Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TRA yavuka lengo la ukusanyaji kodi mwezi Julai

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imevuka lengo la ukusanyaji wa kodi wa jumla ya kiasi cha shilingi trilioni 1 sawa na asilimia 95.6 tofauti na lengo lililokuwa limekusudiwa la kukusanya trilioni 1.1 kwa mwezi Julai 2016.

Kiasi hicho ni sawa na ongezeko la asilimia 15.43 ukilinganisha na makusanyo ya awali ya mwaka 2015 ambapo mamlaka hiyo ilikusanya jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 914.

Takwimu hizo zimetolewa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jjijini Dar es Salaam.

“Kwa mwezi Julai mwaka huu makusanyo yameongezeka kwa asilimia 15.43 ukilinganisha na kipindi cha mwezi Julai 2015 ambapo tulikusanya shilingi Bilioni 914” alisema Kayombo.

Aidha aliongeza kuwa mamlaka imeweka mikakati thabiti ya kuhakikisha kuwa inafikia au inavuka lengo la Serikali la kukusanya shilingi trilioni 15.1 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 huku mkakati mmoja wapo ukiwa ni kuhakikisha kuwa walipa kodi wapya wanasajiliwa zaidi.

Bw. Kayombo aliongeza kuwa mkakati mwingine ni kuhuisha taarifa za walipa kodi kwa kuhakikisha kwamba namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN) zisizotumika zinafutwa katika mfumo wa TRA.

Pia amefafanua kuwa maandalizi ya kuhuisha taarifa za walipa kodi yapo katika hatua za mwisho ikiwemo upigaji picha,uchukuaji wa alama za vidole pamoja na vielelezo muhimu.

TRA inawakumbusha wananchi kuhakikisha wanakagua tiketi/risiti zao za manunuzi na kuangalia usahihi wa pesa walizolipa na uhalali wa risiti yenyewe.


Idara ya Uhamiaji inawashikilia watumishi wawili wa Serikali ambao si rai wa Tanzania.

$
0
0
Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Kanda ya Dar es Salaam John Msumule akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati alipokuwa akitoa taarifa ya kukamatwa kwa watumishi wawili wa Serikali ambao sio raia wa Tanzania mapema hii leo jijini Dar es Salaam.


Watuhumiwa ambao sio raia wa Tanzania waliokuwa wakifanya kazi serikalini wakiwa chini ya ulinzi wa askari wa Uhamiaji, kushoto ni Bw. Bahilanya Milingita aliyekuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)na kulia ni Dkt. Esther Green Simon Mwenitumba ambaye alikuwa Mganga Mkuu Kituo cha Afya Mburahati.

Bw.Bahilanya Milingita maarufu kwa jina la Roy Bilingita raia wa Congo ambaye anatuhumiwa kuingia nchini mwaka 1986 na kufanya kazi katika Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  kinyume na sheria za nchi.

Dkt. Esther Green Simon Mwenitumba raia wa Malawi ambaye alikuwa Mganga Mkuu katika kituo cha Afya Mburahati anatuhumiwa kufanya kazi Serikalini wakati si raia wa Tanzania.

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Kanda ya Dar es Salaam John Msumule wakati alipokuwa akitoa taarifa ya kukamatwa kwa watumishi wawili wa Serikali ambao sio raia wa Tanzania mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 
Picha zote na Eliphace Marwa-Maelezo

Katibu Mkuu wa Bavicha Taifa Julius Mwita Atiwa Mbaroni

$
0
0
KATIBU Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha) Julius Mwita amekamatwa na Jeshi la Polisi mchana huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
 
Mwita na vijana wengine watatu ambao hawakufahamika majina yao mara moja wamekamatwa kwa sababu ambazo hazijafahamika mpaka sasa wakati wakisubiri Tundu Lissu Mwanasheria Mkuu wa Chadema kufikishwa mahakamani hapo.

Mwandishi ameshuhudia Mwita na vijana wawili wakikamatwa ndani ya eneo la mahakama na kuingizwa ndani ya gari ya polisi yenye namba za usajili PT 1848.

Kijana mwingine mmoja amekamatwa akiwa nje ya uzio wa mahakama hiyo ambapo askari waliojihami kwa silaha za moto wameimarisha ulinzi ndani na nje ya mahakama ya Kisut.

Vijana wote wanne tayari wameondolewa mahakamni hapo na gari ya polisi ambapo inaaminika kuwa watapelekwa Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es salaam kwaajili ya mahojiano.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 9 & 10

$
0
0
MTUNZI:EDDAZARIA G.MSULWA

Tukavaa nguo zetu haraka haraka baada ya kuona tupo sawa nikachungulia dirishani na kumuona John akiwa amejishika kiuno huku hajui wapi tulipo
“Oya John sisi tupo huku”
“Ahhh mwanagu hukuwa unanisikia kipindi ninakuita au?”
“Sijasikia bwana tatizo lako wewe unawenge sana”

Nilizungumza huku nikitoka katika chumba tulichokuwa huku nikiwa na trey nne sisizo na mayai.Nikaingia katika banda la kuku na kuchukua kindoo kidogo kilicho na mayai kisha nikatoka nacho na kuanza kupanga yai moja baada ya jengine huku Madam Rukia akitoka akiwa ameshika trey mbili zisizo na mayai

‘”Wewe mbona umesimama humsaidii mwenzako katika kupanga mayai”
“Madam hapa nilipo nimechoka kama nini ninaogopa ninaweza nikayavunja hayo mayai ikawa ni kesi juu ya kesi”
John alizungumza huku akiwa anatafuta sehemu ya kukaa kabla hata hajakaa akasikia redio ya madam ikitoa sauti ya mziki.

“Umeme huo umerudi ngoja nikamalizie mechi yangu”
John akatoka mbio na kutuacha mimi na madam tukicheka kwani kwa vitendo anavyovifanya John ni sawa na mtoto mdogo wa kidato cha kwanza
“Hivi huyu mwenzako anaakili nzima”
“Ndio tena ndio anayetushikia darasani”
“Ehhee makubwa basi mshauri akue aache utoto”
“Sawa”

Tukaendelea na kazi ya kuyapanga mayai kwenye tery huku mara kwa mara tukiwa tunatazamana kwa macho ya wizi wizi.Tukamaliza tukasaidiana kuzibeba trey hizo hadi kwenye meza ya sebleni kwake

“Alafu Eddy kama utahitaji kuoga bafu hilo hapo kwani ninakuona unatokwa na jasho”
“Sawa madam….Vipi chai tunakunywa au ndio siku inapita kavu?”
“Ngoja niwachemshie mayai mangapi mangapi yatawatosha?”
“Kumi kumi”
“Eddy mwenzako anakazi ya kuakia wakati hata kuokota yai hata moja kwenye banda hajaokota”
“Mwaya madam usimsikilize huyu mayai mawili mawili yanatutosha”

Madam akaondoka akaingia kwenye chumba nikagundua kitakuwa ni jiko kwani nilisikia akigonganisha visufuria vinavyoonekana vimewekwa kwenye mpangilio usio mzuri.Nikaingia katika bafu aliloninyesha Madam Rukia nikavua nguo zangu na kufungua maji ya bomba la mvua nikabaki nimesimama huku mawazo juu ya ndoto niliyo iota yakanijia upya.

“Hivi si nilienda kuoga baada ya kupanda kitandani?”
Sikuwa na kumbukumbu za kutosha kama wakati nilipo panda kitandani kuupumzisha mwili wangu nilikwenda kuoga au usingizi ulinipitia na kuanza kuota vitu vya ajabu.Nikasimama kwenye mchuruziko wa maji kisha nikaanza kujisugua kila kona ya mwili wangu.Nikamaliza kuoga na nikamuomba Madam anipe msaada wa wa taulo la kujifutia maji.Akampa John na akaniletea bafuni,Nikajifuta maji kisha na kuvaa nguo zangu za shule,sikuwa na jinsi zaidi ya kuzivaa hivyo hivyo japo zina nuka jasho kwa mbali

Nikarudi sebleni na kumkuta John akiwa anaendelea kunywa chai,nikajumuika naye.Tukamaliza kunywa chai.Nikamuomba Madam Rukia anipatie japo pafyumu ili mwili uishiwe na kajiarufu ka jasho ambacho kalianza kunikera
“Ingia ndani kwangu utakuta dressing table utachagua ni pafyumu gani unayohitaji”

Nikaingia chumbani kwa Madam Rukia na nikaanza kutafuta ni pafyumu gani nitaweza kupulizia kwa bahati nzuri nikakuta body spry kama yangu.Nikaanza kujipulizia taratibu huku nikiwa nimefungua vifungo vya shati ili niweze kujipulizia katika makwapa vizuri huku nikiwa ninacheza.Mlango ukafungulia na Madam Rukia akaingia na akaanza kunishangaa kwa jinsi ninavyo cheza cheza.

“Kumbe wewe na rafiki yako akili yenu ni moja?”
“Kwanini Madam?”
“Kinacho kuchezesha chezesha hapo wewe ni kipi wakati wezako tunakusubiri?”
Nikanyamaza kimya,Madam Rukia akapiga hatua na kunifuata na kuanza kunifunga vifungo huku akinitazama usoni
“Mery anaonekana ana faidi”
“Ana faidi nini?”

Kigwangalla afanya ziara ya Kushtukiza Katika kliniki ya ForePlan.....Awapa Polisi masaa 24 kumkamata Dk Mwaka

$
0
0
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kingwangalla ameagiza Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam kumkamata tabibu maarufu Juma Mwaka ndani ya saa 24

Dk. Kigwangalla ametoa amri hiyo leo jijini Dar es Salaam alipokitembelea tena kituo cha Fore Plan kinachomilikiwa na tabibu huyo maarufu kwa jina la ‘Dk. Mwaka.’

Serikali ilitangaza kukifungia kituo hicho cha afya na vingine vitatu mwezi mmoja uliopita kwasababu zilizoelezwa kuwa ni kutoa huduma kinyume na sheria ambapo kituo cha tabibu Mwaka kilidaiwa kufungiwa kwa mmiliki kujiita daktari badala ya tabibu!

Hata hivyo wiki moja baada ya kuifungia kliniki hiyo kutoa huduma  zake, iliendelea kujitangaza kuwa inaendelea kufanya kazi kama kampuni ya ushauri na huduma za kiafya na siyo kliniki tena.

Kutoka jina la awali Fore Plan Clinic ilianza kujitangaza kama Fore Plan Company kitendo ambacho Dk. Kingwangalla amekitaja kuwa ni kinyume na sheria na kuagiza tabibu huyo akamatwe haraka iwezekanavyo.

Tundu Lissu Asomewa Mashitaka Matatu Mahakamani

$
0
0

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameshtakiwa kwa makosa matatu la kwanza kutoaa maneno ya uchochezi kwamba Agosti 2 katika Mahakama ya Kisutu kwa nia ya kujenga chuki kwa wananchi dhidi ya Rais na Serikali alitoa maneno ya uchochezi.

Shtaka la pili pia uchochezi kwamba Agosti 2 katika mahakama hiyohiyo kwa nia ya kudharau mhimili wa utoaji haki, alisema kuwa hawezi kufungwa kwa mashtaka na kesi ya upuuzi na shtaka la tatu ni la kudharau mahakama akidaiwa kuwa tarehe hiyohiyo mahakamani hapo, alitoa maneno ya uchochezi kuwa hawezi kufungwa kwa kesi na mashtaka ambayo ni upuuzi na ya kimagufulimagufuli

Hatimaye Tundu Lissu Aachiwa Kwa Dhamana Baada ya Mvutano Mkali wa Kisheria

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Mhe. Tundu Lissu alipewa dhamana saa tatu usiku wa kuamkia leo  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, baada ya kukana mashitaka matatu ya uchochezi aliyosomewa.

Lissu alitimiza masharti ya dhamana baada ya mvutano mkali wa zaidi ya saa 5 na kujidhamini mwenyewe kwa dhamana ya shilingi milioni 10, na kesi yake imeahirishwa hadi Agost 19, 2016.

Mapema jana Katika Mahakama ya Hakimu MkazI Kisutu, ulinzi uliimalishwa tangu saa mbili asubuhi ambapo askari polisi waliokuwa na silaha walikuwa wakizunguka huku na huko kuhakikisha wafuasi wa chama hicho hawakusanyiki katika eneo la mahakama, huku kukiwa na matarajio ya kuwa wakati wowote atafikishwa mahakamani hapo.

Viongozi mbalimbali wa chama hicho nao walikuwepo katika mahakama hiyo kufuatilia kesi hiyo ya Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki.

Majira ya saa nane mchana Mhe Lissu alifikishwa mahakamani na kupandishwa kizimbani.

Akisomewa Mashataka na Wakili wa Serikali Paul Kaduche mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Cyprian Mkahe ilielezwa kuwa Mhe Tundu Lissu alifanya makosa hayo matatu Agost 2 mwaka huu, katika maeneo ya mahakama hiyo, kwa kutoa maneno ya uchochezi, maeneno ya dharau katika mfumo wa utoaji haki pamoja na kuidharau mahakama ya Kisutu.

Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na baadaye ukatokea mvutano mkali wa kisheria juu ya uhalali wa dhamana ambapo mawakili wa serikali walikuwa wakipinga mtuhumiwa huyo kupewa dhamana.

Baada ya mvutano wa zaidi ya saa 5, kuanzia saa 10 jioni hadi saa tatu usiku,  hakimu alikubali hoja za upande wa utetezi na kutoa dhamana baada ya Lissu kukamilisha masharti ya dhamana hiyo.

Mara baada ya kuchiwa, Lissu akiongozana na baadhi ya viongozi wa chama chake, aliondoka mara moja mahakamani hapo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Agosti 6


Oparesheni UKUTA Ya Chadema Yapigwa Marufuku Dar es Salaam

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ameliagiza jeshi la polisi mkoa wa Dar es salaam kuhakikisha kwamba sheria zinafuatwa na kusiwepo kitu kinaitwa UKUTA ili wananchi waendelee na kazi zao kama kawaida.

Akizungumza jana na kikosi cha kutuliza ghasia katika kambi ya Ukonga Jijini Dar es salaam Mkuu wa Mkoa alisema kwa kuwa askari wanafahamu sheria wasisubiri mtu yeyote kuja kuwakumbusha juu ya jambo hilo au maelekezo mengine kwa kuwa Amiri Jeshi ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameshaagiza kinachotakiwa ni utekelezaji.

‘’Msisubiri maelekezo yoyote kutoka juu, asiwepo mtu yeyote akafunga duka kwa sababu ya UKUTA, nyie ni matrekta hakuna UKUTA unaweza kusimama mbele yenu, mimi kama Mkuu wa Mkoa ninaamini hatutakuwa na vurugu kwenye Mkoa wetu na hatuwezi kuruhusu vurugu kwa kuwa tunajua madhara ya vurugu’’ Alisema Makonda.

Aidha kwa upande wake Kamanda wa Oparesheni Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Lucas Mkondya alisema jeshi la polisi lipo vizuri na vijana wameandaliwa vizuri na wameandaliwa kuwa tayari siku nyingi na hakuna mtu yeyote atakayethubutu kufanya UKUTA na watakaofanya hivyo watazimwa kabla hawajafanya chochote.

Kamada aliwataka wananchi wote Jijini Dar es Salaam kuto jitokeza kwenye oparesheni UKUTA kwa kuwa maandamano hayo siyo halali na watakaojitokeza watapata matatizo yasiyowahusu.

Oparesheni UKUTA ilitangazwa na CHADEMA ikiwa na maana Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania na ikatajwa tarehe Mosi Septemba nchi nzima chama hicho kitafanya mikutano ya hadhara jambo ambalo limepingwa na serikali kuanzia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kufuatia wakuu wa mikoa.

TRA kuanza kukusanya kodi kwenye nyumba za kupanga

$
0
0

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza kuanza kutembelea nyumba hadi nyumba kuhakiki gharama za upangishaji ili kukokotoa na kukusanya kodi sahihi ambayo ilikuwa haifiki serikalini. 

Hivyo, wamewataka wananchi kutunza kumbukumbu za mikataba ya pango ili itakapohitajika na maofisa wa mamlaka hiyo wawapatie.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati akielezea kuhusu makusanyo ya kodi kwa mwezi Julai, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema hatua hiyo ni moja ya mikakati ya kuongeza ukusanyaji wa mapato.

Alisema kwa Julai, TRA imekusanya Sh trilioni 1.055 sawa na asilimia 95.6 ya lengo la kukusanya Sh trilioni 1.103 iliyopangiwa na serikali kwa mwezi huo.

Alisema ikilinganishwa na kipindi kama hiki kwa mwaka jana, TRA ilikusanya Sh bilioni 914 ikiwa ni ongezeko la asilimia 15.43 ya makusanyo ya mwezi huu huku kwa mwaka wa fedha 2016/2017, TRA imepewa lengo la kukusanya Sh trilioni 15.1 ikilinganishwa na lengo la mwaka jana la Sh trilioni 13.32.

“Natoa wito kwa wapangaji na wapangishaji kujiepusha na aina yoyote ya udanganyifu katika suala zima la kodi halisi ya pango kwa kuwa inaweza kuwasababishia kushtakiwa endapo udanganyifu huo utabainika,” alieleza Kayombo.

Kwa sasa, wapangaji wengi hawalipi kodi serikalini baada ya kupanga nyumba, na badala yake wamekuwa wakilipa fedha za pango kwa wamiliki wa nyumba ambao wengi wao pia hawalipi kodi serikalini zaidi ya kulipia kodi za majengo.

Wapangaji wamekuwa wakilipishwa kodi ya pango kuanzia ya miezi sita hadi mwaka moja na kodi hizo zimekuwa zikitofautiana kutokana na hadhi ya nyumba, eneo ilipo, ukubwa wake na huduma ilizonazo kama maji na umeme.

Aidha, Kayombo alisema pia mamlaka hiyo itatembelea waajiri katika maeneo mbalimbali kuhakiki na kukagua usahihi wa orodha na malipo ya ajira ili kujiridhisha kama kodi za ajira zinakokotolewa na kulipwa serikalini inavyostahili.

Alisema mbali na mkakati huo, TRA imeweka mikakati ya kuhakikisha walipakodi wapya wanasajiliwa zaidi pamoja na kuhuisha taarifa za walipakodi kwa kuhakikisha Namba za Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) zisizotumika zinafutwa katika mfumo wa mamlaka.

“Maandalizi ya kuhuisha taarifa za walipakodi yako katika hatua za mwisho yakihusisha upigaji picha, kuchukua alama za vidole pamoja na vielelezo muhimu vya mlipakodi ili kuhakikisha kila biashara inakuwa na TIN moja tu yenye taarifa sahihi na za uhakika,” alifafanua.

Alisema TRA imeboresha mifumo yake ili kupunguza au kuondoa changamoto za kutopatikana kwa mtandao ambayo mara nyingi huathiri makusanyo ikiwa ni pamoja na kuunganisha mifumo ya TRA na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ili kuhakikisha mapato ya serikali yanakusanywa kwa usahihi na wakati.

Pia wanaendelea kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato kwa kuhakikisha wafanyabiashara wote wanaostahili kutumia mashine za kielektroniki za kodi (EFDs) wanazitumia ipasavyo pamoja na kuwakagua wanunuzi wanapotoka madukani kwa lengo la kuhakikisha wana risiti halali na sahihi kwa manunuzi yao. 

Kayombo alisema TRA inawaasa wananchi kuhakikisha wanakagua risiti zao za manunuzi na kuangalia usahihi wa fedha walizolipa na uhalali wa risiti yenyewe.

“Tunatoa wito kwa umma kutoa risiti wakati wa kuuza na kudai risiti wakati wa manunuzi ya bidhaa au huduma kwani sheria ya fedha ya mwaka huu imerekebisha sheria ya usimamizi wa kodi na wasiodai risiti kwa manunuzi yoyote watapata adhabu ya Sh elfu thelathini hadi Sh milioni moja na nusu,” alisema.

Alisema kwa sheria hiyo kutotoa risiti na kutodai ni makosa kwa mujibu wa sheria na hatua zitachukuliwa kwa wale watakaobainika kutotoa risiti au kutodai risiti wakati wa mauzo na manunuzi.

Alisema wanaendelea kukusanya mapato na kutoa elimu kwa wananchi hasa mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi kama Sheria ya Fedha ya mwaka 2016 iliyopitishwa hivi karibuni ili kujenga uelewa na kukuza ridhaa ya kulipa kodi kwa hiari.

Tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, Rais John Magufuli amekuwa akisisitiza Watanzania kujenga tabia ya kutoa na kudai risiti kwa kusisitiza ‘ukinunua dai risiti na ukiuza toa risiti.’

Basi la Kisbo laua watu 3 Morogoro

$
0
0

WATU watatu wamekufa papo hapo na wengine wanane kujeruhiwa baada ya basi lenye namba za usajili T 402 CRY aina ya Scania mali ya Kampuni ya Kisbo – Safari kupinduka mkoani Morogoro. Basi hilo lilikuwa likitoka mkoani Tabora kwenda Dar es Salaam.

Imeelezwa kuwa basi hilo lilipinduka wakati likijaribu kukwepa gari lingine eneo la Kwambe, wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro kwenye barabara kuu ya Dodoma – Morogoro.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonce Rwegasira alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 12: 30 jioni, juzi, mwaka huu eneo la Kwambe, kata ya Dumila, tarafa ya Magole wilayani Kilosa mkoani Morogoro kwenye barabara kuu ya Dodoma- Morogoro.

Alisema basi hilo likiendeshwa na Davis Samora (38) mkazi wa Dar es Salaam liliacha njia na kupinduka wakati likijaribu kukwepa gari lenye namba za usajili T957 BUV aina ya Scania lenye trela namba T 919 BVA likiendeshwa na dereva asiyefahamika akitokea Morogoro kwenda Dodoma na ambaye alikimbia baada ya ajali kutokea.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, dereva huyo alijaribu kuyapita magari matatu mbele yake bila tahadhari na kusababisha ajali hiyo.

Kaimu huyo alitaja majina ya waliokufa kuwa ni Francis Shija (70) mkazi wa Nzega, mkoa wa Tabora, mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 45 hadi 50 ambaye hajatambulia jina , pamoja na mtoto mdogo wa kiume ambaye bado hajatambuliwa kwa jina na umri wake ni kati ya miaka mitatu hadi minne.

Aliwataja majeruhi waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro ni Kinazi Machum (38), ambaye ni Mhandisi na Mkazi wa Tabora, Mathei Fidelis (30), mkazi wa Singida na Baraka Ruta (4) mkazi wa Mwanza.

Wengine ni Juma Bilal (30) mkazi wa Nzega, Ebebeza Richard (22) mkazi wa Mbeya, Hamis Mogela (30) mkazi wa Nzega, Pili Waziri (44) mkazi wa Tabora na Prisca Shija (30) mkazi wa Nzega na wote wanaendelea vyema, wakati maiti wakiwa wamehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali hiyo ya Rufaa.

Kaimu Kamanda alisema kuwa, polisi wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa ambaye ni dereva wa gari T 957 BUV aina ya Scania lenye trela namba T 919 BVA ili aweze kufikishwa katika vyombo vya sheria .

Mgeja Ampinga Rais Magufuli

$
0
0

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, amesema hatua ya Rais John Magufuli kuzuia kufanyika kwa mikutano ya kisiasa nchini, imelenga kuminya demokrasia na serikali kutaka kutokosolewa.

Mgeja, ambaye kwa sasa ni mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Mendeleo (Chadema), alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa hatua hiyo haikubaliki katika nchi ya kidemokrasia duniani kwa kuwa uhai wa vyama vya siasa upo katika mikutano.

Pia amemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, kushughulikia migogoro ya vyama badala ya kusubiri hadi nchi ikielekea katika mgogoro mkubwa.

Alisema kauli ya Rais Magufuli kwamba shughuli za kisiasa hadi mwaka 2020, inakiuka katiba kwa kuwa mikutano na shughuli za vyama vya siasa vipo kikatiba.

Alieleza kuwa kinachotokea sasa kwa viongozi wa upinzani ni kupigania demokrasia hali ambayo inaweza kuhatarisha amani ya nchi.

“Serikali inakosolewa kupitia mikutano ya vyama vya siasa na serikali isitupangie cha kuzungumza. Kutokana na kauli ya rais tunaonya likitokea lolote katika mikutano ambayo itafanyika nchi nzima, kupitia operesheni ya Umoja wa Kuondoa Udikteta Tanzania (Ukuta), Rais atawajibika iwapo nguvu ya jeshi polisi itatumika,” alisema.


Salam za Wema Sepetu kwa mtoto wa Diamond Platnumz ‘Tiffah’

$
0
0
Msanii wa filamu Wema Sepetu anaendelea kuuthibitishia umma kwamba hana tena kinyongo na Ex wake wa zamani Diamond Platnumz baada ya Jumamosi hii kumwandikia ujumbe mzuri bintiye Diamond, Tiffah katika siku yake ya kuzaliwa.

Wawili hao hivi karibuni wameonyesha kushirikiana mambo kadhaa katika mitandao ya kijamii licha ya wiki mbili zilizopita kusambaa kwa tetesi ya kurudiana na baadae kukanushwa na Wema Sepetu.

Muigizaji huyo kupitia instagram ameandika ujumbe huu:

Happy Birthday Princess Tee…🎈🎉🎁🎊🎀💝 May Allah bless your precious lil self… You will definitely turn out to be a phenomenal young woman… Princess_tiffah.

Jumamosi hii bintiye Diamond, Tiffah, ametimiza mwaka mmoja ambapo amewashukuru wote waliomtakia heri katika siku hiyo.

“Today a year ago at 4:40 am in the wee hours of the morning I was brought into this world. Thank-you for all my bday wishes & God bless all of you😘. HAPPY BIRTHDAY TO ME,” Ujumbe huu uliandikwa instagram ya binti huyo.

Kwa upande wa Diamond, ameandika:

    Princess_tiffah You are certainly the most beautiful gift that i have received in my lifetime….This day is very important for us and to everyone who knows you…Only God Knows how much you mean to me…am so Proud for the first time in my Life to wish my own daughter Happy Birthday… trust me, in my Heart you are the most wonderful daughter in the whole world!….May you always be surrounded with beauty and happiness!…..My Angel, my little Cupcake, my sweet daughter, My Miss World, me and Your Cute Mom loves you so much…..Happy Birthday! @princess_tiffah 🎉🎂🎉

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 27

$
0
0

MTUNZI: ENEA FAIDY
...... MR ALOYCE alibaki kimya akiwa ametulia kimya kama vile amegandishwa na gundi ngumu. Haja ndogo ilipita taratibu katikati ya mapaja yake na kushuka chini ardhini. 

Alitamani ardhi ipasuke ili walau akajifiche chini ya ardhi kuliko kuendelea kushuhudia tukio lililokuwa linaendelea kwa wakati ule. 

Akili ilisimama, mwili ulinyong'onyea kwani hakuwa na lolote la kuweza kufikikiria kwa wakati ule. "Nimekamatika kwenye mtego" ndilo wazo pekee lililomjia akilini mwake.

Chatu yule aliendelea kujiviringisha kwa madaha na mbwembwe nyingi mwilini mwa Mr Aloyce na kumfanya mwanaume yule ajihisi mfu aliyebakisha roho yake tu kabla ya mazishi. 

"Nisaidie Mungu wangu" Mr Aloyce alisali kimoyo moyo akiamini kwamba huenda Mungu atasikia maombi yake na kumkumkumbuka katika Mateso yake. Machozi hayakumtoka hata chembe kwani hofu ilimzidia mpaka chozi lilimkauka.

Akiwa katika hali hiyo ngumu isiyoelezeka Mr Alloyce hakuona mtu yeyote wala dalili ya kiumbe chochote katika eneo lile. Ghafla upepo mkali ukapuliza eneo lile, ulikuwa kama kimbunga kinachoweza kuleta maafa kwa makazi ya watu.

Mr Aloyce alijishangaa sana kuona mwili wake ukiwa mwepesi sana tena umejiachia kupita kiasi. Moyo wake ukafurahi na akatumia nafasi hiyo kujitazama mwilini mwake, akagundua yule chatu hayupo tena mwilini mwake Bali amesogea pembeni kidogo na kujituliza kama gogo.

Macho yalimtoka kama njugu akimtazama yule Chatu, ghafla akapigwa na mshangao wa ajabu baada yule chatu kubadilika umbile na kuwa na umbo la mtu. Mr Alloyce akamkazia macho MTU yule aliyetokana na chatu.

 Hakuamini macho yake pale alipogundua mtu yule alikuwa mkewe, Aloyce alitetemeka sana. Ndipo mwanamke yule alipoachia kicheko kikali sana huku akimsogelea Mr Aloyce. "Nilikukumbuka sana mume wangu.. Ila nasikitika unaniogopa" alisema mwanamke yule mwenye sura na umbile la mama Eddy. Mr Aloyce alitetemeka sana, akapiga hatua za kinyumenyume kumkwepa mwanamke yule.
 
"Mume wangu! Mbona unaniogopa?" Alisema mwanamke yule.


Waziri wa Kilimo Awanyooshea Kidole Maofisa Ugani Wanaoomba Rushwa

$
0
0

WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba amewanyooshea kidole maofisa ugani wa mifugo na uvuvi kwa maelezo kuwa wameacha kutimiza majukumu yao na badala yake wanakamata zana haramu za uvuvi, kuuza dawa na kuomba hongo.

Dk Tizeba alisema hayo juzi alipotembelea maonesho ya kitaifa ya mifugo katika viwanja vya maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Maonesho ya Kilimo Kanda ya Kati Nzuguni mjini Dodoma.

Alisema maofisa ugani upande wa kilimo, ufugaji na uvuvi hawawajibiki ipasavyo na wamejibadilisha kuwa wafuatiliaji na wakamataji wa zana haramu za uvuvi, kuuza dawa za mifugo na kupokea hongo.

Pia alisema maofisa nyama wamebaki kuchukua baadhi ya nyama kama hongo na kuruhusu nyama kuuzwa bila kukaguliwa kitaalamu.

Alimuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Mary Mashingo kufuatilia utendaji kazi wa Baraza la Usajili wa Maofisa Ugani hao, huku akimtaka pia mwenyekiti wake wa bodi hiyo kumpatia mpango kazi walionao na changamoto zilizopo katika kuwasimamia ili wawajibike vyema zaidi.

Dk Tizeba alisema baraza hilo, mwenyekiti wake wa bodi kuhakikisha kuwa anatengeneza mfumo utakaotoa vibali vya muda utakaowezesha bodi yake kuwapima utendaji wao kwanza kabla ya kuwapatia usajili wa kudumu.

Pia alimuagiza katibu mkuu kutoa maagizo kwa halmashauri zote nchini ili maofisa ugani hao wanapotekeleza wajibu wao chini ya usimamizi wa wakurugenzi wao wawe na mfumo ulio wazi na wenye tija katika kuwahudumia walengwa vizuri zaidi na si kama wanavyofanya sasa kwani hawawajibiki na hawasimamiwi ipasavyo.

Ofisa Mifugo wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Gracian Mwesiga alisema inawezekana kuwepo kwa maofisa mifugo wasiotimiza majukumu yao, lakini kwa mwenendo wa sasa wa serikali wanatakiwa kupendekeza na kupitisha sheria itakayompa meno mwenyekiti wa bodi ya usajili wa maofisa ugani ikiwamo kufuatilia utendaji wao baada ya kuwasajili.

“Usimamizi wa maofisa mifugo upo kwenye halmashauri na si katika baraza ambalo kazi yake ni kusajili wataalamu,” alisema Mwesiga.

Wazazi Wamuua Mtoto Wao Kwa Kipigo

$
0
0
MWANAFUNZI aliyekuwa akisoma Darasa la Saba katika Shule ya Msingi Zimba, Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga, Susana Kauzeni (15) ameuawa baada ya kupigwa na wazazi wake wakimtuhumu kuwa ni mtoro sugu wa shule.

Ofisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga (Shule za Msingi), Peter Fusi amesema kuwa mwanafunzi huyo alizikwa kijijini humo Julai 23, mwaka huu.

“Baba na mama yake walichangia kumpiga binti yao huyo wakimtuhumu kuwa ni mtoro sugu wa shule pia nyumbani amekuwa haonekani. Baba yake mzazi amekimbia baada ya kufanya uhalifu huo huku mama yake akiwa ameshikiliwa na Jeshi la Polisi,” alieleza Fusi.

Fusi alieleza kuwa kuanzia Agosti 3 na 4, mwaka huu alitembelea baadhi ya shule za msingi zilizopo kwenye Bonde la Ziwa Rukwa ikiwemo Shule ya Msingi Zimba kufuatilia kazi ya utengenezaji wa madawati mapya kwa ajili ya shule za msingi pia kufuatilia takwimu sahihi za wanafunzi ili kubaini wanafunzi hewa.

“Nilipofika kwenye Shule ya msingi Zimba, Mratibu Elimu Kata, Daudi Moga na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Fidelis Mwangurumba walithibitisha kutokea kwa mauaji hayo ya mwanafunzi huyo,” alisema.

Kwa mujibu wa Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mwangurumba, mwanafunzi huyo alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi watoro sugu shuleni hapo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo.

Katibu wa Chadema Kanda ya Ziwa Akamatwa Akituhumiwa Kufanya Uchochezi Kwa Kutumia Mitandao ya Kijamii

$
0
0

Wakati Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu akiwa nje kwa dhamana baada ya kupandishwa kizimbani kwa makosa matatu yakiwamo ya uchochezi, Jeshi la polisi mkoani Geita limevamia Hoteli ya KG iliyopo mjini Geita aliyokuwa amefikia Katibu wa Chadema Kanda ya Ziwa, Meshack Miku na Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Geita, Neema Chazaile na kuwashikilia kwa tuhuma za uchochezi wa kutumia mitandao ya kijamii. 

Taarifa zilizopatikana kutoka kwa uongozi wa Chadema Mkoa wa Geita na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa, Mponjoli Mwabulambo zimedai kuwa katibu huyo alikamatwa jana saa 12 asubuhi. 

Katibu wa Chadema Mkoa wa Geita, Sudy Mtanyagala alidai kwamba askari wa polisi zaidi ya 10 wakiongozwa na Kamanda wa Upelelezi Mkoa (RCO) waliizunguka hoteli aliyokuwa amelala katibu huyo wakidai wanatafuta majambazi yenye silaha.

 Mtanyagala alidai kuwa polisi hao waliingia chumba baada ya chumba na walipofika katika chumba cha mwisho ambacho ndicho alichokuwa amelala katibu huyo walimkamata na kuchukua simu yake. 

Alisema baada ya kumkamata walisoma nyaraka za chama alizokuwa nazo kisha kumtaka yeye na mwenyekiti wa Bavicha kuongozana na polisi hadi kituoni kwa uchunguzi zaidi.
 
 Alisema katibu huyo wa kanda pamoja na mwenyekiti wa Bavicha mkoa walikuwa wakijiandaa kwa kwenda katika ziara Wilaya ya Nyang’wale ambako wangefanya mikutano ya ndani na viongozi wa chama hicho. 

Katibu wa Chadema Wilaya ya Geita, Hellena Thobias alisema walipata taarifa za kukamatwa kwa viongozi hao asubuhi na kufika polisi. 

Alisema baada ya kufika polisi, maelezo yalibadilika na kuelezwa katibu wao anatuhumiwa kwa uchochezi kwa kutumia mitandao ya kijamii. 

Alisema wamejitahidi kuomba dhamana lakini imeshindikana baada ya kuelezwa kuwa watuhumiwa hao watakuwa chini ya uangalizi wa polisi kwa uchunguzi zaidi. 

“Polisi wametunyima dhamana hadi saa 10 jioni tuko polisi tumeomba dhamana wamekataa sijui ni sheria gani inayomzuia mtu kupata dhamana lakini pia sijui ni sheria gani ya polisi kumnyang’anya mtu simu yake bila ridhaa na kuichunguza. Hatutanyamaza juu ya uonevu huu,” alisema. 

Alisema Serikali imekataza mikutano  ya hadhara na kueleza kusikitishwa kwake na hatua ya jeshi la polisi kufuatilia hadi mikutano ya ndani ya chama hicho ambayo ni haki yao kikatiba. 

Akizungumza kwa simu na mwandishi, Kamanda Mwabulambo alikiri jeshi lake kuwashikilia katibu huyo wa Chadema wa kanda na mwenyekiti wa Bavicha mkoa lakini akasema yupo nje ya ofisi hivyo hawezi kulizungumzia jambo hilo kwa undani.

John Shibuda Amkingia Kifua Rais Magufuli

$
0
0

Katibu Mkuu wa Chama cha Ada Tadea, John Shibuda amesema Rais John Magufuli “ni katili kwa wahujumu wa ustawi na maendeleo ya Taifa na rafiki kwa waadilifu”, na kuwataka Watanzania kumuunga mkono kwa ukatili huo ambao amesema unabezwa na baadhi ya watu.

Shibuda, ambaye alikuwa mbunge wa Maswa Magharibi kwa tiketi ya Chadema na CCM kwa vipindi tofauti, alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Shinyanga.

Alisema wanaodai Rais Magufuli ni dikteta hawajui viwango vya ubora wao katika kutoa hukumu hiyo na kuwataka kuchagua kupendezesha waadilifu ili kwenda peponi au waovu waliojipanga kwenda jehanamu.

“Ndugu zangu ukweli haulogeki. Mahimizo ya Rais si udikteta, bali ni dhamira ya kuibua msisimko wa uhuru na maendeleo na uhuru ni kazi na asiyefanya kazi asinufaike na jasho la Watanzania,” alisema Shibuda ambaye anasifika kwa uwezo wake wa kutumia vizuri lugha ya Kiswahili.

 Shibuda alisema kama Magufuli ni katili, basi dini zote ni katili kwa kuwa zina amri za Mungu ambazo zinawakataza watu kufanya mambo wanayoyapenda.

Alisema ndiyo maana viongozi wa dini nao wamekuwa wakisisitiza uadilifu, jambo ambalo Rais Magufuli analifanya.

“Napongeza ukatili wa Rais kukemea maovu,” alisema Shibuda.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano imekuja katika dunia ya mabadiliko ya mila, jadi na utamaduni wa utendaji wa umma na kukomesha uzembe katika uwajibikaji, ufisadi na kuleta msisimko unaoshangiliwa na jamii na kuondoa zomeazomea dhidi ya Serikali.

Kiongozi huyo wa upinzani alisema ajenda ya vyama vya upinzani imenyauka na kuvitaka kuacha kutafuta mfereji wa kutorokea.

 Badala yake, alivitaka vyama vya upinzani kujipanga upya ili viwe na mtazamo mpya wa utendaji wa shughuli za kisiasa.

Aliifananisha Serikali ya Awamu ya Tano na mabadiliko ya tabianchi duniani, akisema Taifa limepata Rais mwenye utumishi changamfu na kugusa hisia za jamii.

“Vyama vya upinzani viache siasa za mipasho na vijembe. Siasa hizi hazitatui kero za umaskini, ujinga, uchumi wa kaya na wananchi,” alisema Shibuda.

“Wanasayansi walianza na dawa ya panado zakutuliza maumivu, lakini leo kuna dawa tatu na mseto kwa kuwa walishindana kugundua dawa bora, basi na wapinzani wawe na vikosi kazi vya kubuni tiba mbadala ya kutengua utumishi wa Rais Magufuli,” alisema Shibuda.

Alisema hakuna chama chochote cha kisiasa Tanzania ambacho kipo kwa masilahi ya kukweza chama kingine, bali kila chama kipo kwa ajili ya kugombania kushika hisia za jamii na kuwa na dola na wala chama hakilazimishwi kufungamana na tafsiri ya chama kingine kwani kina sera zake zaidi ya kufungamana siasa na itikadi ya chama chenyewe.

Alisema vyama vinaweza kuwa na ushirikiano wenye dhamira sahihi ya kukuza masilahi ya jamii, ndiyo maana chama chake cha Ada Tadea kinashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Shibuda aliwataka wanasiasa kuwa na mawazo makini ya kunufaisha fikra za Watanzania.

Polisi Waendelea Kumsaka Dr. Mwaka

$
0
0

Mmiliki wa kituo cha Foreplan Clinic, Juma Mwaka, maarufu Dk Mwaka’ bado hajauepuka mkono wa Serikali na sasa Jeshi la Polisi limesema linataka limtie mikononi mwake ndani ya saa 24. 

Tangu Baraza la Mawaziri la Serikali ya Awamu ya Tano liapishwe mapema mwaka huu, Dk Mwaka, ambaye ni tabibu wa tiba mbadala amekuwa kwenye hali ngumu. 

Sakata lake lilianza baada ya Naibu Waziri wa Afya, Dk Hamisi Kigwangalla kufanya ziara ya kushtukiza kwenye kituo chake kilichoko Buguruni, lakini hakumkuta na kuamua kuagiza awasilishe nyaraka zake wizarani. 

Siku chache baadaye kituo hicho kiliendelea na shughuli zake za tiba, kikijitangaza kwenye vituo vya redio na televisheni na kudhamini mashindano, lakini Serikali ilitangaza kukifunga takriban wiki mbili zilizopita. 

Juzi, Dk Kigwangalla alifanya tena ziara ya kushtukiza na kukuta lundo la dawa za asili, kitu kilichomfanya aamini kuwa kituo hicho kinaendelea na shughuli zake kinyume na agizo la Serikali na hivyo kuagiza tabibu huyo akamatwe. 

Jana, Kamanda wa Polisi wa Ilala, Salum Hamdan alisema jeshi lake linaendelea kumsaka Dk Mwaka kama lilivyoagizwa na Waziri Kigwangalla. 

 “Vijana wangu wapo kazini kuhakikisha wanampata ndani ya saa 24,” alisema Kamanda Hamdan. 

“Nia ni kumfikisha mahakamani, lakini tutafanya hivyo endapo tutakuwa na ushahidi wa kutosha kuhusu madai dhidi yake, kama kudanganya umma kwa kujiita daktari, kuvaa mavazi na kutumia vifaa vinavyopaswa kutumiwa na madaktari na si waganga wa tiba mbadala. 

“Kosa jingine kama yalivyoainishwa ni pamoja na kukiuka agizo la kufungiwa na kuendelea kutoa tiba ndani ya jiji na nje kama vitabu vilivyokutwa ofisini kwake.” 

Baada ya kupata kibali cha Jeshi la Polisi juzi, Dk Kigwangalla aliingia ndani ya jengo kukagua na kukuta wateja wakiendelea kumiminika kufuata huduma, wengi wao wakiwa kina mama. 

Mara baada ya kufanya upekuzi na kukuta ndani ya jengo hilo kuna dawa, Dk Kigwangalla alizungumza na wateja hao. 

“Nimekuja kufuata huduma na hata juzi nilikuwa hapa. Taarifa kuwa kituo hiki kimefungiwa ninazo, lakini naona kila siku kwenye matangazo anayotoa kuwa bado anatoa huduma na kweli nikija hapa napata,” alisema mwanamama aliyejitambulisha kwa jina moja la Agnes na kukataa kutaja jina la pili.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images