Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Aiagiza Wizara Ya Kilimo, Mifugo Na Uvuvi Kuwachukulia Hatua Watendaji Wote Waliohujumu Ushirika

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananachi wakati lipotembelea maonyesho ya wakulima Nanenane kwenye uwanja wa John Mwakangale jijini Mbeya Agosti 8, 2016. Kushoto kwake ni mkewe Mary
*******

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuhakikisha inafufua sekta ya ushirika na kuwachukulia hatua kali watendaji wote waliohujumu ushirika na kusababisha machungu kwa wanaushirika ili iwe fundisho kwa wengine.

Pia ameitaka Wizara hiyo kupitia upya sekta ya ushirika kwa kuanza na viongozi walipo ndani ya wizara hadi mikoani kuhakikisha kama wanafanya kazi zao ipasavyo na kuwaondoa watakaobainika kwa uzembe.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo leo (Jumatatu, Agosti 08, 2016) wakati akifunga maadhimisho ya sherehe za nane nane kwa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yaliyofanyika kwenye uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.

Hata hivyo Waziri Mkuu amesema mkulima, mfugaji na mvuvi mdogo au mmoja mmoja hawezi kupunguza umaskini bila ya kuwa na chombo cha kuwaunganisha na kuwapa nguvu ya kutetea bei ya mazao yao kama ushirika. Aidha, ushirika imara utawasaidia kutafuta soko, kupata mikopo ya riba nafuu.

Amesema pamoja na umuhimu wa kuwepo kwa ushirika, tasnia hiyo imewaumiza wakulima wengi na kuwafanya kukata tamaa katika uzalishaji kutokana na usimamizi mbovu, ubadhirifu na ubabe wa baadhi ya viongozi wa ushirika.

“Wahimizeni na kuwashawishi wakulima, wafugaji na wavuvi kujiunga katika vikundi vya ushirika vya uzalishaji na SACCOS. Aidha, elimu ya ushirika inayotolewa kwenye maonesho ya mwaka huu, iwe changamoto kwenu kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu,” amesema.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amesema Serikali haitamvumilia mfugaji anayelisha katika maeneo ya hifadhi na vyanzo vya maji, Wakuu wa Mikoa na Wilaya waendelee kulinda maeneo hayo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha alisema sekta ya kilimo imekuwa na mafanikio makubwa ambapo katika kipindi cha miaka mine mfululizo nchi imeweza kuzalisha chakula cha ziada, ambapo kwa mwaka huu imezalisha kwa asilimia 123.

“Mafanikio hayo yanachangiwa jitihada za Serikali katika kutoa ruzuku ya pembejeo, taasisi za utafiti ambazo zimekuwa zikitafiti aina bora ya mbegu zikitafuta mbegu bora na wakulima walioamua kuwekeza kwenye kilimo,” alisema.

Naibu Waziri Ole Nasha alisema katika ukanda wa Nchi za Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ni nchi mbili tu za Tanzania na Zambia kati ya nchi 15 za jumuia hiyo hazikabiliwiu na baa la njaa.

Licha ya mafanikio hayo Naibu Waziri huyo aliwaomba wakulima kuendelea kuzalisha kwa kufuata kanuni bora za kilimo pamoja na kutumia pembejeo bora.

Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Ladislaus Mwanakatwe ameipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuwatetea pamoja na utatuzi wa kero za muda mrefu zilizokuwa zinawakabili wakulima ikiwemo ya tozo.

Hata hivyo Mwanakatwe ameiomba serikali kuitafutia ufumbuzi changamoto ya upatikanaji wa masoko ya uhakika ya mazao ya kilimo. Pia ameomba Serikali iwezeshe Benki ya Kilimo (TADB) kufungua matawi katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ili wakulima wake waweze kupata mikopo kwa urahisi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 08, 2016.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Hamisi Kigwangalla Amkana Dr Mwaka

0
0

Kuna baadhi ya magazeti na mitandao imekuwa ikiandika kuwa Dkt. Kigwangalla amesoma high school na aliyekuwa 'Tabibu', Ndg. Juma Mwaka, shule ya Kigoma Sekondari na kwamba walikuwa marafiki; hizi ni habari za uongo, za kupika zenye kupotosha ukweli ili kuwaaminisha watu kuwa 'wanajuana' na pengine wana ugomvi 'binafsi'.

Nimekuwa nikimpuuza kwa sababu sikuwa na haitotokea nikawa na nia mbaya dhidi ya mtanzania mwenzangu yeyote kwa sababu tu mimi nina dhamana ya uongozi. Sinaga tabia hiyo.

Uongo ukirudiwa rudiwa hubadilika na kuwa ukweli. Leo nimeamua, hapa chini, kukanusha ili watanzania pia mumpuuze, tuendelee kuimarisha huduma za tiba asili na tiba mbadala kutoka kwa matabibu wa kweli wanaofuata taratibu na siyo wasanii kama huyu. Uongo ama uzushi dhidi yangu mimi binafsi kamwe hautonirudisha nyuma mimi kama mtumishi wa umma. Lazima ifike mahali tujenge nchi ya watu 'serious' wanaofuata Sheria, Kanuni na Taratibu. Wanaoheshimu Serikali. Kwenye Afya za watanzania hatuwezi kuvumilia usanii, lazima tuwalinde walaji. Hili ni jukumu tulilopewa na Mhe. Rais. Tutasimamia Sheria ipasavyo. Hatutolegeza hata kidogo.

1. Sikusoma 'high school' Kigoma Sekondari. Nimesoma O'level (form I - IV) Kigoma Sekondari. High School nilisoma Shinyanga Sekondari. Sikumbuki kusoma katika shule zote hizi mbili na mtu mwenye Jina Hilo. Kama alisoma Kigoma Sekondari labda mbele yangu ama nyuma yangu. Pia kipindi nasoma Kigoma Sekondari, hakukuwa na 'high school'.

2. Ndg. Juma Mwaka hajawahi kuwa rafiki wala adui yangu. Sina ugomvi binafsi. Nafanya kazi ya kusimamia Sheria ya tiba asili na tiba mbadala ipasavyo.

3. Naithamini tiba asili na tiba mbadala na Ndiyo maana nimeongoza Wizara ya Afya kufanya Mapinduzi makubwa kwenye eneo hili, ikiwemo kuweka utaratibu mzuri na rahisi zaidi wa kusajili watoa huduma, dawa zao, mazingira wanapotunzia dawa, wasaidizi wao, viwanda vyao, na pia kuweka mikakati ya uanzishwaji wa viwanda vya dawa za tiba asili na tiba mbadala sambamba na kufanyia utafiti dawa zao na kudhibiti ubora wa dawa zenyewe na dozi wanazowapa wateja.

4. Muulizeni Ndg. Juma Mwaka anaposema ana ugomvi 'binafsi' na mimi, anamaanisha nini, ugomvi upi? Juu ya nini? Awape taarifa kamili. Mimi Sina ugomvi naye. Kwanza sikuwahi kumjua kabla ya ziara yangu ya kikazi pale Foreplan, ntakuwaje na ugomvi na mtu nisiyemjua? Si utakuwa ujuha huo?

5. Mnaofuatilia suala hili mtakeni Ndg. Juma Mwaka awape majibu ya Msingi ya hoja za wakaguzi kutoka Wizara ya Afya. Mimi nilikuwa msimamizi nikiwapa nguvu wataalam wafanye kazi yao. Wataalamu walikuwepo, nao ana ugomvi nao 'binafsi'? Mwambieni awajibu kama dawa za tiba ya kisasa kukutwa kwenye eneo lake la kazi ilikuwa halali? Alikuwa na vibali vya kutunza zaidi ya maboksi 200 ya dawa? Alikuwa na vibali vya kutunza zaidi ya magunia 10 ya dawa za tiba asili na tiba mbadala baada ya kufutiwa usajili? Alikuwa na uhalali wa kuendelea kutangaza kwenye vyombo vya habari kuwa wateja wake wafuate dawa pale ili wasikatishe dozi? Tena kinyume na katazo la Baraza la tiba asili na tiba mbadala! Yeye yuko juu ya Serikali? Yuko juu ya Sheria? Ama anadhani anaweza kuidhihaki na kuiogofya Serikali?

6. Baada ya ziara yangu ya December 2015, ambapo sikutoa maelekezo ya kumfungia wala kumfutia kibali, niliwaelekeza Baraza la Tiba Asili na Tiba mbadala kuwa wawaite wawaelekeze matabibu wote wafuate Sheria, kanuni na taratibu. Waliitwa. Wakaelekezwa. Waungwana wakatii. Yeye hakutii, wakamfuta. Baada ya kufutiwa usajili, akaendelea kujitangaza na kutoa huduma, yeye ni nani?

7. Kufanya haya ni kuvunja sheria za nchi. Na makosa haya yana adhabu zake. Sisi kama Serikali tumeagiza hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake. Serikali ina mkono mrefu, itamkamata. Itamtia nguvuni na atafikishwa mahakamani. Ataenda kujitetea huko kuwa ana 'ugomvi binafsi' na Naibu Waziri Kigwangalla!

Mwisho, aende akafuatilie kisa cha mfanyabiashara wa kigiriki aliyesema ameiweka Serikali mfukoni - Mwalimu Nyerere alimfanya nini!

Dkt. Hamisi Kigwangalla, MB.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Agosti 9

Vyuo Vya Udereva Visivyo Na Sifa Mbioni Kufungwa

0
0

JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limesema litavifungia vyuo vyote vinavyotoa mafunzo ya udereva nchini bila ya kuwa na  sifa.

Kauli hiyo ameitoa Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Kamishina wa Polisi (DCP) Mohamed Mpinga wakati akifungua mkutano wa pili wa Chama cha Shule Binafsi za Udereva Tanzania (Chashubuta) uliofanyika Dar es Salaam jana.

"Kuanzia sasa Jeshi la Polisi halitasita kukifungia chuo chochote cha udereva kitakachokosa sifa kwani kwa kulea shule mbovu tutaendelea kupata ajali na hivyo kuongeza vifo na majeruhi" alisema Mpinga.

Mpinga alisema kwa mujibu wa sheria ya shule za udereva sura 163 ya 1965 (R.E 2002) mpaka sasa jeshi la polisi limesajili shule za udereva 260 ambazo zitategemewa kutoa madereva bora wenye ueledi wa kutosha kutokana na kuwa chanzo kikubwa cha ajali ni makosa ya kibinadamu ambayo yanafanywa na madereva.

Alisema jeshi hilo litafanya msako nchi nzima kuvibaini vyuo ambavyo havina sifa na wamiliki wake kuchukuliwa hatua na kuwafikisha kwenye mkono wa sheria.

Mwenyekiti wa Chashubuta Taifa, Robert Mkolla wakati akisoma risala yao mbele ya Mpinga ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mkutano huo, alisema moja ya changamoto waliyonayo ni baadhi ya wadau wa sekta ya usafiri na usafirishaji kutoona mchango mkubwa unaofanywa na shule za udereva za watu binafsi wakiamini kuwa vyuo vinavyotoa elimu nzuri ni vile vya serikali pekee.

Mkolla alimuomba Kamanda Mpinga uboreshwaji wa mitaala mara kwa mara ili kwenda na mahitaji ya barabara, vyombo na wakati na shule hizo ziwe zinashirikishwa katika kutoa michango ya uboreshaji wa mitaala hiyo.

Serikali yapanga kurasimisha kazi za sanaa nchini

0
0

Serikali kupitia Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo imedhamiria kurasimisha kazi ya sanaa kuwa shughuli rasmi ya kiuchumi katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokuwa akizundua msimu wa tatu wa kipindi cha televisheni cha kusaka vipaji vya wasanii chipukizi cha Club Raha Leo Show na kuahidi kutoa ushirikiano kwa wadau wa sanaa na wasanii ili kufanikisha azma ya serikali ya kurasimisha sekta hiyo kuwa rasmi kama shughuli ya kiuchumi.

“Tutashirikiana na nyinyi katika kuiendeleza sekta ya sanaa nchini ili kuwezesha vijana wengi wenye vipaji kuweza kujiajiri na kuajiri wengine kupitia kazi zao za sanaa” alisema Mhe. Nape.

Mhe. Nape Moses Nnauye amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kudhamini mashindano mbalimbali ya kuibua vipaji vya wasanii chipukizi ili kuweza kufikia malengo ya kuendeleza sekta ya sanaa nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt Ayoub Rioba amesema kuwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) litaendelea kushirikiana na wadau wa sanaa nchini kuibua na kuendeleza vipaji vya wasanii mbalimbali ili kuwezesha sanaa kuwa ajira rasmi katika kuinua kipato cha msanii na uchumi wa taifa kwa ujumla.

Naye Mratibu wa Club Raha Leo Show Bibi. Susan Mungi amesisitiza wasanii kuheshimu kazi zao na kuzifanya kwa ustadi mkubwa kwani ndio nyezo muhimu katika kuendeleza kazi ya sanaa nchini kwa kuifanya kuwa kazi mojawapo ya kiuchumi.

Club Raha Leo Show ilianzishwa kama Kipindi cha redio kilichorushwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na baadae kuwa shindano kubwa Tanzania la kusaka, kuibua na kuendeleza vipaji vya wasanii wanaochipukia nchini, na huu ni msimu wa tatu wa shindano hilo.

Nay wa Mitego kuachia video ya wimbo ‘Pale Kati’ Jumatano hii

0
0

Rapper Nay wa Mitego amedai ametimiza matakwa aliyopewa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) baada ya kufungiwa kwa wimbo wake wa ‘Pale Kati’, ambapo Jumatano hii taachia version ya kwanza ya video ya wimbo huo.

Nay amewataka mashabiki wake wa muziki wa kimataifa kukaa mkao wa kula.

“Mimi na BASATA tulishamalizana, wao walinipa maazimio na mimi nimeshayatekeleza, kwa hiyo na mimi naendelea na issue zingine,” alisema Nay.  

“Jumatano hii mashabiki wangu Wakimataifa pamoja na wa kwenye mitandao ya kijamii wakae mkao wa kula, naachia video,”

Rapper huyo alisema wimbo wa ‘Pale Kati’ una nguvu kubwa sana na unafanya vizuri katika baadhi ya nchi kama Kenya, Uganda pamoja na Ghana, na ndio maana ameamua kuanza kutoa video kwa ajili ya kimataifa kwanza.

Pia amewataka mashabiki wa muziki wake kuendelea kusubiria mambo mazuri kwani wimbo huo una video nne.

Lowassa Aibukia Nanenae Morogoro na Kutoa Ushauri Mzito Kwa Wakulima

0
0
WANANCHI wametakiwa kutumia tafiti zilizopo ili kuboresha kilimo kuwa cha kisasa na chenye tija ili kiweze kuwakwamua na umaskini.

Ushauri huo ulitolewa na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa baada ya kutembelea mabanda kwenye uwanja wa maonyesho ya kilimo wa Mwalimu J. K. Nyerere mjini Morogoro juzi.

Lowassa alieleza kuvutiwa na mafanikio makubwa na ubunifu kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza zaidi katika maonyesho hayo siku za usoni kwa kujifunza.

Aidha, Lowassa aliwashauri vijana kutumia maonyesho kama hayo kuwasilisha tafiti walizozifanya katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, ili Watanzania wengi waweze kuzitumia kwa manufaa ikiwamo kujifunza na kubadilisha utendaji wa mazoea na kuwa wa kisasa kwa faida yao na taifa.

Lowassa alisema maendeleo duniani yanafikiwa kutokana na tafiti na kushauri kama Watanzania watatumia vyema matokeo ya tafiti zinazoendelea kufanywa na wataalamu, wataweza kufika mbali.

Katika ziara hiyo Lowassa alivutiwa na banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambamo alipongeza shughuli za uzalishaji wa kisasa wa mazao mbalimbali ikiwamo mboga.

JKT ilikuwa ikionyesha kilimo cha kutumia nyumba ya kijani (green house), ufugaji wa kisasa wa mbuzi wa maziwa, kuku, uvuvi na teknolojia nyingine zinazohusu sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Maonyesho hayo ambayo kitaifa yalikuwa mkoani Lindi, yalifikia kilele jana kwa kuhutubiwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Godbless Lema Amtumia Waraka Mzito Rais Magufuli

0
0

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), amemuandikia waraka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli akimsihi kuruhusu kufanyika kwa mikutano ya kisiasa nchini bila kujali mipaka ya majimbo.

Lema amepaza sauti yake kupitia waraka wake kwa Rais Magufuli, uliosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, waraka ambao alithibitisha kuwa ni wake.

Katika waraka huo, Lema ambaye pia na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alimsihi Rais Magufuli kuviruhusu vyama vya siasa kufanya mikutano hiyo kwani ni sehemu ya matakwa ya katiba.

Alitahadharisha kuwa endapo mambo yaliyoruhusiwa kikatiba hayataruhusiwa, ipo siku amri za utekelezaji wa masuala muhimu kikatiba hazitachukuliwa kwani hakutakuwa na sababu ya kuheshimu katiba na utawala wa sheria.

“Kama hatuwezi kufanya tunayoruhusiwa na Katiba, na anayetuzuia mamlaka yake yametokana na Katiba, hakika mbegu inayopandwa ni hatari kwa ustawi wa Taifa, ipo siku amri ya utekelezaji juu ya masuala muhimu haitachukuliwa kwa sababu umuhimu wa kuheshimu katiba na utawala wa Sheria hautakuwepo,” aliandika.

Lema alimueleza Rais Magufuli kuwa Siasa ni kazi kama zilivyo kazi nyingine na kwamba mfumo huo ndiyo chanzo cha madaraka waliyonayo hapa nchini.

“Mheshimiwa Rais, siasa ni kazi na ndiyo maana wewe ni rais kwa sababu ya siasa, na mimi ni mbunge kwa sababu ya siasa, tena ni kazi muhimu sana tu kwani ndio mfumo pekee unaotafuta utawala wa ngazi mbalimbali na wa juu kabisa katika nchi,”

Aidha, Lema alimsemea kwa Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekitiwa CCM, Msemaji wa chama hicho, Christopher Ole Sendeka kwa kukiuka amri aliyoitoa Rais kwa kufanya mkutano Longido ambako sio jimbo lake.

“Mheshimiwa Rais, jambo hili litaleta mpasuko katika taifa letu, ni kauli inayopaswa kurekebishwa haraka. Hivi karibuni, msemaji wa CCM, Ole Sendeka alifanya mkutano Longido. Je, Ole Sendeka ni Mbunge wa Longido? Au polisi wa Mkoa wa Arusha hawakusikia tamko lake? " Alihoji.

Mbunge huyo alisisitiza kuwa Chadema itafanya maandamano Septemba Mosi mwaka huu, huku akihoji madhara yanayoweza kujitokeza siku hiyo, hivyo akamuomba Rais kutengua amri yake ya kuzuia mikutano ya hadhara

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Freeman Mbowe na Tundu Lissu Waitwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi

0
0

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu wameandikiwa barua na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, wakitakiwa kujieleza kwa matamko yao waliyoyatoa katika siku za hivi karibuni.

Lissu amekiri kupokea barua kutoka kwenye Sekretarieti hiyo akieleza kuwa imeandikwa na Jaji mmoja mstaafu ambaye hata hivyo hakumtaja jina.

“Ni kweli mimi na Mwenyekiti Mbowe tumepata barua hiyo. Ni barua ya ajabu ambayo imeandikwa na mtu aliyewahi kuwa Jaji wa mahakama kuu,” Lissu anakaririwa na Mwananchi. “Sitaki kuzungumza mengi kwa sasa, Jumatano nitalizumzia vizuri jambo hili,” aliongeza.

Hata hivyo, Kamishna wa Sekretarieti, Jaji Mstaafu Salome Kaganda alieleza kutofahamu chochote kuhusu barua hiyo iliyodaiwa kuwafikia viongozi hao wa Chadema.

“Mimi sifahamu kuhusu suala hilo, sina taarifa,” Jaji Kaganda alimueleza mwandishi wa gazeti hilo.

Hata hivyo, hali hiyo imeibua maswali kwani viongozi hao wa siasa ambao pia ni wabunge, hawana sifa za kuwa watumishi wa umma na hakuna kiapo cha utumishi wa umma kinachowabana.

Mbowe na Lissu walihojiwa hivi karibuni na Jeshi la Polisi kutokana na matamshi yao wakati wa kutangaza Operesheni UKUTA. Lissu anadaiwa kutoa kauli za kichochezi na kuidharau mahakama.

Mahakama Kuu Yampunguza MAKALI Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP)

0
0

MAMLAKA ya kugomea dhamana za watuhumiwa aliyokuwa nayo Biswalo Mganga, Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), sasa imeondolewa na mahakama kuu.

Awali, DPP alikuwa na uwezo wa kuzuia  dhamana za baadhi ya watuhumiwa kwa namna alivyoona inafaa licha ya kuwepo kwa malalamiko ya uhalali wa kuzia dhamana hizo.

Miongoni mwa sababu ambazo zimekuwa zikitolewa na DPP  ni maslahi ya umma hivyo kusababisha haki ya kupata dhamana kuwa ngumu.

Kwa kuwa hatua hiyo inakiuka Katiba ya Tanzania, Mahakama Kuu imefikia uamuzi wa kumwondolea mamlaka hayo DPP.

Kifungu kilichokuwa kikimpa mamlaka DPP ya kuzuia dhamana ni 148 (4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) na kwamba, kinakwenda kinyume na Ibara ya 13 (6) (a) ya Katiba ya Tanzania.

Uchambuzi wa udhaifu wa kifungo hicho kilichokuwa kikitumiwa na DPP ulitolewa na Majaji Sekieti Kihiyo na Dk. John Ruhangisa wakiongozwa na Jaji Kiongozi Shaaban Lila.

“Imeamriwa mtuhumiwa aliye chini ya ulinzi wa polisi au mtuhumiwa yoyote, anatakiwa kupewa haki yake ya kujitetea kabla ya haki hiyo haijazuiliwa na mkurugenzi wa mashitaka kwa pingamizi la kuwanyima dhamana,” sehemu ya taarifa ya majaji hao imeeleza hivyo.

Kifungu cha 148 (4) kinasema;“bila kujali kitu chochote kilichopo kwenye kifungu hiki, hakuna afisa polisi wala mahakama atakayeweza, baada ya mtu kukamatwa na wakati anasubiri shauri au rufaa, atathibitisha kwa maandishi kwamba kuna uwezekano kwa usalama au maslahi ya Jamhuri.

“…na cheti kilichotolewa na Mkurugenzi wa Mashitaka chini ya kifungu hiki kitaanza kutumika kuanzia terehe kitakapowasilishwa mahakamani au kutaarifiwa kwa afisa msimamizi wa kituo cha polisi na kitaendelea kutumika hadi mwenendo utakapohitimishwa ama mkurugenzi wa mashitaka atakapokiondoa.”

Kuondolewa kwa mamlaka ya DPP kuzuia dhamana za watuhumiwa kulitokana na kupelekwa pingamizi la kikatiba lililowasilishwa na Jeremiah Mtosebya, Mkazi wa Jiji la Dar es Salaam ambaye amesema kifungu hicho kinakiuka Katiba ya Tanzania.

Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa agundua Ufisadi wa Kutisha soko la Mwanjelwa.......Amuagiza CAG Afanye Ukaguzi

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenda kufanya ukaguzi maalumu katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya baada ya kuwepo kwa ubadhilifu katika ujenzi wa soko la Mwanjelwa.

“Inasikitisha ujenzi wa soko hili kuingia ubabaishaji. Ujenzi wa soko ungegharimu sh bilioni 16 ila sasa watendaji wamefanya mambo ya hovyo na kufikia sh bilioni 26 hatuwezi kuwavumilia lazima hatua zichukuliwe kwa wote watakaobainika katika ubadhilifu huu,” alisema.
 
Pia amempa siku tatu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla kufanya uchunguzi na kubaini nani aliyetafuna sh milioni 489 zilizotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya uendelezaji wa soko hilo ambazo hazijulikani zilipo.

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo leo (Jumanne, Agosti 09, 2016) wakati alipofanya ziara ya kushitukiza katika soko la Mwanjelwa na kubaini ubadhilifu wa fedha katika ujenzi wa soko hilo.

Waziri Mkuu amesema mara baada ya CAG kumaliza kufanya ukaguzi atatoa taarifa na mtu yeyote atakayetajwa katika ripoti hiyo kuwa amehusika na ubadhilifu huo atawajibika hata kama yuko nje ya Jiji la Mbeya.

Alisema kitendo cha kuongeza gharama za ujenzi wa soko hilo kutokana na kuchelewa kwa ujenzi wake kinaisababishia Halmashauri yaJiji kulipa sh milioni 200 kila mwezi kwa ajili ya marejesho, hivyo aliagiza aliyesababisha gharama hizo asakwe na achukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amemtaka Mkuu wa Mkoa Mbeya, Amos Makalla kuhakikisha mtu aliyepangishwa katika kibanda cha kukusanyia uchafu sokoni hapo anaondolewa haraka na kurudishiwa fedha zake ili kibanda hicho kitumike kama ilivyokusudiwa.

Pia alimuagiza Mkuu huyo wa Mkoa kufanya ukaguzi katika vyumba vya maduka sokoni hapo na ifikapo Jumatatu mtu hajaweka mali anyang’anywe na kupangishwa kwa mtu mwingine mwenye kuhitaji.

Alisema hayo baada ya baadhi ya wafanyabiashara kulalamika kuwa kuna watu wamechukua vyumba vingi vya maduka kwa ajili ya kuvipangisha kwa wafanyabiashara kwa gharama kubwa tofauti na inayotozwa na Halmashauri, hivyo kunyima nafasi kwa walengwa kunufaika na soko hilo.

Mmoja wa wajasiriliamali sokoni hapo Mohammed Said alisema watu wameshika vyumba na kuviuza kwa sh milioni 20 hadi 40 kulingana na eneo kilipo chumba jambo linalosababisha baadhi ya wafanyabiashara kushindwa kupata nafasi katika soko hilo.

Awali Mkuu wa Mkoa alisema soko hilo linakabiliwa na matatizo mbalimbali kwani hata wahanga waliokuwa wanafanya biashara kabla ya soko kuungua moto hawakupewa kipaumbele wakati wa upangishaji wa vyumba vya maduka.

Kuhusu suala la kukosekana kwa wateja sokoni hapo Makalla amewataka wafanyabiashara wote wanaofanya shughuli zao katika maeneo yasiyokuwa rasmi kuhamia sokoni hapo mara moja.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 08, 2016.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya13 & 14

0
0
MTUNZI:EDDAZARIA G.MSULWA

 .....Machozi yakaanza kunitiririka kwa wingi huku moyo wangu ukijawa na maumivu ni kwanini nilizungumza kitu kama kile,nikautoa mkono wangu koo ni mwa mama na kumkumbatia na kukiweka kachwa chake begabi mwangu na kuanza kumbembeleza taratibu.

“Eddy mwangu kwa nini unataka kuwa kama huyu baba yako?”
“Mama ninakuomba unisamehe sio kusudio langu kuzungumza hivyo”
 
Nikaendelea kumbembeleza mama taratibu hadi akanyamaza na taratibu usingizi ukaanza kumpitia baada ya muda kidogo akalala,Nikachukua shuka lake na kumfunika vizuri kisha nikatoka ndani ya chumba chake huku nikizima taa ya chumbani kwake na kushuka gorofani na kukaa kwenye sofa huku maneno ya mama akiwa anazungumza na dokta yakaaza kunirudia taratibu katika akili yangu huku yakiwa yanapita kama kanda wa video aina ya VHS.Kitu kinacho niumiza kichwa sana ni nani baba yangu na kitu kingine watu wengi wanasema ninafanana sana na baba yangu.

“Au mama atakuwa amechoka ndio maana akazungumza hivi?.........ila hata kama ni kuchoka itakuwaje akamwambia daktari mtu asiye husika katika familia yetu?”

Nikaendelea kujiuliza maswali yasiyo na majibu kiasi ya kujikuta taratibu nikiaanza kupitiwa na usingizi na kujikuta nikilala kwenye kochi.Nikaanza kuisikia sauti ya mama kwa mbali ikiniita taratibu huku akionekana akiomba msaada,Nikayafumbua macho yangu na kuuta mlango wa kuingilia hapa sebleni nikatazama nje na kukuta bado kuna giza jingi.

Nikanyanyuka kwa haraka na kwenda chumbani kwa mama nikakuta mlango wake ukiwa wazi nikaingia na kukuta kuna mwanaume yupo juu yake akimkaba huku kichwani kwake akiwa amevaa maski(Kinyago).Nikachukua chombo cha udongo kilichowekewa uwa la pambo na kwenda kumpiga nalo la kichwani na akaangukia kwa pembeni baada ya kuniona mimi akachomoka na kukimbia sikumjali zaidi ya kumuangalia mama kama yupo sawa au laa.Mama akanyanyuka huku akiwa anakooa huku akiwa amejishika koo.

“Mama unajisikiaje?”
“Vizuri mwangu fungua hiyo droo yangu ya kabati na unitolee bastola yangu”

  Nikafanya hivyo na kuitoa bastola yake kisha mama akanyanyuka kitandani na kuvaa raba zake za kufanyia mazoezi na taratibu tukaanza kutoka ndani kwa umakini wa hali ya juu huku na mimi nikifuata kwa nyuma.Tukashuka chini na kutoka nje kabisa ambapo kwa safari hii mlango ulikuwa umefungwa.Tukazunguka nyumba nzima kutazama kama kuna usalama kwa bahati nzuri kuna usalama.Tukaelekea getini ambapo hukaa askari ila hatukumkuta na wala hapakuwa na kitu chochote kinacho ashiria kuna tatizo lililo tokea katika eneo hilo.“Eddy kimbia kaniletee simu yangu ndani.”

  Nikaanza kujikongoja kongoja huku nikipiga hatua za haraka nikaamini kuwa mama amesahau kuwa mimi ni mgonjwa.Nikapanda ngazi kwa mwendo wa haraka kidogo kitendo cha kushika kitasa cha mlango wa kuingilia chumbani kwa mama nikasikia milio mitatu ya risasi ikitokea nje.Nikabaki nikiwa nimesimama huku miguu yote ikiwa inaanza kuishiwa na nguvu.Nikaaona hakuna haja ya kuingia ndani kuchukua simu moja kwa moja nikakimbilia jikoni na kuanza kukitafuta kisu ila sikukiona zaidi ya kuona Umma wa kulia chipsi,nikiona unanitosha kwenda kupambana na kitu chochote bitakacho kutana nacho nje.

 Nikafungua mlango na kujikuta mapigo ya moyo yakianza kuenda mbio huku wasiwasi ukiinza kunikamata mwili wangu kwani katika sehemu nilipomuacha mama sikumuona,Nikajikuta ninaaza kupata kiwewe cha miguu kila nikijaribu kusogea mbele ninajikuta ninashindwa sasa sikujua ni woga ndio unachangia kwani sikujua ni wapi mama yupo.Nikiwa bado nimesimama nikasikia mlio mwengine wa risasi ukitokea nje ya geti kwa mshtuko nusu nijikojolee kwani sikujua huo mlio ni nani aliyepigwa nao kwani kipindi nipo mdogo mara kwa mara baba alikuwa akinifundisha jinsi ya kutambua milio ya risasi pale inapokuwa imempiga mtu au kumkosa na moja kwa moja mlio niliousikia nikajua moja kwa moja risasi iliyolia imetua kwenye mwili wa mwanadamu.
   
 Nikajikaza kiume na kuanza kupiga hatua za kwenda nje ila kwa umakini huku uma wangu nikiwa nimeushika kwa umakini wa hali ya juu huku nikiwa makini kwa chochote kitakachojitokeza huku mwili mzima jasho lilinimwagika.Nikafungua geti dogo taratibu huku nikiwa nimetanguliza kichwa,Nikamkuta mama akiwa amesimama na askari kama watano wakiwa na bunduki zao mikonini huku kukiwa na mtu mmoja akiwa amelala chini huku mwili wake ukiwa unavuja damu nyingi.Nilicho kikumbuka kwa haraka haraka ni nguo alizo zivaa mtuu huyo na kukumbuka ni yule mtu niliyempiga na bakuli la dongo lililo kuwa na uwa la pambo.

“Alafu bado kijana mdogo sana”
“Ndio huyu nahisi ametuwa na mtu wa humo ndani kwako kwa maana haiwezekani ajiamini kiasi kwamba ya kujua moja kwa moja chumani kwako”
“Hilo usemalo litakuwa na ukweli ndani yake”.

 Mama akaendelea kujadiliana na askari wanaolinda eneo tunaloishi akiwemmo na askari wetu huku mama akimshushia lawama askari wetu ni kwa namna gani mtu anaingia ndani pasipo yeye kufahamu,askari wengine wakaja na gari lazo na kuchukua maiti huku wakimchukua askari wa getini kwetu kwenda kumuhoji maswali.

Bw. Hassan Abbas ateuliwa kuwa mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO)

0
0

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye amemtangaza  Bw.Hassan Abbas kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO  na Msemaji Mkuu wa Serikali  kuanzia Agosti 5 Mwaka huu.

Uteuzi huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma Namba 8 ya mwaka 2002 kifungu Namba 6(1)(b) kufuatia uhamisho wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara hiyo Bw. Assah Mwambene uliofanyika  tarehe 7 Machi 2016 kwenda Wizara ya Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mhe.Nape Moses Nnauye ametoa wito kwa Wanahabari na Wananchi  kwa ujumla kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Bw Abbas atakapokuwa anatekeleza majukumu yake.

“Ninawaomba Wanahabari na Watanzania kwa ujumla mumtambue Bw Abbas na mtoe ushirikiano unaostahili katika utendaji wa kazi zake”.Alisema Mhe. Waziri.

Aidha Mhe. Waziri Nape alimpongeza Bibi Zamaradi Kawawa aliyekuwa anakaimu nafasi hiyo kwa  kujituma na kusimamia majukumu yote ya Idara kwa ukamilifu na uadilifu.

Kwa upande wake Mkurugenzi huyo mpya amekubali uteuzi huo na ameahidi kuitumikia nafasi hiyo kwa uadilifu mkubwa na ameomba ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wafanyakazi wa Idara ya Habari Maelezo na Watanzania kwa ujumla.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Hassan Abbas  alikuwa ni Meneja Habari na Mawasiliano katika Ofisi ya Rais inayosimamia Utekelezaji wa Program ya Matokeo Makubwa sasa (President`s Delivery Bureau).

AUDIO: Tundu Lissu Amjibu Rais Magufuli

0
0
Jumanee ya leo August 9 2016 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekutana na waandishi wa habari Dar es salaam kutoa taarifa kwa umma kuhusu taarifa za vitisho wanazokuwa wakizipata kutoka serikalini.

Mwanasheria wa chama hicho Tundu Lissu amesema hakuna mtu toka Chadema anayetaka kumjaribu mtukufu Rais na wala hakuna anayetaka kukamatwa na Polisi  kwa sababu mahabusu sio pazuri.

"Tunachotaka kukifanya ni ambacho kipo katika katiba, mikutano na maandamano ya kisiasa kwakuwa ni halali. Kama kufanya hivyo Rais Magufuli anafikiri tunamjaribu hayo ni mawazo yake" Amesema Tundu Lissu

==> Bofya  Hapo chini kumsikiliza

Mfumuko Wa Bei Wa Taifa Wa Mwezi Julai 2016 Umepungua Hadi Asilimia 5.1.

0
0

Na. Aron Msigwa – Dar es salaam.
OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU (NBS) imetangaza mfumuko wa Bei wa Taifa wa mwezi Julai 2016 na kueleza kuwa umepungua hadi kufikia asilimia 5.1 kutoka asilimia 5.5 iliyokuwepo mwezi Juni mwaka huu.

Akitangaza taarifa ya mfumuko wa Bei wa Taifa wa mwezi Julai, 2016 leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Bw. Ephraimu Kwesigabo amesema kuwa kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2016 imepungua ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2016.

Ameeleza kuwa kupungua kwa mfumuko wa Bei wa mwezi Julai 2016 kumechangiwa na kupungua kwa kasi ya bei ya baadhi ya bidhaa za vyakula na zile zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Julai 2016 zikiwemo bidhaa za samaki kwa asilimia 6.6, mafuta ya kupikia asilimia 4.9 na maharage kwa asilimia 1.9 huku bei zisizo za vyakula zikihusisha ni gesi kwa asilimia 21.5, mafuta ya taa 9.4 na dizeli kwa asilimia 10.3.

Kwa upande wa bidhaa zisizo za vyakula zilizoonesha kupungua bei ni pamoja na bidhaa za gesi kwa asilimia 21.5, mafuta ya taa kwa asilimia 9.4 na dizeli kwa asilimia 10.3.

Aidha, ameeleza kuwa pamoja kupungua huko, kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2016 kwenye baadhi ya bidhaa umeonesha kuongezeka katika kipindi hicho hasa kwenye kama mchele, mahindi, unga wa mahindi, vyakula kwenye migahawa na mkaa.

Bw. Kwesigabo amesema kuwa Fahirisi za Bei nazo zimeongezeka hadi kufikia 103.50 mwezi Julai, 2016 kutoka 103.47 za mwezi Juni 2016, ongezeko ambalo limechangiwa na kuongezeka kwa bei ya baadhi ya bidhaa za vyakula zile zisizokuwa za vyakula.

Amesema ongezeko hilo la Fahirisi linahusisha kundi la bidhaa na huduma za vyakula na vinywaji baridi, Vinywaji vyenye kilevi na bidhaa za Tumbaku, Mavazi ya nguo na viatu, nishati, maji na Makazi pamoja na Samani, vifaa vya nyumbani na ukarabati wa nyumba.

Kundi lingine linahusisha gharama za Afya, usafirishaji, Mawasiliano, Utamaduni na Burudani, Elimu, hoteli na migahawa pamoja na bidhaa na huduma nyinginezo ambazo jumla ya Fahirisi za Bidhaa hizo kwa mwezi huo zimefikia 103.50.

“Baadhi ya bidhaa zilizo sababisha kuongezeka kwa Fahirisi ni pamoja na mafuta ya kupikia asilimia 1.1, samaki wabichi asilimia 6.0, matunda asilimia 4.9, maharage makavu kwa asilimia 2.7, ndizi za kupika asilimia 1.9 na mahindi kwa asilimia 1.5” Amesisitiza Kwesigabo.

Mbali na hilo ameeleza kuwa Mfumuko wa Bei wa Bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Julai 2016 umepungua hadi kufikia asilimia 7.6 kutoka asilimia 8.1 ya mwezi Juni 2016.

Kwa upande wa uwezo wa shilingi ya 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 96 na senti 62 mwezi Julai 2016 ikilinganishwa na shilingi 96 na senti 65 ya mwezi Juni, 2016.

Aidha, hali ya Mfumuko wa Bei kwa baadhi ya nchi za Afrika Mashariki imeonesha kuwa nchi ya Kenya Mfumuko wa Bei wa mwezi Julai umeongezeka hadi kufikia asilimia 6.39 kutoka asilimia 5.80 za mwezi Juni, 2016, Uganda ikiwa na Mfumuko wa Bei uliopungua wa asilimia 5.1 kwa mwezi Julai kutoka asilimia 5.9 za mwezi Juni, 2016.

Tundu Lissu: Barua ya Sekretarieti ya Maadili ni njama ya kutengeneza mazingira ya kisheria kunivua Ubunge

0
0

TUMECHOKA kuvumilia! Ni kauli ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baada ya kudai kusakamwa na Serikali .

Chama hicho kimetoa kauli hiyo leo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, baada ya Jaji Mstaafu, Salome Kaganda ambaye ni Kamishna wa Maadili na Mtendaji Mkuu wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuwaandikia barua viongozi wa chama hicho akiwatuhumu “kukiuka masharti ya Hati ya Ahadi ya Uadilifu wa Viongozi wa Umma.”

Jaji Kaganda aliwaandikia barua viongozi hao tarehe 4 mwezi huu ambapo Chadema wameitaka sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kuacha vitisho kwa viongozi wa chama hicho.

Walioandikiwa barua hiyo ni Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Chadema na Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa chama hicho.

Vincent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema amesema, kwa mujibu wa barua ya Jaji Kaganda, katika tarehe, muda na siku ambayo haijulikani, viongozi hao wa Chadema walitoa matamshi ambayo yanachochea wananchi kutotii sheria, kufanya vurugu, kudharau misingi ya demokrasia iliyopo nchini na kutishia usalama wa nchi.

“Hata hivyo, Jaji Kaganda hakuyataja matamshi hayo wala kuyafafanua. Aidha, alidai kwamba matamshi hayo yanatokana na maazimio yaliyofikiwa na kikundi cha watu wachache nje ya Bunge,” amesema Dk. Mashinji.

Licha ya  kudai kwamba, maazimio ya kikundi hicho yanapuuza utangamano, utulivu na usalama wa wananchi wengine kinyume na dhana ya maslahi mapana ya umma, Jaji Kaganda hakukitaja kikundi hicho cha watu wachache nje ya bunge huku pia akidai matamshi ya viongozi hao yalilenga ‘kushamirisha ‘ maslahi yao binafsi na maslahi ya Chadema.

“Mheshimiwa Mbowe ni Mwenyekiti wa Taifa wa chama kikuu cha upinzani hapa nchini. Ni kiongozi wa chama ambacho mgombea urais wake alipata zaidi ya kura milioni sita kati ya kura 15 milioni zilizopigwa kwenye uchaguzi mkuu wa urais mwaka jana.

“Ni mbunge wa kuchaguliwa na kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Katika Bunge. Ni mtu na kiongozi anayejulikana na kuheshimika ndani na nje ya Tanzania. Kusema kuwa kiongozi huyo anaongoza kikundi cha watu wachache nje ya Bunge kwenyewe ni kuonesha maadili yenye mashaka kwa mwandishi wa barua hiyo,” amesema Dk. Mashinji.

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki  ameeleza kushangazwa na barua ya Jaji Kaganda akisema;

“Ni vigumu kuamini kwamba, barua hii imeandikwa na mwanasheria na mtu ambaye amewahi kushikilia madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

“Barua ambayo haina maelezo yoyote ya kile kinachodaiwa kuwa kosa; haitaji tarehe, siku, muda au mahali kosa hilo lilipotendeka.

“Haitaji vifungu vya sheria yoyote iliyokiukwa na wala kuonyesha kama sekretarieti ya maadili ya Viongozi wa Umma ina mamlaka kisheria ya kushughulikia kosa hilo, in onyesha mapungufu makubwa ya kitaaluma na kiuandishi ya kamishna wa maadili na katika mazingira ya kawaida, ingestahili kupuuzwa,” amesema Lissu.

Kwa mujibu wa Lissu ambaye ni mwanasheria wa chama hicho, Chadema haiwezi kuipuuza barua hiyo na kwamba, inaashiria kuwepo kwa njama za kuwafungulia mashtaka katika Mahakama ya Maadili Viongozi hao ambao ni wabunge kwa lengo la kuwavua ubunge.

Aidha, mojawapo ya vigezo vya kikatiba vya mtu kukosa sifa ya kuwa mbunge ni pamoja na kuhukumiwa na kupewa adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa uaminifu au kwa kuvunja sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, kamishna wa maadili ana mamlaka ya kuchunguza tuhuma za ukiukwaji wa maadili ya viongozi wa umma na kuunda mahakama (Tribunal) ya kusikiliza tuhuma hizo na kupeleka taarifa ya mashauri hayo kwa kamishna ambaye atapaswa kuwasilisha nakala za taarifa hiyo kwa rais na spika wa Bunge.

“Rais Magufuli na washauri wake wanafahamu ugumu wa kutumia mahakama za kawaida kwa lengo la kukandamiza wapinzani.

“Licha ya matatizo yake mengi, Mahakama ya Tanzania imedhihirisha mara nyingi uwezo wa kulinda uhuru wake na kutokuwa tayari kutumika kwa malengo ya kisiasa ya watawala.

“Sasa Magufuli (Rais John Magufuli) na washauri wake wanaandaa mazingira ya kuitisha Mahakama ya Kangaroo watakayoidhibiti wao ili kuhakikisha wanawakandamiza viongozi wakuu wa chama chetu.

“Kama ambavyo tumethibitisha mara kwa mara chama chetu hakitakuwa tayari kuona viongozi wake wakikandamizwa kwa kutumia kivuli cha maadili ya viongozi wa umma. Tutapambana na njama hizo. Kwa uthabiti na kwa weledi ule ule ambao tumepambana na njama nyingine za aina hiyo katika siku za nyuma,” ameeleza Lissu.

Aidha Jaji Kaganda amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la leo akikana kujua kuhusu barua hiyo huku akisema “mimi sifahamu kuhusu suala hilo, sina taarifa.”

==> Wasikilize Hapo chini wakiisoma barua hiyo

Uchawi Ni Utumwa : Nilimlisha Mume Wa Mtu Limbwata La Nyama Ya Bundi- Sehemu Ya Pili

0
0
SEHEMU  YA  PILI….

NASHIRIKI   KUMFUNGA  KICHAWI  MUME  WA  MTU….
Katika  makala  yangu  yaliyopita , nilieleza  jinsi  mungu  wa  kabili alivyo  niambia  kuwa  nina  nyota  ya  uganga  na  hivyo  ninatakiwa  kusimikwa uganga.

mungu  wa  kabili  aliniambia  ili  nifundishwe  uganga  ni  lazima  nianze  kufundishwa  kuhusu  uchawi  kwanza, kwa  sababu  kazi  yangu  kubwa  katika  uganga  itakuwa  ni  ' kupambana  na  uchawi ". ( NI  UNAFIKI  MKUBWA  KUSEMA  ETI  MGANGA  ANAPAMBANA  NA  UCHAWI, KWA  SABABU  MGANGA  NA  MCHAWI  LAO  NI  MOJA, NA  SIKU  ZOTE  HUSHIRIKIANA ...KADRI  UNAVYO  FUATILIA  WARAKA  WANGU  NDIPO  UTAKAPO  GUNDUA  UNAFIKI  WA  WAGANGA  KUHUSU  HOJA  HII  DHAIFU ).

mungu  wa  kabili  aliniambia  ni  lazima  nianze  kwanza  kwa  kupewa  elimu  ya  msingi  ya  uchawi  kabla  ya  kufundishwa  uganga  na  hatimaye  kusimikwa  uganga  rasmi.

Nilifundishwa  mambo  mengi  sana  ya  kichawi  na  katika  mfululizo  wa  makala  haya  nitayaelezea  yale  muhimu  na  ninayo  yakumbuka  vizuri.

Lengo  langu  ni  kuwafungua  watu  macho  kuhusu  ulimwengu  wa  wachawi, jinsi  unavyo  fanya  kazi  na  jinsi  unavyo  weza  kujikinga  ama  kujiepusha  nao.

Vile  vile lengo  langu  ni  kuwaonyesha  watu  jinsi  uchawi  unavyo wafanya  watu  kuwa  watumwa  katika  maisha  yao  ya  kila  siku..

NAFUNDISHWA  UCHAWI  WA  KUPIGA  MAFUNDO  AMA  KUFUNGA  MAFUNDO...
Huu  ni  aina  ya  uchawi   ambao  kila  mchawi  hufundishwa. Ni  uchawi  unao  tumika  sana  miongoni  mwa  wachawi.

Uchawi  wa  kufunga  mafundo  ni  uchawi  unao  fanyika  kwa  ajili ya  kuwafunga  watu  katika  vifungo  vya  aina  mbalimbali, kama  vile  kutokuzaa, kutokuoa  ama  kuolewa, biashara  kutokufanikiwa, mtoto  kutokukua,  nakadhalika.

Uchawi  huu  unaweza  kufanyika  kwa  lengo  la  kumkomoa  na  kumtesa  mfungwaji , kumshinikiza  mfungwaji  au  kumfurahisha  na  kumstarehesha  mfungaji.

MAMBO  MAKUU  MATATU  MUHIMU  KATIKA  UCHAWI  WA  KUPIGA  MAFUNDO.

Katika  uchawi  wa  kupiga  mafundo  ama  uchawi  wa  kuwaweka  watu  kwenye  vifungo  mbalimbali, kuna  mambo  makuu  matatu  ya  msingi.

JAMBO  LA  KWANZA  NI  MFUNGAJI ( Yaani  mtu  aliekusudia  kumfunga  mwenzake  kichawi  )

JAMBO  LA  PILI  NI  MFUNGWAJI  (  Yaani  mtu alie  kusudiwa  kufungwa )

JAMBO  LA  TATU  NI  KIFUNGO  CHENYEWE.  (  Yaani  jambo  au  kitu  ambacho  kitatumika  kumfunga  aliye  kusudiwa  kufungwa )

Nitaelezea  kwa  ufupi  jambo  moja  hadi  jingine. Naanza  na  jambo  la  kwanza  ambalo  ni  MFUNGAJI.

MFUNGAJI  NI  NANI  KATIKA  UCHAWI ?  Katika  uchawi  mfungaji  ni  mtu  alie  kusudia  kumfunga  mtu  mwingine  kichawi.  Mtu  huyu  anaweza  kuwa  mchawi ( mlozi), mganga  ( ambae  pia  ni  mchawi ), jini, pepo, mzimu  au  mtu  mwingine  yoyote  ambaye  si  mchawi  wala  mganga  ambaye  ameenda  kwa  mchawi  ama  mganga, kwa  ajili  ya  kutafuta  msaada  wa  kichawi  wenye  lengo  la  kumfunga  kichawi  mtu  mwingine..

MFUNGWAJI :  Mfungwaji  ni  mtu  aliye  kusudiwa  kufungwa  na  mfungaji.  Mfungwaji  ni  ni  jambo  au  hali  yoyote  iliyo  kusudiwa  kufungwa  na  mfungaji. Mfungwaji  ni  jini, pepo  au  mzimu  wowote  ulio  kusudiwa  kufungwa  na  mchawi.  Mfungwaji  ni  mnyama, mmea  au  mali  yoyote  iliyo  kusudiwa  kufungwa  na  mfungaji.

Mfungwaji  anaweza  kuwa  mume  wa  mtu, mke  wa  mtu, mtoto  mchanga, mchungaji, padre, imamu, mimea, mazao au  kitu  chochote  kile  unacho  weza  kukifi9kiria.

KIFUNGO   CHA  KICHAWI :  Katika  ulimwengu  wa  wachawi, kifungo  ni  ile  hali  au  jambo  ambalo  limekusudiwa  kwa  mfungwaji.  Hali  au  jambo  hilo  laweza  kuwa  ugumba, utasa, mimba  kutoka, kifo, biashara  kushindwa,  chuma  ulete, mapenzi, undondocha, umalaya, ukichaa, uwehu  nakadhalika...

Pia  kifungo  huusisha  KAMBA  ZA  KICHAWI  ama  KAMBA  ZA  KUZIMU.

Hivyo  basi  ili  kifungo  cha  kichawi  kiweze  kufanya  kazi  ni  lazima, awepo  mfungaji, mfungwaji  na  kifungo  chenyewe...

JINSI  WATU  WANAVYO  WAFUNGA  KICHAWI  WATU  MBALIMBALI..
Nikiwa  kama  mwanafunzi  wa  mungu  wa  kabili, nimeshiriki  katika  kuwafunga  kichawi  watu  mbalimbali.

Katika  ulimwengu  wa  wachawi, binadamu  amegawanyika  katika  sehemu  kuu  tatu  ambazo  ni  MWILI, NAFSI  NA  ROHO.
Kwa  lugha  nyingine, wachawi  wana  amini  kuwa  mwanadamu  ni  roho  yenye  nafsi  ambayo  inaishi  kwenye  nyumba  ya  udongo  iitwayo  mwili.
 Hivyo  basi  mfungaji  anapotaka  kumfunga  mtu  kifungo  anatakiwa  kuelewa  anataka  kumfunga  mtu  huyo  kifungo  cha  wapi. Cha  mwili, nafasi  au  roho ?

KIFUNGO   CHA  MWILI :    Wachawi  wana  amini  kuwa mwanadamu  aliumbwa  kwa  udongo.  Hivyo  basi  wanapotazama  mwanadamu   katika  macho  ya  kiroho  humuona  kama  udongo  kabisa.

Na  kwa  kuwa  binadamu  kwao  ni  udongo, basi  wachawi  wanaweza  kkutumia  maarifa  ya  kichawi  kupanda  chochote  katika  mwili  wa  mwanadamu  na  kitu  hicho   kikakua  na  kuota.

Katika  ulimwengu  wa  wachawi, kinacho  ongeza  thamani  ya  mwili  wa  mwanadamu, ni  mapando  yaliyo pandwa  katika  mwili  wa  mtu  huyo.

Aina  ya  vitu  vilivyo pandwa  kwenye  mwili  wako, ndio  itakayo  amua, aina  ya  kifungo utakacho  fungwa.

Kama mwili  wako ni  mweupe, basi  utafungwa  kifungo  cha  kawaida, na  kama  katika  mwili  wako, imepandwa   ngome  imara  basi  hata  nguvu  ya  uchawi  itakayo  tumika  itakuwa  kubwa  zaidi.

Ukisikia  mchawi  anakwambia  nipe  jina  la  mama  wa  mtu  unayetaka  kumroga  basi  jua  anataka  kutazama  mwili  wa  mtu  huyo  umepandwa  kitu  gani...

Ukisikia  mtu  ni  mzito  katika  uchawi  basi  jua  mwili wake  umepandwa  vitu  vizito  pia.

JINSI  WACHAWI  WANAVYOPANDA  MAPANDO  MBALIMBALI  KWENYE  MWILI  WA  MWANADAMU..

Wachawi  hupanda   mapando  mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  kwa  kutumia  njia  mbalimbali, mojawapo  kati  ya  njia  hizo  ni  pamoja  na  kuchanjwa,  kuogeshwa  dawa  pamoja  na  kulishwa  dawa.

Njia  nyingine  wanatumia  migomba, udongo  na  mti  mmoja  wa  porini  ambao  jina  lake  silikumbuki  vizuri.

Kwa  kutumia  maarifa  ya  uchawi, wachawi  wanaweza  kupanda  kitu  chochote  wanacho  jisikia  katika  mwili  wa  mtu  walie  mkusudia.

SHUHUDA  ZA  WATU  WALIO  FUNGWA   VIFUNGO  MBALIMBALI  KICHAWI....

Kwa  muda  wa  miaka  mitatu  na  ushee  ambao  nimekuwa  nikifanya  kazi  kama  mwanafunzi  wa  uchawi  wa  mungu  wa  kabili, nimeshiriki  katika  kuwafunga  kichawi  watu  mbalimbali. Zifuatazo  ni  baadhi  ya  shuhuda  za  watu  ambao  nilishiriki  katika  kufungwa  kwao.

NASHIRIKI  KUMFUNGA  MWANAUME  KICHAWI ….
Kuna  mwanamke  mmoja   tajiri na  mwenye  uwezo  mkubwa  tu  kifedha, alileta  kesi  kilingeni  kwa   mungu  wa  kabili.  Kesi  ilikuwa  hivi, yeye  alikuwa  amefunga  ndoa  na  mwanaume  asiye  na  kipato, lakini  mwanaume  alikuwa  si  muaminifu  katika  ndoa .

Mapenzi  yalikuwa  ya  upande  mmoja. Mwanamke  alikuwa  anamudumia  mwanaume  kwa  kila  kitu  lakini  mwanaume  alikuwa  haridhiki. Na  mpaka  mwanamke  huyo  anafika  kilingeni  kwa  mungu  wa  kabili, mwanaume  alikuwa  ameondoka  kwa  mwanamke  (  walikuwa  wanaishi  kwenye  nyumba  ya  mwanamke ) na  kwenda  kuishi  kwa  mwanamke  mwingine  kwa  zaidi  ya  miezi  minane.    Mwanaume  huyo aliondoka  baada  ya  kutokea  ugomvi  mkubwa  kati  yao, chanzo  kikiwa  ni  wivu  wa  kimapenzi.  Mwanamke  alikuwa  akimtuhumu  mwanaume  kwa  kutoka  nje  ya  ndoa.

Mwanaume  huyo  alikuwa  amempa  ujauzito mwanamke  huyo  wa  pembeni. Mwanamke  huyo  wa  pembeni  nae  alikuwa  na  uwezo  wa  kifedha.

Mwanamke  alikuwa  anaomba  kusaidiwa,  ufanyike  uganga, huyo  mwanaume  arudi  mwenyewe  nyumbani, na  atakapo  rudi  nyumbani  atulie  na  kumuheshimu  mke  wake.   Pili  watenganishwe  mwanaume  huyo  na  mwanamke  wake  wa  pembeni, mimba  ya  mwanamke  huyo  itolewe na mwisho  mwanamke  huyo  atiwe  mikosi

Mungu  wa   Kabili  akaagiza  vipatikane  vitu  vifuatavyo :  Kamba  ambayo  mtu  ametumia  kujinyonga,  nguo  za  marehemu  ambazo  alikufa  nazo, kipande  cha  sanda  ambacho  kimekatwa  kutoka  kwenye  sanda  iliyo valishwa  mwili  mwa  marehemu, mchanga  wa  njia  panda  saba,  sindano  arobaini, shahidi la  kaburini  pamoja  na  udongo  wa  kaburi  alilozikwa  mwanaume,  maji yaliyo  tumika  kuoshea  maiti ya  mwanamke, kamba  iliyo  tumika  kumfunga  kondoo,  mafuta  ya  msukule,  yai  la  bundi,  jani  lililo letwa  lenyewe  na  upepo  na  likadakwa  kabla  halijafika  chini,  kondoo, punda  mwenye  alama  ya  msalaba  mgongoni, bundi  wa  kichawi, kobe  wa  kichawi  ( Hapa  naomba  nifafanue jambo;, wachawi  huwa  wana  namna  yao  ya  kuwaita majini walio  katika  maumbo  ya  wanyama, ndege  na  wadudu  mbalimbali. Ukisikia  mnyama  wa  kichawi  basi  jua  huyo  sio  mnyama  wa  kichawi  bali  ni  jinni amegeuzwa  na  kufungwa  katika  umbo  la  mchana ) , maji  yaliyo  tumika  kuchambia  sehemu  za  siri za  mwanamke  ambayo  yanatakiwa  yaletwe  na  mwanamke  mwenyewe, maji  ya  kwanza  ambayo  mwanamke  ameyatumia  kunawia  uso,  funza  walio nyonya  damu  ya  maiti  ya  binadamu , funza  wa  bundi  pamoja  na  unyayo  wa  mwanaume  huyo  akiwa  anaingia  ndani  na  sio  akiwa  anatoka.

Mungu  wa  kabili  akaagiza  pia  wapatikane  njiwa  wawili  jike  na  dume, ndege  wawili  wa  porini  ambao   sifa  zao  zipo  hivi, ukimkamata  ndege  huyo  na  kumfunga  kwa  kamba  sehemu  yoyote  ile, iwe  ni  porini  huko  huko  au  kwenye  banda, kesho  yake  asubuhi utakuta  kamba  imejifungua  na  ndege  ondoka,  katika  jamii  ya  ndege  hawa, dume  huwa  dogo  kwa  umbo  kuliko  jike, na  dume ndio  huatamia  mayai.

Ndege  hawa, wana macho mekundu na mkia mrefu, na ukucha wa kidole kikabilicho nyuma ni mrefu sana . Ndege  hawa  wana  mabawa  ya  kahawia  nyekundu  na  kichwa  chenye  rangi  nyeusi.

Chakula  kikuu  cha  ndege  hawa  ni  wadudu, mijusi, nyoka na wanyama wadogo, mayai  ya  ndege  na  wadufu  mbalimbali, makinda  ya  ndege  mbalimbali, matunda na mizoga pia.

Vichali  vya  ndege  hawa  hujengwa kwenye  eneo  lenye  miti  mingi  na  hufungwa  kwa  juu.

Kuna  mnyama  mmoja  anapatikana  porini. Chakula  kikuu  cha  mnyama  huyo  ni  asali. Ana  sifa  ya  kuwa  na  makucha  marefu na  yenye  nguvu  sana. Huwa  anaishi peke  yake  porini  katika  shimo  ambalo  anakuwa  amelichimba  yeye  mwenyewe…

Na anapochimba  shimo  lake, hukaa  ndani  ya  shimo  hilo  kwa  muda  wa  dakika  kumi  tu.

Jino  la mnyama  huyu  hutumiwa  na  wachawi  katika  kutengeneza  dawa  ya  bahati  nasibu.Yani  kama  unacheza  bahati  nasibu  ama  unaenda  kwenye  ushindani  wowote  ule  iwe  ni  michezo, kazi, uongozi  nakadhalika, halafu  ukachanjwa  dawa  iliyo  tengenezwa  kwa  kutumia  jino  la  mnyama  huyo  basi, lazima  utashinda  hata  kama  mnaogombania  nafasi  hiyo  mpo  elfu  kumi  na  anae  hitajika  ni  mtu  mmoja.

Dume  la  mnyama  huyu  huwa  na  wivu  sana  kwa  jike  lake, na mara  nyingi  hutembea  nyuma  ya  jike  huku  akiwa  ameziba  sehemu  za  siri  za jike huyo. Basi  ikitokea  hata  jani  likigusa  kwa bahati  mbaya  sehemu  za  siri  za  jike  la  dume  la  mnyama  huyo, litararuliwa  na  kupigwa vibaya  sana  na  mnyama  huyo.

Mungu  wa  Kabili  akaagiza  apatikane  mnyama  huyo, jike  pamoja  na  dume  lake. Pamoja  na udongo  wa  kwenye  shimo  lilitumiwa  na  mnyama  huyo.

Vitu  vingine  mungu  wa  kabili  akasema,  wapatikane  njiwa  wawili  jike  pamoja  na  dume.

Kazi  nyingi  za   Mungu  wa  Kabili  huwa  anazifanya  nyakati  za  usiku  na  huzifanya  kwa  kushirikiana  na  watu  wanaoitwa  malaika  wa  mungu  wa  kabili. Hawa  malaika  wa  mungu  wa  kabili, ni  wachawi  wazito  wazito.

Malaika  wa  mungu  wa  kabili  wapo  karibu  katika  kila  kona  ya  nchi  hii  na  nchi  jirani, hususani  Kongo .

Ndio  maana  ninasisitiza  kwamba, mungu  wa  kabili  ni  mchawi  na  wakala  wa  shetani.

Kabla  sijaendelea, naomba  nifafanue  kitu kimoja, kwamba   waganga  wapo  wa  aina  kuu  mbili, aina  ya  kwanza  ni  wale  wanao  agua  kwa  njia  za  kawaida  tu, na  aina  ya  pili  ni  ile  ya  waganga   wanao  agua  kichawi.

Mungu  wa  Kabili  ni  mganga  anae  agua  kichawi, na  ndio  maana  kazi  zake  nyingi  hufanyika  nyakati  za  usiku  na  huzifanya  kwa  kushirikiana  na  wachawi…

Mungu  wa  Kabili  alisema kamba  ambayo  mtu  ametumia  kujinyonga,  nguo  aliyo  kufa  nayo  marehemu,  jani  lililo letwa  lenyewe  na  udongo  wa  kwenye  shimo  alilo  tengeneza  mnyama  niliye  muelezea  hapo  juu, shahidi  la  kaburi , udongo  wa  kaburini  pamoja  na  kipande  cha  sanda  kilicho katwa  kutoka  kwenye  sanda  iliyo  tumika  kumfunika  marehemu,   hutumika  katika  kutengeneza  uchawi  wa  kumuita  ama  kumvuta  mpenzi  au  mtu  yoyote  aliye  kimbia.

Kamba  iliyo  tumika  kumfunga  kondoo, hutumika  katika  kutengeneza  uchawi  wa  kumfunga  mume, mke , mchumba, mfanyakazi  nakadhalika.

Kobe  wa  kichawi  hutumika  katika  kutengeneza  uchawi  wa  kumuinamisha  na  kumfunga na  kumtuliza   mume  au  mke.   Mke  au  mume  aliye fanyiwa  uchawi  huu, huwa  ni  mtu  wa  kuwa  ndani  wakati  wote, akitoka  nje  basi  labda kaenda  kazini, hospitali, kanisani,msikitini  au  msibani.

Bundi wa  kichawi  hutumika  kutengeneza  uchawi  wa  kumlisha  mwanaume  na  kumfanya  kuwa  mtumwa  wa  mwanamke  wake  katika  siku  zote  za  maisha  yake.

Maji yaliyo  tumika  kuoshea  maiti, funza walio nyonya damu  ya  maiti  ya  mtu au  maiti  ya  msukule, hutumika  katika  kutengeneza  uchawi  wa  kumfanya mke  au  mume  akupende  wewe  peke yako  tu, na  awe  sawa sawa  na mtu  aliye  kufa  na  kuoza  juu  yako.

Uchawi  huo  humfanya  mtu  aliyefanyiwa  kama  ni  mwanaume, basi  asikumbuke  chochote  kuhusu  mwanamke  au  mke  aliye  kuwa  nae  kabla, hadi  siku  atakayo  kuwa  anaingia  kaburini  ndio atakumbuka  kumbe  alikuwa  amemuoa  mwanamke  Fulani. ( NDUGU  ZANGU, MKIONA  AU  KUSIKIA  MWANAUME  AMA  MWANAMKE  KAIKIMBIA  NA  KUISAHAHU  FAMILIA  YAKE, BASI  JUENI  KUWA  AMEFANYIWA  UCHAWI  WA  AINA  HII  . MUNGU  AWAEPUSHIENI  MBALI  NA  USHETANI  HUU. NI HATARI  SANA  )

Mafuta  ya  msukule  yana  matumizi  mengi  sana  katika  uchawi, katika  habari  ya  ulozi  wa  mapenzi    hutumika  katika  kumfanya  mke, mume,mchumba, boyfriend au  girlfriend  asionekane  na  watu  wengine..

Haya  mafuta  ya  msukule  ni  tofauti  na  mafuta  ya  usiku. Mafuta  ya  usiku  ni  mengine  na  mafuta  ya  msukule  ni  kitu  kingine.

Pia  mafuta  ya  msukule  ni  tofauti  na  maji  ya  msukule. Mafute  ya  msukule  yanatengenezwa usukuleni,  ilihali  maji  ya  msukule  yanatoka  kuzimu.

Kuzimu  kuna  mito  saba. Kila  mto  una  matumizi  yake. Kati  ya  mito  hiyo, upo  mto  ambao  maji  yake  yana tumika  katika kuwafanya  watu  wasahahu  kila  kitu  walicho  kuwa  wanakifahamu  kabla  hawajanyweshwa  maji  hayo.

Maji  hayo  hutumiwa  na  watu  wanao  chukua  watu  misukule. Msukule  anapo  chukuliwa  hunyweshwa  maji  hayo. Na  mara  tu  anapokunywa  maji  hayo, husahau  kabisa  kila  kitu  alicho  kuwa  ana  kifahamu. Husahau  kama  Alisha  wahi  kuwa  na  maisha  mengine, husahau  kama  alikuwa  na  wazazi, ndugu, jamaa, marafiki  nakadhalika.

Ndio  maana  basi wachawi  wakishamchukua  mtu  msukule, mara  baada  ya  ndugu  zake  kufanya

“  mazishi  hewa “  wachawi  humpeleka  mtu  huyo  hadi  katika  nyumba  aliyokuwa  anaishi pamoja  na  nyumba  wanapoishi  ndugu  zake  na  kumuonyesha  ndugu  zake… Asipo watambua  ndugu  zake, basi  wanashangilia  kwamba, ule  uchawi  wao  umefanya kazi.

Hapa  sizungumzii  hayo  maji  ya  msukule, ninazungumzia   mafuta  ya  msukule  ambayo  hutengenezwa  usukuleni.

Kujua  kama  mafuta  hayo  ni  msukule, ukijipaka basi  hata  kwenye  kioo  huwezi  kujiona.

Tulianza  kwa  kufanya  zoezi  la  kwanza, ambalo  ni  kutengeneza  uchawi  wa  kumuita  mume  wa  Yule  mama, ambapo  mama  Yule  alipewa  dawa  hizo  na  kwenda  kuzitumia  kumuita  kichawi  mume  wake.

Baada  ya  mume  kurudi  nyumbani, mama  Yule  alifanya  kama  ali vyo  agizwa, yani  kuchota  mchanga  wa  mahali  alipo  kanyagia  mume  wake  wakati  anaingia  nyumbani  hapo.

Hivyo  mama  Yule  alikuja  na  mchanga  alio  mchota  mume  wake, maji  ya  kwanza  aliyo  tumia  kuoshea  uso  wake, maji  aliyo  tumia  kuoshea  sehemu  zake  za  siri, sindano  arobaini  pamoja  na  njiwa  wawili  jike  na  dume.

Maji  aliyo  tumia  kuoshea  uso  wake  kwa  mara  ya  kwanza, yalichanganywa na  dawa  zingine  kwa  ajili  ya  kutengeneza  uchawi  wa  kumfanya  mwanaume  wake  awe  anamuona  yeye  tu,   njiwa  wawili  jike  na  dume  ( wapenzi ) walichinjwa  kwa  tambiko  maalumu, wakapasuliwa, mioyo yao ikachukuliwa  ikawekwa  kwenye  chungu  na  kukaushwa  pamoja  na  dawa  nyingine  kama  saba  hivi za  kichawi, ambazo  mume  hulishwa  na  kumfanya  kuwa  muaminifu  kwa  mke  wake, na  mke  akilishwa  basi  nae  huwa  muaminifu  kwa  mume  wake.

Sehemu  iliyo  baki kwa  mwili wa  njiwa  nayo ilitumika kupikwa   pamoja  na  maji  yaliyo  tumika  kuoshea  sehemu  za  siri za  mwanamke  huyo pamoja  na  dawa  nyingine  nyingi  za  kichawi, ambazo  zingetumika  kumyweshwa  na  kumuogesha  mwanaume.

Baada  ya  zoezi  hilo  la  kwanza  kukamilika, lilibaki  zoezi  la  pili  ambalo  ni  kumfunga  mwanaume kwa  mke  wake,  zoezi  la  tatu   ni  kumtenganisha  mume  na  mwanamke  wake  wa  pembeni, zoezi  la  nne  ni  kutoa  ujauzito  wa  mke  wa  pembeni  mwa  mwanaume huyo, zoezi  la  tano  ni  kumtia  mikosi  mwanamke  huyo.

ZOEZI   L A  KUMFUNGA  MTU  KICHAWI.
Zoezi  hili  lilifanyika  njia  panda  kuanzia  saa  sita  kamili  usiku.  Zoezi  hilo  tulilifanya  mimi, mungu  wa  kabili, mwanamke  aliye  taka  kumfunga  mwanamke  mwenzake, wasaidizi watatu  wa  mungu  wa  kabili  pamoja  na  kikundi  cha  wachawi wapato  arobaini.

Zoezi  lilifanyika  njia  panda iliyokuwa  imezungukwa  na  moto  wa  kichawi  ambao  wao  wachawi  wanauita  chenge.

Mungu  wa  kabili  aliniambia, zoezi  la  leo  litakuwa  zito  kidogo  kwa  sababu, tuna  kazi  nyingine  kubwa  ya  kumfanya  mtu  asionekane  duniani.

Kwa  hiyo  tutaanza  na  kazi  ya  huyu  mama, halafu  tukimaliza  hapo tutaendelea  na  kazi nyingine. Ninataka   ujifunze  kuhusu  uchawi wa  namna  ya  kumfanya  asionekane  duniani.

Kwanza  tulifika  njia  panda, majira  ya  saa sita  kamili  za usiku. Tulikuwa  mimi, mungu  wa  kabili, mama  mwenye  kutaka  kumfunga  mume  wake,  pamoja  na  wasaidizi  watatu  wa  mungu wa  kabili.

Wote  tulikuwa  tumevaa  mavazi  wanayo  vaa  wachawi  wanapo enda  kuroga  pamoja  na  kupakwa  unga.

Mungu  wa  kabili  alisema, ataanza  kwa  kuwaita  kwanza  wachawi, watakapo  fika  ndio  tutaanza  kazi  yetu.

Akasema lakini  kabla  ya  zoezi  la  kuwaita  wachawi  kufanyika, nitaanza  kwa  kuchanjwa  dawa  itakayo  nipa  uwezo  wa  kuwaona wachawi….

Kuna  mti  mmoja, unapatikana  porini, mti  huo ukikomaa, urefu  wake  hauzidi wa  mtoto wa miaka saba, una magamba  kwa  mbali  na  rangi  yake  ni nyeupe.

 Mti  huu  ukikauka  ukausaga  unga  wake huwa  mweupe  kama    mti  wenyewe.

Ukichukua  unga  wa  mti  huu  halafu  ukajipaka usoni  unakuwa  na  uwezo  wa kuwaona  wachawi.

Ukichanjiwa  mti  huu  kwenye  pande  saba  za  mwili  wako, ukijipaka  unga  wa  mti  huu  usoni  halafu ukatembea   mtaani  wakati  wa  mchana, unaweza kuona  mambo  yote  yanayofanyika  katika  siri kubwa  kama  vile  wachawi  wakiwa  wanawanga au  wanafanya  shughuli zao  wakiwa  uchi.

Mti  huu  unakupa  uwezo  wa  kuwaona misukule.

Vilevile  mti  huu  unauwezo  wa  kukimbiza nyoka  mfano  ukiwa  na  kipande  cha  mti  huu

mfukoni  au  ukiwa  umechanjiwa  mti  huu halafu  ukawa  unatembea, kama mbele  yako  kuna  nyoka  atakimbia  kabla hujafika.

Hata  ukikaa  mahali  kama  kuna  nyoka hawezi kukaa  hapo, atakimbia tu…

Mungu  wa  Kabili  alianza  kwa  zoezi  la kunichanja  katika  pande  saba za  mwili wangu,na  kunipakaa  unga  wa  mti  huo,  pamoja  na  kunipaka  mashavuni, kidevuni  na  usoni.

Baada  ya  zoezi  hilo  kukamilika, Mungu wa  Kabili, alisema  maneno  yake  ya  kiganga  halafu  akaanza  kupuliza  FILIMBI  YA  KICHAWI.

Naomba  nifafanue  kitu  kimoja  hapa, FILIMBI  YA  KICHAWI, hutengenezwa  kwa  kutumia UUME  WA  MTOTO MDOGO  na  wapokosa  uume  wa  mtoto  mdogo, hutumia  hata  uume  wa  mtu  mzima,lakini  kipaumbele chao  huwa  ni uume  wa  mtu  mzima.

Sharti  moja  la  kuchukua  uume  kwa  ajili  ya  kutengenezea  filimbi  ya  kichawi, huwa  ni  lazima  mtoto  huyo  awe hai, kamwe  uume  hauchukuliwi  mtoto  akiwa  amekufa, bali  unachukuliwa  mtoto  akiwa  hai  na  huchukuliwa  kichawi.

Jinsi  wanavyo  chukua   uume  wa  mtoto  kichawi, huuchukua  na  kuubadilisha  na  kipande  cha  mgomba  wa  ndizi. (  WACHAWI  WANA  AMINI, MTI  WA  MDIZI  UNA  UHUSIANO  WA  KINASABA  NA  BINADAMU.. NA  UNAFANANA  SANA  NA  BINADAMU, KUANZIA  MFUMO  WA  NGOZI, UZAZI  NAKADHALIKA, NITALIELEZEA  KWA  KINA  SIKU  ZIJAZO )

Kuna  mti  mmoja  unapatikana  porini,  mti  huu  ni  miongoni  mwa  miti  mikuu  ya  wachawi, una  matumizi  mengi  ikiwa  ni  pamoja  na  kupasua  makaburi  kuongea  na  mizimu.

Lakini  pia  mti  huu  unatumika kuhamisha  vitu  kutoka   katika  sehemu  moja  ya  mwili  wa mtu  kwenda  katika  sehemu  nyinginezo  za  mwili wa  mtu  huyo, au  kutoka  kwenye  mwili  wa  mtu  huyo  kwenda  kwa mnyama, ndege, mdudu, kaburini, pangoni n.k, au  kutoka  kwa  mnyama, mdudu, mmea, eneo n.k  kwenda  kwa  mwanadamu.

Kwa  mfano  siku moja kuna  mama  mmoja  mtu mzima, ambaye  ni  mwana  ukoo  wa  mungu  wa  kabili, aliletwa  kilingeni  kwa  mungu  wa  kabili  kwa  ajili  ya  kutibiwa. Yeye  alikuwa  na kidonda  maeneo  ya  sehemu  zake  za  siri. ( Kwenye kalio ).

Kwa  mujibu  wa  mila  na  desturi  za Tanzania, mungu  wa  kabili  asingeweza   kumuona  mama huyo  akiwa uchi  ili  amtibie, hivyo  alicho  kifanya  ni  kuhamisha  kidonda  cha  mama  huyo  kutoka  makalioni  kwenda  mkononi , akakitibu  kwa  kutumia  dawa  inaitwa  mruturutu  pamoja  na  dawa  nyingine kama aina  kumi  na mbili  na  kukifunga..   Baada  ya  siku  kadhaa   kidonda  kilicho  hamishiwa  mkononi  kikawa  kimekauka na  baada  ya  kukauka  kidonda  cha  mkononi  basi  na  cha  makalioni  kikawa  kimekauka.

Siku  nyingine  aliletwa  mtoto  mdogo na wazazi  wake  akiwa  ameshikwa  na homa  kali  sana,  tatizo  la  mtoto  huyo  ambaye  umri  wake  ilikuwa ni  kama  miaka  miwili  na  nusu  hivi, alikuwa  hataki  kunywa  dawa, hata  kulazimisha.   Tulipojaribu   kumlazimisha   akawa  anauma  meno.  Kujaribu kumminya  mdomo, ili  aachame akatuzi  nguvu  kwa  sababu  tulikuwa  tunamminya  kwa  tahadhari,  vinginevyo  tungeweza  hata  kumvunja  shingo.

Baba  wa  mtoto  akawa  amepanick  anajua  atampoteza  mtoto  wake. Alivyo  kuja  mungu  wa  kabili, kwa  kutumia  ule  mti wa  kuhamisha  vitu, akahamisha  homa  ya  Yule  mtoto  kwa  baba  ake  na  kuanza  kumpa  dawa baba  yake, baba  mtu  alivyopata  nafuu, basi  mtoto nay eye  akawa  amepona..

Hivyo  basi, wachawi  wanapotaka  kuchukua  uume  wa  mtoto  kwa  ajili  ya  kutengeneza  filimbi  za  kichawi, hutumia  mti  huo, kubadilisha  uume  wa  mtoto  huyo na  kipande  cha  mgomba  wa  ndizi. Na inapotokea  hali  hii, mtoto  huyo  huwa  hanithi, kwa  sababu  uume  wake  unakuwa  umechukuliwa  msukule,unatumiwa  na  watu wengine  huko.

Tofauti  kati  ya  watu wazima  na  watoto  wadogo  ni  kwamba,  uume  wa  watoto  wadogo, huchukuliwa  kwa  ajili  ya  kutengeneza  filimbi  za  kichawi, wakati  uume  wa  watu  wazima, hubadilishwa  kwa  sababu  nyinginezo  kama  vile, kutoa  adhabu  kwa  muhusika  nakadhalika.

Basi , muda  mfupi  baada  ya  Mungu  wa  Kabili  kupiga  filimbi  yake ya  kichawi, lilijitokeza  kundi  la  wachawi  ambao  idadi  yao  inaweza  kufika  arobaini  au  zaidi.

Baadae  nikaja  kugundua kuwa , wachawi  hao  walikuwa  wametumwa  na  mungu  wa  kabili  kumletea  vitu  mbalimbali, kama  wale  funza  walio nyonya damu za  maiti  na damu  za  maiti  za  misukule, mafuta  ya  misukule,  wale  wa  wanyama  na  ndege  nilio  wataja  hapo  juu  nakadhalika.

Wachwai  walipo  fika  katika  eneo  hilo, walisema “ Mkuu  Tumeitikia  wito  wako, na  tumefanya  kama  ulivyo  tuagiza “.

Baada ya  hapo  kila  mmoja  akaonyesha  vitu  vyote  alivyo  agizwa nakadhalika.

Vilianza  kutolewa  vifaa  vya  kazi  ( ambao  wao  wachawi  wanaviita  vizimba )  kwa  ajili  ya  kazi  ya  kumfunga  mume  wa  Yule  mama.

Vitu  hivyo  vilipikwa  kichawi kisha  mama  Yule  akakabidhiwa  huku  akipewa  maelekezo  ya  kwenda  kufanya.

Alipewa  dawa  za  kwenda  kumlisha  mwanaume  Yule, kumuogesha pamoja  na  kumfunga. Nilicho  kisikia  baadae  ni  kwamba, mwanaume  Yule  aligeuka  na  kuwa  kama  zezeta  kwa  mama  Yule.

Baada  ya  zoezi  la  kumfunga  mwanaume  Yule  kukamilika, lilifuatia  zoezi  la  kumtenganisha  na  mwanamke  wake  wa  pembeni.  Kuwafanya   wasikutane  tena  hadi  siku  wanaingia  kaburini.

Katika  zoezi  la  kuwatenganisha  mwanaume  Yule  pamoja  na  mwanamke  wake  wa  pembeni, zilichukuliwa  nyayo  za  Yule  mwanaume, pamoja  na  nyayo  za  mwanamke  wake  wa  pembeni  ambazo  zilipatikana  kichawi.  Lilitumwa  jinni  kwenda  kuchukua  nyayo  za  mwanamke  huyo ambazo  tayari  tulikuwa  nazo  kabla  ya  kwenda  kuroga.

Nyayo  za  mwanaume  huyo  zilichukuliwa  na  kwenda  kufungwa  kichawi  kwenye  mlima  mmoja  ambao  hutumiwa  sana  na  wachawi. Na  nyayo za  mwanamke  wake  wa  pembeni  zilichukuliwa  na  kwenda  kufungwa   kichawi  kwenye  mlima  mwingine  ambao  nao  pia  hutumiwa  sana  na  wachawi.

Maneno  yaliyokuwa  yakitamkwa  wakati  tunafunga  na  kuzika  zile  nyayo   kwenye  hiyo  milima  yalikua   ni pamoja  na  :

“     WEWE  ( JINA  LA  MWANAUME )  SIKU  YA  LEO, NIMEKUTENGANISHA  NA  (  JINA  LA  MWANAMKE).  HADI  SIKU  YA  KUFA  KWENU.  WEWE  ( MWANAUME)  PAMOJA  NA WEWE  (MWANAMKE )  HAMTAONANA  WALA  KUONANA  SEHEMU  YOYOTE  ILE  DUNIANI, HADI  SIKU  MNAINGIA  KABURINI.

KAMA  AMBAVYO W EWE  MLIMA ( JINA  LA  MLIMA )  HAUWEZI  KUKUTANA  NA  MLIMA ( JINA  LA  MLIMA ), BASI  VIVYO  HIVYO.  WEWE  (  JINA  LA  MUME )  PAMOJA  NA  WEWE  ( JINA  LA  MKE)  HAMTAKAA  MKUTANE  KATIKA  SIKU  ZOTE  ZA  MAISHA  YENU.

LAKINI  KAMA  WEWE  (  JINA  LA  MLIMA ) NA W EWE  ( JINA  LA  MLIMA ) MNAWEZA  KUKUTANA, BASI  HATA  (  JINA  LA  MWANAUME )  NA  ( JINA  LA  MWANAMKE  ) WANAWEZA  KUKUTANA.

Uchawi  huu  ulisindikizwa  na  tambiko  la  kuchinja  mnyamna  anaepandwa  na  mwanadamu.

Ndugu msomaji, usiombee  kufanyiwa  uchawi  huu.  Maana  hata  kama  imekusudiwa  wewe  na  mama  yako  mzazi  msionane, basi  hamtaonana  mpaka  siku  mnaingia  kaburini.

Baada  ya  zoezi  hili  kufanyika, lilifanyika  zoezi  la  kutoa  kichawi   ujauzito  wa  mwanamke wa  pembeni  wa  mume  wa  Yule  mama  aliye leta  mashitaka  kwa  mungu  wa  kabili.

Mungu  wa  Kabili  alichukua  yai  moja  la  bundi  ya  yai  moja  la  kuku. Kwanza  akachukua  fimbo yake ( ile  ya  kubadilisha  vitu ), akainyoosha  juu, halafu  akaipiga  ardhini  kisha  akaigusa  gusa  kwenye  tumbo  la  Yule  mama,. Alifanya  hivyo  kama  mara  saba   hivi.

Baada  ya  hapo  alichukua  lile  yaio  la  bundi, akalisugua    kwenye  tumbo  la  Yule mama kama  mara  saba  tena.

Alipomaliza  kusugua  lile  yai  la bundi kwenye  tumbo  la  Yule  mama. Akacheka  sana ( Kicheko  cha  kichawi ) Halafu  akachukua  yai  la  kuku  wa  kienyeji,  akaliweka  karibu  na  mdomo  na  kulisemesha kwa  kama  dakika  tatu  halafu  akalisugua  tena  kwenye tumbo  la  Yule  mama  kwa dakika  kadhaa, baada  ya  hapo  akalipasua  kwennye  chungu..

Mungu  wa  kabili  alisema, lengo  lake  lilikuwa  ni  kutaka  kujua hiyo mimba  ni  ya  jinsia  gani, pili ni  ya  watoto  wangapi, na  tatu  ni je  mwanamke  huyo  atajifungua  salama  au.

Mungu  wa  kabili  alisema, kabla  haujaitoa  mimba  ya  mtu, inabidi  ujue  kwanza  mimba  hiyo ni  jinsia  gani, na je  ni  ya  mtoto  mmoja  au  mapacha.

Mungu  wa  kabili  akasema, ukitaka  kujua  kama  mimba  ni  ya  mtoto  mmoja, baada  ya  kufanya  tambiko  hilo  nililo  lionyesha  hapo  juu, utapasua  yai  kwenye  chungu cheusi na  kisha.

Katika  chungu  hicho,   kiini  cha  njano  kikiwa  kikubwa  peke  yake, basi  atajifungua  mtoto mmoja,  vikiwa  viini  viwili, basi  watoto  mapacha, kama  ni  mtoto  wa  kiume, kuna  herufi Fulani utaiona  hapo, na  kama  ni  wa  kike, pia  kuna  herufi  utaiona, na  kama  ukiona  kuna  damu  damu, basi  jua  wakati  wa  kujifungua, eidha  mtoto  atakufa na  mama  atapona, au  mtoto atapona  na  mama  atakufa, au  wote  watakufa.

Majibu  hayo ndio  yatakayo  kuongoza  katika  kufanya  maamuzi ya kutoa  au  kutotoa  mimba.

Mungu  wa  kabili  akaniambia, kuna  herufi  Fulani, ukiiona  basi  kamwe  usijaribu  kutoa  hiyo  mimba, hata  kwa  gharama  yoyote. Kwa  sababu  ukijaribu  kufanya  hivyo,  jambo  baya  sana  litatokea  katika  maisha  yako….

Kwa  bahati  nzuri

UNAJUA  TULIONA  NINI  KWENYE  HILO  YAI? FUATILIA  SIMULIZI  LANGU  HAPA  HAPA,  SIKU  YA  KESHO. NITAELEZEA  KITU GANI KILITOKEA. PIA  NITAKUWA  NIKIWEKA  USHUHUDA  WANGU  HUU, KUPITIA  : www. shuhudazaajabu.blogspot.com

MSISITIZO WANGU  KWENU  WATANZANIA  WENZANGU,  WAGANGA  WA  TUNGULI,WENGI W AO  NI  WACHAWI. HUYU  MGANGA  AITWAYE   mungu  wa  kabili, NI  MCHAWI.

NAONA  WATU WENGI  TENA  WENGINE  WASOMI, NA  WENYE  KAZI  NA  NAFASI NZURI TU WAMEKUWA  WAKIMBILIA  NA  KUMUONA  KAMA  MUNGU  KWAO. NAKUOMBA  USIKUBALI  KWENDA  KWA  MGANGA  HUYO  MCHAWI,. KWA  SABABU  NI  WAKALA  WA  SHETANI.. UKIENDA  KWAKE. UTAKUWA  UMEJIUNGANISHA  NA  UTAWALA  WA  KUZIMU….

NAMBA   ZA   SIMU ZA  HUYO  MUNGU  WA  KABILI   NI : 0744 000 473.

USIPIGE  NAMBA  HIZO  TAFADHALI. NI NAMBA  ZA  WAKALA  WA SHETANI  AITWAYE  MUNGU  WA  KABILI.

MUNGU  AWALINDE  NA  AWAONGOZE  KUTENDA  YALIYO MEMA.

RC Mongella Atoa Ufafanuzi Kuhusu Ziara Ya Rais Magufuli Mkoani Mwanza.

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (kulia) akitoa taarifa ya ujio wa Rais Magufuli mkoani Mwanza. Kushoto ni Katibu Tawala mkoani Mwanza, CP.Clodwig Mtweve.

****
Judith Ferdinand (BMG), Mwanza
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, anatarajia kufanya ziara fupi ya kikazi mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, leo amesema, Rais Magufuli atafanya ziara ya siku mbili kuanzia kesho agost 10 na 11, ambapo atapokelewa hiyo kesho wilayani Sengerema akitokea Chato mkoani  Geita alikokuwa na mapumziko mafupi.

"Rais Magufuli atawasili kesho asubuhi katika mkoa wetu akitokea Chato mkoani Geita na ataanza ziara katika wilaya ya sengerema kwa ajili ya kuwasalimia wananchi, kuwapa taarifa za mikakati na maendeleo awamu ya tano pamoja na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi". Amesema Mongella.

Pia amesema hiyo kesho Rais Magufuli atasimama maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwasalimu wananchi kabla ya kuwasili wilayani Nyamagana.

Ametanabaisha kwamba Rais Magufuli ataitimisha ziara yake kesho kutwa agost 11, kwa kukagua ujenzi wa daraja la watembea kwa miguu la Furahisha Jijini Mwanza, pamoja na upanuzi wa barabara ya Furahisha hadi Pasiansi ambapo ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa miundombinu hiyo. 

Mongella amewasihi wananchi kujitokeza kwa wingi katika mkutano wa hadhara utakaofanyika kuanzia majira ya saa nanne mchana katika uwanja wa Furahisha ambapo Rais Magufuli atahutubia wananchi baada ya kukagua miradi hiyo ya ujenzi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Agosti 10

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images