtumishi aliyechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo kufukuzwa au kusimamishwa kazi, mchakato wake wote ufanyike ndani ya miezi sita. 

Aliwataka pia wakurugenzi hao kufuata maadili ya viongozi wa umma, kwani wakikiuka watafikishwa kwenye baraza la maadili ya viongozi wa umma ambalo kwa sasa limeongezewa meno. 

Waziri Kairuki aliwataka wakurugenzi hao kusimamia suala la rasilimali watu, kwani utafiti ulionyesha kuwa asilimia 80 hadi 90 ya watumishi wa umma ni watoro.

Alisema katika baadhi ya maeneo kuna wakaguzi na waratibu wa elimu wa kata, lakini hawatembelei shule zao kuona kama walimu wanahudhuria shuleni au la. 

Kadhalika, aliwataka wakurugenzi hao kuachana na tabia ya kuwatumia viongozi wa Serikali walioko chini yao, kama vile watendaji wa kata, vijiji na wenyeviti wa vijiji kuwalimia mashamba yao.

Alisema watakaobainika kufanya vitendo hivyo, watachukuliwa hatua kali za kinidhamu. 

Waziri Simbachawene aliwataka wakurugenzi hao kwenda kuchapa kazi bila kumwonea yeyote. Aliwaambia kuwa kukusanya  mapato kiwe ni kipaumbele chao cha kwanza, kwani kipimo cha mamlaka yoyote kujitegemea ni uwezo wake wa kukusanya mapato. 

Aliwataka wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa wanawatembelea watumishi wao wote ili kujua penye upungufu, idadi yao na hata ikiwezekana kuwajua kwa majina yao. 

Wakurugenzi walioapishwa jana ni Godwin Kunambi (Dodoma) Elias Ntiruhungwa (Tarime), Mwantumu Dau (Bukoba) na Frank Bahati (Ukerewe) Wengine ni Hudson Kamonga (Mbulu), Mwailwa Pangani (Nsimbo), Godfrey Sanga (Mkalama), Yusufu Semuguruka (Ulanga), Bakari Mohamed (Nachingwea), Juma Mnweke (Kibondo), Butamo Ndalahwa (Moshi), Waziri Mourice (Karatu) na Fatma Latu (Bagamoyo). 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe. George Simbachawene.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angella Kairuki akiongea Wakurugenzi wapya mara baada ya kuapishwa jana mjini Dodoma. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe. George Simbachawene. Kushoto kwa Simbachawene ni  Mkurugenzi mteule wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilimanjaro Bi. Butamo Nuru Ndalahwa

Majambazi Yavamia Magari ya Mnadani na Kumuua Dereva Mmoja kwa Risasi

$
0
0
Majambazi wapatao 10 juzi usiku walivamia magari mawili yaliyobeba wafanyabiashara waliokuwa wakitokea mnadani na kumuua kwa risasi, dereva aliyegoma kuwapa fedha na simu.

Dereva huyo, Chrispin Inyangwe (40) alipigwa risasi ya mgongoni alipojaribu kupambana nao.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana eneo la katikati ya vijiji vya Miula na Kalundi vilivyopo Kata ya Kipande wilayani Nkasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alisema wafanyabiashara hao walikuwa wakitokea mnadani na walipofika eneo hilo walikuta mawe yamepangwa barabarani kuzuia magari.

Alisema baada ya kuona mawe hayo, magari hayo yalilazimika kusimama na ndipo majambazi hao waliokuwa na silaha za moto, mapanga na marungu walipoibuka na kufyatua risasi hewani na baadaye kutaka wafanyabiashara hao wasalimishe fedha na simu zao za mkononi.

Kamanda huyo alisema baadhi ya wafanyabiashara walisalimisha fedha na simu zao, na waliokataa walishambuliwa.

Inasemekana kwamba Inyangwe ambaye alikuwa dereva wa gari aina ya Mitsubishi Canter alikaidi kutoa fedha na kutaka kupambana nao, ndipo watu hao waliokuwa na bunduki aina ya SMG walipomfyatulia risasi iliyompata mgongoni na kufariki dunia papo hapo.

Kitendo hicho kiliwafanya wafanyabiashara wengine waliokuwa wakikataa kutoa fedha, kuzisalimisha sambamba na simu zao, ndipo majambazi hao walipowaachia na kukimbia.

Watu 19 waliojeruhiwa walipelekwa Hospitali ya Mkoa mjini Sumbawanga. Kamanda Kyando alisema majeruhi 12 waliruhusiwa kurejea nyumbani na wengine saba wanaendelea na matibabu na kwamba polisi wanaeendelea na msako wa watu hao.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 3 & 4

$
0
0
Mtunzi : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
“Hakikisheni huyu dada nina lala naye usiku wa leo sawa”
Muntar aliwaamrisha wapambe wake na wakamtii na mmoja wao akanyanyuka kwenda kumfatwa Agnes kwenye eneo la kuuzi vinywaji ili kuzungumza ombi la bosi wake analo lihitaji

ENDELEA
“Habari yako dada?”
Kijana wa Muntar alimsalima Agnes ambaya kwa haraka akaliachia tabasamu lake mdomoni na kuufanya uso wake kuzidi kunawiri kwa uzuri

“Salama mamo vipi?” Agnes alizungumza kwa sauti nyororo ya kuvutia hadi muhudumu kiume wa vinywaji akaguna
“Salama.....kwa jina mimi ninaitwa Kibopa na yule pale alavalia cheni nyingi ni bosi wangu anaitwa Muntari”
“Aahaa nashukuru kuwafahamu,Samahani kaka ninaomba unipatie Red’s mbili za baridi kiasi”
“Muhudumu mpe katon nzima pesa nitalipa mimi?”
“Jamani kaka yangu mimi sio mnywaji sana”
“Ahaa usijali nyingine unaweza kunywa leo au hata kesho”
“Asante sana”

Muhudumu akamkabidhi Agnes katoni ya kinywaji alicho muagizia na kibopa akatoa pesa na kumlipia muhudumu.
“Sasa sister kama huto jali ninaomba namba yako ya simu”
Agnes bila wasiwasi akamtajia Kibopa namba yake ya simu,wakaagana ana Agnes akarudi sehemu alipo Rahab
“Jamaa ameshaingia mkenge sasa kazi ni moja sawa”
“Hapo ndipo ninakupendea Ag”
“Chezea mimi wewe,kumbe mtu ukiwa na kalio kubwa nalo linasaidia”
Wakacheka na kufungua vinywaji na kuanza kunywa taratibu.Muntar akakabidhiwa namba na Kibopa na akaipiga na Agenes akaipokea na kama kawaida na sauti yake nyororo aliyobarikiwa kutoka mbinguni akazungumza
“Nani mwenzangu?”
“Ukigeuka upande wako wa kushoto utaniona nimevaa shati jeupe na cheni za dhahabu”
Agnes akageuka na kumfanya Muntar kupunga mkono akimuashiria kuwa ni yeye ndiye aliye mpigia simu
“Mrembo nakuomba basi uje kujumuika name hapa?”
“Naona aibu labda nije na mwezangu”
“Hilo tuu hakuna tatizo ni wewe tuu”
“Sawa ninakuja”

Agnes akakata simu na kumtazama Rahab kwa pamoja wakatabasamu na wakasimama na kuanza kutembea kwa mwendo wa maringo na kupishwaviti na wapambe wa Muntar kisha wakakaa
                                                                       ***
Dokta Wiliama akawashusha kwenye gari Anna,Halima na Fety mbali kidogo na hotel ya Serena huku kila mmoja simu yake ikiwa na salio la kutosha pamoja na picha ya Karim Yussuf kijana mwenye umri mdogo ila anasifika sana kuwa na utajiri mkubwa kutokana na Sheli za mafuta anazo zimiliki kila kona ya mikoa ya Tanzania.Kila mmoja akaingia Hotelini kwa muda wake na kuelekea kuketi katika upande wake ila kwa pamoja wakawa na mawasiliano ya ujumbe mfupi wa meseji.Kutokana ni muda wa jioni hawakuwa na papara kwani watu wengi bado hawakuwa wameingia Hotelini kuendelea na starehe zao.Macho ya Fety yakatua kwa jamaa anayeingia kwenye  mlango wa kuingilia akiwa ameongozana na mwanamke mrembo
{Nimemuona}

Fety akausamba ujumbe kwa wezake ambao wapo maeneo ya tofauti kwenye hoteli na taratibu simu yake akaichomeka kwenye suruali yake na kuendelea kumtazama Karim ambaye moja kwa moja aka anaelekea sehemu yenye milango ya lifti zinazo kwenda juu  na kushuka chini,Kutokan-a na Lifti kutumika ikamlazimu Karimu na mpenzi wake kusimama kwa muda kuzisubiria.

Kwa haraka Fety akasimama na kupiga hatua za haraka kabla hajafika sehemu alipo Karimu,lifti ambayo wanaisubiria ikafunguaka,Karim na mpenzi wake wakingia ila kabla haijajifunga Fety akawahi kuizuia na kuingia
“Habari zenu?”
“Salma”

Karimu kutokana na kutokuwa na aibu akaanza kumshika shika mpenzi wake na kuchezeana katika sehemu zao nyeti.Mcho ya Fety yakawangalia kwa umakini kisha akayahamishia masho yake kwenye kamera mbili za ulinzi zilizopo ndani ya lifti kabla hajafanya kitu chochote akastukia lifti ikisimama hii ni baada ya mpenzi wa Karimu kuminya kitufe cha kuisimamisha lifti.

Kufuma na kufumbua Fety akastukia ngumi kutoka kwa mpenzi wa Karim ikitua kwenye shavu lake na kumsfanya kuweweseka kasha akaanza kuikwepa mikono inayoimjia mwilini mwake kutoka kwa Karimu na mpenzi wake Shamsa mwenye asili ya kiarabu.

Rais Dkt. Magufuli Amuapisha Balozi Dk. Dau Pamoja Na Makatibu Tawala Wa Mikoa Mitatu Ikulu Jijini Dar Es Salaam.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 14 Septemba, 2016 amemuapisha Dkt. Ramadhani Kitwana Dau kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi, Dkt. Ramadhan Kitwana Dau alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF)

Mhe. Balozi Dkt. Ramadhani Kitwana Dau anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Aziz Ponary Mlima ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wakati huo huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli, amewaapisha Makatibu Tawala wa Mikoa mitatu aliowateua mwishoni mwa wiki iliyopita.

Walioapishwa ni  kwanza, Bw. Eliya Mtinangi Ntandu anayekuwa Katibu Tawala wa kwanza wa Mkoa wa Songwe ulioanzishwa rasmi Mwezi Februari 2016.

Pili, Bw. Adoh Stephen Mapunda anayekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara.

Bw. Adoh Stephen Mapunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Benedict Richard Ole Kuyan ambaye amestaafu.

Tatu, Bw. Tixon Tuliangine Nzunda anayekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa.

Bw. Tixon Tuliangine Nzunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Symthies Emmanuel Pangisa ambaye amestaafu.

Baada ya kuapishwa, Mhe. Balozi Ramadhani Kitwana Dau na Makatibu Tawala wote watatu wamekula Kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Salome Kaganda na kushuhudiwa na Rais Magufuli.

Matukio yote yamefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
14 Septemba, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Tixon Nzunda kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Rukwa, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Eliya Ntandu kuwa Katibu Tawala mkoa wa Songwe, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau mara baada ya tukio la uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.

Edward Lowassa ampongeza Rais Magufuli

$
0
0

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amempongeza Rais Magufuli kwa kuondoa urasimu katika taasisi za serikali na kusema hiyo itasaidia kurejesha utendaji kazi kwa ufanisi.

Lowassa ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na mtangazaji wa BBC, John Nene nchi Kenya ambapo alisema urasimu umepungua na hili amejitahiidi lakini kuna mambo baadhi hayako vizuri.

Lowassa hakuwa tayari kusema ni mambo gani haswa hayakua yakienda sawa lakini alimkosoa Rais Magufuli kwa kile alichodaiwa kuwa analeta dalili za udikteta.

Lowassa alikuwa ni mpinzani mkuu wa Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 akigombea kupitia CHADEMA na kuungwa mkono na vyama vinavyounda UKAWA.

Amekosoa pia uamuzi wa serikali ya awamu ya tano kupiga marufuku maandamano, mikutano na vikao vya ndani vya vyama siasa huku vyombo vya habari vikifungiwa na wale wote wanamkosoa wakifikishwa mahakamani.

Akielezea Opersheni UKUTA, Lowassa alisema kuwa walipanga kuandamana ili kupinga dalili za udikteta alizoanza kuzionyesha Rais Magufuli.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15

Waziri wa Ujenzi atoa miezi sita kumaliza upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa mkandarasi Nyanza Road Construction inayojenga barabara ya Furahisha hadi Pasiansi KM 2.8 wakati alipokagua ujenzi wa barabara hiyo, jijini Mwanza.

*****
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemtaka Mkandarasi wa kampuni ya Beijing Construction Engineering Group anayejenga uwanja wa ndege wa Mwanza kumaliza kazi ya upanuzi wa uwanja huo ifikapo mwezi Februari Mwakani.

Profesa Mbarawa ametoa kauli hiyo alipokuwa akikagua kazi ya ujenzi na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza pamoja na daraja la watembea kwa miguu lililopo maeneo ya furahisha, jijini Mwanza.

Profesa Mbarawa amesema kuwa kukamilika kwa ujenzi na upanuzi wa uwanja huo kutaimarisha hali ya usafiri wa anga kwa wakazi wa Mwanza na mikoa mingine na hivyo kukuza shughuli za kibiashara nchini.

“Hakikisheni upanuzi wa uwanja wa ndege huu unakamilika haraka ili kurahisisha na kuboresha huduma za usafirishaji kiwanjani hapa”, alisema Waziri Mbarawa.

Aidha, Profesa Mbarawa amemtaka mkandarasi wa kampuni ya Nyanza Road Construction kumaliza kwa wakati upanuzi wa barabara ya ‘Mwanza-Airport’ eneo linaloanzia Ghana Quarters hadi Uwanja wa Ndege wa Mwanza KM 9.15 pamoja na daraja la watembea kwa miguu la furahisha ili kukuza uchumi na kupunguza kero ya msongamano wa magari katika jiji la Mwanza.

Katika hatua nyingine Prof. Mbarawa amewataka wananchi wa Mwanza kutoharibu miundombinu ya barabara na madaraja ambayo Serikali inatumia gharama kubwa katika utengenezaji wake.

“Naomba muitunze na kuithamini miundombinu hii kwani Serikali inatumia gharama kubwa katika kutengeneza na kukarabati”, alisisitiza Prof. Mbarawa.

Ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza ni mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa uwanja huo unaboreshwa kuwa wa kisasa na wa kimataifa ili kuwezesha ndege kubwa kutua kwa wingi na kuwa kiungo muhimu kwa mikoa 10 ya kanda ya Ziwa na Kati.
Mkandarasi wa kampuni ya Nyanza Road Construction inayojenga barabara ya Furahisha hadi Pasiansi akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipokagua ujenzi wa barabara hiyo jijini Mwanza.

Serikali yatoa majibu ya hatua iliyofikia kuhusu viwanda ilivyovibinafsisha

$
0
0
Serikali inatekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli la kuhakikisha viwanda vilivyobinafsishwa vinafanya kazi linatekelezwa tangu mwezi Novemba mwaka 2015.

Hayo yalibanishwa jana na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Manyoni Mhe. Yahaya Massare lililohusu utekelezaji wa ahadi ya Rais kuvirudisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa lakini havifanyi kazi.

Waziri Mwijage alisema kuwa Serikali kupuitia Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji inaendelea na zoezi la kuchambua mikataba ya mauzo kwa viwanda vilivyobinafsishwa ambavyo ama havifanyi vizuri au vimesimamisha uzalishaji kabisa.

Waziri alibainisha kuwa timu ya wataalamu toka Wizara ya Viwanda na Ofisi ya Usajili wa Hazina walifuatilia na kufanya tathimini kwa kutembelea kiwanda baada ya kiwanda hatua ambayo inasaidia kutafuta ufumbuzi wa matatizo yaliyopelekea kiwanda kutofanya kazi.

Aidha, Waziri Mwijage alisema kuwa uchambuzi wa mikataba ya viwanda hivyo unafanyika kwa ushirikiano na Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na Wizara za kisekta ikiwemo Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Nishati na Madini, pamoja na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Hata hivyo, Waziri Mwijage alisema kuwa katika kutekeleza ahadi hiyo ya Rais, Serikali imetwaa Kiwanda cha Chai Mponde kilichopo wilaya ya Lushoto mkoani Tanga ambacho mwekezaji amekiuka makubaliano ya mkataba.

Mbali na hayo, akijibu swali la Mbunge wa Tabora Mjini Mhe. Emmanuel Mwakasaka lililohusu mpango wa Serikali kujenga maabara ya kupima ubora na kiwango cha asali inayozalishwa hapa nchini.

Waziri Mwijage alisema kuwa Serikali inaendelea kuhimiza ujenzi wa viwanda nchini ikiwemo viwanda vya asali na kuhakikisha vinakuwa na maabara zinazoweza kupima viwango vya msingi.

Waziri Mwijage aliongeza kuwa kuhusu ujenzi wa maabara mkoani Tabora, Wizara itahakikisha wawekezaji wanaofuatilia ujenzi wa viwanda vya asali wanakuwa na maabara za kupima viwango vya msingi vya msingi na kuiachia TBS kuweka viwango vya kitaifa na kudhibiti viwango hivyo.

Na Beatrice Lyimo, MAELEZO, Dodoma

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Profesa Beno Ndulu Atoa Taarifa Kuhusu Hali Halisi ya Uchumi wa Tanzania

$
0
0

1.0    Hali ya Uchumi wa tanzani


1.1  Ukuaji wa Uchumi


Kwa mujibu wa takwimu kutoka Ofisi ya Takwimu ya Taifa, hali ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeendelea kuwa ya kuridhisha. Katika robo ya kwanza ya mwaka 2016, ukuaji wa Pato la Taifa unakadiriwa kuongezeka kwa asilimia 5.5 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 5.7 kipindi kama hicho mwaka 2015 (Kielelezo Na. 1).


Kielelezo Na. 1: Mwenendo wa Ukuaji wa Uchumi Robo ya Kwanza ya Mwaka (Asilimia)


Chanzo: NBS, Ukokotoaji - Benki Kuu



Shughuli zilizochangia ukuaji huu wa uchumi kwa kiasi kikubwa ni pamoja na kilimo (asilimia 11.7), biashara (asilimia 10.6), uchukuzi (asilimia 10.1), sekta ya fedha (asilimia 10.1) na mawasiliano (asilimia 10.0).Shughuli za kiuchumi zilizokua kwa kasi ya juu zaidi katika robo ya kwanza ya mwaka 2016 ni sekta ya fedha (asilimia 13.5), mawasiliano (asilimia 13.4), na utawala wa umma (asilimia 10.2) (Kielelezo Na. 2).


Kielelezo Na. 2a: Ukuaji wa Shughuli Mbalimbali za Uchumi Robo ya Kwanza ya Mwaka (Asilimia)







Kielelezo Na. 2b: Mchango wa Shughuli Mbalimbali za Uchumi katika Ukuaji wa Uchumi Robo ya Kwanza ya Mwaka (Asilimia)







1.2 Matazamio ya Ukuaji wa Uchumi Mwaka 2016


Kwa kuangalia viashiria mbalimbali inaonekana kuwa hali ya uchumi wetu itaendelea kuimarika katika mwaka 2016. Kwa mfano:



Uzalishaji wa umeme nchini katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016 umeongezeka kwa asilimia 14.5 kufikia kWh milioni 3,454.2 ikilinganishwa na kWh milioni 3,016.7 katika kipindi kama hicho mwaka 2015. Ongezeko hili limetokana kwa kiasi kikubwa na jitihada za serikali katika kutumia nishati ya gesi kwenye uzalishaji umeme kufuatia kukamilika kwa bomba la gesi kutoka Mtwara na Lindi hadi Dar es Salaam pamoja na mtambo wa Kinyerezi I.

 Umeme unaozalishwa kwa kutumia nishati ya gesi umeongezeka kwa asilimia 52.2 (Kielelezo Na. 3). Hali hii itasaidia kuongezeka kwa uzalishaji viwandani pamoja na sekta nyingine zinazotegemea nishati ya umeme, na hivyo kuchangia katika kuongeza kwa pato la Taifa.  Gharama ya umeme itashuka pia.



Kielelezo Na. 3: Mwenendo wa Uzalishaji Umeme Nchini

Januari - Juni



Uzalishaji wa saruji katika robo ya kwanza ya mwaka 2016 umeongezeka kwa asilimia 7 kufikia tani elfu 725.4 ikilinganishwa na tani elfu 680.1 zilizozalishwa katika robo ya kwanza ya mwaka 2015. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na ongezeko la uzalishaji wa kampuni ya Dangote ambayo ina uwezo wa kuzalisha tani milioni tatu kwa mwaka (Kielelezo Na. 4).  

Ni matarajio yetu kwamba uzalishaji katika kiwanda cha Dangote chenye uwezo wa tani milioni 3 na katika viwanda vingine vya saruji nchini utaongezeka katika kipindi kilichobaki cha mwaka 2016 kwani mahitaji ya nchi bado ni makubwa kuliko uzalishaji ulivyo hivi sasa.  Aidha kuna miradi mikubwa mingi ya hapo baadaye itakayokuwa na mahitaji makubwa ya saruji kama vile mradi wa reli ya kati.



Kielelezo Na. 4: Mwenendo wa Uzalishaji Sarujii

Januari – Machi



Uagizaji wa malighafi za viwandani kutoka nje umeongezeka kwa asilimia 19.4 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016 kufikia Dola za Marekani milioni 520.2 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2015 (Kielelezo Na. 5)

Hali hii imechangiwa na kuendelea kukua kwa shughuli za uzalishaji viwandani. Ukuaji huu utaendelea kuchangia pato la Taifa kiujumla katika mwaka 2016.



Kielelezo Na. 5: Mwenendo wa Uagizaji Malighafi za Viwandani

Januari – Juni



Mauzo ya bidhaa za viwanda nje ya nchi yameendelea kukua kwa kasi ya kuridhisha. Katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016 mauzo ya bidhaa nje ya nchi yalifikia kiasi cha Dola za Marekani milioni 728.5, sawa na ongezeko la asilimia 15.6 ikilinganishwa na kiasi kilichouzwa kipindi kama hicho mwaka 2015 (Kielelezo Na. 6).



Kielelezo Na. 6: Mwenendo wa Uuzaji wa Bidhaa za Viwandani Nje ya Nchi

Januari – Juni




Makusanyo ya kodi katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016 yameendelea kuwa bora zaidi ikilinganishwa na nusu ya kwanza ya mwaka 2015, ikiashiria kuimarika kwa usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya serikali na kuendelea kuimarika kwa hali ya

uchumi wa nchi.



Mikopo itolewayo na mabenki ya biashara kwenye sekta binafsi, imeendelea kuongezeka kwa kasi ya kuridhisha katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016 kwa Shilingi bilioni 1,167.2, japo ni pungufu ikilinganishwa na ongezeko la Shilingi bilioni 1,577.5 la mwaka 2015. Ongezeko hili linaendana na malengo ya sera ya mwaka 2015/16 ambayo yanajumuisha utulivu wa mfumuko wa bei (Kielelezo Na. 7).



Kielelezo Na. 7: Mwenendo wa Ongezeko la Mikopo kwa Sekta Binafsi

Januari - Juni



Chanzo: Benki kuu



Miradi mikubwa ya viwanda na miundombinu inayoendelea na inayotarijiwa kuanza kazi siku za usoni itachangia katika kuimarisha uchumi. Hii ni pamoja na:

  1. Ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha  kisasa (Standard gauge)
  2. Ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda ambalo litahusu vile vile upanuzi wa bandari  ya Tanga
  3. Ujenzi wa Export Processing Zone ya Kurasini – itakayokuwa mhimili wa biashara kati ya China na Ukanda huu wa Afrika
  4. Mradi wa kuzalisha megawati 240 za umeme wa Kinyerezi II unaoendelea kujengwa.
  5. Miradi ya kupanua viwanja vya ndege nchini kwa mfano- Dodoma, na mingine inayoendelea -katika viwanja vya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya n.k.
  6. Ujenzi wa maghala ya taifa ya kuhifadhi chakula yenye uwezo wa kuhifadhi tani 350 yatakayojengwa kwa msaada wa Serikali ya Hungary katika sehemu mbalimbali nchini hususan katika mikoa inayozalisha mazao ya nafaka kwa wingi.
  7. Kiwanda cha kuzalisha saruji cha Dangote kilichopo Mtwara ambacho kipo mbioni kuzalisha kulingana na uwezo wake (full capacity);
  8. Kiwanda cha kutengeneza marumaru cha Mkuranga, Pwani ambacho ujenzi wake unaendelea
  9. Kiwanda cha kuzalisha mbolea mkoani Lindi - kinajengwa
  10. Kiwanda cha bidhaa za chuma – mkoani Pwani ambacho kiko mbioni kukamilika.


Kwa kuzingatia mwenendo wa viashiria mbalimbali vya shughuli za uchumi, ni dhahiri kwamba hali ya uchumi wa Tanzania ni nzuri na inatoa matumaini makubwa kwamba shughuli halali za kiuchumi zinaendelea kutekelezwa kama ilivyotarajiwa hapo awali hivyo lengo la ukuaji wa pato la Taifa la asilimia 7.2 kwa mwaka 2016 litafanikiwa. 

Hii inachangiwa pia na ukweli kwamba serikali ya awamu ya tano imejipanga katika kuimarisha uchumi endelevu usiokuwa na mianya ya rushwa; usimamizi thabiti wa rasilimali za umma; na ujenzi wa miundombinu bora kwa lengo la kujenga uchumi wa viwanda chini ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano.



1.3  Mwenendowa Mfumuko wa bei


Wastani wa mfumuko wa bei katika miezi sita ya kwanza ya mwaka 2016 umeendelea kuwa mzuri ukiendelea kushuka hadi kufikia asilimia 5.5 mwezi Juni 2016 na asilimia 4.9 mwezi Agosti 2016 kutoka asilimia 6.8 mwezi Desemba 2015 (Kielelezo Na. 8). 

Kushuka huku kwa wastani wa mfumuko wa bei kulichangiwa zaidi na bei zisizojumuisha bei za vyakula na nishati (core inflation) zikifuatiwa na zile za nishati na mafuta. Wastani wa mfumuko wa bei usiojumuisha bei za vyakula na nishati (core inflation), ambao ni kiashiria sahihi zaidi cha utekelezaji wa sera ya fedha, umeendelea kubaki katika viwango vya chini (wastani wa asilimia 2.8 katika miezi sita ya mwanzo ya mwaka 2016) kutokana na hatua mbalimbali thabiti za sera ya fedha na bajeti katika kudhibiti ujazi wa fedha na ukwasi katika uchumi.



Mfumuko wa bei unatarajiwa kuendelea kubakia katika viwango vya tarakimu moja katika siku zijazo na kufikia lengo la muda wa kati la asilimia 5. 

Hii ni kutokana na matarajio ya hali nzuri ya hewa itakayochangia kupungua kwa kasi ya kuongezeka kwa bei za vyakula, pamoja na ongezeko dogo la bei ya mafuta nchini inayotokana na mwenendo wa bei ya mafuta katika soko la dunia, na utulivu wa thamani ya Shilingi. 

Pia, mwendelezo wa sera thabiti ya fedha, usimamizi mzuri wa matumizi na mapato ya Serikali, na upatikanaji wa umeme utokanao na gesi ambao utasaidia kupunguza gharama za uzalishaji viwandani vitaendelea kuimarisha utulivu wa mfumuko wa bei. 

Hata hivyo ni muhimu kuzingatia kuwa upungufu wa mavuno ya mazao ya chakula uliojitokeza kwa baadhi ya nchi za ukanda wa kusini mwa Afrika unaweza kusababisha shinikizo la mfumuko wa bei katika siku za usoni.


Kielelezo Na. 8: Mwenendo wa Mfumuko wa Bei (Badiliko la Miezi 12)


Chanzo: Benki kuu


1.4 Utekelezaji wa Sera ya Fedha


Ili kufikia malengo ya serikali ya kuimarisha uchumi na kudumisha utulivu wa mfumuko wa bei, Benki Kuu imeendelea kutekeleza sera ya fedha inayolenga kudhibiti ukwasi ili uendane na mahitaji halisi ya uchumi. Ongezeko la fedha taslimu (reserve money) ambacho ni kipimo cha ukwasi kwenye uchumi limeendelea kubakia ndani ya malengo katika kipindi chote cha miezi sita ya kwanza ya mwaka 2016. 

Katika kipindi hicho ujazi wa fedha taslimu ulikua kwa wastani wa asilimia 11.6; wakati ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) ulikua kwa wastani wa asilimia 14.4, ikiwa ni ndani ya makadirio ya ukuaji usiozidi asilimia 16.0 kwa mwaka 2015/16.

Wakati huohuo sekta ya fedha imeendelea kuchangia ukuaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi kwa kasi nzuri ya kutoa mikopo kwa wakati na kwa kiwango cha kutosha. Mikopo kwa sekta binafsi ilikua kwa wastani wa asilimia 21.3 katika miezi sita ya kwanza ya mwaka 2016, sawa na kiwango kilichopatikana katika kipindi kama hicho mwaka 2015. 

Mikopo mingi kwa sekta binafsi ilielekezwa kwenye shughuli za biashara kwa wastani wa asilimia 19.3 ya jumla ya mikopo yote, shughuli za watu binafsi wastani wa asilimia 19.0, uzalishaji viwandani wastani wa asilimia 10.6, uchukuzi na mawasiliano wastani wa asilimia 7.9, na shughuli za kilimo asilimia 7.8.

Benki Kuu inaendelea kutekeleza sera madhubuti ya fedha kwa kutumia zana mbalimbali za sera ili kuhakikisha kwamba mahitaji ya ukwasi kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi yanafikiwa bila ya kuchochea mfumuko wa bei.



1.5     Mwenendo wa Thamani ya Shilingi ya Tanzania


Thamani ya Shilingi imeendelea kuwa tulivu katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016, kufuatia hatua mbalimbali za sera ya fedha zilizochukuliwa na Benki Kuu katika kusimamia hali ya ukwasi kwenye uchumi pamoja na mwenendo wa uchumi ndani na nje ya nchi. 

Kuimarika kwa sekta ya nje kulikotokana na ongezeko la mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi na kupungua kwa thamani ya bidhaa zinazoagizwa kutoka nje kumechangia katika utulivu wa thamani ya shilingi. 

Kupungua kwa thamani ya bidhaa kutoka nje kumechangiwa zaidi na kupungua kwa bei ya mafuta katika soko la dunia. Katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo ya mwaka 2016 Shilingi imekuwa ikibadilishwa kwa kati shilingi 2,180 hadi 2,190 kwa dola moja ya Marekani (Kielelezo Na. 9).



Kielelezo Na. 9: Mwenendo wa Thamani ya Shilingi



Chanzo:Benki kuu



Hali hii ya utulivu wa thamani ya Shilingi kwenye soko huru la fedha inadhihirisha kuwa sera thabiti za uchumi pamoja na mwenendo mzuri wa urari wa mapato ya fedha za kigeni, ndio jawabu la kulinda thamani ya shilingi dhidi ya fedha za kigeni na sio kudhibiti matumizi ya dola kama ambayo imekuwa ikidaiwa mara kwa mara. 

Nchi zenye udhibiti mkubwa wa fedha za kigeni mfano Afrika Kusini imeshuhudia kuyumba sana kwa thamani ya fedha yake tofauti na shilingi ya Tanzania.

Hivyo nguvu kubwa inapaswa ielekezwe katika kuboresha mazingira ya uwekezaji katika sekta mbalimbali hususan zile zinazoboresha urari wa malipo ya nje kama vile utalii, viwanda, uchimbaji madini, kilimo n.k. Ikumbukwe kuwa uhuru wa kumiliki na kutumia fedha za kigeni nchini Tanzania uliwekwa kama hatua ya kukabiliana na hali iliyokuwepo miaka ya 1980 ya kuadimika sana kwa fedha za kigeni na mchango wa uhuru huo tumeuona katika kuwepo kwa fedha za kigeni za kutosha. 

Nchi zilizojaribu kuondoa uhuru huo, mfano Zambia, zimeshuhudia kutoweka kwa fedha za kigeni kwenda nje. Hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kuhimiza na kuweka mazingira mazuri ya uzalishaji na kuondokana na fikra za kuingilia soko huru kama jawabu la kulinda thamani ya shilingi.


1.6  Mwenendo wa Sekta ya Kibenki


Katika miezi sita ya kwanza ya mwaka 2016, sekta ya kibenki imeendelea kukua ikichangiwa na uanzishwaji wa taasisi mpya za kifedha ikiwemo Benki ya Waalimu Tanzania (Mwalimu Commercial Bank Plc) na Canara Bank (Tanzania) Limited. Takwimu za awali za tathmini ya hali ya mabenki yetu zinaonesha kuwa mabenki yetu ni imara na salama, yakiwa na mitaji na ukwasi wa kutosha. Kufikia mwezi Juni 2016, kulikuwa na jumla ya benki na taasisi za fedha zinazosimamiwa na Benki Kuu zipatazo 65 zenye matawi 739 nchini kote.

Kiwango cha mitaji kikilinganishwa na mali iliyowekezwa (total capital to total risk weighted assets and off-balance sheet exposures) kilikuwa asilimia 17.17 kikilinganishwa na kiwango cha chini kinachotakiwa kisheria cha asilimia 12.0. Hali ya ukwasi ambayo hupimwa kwa kuangalia uwiano kati ya mali inayoweza kubadilishwa kuwa fedha taslimu na amana zinazoweza kuhitajika katika muda mfupi (liquid assets to demand liabilities) ulikuwa asilimia 37.03 ukilinganishwa na uwiano wa chini unaohitajika kisheria wa asilimia 20 (Jedwali Na. 1).

Amana za wateja katika mabenki zilipungua kutoka shilingi trilioni 20.52 mwezi Desemba 2015 kufikia shilingi trilioni 20.24 mwezi June 2016. Miongoni mwa sababu zilizochangia kupungua kwa amana kwenye mabenki ni pamoja na uamuzi wa Serikali kuhamisha sehemu ya fedha za taasisi na mashirika ya umma kutoka mabenki ya biashara kwenda Benki Kuu ya Tanzania. Aidha mikopo (loans and overdafts) iliongezeka kutoka shilingi trilioni 15.28 mwezi Desemba 2015 hadi kufikia shilingi trilioni 15.67 mwezi Juni 2016.

Upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi wasiofikiwa na mabenki umeendelea kuongezeka kutokana na ubunifu wa mipango ya utoaji wa huduma za malipo ya rejareja kupitia simu za mikononi, pamoja na huduma za uwakala wa mabenki (agent banking services).


Kiujumla kwa kuangalia viashiria vyote vya msingi hali ya ukwasi wa benki imeendelea kuwa ya kuridhisha. Benki Kuu katika kusimamia majukumu yake ya kisera, imeendelea kutoa mikopo ya muda mfupi kupitia “reverse repos” pamoja na kununua fedha za kigeni zinazotokana na mauzo ya bidhaa nje ya nchi kutoka kwenye benki. Kwa viashiria hivi ni dhahiri kwamba uamuzi wa serikali wa kuagiza fedha zake zote kuwekwa kwenye akaunti maalum Benki Kuu hakujasababisha sekta ya kibenki kutokuwa na ukwasi wa kutosha na kuacha kukopesha kwa sekta binafsi kama inavyofikiriwa na baadhi yetu.



Ni vyema jamii ya Watanzania ikafahamu kwamba akaunti ambazo fedha za mashirika zimehamishiwa Benki Kuu ni akaunti za kukusanya mapato tu. Akaunti za matumizi bado ziko katika benki za biashara ili kuyawezesha mashirika kufanya malipo kupitia akaunti hizo. Hivyo, bado benki za biashara ni kiungo muhimu kati ya mashirika ya umma na watoa huduma kwa mashirika hayo. Pia hali ya utoaji mikopo kama tulivyoona awali ni nzuri na watanzania wanaendelea kuhudumiwa na benki zetu kama inavyotarajiwa.



Jedwali Na. 1: Viashiria vya Uimara wa Sekta ya Fedha







1.7 Sekta ya Nje na Akiba ya Fedha za Kigeni


Katika miezi sita ya kwanza ya mwaka 2016, nakisi ya urari wa biashara ya bidhaa, huduma na uhamisho mali nchi za nje (current account deficit) ilipungua kwa asilimia 61.7 na kufikia nakisi ya dola za Kimarekani milioni 970.4, kutoka nakisi ya dola za Kimarekani milioni 2,532.5 mwaka 2015. Kupungua huko kulitokana zaidi na ongezeko la thamani ya bidhaa za viwandani, mapato yatokanayo na utalii na huduma za usafirishaji nje ya nchi, pamoja na kupungua kwa thamani ya bidhaa zilizoagizwa kutoka nje ya nchi hususan bidhaa za mitaji, na bidhaa za matumizi ya kawaida. 

Katika kipindi cha miezi sita iliyoishia Juni 2016, kikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliotangulia, thamani ya bidhaa na huduma zilizouzwa nje ya nchi ziliongezeka kwa asilimia 14.2 na kufikia dola za Kimarekani milioni 4,473.2 wakati thamani ya bidhaa na huduma toka nje zilipungua kwa asilimia 18.3 na kufikia dola za Kimarekani milioni 5,360.7

Hazina ya fedha za kigeni imeendelea kuwa ya kuridhisha na kuendelea kukidhi mahitaji ya fedha za kigeni kwa ajili ya kuagiza bidhaa na huduma nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na kuongeza imani kwa wawekezaji katika uchumi wetu; japo kumekuwepo na ucheleweshwaji wa fedha za wahisani na mikopo ya kibiashara kutoka nje ya nchi.

 Hadi mwezi June 2016, akiba ya fedha za kigeni ilifikia dola za Kimarekani milioni 3,870.3 ambazo zinatosheleza kuagiza bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi kwa takriban miezi 4. Wakati huo huo, rasilimali za fedha za kigeni za mabenki (gross foreign assets) zilikuwa kiasi cha dola za Kimarekani milioni 835.0

1.8  Deni la Taifa


Deni la Taifa limeendelea kuongezeka na kufikia dola za Kimarekani milioni 20,851 mwishoni mwa mwezi Juni 2016, kutoka dola za Kimarekani milioni 19,861 mwezi Desemba 2015. Deni la nje liliongezeka kwa asilimia 2.6 na kufikia dola za Kimarekani milioni 16,281 mwezi Juni 2016 (sawa na asilimia 77.8 ya deni la taifa), kutoka dola za Kimarekani milioni 15,864 mwezi Desemba 2015. Hii ilitokana na kuongezeka kwa mikopo mipya pamoja na malimbikizo ya malipo ya madeni. 

Katika deni hilo la nje, asilimia 83.4 ni deni la Serikali na taasisi za umma. Pamoja na ongezeko hilo, takwimu zinaonyesha kuwa deni letu bado ni stahimilivu. Kwa mfano, deni la nje kwa thamani ya sasa (Net Present Value) ni karibu ya asilimia 20 ya Pato la Taifa, ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 50 ya Pato la Taifa (Sept-15 DSA). Hii inaonyesha kuwa bado kuna nafasi kubwa ya kukopa bila kuhatarisha ustahimilivu wa deni letu.

Deni la ndani liliongezeka kufikia shilingi bilioni 10,038.4 mwishoni mwa mwezi Juni 2016 kutoka shilingi bilioni 8,597.0 mwezi Desemba 2015.

 Ongezeko hilo lilitokana na Serikali kukopa kupitia dhamana na hati fungani ajili ya kugharamia bajeti ya Serikali kwa mwaka 2015/16, ikichangiwa pia na kupungua kwa misaada na mikopo kutoka nje.

Jedwali Na 2 linaonyesha vyanzo vya fedha za Serikali na matumizi yake katika kipindi cha miezi 6 kuanzia Januari hadi Juni 2016. Kama inavyoonekana jumla ya mapato ya ndani ilikuwa shilingi bilioni 7,267 wakati matumizi ya kawaida (ukiondoa riba) yalikuwa shilingi bilioni 6,488, hivyo mapato yalitosha kulipia matumizi ya kawaida ya Serikali. Hii ni kuonyesha kwamba madeni ya nje na ndani yalitumika kwa ajili ya miradi ya maendeleo pamoja na kurejesha madeni yaliyopita.



Jedwali Na. 2: Vyanzo vya Fedha vya Serikali na Matumizi Yake (Shilingi bilioni)


































































































Waziri Mkuu: Wekeni majina ya mitaa Dodoma Mjini, Chamwino

$
0
0
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameziagiza mamlaka za serikali za mitaa nchini kuweka haraka majina katika barabara na mitaa katika maeneo yao, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi.

Waziri Mkuu pia ameelekeza taasisi za serikali kuzipa kipaumbele kwa Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino katika Mkoa wa Dodoma wakati wa kutekeleza mpango huo.

“Dodoma na Chamwino ndio yawe maeneo ya kipaumbele wakati wa kutelekeza mradi hiyo kwani serikali imeshabainisha nia yake ya kuhamisha mji mkuu wa nchi kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma,” amesisitiza.

Waziri Mkuu Majaliwa ametoa maelekezo hayo jana wakati wa Uzinduzi wa Muongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini hapa pamoja.

Amewataka mawaziri na mamlaka husika kukamilisha kuweka majina ya mitaa na barabara ifikapo Desemba, mwaka huu. Amezitaka taasisi za umma na binafsi, kuweka kipengele cha anwani za makazi ili kutekeleza mpango huo wa maendeleo.

Alizitaja taasisi hizo kuwa ni pamoja na Wakala wa Barabara wa Tanzania (Tanroads), Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) na Mipango Miji na Mradi wa Kuboresha Miji. Alisema mpango huo mpya utaboresha mpangilio wa miji, utasaidia masuala ya ulinzi na usalama, huduma za kijamii na kuboresha mazingira ya biashara na uchumi nchini.

“Itakuwa rahisi kukusanya kodi za serikali kwa sababu itakuwa rahisi kutambua na kufuatilia walipa kodi katika maeneo yao," amesema.

Mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Posta ya Mwaka 2003 na Azimio la Umoja wa Posta Duniani (UPU) lililofikiwa Doha, Qatar mwaka 2012, lililotaka nchi zote duniani kuhakikisha kuwa kila mtu anakuwa na anuani. Kamu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Christine Mndeme alimhakikishia Waziri Mkuu kuwa mamlaka za Dodoma, zimeanza kutekeleza mpango huo wa kuweka anuani katika mitaani na kwenye barabara za mji huo mkuu.

“Mpango wetu Dodoma ni kuipa mitaa na barabara majina ya viongozi waliohai na waliokwishafariki kutokana na mchango wao hapa nchini kama vile Pius Msekwa, Job Lusinde, Hayati Rashid Kawawa na George Kahama,” alisema Mndeme.

Nchini Tanzania mradi wa majaribio, ulianzia Mkoa wa Dar es Salaam na Arusha na baadaye ulifuatia Mkoa wa Dodoma na mpango ni kukamilika Juni, 2018.

Kompyuta zenye majibu ya waliopima ukimwi zaibwa

$
0
0

Kompyuta mpakato zenye majibu ya watu waliopima ukimwi pamoja na majina yao zimeibwa mkoani Tabora.

Kompyuta hizo zipatazo 30 zenye thamani ya Sh70 milioni, zimeibwa kwenye ofisi ya shirika lisilo la kiserikali la Jhpiego linaloshughulika na masuala ya Ukimwi na tohara.

Kompyuta hizo zimeibwa mwishoni mwa wiki kwenye ofisi hiyo iliyo jirani na ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Hamis Issa amesema tayari taarifa za tukio hilo zimewafikia  na wanaendelea na uchunguzi wa kina kufahamu kilichotokea.

Inadaiwa kuwa kompyuta hizo, zina majina ya watu waliopima VVU na majibu yao.

“Kinachotatiza ni kwamba kama majina ya watu wenye virusi yakijulikana itakuwa ni utata mkubwa kwani ofisi hiyo itakuwa imewaweka katika wakati mgumu pasipo wao kupenda,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Mkurugenzi wa Jhipego, Dk Albert Komba amethibitisha kutokea kwa wizi huo.

JK Atoa Ya Moyoni Kuhusu Rais Magufuli Kutokwenda Zambia

$
0
0
Rais mstaafu, Jakaya Kikwete ameunga mkono uamuzi wa Rais John Magufuli kuahirisha safari kwenda nje ya nchi ili kushiriki katika maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera.

Kikwete amesema uamuzi huo ni wa busara kwa kuwa Serikali inatakiwa kufanya juhudi za makusudi kushughulikia tatizo hilo.

Kikwete aliyemtumia salamu za pole Dk Magufuli na waathirika wa tukio hilo, amesema misaada ya haraka na dharura inahitajika ili waathirika waendelee kupata huduma zote muhimu hasa za kibinadamu.

Kiongozi huyo mstaafu ameyasema hayo  katika hafla ya makabidhiano ya nyumba 22 za watumishi wa afya, 10 zikiwa Chalinze, mbili Bagamoyo na nyingine 10 Mafia zilizojengwa na Taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Pwani.

“Ndugu zangu pamoja na leo hii tunakabidhiana nyumba 22 za watumishi wa afya mkoani kwetu, naomba tusimame tuwakumbuke wenzetu waliopoteza maisha katika tetemeko la ardhi huko Bukoba na pia natumia fursa hii kutoa pole kwa waathirika wote na Rais Dk Magufuli,” amesema.

Ameongeza kuwa: “kiukweli amefanya uamuzi wa busara kuahirisha safari yake ili kushiriki katika maafa haya.”

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika Kituo cha Afya Msoga, Chalinze.

Serikali Yabariki Wenye Jinsia Mbili Kuchunguzwa

$
0
0
 
Mamlaka  ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali itakuwa na uwezo na mamlaka ya kuchunguza watu waliozaliwa na jinsi mbili na kubaini jinsi tawala yenye nguvu zaidi. 

Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wa Mwaka 2016, uliopitishwa juzi usiku saa nne bungeni unampa Mkemia Mkuu mamlaka ya kuchunguza na kubaini jinsi ya mtu na kutatua utata kwa mtu atakayekuwa amezaliwa na jinsi mbili.

“Waheshimiwa wabunge naona wengi wenu mnadhani mkemia mkuu kazi yake ni kuchunguza vinasaba kubaini uhalali wa mzazi na mtoto, maana naona wabunge wengi wamelishabikia hilo, lakini katika teknolojia ya vinasaba yanahusu pia utambuzi wa jinsi, watu unakuta wanawake au wanaume wanazaliwa jinsi ya kike na kiume, kwa hiyo tunaangalia jinsi tawala ni ipi ina nguvu,” alisema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

Ummy alikuwa akijibu michango ya wabunge waliochangia wakati wa kujadili Muswada wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu 2016 kabla ya kuupitisha juzi usiku, waliotaka mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu kutoa elimu kwa wananchi juu ya shughuli zake.

Alisema kwa sheria hiyo, sasa mkemia mkuu kupitia maabara yake anaweza kusema jinsi ya kike au ya kiume ndio yenye nguvu, lakini pia kuna suala la kuhakikisha utambuzi wa mwanadamu hasa wakati yanapotokea majanga pamoja na watu wanaosafiri kwa makundi.

Alikubaliana na wabunge kuwa iko haja ya kuwaelimisha wananchi juu ya kazi za maabara ya mkemia mkuu ambao wengi wao wanadhani inafanya kazi hiyo tu ya kubaini vinasaba vya mzazi na mtoto, lakini sasa wafahamu hata waliozaliwa na jinsi mbili wanaweza kutegua utata huo kwa kubaini jinsi tawala au jinsi yenye nguvu zaidi kama ni ya kiume au ya kike.

Alisema Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imekuwepo kihistoria tangu mwaka 1890 na imekuwa chombo cha kiserikali cha uchunguzi cha kikemia wa kimaabara kwa bidhaa mbalimbali na kuongeza kuwa imekuwa ikifanya uchunguzi wa kikemia wa vyakula, dawa na vipodozi hasa pale inapotokea utata au kuhusisha masuala ya kesi za jinai.

Akifafanua zaidi, alisema kwa upande wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wao wanafanya udhibiti wa ubora wa chakula, dawa na vipodozi na maabara hii inafanya uchunguzi wa kikemia.

“Maabara ya Mkemia Mkuu kazi yake ni kufanya uchunguzi wa kikemia, vinasaba, kesi za jinai na sayansi jinai. Chombo hiki hakipimi kudhibiti ila kufanya uchunguzi kwa ajili ya vitu vyenye maslahi ya taifa au masuala yenye utatanishi na ushindanishi,” alisema waziri huyo.

Akitoa mfano wa mahindi, alisema kulikuwa na tatizo la sumu kuvu, kwa hiyo mkemia mkuu anafanya uchunguzi wa kimaabara na kusema wamekuta mahindi yana sumu au la, au anaweza mfanyabiashara kuleta maziwa ya mtoto TFDA ikapata mashaka, mkemia mkuu atayafanya uchunguzi wa maabara atasema kama kuna sumu ama kuna kemikali isiyo salama kwa matumizi wa binadamu.

“Baada ya uchunguzi wa kimaabara mwenye jukumu la kusema mahindi haya yasiuzwe au maziwa haya yasiuzwe ni TFDA na sio maabara ya mkemia mkuu. Vile mfanyabiashara anaweza kuleta bidhaa, TFDA ikaitilia mashaka, kwa hiyo huyu mwenye bidhaa anaweza kukata rufaa kwa mkemia mkuu ili apimiwe bidhaa yake kuithibitishia TFDA kuwa bidhaa yake ni salama,” alisema.

Waziri Ummy alikuwa akijibu hoja za wabunge, ambao walikuwa wana hofu kuwa Maabara ya Mkemia Mkuu inaweza kuingilia kazi za taasisi kama TFDA na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Alizungumzia pia kuhusu kuipa mamlaka ya mwisho maabara hiyo, akisema katika nchi zote duniani zenye maabara hizo, lazima serikali iwe na msemaji wa mwisho wa uchunguzi wa masuala ya kimaabara na kikemia, vinasaba, sayansi jinai na kesi za jinai, lakini pia haifuti sheria wala maabara zingine za uchunguzi zilizoanzishwa kwa mujibu wa sheria mbalimbali.

Kuhusu kutenga bajeti ya kutosha, Ummy alisema serikali imepokea maoni ya wabunge na kuwa baada ya kupitisha muswada huo maabara hiyo imepewa hadhi ya mamlaka na sasa imepewa hadhi na hivyo fungu lake lazima liwe zuri kwa ajili kuendesha shughuli za maabara lakini pia kuajiri watumishi 400 kwani waliopo sasa 192 hawatoshi.

Waziri Ummy alisema wamepokea ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, kufanya uchunguzi wa matumizi ya shisha na kuongeza kuwa tayari mkemia mkuu alifanya uchunguzi na kubaini watumiaji wa shisha wanachanganya bangi, heroine na kokeni na ndio maana serikali ilipiga marufuku kuitumia.

Hata hivyo, alisema sasa itajikita zaidi kuchunguza ili kubaini viambata kiasi gani vilivyopo katika shisha na kwa nini serikali iendelee kupiga marufuku matumizi ya shisha nchini.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images