Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

RIWAYA MPYA: She is My Wife- Sehemu ya 1 & 2

0
0


 Mtunzi : EDDAZARIA G.MSULWA
 Mioyo ya watu wengi wanao jishuhulisha nje ya eneo hili la Benki hii ya kijamii baada ya kundi la wasichana wapatao watano wakiwa na  bunduki zenye uwezo mkubwa wakiwa na kazi moja iliyo wapeleka katika eneo hili ambayo si nyingine zaidi ya kushambulia askari yoyote atakaye jipendekeza katika shuhuli ya uibaji wao wa fedha ambao wameidhamiria kwa siku nyingi na leo ndio hitimisho la mipango yao.Wamejitolea kufa na kupona huku kila mmoja akiwa makini sana na upigaji wake wa risasi zinazo toka kweye unduki zao za kila aina.

Wasichana wawili wakaingia ndani na mkuwalaza chini wahudumu wote wa benki pamoja na wateja ambao wapo ndani ya benk hii na hawakuwa na huruma kwa yoyote aliye inyanyua shingo yake kwa madai ya kuwatazama ni kina nani ambao wanafanya kazi hiyo na ambaye alijaribu kufanya hiyo basi risasi kadhaa kama si mbili basi ni zaidi ya mbili zinatua kwenye mwili wake

Wakamkamata meneja wa benki na kumuamrisha awapekeke kwenye chumba cha kuhifadhia pesa hizo na bwana Turma hakuwa na ubishi zaidi ya kuongoza hadi kwenye chumba wanacho hifadhia pesa pamoja na vito vya dhamani kama madini ya kila aina yenye dhamani kubwa sana katika mauzo yake.

Agnes akashusha mabegi makubwa matatu chini alilokuwa ameyabeba mgongoni na akayafungua na akaanza kazi ya kuviingiza vibunda vya pesa pamoja na vipande vya madini,begi lakwanza likajaa na akahamia kwenye begi jengine na kazi ikawa ndio hiyo hiyo ya kuweka pesa kwenye mabegi hadi mawili yakajaa babisa na jengine likafika nusu
“Anna take it”(ana chukua hilo)

Agnes akamsukumia Anna begi moja ambaye kwa wakati wote alikuwa amaishika bunduki yake kiumakini na kuielekezea kwa bwana Turma.Wakati ndani yakiendelea Alima,Rahab na Fety kazi yao ikwa nikuhakikisha hakuna kiumbe yoyote ambaye anaweza kujipenyeza na kufika katika eneo la nje ya banki.Gari tatu za watu binafi zilizo kuwa zinajaribu kukatisha katika eneo la karibu yao wakijifanya ni vichwa ngumu hawaelewi ni kitu gani kinacho endelea walizishambulia kwa risasi nyingi na kuwaua madereva pamoja na watu walimo ndani ya gari hizo
“R nenda kacheki ndani waambie waache pozi hapa nje hali ishakuwa tete”

    Fety alizungumza huku sura yake akiwa ameiziba na kofia maalumu ambalo limetobolewa sehemu za macho tuu na kofia lake linafanana na wezake wote waliomo ndani huku wakiwa wamevalia majaketi maalumu ya kuzuia risasi kupenya(bullet proof) huku suruali zao zikiwa ni nyeusi zenye mifuko mingi pamoja  na viatu vyeusi vya jeshi.

Rahab akaingia na kumuona askari mmoja akijaribu kunyata akielekea kwenye chumba cha kuhifadhia pesa huku akiwa na bunduki mkononi,Rahab hakufanya masihara zaidi ya kufyatua risasi zipatazo tato zilizo ukatisha uhai wa askari huyo na kumuangusha sakafuni kama mzigo na watu wengine wakavifunika vichwa vyao huku baadhi yao wakishindwa kuzizuia haja zao ndogo

Ikamlazimu Anna kuchungulia baada ya kusikia milio ya bunduki na kumuona Rahab akiwa anamgeuza geuza askari ailiye mpiga risasi kwa kutumia mguu kuhakikisha kama amefariki dunia au laa.

“Oya best fanyeni fasta tuibuke zetu hao machalii huko nje wamesha aanza kubweka kama bweha si munajua tena”
“Ndio tumemaliza njoo unyanyue hii ishu hapa”
Rahab akaingia na kuchukua begi lenye pesa nusu na kuliweka mgongoni na wakatoka wakiwa wameongozana huku kila mmoja akiwa ameishika bunduki yake vizuri
“Simameni juu wote”

Rahab alizungumza na kuwafanya wezake kushtuka
“Wewe unataka kufanya ishu gani tena twende zetu”
“Ngojeni musiwe na papara wanangu huko nje kimesha nuka na tukitoka hivi hatuwezi kufika mbali”

Wakamuacha Rahab afanye anacho taka kukifanya,Rahab akawaamrisha watu wote kuvua nguo zao hakujali kama kuna mkubwa au mdogo,msichana au mvulana wote jukumu lilikwa ni moja.Watu wote wakavua nguo zao zote na kubakiwa kama walivyo zaliwa na wote akawaamuru kufungua milango ya benki na kutoka nje na kukimbia la sivyo wote atawachakaza kwa risasi.

Alima na Fety wakashangaa kuona kundi kubwa la watu wakitoka wakiwa wapo uchi wakikimbia,Rahab,Anna na Agnes wakatoka wakijichanganya kwenye watu hao na Rahab akamrushia begi Fety na akaanza kuwashambulia askari ambao ndio wanasimamisha gari lao ili wapambane nao.

Rahab akaendelea kuwashambulia askari wapatao wanne na kuwafanya wapoteze maisha na wezake tayari walisha ingia ndani ya gari lao aina ya Rage rover,Idadi kubwa ya watu waliomo kwenye eneo hili wakaanza kutawanyika kila mmoja kuyanusuru maisha yake na kama mtu alihisi kama hayapendi maisha yake basi alijikuta akijerushiwa na wasichana hawa wenye roho za kikatili huku wakirusha mabomu ya machozi yapatayo kumi yaliyosababisha moshi mwingi katika eneo hili na watu wengi wakajikuta wakitokwa na machozi pasipo kupenda

Rahab akatupa bunduki yake na kuichomoa bastola yake na kujichanganya kwenye watu wanao kimbia kimbia wakiwa wamechanganyikiwa huku wezake wakiwasha gari lao na kutokomea wasipo pajua.

Dickson fundi maarufu wa baiskel eneo la benki ya biashara iliyo vamiwa na majambazi,naye akawa ni miongoni mwa watu walio jilaza ndani ya kiduka chake huku wakisubiria heka haka za majambazi kutoweka isitoshe moshi wa mabomu ya machozi ukiwaadhiri sana.Akastukia msichana akiingia ndani ya kiduka chake cha na kumuomba hifadhi ya muda,Dickson hakuweza kubisha kutokana na msichana huyo kushika bastola mkononi na kwa haraka akatambua ni miongoni mwa wale majambazi walio ivamia benki

“Ingia humo ndani”
Dickson akamuongoza Rahab kuingia ndani ya kijichumba anacho hifadhia spea mpya za baiskeli anazo ziagizia kutoka Zanzibar.
“Kaka ninakuomba usiseme chochote kwa mtu yoyote sawa”
“Sawa nimekuelewa”

Katika siku ambayo Polisi wanapata shida sana ni siku hii ambayo Benki ya CNB kuvamiwa na majambazi na kushindwa kumkamata jambazi hata mmoja na isitoshe wananchi wamedhalilishwa kwa kutembezwa uchi .Msako mkali ukaanza kufanyika katika jiji la Dar es Salaam na kila gari zinazo kwenda mikoani ni lazima zikaguliwe na kitu ambacho kinawaumiza akili askari ni kutoweza kuwafahamu majambazi hao japo kila wanapo wahoji hoji wahanga wa tukio hilo akiwemo meneja wa Benk ambaye muda wote analia kama mtoto mdogo anadai kuwa majambazi hao ni wasichana tena wanao onekana kuwa na umri wa miaka kati ya 21 hadi 25

“Huko nje vipi polisi wapo bado?”
Rahab alimuuliza Dikson ambaye anakazi ya kuchungulia nje kuangalia ni kitu gani ambacho kinaendelea
“Ndio wapo wanatoa toa maiti za watu walio kufa na kuweka mikanda ile ya njano”
“Ahaa powa”

Rahab akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine na kubakiwa na boxer na kumfanya Dikson kumshangaa jinsi uzuri wa Rahab ulivyo kwani ni mrefu kiasi,sura yake ndogo iliyo jengwa na macho malaini na mazuri ya kuvutia,pua ndogo iliyo chongoka kidogo na unaweza kusema ni jamii ya mabinti warembo wa kisomali,Wembamba wake unavigezo vya kumfanya kuwa miongoni mwa wasichana wanao stahili kugombania umisi Tanzania hata umisi wa Dunia.

Rangi yake ya mwili ya kahawia inazidi kuufanya mwili wake kuwa kivutio kizuri mbele ya macho ya Dikson na kumfanya abaki akiwa amemtizama kwa dakika kadhaa gafla akajikuta akitazamana na mdomo wa bastola iliyo shikwa na Rahab
“Usishangae sana kijana”

Rahab alizungumza huku akiishusha bastola yeke chini na kumafanya Dickson kuirudiasha sura yake kwenye tukio la askari wanaondelea kufanya mahojiano na watu walio kuwepo katika eneo hili.Dickson akamshuhudia bodo boda mmoja wa pikipiki akizungumza na askari wawili ambao akanyoosha kidole chake kilipo kiduka chake akiashiria kuna kitu wakakitazame ndani ya kiduka hiki na taratibu askari wakaanza kupiga hatua za kuelekea kwenye kaduka ka Dikson

“Shiiti polisi wanakuja huku”
“Wapo wangapi?”
“Wawili”
“Wameshika bunduki mkononi”
“Sasa wewe jikaushe na atakaye ingia humu ndani halali yangu”
“Mmm”
Tayari polisi wamesha fika nje ya duka la Dickson na kuanza kulitazama tazama kwa umakini


Rais Magufuli Aahirisha Safari Yake Ya Zambia

0
0


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameahirisha ziara yake  ya siku tatu Nchini Zambia  ambapo pamoja na mambo mengine ilikuwa ahudhurie Sherehe  za kuapishwa kwa Rais Mteule wa Sita wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu, ili aweze kushughulikia tatizo laTetemeko la ardhi lililosababisha vifo vya watu 16, mamia wakiwa wamejeruhiwa na nyumba kadhaa  zimebomoka Mkoania Kagera

Kufuatia kuahirishwa kwa ziara hiyo Mheshimiwa Rais Dkt.Magufuli amemtuma Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Kumuwakilisha katika Sherehe hizo za kuapishwa kwa Rais Mteule wa Sita wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu

Sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule wa Sita wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu zinatarajiwa kufanyika kesho tarehe 13 Septemba, 2016 katika jiji la Lusaka


Jaffar Haniu
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
Dar es salaam


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 12

Basi la JM Luxury Lapata Ajali na Kuua Watu Wanne

0
0
WATU wanne wamekufa huku sita wakijeruhiwa katika ajali ya basi, lililogonga lori katika eneo la njiapanda ya Kolandoto mkoani Mwanza.

Ajali hiyo ilihusisha basi la Kampuni ya JM Luxury kuligonga lori aina TATA, lenye namba za usajiri T218 ABY, la Kampuni ya Birichand lililokuwa likitoka mjini Shinyanga kwenda Kishapu.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, Elias Mwita alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo saa 11 .15 alifajiri jana.

Alieleza kuwa ajali hiyo ilitokana na mwendo kasi wa basi hilo lililokuwa likitoka Shinyanga kwenda Mwanza.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, watu wanne waliokufa walikuwa ndani ya lori, ambalo liligongwa na basi upande wa kulia.


Alisema mbali na kuwa katika mwendo kasi, basi hilo lilitaka kulipita lori hilo ambalo lilikuwa linaanza kukata kona kuelekea wilayani Kishapu, hivyo kuligonga kwenye kichwa na kusababisha vifo hivyo.

Kamanda Mwita hakutaja waliokufa katika ajali hiyo, lakini alisema miili yao imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga.

Majeruhi wamelazwa hospitali hiyo na Hospitali ya Kolandoto. Alitaja majeruhi wanne waliolazwa katika Hospitali ya Kolandoto kuwa ni Salehe Kassim (46) ambaye ni dereva wa basi na Mohamed Ahmed (39) ambaye ni kondakta wa basi.

Abiria waliolazwa ni Valencia Magingi (34) aliyepo Hospitali hiyo ya Kolandoto na waliolazwa Hospitali ya Mkoa ni Joseph Mkunda (58) na Salome Paulo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa, Dk George Herberth alikiri kupokea majeruhi wawili ambao ni Salome Paulo aliyepata majeraha na kuvunjika mguu wa kulia ambaye anaendelea na matibabu huku Joseph Mkunda akipata matibabu na kuruhusiwa kuondoka. Miili ya waliokufa imehifadhiwa hospitalini hapo.

Waziri Mkuu Aongoza Wananchi Kuaga Miili Ya Waliokufa Kwa Tetemeko

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameongoza maelfu ya wananchi wa Manispaa ya Bukoba mjini kuaaga miili ya watu 16 waliofariki kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea  Jumamosi, 10 Septemba, 2016 mkoani Kagera.

Tetemeko hilo imesababisha vifo vya watu 16 na wengine 253 kujeruhiwa. Pia limesababisha maelfu ya wananchi kukosa makazi baada ya nyumba 840 kuanguka na nyingine 1264 zikipata nyufa yakiwemo majengo 44 ya taasisi mbalimbali za umma.

Kufuatia tukio hilo Waziri Mkuu ambaye alimuwakilisha Mheshimiwa Rais, Dk. John Magufuli amewaomba wananchi kuwa watulivu wakati Serikali ikiendelea kufanya tathmini ya athari zilizotokana na maafa hayo.

“Poleni sana tukio hili ni kubwa na halijawahi kutokea nchini. Haya yote ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu. Tuendelee kuwa na imani na watulivu  Serikali ipo pamoja nanyi na haitawatupa mkono,” amesema.

Waziri Mkuu amesema Kamati ya Maafa ambayo ipo katika Ofisi ya Waziri ya Mkuu itakwenda wilaya za Kyerwa, Karagwe na Bukoba mjini kwa ajili ya kufanya tathmini na kubaini athari zilizosababishwa na tetemeko hilo na kuona namna ya kuwasaidia waathirika.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amewaagiza viongozi wa mkoa huo kuchukua hatua za haraka kwa kuwatafutia eneo salama la kulala wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyakato ambayo mabweni yake yote yameathirika na tetemeko hilo na hayafai kutumika.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya kutembelea shule hiyo na kujionea namna mabweni ya shule hiyo yalivyopata nyufa hali iliyosababisha wanafunzi kulala uwanjani.

Pia Waziri Mkuu ameiagiza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuangalia kama kuna tetemeko linguine linaweza kutokea nchini ili Serikali iweze kuchukua tahadhari pamoja na kutoa elimu kwa umma namna ya kujikinga.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu, Salum Kijuu amesema kwa sasa wanaendelea na jukumu la kuwatafutia makazi wananchi ambao nyumba zao zimeanguka. Pia mkoa unaendelea kufanya tathmini ya kina kujua athari zilizosababishwa na tetemeko hilo.

Awali Waziri Mkuu alitembelea Hospitali ya Mkoa wa Kagera ambako majeruhi 170 wamelazwa na kutoa pole na kwamba anawaombea kwa Mwenyezi Mungu wapone haraka na wenye matatizo ambayo yanahitaji matibabu kwenye hoispitali kubwa Serikali itahakikisha wanapelekwa huko na kuhudumiwa.

 IMETOLEWA NA:             
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Pichani kulia ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimuelekeza jambo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salim Mustafa Kijuu ,kabla ya kuanza sala ya pamoja ya kuwaaga na kutoa heshima za mwisho kwa miili ya marehemu,waliokumbwa na tukio la tetemeko la Ardhi
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimuelekeza jambo Mbunge wa jimbo la BUkoba Mjini,Mh Wilfred Lwakatare,kabla ya kuanza sala ya pamoja ya kuwaaga na kutoa heshima za mwisho kwa miili ya marehemu,waliokumbwa na tukio la tetemeko la Ardhi

Watu waamua kulala nje ya nyumba Bukoba baada ya Tetemeko Kutokea kwa Mara ya Pili

0
0
September 10 2016 lilitokea tetemeko la ardhi Kagera kanda ya ziwa Tanzania lenye kipimo cha 5.7 na kusababisha vifo vya watu 16 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa ambapo ndani ya saa 24 baadae (September 11 saa tano kasoro usiku) likatokea tena tetemeko jingine.

Tetemeko hilo la pili ambalo ni dogo halijaripotiwa kusababisha majeruhi au vifo mpaka usiku wa saa nane lakini limeleta hofu kwa wakazi wa Bukoba ambao baadhi wameamua kutoa magodoro nje ya nyumba zao na kulala kwa kuhofia tetemeko linaweza kutokea tena usiku na kuwakuta ndani ya nyumba zao.

Ccm Yatuma Salamu Za Rambirambi Kwa Waathiriwa Wa Tetemeko La Ardhi Kanda Ya Ziwa

0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za janga la tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10/09/2016 katika Mkoa wa Kagera na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mwanza na Shinyanga.

Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za rambi rambi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu kufuatia vifo vilivyotokana na tetemeko hilo.

Katika salamu zake Ndg Kinana amesema Chama cha Mapinduzi kinatoa pole kwa wahanga na kwa familia, ndugu na jamaa waliopoteza wapendwa wao katika janga hilo.

Chama cha Mapinduzi kipo pamoja na wahanga, kushirikiana nao kwa hali na mali katika kipindi hiki kigumu.WanaCCM nchi nzima tunamuomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu pema peponi.

Amina.

Imetolewa na:-
CHRISTOPHER OLE SENDEKA (MNEC)
MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

Tarehe 11/09/2016.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 45 & 46 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

0
0

Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

Ilipoishia...
“nani kachanganyikiwa”
Nilishindwa kuvumilia ikanibudi nizungumze,taratibu nikiwa ninashuka kwenye ngazi na mkononi nikiwa nimeshika bastola na kuwafanya mama na sheila kustuka

Endelea.....
Sheila kwa haraka akarudi nyuma ya mama na kujificha,mama akanitazama kwa macho yaliyo jaa mshangao
“eddy mwanangu unataka kufanya nini?”
“nataka kujua huyu mwanamke kwa nini amesema kuwa mimi nimechanganyikiwa”
“hujachanganyikiwa mwanangu,tulikuwa tunazungumza kuhusiana na baba yako mzee godwin kwamba amechanganyikiwa”

“mama na wewe unashiriki zambi ya uongo?”
“kweli mwanangu,aliniambia kuwa amemuona sehemu fulani katikati ya jiji akiwa anaruka ruka”
Nikamtazama mama kisha nikakaa kwenye sofa na kuiweka bastola pembeni yangu.Sheila akabaki akinitazama huku akiwa hana la kuzungumza.Wote wakaka na kunitazama,ukimya ukatawala ndani ya dakika kadhaa mama akaamua kuuvunja ukimya.

“eddy na hiyo bastola yangu unakwenda nayo wapi?”
“kuna kazi ninataka kwenda kuifanya”
“eddy mwanangu,hembu niambie ni nini tatizo linalo pelekea kuwa na roho kama hiyo kwa maana umerudi hujazungumza na mimi vitu vingi zaidi ya kwenda kulala?”

“mama bado mimi nipo,tutazaungumza kila kitu”
“sawa,ila kwanini ume......”
Nikauona mguu wa rahma ukiukanyaga mguu wa mama na kumfanya asiimalizie sentesi yake.
“kwa nini umekaa huko mbali pasipo kuwa kunijulisha?”
“huyo hajakuambia?”
“yeye atajuaje mtoto wa watu?”
“ahaa mama hiyo mada tutazungumza kesho.Oya ninaomba funguo”
“za nini?”
Sheila alizungumza kwa sauti ya upole na yenye unyeyekevu mkubwa

“funguo za gari na nyumba yako.”
Sheila akafungua pochi yake na kunipa.
“mbona umevaa nguo hizo hizo ulizo kuja nazo?”
Nikajitazama  kuanzia chini hadi juu,nikarudi chumbani kwangu na kuvaa nguo zangu vizuri,nikaichomeka bastola kiunoni mwangu na kuifunika na tisheti nyeusi niliyo ivaa,nikurudi sebleni.

“wewe twende basi home”
Sheila akatazama na mama kisha akanitazama na mimi
“mmmm nitalala na mama”
“hutaki au?”
“eddy muache mwenzako alale hapa,kwani huku kwake unakwenda kufanya nini?”
“kulala”
Nikataka kutoka na mama akaniita

“bastola yangu ipo wapi?”
“nimeirudisha”
“wapi?”
“kwani mama ilikuwa wapi?”
“basi baba nenda salama”
Nikatoka na kuufunga mlango vizuri.Nikasimama pembeni ya dirisha na kusikilizia ni nini mama na sheila watakizungumza,kwa kupitia uwazi ulioachwa na dirisha nikawaona wakikaa kwenye sofa

“mbona mwanangu amebadilika namna hii?”
“mama wee acha tuu,eddy mimi ninampenda ila kwa hapa alipo fikia ninamuogopa mama”
“mmmm usimuogope”
“mama eddy kuna kipindi alipokuwa na hasira mimi nilikuwa nikimtuliza  na kumsogelea,ila sasa hivi mmmmmm ni bora nimtoroke toroke hadi atakapo kaa sawa”

“itabidi nitafute madaktari watakao muhudumia”
“ni kweli mama,yaani mtu anazungumza kwa sauti nzito kama simba dume”
“ila mwanangu huyu anaugonjwa wa asira,mimi wala simshangai sana kwani kuna kipindi akiwa mdogo alisha wahi kumuua mwenzake shule kwa kumpiga na chupa ya soda kichwani”
“weeeee?”

“ooohhh ilikuwa ni kesi kubwa kilicho muokoa ni udogo wake kwa alikuwa na miaka mitano”
“mama ina maana eddy kuua hakuanza leo?”
“eddy mwangu akiwa na hasira si mtu wa kumsogelea,nilisha mpeleka hadi kwa wachungaji wamuombee ila wapii.Nilijaribu kutafuta wana saikology labda wakae nao ila imeshindikana.Kila dawa ambayo niliambiwa inafaa kwa kipindi hicho kuwa kama kitulizo cha ugonjwa wake ila wapi?”

“mmmm”
“yaani na haya matatizo yaliyo tokea hichi kipindi cha hivi karibuni naona pia yanachangia sana”
Nikataka kuondoka niwahi ninapotaka kwenda ila swali la sheila likanifanya nipige hatua kadhaa kurudi dirishani
“kweli mama,hivi mzee godwin yupo wapi?”
“hadi leo sijamuona,mimi mwenyewe ninafanya uchunguzi nije kumuona ila hadi sasa hivi sijapata jibu”


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aongoza Swala Ya Idd El Haji Viwanja Vya Mwembe Yanga Temeke Jijini Dar Es Salaam

0
0


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitoa hutuba katika swala ya Idd El Haji iliyofanyika Viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo asubuhi.
 Swala ikiendelea.
Waziri Mkuu alivyojumuika na waislam wenzake katika swala hiyo.
 Sheikh Abdu Kadri akiongoza swala ya Idd El Haji 
 Sheikh Nurudin Kishki akihutubia baada ya swala hiyo.
 Waumini wa dini ya kiislam wakishiriki swala hiyo.
Waumini wa dini ya kiislam wakiswali.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Chadema yatoa salamu za rambirambi Kwa Waathiriwa Wa Tetemeko La Ardhi Kanda Ya Ziwa

0
0

Chadema kimetoa salaam za pole kwa wananchi wote walioathirika na tetemeko la ardhi katika maeneo ya mikoa ya Kagera, Mwanza, Tabora na kwingine, tukio ambalo limesababisha vifo vya watu 16, majeruhi na uharibifu mkubwa wa mali.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari ya Chama hicho, Tumaini Makene, chama hicho kimetoa wito kwa Watanzania wote katika maeneo yaliyopatwa na tetemeko hilo na wengine kutoka nje ya sehemu hizo, kuguswa na tukio hilo na kuwiwa kuwasaidia waathirika wa tukio hilo katika wakati huu mgumu wa kukabiliana na athari zilizotokana na janga hilo.

Imesema viongozi wa chama katika ngazi mbalimbali, wabunge, madiwani na wanachama wote wa Chadema wataungana na kusaidiana kwa kila hali na wote walioathirika na tukio hilo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Septemba 13

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa awataka watanzania kudumisha amani

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaomba viongozi wa dini zote kutumia nyumba za ibada kuwahamasisha waumini wao umuhimu wa kulinda na kudumisha amani na utulivu uliopo nchini.

Amesema Serikali itahakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa nchini ili Watanzania wawe na uhakika wa kuendelea kufanya kazi zao za kuwaingizia kipato na kuwaletea tija.

Waziri Mkuu ametoa wito huo jana (Jumatatu, Septemba 12, 2016) wakati akizungumza na waumini wa dini ya kiislam mara baada ya kumaliza kuswali sala ya Eid El Haji kwenye viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke Dar es Salaam.

“Serikali itaendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yote nchini. Wito wangu kwa viongozi wa dini msisitize waumini juu ya utunzaji wa amani pamoja na kukemea vitendo viovu ili Taifa lizidi kusonga mbele,” amesema.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amewasisitiza wananchi kuendelea kuwaombea mahujaji waliopo mjini Makka na Madina nchini Saudi Arabia wakiendelea na ibada ya hijja warudi salama.

Pia Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi kuwasaidia kwa hali na mali watu waliokumbwa na tetemeko la ardhi mkoani Kagera ambako jumla ya watu 16 walifariki na wengine 253 kujeruhiwa.

Pia maelfu ya wananchi kukosa makazi baada ya nyumba 840 kuanguka na nyingine 1264 zikipata nyufa yakiwemo majengo 44 ya taasisi mbalimbali za umma

Awali akisoma hutuba ya Eid viwanjani hapo Sheikh Nurdin Kishki alisema dini ya Uislamu ni dini ya amani hivyo amewaomba waislamu kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani yakiwemo mauaji ya watu wasiokuwa na hatia.

Sheikh Kishki amesema ni muhimu watu kulinda amani kwani ikitoweka ni vigumu kuirudisha, alitolea mfano wanachi wa nchi za Libya na Misri ambazo hadi sasa zimeshindwa kuirudisha.

Amesema mtu yeyote anayejihusisha na vitendo vya uwamwagaji wa damu, kudhulumu mali za watu pamoja na kuwavunjia heshima wenzake atakuwa ameangamia, hivyo amewataka Watanzania hususan wakazi wa Temeke kujiepusha navyo.

“Temeke sasa inaongoza kwa matukio ya mauaji, wanaua hadi walinzi. Askari wameuawa bila hatia, jambo hili linasikitisha sana. Watu waliokuwa wanafanya kazi ya kulinda raia na mali zao wanauawa bila ya hatia! Ameongea kwa masikitiko na kuwaomba Watanzania wajiepuszhe na vitendo hivyo.

Katika hatua nyingine Sheikh Kishki ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuonyesha dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo hivyo amewaomba wananchi wawe mstari wa mbele kutoa ushirikiano ili taifa liweze kusomba mbele.

“Ndugu zangu tumepewa heshima kubwa leo kuswali Eid na Mheshimiwa Waziri Mkuu tena amekuja hapa kwenye viwanja hivi vya Mwembe Yanga, hii inaonyesha ukaribu wa viongozi wetu wakuu kwa wananchi wao hususan wa hali ya chini,” amesema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Makamu Wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan Awasili Lusaka Kumwakilisha Rais Dkt. Magufuli Kwenye Sherehe Za Kula Kiapo Rais Wa Zambia Edgar Lungu

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akilakiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Michezo na Maendeleo ya Watoto Mhe. Agnes Musunga mara baada ya kutua  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka, Zambia, leo Jumatatu Septemba 12, 2016  tayari kwa kumuwakilisha Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa rais wa sita wa nchi hiyo Mhe. Edgar Lungu leo Jumanne Septemba 13, 2016 katika uwanja wa Mashujaa jijini Lusaka

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea shada la maua  mara baada ya kutua  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka, Zambia, leo Jumatatu Septemba 12, 2016  tayari kwa kumuwakilisha Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa rais wa sita wa nchi hiyo Mhe. Edgar Lungu leo  Jumanne Septemba 13, 2016 katika uwanja wa Mashujaa jijini Lusaka.

Taarifa rasmi ya serikali kuhusu tetemeko la ardhi mkoani Kagera

0
0

1 Tukio la tetemeko:

Tarehe 10/09/2016 saa 9 na dakika 27 mchana kumetokea tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
 
Kitovu cha tetemeko hilo ni kwenye makutano ya latitudo 10 06’ na longitudo 31055’ eneo ambalo ni kilomita 20 kaskazini mashariki mwa kijiji cha Nsunga na kilomita 42 kaskazini magharibi mwa mji wa Bukoba (Picha Namba 1 na 2). Kitovu hicho kilikuwa kilomita 10 chini ya ardhi kwenye eneo hilo.

Picha Namba 1: Kitovu cha tetemeko la ardhi Kagera (Mduara)
Picha Namba 2: Kitovu cha tetemeko la ardhi Kagera (Nyota nyekundu)
 
Nguvu za mtetemo wa ardhi wa tetemeko hilo ni 5.7 kwa kutumia skeli ya “Richter” ukubwa ambao ni wa juu sana kiasi cha kuleta madhara makubwa. Kutokana na ukubwa huu maeneo mengi ya mkoa wa Kagera ikijumuisha mji wa Bukoba yamepatwa na madhara makubwa sana ikijumuisha nyumba nyingi kupasuka (Picha Namba 3 na 4), watu wengi kujeruhiwa kwa kuangukiwa na vifusi na kuta za nyuma ambapo inakisiwa kuwa watu 13 wamepoteza maisha yao.

Picha namba 3: Nyumba iliyobomolewa na tetemeko la ardhi Bukoba.
Picha namba 4: Nyumba ziliyobomolewa na tetemeko la ardhi Bukoba.
 
2 Sababu za kutokea tetemeko hilo:
Kwa kuwa kitovu cha tetemeko hilo kiko chini sana ya ardhi (Km 10) na kwa kutafasiri umbile la mawimbi ya tetemeko hilo yaliyonakiliwa na vituo vya kupimia matetemeko ya ardhi (Picka Namba 5) inaonekana kuwa tetemeko hilo limetokana na misuguano ya mapange makubwa ya ardhi iliyopasuliwa na mipasuko ya ardhi mithili ya mipasuko kwenye bonde la ufa. Kwa kuwa eneo lililokumbwa na tetemeko la ardhi liko karibu na mkondo wa magharibi wa bonde la ufa la Afrika Mashariki inakisiwa kuwa mtetemo huu umesababishwa na kuteleza na kusiguana ka mapande ya miamba juu ya mipasuko ya ardhi ya bonde hilo la ufa.

Picha Namba 5: Umbile la mawimbi ya tetemeko la ardhi la tarehe 10 Septemba mkoani Kagera.
 
3 Upimaji wa matetemeko ya ardhi.
Mapaka sasa na duniani kote hakuna vifaa au taratibu za kuweza kutabiri utokeaji wa matetemeko ya ardhi. Vifaa vyote na taratibu zote za kuratibu/kupima matetemeko ya ardhi vinapima ukubwa na tabia ya tetemeko baada ya tetemeko kutokea.
 
4 Tafiti za kina.
Wakala wa Jiolojia Tanzania umepeleka wataalamu katika eneo la tukio ili kuendelea kufanya utafiti wa kina juu ya tetemeko hilo. Taarifa zaidi juu ya tukio hili zitaendelea kutolewa kulingana na matokeo ya tafiti hizo pamoja na tafasiri ya taarifa na takwimu za matetemeko ya ardhi zinazonakiliwa na vituo vya kupimia matetemeko ya ardhi nchini hususan kituo cha Geita ambacho ndicho kilicho karibu sana na eneo la tetemeko hili .
 
5 Mambo Muhimu ya Kuzingatia Kuepuka Madhara Yanayoweza Kusababishwa na Tetemeko la Ardhi
i. Kabla ya tukio:
(a) Elimu ya tahadhari inapaswa itolewe ili kila mmoja aelewe nini cha kufanya linapotokea tetemeko la ardhi ikiwa ni pamoja na kupata mafunzo kutoka kwa watu wa msalaba mwekundu kuhusu namna ya kuhudumia majeruhi ama wahanga na pia jeshi la zima moto ili kupata elimu kuhusu namna ya kutumia kizimamoto. Elimu na mafunzo hayo yatasaidia kuwaweka watu katika hali ya tahadhari na hii itasaidia kupunguza taharuki wakati wa tukio kwa vile watakuwa sasa wanajua namna ya kuchukua tahadhari.
(b) Kufanya mazoezi ya kuchukua tahadhari hizo mara kwa mara ili kujizoesha kwani mara nyingi wakati wa matukio ya majanga kama hayo watu huchelewa kuchukua uamuzi wa haraka kujinusuru kwani huwa bado wanajiuliza kwamba wafanye nini. Hivyo mazoezi ya mara kwa mara ya jinsi ya kuchukua tahadhari humfanya mtu kufanya uamuzi wa haraka pindi tukio linapotokea.
(c) Wananchi pia wanashauriwa kujenga nyumba bora na imara kwa kuzingatia viwango halisi vya ujenzi, kuweka misingi imara wakati wa ujenzi, kupata ushauri wa kitaalamu wa aina ya majengo yanayofaa kujengwa katika eneo husika kulingana na ardhi ya mahali hapo, kuepuka ujenzi wa nyumba katika miinuko mikali yenye kuambatana na mawe/ miamba (suspended boulders) na kuepuka ujenzi wa makazi katika maeneo tete yenye mipasuko ya miamba (faults) na uwezekano mkubwa wa kutokea matetemeko.

ii Wakati wa tukio:
(a) Wakati wa tukio la tetemeko la ardhi unashauriwa kukaa mahali salama kama vile sehemu ya wazi isiyo na majengo marefu, miti mirefu na miinuko mikali ya ardhi. Watu wanashauriwa kukaa nje ya nyumba katika sehemu za uwazi.
(b) Endapo tetemeko litakukuta ukiwa ndani ya nyumba unashauriwa ukae chini ya uvungu wa meza imara, ama kusimama kwenye makutano ya kuta na pia ukae mbali na madirisha na makabati ya vitabu, vyombo au fenicha ili kuepuka kuangukiwa na vitu hivyo.
(c) Unashauriwa usitembee umbali mrefu kwa lengo la kutafuta mahali salama kwa sababu tetemeko la ardhi hutokea ghafla na huchukua muda mfupi. Takwimu zinaonesha kwamba watu wanaotaharuki na kukimbia ovyo wakati wa tukio la tetemeko ndio hupata madhara ama kuumia.
(d) Salimisha macho yako kwa kuinamisha kichwa chako wakati wa tukio.
(e) Baki mahali salama hadi hapo mitetemo itakapo malizika na kisha ujikague kuona kama hujaumia na ndipo utoe msaada kwa wengine ambao watakuwa wameumia.
(f) Ondoka mahali ulipo kwa uangalifu kuepuka vitu ambavyo vitakuwa vimedondoka na kuvunjika kwani vinaweza kukudhuru.
(g) Jiandae kwa mitetemo itakayofuata baada ya mtetemo mkuu. Tetemeko kuu huwa mara nyingi linafuatiwa na mitetemo mingi midogo midogo.
(h) Kumbuka kuwa matukio ya matetemeko ya ardhi huweza kuambatana na moto hivyo jihadhari na matukio ya moto kwa vile tetemeko la ardhi linaweza kusababisha kupasuka kwa mabomba ya gesi au kukatika kwa nyaya za umeme ama kuharibika kwa vifaa vinavyotumia umeme na kusababisha hitilafu ya umeme.
(i) Kama uko nje ya jengo wakati tetemeko linatokea unashauriwa kubaki nje, simama mahali pa wazi na uwe mbali na majengo, miti mikubwa, nguzo na nyaya za umeme na ujikinge kichwani kadri inavyowezekana kwani paa za nyumba, miti, nguzo na nyaya za umeme vinaweza kudondoka na kuleta madhara.
(j) Endapo utakuwa unaendesha chombo cha moto wakati wa tukio la tetemeko la ardhi unashauriwa usimame kwa uangalifu sehemu salama na usubiri hadi mitetemo imalizike ndipo uendelee na safari yako kwani tetemeko linaweza kusababisha barabara au madaraja kukatika.
(k) Endapo utakuwa kwenye maeneo ya miinuko au milima uwe mwangalifu ili kuepuka kuporomokewa na mawe au kuangukiwa na miti,
(l) Baada ya mitetemo kumalizika endapo itakulazimu kuondoka mahali ulipo ukiwa katika jengo refu unashauriwa kutumia ngazi badala ya lifti au kipandishi.

iii Baada ya tukio:
(a) Wananchi wanashauriwa baada ya tukio kuzima umeme katika majengo ili kuepuka kutokea kwa hitilafu ya umeme kwani mitetemo huenda ikaendelea tena.
(b) Kukagua majengo kwa uangalifu ili kuhakikisha kama hayakupata madhara kama vile nyufa n.k,na kwamba yanaweza kuendelea kutumika na kama ikibidi basi unashauriwa kuwaita wataalamu wa majengo ili wayafanyie ukaguzi.
(c) Endapo utaangukiwa na vitu vizito usijaribu kutumia nguvu nyingi ili kujinasua kwani hujui vitu hivyo vina uzito kiasi gani, omba msaada kwa kuita kwa sauti lakini usifanye hivyo mara nyingi ili usipoteze nguvu nyingi mwilini maana hujui ni lini utaokolewa,
(d) Toa msaada unaowezekana kwa watu walioathirika na tetemeko na utoe taarifa kwa vyombo vinavyohusika na uokoaji.
 
Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST)
S.L.P. 903
Dodoma
Tanzania
Simu: 0262323020
Tovuti: www.gst.go.tz

Rais Kenyatta, Mbowe watoa msaada kwa waathirika wa Tetemeko la Ardhi Kagera

0
0

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyatta amezungumza kwa njia ya simu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kumpa pole kufuatia vifo vya watu na madhara mengine yaliyotokana na tetemeko la ardhi mkoani Kagera.

Tetemeko lililotokea mkoani Kagera Septemba 10, limesababisha vifo vya watu 16, kuacha watu 253 wakiwa na majeraha mbalimbali ya mwili na nyumba zaidi ya 1000 zikiwa zimebomolewa.

Taarifa kutoka kwa msemaji wa Rais Kenyatta alisema kuwa Rais Kenyatta ameahidi kutoa msaada wa mabati, blanketi na magodoro ili kuwasaidia watu wasio na makazi mkoani Kagera.

Msaada huo utasafirishwa kwa ndege na Jeshi la Kenya Jumanne  hii Septemba 13  hadi mkoani Kagera ambapo ndipo palipopata madhara.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, jana aliwasili mjini Bukoba kuwatembelea waathirika na kutoa mkono wa pole kwa kaya 16 za waliofikwa na misiba kutokana na tetemeko hilo la ardhi.

Mbowe alitoa shilingi milioni 2.1 kwa ajili ya kaya hizo, mifuko 150 ya sementi kwa familia 15 ambazo zimepoteza makazi ambapo kila kaya ilipata mifuko 10.

Mwenyekiti huyo wa Chadema aliambatana na viongozi wengine wa  Chadema mjini humo pamoja na Mbunge wa Bukoba Mjini, Willfredy Rwakatale na Mbunge wa viti maalum (CUF), Saverina Mwijage, walitoa sukari sukari kilo 25 pamoja na mchele kilo 50.

“Ndugu zangu, tukio hili sio la Serikali au chama chochote, ni jambo la kitaifa. Serikali inapaswa kutenga fungu kubwa kwa ajili ya kuisaidia jamii,” Mbowe anakaririwa.

Akiwa katika shule ya Sekondari ya Ihungo iliyobomolewa na tetemeko la ardhi na kusababisha wanafunzi kukosa madarasa ya kusomea, Mbowe ambaye pia alisoma katika shule hiyo alitoa misaada mbalimbali.

Rais John Magufuli alilazimika kuahirisha safari yake ya kuhudhuria kuapishwa kwa Rais wa Zambia, Edgar Lungu kutokana na janga la tetemeko la ardhi, badala yake alimtuma Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kumuwakilisha.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Vitambulisho vya Taifa Kubadilishwa kuanzia Jumatano Septemba 14, 2016

0
0
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inatarajia kubadilisha vitambulisho vyote vya zamani ambavyo havina saini, huku ikitarajia kutoa vitambulisho vipya vyenye saini kwa wananchi wote, waliokamilisha taratibu za usajili na utambuzi kwa kuchukuliwa alama za kibayolojia, ikiwemo alama za vidole, picha na saini ya kielektroniki.

Aidha, inatarajia kutoa vitambulisho vipya kuanzia Septemba 14, mwaka huu katika ofisi zote za Nida za wilaya. 

Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Andrew Massawe, ilisema kwa sasa vitambulisho vya zamani vitaendelea kutumika sambamba na vipya huku taratibu za kuvibadilisha zikiendelea.

‘’Kutokana na uwepo wa njia nyingi na salama za kusoma taarifa za mwombaji zilizomo ndani ya kifaa maalumi kilichofichwa kwenye kadi ya mtumiaji; ndiyo maana vitambulisho vya zamani vitaendelea kutumikakatika huduma mbalimbali zinazohitaji kumtambua mtumiaji kabla ya kupata huduma,’’ alisema Massawe.

Alisema kuwa ofisi za wilaya zilizoanza usajili wa vitambulisho hivyo vipya kwa Tanzania Bara na Zanzibar ni mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro, Tanga, Arusha, Kilimanjaro, Ruvuma na Dodoma.

‘’Waombaji wote ambao vitambulisho vyao viko tayari watatumiwa ujumbe mfupi wa maandishi katika simu zao za mkononi kuwafahamisha kufika vituo vya usajili kuchukua vitambulisho vyao,’’ alisisitiza Massawe.

Alifafanua kuwa wananchi ambao hawakuwahi kusajiliwa na wana umri wa miaka 18 na kuendelea na kwa mikoa ambayo tayari kuna ofisi za usajili, wajitokeze kwa wingi kusajiliwa ili kupata vitambulisho hivyo.

‘’Kwa wale ambao walisajiliwa kupitia Daftari la Kudumu la Mpiga Kura la Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Nida iko mbioni kuanza kutoa nambari za utambulisho wakati taratibu za uzalishaji zikiendelea,’’ alisema.

Pia aliwakumbusha wananchi kutunza vitambulisho vyao ili kuepuka gharama kwani kitambulisho cha awali kilitolewa bure na iwapo kitapotea, ili kupata kingine lazima mtumiaji alipie.

Aliongeza kuwa kwa sasa vitambulisho hivyo vimeanza kutumika katika baadhi ya huduma hususani kwenye benki kwa ajili ya kufungua akaunti na kuthibitisha taarifa za mtu kabla ya kupata huduma.

Mrema Awapongeza Wabunge wa UKAWA Kwa Kukubali Kurudi Bungeni

0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Taifa, Augustine Mrema amewapongeza wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kwa kuamua kuacha kususa kuhudhuria vikao vya Bunge kushinikiza Naibu Spika, Tulia Ackson ajiuzulu au aondolewe kwenye wadhifa huo.

Mgomo huo ulisababisha wabunge wa Ukawa kutoshiriki kwenye Bunge la Bajeti, jambo ambalo limesababisha bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ipitishwe bila wabunge wa upinzani kuijadili na kuchangia mawazo yao bungeni.

Kwa mujibu wa barua yake kwenda kwa Spika wa Bunge Job Ndugai, Mrema ameeleza athari ya mgomo huo wa Ukawa kuwa ni kusababisha bajeti ya serikali ipitishwe kwa mawazo ya upande mmoja wa chama tawala.

Aidha, ilieleza kwamba mawazo ya wananchi kutoka kwenye majimbo yanayoongozwa na wabunge wa Ukawa yalikosekana, hivyo kuwafanya wabunge hao kuwanyima haki wapiga kura wao, kwa kuwakosesha uwakilishi kwenye Bunge la Bajeti.

“Bunge la bajeti ni kikao nyeti kwa vile linajadili na kupitisha mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka husika, ambayo yanamhusu na kumgusa kila mwananchi, hivyo haikuwa busara kwa wabunge wa Ukawa kususa vikao vya Bunge la Bajeti na kuwafanya wapiga kura wao wakose uwakilishi kwenye kikao nyeti kama hicho,” alisema. 

Mrema alisema, kuwepo kwao bungeni kungeweza kusaidia kuboresha bajeti hiyo kutokana na michango yao ya mawazo ambayo wangeyatoa na kupata bajeti bora zaidi kwa manufaa ya taifa.

“Sisemi kwamba bajeti iliyopitishwa ni mbaya, lakini kuwepo kwa wabunge wa upinzani kungesaidia kuboresha ili iwe nzuri zaidi kwa manufaa ya wapigakura wao waliowachagua majimboni mwao,” alisema.

Alisema “Hata kama Naibu Spika alikuwa na kasoro katika utendaji wake wa kazi, lakini Ukawa hawakupaswa kususa vikao vya bunge hilo, badala yake wangetafuta ufumbuzi wa suala kwa kufuata njia za kikatiba na kisheria, ikiwemo kutumia kanuni za Bunge.”

Alisema kwa kususa vikao vya Bunge, Ukawa wamesababisha madhara makubwa kwa wananchi hususani wapigakura wao ambayo hawawezi kulipika na wanaweza wakawaadhibu kwa kosa hilo kwenye Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020, kwa sababu wananchi waliwachagua ili kwenda kuwawakilisha bungeni na si kwenda kususia vikao vya Bunge.

“Sisi TLP tunaona kwamba Ukawa wamedhoofisha upinzani badala ya kuimarisha upinzani kama wenyewe wanavyodai, kwani huwezi kuimarisha upinzani kwa kususia vikao vya Bunge hususani Bunge la Bajeti,” alisema.

Alisema Ukawa wanapaswa kujifunza kwamba kususa vikao si mwarobaini wa kutatua mgogoro ya kisiasa, bali migogoro ya kisiasa hutatuliwa kwa kupitia njia za vikao na mazungumzo. 

Hata hivyo, alisema madhara yaliyopatikana kutokana na mgomo huo hayawezi kulipika kwa sababu Bunge la Bajeti limeshapita na haliwezi kurudiwa.

Serikali Yawaita Wafanyabiashara na Mabalozi kuchangia maafa ya tetemeko la ardhi Kagera

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameongea na Mabalozi na Wawakilishi wa wafanyabishara Ikulu jijini Dar es Salaam kutoa taarifa ya tatemeko la ardhi na maafa yaliyotokana tarehe 10 September 2016. 

Waziri Majaliwa amewaomba wawakilishi hao kutoa misaada mbalimbali ili kuungana na Serikali kuwasaidia walioathirika mkoani Kagera.

Baadhi ya Taasisi na Balozi zilizo ahidi kutoa michango ni:-
Ubalozi wa China – Milioni 100
Ubalozi wa Kuwait – Euro 10,000
Ubalozi wa Kenya- wametoa mabati na malazi
Kampuni ya China Mercharnt Group – Mil 100
Mo Dewji – Milioni 100
Toyota Ltd – Milioni 10
TBL – Milioni 100
Woolworth -Milioni 20
Sahara Tanzania – Milioni 20
Azania Group – Milioni 20
Kagera Sugar -Milioni 100 na Tani 10 za sukari
Nosime Group- Milioni 75
Tanga Cement – Mifuko 1000 ya Saruji
Reginald Mengi – Milioni 110
Protas Ishengoma- Wakili na mhanga wa tetemeko Milioni 5
GBP, MOIL,&OILCOM- Watajenga shule mbili zilizoharibika

Vile vile Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ametangaza matembezi ya kukumbuka janga hilo na kuahidi wananchi wote na mashirika mbalimbali kujitokeza katika matembezi hayo yatakayo fanyika siku ya Jumamosi asubuhi katika maeneo ya Masaki.
 
Taarifa zaidi za Matembezi haya zitatolewa katika vyombo vya habari.

Serikali Yasema Waliosoma shahada za sayansi Watapewa Mafunzo ya Muda Mfupi ya Ualimu ili Kukabiliana na Tatizo la Upungufu wa Walimu

0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, Dodoma

Serikali imeanza kupanga walimu wa sayansi moja kwa moja katika shule badala ya Halmashauri kama ilivyokuwa awali ili kuleta uwiano sawa wa walimu katika shule mbalimbali nchini.
 
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Suleman Jaffo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Muleba Prof. Anna Tibaijuka lililohusu mkakati wa Serikali katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu.
 
Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa Serikali imeandaa mkakati wa kuwaajiri wahitimu wa shahada za sayansi ambazo siyo za ualimu baada ya kuwapa mafunzo ya muda mfupi kuhusu mbinu za ufundishaji na maadili ya ualimu ili kukabiliana na changamoto ya walimu wa sayansi nchini.
 
Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa tayari kibali kimeombwa katika Ofisi ya Rais Utumishi kwa ajili ya utekelezaji huo, ambapo Serikali imepanga kuajiri walimu wastaafu wenye uwezo wa kufundisha waliokuwa wanafundisha masomo ya sayansi kwa mkataba ili kupunguza pengo lililopo.
 
Aidha, Naibu Waziri Jaffo amebainisha kuwa Serikali inafanya tathimini ya mahitaji ya walimu wa masomo ya sanaa kwa kila Halmashauri ili kubaini maeneo yenye ziada na yenye upungufu ili kusawazisha.
 
“Mpango wa Serikali uliopo ni kuwahamasisha walimu wa ziada wa masomo ya sanaa kwenda kufundisha katika shule za msingi ndani ya Halmashauri husika, ambapo kabla ya kuanza utekelezaji wa mabadiliko haya Serikali itatoa waraka maalumu kwenda katika Halmashauri zote nchini” amefafanua Naibu Waziri huyo.
 
Akizungumzia kuhusu utaratibu wa mafunzo ya walimu Mhe. Jaffo amesema kuwa Halmashauri moja haiwezi kuwa na mfumo wa peke yake wa kuandaa walimu hali ambayo iltakuwa ni vigumu kuthibiti ubora wa mafunzo hayo kwa walimu.
 
Hata hivyo amesema kuwa Serikali itaendelea kuongeza udahili wa walimu wa sayansi katika vyuo vya ualimu kadri watakavyojitokeza ili kukidhi mahitaji yaliyopo
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images