Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Profesa Semboja adai Ukubwa wa deni la taifa hauwezi kuyumbisha uchumi

$
0
0

Na: Frank Shija, MAELEZO
Ukubwa wa deni la taifa siyo jambo linaloweza kusababisha kuyumba kwa uchumi wa nchi, kinachooneka ni kuendela kuaminiwa kwa Tanzania ndani na nje ya nchi jambo linalopelekea tuna pata fursa ya kukopesheka kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Mchambuzi wa masuala ya kiuchumi, Profesa Haji Semboja alipofanya mahojiano maalum na mwandishi kutoka Idara ya Habari, MAELEZO kuhusu hali ya uchumi ilivyo kutokana na ongezeko la deni la Taifa leo Jijini Dar es Salaam.

“Ukubwa wa deni la taifa siyo mzigo mbaya, ni mzigo wa kimaendeleo. Unnecessary devil” Alisema Profesa Semboja.

Aliongeza kuwa kutokana kwa imani waliyo nayo wahisani ndani na nje ya nchi ndiyo maana washirika wetu wanatukopesha fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama ambavyo tumeshuhudia ujenzi wa Daraja la Kigamboni, hivi karibuni tutanufaika na usafiri wa ndege”. Alisema Profesa Semboja.

Aidha amempongeza Rais wa Awamu ya Tano Mhe. Dkt. Jonh Pombe Joseph Magufuli kwa hatua alizochukua za kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuondoa safari za nje zisizo za rasmi pamoja na kupiga vita vitendo vya rushwa.

Semboja aliendelea kusema kuwa kinachofanyika hivi sasa ni Serikali ya awamu ya Tano kulipa madeni ya watangulizi wake huku ikitekeleza miradi ya maendeleo jambo linaloongeza imani miongoni mwa wahisani.

Hata hivyo alionya juu ya matumizi mabaya ya rasilimali fedha kuwa zinasababisha kushindwa kutekeleza wajibu wa kulipa deni kwa wakati na kupelekea kulimbikiza madeni jambo ambalo si sahihi.

Alitajaa baadhi ya matumizi mabaya ya fedha kuwa ni pamoja na safari za nje na ndani ya nchi zisizokuwa na tija, ulevi, kupelekea fedha katika miradi isiyopangwa na mengine.

Wananchi wametakiwa kutoyumbishwa na waelewi kuwa kupitia fedha zinazokopwa wanufaika wakuu ni wananchi wenyewe, mfano fedha zitakazo tumika kujenga Nyumba za Magomeni ambazo Mhe. Rais amehaidi waliokuwa wakazi wake kuishi bila kulipia kwa kipindi cha miaka mitano zikitokana na mikopo hiyo wananufaika.

Makamu Wa Rais Atembelea Kituo Cha Kuchakata Gesi .....awataka wafanyakazi kufanya kazi kwa uzalendo

$
0
0
Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewataka wafanyakazi wa kiwanda cha kuchakata gesi asilia kilichopo Madimba mkoani Mtwara wawe wazalendo na wafanye kazi kwa bidii katika kulinda na kuutunza uwekezaji huo mkubwa ambao serikali inautegemea katika uzalishaji wa nishati ya umeme wakati taifa linaelekea kwenye nchi ya viwanda.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wafanyakazi na watendaji wa kiwanda hicho baada ya kutembelea kiwanda kwa mara ya kwanza tangu ashike wadhifa huo kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa kiwandani hapo akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Mtwara.

Amesema kiwanda cha kuchakata gesi asilia ni hazina kubwa  kwa Taifa hivyo ni kikalindwa na kutunzwa ipasavyo kutokana na umuhimu wake katika uzalishaji wa nishati ya umeme kwa maendeleo ya nchi.

Makamu wa Rais pia amewashukuru na kuwapongeza wafanyakazi wa kiwanda hicho cha kuchakata gesi asilia cha Madimba na amewahakikishia kuwa serikali itaendelea kuwajali na kuwathamini katika utendaji wao wa kazi na kwamba serikali itahakikisha wafanyakazi wa kiwanda hicho wanapewa motisha ya kutosha ili waongeze maradufu utendaji wao wa kazi ili malengo ya serikali ya kuleta maendeleo kwa wananchi kupitia viwanda inatimia kwa sababu taifa litakuwa na nishati ya umeme ya uhakika.

Makamu wa Rais amewataka watendaji wa Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC) ambalo linasimamia mradi huo kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kusaidia huduma za jamii katika vijiji vinavyozunguka mradi huo kila mwaka ili wananchi waweze kuwa walinzi wa mitambo hiyo.

Akitoa maelezo mafupi ya mradi huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. James Mdoe amesema kiwanda hicho kina uwezo wa kuchakata gesi ya futi za ujazo milioni 210 kwa siku.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba Mhandisi Leonce namna gesi inavyopokelewa na kuchakatwa na kusafirishwa kwa watumiaji.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiangalia mfumo wa uendeshaji na usalama wa kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba mkoani Mtwara.

Viongozi wa Afrika Mashariki Waigomea Ulaya....Wajipa Miezi Mitatu Kuutafakari Mkataba wa EPA

$
0
0
JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC), imeiomba Jumuiya ya Ulaya (EU), iipe muda wa miezi mitatu kujua hatima ya wao kusaini Mkataba wa Kiuchumi na Jumuia hiyo (EPA).

Uamuzi huo ulifikiwa jana Ikulu Dar es Salaam na viongozi wa Jumuiya hiyo baada ya kikao cha 17 kilichodumu kwa takribani saa sita.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Mwenyekiti wa EAC, Rais John Magufuli alisema kikao hicho kilikuwa na ajenda nne, ila ya EPA ilikuwa ngumu kulingana na uzito wake.

Alitaja ajenda hizo kuwa ni ripoti ya mgogoro wa Burundi, kuingizwa rasmi kwa Sudan Kusini kwene Jumuiya, kupitishwa kwa Naibu Katibu Mkuu wa EAC na EPA.

Rais Magufuli alisema viongozi wote kwa pamoja walikubaliana kupewa muda wa miezi mitatu ili Sekretarieti ya EAC iangalie na kupitia masharti ya EPA kabla ya kusaini ili kila mmoja afaidike.

Hata hivyo nchi ambazo zilishasaini makubaliano hayo kutoka Jumuiya hiyo ni Kenya.

Alisema katika kikao hicho, walibaini mambo 10 ambayo yanapaswa kuangaliwa kabla ya kufikia uamuzi kwa maslahi ya nchi na wananchi.

Mwenyekiti alitaja mambo ya kuangaliwa kuwa ni kwa namna gani nchi za EAC zitafaidika, njia gani itatumika kuzuia bidhaa za kilimo na kulinda wakulima.

Maeneo mengine ni usawa, makusanyo yatokanayo na bidhaa zitakazoingizwa, Burundi itasainije huku ikiwa imewekewa vikwazo na EU, kujitoa kwa Uingereza EU na athari zake, kukosekana kipengele cha kuruhusu nchi zingine kujihusisha na nchi za EAC kibiashara, kukosekana ushuru wa forodha na kipengele cha nchi kujitoa pale inapoona haijaridhika na mkataba.

Rais Magufuli alisema mkataba huo ukisainiwa kwa wakati huu, nchi wanachama zinaweza kuingia kwenye mtego mbaya.

“Tumejadiliana kwa muda mrefu ila mjadala mkubwa ulikuwa suala la EPA ambapo tumekubaliana tupewe miezi mitatu ili tukutane Januari na kutoa uamuzi wa pamoja,” alisema Magufuli.

Alisema Tanzania iko kwenye mkakati wa kujenga viwanda, hivyo ni lazima iwe makini katika kusaini mkataba huo.

Aidha, aliiomba EU kutoiadhibu Kenya kutokana na uamuzi huo kwani nia yao ni nzuri hivyo wapewe nafasi.

Mwenyekiti huyo alisema viongozi wote walikubaliana kuiidhinisha Sudani Kusini kuwa mwanachama wa EAC na Christopher Bazivamo kutoka Rwanda kuwa Naibu Katibu Mkuu Mpya na mapendekezo ya kutatua mgogoro wa Burundi.

Rais Magufuli ateua Makatibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa na Mara

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 09 Septemba, 2016 amemteua Bw. Ado Steven Mapunda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara.


Bw. Ado Steven Mapunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Benedict Richard Ole Kuyan ambaye amestaafu.

Pia, Rais Magufuli amemteua Bw. Tixon Tuliangine Nzunda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa.

Bw. Tixon Tuliangine Nzunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Symthies Emmanuel Pangisa ambaye amestaafu.

Tarehe ya kuapishwa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa walioteuliwa itatangazwa baadaye.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam

09 Septemba, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Septemba 10

Tamko La Waziri Wa Afya, Maendeleo Ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto Kuhusu Watoto Waliomaliza Elimu Ya Msingi Lililotolewa Tarehe 09/09/2016

$
0
0

TAMKO LA MHESHIMIWA UMMY MWALIMU (MB) WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KUHUSU WATOTO WALIOMALIZA ELIMU YA MSINGI LILILOTOLEWA TAREHE 09/09/2016

Ndugu Wanahabari, Nitumie fursa hii kupitia kwenu kuongea na watoto wa Tanzania, wazazi / walezi na jamii kwa ujumla katika kipindi hiki muhimu ambacho watoto wetu wamemaliza Elimu ya Msingi.  Kwa niaba yangu na kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza watoto wote waliomaliza mtihani wa Taifa wa kuhitimu Elimu ya Msingi mwaka huu, Hongereni sana!. Ni jambo la ufahari kwetu sisi wote kama wazazi/ walezi na Taifa kwa ujumla kwani hii ni fursa adhimu kwa ustawi na maendeleo ya mtoto na ni moja ya njia ya kutimizwa kwa haki ya msingi ya mtoto ya kuendelezwa ambayo inamjengea mtoto msingi imara wa maisha yake ya baadae. Pongezi zangu nyingi kwa watoto wote wa kike na wa kiume walioweza kufikia hatua hii muhimu kwa maendeleo na ustawi wao.

Ndugu Wanahabari, Takwimu zinaonyesha kuwa, wanafunzi 795,761 (wavulana 372,883 sawa na asilimia 46.86 na wasichana 422,878 sawa na asilimia 53.14) wamesajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka huu. Hivyo ningependa kutumia fursa hii kuwaasa watoto waliomaliza darasa la saba kutojihusisha na tabia au vitendo vyovyote vinavyo hatarisha afya, usalama na maendeleo yao, kama vile kujihusisha kwenye masuala ya ngono, matumizi ya madawa ya kulevya na vileo katika kipindi hiki cha kusubiri matokeo ya mitihani yao.

 Watoto wetu wa Kike na Kiume wajitambue, na wajue kuwa wao ni hazina ya pekee katika maendeleo ya nchi yetu. Kipindi hiki wakitumie vizuri kwa kuwa waadilifu, waaminifu, wenye bidii na kuzingatia kanuni za nidhamu na tabia njema huku wakijiandaa kwa ajili ya kuendelea na elimu ya Sekondari. Tukumbuke kuwa Serikali imekusudia kumpa kila mtoto nafasi ya kupata elimu ya Sekondari. Msingi tayari umeshawekwa na Rais wa Awamu ya tano, Mheshimiwa John Pombe Magufuli wa kutoa Elimu ya Sekondari bure. Hivyo tusingefurahi mmojawapo kati ya watoto hawa waliomaliza elimu ya msingi jana akaikosa nafasi hii kwa sababu zinazoweza kuzuilika. Nawaasa watoto wote kutumia kipindi hiki kwa kukataa kurubuniwa, kushawishiwa na kujiingiza katika mambo yenye kuhatarisha afya, usalama na maendeleo yao.

Ninawataka Wazazi wenzangu, Walezi na jamii kwa ujumla:-
Kutowaozesha watoto wote wa kike waliohitimu darasa la saba mwaka huu wakati wa kipindi hiki cha kusubiria matokeo yao, iwe ni kwa sababu yoyote ile au kwa lengo la kujipatia mali kwa njia ya mahari. Kila Mzazi/Mlezi anapaswa kutambua umuhimu wa mtoto wake kuendelea kielimu, na kukua kimwili na kiakili kabla ya kuingia katika ndoa. Ieleweke kuwa Elimu ya watoto wa kike ni moja ya njia bora za kupunguza umaskini katika mataifa yanayostawi. Kila mwaka wa elimu kwa mwanamke utaongeza mapato yake ya baadae kwa asilimia 15, ikilinganishwa na asilimia 11 kwa wanaume. Aidha, Kila mwaka wa mtoto wa kike kuwa shule humuepusha na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) mara 7.

Pia, uzoefu unaonyesha kuwa, kila mwaka wa kuelimika humsaidia msichana kufanya maamuzi bora yake na ya familia yake. Benki ya Dunia ilibainisha ya kwamba kila mwaka wa elimu huzuia vifo 2 vya uzazi katika wanawake 1000 kila mwaka!. Kwa hiyo kumpa mtoto wa kike fursa ya elimu inamsaidia sio yeye tu kukua kiakili na kimwili lakini pia inamnusuru na ndoa na mimba za utotoni na kuchangia maendeleo yake, ya familia yake na jamii kwa ujumla. Ni vyema jamii hasa wazazi na walezi wafahamu kuwa ndoa kwa wasichana sio njia muafaka ya kutatua changamoto za kifedha za wazazi/walezi. Bali elimu ndio njia bora ya kutatua changamoto hizo.

Kuwalinda watoto wote wa kike na wa kiume waliohitimu darasa la saba mwaka huu dhidi ya vitendo vyote vya Ukatili, hasa kwa watoto wa kike kupewa mimba au kuwahusisha katika mahusiano ya kimapenzi. Kwa mujibu wa Sheria ya makosa ya kujamiiana ya mwaka 1998 ambayo imefanyiwa marekebisho na kuhuishwa kwenye Makosa ya Jinai (Penal Code Cap 16)  inaelekeza kuwa ni kosa la jinai  kwa mtu yoyote kumlaghai mtoto wa chini ya miaka  18 kwa kumpa mimba au kufanya nae mapenzi.

 Kifungu cha 130 (e) cha Sheria hii kinaeleza wazi kuwa “Ni kosa kwa mtu wa jinsia ya kiume kumbaka msichana au mwanamke; kwa ridhaa au bila ya ridhaa akiwa chini ya umri wa miaka kumi na nane. Mtu yeyote atakayetenda kosa la kubaka atawajibika kwa adhabu ya kifungo cha maisha au kifungo kisichopungua miaka thelathini. Aidha, Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009 Kifungu cha 83 kinaelekeza kuwa ni kosa kumuhusisha mtoto katika kazi, biashara au mahusiano yoyote yenye mlengo wa kingono iwe ni kwa malipo au bila malipo.

Mkono wa Serikali ni mrefu. Tutahakikisha tunawakamata na kuwafikisha Mahakamani wale wote watakao kwenda kinyume na sheria hizi.

Aidha, natoa Rai kwa wananchi wote kuendelea kutoa taarifa kwa mamlaka husika za Serikali za Mtaa, Kijiji, Kata, Wilaya na hata katika Madawati ya Jinsia na Watoto yaliyopo Polisi, pale watakapobaini mzazi au mlezi au taasisi anaenda kinyume na jitihada za serikali za kumuendeleza mtoto kielimu hasa katika kudhibiti ndoa za watoto waliomaliza Elimu ya Msingi hususan katika kipindi hiki cha kusubiri matokeo yao.

Vunja ukimya toa taarifa kwa maendeleo ya watoto wetu.
Nawatakia kila la kheri watoto wote wa Tanzania katika kipindi hiki cha kusubiri matokeo yao ya mtihani wa Elimu ya msingi.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu wabariki watoto wa Tanzania.

Imetolewa na:-
UMMY A. MWALIMU (MB)
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,
WAZEE NA WATOTO
DODOMA
09/09/2016

UKAWA Wapanga Kulifikisha Jeshi la Polisi Mahakama Kuu

$
0
0

Ukawa wamedai wafuasi wake 38 wapo rumande za polisi kwa muda mrefu, huku Chadema ikisema Jumanne ijayo itawasilisha ombi Mahakama Kuu kutaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini aitwe kueleza sababu za kushindwa kuwafikisha watuhumiwa mahakamani.

Jana, Chadema wametoa taarifa kwenye vyombo vya habari wakisema Jeshi la Polisi linawashikilia wanachama wake 10 kwa zaidi ya wiki mbili sasa, wakati CUF ilidai wanachma wake 28 wako kwenye mahabusu za polisi kwa muda mrefu.

Mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu  aliwaambia waandishi wa habari kuwa Jumanne watawasilisha ombi Mahakama Kuu kutaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Ernest Mangu aitwe mahakamani kueleza sababu za kutowafikisha mahakamani watuhumiwa hao.

Lakini, Mkurugenzi wa Upelelelzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athumani amepinga madai ya watu kukamatwa kwa sababu za kisiasa pia alivitaka vyama hivyo kwenda vituo vya polisi kuangalia makosa yaliyotendwa kama yanahusiana na uanachama wa vyama vyao.

Lissu amesema watu hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika mikoa mbalimbali ukiwamo wa Songwe na walisafirishwa hadi Dar es Salaam na kuwekwa mahabusu katika vituo vya polisi Kanda Maalamu ya Dar es Salaam.

“Ikifika Jumanne ijayo kama watu hawa 10 hawatapelekwa mahakamani wala polisi kuwaachia kwa dhamana, tunakwenda  kufungua maombi ya kuwaita IGP au DCI kwa sababu Mahakama Kuu ina mamlaka ya kuamuru mamlaka yoyote ya Serikali inayoshikilia mtu, kumwita mkuu wa mamlaka kueleza kwanini inamshikilia mtuhumiwa kwa muda uliozidi kisheria.

“IGP na wasaidizi wake akiwamo DCI, wataieleza Mahakama Kuu kwanini wanashikilia watu hao kwa muda mrefu. Kati ya watuhumiwa hao, wawili wapo kituo cha Kanda Maalumu (Central Police) na nane wapo Oysterbay,” alisema Lissu.

Wanaodaiwa kushikiliwa Kanda Maalumu waliotajwa na Idara ya Habari ya Chadema ni Ben Nzogu na Mussa Sikabwe wakati wanaodaiwa kuwa Oysterbay ni Aristotle Mgasi, Hosia Mbuba na Ignasia Mzenga,

Wengine ni Mdude Nyangali, Shakira Abdallah Makame, Dk David Nicas, Juma Salum na Suleiman Said.

Lissu, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki alisema wapo katika hatua za mwisho za kuandaa hati ya kupeleka Mahakama Kuu endapo watu hao hawatapewa dhamana na polisi au kupelekwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Lissu, watu hao wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kutoa na kusambaza katika mitandao ya kijamii maneno yasiyomfaa Rais John Magufuli, huku wengine wakituhumiwa kwa kosa la studio yao kutengeneza wimbo wenye uchochezi.

“Hawa ni watu wadogo sana, ndiyo maana wanafanyiwa hivi. Ingetokea kwangu mimi au Mbowe (Freeman), mngeona kesho yake tumepelekwa mahakamani. Jamani mahabusu siyo kuzuri, niulizeni mimi,” amesema Lissu.

Mwanasheria huyo ameongeza, “sheria inasema mtu anatakiwa ashikiliwe na polisi kwa saa 24 na baada ya hapo anapelekwa mahakamani isipokuwa akikamatwa siku zisizo za mahakama, lakini kwao hawa wenzetu ni kinyume na wanazidi kuteseka,” alisema Lissu.

Lissu alidai alikutana na watuhumiwa hao wakiwa katika mahabusu na alielezwa mateso wanayoyapata baada ya kupelekwa sehemu fulani ambayo walikwenda kushughulikiwa na kikosi kazi kinachojumuisha vyombo vya ulinzi.

“Huwa wanachukuliwa kutoka mahabusu usiku na kupelekwa mikocheni kwenye kituo cha mateso. Wanavuliwa nguo na wanapigwa hadi kuvuja damu. Wanawekwa katika vituo vya polisi zaidi ya wiki mbili bila kupelekwa mahakamani kwa sababu tu ya tuhuma.

“Katiba ya nchi, Ibara ya 13, ibara ndogo ya sita inapiga marufuku mtu kuteswa, kudhalilishwa na kuwapa adhabu ya kinyama. Lakini, Tanzania ya leo kuna sehemu imeandaliwa kwa ajili ya kuwatesa watu,” alisema Lissu.

Mbali na watu hao 10, Lissu alisema amepata taarifa zisizo rasmi kuwa watu wengine 73 ambao hawajafahamika kutoka mikoani, nao wanashikiliwa kwa makosa mbalimbali ikiwamo kutoa maoni ambayo hayampendezi kiongozi wa nchi.

“Wakifika hapa Dar, mwenyewe mamlaka ya kuwashughulikia ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa  Makosa ya Jinai (DCI), siyo mkuu wa upelelezi wala kamanda wa mkoa husika.

“Sitaacha kusema ukweli, nitaendelea kusema kutokana na mambo mabaya yanayofanyika katika nchi hii,” alisema Lissu.

Katika hatua nyingine, Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa CUF, Mbarara Maharagande amesema tatizo kama hilo pia linawakabili wanachama wa chama hicho, lakini hawatarudi nyuma kuwapigania.

Amesema Tanzania Bara wapo wanachama 10 kutoka mikoa ya Tanga na Mtwara ambao wanashikiliwa na polisi kwa muda mrefu kwa tuhuma za kisiasa, huku Pemba na Unguja wakiwa 18 wanaotuhumiwa kukata mikarafuu.

“Viongozi wetu wa ngazi husika bado wanapambana na suala hili. Tutahakikisha wanapelekwa mahakamani ili sheria ifuate mkondo wake,” alisema Maharagande.

Akizungumzia madai hayo, DCI Athuman Diwani amesema polisi katika utendaji kazi inaangalia kosa alilolifanya mhalifu na kwamba hawaangalii kilichofanywa na mwanachama wa chama fulani.

Alipoulizwa sababu za kuchelewa kuwapeleka watuhumiwa hao mahakamani, DCI alimtaka Lissu awasiliane na wapelelezi kujua sababu za kuchelewa kwa kuwa kuna sababu nyingi za mtuhumiwa kupelekwa mahakamani.

“Mojawapo ya sababu ni mahojiano yanayoyafanyika kati ya mtuhumiwa na polisi kuhusiana na makosa aliyoyatenda,” alisema.

Mkurugenzi huyo aliongeza,“Lakini nimesikia kuwa wanakwenda mahakamani, waache waende kwa sababu ni haki ya kila Mtanzania,” alisema Athuman.

Hata hivyo, alisema jana kuna watuhumiwa wengi walipelekwa mahakamani, hivyo huenda watu anaowasema Lissu wakawa ni miongoni mwao.

Pia, aliwataka viongozi wa CUF kwenda polisi na kueleza kuwa watu waliokamatwa ni watu wao, ili jeshi hilo liangalie uhusiano wa makosa na uanachama wao.

Kuna Chakula Cha Kutosha Nchini- Waziri Tizeba

$
0
0

Na Beatrice Lyimo- MAELEZO.
Serikali imetoa kauli kuhusu hali ya chakula nchini na kusema kuna chakula cha kutosha pamoja na ziada ya asilimia 123. Ziada hiyo ya chakula inatokana na uzalishaji wa msimu wa mazao mwaka 2015/2016 ambao unapelekea upatikanaji wa chakula kwa mwaka 2016/2017.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba jana mjini Dodoma alipokuwa akitoa kauli ya Serikali kuhusu hali ya chakula nchini.

“Takwimu zinaonesha upatikanaji na mahitaji ya chakula nchini ni wa kuridhisha kwa kiwango cha utoshelevu wa ziada kwa asilimia 123” Dkt. Tizeba.
 
Katika kufafanua hali hiyo, Dkt. Tizeba alisema kuwa kulingana na takwimu zilizopo hali ya upatikanaji na mahitaji ya chakula nchini inautoshelevu wa ziada kwa asilimia 123 ambapo nafaka ni asilimia 113 na mazao yasio ya nafaka ni asilimia 140 ambapo viwango vya ziada kwa mazao yote ya chakula ni tani 3,013,515.
 
Dkt. Tizeba aliongeza kuwa Wakala wa Hifadhi ya Chakula ya Taifa (NFRA) inauwezo wa kuhifadhi jumla ya tani 246,000 ambapo kufikia Septemba 6, ilikuwa na akiba ya tani 67,506.920 za chakula kinachojumuisha mahindi, mpunga na mtama.
 
Pia alisema kuwa Serikali inaendelea na mpango wake wa kuiongezea NFRA uwezo wa kuhifadhi chakula katika kanda sita baada ya kupata mkopo wa dola za Kimarekani million 55 kutoka Serikali ya Poland ambazo zitatumika kujenga vihenge vyenye uwezo wa kihifadhi tani 190,00 na maghala yenye uwezo wa kuhifadhi tani 60,000.
 
Kuhusu muda wa Serikali wa kutoa vibali vya kuuza chakula nje ya nchi, Dkt Tizeba alisema kuwa lengo ni kutoa nafasi kwa Serikali kukamilisha taarifa ya tathimini ya awali ya uzalishaji wa mazao ya chakula kwa mwaka 2015/2016 na hali ya upatikanaji wa chakula kwa mwaka 2016/2017.

Mbali na hayo, Dkt Tizeba alisema kuwa katika kuboresha hali ya usalama wa chakula nchini, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi inapitia upya mfumo wa utoaji wa vibali vya kusafirisha chakula nje ya nchi ili kuwezesha ufuatiliaji wa karibu kuliko ilivyo sasa.
 
Aidha, Dkt. Tizeba alisema kuwa utoaji wa vibali vya kusafirisha mazao nje umejitokeza baada ya kuona chakula kinasafirishwa nje bila kufuata utaratibu maalumu ambapo wafanyabiashara wa nchi jirani walijihusisha kununua vyakula vikiwa bado mashambani kabla ya kuvunwa.
 
Aidha, alitoa wito kwa wananchi kuhifadhi chakula cha kutosha kwa matumizi katika kaya ambapo ameitaka sekta binafsi kuendelea kushiriki katika kutoa masoko ya kununua na kuuza mazao katika maeneo yenye uhaba.
 
Kuhusu hali ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayoikabili dunia ikiwamo upungufu wa mvua , Dkt Tizeba alisema kuwa Serikali itaendelea na juhudi za kuhimiza na kupanua kilimo cha umwagiliaji mashambani kwa kuimarisha miundombinu iliyopo na uvunaji wa maji ya mvua ili kuongeza uzalishaji wa mazao wenye tija. 
 
Hata hivyo, Serikali inaendelea kuhamasisha na kuelimisha wafanya biashara kuuza unga nje ya nchi badala ya mahindi au mchele badala ya mpunga ili kuendana na Sera ya kuendeleza Viwanda nchini na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo.

UKAWA Watibuana Tena na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson

$
0
0

Mvutano umeibuka kati ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson na wasemaji wa kambi ya upinzani walipokuwa wakisoma maoni yao kuhusu miswada iliyowasilishwa bungeni baada ya kusoma utangulizi uliokuwa nje ya hoja.

Katika Bunge la Bajeti lililoisha Juni mwaka huu, upande wa Kambi ya Upinzani Bungeni uliingia kwenye mgogoro na Dk Tulia, hali iliyosababisha wabunge kutoka vyama vinavyounda Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi) kutoka bungeni kila Naibu Spika alipokuwa akiendesha vikao.

Jana, ilikuwa mara ya kwanza tangu wabunge wasusie vikao vinavyoendeshwa na Dk Tulia kukubali kuwapo ndani ya Bunge, hatua iliyotokana na viongozi wa dini kuingilia kati sakata hilo.

Tangu kuanza kwa Mkutano wa Nne wa Bunge la 11, imepitishwa miswada miwili huku wapinzani wakisoma utangulizi wa maoni kueleza jinsi wanavyobanwa kufanya shughuli za siasa.

Hata hivyo, jana ilikuwa ni tofauti baada ya Dk Tulia kuwabana wawasilishaji wa miswada ya Sheria ya Uanzishaji wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, ambao ulisomwa na Dk Godwin Mollel na aliyesoma Muswada wa Uanzishaji Baraza la Watalaaluma wa Kemia ni Ester Matiko.

Katika maoni yao, Matiko na Dk Mollel walieleza jinsi Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanavyowapiga na kuwakamata wananchi wanaojadili masuala ya siasa. Dk Mollel alipinga watu kunyimwa haki ya kutoa maoni, kufanya mikutano ya hadhara na maandamano. “Tupinge unyama unaondelea dhidi ya Watanzania wenzetu,” alisema Dk Mollel.

Hata hivyo, kabla ya kumaliza kile alichokuwa akitaka kusema Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu), Dk Abdallah Posi aliomba mwongozo kwa kutumia kifungu namba 68 (1) akitaka msemaji kujielekeza katika hoja kama kinavyotaka kifungu 86.

Baada ya Dk Tulia kutoa mwongozo wa kutaka kuacha kusoma maneno ya utangulizi huo, Dk Mollel alitii na kuendelea na hoja iliyokuwa mezani. 

Hali ilizidi kuwa mbaya baada ya Matiko kuingia kusoma maoni ya kambi hiyo kuhusu Muswada wa Sheria ya Uanzishwaji wa Baraza la Wanataaluma wa Kemia.

“Watanzania wote wenye mapenzi mema tupinge vyombo vya dola vinavyotumika kufanya shughuli za siasa,” alisema Matiko.

Licha ya Dk Possi kuomba mwongozo wa Spika, Matiko aliendelea kusoma maneno ya utangulizi ambayo aliambiwa asiyasome.

Wakati mvutano huo ukiendelea, baadhi ya wabunge wa upinzani walisimama kupinga uamuzi wa Dk Tulia wakitaka wasemaji hao kuendelea kusoma utangulizi.

Hata hivyo, Dk Tulia aliwataka kukaa chini huku akimtaja Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee kwa zaidi ya mara mbili akimsihi kukaa hali aliyokubaliana nayo.

Rais Magufuli Kuwa wa Mwisho Kuhamia Dodoma

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Rais John Magufuli atakuwa wa mwisho kuhamia Dodoma na kupokewa na watumishi wa Serikali.

Rais Magufuli akihutubia Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM Julai 23 mwaka huu, mkoani hapa alitoa tamko la Serikali kuhamia Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa uamuzi ulitolewa mwaka 1973.

Akizungumza Jumatano wiki hii, katika kipindi cha Safari ya Dodoma kilichoandaliwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Majaliwa alisema utaratibu wa kuhama umepangwa kutekelezwa kwa awamu sita.

Alisema awamu ya kwanza itaanza mwezi huu hadi Februari mwakani, ikiongozwa naye, mawaziri wote, makatibu wakuu, naibu katibu mkuu na idara angalau moja.

“Awamu ya pili itaanza Machi hadi Agosti, 2017. Katika kipindi hicho makatibu wakuu watapendekeza na kuomba fedha bungeni kwa ajili ya kazi hiyo,” alisema.

Kwa utaratibu wa Bunge, mikutano ya bajeti huanza Aprili hadi Julai ili kujadili na kuidhinisha mapato na matumizi ya Serikali ya mwaka mpya wa fedha.

Majaliwa alisema awamu ya tatu itaanza Septemba hadi Februari, 2018 na zitaendelea nyingine, ya mwisho ikiwa mwaka 2020.

Akizungumzia miundombinu, Majaliwa alisema Dodoma ina barabara za kutosha, nyingi zikiwa za lami na hata zisizo za lami zinapitika vizuri.

Majaliwa alisema kuna barabara ya kuunganisha mikoa mingine kama vile Singida, Morogoro na Iringa, hivyo kuwafanya watu kuingia na kutoka mjini hapa kwa urahisi. Kwa upande wa masoko, alisema yapo makubwa yenye vyakula vya kutosha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu), Jenista Mhagama hivi karibuni alisema ujenzi wa makazi, uzio na ofisi binafsi za waziri mkuu umekamilika.

Mhagama alisema kilichobaki ni kazi ya uboreshaji wa mandhari ya eneo la makazi hayo yaliyoko Mlimwa, mjini hapa na barabara za kuunganisha kati ya makazi hayo na nyingine kubwa.

Alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa

Dodoma, Jordan Rugimbana kuhakikisha mandhari ya eneo hilo yanaboreshwa ikiwa ni pamoja na kupanda maua.

Rugimba pia alipewa jukumu la kusimamia ujenzi wa barabara zinazounganisha makazi hayo na nyingine zilizopo maeneo hayo.

Viongozi wa UKAWA Wakutana Faragha Ofisini Kwa Lowassa

$
0
0
Siku moja baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kuwasimanga viongozi wa Ukawa kuhusu namna walivyompokea Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kumteua kuwa mgombea urais, viongozi hao jana walikutana katika kikao kilichotarajiwa kujadili suala hilo.

Kikao hicho cha Ukawa kimekuja zikiwa zimepita siku nne baada ya Lowassa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kukutana nyumbani kwa Lowassa Jumatatu ya wiki hii.

Juzi, katika mahojiano na kituo cha redio cha Clouds FM, Profesa Lipumba alisema mkutano wa chama hicho ulioridhia Lowassa kuingia Ukawa ulifanyika Zanzibar bila yeye kuambiwa, kitendo kinachoonyesha kuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad alikuwa akimzunguka.

Mbali na tuhuma hizo, kiongozi huyo alieleza kuwa hatakuwa tayari kuona CUF ikinunuliwa kwa bei chee na Lowassa au Chadema hata kama atakuwa nje ya chama hicho.

Jana jioni, viongozi wa vyama hivyo walikutana faragha kwenye ofisi za Lowassa zilizopo Mikocheni. Haikuweza kufahamika mara moja ajenda za kikao hicho lakini habari kutoka ndani ya vyama hivyo zilisema pamoja na mambo mengine kilitarajia kujadili shutuma zilizotolewa na Profesa Lipumba.

Suala jingine lililotarajiwa kujadiliwa na viongozi hao washirika wa Ukawa ni mkakati wa pamoja wa namna ya kuendesha shughuli za siasa katika kipindi ambacho imetolewa amri ya kuzuia maandamano na mikutano ya siasa.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria kikao hicho ni mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale-Mwiru aliyewasili saa 10.56 jioni, Mwenyekiti wa Ukuta Profesa Mwesiga Baregu aliyewasili saa 11.06 akafuatiwa na Maalim Seif saa 11.13, na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe saa 11.18 jioni.

Mbali na kikao hicho, viongozi mbalimbali wa CUF, walijitokeza kumjibu Profesa Lipumba aliyejiuzulu uenyekiti katika kipindi cha mapambano ya kukiondoa madarakani chama tawala, CCM, lakini kauli ya pamoja ya viongozi hao ndiyo inasubiriwa kukata mzizi wa fitina.

Juzi, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema Profesa Lipumba ni “kigeugeu” huku Mbowe akisema “hakutegemea maneno hayo yangetoka kwa mtu kama Profesa Lipumba.”

Jana asubuhi akitumia kituo cha Clouds FM, Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano wa CUF, Mbarara Maharagande alisema siyo kweli kwamba Profesa Lipumba hakushirikishwa katika ujio wa Lowassa bali yeye ndiye aliyepeleka taarifa katika Baraza Kuu la chama kwamba Ukawa wamekubaliana kumsimamisha Lowassa.

“Alichokuwa anakifanya Maalim Seif ni haki yake kikatiba kushirikiana na viongozi wengine wa Ukawa. Mbona yeye alikwenda kumfuata Mzee Joseph Warioba kumshawishi agombee urais?” alihoji.

Maharagande alisema CUF walimtazama Lowassa kama sura ya kuleta mabadiliko kwa yale waliyokuwa wakiyataka katika Ukawa. 

“Profesa Lipumba alimtazama Lowassa kama mtu wa kawaida, lakini CUF walimtazama kama kiongozi mwenye ushawishi mkubwa kwa sababu ya uwezo wake wa kuunganisha wanasiasa,” alisema.

Pia, jana mchana Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu alisema Profesa Lipumba ambaye ni msomi ameanguka kifikra kutokana na kauli zake na ukweli uliopo.

Lissu, ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki alitoa kauli hiyo baada ya kuulizwa swali na waaandishi wa habari katika mkutano wake jana waliotaka kujua msimamo wake kutokana na matamshi aliyoyatoa Profesa Lipumba.

“Kwa kifupi ya Profesa Lipumba yasiwasumbue CUF na wala Chadema hayatusumbui. Wanaosumbuka ni wale wanaomtumia Profesa, kwa sababu ukweli uko wazi kutokana na mambo yaliyojitokeza baada ya ujio wa Lowassa,” alisema Lissu.

Alisema katika chaguzi zote ambazo Profesa Lipumba alikuwa akigombea urais, CUF Bara haikuwahi kupata viti vya ubunge zaidi ya viwili lakini mwaka jana kimepata viti 10 kutokana na ushirikiano wa Ukawa.

Lissu aliwahi kumwelezea Lowassa kuwa pamoja na shutuma nyingi anazorushiwa nchini bado ni tembo katika uwanja wa siasa ambaye “ukifumba macho yupo, ukisema hayupo, yupo pale.”

Lowassa kama “jongoo mpenda watu na watu hawampendi” alisababisha zogo kubwa ndani ya CCM wakati wa mchakato wa kuteua mgombea urais na jina lake lilipokatwa aliamua kutulia.

Kutokana na ushawishi mkubwa alionao katika jamii, Chadema walimfuata kumwomba ajiunge nao na akateuliwa kuwa mgombea urais na baadaye alinadiwa kwa vyama vinavyounda Ukawa vya CUF, NCCR-Mageuzi chini ya James Mbatia na NLD chini ya hayati Dk Emmanuel Makaidi.

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Katibu Tawala Songwe na Wakurugenzi wa Halmashauri 13

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Septemba, 2016 amemteua Bw. Eliya Mtinangi Ntandu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa nafasi ya Katibu Tawala Mkoa wa Songwe ilikuwa wazi na uteuzi huu umeanza leo.

Bw. Eliya Mtinangi Ntandu pamoja na Makatibu Tawala walioteuliwa jana tarehe 09 Septemba, 2016 ambao ni Ado Steven Mapunda aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara na Bw. Tixon Tuliangine Nzunda aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa wataapishwa katika tarehe itakayotangazwa baadaye.

Wakati huo huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya 11, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji 1 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa 1 ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi katika Halmashauri hizo.
 
Wakurugenzi walioteuliwa ni kama ifuatavyo;

1.      Godwin Emmanuel Kunambi - Manispaa ya Dodoma
2.      Elias R. Ntiruhungwa             - Mji wa Tarime
3.      Mwantumu Dau                     - Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
4.      Frank Bahati                          - Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe
5.      Hudson Stanley Kamoga        - Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu
6.      Mwailwa Smith Pangani         - Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo
7.      Godfrey Sanga                       - Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama
8.      Yusuf Daudi Semuguruka      - Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
9.      Bakari Kasinyo Mohamed     - Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
10.   Juma Ally Mnwele                 - Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo
11.   Butamo Nuru Ndalahwa       - Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
12.   Waziri Mourice                    - Halmashauri ya Wilaya ya Karatu
13.   Fatma Omar Latu                 - Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo

Wakurugenzi wa halmashauri wote 13 walioteuliwa wanatakiwa kuripoti Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mkoani Dodoma siku ya Jumanne tarehe 13 Septemba, 2016 kwa ajili ya kupata maelekezo zaidi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Septemba, 2016

Tetemeko kubwa la Ardhi laikumba mikoa ya Mwanza na Kagera..

$
0
0

Mchana wa  leo Mikoa ya Kanda imekumbwa na tetemeko la ardhi ambapo nyumba kadhaa zimebomoka na inadaiwa kuna vifo kadhaa


RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 43 & 44 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

Ilipoishia....
Nikapata matumaini ya uwepo wake na moja kwa moja nikaufungua mlango wake na sikuamini macho yangu baada ya kumkuta akiwa ananyonyana denda na mwanaume mwengine ambaye kwa haraka nikamtambua ni derick mume wa madam mery

Endelea...
Sheila akastuka sana kuniona nikiwa nimesimama mbele yao,hata derick ambaye mimi na yeye ni maadui kama paka na paya akakastuka sana na wakaachiana.Macho yangu kwa hataka nikayazungusha katika enoe la chini kutafuta kitu kizuri ambacho ninaweza kupambana nacho ila sikuona.Nikatazama nje nikaona kupande cha mbao kilicho chongonga vizuri na kina unene mkubwa kiasi.

Nikakifwata kwa haraka na kurudi ndani na kumkumba derick ambaye alikuwa anakimbilia kuufunga mlango kwa ndani,akaanguka vibaya na kunipa nafasi ya kuanza kumshambulia kwa haraka.Kwa nguvu zangu zote nikakitulisha kipande cha mbao kwenye magoti yake na kumfanya anguke chini    akitoa ukulele wa maumivu makali.

Sheila akaanza kubabaika kwani siku zote ananijua nikiwa na hasira ninakuwa ziadi ya  mnyama mkali,kwa kutumia kigoti ya mguu wa kulia nikakitulisha kwenye kidevu cha derick na kumfanya arushwe juu kidogo huku meno kadhaa yakidondoka sakafuni
“eddy utamuua.....”
“wewe malaya funga bakuli lako”

Derick akajaribu kurusha teke,nikalidaka huku nikimtazama kwa hasira.Nikamsukuma na akajigonga kwenye kabati lenye tv na redio kubwa.Derick akaanza kutokwa na machozi akijaribu kuniomba msamaha ila sikumuelewa kabisa kwa kitu anacho niambia.

Kwa kutumia gongo nikaanza kumshambulia kwenye miguu yake,nikitumia nguvu zangu zote kuiamiza kwa kipande cha mbao na kuzidi kumpa maumivu derick.Sheila akanidandia mgongoni akijaribu kunizuia,nikageuka na kumshika sheila kichwa chake na kumtazama kwa macho makali.Nikampiga kichwa kichwa cha uso na kumfamya ayumbe kama tiara,nikampiga buti nililo muangushia kwenye sofa na kuanza kulia kwa maumivu kalali.

Nilipo hakikisha miguu ya derick haifanyi kazi yoyote,nikaingia jikoni na kuchukua kishoka cha kukatia nyama chenye makali,kabla sijatoka nikaona kamba ikiwa kwenye mfuko.Nikavichukua kwa pamoja na kutoka sebleni na kumuona derick akijiburuza akijaribu kwenda nje huku akilia.Nikaishika miguu yake na kumburuza hadi alipo sheila,
“eddy mpezi wangu,nakuomba unisamehe....Nisikilize nakuomba”

Sikuwa na haja ya kumsikiliza sheila,nikamshika sheila kichwa chake na nikachukua vipande vya vitambaa vya masofa na kumkandamiza navyo mdomoni na kumfanya ahangaike agaike,nikamfunga kwenye mikono na miguu.Derick wakati wote anakoroma kwa kulia na maumivu.Nikatoka nje na kulifunga geti na kurudi ndani na kuufunga mlango wa kuingilia
“sheila naamini mimi kwako si wakusimuliwa,ninaroho ya binadamu na shetani.....Leo nahitaji unijue mimi ni nani?”

Nilizungumza kwa hasira na sauti nzito iliyo jaa mikwaruzo mingi.Nikamshika derick mkono wake wa kulia,kumbukumbu ya mwanangu alivyompiga chini ikapita kwa haraka kichwani kwangu,nikanyang’ata meno yangu kwa hasira.Nikachukua kishoka na vidole vya derick nikavilaza sakafuni huku nikivikandamiza kwa kutumia mkono wangu wa kushoto
“no...Usinifa.......”

Nishoka kikatua kwenye vidole vyake na kuvitawanyisha kwenye sakafu,dericka akatoa ukulele mkali ila nikamzaba ngumi ya shavu na akabaki akigugumia.Sheila akabaki akiwa ameyatoa macho kama amepigwa mshale wa mgongo.Nikavikunyanya vidole vyake vyote na nikaviweka kwenye meza ya kioo.
“derick leo utakufa kifo cha taratibu kama mwanangu ulivyo mfanya.”

Nikavua tisheti niliyo ivaa,nikaingia jikoni na kuchukua sahani na kurudi nayo ndani sebleni.Nikamfunga derick akamba za miguu,nikamsokomeza vitambaa na yeye kwenye mdomo.Nikauchukua mkono wake wa kushoto ulio na vidole vyake kamili.

Nikamtazama machoni kwa macho ya dharau,kisha nikaupitisha katikati ya miguu yangu na akabaki akinitazama,nikaizungusha miguu yangu na kuusababisha mkono kutoa mlio wa kuvunjika mifupa iliyopo kwenye mkono wake.Dericka akaendelea kulia huku akigaragara chini.Nikaibaeba sahani yenye vidole hadi jikoni,nikaweka kikaangio kwenye jiko la gesi na kuliwasha,nikamimina mafuta mengi ya kula kisha nikavidumbukiza vidole vyote kwenye kikaangio na kuongeza moto ili viive haraka na kurusi sebleni.

Sheila akanitazama huku machozi yakimwagika,mlio wa simu kutoka kweney mfuko wa suruali ya derick ukaanza kusikika.Nikaitoa simu yake ikiita na kukuta ni madam mery ndio anapiga simu kwani imeandikwa ‘wife’ na pembeni kuna picha yake.Nikamtazama sheila na kumfwata,nikamshika nywele za kichwa chake.

“sikia wewe malaya,zungumza na huyu mjinga mwenzako.Jitambulishe kuwa wewe ni mke mwenzake sawa?”
Sheila akatingisha kichwa,simu ikakata na baada ya muda ikaanza kuita tena,nikamtoa sheila vitambaa mdomoni.
“zungumza naye”

Nikaminya kitufe cha kupokea na kuiweka simu iwe kwa sauti kubwa(laudspeker) na kuisikia sauti ya madam mery ikaanza kuzungumza
“haloo mume wangu”
“wewe mshenzi nimekuambia achana na mpenzi wangu.”
“kwani wewe ni nani na namba ya mume wangu umeipataje?”

Mtangazaji wa Clouds Tv ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Wilaya

$
0
0

Leo Septemba 10, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya 11, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji 1 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa 1 ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi katika Halmashauri hizo.


Miongoni mwa Wakurugenzi wa Halmashauri walioteuliwa, yumo pia mtangazaji wa kipindi cha Clouds 360 cha Clouds Tv kinachorushwa kila siku kuanzia jumatatu hadi Ijumaa.

Hudson Stanley Kamoga ameteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara.

Hii sio mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kuteua watangazaji kushika nyadhifa mbalimbali kwani alimteua aliyekuwa Mtangazaji wa ITV, Godwin Gondwe kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni.

Wakurugenzi wengine walioteuliwa leo ni pamoja na;-

  1. Mwailwa Smith Pangani – Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo
  2. Godfrey Sanga – Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama
  3. Yusuf Daudi Semuguruka – Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
  4. Bakari Kasinyo Mohamed – Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
  5. Juma Ally Mnwele – Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo
  6. Butamo Nuru Ndalahwa – Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
  7. Waziri Mourice – Halmashauri ya Wilaya ya Karatu
  8. Fatma Omar Latu    – Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo
  9. Godwin Emmanuel Kunambi – Manispaa ya Dodoma
  10. Elias R. Ntiruhungwa – Mji wa Tarime
  11. Mwantumu Dau – Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
  12. Frank Bahati – Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 11

Rais Magufuli Atuma Salamu Za Rambirambi Na Pole Kagera Kufuatia Watu Kadhaa Kupoteza Maisha Na Nyumba Kubomolewa Kwa Tetemeko La Ardhi

Swala Ya Eid Kuswaliwa Bakwata Makao Makuu Kinondoni Jijini Dar Es Salaam

Makamu wa Rais atoa onyo kwa wanaosafirisha Korosho kwa Magendo

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemaliza ziara yake ya siku NNE mkoani Mtwara kwa kuwahakikishia mamia ya wakazi wa wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara kuwa serikali imetenga zaidi ya bilioni 170 kwa ajili ya utekeleza wa mradi mkubwa wa maji katika wilaya hiyo ili kuondoa tatizo la uhaba wa maji kwa  wananchi wa Tandahimba.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti wakati akihutubia mkutano wa hadhara mjini Tandahimba na wakati amesimamishwa njiani na wananchi wa vijiji vya Kitama I na Kitama II  ambao walitaka kumsalimia akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Tandahimba mkoani Mtwara.

Makamu wa Rais amesema mkakati wa serikali wa sasa unalenga kuhakikisha wananchi wa Tandahimba na wa maeneo mengine nchini wanapata maji safi na salama hali ambayo itaondoa usumbufu wa wananchi kutumia muda mwingi kutafuta maji badala ya kufanya shughuli za maendeleo.

Amesema anaimani kubwa kuwa mradi huo wa maji utakapokamilika wilayani Tandahimba mkoani Mtwara utakuwa ni suluhu ya kudumu ya uhaba wa maji kwa wananchi hao wa Tandahimba.

Kuhusu usafirishaji wa korosho kwa njia ya magendo, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ameonya kuwa serikali kamwe haiwezi kuwavumilia watu wanaofanya vitendo hivyo na watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria ili kukomesha tabia hiyo.

Makamu wa Rais amesema kuwa biashara ya magendo ya korosho inainyima serikali mapato mengi ambayo yangesaidia shughuli za maendeleo za wananchi hivyo ameuagiza uongozi wa mkoa wa Mtwara uchukue hatua za kukomesha biashara hiyo haramu ambavyo ameifananisha na uhujumu uchumi kwa serikali.

Kuhusu ubovu wa barabara kutoka mjini Mtwara hadi wilaya ya Tandahimba, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema serikali itajenga kilomita 50 za awali kwa kiwango cha lami katika barabara hiyo ili kuimarisha shughuli za usafiri na usafirishaji kati ya Mtwara mjini na wilaya ya Tandahimba.

Makamu wa Rais pia ameuagiza uongozi wa mkoa wa Mtwara kukutana haraka na Watendaji wa Wakala wa Barabara wa mkoa wa Mtwara ili kujadiliana kuhusu namna gani ujenzi huo utakavyotekelezwa.

Akiwa mjini Tandahimba, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ameshiriki katika zoezi la utoaji wa zawadi mbalimbali kwa uongozi wa shule ya sekondari ya Tandahimba kwa kuingia katika shule 10 bora kitaifa katika matokeo ya Kidato cha  Sita ambapo Kampuni ya Startimes imetoa hundi ya shilingi milioni Mbili kwajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wilayani humo.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Mtwara.

10-Sep-2016

Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 120

$
0
0
Tetemeko  la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nchini na watu zaidi ya 10 wamekufa na wengine 120 wamejeruhiwa huku majengo mengi yakibomoka.

Mikoa iliyoripotiwa kuathiriwa kwa tetemeko hilo ni Kagera, Mwanza na Mara. Pia tetemeko hilo limeukumba mji wa Kampala na Rakai nchini Uganda jana saa 9.27 alasiri.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi alisema tetemeko hilo limetokea saa tisa alasiri na zaidi ya watu 10 wamekufa.

Awali, akizungumza kwa simu kutoka jiijini Dar es Salaam, Kamanda Ollomi alisema watu wanane walikufa na baadaye alisema idadi hiyo iliongezeka na kwamba alipata taarifa kutoka hospitali ya mkoa kuwa wamepokea miili ya watu 10 na wameihifadhi.

Alisema tisa kati ya waliokufa ni wakazi wa Manispaa ya Bukoba na mmoja ni mkazi wa wilayani Karagwe.

Kamanda alisema miongoni mwa majeruhi wamo wanafunzi 15 wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo na wapo katika hospitali ya mkoa wanaendelea kupatiwa huduma. Alisema bado vikosi vya uokoaji likiwemo Jeshi la Polisi na Zimamoto vinaendelea na uokoaji.

Alisema watu waliojeruhiwa na waliokufa wamedondokewa na kuta, vifusi na vyombo vya ndani.

Alisema wengine walikufa kwa mshituko unaosababishwa na shinikizo la damu na nyumba zaidi ya 40 zimeathirika.

“Ni kweli tetemeko la ardhi limetokea na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali za watu, vifo pamoja na majeruhi na bado tunaendelea kupokea taarifa zaidi,” alisema Kamanda Ollomi na kuongeza kuwa mpaka jana jioni walikuwa wakiendelea kupokea taarifa kutoka sehemu mbalimbali za mkoa huo kuhusu vifo na majeruhi.

Wakala wa Jiolojia waelezea ukubwa wake
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), Profesa Abdulkarim Mruma alisema tetemeko hilo ni kubwa kwa nusu ya kipimo cha juu cha Ritcher10 na limezidi kipimo cha chini cha ukubwa wa Ritcher tatu. Alisema limezidi lililotokea Dodoma hivi karibuni.

Profesa Mruma alisema tetemeko hilo limetokea katika mpaka wa Tanzania na Uganda, kilometa 47 kaskazini mwa Bukoba mkoani Kagera na sababu ni mpasuko wa ardhi katika Bonde la Ufa la magharibi karibu kabisa na Ziwa Victoria .

Amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwani kwa kawaida linapotokea tetemeko kubwa kama hilo hufuatiwa na matetemeko madogo na ardhi hutulia baada ya siku mbili mpaka tatu. 

“Kwa wakati huu ili kuepuka madhara zaidi, litakapotokea watoke nje ya nyumba na kukaa mbali na miti kwenye uwanja wa wazi na wanaoendesha magari waache mara moja,” alisema Profesa Mruma.

Alisema kwa sasa wataalamu katika kituo chao cha kupimia matetemeko cha Geita wanaendelea kupata takwimu zaidi kutokana na kuwa mpasuko wa tetemeko hilo umekuwa karibu sana na ziwa Victoria na baadaye watatoa taarifa kuhusu tukio hilo kwa undani.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images