Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Oparesheni UKUTA: Msajili wa Vyama Aitisha Mazungumzo ya Siku Mbili Kwa Vyama Vyote ili Kusaka Suluhu

$
0
0
MSAJILI wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, ameitisha Baraza la Vyama vya Siasa ili kunusuru mvutano uliojitokeza kati ya Jeshi la Polisi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Jaji Mtungi amevitaka vyama vya siasa vilivyotangaza kufanya maandamano na mikutano isiyo na tija nchi nzima kuacha, badala yake warudi kwenye meza ya mazungumzo ili kuondoa tofauti zinazojitokeza.

Kauli ya Jaji Mutungi imekuja baada ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) nao kutangaza maandamano ya amani kwa ajili ya kupongeza utendaji kazi wa Rais Dk. John Magufuli, huku Chadema kikiitisha maandamano na mikutano isiyo na kikomo nchi nzima, ambayo imepewa jina la Operesheni Ukuta.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Jaji Mutungi alisema kufanyika kwa maandamano na mikutano hiyo, hakuwezi kuondoa changamoto za kisiasa zilizopo, hivyo basi wanapaswa kukaa kwenye meza moja kwa ajili ya kujadili tofauti zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.

“Ninawaomba wale wote wenye lengo la kuitisha maandamano na mikutano ya kisiasa kuacha kwa sababu haiwezi kusaidia kuondoa changamoto zilizopo, bali tunapaswa kukaa kwenye meza moja ya mazungumzo ili tuweze kujadili tofauti hizo na kuzipatia majibu,” alisema Jaji Mutungi.

Aliongeza kuwa licha ya kuwapo kwa jitihada za viongozi mbalimbali kujadili suala hilo, lakini vyama hivyo vimeonekana bado vikiendelea na misimamo yao ya kuitisha mikutano na maandamano yasiyo na kikomo, jambo ambao linaweza kuleta hofu kwa wananchi.

Jaji Mutungi alisema katika kipindi hiki ambacho wananchi wametulia, hakuna haja ya kuwatia hofu au wasiwasi ili ionekane kuwa nchi ina ombwe kubwa la uongozi, jambo ambalo linaweza kurudisha nyuma juhudi za kuleta maendeleo.

Alisema kutokana na hali hiyo, wananchi wanapaswa kuheshimu utawala bora na kuacha kujadili mambo ambayo yanaweza kuvuruga amani, badala yake wanapaswa kuangalia mustakabali wa taifa kwa kufanya kazi na kuleta maendeleo.

“Wananchi wanapaswa kuondoa hofu kuhusiana na migongano ya kisiasa inayojitokeza, kwa sababu hakuna ombwe la uongozi, badala yake wanapaswa kufanya kazi kwa masilahi ya taifa ili waweze kuleta maendeleo,” alisema.

Aliongeza kuwa kutokana na hali hiyo, ameamua kuitisha mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa ambalo linashirikisha vyama 22, vikiwamo CCM na Chadema wajadili mambo mbalimbali ikiwamo migongano ya kisiasa, ili waweze kuendesha shughuli zao kistaarabu.

Alisema mkutano huo utafanyika Agosti 29 na 30 mwaka huu ukishirikisha wadau mbalimbali.

Jaji Mutungi alisema kutokana na hali hiyo, Agosti 26 kutakuwa na kikao cha kuratibu mkutano huo ambao anaamini ni muhimu kwa ajili ya kuleta maridhiano baada ya tofauti za kisiasa zilizojitokeza.

“Baraza hili ni forum muhimu ya upatikanaji wa maridhiano ya kisiasa kama kuna tofauti zilizojitokeza, kuliko kuitisha mikutano na maandamano yasiyo na tija ambayo yanaweza kusababisha wananchi kupata hofu,” alisema.

Alisema hakuna jambo lenye ugumu katika suala hilo, kwa sababu migongano iliyopo inajadilika ikiwa ni pamoja na kupitia baadhi ya vifungu vya kisheria kwa ajili ya kufatuta mwafaka.

Akizungumzia suala la Chama cha Wananchi (CUF), Jaji Mutungi alisema  migongano iliyopo kwenye chama hicho anaijua, lakini kwa sasa hawezi kuzungumzia lolote kwa sababu mkutano ujao utashirikisha vyama vyote kikiwamo CUF.

“Mimi ni mlezi wa vyama vya siasa… CUF ni miongoni mwa watoto wangu, najua udhaifu wa vyama vyote kikiwamo CUF hadi ubora wao, hata migongano iliyojitokeza ndani ya chama hicho naijua, lakini kwa sasa nashindwa kuongea lolote kwa sababu tuna mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa ambalo litajadili mambo mbalimbali, ikiwamo suala la mgogoro wa CUF,” alisema Jaji Mutungi.

Kutokana na hali hiyo, aliwataka wanachama wa chama hicho kuondoa hofu kwa sababu suala hilo litapatiwa ufumbuzi kwa kuondoa tofauti zilizopo.

Jaji Mutungi aliyesema hayo huku wafuasi wa aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, wakidai kwenda katika ofisi yake kumweleza mambo mbalimbali, ikiwamo ya ukiukwaji wa taratibu za kisheria na kumwondoa kiongozi huyo kwenye nafasi yake uliofanywa na wafuasi wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad.

Katika hatua nyingine, Chadema kimesema kimesikia wito wa Jaji Mutungi wa kuitisha mazungumzo ambayo iwapo yatatawaliwa na nia njema na dhamira safi ya kuheshimu Katiba ya nchi, yanaweza kuwa na manufaa kwa Watanzania wote.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama  hicho, Tumaini Makene, ilisema hatua hiyo inaweza kuleta manufaa kama Jaji Mutungu hataegemea upande wa Serikali.

“Wakati Msajili wa Vyama akitoa kauli ya kuzuia kile anachokiita ‘kutunishiana misuli’, Jeshi la Polisi katika maeneo mbalimbali limeingilia vikao vya ndani vya chama na kuzuia visiendelee. Hiyo yote ni kinyume  na sheria, taratibu na mamlaka yao.

“Mbali na kuzuia vikao vya ndani, Jeshi la Polisi linashikilia watu mbalimbali, wakiwamo wafuasi, mashabiki, wanachama, viongozi wetu  kwa kushiriki vikao hivyo, wakitekeleza wajibu na haki zao za kikatiba na kisheria.

“Wakati tunasubiri meza ya mazungumzo kupitia Baraza la Vyama, tunapenda kusisitiza kuwa Chadema itasimama imara kuhakikisha misingi ya demokrasia na utawala unaozingatia Katiba na sheria unafuatwa,” ilisema taarifa hiyo.

Waziri Mkuu aagiza Matapeli wa Milioni 50 za Magufuli Wakamatwe

$
0
0

SIKU moja baada ya Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kutangaza kuiva kwa Mpango wa Serikali wa kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameonya juu ya kuwepo kwa matapeli katika mpango huo.

Amewatahadharisha wananchi kuwa makini na kujiepusha na matapeli wanaopita katika maeneo yao na kuwataka wachange fedha za kuanzisha vikundi ili wapewe fedha hizo na serikali.

Akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Majimoto, Halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele mkoani Katavi jana, Waziri Mkuu aliwataka wananchi kukaa macho na matapeli katika fedha hizo maarufu kama mabilioni ya Rais John Magufuli.

“Serikali bado hatujaanza kusambaza fedha hizo. Jihadharini na hao matapeli na wezi hivyo wakija kwenye maeneo yenu wakamateni. Zoezi hilo likianza mtajulishwa kupitia halmashauri zenu,” aliwasisitiza.

Alitoa onyo hilo siku moja baada ya NEEC kutoa onyo kama hilo juzi kwa kusema kumekuwa na taarifa kutoka sehemu mbalimbali nchini kuwa kuna baadhi ya taasisi na watu binafsi wanawadanganya wananchi kuwa fedha hizo zitapitia kwenye taasisi zao na kuwataka kujisajili nao ili waweze kufaidika na fedha hizo, jambo ambalo si la kweli.

Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Beng’i Issa alisema fedha hizo zimelenga kukopesha vikundi vya wajasiriamali kupitia Vyama vya Ushirika vya Akiba na Mikopo (Saccos) na vikundi vya kifedha vya kijamii vikiwemo Vicoba kwa ajili ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi.

Mpango huo uliobatizwa jina la Fedha za Mfuko wa Mzunguko, unalenga kukabiliana na tatizo la mitaji kwa ajili ya kuendesha shughuli za kiuchumi kwa wananchi wanaoishi maeneo ya mijini na vijijini.

“Watu na taasisi hizo zinazowadanganya wananchi zimekuwa zikiwatoza viwango mbalimbali vya fedha kwa kile wanachodai ni ada ya usajili ili vikundi hivyo vya wananchi viweze kusajiliwa na kutambuliwa kuweza kufaidika na mamilioni hayo kwa kila kijiji,” alisema Issa.

Kwa wakati tofauti Serikali ya Awamu ya Tano imesisitiza kuwa itakuwa macho ili kuhakikisha fedha hizo zinafanya kazi iliyokusudiwa na kuwafikia walengwa.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu jana alikagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kavuu linalojengwa na Kampuni ya Nandra Engineering & Construction Ltd ya Morogoro na kumtaka mkandarasi kulikamilisha haraka. 

Ujenzi wa daraja hilo lenye urefu wa meta 85.34 wenye thamani ya Sh bilioni 2.7 unagharimiwa na serikali kwa asilimia 100.

Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 24 Agosti, 2016 amemteua Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Modestus Francis Kipilimba alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Dkt. Modestus Francis Kipilimba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Rashid Othman ambaye amestaafu.

Dkt. Modestus Francis Kipilimba ataapishwa leo mchana tarehe 24 Agosti, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Bw. Robert Msalika kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Robert Msalika alikuwa Afisa Ubalozi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Bw. George Madafa kuwa Balozi na nchi atakayopangiwa itatajwa baadaye.

Wakurugenzi na Naibu Wakurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa waliopo wanaendelea na nafasi zao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
24 Agosti, 2016

Waziri Mkuu: Hakuna Mwanasiasa Atakayeruhusiwa Kuvuruga Amani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha inalinda amani ya nchi kwa gharama zozote na kamwe haitoruhusu mwanasiasa yeyote kusababisha vurugu zitakazochochea uvunjifu wa amani.

“Hatuzuii kuwa na vyama vya siasa ila haturuhusu vurugu kupitia vyama vya siasa na hakuna jambo lisilokuwa na mipaka. Mambo ya kuhamasishana kufanya vurugu hatutayaruhusu, tunataka watu wafanye kazi,” alisisitiza.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumanne, Agosti 23, 2016) wakati akizungumza na viongozi wa dini pamoja na wazee wa mkoa wa Rukwa mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Alisema Serikali inataka Watanzania wawe na uhakika wa kuendelea kufanya kazi zao za kuwaingizia kipato na kuwaletea tija, hivyo suala la kudumisha amani ni muhimu kwani vurugu zikitokea hawatakuwa na mahali pa kukimbilia na hakuna shughuli ya maendeleo itakayofanyika.

“Suala la uhamasishaji wananchi juu ya utunzaji wa amani ni la lazima hivyo viongozi wa dini na wazee kwa pamoja tushirikiane katika kukemea vitendo vya uchochezi kwasababu vurugu zikitokea Watanzania hatuna mahali pa kukimbilia,” alisema.

Aidha, Waziri Mkuu aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kuliombea taifa pamoja na viongozi wake kwa sababu kazi ya uongozi ni ngumu na inachangamoto nyingi.Pia aliwaagiza viongozi wa dini wa mkoa wa Rukwa kuharakisha uundwaji wa Kamati ya Amani ya mkoa huo.

Awali, Sheikh wa mkoa wa Rukwa, Sheikh Rashid Akilimali amesema madhehebu ya dini hayawezi kuvuruga amani ya nchi ila anahofu na viongozi wa vyama vya siasa kutokana na vitendo vyao vya kuhamasisha vurugu.
 
Kufuatia hali hiyo Sheikh Akilimali aliwaomba wanasiasa nchini kutovuruga amani kwani machafuko yakitokea watashindwa kufanya ibada mbalimbali ikiwemo kufunga mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Sheikh Akilimali alisema kwa sasa wananchi wako huru kwenda kufanya ibada misikiti na makanisani kutokana na uwepo wa amani, hivyo aliwasisitiza wanasiasa kutothubutu kuichezea amani.

“Tafadhalini wanasiasa msituharibie amani ya nchi yetu. Amani haichezewi tunaona kwa wenzetu wanavyohangaika, wanaishi kwa tabu sisi hatujazoea  kukimbia. Sisi Watanzania ni moja na tunaishi kwenye nyumba moja hivyo hatuna budi kushirikiana kuilinda amani yetu,” alisema.

Kwa upande Katibu wa Wazee mkoani Rukwa, Kanali Mstaafu, John Mzurikwao alimuomba kiongozi huyo kuwasaidia  kutatua kero mbalimbali zinazoukabili mkoa huo zikiwemo za malipo ya pembejeo kwa mawakala wa kilimo pamoja na mgogoro wa ardhi katika shamba ya Efatha.

Waziri Mkuu alisema suala la malipo kwa mawakala wa pembejeo za kilimo linafanyiwa kazi na watalipwa baada ya Serikali kukamisha zoezi la uhakiki wa madeni hayo ili kujiridhisha kama kweli wakulima wapatiwa pembejeo na kwa kiwango gani.

Rais Magufuli mgeni Rasmi Mkutano wa 32 wa ALAT

$
0
0

Habari/Picha Na Ally Daud.
Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Nchini (ALAT) ambao utafanyika mwishoni mwa mwezi ujao mkoani Musoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Makamu Mwenyekiti wa ALAT Bw. Stephen Mhapa amesema kuwa, katika mkutano huo wanatarajia Rais Magufuli kuwa mgeni rasmi ili kufikia malengo ya mkutano huo.

“Tumeamua kumuomba Mheshimiwa Rais kuwa mgeni rasmi kwa ajili ya kupata matunda mema ya mkutano huo kutokana na kauli mbiu yake ya Hapa Kazi Tu ili kuendana na kasi hiyo katika kuleta mendeleo na uongozi bora nchini,” alisema Bw. Mhapa.

Aidha Bw. Mhapa amesema kuwa uzinduzi wa mkutano huo utaendana na ukabidhishaji wa zawadi kwa mshindi wa shindano la Halmashauri bora kwa mwaka 2016  ambapo mshindi atayechaguliwa na wananchi kwa wingi atakabidhiwa Trekta yenye thamani ya shilingi milioni 56 ili kuinua shughuli za kimaendeleo.

Mbali na hayo Bw. Mhapa ameongeza kuwa mkutano huo utadhaminiwa na Benki ya NMB kwa kupokea kiasi cha shilingi milioni 206 ambazo milioni 56 zitatumika kugharamia zawadi na milioni 150 kugharamia mkutano huo.

Kwa upande wa Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Serikalini kutoka benki ya NMB Bi. Domina Feruzi amesema kuwa wameamua kufadhili mkutano huo ili kurahisisha shughuli za kimaendeleo na kupata uongozi bora kwa faida ya watanzania.

“Tumeamua kudhamini mkutano huo ili kuweza kurahisisha shughuli za kimaendeleo na kupata viongozi bora kwa kupitia mashindano ya Halmashauri Bora mwaka 2016,”amesema Bi. Domina.

ALAT imekuwa na utaratibu wa kutoa zawadi kwa Halmashauri bora kwa mwaka wa pili sasa ambapo imesaidia Halmashauri nyingi kufanya vizuri katika ukusanyaji mapato na uboreshaji wa miundo mbinu na mazingira kwa ujumla.

Jeshi La Polisi Lahusisha Mauaji ya Polisi Wanne na Sakata la Oparesheni UKUTA.........Lapiga Marufuku Mikutano yote ya Ndani ya Vyama vya Siasa

$
0
0
KUFUATIA mauaji ya askari wanne yaliyotokea Kata ya Mbande Temeke kwa watu wanaodhaniwa ni majambazi kuvamia benki ya CRDB na kuwaua askari hao kwa kutumia silaha za moto jeshi la Polisi limetangaza kiama na kuwataka wahusika wote kujisalimisha.

Katika hatua nyingine jeshi la polisi limehusisha tukio hilo na Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (UKUTA) kufuatia matamko ya baadhi ya viongozi wa kisiasa ambao wamesikika katika majukwaa ya kisiasa wakihamasisha wafuasi wao wawashambulie askari wa Jeshi la Polisi.

Kauli hiyo imetolewa  na Kamishna Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijan Mssanzya (CP), wakati akizungumza waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana ambapo pia alikiri kuwa mazoezi yanayofanywa na polisi yamelenga kukabiliana na Ukuta.

Akizungumza kwa hisia CP Mssanzya pia amepiga marufuku  mikutano ya ndani yenye viashiria vya uchochezi na hata ikifanyika kwenye majukwaa watamshusha muhusika na kumfikisha kwenye mkono wa sheria.

Amesema Jeshi  hilo limebaini kwamba mikutano hiyo imekuwa ikitumika kuchochea wananchi na kuwahamasisha kuvunja sheria za nchi na kufanya mapambano na jeshi la polisi

"Kwasababu hiyo basi,kwa hali ya kutumia mikutano ya ndani kuchochea watu kuvunja sheria na kupambana na askari, hivyo basi kuanzia sasa jeshi la polisi nchini linapiga marufuku mikutano yote ya ndani" amesema.
 
Aidha CP  Mssanzya  aliwataja askari waliouawa katika tukio hilo wakati wakibadilishana lindo kuwa ni  E.5761 CPL Yahya, F.4660 CPL Hatibu, G 9524 PC Tito na G 9996 PC Gastoni na raia wawili waliojeruhiwa aliowataja kuwa Ali Chiponda na Azizi Yahya wote wakiwa wakazi wa Mbande.

"Katika tukio hilo majambazi ambao idadi yao haikufahamika walifanikiwa kupora silaha mbili aina ya MSG na lisasi 60 na hakuna pesa wala mali ya benki hiyo kuibiwa au kuharibiwa, ni dhahiri kuwa waharifu hao walikuwa na kusudio moja tu la kuwashambiulia askari polisi, " alisema.

Alisema katika hali ya kushangaza baada ya tukio hilo kuna baadhi ya watu waliandika mitandaoni kubeza na kukeji mazoezi ya kawaida ya jeshi la polisi na wengine waliandika ujembe wa kushabikia tukio hilo la kuuawa kwa askari polisi huku wengine wakidiriki kuandika ujumbe unaosema endapo watapigwa na polisi Srptemba1 mwaka huu basi viongozi wa jeshi hilo wawaondoe askari wanaoishi uraiani na kuwarudisha kambini.

Aliongeza kuwa jeshi la polisi limejipanga vyema kukabiliana na matukio yote ya uvunjifu wa amani nchini.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.

Ufafanuzi Kuhusu Wasiokopeshwa Mikopo Na HESLB Kudaiwa

$
0
0
1.0   UTANGULIZI

Kumekuwepo na taarifa zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari, hasa gazeti la Jamboleo toleo namba 2541 la 23 Agosti, 2016 kuhusu Bodi ya Mikopo kuwadai wasionufaika na mikopo. Taarifa hizi zinalenga kuleta hofu na mkanganyiko usiokuwa wa lazima kwa wadau. Kufuatia hatua hiyo Bodi ya Mikopo inapenda kutoa ufafanuzi wa suala hili kama ifuatavyo:-

2.0 MADAI KUHUSU KUDAIWA MIKOPO KWA WALE WASIONUFAIKA

Bodi ya Mikopo inapenda kuufahamisha Umma kuwa ‘database’ yake ya wanufaika wa mikopo ina taarifa zote muhimu zilizo sahihi. Hii inatokana na utunzaji mzuri wa kumbukumbu za ukopeshaji kuanzia hatua ya utoaji mikopo (loan allocation and disbursement) hadi urejeshaji wake (loan repayment).  Kutokana hamasa na elimu inayotolewa, kumekuwepo na mwitikio mkubwa wa wanufaika wa mikopo na waajiri wao kujitokeza na kuanza kurejesha mikopo. Hivyo, katika utekelezaji wa jukumu hilo, tumebaini kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa baadhi ya wadaiwa kwamba ama hawakuwahi kukopa au hawajawahi kufikia kiwango cha elimu ya juu.

Hadi sasa, imebainika kuwepo kwa baadhi ya wanufaika ambao wanadai hawakujua iwapo fedha walizopatiwa na serikali wakati huo zilikuwa za mkopo. Pia kuna wachache ambao vyeti vyao vilitumiwa na ndugu zao kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu. Katika hali hii, mdaiwa atalazimika kumtaja mtu halisi anayepaswa kukatwa deni hilo ili Bodi iweze kusitisha makato hayo kwake.

Ili kupata ufumbuzi wa malalamiko hayo, Bodi inawataka walalamikaji kuzingatia yafuatayo:

2.1   Kwa mtu anayedai kwamba hajasoma elimu ya juu kwa ufadhili wa serikali au Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu; mtu huyu awasilishe vielelezo vinavyodhihirisha kuwa hakusomeshwa kwa ufadhili wa serikali.

2.2   Kwa mtu anayedai amekatwa mshahara ingawa hajawahi kufikia kiwango cha elimu ya juu; mtu huyo anapaswa kuwasilisha vielelezo vya kiwango cha elimu yake.

2.3   Iwapo kuna mnufaika wa mkopo anadai amekatwa zaidi ya kiwango cha mkopo anaodaiwa; mnufaika huyo anapaswa kuwasilisha vielelezo vinavyothibitisha kumaliza kurejesha deni lake. Itakapothibitika kuwa kuna makato zaidi yalifanyika, basi kiasi kilichozidi kitarejeshwa kwa mhusika.

3.0   HITIMISHO
Bodi inapenda kuwahakikishia wadau wake kuwa imetunza vizuri taarifa zote muhimu za wanufaika wa mikopo ambazo ndizo zinazotumika kwenye zoezi la urejeshaji wa mikopo.  Kasoro ndogo ndogo zinazojitokeza zinatatuliwa kwa kufanya rejea kwenye kumbukumbu zilizopo.

Aidha, Bodi inaendelea kuwahimiza wanufaika wote wa mikopo ambao hawajaanza kurejesha mikopo yao kuhakikisha wanawasilisha taaifa zao ofisi za Bodi au wanajaza taarifa zao kweye fomu ‘Loan Inquiry Form’ iliyopo kwenye tovuti ya Bodi na kuituma kwa anuani ya barua pepe info@heslb.go.tz ili kila mmoja ajulishwe deni lake na kuanza kurejesha.

Kwa mnufaika anayetaka kuanza kurejesha mkopo wake baada ya kuwa amepata taarifa ya deni lake; aweke fedha kwenye akaunti za Benki zifuatazo na kisha kuwasilisha hati ya malipo:

A/C No. 2011100205 – NMB
A/C No. 01J1028467503 – CRDB
A/C No. CCA0240000032 – TPB

Imetolewa na:
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Agosti 24, 2016

Rais Magufuli Amuapisha Mkurugenzi Mkuu Mpya Wa Idara Ya Usalama Wa Taifa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 24 Agosti, 2016 amemuapisha Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Dkt. Modestus Francis Kipilimba ameapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam na mara baada ya kuapishwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa amekula kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Salome Kaganda.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Kipilimba alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Dkt. Modestus Francis Kipilimba amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Rashid Othman ambaye amestaafu.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Bw. Robert Msalika Makungu kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Tanzania Bara.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Robert Msalika Makungu alikuwa Afisa Ubalozi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Bw. George Madafa kuwa Balozi na nchi atakayopangiwa itatajwa baadaye.

Wakurugenzi na Naibu Wakurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa waliopo wanaendelea na nafasi zao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
24 Agosti, 2016
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli akimkabidhi kitendea kazi Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli akimuapisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016.Kushoto akisimamia zoezi hilp ni Kamishina wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe George Masaju na Katibu Mkuu kiongozi Engineer John Kijazi katika picha ya pamoja na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuapishwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016

Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli katika picha ya pamoja na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuapishwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016.
PICHA ZOTE NA IKULU

Makamu Wa Rais Akutana Na Mkurugenzi Mtendaji Wa Benki Ya Maendeleo Ya Afrika Anayeshughulikia Kanda Ya Afrika Mashariki

$
0
0
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imeihakikishia Serikali kuwa itaendelea kuisaidia Tanzania katika kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo uimarishaji wa miundombinu ya barabara katika kuelekea kwenye Taifa la uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Calleb Weggoro alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan 24-Aug-16 ofisini kwake, Ikulu, Dar es salaam.

Dkt. Weggoro alisema amefurahishwa na jinsi serikali inavyoshirikiana na sekta binafsi kupitia Mpango wa Ushirikiano kati ya Sekta Binafsi na sekta za Umma (PPP) katika utekelezaji wa miradi mbalimbali na anaamini ushirikiano huo utakuwa na manufaa kwa Taifa.

Mkurugenzi huyo alimweleza Mheshimiwa Makamu wa Rais  kuwa katika Mkakati wa Kitaifa wa 2016-2020 ulioandaliwa na Benki hiyo umeonesha maeneo matano mapya ambayo yatapewa kipaumbele katika kusaidia nchi za Afrika.

Ametaja maeneo hayo kuwa ni pamoja na masuala ya nishati, chakula, viwanda, utangamano wa nchi za Afrika na kuboresha maisha ya wananchi hasa vijana na wanawake kwa kuwawezesha kiuchumi kwa kuwapatia ajira.

Katika mazungumzo hayo Makamu wa Rais aliishukuru benki hiyo kwa misaada yake ambayo imeiwezesha serikali kutimiza azma yake ya kuleta maendeleo kwa wananchi wake kwenye nyanja za kiuchumi na kijamii.

"Ni matumaini yangu kuwa katika huu mkakati mpya benki itakuwa tayari kuisadia Tanzania na nchi nyingine za kanda ya Afrika Mashariki, maana sote tunahitaji kusonga mbele kimaendeleo," alisema Mheshimiwa Samia.

Katika msafara huo Dkt. Weggoro alifuatana na Mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo ya AfDB Tonia Kandiero ambaye alisema msaada wa benki hiyo katika kuimarisha miundombinu ya barabara ni jambo la msingi na akaelezea kufurahishwa kwake jinsi serikali inavyotekeleza miradi hiyo kwa ufanisi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Kanda ya Afrika Mashariki  Dkt. Nyamajeje Calleb Weggoro,kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Bi.Tonia Kandiero, Ikulu jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Kanda ya Afrika Mashariki  Dkt. Nyamajeje Calleb Weggoro mara baada ya kumaliza mazungumzo, Ikulu jijini Dar es salaam.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 27 & 28 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0


Mtunzi:Eddazaria g.Msulwa
Ilipoishia....
   Nikastukia nikamuona daktri anaye sukuma kitanda akisukumwa na kuanguka chini na macho yangu yakakutana na macho ya baba yaliyojaa hasira hadi yakawa mekundu.Akanishika kifuani na kunivuta na kunitupa chini na kuanukia mgongo na kusababisha maumivu makali kuzidi kunitawala kwenye mwili wangu hususani kifuani mwangu.Madaktari wakataka kumsogelea baba ila akachomoa bastola yeka na kuwafanya madaktari kusita.Mguu wa baba ukatua kifuani kwangu huku ukiwa umevalia buti lake la jesi kisha bastola yake akaikoki tayari kwa kunifyatulia risasi

Endelea...

   Nikastukia baba akitoa ukulele na kuanguka chini na kumuona sheila akiwa ameshika kipande cha mbao kinachoonekana kimechomolewa kwenye benchi huku kikiwa kinavuja damu kwenye sehemu ambayo ilitua kichwani mwa baba.Sheila akaanza kutetemeka baada ya kumuona baba akiwa anavujwa na damu za kichwa,madaktari wakaninyanyua na kunirudisha kwenye kitanda huku hali yangu ikizidi kuwa mbaya na mamcho yangu yakaanza kutawaliwa na ukungu na kwambali nikamuona sheila akishikwa na askari wawili na wakaanza kumtoa enje akiwa ananililia kwa uchungu.Kitanda nilicho kilalia kikaanza kusukumwa taratibu na jinsi ninavyo isililizia hali yangu yenye maumivu makali ya mwili nikajikuta macho yangu yakitawaliwa na ukungu mwingi na sikujua ni kitu gani kinacho endelea.

                                                    *****

 Baridi kali ikaanza kunisumbua mwili wangu na kujikuta nikianza kufumbua macho yangu na kujikuta nikitazama sehemu ya juu ambayo kwa haraka haraka sikujua nipo wapi.Mwili wangu ukawa umebanwa kidogo na na kwa haraka haraka nikagundua kuwa nipo kama nilivyo zaliwa kwani kiwamgo cha baridi kilitawala mwili wangu mzima,nikajariu kujigeuza ila nikajikuta nikishindwa na nikaanza kujisukuma na kumbukumbu za akili yangu ikagundua kuwa sehemu niliyopo ni katika majokofu ya kuhifadhia miili ya watu walio fariki dunia.

Nikajaribu kuita ila sikusikia msaada wa mtu wa aina yoyote wala kitu kikitembea nje ya majokofu hayo,nikazidi kujitahidi huku miguu yangu nikiigonga gonga kwenye sehemu ya chini ya jokofo ambapo ndipo miguu yangu ilipo elekea na kujikuta sehemu niliyo ilalia ikienda mbele na kufunguka.Nikaendelea kujikaza huku nikizisidi kujitahidi kujitoa ndani ya jokofu hili na chakumshukuru mungu nikafanikiwa kulifunua kwa uwazi mdogo ulio niruhusu kuitoa mikono yangu kwa nje na kujivuta na likafunguka na kupata uwezo wa kukaa na kitako na kuanza kushangaa.

Woga ukaanza kunitawala na baada ya kujikuta nikiwa nimeshonwa katikati ya kifua changu na kitu kingine kilichoizidi kuniogopesha ni miili mingi ya watu walio lala chini huku wakiwa wamefunikwa malailoni yanayo waonyesha vizuri huku miili yao ikiwa imeharibiwa sana huku wengine vichwa vyao vikiwa vimepasukwa na kurudishiwa rudishiwa kiasi kwamba wanatisa kwa muonekano wao.Nikashuka kwenye jokofu nililo kuwepo na taratibu nikaanza kuutafuta mlango wa kutokea katika chumba hichi na kabla sijauona nikastukia taa za chumba zikizima na giza kali likazidi kutawala.

Nikajikaza na sikutaka kuuruhusu woga kutawala katika mwili wangu kwa wakati huu,nikapapasa papasa ukutani kwa dakika zaidi ya mbili na kufanikiwa kukuta mlango na kabla sijaufungua nikasikia watu wakizunumza kwa nje
“muambie huyo mudi awashe hilo genereta la upande huu kuna maiti tunataka kuziingiza humu”

“kwani hao nao wametokea wapi?”
“kuna basi limeanguka na kuua watu ishirini”
“sasa huku ndani si kumejaa hadi maiti nyingine tumeziweka chini tutafuta ustaarabu wa kuwatoa kesho wakazikwe na manispaa kwa maana hata ndugu zao hawajitokezi”
“hawa tutawaweka hivyo hiyo bwana kwani hatuna seemu nyingine ya kwenda kuwaweka na hospitali zote za wilaya mochwari zao ni ndogo”

Watu waliopo nje wakaendelea kujibishana nikataka kupiga kelele za kuomba msaada ila roho yangu ikasita na kujua ni lazima watu waliopo nje wataogopa na kukimbia na ningelisitisha zoezi zima la wao kuingiza maiti wanazo zizungumzia,taa zikawaka na mlango nikausikia ukifunguliwa na baada ya dakika kakika moja mlango ukafunguliwa
“hembu shika huko vizuri usije ukamuachia”

Gafla umeme ukakatika na kuwafanya watu walio ibeba maiti wanayo taka kuuingiza kuanza kutukana matusi mazito na kwakupitia uwazi mdogo wa mlango nikastukia kuona wakiondoka kwa hasira huku maiti wakiwa wameilaza chini na sikujua ni wapi wanapo elekea,nikachungulia nje na kukuta kuna giza ila mwanga wa mbalamwezi uliweza kunisaidia kuona baadhi ya majengo na kungundua bado nipo sehemu ya muhimbili.Nikaanza kuoiga hatua za haraka na kutoka ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti na nikafika kwenye jengo ambalo nikakuta kamba nyingi zikiwa zimeanikwa makoti meupe ya madaktari.Nikalishusha moja kwenye kamba na kulivaa kwa haraka kisha nikachukua suruali nyepe na kuivaa na muonekanao wangu ukawa kama wauduzi wa kiume kwenye hospitali hii.

Nikaanza kutembea kuelekea getini huku miguuni nikiwa nipo peku peku na nikafanikiwa kutoka pasipo walinzi kunitilia mashaka ya aina yoyote.Nikatafuta sehemu na kukaa huku akili yanu ikianza kufikiria ni kitu gani kilicho wafanya madaktari hadi wakanipeleka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.Nikajikuta nimejishika tama na kugundua mashavu yangu yamejaa ndevu  nyingi na kwaharaka haraka nikagundua ni kipindi kirefu nimekaa hospitali kwani ndevu zangu huchukua muda mwingi sana katika kuota na kuwa ndefu kama nilivyo zikuta sasa.

Nikapata wazo la kwenda nyumbani kwa sheila japo ni mbali sana na sehemu niliyopo nikaona sina budi kufanya hivyo.Nikapiga moyo konde na kunyanyuka sehemu niliyo kaa na kuanza kutembea japo njaa kali inanisumbua tomboni kwangu ila nikajitahidi kwenda kutembea kwa haraka ili niweze kufika.

Nikatumia kama masaa mawili na kufika nyumbani kwake na kukuta ukimya mwingi ukiwa umetawala ila kitu kingine kilicho anza kunipa wasiwasi ni nyasi nyingi na ndefu zilizo oto nje ya geti lake na kwaharaka nikajua sheila hayupo ndani ya nyumba yake kwa maana kama angekuwepo kusingekuwa na nyasi nyingi huku geti lake likiwa lemetawaliwa na vumbi jingi.Ikanibidi kuchungulia kwenye eti lake ili kujionea mwenyewe nikipingana na mawazo yagu ya kusema sheila hayupo ndani ya nyumba yake.Giza lilitawala kwenye nyumba yake na hapakuwa na dalili yoyote ya mtu kushi na jinsi mlango tulivyo ufunga siku ya mwisho ndivyo jini ulivyo kwa sasa.Nikashusha pumzi nyingi huku nikitazama wapi nielekee na mbaya zaidi sikua na jirani yoyote wa sheila ninaye mjua ambaye ninaweza kumuulizia habari za sheila

Hali ya uchunu ikaanza kunitawala na kwa mbali machozi yakaanza kunilenga lenga na kujikuta nikitamani utokee muujiza sheila kusimama mbele yangu,wazo la kuwa na mama likaanza kunijia ila kutokana na kuchoka nikashidwa kujua kama nitaweza kwenda nyumbani ambapo tulikuwa tunaishi ila woga ukaanza kunijia kwani kumbukumbu ya baba siku alivyokuwa akinipiga ikanijika kichwani kama mkanda wa video ila ukakata gafla baada ya kusikia mnguruo wa mbwa ukitoka nyuma yangu.


==>Endelea Nayo <<Kwa Kubofya  Hapa>>

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 34

$
0
0
Mtunzi:Enea Faidy

...Lakini cha ajabu kila alipomsogelea binti yule naye alikaza mwendo zaidi. Mama Dorice alishuhudia jinsi ambavyo mwanaye alitembea kwa madaha sana.

"Doriiiice!" Aliita kwa sauti lakini yule msichana alipogeuka hakuwa Dorice tena ilikuwa ni sura ya msichana mwingine kabisa. Mama Dorice alichanganyikiwa sana, ni kwanini hali inakuwa vile? Lakini hakupata jibu. Kaka yake alimfata haraka na kumshika mkono.
"Dada utagongwa na magari... Kwani unamfata nani?" Aliuliza kwa mshangao kwani yeye hakumwona MTU yeyote.
"Namfuata Dorice..."
"Huyo Dorice yuko wapi maana tangu tupo kule unamfuata tu?"

"Sio yeye.. Nimemfananisha...."
"Dada bwana usiwaze sana.... Ona sasa mpaka watu wanakushangaa ujue.. Unaita kila mtu Dorice..."
"Lakini Mimi nilimwona kabisa kaka...."
"Haya tuondoke"
Mama Dorice alikuwa bado anaifikiria ile hali, akajua lazima kuna kitu kinaebdelea kuhusu Dorice, kwanini amfananishe kiasi kile lakini bado hakuwa na jibu sahihi.

Wakati wa safari ulipowadia, waliingia kwenye basi na kukaa kwenye siti zao.Walisafiri kwa mwendo kidogo, ndipo macho ya mams Dorice yalipotua kwenye sura ya yule binti aliyemwona toka wakiwa kituo cha mabasi Jana yake. Na alikuwa amevaa nguo zile zile, alikaa Pembeni yake. Moyo ulimpasuka kwa mshtuko akafikinya macho yake na kumtazama tena binti yule aliyeachia tabasamu mwanana. Akamsalimu mama Dorice. Mama Dorice alishangaa, kilichomshangaza zaidi ni kwamba alipoingia kwenye gari hakumwona MTU yule na hata alipokaa hakukaa na binti yule. Sasa imekuaje yupo nae?
 
"Mama nilikuona sehemu!"
"Mh hata Mimi nilikuona!" Alisema mama Dorice.
"Kwanini ulikuwa unanifata?" Aliuliza binti yule ambaye kila wakati alipenda kutabasamu.
"Nilikuwa na kufananisha na mwanangu" alisema mama Dorice.

"Mwanao? Anaitwa Dorice?"
"Ndio... Umemjuaje?"aliuliza mama Dorice lakini msichana yule alicheka sana kitendo kilichomshangaza mama Dorice.
"Mama we si uliniita Dorice?"
"Eeh ndo jina lake.." Wakati wakiendelea na mazungumzo Yale mjomba wake Dorice alimshangaa sana dada yake.
"Dada mbona unaongea peke yako? Unajibizana na nani?"


==>Endelea  Nayo <<kwa Kubofya Hapa>>

Kingunge Ngombale Mwiru Avunja Ukimya.......Amtaka Mkapa na Ali Hassan Mwinyi Wamshauri Rais Magufuli Afanye Mazungumzo na Chadema Kuhusu Oparesheni UKUTA

$
0
0
Aliyekuwa kada wa CCM, Kingunge Ngombale Mwiru  amewaomba  marais wastaafu, Rais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa kuzungumza na Rais John Magufuli ili aitishe kikao kati ya Serikali na Chadema kwa ajili ya kusitisha maandamano yaliyopangwa kufanyika Septemba Mosi.
 
Kingunge  ametoa kauli hii  leo nyumbani kwake jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari  wakati akiongelea  mvutano kati ya Chadema na serikali unaoendelea kwa sasa.

Chadema kimeingia kwenye mvutano mkubwa na serikali kutokana na dhamira yake ya kufanya mikutano na maandamano nchi nzima chini ya mwavuli wa Umoja wa Kupinga Udikteta (Ukuta).

Hivi karibuni, Rais John Magufuli alisisitiza kutoruhusu maandamano na mikutano ya kisiasa na kuagiza kuwa, wanaotaka kufanya mikutano wafanye ndani ya mipaka ya majimbo yao na si vinginevyo jambo ambalo Chadema wanapinga.

Hali hiyo imeibua mtikisiko mkubwa nchini huku kada mbalimbali ikiwa ni pamoja na viongozi wa dini, wanasiasa, wasomi na wananchi wa kawaida wakitaka kupatikana suluhu kabla ya Septemba Mosi, tarehe iliyopangwa kuanza maandamano na mikutano hiyo.

Kwenye mkutano wake na wanahabari Kingunge anawalaumu viongozi wastaafu wakiwemo marais pamoja na mawaziri wakuu kwa kukaa kimwa wakati huu ambao nchi inatikishwa huku Katiba ya Jamhuri ikisiginwa.

Miongoni mwa viongozi wanaolalamikiwa kutosikika ama kuchukua hatua zozote ili kuilinda Katiba ni pamoja na Marais Wastaafu, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Aman Abeid Karume (Zanzibar).

Viongozi wengine waliotajwa ni Mawaziri Wakuu Wastaafu, Cleopa Msuya; Jaji Mstaafu, Joseph Warioba.

“Mzee Mwinyi yupo kimya, Mkapa kimya, Warioba kimya, Cleopa Msuya kimya, Amani Karume kimya,” amesema Kingunge na kuongeza;

“Ukimya huu unatokana na nini? Hawa wote waliwahi kula viapo vya utii kwa Katiba. Mimi nahoji, wazee wenzangu vipi mnakuwa kimya? Nawaambia kuwa mnachofanya si sawa.

“Naomba wazee wote tujitokeze kuhesabiwa katika hili la uvunjifu wa Katiba na sheria.”

Kingunge ambaye alihamia Chadema akitokea CCM kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kutokana na kutoridhishwa na namna mchakato wa kumpata mgombea urais kutoka chama hicho amesema, Chadema inatumia haki yake ya kikatiba.

“Naomba Rais Magufuli, akubali kuitisha kikao na Chadema ambacho pia wazee wastaafu watahudhuria, akifanya hivyo hata sisi wazee tutawageukia Chadema na kuwambia wasitishe mpango wao wa maandamano,” amesema.

Amesema kwamba, kibaya zaidi Jeshi la Polisi linaandaa bunduki kwa ajili ya kupambana na raia ambao hawana kitu na kuwa, hali hiyo haipaswi kuvumiliwa.

Mwanasiasa huo amesema, Chadema wameamua kutetea haki yao ya kikatiba na kisheria kwa kufanyaa maandamano kote nchini, na kina wafuasi wengi hivyo si jambo la kubeza.

“Upande wa pili, lipo Jeshi la Polisi na watawala ambao wanaahidi kuwakabili. Kwa bahati mbaya polisi na watawala hawatetei Katiba wala Sheria,” amesema.

Amesema kuwa, Tanzania kwa sasa inakabiliwa na ombwe la uongozi na kwamba, nchi imekosa watawala wenye sifa thabiti ya kuongoza taifa.

“Kwa hakika, tatizo kubwa la sasa la nchi yetu ni ombwe la kiuongozi, kwasababu kama ni watawala tunao kweli kweli, lakini tunachokosa ni watawala wenye maarifa ya kiuongozi.

“Inashangaza kuona wazee wastaafu kukaa kimya wakati nchi inakabiliwa na tatizo linaloweza kutuangamiza.

“Upande mmoja unanoa mapanga, unaanda bunduki kwa ajili ya kuchinja na kuua na upande wa pili wapo raia tu, tena wasio na silaha zozote.”

Kingunge anasema, wananchi ambao serikali na Jeshi la Polisi wanajiandaa kupambana nao, wanalilia Katiba na sheria zifuatwe.

“Laiti kama Chadema wangekuwa hawatetei Katiba na sheria, kungekuwa na kila sababu ya kuwashughulikia, lakini kwa kuwa wanatetea Katiba na sheria, kuna umuhimu wa kuyapa uzito madai yao,” amesema Kingunge.

Mwanasiasa huyo amesema kuwa, mvutano wa sasa sio wa Chadema na serikali isipokuwa ni suala la wananchi wote wa wenye mapenzi mema na taifa lao.

“Hili ni suala la kila mtu anayependa utawala wa Katiba, Sheria na Utawala Bora,” amesema.

Waziri Mkuu: Watumishi Watakaokula Fedha Za Chf Wafukuzwe Kazi Na Na Wafikishwe Mahakamani

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kufukuzwa kazi na kufikishwa mahakamani kwa watumishi wote wa sekta ya afya watakaobainika kula fedha zinazochangwa na wananchi kwa ajili ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Pia amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Stephen pamoja na Mganga Mkuu wa mkoa huo, Dk. John Gurisha kusimamia na kulinda fedha  za CHF zinazochangwa na wananchi  na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Agosti 24, 2016) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye jimbo la Kwela, Tarafa ya Mtowisa wilayani Sumbawanga.

"Kitendo cha kula fedha zinazochangwa na wananchi kwa lengo la kupata huduma za afya kinawafanya wakatetamaa ya kuendelea kuchangia mfuko huo. Kama wako watumishi wenye tabia hizo waache mara moja," amesisitiza.

Mbali na kutoa agizo hilo kwa uongozi wa mkoa wa Rukwa, pia Waziri Mkuu amewataka wananchi kujiunga na CHF kwa sababu mfuko huo utawawezesha  kupata huduma za matibabu bure wao na familia zao katika kipindi cha mwaka mzima.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amesema barabara ya kutoka Ntendo hadi Muze ye urefu wa kilometa 85  itajengwa kwa kiwango cha lami ili iweze kupitika kwa urahisi na kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa wakati.

“Mimi nilidhani mlima wa Kitonga ndio mkali kuliko yote na eneo la Sekenke ndio linatisha zaidi!. Kumbe barabara ya kuja huku Mtowisa ndiyo inatisha zaidi kuliko zote. Lazima tuweke lami ili iendelee kupitika kwa urahisi zaidi,” amesema.

Akizungumzia ombi lililotolewa na mbunge wa jimbo la Kwela, Ignas Malocha la kutaka tarafa hiyo ya Mtowisa kuwa wilaya au halmashauri, Waziri Mkuu amesema analichukua na kwenda kulifanyia tathmini na majibu atayapata kupitia uongozi wa mkoa.

Malocha alisema jimbo la Kwela linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya miundombinu ya barabara hali inayosababisha wananchi kushindwa kusafirisha mazao yao kwa urahisi.

Pia aliomba ukanda huo wa bonde la mto Rukwa upandishwe hadhi na kuwa wilaya au halmashauri ili kusogeza huduma za kijamii karibu na wananchi.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Rukwa, Mhandisi Masuka Mkina ameelezea mkakati wa kuboresha miundombinu ya barabara mkoani hapa ikiwemo ya kutoka Ntendo hadi Muze wilayani iliyopo wilayani Sumbawanga.

Mhandisi Mkina amesema Serikali imetenga jumla ya sh. milioni 170 kwa ajili ya kuweka zege kwa ajili ya kurahisisha upandaji wa mlima hasa kwenye eneo la Kizungu katika barabara ya kutoka Ntendo hadi Muze.
 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, AGOSTI 24, 2016.

Atakayevamia Msitu Faini Mil. 70, Jela Miaka Saba- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kuvunja sheria kwa kuvamia na kuharibu mazingira ya msitu wa Mfili ambao ndiyo chanzo pekee cha maji cha Wilayani Nkasi atatozwa faini ya sh. milioni 70 pamoja na kifungo miaka saba jela.

Katika kuhakikisha hatua zinachukuliwa Waziri Mkuu amemkabidhi mkuu wa wilaya ya Nkasi, Said Mtanda kitabu cha sheria kitachomuangoza katika kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kufanya uharibifu katika chanzo hicho cha maji.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumanne, Agosti 23, 2016) wakati akizungumza na wananchi wa mji Mdogo wa Namanyere katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanya vya Sabasaba.

“Mkuu wa wilaya akishindwa kuwachukulia hatua za kuwaondoa wananchi na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watu wote waliovamia maeneo ya hifadhi za misitu na kuanzisha makazi au kufanya shughuli za kijamii naye atakuwa jipu,” alisema.

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa maeneo mengi nchini yanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji baada ya wananchi kuvamia katika vyanzo vya maji na kufanya shughuli za kibinadamu hivyo kusababisha vyanzo vingi kukakuka

“Serikali haitakubali kuona mtu anaharibu chanzo cha maji. Wananchi mnatakiwa kuwa walinzi wa maeneo hayo na atakayekutwa anachunga mifugo, analima, kukata nyasi au kufanya shughuli zozote za kijamii ndani ya maeneo hayo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Awali Waziri Mkuu alikagua mradi wa upanuzi wa bwawa la maji Mfili ambalo mwanzo lilikuwa na ujazo wa lita 1,500 ambapo litakapokamilika litakuwa na ujazo wa lija 248,067 hivyo kuwezesha wakazi 82,689 kunufaika.

Akizungumza kwenye eneo la mradi mara baada ya Waziri Mkuu kuwasili, Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Nkasi, Julius Kaondo alisema hadi kukamilika mradi huo unatarajiwa kugharimu sh trilioni 1.011 ambapo Wizara ya Maji na Umwagiliaji imetoa sh. milioni 500 na OOfisi ya Rais TAMISEMI itatoa sh. milioni 500.

Mkurugenzi huyo alisema mradi unakabiliwa na changamoto ya ukosefu umeme ppamoja na mitambo ya kusukuma maji kwa kutumia nishati ya umeme, ambapo aliiomba Serikali kuipatia halmashauri hiyo sh. milioni 222.576 ikiwa ni gharama za kupeleka umeme kwenye eneo la mradi na kununua mitambo.

Mbali na kutembelea mradi wa upanuzi wa bwawa, pia Waziri Mkuu alitembelea hospitali teule ya wilaya ya Nkasi na kuzindua wodi mpya yenye uwezo wa kulaza wagonjwa 72 kwa wakati mmoja

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU, JUMATANO, AGOSTI 24, 2016.

Utata kuhusu mashahidi wagubika kesi ya Tundu Lissu, yaahirishwa hadi Sept 6, mwaka huu.

$
0
0

Mvutano kuhusu maelezo ya mlalamikaji katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, baina ya mawakili wa upande wa  mashtaka na upande wa utetezi ulikwamisha usikilizwaji wa kesi hiyo.

Katika kesi hiyo Lissu ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anadaiwa kutoa kauli za uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Anadaiwa kuwa Juni 28, mwaka huu, Lissu akiwa katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alitoa kauli za uchochezi kuwa:
 
“Mamlaka ya Serikali mbovu ni ya kidiktekta uchwara inahitaji kupingwa na kila Mtanzania kwa nguvu zote, huyu dikitekta uchwara lazima apingwe kila sehemu. Kama uongozi utafanywa na utawala wa kijinga nchi inaingia ndani ya giza nene.’’

Kesi hiyo ilitarajiwa kuanza kusikilizwa leo kwa upande wa mashtaka kuanza kutoa ushahidi.Wakili wa Serikali Bernard Kongola aliieleza mahakama kuwa walikuwa na mashahidi wawili ambao aliwataja kuwa ni Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Kimweli na Staff Sajenti Ndege.

Hata hivyo kabla ya kesi hiyo kusikilizwa, kiongozi wa jopo la mawakili wa Lissu, Peter Kibatala aliiomba mahakama wapewe maelezo ya mlalamikaji katika kesi hiyo kabla ya kufanya jambo lolote, jambo ambalo liliibua mvutano wa hoja baada ya kupingwa na upande wa mashtaka.

Wakili Kongola aliieleza mahakama kuwa mlalamikaji katika kesi hiyo ambaye ni Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, si miongoni mwa mashahidi wao wanaokusudia kuwaita mahakamani.

Pia alisema kuwa kwa mujibu wa sheria hawalazimiki kutoa maelezo hayo ya mlalamikaji kwa mtu ambaye si shahidi.

Akijibu hoja hizo, Wakili Kibatala alidai kuwa taarifa ya huyo mlalamikaji ndio chanzo au iliyosababisha kesi hiyo na kwamba iwapo watamleta au hawatamleta lakini maelezo yake ni sehemu ya kesi hiyo.

Alidai kuwa hata mashtaka yaliyopo chini ya sheria ya magazeti ni ya muhimu na kwamba hawawezi kujitetea bila kuyaona  na kwamba hata kama upande wa mashtaka hautamuita, wao wataiomba mahakama aitwe kwa lazima.

Hivyo aliiomba mahakama iulazimishe upande wa mashtaka uwapatie maelezo hayo ya mlalamikaji.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Dk Yohana Yongolo aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 6, mwaka huu, atakapotoa uamuzi, baada ya kupitia vizuri hoja za kisheria za pande zote.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Agosti 25

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Hotuba ya Edward Lowassa alipokuwa Iringa Jana

$
0
0

Leo(Jana)  nimewatembelea ndugu zangu wa Kilolo - Iringa kuwashukuru na kuwaeleza kuwa tulishinda na ndio maana hawa mabwana wakubwa wanapata tabu sana Na Sisi.
 
Miezi michache iliyopita nilitangaza kuanza ziara ya kushukuru wananchi kwa kura Million 6 wakazuia mikutano ya hadhara na kama haitoshi wakazuia mikutano ya ndani pia ninayotaka kuhudhuria ,imefikia mahala wanatisha hadi wafanyabiashara wanaotukodishia kumbi za mikutano.

CHADEMA chama chetu ni kikubwa sana , kinawatesa , tumewachapa kweli kweli uchaguzi Mkuu 2015, tumewashinda katika majiji na miji mikuu kiasi wanapata Tabu , wageni toka Nje wakija pale Airport Rais huwa anaulizwa kuhusu mameya wetu na anapata kigugumizi kutambulisha kuwa hawa ni wapinzani.
 
Ni jambo la kufurahia na sababu ya sisi kutokata tamaa.
Ni ishara kwamba tunaweza.

Pili Uchaguzi Mkuu ujayo 2020 tutashinda tukiwa wamoja , tuwe wamoja na wanajua sisi ni wamoja . Na nawasihi tuendelee kuwa wamoja hivi hivi, tusiruhusu vitisho vitutenganishe.. Hakuna nguvu kubwa kama ya Umma.
 
Uongozi ni dhamana na njia pekee njema ya kuongoza ni meza ya makubaliano na sio vitisho kwa wananchi kama ilivyo sasa.

KUHUSU UKUTA .
Jambo hili la UKUTA ni kubwa mno si jambo dogo hata kidogo .Jana balozi wa Marekani aliwatumia ujumbe raia wake wajiandae kuondoka tarehe 1 September kwa hofu walionayo. Hata Mimi nina hofu kama tusipotekeleza hili nchi itakuwa wapi hapo baadae. Haiwezekani mtu mmoja ajiamulie tuu kila jambo na kuvunja katiba .

Wasuluhishi wanasema tuzungumze , tunakubali kuzungumza ,lakini tuzungumze nini ikiwa mtu anavunja Katiba na hawamuonyi hawamshauri hii si sawa kabisa. 

Mtu mmoja anajiamulia kuvunja katiba anazuia mikutano anazuia mikutano ya ndani na wasuluhishi hawamuonyi ,nasema kabla ya kuja kwetu wakamueleze yeye kwanza matendo yake .

POLISI niwaeleze duniani kote maandamano ni haki ya msingi kabisa , police wakiua raia au wanachama wetu tuwaarifu dhahiri tutagoambana nao mmoja mmoja, hatutahangaika na jeshi tutahangaika Na Polisi aliefanya mauaji, alie fyatua risasi ajue dhahiri tutamshitaki ICC . 

Ni bora tufilisike ,tutaabike lakini tutawalinda watanzania Na waandamanaji wetu wote nchi nzima Kata zote kama tulivyo kubaliana.
 
Ni aibu vyombo vya dola vinatumia nguvu kubwa kutisha watu wasio hata na fimbo.

Tabia za baadhi ya viongozi ni mbovu sana , wanavunja Katiba Na kukanyaga demokrasia , hili hatuwezi kuliruhusu litokee Tanzania hata kidogo. Zipo jitihada za usuluhishi hatuna shaka nazo lakini wajue jambo tunalolipigania liko wazi ni Katiba wamwambie aruhusu mikutano na haki za kidemokrasia .

Tujitokeze kwa wingi sana September 1, tuandamane bila kuharibu Mali ya mtu kama tulivyofanya wakati Wa kuchukua Fomu pale buguruni ,Tume hadi Kinondoni bila hofu .

Tuna chama Imara sana CHADEMA kinacho tetea Uhuru ,haki ya mwananchi , maendeleo na ustawi wa nchi . Tunawapenda sana, ninawapenda Na Ahsanteni.

Rais Magufuli apokea taarifa ya Ujenzi wa Bomba la mafuta kutoka Uganda hadi bandari ya Tanga.

$
0
0

Makamu wa Rais wa Kampuni ya Total Afrika Mashariki Bw. Javiero Rielo amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa maandalizi ya kuanza kwa ujenzi wa bomba la mafuta la kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania yanaendelea vizuri na kwamba kampuni hiyo imedhamiria kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa mafanikio.

Bw. Javiero Rielo amesema hayo jana tarehe 24 Agosti, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na Rais Magufuli kwa lengo la kumpa taarifa juu ya maendeleo ya maandalizi ya kuanza kwa ujenzi wa bomba la mafuta.

Mradi huo utahusisha ujenzi wa bomba lenye urefu wa kilometa 1,410 ambalo litasafirisha mafuta ghafi kutoka ziwa Albert nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania na unatarajiwa kuzalisha ajira za moja kwa moja 1,500 na ajira zisizo za moja kwa moja 20,000.

Gharama za mradi wa ujenzi wa bomba hilo zinatarajiwa kuwa takribani Dola za Kimarekani Bilioni 4 na Kampuni ya Total inasema fedha hizo zipo tayari.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Rais Magufuli amesema anaamini kuwa mradi huo utakuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania, Uganda, Kampuni ya Total na nchi jirani.

Amebainisha kuwa pamoja na kwamba Tanzania ipo katika mazingira mazuri ya kutekeleza mradi huo, Serikali yake itatoa ushirikiano mkubwa ili kufanikisha mradi huo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi watatu wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Mabalozi waliowasilisha hati zao ni Mhe. Ian Myles – Balozi wa Canada hapa nchini, Mhe. Prasittiporn Wetprasit – Balozi wa Thailand hapa nchini mwenye makazi yake Mjini Nairobi nchini Kenya na Mhe. Harald Gunther – Balozi wa Austria hapa nchini mwenye makazi yake Mjini Nairobi nchini Kenya.

Pamoja na kuwasilisha hati zao za utambulisho Mabalozi hao wameelezea kufurahishwa na mahusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya nchi zao na Tanzania na wameahidi kufanya kazi bega kwa bega na Serikali ya Tanzania ili wananchi wa pande zote wanufaike na matokeo ya ushirikiano huo hususani katika uwekezaji na biashara.

Kwa upande wake Rais Magufuli amewahakikishia Mabalozi hao kuwa Serikali yake itaendeleza na kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na nchi hizo na ametoa wito kwa Mabalozi hao kuzishawishi zaidi nchi zao na wawekezaji katika nchi hizo kushirikiana na Tanzania katika ujenzi wa viwanda, uongezaji thamani ya madini, kuendeleza kilimo hususani kilimo cha umwagiliaji, uzalishaji wa nishati na biashara mbalimbali.

Pia Rais Magufuli ametoa wito kwa Mabalozi wa Thailand na Austria kuanzisha ofisi za Ubalozi hapa nchini ili kurahisisha na kuharakisha shughuli za kibalozi.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
24 Agosti, 2016

Mahabusu Ajinyonga Arusha

$
0
0

Mahabusu aliyekuwa akishikiliwa katika kituo kikuu cha polisi jijini Arusha aliyetambulika kwa jina la Victoria Wenga (51) mkazi wa Lemara jijini Arusha amejinyonga hadi kufa usiku wa kuamkia jana kwa kutumia shuka lake bila kuacha ujumbe wowote.

Marehemu alikamatwa Agosti 21 mwaka huu majira ya Alfajiri kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba yake na maduka yake mawili kutokana na ugomvi wa kifamilia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alikiri kutokea kwa tukio hilo katika Kituo cha Kikuu cha Polisi saa 6:20 usiku jana wakati wenzake wakiwa wamelala.

“Polisi wa zamu alisikia kelele kutoka kwenye chumba cha mahabusu wa kike ambapo polisi walijitahidi kuokoa maisha ya mahabusu huyo, lakini ilishindikanika,” alisema Kamanda Mkumbo.

Mahabusu huyo, ambaye ni mkazi wa Lemara jijini Arusha, alijinyonga kwa kutumia shuka lake alilokuwa anatumia kujifunikia wakati yuko mahabusi. Mtuhumiwa huyo, alijinyonga kabla ya kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka yake.

“Jana ilikuwa afikishwe mahakamani kujibu kosa lililokuwa linamkabili,” alisema Kamanda Mkumbo na kuwahakikishia kuwa hali ya usalama kituoni hapo na tukio hilo, havihusiani na sababu zozote za kiusalama.

Marehemu Victoria anadaiwa kuwa na ugomvi wa kifamilia na mume wake aliyetambulika kwa jina la Edward Wenga akimtuhumu kuzaa nje ya ndoa kinyume na utaratibu.

Imeelezwa kuwa  hicho ndo chanzo cha marehemu kufikia hatua ya kuteketeza mali walizochuma na mume wake ambazo ni maduka mawili na nyumba ya kuishi.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuifadhia mahiti Hospitali ya Mount Meru.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images