Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Chadema yazindua Operesheni UKUTA....Yatangaza Kufanya Maandamano na Mikutano ya Hadhara Nchi Nzima Kuanzia Septemba 1

$
0
0
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) MAAZIMIO YA KIKAO CHA KAMATI KUU ILIYOFANYIKA HOTELI YA BAHARI BEACH LEDGER PLAZA, 23-26 JULAI, 2016

1.0 UTANGULIZI
Kamati Kuu ya dharura ya Chama iliketi kuanzia tarehe 23-26 Julai, 2016 Jijini Dar Es Salaam na ilikuwa na ajenda moja mahsusi ambayo ni kujadili hali ya siasa na uchumi wa Taifa tangu serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani mwezi Novemba, 2015.

Mwenendo wa serikali hii ya CCM ya awamu ya tano, chini ya Rais John Magufuli, ni dhahiri kuwa umeamua kuiweka demokrasia kizuizini na kuleta utawala wa Kidikteta katika nchi yetu.

  1. MATUKIO MAHSUSI YA UKANDAMIZAJI WA HAKI NA DEMOKRASIA
NCHINI
  1. Kupiga Marufuku Mikutano ya Vyama vya Siasa: Serikali kupitia Waziri Mkuu na hatimaye Rais na jeshi la Polisi walitangaza kwa nyakati tofauti kwamba ni marufuku kwa vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa mpaka mwaka 2020 ili kuipa Serikali nafasi ya kufanya kazi. Huu ni uvunjaji wa Ibara ya 20 (1) ya Katiba. Aidha, katazo la mikutano ya siasa linakiuka Sheria namba 5 ya Vyama vya siasa ya mwaka 1992 kifungu cha 11 ambayo imetoa haki kwa vyama vya siasa kufanya kazi ya siasa.
2.2 Kupiga Marufuku Urushwaji wa moja kwa moja (live coverage) wa Mijadala ya Bunge: Katazo hilo ni kinyume na Katiba ibara ya 18 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inatoa uhuru wa maoni na uhuru wa kupata habari kwa kila mwananchi.

2.3 Kudhibiti Wabunge wa Upinzani Bungeni: Serikali imejificha nyuma ya kiti cha Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson Mwansasu (Mb) ili kuwadhibiti Wabunge wa Upinzani Bungeni kwa lengo la kuwanyamazisha wasiikosoe Serikali.

Ikumbukwe kwamba Dkt. Tulia akiwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa ni mtumishi wa umma asiyepaswa kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa; lakini ghafla anaonekana akigombea nafasi ya Naibu Spika kupitia CCM. Hivyo yupo Naibu Spika ambaye ni mteule wa Rais. Swali: Anawajibika kwa nani kati ya Bunge na Rais?
 
Kuingilia Mhimili wa Mahakama: Serikali ya CCM kupitia Rais, kwa nyakati tofauti imeonekana kujaribu kuingilia uhuru wa Mahakama jambo ambalo ni hatari kwa utoaji wa haki nchini. Katika hotuba yake, wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria duniani Rais alinukuliwa akisema kwamba Mahakama iwahukumu harakaharaka watu waliokwepa kodi halafu atatumia asilimia fulani ya fedha ambazo zitakuwa zimepatikana kutokana na faini za wale walioshindwa kesi kuwapa Mahakama.

Muswada wa Sheria ya Haki ya kupata habari –Serikali imepeleka Bungeni Muswada wa Sheria ya Haki ya kupata habari. Sheria hii imeweka adhabu kubwa sana kwa waandishi kama vile kifungo cha miaka 15 na kisichozidi miaka 20 kwa mujibu wa kifungu cha 6(6)

Kupuuza Utawala wa Sheria: Tarehe 24 Juni, 2016 wakati wa uzinduzi wa siku ya usalama wa raia, Rais Magufuli alinukuliwa akiwaruhusu polisi kuwaua majambazi bila kuwafikisha mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake. Aidha aliuagiza uongozi wa Jeshi la Polisi kuwapandisha vyeo watakaowauwa majambazi. 

Serikali hii inatishia ukuaji wa uchumi
Tangu serikali ilipoingia madarakani hali ya ukuaji wa uchumi na hata uwekezaji wa mitaji imekuwa ikiporomoka kwa kasi kubwa sana nchini mwetu na hata baadhi ya wawekezaji wanaondoa mitaji yao kutokana na serikali hii kukosa mwelekeo unaoeleweka wa Kiuchumi.
 
Serikali za mitaa kunyanganywa mapato na serikali kuu.
Baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 tulifanikiwa kushinda maeneo ya Majiji ya DSM, Mbeya,Arusha na Miji mikubwa ya Iringa, Moshi,Bukoba,Babati,Tunduma na mingineyo ya maeneo ya mijini ambayo kwa kiasi kikubwa wanategemea sana kuendesha Halimashauri hizo kwa kutumia kodi ya Majengo Kodi ya Majengo inachangia kati ya 30% hadi 60% ya mapato ya ndani ya Mamlaka za Miji.

2.9 Diplomasia na mahusiano ya kimataifa

Hivi karibuni serikali imetoa maelekezo kupitia mawasiliano yake na Mabalozi (NoteVerbale) kuelekeza kuwa kabla ya Mabalozi au maofisa wa Ubalozi kukutana na asasi zisizo za kiserikali au vyama vya siasa ni lazima kwanza waombe kibali cha serikali kupitia Wizara ya Mambo Nje.

Utaratibu huu unaminya uhuru wa mabalozi na wanadiplomasia mbalimbali kufanya kazi zao nchini na ni utaratibu ambao unakiuka utamaduni uliokuwepo awali na pia unakiuka masharti ya Mkataba wa Vienna kuhusu mahusiano ya Kibalozi Duniani.

2.10 Uteuzi wa Wakurugenzi wa Halimashauri

Uteuzi wa Rais wa Wakurugenzi wa Halimashauri na Makatibu Tawala wa Wilaya haukuzingatia sheria za utumishi wa umma na badala yake umezingatia kigezo cha Ukada zaidi badala ya weledi na historia katika utumishi wa umma kama ambavyo sheria zinataka, zaidi ya wakurugenzi 80 na Makatibu tawala zaidi ya 40 waligombea kura za maoni ndani ya CCM 2015.

2.11 ZANZIBAR

Kwa sababu ya hasira ya kukataliwa kwa CCM, vikosi vya ulinzi na hasa Jeshi la Polisi vimekuwa vikishiriki katika vitendo kadhaa vya ukiukwaji wa haki za raia huko Zanzibar ambapo kwa zaidi ya miezi miwili sasa, wamekuwa wakipita katika vijiji na kuwapiga, kuwatesa, kuwakamata, kuwatishia na hata kuharibu mali za wananchi na mifugo yao

Tunawataka wananchi wa Unguja na Pemba waendelee kuikataa Serikali haramu iliyopo madarakani huko Zanzibar kwa njia za amani .

3.0 MAAZIMIO YA KAMATI KUU

Baada ya majadiliano Kamati Kuu imeazimia ifuatavyo;
Septemba 1, siku ya mikutano ya hadhara nchi nzima
Kamati kuu imeagiza ngazi zote za chama kuanzia ngazi ya msingi, Kata, Majimbo, Wilaya, Mikoa, Kanda, Mabaraza na Taifa kukaa vikao vyake vya kikatiba na imeelekeza ajenda ya vikao hivyo kuwa ni kujadili hali ya siasa, hali ya uchumi na maandalizi ya mikutano ya hadhara ya tarehe 01 Septemba, 2016 nchi nzima.
 
Wanasheria wa Chama kuchukua hatua
Kamati Kuu imewataka wanasheria wa chama kukaa na kuyatazama mambo yote ambayo yametokea na kuchukua hatua za kisheria kwa lengo la kuyatafutia suluhisho la kisheria.
 
OPERESHENI UKUTA
UMOJA WA KUPAMBANA NA UDIKTETA TANZANIA (UKUTA)

UTANGULIZI

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika utangulizi kuna maneno yameandikwa na ambayo yamekaziwa na sheria namba 15 ya mwaka 1984 ibara ya 3 na sheria namba 1 ya mwaka 2005 ibara ya 3. Katika utangulizi huo wa katiba yetu imeandikwa kama ifuatayavyo;

“KWA KUWA Sisi wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani” “NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia, ambayo Serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu:”

“KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kwa niaba ya Wananchi kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya Demokrasia ujamaa na isiyokuwa na Dini”

Aidha kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzana ibara ya 3 (1) inasema kuwa “Jamhuri ya Muungano ni Nchi ya Kidemokrasia na ya kijamaa, isiyokuwa na dini, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa”

Ni wazi sasa kuwa kuna tishio kubwa dhidi ya ukuaji wa Demokrasia hapa Nchini mwetu kutoka kwa viongozi wa serikali hii ya awamu ya tano kukandamiza Demokrasia na madhara ya kukandamizwa kwa demokrasia yameshaanza kulitafuna taifa letu.

Ni dhahiri kuwa kama raia wema tuna wajibu na haki ya kuilinda na kuitetea Katiba ya Nchi na kuhakikisha kuwa haivunji na yeyote na misingi ya Kidemokrasia ambayo ilijengwa kwa miongo mingi inaendelea kuimarika, kulelewa na kukuzwa mara dufu.

3. 4 KWANINI UKUTA NI MUHIMU !

Wakati wa Ufashisti wa Adolf Hitler huko Ujerumani unaanza kuchipua kabla ya kukomaa alianza kuchukua hatua mbalimbali za kuwanyamazisha Wajerumani kwa njia mbalimbali ili aweze kutawala kwa mkono wa Chuma.

Alikuwepo Mchungaji mmoja anayejulikana kwa jina la Martin Niemoller na ambaye alikuwa akimsemea Hitler kwa kila hatua ambazo alikuwa anachukua dhidi ya makundi mengine katika jamii ya wajerumani bila kujua kuwa lilikuwa ni suala la muda tu kabla hata yeye hajafikiwa na mkono wa Chuma wa Hitler.

Mchungaji huyu ni maarufu sana kwa msemo wake ambao aliutoa alipofikiwa na mkono wa Hitler ambao ulimpelekea kuishia jela kwa miaka 7 na wakati huo hapakuwa na

mtetezi wa kumsemea, alisema hivi;

First they came for the Socialists, and I did not speak out— Because I was not a Socialist. Then they came for the Trade Unionists, and I did not speak out— Because I was not a Trade Unionist. Then they came for the Jews, and I did not
speak out— Because I was not a Jew. Then they came for me—and there was no one left to speak for me.

3.5 HALI TANZANIA IKOJE?

Tangu utawala wa awamu ya Tano ulipoingia madarakani mwezi Novemba, 2015 umechukua hatua mbalimbali za kubinya Demokrasia na kuua dhana ya utawala bora kwa njia mbalimbali.

Yapo makundi ya kijamii ambayo tayari yameshaumizwa au kubinywa na watanzania walio wengi wanakaa kimya kwa sababu wao sio sehemu ya kundi husika ambalo limenyimwa haki au kwa kuwa hajafikiwa moja kwa moja.
  1. 3.6 KWANINI NI MUHIMU KUJENGA UKUTA.
  • Rais alipiga marufuku safari za nje kwa watumishi wa umma- sikusema kwa kuwa mimi sikuwa mtumishi wa umma
  • Rais aliitaka mahakama kuu iwahukumu wafanyabiashara ambao wana kesi za kodi na serikali lazima ishinde-sikusema kwa kuwa sikuwa mfanyabiashara na wala sikuwa na kesi ya kodi
  • Serikali iliingilia Bunge na kupanga kamati za kudumu za Bunge-sikusema kwa kuwa mimi sikuwa mjumbe
  • Serikali ilizuia matangazo ya Bunge live-sikusema kwa kuwa mimi sio Mbunge
  • Wabunge wa Upinzani kunyanyaswa Bungeni na kuonewa –sikusema kwa kuwa mimi sio UKAWA
  • Hotuba za Upinzani kufutwa Bungeni kinyume cha Kanuni za Bunge –sikuwa mpinzani nilikaa kimya Bunge kurejesha fedha zake kwa Rais kinyume cha sheria –sikusema kwa kuwa halinihusu
  • Tume ya Taifa ya Uchaguzi kurejesha fedha kwa Rais kinyume cha sheria – sikusema kwa kuwa Tume hainihusu
  • Serikali Kuwafukuza na kuwadhalilisha wanafunzi wa UDOM –sikusema kwa kuwa sina ndugu wala mtoto anayesoma UDOM.
  • Mikutano ya kisiasa kupigwa Marufuku –sikusema kwa kuwa mimi sio mwanasiasa
  • Wafanyabiashara kupelekewa bili kubwa za kodi na hata kuzuiliwa kwa Akaunti zao-sikusema kwa kuwa mimi sio mfanyabiashara
  • Uchumi unaporomoka kwenye sekta zote nchini -sikusema kwa kuwa mimi sijawahi kumiliki uchumi
  • Fao la kujitoa limeondolewa kwenye Mifuko ya hifadhi ya jamii, sikusema kwa sababu mimi si mwanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii.
  • Mashirika na Makampuni kuanza kupunguza wafanyakazi kutokana na kuporomoka kwa uchumi –sikusema kwa kuwa sijapunguzwa kazini
  • Mabalozi na wanadiplomasia kuzuiliwa kukutana na viongozi wa kisiasa bila kibali cha serikali- sikusema kwa kuwa halinihusu
  • Watumishi wa umma kulazimishwa kwenda kinyume na sheria na kanuni za utumishi wa umma wametakiwa kuwa Makada wa CCM –sikusema kwa kuwa mimi sio mtumishi wa umma
  • Ukaguzi wa vyeti vya kidato cha nne na kutumika kama msingi wa kufukuza watu kazi hata kama ni Maprofesa –sikusema kwa kuwa hawajaja kwenye sekta yangu
  • Watumishi wa umma kutumbuliwa majipu bila kufuatwa kwa sheria na kanuni za utumishi wa umma –sikusema kwa kuwa mimi sikutumbuliwa
  • Mawakili kuunganishwa kwenye kesi za wateja wao wanapoenda kuwatetea – sikusema kwa kuwa mimi sio wakili
  • Waalimu kukatwa mishahara iwapo dawati litavunjika kwenye shule yake – sikusema kwa kuwa mimi sio mwalimu
  • Kupotezwa kwa wana CCM ambao watapinga kauli ya Mwenyekiti au kuwa na maoni tofauti-sikusema kwa kuwa mimi sio mjumbe wa vikao vya CCM .
  • Muswada wa sheria ya haki ya kupata habari na adhabu ya kifungo cha miaka 15-20- sikusema kwa kuwa mimi sio mwandishi wa habari
  • Viongozi wa dini kudhalilishwa –sikusema kwa kuwa mimi sio kiongozi wa dini
  • Unyanyasaji na udhalilishaji wa wananchi Zanzibar –sikusema kwa kuwa mimi sio mzanzibari
3.7 TUCHUKUE HATUA!

Kwa kuwa wewe tayari umeshafikiwa hauna budi kujenga UKUTA ili kuzuia wengine wasidhurike na utawala huu.
  1. Kwa kuwa wewe hujafikiwa na ndio maana husemi wenzako wanapofikiwa, njoo tujenge UKUTA ili ukifikiwa awepo wa kusema
  2. Tuungane Tujenge UKUTA ili kuzuia uchumi wetu kuporomoka
  3. Njoo Tujenge UKUTA kuzuia Udikteta huu
  4. Tujenge UKUTA tuilinde Katiba yetu
  5. UKUTA huu ni wa wananchi wote bila kujali dini, kabila, chama cha siasa au rangi
Historia inaonyesha kuwa Duniani pote Hakuna utawala uliwahi kuushinda UKUTA wa wananchi .Na hii ndio Nguvu ya Umma. Kila mmoja achukue hatua popote alipo ya kujenga UKUTA!

Imetolewa na;

…………………….

Freeman A Mbowe

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa

27 Julai, 2016

Bodi ya Mikopo yatangaza majina 1,091 ya wadaiwa Ambao Hawataki Kulipa (Awamu ya kwanza).....Bonyeza Hapa Ujitazame Kama na Wewe Jina Lako Lipo

$
0
0

Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB), inawaarifu wadaiwa wote ambao mpaka hivi sasa hawajaanza kulipa mikopo waliochukua kipindi wanasoma, na wenye majina yao kwenye orodha hii kwamba wamevunja mkataba kutokana na sheria ya bodi hiyo No. 9 ya 2004 (kama ilivyorekebishwa) sehemu ya 19 (1).
 
Na wanataarifiwa kwamba, kulingana na sheria hiyo ya bodi (HESLB)  No. 9 ya 2004, Bodi imedhamiria kutenda yafuatayo:-
 
(i) Bodi itachukua hatua za kisheria kulingana na kipengele cha 19 (a) (1) cha sheria ya bodi.
 
(ii) Mdaiwa atapewa penati ya 5%  juu ya ile 5% iliyokua ikitozwa kabla kwa kila mwezi kwenye deni lililobakia au alilonalo.
 
(iii) Mdaiwa ataongezewa gharama za kumtafuta alipo ili alipe deni zilizoingiwa na bodi.
 
(iv) Mdaiwa atawekwa kwenye ‘blacklist’ na maelezo yake yatapelekwa  kitengo cha kumbukumbu ya wakopaji na hivyo kushindwa kukopa sehemu nyingine yoyote.
 
(v) Mdaiwa atazuiliwa kupata udhamini wa Serikali au udahili wa masomo ya juu kwenye vyuo vyovyote ndani na nje ya nchi.
 
(vi) Maelezo yao yatapelekwa kwenye Wizara ya mambo ya ndani, kitengo cha Uhamiaji na balozi zote ambako watakataliwa safari zozote za kwenda nje ya nchi.
 
Wadaiwa wote ambao majina yamechapishwa kwenye magazeti na kwenye tovuti ya bodi ya mikopo (Bonyeza hapakuyasoma majina hayo) wanatakiwa kulipa madeni yao mapema iwezekanavyo kuzuia wao kupata adhabu hizo zilizotajwa hapo juu.

==>Bonyeza Hapa Kuyasoma Majina Hayo

Rais Magufuli awaapisha Viongozi wa Tume ya Utumishi wa Walimu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Bw. Oliva Paul Joseph Mhaiki kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC).

Aidha, Rais Magufuli amemuapisha Mwl. Winifrida Gaspar Rutaindurwa kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC).

Rais Magufuli alifanya uteuzi wa Mwenyekiti na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu tarehe 15 Julai, 2016.

Viongozi hawa wanakuwa wa kwanza kuongoza Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) tangu Tume hiyo ilipoundwa kwa mujibu wa sheria ya Tume ya Utumishi wa Walimu Namba 25 ya mwaka 2015 ikiwa na majukumu ya kusimamia na kuratibu masuala yanayohusu utumishi wa walimu.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma

27 Julai, 2016

Waziri Mhagama na Manaibu wake kuhamia Dodoma wiki ijayo

$
0
0
Habari/Picha Na Jonas Kamaleki
Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu,Bunge, Kazi, Ajira na Watu Wenye Ulemavu itahamia Dodoma juma lijalo kufuatia agizo la Mhe. Rais John Pombe Magufuli la Serikali kuhamia Dodoma.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi ,Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama wakati akiongea na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zilizoko chini ya ofisi hiyo.

“Mchakato wa kuhamia Dodoma umekwisha kilichobaki kwa sasa ni utekelezaji, mimi na manaibu mawaziri wangu tunahamia juma lijalo ili tukamkaribishe Mhe. Waziri Mkuu anayehamia Septemba mwaka huu,” alisema Mhagama.

Mhagama amesema kuwa kila kiongozi anayehamia Dodoma inabidi awakute walio chini yake tayari wamekwishahamia ili kumpokea, hivyo akawataka na watendaji ambao wako chini yake watangulie kwa ajili ya kumpokea yeye na viongozi wenzake.

Aidha, Waziri huyo amesema kwa sasa hakuna mjadala wa kuhamia Dodoma lilobaki ni utekelezaji  tu wa kuhamia Makao Makuu.

Mhagama amesema kama kuna Taasisi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu imetenga fedha kwenye bajeti kwa ajili ya ujenzi, shughuli hiyo ikafanyike Dodoma ambako Serikali inahamia. Kwa kusema hivyo kadhalika na ofisi au Wizara nyingine za serikali ambazo zimetenga fedha ya ujenzi wakajenge Dodoma.

Suala la kuhamia Dodoma sio geni bali limekewepo kwa kipindi kirefu ila utekelzaji wake ndio ulikuwa bado; pia katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 suala hili lipo, alisema Mhagama na kuongeza kuwa kipindi cha nyuma Wizara saba (7) ziliwahi kuhamia Dodoma na kwa sasa Wizara inayoshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) iko Dodoma.

Waziri Mhagama ameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuanza ujenzi wa jengo lake mjini Dodoma na kusisitiza kuwa Wizara na Taasisi nyingine za Serikali kuiga mfano huo kwa kujenga ofisi zao Dodoma.

“Kwa kuwa sisi ni waratibu wa wizara zote inabidi tuunde kikosi kazi kitakachofanya kazi ya uratibu wa kuhama kikiwa Dodoma ili kuwawezesha na watumishi wenzetu kutekeleza agizo la Mhe. Rais la serikali nzima kuhamia huko,”alisema Mhagama.

Mhagama amesema kuwa Mamlaka ya Ustawishaji wa Makao Makuu Dodoma (CDA) wameshafanya kazi nzuri ya upimaji eneo la serikali ambalo litatumika kwa ajili ya ofisi.
 
“Tumefika mwisho wa mchakato sasa ni utekelezaji na tunataka watumishi walielewe vizuri suala hili na wawe tayari kulipokea,”alisisitiza Mhagama.

Kuhamia Dodoma katika kipindi hiki kunatokana na agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alillolitoa tarehe 25 Julai, 2016 mjini Dodoma kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao ulimchagua kuwa Mwenyekiti wa tano wa chama hicho tawala.

Mkataba Kati Ya TTCL Na Bhart Airtel Waisha Rasmi

$
0
0

Serikali imehitimisha ubia kati ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), na Kampuni ya Bhart Airtel ya India kwa kuilipa kampuni hiyo Shilingi Bilioni 14.9 na hivyo kuirudisha TTCL mikononi mwa Serikali kwa asilimia miamoja.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema hatua hiyo ni mkakati wa Serikali wa kuiwezesha TTCL kujitegemea ili kuzalisha faida, Kuimarisha Miundombinu yake, na kutoa gawio Serikalini.

“Tunawataka TTCL mjipange vizuri mjitangaze ili muwe kampuni kubwa na bora ya mawasiliano hapa nchini”, amesema Prof. Mbarawa.

Waziri Prof. Mbarawa amesema katika kuiongezea nguvu TTCL Serikali itawapa kituo cha  Kutunza Taarifa cha Kijitonyama (Internet Data Center) ili ikisimamie na hivyo kujipatia mapato kupitia gharama za uendeshaji na usimamizi wa kituo hicho.

Amewataka wafanyakazi wa TTCL kufanya kazi kwa bidii, kasi, uaminifu, ubunifu na kuulinda Mkongo wa Taifa ili uwawezeshe kuwa na huduma bora na za uhakika wakati wote.

“Tumetumia fedha za mkongo wa taifa kumlipa mbia mwenzenu bhart airtel ili kuiwezesha TTCL kumilikiwa na Serikali kwa asilimia miamoja hivyo changamoto inayowakabili sasa ni kufanya mabadiliko makubwa katika upande wa kutafuta masoko ili kuweza kuongeza idadi ya wateja na kufanya kazi kwa faida”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Aidha Prof Mbarawa amesema katika kuijali TTCL, Serikali imeipa masafa ya 1800 na masafa ya 2100 na itawaongezea masafa ya 800 yatakayowawezesha kuwa na huduma ya 4G LTE yenye  mtandao wenye kasi na hivyo kuiongezea wateja hususani katika huduma za data.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL,  Profesa Tolly Mbwete amesema TTCL imejipanga kutoa huduma zake katika maduka makubwa, hospitali, stesheni za treni, mabasi ya mwendokasi na viwanja vya ndege katika jiji la Dar es salaam na Miji mikubwa ili kuwawezesha wananchi kunufaika na huduma za mtandao na data wakati wote.

Naye,  Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura, ameishukuru Serikali kwa fursa mbalimbali inazoipa kampuni hiyo na kumhakikishia Waziri Prof Mbarawa kuwa katika kipindi cha miezi mitatu ijayo matokeo ya mkakati wa mabadiliko ya kibiashara yataanza kuonekana.

Dkt. Kazaura amesema kuwa tayari watumishi wenye mtazamo wa mabadiliko ya kiteknolojia wameajiriwa na wengine watapewa mafunzo ili kuhimili soko la kibiashara na kuiwezesha TTCL kunufaika na miundombinu yake iliyopo nchi nzima.

Waziri Prof. Mbarawa alikuwa akizungumza na Menejimenti na wafanyakazi wa TTCL ikiwa ni utaratibu aliojiwekea kuzungumza na wafanyakazi na taasisi zilizopo chini ya Wizara yake.

Habari Zlizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya July 28

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 21

$
0
0

Mtunzi: Enea Faidy
... MR ALOYCE alichanganyikiwa sana baada ya kukuta damu ikiwa imetapakaa sakafuni chumbani kwa mwanaye. Alipigwa na butwaa huku hofu ya kuondokewa na mwanae ikiwa imemvaa ghafla.

"Eeeddy!" Alijikuta anaita kwa sauti Kali ili kama Eddy yupo mbali asikie na aitikie wito ule ambao ungemwondolea wasiwasi Mr Alloyce. Lakini wito ule haukuitikiwa na mtu yoyote zaidi ya ukimya uliokuwa umetawala ndani ya jumba lile la kifahari.

Mr Alloyce alijaribu kuita tena na tena lakini bado hakuitikiwa. Simanzi ikamjaa tele, akajua tayari amepata pigo lingine zito kabla hata kidonda cha mwanzo hakijapona kwani ndio kwanza kilikuwa kibichi.

"We Mungu wangu nimekukosea nini Mimi mbona unaniadhibu hivi? Nihurumie uikomboe familia yangu" alilia mr Alloyce akiwa amejibwaga sakafuni kwenye korido ya kuelekea sebuleni. Machozu yalimchuruzika kama mvua huku yakiteremka kama vijito kuelekea kwenye marumaru za rangi ya maziwa zilizochanganyika na weupe.

"We Mungu nitaishi vipi Mimi na upweke huu? Sina mke, sina mtoto?" Alilalamika kwa majonzi mr Alloyce. Aliwaza mengi sana yaliyozidisha simanzi yake moyoni, moyo wake ukajawa na maumivu makali sana kama mtu aliyechomwa na mkuki wa moto katikati ya moyo wake.

"Bora na Mimi nife kuliko kubaki kwenye hali kama hii...!" Aliwaza Mr Alloyce kisha akainuka pale sakafuni na kuelekea chumbani kwake. Aliingia chumbani na kuwasha taa, kisha akaisogelea droo ya dressing table akaifungua na kuanza kupekuapekua vitu.

Alipekua kwa muda kisha akapata karasi ya ranging ya kaki akafunua kwa umakini kisha akazikuta dawa alizozihitaji. Kulikuwa na vidonge Vingi sana ndani ya pakiti ile kaki, akavibeba na kuirudisha droo kama ilivyokuwa akatoka kuelekea sebuleni.

Alifika sebuleni na kuliendea jokofu ili achukue pombe Kali anywe pamoja na vile vidonge ili aondokane na ulimwengu huu wa mateso ambao alihisi umemtenga baada ya kumtenganisha na wapendwa wake. Akiwa anafungua jokofu na kichukua chupa moja ya konyagi ghafla alishtuka sana. 

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) Chakanusha vyuo vyake kuzuiwa Kudahili

$
0
0

CHUO Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT), kimetoa ufafanuzi wa taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa vyuo vyake vishiriki vimezuiwa na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) kufanya udahili wa wanafunzi.

Taarifa hizo zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zimedai kuwa vyuo vishiriki vya SAUT ambavyo ni Stella Maris Mtwara University College (STEMMUCO) na Archbishop James University College (AJUCO) vimefungiwa na TCU kufanya udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Makamu Mkuu wa Chuo cha SAUT, Dk Thadeus Mkamwa, taarifa hizo ni za upotoshaji na kuwa hawajapokea taarifa kutoka TCU ikivizuia vyuo hivyo viwili kufanya udahili.

Aidha, Dk Mkamwa aliiomba jamii na wadau wa elimu kwa ujumla kupuuzia taarifa hizo kwa kuwa zina uwezekano wa kuwa ni mbinu chafu zinazofanywa na baadhi ya watu kuuhadaa umma hasa katika kipindi hiki ambacho ni muafaka kwa waombaji kufanya maombi katika vyuo vikuu.

“Tunauomba umma wa Watanzania kufahamu kuwa, Chuo Kikuu cha SAUT na vyuo vyake vikuu vishiriki vilivyotajwa hapo juu vinaendelea na udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2016/2017,” alisema Dk Mkamwa.

Alisema SAUT ni Chuo Kikuu kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Tanzania, na kwamba kimepiga hatua kubwa katika kujiendeleza na kufanikiwa kuanzishwa kwa vyuo vingine vikuu vishiriki vya SAUT ambavyo ni STEMMUCO kilichopo Mtwara, AJUCO kilichopo Songea na Jordan University College (JUCO) kilichopo Morogoro.

Vyuo vingine ni St. Francis University College of Health and Allied Sciences (SFUCHAS)- Morogoro, Archbishop Mihayo University College (AMUCTA)- Tabora, na Cardinal Rugambwa Memorial University College (CARUMUCO) kilichopo Bukoba, Marian University College (MARUCO) kilichopo Bagamoyo.
 
Dk Mkamwa aliongeza kuwa, chuo kimeweza kuanzisha vituo vingine vitatu vya SAUT vilivyoko Mbeya, Arusha na Dar es Salaam.

Magufuli aahidi kuboresha maslahi ya watumishi CCM

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa mara ya kwanza amekutana na kuzungumza na wajumbe wa Sekretarieti ya chama hicho.

Magufuli pia amekutana na  wafanyakazi wa CCM Makao Makuu katika Ofisi za Chama hicho Mjini Dodoma ikiwa ni siku tano tangu achaguliwe kuwa Mwenyekiti wa Tano wa Chama hicho.

Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amekutana na watendaji hao wa CCM kwa lengo la kuwasalimia, kupokea maoni na ushauri wao juu ya utendaji kazi ndani ya Chama.

Katika mazungumzo hayo, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewapongeza watendaji wote wa Chama Cha Mapinduzi kwa kazi kubwa wanayoifanya na kwa namna ya pekee kwa jinsi walivyotoa mchango mkubwa kuhakikisha CCM inapata ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.

Pia amewataka kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na maarifa kwa lengo la kuendelea kukiimarisha Chama hicho ambacho kimebeba dhamana ya kuongoza Serikali kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Dkt. Magufuli amewahakikishia kuwa chini ya uongozi wake atafanyia kazi changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi wa CCM ikiwemo maslahi duni, vitendea kazi na kuondoa utegemezi.

Aidha, Dkt. Magufuli amewataka watumishi wa chama kutoa ushirikiano katika zoezi la uhakiki wa mali za Chama litakalosimamiwa na sekretarieti ya chama na ameahidi kuwa atahakikisha mapato yatokanayo na vyanzo vya mapato vya chama yanatumika ipasavyo.

Kwa upande wao watumishi wa CCM wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Ndugu Abdulrahaman Kinana wamempongeza Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kwa asilimia mia moja na wajumbe wa Mkutano Mkuu uliofanyika tarehe 23 Julai, 2016 Mjini Dodoma kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa.

Watumishi hao wamemuahidi kuendeleza utumishi uliotukuka na wameelezea matumaini yao ya kuboreshewa maslahi.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Mjumbe wa Kamati Kuu na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

Picha ya Mtanzania anayeteswa na Mchina yampeleka Mwigulu Geita

$
0
0
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba amewasili mkoa wa Geita kwa ziara ya kikazi, kubwa ikiwa ni kufuatia taarifa za mateso na mauaji yaliyodaiwa kufanywa na raia wa China wanaomiliki sehemu ya mgodi wa Nyamhuna uliopo Katoro, Geita dhidi ya wafanyakazi/vibarua ambao ni Watanzania.

Takribani wiki moja sasa kumekuwa na  hali ya sintofahamu dhidi ya picha zinazoenezwa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari zikionesha raia wa Tanzania anayefanya kazi kwenye mgodi tajwa akiteswa na kufanyiwa vitendo ya kinyama na mwajili wake ambaye ni raia wa china.

Ilimlazimu Waziri mwenye dhamana na usalama wa raia na mali zao kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani  ya Nchi kufika eneo la mgodi kujiridhisha kwa taarifa zilizotapakaa na kubeba simanzi kwa Watanzania.

Mwigulu Nchemba amejiridhisha kuwa kulikuwepo na tukio hilo la Mtanzania kuteswa na mwajiri wake, kipigo kilichosababisha kupoteza fahamu na siyo kifo.

Hatua za awali Waziri Nchemba alizozifanya ni kwenda gereza la Geita mjini alikohifadhiwa kijana huyo kwa madai ya kushitakiwa na mwajiri wake kwa kosa la wizi lililosababishwa apigwe.

Katika mahojiano ya Waziri Mwigulu Nchemba na kijana huyo, Mwigulu alibaini kuwa kijana huyo aliyepo gerezani ndiye mhusika hasa wa tukio lile kwa uthibitisho wa makovu yaliyopo mwili mwake na mavazi aliyovalia wakati anateswa na akiwapo gerezani.

Katika hali hiyo, ilimlazimu, Mhe. Mwigulu kwenda mgodini akiwa ameambatana na kijana huyo kwa ajili ya kutambua waliofanya vitendo hivyo vya kinyama. 

Katika oparesheni hiyo, kijana aliyeteswa na kujeruhiwa aliwabaini Watanzania 5 ambao ni walinzi wa eneo hilo na Mchina mmoja walioshirikiana kumpiga, kumtesa na kumjeruhi.

Kufuatia utambuzi huo na maelezo ya wahusika, Nchemba akaagiza wahusika wakamatwe mara moja na akaondoka nao kwa hatua zaidi za kisheria.

Katika hali nyingine ya kusikitisha, Waziri Nchemba amebaini uwepo wa wahamiaji haramu raia wa China katika mgodi huo ambapo nyaraka za uhamiaji mkoa wa Geita zinaonesha raia 28 wenye vibali ndio waliruhusiwa kukaa kwenye mgodi huo, lakini katika operasheni ya kushitukiza aliyoifanya Mhe. Nchemba amebaini uwepo wa raia wa china zaidi ya 50 wanaoishi katika mgodi huo kinyume na sheria.

Hivyo amemuagiza Mkuu wa Mkoa na timu yake ya uhamiaji kuhakikisha wote wasio na vibali wanakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Rais Magufuli kuhutubia mkutano wa hadhara Jumapili Wilayani Kahama

$
0
0

Rais John Magufuli anatarajia kufanya ziara wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambako atafanya mkutano wa hadhara kuwashukuru wananchi kwa kumpigia kura nyingi katika Uchaguzi Mkuu uliopita. 

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Fadhili Nkulu alisema jana kwamba Rais Magufuli atawasili hapa Jumamosi jioni kabla ya kufanya mkutano wa hadhara Jumapili. 

Nkulu aliwataka wananchi wa Kahama na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi kumlaki kiongozi huyo katika ziara hiyo ambayo alisema: “Lengo lake ni kuwapongeza wananchi wa Kahama kwa kumpa kura nyingi katika Uchaguzi Mkuu uliomalizika mwaka jana.” 

Alisema ziara hiyo ni muhimu kwa kuwa ni ya kwanza mkoani Shinyanga akianzia na Kahama. 

“Tujipongeze wananchi kutokana na kupata bahati ya wilaya chache zilizotembelewa na kiongozi huyu, Kahama imekuwa mojawapo,” alisema Nkulu. 

Alisema kwa kuwa Jumamosi ni siku ya usafi kitaifa, kila mmoja wilayani humo ahakikishe anaweka mazingira katika hali ya usafi na kuwaonya wafanyabiashara kuwa atakayeshindwa kufanya hivyo hataruhusiwa kufungua biashara. 

“Nitafanya ukaguzi Jumamosi kuhakikisha kila mtu anashiriki usafi. Hilo ni agizo la kitaifa kwa sasa lazima kila mmoja awajibike, nimewaagiza watendaji wote wa kata kusimamia hilo,” alisema Nkulu. 

Alisema wananchi watatangaziwa ratiba yote ya Rais Magufuli kwenye gari la matangazo ambalo litazunguka mji mzima wa Kahama kuwaeleza muda na eneo ambalo kiongozi huyo atafanyia mkutano.

Wanaotengeneza Vyeti bandia vya Serikali Wapewa Mwezi Mmoja kujisalimisha

$
0
0

MPIGACHAPA Mkuu wa Serikali, Cassian Chibogoyo, ametoa   mwezi mmoja kwa watu wanaojihusisha na utengenezaji wa vyeti bandia vya Serikali kujisalimisha kabla hawajachukuliwa hatua za  sheria.

Hivi karibuni Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam liliwakamata watu watatu ambao walikutwa na vyeti bandia vya kidato cha nne, vyeti vya uuguzi, stika za Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), vyeti vya kuzaliwa na   vyuo vya ufundi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Chibogoyo alisema wanakusudia kuendesha msako nchi nzima kuwabaini watu hao na kuwachukulia hatua za  sheria.

“Baada ya muda tuliotoa kuisha tutafuatilia mkoa hadi mkoa kuhakikisha tunadhibiti nyaraka bandia,” alisema Chibogoyo.

Aliwataka Watanzania kuacha kutumia vibaya bendera, nembo na wimbo wa taifa kwa sababu  ni vielelezo vya taifa.

Alisema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na ile inayopendekezwa, zote zinaelekeza kuhusu matumizi bora ya vielelezo vya taifa kama vile bendera, nembo na wimbo wa taifa.

“Bendera iheshimiwe, hairuhusiwi kupeperusha bendera iliyotoboka, kupauka au chafu. Katika maeneo mengine unaweza kukuta bendera inapandishwa au kushushwa lakini watu wamekaa chini na wengine wanaendelea na shughuli zao,” alisema Kibogoyo.

Mamia wafurika kununua viwanja Dodoma

$
0
0

MAMIA ya wananchi wameanza kupeleka maombi ya viwanja katika ofisi za Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA), imeelezwa.

Hali hiyo imetokea baada ya Rais Dk. John Magufuli kutangaza nia ya Serikali kuhamia mjini hapa kwa kuwa ndiko yaliko makao makuu ya nchi.

Kutokana na idadi kubwa ya watu wanaofika katika ofisi za Idara ya Ardhi katika mamlaka hiyo, Jeshi la Polisi mkoani hapa limelazimika kuimarisha ulinzi ili kukabiliana na hali hiyo.

Mmoja wa watu waliokutwa ofisini hapo na kujitambulisha kwa jina la Salum Kijuu, mkazi wa Area A, alimwambia mwandishi wa habari hizi aliyeshuhudia mamia ya watu ofisini hapo jana, kwamba alifika ofisini hapo kulipia kiwanja chake kilichopo eneo la Miganga.

“Kaka hii foleni ya watu karibia wote wanaulizia viwanja, mimi nimekuja kulipia kiwanja changu ili niweze kukimiliki kihalali kwani mambo yameshabadilika,” alisema Kijuu.

Wakati hali ikiwa hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa CDA, Paskasi Muragili, alisema ardhi mjini hapa itauzwa kwa bei ya kawaida ili watu wengi waweze kumiliki viwanja.

“Kwa mfano, ‘square’ mita moja ya kiwanja cha makazi itauzwa kwa Sh 5,500 hadi Sh 10,000 katika maeneo ambayo kitaalamu tunayaita ‘medium density’.

“Kwa sasa maeneo yanayouzwa ni Miganga na Mkalama yaliyopo nje kidogo ya mji wa Dodoma.

“Viwanja kwa ajili ya uwekezaji mkubwa ‘square’ mita moja itauzwa kwa Sh 13,300 na maeneo hayo kitaalamu tunayaita ‘low density’.

“Pamoja na uwepo wa mahitaji makubwa, nasema ardhi ipo ya kutosha, yaani hata kama watakuja wananchi wote wa Dar es Salaam, watapata ardhi ya kutosha.

“Narudia tena, ardhi ipo ya kutosha, hata kama watu watakuja baada ya miaka 30, wataipata kwa sababu hata Mwalimu Nyerere alipoamua Dodoma iwe makao makuu, alijua kuna ardhi ya kutosha kwa idadi yoyote ya watu,” alisema Muragili.

Akizungumzia mpangilio wa mji utakavyokuwa, alisema mji wa kiserikali utaanzia katika Kijiji cha Mtumba hadi eneo la Ikulu ndogo ya Chamwino, ambako kutakuwa na ofisi za wizara na mabalozi.

“Mji wa kibiashara, utakuwa ni eneo lote la mji wa Dodoma kwa sababu hii ramani ninayokwambia iko katika ‘master plan’ ya mwaka 2010-2030 ya kuhakikisha makao makuu ya nchi yanakuwa vizuri kuanzia kwenye barabara za kuingia na kutoka ili kusiwe na msongamano wa aina yoyote,” alisema.

Pamoja na hayo, mkurugenzi huyo alitoa angalizo kwa wanaohitaji kununua viwanja mjini Dodoma na kusema watatakiwa kupitia CDA kwa kuwa ndiko vinakopatikana.

“Viwanja tusinunue kienyeji, tufuate taratibu kwani najua watatokea wapigaji wa dili watakaowaumiza watu. Nawaombeni mje ofisini kwetu, kama mnataka viwanja mtapata tu kwa kufuata utaratibu,’’ alisema.

Naye Ofisa Uwekezaji wa CDA, Abeid Msangi, alisema wametenga maeneo maalumu ya Itega na Njendengwa kwa ajili ya kujenga mahoteli makubwa na nyumba mbalimbali za kupanga.

“Lakini kwa sasa eneo la Itega limeshajaa, ila Ndejengwa tumetenga zaidi ya ekari 1,500 kwa ajili ya uwekezaji mkubwa.

“Kuonyesha kwamba tulijipanga mapema katika eneo la uwekezaji, kule Ndejengwa miundombinu iliishafika mapema, kwani kuna maji, umeme pamoja na barabara za lami,” alisema Msangi.

Hivi karibuni, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisema watazalisha umeme wa megawati 60 ili kuondoa tatizo la kukatika kwa umeme katika Mkoa wa Dodoma.

Profesa Muhongo alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa kujenga njia ya kusafirisha umeme wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Shinyanga kupitia Dodoma na Singida.

Naye Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka, Mkoa wa Dodoma (Duwasa), David Pallangyo, ameshasema wamejipanga kuhakikisha maeneo yatakayopimwa, yanapata maji safi na salama.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mkoa wa Dodoma, Bernard Chimagu, naye alishasema wamejipanga kukabiliana na ongezeko la magari.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 3 & 4

$
0
0
Umri: 18+
Mtunzi:Eddazaria G.Msulwa

 ILIPOISHIA
Nilizungumza kwa kujishtukia huku karoti yake ya bandia nikiificha kwa nyuma ili asiione.Madam Mery akanitazama  kwa macho yanayo ashiria kitu ila sijui ni kiti gani na taratibu akaanza kupita mbele yangu na kwenda alipo tundika taulo lake na kuanza kujifuta maji huku akiwa amenipa mgongo huku mguu wake mmoja akiuweka juu ya meza kisha akainama kidogo ili kuvifikia vidole vya mguu huo alio uweka katika meza na khanga aliyoivaa kwa jinsi ilivyonaatana na mwili wake imeingia kidogo katikati ya mstari wa makalio yake na kuyafanya yagawanyike kama vilima viwili vya Kibo na Mawezi tunavyoviona katika mlima Kilimanjaro

ENDELEA
Madama akaendelea na kazi yake ya kujifuta maji pasipo kunijibu chochote.Nikapiga hatua za taratibu huku nikinyata kuelekea mlango wa kutokea ndani ya chumba hicho kabla sijaufungua Madam Mery akaniita
 
“Eddy unakwenda wapi?”
Swali la Madam likanifanya nikae kimya wala sikujua nijibu kitu gani kwani ninapokwenda ninapajua ni sebleni ila jinsi ya kuzungumza nikajikuta mdomo mzima unakuwa mzito kama ninakunywa uji wa dengu.

Madam akageuka na kunitazama jinsi ninavyo babaika mlangoni nilipo simama
“Umeficha nini huko nyuma kwako?”
“Eheeee!”
“Nikitu gani ulicho kificha huko nyuma kwako?”
 
Nikakaa kimya huku nafsi yangu ikinishawishi niitoe karoti ya bandia niliyoikuta chini ya uvungu nikitafuta panya kuepuka kujiongezea matatizo kwani hapo nilipo ninatatizo la kusimamishwa masomo kwa wikimoja.Nikaitoa karoti yake ya bandia na kumuonyesha Madam nikadhani atakasirika ila nikashangaa akitabasamu na kutoa kicheko kidogo
 
“Iweke tu hapo kwenye kitanda”
Nikaiweka kitandani huku akiwa ananitazama kwa umakini.Nikafungua mlango na kutoka na kwenda sebleni kukaa huku nikiyasikilizia mapigo yangu ya moyo jinsi yanavyo kwenda kwa kasi japo kuna baridi kali ila jasho usoni lina nitiririka.

Baada ya muda kadhaa Madam Mery akatoka chumbani kwake huku akiwa amevalia nguo nyingine zilizo mpendezesha na kuzifanya umbo lake kuonekena viziri huku nywele zake ndefu akiwa amezibana kwa nyuma

“Sasa mwanangu mimi ninaondoka tutaonana mchana.Kama utahitaji kunywa chai utachukua mkate kwenye  friji pia kuna soseji kama wewe ni mlaji unaweza kuzila”
 
“Sawa Madam je chai ipo wapi?”
“Chai sijapika.Njoo nikuonyeshe jikoni”
Nikanyanyuka na Madam akaende kunionyesha jiko lililopo humo humo ndani ya nyumba yake ambayo kila kitu muhimu kinachohitajika katika nyumba kipo ndani na imezungushiwa ukuta mrefu.
“Si unaweza kutumia jiko la gesi?”
“Ndio”
“Basi ukiwa na njaa chai utakuja kuipikia hukuu.Eheee kuna jengine?”
“Mmmmm hakuna”
“Sasa mbona hujaniuliza visufuria vipo wapi au utapikia mikono yako?”
 
Madam alizungumza huku akinipiga kibao kidogo cha shavuni huku akitabasamu na kunifanya nibaki ninashangaa.Nikazidi kushangaa zaidi pale Madam Mery alipo nipiga busu la mdomoni na kutoka ndani ya chumba hicho cha jiko huku akitingisha makalio yake na kuelekea zake shule hata visufuria akasahau kunionyesha ameviweka wapi.

Nikarudi sebleni nikachungulia dirishani kama Madam Mery tayari ameshatoka getini.Nikamuona ndio analibana vizuri geti la kuingilia katika nyumba hii.Nikaiwasha TV(Luninga) ambayo mwanzoni nilikuwa nimeizima kutokana na filamu ya.......

==> Endelea Nayo  <<kwa  Kubofya  Hapa>>

Rais Magufuli Atengua Uteuzi Wa Mwenyekiti Wa Bodi Ya Mfuko Wa Barabara, Dkt. James Wanyanza Na Kumteua Bw. Joseph Odo Haule Kushika Nafasi Hiyo

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara (Road Fund Board) Dkt. James Munanka Wanyancha.

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi iliyotolewa leo Mjini Dodoma imeeleza kuwa Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kuanzia leo tarehe 28 Julai, 2016.

Kufuatia kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua Bw. Joseph Odo Haule kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Mfuko wa Barabara.

Uteuzi wa Bw. Joseph Odo Haule umeanza leo tarehe 28 Julai, 2016.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Joseph Odo Haule alikuwa Meneja wa Mfuko wa Barabara (Road Fund).

Wajumbe wengine wa Bodi ya Mfuko wa Barabara wanaendelea katika nafasi zao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma

28 Julai, 2016

Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Viwanda Na Biashara

Eliud Tawi Nyauhenga Ateuliwa Kuwa Kaimu Meneja Mfuko Wa Barabara Ya Wizara Ya Ujenzi,uchukuzi Na Mawasiliano.

Video: Papa Francis aanguka ghafla akiongoza Misa Poland

$
0
0
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amepata ajali ya kuanguka ghafla alipokuwa akitembea kuelekea kwenye jukwaa lililoandaliwa kwa ajili ya kuendesha ibada, Czestochowa nchini Poland.

Papa Francis mwenye umri wa miaka 79 alisaidiwa kwa haraka na wasaidizi wake na kufanikiwa kuamka na kuendelea na safari hadi kwenye kiti kilichoandaliwa.

Kwa bahati nzuri, kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki alionekana kuwa katika hali yake ya kawaida ambapo aliendelea kuongoza ibada hiyo iliyokuwa ikirushwa moja kwa moja kupitia vituo mbalimbali vya runinga na kuangaliwa na mamilioni ya watu.

Kwa mujibu wa Daily Mail, Papa Francis anasumbuliwa na ugonjwa unaojulikana kama Sciatica, ugonjwa ambao wakati mwingine hushusha maumivu ya ghafla kwenye miguu kutoka mgongoni.

Kauli ya CCM baada ya CHADEMA kutaja siku ya maandamano

$
0
0
Jana tarehe 27/7/2016 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), walitoa kauli kwa Waandishi wa Habari kupitia Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Ndugu Freeman Mbowe (Mb). Tamko hilo kama ilivyo kawaida ya CHADEMA lilijaa uongo mwingi na ghiliba nyingi za kibabaishaji na kuthibitisha ukweli kuwa kwa hakika kutokana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dr. John Pombe Magufuli wapinzani nchi hii wamekosa ajenda na hivyo njia peke yake wanayoona inafaa ili waendelee kufanya utapeli ni kutunga uongo, kujiaminisha katika uongo huo na kuusambaza uongo huo ili kujaribu kupata wafuasi.

Katika uongo na uzushi huo walioutangaza jana, CHADEMA wanasema wameamua kufanya mikutano na maandamano nchi nzima kwa tarehe waliyoitaja na maandamano hayo yatafanyika chini ya operesheni waliyoiita UKUTA. Kimsingi hoja walizozitumia kufikia uamuzi wao bila kuzirudia zimejaa upotoshaji na uongo uliokithiri. Kwa mfano wanadai Serikali imezuia mikutano yote ya vyama vya siasa, huku wakijua kuwa ni uongo kwani Serikali haijazuia mikutano kwenye majimbo yao, Wabunge wako huru kufanya shughuli zao kwenye majimbo yao, na tumeona Wabunge wakifanya shughuli zao majimboni bila shida wakiwemo hao wa vyama vya upinzani.

Lakini vyama vya siasa kufanya shughuli kwa mujibu wa katiba ya vyama vyao sio jambo lililozuiliwa pia, ndiyo maana tumeshuhudia vyama vikifanya mikutano yao ya kikatiba bila tabu.

Lakini mfano mwingine wa hoja za uongo na uzushi, ni hoja eti ya Serikali hii ya Awamu ya Tano kuwa ya kidikteta. Udikteta hasa unaosemwa na Chadema ni upi? Ni huu wa kushughulikia watumishi hewa? Ni huu wa kuwabana wakwepa kodi? Ni huu wa kupunguza na kudhibiti safari za nje? Ni huu wa kubana matumizi ya Serikali? Ni huu wa kufukuza wabadhirifu na wazembe kazini? Hivi udikteta huo ni huu wa kushughulikia mafisadi mpaka kuanzisha mahakama yao? CCM inaamini Watanzania walio wengi wanaunga mkono hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli na Serikali yake, sasa kama kwa Chadema hatua hizi ndiyo tafsiri yake ni udikteta basi bila shaka wao ni sehemu ya mfumo mbovu ndiyo maana wako tayari kuleta vurugu ili wautetee.

Kwa kuwa CHADEMA wamezoea kujenga Chama chao kwa harakati zinazohusisha kumwaga damu za Watanzania wasiokuwa na hatia, ukweli huu wa maelekezo ya Serikali hawausemi, isipokuwa wanafanya juhudi kubwa kuhakikisha wanafanya mambo ambayo mwisho wa siku yatasababisha vurugu, uvunjifu wa amani na umwagaji damu.

Lakini pengine ni muhimu Watanzania na wapenda amani nchini na duniani wakajiuliza ni kweli kuwa lengo la hizi vurugu na maandamano haya ni la kujenga na si kubomoa? Kwa nini kila operesheni ikifanywa na CHADEMA huwa inaambatana na umwagikaji wa damu za Watanzania wasiokuwa na hatia? Wakati wa Maandamano hayo inapotokea madhara ni kwa nini waathirika huwa sio viongozi waanzilishi wa maandamano hayo wala wake au waume zao au watoto wao au hata ndugu zao wa karibu bali huwa ni watu wengine nje ya hao ndugu zao wa karibu? Mpaka lini damu za Watanzania wasio na hatia zitaendelea kutumika kutafuta umaarufu wa CHADEMA na viongozi wake?

Hii ni kwa faida ya nani hasa? Kwa nini pamoja na kuelekezwa namna bora ya kufanya siasa wao huwa hawataki kufuata utaratibu? Hivi ni kweli kuwa hawajui bila kufuata utaratibu jambo lolote huwa ni vurugu?

Chama Cha Mapinduzi kinapenda kuwakumbusha Watanzania kuwa ni vizuri kutafakari na kujiuliza maswali ya msingi kabla ya kuamua kushiriki au kuruhusu watoto wetu kwenda kuwa kafara ya walafi wachache wa madaraka. Ni vizuri tukayakumbuka matukio kwenye operesheni kama hizi yaliyopoteza maisha ya vijana wetu na matokeo ya kila operesheni. 

Pamoja na ukweli kuwa hakuna operesheni yeyote kati ya zote zilizowahi kufanywa na Chadema ambayo imewahi kuwasaidia Watanzania wa kawaida zaidi ya kujenga umaarufu wa viongozi wachache wa Chadema na kuneemesha matumbo yao na ya familia zao, operesheni zote zimepoteza maisha ya Watanzania kadhaa wasiokuwa na hatia wala wasiofaidika kwa lolote na operesheni hizo.

Kama nia ni njema kwa nini hawataki kufuata Sheria na taratibu tulizojiwekea? Demokrasia gani isiyokuwa na mipaka? Demokrasia bila mipaka ni fujo. Tunaomba vyombo vinavyohusika visisite kuchukua hatua zinazostahili bila kumuonea mtu lakini bila kufumbia macho vitendo vyenye lengo la kuwahujumu Watanzania waliowengi walioamua kuchapa kazi kuitikia wito wa Rais na Serikali ya Awamu ya Tano ya kufanya kazi.

Lakini pia tunawashauri Watanzania, wapenda amani, utulivu na maendeleo kupuuza wito wa vurugu na uvunjifu wa amani badala yake wajikite kwenye kuchapa kazi na kujitafutia maendeleo yao kwa kufanya kazi kwa bidii.

Maendeleo hayaji kwa maandamano, maendeleo huja kwa kuchapa kazi kwa bidii. Maendeleo hayaji kwa vurugu na fujo nchini, bali amani na utulivu ni vichocheo muhimu vya maendeleo ya kweli.

Imetolewa na:-
Christopher Ole Sendeka (MNEC),
MSEMAJI WA CHAMA
28/07/2016

Msajili wa Vyama vya Siasa alaani tamko la CHADEMA

$
0
0
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi amelaani vikali  tamko la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) lililotolewa jana tarehe 27 Julai, 2016 kupitia vyombo vya habari, kuhusu hali ya demokrasia ya vyama vingi hapa nchini la kuazimia kufanya mikutano na maandamano nchi nzima akidai kuwa tamko hilo ni la kichochezi lililolenga kuleta uvunjifu wa Amani.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha Ofisi ya Msajili wa Vya Siasa na kusainiwa na Jaji Francis Mutungi imebainisha kuwa tamko hilo linaenda kinyume na Sheria ya Vyama vya Siasa namba 5 ya mwaka 1992 kifungu 9 (2) (c) inayokataza chama cha siasa kutumia au kuhamasisha matumizi ya nguvu au vurugu kama njia ya kufikia malengo yake ya kisiasa.

“Nimepokea kwa masikitiko tamko la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) lililotolewa jana tarehe 27 Julai, 2016 kupitia vyombo vya habari, kuhusu hali ya demokrasia ya vyama vingi hapa nchini. Tamko hilo limejaa lugha ya uchochezi, kashfa, kuudhi na lenye kuhamasisha uvunjifu wa amani. Ili kuepuka kurejea tamko lote, nimeona ni vyema nitoe mfano wa maneno yafuatayo yaliyosemwa, ambayo yanakiuka Sheria ya Vyama vya Siasa”. Ilisema taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo iliongeza kuwa kifungu cha 9(2) (f) kinakataza chama cha siasa kuruhusu viongozi au wanachama wake kutumia lugha ya matusi, kashfa na uchochezi ambayo inaweza kusababisha au ikapelekea kutokea uvunjifu wa amani. Vile vile kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa, Tangazo la Serikali namba 215 la mwaka 2017, zinakataza chama cha siasa kutumia lugha za matusi, kashfa, uongo na uchochezi.

Nakuongeza kuwa kanuni ya 5(1) (d) inakitaka kila chama cha siasa kutotoa maneno yoyote au maandishi ambayo ni uongo. Kuhusu mtu yoyote au chama cha siasa chochote.

Katika taarifa yake Jaji Mutungi amesema kutokana na Kanuni hizo tamko la CHADEMA ni ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa.

Aidha, hii siyo mara ya kwanza kwa CHADEMA kutumia lugha za namna hii za kuhamasisha uvunjifu wa amani (civil disorder).

Natumia fursa hii kukemea tamko hilo hadharani, kwa mujibu wa kanuni ya 6(2) ya Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa. Pia nawaasa CHADEMA wasiendeleze tabia hii.

Jaji Mutungi ametoa rai kwa  Viongozi wa Vyama vya Siasa  waonyeshe ukomavu katika medani za Siasa badala ya kujikita katika vitendo, kauli au matamshi yenye mlengo wa kusababisha uchochezi au kufarakanisha Umma na Serikali yao.

Katika tamko lao CHADEMA wameitangaza siku ya tarehe mosi Septemba kama ni siku maalum kwao kufanya mikutano nchi nzima ikiwamo maandamano ambapo ngazi zote za chama kuanzia ngazi ya msingi hadi Taifa zitahusika.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images