Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Natural Beauty Product

0
0


NATURAL BEAUTY PRODUCT Ni kampuni inayosifika kwa kutoa bidhaa original  zenye matokeo mazuri na ya haraka zaidi bila kemiko wala madhara  yoyote.  tunazo za:-👇👇👇👇 
1. Kutengeneza shepu hipsi na makalio kwa:- (a) Vidonge maalum @ 150,000/= (b) Dawa ya kunywa au kupaka @  120,000/=
2. Kupunguza au kuongeza maziwa @ 90,000/=
3. Kushepu miguu kuwa (Chupa ya bia)@ 90,000/=
4. Kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @ 100,000/=


5. Kuondoa mipasuko au (Michirizi) @ 90,000/=
6. Kuwa softi na mweupe mwili mzima kwa:- (a)mafuta @ 90,000/= (b) Vidonge @ 150,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima @ 120,000
8. kupunguza tumbo na manyama uzembe kwa:- (a) Mkanda original wa MICRO COMPUTER @ 150,000/= (b) Mkanda wa kawaida au dawa ya kupaka @ 120,000/= (c)  Dawa ya kunywa @ 100,000/=


9. Kuondoa chunusi na madoa sugu @ 90,000/=
10. Kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @ 90,000/=
11. Kuondoa mvi milele na zisiludi tena @ 100,000/=
12. Kuongeza uume na nguvu za kiume kwa:- (a) Gel ya kupaka @ 100,000/=  (b)  Vidonge maalum @ 120,000/= (c)  Mashine original ya HANDSOME UP @ 170,000/=
13. Kuondoa vinyweleo @ 80,000/=


14. kuotesha nywele kwenye kipara @ 100,000/=
15. Kuondoa makovu sehemu yoyote @ 90,000/=
 N.K Kwa mawasiliano  piga simu namba 065 9618585 au 0759029968. Popote ulipo utapata huduma zetu pia bidhaa  zetu zote zinagarantii na risiti ili kuhakikisha mafanikio yako karibu sana.

   Follow follow follow
      👇👇👇
@Natural2162
@Natural2162
@Natural2162
@Natural2162
 
Kwa wateta wa mikoani tunasafilisha kwa njia ya mabasi mzigo unaupata bila tatizo lolote.

Rais Magufuli Azungumzia Tukio la Maalim Seif kukataa mkono wa Rais Shein

0
0
Rais John Magufuli amemshangaa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kwa kuidhinisha fedha za matibabu ya mpinzani wake wa kisiasa, Maalim Seif Sharif Hamad wakati alikataa kumpa mkono wa salamu walipokutana kwenye mazishi wiki mbili zilizopita. 

“Mtu mmekutana kwenye msiba, mahali kwenye majonzi, mnamsindikiza marehemu. Kwa unyenyekevu wako Dk Dhein ukatoa mkono wako kumsalimia mtu fulani. Huyu mtu akakatalia mikono yake na bado asubuhi yake ukasaini fomu zake za kwenda kutibiwa nje ya nchi?” alisema Magufuli. 

“Haya ni mapenzi makubwa sana. Amekataa mkono wako. Huyohuyo akiugua unampeleka hospitali. Akitaka kusafiri nje, unasaini na unampa na fedha na posho za kwenda nje. Mimi nisingeweza.” 

Rais ametoa kauli hiyo jana wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kisiwani Unguja ambako amekwenda kushukuru wananchi kwa kumchagua kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita. 

Visiwani Zanzibar, uchaguzi wa Rais, wawakilishi na madiwani uliingia dosari siku ya mwisho ya kutangaza matokeo. Mwenyekiti wa Tume ya Ucha- guzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani Oktoba 28 mwaka jana, siku ambayo alitarajiwa kutangaza mshindi wa mbio za urais. 

Alifuta wakati matokeo ya majimbo 31 yakiwa yameshatangazwa na kubakia tisa ambayo yalishahakikiwa na kusubiri kutangazwa huku baadhi ya washindi wa viti vya uwakilishi wakiwa wameshatangazwa na kupewa vyeti. 

Jecha alisema kulikuwa na ukiukwaji wa sheria na kanuni za uchaguzi na kutangaza uchaguzi mpya Machi 20, lakini chama kikuu cha upinzani visiwani humo, CUF kikasusia na tangu wakati huo uhusiano baina ya wafuasi wa vyama hivyo umeharibika. 

Uhasama huo ulifikia kiwango cha juu wakati Maalim Seif alipokataa kumpa mkono Dk Shein walipokutana kwenye mazishi ya Rais wa Pili wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi kitendo kilichomfanya Rais Magufuli aeleze yake ya moyoni jana. 

Akishangiliwa na wananchi, ambao wengi walivalia fulana za rangi za njano na kijani ambazo hutumiwa na CCM, Rais Magufuli alisema Dk Shein ni mpole na kama angekuwa na moyo kama wake, hali ingekuwa tofauti baada ya kufanyiwa kitendo hicho cha Maalim Seif. 

“Niutoe mkono wangu, uukatae halafu kesho niende ofisini kukusainia wewe (akaongea kilugha). Ndiyo maana nasema wewe ni special. Nafikiri wanapotoka malaika wewe ndiyo unafuata. Kama mtu anaukataa mkono wako, na wewe kataa kufanya mambo yake, ajifunze kwamba na wewe mkono wako una thamani.” 

Alisema anaomba Mungu amsaidie kumpa angalau nusu ya moyo wa Dk Shein na kuomba Mungu ampe Dk Shein nusu ya roho na mawazo yake ili Zanzibar iende bila kelele za aina yoyote. 

“Jana nilikwambia angalau uongeze kaukali kidogo. Umefanya mambo makubwa sana katika nchi hii. Tulishazungumza na wewe umezungumza kwamba kwa mujibu wa Katiba, uchaguzi umekwisha, ukisharudiwa umekwisha. Utarudiwa tena mwaka 2020, wazunguke waimbe lakini wewe ndiye rais,” alisema. 

Magufuli alisema upendo na unyenyekevu alionao Dk Shein ni wa hali ya juu kwani licha ya mikikimikiki aliyoipata kutoka kwa wapinzani, ameendelea kuwaingiza katika Serikali yake, jambo ambalo yeye hawezi kulifanya. 

“Mimi nilipata ushindi kwa asilimia 58, lakini hakuna mtu kutoka chama kingine atakayekanyaga mguu kwenye Serikali yangu. 

"Mzee huyu ana moyo wa tofauti, namuomba Mungu apate hata robo ya moyo wangu maana amekuwa mpole mno,” alisema Dk Magufuli. 

Rais Magufuli alisema licha ya maendeleo yaliyopo, bado wapo Wazanzibari (hakuwataja majina) wanaokwenda nje ya nchi na kuwazuia wageni na watalii kuacha kutembelea visiwa hivyo. 

“Mwenyeji anakuja na kuwaambia wageni wasije hapa na wao wamempuuza. Bado wageni wanakuja. Ukigombea mwaka wa kwanza ukashindwa, mwingine ukashindwa, mwingine ukashindwa, huwezi kujifunza hata kwenda kuuza nyanya sokoni kwamba biashara hii imekataa kwako,” alisema na kuongeza:

“Kwani hakuna wengine ambao wanakuja? Kuna mtu alitegemea kwamba nitakuwa Rais, hata kuota.Lakini nimekuwa waziri kwa miaka 20 sikujaribu hata siku moja kugombea (urais). 

“Unajua vyeo hivi vinaletwa na Mungu, hata uzunguke namna gani, hata ufuge ndevu namna gani hata unyoe. Kama kasema hapana ni hapana tu, ndiyo maana nasema watu, ni shetani kama sivyo, basi ana moyo wa kishetani na mtu anayefarakanisha mke na mume kwa itikadi za vyama vyao pia ni shetani. 

CUF Wamjibu Rais Magufuli........Wadai Maalim Seif Hawezi Kubembeleza Haki yake ya Kikatiba

0
0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI​
Imetolewa leo Tarehe 4/9/2016​


MWENYEKITI WA CCM, RAIS JOHN MAGUFULI AACHE KUTUMIA MAMLAKA YAKE VIBAYA AHESHIMU MISINGI YA HAKI,DEMOKRASIA, KATIBA NA SHERIA ZA NCHI YETU​
Waheshimiwa wanahabari,
Awali napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru kwa kuitikia wito wetu, nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kutupasha habari mbalimbali zinazohusiana na hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ndani ya nchi yetu na nje ya mipaka yake.
Lakini pia kuwapa pole kutokana na namna mnavyotekeleza majukumu yenu katika mazingira magumu ya hofu na vitisho vinavyofanywa na watendaji wa serikali ya awamu ya tano.
Nitumie fursa hii pia kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza rasmi kuzungumza na vyombo vya habari toka BARAZA KUU LA UONGOZI CUF TAIFA liniamini na kunipa dhamana kubwa ya utendaji na usimamizi wa chama chetu kwa kuniteua kuwa MWENYEKITI WA KAMATI YA UONGOZI WA CHAMA CHETU CHA WANANCHI CUF TAIFA, tukisimamia majukumu yaliyopaswa kufanywa na Mwenyekiti wa Chama Taifa na Makamu Mwenyekiti Taifa.
Naahidi nitatekeleza wajibu wangu kwa uaminifu mkubwa na weledi wa hali ya juu kwa madhumuni ya kuwaletea watanzania mabadiliko sahihi ya maendeleo ya kisiasa na kiuchumi wanayoyataka katika Taifa letu.

Waheshimiwa wanahabari,
Tumewaiteni na kuomba kuzungumza nanyi kwa lengo la kujibu kauli zilizotolewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli alizozitoa juzi na jana (tarehe 2-3/9/2016) katika mikutano ya hadhara aliyoifanya katika kisiwa cha Pemba, uwanja wa Gombani na Unguja katika uwanja demokrasia (Kibandamaiti) na kupitia nyinyi tufikishe ujumbe wetu kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais JOHN MAGUFULI na watanzania kwa ujumla. Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli amezungumza mambo mengi na pia amejikita katika kutoa kauli za dhihaka na mipasho dhidi ya Chama cha Wananchi CUF na katibu mkuu wetu Maalim Seif Sharif Hamad jambo ambalo tunaamini kwa hadhi na heshima ya nafasi yake na hadhi ya taasisi ya urais hakupaswa kufanya hivyo kama kiongozi wa nchi.
Pamoja na masuala mengine Mwenyekiti wa CCM, Rais JOHN MAGUFULI amesema amekwenda kuwashukuru wananchi wa Unguja na Pemba kwa kumchagua yeye pamoja na Dokta Ali Mohamed Shein, amewahahakishia Wazanzibari kuwa atailinda amani ya nchi kwa nguvu zake zote na yeyote atakayejaribu kuivuruga amani atamshughulikia kwa nguvu zake zote bila huruma, ataulinda Muungano kwa nguvu zake zote na lazima uendelee kudumu katika kipindi chote cha utawala wake.
Tatu, amezungumzia maendeleo – Maji, viwanda, miundombinu, uvuvi na kadhalika lakini pia amezungumzia kuitunza amani akitolea mifano ya nchi zisizokuwa na amani ikiwemo Libya, Iraq, Syria, Somalia na mauaji ya kimbali yaliyotokea Rwanda mwaka 1994.
Magufuli amepongeza aliyooiita “kazi nzuri ya majeshi” nadhani kwa kuisaidia kupata ushindi na kuwathibiti wanaotaka mabadiliko na amempongeza Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa ZEC, kwa kufuta uchaguzi wa tarehe 25/10/2016 uliompa ushindi Maalim Seif Sharif Hamad, na kumuombea apewe tuzo kwa kazi nzuri aliyoifanya.
Anashangaa kwanini Dokta Shein ameunda serikali kwa kuvishirikisha vyama vingine wakati alishinda (Shein) kwa asilimia 99 huku akijigamba kuwa yeye kamwe hawezi kuingiza na hataingiza mtu hata mmoja kutoka upinzani katika serikali yake pamoja na kupata ushindi wa asilimia 58 anasahau kuwa hivi karibuni amemteua Mwenyekiti wa TLP Mhe. Agustino Lyatonga Mrema, kuwa Mwenyekiti wa bodi ya PAROLE.

MSIMAMO WA CUF JUU YA KAULI ALIZOZITOA RAIS MAGUFULI:

1. THE CIVIC UNITED FRONT (CUF CHAMA CHA WANANCHI) kimesikitishwa na kauli zisizofaa kwa heshima na hadhi ya taasisi ya urais na nafasi yake kama kiongozi wa nchi kutoka kauli za uchochezi, kupandikiza chuki na uhasama, kuwagawa wananchi na kutaka kujenga chama chake kwa njia ya vitisho na kutumia vyombo vya dola.
Tunamtaka Mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli atambue kuwa hatoweza kujenga umoja wa watanzania kwa kutoa kauli za kuimarisha chuki, uhasama na kutosimamia haki, na kuunga mkono vitendo vya uvunjaji wa demokrasia na sheria za nchi.
Rais Magufuli hawezi kuwa mfano wa kuigwa kwa vizazi vijavyo katika mikakati ya mataifa masikini ya kulinda sheria, haki za kiraia, utawala bora na kuleta maendeleo shirikishi (Inclusive Develeopment).

2. Kauli nyingi za kuchochea chuki na uhasama alizozitoa Rais Magufuli si za kwanza wala si ngeni kwa Wazanzibari. Kisiasa wazanzibar na hasa wafuasi wa CUF (ambao ni wengi) wamekuwa waathirika wakubwa wa matumizi makubwa ya ukandamizaji na unyanyasaji iunaofanywa kikatili sana kupitia MAJESHI, MAZOMBI, JANJAWIDI nakadhalika.
Mauaji yaliyofanywa na Serikali ya CCM chini ya utawala wa serikali ya awamu ya Tatu iliyoongozwa na Benjamini William Mkapa Januari 26-27, 2001 yalisababisha watu 46 kuuliwa na vyombo vya Ulinzi, watu 38 wameuwawa kwa kificho mpaka leo hawajaonekana. Watanzania 658 waliojeruhiwa, na 135 waliopata vilema vya kudumu katika maisha yao.
Aidha zaidi ya wazanzibar 4000 waliishi kama wakimbizi Shimoni, Mombasa nchini Kenya, orodha yao tumeiambatanisha na taarifa hii. Kama kweli Rais Magufuli anataka kulinda amani ya Tanzania haiwezekani kuwa raia wamekuwa wakipigwa na kuteswa na kukatwa viungo vyao na kuporwa mali zao na vikosi vya majeshi, Mazombi na akiwa kimya na kutoa kauli za kubariki vitendo hivyo.
Kwa mtizamo wa Magufuli, ukatili na uhuni unaotendwa na MAZOMBI ukiungwa mkono na vikosi vya majeshi ya SMZ na vile vya Muungano eti ndiyo ulinzi wa amani. Lakini, Kauli mfano wa hizi zimewahi kutolewa na watangulizi wake na viongozi wa Zanzibar waliopita.
Hata hivyo mwisho wa yote hawakuweza kufanikiwa kuwahadaa wazanzibari kudai haki yao na mwaka hadi mwaka wazanzibar wanaotaka mabadiliko wawekuwa wakiongezeka na kuidhihirishia dunia kuwa hawawezi kuvunjwa moyo na vitisho, hujuma na ukandamizaji.

3. Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli amemsifia Dokta Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wazanzibar kwa kura nyingi. Jambo hili linachekesha na kustaajabisha dunia, kwani Hata mtoto mdogo anayeishi Zanzibar au Tanganyika anatambua kuwa Dr. Shein si rais halali wa Zanzibar.
Ni rais aliyeingizwa madarakani kwa kile kinachoweza kuitwa “tyranny of the highest order of the African Power Mongers who are ready to shed blood for power” yaani “udhalimu wa kiwango cha juu kabisa kinachofanywa na viongozi waroho wa madaraka ambao wako tayari kumwaga damu ili watawale”.
Katika uchaguzi halali wa tarehe 25/10/2016. Wazanzibar walimchagua kwa kura nyingi kabisa, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa Rais wao. Wazanzibari wanajua hivyo, Watanzania wanajua hivyo, Waafrika wanajua hivyo na dunia inaimba wimbo huo. Kujidanganya kuwa Dokta Shein ni rais halali wa Zanzibar ni uotaji wa ndoto ya mchana kuwa Tanzania ina viwanda kila kata na kila kijiji, ndoto ambayo kwa aina ya uongozi wa John Magufuli haiwezi kutimia.

TAKWIMU ZA MATOKEO YA UCHAGUZI WA TAREHE 25/10/2015:

Wapiga kura wote wa NEC Zanzibar ni 417,882. Kura alizopata LOWASSA 211,033 = 50.05% kura alizopata MAGUFULI ni 194,317= 46.50% Ushindi wa kura za lowassa dhidi ya Makufuli ni 16,721.

ZEC wapiga kura wote ni 402,354. Kura alipigiwa Maalim Seif ni 207,847 =53.32%. kura alizopata Dokta Ali Mohamed Sheni ni 182,011 =46.68%. Ushindi wa Maalim Seif Sharif Hamad dhidi ya Dk Sheni ni kura 25,836.

Kwa matokea haya ni wazi kuwa Wanzanzibar wameikataa CCM. Wazanzibar hawakuwachagua wagombea wa CCM John Magufuli na DK Shein wake.

4. THE CIVIC UNITED FRONT (CUF CHAMA CHA WANANCHI) kinaendelea na msimamo wake uliotolewa na kikao cha Baraza KUU la uongozi Taifa kilichofanyika tarehe 2-3 April, 2016 wa kutoyatambua matokeo ya uchaguzi huo haramu na batili, na kwa msingi huo halimtambui Dk. Ali Mohamed Shein kuwa Rais wa Zanzibar, haliwatambui waliotangazwa kuwa Wawakilishi na wala haliwatambui waliotangazwa kuwa Madiwani. Baraza Kuu linaungana na wananchi wa Zanzibar waliokataa kuwapa uhalali watu hao na kwa hivyo halitoitambua Serikali, Manispaa na Halmashauri za Wilaya zitakazoundwa na watu hao.
CUF itaendeleza msimamo wake wa kutoshirikiana na Serikali haramu iliyoundwa na dokta Shein kutokana na uchaguzi batili uliofanyika kinyume na Katiba ya Zanzibar, kinyume na Sheria ya Uchaguzi.
Kwa vyovyote vile, Serikali ya dokta Shein haitakidhi matakwa ya Katiba ya Zanzibar na hivyo CUF haitoshiriki kwenye uvunjaji wa Katiba ya nchi.

5. Chama Cha Wananchi CUF, kinaendelea na msimamo wake wa kuutambua uchaguzi mkuu uliokuwa halali, huru, wa haki na uliofanyika katika hali ya amani na utulivu wa tarehe 25 Oktoba, 2015 na pia linayatambua matokeo yake ambayo yanaonyesha wazi kwamba chaguo la Wazanzibari ni CUF na Maalim Seif Sharif Hamad Kitendo cha zaidi ya asilimia 80 ya Wazanzibari kususia uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016 kimezidi kuyapa nguvu maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba, 2015 mbele ya macho ya Watanzania na kwa Jumuiya ya Kimataifa.
Chama cha CUF na Viongozi wake hawawezi kuyumbishwa na watu wenye weledi mdogo sana na siasa za Zanzibar, kama alivyoonesha Rais John Pombe Magufuli. Vitisho vyote vilivyotolewa na Magufuli dhidi ya wanaosimamia HAKI SAWA KWA WOTE na misingi ya kidemokrasia, havitarudisha nyuma juhudi za kuijenga Zanzibari na Tanzania mpya.

6. Tunamtaka Mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli afahamu kuwa stahiki zote anazopewa Maalim Seif zipo kisheria kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama wanavyopewa viongozi wastaafu wengine hapa nchini.
Stahiki hizo si hisani inayotoka mfukoni mwa kiongozi yeyote Yule. Wala si fedha za CCM, ni fedha za watanzania zinazotokana na makusanyo ya kodi zinazolipwa na wananchi.
Sheria ya Mafao ya Viongozi wastaafu wa Kisiasa ya Zanzibar (The Political Leaders Retirement Benefits Act) namba 6 ya mwaka 1999 iliyopitishwa na Dr. Salmin Amour tarehe 15 Mei 2000) imeeleza wazi kuwa viongozi wote wa kisiasa waliohudumu katika serikali ya Zanzibar kuanzia mwaka 1995 kwenda mbele watakuwa na haki isiyoondolewa kwa namna yoyote, ya kupokea stahiki zote muhimu kama viongozi wastaafu.
Rais Magufuli amekuwa rais wa kwanza Tanzania mwenye kutoa kauli zenye ukakasi kwa jamii, zenye kugongana na tabia ya kufanya maamuzi bila kuangalia katiba na sheria za nchi. kwake yeye urais siyo taasisi, ni mtu, kwa Magufuli urais ni ubabe, dhuluma, vitisho, kukandamiza na kutojali katiba na sheria za nchi.
Huenda Taifa letu limepata janga kubwa la kitaifa katika awamu hii ya uongozi wa nchi. Ni jambo la aibu sana kuona rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavunja sheria za nchi yake na anamhamasisha rais wa Zanzibar afanye kama anavyofanya yeye.

7. Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli anazungumzia kulinda amani bila kuzungumzia kulinda haki. Na wakati huo huo anachochea matumizi makubwa ya kijeshi yasiyozingatia sheria kwa wananchi. Mifano aliyoitoa ya nchi zilizoingia katika uvunjifu wa amani haina uhusiano kabisa na masuala yanayoendelea katika nchi yetu.
Rais Magufuli anasahau kuwa nchi hizo anazozitolea mifano, ziliharibiwa kwa sababu ya kuwa na viongozi walioamini katika nguvu za kijeshi (kama yeye) kuliko uongozi wa kidemokrasia na wa kufuata sheria. Raia wa nchi hizo anazozitaja Magufuli walinyimwa haki za msingi za muda mrefu na watawala ndipo wananchi walipoanzisha harakati za kujikomboa, majeshi yaliyoziunga mkono hayakuweza kuzima nguvu ya mabadiliko.
Ni jambo lisilokubalika hata kidogo kuwa na rais ambaye kila kukicha mahubiri yake ni namna gani “majeshi yake yatawashughulikia raia wa nchi yake”.
Hizi ni hotuba zinazowafanya wananchi wajiandae kisaikolojia kupambana na majeshi yao. Watanzania hawakumchagua Magufuli ili ayaandae majeshi kwa ajili hiyo, alikabidhiwa nchi hii ikiwa na amani na CUF haitakuwa tayari kumuona anaiingiza katika migawanyiko, vitisho na visasi ambavyo vinaweza kuzaa machafuko.

8. Kitendo cha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar –ZEC (Jecha SALIM Jecha) kuhudhuria na kushiriki katika mkutano wa CCM uliofanyika Unguja ni ushahidi tosha kuwa tume ya uchaguzi ya ZEC si chombo kilicho huru na kwamba tume hiyo ipo hapo kuhakikisha kuwa Serikali ya CCM haiondolewi madarakani na wananchi wanaotaka mabadiliko ya uongozi wa kisiasa nchini na kwamba ZEC ni tawi la CCM linalotekeleza matakwa yao.
Kwa msingi huo huo, CUF na vyama vingine ambavyo vinapigania mabadiliko hapa Tanzania vitaendeleza mipango imara ya kupigania kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi Zanzibar na Tanzania Bara (NEC na ZEC).
Ni jambo lisilokubalika hata kidogo kujisifia ushindi wa kupora katika uchaguzi kutokana na kupendelewa na Tume ya Uchaguzi ikishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama.

9. Tunamtaka Mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli atambue kuwa; CUF ni taasisi kubwa ya kisiasa nchini iliyo na wawakilishi wa kuchaguliwa na wananchi kutoka kila kona ya nchi yetu, CUF ina wabunge 18 kutoka Pemba, inawabunge wanne (4) kutoka unguja, inawabunge 10 kutoka Tanzania bara.
CUF ni chama cha kitaifa kweli, na tangu mwaka 1995 mpaka sasa CCM haijawahi kupata kiti hata kimoja cha uwakilishi toka Pemba. Magufuli asaidiwe na chama chake, kwamba matamanio yake ya kuifanya Tanzania iwe nchi ya mapambano ya kijeshi na raia hayatafikiwa.
Akumbushwe kuwa kauli zake zimejaa uchochezi wa kila namna anajaribu kuwaghadhibisha wananchi (Provoke), ghilba za kisiasa za waziwazi na nia ovu iliyojaa visasi. Kauli za namna hii akiendelea kuzitoa katika kipindi cha miaka yake mitano, ataimaliza huku kila mtanzania akijiridhisha kuwa nchi ilipata rais ambaye hakujua nini maana ya urais, na kwa vyovyote vile hakuwatendea haki waliomchagua.

Mwisho:

Sote tunatambua kuwa Serikali ya CCM kwa kumtumia Mwenyekiti wake, Rais John Magufuli imeshindwa katika ulingo wa kisiasa kwa kushindana kwa hoja, imekosa uvumilivu wa kisiasa na badala yake inaendesha nchi kwa mfumo wa mabavu bila kuzingatia sheria, haki na wajibu, taratibu na kanuni. Hebu tujiulize, ni nchi gani duniani ambayo ilishinda NGUVU YA UMMA INAYOTAKA MABADILIKO?

Madhumuni ya harakati za kupigania uhuru wa nchi yetu miaka ya 1953-1961 yalikuwa na lengo la kutuondoa watanganyika kutoka katika utumwa, unyonyaji, unyanyasaji, ukandamizaji, ubepari na ubeberu wa rasilimali za Taifa letu na watu wake. Jeshi la mkoloni lilikuwa likitumika kuwadhalilisha wazee wetu.
Leo hii baada ya miaka 55 ya kujitawala, tukiwa ndani ya mfumo halali wa kisheria wa demokrasia ya vyama vingi nchini, serikali ya CCM kwa kumtumia Rais John Magufuli inaturudisha nyuma na kufanya vitendo vibaya zaidi kwa raia wake kuliko ilivyokuwa ikifanywa na wakoloni! Cha kusikitisha takwimu hazionyeshi jeshi la polisi lilipotumia nguvu kubwa kupambana na raia kisha raia wakafungua mashtaka mahakamani, Serikali (Jeshi la polisi) ni lini lilishinda kesi hizo. Mauaji ya mwandishi David Mwangosi ni ushahidi wa hili na kesi nyingine nyingi orodha ni ndefu ambazo zikifikishwa mahakamani haki inaangukia kwa walioshtakiwa?
Tunamtaka Rais Magufuli atambue kuwa kamwe hatoweza kuzuia nguvu kubwa ya watanzania iliyo tayari kuleta HAKI SAWA KWA WOTE na mabadiliko sahihi ya kisiasa, kiuchumi, kijamii, na kuboresha hali za maisha na kipato cha mtanzania kwa kutumia vyema rasilimali za nchi yetu. Tuna kila sababu ya kuunganisha nguvu zetu kama watanzania kumzuia Rais kwa njia ya amani asiendelee kuikanyaga katiba ya nchi aliyoapa kuilinda.
Tunahitaji Taifa letu liwe salama na hatuhitaji kwa namna yeyote ile uvunjwaji wa sheria na matumizi ya nguvu kubwa za vyombo vya dola yanayoandaliwa na rais mwenyewe ili yafanywe dhidi ya wananchi wadai demokrasia.

THE CIVIC UNITED FRONT (CUF- Chama Cha Wananchi) Kinawataka watanzania wote bila ya kujali itikadi za vyama vyetu kusimama imara kutetea misingi ya uongozi wa Taifa letu kwa kuilinda na kuihifadhi katiba na sheria za nchi yetu na kuhakikisha zinaheshimiwa, zinafuatwa na kuhifadhiwa na kila mmoja wetu.

THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-Chama Cha Wananchi) tunawahakikishia watanzania wote kuwa daima tutaendelea kusimama imara na kuwaunganisha watanzania wote ili kuimarisha umoja na mashirikiano baina yetu ya KUDAI HAKI SAWA KWA WOTE NA DEMOKRASIA YA KWELI kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

HAKI SAWA KWA WOTE
___________________________

JULIUS MTATIRO
MWENYEKITI KAMATI YA UONGOZI CUF -TAIFA
juliusmtatiro@yahoo.com

Mawasiliano:

Salim Bimani - 0777414112
Mkurugenzi habari, uenezi na mahusiano na ummah

Mbarala Maharagande
Naibu Mkurugenzi

maharagande@gmail.com
0784 001 408

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 37 & 38 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

0
0
Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

Ilipoishia...
Roho ya huruma ikaniingia na kujikuta nikianza kukimbia na kuwakumba watu waliopo mbele yangu na kujikuta nikisimama gafla huku macho ni kiwa nimeyatoa kiasi kwamba hasira ikazi kunipanda hii ni baada ya kumkuta ni mama yangu ndio anaye pigwa na askari hawa wanao onekana hawana huruma kabiasa wa watumwa walipo ndani ya hili pango.

Endelea....
Nikajirusha juu ya mwili wa mama yangua na kumkumbatia kitendo kilicho zidisha hasira ya askari hawa na wakaanza kunishambulia mimi kwa kunipiga,sikaanza kusikia uzito mwengine ukija juu yangu na nikagundua kuwa watumwa wengine wamepatawa na roho ya huruma na wao mwaneamua kufanya kama nilivyo fanya mimi na kwa umoja wetu ikawalazimu askari kusitisha zoezi lao la kutupiga.

Wakatuamuru tuweze kurudi kwenye kazi za kuvunja miamba,nikamnyanyua mama taratibu huku uso wake ukiwa umejawa na damu zilizo changanyikana na machozi mengi.Nikamshika mama huku akiwa hatambui ni nani aliye mshika na kabla sijamsemesha kitu cha ina yoyote askari mmoja anisukuma ili nimuechie mama kisha akamshika mama mkono na kuanza kumburuza kitendo kilicho zidi  kunipandisha hasira ila kabla sijhamfwata nikastukia nikichapwa na fimbo aina ya mkia wa taa iliyo jizungusha kwenye tumbo langu na kunirudisha nyuma baada ya askari aliye nichapa kafanya hivyo bila ya huruma.

Nikamshuhudia mama akipotelea gizani kwenye pango pamoja na askari aliye mchukua na sikuwa na lakufanya zaidi ya kuendelea kupokea kichapo cha kuchapwa nikiamrishwa kwenda kufanya kazi upasuaji wa mame.Nikaokota moja ya nyundo huku nikiwa na hasira na uchungu mwingi na kuaza kuvunja mwamba amabao wenzangu wanaendelea kuuvunja.Kitu ambacho nimegundua ni kwamba watu wengi waliomo humu ndani wamelishwa makaa ya mawe moto ambaya sio rahisi kwa mtu kuweza kuzungumza chocheta zaidi ya kutoa miguno.

Hali ya maisha ikazidi kuwa ngumu kwa upande wangu kadri ya siku zinavyo zidi kwenda sikuweza kumuona mama yangu japo ninaendelea kufanya juhudi ya kuchunguza ni wapi alipo mama na sikuwa ninafahamu kama yupo hai au tayari amesha fariki,mwili wangu ukazidi kudhohofika kutokana na chakula finyu tunacho pewa asubuhi na jiono,asabuhi tunakunywa kikombe kidogo cha uji usio na kadha ya aina yoyote na usiku tunapewa viazi viwili vilivyo chemshwa na huo ndio mlo wa siku moja na mbaya zaidi chakula ni chakugombani usipo fanya hivyo unaweza kukaa siku mbili hadi tatu pasipo kula.

Watu wengi wanazidi kufa kutokana na njaa inayo andamana na kazi ngumu kwa upande wangu kifua kianza kuniuma sana ikafikia hatua nikaanza kukohoa na makohozi yangu yamechanganyikana na damu nyingi.

“hapana siwezi kufa humu ndani”
Nimawazo ambayo yakawa yanajirudia rudia kichwani kwangu kadri siku zinavyo zidi kwenda,mbaya zaidi sikuweza kujua upi ni usiku na upi ni mchana hii ni kutokana na muda wote tuliopo ndani ya pango mataa makubwa yanawaka,kila ninapo jitazama mwili wangu ninajikuta nikimwagikwa na machozi kwani mbavu zangu unaweza kuzihesabu,mikono na miguu yangu imekondeana sana.Nyele zangu zimekosa uhusiano mzuri kichwani vidonda vingi ambavyi vingine vimefikia hadi hatua ya kutoka na funza vikaendelea kunitesa mwili wangu.

“mungu wangu ninaomba unipe nguvu na juhudi katika hili”
Nikaanza kufanya kazi ya kutafuta ni wapi ninaweza kupata njia ya kutokea na kwa bahati nzuri katika uvunjaji wangu wa miamba nikaona sehemu yenye ufana wenye kijisihimo kidogo,nikawatazama askari waliopo ndani humu na hakuna aliye nifwatiliza nikapiga hatua za taratibu na kuchungulia kwenye shimo na kuona mwanga kwa mbali na akili yangu ikatambua utakuwa ni mwanga wa jua.

Kengele ya kwenda kupata chakula cha jioni ikagongwa na nikatupa sururu niliyo nayo chini na kuchomoja kwa kasi kuwania chakula ambacho nikikosa leo itakuwa siku yangu ya pili kukosa chakula.Japo mwili wangu umedhohofika nikajikaza katika kugombani viazi na kupata viazi vitatu,nikakaa kwenye sehemu ambayo siku zote huwa  ninapenda kukaa na kuanza kuvisakamia viazi kwa fujo

Nikastukia nikiguswa mguu na binti mdogo na akaniwekea mkono kwa ishara ya kuniomba kiazi kimoja ambacho nimebaki nacho mkononi.Nikamtazama kwa jinsi alivyo kondeana hadi sura yake imejaa vishimo shimo vilivyo kosa nyma kwa kukondeana.Taratibu nikampa kijikiazi nilicho nacho na chote akakiweka mdomoni na kuanza kukitafuna kwa haraka na inavyo onyesha ana njaa kuliko mimi.Akanishukuru kwa kuikutanisha mikono yake kwa pamoja huku akiinama na akanyanyuka taratibu na kuondoka.

Tukuruhusiwa kwenda kulala kwenye mapango yetu ambayo milango yake ni ya chuma na katika chumba kimoja cha pango tunalala watu si chini ya thelathini na tangu niingie kwenye hili pango sikuwahi kuona hata siku moja watu wakienda kuoga kwahi maji tunayo kunywa ni machafu sana na yapo kwenye kijikisima kimoja kidogo.Harufu ya uchafu wa miili yetu siku zote inanikusesha raha ya kulala na hususani loe kidogo ninajambo la kuliwazia kichwani kwangu kutokana na ufana nilio uona ninaimani utanisaidia katika kutoroka ndani ya hili pango.

Muda wa kuamshwa ukawadia na tukatoka ndani ya vyomba vyetu na kuelekea sehemu za utendaji wetu wa kazi na kitu cha kwanza kufika kwenye sehemu yangu nikawa na kazi ya kuvujunya ufa nilio uona,ugumu wa mwamba huu hakunifanya nife moyo zaidi ya nilicho kifanya ni kuendelea kuvunja hadi ikafikia kipindi matumaini yakaaza kuja,filimbi ya dharura ikapangwa na tukakusanyika kwenye eneo la moja na askari wakaanza kutupanga mistari mitatu na tukasubiria nini tunacho taka kuambiwa.

Nikawaona watu wanne walio valia vizuri na nikamgundua mmoja wao ambaye ni baba yangu mkubwa mzee godwin akiwa ameongozana na watu wengine watatu ambao sikuwajua.Mukuu wa askari wa eneo hili akawapokea kwa unyeyekevu mkubwa na kuanza kuwapitisha kwa kwenye mistari mmoja baada ya mwengine kama vile raisi anaye kagua gwaride la wanajeshi.

Sura yangu nikaiinamisha chini ili asiweze kunijua kwa haraka na kabla ya kunifikia mimi akahamia kwenye mstari wa nyuma yetu na kuendelea kuwatazama watumwa wezangu tuliopo kwenye eneo hili,wakamaliza kazi hii na wakapanda kwenye ofisi ya mkuu wa eneo hili huku wakizungumza na kucheka kwa furaha.

Uchungu na maumivu makali yakaendelea kuutesa moyo wangu ila sikuwa jinsi,tukarudi kwenye sehemu zetu na kuendelea na kazi hata kengele ya uji ilivyo gonga sikuwa na haja ya kwenda kugombania uji.Nikaendelea kupasua mwamba huu na kugundua mawe haya nikiyagonganisha kwa pamoja yanaweza yakazalisha moto kutokana na chechezake.Nikawaona askari wanao tusimamia wakielekea walipo kwenda baba na wezake wakionekana kujawa na furaha hapa ndipo nikaamini kuwa baba mkubwa ndio mmiliki wa hili eneo.

Kwa bahati nzuri nikaona kamba moja ambayo hutumia katika kubutia mawe makubwa,nikaichukua na kwenda moja kwa moja kwenye mapipa yenye mafuta ya petrol ambayo yanatumika kuendeshea majenereta yanayo washa taa za humu ndani,kwa haraka nikaichovya kamba kwenye pipa lenye mafuta na kabla sijaondoka eneo lenye mapipa nikaona kidungu kidogo cha maji ya lita moja na nusu.

Nikakiokota na kuchota mafuta nusu na kurudi katika eneo lenye ufa,kwa uzuri ni kwaba sehemu yenye ufa juu yake ndipo zilipo ofisi za wakuu wa hii sehemu na haikuw ni raisi kwa wao kuniona kutokana nipo chini shana na pameingia ndani.Wezangu tayari wamesha toka kunywa uji na wanaendelea na kazi zao za upasuaji wa mawe na kelele za upasuaji wa mawe zikazidi kunipa moyo wa kwamba sio rahisi kwa maaskari kuweza kusikia kitu cha aina yoyote.

Nikaiingiza kamba kwenye mdomo wa kidungu nilicho kiokota japo kamba ni nene kiasi ila nikajitahidi kuigandamiza hivyo hivyo na ikaingia kiasi kidogo.Nikakichomeka kidungu sehemu yenye ufa na kabla sija ondoka kwenye eneo hili msichana aliye niomba kiazi jana usiku akanifwata na kunigusa mkono na kwa ishara akaanza kunielekeza kitu ambacho haikuwa si raisi kwa mimi kuielewa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Awasili Dodoma Kwa Ajili Ya Bunge

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Lugimbana  baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma Septemba 4, 2016 kwa ajili ya vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza Septemba 6, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa akisalimiana Septemba 4, 2016  na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma kwa ajili ya vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza Septemba 6, 2016. 

Polisi wafyatua risasi na mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Prof. Lipumba

0
0
Jeshi la Polisi limelazimika kufyatua risasi angani na kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Prof. Lipumba waliokuwa wakimzuia mwenyekiti wa muda wa CUF, Julius Mtatiro, kuingia ofisini eneo la Buguruni.

Wafuasi hao wameeleza kuwa wameamua kumzuia kwani Msajili wa Vyama vya Siasa ametaka shughuli zozote ndani ya CUF zisiendelee hadi hapo mgogoro wa uongozi utakapotatuliwa.

Itakumbukwa hivi karibuni CUF kilimteua Julius Sunday Mtatiro kuwa mwenyekiti wa muda baada ya mwenyekiti aliyekuwepo, Prof. Lipumba kijiuzulu Agosti 2015.

Julius Mtatiro leo amefanya mkutano na waandishi wa habari  katika ofisi za Makao Makuu ya CUF, Buguruni, Dar es Salaam ili kuzungumzia kauli zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli akiwa visiwani Zanzibar.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Septemba 5

Uhuru Kenyata Akanusha Kuwepo Mvutano Wa Kiuchumi Kati Ya Tanzania Na Kenya

0
0

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Jumamosi alikanusha ripoti za vyombo vya habari kwamba kuna mvutano baina ya Kenya na Tanzania.

Akizungumza mjini Mombasa wakati wa ufunguzi gati la makontena katika bandari ya Mombasa, Kenyatta alipuuzia maneno kwamba kuna mvutano wowote na badala yake akasema kuwa nchi hizo zinasaidiana.

Alisema anaona kwenye vyombo vya habari kwamba kuna “mgogoro baina yetu, lakini nataka kusema wazi wazi kwamba Kenya na Tanzania hazina mgogoro wowote baina yao,” alisema.

Kenyatta alisema uchumi wa nchi hizo mbili umefungana kwa miaka mingi na ni kwa ajili ya faida ya watu wa nchi hizo mbili.

Alitaja kufunguliwa kwa njia inayojulikana kama “northern frontier” ambayo itaunganisha bandari ya Mombasa kupitia mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania, hadi Bujumbura, Burundi – njia ambayo itafupisha urefu wa kutoka Bujumbura hadi Mombasa kwa kilomita 300 nzima.

“Afrika Mashariki haiko katika mashindano ya wenyewe kwa wenyewe,” alisema Kenyatta. “Afrika Mashariki inashindana na dunia. Tunataka kujaliana (pale penye mapungufu). Tunataka tutumie nguvu zetu ili kukua, kuendeleza na kuinua uchumi wetu,” alisema.

Kutokuwepo kwa Rais John Magufuli wa Tanzania katika mkutano wa hivi karibuni wa kimataifa na Tokyo mjini Nairobi kulizusha uvumi kuhusu uhusiano wa nchi za eneo hilo.

Kiongozi huyo wa Tanzania ametembelea Uganda na Rwanda tu tangu achukue madaraka Oktoba mwaka jana ukilinganisha na rais aliyemtangulia Jakaya Kikwete ambaye alikuwa akisafiri sana nchi za nje.

Rais Magufuli pia hakuhudhuria mikutano karibu mitano ya kimataifa, ikiwa ni pamoja na mkutano wa shirika la biashara duniani na mikutano mikuu ya AU mjini Addis Ababa na ule wa Kigali Rwanda hivi karibuni.

TRA yavuka lengo la makusanyo ya kodi kwa mwezi Agosti.

0
0
Katika harakati za kuhakikisha kuwa Mapato yote stahiki yanakusanywa ipasavyo na kwa Wakati, Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA imejiwekea mikakati mbalimbali ya kuongeza wigo wa vyanzo vya Mapato pamoja na kukusanya Mapato kikamilifu.

Mikakati hiyo ni kama ifuatavyo;
Kulifanya eneo la Kariakoo kuwa Mkoa Maalumu wa Kodi kutokana na eneo hilo kuwa kitovu cha biashara hapa nchini na kuhakikisha kila mfanyabiashara anakuwa na Mashine ya Kielektroniki ya kodi (EFDs) na kuitumia ipasavyo.

Katika kutekeleza hilo Mawakala wote wa EFDs wamefungua ofisi ya pamoja katika jengo la Al-Falah Towers lililopo mtaa wa Msimbazi Kariakoo ili kurahisisha upatikanaji wa mashine hizo na kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara katika matumizi ya mashine hizo.

Aidha Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi TRA Bw. Richard Kayombo ametoa wito kwa wananachi na wafanyabiashara kujitokeza kuhakiki taarifa zao za usajili wa TIN kabla ya Tarehe 15 Oktoba 2016 katika vituo vifuatavyo kwaajili ya zoezi hilo kwani muda hautaongezwa baada ya tarehe hiyo maana baada ya tarehe hiyo zoezi hili litahamia mikoa mingine;

Vituo hivyo vya uhakiki ni pamoja na:
  • Mkoa wa Kodi Ilala: Jengo la Mariam Tower (Shaurimoyo) na 14Rays (Kariakoo-Gerezani)
  • Mkoa wa Kodi Kinondoni: Jengo la LAPF (Kijitonyama) na Kibo Complex (Tegeta) na ofisi za TRA Kimara
  • Mkoa wa Kodi Temeke: Uwanja wa Taifa na Ofisi za TRA Mbagala- Zakiemu
  • Wilaya ya Kigamboni – Ofisi za TRA Kigamboni
Pamoja na kuhakiki taarifa zao, wafanyabiashara wote ambao hawana TIN nchini wanaombwa kufika katika ofisi ya TRA iliyoko karibu nao ili kujisajili kuepuka kukumbwa na msako unaondelea hivi sasa nchi nzima pamoja na uhamasishaji

Wakati huo huo Bw. Kayombo amewahimiza wamiliki wa vituo vya mafuta kutekeleza agizo la Serikali la kufunga mashine za EFDs kabla au ifikapo tarehe 30 Septemba 2016 kwani kinyume na hapo ukaguzi utaanza kufanyika kuanzia tarehe 1 oktoba na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale wote watakaobainika kukiuka agizo hilo.

Katika kuhakikisha kwamba kodi ya ongezeko la thamani VAT inakusanyawa kwa Wakati Mamlaka inawakumbusha walipakodi wote waliosajiliwa na Kodi ya Ongezeko la Thamani -VAT kuwasilisha ritani ya kila mwezi kabla au tarehe 20 ya kila mwezi badala ya tarehe 27 iliyokuwepo kabla ya mwaka hu wa fedha.

Kwa upande wa walipa kodi zaa makadirio na kodi za makampuni (Corpoaration Tax) wanakumbushwa kulipa kodi zao mapema mwezi hu wa tisa badala ya kusubiri msongamano mwisho wa mwezi ambao unaweza kuwasababishia usumbufu

Hivyo hivyo walipakodi wote wanaodaiwa madeni ya kodi za nyuma au malimbikizo wanakumbushwa kutembelea Mameneja wa mikoa, Wilaya na ofisi mbali mabli za TRA zinazowahudumia ili kujadiliana namna ya kulipa madeni hayo.

Kutokana na mikakti mizuri iliyowekwa na uiongozi wa TRA na serikali Mpaka sasa baadhi ya mikakati hiyo imeanza kuonyesha mafanikio na mwelekeo mzuri wa makusanyo ambapo kwa kipindi cha mwezi Agosti 2016 TRA imekusanya Trillioni 1.158 ikilinganishwa na lengo la Trillion 1.152 ambayo ni asilimia 100.57  ambapo Mwezi Agosti Mwaka 2015 TRA ilikusanya Billion 923.

Wito wetu kwa wanahabari na wananchi kwa ujumla ni kuendelea kutuunga mkono kwa kuhimiza kutoa risiti pamoja na kudai risiti katika kila manunuzi pamoja na kutoa taarifa za dalili za ukwepaji wa kodi wa aina yoyote mahali popote nchini

‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’

Richard Kayombo

MKURUGENZI WA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI

Wabunge wa Upinzani Kuanza Vikao vya Kutafuta Suluhu na Naibu Spika

0
0
Kambi rasmi ya upinzani imepanga kufanya vikao vya kujadili suluhu ya kudumu ya mgogoro na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson uliosababisha wabunge wanaounda Ukawa kususia vikao vinavyoendeshwa na kiongozi huyo.

Vikao hivyo vinapangwa kufanyika wakati mkutano wa nne ukianza rasmi kesho, baada ya kuahirishwa mwishoni mwa Juni mwaka huu wakati wa mkutano wa Bajeti. 

Mbunge wa Vunjo (NCCR- Mageuzi), James Mbatia alieleza jana kuwa uamuzi wa kufanya vikao hivyo umefikiwa baada ya upinzani kukaa kikao na viongozi wa dini Agosti 24 mwaka huu ili kutafuta suluhu ya kudumu. 

“Kikao cha kwanza tutakaa kamati ya uongozi ya wabunge wa upinzani kujadili suala hilo na baadaye tutamaliza na kikao cha wabunge wote ili kubaini njia endelevu za kumaliza jambo hilo,” alisema Mbatia ambaye ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi. 

Wabunge wa Ukawa wamekuwa wakisusia vikao vinavyoendeshwa na Naibu Spika kwa madai ya kutoridhishwa na uongozi wake tangu Mei mwaka huu, baada ya Dk Tulia kukataa kujadili hoja ya kufukuzwa wanafunzi zaidi ya 8,000 stashahada ya ualimu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom). 

Hata wakati wakisubiri kufanyika vikao hivyo ambavyo Mbatia hakutaka kuelezea kwa undani, upinzani ulitangaza kurudi bungeni baada ya mkutano wao na viongozi wa dini. 

Katika mkutano na wanahabari Agosti 25, Mbatia kwa niaba ya vyama vilivyoshiriki mkutano huo wakiwamo ACT-Wazalendo, alisema wangejadiliana namna ya kufanikisha jambo hilo kama sehemu ya kutii ushauri wa viongozi hao wa kiroho. 

Hata hivyo, haijawekwa bayana iwapo kesho Ukawa wataendelea na vikao hata kama Dk Tulia ataendelea kuongoza kiti hicho ama la. 

Mbatia alisema jana kuwa watatoa taarifa rasmi leo namna vikao hivyo vitakavyofanyika na siku husika. 

Kuhusu kupata taarifa ya mwenendo wa mchakato wa kutafuta maridhiano ulioelezwa na Spika Job Ndugai hivi karibuni, Mbatia alisema hawajapata chochote na wao wanasikia kwenye vyombo vya habari kama wengine. 

Alipoulizwa ni lini vikao vya maridhiano kati ya pande hizo yataanza, Ofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bunge, Owen Mwandumbya alisema Spika anatarajiwa kufika ofisini leo na kwamba kama ataona kuna haja ya kufanya hivyo atapanga utaratibu wa namna anavyoona inafaa. 

Mtandao hatari wa Majambazi Wanaswa Dar es Salaam

0
0
Watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wanadaiwa kukamatwa na polisi wakiwa na zana mbalimbali ambazo hutumiwa na vyombo vya ulinzi zikiwamo silaha za vita na sare za polisi.

Vitu hivyo vinadaiwa kutumiwa na watu hao kufanya   ujambazi.Inadaiwa kwamba watu hao ni wale waliovamia na kuiba fedha katika jengo la Sophia House lililopo Keko   Dar es Salam wakiwa wamevaa sare za polisi na kutumia gari   ya Noah.

Taarifa  kutoka chanzo cha kuaminika zinaeleza kwamba watu hao ni pamoja na mwanamke mmoja aliyekamatiwa   Bunju  katika Manispaa ya Kinondoni ambako vilikutwa vitu vyote vilivyoporwa na wanaume wawili waliokamatiwa   Mbagala Manispaa ya Temeke,   Dar es Salaam.

Chanzo hicho kilieleza kwamba silaha zilizokamatwa  ni pamoja na bunduki tatu za SMG na risasi zake 260, bastola 16 na risasi zake 526, panga moja na michimbiko mitatu ya kung’olea mageti..

Vitu vingine ni   pingu za chuma 45 na tatu za plastiki, ‘radio call’  12 , kamera ya CCTV moja, gari moja   ya Noah, sare ya polisi jozi moja, ‘pump action tatu na mkasi mmoja.


RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 40

0
0
MTUNZI:ENEA FAIDY

....Eddy alisimama kwa muda huku akiyashangaa yote yanayoendelea. Alishindwa kuamini kama kinachoendelea pale kilikuwa na ukweli ndani yake.  Alifuta macho yake na kutazama tena,  safari hii macho yake yalitua moja kwa moja kwa Doreen aliyekuwa amepiga magoti mbele yake huku akilia kwa uchungu na majuto mengi.

"Nisamehe Eddy kwq kukufanyia ukatili huu. Nimekutesa sana wewe na familia yako... Nisamehe tafadhali" alisema Doreen huku akilia kwa uchungu hali iliyodhihirisha majuto aliyokuwa nayo moyoni mwake. Hata hivyo Eddy hakuweza kuzungumza chochote zaidi ya kumtazama Doreen kwa hasira huku machozi yakimtiririka machoni mwake.

 Aliumanisha meno yake kwa hasira huku akitamani kuiondoa roho ya Doreen kwani mateso aliyompa maishani mwake ilikuwa ni vigumu kusahaulika. Mateso aliyokuwa nayo yalijaa fedheha na aibu isiyositirika. Machozi yalimshuka taratibu machoni mwake huku akimtazama Doreen.

"Naomba unisamehe Eddy ili adhabu ninayopata ipungue walau kidogo... Nateseka Eddy" Doreen alizidi kumsihi Eddy lakini maneno yake ilikuwa ni kama kujilisha upepo kwani Eddy hakuukubali  msamaha wake.

Wanawake waliokuwepo eneo lile walijisikia aibu kwa kuona wanawake wenzao wapo uchi wa mnyama. Wakatoa khanga zao na kuwapa akina Doreen wazivae lakini hata hivyo ilikuwa vigumu kwa akina Doreen kupokea khanga zile kwani maumivu yalikuwa Makali mno kwenye miili yao. Kila Mara walihisi moto ukiwawakia katika ngozi zao. Ikawabidi wanawake wale wawafunike kwa lazima ili kuwasitiri.

Ghafla mwili wa Maimuna ukaanza kubadilika na kuwa mweusi kama mkaa. Akajiviringa viringa kama nyoka pale sakafuni huku akitoa mlio kama wa mbuzi kisha akatoweka mbele ya macho ya watu. Wote waliogopa sana, baadhi ya watu walijikaza kisabuni na kuendelea kubaki pale huku wengine wakikimbia sana na kuondoka eneo lile.

Doreen alibaki pale huku akiendelea kumsihi Eddy amsamehe. Lakini Eddy alikuwa na moyo mgumu sana wa kumsamehe kiumbe yule.
"Hustahili kuishi Doreen... Kufa tu.." Alisikika Eddy kwa sauti iliyojaa hasira.
"Kweli! Afe tu huyu! Tumuue!" Walisikika Raia waliokuwepo eneo lile.
"Nitakufa ndio ila naomba unisamehe.. Najua nimekukosea sana... Sitaki nife kabla hujanisamehe!" Alisema Doreen.

"Kwa mateso uliyonipa siwezi kukusamehe... Umenitesa sana... Sijui nani amekuadabisha namna hii na kukudhalilisha hivi... Amenifurahisha sana" alisema Eddy kwani hakujua lolote linaloendelea kuwa Dorice ndiye aliyefanya yote hayo.

"Na kwa jinsi ulivyonifanyia.. Daima siwezi kumwamini mwanamke! Naapa!" Alisema Eddy lakini kuna sauti ilimnong'oneza masikioni mwake

"Usiseme hivyo... Niamini Mimi" Eddy alishtuka sana akaangaza macho huku na kule pasipo kuona mtu aliyemnong'oneza. Sauti ile haikuwa ngeni sana masikioni mwake ila alishindwa kujua ilikuwa ya nani. Akatafakari kwa muda kisha akaipotezea sauti ile na kuendelea kumtazama Doreen.

"Eddy hutaki kunisamehe?" Aliuliza Doreen kwa sauti ya upole. Eddy akatafakari kidogo, akagundua kutomsamehe binadamu mwenzake ni kosa kubwa kwani yeye hutenda dhambi nyingi lakini husamehewa na Mungu.
"Nimekusamehe.. Ila sitokusahau!"
"Asante..."
 

Ambari Nyeupe Ni Tiba Ya Kuongeza Ukubwa Wa Maumbile Ya Kiume Yaliyo Sinyaa.

0
0
Ipo  idadi  kubwa  ya  wanaume  wanao  kabiliwa na  changamoto  ya  kuwa  na  maumbile  madogo  ya  kiume.  

Kama  wewe  ni  mwanaume  ulie  katika  kundi  hili, unaweza  kujitibu  tatizo  lako  kwa  kutumia dawa  asilia  itokanyo  na  AMBARI  NYEUPE.

Ambari  nyeupe  nyeupe  ikichanganywa  na  dawa  nyingine  tatu  za  asili,  hutumika  kama  tiba  ya  kuongeza  ukubwa  wa  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa.

Kwa  mahitaji  yako  ya  dawa  hii, fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  asilia  la  NEEMA  HERBALIST & NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini Dar  Es  Salaam, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo la  UBUNGO  PLAZA.

Wasiliana  nasi  kwa  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84

Na kwa  taarifa  Zaidi  kuhusu  huduma  zetu,  tutembelee  katika  blogu  yetu :

Taarifa Ya Ajali Ya Basi La Hood Likitokea Mbeya Kwenda Arusha

Naibu waziri Tamisemi,Selmani Jafo anusurika kifo ajalini Mbeya

0
0
Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jafo amepata ajali eneo la Katela Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe Mbeya.

Ajali hiyo imehusisha gari dogo aina ta Corola iliyokuwa ikotokea Mbeya kwenda Rungwe na Naibu Waziri Selemani Jafo alikuwa akitokea Tukuyu kikazi.

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja amesema katika gari Waziri walikuwa watatu, Waziri Jafo mwenyewe Katibu wake na Dereva na wote walitoka salama katila ajali hiyo.

Alisema baada ya kupata ajali hiyo walipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambapo walifanya uchunguzi kama wameumia kwa ndan au laa! Lakin bahat nzuri Daktari aliyewafanyia uchunguz alisema hakuumia popote ni wazima.

Alisema baada ya hapo Waziri na watu waliendelea na safari yao kuelekea mjini Dodoma kwa ajili ya kuwahi vikao vya Bunge
Gari lililoigonga gari la Naibu Waziri likiwa limetupwa korongoni.
Askari wa usalama barabaran wilayani Rungwe, Mbeya wakipima ajali ilivyotokea
Picha zote kwa hisani ya Mbeya yetu

Waziri Mkuu Majaliwa na Spika Job Ndugai Wakutana kujadili maridhiano ya Vyama Vya Siasa

0
0
Ikiwa imesalia siku moja kabla ya mkutano wa nne wa bunge la kumi na moja kuanza hapo kesho September 6 2016 leo Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Spika wa bunge Job Ndugai pamoja na viongozi wengine katika ofisi za bunge zilizopo Dodoma kwa lengo la kufanya kikao cha maridhiano ya vyama vyote.

Hapa kuna picha tano  wakati wa majadiliano hayo yalipokuwa yakifanyika..

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Septemba 6

BAKWATA yatangaza siku ya Sikukuu ya Eid ya kuchinja.

Serikali Yakusudia Kuwapeleka Watoto Wa Mitaani Katika Mafunzo Ya JKT Ili Kusaidia Uzalishaji Mali

0
0

Na Ismail Ngayonga - Maelezo.
SERIKALI inakusudia kuwapeleka katika kambi za mafunzo  ya Jeshi la Kuujenga Taifa (JKT) watoto wa mitaani wenye umri wa zaidi ya miaka 18 ili wajifunze  stadi za kazi na shughuli  za uzalishaji mali.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu  wakati wa mahojiano maalum katika kipindi cha Tunatekeleza kinachoandaliwa na Idara ya Habari (MAELEZO) na Televisheni ya Taifa (TBC1).

Waziri Ummy alisema hatua hiyo inalenga kuliwezesha kundi hilo la vijana kujihusisha na shughuli za uzalishaji mali badala ya kuzurura hovyo mitaani sambamba na kujihusisha na tabia na vitendo  vinavyokiuka maadili katika jamii.

Alisema tayari  watendaji wa Wizara yake kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Waziri Mkuu tayari wamekutana kujadiliana kuhusu suala hilo ili kuangalia namna bora zaidi ya kusadia kundi hilo.

Alifafanua kuwa vituo vingi vya kulelea watoto hao vimekuwa na watoto waliozidi umri wa miaka 18, ambapo kwa mujibu wa sheria hawatakiwi kuwa katika vituo hivyo na kuongeza kuwa  ofisi yake itahakikisha zoezi la kuwapeleka katika mafunzo hayo linatekelezeka.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy alipiga marufuku tabia za baadhi ya watu,  asasi na vikundi kuanzisha vituo vya kulea watoto yatima pasipo kuwa na usajili  kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Kwa mujibu wa Waziri Ummy alisema tayari ofisi yake imetoa maelekezo kwa Kamishina wa Ustawi wa jamii kufanya tathimini na utafiti wa kina kuhusu vituo vya kulea watoto yatima, ambapo iwapo kutabainika vituo vitakavyokosa sifa hatua za kisheria zitachuliwa kwa wahusika.

Kuhusu chanjo, Waziri Ummy alisema Serikali itaanza kutoa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa watoto wenye umri wa miaka 9-13 ili kukabiliana na changamoto ya maradhi hayo nchini.

Waziri Ummy aliwataka wazazi kutoa ushirikiano pindi zoezi hilo litakapoanza kwa kuwa halitakuwa na madhara ya kiafya kwa watoto wao.

Aidha, alisema  Serikali imekuwa ikipoteza kiasi kikubwa cha fedha kila mwaka kwa ajili ya matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo saratani ya shingo ya kizazi kwa akina mama ambayo inaambukizwa na virusi vinavyojulikana kwa jina la Human Papiloma Virus (HPV).

“Tumeamua kuteua kundi la watoto wa lika huo kwani wengi wao katika umri huo wanakuwa bado hawajaanza kujihusisha na vitendo vya mapenzi”  alisema Waziri Ummy.

Alisema katika bajeti ya mwaka 2016/17 Serikali imepanga kuipatia taasisi ya saratani ya ocean road  kiasi cha Tsh. Bilioni 3 kwa ajili ya ununuzi wa madawa, ikilinganishwa na kiasi cha Tsh. Milioni 600 zilizokuwa zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2015/16.

Akizungumzia changamoto iliyojitokeza hivi karibuni ya ukosefu wa chanjo katika vituo vya huduma ya hivi nchini, Waziri Ummy alisema suala hilo litakuwa historia hivi karibuni kwani tayari Serikali imeagiza kutoka nje ya nchi baadhi ya chanjo hizo.

Wizara ya Elimu Yawaasa Vijana Kutumia Elimu Kujiajiri

0
0

Na Jacquiline Mrisho-Maelezo
SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imewaasa vijana waliomaliza shule kuacha kujibetweka bali watumie elimu waliyoipata kujitafutia ajira ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira nchini.

Kauli hiyo imetolewa jana Jijini Dar es Salaam na Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Nicholaus Bureta wakati wa ufunguzi wa mkutano wa vijana wa Afrika unaojadili changamoto zinazowakabili vijana katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Bureta alisema kuwa Serikali  inatoa elimu bora ili kuhakikisha vijana wanapata uwezo na maarifa yatakayowasaidia kujiajiri hata wasipopata nafasi za kuajiriwa katika taasisi na ofisi za umma pamoja na kuitumia elimu hiyo katika kupambana na vitendo vya rushwa.

“Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 inatutaka tuwe na watanzania walioelimika na wenye mtazamo chanya ambao utahakikisha jamii yetu inabadilika kufikia uchumi wa kati hivyo vijana msikae kusubiri ajira bali mjifunze jinsi ya kujiajiri kutokana na elimu mliyoipata mashuleni”, alisema Bureta.

Kwa upande wake Afisa Habari wa Umoja wa Mataifa (UN), Stellah Vuzo aliwapongeza vijana hao kuamua kukusanyika kuchangia mawazo yao juu ya matatizo yanayowakabili kwani vijana wana nafasi kubwa ya kuhakikisha malengo mbalimbali yanatekelezeka.

Aidha, aliongeza kuwa Umoja wa Mataifa umemteua balozi kijana ambaye anashughulikia ajira za vijana hivyo aliwaomba vijana walioshiriki katika mkutano huo kuyafikisha mawazo hayo kwa balozi huyo ili yaweze kupatiwa ufumbuzi.

Naye Mkuu wa Utafiti kutoka Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (PCCB), Daniel Pundu alisema kuwa tatizo la rushwa haliwezi kuisha endapo vijana hawatashirikishwa hivyo amewasisitiza vijana kushirikiana na Serikali kuchukua hatua za kupambana na rushwa ili kuhakikisha rushwa inaondoka.

“Tunajua kuwa vijana ndio nguvu kazi ya Taifa na ndio sababu tunawasisitiza kupambana na rushwa, kwa kulitambua hilo Serikali imeanzisha vilabu vya wapinga rushwa katika shule za sekondari na vyuo vikuu vikiwa na lengo la kuhakikisha vijana wanahusika kwenye mapambano hayo”, alisema Pundu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images