Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Umoja wa Mataifa Wamsifu Rais Magufuli Kwa Kupambana na Rushwa na Kukusanya Mapato Mengi

$
0
0

SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limeeleza kuridhishwa kwake na utendaji wa Rais John Magufuli katika mapambano ya rushwa, kuongeza uwajibikaji na ukusanyaji wa mapato.

Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini, Alvaro Rodriguez, alisema hayo jana katika semina ya wabunge kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikipambana na rushwa na kusimamia kwa karibu ukusanyaji mapato, hali aliyosema itasaidia maendeleo kwa kuwa hakuna nchi iliyoendelea bila kuchapakazi.

Rodriguez alisema mbali na kuona maendeleo katika baadhi ya mikoa na mitaa, ameona jitihada hizo za Serikali na amefurahishwa na kuridhika nazo.

Mwakilishi huyo pia alisema Serikali ya Tanzania na Ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN), zimekuwa zikifanya kazi pamoja katika harakati za usambazaji wa malengo ya dunia kwa Watanzania.

Alisisitiza umuhimu wa malengo hayo kueleweka kwa wabunge, ili katika jukumu lao la kuisimamia Serikali, wawe mabalozi wa utekelezaji wa malengo hayo katika ufuatiliaji kwenye ngazi zote za utawala.

Awali akifungua semina hiyo, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson aliwataka wabunge kuoanisha malengo hayo na malengo ya Dira ya Taifa ya 2025 pamoja na malengo ya Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano wa 2016/2017 mpaka 2020/2021 ambao ulishafikishwa bungeni.

Dk Tulia aliwataka wabunge kila mmoja kuyaelewa vizuri malengo hayo ili kila mmoja ashikilie mahali atakapofuatilia Serikalini wakati wa utekelezaji wake.

Miongoni mwa malengo hayo ni pamoja na kutokomeza umasikini wa kila aina, kufuta njaa kwa kuhakikisha kuna kuwa na uhakika wa chakula bora kwakuboresha kilimo endelevu, kuhakikisha watu wote wanakuwa na afya bora nakupata huduma za afya na kupunguza utofauti wa kipato.

Akitoa mada katika semina hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Paul Kessy, alisema Tanzania imeshiriki kwa kiasi kikubwa katika maandalizi ya malengo hayo na hivyo mchango wake kuwa sehemu ya maudhui ya malengo hayo endelevu kwa maslahi mapana ya taifa na watu wake.

Kwa mujibu wa Kessy, sehemu ya mchango wa Tanzania katika kuunda malengo hayo, ilikuwa ni kutaka malengo hayo yahakikishe kuwa baadhi ya masuala ambayo hayakukamilika katika utekelezaji wa Malengo ya Milenia yanazingatiwa katika malengo endelevu.

Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na kupunguza umasikini, upatikanaji wa ajira na kukuza uwezo wa nchi masikini hasa katika maendeleo ya teknolojia.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yawashukia Waangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU)

$
0
0

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ufafanuzi kuhusu ripoti ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana, iliyowasilishwa na Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU).

NEC imesisitiza kwamba ripoti hiyo imebainisha mapungufu ambayo hayapo kwenye sheria na taratibu, zinazoiongoza tume hiyo.

Miongoni mwa mapungufu waliyoyatoa waangalizi hao ni Suala la Uchaguzi wa Zanzibar, Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 na haki ya wagombea binafsi kugombea nafasi katika uchaguzi wowote wa Tanzania Bara na Zanzibar, mgawanyo wa majimbo na uwazi wa kuhesabu kura.

Akitoa ufafanuzi huo, Mkurugenzi wa NEC, Ramadhan Kailima alisema kuwa kwa mujibu wa sheria, waliwapa nafasi hiyo waangalizi wa ndani na nje kuangalia uchaguzi wa Tanzania Bara , kama unaenda kulingana na Katiba, sheria na taratibu za uchaguzi huo.

Alisema kuwa katika ripoti hiyo, waangalizi hao wamezungumzia uchaguzi wa Zanzibar, ambao NEC hawahusiki nao na kwamba wamefanya makosa, kwa kuwa wao walikuwa waangalizi wa uchaguzi wa Tanzania Bara na sio Zanzibar.

‘’Waangalizi wowote wa uchaguzi wanapoomba kibali kuangalia uchaguzi, wanatakiwa kufuata taratibu kwa kutambua kwamba kuna NEC na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC). Sisi tulitoa kibali kwa waangalizi hawa kuangalia uchaguzi wetu na sio wa Zanzibar,’’ alisema.

Aliongeza kuwa, ‘’hawakupaswa kuingiza katika ripoti yao masuala ya uchaguzi wa Zanzibar ulivyokuwa, badala yake wangeeleza kama NEC hatukufuata sheria na taratibu kwenye uchaguzi huu wa Tanzania Bara.”

Alisema pia kuwa waangalizi walitakiwa kuangalia uchaguzi huo na sio kupendekeza kwamba uchaguzi ulitakiwa kuwa vipi. 

Kuhusu suala la mgombea binafsi, alisema Katiba iliyopo sasa haijaruhusu, hivyo wasingeweza kuweka wagombea hao, kwani Katiba ingewabana.

Kailima alisema kuwa endapo Katiba Inayopendekezwa ingepitishwa, waangalizi hao wangeweza kuhoji kwa nini hakukuwepo na mgombea binafsi, kwani ndiyo inaeleza kuhusu mambo hayo.

Akizungumzia mgawanyo wa majimbo, Kailima alisema kuwa kila halmashauri ya mji na wilaya ni jimbo na kwamba hawapaswi kulinganisha kati ya Halmashauri ya Temeke yenye watu 419,612 na jimbo la Madaba lenye watu 27,502, kuwa mgawanyo wake haukufuata uwiano.

Alisema kuwa mgawanyo wa majimbo, huzingatia mambo mengi, ikiwemo jiografia ya eneo lenyewe. Alieleza pia kuwa NEC haijawanyima haki Wazanzibari kwa kutoongeza idadi ya majimbo, kwa kuwa Bunge ambalo lilitakiwa kujadili, lilikuwa limekamilisha kazi yake.

Alisema kwamba ZEC yenyewe ilichelewa kutangaza mabadiliko hayo ya majimbo kutoka 50 hadi 54.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa kwa mara ya kwanza Tanzania matokeo ya uchaguzi wa Madiwani na Wabunge yalikuwa yanabandikwa kwenye vituo vya kupigia kura pamoja na matokeo ya awali ya Rais.

Alisisitiza kuwa matokeo yote, yalikuwa yanasainiwa na wawakilishi kutoka vyama mbalimbali vya siasa na kutangazwa kwa wananchi.

Aidha, alisema kuwa hawakuweza kutangaza wabunge wa viti maalumu kabla ya uchaguzi, kwani kisheria wanachagua wagombea hao baada ya kujua idadi ya kura ya asilimia tano zilizopata chama, hivyo wasingeweza kutangaza kabla ya uchaguzi.

Hata hivyo, alisema kuwa Tume hiyo imepokea mapendekezo yao na itayafanyia kazi ikiwemo kuwa na watumishi kwa ngazi zote. Kailima alisema kuwa hali hiyo, itawasaidia kujua namna ya kuwaadhibu watumishi ambao watakiuka utaratibu wa NEC.

‘’Pia tutaongeza muda wa daftari la kupiga kura kuhakikisha kwamba kwa mwaka linakuwepo mara mbili ili wapiga kura wote waangalie. Lakini suala la Sheria ya Makosa ya Mtandao wanatakiwa kulipeleka kwa wahusika na mengine kwa serikali kwani sisi kama NEC hatuhusiki nayo,’’ alisema.

UKAWA Wamkimbia Naibu Spika nje ya Bunge

$
0
0

MSIMAMO wa wabunge wa upinzani wa kususia kushiriki vikao vya Bunge vinavyoongozwa na Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson umechukua sura mpya.

Jana wabunge hao walitoka ndani ya ukumbi wa Pius Msekwa uliopo bungeni mjini Dodoma  baada ya kiongozi huyo kupewa nafasi ya kufungua semina ya wabunge kuhusu Malengo Endelevu ya Dunia.
 
Semina hiyo ilikuwa imeandaliwa na Umoja wa Mataifa kupitia mpango wake wa kufanya kazi pamoja (Delivering as One).

Wabunge wa upinzani wanaotoka vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), walitoka ndani ya ukumbi huyo baada ya Naibu Spika huyo kupewa nafasi ya kufungua semina hiyo iliyoanza saa nne asubuhi.
 
Wabunge hao walirejea ukumbini na kushiriki semina hiyo baada ya Dk. Ackson kumaliza kuwasilisha hotuba yake.
 
Kususa kwa wabunge hao jana kulikuja baada ya kuwa walikuwa wamesusa kuhudhuria vikao vya Bunge vilivyoongozwa na Dk. Ackson kwa siku nne mfululizo mpaka Ijumaa.
 
Kambi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikifanya hivyo dhidi ya Naibu Spika huyo tangu uongozi wa kambi hiyo utangaze kutokuwa na imani naye Jumatatu.
 
Tayari wabunge hao wamewasilisha hoja ya azimio la kutaka kumng'oa madarakani yenye sababu sita.
 
Jumanne iliyopita, kambi hiyo ilianza utaratibu huo wa kutoka kwenye ukumbi wa Bunge mara tu baada Naibu Spika kuingia.
 
Upinzani unachodai kutoridhishwa na uendeshwaji wa chombo hicho cha kutunga sheria chini ya Naibu Mwanasheria Mkuu huyo wa zamani wa serikali.
 
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, alitangaza Jumatatu kuwa upinzani hauna imani na Naibu Spika na hautakuwa tayari kushiriki vikao vinavyoongozwa na kiongozi huyo wa Bunge hadi pale "haki itakapopatikana".
 
Kutokana na msimamo huo, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe, aliuomba uongozi wa Bunge kutolipa mishahara na posho za wabunge wa kambi hiyo waliosusa Jumanne.
 
Hata hivyo, Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa, aliponda pendekezo hilo .
 
"Kama tuliacha posho ya Sh. milioni 30 za Bunge la Katiba, itakuwa hii ya vikao vya Bunge la Bajeti ambayo haifiki hata milioni tano?” Alihoji Mchungaji Msigwa.
 
"Hoja hapa si fedha, hoja ni misingi ya uendeshaji wa Bunge. 
 
"Hatuwezi kukubali kuburuzwa eti kwa sababu tunapewa posho."


Waliotimuliwa UDOM Waibuka, Watishia Kuishitaki Serikali

$
0
0

Sakata Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) limezidi kupanuka baada ya wanafunzi waliorudishwa nyumbani kupinga kuitwa vilaza.

Jana wawakilishi wa wanafunzi hao ambao waliambatana na viongozi wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), walisema wanapinga pia hatua ya kutimuliwa chuoni.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Gibson Johnson alisema wanasikitika kuona wanavyozushiwa tuhuma mbalimbali kuhusiana na wao kujiunga na chuo hicho.

Alisema wamekuwa wakijiuliza sababu za Serikali zinazotaka kuhalalisha kutimuliwa kwao chuoni kuwa hawakuwa na sifa, jambo ambalo si la kweli.

 “Siyo kweli kwamba sisi ni vilaza (wanafunzi wasiofanya vizuri darasani) na waliofeli na kupata daraja sifuri.

“Sisi ni wanafunzi tuliofaulu kwa viwango vilivyohitajika kwa daraja la kwanza hadi la tatu na tulipangiwa shule za kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita, lakini tulibadili na kuamua kujiunga Udom, hivyo tunaomba Serikali itumie busara zake.

“Hatuwezi kwenda kusoma kidato cha tano na sita kwa kuwa tumepoteza muda wetu.”

Alisema wanamshauri Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako na Rais John Magufuli kutumia busara kuwarudisha chuoni kumalizia masomo yao.

Katibu Mkuu wa TSNP, Alphonce Lusako aliitaka  Serikali ichukukue hatua kwa waliohusika kudahili wanafunzi wasio na vigezo na kuwawajibisha.

“Lakini pia wanafunzi wafidiwe fedha na muda waliopoteza kwa wakati wote waliokuwa chuoni, kama hawatapewa haki zao, sisi tutashirikiana na wadau wa elimu zikiwamo asasi za utetezi wa kisheria kutafuta haki mahakamani,alisema Lusako.

Udom yazungumza
Ofisa uhusiano wa Udom, Beatrice Baltazali alisema wanafunzi hao wote walifaulu vizuri wakiwa na daraja la kwanza, pili na wachache daraja la tatu.

“Wanafunzi wote walikuwa na nafasi ya kwenda kidato cha tano, lakini kwa kuwa waliahidiwa ajira, waliona wapitie huku kwa kuwa watapata ajira ya moja kwa moja,” alisema.

Beatrice alisema walimu wa Udom walikuwa wanalipwa fedha za ziada kuwafundisha wanafunzi wa programu hiyo kwa kuwa walikuwa wanatumia muda mwingi zaidi ya kiwango walichokuwa wamepangiwa.

“Kutokana na madai ya malipo hayo, mkaguzi wa ndani aligundua kuna tatizo, ndiyo walimu nao wakaamua kugoma, wanafunzi wakawa hawafundishwi Serikali ikaamua warudishwe nyumbani,” alisema Beatrice.

Rais Magufuli Ahudhuria Ibada Katika Kanisa La Maombezi La Mchungaji Antony Lusekelo ‘Mzee Wa Upako’ Ubungo Kibangu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amelitembelea Kanisa la Maombezi linaloongozwa na Mchungaji Antony Lusekelo (Mzee wa Upako) lililopo Ubungo Kibangu Jijini Dar es salaam na kuwaahidi waumini wa kanisa hilo kuwa Serikali yake itatengeneza barabara ya kutoka Ubungo Kibangu hadi River Side ambako itaungana na barabara ya Mandela.

Rais Magufuli ambaye amezungumza katika ibada ya asubuhi ya Kanisa hilo iliyofanyika leo tarehe 05 Juni, 2016 amesema amepita katika barabara hiyo ambayo imekuwa ikitumiwa na waumini wa kanisa hilo na wananchi wengine wa eneo la Ubungo Kibangu kwa lengo la kujionea hali halisi.

Aidha, Rais Magufuli amempongeza Kiongozi wa Kanisa hilo Mchungaji Antony Lusekelo maarufu kwa jina la Mzee wa Upako kwa huduma ya maombezi anayoitoa kwa waumini wake na watazamaji wanaofuatilia vipindi vyake vya Mahubiri kupitia Luninga.

“Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa mahubiri yako, kwa hiyo mahubiri unapoyatoa yanasambaa, kwa kweli mimi na familia yangu huwa yanatubariki sana, kwa hiyo nataka kukuthibitishia ninakupenda sana.

“Ndio maana kuna siku moja, ulizungumza kuhusu shida ya barabara yako ikabidi nitafute mbinu za namna gani tunaweza kuishughulikia kwa utaratibu ulio wazi, nikamtuma meneja wa barabara wa Mkoa wa Dar es salaam, akaja, akaipitia na akafahamu changamoto zilizopo, akafanya upembuzi yakinifu na usanifu, nataka kukuthibitishia kuwa fedha za kutengenezea barabara hii zipo” Amesema Dkt. Magufuli huku akishangiliwa na waumini.

Kwa upande wake Kiongozi wa Kanisa la Maombezi Mchungaji Antony Lusekelo (Mzee wa Upako) amemshukuru Rais Magufuli kwa kulitembelea kanisa hilo, na amemuombea heri katika uongozi wake ili aweze kufanikisha azma ya kuliletea taifa maendeleo ikiwemo mpango wa kuanzisha viwanda.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
05 Juni, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 6

Mikataba ya Polisi Yaitishwa Wizarani

$
0
0
BAADA ya Rais John Magufuli kuizungumzia mikataba ya ujenzi ya Jeshi la Polisi iliyoingia na wawekezaji, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ameitisha mikataba yote ya jeshi hilo.

Jeshi la Polisi nchini limetakiwa kuwasilisha mikataba ya miradi ya ujenzi wa nyumba za kuishi askari eneo la Kunduchi, Mikocheni pamoja na Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar es Salaam pamoja na ule wa majengo mbalimbali ya mwekezaji ambaye Jeshi la Polisi limeingia mkataba naye.

Agizo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira ikiwa ni miezi miwili tu tangu Rais Magufuli kuzungumzia mikataba hiyo na kuitilia shaka wakati akifungua kikao kazi cha makamanda wa Polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa mikoa na vikosi mjini Dodoma.

Meja Jenerali Rwegasira alisema mradi huo ni mkubwa na wa muda mrefu na hivyo ameliagiza jeshi hilo kuuwasilisha mkataba huo, ambao utekelezaji wake unaendelea ili aufahamu vizuri mkataba huo, unaolihusisha Jeshi la Polisi na Mwekezaji wa Kampuni ya Mara World Tanzania Limited.

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo jana kwa vyombo vya habari, Katibu Mkuu huyo ametoa agizo hilo muda mfupi baada ya kukagua miradi hiyo katika maeneo ya Kunduchi na Mikocheni, ambako zinajengwa nyumba za kuishi askari wa Jeshi la Polisi na kwamba ujenzi wake bado unaendelea.

Mradi mwingine alioutembelea ni ujenzi wa Kituo cha Polisi eneo la Polisi Oysterbay na kuona maendeleo ya ujenzi huo sambamba na kufahamu hatua iliyofikiwa hadi sasa katika maeneo hayo ya Jeshi la Polisi.

Katika mradi huo wa Ujenzi wa Kituo cha Polisi Oysterbay, unaotekelezwa na mwekezaji Kampuni ya Mara World Tanzania Limited, pia kutajengwa ofisi za kukodisha, hospitali, maduka makubwa na hoteli.

Rais Magufuli wakati akihutubia makamanda hao wa Polisi Aprili mwaka huu, alisema miongoni mwa vitu ambavyo vinalisumbua jeshi hilo ni mikataba ya hovyo akisisitiza umuhimu wa fedha za jeshi hilo kutumika vizuri.

Rais Magufuli alisema kuna taarifa zinaonesha Jeshi la Polisi, limekuwa likihusishwa na matumizi mabaya ya fedha, hali inayoongeza ukubwa wa matatizo yanayokwamisha utendaji wake wa kazi.

Alitoa mfano wa taarifa za matumizi mabaya ya fedha, zinazotolewa kwa ajili ya kununua vifaa na sare za askari ama mikataba yenye mashaka inayotiwa saini kati ya Polisi na wawekezaji kuwa ni baadhi ya mambo yanayoongeza hali ngumu ya utendaji kazi kwa jeshi hilo.

“Oysterbay pale ni eneo ambalo ni zuri sana, kila mmoja anajua, mmeingia kwenye mikataba mnayoijua ninyi, mkapewa mtu anawajengea pale, sifahamu kama majengo hayo yanafaa.

“Palikuwa na ubaya gani eneo la Oysterbay likawa na hati, mkaitumia hiyo hati kwenda kukopa benki na kujenga nyumba hata za ghorofa 20 pale, mkaweka kitega uchumi na polisi wenu wakakaa pale?

“Nimesema lazima nizungumze kwa uwazi, nisiposema kwa uwazi nitajisikia vibaya nikimaliza mkutano huu. Nataka muelewe na muelewe ukweli mwelekeo ninaoutaka mimi,” alisema Rais Magufuli.

Bunge Kuzungumzia Sakata la Naibu Spika, Dk Tulia Ackson

$
0
0

KATIBU wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah leo ataeleza kinachoendelea kuhusu kusudio la Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutaka kumwondoa madarakani Naibu Spika, Dk Tulia Ackson (pichani).

Kambi hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe katika migomo yake dhidi ya vikao vinavyoongozwa na Dk Ackson, iliwasilisha kusudio hilo kwa Ofisi ya Spika wa Bunge wiki iliyopita kwa maelezo kuwa haina imani naye.

Kwa mujibu wa Dk Kashillilah, ataeleza kinachoendelea leo baada ya kumaliza kupitia taratibu zote na kujiridhisha kuhusu kila hatua inayopaswa kufuatwa kuhusu suala la aina hiyo.


“Nitaeleza kinachoendelea kesho (leo) baada ya kujiridhisha kuhusu taratibu zinazopaswa kufuatwa kuhusu suala hilo,” alisema.

Katika kusudio hilo lililowasilishwa na Mbunge wa Simanjiro, James ole Millya, Kambi hiyo ya Upinzani ilieleza mambo sita yaliyoisukuma kuona kuwa Dk Tulia hafai kuendelea kushika kiti cha Naibu Spika.

Mambo hayo ni upendeleo kwa wabunge wa CCM, kusimamia maslahi ya Serikali badala ya umma, kutokuwa mwanasiasa, jambo linalomfanya akose uzoefu wa kuendesha vikao vya Bunge, ubabe, unyanyasaji kwa wabunge wa upinzani na kusimamia fedha za Mfuko wa Bunge zirudishwe kwa Rais.

Millya alisema walipeleka kusudio hilo kwa Ofisi ya Spika kwa kuzingatia ibara ya 85(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayozungumzia hatua za kuchukua ili kumwondoa madarakani Naibu Spika.

Ibara hiyo inasema, “Naibu Spika atakoma kuwa Naibu Spika na ataacha kiti cha Naibu Spika ikiwa mtu huyo ataondolewa kwenye madaraka ya Naibu Spika kwa azimio la Bunge.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa ili hoja hiyo ijadiliwe bungeni italazimika kujadiliwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge ambayo nayo inahitaji theluthi moja ya saini za wabunge wote.

Hotuba ya Zitto Kabwe katika uzinduzi wa “Operesheni Linda Demokrasia Nchini”.

$
0
0
Ndugu Wananchi, Nawashukuru sana kwa kujitokeza kwenu kuitikia wito wetu wa kuja kutusikiliza. Tumewaita hapa ili kuwaeleza kinachoendelea katika nchi yetu hivi sasa na madhara makubwa yanayoweza kutokea iwapo hatutosimama kidete dhidi ya mbinu zozote za kufifiza na kuminya demokrasia na misingi ya uwajibikaji katika nchi yetu.

Mwaka 2015 tulikwenda kwenye uchaguzi kuchagua madiwani, wabunge na Rais. Baada ya Uchaguzi kumalizika Serikali mpya iliundwa na Serikali za Mitaa (Halmashauri) kuundwa. Nawapongeza wananchi wote kwa kuendesha zoezi la uchaguzi kwa amani na kuweka heshima ya nchi yetu mbele.

Baada ya uchaguzi tumeona viongozi wapya wakichukua hatua mbalimbali nzuri na mbaya, zenye kujenga na kubomoa, zenye kuimarisha demokrasia na zinazobomoa demokrasia. Tumeshuhudia maamuzi mengine ambayo yanatia khofu, kwamba ingawa tunaona dhamira ya dhati ya kupambana na Ufisadi, lakini pia tunaona mbinu za chini chini za kutokomeza Demokrasia ya nchi yetu ambayo tumeijenga kwa jasho na damu.

Mkutano wetu wa leo utagusia baadhi ya maeneo ambayo tunadhani ni vihatarishi vya ustawi wa wananchi wetu na ambavyo lazima tuanze kuvipinga mapema sana kabla havijaota mizizi. Ndugu Wananchi, Baadhi ya maeneo tutakayozungumza leo ni pamoja na;
  1. Wabunge kusimamishwa kazi za Bunge
  2. Maamuzi ya Serikali kuhusu Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma
  3. Hali ya Zanzibar
  4. Mwelekeo wa Bajeti ya Kwanza ya Serikali ya Rais Magufuli
  5. Tishio la Nchi kuelekea kwenye Utawala wa Imla wa MTU mmoja
Wabunge Kusimamishwa Kazi.
Ndugu Wananchi, mnamo tarehe 30 Mei, 2016 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Naibu Spika lilipitisha Azimio la Bunge la kuwasimamisha kazi wabunge 7 kwa vipindi mbalimbali. Wabunge wawili, ndugu Esther Bulaya na ndugu Tundu Lissu walisimamishwa Mikutano miwili ya Bunge. Wabunge Wanne, ndugu Halima Mdee, Ndugu Pauline Gekul, Ndugu Godbless Lema na Mimi ninayezungumza nanyi tulisimamishwa mkutano mmoja, huu unaoendelea wa Bajeti, na mbunge mmoja ndg John Heche Suguta amesimamishwa vikao 10 vya mkutano huu wa tatu unaoendelea.

Sababu iliyoelezwa na Bunge ni kwamba wabunge hawa walifanya fujo siku ya tarehe 27 Januari, 2016 kufuatia hoja niliyoitoa Bungeni ya kutaka mjadala kuhusu sababu za hovyo na za uongo zilizotolewa na Serikali kuhusu uamuzi wa kuzuia Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) pamoja na televisheni binafsi (Star tv na Azam) kuonyesha moja kwa moja mikutano ya Bunge.

Ndugu Wananchi, mimi binafsi pamoja na wabunge wengine 6 hatukufanya fujo yeyote ndani ya Bunge. Kosa letu kubwa ni kutaka kuhoji maamuzi ya Serikali ambayo kwa maoni yetu hayana msingi wowote. Serikali inasema ninyi Wananchi hamfanyi kazi kwa sababu Bunge linaonyeshwa wakati wa kazi. Hata hivyo Serikali hiyo hiyo inatwambia kuwa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita uchumi wa Tanzania ulikua kutoka tshs 16 trilioni mwaka 2005 mpaka tshs 99 trilioni mwaka 2015. Kipindi chote hiki Bunge lilikuwa linaonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Taifa (TBC) na televisheni ya StarTV.

Kama mngekuwa hamfanyi kazi Uchumi usingekua kwa kiwango hicho cha asilimia 600 ndani ya Muongo mmoja wa uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Utawala wa Rais John Magufuli unataka kutuaminisha kuwa ukiwa na Bunge ‘live’ watu hawafanyi kazi lakini uongozi uliopita umedhihirisha kwa ushahidi kuwa ukipanua demokrasia na kuwaonyesha wananchi kila kinachoendelea Bungeni uwezo wa kazi unaongezeka na uwezo wa wananchi kuwajibisha viongozi wao unaongezeka.

Hivyo Serikali kuamua kuficha Bunge ni mbinu za kuendesha Serikali kwenye giza ili kufanya maamuzi ambayo baadaye ionekane Serikali tu au Rais tu ndiye mfanya kazi. Ndio maana mikutano yote ya Rais anapohutubia huonyeshwa moja kwa moja lakini sio Bunge.

Wananchi, Wabunge wamesimamishwa kwa sababu ya kukataa Bunge kuendeshwa kwenye giza. Wabunge waliosimamishwa walisimama kidete kuhoji sababu za Serikali kufikia maamuzi hayo. Walitaka kujua kwanini Serikali imekuwa kigeugeu kwa kubadilisha badilisha sababu zake za kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya Bunge.

Wakati mmoja Serikali ilisema sababu ni gharama, kama ni hivyo ni kwanini walizuia StarTV na AzamTV kuonyesha moja kwa moja? Ni dhahiri wananchi Serikali inataka kuendesha mambo yake kwa uficho kwa sababu kuna maamuzi inataka kufanya na haitaki wananchi mjue mapema maamuzi hayo. Serikali inaturudisha nyuma badala ya kwenda mbele.

Wananchi, wabunge waliosimamishwa ni wabunge wenye uwezo wa kujenga hoja. Kuna wengine wamebaki Bungeni wenye uwezo mkubwa tu wa kujenga hoja, lakini hawa saba waliosimamishwa ni wabunge waliojidhihirisha kwa muda mfupi kwa baadhi yao kama ndugu Heche, kwamba wanaweza kusimamia hoja zao bila woga. Swali la kujiuliza ni, tukio ambalo limetokea mwezi Januari ni kwanini lifanyiwe mwezi Juni tena wiki moja tu kabla ya Waziri wa Fedha kuwasilisha Bungeni Bajeti ya Serikali?

Katika waliosimamishwa ni pamoja na Waziri Kivuli wa Fedha, ndg. Halima Mdee na Waziri Kivuli wa zamani wa Fedha ambaye anazungumza nanyi leo (Zitto Kabwe). Kuna nini? Nitawaeleza katika hoja ya Bajeti. Kimsingi Utawala wa Rais Magufuli umepanga kupandisha kodi za wananchi masikini na uliona uwepo wetu bungeni utatibua mipango yao.

Rais na wenzake ndani ya CCM hawapendi kusikia hoja zinazowapinga, hawana uvumilivu wa kukosolewa na hivyo walipanga kuhakikisha kuwa baadhi yetu hatutakuwepo kwenye mjadala wa Bajeti ili kufanikisha malengo yao ya kufanya maamuzi yatakayowandamiza wananchi. 

Nitaeleza vizuri hili baada ya muda kidogo. Hivyo nataka Watanzania wajue kuwa kusimamishwa kwetu ni ajenda maalumu ya Serikali ya Rais Magufuli kufunika mjadala wa Bajeti kwa sababu inajua kuwa tunajua inachopanga kufanya dhidi ya mafukara wa nchi yetu.

Sisi hatutakaa kimya, tutatumia wenzetu waliopo Bungeni kuyasema haya na pia tutazungumza na wananchi kuwaeleza pia. 

Tutatumia mikutano yetu mbalimbali bila kujali itikadi za vyama vyetu kuhakikisha kuwa Wananchi wanajua kila kinachoendelea na kuwataka kuunganisha nguvu kukataa udikteta unaonyemelea nchi yetu.

Wanafunzi 7800 Kufukuzwa Chuo Kikuu Cha Dodoma.
Ndugu Wananchi, mmesikia sakata la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma waliokuwa wanasomea programu maalumu ya Ualimu wa Sayansi. Hawa ni watoto wa Watanzania masikini waliokubali kuacha kwenda Kidato cha Tano na cha Sita (A level) na kukubali kusomea diploma ya Ualimu ili wakawafundishe watoto wa masikini wenzao. Wanafunzi hawa hawakuanzisha wao program hii, ilianzishwa na Serikali na kupitishwa na Baraza la Mawaziri ambalo Rais Magufuli alikuwa mjumbe na alishiriki kikao hicho kwa mujibu wa kumbukumbu za Baraza la Mawaziri.

Rais Magufuli hakupinga mpango huu na aliubariki kama Wenzake walivyofanya na kuanza kutekelezwa. Lengo na program hii ni kuondoa tatizo la walimu wa masomo ya Sayansi. Tanzania ina uhaba wa walimu wa Sayansi 26,000 (Kwa Utafiti wa Mwaka 2014) na tukienda kwa utaratibu wa kawaida tutahitaji miaka 20 kuziba pengo hilo.

Program hii ilianzishwa ili kuziba pengo hili kwa muda mfupi, na vijana waliitikia wito huu wa kizalendo kuhakikisha wadogo zao hawakosi walimu siku za usoni. Serikali ya awamu ya Tano imewafukuza vijana hawa 7800 kutoka chuoni ndani ya masaa 24 kwa makosa ambayo sio yao.

Wananchi, hatusemi kuwa program haikuwa na kosoro. Zilikuwepo ikiwemo kudahili wanafunzi wengi zaidi ya ilivyotarajiwa na kudahili wanafunzi 88 kati ya 7800 ambao walikuwa na daraja la nne (Div 4) katika masomo yao. Lakini aliyedahili sio watoto hawa bali ni Serikali yenyewe, kwanini waadhibiwe watoto?

Bunge lilipotaka kujadili hoja hii au hata kuipeleka kwenye kamati ya Bunge kuifanyia uchunguzi na kutoa mapendekezo Naibu Spika alizuia hoja ya mbunge Joshua Nasari bila sababu za msingi. Wabunge wote bila kujali vyama vyao walitaka hoja ijadiliwe na kuweza kupata majawabu. Mbona wakati wa Uongozi wa awamu ya 4 tulijadili hoja ya mgomo wa madaktari na kisha kupelekwa kwenye kamati ya husika ya bunge kupata suluhisho la kudumu? Kwanini Utawala wa Rais Magufuli hautaki Bunge lifanye kazi yake? Mbona yeye Rais kaenda kujadili jambo hilo huko Chuo Kikuu mlimani?

Wananchi, Rais Magufuli anafikia kuita watoto wetu Vilaza? Rais huyu anayesema yeye ni Rais wa masikini anaita watoto wa masikini Vilaza. Vijana hawa Wazalendo waliojitoa muhanga kuacha kwenda kidato cha Tano ili wasome kuwa Walimu na kulea kizazi kijacho Rais wao anawaita vilaza. Rais sifa zimempanda kichwani. Rais Magufuli hana budi kuwaomba radhi vijana hawa na wazazi wao.

Kitaaluma Rais ni Mwalimu, anajua madhara ya kisaikolojia kufuatia maneno aliyoyasema. Ni sawa na Jenerali wa Jeshi anayetukana askari wake walio Mstari wa mbele. Hata Baba wa Taifa hakuthubutu kamwe kuita wanafunzi Vilaza hata kama walimuudhi kiasi gani.

Rais Magufuli anaongea mno, sio sawa kwa Kiongozi. Rais ajue kuweka akiba ya maneno. Yeye ni Kiongozi wa wote, wenye akili na Vilaza. Yeye anapaswa kuwa wa mwisho kuongea ili watu waweze Kukata rufaa kwake. Yeye akishaongea wananchi ‘aggrieved’ (walioonewa Au kukosewa) waende kwa nani? Waende kwa mungu?

Tunamtaka Rais awarudishe wanafunzi Hawa Chuoni mara moja na wale wanafunzi ambao itaonekana hawakuingia kwenye programu kihalali (ambao Ni 88 Tu) waondolewe badala ya kuadhibu watoto wote kwa makosa ya wachache ambao ni asilimia 5 tu ya wote. 

Makosa madogo ni mambo ya kawaida katika Jamii. Yeye Rais ni mfano mzuri wa hili kwani naye mbona aliteua Waziri mlevi na kurekebisha kwa kumfukuza peke yake?, mbona hakufukuza Baraza zima la mawaziri kwa ulevi wa Waziri mmoja?

Zanzibar.
Ndugu Wananchi mnajua mara baada ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar kufutwa chama chetu kiliweka msimamo wa wazi kwamba kinatambua ushindi wa Maalim Seif Sharif Hamad kama Rais aliyechaguliwa na Wazanzibari na anayepaswa kula kiapo na kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Tuliandika pia masuala 10 muhimu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuyafanyia kazi, na moja ya jambo tulilomtaka Rais Magufuli Kulifanyia kazi ni suala la demokrasia ya Zanzibar. 

Rais hakusikia wito wetu na aliruhusu ufutwaji usio halali, kisiasa wala kisheria wa uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 25, 2015.

Tunarudia kusisitiza kuwa Chama chetu cha ACT Wazalendo hakiutambui uchaguzi wa marudio wa Zanzibar uliofanyika mwezi Machi mwaka 2016 pamoja na matokeo yake yote. Kwa maana hiyo hatutambui Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Baraza la Mawaziri la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na Pia Rais wa Zanzibar.

Wananchi, Hivi karibuni kumekuwa na kuongezeka kwa sintofahamu huko Zanzibar kufuatia Mgombea Urais aliyeshinda na kunyanganywa ushindi wake kwenda kwa wananchi kuzungumza nao. 

Hali hii imepelekea jeshi la polisi kumhoji Maalim Seif na siku mbili baadaye Dkt. Shein kutamka kuwa hamwogopi Maalim Seif kwa sababu “Hana vifaru na mizinga”.

Tunalaani kauli hii ya Dkt. Shein ya kutisha kwa vifaru na mizinga. Kamwe huwezi kuzima haki za Wananchi kwa vifaru na mizinga. Dkt Shein akumbuke kuwa Sultan alikuwa na jeshi, vifaru na mizinga na ulinzi wa Dola kubwa kama Uingereza lakini aliangushwa na wananchi wa Zanzibar mwaka 1964.

Dkt Shein akumbuke kuwa nchi kadhaa duniani zilikuwa na madikteta wenye vifaru na mizinga lakini waliondoka. Dkt Shein afute kauli yake hii na kuacha vitisho badala yake aanze mchakato wa kupata maridhiano ya jamii ya Zanzibar. Hatutaki kurithi damu, tunataka kurithi nchi yenye amani, haki na demokrasia.

Wananchi, sisi ACT Wazalendo, tunajua hali mbaya ya kisiasa iliyopo Zanzibar na mkwamo uliopo hivi sasa Kisiasa, Kijamii na Kiuchumi. Hata hivyo ni lazima tupate jawabu kupitia sanduku la kura. 

Tunapendekeza kuwa Vyama vikuu vya siasa Zanzibar vikubali ‘kufa kidogo’ yaani ‘to die a little’, kwa vyote kukubali kuwa Chaguzi zote Mbili, wa Mwaka 2015 na ule wa mwaka 2016 zilikuwa batili, zifutwe na Uchaguzi Mkuu mpya uitishwe.

Uchaguzi huo utanguliwe na Serikali ya Mpito itakayohusisha vyama vyote vya siasa na baadhi ya wanajamii wanaoheshimika na Wazanzibari wote ili kujenga kuaminiana. 

Tunadhani hii itatupa nusra kwa Zanzibar. Tunawaomba Wazanzibari watumie mwezi mtukufu wa Ramadhani kutafakari maoni haya na wote kwa pamoja baada ya Ramadhani kuja na jawabu ya hali ya kisiasa. Tunatamani Zanzibari irudi kwenye hali ya kawaida na ishamiri. 

Zanzibar ikiingia kwenye mtafuruku Tanzania nzima itakuwa kwenye mtafaruku. Ni dhahiri kuwa Rais Magufuli ameshindwa kutoa uongozi kwenye suala hili na hivyo ni wajibu wa Wazanzibari wenyewe kukaa na kupata mwafaka wa kijamii na kusonga mbele.

Bajeti ya 2016/17.
Wananchi, kuanzia tarehe 8 mwezi Juni, 2016 Bunge litakuwa kwenye mjadala wa Bajeti ya kwanza ya Serikali ya Rais Magufuli. Rais ameleta mapendekezo ya Bajeti ya shilingi 29.5 trilioni. Katika makadirio haya vyanzo vya ndani ni shilingi 18.5 trilioni na misaada ni shilingi 3.6 trilioni. Serikali inatarajiwa kukopa jumla ya shilingi 7.4 trilioni.

Mwaka 2015/16 Serikali ilitarajiwa kukusanya jumla ya shilingi 13.8 trilioni, hivyo ndani ya mwaka mmoja wa fedha Utawala wa Rais Magufuli unataka kukusanya shilingi 4.7 trilioni zaidi sawa na ongezeko la asilimia 25. Kwa ufupi ni kwamba Serikali haina budi kuongeza kodi kwa kiwango cha asilimia 25 ili kuweza kutimiza malengo yake ya makusanyo.

Wananchi, mtakumbuka kuwa mara baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani tulikuwa tunaelezwa kodi iliyokusanywa kila mwezi na tuliona wafanyabiashara wakikabwa koo kwa kukwepa kodi. Hata hivyo ongezeko la Makusanyo lilikuwa kwa miezi 2 tu ya Novemba na Disemba kwani kuanzia mwezi Janauri makusanyo yalianza kuendana na hali halisi ya uchumi wa nchi yetu na ndio maana mbwembwe za makusanyo hazisikiki tena hapa nchini.

Ukweli ni kwamba Rais alikuwa anakusanya ‘arrears’ na hapakuwa na hapajakuwa na mbinu mpya za kukusanya mapato ya Serikali. Maeneo muhimu yanayopoteza mapato kama vile makampuni ya nje kutumia mbinu za kihasibu kukwepa kodi hayajatazamwa kabisa na Rais na wasaidizi wake.

Hivyo, Serikali imeamua kurudi kwa wanyonge kuwaminya na kodi ikianzia kuchukua kodi zote za Majengo kutoka kwenye Halmashauri zetu. Kodi za majengo ndio chanzo kikuu cha mapato ya Halmashauri zetu za Miji, Manispaa na Majiji. Uamuzi wa Serikali kuchukua chanzo hiki cha mapato utapelekea Halmashauri zetu kushindwa kuzoa taka na hata kutoa huduma kwa wananchi.

Hata hivyo wananchi uamuzi huu ni kwa sababu Halmashauri nyingi za Miji zinaongozwa na vyama vya Upinzani kama vile Manispaa ya Kigoma Ujiji, Manispaa ya Iringa, Arusha jiji, Ilala, Kinondoni, Mbeya Jiji nk. Utawala wa Rais Magufuli unataka kuhakikisha kuwa Manispaa zinaoongozwa na vyama vya upinzani zinashindwa kutoa huduma. Duniani kote kodi za majengo hukusanywa na Serikali za Mitaa. Katika Bajeti ya mwaka huu kodi hizi zitaongezwa maradufu.

Wananchi, Serikali inatarajia kupandisha ushuru kwenye soda, vilevi na sigara pia kwa mujibu wa vitabu vya Bajeti vilivyogawiwa kwa wabunge. Hata kodi kwenye gharama za kupiga simu zitaongezwa kwa zaidi ya asilimia 10. Eneo la ushuru peke yake Serikali inataka kukusanya shilingi 1.2 trilioni kutoka shilingi bilioni 900 za mwaka uliopita. Hii ni nyongeza ya shilingi 300 bilioni zaidi kutoka Bajeti ya mwaka 2015/16.

Maeneo haya mawili peke yake (kodi za majengo na ushuru wa bidhaa) yataongezewa kodi kiwango cha kuumiza sana wananchi wa kawaida. Hii ndio sababu Serikali imefukuza baadhi ya wabunge mahiri bungeni ili kulainisha upitishwaji wao wa viwango hivi vya kodi. Hata hivyo tutatumia wabunge waliobakia Bungeni kuhakikisha kuwa kodi kwa wananchi masikini haziongezwi kiholela.

Wananchi, sisi tunaamini kuwa Bajeti ya shilingi 29.5 trilioni ya Utawala wa Magufuli sio bajeti halisi kwani makadirio yao hayazingatii ukuaji wa uchumi na yana lengo la kuchukua fedha kutoka kwa wananchi kupeleka Serikali jambo ambalo litadidimiza uchumi wa nchi yetu.

Tishio la Demokrasia.
Wananchi jambo la mwisho ambalo ninataka kuwaeleza ni tishio lililopo mbele yetu dhidi ya demokrasia ya vyama vingi. Hatua mbalimbali ambazo Utawala wa Rais Magufuli unachukua ni ishara ya kutengeneza utawala wa Kiimla. Rais ndiye anayejua kila kitu na ndiye anayeamua kila kitu. Hii ni hatari sana kwa nchi yetu na ni lazima kuchukua hatua mahususi kumkatalia Rais mwanzoni kabisa ili asizoee.

Tunarudia kuwa tulimuunga mkono Rais toka mwanzo katika vita dhidi ya Ufisadi, kwani ni vita muhimu na lazima ipiganwe bila kujali itikadi za vyama. Hakuna namna unaweza kumlaumu Rais anapochukua hatua za kusafisha Uvundo katika nchi. Tutaendelea kumwunga mkono katika eneo hilo.

Wananchi, hata hivyo Rais anatia Khofu mno katika ujenzi wa mfumo wa uwajibikaji. Tanzania ina vyombo vya kuimarisha uwajibikaji, ikiwemo Bunge la Jamhuri ya Muungano na Pia Ofisi ya Ukaguzi ya Taifa. Rais anataka kupigana dhidi ya ufisadi nje ya mfumo jambo ambalo ni la hatari sana kwa nchi kwani akitoka yeye tutaanza upya.

Inawezekanaje Kiongozi anayepambana na rushwa akavunja nguvu ofisi ya ukaguzi ya Taifa kwa kumnyima Bajeti Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG)? Rais amediriki hata kuvunja Katiba na sheria ya ukaguzi, kwani Bajeti ya CAG haipangwi na Serikali bali hupangwa na Kamati ya Bunge. Rais ameenda kinyume na sheria na badala yake kapanga mwenyewe Bajeti ya CAG? Toka lini mkaguliwa akapanga bajeti ya anayemkagua? Kamati ya Bunge ilipanga Bajeti ya tshs 69 bilioni kwa CAG lakini Serikali (mkaguliwa) imeipiga panga mpaka tshs 32 bilioni. Hii ni moja ya mfano dhahiri kabisa wa Serikali kuanza kuvunjavunja vyombo vya uwajibikaji.

Wananchi, hivi sasa kuna Ukosefu wa Sukari nchini. Rais alisimama kwenye Vilinge vya Siasa, akatoa matamko makali kwamba kuna Wafanyabiasha wameficha sukari na tukaonyeshwa sukari hiyo. Hata hivyo baada ya siku chache vyombo kama PCCB na TRA vikasema sukari ile ni halali. Inakuwaje Rais alitamka maneno yale bila ya kushauriana na vyombo? Ni dhahiri Rais anaongea na kuropoka tu na kutaka kujenga utawala wa Kimla. Leo bado kuna shida ya sukari na sukari ambayo serikali inasema iliagiza haionekani. Ipo wapi?

Wananchi, Rais Huyu Huyu alikwenda Benki Kuu na kusema nusu ya wafanyakazi pale ni hewa. Mpaka leo hatujaona hao wafanyakazi hewa wa BoT. Rais alikwenda tu kwa kupata maneno ya kuokoteza barabarani na kutoa matamko ambayo yanashusha hadhi ya Benki, lakini Rais anashindwa kutoka mbele kusema alikosea. Tunajenga mfumo mbaya sana wa uongozi wa Nchi.

Leo tunataka kumwambia Rais kuwa aongoze, asitawale. Rais awe na Utu na wananchi wake. Rais awe anasikiliza kwanza na kuchambua mambo kabla ya kusema chochote mbele ya hadhara. Rais awe wa mwisho kusema ili kama kuna rufaa Watu waseme kwake. Vinginevyo Rais anataka kujenga utawala wa Kiimla, tutamkatalia wazi wazi.

Wananchi, nimalizie kwa kusema yafuatayo. Rais John Magufuli amesema kuwa yeye amejitoa muhanga kupambana na ufisadi. Sisi tunalazimika kujitoa muhanga Kulinda Demokrasia.

Ni imani yetu kuwa Ufisadi utapigwa vita kikamilifu sio kwa kutegemea nia ya mtu mmoja bali kwa kuboresha na kutumia misingi ya demokrasia kwa kujenga taasisi madhubuti zitakazomaliza janga la ufisadi bila ya kutegemea nia ya Rais.

Sisi tunaamini kuwa ni jukumu letu kusimama kujitoa mhanga kuzuia maafa ya kitaifa yatakayoweza kutokea kutokana na makosa ya kukandamiza demokrasia na uhuru wa mawazo kwa kuhoji, kukosoa na kurekebisha makosa hayo sasa bila kuchelewa.

Tunamwunga mkono Rais kutokomeza Ufisadi lakini TUNAMPINGA Rais Kutokomeza Demokrasia. Demokrasia yenye misingi madhubuti ya Uwajibikaji ndio jawabu sahihi dhidi ya ufisadi na unyonyaji nchini kwetu.

Nawashukuru sana.
Zitto Ruyagwa Kabwe
Dar es Salaam
Juni 5, 2016

Polisi Jijini Mwanza Wapambana na Majambazi kwa Saa 16.....Wakamata Silaha Nzito, Watatu Wauawa

$
0
0


Watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi,wameuawa katika majibizano ya risasi na askari polisi mkoani Mwanza,alfajiri ya kuamkia jana jumapili katika mapango ya mlima wa Utemini yaliyopo kata ya Mkolani jijini Mwanza.

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Ahmed Msangi,amewataja majambazi waliouwa katika majibizano ya risasi usiku kucha kuwa ni Omar Francis Kitaleti mkazi wa Nyegezi Kona,said Khamis Mbuli maarufu kama fundi bomba mkazi wa bugarika na jambazi mwingine ambaye jina lake bado halijafahamika.

Amesema majambazi hayo yalikuwa yamejificha kwenye mapango ya mlima wa Utemini kabla ya askari polisi kufanikiwa kuyaua.

Jambazi mmoja aliyeuawa ambaye hajafahamika jina lake mwenye umri kati ya miaka 20 hadi 25 alikuwa akiwashambulia polisi kwa kutumia bastola ambapo baada ya polisi kumpiga risasi walimpekua na kumkuta akiwa na bastola aina ya Chinese,iliyokuwa na risasi tatu ndani ya magazine,huku majambazi wengine waliokuwepo kwenye mapango hayo wakiendelea kujibishana kwa risasi na askari polisi.

Kamanda Msangi ameongeza kwamba Ijumaa Juni 3,askari polisi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama,walimkamata Omar Francis Kitaleti kwa jina maarufu kiberiti,mkazi wa Nyegezi Kijiweni ambaye alikuwa akituhumiwa kuhusika katika matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha kwenye maduka ya M-pesa,Tigo Pesa na Airtel money jijini Mwanza ambaye baada ya kuhojiwa alikiri kuhusika katika matukio hayo na aliwataja wenzake anaoshirikiana nao na mahali walipojificha.

Amesema ilipotimu majira ya saa kumi na moja kamili jioni siku ya Jumamosi Juni 4,polisi walifika katika mlima huo na walipoyakaribia mapango hayo ghafla walianza kushambuliwa kwa risasi na majambazi waliokuwa wamejificha ndani ya mapango hayo.
Omary Francis Kitaleti @Kiberiti, mmoja wa majambazi aliyeuawa na wenzake kwa risasi.

Katika mapambano hayo ya risasi na askari polisi,risasi hizo ziliweza kumpata jambazi mwenzao aitwaye Omary Francis Kitaleti aliyekuwa anawaongoza askari polisi na kufariki dunia papo hapo, na risasi nyingine ilimjeruhi askari kwenye unyayo wa mguu wake wa kulia.

Amesema polisi kwa kutumia mbinu za medani za kivita waliweza kuzingira maeneo hayo ya mlima wa utemini hadi alfajiri ya kuamkia Jumapili Juni 5,huku wakijibishana risasi na majambazi hao na baada ya kuona yamezidiwa nguvu huku kukikaribia kupambazuka ndipo yalipoamua kuondoka ndani ya mapango hayo kwa kurusha bomu moja la kutupa kwa mkono huku yakizidisha mapigo ya risasi kwa kutumia silaha walizokuwa nazo.

Ameongeza kuwa polisi wamekamata bunduki moja aina ya SMG iliyokuwa na risasi nane na kisu kimoja.

Kamanda Msangi amesema majambazi watatu walifanikiwa kutoroka kutoka kwenye mapango hayo kuelekea maeneo ya Nyasaka na baada ya jambazi mmoja kubaini kuwa askari polisi walikua wanamfuatilia alitoa bunduki  na kutaka kuwapiga askari polisi lakini polisi waliweza kumuwahi na kumfyatulia risasi sehemu mbalimbali za mwili wake na kufariki dunia papo hapo.

Amesema askari polisi wamefanya upekuzi kwenye mapango ya mlima wa Utemini na kufanikiwa kupata vitu mbalimbali vilivyoachwa na majambazi hao ambavyo ni pamoja na risasi nne,kisu kimoja chenye damu,kofia ya kuficha uso nyeusi moja (mask),jiko la stove,masufuria ya kupikia, unga wa mahindi,sukari,dagaa,chakula kilichopikwa,ngoma mbalimbali,na simu tatu za mkononi.

Askari aliyejeruhiwa amelazwa hospitali ya rufaa ya bugando na hali yake inaendelea vizuri,polisi bado wanaendelea na msako wa kuwatafuta majambazi waliofanikiwa kutoroka.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, akiongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo alitembelea kwenye mapango ya Utemini na kuwaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi katika kuwafichua wahalifu

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Msanii Diamond Atoa Msaada Wa Madawati 600 Kwa Mkuu Wa Mkoa Wa Dar Es Salaam Mhe. Makonda

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akimpongeza Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' mara baada ya kumtembelea ofisini kwake na kutoa mchango wake wa madawati yapatayo 600 kwa ajili ya kuchangia maendelea ya mkoa. 

Akiongea katika makabidhiano hayo msanii huyo alisema ni jambo jema kwao kuweza kujitolea mchango huo ili kuweza kumuunga mkono Mhe. Makonda katika kukabilana na changamoto za elimu.
 
Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' akiongea mara baada ya kukabidhi msaada wa madawati yapatayo 600 kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda ili kuweza kupunguza tatizo la wanafunzi kukaa chini. Makabidhiano hayo yalifanyika leo Juni 6, 2016 ofisini kwa mkuu wa mkoa jijini Dar es Salaam.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akitoa shukrani zake za pekee kwa Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' kwa kuweza kutoa madawati 600 ikiwa ni mchango wake katika elimu ya kuweza kufanya wanafunzi kukaa sehemu salama. Mhe. Makonda alisema kuwa wakati umefika kwa wasanii wakaweza kujitoa katika jamii ambayo imekuwa ikiwapa wao sapoti na msanii Diamond amekuwa wa kwanza kuonyesha moyo wa pekee kwa kurudisha fadhila.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa WCB mara baada ya kumtembelea ofisini kwake.

Taarifa ya Ofisi ya Spika kuthibitisha kupokea hoja ya kumeondoa madarakani Naibu Spika

$
0
0

Ofisi ya Spika imepokea taarifa ya kusudio la kuleta Bungeni Hoja ya kumwondoa madarakani Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) iliyowasilishwa na Mbunge wa Simanjiro Mhe. Mhe. James Kinyasi Millya siku ya Jumatano tarehe 1 Juni, 2016.
 
Utaratibu huo ni wa Kikatiba na upo chini ya Ibara ya 85(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 ambapo pia umeainishwa katika Kanuni ya 138 (1), ya kanuni za Kudumu za Bunge kuhusu utaratibu wa Kumwondoa Naibu Spika Madarakani.
 
Baada ya kupokea kusudio hilo, Kanuni za Bunge zinamtaka Spika kuiwasilisha hoja hiyo katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili ifanyiwe kazi.
 
Kutokana na msingi huo wa kikanuni, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (Mb) anakusudia kuliwasilisha swala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kama Kanuni inavyoelekeza ambapo kamati hiyo itaangalia msingi wa hoja na endapo itaridhika, kanuni inaitaka Kamati kuwasilisha hoja hiyo Bungeni ili ijadiliwe. 

Aidha, Kanuni ya 138 (3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, inamtaka Spika kukalia kiti wakati wa mjadala wa hoja ya kumwondoa Naibu Spika Madarakani.
 
Hivyo basi, suala lililowasilishwa na Mhe. James Kinyasi Millya kuhusu kusudio la kumwondoa Naibu Spika Madarakani, tayari limepokelewa na lipo katika Ofisi ya Spika kwa ajili ya utekelezaji wa masharti ya Kanuni.

Imetolewa na,
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
Ofisi ya Bunge
DODOMA
6 Juni, 2016.

Waziri Mkuu : Mataifa Yaliyoendelea Yashirikiane Na Serikali Ya Tanzania Kuwahudumia Wakimbizi

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameyaomba mashirika ya Kimataifa na Nchi zilizoendelea zishirikiane na Serikali ya Tanzania katika kuwahudumia wakimbizi.

“Kwa sasa tunashirikiana na UN (Umoja wa Mataifa) kuwahudumia wakimbizi, hivyo tunaomba mataifa mengine nayo yatusupport katika jambo hili,” amesema.Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo leo (Jumatatu, Juni 6, 2016) alipofanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji, Mhe. Dibr Reynders ofisini kwake Bungeni, Dodoma.

Amesema Tanzania inahifadhi jumla ya wakimbizi 165,000 kati ya 230,000 walioko katika nchi za Maziwa Makuu, ambapo bajeti ya Serikali haitoshelezi kuwapa huduma wanazostahili.Waziri Mkuu Majaliwa amesema wakimbizi hao wanaishi kwenye kambi mbalimbali nchini zikiwemo za Nyarugusu na Nduta zilizoko wilayani Kasulu na Kibondo ambazo alizitembelea Desemba mwaka jana.

Amesema wakimbizi hao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za uhaba wa maji safi, ufinyu wa huduma za afya na elimu na uharibifu wa mazingira .Amesema wengi wa wakimbizi hao ni raia wa Burundi, Kongo na Rwanda, pia amemuomba Mhe. Reynders atakapofika Burundi akahamasishe amani.

Pia Waziri Mkuu Majaliwa amesema Tanzania inakkaribisha wawekezaji kutoka nchini Ubelgiji na mataifa mengine kuja kuwekeza katika Sekta za Viwanda, Nishati na Miundombinu.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa amesema hali ya siasa visiwani Zanzibar ni ya utulivu na Rais Dk. Ali Mohamed Shein anafanya kazi vizuri kwa kushirikiana na vyama vya upinzani.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mhe. Reynders aliyetaka kujua hali ya kisiasa inavyoendelea visiwani huko.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
06 Juni, 2016 .

Makamu Wa Rais Mhe. Samia Azindua Jukwaa La Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania Na Akaunti Ya Malaika Leo

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Bi Samia Suluhu Hassan leo hii amezindua jukwaa la kuwezesha wanawake na akaunti maalum ya mikopo ya MALAIKA inayolenga kuwawezesha wanawake wa hali ya chini kiuchumi kupitia Benki ya wanawake katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika uzinduzi huo Mheshimiwa Samia Suluhu amesema kuwa lengo la kuanzishwa kwa jukwaa hilo ni kuwapa uwezo wanawake waweze kutoka katika sekta isiyo rasmi na kuingia katika sekta rasmi na hivyo kuwainua kiuchumi kwani mchango wa mwanamke mpaka sasa bado haujaongezeka thamani.

Aidha Bi Samia ameagiza kuwa kuanzia sasa asilimia 35% ya tenda za serikali za mitaa ziende kwa wanawake na vijana ili kuwawezesha kiuchumi na kuwataka wanawake kubadilika kifikra na hata wanapopata mikopo hii wawe na nidhamu katika matumizi yake.

Hata hivyo Mhe. Suluhu ametoa rai kwa mabenki kufikisha huduma zao vijijini ili huduma ya mikopo iwafikie wanawake wachangie uchumi wa dunia na sio tu kwa familia huku akiwahimiza wanawake kupendana,kushirikiana na kusaidiana.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Dkt.Hamisi Kigwangala amesema kuwa serikali imeendelea kusaidia wanawake katika Nyanja mbalimbali ikiwemo kuweka usawa wa jinsia kwa wanawake kiuchumi ,kutoa vikwazo katika masoko na kuondoa mila kandamizi.

Aidha Dkt Kigwangala ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ya biashara kwa wanawake kwa kufanya mafunzo ya ujasiliamali na kuweka sera nzuri ambayo yote haya yameainishwa katika ilani ya chama cha mapinduzi ya 2015-2020 uku akieleza mafanikio makubwa ya benki ya wanawake ambayo mpaka sasa imetoa mikopo yenye thamani ya bilioni 86.

Uzinduzi wa Jukwaa hilo na akaunti ya MALAIKA ya mikopo uliendana na mada mbalimbali kutoka kwa wadau mbalimbali kama Crdb,Benki ya wanawake,Nssf ,Wizara ya Viwanda na Biashara na Tcra. 

Serikali Yaondoa tozo ya uhakiki na Usajili wa Viwanda Vidogo Vidogo.

$
0
0

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Prof Adolph Mkenda amesema kuwa serikali imeondoa tozo ya uhakiki wa viwango vya ubora na usajili katika kuanzisha viwanda vidogovidogo katika shirika la viwango Tanzania Tanzania(TBS) ambao sasa unafanyika bure.

Prof Mkenda ameyasema hayo alipokuwa akitoa mada katika uzinduzi wa Jukwaa la kuwezesha wanawake na akaunti ya mkopo ya MALAIKA ambayo imeanzishwa katika benki ya Wanawake Tanzania.

Aidha amesema ameagiza kwa wilaya na vijiji kuanzisha viwanda kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wanaunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya Tano na kuinua uchumi wa nchi yetu.

“Bidhaa za kilimo kwa sasa zinapewa dhamana na hivyo basi nawaimiza wanawake waanzE kuanzisha viwanda vidogovidogo kwani uanzishwaji wake ni bure.”Alisema Prof Mkenda.

Pia alisema kuwa kipato cha kati nchini kinaongezeka siku hadi siku na kuwataka wanawake kutolima kwa mazoea na kuwataka wafanye biashara kwa faida kwa kutumia teknolojia sahihi ili kuongeza uzalishaji.

Katika upande mwingine aliwataka wanawake kutokata tamaa katika kujiinua kiuchumi kwani Serikali ya awamu ya tano iko makini na inaweka mazingira mazuri kwa wanawake kama kuondoa tozo zisizokuwa za lazima ili kuvutia wawekezaji wa viwanda vidogo vidogo.

Katika uzinduzi huo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Bi Samia Suluhu Hassan alizindua jukwaa hilo na akaunti ya mikopo ya wanawake ya MALAIKA kupitia benki ya wanawake ambayo akaunti hiyo itakuwa na mikopo yenye riba nafuu ya asilimia 5 kwa muda wa miezi sita,mafunzo yanatolewa bure,hamna haja ya kuleta mchanganuo wa mahesabu na hakuna hitaji la dhamana yenye lengo la kuwakwamua wanawake kiuchumi.

Marekani yaipatia Tanzania dola milioni 800 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo

$
0
0
Marekani itatoa dola milioni 800 kwa Tanzania kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Mark Childress aliyekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema kutolewa kwa fedha hizo ni uthibitisho kuwa kutotolewa kwa fedha za awamu ya pili ya mradi wa changamoto za milenia (MCC-2) hakujaondoa uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na Marekani ikiwemo utoaji wa misaada ya maendeleo.

"Tumezungumza mambo kadhaa, na wiki hii Tanzania na Marekani kupitia shirika letu la misaada la USAID tunatarajia kutiliana saini mkataba wa zaidi ya dola milioni 400 kwa ajili ya mwaka ujao, pia tumezungumza kuwa kutakuwa na dola milioni 800 zitakazotolewa na Marekani kwa ajili ya miradi mbalimbali na hii haihusiani na MCC.

"Ukweli ni kwamba tunayo mengi ya kufanya pamoja katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, elimu na kilimo na tutafanya kila juhudi kuhakikisha haya yanafanikiwa" Amesema Balozi Mark Childress muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo na Rais Magufuli.

Kwa upande wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali yake ya awamu ya tano itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na Marekani na kwamba fedha za msaada kutoka Marekani ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania.

"Amekuja kutuhakikishia kwamba watatoa hela kwa ajili ya Tanzania na anasema sasa hivi watatoa zaidi ya dola milioni 800, na mkataba mwingine tunaweza tukasaini hata kesho wa dola milioni 410, anasema kutotoa hela za MCC hakuna maana kupotea kwa urafiki wa Tanzania na Marekani, urafiki wa Tanzania na marekani upo pale pale na sasa wanaongeza hela nyingi zaidi katika kuonesha kwamba juhudi za HAPA KAZI TU zinaendelea" amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo Rais Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji Mhe. Didier Reynders Ikulu Jijini Dar es salaam, ambapo viongozi hao wamezungumzia kuendeleza na kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizi mbili hususani katika maendeleo.

Pamoja na kuzungumzia miradi ya ushirikiano inayotekelezwa kati Tanzania na Ubelgiji katika mkoa wa Kigoma, viongozi hao pia wamekubaliana kuongeza ushirikiano katika biashara na uwekezaji ambapo Mhe. Didier Reynders ameahidi kushawishi kampuni nyingi za Ubelgiji kuja kuwekeza hapa nchini.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Italia hapa nchini Mheshimiwa Luigi Scotto ambaye amemaliza muda wake wa miaka mitatu.

Balozi Luigi Scotto amesema katika kipindi chake amewezesha kuongezeka kwa biashara kati ya Italy na Tanzania kwa asilimia 35 na ameielezea Tanzania kuwa ni nchi nzuri aliyoipenda na kwamba ataendelea kutangaza fursa zilizopo Tanzania huko Italia na kwingineko.

Mapema leo asubuhi, Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametia saini kitabu cha maombelezo katika Ofisi ya Ubalozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Nchi za Kiarabu ya Saharawi iliyopo Mikocheni Jijini Dar es salaam, kufuatia kifo cha Rais wa nchi hiyo Mohamed Abdelaziz aliyefariki dunia Jumanne iliyopita tarehe 31 Mei, 2016.

Rais Magufuli ambaye amepokelewa na Balozi wa Saharawi hapa nchini Mhe. Brahim Salem Buseif amesema Marehemu Mohamed Abdelaziz ambaye pia alikuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Polisalio Front, atakumbwa kwa juhudi zake za kupigania ukombozi na uhuru wa Saharawi.

"Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Tanzania napenda kutoa salamu zangu za pole kwa Serikali na wananchi wa Saharawi kwa kumpoteza kiongozi ambaye alijitoa kwa ajili ya kupigania ukombozi na uhuru wa Jamhuri ya Saharawi.

"Namuombea kwa Mwenyezi Mungu, aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina" Amesema Dkt. Magufuli katika salamu hizo.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam

06 Juni, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 7

Mikopo ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St Joseph (SJUIT) Yafutwa......Waliokuwa chini ya Programu ya Miaka Mitano ya Ualimu Watakiwa Kurudi Diploma

$
0
0
WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha St Joseph (SJUIT) Kampasi ya Arusha (kilichofutiwa usajili), waliokuwa chini ya programu ya shahada ya miaka mitano ya ualimu wa sayansi, wametakiwa kusoma ngazi ya cheti au stashahada. 

Kama watataka kusoma ngazi ya juu, watapaswa kuomba upya udahili.

Aidha, Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imesema wanafunzi waliokuwa wakipata mkopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), mikopo yao pia imesimamishwa.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Simon Msanjila alitoa agizo hilo jana kupitia taaarifa kwa vyombo vya habari. 

Profesa Msanjila alisema hatua hiyo, inatokana na kubainika kwamba wanafunzi hao hawastahili kusoma shahada na pia hawakustahili kupewa mkopo.

“Tunawafahamisha wanafunzi wa SJUIT waliokuwa kwenye programu ya miaka mitano kwamba watatakiwa kuishia daraja la cheti na stashahada... Kama wanafunzi hao watataka kuendelea na masomo ya juu, watatakiwa kuomba upya,” ilisema taarifa hiyo.

Februari 25, mwaka huu, Wizara kupitia Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) baada ya kujiridhisha kuwa Kampasi ya Arusha ya Chuo Kikuu cha Mt. Joseph Tanzania imepoteza sifa na vigezo vya kuendelea kutoa elimu ya chuo kikuu, ilifuta kibali cha kuanzishwa kwake.

Iliidhinisha uhamisho wa wanafunzi wote, waliokuwa wanasoma katika Kampasi hiyo ya Arusha kwa gharama za Chuo Kikuu cha SJUIT. 

Aidha, ilifuta udahili wa wanafunzi wapya katika programu ya shahada ya miaka mitano ya ualimu wa sayansi.

Ilielekeza wanafunzi waliokuwa wakiendelea na masomo katika programu hiyo, wahamishiwe katika Kampasi ya Luguruni, Dar es Salaam. 

TCU ilielekeza kwamba wanafunzi watalazimika kwanza kuhitimu katika ngazi ya Stashada, kama ilivyokuwa imeidhinishwa na Tume hapo awali. 

Wanafunzi waliohamishiwa kwenye vyuo mbalimbali, waendelee na masomo.

Taarifa hiyo ilisema wakati wa mchakato wa uhamisho, wanafunzi wote walihakikiwa kubaini kama wanakidhi vigezo vya kusoma kwenye ngazi hiyo. 

Wanafunzi wote waliokuwa wakisoma programu hiyo ya miaka mitano, walihamishiwa kwenye Kampasi ya Luguruni, jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo kutokana na mchakato wa uhakiki, baadhi ya wanafunzi walikutwa hawana sifa za kujiunga na mafunzo hayo ya ualimu. 

Wale waliobainika kuwa na sifa, walitaarifiwa kuendelea na masomo kwenye kampasi hiyo ya Luguruni.Wanafunzi katika kundi hili waliobainika kuwa na vigezo, walitaarifiwa kuendelea na masomo katika Kampasi ya Luguruni. 

"Maana ya kuwa na vigezo vya ufaulu tunavyovizungumzia hapa ni kwamba wanafunzi husika wamefaulu katika masomo lengwa yanayowawezesha kusoma Cheti cha Ualimu Daraja “A” ambacho ni kigezo cha kwanza kwa mujibu wa mtaala wa programu hiyo."

Wabunge wa Upinzani Wanaosusia Vikao vya Bunge Wataendelea Kulipwa Posho Zao

$
0
0

Udhaifu wa Kanuni za Bunge katika kufafanua mambo mbalimbali ya uendeshaji wa Bunge, umeelezwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwa unatakiwa kurekebishwa ili kutoa nafasi ya Kiti cha Spika kutoa uamuzi dhidi ya vitendo visivyokubalika vinavyoendelea ndani ya Bunge.

Amesema hayo jana alipokuwa akitoa majibu wa muongozo alioombwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge Nkasi Kaskazini, Ally Keissy (CCM) kuhusu uhalali wa posho wanazolipwa wabunge wa Kambi ya Upinzani, ambao wamekuwa wakiingia bungeni kusaini posho na kwenda kupumzika.

Dk Tulia alisema tangu Mei 30, mwaka huu, wabunge hao wamekuwa wakiingia bungeni kusaini posho na kuondoka kwenda kupumzika, jambo lililosababisha Dk Mwakyembe kuomba muongozo kama malipo hayo ni haki kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya Katiba ya 23.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 23, ibara ndogo ya kwanza na ya pili; “Kila mtu, bila ya kuwapo ubaguzi wa aina yoyote, anayo haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake, na watu wote wanaofanya kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo kulingana na kiasi na sifa za kazi wanayoifanya.Kila mtu anayefanya kazi anastahili kupata malipo ya haki.” 

Akitoa muongozo wake kama malipo hayo ya posho ni halali kwa mujibu wa Katiba au la, Naibu Spika alisema ametumia uamuzi wa Kiti cha Spika uliotolewa Aprili 27, 2016 kuhusu muongozo kama huo.

Alisema Kiti cha Spika katika muongozo huo wa Bashe, kilinukuu Katiba Ibara ya 73 inayosema, “Wabunge wote wa aina zote watashika madaraka yao kwa mujibu wa Katiba hii, na watalipwa mshahara, posho na malipo mengine kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.”

Mbali na malipo hayo kulindwa na Katiba, Dk Tulia alisema pia Sheria ya Uendeshaji wa Bunge Sura ya 15 na 19 Kanuni za Bunge zinaelezea kuwa mbunge anapohudhuria vikao vya Bunge, atalipwa posho.

Dk Tulia alisema vitendo vya kutohudhuria mjadala wa Bunge havikubaliki kwa kuwa havikidhi matakwa ya Katiba Ibara ya 23, lakini akasema pamoja na Kiti cha Spika kusisitiza kuwa kutohudhuria mjadala hakukubaliki, lakini kuna haja ya kubadili sheria ili mbunge alipwe baada ya kumaliza kazi.

Pia alisisitiza kuwa Kanuni za Bunge zinazotumika katika kuwalipa posho, hazijaeleza kwa uwazi maana ya neno mahudhurio, hivyo nazo zinahitaji marekebisho kudhibiti hali hiyo.

Baaada ya kutoa muongozo huo, Keissy alisimama na kuomba muongozo mwingine na alipopewa nafasi, aliomba utaratibu wa kutumia mashine za kielektroniki kusaini mahudhurio, ubadilishwe na badala yake urejeshwe ule wa zamani wa mbunge kusaini katika karatasi.

Dk Tulia akijibu muongozo huo, alisema hata ukirejeshwa utaratibu huo, mbunge anaweza kusaini katika karatasi saa tano na kuondoka kwenda Dar es Salaam na kusisitiza kunahitajika marekebisho ya Kanuni za Bunge ili neno mahudhurio, lipewe ufafanuzi wa wazi.

Hata hivyo, aliahidi kuwasiliana na Katibu wa Bunge ili kuona utaratibu mzuri wa wabunge kusaini posho katika wakati wa sasa. 

Baada ya muongozo huo wa Naibu Spika, Msemaji wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu alidai wao wataendelea kususia vikao vyote vya Bunge vinavyoongozwa na Naibu Spika kwa madai kuwa anatumia Kanuni za Bunge, kuwakandamiza.

Akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu Mkataba wa Kimataifa wa Udhibiti wa Matumizi ya Dawa na Mbinu za Kuongeza Nguvu Michezoni, Mbilinyi alisema wabunge wa Kambi ya Upinzani wanaposusa hawarudi nyumbani kupumzika, bali wanashinda katika maktaba ya Bunge kufanya kazi.

Mbilinyi alisema ni heri wabunge wa Kambi ya Upinzani wanaoshinda katika maktaba ya Bunge, kuliko wa CCM wanaohudhuria vikao hivyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images