Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Chadema Watangaza Safu ya Maandamano ya UKUTA.......Lowassa Amepangiwa Mbeya, Katibu Mkuu Kapangiwa Mwanza

$
0
0

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe jana alitangaza mkakati wa chama hicho kufanikisha mikutano na maandamano ya walichokiita Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), huku jeshi la polisi nao wakijiandaa kukabiliana nao. 
 
Mbowe aliitaja mikakati hiyo ikiwamo kamati za kuhamasisha Ukuta ambapo aliyekuwa mgombea urais kupitia Ukawa Edward Lowassa amepangiwa Mbeya, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji atakuwa Mwanza, Makamu Mwenyekiti Profesa Abdallah Safari atakuwa Tabora huku Mwenyekiti wa Bawacha Taifa, Halima Mdee na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Mabere Marando wakipangiwa Dar es Salaam. 
 
Alisema yeye (Mbowe) ataongoza Kanda ya Kaskazini wakati Profesa Mwesiga Baregu amepewa jukumu la kufafanua Ukuta kwa taasisi za kimataifa, viongozi wa dini na wastaafu.
 
Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Tundu Lissu na mawakili 12 wao watajifungia Dar es Salaam kufungua kesi 21 kutetea mikutano. 
 
Lakini, Jeshi la Polisi limesema litatoa taarifa rasmi baadaye huku CCM wakisisitiza msimamo wao wa kupinga maandamano hayo. 
 
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Bulimba alisema jeshi hilo litatoa taarifa siku chache zijazo. “Tutawaita na tutazungumza, naomba tujaribu tu kuvuta subira,”alijibu kwa ufupi msemaji huyo wa polisi. 
 
Hata hivyo kikosi cha Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) katika mikoa mbalimbali ikiwamo Dar es Salaam na Kilimanjaro walionekana wakifanya mazoezi wakiwa na silaha na magari ya maji ya kuwasha kwa siku tofauti. 
 
CCM watoa ushauri
Msemaji wa CCM, Christopher ole Sendeka alisema licha ya chama kuzungumza mara kadhaa, wanatarajia kutoa tamko kwa lengo la kuwaeleza Watanzania tahadhari juu ya mchezo unaojaribiwa na Chadema. 
 
Sendeka alisema viongozi wa dini na makundi mbalimbali yameshauri juu ya mipango yao, lakini hawataki kusikia. 
 
 “Jambo hilo limezungumzwa mara nyingi sana, viongozi wa dini wameshasema, watu wenye mapenzi na nchi yao wakishauri waache huo mchezo wao ambao sidhani kama watafanikiwa, kwa hivyo tunatarajia kutoa tamko letu siku yoyote kuanzia kesho (leo),”alisema. 
 
Mbowe na safu yake
Akizungumza wakati akifungua mkutano wa viongozi wa Chadema Kanda ya Kaskazini jana katika Hoteli ya Coridol Springs jijini hapa, Mbowe alisema chama hicho kimejipanga kufanya mikutano na maandamano ya amani nchi nzima Septemba Mosi ili kutetea utawala wa sheria na Katiba. 
 
Mbowe alisema Rais Magufuli aliapa kuilinda Katiba, Wabunge waliapa kuilinda Katiba, madiwani waliapa kuilinda Katiba ili nchi iongozwe katika misingi ya sheria na utawala bora. 
 
Alisema haiwezekani nchi kuongozwa kwa matamko ambayo yanakiuka katiba na Chadema kama chama kikuu cha upinzani kina wajibu wa kuishauri na kuikosoa serikali na hawawezi kukaa kimya. 
 
Alisema matamko ya Rais kuwa hakuna ruhusa ya kufanya mikutano ya kisiasa kwa vyama vingine na kuacha chama chake kufanya mikutano na pia kuzuia mikutano hadi mwaka 2020 haikubaliki. 
 
“Sisi tunataka nchi iongozwe kwa kufuata sheria na siyo matakwa ya viongozi ambayo yanakinzana na sheria na Katiba ya nchi,” alisema Mbowe. 
 
Alisema wanafanya mikutano na maandamano kama sehemu ya kueleza malalamiko yao, hasa kutokana na kauli za viongozi ambazo zinakiuka sheria.
 
Mbowe alisema vyama vyote vikiamua kukaa kimya na kuacha mambo yaliyotokea Zanzibar, yaliyotokea Dodoma na yanayotokea sasa kutokana na kauli za viongozi, ni wazi nchi haitakuwa salama. 
 
“Tukiamua sote kujifanya wanafiki kusema hewala nchi haitakuwa salama itazaa taifa la watu wenye hofu na ndiyo sababu tumeamua kamati kuu kuanzia sasa kufanya kazi kila siku kuisaidia sekretarieti,” alisema. 
 
Mbowe alisema kutokana na unyeti wa Ukuta, Kamati Kuu ya Chadema imeunda kamati ndogo tano, ambazo zitasaidia kufikiwa malengo yaliyokusudiwa kwa kuhusisha taasisi na vyombo vingine. 
 
Alisema pia kuna kamati ya maandalizi ya Ukuta ambayo tayari imeanza kazi ya kufafanua maamuzi ya kamati kuu, ambayo sasa imesambaa katika kanda zote kutoa elimu kwa viongozi wa Chadema. 
 
“Katika kanda zote nchi nzima viongozi watakwenda kuzungumza na wanachama wa kada zote na kuwaelimisha kwanini Kamati Kuu imefikia maamuzi ya kuanzisha Ukuta kabla ya kushiriki mikutano na maandamano Septemba Mosi,” alisema

Mrithi wa Prof Lipumba CUF Kupatikana Leo

$
0
0

Historia kuandikwa leo. Ndivyo unavyoweza kusema wakati wajumbe zaidi ya 700 wa Mkutano Mkuu wa dharura wa CUF watakapomchagua mwenyekiti mpya wa chama hicho kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Ibrahim Lipumba aliyejiuzulu wadhifa huo Agosti mwaka jana.

Profesa Lipumba aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho kikuu cha upinzani kuanzia 1995 hadi mwaka jana, aliachia ngazi kwa kile alichodai kupinga uamuzi wa viongozi wa vyama vinavyounda Ukawa kumpokea Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Baada ya profesa huyo wa uchumi aliyegombea urais mara nne kujiweka kando, CUF iliunda kamati ya watu watatu chini ya uenyekiti wa Twaha Taslima, kukiongoza chama hicho hadi hapo utakapofanyika uchaguzi mwingine wa viongozi.

Katika uchaguzi huo utakaofanyika katika ukumbi wa Blue Pearl, atapatikana mwenyekiti mpya na kuingia katika kumbukumbu ya kuwa mwenyekiti wa nne wa chama hicho.

Waliowahi kuwa wenyeviti wa chama hicho ni Profesa Lipumba, Musobi Mageni na James Mapalala.

Wanaogombea uenyekiti ni Abdul Omary Zowo , James Mahangi , Joseph Rhobi , Juma Nkumbi , Salum Barwany, Selemani Khatibu, Zuberi Kuchauka, Riziki Mngwali na Twaha Taslima.

Wanaowania nafasi ya makamu mwenyekiti ni Dk Juma Ameir Muchi, Juma Duni Haji, Mussa Haji Kombo na Salim Abdallah Bimani.

Chama hicho kilionekana kama kitayumba baada ya Profesa Lipumba kujiuzulu, lakini kilivuka kigingi hicho na katika Uchaguzi Mkuu uliopita kilishinda viti 10 vya ubunge Tanzania Bara, ikiwa ni mara ya kwanza tangu kilipoanzishwa.

Hata hivyo, chama hicho, kwa upande wa Zanzibar hakikupata nafasi ya wabunge wala uwakilishi baada ya kususia uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20.

Uchaguzi huo wa marudio ulifanyika baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kufuta Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015. 

Neno la Mwisho la Mkuu wa Mkoa wa Arusha Felix Ntibenda Aliyetumbuliwa Juzi na Rais Magufuli

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliyeondolewa, Felix Ntibenda amekabidhi ofisi huku akitoa neno la mwisho la kuwakaribisha Kigoma baadhi ya maofisa waliokuwapo kwenye hafla hiyo.

“Karibuni sana Kigoma,” ndiyo lilikuwa neno la mwisho kwa Ntibenda alilolitoa baada ya kukabidhi ofisi kwa Mkuu wa Mkoa mpya Mrisho Gambo, hafla iliyofanyika kwa muda mfupi.

Ntibenda aliyehamishiwa ofisi ya Waziri Mkuu, baada ya kusema neno hilo alipanda gari na kuondoka. 

Kabla ya makabidhiano,alikuwa wa kwanza kufika ofisini saa 3.30 asubuhi na kulazimika kusubiri hadi 5.05 asubuhi, alipowasili mkuu mpya wa mkoa Gambo aliyeapishwa Ikulu jijini Dar es Saalam juzi na Rais John Magufuli. 

Gambo kabla ya uteuzi huo alikuwa mkuu wa wilaya ya Arusha na aliwasili ofisini akiwa ameambatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama.

Aliingia ofisini kwake na kukutana na Ntibenda, ambapo walifanya makabadhiano na kutoka huku wakizungumza.

Makabidhiano hayo yalifanyika haraka kwa kile ambacho kilielezwa na mkuu mpya wa mkoa kutakiwa kusafiri kwenda Loliondo kupokea Mwenge wa Uhuru.

Katibu Tawala, Richard Kwitega alisema Gambo baada ya makabidhiano alikuwa na ratiba moja tu kuzungumzia mbio za Mwenge wa Uhuru ambao leo unaingia mkoani hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Gambo alisema jana alitarajia kuzungumzia mbio za Mwenge pekee na kwamba unatarajiwa kuzindua miradi yenye thamani ya Sh12.9 bilioni.

UVCCM wampokeaGambo 
Kama ambavyo, ilitarajiwa jana, viongozi wa UVCCM Mkoa wa Arusha wakiongozwa na mwenyekiti wao, Lengai ole Sabaya walijitokeza katika mapokezi ya Gambo. 

Sabaya alisema wanampongeza Rais Magufuli kwa kusikiliza kilio chao na pia kumteua kijana kuongoza mkoa.

“Sisi kama UVCCM tumekuja hapa kumpongeza mkuu mpya wa mkoa na tuna imani naye sana kuwa atasaidia maendeleo ya mkoa huu,” alisema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Agosti 22

Rais Magufuli Amteuwa Bw. Gabriel Fabian Dagarro Kuwa Mkuu Wa Wilaya Ya Arusha

Askari wa Upelelezi Mwanza Auawa Baa......6 Watiwa Mbaroni, RPC Msangi Anena

$
0
0

Kwamba tarehe 21.08.2016 majira ya 10:00 usiku katika eneo la club ya villa park resort kata ya kirumba wilaya ya ilemela mkoa wa mwanza, askari namba g.5092 pc john nyange wa ofisi ya mkuu wa upelelezi na makosa ya jinai mkoa wa mwanza (rco), aliuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali eneo la shingoni na mtu aliyekuwa anaugomvi nae.

Inadaiwa kuwa marehemu alikua na ugomvi wa muda mrefu na mtu aliyejulikana kwa jina magina hussein miaka [27] fundi computer msukuma na mkazi wa mtaa wa kigoto, ambapo marehemu alikuwa akimdai bwana magina hussein computer aina ya laptop.  Ndipo usiku wa leo majira tajwa hapo juu walikutana eneo la club ya villa park huku mtuhumiwa wa mauaji hayo ikisemekana kuwa alikuwa na wenzake watano ndipo walimvamia na kumchoma na kitu chenye ncha kali shingoni na kufariki dunia njiani wakati akipelekwa hospitali.

Marehemu kwa sasa alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha stefano moshi memorial university college cha mjini moshi, alikuwa anasomea shahada ya sayansi ya habari na mawasiliano mwaka wa pili, aidha alirejea mwanza baada ya kupata likizo kuja kuiangalia familia yake ndipo umauti ukamkuta.

Watuhumiwa sita akiwepo magina selemani ambaye alikuwa na ugomvi na marehemu pamoja na wenzake watano wamekamatwa, wapo katika mahojiano na jeshi la polisi huku uchunguzi kuhusiana na kifo hicho ukiwa bado unaendelea,  pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani, mwili wa marehemu  umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya bugando kwa uchunguzi.

Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi ahmed msangi anatoa wito kwa wananchi wa jiji na mkoa wa mwanza, kwamba jeshi la polisi mkoa wa mwanza limesikitishwa na kifo cha askari huyu kwani limempoteza askari kijana ambaye bado jeshi lilikuwa linamtegemea. 

Lakini pia anawataka watu wenye tabia za kujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga wengine hadi kufikia kupoteza maisha kuwa wanafanya kosa la jinai, na kama watu wanadaiana wafuate taratibu za kisheria zilizowekwa ili kuepusha vifo vinavyoweza kuepukika, hivyo jeshi la polisi linawataka kuacha tabia hiyo mara moja kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Imetolewa na:
Dcp: ahmed msangi

Kamanda wapolisi (m) mwanza

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Atembelea Kijiji Cha Katumba Wilayani Mpanda,azindua Mnara Uliojengwa Na Wakimbizi Waliopewa Uraia Wa Tanzania

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa wakimbizi waliopewa uraia wa Tanzania na kuitumia vibaya nafasi hiyo kwa kuingiza watu wengine  kinyume cha sheria watanyang’anywa na kurudishwa walikotoka.
 
Aidha, Waziri Mkuu amewaomba viongozi wa dini wawe wanawaelimisha waumuni wao umuhimu wa kulinda amani na kuishi kwa kufuata sheria na taratibu za nchi husika. 
 
Kauli hiyo imetolewa jana (Jumapili, Agosti 20, 2016) na Waziri Mkuu wakati akizungumza na waliokuwa wakimbizi wa Burundi ambao kwa sasa wamepewa uraia wa Tanzania wanaoishi katika Kata ya Katumba, Halmashauri ya Nsimbo wilayani Mpanda. 
 
“Wakimbizi waliopewa uraia wameendelea kuingiza ndugu zao. Naagiza kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ifanye ukaguzi katika kambi zote kwa sababu zimegeuzwa kuwa maficho ya kuwahifadhi watu wanaoingia nchini bila ya vibali,” alisema. 
 
“Hakikisheni mnachukua hatua kwa wote watakaoingiza watu kinyemela katika kambi za wakimbizi za Mishamo na Katumba. Pia msiruhusu watu kuleta silaha kwenye maeneo haya. Tanzania watu wanaoruhusiwa kutembea na silaha ni askari tu,” alisisitiza. 
 
Waziri Mkuu alisema lazima ulinzi uimarishwe katika maeneo ya mipakani na wasipofanya hivyo watu wengi wataingia nchini bila ya kuwa na vibali hivyo kusababisha ongezeko kubwa la idadi ya watu. 
 
Wakati huo huo Waziri Mkuu ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda wasiwaudhi wakulima na wafanyabiashara wadogo kwa kuwatoza ushuru  kwenye mazao wanapotoka shambani kama debe moja la nafaka na wanaouza bidhaa ndogo ndogo. 
 
“Mkulima ametoka shambani na debe moja la mahindi unamtoza ushuru maana yake nini? Halmashauri tusitafute mgogoro katika hili. Tafuteni biashara za kutoza ushuru, mkulima anatoka kijiji cha Kanoge anakwenda kijiji cha Ikongo ushuru wa nini?" Waziri Mkuu alihoji. 
 
Waziri Mkuu alisema“Tumewasisitiza mkusanye kodi lakini siyo hivyo. Mkiendelea kutoza ushuru kwa wakulima wanaotoka shambani na mahindi kidogo mtasababisha wakate tamaa ya kulima,”. 
 
Akisoma taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Katavi jana jioni (Jumamosi, Agosti 20, 2016) mara baada ya Waziri Mkuu kuwasili mkoani hapa Mkuu wa mkoa, Meja Jenerali (Mstaafu) Raphael Muhuga alisema mkoa una jumla ya wakimbizi 6,918 wanaoishi katika kambi za Mishamo na Katumba ambapo kati yake wakimbizi 2,150 waliomba uraia wa Tanzania na kunyimwa. 
 
Alisema wakimbizi 2,489 walichagua kurejea nchini kwao Burundi ila bado wapo katika kambi hizo huku wengine 653 waliomba uraia lakini majina yao hayakuonekana kwenye orodha ya waliokubaliwa wala kukataliwa uraia hivyo mkoa unaendelea kufuatilia ili kujua hatma yao. 
 
Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa wakimbizi wengine sita walichagua kubaki nchini lakini hawakuomba uraia, 398 waliomba uraia ila fomu zao hazikukamilika,249 waliomba uraia ila majina yao hayakurudi huku wengine 973 hawakusajiliwa walipoingia nchini mwaka 2007/.2008.
 
 IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, AGOSTI 21, 2016.

Waziri Mkuu: Hatua Zichuliwe Kwa Watumishi Wanaoiba Dawa

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri nchini kuwachukulia hatua watumishi wote wa sekta ya afya wanaojihusisha na wizi wa dawa.

“Fuatilieni na kuwachukulia hatua watumishi wa Zahanati wanaoiba dawa. Hawa hawana nafasi ya kuendelea kufanya kazi kwa sababu ni wauaji,” alisema. 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo juzi jioni (Jumamosi, Agosti 20, 2016) wakati akipokea taarifa ya mkoa wa Katavi mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Alisema kila kiongozi kwenye eneo lake ahakikishe dawa zinazopelekwa na Serikali kwa ajili ya kuwahudumia wananchi zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Pia ameitaka Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kujenga duka la dawa mkoani Katavi kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa dawa katika mkoa huu pamoja na mikoa jirani.

Wakati huo huo Waziri Mkuu aliwataka Waratibu wa Elimu katika ngazi ya Kata na Wakuu wa shule za sekondari wasiokuwa na shahada waende wakasome kama wanahitaji kuendelea kuwa na wadhifa huo. 

Alisema Mratibu wa Elimu katika ngazi ya Kata ni lazima awe na shahada ili aweze kutekeleza majukumu yake ya kusimamia utolewaji wa elimu katika shule za sekondari na msingi.

Kwa upande wa walimu wakuu katika shule za msingi, Waziri Mkuu alisema ni lazima wawe na diploma, hivyo aliwataka walimu wakuu wote wasiokuwa na diploma kwenda kusoma kabla hawajaondolewa kwenye wadhifa huo.

Alisema Serikali imetenga zaidi ya sh. bilioni tano kwa mwezi ambazo ni posho ya madaraka, ambapo Waratibu Elimu Kata wanapewa sh 250,000 kwa mwezi huku Wakuu wa shule za sekondari na walimu wakuu katika shule za msingi wanapewa sh. 200,000.
 
Awali Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali (Mstaafu) Raphael Muhuga alisema mkoa umeendelea kuongeza bajeti ya dawa ili kuhakikisha dawa zinapatikana katika ngazi zote za kutolea huduma.

“Mwaka 2012 bajeti ya dawa na vifaa tiba ilikuwa sh. Milioni 558 ambayo ilitosheleza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa asilimia 70. Katika bajeti ya mwaka 2016/2017 mkoa umetengewa jumla ya sh bilioni 1.3 ambayo tunaamini itamaliza tatizo la upatikanaji wa dawa na vifaa tiba,” alisema.

Mkuu huyo wa mkoa alisema mfumo mpya wa usambazaji dawa kupitia MSD umesaidia dawa, vifaa tiba na vitendanishi kupelekwa moja kwa moja hadi katika ngazi ya zahanati hali iliyosaidia dawa kufika kwenye vituo vya kutolea huduma kwa asilimia 100.

Mapema jana Waziri Mkuu alifanya ziara katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda ambapo alisema Serikali itahakikisha hospitali hiyo inaongezewa huduma zaidi kwa sababu ni ya wilaya ila inahudumia wagonjwa wa mkoa wote.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, AGOSTI 21, 2016.

Wakili Atolea Ufafanuzi Madai ya Reginald Mengi Kuitwa Mahakamani Kujieleza Kwa Nini Asifungwe

Audio: Godbless Lema (Mb) amjibu Waziri Mwigulu Nchemba kuhusu Maandamano Septemba 1

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba amezungumza na kusema kuwa CHADEMA wasithubutu kuandamana kwani kwa kufanya hivyo si kuwa watakuwa wanatingisha kiberiti cha njiti, bali watakuwa  wanachezea gesi. Amesema kuwa sio kila kitu mtu anatakiwa kujaribu kwa sababu vingine huenda vikakuumiza.

Waziri ameyasema maneno hayo akiwaasa viongozi wa CHADEMA kutupilia mbali mpango wa maandamano na mikutano ya siasa nchi nzima Septemba Mosi.

Kufuatia kauli hiyo ya Waziri, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema haya. Msikilize hapa chini.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) Astaafu

$
0
0

MKURUGENZI Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Rashid Othman amestaafu rasmi wadhifa huo, huku akitajwa kuwa miongoni mwa viongozi waliofanya kazi nzuri wakiongoza taasisi hiyo nyeti.

Habari za uhakika kutoka ndani ya serikali, zilizopatikana jijini Dar es Salaam jana, zilisema kuwa Othman alistaafu rasmi wadhifa huo Agosti 19, mwaka huu akiwa ameiongoza taasisi hiyo tangu Agosti 20, 2006 ikiwa ni takribani miaka 10.

Kiongozi huyo aliteuliwa na Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kuwa Mkurugenzi Mkuu ili kuziba nafasi iliyoachwa na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa wakati huo, Cornel Apson Mwang’onda.

Aliapishwa Ikulu Dar es Salaam Agosti 21, 2006. Kabla ya uteuzi wake, Othman alikuwa Mkuu wa Utawala na Utumishi wa Idara hiyo ya Usalama wa Taifa na kufanya kazi nzuri, iliyochangia kumwezesha kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu.

Awali, Othman alitakiwa kustaafu mwaka 2013 kwa mujibu wa sheria, lakini aliendelea kuongezewa mkataba wa mwaka mmoja mmoja hadi alipokubaliwa kustaafu rasmi Ijumaa iliyopita.

Lipumba Aipasua CUF.......Wajumbe Warushiana Viti na Kutukanana, Mkutano Wavunjika

$
0
0

Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Wananchi (CUF), uliofanyika jana jijini Dar es Salaam ukilenga kuwachagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ulivunjika baada ya wajumbe kuanza kurushiana viti na matusi baada ya kupishana katika hoja ya kumtosa aliyekuwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba.

Profesa Lipumba alijiuzulu nafasi yake kabla ya kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka jana akieleza kuwa roho inamsuta kumnadi mgombea urais aliyeungwa mkono na vyama vya Ukawa. Lakini mwaka huu alirejea na kuandika barua akiomba kurejea kwenye nafasi yake hali iliyozua sintofahamu.

Taarifa kutoka ndani ya Mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe 832 walihudhuria lakini hoja ya kumjadili Profesa Lipumba ilipofikiwa, baadhi ya wajumbe ambao wanamuunga Mwenyekiti huyo wa zamani walizua vurugu wakipinga utaratibu uliotumika.

Baadhi ya wajumbe hao waliwaambia waandishi wa habari kuwa viongozi waliopo madarakani walifanya ubabe kwa kulazimisha kura ya kukubali au kukataa ombi la Lipumba ipigwe kwa uwazi na sio siri kama Katiba inavyoeleza.

“Haki haikutendeka, ni ubabe. Wala mkutano haikuzingatia kutimia kwa akidi. Tulilazimishwa kupiga kura kwa kunyoosha mikono wakati mazingira yaliyopo na usahihi, kura ni siri,” mmoja wa wajumbe hao alikaririwa.

Baada ya kupiga kura za wazi, Lipumba alipata kura 14 kati ya kura 832 hivyo kuonekana kukataliwa kwa kishindo, lakini vurugu zilizuka ghafla kutokana na maamuzi hayo na mkutano ukashindwa kufanikisha zoezi zima la kuwapata viongozi hao wapya.

Katika hatua nyingine, Juma Haji Duni alijiengeu katika kinyang’anyiro cha uchaguzi huo, baada ya baadhi ya wajumbe kusisitiza kuwa katiba inamtaka mtu aliyejiuzulu na kuhamia chama kingine kusubiri miaka miwili ili agombee nafasi ya uongozi ndani ya chama pale atakaporejea.

Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mipango wa CUF, Shaweji Mketo, alisema kuwa Duni alijiondoa kutokana na maadui wa Ukawa kutaka kukihujumu chama hicho.

Mkutano huo umeahirishwa hadi utakapotangazwa tena.

Wassira Aiomba Serikali Izungumze na Chadema ili Kumaliza Malumbano

$
0
0

Aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Chakula na Kada mkongwe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wassira ameomba wasaidizi wa Rais John Magufuli kumshauri kufanya mazungumzo na viongozi wa upinzani ili kuepusha madhara yanayoweza  kutokea kutokana na maandamano yanayopangwa kufanyika Septemba 1.

Wassira ameeleza kuwa washauri hao wanapaswa kufanya hivyo kwani bado nafasi hiyo ipo kuliko kuacha Rais aingie vitani na wananchi wake kwani madhara yatawapata Watanzania wote.

“Wazungumze ili wasimuingize Rais kupigana na watu wake kwa maana wote tutapoteza. Kwa nini uweke askari polisi wote hao, msimweke Rais kwenye vita na watu wake,” Wassira anakaririwa na Jambo Leo.

“Kinachohitajika ni wasaidizi wa Rais kumshauri ili kuhakikisha kuwa tofuati zilizopo baina yake na vyama vya upinzani haziendelei ili kuepusha madhara yanayoweza kuzuilika, itafutwe suluhu,” aliongeza.

Akizungumzia uamuzi wa Serikali kupiga marufuku kufanyika kwa mikutano na maandamano, alisema kuwa tatizo linaweza kuwa ni aliyekuwa Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa.

Alisema kuwa hii inatokana na joto la uchaguzi lililokuwepo pamoja na nia ya Lowassa kuzunguka nchi nzima kuwashukuru wapiga kura, kungeweza kuzua tafrani kubwa kwani alipata kura nyingi na alikuwa akidai ameshinda kwa asilimia 62.

“Ukiwaruhusu kufanya mikutano na ukwaambia kuwa atakayekuja kutoa shukurani ni Lowassa, ambaye amekuwa akipinga kushindwa ni sawa na kurejesha hali ya uchaguzi kipindi hiki,” alisema.

Alitaka Serikali kutoa elimu ya wazi kwa umma kuhusu sababu zinazopelekea kukataza kufanyika kwa mikutano ili kuweka mambo sawa.

“Kama mimi hapa nimetaja sababu kwamba inawezakana kuwa ni Lowassa. Sasa na wao Serikali waseme tu tunapiga marufuku mikutano na maandamano… wataje [sababu]na kuzifafanua,” alieleza.

Hata hivyo, Wassira aliwataka Chadema kusitisha adhma yao na kuhakikisha wanafuata utaratibu ili kupata haki ya kufanya maandamano na mikutano ambayo alieleza kuwa kila Katiba ya nchi duniani imeiweka, lakini bila kufuata utaratibu haiwezi kuruhusiwa.

Lowassa, Mbowe na Katibu Mkuu Chadema Waanza Mikakati ya UKUTA

$
0
0

Siku moja baada ya Chadema kutangaza safu ya Ukuta, viongozi wa chama hicho wameanza kutawanyika mikoani kuanza kutoa elimu ya mpango huo. 

Wakati mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe akiwa Kanda ya Kaskazini aliyekuwa mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa alikuwa mkoani Mbeya na jana alishiriki ibada na kuanza vikao vya mkakati huo. 

Mbowe jana alikutana na viongozi wa kanda hiyo na kuunda kamati zitakazokwenda katika majimbo yote 35 ya uchaguzi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara kutoa elimu. 

Mbowe alisema katika kikao hicho, ambacho ni mfululizo wa vikao vinavyoendelea kanda zote nchini, wamekubaliana kutoa elimu ya dhana ya Ukuta. 

Hata hivyo, alisema bado chama hicho kimetoa fursa ya mazungumzo kwa taasisi yoyote ili kuhakikisha mgogoro uliosababisha Kamati Kuu kuunda Ukuta. 

Wakati Mbowe akisema hayo, Lowassa ametua katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini inayojulikana kama Kanda ya Nyasa akiwa na mambo matatu makubwa. 

Aliwasili jana asubuhi kwa ndege ma kwenda moja kwa moja kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Forest akiwa na viongozi wa chama hicho wa kanda pamoja na wabunge mbalimbali wa majimbo ya mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa, Songwe, Rukwa na wale wa viti maalumu. 

Waziri Mkuu huyo wa zamani, alishiriki ibada ya kawaida na alipokea zawadi ya nyimbo zilizowekwa kwenye ‘flash’ kutoka kwa wanakwaya wa kanisa hilo huku naye akiwachangia kwa kuendesha harambee ya papo kwa papo kutoka kwa viongozi alioongozana nao. 

Katika harambee hiyo, zilipatikana Sh4 milioni zikiwamo Sh 1 milioni ambazo aliahidi kuzitoa. 

Kabla ya ibada kumalizika, Lowassa na ujumbe wake waliondoka kwenda kwenye kikao cha Baraza la Chadema la Kanda. 

Katibu wa Kanda hiyo, Frank Mwaisumbe alitaja mambo matatu makubwa kutoka kwa Lowassa kuwa la kwanza alihimiza wanachama wote kuimarisha umoja na kufuta mipasuko iliyotokea wakati wa uchaguzi. 

Pili, aliwasihi wana Chadema wote kuwa jasiri kwa kupigania haki na kujitambua na la tatu ni kujiandaa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika 2019 na Uchaguzi Mkuu wa 2020. 

Mwaisumbe alisema baada ya kikao cha jana, leo Lowassa anaanza kutembelea majimbo ambako atakuwa na vikao vya ndani katika majimbo ya Mbeya Vijijini, Mbozi na Tunduma na kesho atakuwa kwenye majimbo ya Nkasi Kaskazini na Kusini na Sumbawanga wakati kesho kutwa atakuwa Mbarali, Makambako, Njombe Mjini na Mafinga. Agosti 25 atakuwa Iringa Mjini na Kolo. 

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji yupo Kanda ya Serengeti inayojumuisha mikoa mitatu; Simiyu, Shinyanga na Mara na jana aliwataka Watanzania kuwapuuza watu wanaodai chama hicho kimejipanga kufanya vurugu Septemba Mosi akisisitiza kuwa maandamano yatakayofanyika ni ya amani. 

Alisema kamwe hawawezi kuvunja sheria na Katiba ya nchi na kwamba kinachofanyika kipo kwa mujibu wa sheria.

 “…Nawaomba Watanzania wote watuunge mkono maana tunachokwenda kukifanya ni kwa ajili ya kuwanusuru watoto wetu wasiingie kwenye matatizo maana kinachoendelea kinakwenda kuondoa demokrasia na utawala bora,” alisema.

VIDEO: Mbatia aizungumzia kauli ya Spika kuhusu maridhiano baina ya UKAWA na naibu Spika

$
0
0
Jana August 21 2016 kupitia kipindi cha funguka kinachorushwa na kituo cha television cha Azam Tv, mbunge wa Vunjo na mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia aliizungumzia kauli iliyotolewa na Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano kuwa anakusudia kutafuta maridhiano baina ya wabunge wanaounda umoja wa katiba, UKAWA na naibu Spika.

Mbatia alisema, Kauli ya Spika Ndugai ni kauli yenye kuleta matumaini kwa sababu wao ndani ya wabunge wa upinzani walichokuwa wanataka ni  maridhiano....

Msikilize hapo chini akiongea

VIDEO: Mbatia Amshangaa Magufuli ‘Kuwaziba Midomo ’ Wapinzani

$
0
0
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia amesema kitendo cha Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli  kuendelea na mikutano ya kisiasa mikoani na kuwazuia viongozi wa vyama vingine vya siasa ni kutaka kukwamisha demokrasia nchini.

Akizungumza jana katika kipindi cha Funguka kinachorushwa na Televisheni ya Azam, Mbatia alisema Rais Magufuli akiwa Singida, aliviponda vyama vya upinzani kuwa vimekufa.

“Akiwa Singida Magufuli alisema vyama vya siasa vya upinzani vimekufa na kuvilinganisha na nyoka aliyekanyagwa kichwa na kubakiwa na mkia tu unaocheza cheza,” alisema.

Alisema Agosti 12, mwaka huu Magufuli alikuwa mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam  akizungumza na wanachama wake  na kuonyeshwa na televisheni mbalimbali akikijenga chama chake.

“Nani anakwenda kuweka rekodi vizuri huko mikoani  kwa anayoyasema Magufuli kama anazuia wapinzani wasifanye siasa? Kwa hiyo yeye anajenga chama chake lakini anazuia wapinzani wasifanye hivyo,” alisema.

Alisema ikumbukwe kuwa Tanzania ni ya watu wote na wanatakiwa kufuata sheria na utaratibu uliowekwa na si vinginevyo.

Msikilize hapo chini akiongea

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Viongozi Wa Kisiasa Watakiwa Kuwa Wavumilivu.

$
0
0

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum

Na Sheila Simba-MAELEZO


Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum ametoa wito kwa viongozi wakisiasa Nchini, kuwa wavumilivu ili kulinda Amani ya Nchi.


 Sheikh Alhad ameyasema hayo leo, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam ambapo amewataka viongozi hao kutii mamlaka iliyoko kwani mamlaka hiyo imewekwa na Mungu na hivyo ni vema kutafuta njia nyingine kumaliza matatizo yanapotokea.


“Ipo haja ya kuvumiliana kwa ajili ya Taifa letu, kwani yanapotokea machafuko waathirika wakubwa ni wanawake, watoto na vijana wetu ambao wanaweza kupata madhara makubwa na hata kupoteza maisha’’alisema Alhad


Akizungumzia maandamano ya ukuta yaliyopangwa kufanyika Septemba Mosi, amesema kuwa kauli ya kuzuia maandamano hayo imetolewa na Rais wa Nchi na kuomba kauli hiyo kuchuliwa kwa uzito wa kipekee, kwani busara ni kusikiliza mamlaka imesema nini na kutii kauli hiyo ya Rais.


“Nawashauri  Watanzania wenzangu, viongozi wangu wa kisiasa jambo hilo si vyema tukashiriki kwani kutotii mamlaka ni dhambi ndivyo vitabu vya dini vinanavyosema,’’ alifafanua Sheikh Alhad


Ameongeza kuwa suala la kulinda amani ni la watanzania wenyewe kwa kusaidiana na Jeshi la Polisi ili kuhakikisha amani inaendelea kuwepo, kwani ni rahisi kupoteza amani tuliyonayo lakini ni vigumu kurudisha amani.


Amesema kuwa vijana wasikubali kutumika kwa maslahi ya watu wengine kwani kufanya hivyo ni kushindana na dola na kutolea mfano wa machafuko yanayoendelea kwa baadhi ya Nchi Duniani na kupelekea mataifa hayo kutokalika kutokana na vurungu za kisiasa.


Aidha amewaomba vijana kutokubali kulitia doa Taifa, kwani Tanzania inafahamika ni kisiwa cha Amani Duniani na inapaswa kulinda heshima hiyo ili kuendelea kutunza amani ya Watanzania wote bila kujali tofauti za kisiasa.


Amewaomba viongozi hao wa kisiasa kuwasilisha malalamiko yao kwa njia tofauti kwani Serikali iliyopo madarakani ni sikivu na ipo kwa ajili ya wananchi wote.


Taarifa ya Jeshi la Polisi Kwa Vyombo Vya Habari

$
0
0

Katika siku za hivi karibuni, kumekuwepo na mitazamo tofauti miongoni mwa jamii kufuatia kuonekana kwa askari polisi wakifanya mazoezi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kufuatia hali hiyo, jeshi la polisi nchini, linatumia fursa hii kuwatoa hofu wananchi kwamba mazoezi hayo ni ya kawaida kwa askari wa jeshi la polisi

Aidha, jeshi la polisi linawataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kawaida kwa sababu mazoezi hayo hayalengi kuzuia shughuli zozote halali zinazofanywa na wananchi.

Imetolewa na:
Advera John Bulimba – Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP)
Msemaji wa Jeshi la Polisi,
Makao Makuu ya Polisi.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 25 & 26 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0

 Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

 
Ilipoishia...
Nikambusu sheila mdomoni na kufungua mlango na kutoka na moja kwa moja nikashuka hadi kwenye chumba alicho nielekeza  sheila.Nikagonga mlango mara tatu na suti ya kike iliyopo ndani ya chumba hicho ikaniruhusu niingie.

Nikafungua mlango na kuwakuta manesi watatu wakiwa wameshika mashavu yao huku wakionekana wanyongea na macho yao wameyaelekezea kwenye kioo cha tv iliyopo ndani ya chumba hicho.

Na mimi ikanibidi ninagalie wanacho kitazama na kukuta mipigo ya moyo yakiende kwa kasi baada ya kuiona ndege kubwa ikiwa imeanguka huku inawaka moto na kutoa moshi mwingi na mweusi huku kikosi cha zima moto ambacho sikujua ni cha nchi gani wakijitahidi kuzima moto kwa kutumia magari yao maalumu ya kuzimia moto huku baadhi ya miili inayoonekana kuwa imefariki ikitolewa ndani ya ndege hiyo

Endelea...
“karibu kaka yangu tukusaidie nini?”
Nesi mmoja aliniuliza swali ila sikumjibu nikabaki nikiitazama taarifa inayorushwa kupitia kituo cha televishion ya sky news kinachopatikana nchini uingereza.Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio kana kwamba nimekimbia umbali mrefu pasipo kupumzika.Nikayasoma maandishi makubwa yaliopo ubavuni mwa ndege hiyo na kukuta yameandikwa emirates kiasi kwamba nikajikuta nikishusha pumzi taratibu na manesi wote wakabaki wakinitazama.

“kaka kaka”
“naam”
“mbona unashangaa?”
“ninatazama hiyo taarifa ya habari”
“inasikitisha sana kwa maana watu wote waliopo kwenye hiyo ndege wamefariki”
“imekuwaje hiyo ndege ikaanguka?”
“ilianguaka kipindi inapaa imesababishwa na hali ya hewa kutokuwa nzuri”
“imeangukia nchi gani?”
“imeangukia tailand”

Kidogo nafsi yangu ikapata unafuu na tabasanu likarudi usoni mwangu taratabu kwani nilidhani itakuwa ni ndege ambayo amepanda mama.Nikawaomba dawa za kutuliza maumivu ya kichwa wakanipatia pamoja na maji nikazinywa na kuwashukuru na kuondoka na kuwaacha wakiendelea na shughuli zao.Nikaenda kwenye maduka ya simu ambayo hayakuwa mbali sana na hopsitali na kununua simu kwa ajili ya sheila na kupitia kwenye sehemu wanapouza chipisi.Nikanunua chips za kutosha na kurudi hospitali na kumkuta sheila akizungumza na madaktari.
“hali yako inazidi kuridhisha na baada ya siku kadhaa tunaweza kukupa ruhusa ya kutoka hospitali”

“kwani hamuwezi kunipata hata leo?”

“kwa leo ni vigumu inabidi umalizie dozi yako ya vidonge na sindano za kukausha kidonda na baada ya hapo tutakuwa huru katika kukuruhusu.”

Tukakaa hospitalini siku mbili huku nikiendelea kumuuguza sheila na ndani ya siku mbili sikuweza kupata taarifa yoyote kuhusiana na mama juu ya kupatikana kwa ndege yao ambayo imetekwa na watu wasio julikana.Sheila akaruhusiwa kutoka hospitalini na akapewa vidonge ambavyo endapo atajisikia maumivu ameze.Nikapepeleka gari gereji kufanyiwa ukarabati wa vitu vidogo vidogo na kumuacha sheila akijiandaa kwa ajili ya safari ya kurudi dar es salaam.

“kaka hii gari umeinunua wapi?”
“kwa nini?”

“nina mwaka wa 21 tangu nianze kutengeneza magari ila sijawahi kuiona gari ya dizain hii kwa maana mmmm imekusanya mambo mengi”
“ahaaa hizi gari mbona zipo ukihitaji unazipata tuu”
“aise ila hii gari si chini ya milioni mia na kitu”
“imezidi zaidi ya hapo”

Niliendelea kuzungumza na fundi mkuu wa gareji ambayo nimeileta gari yangu,nikastukia nikiguswa bega kwa nyuma nikageuka na kukutana na sura ya madam rukia na kunifanya nistuke kiasi kwamba mapigo ya moyo yakaaza kunienda mbio.

“mbona unastuka eddy?”
“ha.....Pana nimeshangaa tu kukuona hapa”
“wife(mke) unajuananaye huyo kijana?”
Fundi gereji aliuliza swali na kujikuta nikizidi kupata kigugumizi chakuzumza kiasi kwamba nikaabaki nimekaa kimya

“ndio ni mwanafunzi wangu wa kidato cha tano,huyo ndio chanzo cha shele yetu kufungiwa”
“kaka sura yako inaonyesha mpole kumbe ni mkorofi kiasi hicho?”

“hapana mambo ya kawaida”
Nilizungumza huku nikibabaika kwani kila nikimtazama madam rukia ninakumbuka tukio lililotokea porini na jinsi nilivyo fanya naye mapenzi kwenye kichaka isitoshe nikakumbuka niliusikia mlio wa bunduki na kujua ni lazima atakuwa ameuawa na mkuu wa shule.

“ehee lete story edy ile siku ilikuwaje?”
Madam rukia aliniuliza swali baada ya mume wake kuondoka na kuingia kwenye moja ya chumba na kuanza kuzungumza  na wafanyakazi wake.Nikamuadisia madam rukia kuanzia tulipo achana hadi nikafika hopsitalini na yeye akaanza kuniadisia tangu tulipo achana.

“mimi ile siku bwana nilikutana na vijana ambao ni wanakijiji cha karibu kwenye ule msitu wenyewe walikuwa wanakwenda kuwinda.....Sasa pale ulipo niacha mkuu wa shule na wezake si wakawa wananifwata basi wale vijana wakatanda ile sehemu tuliyopo na kuanza kuwashambulia waalimu na kuwatoa mbio za kufa mtu basi ikawa ndio pona pona yangu”

“mbona nilisikia mlio wa bunduki alipigwa nani?”
“ahh mkuu wa shule si alikuwa anajifanya kidume anapiga bastola juu hewani ili kuwatisha wale vijana......Wee alipigwa gongo moja la pua hata sijui ile bastola aliitupia wapi nilisikia akitoa ukulele wa uwii na kuanza kukimbia....Sasa na ile miguu yake yenye matege ya kaekejea upande mmoja ungekuwepo ungecheka”

“mmmm sasa ulirudije mjini?”
“wale vijana wakaniazimisha simu na nikampigia my husband(mume wangu) nikamuelekeza nilipo akaja kunichukua na tukarudi mjini pamoja”
“ulimuambia jamaa kuhusiana na jinsi ulivyo fika porini?”

“ndio ila nilimuambia kuna majambazi ndio waliniteke...Ehee madam merry anaendelea vizuri amefanyiwa upasuaji na kizazi chake kimerekebishwa vizuri ila sasa hivi yupo powa”

Madam rukia alibadilisha mada baada ya mume wake kufika katika eneo tulilopo na sikuwa na haja ya kujiuliza ni kwanini amebadilisha mada nikajua moja kwa moja ahitaji mumu wake atambue kuwa mimi nilikuwa naye porini

“hivi wamesemaje kuhusiana na swala zima la shule kuendelea?”

“wamesema watatoa tangazo kwenye vyomba vya habari pele shule itakapo funguliwa ila kwa sasa wameunda tume ya madai yaliyopelekea shule kufungwa ambayo itachunguza kila kitu na wanafunzi walio kamatwa na polisi wapo wengine wanahojiwa”

“sasa hiyo tume watatumia muda gani kuchunguza hayo madai yato kwa maana siku zinakwenda mbele na masomo ndio hivyo yamesimama?”

“mimi wala sielewi ila kidato cha sita na cha nne wamesambazwa kwenye shule za jirani ili kuendelea na masomo hadi pale majengo yatakapo fanyiwa ukarabati nao ndio watarudi”
“ahaaa....”
“wewe sasa hivi unakwenda wapi dar au kwa marry?”
“huyo merry mimi wala sihiaji kumsikia kwa maana mume wake amenizingu sana majuzi”
“wee amekuonea wapi?”
“si nilikwenda kumcheki hospitalini sasa nikawakuta wana mazungumzo yao basi mimi ikanibidi niwaache niondoke zao basi jamaa akanifwata na kuanza kunipiga vibao mbele za watu na mimi nikampiga basi mambo yakaharibika pale hospitali nikaamua kumpotezea”

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images