Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

James Lembeli: Nipo Tayari Kurudi CCM

$
0
0
MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kahama, James Lembeli, ameibukia katika mkutano wa Rais, Dk. John Magufuli, huku akimwomba kiongozi huyo kuhakikisha anakisafisha Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Lembeli ambaye mwaka jana alijiengua ndani ya CCM na kujiunga na Chadema, alisema ikiwa Rais Magufuli atafanya hivyo, yuko tayari kurejea CCM.

Mwanasiasa huyo aliondoka CCM kwa kile alichodai kuwa chama hicho kimekithiri vitendo vya rushwa pamoja na unafiki miongoni mwa wanachama na viongozi wake.

Lembeli alizungumza jana mjini Kahama baada ya kuitwa kuwasalimia wananchi katika mkutano wa Rais Magufuli, ambaye anaendelea na ziara yake ya kuwashukuru Watanzania kwa kumchagua.

“Iwapo mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli  atakisafisha chama hicho basi na mimi ninaweza kurudi katika chama hicho kwa lengo la kuwahudumia wananchi,” alisema Lembeli.

Alimshukuru Rais Magufuli kufika wilayani Kahama, ambapo alisema hana kinyongo na kwamba ataendelea kusalimiana na watu mbalimbali, kwani kubadili msikiti si mwisho wa uislamu.

“Kama Rais Magufuli, atakisafisha chama hicho sina budi kurudi kundini kwani kwa sasa bado nasubiri kiongozi huyo aisafishe CCM,” alisema

Akizungumza na wananchi wa Mji wa Kahama, Rais Dk. Mgufuli, alisema yote aliyoyaahidi atayafanyia kazi na kuongeza kuwa hatalewa madaraka ya urais na kuwataka Watanzania kumtanguliza Mungu katika kazi wanazozifanya za kila siku.

“Wana Kahama tambueni kuwa Lembeli ni rafiki yangu wa siku nyingi na kuwepo kwake hapa ninategemea mabadiliko makubwa kutoka kwake na ninakushauri urudi Tanzania kwani ulikokwenda ulikuwa umepotea njia,” alisema Rais Mgufuli.

Pamoja na hali hiyo Rais Magufuli, alimtaka Lembeli, kurejea ndani ya CCM kwani chama alichokuwa nacho kwa sasa ndipo walipo mafisadi aliokuwa akiwazungumzia kila siku.

Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM taifa, alisema katika kuonesha dhamira ya kupambana na ufisadi, tayari Serikali yake imetenga Sh bilioni 2.5 kwa ajili ya kuwashughulikia mafisadi.

“Ninakuomba Lembeli urudi kundini mimi ninakujua unavyowapenda wananchi wako wa Kahama na ukirudi sita kukata mkia kwani huko ulikokwenda umepotea njia na mimi ndiyo mwenyekiti ninayewapinga wasaliti ambao asubuhi wapo CCM jioni wapo upinzani,” alisema Magufuli.

Awali akizungumza katika mkutano huo kwa niaba ya vyama vya upinzani, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Wilaya ya Kahama, Rajabu Yahaya, alimpongeza Rais Magufuli na kusema kuwa kazi inayofanywa kwa sasa na kiongozi huyo ndiyo ilikuwa ikipiganiwa na wapinzani kwa miaka yote.

Hapa chini ni maneno ya James Lembeli katika mkutano huo.

Mikojo ya walevi kutumika kutengenezea bia

$
0
0
GHENT, Ubeligiji
WATUMIAJI wa pombe sasa wataweza kupata auheni ya bei ya vinywaji hivyo, baada ya wanasayansi kugundua kifaa maalumu kitakachotumika kubadilisha mikojo ya walevi kutumika kutengenezea bia.

Kugunduliwa kwa kifaa hicho ni mkombozi kwa wamiliki wa viwanda vya pombe ambapo wataweza kupata malighafi ya kutengenezea bia kwa urais.

Kinatarajiwa kufungwa kwenye vyoo vya baa mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa mikojo hiyo ya walevi.

Kifaa hicho ambacho kitakuwa kikitumia umeme wa jua pia kitakuwa na uwezo wa kubadili mikojo hiyo kutumika kama maji ya kunywa.

Timu ya watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Ghent nchini Ubeligiji, walisema kifaa hicho kitaanza kutumika hususan maeneo ya mijini kwenye nchi zinazoendelea.

Licha ya kuwepo kwa mashine maalum yenye uwezo wa kutibu maji machafu ikiwemo mkojo kisha kutumika kwa matumizi mengine muhimu ya binaadamu, wataalamu hao wamesema kifaa hicho walichokigundua kinauwezo zaidi wa kuyatibu maji hayo bila kutumia nguvu ya umeme.

Dk. Sebastiaan Derese, alisema kifaa hicho kitakuwa kikitunza mikojo kwenye tangi maalum ambalo litatumika kutibu kisha kutumika kama malighafi ya kutengenezea bia.

Kwa mara ya kwanza kifaa hicho kilianza kutumika kwenye tamasha la muziki ililofanyika mjini humo ambapo jumla ya lita 1000 za mikojo, zilikusanywa kisha kutengenezewa bia.

Alibainisha kuwa, bia zilizotengenezwa kupitia mikojo hiyo imewavutia wanywaji wengi hususan kwenye matamasha mbalimbali.

Waziri Mkuu: Wakurugenzi Watakaotoa Taarifa Za Uongo Kufutwa Kazi

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitasita kuwaondoa katika nyadhifa zao Wakurugenzi wote watakaoshiriki katika kutoa taarifa za uongo kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Serikali inatoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ambapo  kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakiandika taarifa za uongo kuwa mradi umekamilika wakati haujajengwa, hivyo wakurugenzi watakaoshiriki kutoa taarifa zisizokuwa sahihi wataondolewa,” alisema.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana jioni (Jumapili, Julai 31, 2016) wakati akipokea taarifa ya mkoa wa Morogoro mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Alisema alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakurugenzi katika halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatembelea miradi yote inayojengwa katika maeneo yao ili kufanya ukaguzi na kujiridhisha kama thamani yake inalingana na kiasi cha fedha kilichotolewa.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amesema Serikali aihitaji Halmashauri kutoa ajira za mikataba kwenye kada zilizopo katika muundo wa ajira hivyo ameziagiza halmashauri zote nchini kufanya mapitio ya watumishi wa mikataba.

“Tumeruhusu kuajiri kwa mikataba walimu wa masomo ya sayansi kwa kipindi cha miaka miwili tena kwa waliostaafu. Kuna kada zilizoko katika muundo wa ajira hizo hatuhitaji watumishi wa mikataba wakiwemo madereva msiwatumikishe kwa mikataba watakosa stahili zao,” alisema.

Akizungumzia suala la watumishi hewa mkoani Morogoro Waziri Mkuu alisema ni vema wakaendelea kufanya uchunguzi na ifikapo mwisho wa mwezi huu wawe wamekamilisha taarifa na kuanza kuchukua hatua kwa waliohusika kwa waliohusika.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk. Stephen Kebwe katika taarifa yake aliyoiwasilisha kwa Waziri Mkuu alisema mkoa unaendelea kutekeleza agizo la Rais Dk. John Magufuli la kuzitaka taasisi zote za Serikali kufanya uhakiki wa mishahara hewa na malipo batili ya watumishi.

Alisema mkoa umebaini watumishi hewa 315 ambao wameisababishia Serikali hasara ya sh. bilioni 2.132 ambapo timu ya uhakiki bado inaendelea na zoezi hilo na taarifa kamili itatolewa mara kazi hiyo itakapo kamilika.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Wafanyabiashara Wawili Wauawa Gesti Dar es Salaam

$
0
0

Watu wawili wamekutwa wamefariki katika nyumba ya wageni ya Kings Rest House iliyopo Mtaa wa Bumila, Gongo la Mboto jijini Dar  huku miili yao ikiwa imeungua moto. 

Mmiliki wa gesti hiyo, Damian Mng’ong’o alisema alifuatwa kanisani jana saa 1.30 asubuhi na kuambiwa kuna chumba kimoja katika gesti yake kinafuka moshi na aliondoka kanisani kuelekea ilipo nyumba hiyo. 

Alisema alipofika aliona moshi bado unafuka huku nje kukiwa na umati mkubwa wa watu wakishangaa.

“Tulifanya uamuzi wa kufungua mlango lakini hatukuona mtu yeyote chumbani, ndipo mmoja wa wafanyakazi alipofungua mlango wa choo ndani ya chumba tukakuta maiti mbili zikiwa zimechomwa. "

Alisema mhudumu wa gesti alitueleza kuwa jana (juzi) saa tano asubuhi alikuja mwanamume mmoja akachukua chumba na baadaye jioni alikuja kijana mwingine wakawa wameingia wote katika chumba hicho. 

“Baada ya muda nilipiga simu polisi kuripoti tukio hilo nao waliwasili ndani ya muda mfupi wakafanya uchunguzi wao na kuhoji baadhi ya watu, baadaye wakawaleta madaktari kupima, kisha wakaondoka na maiti hizo mbili kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya hatua nyingine.” 

Mfanyakazi wa jikoni katika gesti hiyo ambaye hakupenda jina lake litajwe alisema watu hao waliofariki ni wafanyabiashara wanaouza ng’ombe katika mnada wa Pugu na mara nyingi wakija Dar es Salaam hufikia hapo. 

“Wengi wanaofanya biashara ya ng’ombe wakija hufikia hapa, mpaka sasa sijajua kilichotokea kwa hawa waliokufa, lakini tukio hili limewashtua wenzao kwani baadhi walipoona tukio hili wameingiwa na hofu na kuondoka,” alisema. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alisema wanaendelea kuchunguza na taarifa za awali hazijathibitisha kama waliuawa hapo gesti au sehemu nyingine na kupelekwa hapo. 

“Kuna viashiria kuwa huenda waliuawa wakaletwa pale kwani wana alama ya kamba katika shingo kama vile kuna mtu aliwanyonga na katika matumbo yao kuna majeraha kama wamechomwa kitu chenye ncha kali,” alisema na kuongeza: 

“Mpaka sasa uchunguzi unaendelea na Jeshi la Polisi linafanya kazi yake na tunasubiri taarifa kutoka kwa wataalamu wa masuala ya uchunguzi na alama za vidole ambayo itaeleza kwa nini wao waungue lakini nguo zao zisiungue. Pia kitanda na vitu vingine visiungue na kwa nini watu waende kuzima moto, wakati watu wameshafariki,” alisema Hamduni. 

Hamduni alisema mmoja wa waliofariki alijiandikisha kama Lameck Ludovick, mfanyabiashara na mkazi wa Dar es Salaam. 

Waziri Mkuu Aitaka Wizara Kuweka Mikakati Ya Kuendeleza Uvuvi Katika Kina Kirefu Cha Bahari

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuweka mikakati endelevu ya kuwawezesha wananchi kuvua katika maji ya kina kirefu cha bahari kwa kutumia meli kubwa na za kisasa ili Taifa liweze kunufaika na rasilimali hiyo ambayo imekuwa ikichukuliwa na wavuvi wenye vyombo vya kisasa kutoka nje ya nchi.

Aidha, amezitaka halmashauri zote nchini ziweke mikakati na mipango ya kuifanya mito na maziwa mbalimbali nchini kuwa na uvuvi endelevu kwa kufuatilia kwa karibu shughuli za wavuvi na kuwaadhibu wote watakaovua kinyume na sheria.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatatu, Agosti 01, 2016) wakati akifungua maadhimisho ya 23 ya sherehe za maonesho ya wakulima Kanda ya Mashariki katika Uwanja wa Mwalimu J.K Nyerere yanayofanyika katika mkoa wa Morogoro ambapo amesema bado nchi haijaweza kutumia rasilimali hiyo kikamilifu.

Amesema halmashauri zinatakiwa zihamasishe vijana kuunda vikundi vya kuanzisha miradi ya kufuga samaki katika maeneo yao na wewezeshwe kupata teknolojia ya ufugaji huo.

Akizungumzia vikundi vya wajasiariamali wanaovua katika maeneo ya bahari na maziwa alishauri waelimishwe kuhusu namna ya kupata mikopo ya kununulia zana bora za kisasa za uvuvi ili shughuli zao ziwe na tija.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amesema wakulima wanatakiwa  kuzingatia matumizi ya kanuni bora za kilimo ikiwemo matumizi sahihi ya zana za kisasa, pembejeo na viuatilifu vilivyopendekezwa na wataalam ili kufanikisha mapinduzi ya kilimo kuelekea kilimo cha biashara.

Akizungumzia kuhusu suala la usindikaji alisema wakati anatembelea mabanda mbalimbali alipata fursa ya kuona teknolojia zinazoweza kutumiwa na wakulima, wafugaji na wavuvi katika kuongeza uzalishaji bora wenye tija.

Amesema amefurahi kuona wakulima, wafugaji na wafanyabiashara wa mazao, pembejeo na zana za kilimo wana ari kubwa ya kushiriki katika kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo ili kwenda sambamba na kasi ya Serikali ya kuifanya nchi kujitosheleza kwa chakula na kuendeleza uchumi wa viwanda.

“Naamini kuwa pamoja na lengo la kujitosheleza kwa chakula, wakulima, wafugaji na wavuvi wataongeza ari ya uzalishaji kwa kushirikiana na sekta za umma na binafsi katika kuvipatia viwanda vyetu malighafi na kuongeza thamani ya mazao,” alisema.

Kufuatia hatua hiyo Waziri Mkuu aliziagiza halmashauri zote kuhamasisha uanzishaji na uendelezaji wa viwanda vidogo vya kusindika mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi kwa kushirikisha taasisi za umma na binafsi, mashirika na vikundi vya ujasiriamali katika maeneo yao.

Akizungumzia namna Serikali ilivyojipanga kutatua changamoto ya migogoro baina ya wafugaji na wakulima Waziri Mkuu alisema wafugaji wenye mifugo mingi watahamishiwa katika vitalu vinavyomilikiwa na ranchi za Taifa na wenye mifugo michache watatengewa maeneo katika vijiji.

Awali Waziri Mkuu alitembelea baadhi ya mabanda na maeneo ya vipando vya mazao mbali mbali yaliyoko katika viwanja hivyo ambapo alisema ameridhishwa na juhudi zilizofanyika katika maandalizi ya maonesho ya mwaka huu ikiwa ni pamoja na uendelezaji wa uwanja huo.

“Napenda kutoa pongezi za dhati kwa kujenga miundombinu na nyumba za kudumu za kufanyia maonesho. Aidha, natoa shukrani za pekee kwa Halmashauri zetu, Mashirika yetu ya Umma na binafsi; na watu binafsi ambao wamejenga na wanaendelea kujenga majengo mazuri na ya kudumu,” alisema.

Pia alizindua jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Temeke na kusema kuwa uboreshaji wa viwanja hivyo unaonesha jinsi wadau wote katika sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi na ushirika wanavyotambua umuhimu wa maonesho hayo kama njia ya kuongeza maarifa na kumuenzi mkulima, mfugaji na mvuvi kwa kutambua mchango wao katika uchumi wa Taifa.

Kauli mbiu ya maonyesho hayo kwa mwaka huu ni kilimo, mifugo na uvuvi ni nguzo ya maendeleo: vijana shiriki kikamilifu   (“HAPA KAZI TU”) 
        
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 01, 2016.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa Afungua Maonyesho Ya Nanenane Mororogoro

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva wakati alipotembelea Banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika Monyesho ya Wakulima Nane mjini Morogoro Agosti 1, 2016, Kushoto ni mkewe Mary. 

Waziri Mkuu, Kassim Majliwa na Mkewe Mary (kulia kwake)wakitazama kilimo cha mbogamboga kwa mtindo wa kilimo kichuguu wakati walipotembelea banda la Chuo Kikuucha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwenye maonyeshoya Nanenane mjini Morogoro Agosti 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakitazama viatu vilivyotengenezwa katika gereza la Karanga mkoani Kilimanjaro wakati alipotembelea banda la Magereza katika maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoroo Agosti 1, 2016, kulia ni Mratibu wa Magereza wa maonyesho hayo na Mkuu wa Gereza la Mtego wa Simba, Oman Msekwa. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (Kulia kwake) wakatazama bwawa la samaki na banda la kufugia bata wakati alipotembelea banda la Magereza katika monyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro Agosti 1, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakitazama mboga zilizokaushwa na mtambo wa kukaushia mboga hizo katika katika maonyesho ya wakulima Nanene nane mjini Morogoro Agosti 1, 2016
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizundua Banda la Maonyesho la wilaya ya Temeke kwenye maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro Agosti 1, 2016. Kushoto ni mkewe Mary.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizundua Banda la Maonyesho la wilaya ya Temeke kwenye maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro Agosti 1, 2016. Kulia kwake ni mkewe Mary na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam , Paul Makonda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama bidha mbalimbali zinazotokana na zao la mronge zikiwema, dawa, mafuta na sabuni wakati alipoembelea meza ya Bibi Salome Kaiza (kulia) kwenye banda la wilaya ya Tameke katika  maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro, Agosti, 1, 2016. Kulia kwake ni Mkewe Mary.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakitazama matikiti maji wakati walipotembelea meza ya Bwana Diocresty Theonesy kwenye banda la wilaya ya Temeke katika maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro Agost 1, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakipokezana tikiti maji wakiwa kwenye meza ya Bwana Diocresty Theonesy kwenye banda la Wilaya ya Temeke katika Maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro Agost 1, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakikagua mtama uliopandwa kwenye eneo la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika maonyesho ya wakulima Nanenane mjini Morogoro Agost 1, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Rais Magufuli Amaliza mgogoro wa makazi Magomeni Kota

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imemaliza mgogoro wa makazi wa Magomeni Kota uliodumu kwa kipindi kirefu.Hayo yamesbainishwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi wakati akiongea na Kamati ya Mgogoro wa Makazi ya Magomeni Kota mbele ya waandishi wa habari.

“Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefuta hati na mikataba yote inayohusiana na ardhi ya yaliyokuwa makazi ya Magomeni Kota, Dar es Salaam”,alisema Lukuvi.

Kwa mujibu wa Lukuvi Rais ameondoa umiliki wa eneo hilo toka Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na kumilikisha Serikali Kuu ambayo ndiyo itakayosimamia ujenzi wa nyumba 644 ambazo zitauzwa kwa bei nafuu kwa waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota.

“Tutajenga nyumba 644 na kuwauzia kwa bei ya jengo na siyo ya ardhi ili kuwapeni unafuu katika kununua,”alisema Lukuvi huku akishangiliwa na baadhi ya wakazi wa Magomeni.

Aidha, Lukuvi amesema kuwa anampongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kumaliza mgogoro huu ambao umedumu kwa muda mrefu na kuongeza kuwa ameagiza timu ya wataalamu wa Wizara kupima na kuchora michoro kwa ajili ya ujenzi.

Lukuvi amesema katika eneo hilo zitajengwa nyumba za heshima ambazo kila moja itakuwa na vyumba vitatu ili kukidhi mahitaji ya kifamilia kwani watu hawa wamekaa kwa miaka takribani 50 hadi wameshapata wajukuu. Ameongeza kuwa kila mmiliki wa nyumba hiyo atapewa hati yake hata kama nyumba hiyo itakuwa kwenye ghorofa.

Lukuvi amesema kuwa Rais ameagiza maeneo kama ya Magomeni Kota katika mikoa ishirini ya Tanzania Bara nayo yatakuwa katika mfumo huo wa Magomeni. Kwa mujibu wa Lukuvi wazee ambao wanakaa kwenye nyumba kama hizo sehemu nyingine wasiondolewe kwani hao walikuwa watumishi wa umma hivyo Rais amesema wasibughudhiwe.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Mgogoro wa Makazi Magomeni Kota, George Abel ameshukur Mhe Rais Magufuli na Wazir Lukuvi kwa kutatua mgogoro huo ambao anadai umewasumbua sana.

Ameahidi kutoa ushirikiana kwa Serikali pindi suala la ujenzi litakapokuwa linaendelea ili kuhakikishaujenzi unaenda haraka.Naye Wakili ambaye alikuwa akiendesha kesi hiyo kabla ya Mhe. Rais kuingilia kati, Mhe. Twaha Tasilima ameonyesha kuridhishwa na utendaji wa Rais Magufuli.

“Rais Dkt Magufuli na Mhe. Waziri Lukuvi ni watu wa vitendo na si maneno na kweli wanawajali wanyonge, nawashukuru sana,”alisema Tasilima.

Uamuzi wa kurudisha eneo hilo kwenye Serikali Kuu umetolewa na Rais Magufuli tarehe 10/7/ 2016.

Rais Magufuli Ahitimisha Ziara Ya Siku Nne Mikoa Ya Singida, Tabora Na Shinyanga

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akihutubia wananchi wa Katoro na Buseresere wakati akielekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Agosti 1, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Mdini Mhe. Dkt Medard Kalemani baada ya kuhutubia wananchi wa Katoro na Buseresere wakati akielekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Agosti 1, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na madiwani na viongozi wa Katoro na Buseresere baada ya kuhutubia wananchi wakati akielekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Agosti 1, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimsabahi mtoto Shabani Kalemani (miezi 8) na mama yake Asha Simon baada ya kuhutubia wananchi wa Katoro na Buseresere wakati akielekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Agosti 1, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa kwa furaha kijijini Bwanga wakati akielekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Agosti 1, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia wananchi kijijini Bwanga wakati akielekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Agosti 1, 2016

Mrema akutana na Madereva Bodaboda wa Kinondoni........Awataka wampe majina ya polisi wanaowalazimisha kutoa rushwa

$
0
0
Mwenyekiti wa Parole Augustino Mrema amewataka madereva bodaboda kote nchini kujiepusha na tabia za kushiriki maandamano ya kisiasa yanayoandiwa na baadhi ya wanasiasa kwa lengo la kuvunja sheria za nchi.

Pia amewaagiza waendesha bodoboda Kinondoni wampe majina ya polisi wanaowalazimisha kutoa rushwa ili ayakabidhi kwa rais Magufuli
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole Mhe. Augustine Mrema ( Mwenye Kofia Katikati) akisisitiza jambo kwa madereva wa pikipiki toka Wilaya ya kinondoni wakati alipokutana nao ili kusikiliza kero mbalimbali wanazokutana nazo wakiwa katika kazi zao mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Madereva wa pikpiki Wilaya ya Kinondoni Bw. Almano Mdede akifafanua jambo kwa madereva pikipiki wa Wilaya ya Kinondoni wa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole Mhe. Augustine Mrema (katikati) alipowatembelea madereva hao na kusikiliza kero mbalimbali wanazokutana nazo wakiwa katika kazi zao mapema hii leo jijini Dar es Salaam,kushoto ni Katibu wa Madereva Pikipiki Wilaya hiyo Bw. George Mbwale.
Baadhi ya madereva Pikipiki wa Wilaya ya Kinondoni wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole Mhe. Augustine Mrema (hayupo pichani) alipokutana nao ili kusikiliza kero mbalimbali wanazokutana nazo wakiwa katika kazi zao mapema hii leo jijini Dar es Salaam. Picha zote na Eliphace Marwa -Maelezo

Taarifa Toka Ikulu: Rais Magufuli Katoa Maagizo Mazito Kwa Viongozi Wote Hapa Nchini........Pia Katoa Onyo Kali Kwa Walimu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaagiza viongozi wote wa kuanzia ngazi ya Mkoa hadi Kitongoji hapa nchini kufuatilia matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutoa elimu bila malipo kwa lengo la kudhibiti mianya ya matumizi mabaya ya fedha hizo.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo tarehe 01 Agosti, 2016 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Mnadani na kuwajumuisha wananchi wa Katoro na Buseresere Mkoani Geita.

Katika agizo hilo Dkt. Magufuli amewaonya walimu ambao wameanza kufanya udanganyifu kwa kuandikisha idadi kubwa ya wanafunzi kuliko idadi halisi kwa lengo la kupata mgao mkubwa wa fedha za ruzuku na amesema Serikali itachukua hatua kali dhidi ya yeyote atakayebainika kufanya hivyo.

"Ninafahamu mgao wa fedha hizo hutolewa kulingana na idadi ya wanafunzi waliopo, wapo baadhi ya walimu ambao wameanza kuandika wanafunzi hewa katika shule zao, ili kusudi aletewe hela nyingi kuliko idadi ya wanafunzi waliopo, wanafunzi kama wapo laki nne yeye anasema shule yangu hii ina wanafunzi laki tano, ili kusudi hela zikija za wanafunzi laki tano, za wanafunzi laki moja wagawane.

"Napenda nitoe wito kwa walimu Tanzania nzima, mnatafuta matatizo, narudia mnatafuta matatizo, msijaribu kula hela ya Serikali" Amesema Rais Magufuli.

Pamoja na agizo hilo, Rais Magufuli pia ametaka viongozi wa ngazi zote katika Mikoa kuhakikisha wana takwimu za idadi ya wanafunzi katika shule zote zilizopo katika maeneo yao ili kurahisisha ufuatiliaji wa fedha hizo na amesema kuwa kuanzia sasa ataanza kutembelea shule kwa kushitukiza na kwamba kiongozi atakayeonekana kutojua takwimu itakuwa ni uthibitisho kuwa hatoshi kuendelea na wadhifa alionao.

"Na nitoe wito kwa viongozi wa Mikoa, Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Makatibu Tarafa, Watendaji wa Kata, Wenyeviti wa Vijiji, kila mmoja awe na idadi ya wanafunzi waliopo katika shule zao, hatutaki kuwapunja wanafunzi hela ambayo wanatakiwa kupata, lakini pia hatutaki kutoa hela ambayo haitakiwi" Amesisitiza Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ambaye ametumia mkutano huo kueleza juhudi mbalimbali zilizofanywa na Serikali yake ya Awamu ya Tano, kutekeleza ahadi yake ya kujenga Tanzania Mpya pia amewataka viongozi na watendaji wa Serikali kutekeleza wajibu wao kwa kutembelea wananchi wanaowaongoza badala ya kukaa muda mwingi ofisini huku akisisitiza ofisi hizo kuwepo katika maeneo yenye shughuli husika.

Aidha, Dkt. Magufuli amekosoa utaratibu unaotumiwa na Halmashauri nyingi za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya kutumia mawakala katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri akisema mawakala hao wamekuwa wakitumia utaratibu huo kukusanya fedha nyingi na kisha kuwasilisha kiasi kidogo katika Halmashauri husika.

"Hivi kwa nini Halmashauri msingekuwa na maafisa wenu wazuri na mkawa na mashine za kielektroni kwa ajili ya kukusanya fedha? Amehoji Dkt. Magufuli na kuongeza kuwa;

"Tena mawakala wengine ndio hao hao wamekuwa wakikusanya kodi hata kwa wananchi wanyonge wenye vibiashara vidogo vya kuuza mchicha bila hata kuwaonea huruma"

Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amemaliza ziara yake ya siku nne katika Mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Geita na yupo nyumbani kwake Chato Mkoani Geita kwa mapumziko mafupi.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Chato

01 Agosti, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Agosti 2

Ugonjwa wa Sumukuvu Wahatarisha Maisha Nchini........Umeua Watu 14 Mpaka sasa Huku 54 Wakiwa Wanaugua Ugonjwa Huo

$
0
0

Watu 14 wamefariki dunia katika wilaya za Chemba mkoani Dodoma na Kiteto mkoani Manyara kutokana na ugonjwa unaojulikana kitaalamu kama ‘Aflatoxicosis’ unaosababishwa na sumu kuvu (Aflatoxins) kwenye nafaka iliyoharibika.

Hayo yamesema na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya magonjwa ya milipuko na magonjwa mengine leo jijini Dar es Salaam.

“Ugonjwa uliosababishwa na sumu kuvu (Aflatoxins) uliripotiwa kwa mara ya kwanza tarehe 13 Juni, 2016 katika wilaya za Chemba mkoani Dodoma na baadaye mkoani Manyara katika wilaya ya Kiteteo” alisema Waziri Ummy na kuongeza kuwa:

“Wagonjwa walikuwa na dalili za kuumwa tumbo, kuharisha, kutapika, tumbo kuvimba na kuwa manjano sehemu mbalimbali za mwili ambayo inaashiria kuathirika kwa ini”

Alisema mbali na vifo hivyo, hadi kufikia Julai 31 mwaka huu wagonjwa 54 waliripotiwa kuugua ugonjwa hu huku wagonjwa wanne wakilazwa kutokana na kuugua.

“Hadi kufikia tarehe 31, July 2016 kulikuwa na wagonjwa 54 na watu 14 walipoteza maisha kutokana na ugonjwa huo.Aidha katika wiki iliyopita aliripotiwa mgonjwa mmoja mpya kutoka wilaya ya Kondoa” alisema Waziri Ummy na kufafanua kuwa:

“Jumla ya wagonjwa waliolazwa wodini ni wanne kati yao mmoja yupo Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na watatu wapo katika Hospitali ya Kondoa”

Waziri Ummy alitaja wilaya zilizoripoti wagonjwa hao na idadi ya wagonjwa kuwa ni wilaya ya Chemba wagonjwa 38, Kondoa wagonjwa tisa , Kiteto wagonjwa watatu, Chamwino wagonjwa wawili na Dodoma Manispaa  mgonjwa mmoja.

“Vijiji vilivyoathirika zaidi na ugonjwa huo ni kutoka wilaya ya Chemba ambavyo ni Kinkima, Itolwa, Mwailanje na katika wilaya ya Kondoa ni kijijini cha Ubembeni” alisema Waziri Ummy.

Hivyo, aliitoa hofu familia iliyopoteza watu wanne katika kijiji cha Mwaikuzabe na kusema vifo hivyo havihusiani na uchawi au kuwekewa sumu bali ni chakula cha siku ile kilithibitika kwamba kilikuwa na sumukuvu.

Kufuatia athari hizo Serikali itafanya uchunguzi wa kina katika wilaya kumi  za Chemba, Kondoa, Chamwino na Kiteto na wilaya nyingine za mikoa ya Sindida, Dodoma na Manyara zinazopakana na wilaya hizo.

Alisema uchunguzi huo unalenga kubaini hali ya usalama wa vyakula vinavyotumiwa na jamii ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo na kuwaathiri wananchi wengi zaidi wanaoishi katika wilaya hizo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taifa wa Afya wa Wizara hiyo Dkt. Fausta Mosha alisema wizara imeandaa  vipepereshi vyenye maelekezo yanayotoa elimu juu ya kijikinga kwa kuandaa chakula kuanzia hatua ya uvunaji shambani hadi wakati wa kula.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Otilia Gowelle alisema njia bora ya kupambana na ugonjwa huo ni kuukinga kwa kuhakikisha sumu kuvu haizalishwi kutoka kwenye nafaka.

Akifafanua kuhusu udhibiti, Waziri Ummy alisema wanashirikiana na Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi kutoa elimu kwa wananchi juu ya njia sahihi ya uhifadhi na uandaaji wa chakula utakaosaidia kupunguza kiasi cha sumukuvu kwa nafaka ambazo hazijaharibika sana.

“Njia hizi ni pamoja na kuhifadhi nafaka zilizokauka vizuri na kuchambua nafaka zilizoharibika (zilizooza, kuvunjika, zilizobadilika rangi), kukoboa mahindi kabla ya kusaga au kuacha kutumia nafaka zitakazoonekana kuharibika rangi” alisema.

Waziri Ummy alisisitiza Serikali kuendelea kuimarisha mikakati ya kitaifa ya kupunguza uchafuzi wa sumukuvu katika vyakula, ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo wa kupima sumukuvu katika damu na choo kidogo miongoni mwa taasisi za ndani ya nchi.

Inaelezwa kuwa ugojwa wa‘Aflatoxicosis’unaosababishwa na sumu kuvu (Aflatoxins) kwenye nafaka uliwahi kutokea nchini Kenya mwaka 2004 na kusababisha vifo vya zaida ya watu 100 huku wengine 200 waliathirika.

Dereva Ajali ya City Boy Iliyoua watu 30 Ajisalimisha Polisi

$
0
0
MMOJA wa madereva waliosababisha ajali ya mabasi ya Kampuni ya City Boy iliyotokea Julai 4, mwaka huu na kutoroka, Boniface Mwakalukwa (37), amejisalimisha mikononi mwa polisi na kufikishwa mahakamani.

Mwakalukwa ambaye ni mkazi wa jijini Dar es Salaam jana aliunganishwa kwenye mashitaka na dereva mwenzake Jeremiah Semfungwe (34) wote kwa pamoja wakikabiliwa na makosa 30 ya kuua bila kukusudia.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Singida, Joyce Minde ilidaiwa kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo Julai 4, mwaka huu saa 8.15 mchana wakati wakiendesha mabasi aina ya Scania yenye namba za usajili T 247 BCD na T 331 DCE kwa kuyagonganisha.

Ilidaiwa kuwa kitendo hicho ambacho kilitokea Kijiji cha Maweni wilayani Manyoni kilisababisha vifo vya abiria 30 na majeruhi 54. Wakili wa Serikali, Petrida Muta alidai kuwa siku ya tukio watuhumiwa wakiwa ni madereva wa Kampuni ya City Boys, bila kukusudia, walisababisha vifo vya abiria hao kinyume na Kifungu 195 na 198 cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 Toleo la Kwanza.

Ingawa Wakili wa washitakiwa, Francis Kitope aliiomba Mahakama iwape wateja wake dhamana kwa kuwa chini ya Kifungu 148 cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai, kosa hilo linadhaminika, Wakili wa Serikali Muta alipinga dhamana hiyo.

Muta ambaye aliwasilisha Hati ya Kiapo mbele ya Mahakama hiyo, alidai kuwa kwa kufanya hivyo usalama wa washitakiwa utakuwa hatarini kwa kuwa ndugu wa marehemu na majeruhi bado wana hasira kutokana na ajali hiyo kuwa bado haijasahaulika.

Aidha, Muta aliendelea kudai kuwa baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo hali zao bado ni mbaya na hatma yao haijulikani, hivyo si vyema washitakiwa kupewa dhamana wakati huu. Kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika, washitakiwa wamerejeshwa rumande hadi Agosti 4, mwaka huu kesi yao itakapotajwa tena.

Wafungwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kumbaka Mama Mbele ya Mumewe na Watoto

$
0
0
MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya imewahukumu kutumikia kifungo cha maisha jela vijana wawili wakazi wa wilayani Chunya mkoani humo kutokana na kosa la ubakaji wa mwanamke mmoja waliyemtendea kitendo hicho mbele ya watoto wake.

Kadhalika, mahakama hiyo imewahukumu vijana hao wawili kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kutokana na kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha ambapo siku ya tukio walimjeruhi mume wa mwanamke waliyembaka.

Vijana waliokumbwa na vifungo hivyo viwili kutokana na mashitaka mawili yaliyokuwa yakiwakabili ni Ngaru Joseph (32) na Pili Mneme Kapigi (30) wote wakiwa ni wakazi wa wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Awali ilielezwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi Mazoya Luchagula, Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Alice Mkasela kuwa mnamo Julai 10, mwaka huu saa nane usiku nyumbani kwa mlalamikaji katika Kijiji cha Ukwavila wilayani Mbarali washitakiwa walivamia na kuvunja mlango nyumba ya mkazi huyo aliyekuwa amelala na mke na watoto wao.

Luchagula alisema walipofanikiwa kuingia ndani ya nyumba hiyo washitakiwa hao walimjeruhi baba wa familia kwa kumkata na shoka kichwani kisha wakapora fedha kiasi cha Sh 580,000, wakachukua nguo zote za wanafamilia na kisha kumbaka mama wa familia mbele ya mumewe na watoto.

Mwendesha mashitaka huyo alisema wanafamilia hao kupitia mwanga wa taa ya sola waliweza kuwatambua watuhumiwa kabla wazazi hawajapelekwa Hospitali ya Misheni Chimala walikolazwa kwa ajili ya matibabu.

Kutokana na makosa hayo Luchagula aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine walio na tabia hizo wilayani hapa na kwingineko nchini.

Akito adhabu kwa washitakiwa, Hakimu Mkasela alisema ameridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na pande zote mbili na kwamba kwa kosa la kwanza la unyangaji wa kutumia silaha washitakiwa watakapaswa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela na kwa kosa la pili la ubakaji watatumikia kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho kwao na watu wengine.

Awali washitakiwa waliiomba Mahakama kuwapunguzia adhabu wakisema bado umri wao ni mdogo na wanategemewa na familia zao, maombi ambayo yalitupiliwa mbali na hakimu Mkasela.

Bilionea wa Chadema Mustapha Jaffer Sabodo Akitosa Chama Hicho.........Aahidi Kutoa Trilioni 10 za Kuwekeza Dodoma ili Kumuunga Mkono Rais Magufuli

$
0
0
MFANYABIASHARA maarufu, Mustapha Jaffer Sabodo ametangaza kutoa dola za Marekani bilioni 5 (Sh trilioni 10) kwa ajili ya kuwekeza mkoani Dodoma, ikiwa ni njia ya kumuunga mkono Rais John Magufuli kuhamisha makao makuu ya serikali kwenda mkoani humo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Sabodo alisema atawekeza kiasi hicho cha fedha, iwapo serikali yote itahamia mkoani humo, itakuwa ametimiza ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye alitamani kuona mkoa huo unakuwa makao makuu ya nchi.

Alisema alichofanya Rais Magufuli, kimewashinda marais wengine waliomtangulia, hivyo yeye kama mfanyabiashara na mtu mwenye mapenzi makubwa kwa nchi yake, lazima aunge mkono hatua hiyo ya Serikali kuhamia Dodoma ambayo aliita ‘Azimio la Dodoma’.

“Niliposikia anatangaza kwenye televisheni ya taifa kwamba Serikali itahamia Dodoma, ilikuwa mara yangu ya kwanza baada ya miaka mingi kupita, nilitabasamu moyoni, jambo ambalo lilinitokea miaka 10 ya kwanza ya uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere. 

“Leo nimesikia kutoka kwako nimeona ile roho ya Nyerere imezaliwa tena. 

“Kwa hiyo natangaza kuunga mkono Azimo la Dodoma kwa kuwekeza dola za Marekani bilioni 5, ambazo zitatumika kwa ajili ya uwekezaji mkubwa katika huduma mbalimbali za jamii mkoani humo,” alisema Sabodo.

Sabodo alisema atatoa fedha hizo ili zitumike kuwekeza kwenye viwanda kama vya mvinyo, viwanda vya kusindika mihogo na viwanda vingine ambavyo vitahitajika katika mkoa huo.

Alisema kuwepo kwa huduma hizo mkoani Dodoma, kutasaidia kuufanya mji huo kukidhi matakwa ya watumishi wa umma watakaohamia huko.

Mfanyabiashara huyo aliongeza kuwa atafanya uwekezaji mkubwa huo kwa sababu lengo lake ni kuona mji wa Dodoma, unaungana na miji ya jirani kama Mpwapwa, Kondoa na Manyoni ili kutoa fursa ya kupanua huduma mbalimbali katika makao makuu hayo ya nchi.

Sabodo alisema kwamba juhudi zake za kuwekeza katika huduma za jamii kama shule, pia ataziendeleza katika mkoa huo kwa kuhakikisha kwamba zinajengwa shule kadhaa za kisasa, ambazo zitamudu mahitaji ya watu wa eneo hilo.

Kwa upande wa huduma ya afya, Sabodo alisema atatumia umaarufu wake kuwashawishi wamiliki wa Hospitali ya kimataifa ya Apollo ya India ili waje nchini wakashirikiane naye kujenga hospitali ya kisasa, ambayo itakuwa inatoa huduma za kisasa mkoani humo.

“Mnaifahamu hospitali ya Apollo ni wawekezaji wakubwa katika huduma za afya, kwa kusukumwa na hatua hii ya Rais nitaongea nao tushirikiane katika kujenga huduma za jamii katika mji huo,” alisema Sabodo.

Pia alisema atawashawishi wawekezaji wengine kutoka nchi za India, Singapore na kwingineko kuja kuwekeza katika mji huo wa Dodoma katika sekta ya viwanda, kuhakikisha kwamba azma ya Rais Magufuli ya kujenga uchumi wa viwanda inatimia.

Sabodo ambaye alisema wazi kuwa utendaji wa Rais Magufuli, umemvutia kutokana na hatua yake ya kupiga vita rushwa, alitangaza kuwa kuanzia sasa hatatoa tena msaada kwa vyama vya upinzani kama ambavyo amefanya miaka ya nyuma kama njia ya kuimarisha demokrasia nchini.

“Huko nyuma nilikuwa nawapa Chadema fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kuimarisha demokrasia, sasa natangaza tena kwamba sitawapa tena fedha, niwape za nini wakati Rais aliyeko madarakani anafanya kazi ambayo ndio nilikuwa naipigania?"  alihoji Sabodo.

Sabodo ni mfanyabiashara wa kitanzania mwenye asili ya Kihindi ambaye alizaliwa mkoani Lindi. Katika maisha yake amekuwa anafanya biashara katika nchi za Kenya, Ufaransa, India, Sudan na Zimbabwe.

Pamoja na biashara zake, Sabodo amekuwa anajihusisha kuchangia katika miradi ya maendeleo ya huduma za jamii, uimarishaji wa demokrasia nchini na pia alishiriki kutunisha mfuko wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa kuanzisha bahati nasibu.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 5 & 6

$
0
0

 Mtunzi: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
 “Samahani kaka sijui wewe ni nani mwenzangu?”
“Unaniuliza mimi ni nani ndani ya nyumba yangu?”
Moyo ukanipiga paaaa kama jiwe lililotua juu ya bati tena la nyumba ya uswahilini.Nikajua jamaa anaweza akawa mume wa Madam Mery mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio pale jamaa alipoanza kupiga hatua za kwenda chumbani kwa Madam Mery kwani boxer na tisheti ya shule vyote vipo ndani ya chumba hicho na vipo sehemu ya wazi kwa mtu yoyote anayeingia lazima ataviona,na kingine kilichozidi kunipagawisha ni kitanda nilivyo kiacha kimevurugika kwani kinaonyesha hivi hivi kilikuwa ni kiwanja cha mechi za wakubwa

ENDELEA
    Jamaa kabla hajafunua pazia ili aingie ndani simu yake ikaita.Akaitoa kwenye mfuko wa suruali kisha akaipokea na kuanza kuzungumza mazungumzo ambayo yalianza na ndio bosi.Jamaa akanitazama kisha akatoka nje nikahisi mazungumzo yake ni muhimu sana na ya siri sana ndio maana akatoka nje huku begi lake akilivua na kuliweka pembeni ya mlango wa kuingilia chumbani kwa Madam Mery.

Ikawa nafasi kwangu kuingia chumbani nikachukua kila kilicho changu huku shuka lililo changungaka nikilitoa na kulisokomeza mvunguni mwa kitanda na kuliacha godoro likiwa na foronya yake tu pasipo kuwa na shuka,Nikarudi hadi sebleni na kumuona jamaa akirudi ndani kwani mlango aliuacha wazi kidogo.Ikanibidi boxer yangu niiweke mfukoni mwa suruali yangu huku tishet yangu nikiwa nimeishika mkononi huku nikitaka kuivaa

“Dogo unakwenda wapi?”
“Ehee”
”Hujasikia…! Unakwenda wapi?”
“Kununua vitafunio vya chai”
“Dogo mbona unajifanya mjanja sana?”
Maswali ya jamaa yakazidi kunichanganya akili na kunizidisia presha ambayo sikuelewa kama inapanda au inashuka.
“Mjanja wa nini brother?”
“Huendi kununua vitafunio ila sema ninakwenda kununua vitafunwa kwani vitafunio ni hayo meno yako”
“Sawa bro nimekuelewa”
“Ehee kwanza hujaniambia wewe ni nani? Nakuona upo upo tu humu ndani?”

“Mimi ninaitwa Eddy”
“Yuko wapi Mery?”
Nkaanza kufikiria cha kumjibu huku maswali mengine nikijiuliza mwenyewe na kujijibu mwenyewe ndani ya moyo wangu hadi nikapata muafaka wa nijibu nini
“Amelazwa kwenye hospitali ya shule”
“Lini?”
“Leo asubuhi”
Lengo la kumjibu jamaa kiufasaha kila swali analo niuliza ni ili akienda kumuangalia Madam Mery iwe nafasi ya mimi kuondoka katika nyumba hiyo ili nikatafute hata sehemu ya kuishi nikisubiria siku zangu za kusimamishwa masomo ziishe

“Powa dogo vaa tisheti yako unipeleke huku alipolazwa”
Sikuwa na ujanja zaidi ya kuivaa tisheti yangu na kumalizia kuvaa viatu vyangu na kitu kilichozidi kuniweka mpole mbele ya jamaa ni pale alipoitoa bastola yake na kutazama kama inarisasi za kutosha kwenye magazine yake na kuirudisha kiunoni bastola yake huku akionekena kuridhika na risasi zilizomo.

Safari ikaanza huku sote tukiwa kimya ila mimi nimetangulia mbele kama hatua moja huku yeye akifwatia kwa nyuma.Akili yangu ikawa inanituma nipige hatua za haraka haraka na kama kuna uwezekano nikimbie kwani vichochoro vyote ninavijua katika mji huu wa Arusha
“Dogo nasikia kuna majambazi sana wamezuka kipindi cha hivi karibuni?”

“Kusema ukweli bro mimi mwenyewe ninasikia sikia ila sina uhakika kivile.Ila ni juzi kuna benki pale mbele ilivamiwa na pesa zote zikaibiwa”
“Dogo subiri ninunue P.K hapa dukani si utakula?”
“Ndio”

Jamaa akaingia kwenye moja ya duka,nikamchungulia kwenye duka hilo nikamuona yupo bize na muuza duka.Nikaanza kupiga hatua za taratibu huku nikizuga zuga watu waliopo katika eneo hilo wasistukie kitu chochote ili nikifika mbali na duka hilo nianze kukimbia.Kabla sijafika mbali kidogo gafla nikastukia nikiguswa bega kwa nyuma.Nikageuka na kukutana na muuza mahindi
“Oya broo yule jamaa pale mjeda ameniambia nikuletee maindi uchague”

Nikatamani nimtukane muuzaji wa watu ila nikaona hana kosa taratibu nikaanza kuyatazama mahindi yaliyo chomekwa kwenye spoke za baiskeli zipatazo kumi na kuunganishwa katika mti mmoja.Nikachagua muhindi laini laini kwani sikuwa nimekula kitu cha aina yoyote tangu asubuhi.Jamaa akaja hadi tulipo akatoa noti ya elfu kumi na kumpa muuza maindi na kumuambia chenchi akae nayo
“Aisee kamanda wangu Mungu akubariki sana”

Muuza maidi alizungumza kwa lafudhi ya kichaga huku akipiga saluti na kumfanya jamaa acheke ila mimi sikuwa na hata hamu ya kuyakenua meno yangu.Tukaendelea na safari ya kwenda katika hospitali ya shule ambayo haikuwa mbali sana na shule kwani ilikuwa pia inatoa msaada wa kuwahudumia wananchi wa kawaida tofauti na wanafunzi

Tukafika hospitalini na tukakutana na Madam Rukia akiwa nje ya wodi ya wagonjwa,nikamsalimia nikabaki nikiwatazama jinsi  anavyo salimiana na jamaa huku wakicheka kwa furaha na kuonekana wakifahamiana kwa muda mrefu
“Huyo mwenzako anaendeleaje?”
“Kidogo joto lake limeshuka kwani asubuhi hali yake haikuwa nzuri kivile”
“Tatizo lake ni nini haswa?”

“Maleria alikutwa na vidudu sita ndio vimemlaza.”
“Sasa mbona umekaa huku nje?”
“Nilitoka mara moja kupunga punga hewa ila twende ukamuone”
Wakati wote wanazungumza nilikuwa kimya nimetulia kama maji ya mtungini huku moyoni nikifurahia jamaa aingie ndani na mimi niondoke .Jamaa na Madam Rukia wakaanza kuingia ila jamaa akasimama na kuniangalia
“Oya dogo twende ukamuangalie mgonjwa”

“Huyu mwalifu umemtoa wapi?”
Madam Rukia alimuuliza jamaa na kumfanya atabasamu ila kwangu nikazidi kuogopa,cha kumshukuru Mungu jamaa hakulijibu swali la Madam Rukia kwani tayari tulishafika ndani ya chumba alicholazwa Madam Mery.Jamaa akakaa kitandani na kumkumbatia madam na wote kwa pamoja wakawa wanatokwa na machozi ya furaha,sikujua kinacho waliza ni nini

Wakaachiana huku jamaa akianza kumfuta Madam Mery machozi kwa kutumia kitambaa chake na kunifanya roho yangu kuanza kuhisi maumivu ya wivu 

==>Endelea Nayo <<Kwa Kubofya Hapa>>

Goodbless Lema Amvaa Mkuu wa Wilaya Mbele ya Naibu Waziri Suleiman Jaffo

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Goodbless Lema amemvaa Mkuu wa wilaya hiyo, Mrisho Gambo mbele Naibu Waziri Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo akidai anaingilia shughuli za halmashauri kinyume na taratibu.

Lema alimtuhumu Gambo kutoheshimu mipaka yake ya kiutawala kwa kuingilia maamuzi ambayo yamejadiliwa kwenye vikao halali vya halmashauri na kupitishwa na ofisi ya mkuu wa mkoa katika kikao cha wakuu wa idara, maofisa tarafa, waratibu wa elimu kata watumishi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (Auwsa).

“Nimeona nizungumze hapahapa ili naibu waziri ufahamu hali ilivyo hapa. Kwa mfano, Baraza la Madiwani lililopita ndilo lililopitisha kiwango cha posho kwa madiwani kutoka Sh100,000 hadi Sh120,000, jambo la kushangaza DC ameandika barua Tamisemi na nakala kwa Takukuru ili wachunguze jambo ambalo limeshapata baraka za Tamisemi,” alisema Lema.

Alisema pia amekuwa akiingilia utendaji wa watumishi wa halmashauri kwa kuingilia upangaji wa vibanda vya wafanyabiashara kupitia madalali na kusababisha usumbufu.

Lema aliongeza kuwa Gambo pia amekuwa akitaka uwanja ulionunuliwa na mfanyabiashara urudishwe Jiji wakati kesi imempa uhalali aliyenunua kuchukua eneo hilo.

Hali hiyo ilimfanya naibu waziri kuingilia kati na kuahidi kuzishughulikia changamoto hizo na kumpa nafasi Gambo kujibu madai ya Lema ambayo aliyakanusha, likiwamo la kuingilia utendaji kazi wa mamlaka ya maji.

“Mheshimiwa mbunge nataka ujue mimi ndiyo mkuu wa shughuli za Serikali hapa wilayani, muda wowote nina uwezo wa kuingilia kati mambo ambayo naona hayaendi sawa hata kama yupo katibu tawala na viongozi wengine.

"Rais aliona ninafaa, ndiyo maana akaniteua na sihitaji kujifunza namna ya kuwa mkuu wa wilaya, huu ni mwaka tano,” alisema.

Alisema hakuna siasa kwenye maendeleo ya wananchi na kumtaka mbunge atambue kuwa kuhudumia wananchi hakuhitaji maamuzi ya Baraza la Madiwani pekee, kwani kumekuwa na tabia ya kutumia fedha za halmashauri vibaya kulipana posho ambazo hazipo kwa mujibu sheria na kanuni.

Alisema alilazimika kutaka viongozi walio chini yake kupitia hukumu iliyompa mfanyabiashara eneo la Kilombero kama ni halali na kushangazwa na Lema kupinga.

Akizungumzia suala hilo, Jaffo alimtaka Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega kushughulikia changamoto hizo akisema muda wa siasa umepita na wananchi wanahitaji maendeleo.

Pia, alisema Serikali ipo mbioni kuwahamisha watumishi wa halmashauri ya jiji wanaofanya kazi kwa mazoea na kumwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Athuman Kihamia kusimamia wafanyakazi wanaofanya kazi kwa mazoea huku wananchi wakipata shida.

Mzee jela miaka 15 kwa kumiliki silaha Kinyume cha Sheria

$
0
0

Mkazi mmoja wa jijini hapa, Said Shomari (64) amehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumiliki silaha kinyume cha sheria. 

Shomari ambaye ni fundi saa, alitiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu hiyo na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo baada ya mshtakiwa kukiri kosa hilo. 

Alikiri kutenda kosa hilo jana alipopandishwa kizimbani mahakamani hapo na Wakili wa Serikali Adolf Mkini kumsomea mashtaka yaliyokuwa yakimkabili kwa lengo la kumkumbusha, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya usikilizwaji. 

Katika kesi hiyo, Shomari alishtakiwa na mtoto wake, mfanyabiashara Ramadhani Said (40), kwa makosa mawili, moja la kukutwa na silaha na la pili la kukutwa na risasi bila kibali na kinyume cha sheria. 

Katika mashtaka hayo, Shomari alikiri kosa moja la kumiliki silaha na akakana kosa la kumiliki risasi kinyume cha sheria. 

Hata hivyo, wakati Shomari akikiri kutenda kosa hilo moja na kuhukumiwa adhabu hiyo, mtoto wake alikana kutenda makosa hayo yote. 

Awali, akiwasomea mashtaka hayo, Wakili Mkini alidai kuwa Novemba 9, 2015, eneo la Kigogo, wilayani Ilala, mshtakiwa alikutwa akimiliki bastola moja ndogo pamoja na risasi moja bila kuwa na kibali. 

Baada ya kusomewa mashtaka hayo na kuulizwa kama ni kweli au si kweli, ndipo alipokiri kutenda kosa hilo kwa kujibu kuwa ni kweli, hivyo Mahakama ikamtia hatiani. 

“Kwa kuwa mshtakiwa amekiri kutenda kosa kwa shtaka linalomkabili, Mahakama inamtia hatiani na kumhukumu adhabu ya kifungo cha miaka 15 jela.”, alisema hakimu Mashauri. 

Baada ya kutoa hukumu hiyo aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 15, mwaka huu, wakati kesi hiyo itakapoendelea kusikilizwa shtaka moja kwa upande wa Shomari na mashtaka yote mawili kwa upande wa Ramadhani. 

Mrema amtaka Lowassa akubali kwamba alishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana

$
0
0

Mwenyekiti wa Bodi ya Parole ambaye pia ni Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema amemtaka Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa akubali kwamba alishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na akae kimya hadi mwaka 2020.

Mrema aliyasema hayo jana Jijini Dar es Salaam na kusisitiza kwamba alimtaka Waziri Mkuu Mstaafu watoke CCM pamoja kwa kuwa nguvu ya upinzani ilikuwa kubwa sana.

‘’Mimi nitamuuliza 1995 wakati natoka nilikuambia tutoke sasa maji yamechemka tukiweka unga tutakula ugali ukagoma, ukasema unaendelea kula kidogo hadi alipojiuzulu akaendelea na CCM hadi alipotaka kugombea Urais akakataliwa na wenzake ndipo akaja upinzani’’

Mrema aliongeza kwamba Chama cha Mapinduzi kilitakiwa kuondoka madarakani mwaka 1995 ambapo yeye ndiye alikuwa na nguvu kubwa ya kisiasa nchini.

Aidha Mrema amewataka vijana kuwa makini na upinzania kwa kuwa Lowassa alijiunga na upinzani baada ya kunyimwa nafasi ya kugombea Urais ndani ya CCM hivyo wajiepushe na maandamano kwani hayana faida kwao.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images