Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Manji Aendelea Kusubiri Majibu ya Barua Yake Aliyomwandikia Rais Magufuli Kuhusu Sakata la Coco Beach

0
0
Mwenyekiti wa Kampuni za Quality Group Limited (QGL), Yusuf Manji amesema bado anasubiria majibu kutoka kwa Rais John Magufuli juu ya sakata la kuendeleza ufukwe wa Coco, maarufu Coco Beach uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam baada ya kumwandikia barua Desemba mwaka jana.

Manji alisema anatamani suala hilo limalizike kabla ya kuondoka rasmi katika kampuni hiyo mwezi ujao, na kwamba tayari alishamwandikia barua kiongozi huyo wa nchi juu ya usahihi wa mchakato wa zabuni wa kuendeleza eneo hilo la ufukwe wa Bahari ya Hindi.

Mfanyabiashara huyo anasema anashangazwa na baadhi ya viongozi wa Serikali kurudiarudia suala hilo na kusababisha kuwa maarufu kuliko hata Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Kwa mujibu wa mfanyabiashara huyo, suala la Coco Beach ilikuwa ni sehemu ya biashara na kwamba zabuni hiyo walishinda baada ya kutimiza masharti yaliyokuwa yamependekezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, lakini cha kushangaza hali imekuwa tofauti.

Mfanyabiashara huyo alifikia hatua hiyo kufuatia Rais John Magufuli kutangaza eneo hilo liendelee kutumika na watu wa kawaida kwa kile alichosema kuwa kuna mfanyabiashara ambaye anatumia fedha kuwahonga baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo ili kumiliki eneo hilo.

Rais Magufuli ambaye alikuwa akihutubia mkutano wa wafanyabiashara alisema;“Inanifadhaisha sana kuona mfanyabiashara tajiri akihonga maofisa kutumia vibaya fedha za umma kwa manufaa yake binafsi na wakazi kutoka mazingira duni wakishindwa kutumia ufukwe huo kuogelea na kuburudika.”

Hata hivyo, Manji alisema kuwa kampuni yake ilikuwa ikilihitaji eneo hilo kuliendeleza kwa ajili ya biashara na kuhudumia wananchi hivyo iwapo Rais ataridhia linyang’anywe licha ya kushinda zabuni na mahakamani, hawatakuwa na hatua nyingine ya kufanya.

Alisema Rais aliyasema yake na Mahakama ilishafanikisha ushindi wa awamu ya kwanza na Serikali baadaye ilikata rufaa na kwamba mtu yoyote akitaka kusoma kwa nini walishinda kesi ya awali, hukumu iliyotolewa inajieleza.

Manji alieleza kuwa ingekuwa eneo lile linahitajika kwa matumizi binafsi hata wangemwambia aliachie na achukue Jangwani angekubali, lakini kampuni isingekubali kwa sababu eneo lile lilitafutwa kwa ajili ya biashara na mbadala wowote huenda usiwavutie wanahisa.

 “Coco Beach siyo nyumbani kwangu na wala siyo sehemu ambayo lazima niwe nayo au nisiwe nayo. Ni sehemu ambayo kampuni ilihitaji kwa ajili ya uwekezaji,” alisema Manji.

“Wanahisa walitaka kuwekeza lakini iwapo halitapatikana, hawajatufungia milango ya kiuwekezaji kwa kuwa Coco Beach siyo sehemu moja tu duniani ya kuwekeza.”

Tayari QGL ilishaingia ubia na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) mwishoni mwa mwaka jana kutekeleza mradi wa Dola 250 milioni za Marekani (Sh537.5 bilioni) kuendeleza eneo la Bwawani, kwa kuikarabati hoteli hiyo na kujenga mji wa kisasa ambao utakuwa na huduma zote za kisasa katika visiwa hivyo.

Sakata la Kutaka Kumshitaki Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Laibua Mjadala Mzito

0
0
Kauli ya mwanahabari nguli nchini, Jenerali Ulimwengu kutaka Rais Mstaafu Jakaya Kikwete ashtakiwe mahakamani kwa kuitia hasara Serikali imeibua mjadala mzito, huku wasomi wakisema ipo haja ya kubadili Katiba ili mkuu wa nchi aweze kushtakiwa baada ya kuondoka madarakani. 

Wasomi hao walisema ile kauli ya “hakuna aliye juu ya sheria” inapaswa kufuatwa na watu wote, wakitolea mfano Rais wa Brazil, Dilma Roussef aliyeng’olewa na Bunge baada ya kutuhumiwa kukiuka sheria za usimamizi wa akaunti ya bajeti ya nchi hiyo.

Kwa sasa nafasi yake inashikiliwa na aliyekuwa makamu wake, Michel Temer.

Hata hivyo, baadhi ya wasomi wamesema jukumu hilo la kumshtaki rais mstaafu inafaa liachwe mikononi mwa Bunge. 

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imempa kinga rais mstaafu ya kushtakiwa kwa jambo lolote alilofanya alipokuwa madarakani na imetoa mlolongo mrefu rais aliyeko madarakani kuondolewa. 

Juzi wakati akizungumza katika Tamasha la Nane la Kigoda cha Mwalimu Nyerere, Jenerali ambaye pia ni mwanasheria wa kujitegemea alisema Kikwete anapaswa kushtakiwa kwa kuisababishia hasara Serikali kutokana na kuruhusu mabilioni ya shilingi kutumika katika mchakato wa Katiba ambayo haikupatikana. 

Mbali na fedha zilizotumiwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati wa kukusanya maoni, kununulia magari, kulipia pango la ofisi, nyingine zilitumika kurekebisha ukumbi wa Bunge uweze kubeba wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, na kulipa posho ya Sh300,000 kwa siku kwa wajumbe 620 kwa muda wa siku 130. 

“Itabidi (Kigoda cha Mwalimu) mumuite (Kikwete) mwaka ujao, aje aeleze fedha za wananchi zilizotumika katika mchakato ule zilikuwa na sababu gani,” alisema huku akishangiliwa na umati wa watu. 

Jenerali aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya za Hai na Ilala na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, alisema kama mawaziri wa zamani wamepandishwa kizimbani kwa kusababisha hasara, hata Kikwete anapaswa kupelekwa mahakamani kwa kusababisha hasara kwa Serikali na kuzima matumaini ya wananchi, jambo linaloweza kusababisha machafuko nchini. 

Ibara ya 46 sehemu ya (1) ya Katiba inasema wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii, itakuwa ni marufuku kumshitaki au kuendesha mashataka ya aina yoyote juu yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

Sehemu ya (3) inasema isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii. 

Ibara ya 46A sehemu ya (1) inasema bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii, Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii. 

Sehemu ya (2) imeweka masharti kwamba bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama inadaiwa kwamba Rais; (a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; (b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20 (2) ya Katiba. 

Mbali ya Katiba ya sasa kumwekea kinga Rais mstaafu, Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Jaji Joseph Warioba na Katiba Inayopendekezwa zilinakiri kipengele hicho kinachompa Rais mstaafu kinga ya kutoshtakiwa bila kubadili chochote. 

Maoni ya wasomi 
Mhadhiri wa Shule ya Siasa ya Chuo Kikuu  Dar es Salaam (UDSM), Dk James Jesse alisema ili kuondoa kile alichokiita ‘kusumbuliwa’, jukumu la kumshtaki Rais mstaafu au aliyepo madarakani linapaswa kuachwa mikononi mwa Bunge. 

“Katiba imeeleza wazi kwamba ataondolewa madarakani kwa azimio la Bunge. Binafsi nadhani utaratibu huo ndiyo mzuri hata kama atakuwa amemaliza muda wake, hoja ya kumshtaki ianzie bungeni,” alisema . 

Naye Mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia, Innocent Shoo alisema,“Tukizingatia demokrasia za kisasa, rais akitoka madarakani hapaswi kuwa na kinga ya kushtakiwa. Hii inatakiwa iwezekane hata akiwa madarakani ili kuzingatia utawala wa sheria.” 

Katika ufafanuzi wake, Shoo alisema kuwa kutokuwajibika na utamaduni wa kutokujali ni utambulisho wa viongozi wengi barani Afrika huku akinukuu kauli ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kwamba “Afrika inatakiwa kuwa na taasisi imara siyo mwanaume mwenye nguvu.” 

Shoo alisema nchi nyingi barani Afrika hazina chaguzi huru, haziheshimu haki za binadamu na uhuru wa watu na taasisi mbalimbali, mambo aliyodai kuwa yanafaa kumfanya Rais kushtakiwa. 

“Umeona kilichotokea Brazil? Ule ni mfano hai kuwa rais anaposhindwa kufuata sheria na taratibu ashtakiwe tena ashtakiwe hata akiwa madarakani,” alisisitiza. 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sua), Profesa Damian Gabagambi alisema, “Anapaswa kushtakiwa anapomaliza utawala wake na hasa kama wakati akiwa rais alikuwa akifanya mambo ya kulihujumu taifa.” 

Profesa Gabagambi ambaye alikuwa mmoja wa wataalamu walioandaa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), alisema kushtakiwa siyo kufungwa kwa kuwa mtuhumiwa atakwenda mahakamani na kujitetea. 

“Hii itasaidia viongozi wakati wa utawala wao kuheshimu utawala bora na kufuata sheria na Katiba ili kukwepa kushtakiwa, mara wamalizapo kipindi chao cha kuongoza,” alisema. 

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiah Oluoch alisema Katiba inampa Rais kinga ya maisha, jambo ambalo si sahihi huku akieleza kuwa wazo la Kikwete la kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya lilikuwa zuri ila liliharibiwa na wanasiasa. 

“Kinga aliyonayo rais ndiyo inayompa kiburi na ndiyo sababu akiwa madarakani akishauriwa hataki, ila akimaliza muda wake anajuta kwa uamuzi aliouchukua,” alisema Olouch huku akisisitiza kuwa hayo ni maoni yake binafsi si ya CWT. 

Akitolea mfano wa kilichomkumba Rais wa Brazil, Oluoch ambaye alikuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, alisema hata kama nchi nyingine nazo zina kinga kwa marais wao, si lazima Tanzania kubaki na kinga hiyo kwa kuwa kila nchi ina utamaduni na ustaarabu wake. 

“Rais wa Tanzania yupo juu ya sheria. Mfano Benjamin (MkapaRais wa Awamu ya Tatu) amesema anajutia uamuzi wake wa ubinafsishaji na kutowekeza katika elimu. Hayo ni baadhi tu ya makosa wanayoyafanya viongozi wetu,” alisema Oluoch. 

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala alisema kuondoa kinga ya Rais baada ya utawala wake ni hatari kwa usalama na demokrasia ya nchi. 

Alisema kwa kuwa kila kiongozi hufanya maamuzi ya kisiasa ambayo wakati mwingine hayatimii, kuondolewa kwa kinga hiyo kunaweza kukaleta matatizo ya kisiasa kwa siku za mbele.

 “Kuna mtu atakuja kung’ang’ania ikulu endapo atatambua kuwa yupo kwenye hatari ya kufikishwa mahakamani,” alisema Profesa Mukandala na akashauri zianzishwe taasisi makini na imara zitakazokuwa zinamshauri Rais juu ya maamuzi mbalimbali anayoyafanya akiwa madarakani. 

Alisema hakuna haja ya kuwafikisha mahakamani viongozi wa ngazi hiyo, kama makosa yao yalitokana na mtazamo wa kisiasa na kukumbusha kuwa hata Rais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Nyerere alishindwa kutekeleza mkakati wa kuanzisha Vijiji vya Ujamaa kama ulivyoratibiwa sawa na ilivyotokea kwenye Katiba Mpya kipindi cha Rais Kikwete. 

Chama cha Wananchi (CUF) Zanzibar, kimeunga mkono kauli ya Jenerali kuhusu Kikwete kushtakiwa kuhusiana na mchakato wa Katiba ambayo haikupatikana. 

Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salim Bimani alisema CUF inaunga mkono kwa asilimia 100 kauli hiyo, kwa sababu sehemu kubwa ya matatizo yaliyojitokeza na yanayojitokeza Zanzibar yamesababishwa na kutopatikana kwa Katiba Mpya. 

“CUF tungekuwa na uwezo hata leo tungetaka ashtakiwe haraka iwezekanavyo. Kwa sababu Kikwete ni mmoja wa watu aliyevuruga uchaguzi Oktoba 25, mwaka jana,” alisema Bimani. 

Lakini Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vua Ali Vuai alisema maoni ya Jenerali si sahihi na si ya kiungwana kwa kuwa yana lengo la kuleta uchochezi kwa wananchi dhidi ya Kikwete. 

“Huu ni upotoshaji kwa wananchi, kwa sababu Kikwete amefanya mambo makubwa nchini. Sioni sababu ya kusema fedha nyingi zimetumika wakati mchakato huu bado unaendelea, ukisubiri kupiga kura za maoni.

Utafiti: Asilimia 88 ya Wananchi Wanataka Bunge Lirushwe ‘Live’

0
0

TAASISI ya Twaweza imetoa matokeo ya utafiti wake, ambapo imebainika kuwa asilimia 79 ya Watanzania wamepinga uamuzi wa Serikali wa kusitisha matangazo ya moja kwa moja (Live ) ya Bunge.

Katika maoni yao, wananchi hao wamedai kuwa ni haki yao ya msingi kufahamu kinachoendelea katika vikao mbalimbali vya Bunge.

Utafiti wa taasisi hiyo umefanywa katika maeneo tofauti ya Tanzania Bara kupitia mpango wake wa Sauti za Wananchi.

Akitoa taarifa ya matokeo ya utafiti huo jana jijini Dar e Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze,  alisema suala hilo limeonekana kutokuungwa mkono na wananchi wengi.

“Asilimia kubwa ya Watanzania wanapinga uamuzi wa Serikali wa kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge. Suala hili limeonekana kugusa hisia za watu wengi na maamuzi haya ya Serikali yakionekana kutoungwa mkono.

“Katika utafiti huu wananchi nane kati ya 10 wanapinga uamuzi wa hali inayodhihirisha kutoungwa mkono kwa hatua hiyo,” alisema Eiyakuze.

Akizungumzia sababu walizozitoa  wananchi wanaotaka matangazo ya Bunge yarushwe moja kwa moja,  Eiyakuze alisema asilimia 46 walisema yanawafanya waweze kufuatilia utendaji wa wabunge waliowachagua kwa kuwa huko ndio walikowatuma.

“Asilimia 44 wanasema ni muhimu kwa sababu wananchi wanahaki ya kufahamu kinachoendelea bungeni, asilimia 29 wanasema matangazo ya moja kwa moja yalikuwa yanaaminika zaidi kwa watazamaji na wasikilizaji  kuona na kusikia wenyewe kile kinachoendelea tofauti na mfumo wa kurekodi ambapo kuna baadhi ya mambo yanahaririwa.

“Asilimia 16 walidai kuwa inafursa mwananchi kupata taarifa sahihi badala ya kuzisoma kwenye magazeti huku asilimia 16 nyingine wakisema inawasaidia wanachi kufuatilia mijadala ya Bunge kwa wakati”, alisema Eiyakuze.

Pamoja na hali hiyo mkurugenzi huyo alisema katika utafiti huo asilimia 92  ya wananchi walisema kuna umuhimu wa vipindi vya Bunge kurushwa moja kwa moja kupitia Luninga na redio bila kujali gharama zilizoelezwa kuwa ndio chanzo cha kufikia uamuzi huo.

“Asilimia 88 walisema vipindi vya Bunge virushwe ‘Live’ bila kujali gharama ukilinganisha na asilimia 12 ambao waliona ni muhimu suala la bajeti likazingatiwa,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema asilimia 80 wanaona matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni ni muhimu kama yalivyo na asilimia 20 wakisema fedha hizo zitumike kwenye huduma nyinge za jamii.

Akizungumzia suala la vyombo vya habari vya binafsi kuruhusiwa kurusha matangazo hayo,  Eiyakuze alisema wananchi wanaunga mkono vyombo hivyo kuruhusiwa iwapo Serikali imeshindwa kumudu gharama.

Utafiti huo pia umeonesha Watanzinia wanne kati ya kumi wamewahi kuangalia matangazo ya moja kwa moja kupitia Luninga na sita kati ya kumi  wamesikiliza kupitia redio.

Aidha utafiti huo umeonyesha zaidi ya nusu ya wananchi walosema wameangalia au kusikiliza vipindi vya Bunge wamefanya hivyo ndani ya miezi miwili iliyopita.

Hali ilivyokuwa
Januari mwaka huu, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Nape Nnauye, alitoa ufafanuzi bungeni kuhusu hatua ya Serikali kusitisha matangazo hayo kupitia Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC).

Miongoni mwa sababu alizozieleza ni pamoja na kuwepo kwa gharama kubwa ya Sh bilioni 4.2 zinazotumika katika uendeshaji wa matangazo hayo ya moja kwa moja kwa mwaka pia watumishi wa serikali kushabikia Bunge badala ya kuendelea na kazi ofisini.

Hatua ya Serikali kusitisha matangazo hayo iliibua mjadala mkubwa bungeni huku Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, (ACT-Wazalendo) akilitaka Bunge kusitisha shughuli zake ili kujadili taarifa hiyo ya Serikali.

Siku chache baadaye kilio hicho cha ukosefu wa fedha za kuonesha matangazo hayo ya moja kwa moja ambacho kimekuwa kikitolewa na serikali, sasa kilipata ufumbuzi.

Hatua hiyo iliyokana na uamuzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari nchini (TMF), kujitokeza hadharani na kueleza kwamba upo tayari kutoa fedha zinazohitajika ili kuhakikisha haki ya Mtanzania kupata habari kupitia TBC haiingiliwi wala kubughudhiwa kwa hoja yoyote.

Endapo Serikali itakubali ombi hilo, wananchi wataendelea kunufaika na vikao vya moja kwa moja vya Bunge tofauti na pendekezo la serikali la kunakili baadhi ya sehemu na kisha kuoneshwa usiku.

Picha: Muonekano mpya wa Chid Benz baada ya kutoka Sober house

0
0
Msanii wa Bongofleva Chid Benz usiku wa June 15 2016 alipost picha za muonekano wake mpya ikiwa ni siku chache baada ya kutoka Sober house Bagamoyo, alipokuwa amekaa kwa siku kadhaa kama njia ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aitaka Mikoa Yote Kuunda Kamati za Ulinzi

0
0


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kila mkoa unatakiwa kuunda Kamati ya Amani kama njia ya kudumisha amani na utulivu kwenye mikoa yote nchini.

Waziri Mkuu ametoa wito huo jana usiku (Jumatano, Juni 15, 2016) wakati akizungumza na viongozi wa dini wa mkoa wa Dodoma na baadhi ya wazee maarufu wa mkoa huo aliowaalika kwenye futari katika makazi yake mjini Dodoma.

Amesema anatambua kuwa mkoa wa Dodoma uko shwari kwa sababu ya mshikamano uliopo baina viongozi wa dini za Kiislamu na Kikristo. “Nimegundua kuwa siri kubwa ya mkoa wa Dodoma kuwa na utulivu ni kuwepo kwa kamati ya amani yenye viongozi mahiri, kwani sote tunatambua kuwa kazi ya viongozi wa dini ni kuwaimarisha watu kiroho,” alisema.

Waziri Mkuu alisema ziko nchi zinatamani kuwa kama Tanzania kwa sababu wao hawana uhakika wa kulala na kuamka salama asubuhi. “Pamoja na yote sisi tuna uhakika wa asilimia 99 kulala usiku na kuamka salama asubuhi, kwa sababu ya amani iliyopo,” alisema.

Hadi sasa mikoa ambayo imekwishaunda kamati za amani ni Dar es Salaam, Mwanza, Geita, Dodoma, Arusha, Lindi, Mtwara, Tanga na Mbeya.

Akigusia suala la mauaji ya hivi karibuni, Waziri Mkuu alisema anawaomba Watanzania kila mmoja kwa imani yake akemee kwa nguvu matendo hayo kwa sababu yeye haamini kama yamefanywa na Watanzania ambao wamelelewa kwenye misingi ya dini.

“Siamini kama kuna mtoto aliyelelewa kwenye misingi ya Uislamu anaweza kuingia msikitini na kuwaua wenzake wakati wakimwomba Mungu. Na wala siamini kama kuna mtoto aliyelelewa na kukuzwa Kikristo anaweza kuingia kwenye nyumba ya ibada akakuta watu wanasali na kuamua kuwaua. Ninawaomba tukemee kwa nguvu zote tabia hii,” alisisitiza.

Aliwataka watanzania wote wawe na walinzi wa wenzao kwa sababu kila mmoja ana jukumu la kumlinda mwenzake. “Tusiachie majeshi kazi hii kwa sababu kila mmoja na jukumu la kwanza kujilinda yeye mwenyewe na kisha kumlinda jirani yake,” alisema.

Kwa upande wake,  Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh Ahmed Said alisema wanawaombea dua Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu katika kazi za kuleta maendeleo kwa Watanzania. “Pia tutaendelea kuiombea nchi yetu ili Mwenyezi Mungu azidishe amani yake na watu wake waishi kwa amani, upendo na utulivu,”  aliongeza.

Naye Waziri Mkuu mstaafu, Dk. John S. Malecela ambaye alikuwa miongoni mwa wazee maarufu walioalikwa kwenye futari hiyo aliwataka waalikwa wenzake waendelee kuwaombea viongozi wa kitaifa na kusisitiza kuwa kila mmoja ana wajibu wa kuombea amani ya Tanzania ambayo imedumu kwa miaka mingi iendelee kuwepo.

Katika hatua nyingine, Askofu wa Kanisa la Mennonite Tanzania Dayosisi ya Kati, Askofu Amos Muhagachi, ambaye alipewa fursa ya kutoa salamu fupi kwenye hafla hiyo, alisema kwenye mkoa huo hakuna magomvi ya kidini kwa sababu viongozi wa dini zote wanashirikiana kwa karibu sana.

“Hapa Dodoma Maaskofu tunashirikiana vizuri na Masheikh. Hivi sasa, masheikh vijana na wachungaji vijana wameanza kuiga haya tunayofanya, na zaidi ya yote tunashirikiana pia kuwaombea Rais wetu, Makamu wa Rais pamoja na wewe Mheshimiwa Waziri Mkuu,” alisema.

Rais Magufuli Akutana Na Spika Mstaafu Mhe Anne Makinda Pamoja na Balozi Wa Qatar Nchini Ikulu Dar Es Salaam Juni 16,2016

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na kumkaribisha Spika wa Bunge Mstaafu  na mwenyekiti mpya wa  Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Mama Anne Makinda Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16, 2016

Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika mazungumzo na Spika wa Bunge Mstaafu  na mwenyekiti mpya wa  Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Mama Anne Makinda Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16,2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiagana na Spika wa Bunge Mstaafu  na mwenyekiti mpya wa  Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Mama Anne Makinda Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16, 2016 baada ya kufanya mazungumzo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Balozi wa Qatar hapa nchini Mhe Abdallah Jassim Al Maadadi Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika mazungumzo na  Balozi wa Qatar hapa nchini Mhe Abdallah Jassim Al Maadadi Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiagana na Balozi wa Qatar hapa nchini Mhe Abdallah Jassim Al Maadadi baada ya kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16, 2016

Taarifa ya CCM kukanusha Tuhuma Zilizotolewa na Askofu Gwajima

0
0

Bila ya shaka mmepata habari kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuwa siku ya Jumapili ya tarehe 11/06/2016 akiwa kanisani kwake, Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima alitoa kauli za uongo, uchochezi na uchonganishi dhidi ya Chama cha Mapinduzi, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt John Pombe Magufuli, Viongozi wa CCM, Watendaji wa CCM na Serikali ya Awamu ya nne.

Mchungaji Gwajima amedai ati kwamba lipo kundi la wanaCCM wanaozunguka sehemu mbalimbali za nchi wakishawishi wanachama na wakimshawishi Mwenyekiti wa sasa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ili aendelee na Uenyekiti na kuleta hoja ya kutenganisha kofia ya Uenyekiti wa CCM na Urais wa nchi.

Napenda kuwafahamisha wana CCM, wapenzi wa CCM na wananchi kwa jumla kuwa madai hayo ya Mchungaji Gwajima ni uongo mtupu na hayana hata chembe ya ukweli. Ni mambo ya uzushi na hadithi ya kufikirika. 

Watu hao hawapo kwani kama wangekuwepo habari hizo zingekwishajulikana Chamani kupitia mfumo mahiri wa usalama na maadili wa ndani ya Chama cha Mapinduzi. Chama chenyewe kingekwishawatambua watu hao na kuwachukulia hatua zipasazo za udhibiti na nidhamu.

Kama mambo hayo yangekuwepo viongozi wa Chama wa Mikoa, Wilaya na Matawi waliofuatwa wangekuwa ndiyo wa kwanza kuwafichua. 

Habari za namna hiyo hazijapokelewa kutoka popote na kutoka kwa kiongozi yeyote wa Chama. Kama kweli Mchungaji Gwajima anawajua watu hao awataje hadharani na aseme walikwenda kumuona nani, wapi na lini kufikisha ujumbe wao huo hasi dhidi ya CCM.

Napenda kusisitiza kuwa habari za namna hiyo hazipo katika Chama cha Mapinduzi. Kwa hakika kinachoendelea sasa Mikoani na Wilayani ni maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum ambapo Mwenyekiti wa CCM wa sasa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atastaafu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli atachaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya. Hakuna jambo lingine.

Nafurahi kuwafahamisha Viongozi na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi kwamba kazi ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum inakwenda vizuri kabisa.

Shughuli hiyo inasimamiwa na Naibu Katibu Mkuu Bara Ndugu Rajabu Luhwavi kwa niaba ya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. 

Kwa mujibu wa hatua iliyofikiwa sasa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa inaweza kukutana siku yoyote kupanga tarehe ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM kwa uhakika.

Sisi katika Chama cha Mapinduzi hatushangazwi ingawaje tunasikitishwa na kauli za uongo, uchochezi na uchonganishi za Mchungaji Gwajima dhidi ya Chama cha Mapinduzi. 

Ana chuki iliyopitiliza dhidi ya CCM na Mwenyekiti wake. Yeye ni mtu ambae hajawahi kuitakia mema CCM. Hata yeye mwenyewe amekiri kwenye mahubiri yake ya tarehe 11 Juni, 2016 kuwa “alitaka CCM ishindwe katika chaguzi zilizopita na ndivyo anavyotaka iwe hivyo hata sasa, ili Chama chake cha upinzani kishinde.

Mchungaji Gwajima pia hana mapenzi na wala hamtakii mema Rais Dkt John Pombe Magufuli. Kwanza, hakutaka ashinde uchaguzi kwani alimpigania kwa hali na mali mgombea wa UKAWA. Pili, hataki adumu na kufanikiwa katika kazi yake ya Urais, ndiyo maana anatoa ushauri usiokuwa na mashiko na wakihasidi dhidi ya Mheshimiwa Rais. 

Anamshauri ati kwamba atoke Chama cha Mapinduzi na kuanzisha Chama chake. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais lazima awe mwanachama wa Chama fulani cha siasa. Hivyo basi, Rais John Pombe Magufuli akitoka CCM anapoteza Urais na Makamu wa Rais anakuwa Rais na CCM inaendelea kuongoza. Yeye atakuwa hana chake. 

Hivyo Rais wetu atakuwa amepata au atakuwa ameharibikiwa? Huo kweli ni ushauri wa mtu anayedai kuwa na mapenzi mema na Mheshimiwa John Magufuli? La hasha! Huo ni ushauri wa adui yake na wala siyo wa mtu rafiki na mwenye huruma na mapenzi na Rais wetu.

Mchungaji Gwajima anataka kufanya “danganya toto”. Napenda kumhakikishia yeye na genge lake kuwa “CCM hatudanganyiki na Rais Magufuli ndiyo kabisa “hadanganyiki na wala hababaiki”. 

Mheshimiwa John Pombe Magufuli siyo kama Bwana fulani aliyekubali kudanganywa na Gwajima na kudanganyika. Alitoka CCM akiamini kuwa angeshinda. Aliyomtabiria hayakuwa na sasa yeye na wenzake wanajuta na wengi wameanza kukimbia. 

Rais wetu mpendwa na Mwenyekiti wetu mtarajiwa hawezi kudanganyika kiurahisi namna hiyo. Mheshimiwa John Pombe Magufuli ni mtu makini na mahiri.

Shabaha ya Mchungaji Gwajima ni kutaka kuleta mfarakano ndani ya Chama cha Mapinduzi kwa kumchonganisha Rais na Mwenyekiti wa CCM. 

Anachotaka ni kukidhoofisha Chama cha Mapinduzi na kumdhoofisha Rais John Magufuli ili kupalilia Chama chake na mgombea wake washinde uchaguzi ujao.

Napenda kusema kwa kujiamini kuwa hilo halitatokea kamwe. Mwenyekiti Kikwete ni kada aliyelelewa na kupikika vyema na viongozi waasisi wa Chama na Taifa. 

Anaelewa na kuheshimu mila na desturi nzuri ya CCM kuunganisha kofia ya Urais na Uenyekiti. Hawezi kwenda kinyume. Hakung’ang’ania Urais, hawezi kung’ang’ania Uenyekiti na wala hana mpango huo.

Hali kadhalika, hata ushauri wake wa kutaka Marais Wastaafu waondolewe kinga ili washitakiwe, shabaha yake ni ile ile ya kutaka kuleta mfarakano baina ya Rais John Pombe Magufuli na Marais wastaafu kwa lengo lile lile la kutaka kuleta mfarakano ndani ya CCM na nchini. Matumaini yake ni yale yale ya kudhoofisha CCM na Rais wake ili kunufaisha upinzani. Kamwe Rais wetu hatanasa katika mtego huo.

Kwa kweli inasikitisha kuona Kiongozi wa dini akitumia madhabahu takatifu kusema uongo na kupanga fitina na kupandikiza chuki katika jamii. Hatutegemei Kiongozi wa dini kuwa hivyo. 

Hatukupenda kujibizana na Kiongozi wa dini lakini kwa vile ameacha ya dini na kuingilia ya upande wetu tumelazimika kusema. Wahenga wamesema “lisilobudi hutendwa”

Nawaomba wanaCCM na Wananchi kupuuza uongo, uzushi na ushauri hasi wa Mchungaji Josephat Gwajima.

Christopher Ole Sendeka.
Msemaji wa Chama Cha Mapinduzi.

Breaking News: Polisi Waizingira Nyumba ya Askofu Gwajima

0
0
Taarifa zilizotufikia muda huu zinasema Polisi 6 wakiwa ndani ya Landcruiser wamezingira nyumbani kwa Askofu Josephat Gwajima. 

Sababu za kufanya hivyo bado hazijafahamika, tutaendelea kuwajuza kadri tunavyoendelea kupata taarifa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 17

Serikali Mbioni Kufungua Ubalozi mpya Qatar

0
0

TANZANIA inatarajia kufungua ubalozi wake nchini Qatar kwa lengo la kuendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizo huku ikitilia mkazo katika sekta za gesi asilia, utalii, usafiri wa anga na mawasiliano.

Rais, Dk John Magufuli alisema hayo jana Ikulu, Dar es Salaam alipokutana na kuzungumza na Balozi wa Qatar nchini, Abdallah Jassim Al Maadadi. 

Pamoja na kutangaza kuufungua ubalozi wake nchini Qatar, Magufuli amemuomba balozi huyo kufikisha ujumbe kwa Kiongozi wa Qatar, Shehe Tamim bin Hamad Al Thani na Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Qatar kwamba zipo fursa nyingi za ushirikiano zinazoweza kufanyiwa kazi, huku akibainisha uwepo wa gesi asilia zaidi ya futi za ujazo trilioni 57 na mpango wa kufufua Kampuni ya Ndege ya Taifa (ATCL).

“Najua Qatar ina uzoefu katika maeneo hayo na sisi Tanzania tungependa tushirikiane nanyi kuwekeza na kubadilishana uzoefu ili fursa hizo zilete manufaa kwa pande zote mbili,” alisema Rais Magufuli.

Naye Balozi Al Maadadi alimshukuru Rais Magufuli kwa nia yake ya kufungua Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar na kuimarisha zaidi ushirikiano na uhusiano na nchi hiyo, na ameahidi kufikisha ujumbe kwa kiongozi wa Qatar na jumuiya ya wafanyabiashara Qatar waje kuwekeza Tanzania.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ambaye pia Spika mstaafu wa Bunge, Anne Makinda, Ikulu, Dar es Salaam.

Baada ya mazungumzo hayo, Makinda alisema mazungumzo yao yameihusu NHIF na kwamba amemhakikishia kuwa amejipanga kuona mfuko huo uliobeba matumaini ya huduma za matibabu ya Watanzania unaboreshwa zaidi na dosari zinazolalamikiwa na wanachama zinafanyiwa kazi.

Ofisa Usafirishaji wa Kampuni ya Athwal Transport & Timber LTD Afikishwa Kizimbani Kwa Kutoa Rushwa Ili Utingo Akiri Kosa la Wizi

0
0

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imemfikisha mahakamani Ofisa Usafirishaji wa Kampuni ya Athwal Transport & Timber LTD , Godfrey Tarimo, kwa mashitaka ya kutoa rushwa kwa mtumishi wa kampuni hiyo akiri kosa la wizi.

Tarimo alipandishwa kizimbani jana, mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya mkoa wa Tabora Jackton Rushwela .

Wakili wa Takukuru, Simon Mashingia alidai Tarimo alitenda kosa hilo Februari 13 mwaka huu katika Gereza la Uyui mjini hapa.

Wakili Mashingia alidai kuwa siku hiyo mshtakiwa akiwa ni Ofisa Usafirishaji wa ATT alitoa rushwa ya Sh 400,000 kwa Said Hamis ambaye alikuwa utingo wa gari katika kampuni ya ATT.

Akifafanua katika mashitaka hayo, wakili Mashingia alidai kuwa Tarimo akiwa kama wakala wa kampuni alitoa fedha hizo kama kishawishi kitakacho mfanya Hamisi akiri kosa la wizi katika kesi ya jinai namba 13/2015 iliyokuwa inamkabili.

Ilidaiwa kwamba, Hamisi baada ya kupokea fedha hizo alipofika mahakamani alikiri kosa ambapo Hakimu Rushwela alimpa adhabu ya kifungo cha miaka mitano jela. Mwendesha mashitaka alidai, uchunguzi umebaini kuwa Tarimo alipoteza tumbaku iliyokuwa inasafirishwa na magari ya kampuni ya ATT.

Alidai kwamba, ili kampuni hiyo isionekane ina sura mbaya katika biashara, walimbambikia kesi utingo huyo na kumshawishi akubali kuwa ndiye aliiba ili baadaye waweze kumsaidia atoke lakini alihukumiwa kifungo.

Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi Wasomwa .....Waliohukumiwa kwa Rushwa Kunyimwa Zabuni, Mikataba yote Kuwa na Mashuhuda

0
0

MUSWADA wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi wa Mwaka 2016, umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni jana na kuwekwa wazi kwa umma, na moja ya vifungu vinavyopendekezwa ni kuzuia mtu yeyote aliyewahi kuhukumiwa kwa rushwa, kufanya biashara na serikali.

Katika marekebisho hayo yanayopendekezwa na serikali, wizara, taasisi au shirika lolote la serikali wakati wa kufanya biashara na kampuni yoyote, ikibaini kampuni husika au mmoja wa wakurugenzi wake aliwahi kuhukumiwa kwa rushwa, biashara hiyo itasitishwa mara moja na taarifa kutolewa serikalini.

Mbali na watu waliohukumiwa kwa makosa ya rushwa, marekebisho hayo yamependekeza kuwa pamoja na sifa nyingine za viongozi wakuu wa serikali hasa maofisa watendaji wakuu, watapaswa kuwa na sifa ya ziada ya uzoefu katika masuala ya manunuzi.

Katika kukidhi haja ya kuondoa malalamiko ya sheria iliyopo kutumika kuibia nchi, marekebisho hayo yamesisitiza bei za huduma na bidhaa zitakazotolewa ziwe za soko, ununuzi ufanyike moja kwa moja kiwandani badala ya kupitia kwa mtu wa kati na mkataba wa manunuzi, lazima usainiwe mbele ya mashuhuda.

Watuhumiwa wa rushwa
Katika Ibara ya 83 ya Sheria hiyo, imependekezwa ibara ndogo ya pili kwamba shirika au wizara itakaporidhika kwamba kampuni au mtu anayependekezwa kupewa zabuni, amewahi kutangazwa na Mahakama kuwa alishiriki katika vitendo vya rushwa, ufisadi, au ukiukwaji wa taratibu wakati wa kushindania zabuni, ofisi hiyo ya umma itapaswa kukataa pendekezo la kumpa mhusika zabuni hiyo.

Ofisi hiyo ya umma, pia itapaswa kumtangaza mtu huyo au mzabuni ikiwa ni pamoja na wakurugenzi wake, kuwa hawapaswi kupewa zabuni yoyote inayogharimiwa na fedha za umma.

Pia ofisi hiyo ya umma, itapaswa kumtaka huyo mtu au mzabuni, kurejesha sehemu ya fedha aliyopewa kwa ajili ya ununuzi wa bidhaa au huduma au kuzuia sehemu ya fedha iliyopaswa kwenda kwa mzabuni kwa ajili ya ununuzi wa bidhaa au huduma.

Mapendekezo hayo yameendelea kuitaka ofisi husika ya umma ndani ya siku saba baada ya kutangaza kuwa mzabuni huyo, hafai kupewa zabuni inayogharimiwa na fedha za umma, kuwasilisha jina la mzabuni na wakurugenzi wake kwa mamlaka inayotajwa na sheria husika.

Mamlaka hiyo nayo imetakiwa na mapendekezo hayo ya sheria, kwamba baada ya kupata taarifa hiyo, kumfungia mtu au mzabuni husika asipate zabuni yoyote inayogharimiwa kwa fedha za umma, kwa muda usiopungua miaka 10.

Sifa za CEO
Katika mapendekezo kwenye Kifungu cha 23 cha Sheria hiyo, Kifungu Kidogo cha II, kimezungumzia uteuzi wa maofisa watendaji wakuu wa ofisi hizo za serikali.

Kifungu hicho kinaeleza kuwa ofisa mtendaji mkuu, atateuliwa kutoka kati ya wataalamu wenye uzoefu wa angalau miaka 10 katika fani za uhandisi, usanifu wa majengo, sheria, menejimenti ya ununuzi na usambazaji na ukadiriaji majengo.

Fani nyingine zilizotajwa ni pamoja na uongozi wa biashara, mipango ya kiuchumi na maendeleo au katika fani nyingine yoyote, lakini awe na uzoefu usio na shaka katika masuala ya ununuzi wa umma.

Bei ya soko
Katika Kifungu cha Tisa cha Sheria hiyo sehemu (o) imeitaka ofisi ya umma, wizara au taasisi ya umma, kila taasisi imetakiwa kuwa na taarifa ya bei ya soko ya bidhaa na huduma inayotumika mara kwa mara na ofisi husika kutoka katika ofisi husika ya umma ili kuhakikisha bei ya bidhaa na huduma zitakazonunuliwa, zinalingana na za soko.

Katika kuhakikisha ofisi za umma zinanunua bidhaa bora kwa bei ya soko, ununuzi wa umma umetakiwa kwa mujibu wa muswada huo, kufanyika kwa kuzingatia uaminifu wa hali ya juu, ushindani, uwajibikaji, kuzingatia kupunguza gharama, ufanisi, uwazi na kupata thamani ya fedha iliyotumika.

Aidha, ili kupata bei iliyo chini ya soko bila kuathiri ubora wa bidhaa au huduma, ofisi husika kwa nia ya kupata thamani ya fedha na ubora wa juu, imetakiwa kufanya ununuzi wa bidhaa na huduma mahususi moja kwa moja kutoka kwa mtengenezaji, au kiwandani, mwakilishi wa mtengenezaji au wa kiwanda, muuzaji wa jumla au mtoa huduma.

Wawekezaji wa ndani
Mapendekezo ya muswada huo, pia yametaka pale kampuni au taasisi ya umma inapolazimika kufanya ununuzi kutoka nje ya nchi, hasa kama ni suala la ushauri linafanywa na kampuni ya nje ya nchi, ofisi hiyo ya serikali inalazimika kuhakikisha kuna wataalamu wa ndani ya nchi.

Ushiriki huo wa wataalamu na kampuni za ndani katika shughuli za ushauri kutoka nje ya nchi, sheria hiyo imependekeza kuwa, kampuni yoyote ya ushauri ya nje ya nchi, inapoomba kazi katika kazi zinazogharimiwa na fedha za umma, lazima ishirikiane na kampuni, mshauri wa Kitanzania kwa asilimia mpaka 15.

Aidha, kampuni au mshauri huyo wa nje ili apewe zabuni katika shughuli ambazo zinagharimiwa na fedha za umma, kuna kigezo cha kuhakikisha wafanyakazi wa kampuni yake, zaidi ya asilimia 60 ni Watanzania.

Mbali na kuwa na asilimia 60 ya wafanyakazi Watanzania, kampuni husika lazima ieleze kiwango cha bidhaa na huduma zinazozalishwa ndani ya nchi, ambazo itazinunua katika utekelezaji wa shughuli zake.

Muswada huo unatarajiwa kujadiliwa na kupitishwa katika Bunge hili, ili kuzuia matumizi mabaya ya fedha za umma, ambazo katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa 2016/2017, asilimia 40 ya trilioni 29.53, imepelekwa katika miradi ya maendeleo.

Uenyekiti wa Rais Magufuli CCM Waiva......Kamati Kuu ya Chama Hicho Kukutana Dar es Salaam Kesho

0
0

Maandalizi ya CCM kumkabidhi Rais John Magufuli uenyekiti wa chama hicho ili ashike kofia zote mbili, yataanza kesho katika kikao cha Kamati Kuu kilichopangwa kufanyika jijini Dar es Salaam.

Taarifa kuhusu kikao hicho iliyotiwa saini na msemaji wa chama hicho, Christopher ole Sendeka ilisema: “Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM itafanya  kikao cha kawaida siku ya Jumamosi jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kitafanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete.”

Japokuwa taarifa hiyo haikueleza ajenda za kikao, habari kutoka ndani ya chama zinasema kikao hicho cha siku moja kinatarajiwa kujadili masuala mbalimbali, ukiwamo mchakato wa makabidhiano ya kiti hicho katika mkutano mkuu wa chama hicho utakaofanyika mwezi ujao.

Kipindi cha uongozi wa chama kwa Kikwete kitamalizika mwakani, lakini imekuwapo desturi kwa rais mpya kuachiwa kofia hiyo mapema, hivyo Rais Magufuli anatarajiwa kurithi mikoba ya uenyekiti mwezi ujao.

Vilevile, kikao hicho kinatarajiwa kuhitimisha hoja zinazodaiwa kuibuka katika vikao vya ndani vya chama hicho kwamba CCM inataka kuvuruga utaratibu uliodumu kwa muda mrefu wa mwenyekiti kumwachia kijiti Rais aliyeko madarakani.

Madai kuhusu mkakati huo wa ndani yalisambazwa katika mitandao ya kijamii yakimnukuu Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, lakini Ole Sendeka alisema hana sababu yoyote ya kumjibu kiongozi wa dini.

Februari 5, mwaka huu Kikwete alipokuwa anazungumza na wazee wa Manispaa ya Singida alisema sherehe za mwaka huu za maadhimisho ya miaka 39 tangu chama hicho kuanzishwa zilikuwa za mwisho kwake akiwa mwenyekiti, kauli ambayo iliashiria ataachia mapema uenyekiti.

Kwa desturi, wenyeviti wa CCM huwa wanaachia madaraka yao kabla ya muda wa uongozi wao kumalizika.

Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa alikabidhiwa chama na Alhaji Ali Hassan Mwinyi mwaka 1996 badala ya 1997 na Mkapa alimkabidhi Kikwete kiti hicho mwaka 2006 badala ya 2007.

Kulingana na kalenda ya chama hicho, Mkutano Mkuu wa CCM kumchagua mwenyekiti unapaswa kufanyika mwaka 2017, lakini utafanyika mwaka huu kuendeleza utamaduni wa kung’atuka mapema.

Habari kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa kinachoendelea sasa mikoani na wilayani ni maandalizi ya mkutano huo mkuu yanayosimamiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Bara, Rajabu Luhwavi kwa niaba ya Sekretarieti.

“Kikao hicho cha Kamati Kuu ndicho kitakachojadili ajenda za mkutano huo sambamba na kupanga tarehe ya kufanyika kwa mkutano mkuu,” zilieleza taarifa hizo.

Dk Magufuli anatajwa kuwa uongozi wake ndani ya CCM utakuwa wa kasi ya aina yake kutokana na hatua mbalimbali za ‘utumbuaji majipu’ anazozifanya ndani ya Serikali tangu Novemba 5, alipoapishwa kuwa Rais.

Wabunge UKAWA Wasusa Futari ya Waziri Mkuu

0
0

Wabunge wa vyama vinavyounda Ukawa jana walisusia futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ikiwa ni mwendelezo wa hatua za kususia shughuli zote zinazoongozwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson.

Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Riziki Ng’wale, alisema wamechukua hatua hiyo kutokana na Dk Tulia kuwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo. 

“Dk Tulia ndiye mgeni rasmi katika shughuli hiyo ya kufuturisha na sisi tumeamua kuwa hatutashiriki shughuli yoyote inayoongozwa naye,” alisema muda mfupi baada ya kutoka katika kikao cha wabunge wa kambi hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa.

Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea alisema wamekubaliana wabunge wote wa kambi ya upinzani waliofunga watakwenda kufuturu majumbani kwao. 

“Tumekubaliana hatutakwenda kufuturu bungeni na kila mbunge atakwenda kufuturu nyumbani kwake,” alisema.

Uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha wapinzani kilichoketi chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia.

Futari hiyo ilitangazwa na Dk Tulia tangu juzi na kusisitizwa jana baada ya kikao cha Bunge kuahirishwa mchana kuwa ingefanyika kwenye viwanja vya Bunge ambako wabunge wote walialikwa.

Kwa siku zaidi ya 10 sasa, wabunge hao wamekuwa wakisusa vikao vya Bunge vinavyoongozwa na Dk Tulia kwa sababu hawana  imani naye. 

Hali hiyo imefanya bajeti kuu kwa ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17 kuchangiwa na wabunge wa CCM tu baada ya Dk Tulia kuongoza vikao kila siku, akiingia asubuhi na jioni.

Polisi Wamuwinda Askofu Gwajima Kwa Masaa 7 Bila Mafanikio........Ni Baada ya Kusambaa kwa Video Akimsema Vibaya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

0
0
Polisi jana walipiga kambi kwa saa saba kwenye geti la nyumba ya Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, wakitaka kumkamata bila ya mafanikio.

Polisi hao walikuwa kama wageni wa askofu huyo wakisubiri wafunguliwe geti, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 10:10 jioni walipoamua kuondoka wakitumia gari aina ya Toyota Landcruser lenye namba za kiraia, ambalo kwa muda wote huo lilikuwa limeegeshwa pembeni mwa geti hilo.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha takriban miezi 16, kwa askari wa jeshi hilo kwenda nyumbani kwa askofu huyo na kushinda mbele ya nyumba yake kwa saa kadhaa, kabla ya kuondoka bila ya kumtia nguvuni.

Tukio hilo pia linatokea wakati kukiwa kumesambaa mkanda unaotoa sauti ya Askofu Gwajima, ikizungumzia kitendo chake cha kuamua kumuunga mkono Rais John Magufuli na kumshutumu Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ikiitaka afikishwe mahakamani kwa yote yaliyofanyika wakati wa utawala wake ambayo Rais wa sasa anayashughulikia.

Jana, mbele na nyuma ya gari hilo kulikuwa na askari waliokuwa wamevalia kiraia, kila mmoja akionekana kama anafanya shughuli tofauti, lakini wote wakionekana kuwa na lengo moja; kusubiri kufunguliwa lango la nyumba ya Askofu Gwajima.

Mbele ya nyumba walikuwapo askari watatu na raia wawili, mmoja mwanamke na mwingine mwanamume ambao baadaye ilibainika kuwa walikuwa wamezuiwa na askari hao baada ya kuonekana wakitokea mlango wa nyuma wa nyumba hiyo.

Mwandishi  alishuhudia mwanamke huyo akiitwa na askari aliyekuwa ndani ya gari na kuonywa kuepuka kutumika, kisha akarudishiwa simu yake ambayo walikuwa wakiishikilia.

Raia hao walisema, walifika kwenye nyumba hiyo kwa ajili ya kufanya tathmini ya matengenezo na baada ya kumaliza walipokuwa wanatoka wakakutana na askari hao na kukamatwa.

Askari hao wasikika wakisemezana kuwa kuna taarifa zinasambazwa kwenye simu kuwa nyumba ya kiongozi huyo wa kiroho, ambaye aliibuka kuwa maarufu mwishoni mwa mchakato wa Katiba Mpya, imezingirwa, wakati hakukuwa na kitu kama hicho.

Pia, askari hao walisikika wakieleza kushangazwa na kitendo cha wenyeji kutowafungulia geti hilo ili waingine.

“Mtu kama huna tatizo; ni raia mwema. Una sababu gani ya kukataa kufungua mlango? Afungue akutane na sisi wageni wake,” alisema mmoja wa askari hao wakati wakiongea baina yao.

“Tumekuja bila silaha, tunataka kuzungumza naye, hataki kufungua mlango, anataka nini sasa?” alihoji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime alipoulizwa alisema hajatuma askari yeyote nyumbani kwa Gwajima.

“Wapigie makamanda wengine kwa  sababu si kila anayeishi Kinondoni amefanya kosa Kinondoni,” alisema.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema wanamuhitaji askofu huyo.

“Kama uko na Gwajima mwambie tunamuhitaji.” Alipoulizwa wanamuhitaji kwa sababu gani, Kamanda Sirro alisema: “Tumepata clip (mkanda) inayosemekama ni ya kwake. Tunamtaka athibitishe kama hayo maneno ni ya kwake. Na kama ni yeye ameyasema, anaelewa nini kuhusu kile alichokizungumza kwa sababu hayo maneno ni ya kichochezi. Tupo kwenye uchunguzi .”

Askofu Gwajima si mgeni wa matukio kama hayo dhidi ya mamlaka.

Mwaka 2012 aliingia kwenye mzozo na Jeshi la Polisi baada ya kijana mmoja kudai amejisalimisha kanisani kwake kutubu, baada ya kushiriki kwenye tukio la kumteka kiongozi wa madaktari, Dk Steven Ulimboka.

Hata hivyo, Askofu Gwajima aliekeza kuwa kijana huyo hakuwahi kufika kwenye kanisa hilo, wala kukutana naye na kwamba taarifa hizo zililenga kuchafua kanisa lake.

Mwaka 2015, Askofu Gwajima aliingia kwenye mgogoro mwingine na Jeshi la Polisi baada ya mkanda wa sauti ya mahubiri kanisani kwake kutoa maneno yaliyoonekana kukashifu msimamo wa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Dar es Salaam, Kardinali Polycarp Pengo dhidi ya tamko la maaskofu wa Jukwaa la Wakristo la kuwataka waumini wao wasipige kura ya maoni kupitisha Katiba Inayopendekezwa.

Katika sakata hilo, Askofu Gwajima alifunguliwa shtaka la kutoa lugha ya matusi dhidi ya Kardinali Pengo, na kushindwa kuhifadhi silaha na risasi wakati akiwa hospitalini.

Kabla ya kufunguliwa mashtaka hayo, askari walizingira nyumba yake kwa takriban saa saba, lakini hawakufanikiwa na siku iliyofuata kiongozi huyo alijisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam.

Akiwa huko aliugua na baadaye kulazwa. Polisi walitangaza kukamata watu 15 wakiwatuhumu kuwa walikuwa na mpango wa kumtorosha na kukamata silaha hiyo pamoja na risasi walizodai walizikuta kwenye gari.

Mjadala wa Mikoa Masikini Waligawa Bunge

0
0
TAKWIMU kuhusu mikoa mitano masikini zaidi nchini, zimezidi kuzua mjadala bungeni huku wabunge wakizitumia kutaka misaada zaidi katika mikoa yao na wengine wakidai zinawafanya wahofu kwamba kuna ajenda ya siri kwani hawaamini usahihi wake.

Katika mjadala wa jana kuhusu bajeti inayopendekezwa na serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17, aliyeanza kulalamikia takwimu hizo na kukataa kuunga hoja hiyo ya serikali ni Mbunge wa Rufiji, Mohamed Mchengelwa.

Mbunge huyo wa CCM alisema katika utafiti wake, amegundua kwamba waziri alipata takwimu hizo kutoka halmashauri, lakini akasema yeye ametafiti na kugundua kwamba kamwe Pwani haiwezi kuuzidi mkoa wa Mwanza kwa utajiri kama takwimu hizo zinavyoonesha.

Alisema takwimu hizo zinaonesha kana kwamba mkoa wa Pwani, una hali nzuri wakati si kweli, kwani hali ni mbaya, vyama vya msingi takribani vyote vimeanguka na kwamba anapata hisia kuwa takwimu hizo, zimetumiwa kuinyima Pwani mambo mengi katika bajeti inayopendekezwa.

“Rufiji, kwa mfano haijawahi hata kupelekewa trekta… Hali ni mbaya na hata bajeti kwa ajili ya kuinua kilimo Rufiji hakuna. Mimi kama mwanasheria niko tayari kuapa kuonesha kwamba takwimu alizotumia Waziri si sahihi,” aling’aka.

Naye Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega (CCM), alisema anadhani mkoa wa Pwani umewekwa kwenye kundi la mikoa tajiri kwa bahati mbaya, kwani akitazama kila kitu hakiendi vizuri.

“Hata korosho ambalo ndilo zao kuu la biashara mkoa wa Pwani tuko chini, hatuwezi kulingana na wenzetu wa Lindi au Mtwara,” alisema na kutaka waziri aeleze vigezo vilivyotumika kuainisha mikoa yenye hali mbaya kiuchumi nchini na yenye hali nzuri.

Lakini Mbunge wa Nyamagana mkoa wa Mwanza, Stanslaus Mabula (CCM), alitumia takwimu hizo kutaka serikali kuanza kwa kuupa mkoa huo Sh milioni 50 zilizoahidiwa katika kila kijiji ili wananchi wa mkoa huo wapunguze ‘umasikini wao’.


 “Ninaomba hizi shilingi milioni 50, zianzie katika mikoa iliyoainishwa kuwa masikini kwa mujibu wa takwimu za waziri ukiwemo mkoa wangu wa Mwanza,” alisema Mabula.

Naye Mbunge wa Bukoba Vijijini (CCM), Jason Rweikiza alitumia takwimu hizo kutaka serikali kuwaondolea wakulima wa kahawa kodi 26 wanazolazimika kulipa pamoja na kudhibiti ugonjwa wa mnyauko unaoshambulia migomba ili kuwaokoa wananchi wa Kagera na umasikini.

“Kahawa inakatwa kodi 26, kwa nini wananchi wasiwe masikini? Migomba inaelekea kumalizika kabisa kwa sababu ya ugonjwa wa mnyauko, kwa nini wananchi wasiwe masikini,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu, Maria Kangoye anayewakilisha mkoa wa Mwanza alipinga takwimu zinazoonesha kwamba mkoa huo ni miongoni mwa mikoa mitano masikini nchini.

Alisema takwimu za Benki Kuu (BoT) zinaonesha kwamba Mwanza ni mkoa wa pili nyuma ya Dar es Salaam katika kuchangia kwenye Pato la Taifa.

Akiwasilisha bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi ya Mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/17, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alitaja mikoa masikini zaidi kuwa ni Kigoma, Geita, Kagera, Singida na Mwanza; wakati mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Arusha, Pwani na Manyara ndiyo mikoa mitano yenye ahueni ya umasikini nchini.

Akiuliza swali la papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, Oscar Mukasa (CCM), alisema utafiti kuhusu kipato cha kaya, umebaini mikoa mitano inayokabiliwa na umasikini uliokithiri na kumtaka Majaliwa kueleza serikali itafanya nini katika mikoa hiyo ili iondokane na aibu wakati ina fursa za kiuchumi ikiwemo kilimo cha pamba, mibuni na michikichi.

Majaliwa alisema serikali haijaacha jambo hilo kama lilivyo, bali imekuwa ikishawishi wananchi kujianzishia miradi na wengine waunde vikundi, ikiwemo vya Vicoba ili kujijengea mtaji wa pamoja ili waanzishe miradi hiyo.

Alisema kwa Tanzania msingi mkubwa wa kuondokana na umasikini ni kilimo na maeneo ya kulima yapo, ndio maana Serikali inasema ‘Hapa Kazi Tu’ ili watu wajikite katika kilimo.

Tanzania Kuanza Kutumia Kiswahili Katika Mikutano Yote ya Kimataifa

0
0

TANZANIA inatarajiwa kuanza kutumia Kiswahili katika mikutano yote ya kimataifa itakayowakilishwa na viongozi wake baada ya serikali kukamilisha kutuma wataalamu watakaotafsiri lugha hiyo kwa watumiaji wa lugha nyingine duniani.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alisema hayo jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Zainabu Vulu (CCM).

Vulu katika swali lake alihoji namna serikali inavyoenzi lugha ya Kiswahili ambayo ilitumika na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuunganisha Taifa na inatumiaje fursa ya kutumika kwa lugha hiyo kimataifa, kuwa ajira kwa Watanzania.

Akifafanua jibu lake, Majaliwa alisema tayari serikali ilishaamua Kiswahili kuwa lugha rasmi ya kutumika serikalini na hata bungeni na sasa lugha hiyo imekua zaidi na kuwa moja ya lugha rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Kwa mujibu wa Majaliwa, tayari duniani kote vyuo vikuu vimeanza kufundisha Kiswahili, hali iliyosababisha kuongezeka kwa mahitaji ya walimu wa kufundisha lugha hiyo kutoka Tanzania.

Kutokana na uhitaji huo, Majaliwa alisema vyuo vikuu karibu vyote nchini, vinafundisha walimu wa lugha hiyo kwa ajili ya kukidhi mahitaji hayo ya kimataifa, lakini pia serikali inajiandaa kupeleka wataalamu wa kutafsiri Kiswahili kwenda katika nchi mbalimbali.

Alisema lengo la serikali kupeleka wataalamu hao katika nchi mbalimbali ni kuwezesha viongozi kutoka Tanzania wanapokwenda katika mikutano ya kimataifa, watumie Kiswahili na wataalamu hao watoe tafsiri kwenda kwenye lugha nyingine za kimataifa.

Alisema kwa sasa Tanzania imeshapeleka walimu wa lugha hiyo Burundi, Rwanda, Uingereza na Ufaransa ambako wanafundisha lugha hiyo na kati ya lugha kubwa za kimataifa, Kiswahili kama si lugha ya sita ni ya nane.

Naye Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima (CCM), alimtaka Waziri Mkuu kuangalia uwezekano wa kuruhusu wabunge kuwa wajumbe wa kamati za ulinzi na usalama za wilaya na mikoa.

Akijibu ombi hilo, alisema wajumbe wa kamati hizo katika wilaya, mikoa na kitaifa, wameainishwa na Sheria ya Usalama wa Taifa kuwa ni wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, ambao ni tofauti na mbunge ambaye ni mwakilishi wa wananchi kisiasa.

Alisema majukumu yao ni kuangalia hali ya usalama kwa undani, lakini sheria hiyo haijamzuia mbunge au mwananchi yeyote, kwenda kutoa taarifa kama ilivyotokea katika mauaji ya hivri karibuni, ambapo kamati hizo kutokana na ushirikiano kutoka kwa wananchi, wahusika wameanza kukamatwa mmoja baada ya mwingine.

Wabunge wengine wasimamishwa kuhudhuria vikao leo June 17 2016

0
0

Leo June 17 2016 idadi ya wabunge kusimamishwa imeongezeka baada ya Naibu Sika, Tulia Ackson kutangaza kusimamishwa kwa wabunge wawili ambao ni Mbunge wa viti Maalum CHADEMA Suzan Lyimo na Anatropia Theonest.

Mbune Suzan Lyimo amesimamishwa na Bunge kuhudhuria vikao vitano vya Bunge baada ya kubainika kusema uongo kwamba Jeshi la polisi nchini limenunua magari 777 ya washawasha wakati ukweli ni kwamba hiyo ni Idadi ya magari inayopangwa kuingizwa na jeshi hilo kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Licha ya Mbunge kuonesha ushirikiano kwa kamati ya maadili, haki na madaraka ya bunge, kamati imemwona Mbunge ni mzoefu wa shughuli za bunge hivyo anapaswa kusimamishwa vikao hivyo kuanzia June 17 hadi 24 mwaka huu.

Aidha Mbunge Anatropia Theonest amesimamishwa kuhudhuria vikao vitatu vya bunge kwa kosa la kulidanganya Bunge kuwa waziri wa ardhi na nyumba William Lukuvi alichukua ardhi ya wananchi akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Ateuliwa Kuwa Balozi wa Heshima

0
0

KITUO cha Ufundi cha Kilimo na Maendeleo Vijijini (Technical Centre for Agricultural and Rural Cooperation, CTA) kilicho chini ya Umoja wa Ulaya (EU) chenye makao makuu mjini Wageningen, Uholanzi kimemteua Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete kuwa Balozi wa Heshima (Goodwill Ambassador) wa Maendeleo ya Kilimo katika Mabara ya Afrika, Karibiani na Pacific.

Katika barua iliyokabidhiwa na mjumbe wa Bodi ya CTA, Prof. Faustin Kamuzora, CTA wameainisha kuwa Dk. Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, ameteuliwa kwa kutambua mchango na juhudi zake katika kukiendeleza kilimo nchini Tanzania na barani Afrika.

Katika wadhifa wake huo mpya, CTA imemuomba Dk. Kikwete aweze kuiwakilisha katika makongamano ya kimataifa ambapo atazungumzia umuhimu wa kukiendeleza kilimo kwa ajili ya kutoa fursa ya ajira zenye staha na uhakika kwa vijana na wanawake katika nchi za barani Afrika, Karibiani na Pasifiki. Pia ataisaidia CTA katika kuandaa makala na kufanya mahojiano na waandishi wa habari katika nchi mbalimbali.

Dk. Kikwete amekubali uteuzi huo na kuahidi kushirikiana na CTA katika kutekeleza mambo ambayo ameombwa kusaidiana na taasisi hiyo ambayo ni ya ushirikiano wa Umoja wa Ulaya na Kundi la nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki wenye makao makuu mjini Brussels, Ubelgiji.

Prof. Kamuzora ambaye pia ni Katibu Mkuu, Mawasiliano ni mjumbe wa Bodi ya CTA akiwakilisha nchi za ukanda wa Afrika Mashariki kwa miaka mitano tangu 2013 hadi 2018.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images