Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wakurugenzi Watano Tpdc Wasimamishwa Kazi Kupisha Uchunguzi


Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi

$
0
0

POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na kupiga risasi hewani akiwa wodini katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga na kusababisha taharuki kubwa kwa wagonjwa na wauguzi.

Kitendo cha askari huyo kilizua taharuki kubwa kwenye wodi namba tisa ya wanawake na watoto, ambapo akinamama walipiga mayowe kwa hofu huku wakikimbia na kujificha kwenye chumba cha muuguzi wa zamu wakiwaacha watoto wao vitandani.

Akizungumza  kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha kutokea kwa tukio hilo  na kueleza kuwa lilitokea jana alfajiri.

“Chanzo ni ulevi wa kupindukia tulimpima kipimo kikaonesha kiwango cha ulevi kilikuwa juu kupita kiasi alama zikiwa 300 huku kiwango cha kawaida cha kipimo ni alama kati ya 70 na 40 …. Katika tukio hilo hakuna aliyejeruhiwa na bunduki yake ilikuwa na risasi 10,” alisema.

Kamanda Kyando alisema siku ya tukio, askari huyo akiwa na mwenzake walikuwa kwenye lindo akilinda makazi ya Kamanda wa Magereza wa Mkoa, lakini alitoroka lindo na kwenda hospitalini wodi namba tisa, ambako mkewe alikuwa akimuuguza mwanawe aliyekuwa amelazwa hapo kwa matibabu.

Mke wa mtuhumiwa huyo, Theresia Kalonga ambaye naye ni askari Magereza, alikuwa amelazwa na mtoto wao wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 10.

“Mtuhumiwa huyo tunamshikilia huku taratibu za kumkabidhi kwa Kamanda wa Magereza Mkoa wa Rukwa ili aweze kushtakiwa kwa taratibu za jeshi lao kabla ya kufikishwa kwenye mahakama za kiraia, zinaendelea,” alisisitiza Kamanda Kyando.

Akizungumza hospitalini hapo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk John Gurisha alisema askari huyo baada ya kuingia wodini, aliweka silaha yake chini akafunua chandarua na kuanza kuzungumza na mwanawe, kisha katoka nje na kufyatua risasi hewani na kutoboa paa.

“Mtuhumiwa huyo alizua kizaazaa kwani askari wetu waliokuwa lindo hapa hospitalini walilazimika kukimbia ili kuokoa maisha yao baada ya kusikia mlio huo wa risasi na kumuona askari huyo akielekea walipokuwa wamekaa,” alisema na kuongeza kuwa askari huyo aliletwa hospitalini hapo na mwendesha bodaboda ingawa hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa, lakini alisababisha taharuki kubwa hospitalini.

“Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) waliwahi kufika hospitalini hapo na kumtia nguvuni, na bunduki yake ilipokaguliwa ilikutwa ikiwa na risasi kumi,” alisema.

Muuguzi wa zamu wodini humo, Rose Katabi alisema askari huyo alipofyatua risasi akinamama wodini humo walianza kupiga mayowe ya kuomba msaada huku wakikimbia na kuwaacha watoto wao vitandani na kuvamia chumba cha muuguzi kwa ajili ya kusalimisha maisha yao.

“Kwanza kitendo cha kumuona askari huyo akiwa na silaha mkononi, mwili wangu wote ulikufa ganzi nilihisi atatulipua kwa kutupiga risasi za moto …aliiweka silaha yake hiyo chini na kuanza kuzungumza na mwanawe. Aliniuliza kama mtoto wake ameshakunywa dawa, nikamjibu anakunywa dawa mara moja usiku.

“Waliingia walinzi wetu wawili wodini ndipo akaanza, kusema atarudi tena, akatoka nje akiwa katikati ya mlango wa wodini alikoki bunduki yake na kufyatua risasi hewani iliyotoboa paa kisha akaondoka na kutokomea gizani,” alisema.

Kwa upande wa mke wa mshtakiwa huyo, Theresia alisema alipomuona na sare za jeshi na silaha mkononi alimtaka arudi mara moja kazini. 

Walinzi waliokuwa kwenye lindo katika lango kuu la kuingia hospitalini hapo kwa masharti ya kutoandikwa majina yao , walidai kuwa askari huyo alifikishwa hospitalini hapo kwa usafiri wa bodaboda.

“Alitutia shaka baada ya kukataa kusimama, kwani alipitiliza moja kwa moja akiwa na silaha mkononi, tulijawa na hofu kubwa tukaamua kumfuata kwa nyuma hadi akaingia wodi namba tisa alikolazwa mkewe na mtoto wake. Lakini tulipomuona akikoki bunduki yake tulilazimika kukimbia na kwenda kujificha ndipo tukasikia mlio wa risasi,” alisema mmoja wao.

Magufuli: Ni Muujiza Kushikana Mkono na Lowassa

$
0
0

Rais Magufuli amesema anashukuru hafla ya Jubilei ya Miaka 50 ya ndoa ya Rais mstaafu Benjamin Mkapa kuleta muujiza wa kukutana na kupeana mkono na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa

Kauli hiyo aliitoa jana katika hotuba yake Baada ya kumalizika kwa misa takatifu ya maadhimisho ya Juibilei hiyo iliyofanyika katika kanisa la mtakatifu Petro  Oysterbay, Dar es Salaam

==>Msikilize hapo chini akiongea

Godbless Lema Agoma Kula Kwa Saa 48

$
0
0

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ( Chadema) anayeshikiliwa katika mahabusu ya kituo kikuu cha Arusha Mjini amegoma kula kwa zaidi ya saa 48 sasa tangu alipokamatwa

Lema alikamatwa juzi alfajiri akiwa nyumbani kwake Njiro Arusha kwa tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi  na kushawishi watu kwa njia ya mtandao waandamane Septemba mosi.

Jana Meya wa Arusha, Calist Bukhay alisema Lema amegoma kula

Alisema Lema aligoma kula akidai kuwa alifanyiwa udhalilishaji mbele ya watoto wake wakati polisi walipokuwa wakitekeleza agizo la kumkamata.

"Ni kweli amegoma kula tangu jana (juzi) alipokamatwa.Alisema askari polisi walipkwenda kumkamata walimfanyia vitendo vya udhalilishaji mbele ya watoto wake na kumnyanyasa bila kujali yeye ni kiongozi wa wananchi.

"Sasa  yeye ameshikilia msimamo wake kuwa kwa kuwa polisi walikuwa wamepanga kumuua wakati wa kumkamata, basi ni bora akafa kwa njaa.

"Chakula kimekuwa kikipikwa na kupelekwa na mkewe ,lakini bado amegoma kukila.Baada ya tukio hilo, polisi walituita ili kujaribu kumshawishi ale mchana, akagoma" Alisema Meya Calist.

Waziri Lukuvi: Serikali Tumedhamiria Kumaliza Migogoro Ya Ardhi

$
0
0
 Na Sheila Simba- MAELEZO
Waziri wa Aridhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema kuwa Serikali imeanza kazi ya kupima ardhi  nchi nzima kuanzia mkoani Morogoro.

Akizungumza  katika kipindi kipya cha "TUNATEKELEZA" kinachoandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO na TBC1 ,alisema utekelezaji wa zoezi hilo umeanzia mkoani humo ili kupima maeneo ya wakulima na wafugaji na kutatua migogoro ya ardhi Mkoani humo.

“Serikali tumedhamiria kumaliza migogoro ya ardhi, kutimiza ndoto ya Rais Magufuli ya kuondokana na migogoro ya ardhi isiyo na tija inayosababisha watu kupoteza maisha’’Alisema Lukuvi

 Ameongeza kuwa katika upimaji huo wa ardhi serikali inashirikiana na kampuni binafsi zilizosajiliwa ili kumuwezesha mwananchi anayemiliki shamba,kiwanda ,mkulima na mfugaji mwenye eneo  kupimiwa na kuongezewa thamani.

 “Nakuhakikishia katika kipindi cha miaka 10 kila kipande cha ardhi Tanzania kitakuwa kimepangwa na kupimwa utaratibu mzuri utakao mwezesha kila mtumiaji wa ardhi kutumia eneo lake”alifafanua Lukuvi.

Pia ameeleza suala la kuthibiti bei ya kupima ardhi kwa kushirikiana na wapimaji binafsi katika kumfanya kila mtanzania alipe bei halali ya kupima ardhi.

Aidha amesme kuwa Serikali itaweka ukomo wa kumiliki ardhi ili kuondoa tabia za watu kumiliki eneo kubwa la ardhi bila ya kuliemdeleza kwa muda mrefu.
“serikali itaweka muda wa mtu kumiliki ardhi, haiwezekani mtu mmoja amiliki eneo hata bila kulitumia, tabia hii itafika mwisho.”

Akizungumzia suala la wageni kumiliki ardhi alisema kuwa ni marufuku kwa wageni na wawekezaji kununua ardhi vijijini bila kupitia wizara inayohusika.

“Ni marufuku kwa mgeni au mwekezaji kwenda kijijini kununua ardhi bila kuja kwangu au Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),wakifanya hivyo tutawapa ardhi wawekeze, Pia mtu yeyote anayetaka kujenga kiwanda popote afike ofisini kwangu nitampatia ardhi ndani ya siku saba.”alisema Lukuvi

Ameongeza kuwa  Wizara imetenga viwanja 240 kwa ajili ya Viwanda enoa la Kigamboni ili kutimiz lengo la Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.

Mbali na hayo Waziri Lukuvi alisema  wananchi wote waliodhulumiwa viwanja Jijini Dar es Salaam kwa makosa ya watendaji wa Serikali wameanza kupewa  viwanja vingine mbadala.

“Naagiza Halmashauri zote ziwapatie viwanja mbadala wananchi ambao walidhulimiwa viwanja vyao kwa makosa ya watendaji.”


MWISHO

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu ya Agosti 29

Ufafanuzi wa CHADEMA kuhusu taarifa ya kuahirishwa Operesheni UKUTA.

$
0
0

CHADEMA inapenda kutoa taarifa kwa umma kuhusu andiko linalosambazwa mitandaoni likimnukuu Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe kuwa ameahirisha Operesheni UKUTA na maandalizi ya Septemba 1.

Tunaomba umma upate taarifa sahihi kuwa Mwenyekiti Mbowe hajafanya mkutano na waandishi wa habari mahali popote pale kuzungumzia kuahirisha Operesheni UKUTA inayoendela nchi nzima wala kuzuia maandalizi ya Septemba 1.

Kupitia taarifa hii, chama kinawataka viongozi, wanachama, wafuasi, wapenzi na mashabiki wa CHADEMA na Watanzania wote wazalendo na wapenda haki, kupuuza andiko linalosambazwa mitandaoni .

Msisitizo unaendelea kutolewa kuwa Operesheni UKUTA ambayo imelenga kusimamia utawala unaoheshimu Katiba ya Nchi na kulinda sheria na maandalizi yanaendelea nchi nzima.

Imetolewa na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Profesa Lupumba,Magdalena Sakaya na Abdul Kambaya Wavuliwa Uanachama CUF

$
0
0
Chama Cha Wananchi (CUF) kimewasimamisha uanachama aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wa chama hicho upande wa Bara, Magdalena Sakaya.

Uamuzi huo umetolewa jana na Baraza Kuu la Chama hicho lililofanya mkutano wake visiwani Zanzibar kwa lengo la kuwajadili wanachama kadhaa wakiwemo vigogo hao. Sakaya amevuliwa nyadhifa zote ndani ya chama kabla ya kusimamishwa.

Taarifa kutoka ndani ya Mkutano huo zimeeleza kuwa Baraza hilo limewaadhibu wanachama 15 wakiwemo Sakaya ambaye pia ni mbunge wa Kaliua.

Mbali na vigogo hao, wengine waliopigwa rungu na Baraza Kuu la CUF ni pamoja na Katibu wa Baraza la Wazee, Shashi Lugeye, Thomas Malima na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Abdul Kambaya.

Aidha, Baraza hilo limemsimamisha uanachama Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftah Nachuma. Hatua hii inaweka matatani ubunge wa Sakaya na Nachuma kwani wakifikia hatua ya kufukuzwa watakosa sifa za kuendelea kuwa wabunge.

Lipumba na Sakaya hawakupata nafasi ya kujitetea kutokana na kutohudhuria mkutano huo wakati Shashi alipata nafasi ya kujitetea kutokana na uwepo wake lakini utetezi wake haukuzaa matunda. Katiba ya chama hicho haiwapi nafasi wabunge hao kukata rufaa kutokana na uamuzi wa Baraza hilo.

Uamuzi huo umekuja ikiwa ni siku chacha baada ya Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho uliolenga kumchagua Mwenyekiti Mpya kuvunjika kutokana na kuwepo vurugu kubwa baada ya Profesa Lipumba kuingia ndani ya ukumbi huo na wafuasi wake wakitaka barua yake ya kutaka kurejea kwenye nafasi yake ijadiliwe na kukubaliwa.

Hata hivyo, kura zilizopigwa na wajumbe wote zaidi ya 800, ni kura 14 pekee zilizotaka Profesa Lipumba aendelee na nafasi ya uenyekiti.

Lema Aendelea Kugoma kula akiwa mahabusu......Mwanasheria Wake Kufungua Kesi Mahakama Kuu Leo

$
0
0

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), ameendelea kugoma kula kwa siku ya tatu mfululizo tangu alipokamatwa Oktoba 26 mwaka huu, nyumbani kwake mjini hapa, akidaiwa kutoa maneno ya uchochezi.

Lema alikamatwa siku hiyo saa 12 alfajiri akiwa nyumbani kwake, Njiro,  na hadi sasa anashikiliwa katika mahabusu ya kituo kikuu cha polisi mjini Arusha.

Kutokana na kuendelea kugoma kula, Wakili wake, John Mallya amesema leo saa sita mchana atakwenda Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha kufungua kesi ya kutaka mteja wake afikishwe mahakamani.

Malya jana alisema katika kesi hiyo atashirikiana na Chadema kuwashtaki mwendesha mashitaka mkuu wa Serikali na mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai, Mkoa wa Arusha.

Tangu mbunge huyo akamatwe amegoma kula kwa  kile anachodai kupinga udhalilishwaji aliofanyiwa na polisi wakati wa kukamatwa.

Pia, Lema anasema alinyanyaswa mbele ya watoto wake nyumbani kwake huku wakijua yeye ni kiongozi na amechaguliwa na wananchi.

Neema, mkewe Lema,jana alithibitisha kwamba  mumewe amegoma kula.

“Anaendelea kugoma kula mpaka sasa kwa sababu  hata sasa nimetoka polisi asubuhi kumpelekea chakula, lakini amekataa kula.

“Lakini nilipouliza pale polisi kuwa wanampeleka lini mahakamani, nilijibiwa wanaendelea kumhoji,”alisema Neema.

Juzi, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alithibitisha kukamatwa kwa Lema na kueleza kuwa alihojiwa dhidi ya matamshi ya uchochezi na kuwa atafikishwa mahakamani baada ya kukamilika   uchunguzi.

Kwa mujibu wa Kamanda Mkumbo, Lema anatuhumiwa kuwachochea wakazi wa Arusha kuandamana Septemba mosi, mwaka huu kuhamasisha kile kinachoitwa Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta).

Msekwa:watanzania Waache Kufuata Mkumbo

$
0
0
Na Fatma Salum na Sheila Simba, MAELEZO 
Spika wa zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pius Msekwa amewaasa watanzania kuacha kufuata mkumbo wa kisiasa badala yake watii mamlaka ili kuepuka kuvunja sheria na kuleta madhara kwao binafsi na taifa kwa ujumla.

Msekwa aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia masuala mbalimbali kuhusu mwenendo wa siasa za hapa nchini na utendaji kazi wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Alieleza kuwa watu wengi wana hulka ya kufuata mkumbo kwenye mambo fulani bila ya kuchunguza na kufahamu ukweli wake kabla ya kushabikia.

“Ni hulka ya watanzania kushabikia mambo wasiyoyafahamu ilimradi tu yanawafurahisha masikioni   au machoni mwao kwani hata huko mitaani wanakimbilia ngoma bila ya kujua inatokea wapi au inaelekea wapi, hivyo nawasihi wajaribu kuwa makini na mbinu za siasa zinazotumiwa na baadhi ya vyama kwa kuwa nyingine zina madhara ndani yake.” Alisema Msekwa.

Akifafanua mwenendo wa siasa za hapa nchini, Mzee Msekwa alisema kuwa bado wanasiasa wengi hawafuati kanuni za ushindani wa kisiasa katika kutafuta madaraka badala yake wanatumia mbinu ambazo zinavunja sheria za nchi na hatimaye wanapambana na mamlaka.

“Ushindani wa kisiasa ni jambo la kawaida na linalokubalika ingawa ushindani huo ni lazima ufuate sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa ili kufikia lengo, hivyo kubuni vitu ambavyo vinachochea utovu wa nidhamu na uvunjifu wa amani sio jambo zuri, ' alisisitiza.

Aidha, Msekwa alieleza kuwa utendaji wa Mhe. John Magufuli ni wa kuridhisha na wa aina yake kwa kuwa amekusudia kuleta mabadiliko chanya kwa watanzania na kuondoa mfumo wa utendaji kazi kwa mazoea jambo ambalo limesaidia kurudisha nidhamu kwa watumishi wa Serikali.

Akizungumzia uzoefu wake katika masuala ya kuongoza Bunge, alieleza kuwa tofauti ya Bunge la zamani ni kwamba lilikuwa na nidhamu kubwa na linaheshimika lakini Bunge la sasa halina utii na hicho ndio chanzo cha malumbano yanayojitokeza mara kwa mara katika vikao vya Bunge.

Aliongeza kuwa tangu awali wapinzani kazi yao ni kuipinga Serikali iliyo madarakani lakini kwenye Bunge la uongozi wake walikuwa wakipinga kwa kutumia hoja na kufuata kanuni bila ya kudharau mamlaka ya Spika wala Serikali iliyoko madarakani.

“Kanuni zinatoa nafasi kwa mbunge asiyeridhika na maamuzi ya Spika kushitaki kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge, na kamati hiyo itasikiliza na kutoa uamuzi kama mahakama inavyosikiliza lakini wabunge wa sasa hawataki kutumia utaratibu bali hutumia mbinu za tofauti ili waweze kupata sifa ambazo hazina tija kwa wananchi waliowachagua,” alisema.

Msekwa pia amewaasa vyama vya upinzani kutumia mbinu nzuri katika kutafuta madaraka bila ya kuvunja sheria au kuhatarisha amani ya nchi kwani waliowachagua wanategemea zaidi matokeo ya kazi waliyoahidi kuwatumikia kuliko malumbano yasiyo na tija kwa ustawi wao na taifa.

mwisho

Wasomi: JPM Na Lowassa Wameonyesha Kuwa Mazungumzo Yataleta Muafaka.

$
0
0
Na Tiganya Vincent
Wasomi na Wanazuoni mbalimbali wamepongeza hatua ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu zamani  Edward Lowassa kushikana mikono na kusalimiana wakati wa Jubilei ya dhahabu ya miaka 50 ya ndoa ya Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa na Anna Mkapa.

Wanazuoni hao wametoa  kauli hiyo jana katika mahojiano maalum na Idara ya Habari iliyokuwa ikitaka kupata maoni yao kuhusu kitendo kilichoonyeshwa na viongozi hao kwa jamii.

Profesa Kitila Mkumbo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alisema kuwa hatua hiyo imeonyesha kuwa huo ndio Utanzania ulivyo wa kutofautiana bila kugombana.

Alisema kuwa kitendo hicho kimewaonyesha wananchi kuwa mazungumzo yana nafasi kubwa ya kuondoa tofauti zilizopo kuliko kutumia njia nyingine kama vile maandamano na mabavu katika kutafuta ufumbuzi wa baadhi ya matatizo.

“Kukutana kwa viongozi hao na kupeana mikono wakati wa kusalimiana kunakumbusha utamaduni wetu uliojingekea toka siku nyingi wa kutatua matatizo yetu kwa mazungumzo bila kugombana au kutumia mabavu,”alisema Profesa Mkumbo.

Kwa upande wa Profesa Joseph Semboja alisema kuwa amefurahishwa sana na kitendo kilichoonyeshwa na viongozi hao kwani kimeuonyesha ulimwengu kuwa Watanzania ni watu wenye  Amani na upendo.

Alisema kuwa hatua hiyo imeonyesha kuwa Watanzania wanaweza kuwa na tofauti lakini wakaendelea kuishi pamoja na kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii kwa ajili ya maendeleo yao na Taifa lao.

Profesa Semboja aliwataka wananchi kujifunza kutokana na kitendo kilichoonyeshwa na viongozi hao ambao wameonyesha kuwa ni lazima wakae pamoja kwa ajili kushughulikia mambo muhimu ya maendeleo ya wananchi badala kuendeleza tofauti ambazo hazina manufaa kwa Watanzania.

Alisema kuwa ipo haja ya kwenda zaidi ya hapo kwa kuweka utaratibu wa kukaa pamoja na kujadiliana ili kutatua vyanzo vya migogoro kwa ajili ya mustakabali mzuri wa Taifa hili.

Profesa alisema kuwa sio sahihi kutumia mfumo wa jino kwa jino kwani utaratibu huo ndio unaoweza kusababisha kukua zaidi kwa migogoro na wakati mwingine unasababisha umaskini kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kwani muda mwingi wananchi hawana muda wa kushiriki katika shughuli za maendeleo kwa sababu ya migogoro.

Naye Profesa Samwel Wangwe alisema kuwa hatua ya viongozi hao kukutana na kupeana mikono ni ishara kwa Watanzania kujifunza kuwa mazungumzo yana nafasi kubwa katika kuleta muafaka mgogoro wowote kuliko kutunishiana misuli.

Alisema kuwa mazungumzo yana nguvu kubwa katika kuleta upatanishi katika migogoro mbalimbali inatokea katika jamii kuliko kutumia njia nyingine ambazo zinaweza kusababisha vurugu na uharibifu wa mali za watu na upotevu wa maisha ya watu.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali aVItaka vyama vya siasa kuheshimu tamko la polisi

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju aonya vyama vya siasa kutumia maneno yanayovunja amani na usalama wa nchi.

Masaju ambaye amezungumza na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es salaam leo, ametolea mfano Oparesheni UKUTA iliyotangazwa kufanywa na CHADEMA na kusema kuwa ina maneno ya kijeshi yanayotumiwa kwenye shughuli za kihalifu.

Amesema neno UDIKTETA siyo sahihi kwa kuwa nchini Tanzania hakuna udikteta kwa kuwa serikali inafanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria na nchi inaendeshwa kwa kuzingatia mgawanyo wa madaraka wa katika miimili yote mitatu ya dola.

“UKUTA lengo lake ni nini, ni sawa na kuwatenganisha wananchi na serikali yao” Amesema Masaju na kuwataka wananchi kutambua kuwa Septemba Mosi ni siku ya Majeshi nchini huku akishangazwa na CHADEMA kuchagua siku hiyo kuzindua kampeni yao aliyodai kuwa ina lengo la kuvuruga nchi.

Masaju amewataka viongozi wa vyama vya siasa nchini kutii mamlaka za dola ikiwemo Jeshi la Polisi na mahakama iliyowapa mwongozo juu ya ombi la kupinga zuio la jeshi la polisi na pia kufuata ushauri waliopewa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora juu ya kutokuwepo kwa udikteta nchini.

Amesema sababu kuu za kuzuia Oparesheni ni mbili ambazo ni hali ya usalama kutokuwa shwari, pamoja na kutokuwepo kwa udikteta nchini.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 31 & 32 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0

Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa


Ilipoishia...
Emmy akanikaribisha kwenye sehemu anayo ishi ambayo yenye vitu vingi vya dhamani ya hali ya juu.Taratibu emmy akaanza kuvua nguo zake moja baada ya nyingine na kunifanya nibaki nikiwa nimemshangaa kwani sikujua ana maana gani na imekuwaje amevua nguo mbele yangu na kubakiwa na chupi wakati mimi na yeye hatuna mahusiano ya namna yoyote

Endelea...
Emmy akachukua taulo na kujifunga kisha akaingia bafuni na kuniacha mimi nikiwa nimekaa kwenye sofa nikiyatadhimini mazingira ya ndani kwake.Baada ya muda kidogo emmy akatoka bafuni.

“umeshindwa hata kuwasha tv?”
“ahaa hakuna tatizo sana”
“ok ngoja nivae nguo tuelekee hospitalini ukamuone mama”
“sawa”
“ila unajua wodi aliyo lazwa?”
“hapana siijui”
“ok basi tutajua huko huko”

Emmy akaingia ndani kwake na akatoka akiwa amevalia mavazi mazuri kiasi kwamba tamaa za mapenzi zikaanza kunitawala na kujikuta nikimtazama emmy kwa macho ya matamanio
“eddy twende zetu”
“mmmmm”
“twende zetu mbon unanishangaa?”
“ahaa hakuna kitu”

Nikanyanyuka na nikatangulia kutoka nje ila kutokana na baridi kali ikanilazimu kumuomba emmy koti na akarudi ndani na kunichukulia koti lake kubwa na sote tukaingia kwenye lifti na kushuka chini gorofani.
“twende huku kwenye maegesho ya magari”
Tukafika sehemu yenye maegesho ya magari mengi na emmy akafungua gari moja na kuniomba niingie.Safari ikaanza huku kila mmoja akiwa kimya ndani ya gari ila emmy akaamua kuvunja ukimya.

“hivi tanzania wewe unafanya kazi?”
“mimi ni mwanafunzi wa a leve bado”
“ohh kumbe unasoma?”
“ndio”
“kombi gani?”
“pcb”
“mungu wangu pcb wewe....Mbona unaonekana kama hkl?”
“hahaa pcb  halisi...Aafu mbona ndege leo imetua kwenye uwanja wa maputo international airport imekuwaje kutokana tumetua mozambique?”

“ndege ilipata itilafu kwa watu kama sisi tunao jua ndio tumegundua hilo ila ukiwa ni mgeni huwezi kujua kama ndege imeshindwa kuendelea na safari”
“sasa si wangetulipa fidia kwa kwa abiria inakuwaje ndege inakuwa haina uwezo wa kumaliza msafara wake?”
“mimi niliamua tuondoke kutokana wewe umeseme unahitaji kumuona mama yako ila kwa walio baki wakisubiria ndege kutengenezwa watakuwa wamelipwa fidia na kama siku ukiondoka utakwenda kupanda ndege uwanja wa kimataifa wa cape town”
“sawa”

Safari ya kwenda hospitalini haikuchukua muda sana hii nikutokana na wingi wa barabara nyingi zinazo punguza msongamano wa magari.Tukafia hospitalini na moja kwa maja emmy akaenda kwenye katabu kinacho onyesha orodha ya wagonjwa waliopo hapa hospitalini na nikamtajia jina la mama kishha akatumi kama dakika tano kulitafuta na akalipata.

“kumbe mama yako ni waziri?”
“ndio”
“twende ukamuone”
“moja kwa moja tukealekea kwenye chumba alicho lazwa mama na kabla hatujaingia nikamkuta askari mmoja akiwa amesimama nje ya chumba alicho lazwa mama

“hamuruhusiwi kuingia humu ndani nyinyi ni kina nani na munahitaji nini?”
“mimi naitwa dokta emmy samson na mfanyakazi wa hii hospitali”
“naomba kitambulisho chako”
Emmy akatoa kitambulisho chake na kumpa askari aliye simama mlangoni na akakisoma kwa muda kisha akamrushu emmy kuingia ndani na mimi nikataka kuingia ndani ila akanizuia kuingia
“na wewe ni nani?”
“mimi ni mtoto wa huyo mama huko ndani?”
“mbona hatuna maelezo ya aina yoyote kuhusiana kama mgonjwa ana mtoto?”

“mimi ni mwanaye unadhani nitafunga safari kutoka tanzania hadi hapa nije kujipendekeza kwa mama yangu?”
Nilizungumza kwa hasira kiasi kwamba watu walipo karibu na eneo la mlango wa kuingia kwenye chumba alicho lazwa wakaanza kunishangaa
“eddy kuwa mpole ngoja nikamuone mama”
“kijana ninakuoma usimame mbali na hili enoa la sivyo nitakuitia walinzi waje wakutoe”
“eddy tafadhali nakuomba uwe mpole nitazungumza na mama na utamuona tu”

Nijaitahidi kutulia hasira zangu na kusimama pembeni kidogo na chumba alicho lazwa mama huku sura yangu ni kiwa nimeikunja.Emmy akaingia ndani ya chumba na baada ya muda akatoka na kumnong’oneza askari kisha kwa ishara emmy akaniita na nikanyanyuka kwa haraka hadi sehemu waliyo simama kisha askari akaniruhusu kuingia ndani.Macho yangu yakatizamana na mama ambaye kwa muonekana hali yake sio nzuri sana japo nimemkuta amaekaa kitako kwa mwendo wa haraka nikamfwata mama na kumkumbatia huku machozi yakinimwagika.

Tukabaki tumekumbatiana na mama ndani ya dakika kadhaa kisha nikamuachia na kuiona sura yake ikiwa imelowana kwa machozi mengi,mama akanishika mashavuni na kunibusu kwenye paji la uso huku akinichunguza sehemu mbali mbali za mwili mwangu na kunifanya nizidi kububujikwa na machozi
“eddy ni nini kilicho kupata mwanagu?”

Mama aliniuliza huku akiwa anabubujikwa na machozi kiasi kwamba nikashindwa kulijibu swali lake hadi ndani ya dakika tano ndipo nikaanza kumuadisia kila kitu kilicho tokea na jinsi baba alivyo nifanyia kiasi kwamb hadi ninamalizia nikamshuhudia emmy akiinama chini huku akitokwa na machozi.
“eddy mwanagu nakuomba unisamehe”
“nikusamehena nini mama?”
“eddy najua siku zote ulikuwa unahitaji kujua ukweli juu ya baba yako na mimi nikawa nimekuficha ila....”
“mama nimesha lijua hilo kuwa pacha wa baba ndio baba yangu”

“nani amekuambia hivyo?”
“mama dunia haina siri tena hili swala nimeambia na mtu baki kabisa tena ni muandishi wa habari”
“basi eddy tuliache hilo mwanagu kwa maana unazidi kunipa uchungua katika hilo”
Ikanibidi nibadilishe mada ya kuzungu na kuzungumza na kuanza kupiga story za kupoteza mawazo hadi mama na emmy wakaanza kucheka ila sikumuambia mama kuhusiana na swala la shule yetu kuingia kwenye matatizo.

==>Endelea Nayo <<Kwa Kubofya Hapa>>

Waziri wa Habari Nape Nnauye amevifungia vituo vya redio vya Magic FM na Redio 5 ya Arusha kwa madai ya uchochezi.

$
0
0

WAZIRI wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye amezifungia radio mbili kwa muda usiojulikana kwa makosa ya kuandaa vipindi ambavyo vimerushwa hewani vinavyoashiria uchochezi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri Nape amesema kuwa uamuzi wa kuvifungia vituo hivyo umefikiwa baada ya kujirdhisha kuwa kipindi cha Matukio kilichorushwa Agosti 25, 2016 muda wa saa 2 usiku hadi saa 3 na kituo cha utangazji cha Radio 5 pamoja na kipindi cha Morning Magic katika kipengele cha Kupaka Rangi Agosti 17 vilikuwa na maudhui ya uchochezi unaoweza kuleta uvunjifu wa Amani.

Nape amesema kuwa kufuatia hilo amevifungia kwa muda usiojulikana kwani wamekiuka masharti ya kanuni ya 5 (a, b, c na d) , kanuni ya 6 (2a, b na c) na kanuni ya 218 ya huduma za utangazaji ya mwaka 2005.

Wakati vituo hivyo vikifungiwa kwa muda usiojulikana kamati ya maudhui imepewa jukuu la kuviita na kusikiliza kwa kina Zaidi utetezi wao na ni hatua gani zaidi ya kuchukua dhidi yao kwa mujibu wa kanuni ya huduma za utangazaji.

Nape ameendelea kuvitahadhalisha vyombo mbalimbali vya habari kutoshawishika kuvunja sheria na kanuni zinazoongoza tasnia ya habari ili kulinda heshima ya tasnia yetu na wakati huo kuhakikisha nchi inabaki na Amani, Mshikamano na Umoja.

Godbless Lema Apandishwa Mahakamani

$
0
0
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amepandishwa mahakamani katika kesi mbili tofauti.

Kesi ya kwanza namba 351/2016 anatuhumiwa kumtumia ujumbe wa simu wa uchochezi Mkuu wa mkoa Arusha, Mrisho Gambo wenye maneno kuwa “Karibu tutakudhibiti kama mashoga walivyodhibitiwa Uarabuni”

Kesi ya pili namba 352/16 Lema anatuhumiwa kuhamasisha maandamano Septemba Mosi kinyume cha sheria.

Hakimu amepinga hoja za wakili wa Serikali,  Vincent Njau kuzuia dhamana kwa sababu za kiinterejensia kwa usalama wake.

Baadaye vurugu ziliibuka mahakamani wakati polisi wanataka kumpeleka Lema magereza kwa madai kuwa wanadhani wamechelewa, lakini mbunge huyo alipinga hatua hiyo kwa maelezo muda wa mahakama saa 9.30 ulikuwa bado.

Lowassa, Mbowe, Mnyika wakamatwa

$
0
0

Viongozi wa Chadema wamekamatwa na polisi na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema; “Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kikao walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo lililokataza mikutano.”

Waliotakiwa kufika makao makuu ya polisi, ni pamoja na mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe; mjumbe wa Kamati Kuu na waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa; Katibu Mkuu, Vicenti Mashinji na naibu katibu mkuu (Bara), John Mnyika.

Mkutano wa kamati kuu ya Chadema, umeitishwa ili kujadili ufanikishaji wa maandamano ya oparesheni UKUTA.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Agosti 30

Waziri Mkuu Akaribisha Wawekezaji Kutoka Japan.

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewakaribisha wawekezaji kutoka Japan na kusema kwamba kufanyika kwa Mkutano wa Sita wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Bara la Afrika (TICAD VI) jijini Nairobi kumetoa fursa kwa Tanzania na nchi nyingine kukutana na wafanyabiashara wakubwa wenye nia ya kuwekeza barani humo.

Ametoa kauli hiyo Jumapili, Agosti 28, 2016 alipokutana faragha kwa nyakati tofauti na viongozi wa makampuni makubwa ya Japan ambao walikuwa wakihudhuria mkutano huo uliofanyika katika kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha Jomo Kenyatta (JICC) jijini Nairobi, Kenya.

Mkutano wa sita wa TICAD ambao umemalizika jana, ulilenga kuiwezesha Afrika katika sekta ya uchumi na uwekezaji. Ili kufikia lengo hilo, mkutano huo umewashirikisha wadau wa sekta binafsi zikiwemo kampuni binafsi zaidi ya 300 kutoka Japan.

Katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu, Rais wa kampuni ya Sumitomo, Bw. Kuniharu Nakahura, alisema kampuni hiyo imeanza utekelezaji wa mradi wa Kinyerezi II wa kuzalisha umeme wa MW240 kutoka gesi asilia (Gas Fired Combined Cycle Gas Power Plant). Mradi huo ulioanza kutekelezwa Machi 2016, unatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu.

Bw. Nakahura ambaye pia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, alisema kampuni yao inajishughulisha zaidi na utengenezaji wa bidhaa za vyuma, kemikali, ujenzi wa miundominu, na usafirishaji.

Naye Makamu wa Rais wa kampuni ya Toyota Tshuso, Bw. Yasuhiko Yokoi alikutana na Waziri Mkuu na kumweleza jinsi kampuni hiyo kubwa duniani inavyoweza kushiriki na kuchangia maendeleo nchini Tanzania.

Alisema kampuni yao inajishugulisha zaidi na masuala ya miundombinu ikiwemo kuzalisha mitambo ya umeme na mitambo ya bandari. Pia inazalisha bidhaa za kilimo (matrekta, mashine za viwanda vya mbolea na nguo, ujenzi wa maghala ya nafaka), mitambo ya nguvu za umeme wa joto-ardhi na uzalishaji wa magari ya aina mbalimbali.

“Kwa mfano hapa Kenya, tumeweza kutengeneza mitambo midogo ya kisasa ambayo inazalisha mbolea tofauti kulingana na hali halisi ya udongo wa mahali husika. Huwezi kuzalisha mbolea ya aina moja na kuamua kuisambaza kwa nchini nzima. Tunapima udongo wa sehemu moja na kuzalisha mbolea inayofaa kwa udongo ule,” alisema.

Naye Rais wa kampuni ya Marubeni, Bw. Fumiya Kokubu alimweleza Waziri Mkuu kwamba maeneo ambayo wangependa kuwekeza ni kwenye viwanda vya nguo, mbolea, saruji, uzalishaji wa sukari, umeme wa gesi na hasa miradi ya LNG.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu aliwahakikishia wawekezaji hao kuwa Serikali iko tayari kushirikiana nao na akawashauri watume timu za maafisa wao ili wakutanishwe na wadau wa sekta husika.

Alisisitiza kuwa Tanzania hivi sasa imedhamiria kuwa nchi ya uchumi wa viwanda na kwa sababu hiyo inahitaji kuwa na nishati ya kutosha ili iweze kumudu kuendeleza sekta hiyo. “Serikali ya awamu ya tano imeamua kujenga uchumi wa viwanda, tunahitaji kujenga viwanda vya kutosha ili tuweze kusindika mazao ya wakulima ambao wanafikia asilimia 80 ya Watanzania wote. Tunahitaji masoko ya uhakika kwajili ya mazao wanayozalisha,” alisema.

Akiwa kwenye mkutano huo, Waziri Mkuu pia alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya wakimbizi, Bw. Filippo Grandi; Meya wa Jiji la Yokohama, Bibi Fumiko Hayashi; na Makamu wa Rais wa Kwanza wa Sudan, Jenerali Bakri Hassan Saleh.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu alitembelea Maonesho ya Biashara ya Afrika na Japan (Africa-Japan Expo 2016) ambapo Mamlaka ya Kuendeleza Biashara Tanzania (TANTRADE) na wadau wengine kama Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA), Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji (EPZA) walishiriki.

Akiwa huko alitembelea pia mabanda ya Uganda, Rwanda, Sénégal, Kenya, Japan na UN Habitat. Pia alitembelea banda la wajasiriamali wa nguo kutoka Tanzania ambao walishiriki maonyesho hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha Jomo Kenyatta (JICC) jijini Nairobi, Kenya.

Waziri Mkuu alirejea jijini Dar es Salaam jana usiku.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 29, 2016.

Lipumba Aendelea Kung'ang'ania Uenyekiti Wake CUF

$
0
0

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Prof Lipumba ameendelea Kung’ang’ania kiti cha uenyekiti wa chama chake cha CUF na kusema kikao kilichokaa jana visiwani Zanzibar na kufanya maamuzi ya kuwasimamisha uanachama, hakikuwa halali na kilikuwa nje ya katiba ya CUF, sababu mojawapo ikiwa ni kuwekwa kando kwa Naibu Katibu Mkuu Bara, Magdalena Sakaya.

“Kikao hicho  hakikuwa halali, haiwezekani Baraza Kuu linakaa halafu Naibu Katibu Mkuu Bara hajui, wala hakujulishwa, na bado kuna wajumbe wengine hawakuhusishwa” Alisema Prof Lipumba

Lipumba aliongeza kuwa ni kweli alijiuzulu uenyekiti, lakini baadaye aliamua kuandika barua kwa Katibu Mkuu ya kutengua uamuzi wake wa kujiuzulu na sasa yeye ndiye Mwenyekiti halali wa chama hicho.

“Nilimuandikia barua ya kurudi kwenye nafasi yangu, akasema anasubiri ushauri wa kisheria, lakini hadi sasa hakuna kitu, hiyo inamaanisha kuwa sasa mimi naendelea na nafasi yangu, na niko ngangari kama mwenyekiti” Alisema Prof Lipumba.

Aidha aliongeza kuwa alitaka kujieleza katika mkutano mkuu mbele ya wanachama, lakini mkutano ule ukavurugwa.

Kuhusu kuwepo kwa tofauti kati yake na Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, Prof Lipumba amesema kuwa huenda kuna tofauti kwa kuwa mara nyingi huwa hamuelewi jinsi anavyokiendesha chama bila kifuata misingi ya kidemokrasia.

“Katibu Mkuu anamdharau na hampi heshima yake Naibu Katibu Mkuu Bara, mara nyingi huamua mambo yake bila kushirikisha viongozi wengine, halafu sasa anataka kufukuza wanachama, huwezi kuwa na chama halafu ufukuze wanachama, wanachama wanatafutwa duniani kote, halafu wewe unawafukuza, hizo ni dalili za uongozi wa kiimla, kuongoza chama unapaswa kujali demokrasia na siyo kuwa dikteta ndani ya chama” Amesema

Kuhusu Julius Mtatiro kuwa mwenyekiti mpya wa Kamati ya Uongozi, Lipumba amesema kuwa hatambui maamuzi hayo, na wala hamtambui Mtatiro kama kiongozi wa chama hicho bali mjumbe wa Mkutano Mkuu, nafasi ambayo yeye ndiye aliyempa.

“Mtatiro hawezi kuwa mwenyekiti, mimi ndiye mwenyekiti wa chama, Mtatiro alishindwa hata kuongoza mkutano mkuu, ukavurugika, hawezi, simtambui”

CUF Wamteua Mtatiro kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Muda

$
0
0
Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF) limemteua Julius Mtatiro kuwa mwenyekiti wa kamati ya muda ya uongozi hadi utakapoitishwa mkutano mkuu maalumu mwingine baada ya ule wa awali kuvunjika. 

Mtatiro amekubali uteuzi huo na kwamba hawezi kukwepa majukumu hayo muhimu. 

Baraza hilo lililoketi katika kikao chake cha dharura juzi Jumapili mjini Unguja, liliamua pia kusitisha uanachama wa baadhi ya watendaji wake waandamizi, kutoa karipio kali na kuwafukuza baadhi yao. 

Kikao hicho kilichofanyika katika ofisi za makao makuu ya chama hicho, Vuga kilihudhuriwa na wajumbe 47 kati ya 60 na kiliongozwa na Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali. 

Akitangaza maazimio ya kikao hicho jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema katika kutekeleza jukumu hilo, Mtatiro atasaidiana na Katani Mohamed Katani na Severina Mwijage. 

“Maamuzi hayo ni kwa mujibu wa katiba ya CUF kifungu Na.101 na 118, vinavyolipa mamlaka baraza kutekeleza hatua hiyo.” 

Mazrui alisema baraza hilo lilimteua John Bashange kukaimu nafsi ya naibu katibu mkuu wa CUF – Tanzania Bara na Mbaralah Maharangande kukaimu nafasi ya naibu mkurugenzi wa habari, uenezi na uhusiano kwa umma. 

Nafasi zilizojazwa ziliachwa wazi na Profesa Ibrahim Lipumba, Magdalena Sakaya na Abdul Kambaya ambao baraza hilo la dharura lilitangaza kuwasitisha uongozi na uanachama wao. 

“Hatua ya kuitisha baraza la dharura sambamba na maamuzi hayo ilikuja baada ya kushindwa kupata uongozi wa juu wa chama kufuatia kuvunjika na kushindwa kukamilika kwa mkutano mkuu maalumu wa uchaguzi wa Agosti 21 uliofanyika jijini Dar es Salaam,” alisema. 

Alisema kuwa baraza liliamua kusitisha uanachama wa Sakaya kwa kushindwa kutekeleza kifungu cha katiba ya CUF, Na. 122 na kwamba licha ya barua aliyotumiwa kumtaka ahudhurie kikao hicho, hakufika bila ya taarifa yoyote ya msingi. 

Mazrui alisema katika baraza hilo, ilielezwa kuwa Sakaya alidai kuzuiliwa na wazee wa CUF wa Dar es Salaam kwa madai kuwa hicho hakikuwa kikao halali. 

Wengine ambao uanachama wao umesitishwa ni Ashura Mustafa, Mohamed Mnyaa, Kapasha Kapasha, Haroub Shaim, Omar Masoud na Thomas Malima. 

Baraza hilo la CUF lilitangaza kumfukuza uanachama wa chama hicho, Shashu Lugeye, baada ya kumsikiliza na kutoridhishwa na maelezo yake. 

Wanachama waliopewa karipio kali ni Rukia Kassim Mohamed na Othman Mohamed. 

“Chama kimechukua maamuzi  haya kuonyesha dhamira ya dhati na matumaini ya umma wa Watanzania kwamba CUF ndiyo pekee iliyobeba dhana ya mabadiliko,” alisema Mazrui. 

Taarifa kutoka ndani ya Baraza hilo ziliarifu sababu tatu za kuchukua hatua hiyo kuwa ni hasara ya Sh600 milioni kiliyoingia kwa mkutano uliovunjika; njama ovu zilizodaiwa kutekelezwa na baadhi ya watendaji wao; na jaribio la kuchafua taswira ya chama hicho. 

Mazrui alisema mkutano mkuu maalumu, kabla ya ule wa kawaida wa mwaka 2018 kwa mujibu wa Katiba, utafanyika pale chama hicho kitakapopata uwezo wa kifedha. 

Akiandika katika mtandao wake wa Facebok, Mtatiro alisema, “Nimepokea majukumu niliyokabidhiwa na Baraza Kuu la chama changu. Siwezi kuepuka majukumu haya muhimu kwa wakati huu ambapo chama kinahitaji mchango wangu. Niko imara sana, natambua nimepewa majukumu wakati gani na nianze na mguu upi kwenda mbele”. 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images