Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 35 & 36 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA

Ilipoishia...

Daktari aliye kuwa anaendelea kunipiga baada ya kumuona mwenzake akiwa anaaga dunia akaniacha na kwa nguvu zake zote akarusha kirungu chake na kikatua kichwani mwa sheila na akadondoka chini na damu za puani zikaanza kumwagika

Endelea....
Taratiu nikaanza kujiburuza chini hadi sehemu aliyo angukia sheila huku machozi yakinimwagika na kujikuta nikijilaza juu yake na kumfanya daktari aliye mpiga akanza kunipiga tena kwenye mgongo akinimrisha nimuechie sheila ili aendelea kumshuhulikia kwa kipigo.Kila nilipo jaribu kumtingisha sheila sikuweza kuona dalili yoyote ya kuishi kwake na kujikuta nikizidi kumkumbatia kwa uchungu.Nikaanza kusikia makelele yakija kwa nyuma yangu,nikageuza shingo yangu na kuona kundi kubwa la vichaa wakija kwa kasi na kumfanya daktari anaye nipiga kutimka mbio na sikujua ni wapi anapo elekea na wote wakanipita na kuendeleka kumkimbiza dakrari aliye kuwa akinipiga.

Nikaona nikiendelea kujiliza haita saidi zaidi ya kumfanya sheila kuzidi kuzidiwa na kipigo alicho kipata.Nikajikaza na kwabahati nzuri miguu yangu ina nguvu za kutosha nikanyanyuka na kujinyoosha japo nilijawa na maumivu makali ila sikuwa na jinsi.

Nikanyanyua sheila na kutokana na kudhohofika kwake kwa mwili haikuwa ngumu kwangu kumbeba hadi tukafika kwenye kwenye moja ya ofifisi na kuwakuta vichaa wakiwashambulia manesi waliomo ndani ya ofisi.Hali ya hospitali imechafuka kupita maelezo madaktari wanashambuliwa na vichaa ambao wamepandwa na hasira.Kwa bahati nzuri nikaona gari moja ya waogonjwa amayo imesimama nje kwenye maegesho huku dereva wake akichomolewa kwenye gari na kuanza kupewa kipigo kama ilivyo kwa wahudumu wengine wa hospitali ikiwemo walinzi.

Hapa ndipo nikagundua kuwa vichaa tunafahamiana kwa maana kwa kila nilipo pita huku nikiwa nimembeba sheila hapakuwa na anaye nigusa tofauti na wanapo muona muudumu wa hospitali hii.Nikafanikiwa kufika kwenye gari la wagonjwa nakumuingiza ndani ya gari sheila na kwenda upande wa dereva na kuanza kutafuta fungua na sikuweza kuiona ikanibidi nishuke na kuunza kuupapasa mwili wa dereva ulio lala pembezoni mwa gari na kwabahati nzuri nikaiona funguo kwenye mfuko wake wa suruali.

Nikawasha gari na kuondoka hukiwasaidia vichaa kutoka ndani ya hospitali hii baada ya kuligonga geti lililokuwa kimefungwa.Kutokana sikuwa ni mwenyeji sikujua ni wapi nielekee ili kumuwahisha sheila hospitali.Nikasimamisha gari pembezoni mwa arabara huku likiwa linawaka ving’ora na kuichukua simu iliyopo ndani ya hospitali na kuanza kubuni namba ya baba

Kwa mara ya kwanza ikapokelewa na mwanamke ambaye hata lugha hatulewaa na nikajua nitakuwa nimekosea,nikajaribu kufikiria namba nyingi ambazo zinaweza kufanana na namba ya baba na pia namba niliyo ipiga ikapokelewa na kijana na akaanza kumwaga matusi alipoona sizungumzi kitu chochote baada ya kusema haloo.Nikajaribu zaidi ya mara saba nipo kumbukumbu ya namba za baba ziliponijia vizuri kichwani na nikaipiga ikaita kwa muda kisha ikapokelewa
“nani mwenzangu?”
Ilikuwa ni sauti ya baba na kidogo tabasamu likanijia usoni
“mimi eddy”
“eddy……!!”

“ndio ni mimi baba ninaomba msaada wako”
Upo wapi mbona makelele ya king’ora?”
“nipo kwenye gari ya wagonjwa nimetoroka hospitalini ila mimi sio kichaa kama ulivyo dhania”
“ngoja kwanza umesema upo wapi?”
“mimi hapa wala sipajui ila kuna magorofa mafupi mafupi hii na kuna magari mengi yamesimama pembeni”
“umesema upo kwenye gari ya wagonjwa?”

“ndio”
“wewe ndio dereva ua kuna dereva?”
“mimi ndio dereva”
“sasa angalia kwenye upande wa kusoto kuna kijitivii kidogo….”
“ndio nimekiona”
“kiwashe kama hakija washwa na kwenye sehemu ya chini yake kuna batani nane umeziona”
“ndio”

“minya batani iliyo andikwa map”
Nikaiiminya batani ambayo baba aliniambia na ndani ya sekunde kadhaa kukatokea ramani yenye mistari mingi mingi huku kukiwa na kialama chekundu kikiwa kina waka waka
“inakisoma vipi hiyo ramani?”
“inasoema cape town, western cape city”
“subiri tunakuja sasa hivi”

Nikakata simu na kuzima gari na kufungua kijidirisha kilichopo nyuma ya siti yanga na kumuona sheila akiwa amejilaza huku akipumua kwa shida kidogo nikapata matumaini.Ndani ya nusu saa gari mbili zikasimama mbele ya gari nililipo na mtu wa kwanza kushuka ni baba na moja kwa moja akafika kwenye gani na akaonekana kunishangaa jinsi damu zinavyo nivuja.Watu wake wakanitoa ndani ya gari
“baba kuna mtu mwengine huku nyuma”
“ni nani?”
“rafiki yangu”


Vifaa Vyote vya Freeman Mbowe Vilivyokamatwa Jana na NHC Vitauzwa Baada ya Siku 14 Ili Kufidia Deni Analodaiwa

$
0
0

VIFAA vilivyokamatwa jana vya klabu ya usiku ya Bilicanas na ofisi ya gazeti la Tanzania Daima, vyote vinavyomilikiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, vitapigwa mnada na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) siku 14 kuanzia jana, endapo atashindwa kulipa Sh. bilioni 1.2 za deni la pango la miaka 20.

Mbowe alikuwa mpangaji katika jengo la NHC lililopo makutano ya mitaa ya Mkwepu na Indira Gandhi, katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Vyombo hivyo vilikamatwa jana na kampuni ya udalali ya Fosters Auctioneers and General Traders iliyopewa kazi ya kuondoa vifaa hivyo baada ya Mbowe kushindwa kulipa deni hilo ndani ya miezi miwili ya notisi ambayo shirika hilo lilikuwa limempatia.

Meneja wa Kitengo cha Kukusanya Madeni kutoka NHC, Japhet Mwanasenga aliyekuwa akisimamia ukamataji wa vyombo hivyo, alisema Mbowe ana muda wa wiki mbili kuanzia jana kulipa deni la Sh. bilioni 1.172 vinginevyo vitapigwa mnada.

Vifaa vilivyokamatwa ni pamoja na kompyuta, meza na viti.

Alisema taratibu zote zilifuatwa kabla ya kumuondoa mteja wao, ikiwamo notisi na kwamba vifaa hivyo vitashikiliwa kwa muda huo wa wiki mbili.

“Tunashikilia vyombo kwa muda wa wiki mbili na iwapo atashindwa kulipa vitapigwa mnada na dalali, (mdaiwa) akishindwa kulipa anapangishwa mwingine,” alisema.

Alisema shirika hilo linahitaji fedha kwa ajili ya ujenzi na uendelezaji wa majengo yake hivyo mteja ambaye anadaiwa ajiandae kuondolewa wakati wowote na kwamba zoezi la jana ni mwanzo tu.

Baadhi ya watu wamelihusisha tukio la kuondolewa Mbowe katika ofisi hizo na masuala ya kisiasa.

Lakini Mwanasenga alisema uamuzi wa kumuondoa ofisi hizo hauna uhusiano na masuala ya kisiasa.

Alisema wapangaji wa jengo hilo wapo wengi pamoja na wadaiwa na kwamba baada ya mchakato huo kuanza mdaiwa yeyote atakayeshindwa kulipa kodi ataondolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari katikati ya wiki iliyopita, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu alisema pamoja na Bilicanas, shirika linazidai taasisi za umma, binafsi na watu binafsi jumla ya Sh. bilioni 15.

Notisi ya siku 60 ya kuondoka Bilicanaa pamoja na majengo ya wadaiwa wengine ilishatolewa, Mchechu alisema. Notisi hiyo ilikuwa inaisha juzi.

Alisema baada ya muda huo kumalizika, utekelezaji wa kuondolewa katika majengo hayo utaanza ukiambatana na uchukuaji wa hatua za kisheria.

Mchechu alisema mbali ya Bilicanas, wadaiwa wengine ni Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi inayodaiwa Sh. bilioni mbili, Benki ya Azania (Sh. milioni 161) na Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa (Sh. milioni 631).

Wadiawa wengine walitajwa kuwa ni Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Sh. bilioni 1.3), Wizara ya Ujenzi (Sh. bilioni mbili), Tume ya Utumishi (Sh. milioni 109) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Sh. bilioni moja.

Mchechu alisema ukusanyaji wa madeni hayo kwa nguvu ni mkakati wa shirika hilo kukusanya fedha ili kusaidia ujenzi wa nyumba za watumishi wanaohamia Dodoma.

"Mwaka huu ujenzi unaanza Dodoma," alisema Mchechu, hivyo "fedha tunazodai zitatusaidia kukamilisha uwekezaji mjini humo."

Alisema kuwa fedha hizo zitatumika kwa ujenzi wa nyumba za watumishi 300 hadi 500 mkoani Dodoma.
 
Alisema ujenzi huo unatarajia kuanza mara moja na utachukua miezi 12.

Kwa mujibu wa Mchechu, Sh. bilioni 60 za ujenzi wa nyumba hizo zitatokana na fedha za ndani.

Alisema shirika hilo limenunua ekari 240 eneo la Iyumbu, ekari saba Chamwino, nne Bahi na Chemba ekari nne pia ikiwa ni kuunga mkono azma ya serikali ya awamu ya tano kuhamia Dodoma.

Alisema fedha nyingine zitapatikana baada ya nyumba 97 za shirika hilo zilizopo Medeli mjini Dodoma kuuzwa.

UVCCM yaivaa rasmi Chadema kwa kushindwa kufanya Maandamano ya UKUTA

$
0
0
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umewavaa viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kile walichodai kuendesha siasa za maigizo baada ya kushindwa kuzindua Operesheni UKUTA, Septemba 1.

Kupitia taaria yake kwa vyombo vya habari, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, amesema kuwa Chadema walijua kuwa hawana ubavu wa kufanya maandamano na mikutano nchi nzima Septemba 1 na kwamba walichofanya ni kuwatia hofu wananchi.

“UVCCM tulijua, tulielewa na kutambua bayana kwamba Chadema walikuwa wanafanya maigizo katika siasa, hawana ubavu wala jeuri ya kuandamana kwa madai ya kipuuzi na ambayo sio ya msingi kwa mustakabali wa nchi yetu,” alisema Shaka.

Aidha, Shaka alikanusha sababu zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuahirisha maandamano hayo kuwa wameombwa na viongozi wa dini ili waweze kukaa na pande zote kujaribu kutafuta suluhu kwa amani.

“UVCCM inatamka bayana kuwa hakuna majadiliano, mazungumzo wala mijadala itakayojadiliwa kati ya Serikali ya CCM na Chadema. Tunaomba Serikali ya Rais John Magufuli iendelee na mikakati yake ya kisera,” Shaka ameongeza.

Kaimu Katibu Mkuu huyo wa UVCCM alisisitiza kuwa Chadema hawana ubavu wa kufanya maandamano na mikuano nchi nzima Oktoba 1 kama walivyosema, baada ya kushindwa kufanya hivyo Septemba 1.

Shaka amesema wanachokifanya hivi sasa Chadema kinatokana na kushindwa kubuni mikakati ya kufanya siasa ili chama chao kiimarike na kukubarika.

Juzi, Chadema walitangaza kuahirisha uzinduzi wa oparesheni UKUTA nchi nzima, iliyokuwa imepangwa kufanyika jana (Septemba 1) kwa maandamano na mikutano nchi nzima.

UVCCM pia walitangaza kuahirisha maandamano yao ya nchi nzima waliyokuwa wamepanga kuyafanya Agosti 31 kwa lengo la kumpongeza Rais Magufuli kwa kazi aliyoifanya ndani ya kipindi kifupi.

Maandamano ya pande zote mbili yalipigwa marufuku na Jeshi la Polisi nchini.

Oktoba Mosi Yaanza Kugombaniwa.......Makonda Aitangaza Kuwa Siku Ya Kupanda Miti Huku Akiwataka JWTZ Washiriki Zoezi Hilo

$
0
0
Siku moja baada ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza kuahirisha kufanya maandamano na mikutano nchi nzima kupitia oparesheni walioipa jina la UKUTA ( Septemba Mosi) na kisha kuitaja Oktoba Mosi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda nayeye  ameitaja siku hiyo kuwa siku maalum ya kupanda miti. 

Na ili kufanikisha zoezi hilo, Jeshi la Wananchi (JWTZ) limeombwa kushiriki huku mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akizuia mikutano yoyote ambayo itaonekana haina tija.

Chadema ilikuwa imepanga kuzindua operesheni iliyoibatiza jina la Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), kwa kufanya mikutano na maandamano kote nchini, lakini ikatangaza kuahirisha juzi ikieleza kuwa imezingatia ushauri kutoka kwa viongozi wa dini, taasisi na watu mashuhuri. 

“Nimezungumza na watu wa hali ya hewa, wameniambia tukianza mapema miti hii haitakufa. Siku ya Oktoba Mosi kila mtu atakuwa na mti wake, tutawaarifu kupitia wakuu wa wilaya miti itapatikana wapi baada ya taratibu zake kukamilika,” alisema Makonda jana mbele ya Rais Magufuli kwenye mkutano wa 14 wa wahandisi kwenye ukumbi wa Mlimani City. 

Makonda alisema siku hiyo vikosi vya ulinzi na usalama vitashiriki kupanda miti na kumuomba Rais amsaidie na amvumilie ili atende kazi yake ya kuhakikisha mkoa wa Dar es Salaam unakuwa na amani sambamba na kufanikisha kutekeleza mpango huo wa upandaji miti. 

Aidha, makonda alipiga marufuku kufanyika kwa mikutano au maandamano yoyote isipokuwa mikutano itakayokuwa inajadili shughuli za maendeleo.

“Watakaopewa kibali ni wale wanaojadili maendeleo, lakini si wapigakelele. Mikutano kama hii (ya wahandisi) inayojadili masuala muhimu kabisa kwa maendeleo ya nchi, itaruhusiwa bila shaka yoyote.” 

Makonda alisema kampeni hiyo itawahusisha pia wananchi, viongozi wa dini na kamati nzima ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Dar es Salaam na kwamba jumla ya miti milioni 4 inatarajiwa kupandwa siku hiyo. 

Alisema ameamua kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa sababu ni watiifu na wazalendo kwa Taifa wakati kada nyingine zimejielekeza kwenye siasa. 

Hata hivyo, Rais hakuzungumzia maombi hayo zaidi ya kusema kuwa Makonda naye amekuwa mhandisi kutokana na kutoa maelekezo. 

Kabla ya Makonda kutangaza Oktoba Mosi kuwa siku ya kupanda miti, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema wamekutana na viongozi wa dini zaidi ya mara moja kwa ajili ya kupata maoni na ushauri kuhusu maandamano yao, ambayo Jeshi la Polisi liliyapiga marufuku kwa maelezo kuwa yalikuwa na viashiria vya kuvunja amani. 

Baadaye JWTZ ilisema ingeadhimisha kuzaliwa kwa jeshi hilo kwa askari wake kufanya mazoezi na kuonyesha silaha zao za angani na nchi kavu, kufanya usafi mitaani na kujitolea damu, huku likibainisha kuwa linaamini hakungekuwa na maandamano yoyote kwa kuwa yameshazuiwa. 

Katika kuadhimisha miaka 52 ya JWTZ jana, Makonda alishiriki kufanya usafi na askari hao katika kambi ya Lugalo iliyopo wilayani Kinondoni. 

Makonda aliambatana na kamati ya amani ya viongozi wa dini wa Dar es Salaam, ikiongozwa na mwenyekiti wake Alhadi Mussa Salum. 

Makonda aliitaja barabara ya Mwenge –Ubungo kuwa ni miongoni mwa barabara zitakazopandwa miti siku hiyo na watashirikiana na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads). 

CUF Waondolewa Kupisha Mkutano wa Rais Magufuli Pemba

$
0
0

Jeshi la Polisi Wilaya ya Chakechake, Pemba limezuia kufanyika mkutano na vyombo vya habari wa Chama Cha Wananchi (CUF) uliokuwa umepangwa kufanyika leo wilayani humo, kupisha ziara ya Rais John Magufuli itakayoanza leo.

Rais Magufuli anatarajia kuanza leo ziara yake ya kwanza visiwani humo tangu achaguliwe kuwa Mwenyekiti wa CCM. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Ikulu, Rais Magufuli atazulu Pemba leo na kesho atakuwa Unguja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Shekhani Mohamed Shekhani amesema kuwa zuio hilo la mkutano wa CUF ni kwa sababu eneo wanalotarajia kutumia liko jirani na eneo la uwanja atakaokuwa akihutubia Rais Magufuli.

Hata hivyo, Katibu wa CUF wilaya ya Chake Chake, Saleh Nassor Juma alilalamikia maamuzi hayo ya Jeshi la Polisi kwa madai kuwa wao walitaka kufanya mkutano na vyombo vya habari na sio mkutano wa hadhara. Alisema kuwa tayari walishawaeleza Idara ya Habari Maelezo  na waliridhia.

Alisema mkutano huo na waandishi wa habari ulilenga katika kutoa tamko lao kuunga mkono uamuzi uliochukuliwa na Baraza Kuu la chama hicho kumsimamisha uanachama aliyekuwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba pamoja na viongozi wengine 10.

“Niliwakatalia kwa hoja kwamba mkutano na waandishi wa habari ni haki yetu ya kikatiba na tulikwishawataarifu watu wa Idara ya Habari Maelezo juu ya kikao hicho halali ambacho wao pamoja na waandishi wa habari walithibitisha kuwa watahudhuria,” alisema Nassor.

Idara ya Habari Maelezo ilithibitisha kuwa walikubali kufanyika kwa mkutano huo wa CUF na vyombo vya habari lakini baadae walipokea taarifa ya kuahirisha kupisha ugeni wa Rais Magufuli.

Rais Magufuli Awasili Pemba Kwa Ziara Ya Kikazi Ya Siku Mbili

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Asubuhi ya leo tarehe 02 Septemba, 2016 amewasili Kisiwani Pemba ambapo majira ya Alasiri anatarajiwa kuzungumza na wananchi wa Pemba katika Mkutano wa hadhara utakaofanyika katika uwanja wa Gombani ya Kale kisiwani hapa.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Pemba kwa Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli ameelekea katika kijiji cha Wawi Bigilini kilichopo katika Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba ambako amezulu Kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Marehemu Dkt. Omar Ali Juma.

Dkt. Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli wameweka mashada ya maua katika Kaburi la Marehemu Dkt. Omar Ali Juma na wameshiriki Dua ya kumuombea Marehemu iliyoongozwa na Viongozi wa Madhehebu ya Dini ya Kiislamu na Kikristo.

Akizungumza mara baada Dua, Rais Magufuli amesema anamkumbuka Marehemu Dkt. Omar Ali Juma kwa ukarimu wake, upendo, kutojikweza, kutobagua watu na kudumisha amani katika siku zote za maisha yake.

Dkt. Magufuli ametoa wito kwa Watanzania kudumisha kwa vitendo amani aliyoisimamia Marehemu Dkt. Omar Ali Juma.

"Mimi najua huko aliko Marehemu Dkt. Omar Ali Juma anaendelea kuliombea Taifa hili ili hiyo amani aliyoihubiri katika maisha yake, ili huo upendo aliousimamia katika maisha yake, ili huo uchapa kazi kwa ajili ya manufaa ya watanzania wote tuweze kuendeleza kwa mioyo yetu yote" Amesema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli amewashukuru Wanafamili wa Marehemu Dkt. Omar Ali Juma kwa uvumilivu na ustahimilivu wao tangu walipoondokewa na mpendwa wao.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Pemba

02 Septemba, 2016
.
Rais Magufuli akitazama kikundi cha ngoma baada ya kutua Pemba ambapo pia ameenda kuzulu kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk Omary Ali Juma. Baadaye saa tisa alasiri atafanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Gombani ya Kale, Pemba. Picha na Ikulu

Taarifa Ya Jeshi La Ulinzi La Wananchi Wa Tanzania Kufuatia Habari Iliyoandikwa Kwenye Gazeti La Tanzania Daima

$
0
0

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limesikitishwa na taarifa iliyotolewa na gazeti la Tanzania Daima toleo Nambari 4290 la tarehe 01 Septemba 2016, ikihusisha shughuli za Jeshi hilo zinazoendelea katika maadhimisho ya miaka 52 ya kuzaliwa kwake na shughuli za kisiasa.

Tunapenda  kuwataarifu wananchi kwamba kazi ya Jeshi ni kulinda na kutetea maslahi ya Taifa na mipaka ya nchi, aidha, Jeshi letu linafanya kazi kwa kufuata mila, desturi, nidhamu, kanuni na sheria za Kijeshi kwa weledi wa hali ya juu, hivyo lisihusishwe na propaganda zozote za kisiasa kwani Jeshi letu ni lenye maadili ya kitaasisi ya hali ya juu. 

Jeshi ni taasisi ya dola wala si taasisi ya kiitikadi, kwa maana uhusiano wake na wanasiasa ni wakati linapotetea na kulinda maslahi ya wananchi.  Inaombwa kuwa makini katika utoaji wa maelezo au malalamiko, iachwe mara moja vyama vya siasa kuingilia ratiba za Kijeshi.  

Ikumbukwe kwamba tarehe 25 Julai kila mwaka ni siku ya kuwakumbuka Mashujaa wetu waliolitumikia Taifa hili kwa umakini na nguvu zote kwa kuleta mafanikio tunayoyaona, na hii ilipitishwa mwaka 1979 wakati Majeshi yetu yanarudi kutoka Uganda baada ya ushindi wa vita vya Kagera. 

Sherehe ya mapokezi hayo yalifanyika mji wa Bunazi Wilaya ya Misenye wakati huo Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera ilipoanzishwa kuwa tarehe hiyo iwe siku ya Mashujaa na kupitishwa Kisheria,  ikabaki siku ya tarehe 01 Septemba kuwa ni siku ya kuanzishwa kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, hivyo jana tulikuwa tunasherekea siku ya kuzaliwa JWTZ. Ieleweke hivyo na iachwe mara moja kuchanganya shughuli za Kijeshi na mambo ya Kisiasa, viongozi wa kisiasa wekeni kumbukumbu zenu vizuri.

Jeshi linasisitiza wanasiasa ni vizuri wakasoma vema historia ya nchi wanayotaka kuiongoza na wanayoongoza ili kuepusha upotoshaji, lugha na maneno yanayotolewa na viongozi wa kisiasa wenye matakwa binafsi kuhusisha shughuli za Jeshi na siasa zao yanatia ukakasi na kiungulia, awe makini kuongea vitu ambavyo haelewi na kutokuwa makini zaidi aelewe madhara yanayoweza kutokea kutokana na upotoshaji.

Jeshi letu linafanya shughuli zake ki weredi.

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.

Kwa Mawasiliano zaidi: 0784-477638

Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha tano Awamu ya pili.

$
0
0

Ofisi ya Rais -TAMISEMI inatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya Pili (Second Selection) kwa mwaka 2016. 

Jumla ya wanafunzi 3,918 wakiwemo wasichana 2,413 na wavulana 1,505 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi na wanafunzi ambao hawakuripoti awamu ya kwanza.
 
Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 1,864 wakiwemo wasichana 1,099 na wavulana 765 sawa na asilimia 47.58 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 2,054 wakiwemo wasichana 1,314 na wavulana 740 sawa na asilimia 52.42 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara.
 
Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2015 wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili atakuwa amepoteza nafasi hii.
 
Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya pili mwaka 2016 inapatikana kwenye tovuti ya OR-TAMISEMI ya www.tamisemi.go.tz 

Imetolewa na Katibu Mkuu,
OR-TAMISEMI 


RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 38 & 39

$
0
0

 MTUNZI:Enea Faidy

.....Mr Aloyce bado hakumuelewa vizuri mkewe kwa kauli aliyoisema. Kauli ile iliibua utata mkubwa kichwani mwake na kumtaka mkewe amueleze ukweli.


"Niambie mke wangu... Nini kinaendelea? Maana Mimi sielewi!" Alisema Mr Aloyce kwa sauti ya upole ili mkewe amweleze ukweli wote. Lakini kwa bahati mbaya sana Maimuna alisita kueleza ukweli ambao alitaka kumwambia Mr Aloyce.

Viboko mfululizo vilivyosikika kwa sauti kubwa vilimshukia Maimuna na kumfanya ahangaike kupita kupita kiasi. Aligalagala pale chini kama nyoka aliyepondwapondwa kichwa chake. Sauti na yowe la kilio viliibuka kwa Maimuna kwani alishindwa kuvumilia maumivi ya viboko alivyochapwa na MTU asimfahamu.
"Nasemaaa!nasemaaa!" Alisema Maimuna huku akilia.

Mr Aloyce na Mlinzi wake walibaki na mshangao kwani kila walichokiona walihisi ni muujiza tu. Walibaki kimya huku wakimshangaa mwanamke yule.

"Aloyce... Mimi ni mchawiiii.." Alisikika Maimuna na kwa bahati mbaya sana alishindwa kuongea kwa sauti ndogo hivyo sauti ilipaa sana na kuwafanya wapita njia na majirani kujazana sana nje ya geti  kwa Mr Aloyce. Kwa uzito wa adhabu alioipata Maimuna ilimbidi tu aseme ukweli wote uliomwacha mdomo wazi Mr Aloyce.

"Naitwa Maimuna..  Sio mama yake Eddy kama ulivyodhani..." Alisema Maimuna na kumfanya Aloyce ahamaki. Alichanganyikiwa sana na kushindwa kuzungumza.
"Nisamehe Aloyce... Nilikuja kuiteketeza familia yako.... Mkeo alishaliwa nyama ... Mimi nilikuja kumlinda Eddy ili sehemu zake za siri zibaki mikononi mwa Doreen"

"What? Ati nini? Kwanza Doreen ni nani?" Mr Aloyce alijikuta anauliza maswali matatu mfululizo huku hasira zikiwa zimempanda kupita kiasi. Alitamani achukue jiwe zito na kumponda nalo mwanamke yule.
"Ni mchawi... Alikuwa anasoma na Eddy..." Alisema Maimuna huku akilia kwa sauti kubwa.
"Oh! Shit!" Alisikika baba Eddy.

Watu waliokuwa pale nje walizidi kutafuta upenyo wa kuingia mle ndani. Lakini geti lilikuwa limefungwa, kelele nyingi kutoka nje zilizidi kusikika.

"Mchawiiiiii! Mchawiii! Tufungulie tumwadhibu huyo mchawiiii!! Funguaa! Mwanamke mchawi hafai kuishi!!" Sauti zile kutoka nje zilimhamasisha mlinzi kufungua geti na kuwaruhusu watu waingie. Cha ajabu watu wale waliingia wakiwa wameshikilia silaha za aina mbalimbali. Wengine mawe wengine visu huku wengine wakiwa wameshikilia fimbo na mapanga. Hali ilichafuka sana pale ndani.

 Umati wa watu ulikuwa uvamia uwanja wa Mr Aloyce tayari kwa kumwadhibu mchawi aliyesababisha kilio na majonzi katika familia ya ile iliyokuwa imejaa upendo na amani hapo awali."Tuue tu... Afe Huyo" walisema. Ghafla Maimuna akabadilika na kuwa kiumbe tofauti na vile anavyofahamika wote wakashtuka.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Septemba 3

Magufuli: Sitawavumilia Wachochezi Wanaotaka Kuichezea Amani Yetu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi wananchi wa Kisiwa cha Pemba kutokubali kurubuniwa na watu wanaowachochea kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kuwa vitendo hivyo vinarudisha nyuma juhudi za kuwaletea maendeleo na kutatua kero zinazowakabili.

Rais Magufuli amesema hayo  tarehe 02 Septemba, 2016 wakati akihutubia Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Gombani ya Kale Wilaya ya Chakechake Mkoani Kusini Pemba, ambao umehudhuriwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein.

Rais Magufuli amesema Kisiwa cha Pemba kina fursa nyingi za maendeleo ikiwemo Uvuvi wa baharini, Utalii na Kilimo lakini endapo wananchi wataendelea kushabikia uchochezi na vitendo vya kuvuruga amani vinavyofanywa na baadhi ya watu, hakuna mwekezaji atakayekuwa tayari kuwekeza.

""Hawezi akaja mtu kujenga kiwanda wakati hakuna amani, sisi vijana lazima tuwe mstari wa mbele kujenga amani ili wawekezaji waje wajenge viwanda na tupate ajira.

"Hapa Pemba kuna fukwe nzuri ambazo zinafaa kujenga hoteli kubwa za kitalii, nani atakuja kujenga hoteli kama hakuna amani?" Amehoji Rais Magufuli huku akisisitiza kuwa umefika wakati kwa wananchi wa Pemba kubadilika na kujikita katika masuala ya maendeleo.

Hata hivyo Rais Magufuli ameonya kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haitawafumbia macho watu wanaofanya uchochezi unaolenga kuvuruga amani na ameviagiza vyombo vya dola vianze kuwafuatilia wote walioanza kufanya uchochezi huo.

Amesisitiza kuwa uchaguzi umekwisha na kilichobaki sasa ni kwa watanzania kufanya kazi na kujenga nchi yao.

Mapema akimkaribisha Rais Magufuli kuzungumza na wananchi hao, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amewaambia wananchi wa Zanzibar kuwa tangu aingie madarakani yeye na Rais Magufuli wamefanya mambo mengi kwa manufaa ya Watanzania

Dkt. Shein ameongeza kuwa hali ya Muungano ni nzuri na kwamba sehemu kubwa ya kero za Muungano zimetatuliwa huku akibainisha kuwa kwa sasa kazi iliyopo ni kutafuta changamoto mpya za Muungano zenye lengo la kuchochea maendeleo.

Mkutano huo umehudhuriwa na Mke wa Rais Magufuli Mama Janeth Magufuli na Mke wa Rais Shein, Mama Mwanamwema Shein, Mawaziri na viongozi mbalimbali wa Siasa, Dini na Serikali.

Jioni hii (jana)  Rais Magufuli amewasili mjini Unguja ambapo kesho tarehe 03 Septemba, 2016 ataendelea na ziara yake kwa kuzuru kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amaan Karume, kuzuru kaburi na kutoa mkono wa pole kwa familia ya aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi na baadaye atazungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara utakaofanyika katika Uwanja wa Demokrasia Kibandamaiti Mjini Unguja.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Unguja

02 Septemba, 2016

Waziri Mkuu aitaka Wizara ya Elimu kuongeza wataalamu wa Afya nchini.

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi iweke mpango maalumu wa kuongeza wataalamu zaidi katika sekta ya afya ndani ya nchi ili kuipunguzia Serikali gharama za kusomesha wataalam hao nje ya nchi.

Ametoa agizo hilo Ijumaa, Septemba 2, 2016  wakati alipokagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Kampasi ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na Sayansi ya Tiba Muhimbili (MUHAS) na Ujenzi wa Kituo cha Tiba cha Kimataifa cha Muhimbili katika eneo la Mloganzila.

Amesema Serikali zilizotangulia zimefanya kazi kubwa na nchi imefikia hatua nzuri ya kuongeza wataalam ndani ya nchi ambao watakwenda kutatua changamoto ya upungufu wa madaktari bingwa kwenye hospitali za mikoa na wilaya.

Waziri Mkuu amesema ujenzi wa kituo hicho cha tiba cha kimataifa pia utawapunguzia wananchi adha ya kutafuta fedha za kwenda kupata matibabu nje ya nchi. Tayari upasuaji mkubwa wa magonjwa ya moyo umeanza kufanyika nchini.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Bw. Humphrey Polepole awasake watu wote waliohusika na wizi wa lita 1,000 za mafuta ya kuendeshea mitambo katika karakana ya mkandarasi anayejenga Kampasi hiyo.

“Wafanyakazi waache wizi. Lita 1,000 zinaondokaje katika karakana ya mkandarasi? Hii kampuni inayolinda kama imeshindwa kazi iondolewe na Mkuu wa wilaya usimhurumie mwizi,” amesisitiza.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako amesema kukamilika kwa kampasi ya Mloganzila kutasaidia upatikanaji wa madaktari bingwa wengi nchini ambao watapunguza gharama za kupeleka wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.

Awali, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Ephata Kaaya alisema kukamilika kwa hospitali pamoja na kampasi yote ya chuo kutawezesha kupunguza kwa kiasi kikubwa uhaba wa wataalamu wa afya nchini.

Amesema hospitali hiyo itatumika kutoa huduma za afya za kitaalam zaidi kwa magonjwa mbalimbali, hivyo kupunguza idadi ya wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi kwa matibabu. Pia itapunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Ujenzi wa mradi huo umegharimu Dola za Kimarekani milioni 61, ambapo Serikali imetoa Dola milioni 18 na Serikali ya Korea imetoa mkopo wa Dola milioni 43. Kukamilika kwa ujenzi wa kampasi hiyo ya Mloganzila kutawezesha chuo kuongeza idadi ya udahili wa wanafunzi wa fani ya afya kutoka 4,010 hadi 15,000.

Prof. Kaaya amesema mkataba wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa mradi huo ulisainiwa tarehe 12, Desemba, 2014 na ujenzi ulianza mwezi Julai, 2015 na unatarajiwa kukamilika Oktoba, 2016.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

TCU Yatangaza Kuanza Udahili Awamu ya PILI Kwa Wanafunzi wanaojiunga Vyuo Vikuu Ambao Wamekosa Nafasi Kwenye Awamu ya Kwanza

$
0
0

Tunapenda kuutangazia Umma kuwa tulifunga mfumo wa pamoja wa udahili tarehe 31/08/2016 saa sita usiku ili kuchakata maombi ya waombaji waliofanikiwa kuomba udahili kwa mwaka wa masomo 2016/2017.
 
Hata hivyo kutokana na wengine kushindwa kufanikiwa kutokana na sababu mbali mbali, Tume inatangaza kuwa itafungua maombi kwa awamu ya pili kuanzia tarehe 12 hadi 23 Septemba 2016 ili kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili.
  1. Waombaji watakaokuwa wamekosa nafasi kwenye awamu ya kwanza
  2. Waombaji wa kidato cha Sita walioshindwa kuomba katika awamu ya kwanza
  3. Waombaji wenye vigezo vya Stashahada ambao walishindwa kuomba kutokana na matokeo yao kuchelewa kufika NACTE kwa wakati,
  4. Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya “Cambridge” mwaka 2016 na matokeo yao yameshatoka,
  5. Waombaji waliofaulu mitihani ya RPL,
  6. Waliokuwa wanafunzi wa vyuo vikuu watakao kuwa na uthibitisho toka vyuo vyao vya awali.
 
Baada ya hapo Tume haitaruhusu tena maombi ili kuruhusu taratibu zingine za kiudahili kuendelea kwa ngazi ya Bodi ya Mikopo na vyuoni.
 
Asanteni

Imetolewa na 
Prof. Eleuther Mwageni
 Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania 
02 Septemba 2016

Afikishwa Mahakamani Kwa Kumuita Rais Magufuli ni Kilaza

$
0
0

ELIZABETH Asenga (40), mkazi wa jijini Dar es Salaam amepandishwa kortini jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuandika maneno ya kumkashifu Rais John Magufuli kupitia mtandao wa kijamii wa What’s App.

Akisomewa mashtaka yake na Leonard Chalu, wakili wa serikali, mbele ya Hakimu Huruma Shahidi, mwanamama huyo, alidaiwa kufanya kitendo hicho kilicho kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015.

Wakili Chalu alidai kuwa, mnamo tarehe 06 Agosti mwaka huu, mtuhumiwa huyo aliandika kwenye mtandao wa what’s App ujumbe uliosomeka;

“….Rais kilaza kama huyu wetu, angalia anampa Lissu umashaghuli… f****l** lile, kwanza picha yake ukiweka ofisini ni nuksi tupu na ukiamka asubuhi ukakutana na picha yake, siku yako inakuwa ina mkosi mwanzo mwisho.”

Hata hivyo, mshitakiwa Elizabeth, alikana mashtaka hayo huku wakili wa serikali akidai kuwa, upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Mtuhumiwa alipewa dhamana yenye masharti yanayohitaji wadhamini wawili huku kila mmoja akitakiwa kusaini hati ya shilingi 3 millioni.

Kesi hiyo imeahirishwa na inatarajia kutajwa tena mnamo tarehe 22 Septemba, mwaka huu.

Rais Magufuli ataka Jecha apewe Tuzo ya heshima .........Amtaka Dr Shein Apunguze Upole, Watakaomsumbua Awataje Washughulikiwe

$
0
0
RAIS John Magufuli, amemtaka Dk. Ali Mohamed Shein, kumpa tuzo Jecha Salim, mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar, kutokana na kile alichokiita kazi nzuri aliyoifanya visiwani humo mwaka jana, kwa kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu.

Rais Magufuli aliyasema hayo jana  jioni, katika ziara yake ya kikazi visiwani Pemba. Wakati Rais Magufuli akichaguliwa katika uchaguzi wa Oktoba mwaka jana, Dk. Shein alichaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar kufuatia uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi mwaka huu.

“Nampongeza sana Jecha kwa kazi nzuri aliyofanya kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, na kwa kweli Dk. Shein kama kuna  tuzo zako utakazotoa, naomba usimsahau kumpa na Jecha,” alisema Rais Magufuli.

Rai Magufuli pia alimtaka Rais huyo wa Zanzibar kumtaarifu yeye ili awashughulikie watu wote wanaomsumbua visiwani humo au wanaoonekana kumzidi nguvu.

“Rais Shein kama kuna mtu unaona anakusumbua wewe au anakupa tabu nijulishe mimi tu, hata dakika tano hazitapita nitamshughulikia,” ameeleza.

Kauli hiyo inakuja, ikiwa ni zaidi ya miezi kumi sasa tangu hali ya mahusiano baina ya wananchi wa Zanzibar iwe tete, tangu pale Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi visiwani humo (ZEC) alipotangaza kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Mahusiano hayo mabaya yamesababisha, wafuasi wa vyama vya CUF na CCM vyenye nguvu zaidi visiwani humo, kufikia hatua ya kusitisha ushirikiano katika shuguli za kiuchumi na kijamii ikiwemo kutohudhuria misiba na kutonunua bidhaa za mtu wasiyeendana naye kiitikadi.

“Niombe vyombo vya ulinzi na usalama wafuatilie hao wanaokatakata na kuchoma karafuu washughulikiwe bila huruma. Atakayejaribu kuichezea amani, atacheza yeye tena mchezo asiojua kuucheza,” aling’aka Rais Magufuli.

Tangu kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka jana visiwani Zanzibar, hali ya usalama imekuwa si ya kuridhisha.

Nyumba na mashamba ya karafuu yamekuwa yakichomwa moto, huku baadhi ya watu wakitiwa mbaroni  na vyombo vya dola kwa tuhuma hizo

Hatimaye Shamsa Ford Afunga Ndoa na Chidi Mapenzi

$
0
0
STAA wa Bongo filamu nchini, Shamsa Ford amefunga ndoa na Rashidi Said ‘Chidi Mapenzi’ ambaye ni mfanyabiashara wa maduka ya nguo.

Sherehe za ndoa hiyo zilifanyika nyumbani kwa wazazi wa Shamsa eneo la Sinza, Afrikasana jijini Dar es Salaam.
 
 Awali, Shamsa alidumu katika penzi na Dickson Matoke ‘Dick’ na kufanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume aitwaye Terry na kisha  kufunga ndoa ya kimila nyumbani kwa mwanaume huyo, Tarime mkoani Mara ila baadaye waliachana na kuangukia kwa staa wa Bongo Fleva Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’  ambaye penzi lao halikudumu.


Majambazi Yavamia Chuo Huko Tanga......Mlinzi Auawa, Mabweni Yachomwa Moto

$
0
0

Majambazi zaidi ya 15 yamevamia Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (Sekomu) kilichopo Kata ya Magamba, Lushoto mkoani Tanga na kuua mlinzi mmoja, kumjeruhi mwingine baada ya kumpiga risasi begani, kuchoma mabweni na kuharibu mali za wanafunzi waliokuwepo chuoni hapo.

Tukio la majambazi hao kuvamia chuo hicho limetokea usiku wa kuamkia jana wakati hali ya taharuki ikiwa bado haijasahaulika kwa wakazi wa Vikindu wilayani Mkuranga, Mkoa wa Pwani baada ya usiku wa kuamkia Ijumaa ya wiki iliyopita Kikosi Maalumu cha Jeshi la Polisi cha Kupambana na Uhalifu kupambana na genge la watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi au magaidi waliokuwa wakiishi katika nyumba iliyopo eneo hilo.

Wakati tukio la chuoni hapo nalo likiibua shaka, hofu na maswali baada ya majambazi hayo kutoiba chochote licha ya kutekeleza uhalifu huo, lile la Vikundi ambalo msingi wake ulikuwa ni operesheni ya kuwasaka majambazi waliowaua askari wanne wiki iliyopita waliokuwa wakibadilishana zamu ya kulinda Tawi la Benki ya CRDB lililoko Mbande wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, likiwa limegubikwa na utata na sintofahamu huku Kamanda wa Kikosi Maalumu cha Kuzuia Uhalifu, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Thomas Muniko, akiuawa kwa kupigwa risasi.

Licha ya majambazi hayo kutekeleza tukio hilo baada ya kuvamia na kufunga milango kwa nje na kumwaga mafuta na kuchoma moto mabweni huku baadhi ya wanafunzi wakipiga kelele za kuomba msaada na wengine kufanikiwa kutoka kupitia madirisha ya vyoo, lakini Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, amesisitiza kuwa kilichotokea chuoni hapo ni ujambazi na si ugaidi.

Akizungumzia tukio hilo jana kwa waandishi wa habari akiwa chuoni hapo, Wakulyamba, alithibitisha kuwa lilihusisha majambazi kati ya 10 hadi 15 waliovamia chuoni hapo na kuchoma vyumba vya mabweni mawili tofauti ya wanafunzi.

“Tukio hilo ni la ujambazi na si ugaidi. Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa itakaa kikao na kulijadili tukio hilo kisha tutatoa taarifa,” alisema.

Wakulyamba alisema katika tukio hilo mlinzi mmoja wa chuo hicho, Yohana Shemzigwa (34), aliuawa kwa kupigwa na kitu kizito mgongoni na kichwani huku mlinzi mwenzake, Abuu Rajabu, naye amejeruhiwa na majambazi hayo baada ya kupigwa risasi begani.

Pia alisema kuwa majambazi hayo yaliteketeza kwa moto mabweni mawili na kusababisha magodoro, nguo na simu za viganjani za wanafunzi wa chuo hicho kuungua.

Wakulyamba alisema mmoja kati ya majambazi hayo alijeruhiwa vibaya wakati akitekeleza unyama huo baada ya walinzi wa chuo hicho kutaka kumkamata na amepelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto chini ya ulinzi wa polisi huku akiwa mahututi.

Katika hatua nyingine, alitangaza msako wa kuwasaka majambazi hayo ili kuwafikisha katika vyombo vya sheria ili kujibu tuhuma zinazowakabili.

“Niseme kuwa sisi kama Jeshi la Polisi tutawatafuta wahusika wa tukio hili popote walipo usiku na mchana, wawe mapangoni au nchi kavu lazima tutawakamata na kuwafikisha katika vyombo vya kisheria ili waweze kujibu tuhuma zinazowakabili,” alisema Wakulyamba.

Tukio lilivyotokea
Akisimulia tukio hilo jana mmoja kati ya wanafunzi wa chuo hicho, Elizabeth Thobias, alisema lilitokea saa tano usiku wakati wakiwa mabwenini huku wengine wakijiandaa kwenda kujisomea na kulazimika kutoroka ndani ya mabweni hayo kwa kupitia madirisha ya vyoo.

Elizabeth alisema majambazi hayo yalifika chuoni hapo saa nne usiku na kuanza kuondoa vifaa vya kupoozea moto na kufunga milango kwa nje jambo lililowapa wakati mgumu walipotaka kujiokoa.

“Majambazi hayo yalipofika chuoni kabla ya kuanza kutekeleza ujambazi wao walisikika wakijadiliana kwa kuambiana watuchinje kwanza au watuchome moto, mmoja kati yao alisikika akisema moto tu unawatosha. Baada ya kuanza kuchoma moto ndipo tukaanza kukimbilia na kujiokoa kupitia madirisha ya vyoo vya mabweni,” alisema Elizabeth.

Tanga imekumbwa na matukio kadhaa katika siku za nyuma likiwamo lililotokea Februari, mwaka huu baada ya vikosi vya polisi na vile vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kupambana na majambazi yaliyojificha katika Mapango ya Amboni na tukio jingine lilitokea Mei, mwaka huu baada ya polisi kuwaua majambazi wanne walioweka kambi katika mapango hayo.

Pia wakazi wengine wanane wa jijini Tanga walichinjwa na watu wasiojulikana katika tukio lililotokea Juni, mwaka huu katika Kitongoji cha Kibatini kilichopo Kata ya Mzizima

Rais Magufuli Azuru Kaburi La Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume, Aweka Shada La Maua

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 03 Septemba, 2016 ameendelea na ziara yake Visiwani Zanzibar ambapo majira ya Asubuhi amezuru Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amaan Karume lililopo kando ya Ofisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) eneo la Kisiwandui Zanzibar.

Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli wameweka mashada ya maua katika Kaburi hilo na baadaye wameshiriki Dua ya kumuombea Marehemu Sheikh Abeid Amaan Karume na kuombea amani.

Viongozi mbalimbali wa Dini na Siasa akiwemo Rais Mstaafu wa Sita wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume na familia ya Hayati Sheikh Abeid Amaan Karume ikiongozwa na Mjane wa Marehemu Mama Fatma Karume wamehudhuria.

Baada ya kuzuru kaburi la Marehemu Sheikh Abeid Amaan Karume, Rais Magufuli amezuru kaburi la Rais wa Pili wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi lililopo nyumbani kwake Migombani Zanzibar.

Dkt. Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli wameweka mashada ya maua katika kaburi la Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi na pia wametoa mkono wa pole kwa familia ya Marehemu.

Wakizungumza katika Dua ya kuwaombea Marehemu wote wawili Viongozi wa Dini kutoka madhehebu ya Kiislamu na Kikristo wameomba kuwepo kwa amani na upendo kwa watanzania wote kama ambavyo waasisi wa Taifa walipigania.

Baadaye leo Rais Magufuli atazungumza na Wananchi wa Zanzibar katika Mkutano wa hadhara utakaofanyika katika uwanja wa Demokrasia wa Kibandamaiti Mjini Zanzibar.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Unguja


03 Septemba, 2016
.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Pombe Magufuli akitoa heshima zake baada ya akiweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume katika ofisi Kuu ya CCM Makao Kisiwandui mjini Zanzibar leo Agosti 3, 2016.
 Mama Janeth Magufuli, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Pombe Magufuli,  akiweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume katika ofisi Kuu ya CCM Makao Kisiwandui mjini Zanzibar leo Agosti 3, 2016.
 Mama Janeth Magufuli, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Pombe Magufuli,  akitoa heshima baada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume katika ofisi Kuu ya CCM Makao Kisiwandui mjini Zanzibar leo Agosti 3, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Pombe Magufuli,  na viongozi wengine wakiomba dua bada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume katika ofisi Kuu ya CCM Makao Kisiwandui mjini Zanzibar leo Agosti 3, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Pombe Magufuli,  na viongozi wengine wakiomba dua bada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume katika ofisi Kuu ya CCM Makao Kisiwandui mjini Zanzibar leo Agosti 3, 2016.Picha na Ikulu

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 4

Rais Magufuli aahidi kulinda Muungano na kudumisha amani.

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wananchi wa Zanzibar kuwa atasimamia kwa nguvu zote masuala yote yanayohusu maendeleo, kudumisha Muungano wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar na kudumisha amani kwa faida ya wananchi.

Rais Magufuli amesema hayo jana tarehe 03 Septemba, 2016 alipokuwa akizungumza na wananchi wa Zanzibar katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Kibandamaiti Mjini Unguja.

Dkt. Magufuli ambaye aliongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli alisema ili mambo hayo yafanikiwe Wananchi wa Zanzibar hawana budi kukataa kujihusisha na vitendo vya vurugu na kuvunja amani na amewaonya watu wanaochochea vitendo hivyo kuacha mara moja.

Aliwataka wananchi wa Zanzibar kujihadhari dhidi ya wanasiasa ambao wanapandikiza chuki, ubaguzi na fitina, kwani watu hao wanataka kubomoa misingi mizuri ya umoja, upendo na mshikamano wa Taifa uliojengwa na waasisi wa Taifa hili.

Rais Magufuli alimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein aliyehudhuria mkutano huo, kwa hatua mbalimbali anazozichukua kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar huku akibainisha kuwa tatizo la maji linalovikabili visiwa vya Zanzibar litakwisha baada ya kutekelezwa kwa mradi mkubwa wa maji utakaofadhiliwa na Serikali ya India kwa gharama ya Dola za Marekani Milioni 92, na mradi mwingine utakaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa gharama ya Dola za Marekani Milioni 21.

Aidha, Rais Magufuli alivipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kazi nzuri vinayofanya katika kusimamia amani visiwani humo huku akivihakikishia kuwa yeye akiwa kiongozi wao anawaunga mkono.

Pamoja na Rais Shein Mkutano huo ulihudhuriwa na Mke wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume, Mawaziri na Viongozi wa Siasa na Dini.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Unguja

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images