Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Video ya Rais Magufuli Akipigilia Msumari Sakata la Wanafunzi 'Vilaza' Waliofukuzwa UDOM

$
0
0
Video  ya  Rais  Magufuli  Akipigilia  Msumari  Sakata la Wanafunzi 'Vilaza'   Waliofukuzwa UDOM

Muswada Wa Manunuzi Wamtoa Jasho Waziri Wa Fedha Bungeni

$
0
0

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango juzi alibanwa bungeni baada ya wabunge kutaka maelezo ya kina ya sababu za Serikali kushindwa kuwasilisha muswada wa kurekebisha Sheria ya Manunuzi ambao unalalamikiwa kuwa unachochea ufisadi.

Sheria hiyo imekuwa ikilalamikiwa na wadau, wakiongozwa na Rais John Magufuli, kuwa inatoa mwanya kwa wazabuni kupandisha bei za bidhaa wanapopewa mikataba ya Serikali kwa kushirikiana na watumishi wa umma.

Rais Magufuli alilalamikia sheria hiyo kwa mara ya kwanza Novemba mwaka jana wakati akizindua Bunge, akisema inaumiza Serikali na hivyo itafanyiwa marekebisho.

Juzi, wabunge wa CCM walisimama kidete wakimtaka waziri huyo kuwa na majibu yanayoridhisha na kueleza kuwa asipofanya hivyo, wangekwamisha bajeti yake, ambayo hata hivyo ilipita.

Akichangia hotuba ya Wizara ya Fedha, Mashimba Ndaki alisema Sheria ya Manunuzi imekuwa ikisababisha kero kubwa kwa wananchi na kuwasababishia usumbufu usiokuwa na maana.

Ndaki alisema sheria hiyo haifai, lakini inashangaza kuona Serikali imekuwa kimya. Janeth Mbene alisema haiwezekani kuendelea kufumbia macho jambo hilo tena.

Mbene alisema pamoja na udhaifu wa sheria hiyo, Serikali inatakiwa kuangalia upya kwa kuwa yako mashirika mengi ambayo ni mzigo hivyo akaomba yaondolewe na kufutwa.

Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje alisema sheria ya manunuzi ni mchwa unaotafuna kila mali za umma, lakini Serikali inaonekana kufumbia macho.

"Mimi nimekuwa mjumbe wa bodi ya mashirika mbalimbali, lakini utakuta vitu vinavyonunuliwa na watu moja kwa moja, bei inakuwa chini lakini kwa kupitia bei ya Sheria ya Manunuzi inauwa mara mbili yake, huu ni wizi,” alisema Lubeleje.

Mbunge wa viti maalumu (CCM), Ritha Kabati alisema sheria hiyo imekuwa ikiwanyima nafasi wazalendo.

Waziri Mkuu Majaliwa akutana na wawekezaji wa bandari kavu toka marekani

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na wawekezaji wa Bandari kavu kutoka Marekani, Ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma Juni 1, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Watoto Mkoani Iringa Wapigwa Marufuku Kutembea Saa 12 jioni na Kuendelea

$
0
0
Serikali wilayani Iringa imetoa waraka unaozuia watoto wenye umri wa kuanzia miaka 14 kushuka chini, kutotembea usiku kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ulawiti na ubakaji.

Wiki moja iliyopita wananchi walimpiga hadi kumuua kijana aliyefahamika kwa jina moja la Emmanuel (25-30), baada ya kukutwa akimbaka mtoto mwenye umri wa miaka kumi, katika eneo la Mtwivila, Manispaa ya Iringa.

Pia, katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita matukio 36 ya ubakaji yameripotiwa kutokea manispaa hiyo huku watuhumiwa 17, wakitiwa mbaroni.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema hali ni mbaya hivyo kila mzazi na mlezi anapaswa kumlinda mtoto wake.

Kasesela alisema waraka huo unawataka wazazi na walezi kutowatuma watoto kuanzia saa 12.00 jioni. 

“Ni marufuku mtoto kutumwa kuanzia saa 12, wazazi na walezi wanatakiwa kuwalinda na kuwatunza watoto wao kwa kuwahakikishia usalama,” alisema.

Waraka huo pia umezuia watoto kuzurura hovyo mitaani kwa kuwa wabakaji wamekuwa wakitumia mbinu nyingi ikiwamo kuwalaghai kwa pipi au kuwatuma. 

“Ni marufuku watoto kuonekana baa au vilabu vya pombe za kienyeji, ikibainika wamiliki watachukuliwa hatua kali za kisheria,” alisema.

Alisema matatizo ya ubakaji na kuwalawiti watoto yamekuwa sugu na kwamba unahitaji ushirikiano baina ya polisi, wananchi na viongozi kupambana nayo.

“Nimeagiza polisi kuongeza doria na watuhumiwa wanaokamatwa kwa ubakaji, sheria ichukue mkondo wake ili kukomesha hali hii,”alisema.

Aliwaomba viongozi wa dini kusaidia kutoa elimu kwa waumini wao juu ya kuwalinda watoto na kukemea ukatili huo ambao ni hatari ikiwa utaachwa kuendelea.

Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa, Joseph Lyata alisema imani za kishirikina zimechangia ubakaji na ulawiti kwa watoto kukithiri.

Alisema katika uchunguzi wao walibaini vikaratasi vilivyokuwa vikisambazwa mitaani vikishauri wanaume wanaotaka kufanikiwa kimaisha, wabake na kulawiti watoto wadogo kisha wajiunge na dini yao ya ‘freemason’.

“Mtaa wa Semtema ndiyo ulikuwa tishio na huko tuliokota vikaratasi vilivyokuwa vimeandikwa ukitaka kutajirika, jiunge na freemason pia ubake au kulawiti mtoto chini ya miaka 14,” alisema.

Lyata alisema sababu nyingine ni ulevi wa kupindukia na utumiaji wa dawa za kulevya kama bangi.

Alisema kukithiri kwa vitendo hivyo kumeifanya manispaa hiyo kutangaza jambo hilo kuwa ni janga ambalo lazima wapambane nalo kwa kuwasaka wabakaji.

Naibu meya aliwataka polisi kudhibiti vitendo hivyo vinginevyo watoto wataendelea kuteseka.

Alisema wapo watoto wanaofanyiwa ukatili huo majumbani na wengine mitaani. Alisema wameanza kuwatambua watoto wa mitaani na kuwarudisha makwao ili kuwanusuru kubakwa. 

Watoto wasimulia 
Baadhi ya watoto walisema wamekuwa wakifanyiwa vitendo hivyo na vijana waliopo mtaani, hasa nyakati za jioni.

 “Siku hiyo nilitumwa na mama dukani, wakati narudi kuna mtu akanipa hela nimnunulie mafuta ya taa nimpelekee kwake, nilipompelekea akanifanyia hivi,” alisema mtoto huyo.

Alisema mbakaji huyo alimtishia endapo atasema angemfanyia tena ukatili huo bila huruma. 

“Nilimpa mama mafuta, nikaenda kulala nikilia sana niliogopa kumwambia, bahati aligundua kwa sababu sikuwa naweza kutembea na aliponikagua akakuta nimeumizwa,” alisema.

Mama wa mtoto huyo alisema mbali na kuumizwa mwanaye aliambukizwa magonjwa ya zinaa.Aliiomba Serikali kutowanyamazia wanaume wenye tabia ya kuwabaka watoto.

Mtoto mwingine wa kiume alisema kijana asiyemjua alimpatia pipi akijifanya rafiki yake, hali iliyomfanya waongozane hadi mlima wa Semtema, ambako alimlawiti. 

Wananchi walia 
Kukithiri kwa vitendo hivyo kuliwafanya wananchi waandamane hadi kwa mkuu wa wilaya kuomba msaada. Wananchi hao walieleza kuwa kinachowatesa ni watuhumiwa kuachiwa huru na polisi na kurejea mtaani.

“Ndiyo maana tumeamua tutakayemkuta tunammaliza kwa sababu akienda polisi atarudi tu,”alisema Gerald Matibabu.

Wazazi hao walidai vitendo hivyo vimewachosha, na kwamba wapo watoto walioambukizwa magonjwa ya zinaa ikiwamo Ukimwi.

Mwenyekiti wa mtaa wa Semtema wenye wakazi 3,800, Reminus Ndale alisema mpaka sasa idadi ya watoto waliofanyiwa unyama huo kwenye mtaa wake ni wanne.

Alisema kwa kushirikiana na wananchi wameamua kuhakikisha watoto wao wanalindwa na kuwachukulia hatua kali watakaobainika kuwabaka.

Polisi wazungumza 
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, John Kauga alikiri kuwapo kwa vitendo vya ulawiti na ubakaji na kuwataka wananchi kutoa taarifa haraka vinapotokea.

“Kuna matukio mengi pia majumbani, wazazi wasifiche, watoe taarifa kwa polisi ili hatua kali za kisheria zichukuliwe,” alisema.

Aliwataka wananchi kupinga imani za kishirikina zinazowahamasisha kufanya ukatili kwa watoto kwa madai ya kutajirika.

Wananchi Waanza Kuhama Wakiogopa Kuchinjwa Tanga

$
0
0
Ukatili uliofanywa na watu wasiojulikana wa kuwachinja watu wanane wa kitongoji cha Kibatini mkoani Tanga, umesababisha wakazi wa kitongoji hicho kuanza kuyahama makazi yao.

Watu hao walichinjwa usiku wa Mei 31 nje ya nyumba ya mwenyekiti wa kitongoji hicho kwa madai kuwa walisababisha “vijana” wao kukamatwa na polisi baada ya kutoa taarifa zao wakati wakizurura kwenye eneo lao.

Waliouawa katika tukio hilo ni mwenyekiti huyo, Issa Hussein, kaka yake, Mkola Hussein, Hamis Issa, Issa Ramadhani na wengine wawili waliotambulika kwa jina moja la Kadir, Mikidadi na Salum.

Jana baada ya mazishi ya watu hao, mbunge wa Tanga Mjini, Mussa Mbarouk alipeleka lori aina ya Mitsubishi Fusso kwa ajili ya kuwahamisha wanakijiji hao. 

Wakazi wayahama makazi 
 Diwani wa kata ya Mzizima, Fredrick Chiluba alisema wakazi wa Kibatini wameamua kuhamia kitongoji cha Kona-Z kilichopo kijiji jirani Kiomoni.

Mwandishi alishuhudia wakazi takriban 60 wa Kibatini wakitoa vyombo, huku wengine wakiezua mabati kwenye nyumba zao wakati wakisubiri gari ambalo baadaye liliwasili na kuwachukua.

“Wameingiwa na hofu ya kibinadamu na jambo hili lipo moyoni mwa mtu, hivyo huwezi kumng’ang’aniza kukaa hapo wakati anahisi hayupo salama,” alisema Chiluba.

Hadija Hussein alisema wameamua kuhama kwa sababu mara baada ya kukamilishwa kwa shughuli za mazishi ya ndugu zao wanne, ilipofika saa 6:00 usiku, askari waliokuwepo kwenye viwanja vya nyumba ya marehemu Mkola Hussein kulinda usalama hawakuonekana.

“Tulipatwa na wasiwasi mkubwa tulipoona askari na magari yao wameondoka, tukajua sasa na sisi tunakuja kuchinjwa.Hatukupata usingizi kwa hofu, ndipo asubuhi tukaamua kuondoa vyombo,” alisema.

Alisema mbunge alipokwenda kuwahani, walimuomba gari la kuhamisha vyombo vyao ili waondoke kabla jioni haijafika.

Mbunge Mbarouk alisema alipowasili eneo hilo na kukuta hakuna ulinzi, alimpigia simu mkuu wa polisi wa Wilaya ya Tanga ambaye alipeleka askari.

“Nilipowauliza viongozi wa Jeshi la Polisi waliniambia askari wapo wanafanya kazi ya kuzungukia maeneo, lakini haikuwa haki kuwaondoa askari mara tu baada ya kufanyika mazishi,” alisema Mbarouk.

Mbunge huyo alisema ameushauri uongozi wa polisi kupeleka ulinzi hata wanakohamia kwa sababu wauaji lazima watapata taarifa ya waliko na wanaweza kuwatendea chochote.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Paulo alisema askari hawakuwa wameondoka kijijini hapo bali walikuwa wamefanya mbinu za kufanya doria maeneo yanayozunguka kitongoji hicho.

“Usiku huo kwenye kitongoji kulikuwa na kikosi maalumu cha FFU ambacho mimi mwenyewe nilikuwa nakiongoza usiku kucha. Tulikuwa tukifuatilia maficho ya wahalifu, kitaalamu tunaita undercover,” alisema. 

Kamanda huyo alisema wakati polisi ikiendelea na operesheni, si vyema kuwatisha wananchi kwa kuwa tangu yalipofanyika mauaji hayo, askari hawajaondoka. 

RC: Mauaji ya Tanga si ugaidi 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema mauaji yanayotokea katika mitaa ya jijini Tanga na Amboni si vitendo vya kigaidi, bali yanatendwa na kundi la watu wanaotaka kuvuruga amani.

Amesema hii ni vita ya kiuchumi inahusiana na ujio wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda hadi Tanga na kwamba Serikali itahakikisha inawakamata waliohusika.

Alisema hayo alipokuwa akizungumza na viongozi wa Serikali, Halmashauri ya Wilaya ya Muheza pamoja na vyama vya siasa vya wa wilayani humo.

Shigela, ambaye alikuwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza kupokea taarifa ya maendeleo ya kabla ya kuanza ziara wilayani humo, alisema Serikali haiwezi kukubali kuona kundi la watu wachache wanaharibu amani iliyopo.

Profesa Tibaijuka: Wapo Waliochota Fedha za Escrow Lakini Wamenyamaziwa

$
0
0
Jinamizi la kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow bado linamsumbua mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka baada ya kuliibua kwenye semina ya mapambano dhidi ya ufisadi, akichongea wabunge ambao hawajaguswa.

Profesa Tibaijuka alipoteza uwaziri wa nyumba, ardhi na makazi kwenye sakata hilo baada ya kubainika kuwa aliingiziwa fedha zinazoonekana zilitoka kwenye akaunti hiyo iliyokuwa inamilikiwa kwa pamoja na Tanesco na kampuni ya kufua umeme ya IPTL.

Profesa Tibaijuka alikuwa mmoja kati ya viongozi wa ngazi ya waziri, mbunge, jaji na viongozi wa dini walioingiziwa fedha ambazo zinatokana na Sh306 bilioni zilizochotwa kwenye akaunti hiyo.

Akichangia katika semina hiyo inayolenga kuwajengea wabunge uwezo wa kupambana na ufisadi na ambayo iliandaliwa na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Ufisadi (ACFE), Profesa Tibaijuka alisema wakazi wa jimbo lake walimchagua kwa mara nyingine licha ya tuhuma za Escrow kwa sababu hawakuziamini.

Alisema fedha hizo za Escrow zilitoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kwenda benki ya Stanbic na Mkombozi, lakini cha ajabu majina ya watu waliopewa fedha kupitia benki moja yalitolewa na yale ya benki nyingine yalifichwa.

Alisema inakuwaje yeye anakuwa katika tuhuma, wakati aliyempa fedha hizo hatuhumiwi.

Watu waliotajwa kwenye sakata hilo ni wale waliopewa fedha zilizopitia benki ya Mkombozi, lakini hadi sasa wale waliopewa fedha zinazodaiwa kuwa ni taslimu kutoka Stanbic hawajatajwa.

Alisema sheria pekee yake haiwezi kufanya lolote katika mapambano dhidi ya ufisadi na hakubaliani na wabunge wanaosema kuwa hata kama mahakama imeshindwa kuthibitisha ufisadi, watuhumiwa wataifishwe mali zao.

“Sisi wabunge hatukuja kufanya kazi hiyo, tumekuja kutunga sheria ili zisaidie katika kutuongoza,” alisema.

“Ni vyema kuzungumzia unyofu wa watu kwa kuanzia katika shule, makanisa, misikiti na wabunge.”

Aliituhumu Takukuru kuwa inakubali kutumiwa kwa kuchagua kesi za kuchunguza.“Tume ya Maadili ndio usiseme,” alisema.

“Mie nimeshawahi kushtakiwa Tume ya Maadili, najua kuwa kuna mbunge mwenzetu hapa alipata fedha za Escrow, lakini kwa sababu hakuwa mzungumzaji ameondoka bungeni wala hakuna mtu anajua kama alipata. Unaona jinsi ambavyo hawa watu hawako makini,” alisema.

Mbunge wa Hanang (CCM), Dk Mary Nagu alilia na watu aliowaita wazushi kwamba wanawazushia wenzao kuchukua rushwa wakati hakuna ukweli.

Mwakyembe Ataka Mishahara na Posho za Wabunge wa UKAWA Zifutwe.........Keissy Awafananisha na Watumishi HEWA

$
0
0

WABUNGE wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambao wamekuwa wakiingia bungeni kusaini posho na kuondoka, wako hatarini kufutiwa posho kama wataendelea kususa vikao vya Bunge kama walivyotangaza.

Hali hiyo inatokana na hoja zaidi ya mbili zilizowasilishwa kwa Spika wa Bunge kwa njia ya Mwongozo huku moja ikiwasilishwa na Waziri mwenye dhamana ya Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe, zikikusudia kutaka Bunge kufuta posho za wabunge hao.

Akizungumza jana bungeni baada ya kuruhusiwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, Dk Mwakyembe akitumia ibara za Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 na Kanuni za Kudumu za Bunge, alitaka uongozi wa Bunge kutazama upya kama wabunge hao wanastahili kulipwa posho.

Dk Mwakyembe, kwanza alitumia Ibara ya 26 ibara ndogo ya kwanza na ibara ndogo ya pili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo aliinukuu; “Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii Katiba hii na sheria za Jamhuri ya Muungano. Kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria, kuchukua hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba na sheria za nchi.”

Baada ya hapo alinukuu tena Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 23, ibara ndogo ya kwanza na ya pili;“Kila mtu, bila ya kuwapo ubaguzi wa aina yoyote, anayo haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake, na watu wote wanaofanya kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo kulingana na kiasi na sifa za kazi wanayoifanya. Kila mtu anayefanya kazi anastahili kupata malipo ya haki.”

Kwa kuzingatia ibara hizo za Katiba, alisema kwa kutumia nafasi yake ya raia wa Tanzania na Waziri mwenye dhamana ya Katiba na Sheria, alihoji kama haki inatendeka, kulipa posho na stahiki wabunge ambao hawakuingia bungeni wala hawakuwa katika shughuli inayotambuliwa na Bunge, sawa na waliokuwa wakifanya kazi bungeni.

Alitaka Bunge lifafanue kwa kuzingatia ibara hizo za katiba kama ni haki kulipa wabunge hao wa Ukawa, wanaoingia bungeni na kusaini ili walipwe posho, kwa kubonyeza vitufe vya kielektroniki na kuingia bungeni kwa sekunde chache na kutoka kwenda kupumzika. 

Kuhusu wabunge waliosimamishwa kazi na Bunge, Dk Mwakyembe alihoji kama Bunge linazingatia Kanuni ya 75, ama la.

Kanuni hiyo inasema: “Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge na hataingia tena katika sehemu yoyote ya Ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa, na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana na mshahara huo.”

Kabla ya Mwongozo wa Dk Mwakyembe, juzi usiku Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Keissy (CCM) aliomba Mwongozo na aliporuhusiwa alimtaka Naibu Spika aeleze kama kitendo cha wabunge hao wa Upinzani kuingia na kukaa muda mfupi na kutoka bungeni, kinatofautiana na tatizo la wafanyakazi hewa ambao wanapigwa vita na serikali.

“Kweli Mheshimiwa Naibu Spika, serikali inawaona na wewe unawaona, hii si kuiibia serikali? Au na sisi tuanze?” Alihoji Keissy.

Mbali na Keissy, Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma (CCM) aliomba Mwongozo jana na kumtaka Naibu Spika kuzingatia Mwongozo wa Dk Mwakyembe na Keissy, akieleza kuwa kama si dharau kwa Bunge, kumsimamisha mtu kazi, halafu anaruhusiwa kuitisha mikutano ya kibunge jimboni.

Alimtaka Naibu Spika ambaye ni mwalimu wa sheria, akubali iletwe hoja ya kurekebisha Kanuni za Bunge ili adhabu inayotolewa kwa mbunge, imdhibiti asifanye shughuli zozote ikiwemo mikutano ya hadhara wakati wa adhabu.

Akipokea miongozo hiyo, Naibu Spika aliahidi kutolea uamuzi baadaye baada ya kufanya mashauriano huku suala la adhabu likirejeshwa kwa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Wabunge wa Ukawa kuanzia mwanzoni mwa wiki hii waliazimia kususa kuingia bungeni katika vipindi vyote vitakavyoongozwa na Naibu Spika, kwa madai kuwa anawaongoza kibabe kama wanafunzi na kuwa hajui uchungu wa kampeni katika majimbo.

Hata hivyo, juzi Dk Tulia  aliwataka Watanzania wasikubali kupotoshwa na Kambi Rasmi ya Upinzani, iliyoamua kususa vikao anavyoviongoza, kwa kuwa kama wanaona amekosea, kuna fursa ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wake.

Kwa upande wao, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imewasilisha kwa Ofisi ya Spika wa Bunge kusudio la kumwondoa madarakani Naibu Spika wanayemtuhumu kwa mambo sita ikiwemo upendeleo, ubabe na kufanya kazi kwa maslahi ya Serikali, badala ya umma.

Kusudio hilo la maandishi lilipelekwa katika ofisi hiyo jana na kupokelewa na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah kwa niaba ya Spika, Job Ndugai ambaye hakuwepo ofisini wakati huo.

Mbunge wa Simanjiro, James ole Millya (Chadema) ndiye aliyewasilisha kusudio hilo kwa niaba ya kambi hiyo ya upinzani na kuzungumza na wanahabari kuhusu hatua hiyo, katika mkutano na vyombo vya habari.

Magufuli ataka wanaopita kwenye barabara za mwendokasi zichomolewe tairi za magari yao na ziuzwe

$
0
0

Rais John Pombe Magufuli amechukizwa na uharibifu na matumizi mabaya ya miundombinu ya mabasi ya mwendo kasi na kuagiza mamlaka zinazohusika ziwachukulie hatua kwa wasiofuata sheria.

Akiongea wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Maktaba ya kisasa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Rais John Pombe Magufuli amevitaka vyombo vya sheria kuwachukulia hatua kali baadhi ya watu wanaohujumu miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza kuhusu barabara za mwendokasi, Magufuli ametaka wayakamate magari yanayopita kwenye barabara za mwendokasi na yapelekwe kituoni kisha wachomolewe tairi za magari yao na yauzwe na watakuwa wamepata biashara.

Wapinzani Waanika Sababu 6 za Kumng'oa Naibu Spika

$
0
0

Wabunge wa upinzani wameendelea kususia kwa siku ya tatu mfululizo vikao vya Bunge vinavyoendeshwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson tangu walipotangaza hatua hiyo Jumatatu wiki hii kwa kutokuwa na imani naye.

Tangu Jumanne wiki hii wabunge hao wamekuwa wakisusa vikao vinavyoongozwa na kiongozi huyo kwa madai kuwa anaminya demokrasia.

Siku hiyo wabunge hao waliingia bungeni kama kawaida na Dk Tulia alipomaliza tu kusoma dua ya kuliombea Bunge, walitoka hadi kipindi hicho kilipomalizika na naibu spika kumwachia mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kuongoza, ndipo wote waliporudi ukumbini na kuendelea na shu ghuli zao kama kawaida. 

Juzi, wabunge hao wote kama kawaida waliingia bungeni asubuhi na alipoingia Dk Tulia kuongoza kikao hicho, walisimama na kusikiliza dua ya kuliombea Bunge, kisha walitoka na kuwaacha wabunge wa CCM wakiendelea na Bunge.

Siku nzima ya juzi ambayo Dk Tulia aliendesha kikao cha asubuhi na jioni, wabunge hao hawakuhudhuria na ilipofika wakati wa kusoma hotuba ya msemaji wa kambi ya upinzani kwa Wizara ya Fedha na Mipango, David Silinde aliingia ukumbini akitokea nje na kuomba hotuba yake iingie kwenye kumbukumbu rasmi za Bunge kama ilivyo. Kisha akasema: “Sitaisoma hapa kwa kuwa haturidhishwi na mwenendo wa Naibu Spika wa kutuendesha kama watoto.”

Wabunge hao wa upinzani walitoa sababu sita kwanini wanataka Dk Tulia aondolewe madarakani kwa Azimio la Bunge.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwa niaba ya wabunge hao, Mbunge wa Simanjiro, James Millya alizitaja sababu hizo kuwa ni kwanza Dk Tulia ameweka maslahi ya chama chake cha siasa mbele kuliko maslahi ya Bunge, kinyume na Kanuni ya 8(b) ya Bunge.

“Pili, Mei 6 alitumia vibaya madaraka ya kiti cha Spika kwa kutoa uamuzi wa mwongozo ambao ulikuwa unakiuka Ibara ya 12(2) ya Katiba. Muongozo huo uliokuwa unapinga udhalilishaji wa wabunge wanawake,” alisema.

Ya tatu ni kitendo cha Dk Tulia kuvunja Kanuni ya 64(1) (f) na (g) zinazokataza mbunge kutumia lugha ya matusi kwa mbunge mwingine ambapo alinukuliwa akisema “Mheshimiwa Bwege, usionyeshe ubwege wako humu ndani.” 

Alisema ya nne ni Mei 30 kiongozi huyo aliamua kwa makusudi kuvunja Ibara ya 63(2) ya Katiba na kutumia vibaya Kanuni ya 69(2) na 47(4) ya Kanuni za Bunge kumzuia Joshua Nassari kwa upande mmoja na Bunge zima kwa upande wa pili kutimiza majukumu yake ya kikatiba ya kusimamia na kuishauri Serikali.

“Sababu ya tano ni kuwa Mei 26, mwaka huu Dk Ackson akiongoza kikao cha Bunge bila ridhaa ya upinzani alishiriki kufuta sehemu ya hotuba ya msemaji wa upinzani kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kinyume cha kanuni ya 99(9) ya Bunge bila kushirikisha kamati yoyote ya Bunge,” alisema.

Sababu ya sita, Millya alisema kuwa ni kitendo cha Dk Ackson kukataa taarifa ya maoni tofauti, iliyowasilishwa na wabunge wanne wa upinzani.

Vyama vya Upinzani Kufanya Maandamano Nchi Nzima Kupinga Kusimamishwa Wabunge wake 7

$
0
0
TAARIFA KWA UMMA
Leo Juni 3/2016 Chama cha ACT Wazalendo Kimeelezea msimamo wake juu ya uamuzi uliofanywa na Kamati ya Bunge ya Maadili na Madaraka ya Bunge kuwasimamisha wabunge saba wa upinzani akiwemo Mbunge wa ACT Wazalendo Ndugu Zitto Kabwe.

Uamuzi huu wa Kamati ya Maadili ambayo sehemu kubwa ya wajumbe wake ni wabunge wa Chama cha Mapinduzi(CCM) unafuatia msimamo wa wabunge wa upinzani wakiongozwa na Mbunge wa Chama chetu kupigania maslahi ya wananchi kupata habari za bunge.

ACT Wazalendo inaamini Wabunge hawa wametolewa kafara kwa kupinga vikali uamuzi wa Serikali kuzuia matangazo ya Bunge kurushwa moja kwa moja.

Chama kimeandaa mapokezi haya yaliyopewa jina maalum la “Opereshen” Linda Demokrasia, lengo likiwa ni kuwapa nafasi mashujaa waliofukuzwa bungeni kwa ajili ya kusimamia maslahi ya umma, kuelezea kilichotokea na kinachoendelea bungeni ambacho watawala hawataki kijulikane.

Pia katika mkutano wa hadhara Kiongozi wa Chama ndugu Zitto Kabwe atafafanua kwa kina muktadha wa siasa za sasa na hatari ya kuua vita dhidi ya ufisadi kutokana na namna demokrasia inavyofifishwa

Kwa kutambua umuhimu wa utetezi wa maslahi ya wananchi na kuisimamia serikali kupitia Bunge Chama chetu baada ya mkutano wa Dar esSalaam utakaofanyika Jumapili ya Juni 5 mwaka huu katika viwanja vya Mbagala Zakiem, pia Chama kitafanya mikutano mingine mikubwa ya hadhara katika mikoa ya Mwanza ( 11 Juni, 2016), Kigoma (12 Juni, 2016), Mbeya (18 Juni, 2016) na Morogoro (19 Juni, 2016).

Chama imeviandikia barua vyama vya CUF, CHADEMA na NCCR-Mageuzi kuviomba kushiriki kwenye mapokezi hayo.Tunasubiri majibu ya vyama tulivyowaalika kwa kuwaandikia barua kwa kuwa mpaka sasa hawajatujibu rasmi kama watashiriki ama la zaidi ya kutufahamisha kuwa wamepokea barua zetu

ACT-Wazalendo,inaamini “Operesheni Linda Demokrasia” ni muhimu ikapiganwa na vyama vyote pasipo kujali itakadi ya vyama kwa kuwa hoja hiyo ya kutaka Bunge lioneshwe moja kwa moja ilipoibuliwa na Mbunge Ndugu Zitto Kabwe kuhoji hatua ya serikali kubana uwazi Bungeni,wabunge wote wa upinzani walisimama na kuiunga mkono hoja na kuitetea

Ndugu Ado Shaibu Ado
Katibu, Itikadi Uenezi na Mawasiliano ya Umma,
ACT Wazalendo

Serikali Yakanusha Habari Zilizoandikwa na Gazeti la Kiingereza Kuwa Rais Magufuli Anaongoza Nchi Kwa Msukumo

$
0
0

SERIKALI imekanusha habari zilizoandikwa na gazeti la Kiingereza linalotpka kila wiki lililodai kuwa Rais Dk.John Magufuli anaongoza nchi kwa msukumo licha ya kuonekana mzuri na kuwa taarifa hiyo imelenga kuupotosha umma.

Habari iliyoandikwa kwenye gazeti hilo ilikuwa na kichwa kilicho andikwa “Government by gesture, A President who looks good but governs impulsively”

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana wakati akitoa ufafanuzi wa habari hiyo Kaimu  Mkurugenzi wa Idara Habari Maelezo, Zamarad Kawawa alisema taarifa hiyo haikuwa na uzalendo na amewataka wanahabari kuwa makini na habari zenye mlengo wa kupotosha taifa.

“Nawaombeni wanahabari wenzangu kuweni makini na taarifa zenye mlengo wa kupotosha umma” alisema Zamarad.

Akitoa ufafanuzi kuhusu suala la uchumi Meneja Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Daud Biganda alisema taarifa hiyo siyo sahihi na imelenga kupotosha na inavuruga ukweli kwani Tangu Rais Dk.John Magufuli aingie madarakani kwa kipindi cha kati ya mwezi Desemba 2015 na 2016, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimeweza kuandikisha miradi ya uwekezaji ipatayo 551 yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 9,211.88 kati ya miradi hiyo miradi 229 yenye asilimia 42 inamilikiwa na watanzania, miradi 215 yenye asilimia 39 inamilikiwa na wageni na miradi 107 yenye asilimia 19 inamilikiwa kwa njia ya ubia kati ya watanzania na wageni.

Biganda alisema kuwa miradi yote hiyo ya uwekezaji ilitarajiwa kuzalisha ajira zipatazo 55,970 na kuleta matokeo mengine kwa watanzania na kuwa imesajiliwa na TIC.

Kama umepanga nyumba au kupangisha taarifa hii ikufikie kutoka jeshi la polisi Dar es salaam

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kushirikiana na wenye nyumba kuhakikisha wapangaji katika nyumba wanaingia makubaliano ya mkataba na kuwa na picha zao.
 
Hatua hiyo imetokana na kuwepo kwa watu wanaofanya uhalifu katika maeneo mbalimbali na kushindwa kupatikana pindi polisi wafanyapo operesheni kutokana na kupanga kwenye nyumba hizo lakini wakati akiondoka hawaagi na wenye nyumba wanakosa kuwa na taarifa za watu katika nyumba zao.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishina (CP), Simon Sirro amesema kuwa wenye nyumba ambao watashindwa kufanya mkataba bila picha likitokea tukio dhidi ya mpangaji msalaba utamuangukia mwenye nyumba kuhusika katika uhalifu uliofanywa.

Wakati huohuo Jeshi la Polisi linamshirikia Askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), MT 66807 SGT, George Kwisema kwa tuhuma za kukutwa na vipande kumi vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh. milioni 198 vikiwa katika gari yake yenye namba za usajili T.477 AXS aina ya Suzuki Vitara.

Katika tuhuma za vipande vya meno ya tembo wanaoshikiriwa wengine, ni Shafi Muhibu pamoja na Asha Hassan ambao walikutwa katika gari iliyokuwa imebeba meno ya tembo.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi linawashikiria watu watatu kwa tuhuma za kukutwa na sukari mifuko 35 ya Kilogram 50 ambao walikamatwa Chadibwa Mtaa wa Magogoni Kigamboni Mei 31 mwaka huu, ambayo ilikuwa haijalipiwa ushuru na waliokamatwa na tuhuma za sukari ni Said Bakari (25), Mkazi wa Mbagala , Hamadi Selemani pamoja na Bakari Masudi.

Jeshi la Polisi linafanya upelelezi pia wa mtuhumiwa wa aliyewaleta wahamiaji Haramu na kutoweka katika mazingira ya utatanishi akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.

Rais Magufuli Ateua Mwenyekiti Mpya Wa Bodi Ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Prof. Sufian Hemed BUKURURA kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuanzia tarehe 30 Mei, 2016.

Kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter M. Muhongo (Mb.), amewateua wafuatao kuwa  Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPDC kuanzia tarehe 3/6/2016 hadi tarehe 2/6/2019;

1. Mhe. Jaji Josephat M. Mackanja
2. Balozi Dkt. Ben Moses
3. Prof. Abiud Kaswamila
4. Prof. Hussein Hassani Sosovele
5. Dkt. Shufaa Al-Beity
6. Bi. Mwanamani Kidaya

Imetolewa na;
KATIBU MKUU
3 JUNI, 2016

Mwenyekiti Wa Kamati Ya Uchaguzi Ya TFF Abwaga Manyanga, Asema Hatosimamia Uchaguzi Wa Yanga

$
0
0
MWENYEKITI wa kamati ya uchaguzi ya TFF Wakili Aloyce Komba ameamua kujitoa katika kuratibu na kusimamia mchakato wa uchaguzi wa klabu ya Yanga uliopangwa kufanyika tarehe 25 June 2016 na zaidi ametoa sababu 6 zilizomfanya aamue kujiweka pembeni kwenye mchakato huo.

Sababu zilizomfanya Wakili huyo kuachia ngazi ni kama ifuatavyo;

1. Katika mchakato huo nimetuhumiwa kupanga kumhujumu kwa kukata jina la mmoja wa wagombea nafasi ya uenyekiti Bw. Yusuf Manji. Tuhuma ambazo zilitolewa tarehe 2 June kwa waandishi wa habari.

2. Kutokana na tuhuma hizo, Yusuf Manji amesema ni moja ya sababu zilizomfanya achukue fomu za kugombea uchaguzi utakaoratibiwa na Yanga.

3.Tuhuma hizo ambazo ni kubwa kwangu binafsi na zikigusa taaluma yangu ya sheria zimetolewa wakati klabu ya Yanga inahitaji amani, utulivu na mshikamano mkubwa wa wanachama, wapenzi na washabiki wake, hivyo mimi kutokuwa chanzo chochote cha vurugu zinazoweza kutokea.

4. Tuhuma hizo zinahusu mimi kupewa fedha za hongo au rushwa (kiasi hakijulikani) ili nishawishi wajumbe wenzangu wa kamati ya uchaguzi ya TFF kukata jina la aliyekuwa mgombea mtarajiwa, Bw. Yusuf Manji kwasababu ambazo hazijaelezwa.

5. Napaswa kupisha uchunguzi wowote huru wa tuhuma hizo nzito kama zimeshafikishwa katika vyombo vya uchunguzi wa masuala ya rushwa ili mimi nipate fursa ya kujitetea kwa uhuru zaidi.

6.Kwa kuzingatia ushauri wa watu mbalimbali ninaowaheshimu na kuwapenda sana ndani na nje ya klabu ya Yanga hususani wanasheria wengine nguli wa masuala ya michezo kama vile Wakili Sais Hamad El-Maamry, Wakili Sam Mapande, Wakili Alex Mgongolwa na waandishi wa habari waandamizi wa michezo, nimeona nisishiriki mchakato huu kwa kusimamiwa na TFF au hata ukisimamiwa na klabu ya Yanga yenyewe.

Kwakuwa mimi ni muumini mkubwa wa utawala wa sheria na hasa masuala ya katiba na demokrasia katika vilabu na vyama vya michezo, napaswa kuanzia sasa kutoshiriki vikao vyote vinavyohusu mchakato wa klabu ya Yanga nikiwa kama Mwenyekiti au Mjumbe.

Nawaomba Rais wa TFF, Bw. Jamal Malinzi na Katibu Mkuu Selestine Mwesigwa na wajumbe wenzangu wa kamati ya uchaguzi ya TFF, nimemuachia madaraka ya kuratibu na kusimamia uchaguzi wa klabu ya Yanga, Wakili Domina Mideli, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo.

Rais Magufuli kuwa Mgeni Rasmi Kilele cha Maadhimisho ya miaka 50 ya BoT

$
0
0
KILELE CHA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA BENKI KUU YA TANZANIA (1966 – 2016) KUFANYIKA JUNI 22, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu Benki Kuu ya Tanzania ilipoanzishwa.

Sherehe hizi zitafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam tarehe 22/06/2016 ambapo mgeni rasmi atazindua vitabu viwili na kufuatiwa na kongamano litakaloshirikisha wataalam mbalimbali wa uchumi wakiwemo magavana 20 wa benki kuu kutoka nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Mada kuu katika Kongamano hilo itakuwa: “Beyond Aid and Concessional Borrowing: New Ways of Financing Development in Africa and its Implications”, (yaani namna ya kupata fedha za miradi ya maendeleo zaidi ya misaada na mikopo nafuu na athari zake) itakayowasilishwa na Prof. Justin Lin wa Chuo Kikuu cha Peiking, China. 

Mada hii imechaguliwa kwa kuzingatia changamoto ambazo serikali za Afrika zinakumbana nazo katika kugharamia miradi ya maendeleo wakati ambapo misaada na mikopo nafuu imekuwa ikipungua kwa kiasi kikubwa.

Wachumi waliobobea wa ndani na nje ya nchi, wakiwemo magavana 20 kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC) na wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) watashiriki katika kongamano hilo.

Vitabu vitakavyozinduliwa siku hiyo ni (i) “Tanzania: The Path to Prosperity” kinachoelezea masuala yanayohusu sera za uchumi nchini Tanzania ambacho kimeandikwa na wachumi waliobobea wa ndani na nje ya nchi, na kimechapishwa na Oxford University Press. 

(ii) Kitabu cha pili ni cha miaka 50 ya Benki Kuu ya Tanzania kiitwacho “50th Anniversary of the Bank of Tanzania: Evolution of the Bank of Tanzania’s Role and Functions”, ambacho kinaelezea historia, majukumu, mafanikio na changamoto za Benki Kuu katika kipindi cha miaka 50 na matarajio ya Taasisi hii ya Umma katika maendeleo ya taifa katika kipindi cha miaka 50 ijayo.

Aidha, Tarehe 11/6/16 Mheshimiwa Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa atakuwa Mgeni Rasmi kwenye matembezi ya hisani ya wafanyakazi wa Benki Kuu kutoka makao makuu ya Benki hadi viwanja vya Mnazi Mmoja kuchangia ununuzi wa madawati ya shule za msingi kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Benki. 

Wafanyakazi wa Benki Kuu walioko matawini Mtwara, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya, Zanzibar na Chuo cha Benki Mwanza nao pia watafanya matembezi ya hisani kwenye mikoa yao.

Pamoja na matembezi kutakuwa na maonesho yaliyoandaliwa na Benki Kuu katika viwanja vya Mnazi Mmoja yenye lengo la kuwapa wananchi historia ya taasisi hii, ilikotoka, ilipo na inakoelekea katika kutekeleza majukumu yake.

Benki Kuu ingependa kuwakaribisha wananchi kufika kwa wingi kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja siku hiyo ya tarehe 11/6/16 kujifunza mengi kuhusu taasisi hii ya umma.

Aidha, tunawaomba wananchi kufuatilia vipindi mbalimbali vya redio na makala kwenye magazeti ambapo mengi kuhusu historia, changamoto, mafanikio na matarajio ya Benki yataelezwa na viongozi mbalimbali wa Benki wa sasa na waliopita.

Benki Kuu ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya mwaka 1965 na kuanza kutoa huduma rasmi tarehe 14 mwezi Juni mwaka 1966. Katika kipindi cha uhai wake, Benki Kuu ya Tanzania imetimiza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kulingana na mahitaji ya taifa yalivyojitokeza mwaka hadi mwaka.

Imetolewa na:
Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki
03/06/2016

Clarification on the allegations by the Economist- english language weekly Newspaper about our Government

$
0
0


On 28th May 2016, The Economist – English Language Weekly Newspaper published an article with heading “Government by gesture – A president who looks good but governs impulsively”. 

The article, inter alia misinformed the public and readers that since Dr. John PombeMagufuli came into powers last year “the country has become totally uninvestable”. The Tanzania Investment Centre (TIC) would like to point out that the information portrayed by the newspaper is inaccurate, misleading and distortion of facts.

TIC wishes to inform the public and readers of the following facts:-
1.Since President John Magufuli came into power (from December 2015 to May 2016) TIC has registered 551 investment projects worth $ 9,211.88 million. Of all these projects 229 are owned by Tanzanians, 215 projects are owned by foreigners while 107 projects are owned through joint ventures.The projects are expected to employ 55,970people and bring multiplier effects to Tanzanians

The above registered projects by TIC for the past six months (December 2015 – May 2016) shows an increase of 20.31% compared to six months before President Magufuli came to power i.e. June-November 2015 where TIC registered 458 investment projects worth $ 5,727.29 million. Of all these projects 201 are owned by Tanzanians, 159 projects are owned by foreigners while 98 projects are owned through joint ventures. The projects are expected to employ 39,361 people and bring multiplier effects to Tanzanians .

Generally, investments have increased during President Magufuli’s era which shows high investor confidence towards his Government. Attractive laws, peace, stability good and friendly policy as well asconducive investment environment are other major factors that have attracted both FDI and domestic investment during this period in Tanzania.

2.The World Investment Report 2015 indicates that FDI rose by 14.5% in the United Republic of Tanzania. The Report noted that Tanzania, in 2014, regained its FDI inflows compared to the previous three years. 

In fact, its FDI inflows represented its highest level in 2014 given that it attracted slightly $ 2,142 million compared to $ 2,131 million recorded in 2013. This amount is significantly higher than the very low level of $ 640 million between 2005-2007 (pre-crisis). 

This achievement is due to natural gas reserves discoveries in the United Republic of Tanzania. Indeed, Tanzania remains the leading FDI’s recipient in the East African Community.

3. It is true that, the World Bank Doing Business Report 2016 ranked Tanzania 139 out of 189 countries compared to 145 out of 189 in 2014. 

TIC wishes to clarify thatDoing Business provides an aggregate ranking on the ease of doing business based on indicator sets that measure and benchmark regulations applying to domestic small to medium-size businesses through their life cycle. 

Economies are ranked from 1 to 189 by the ease of doing business ranking. Therefore this has nothing to do with the leadership of Dr. John Magufuli.

4.TIC reaffirms the public and readers that Tanzania is still the best place in East Africa to invest due to the fact that the countryis peaceful and stable. Tanzania has a friendly business environment supported by good investment policy and legislation. 

The Fifth Phase Government under the leadership of President Magufuli continues to take measures to improve investment climate as and when need arises. Tanzania’s investment environment continues to offer predictable, transparent and strong long-term proposition to investors. Investment is legally protected against expropriation and nationalization. 

In terms of investment facilitation, the Tanzania Investment Centre (TIC), Zanzibar Investment Promotion Agency (ZIPA) and Export Processing Zone (EPZA) promote, coordinate and facilitate all investments in Tanzania. These are premier ports of call for investors coming to Tanzania through their well-established one-stop shop facilities. Tanzania’s geographic location position makes her as a natural regional business hub. 

Tanzania borders 8 countries, 6 out of which namely Rwanda, Burundi, Uganda, Malawi, Zambia and Eastern part of the Democratic Republic of Congo, uses the Dar es Salaam port and Tanzania’s railways and roads for their sea freight. This presents good opportunities for investment in infrastructure development, trade, transport and logistics.

Therefore the statement that our country has become totally uninvestable has no truth in it and should be completely ignored by the public and readers.
 
Issued by:
ACTING EXECUTIVE DIRECTOR,
TANZANIA INVESTMENT CENTRE (TIC),
SHAABAN ROBERT STREET,
P.O. Box 938,
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Date: 3st May 2016

Mama Janeth Magufuli aahidi kuendelea kusaidia kambi za wazee na watu wenye ulemavu nchini.

$
0
0

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli ameahidi kundelea kusaidia kambi za wazee na watu wenye ulemavu ikiwamo ukoma kutokana na kundi hilo kusahaulika kwa muda mrefu.

Mama Janeth ameyasema hayo wakati wa hafla ya utoaji wa Msaada wa vyakula, Mafuta kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na madawa katika kambi ya wazee na watu wenye ulemavu ya Nandanga iliyopo Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

Aidha Mama Janeth Magufuli amesema kuwa kwa kutambua umuhimu wa kundi hilo mpaka sasa kwa kushirikiana na wadau wengine ameshatoa Misaada katika Kambi 4 za Mikoa ya Dar es Salaam (NUNGE) Mwanza (BUKUMBI), Lindi (NANDANGA) na Mtwara (NKASEKA) ambayo inathamani ya takribani shilini Milioni 250.

Katika hatua nyingine Mama Janeth Magufuli alizindua jiwe la msingi kwenye Jengo la Zahanati Zahanati ya Nandanga itakayorahisisha upatikanaji wa huduma ya afya kwa wakazi wa eneo hilo waliokuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma hiyo.

Naye Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa amemshukuru Mama Janeth kwa uamuzi wa kutembelea kambi hiyo na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kumuunga mkono ili kusaidia watu wenye ulemavu na wazee.

Akiongea kwa Niaba ya Wazee wa Kambi ya Nandanga Mratibu wa Kambi hiyo Bw. Agnerus Chiamba alimshukuru Mama Janeth Magufuli kwa Misaada hiyo kwani itawasadia kwa kiasi kikubwa kutokana na uhitaji waliokuwa nao.

Tanzania Kuanza Kuuza Masafa ya Mawasiliano kwa Njia ya Mnada Kuanzia Mwakani.

$
0
0

TANZANIA itaanza kuuza masafa ya mawasiliano kwa njia ya mnada kuanzia mwakani.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alisema hayo jana baada ya kumaliza mkutano wake na Mtendaji Mkuu wa Nchi wanachama wa Mawasiliano katika Jumuiya ya Madola, Dk Shola Taylor.

“Kuanzia mwakani mnada wa masafa utaanza, zoezi hilo ni jipya hatuwezi kufanya makosa, nina imani tutapata fedha za kutosha, ” alisema.

Waziri Mbarawa alisema masafa hayo yalipatikana baada ya Tanzania kutoka analojia kwenda digitali ambapo masafa 700- 816 yako wazi.

Alisema baadhi ya nchi barani Afrika zimeanza kuuza masafa kwa njia ya mnada na sasa Tanzania itaanza mwakani na kuongeza kuwa nchi za Ghana na Nigeria zimefanikiwa katika hilo na Tanzania inataka kufanya kitu kutokana na mafanikio hayo.

Alisema watakaonunua masafa watatakiwa kuyatumia, vinginevyo wanaweza kunyang’anywa masafa hayo na kuwa wanataka kujipanga vizuri ili sekta hiyo ipate fedha na anaamini Tanzania itafanikiwa katika hilo.

Alisema pia Jumuiya hiyo imekuwa na mikakati mizuri ya ushirikiano kwenye masuala ya kukabiliana na uhalifu wa kimtandao na jinsi ya kushirikiana.

Alisema nchi nyingi zimeweka mikonga ya taifa na kama serikali watapeleka huduma kwenye hospitali na maeneo mbalimbali ya nchi, pamoja na kutengeneza maudhui, kwani katika nchi hakuna maudhui ya kutosha na kutakuwa na mkakati wa kutosha wa kuweza kutayarisha maudhui kwa njia ya kiswahili ili watu wengi wanaufaike na elimu inayotolewa.

Naye Dk Taylor aliipoongeza Tanzania kwa kupiga hatua katika sekta ya mawasiliano na kuongeza kuwa nchi za Afrika zimeanza kuuza masafa kwa njia ya mnada na katika hilo anaamini Tanzania itafanikiwa kutokana na kupiga hatua katika nyanja ya mawasiliano.

Serikali Kutoajiri Madaktari Watakaotaka Kufanya Kazi Mjini Pekee

$
0
0

SERIKALI imetangaza msimamo wake wa kutoajiri madaktari watakaotaka kufanya kazi katika maeneo ya mijini pekee hususan Dar es Salaam, badala yake imesema itawachukua watakaokuwa tayari kuhudumia wagonjwa katika maeneo yote ya nchi.

Aidha, imeonya tabia ya baadhi ya madaktari bingwa kung’ang’ania kufanya kazi mijini na kusema wanawanyima haki wahitaji wa huduma zao katika maeneo ya mengine tofauti na mijini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alitoa msimamo huo jana bungeni mjini Dodoma, wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Tabora Mjini, Emmanuel Mwakasaka (CCM) aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kupeleka madaktari bingwa katika Hospitali ya Mkoa wa Tabora aliyotajwa ina uhaba mkubwa wa madaktari hao.

Ummy alisema, “Madaktari wanaoomba kazi wajiandae kutawanywa na wajue kuwa sasa hatutachukua watakaotaka kukaa mijini hasa Dar es Salaam, kwa kuwa wananchi katika maeneo mengine yasiyo ya mijini wanahitaji huduma zao pia, hasa madaktari bingwa wa wanawake.”

Alisema anatambua changamoto ya uhaba wa madaktari katika hospitali ya mkoa wa Tabora na kwamba utapewa kipaumbele mwaka huu Serikali itakapoanza kutekeleza mpango wa kupeleka madaktari bingwa kwenye mikoa tisa nchini.

“Tabora imefanyiwa tathmini ikabainika ina uhaba wa madaktari, mwaka huu itapatiwa madaktari kwa sababu tuna mpango wa kuwapeleka katika mikoa nane na huo sasa utakuwa ni wa tisa na utapewa kipaumbele,” alisema Ummy.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Suleiman Jaffo wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Moshi Mjini (Chadema), Raphael Michael alisema, ili kuhakikisha ukarabati wa miundombinu ya hospitali ya Mawenzi unafanyika, Serikali imetenga Sh bilioni 1.35 katika bajeti yake ya mwaka 2016/17.

Katika swali lake la msingi lenye vipengele a, b na c, Michael aliuliza ni lini hospitali hiyo itafanyiwa ukarabati iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi na kuiongezea madaktari na wauguzi.

Aliuza pia ni lini Serikali itakubali ombi la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi la kujenga hospitali ya wilaya na je, Serikali itasaidiaje hospitali ya Mawenzi iweze kupata mkopo kutoka Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB), ili iweze kuboresha miundombinu yake.

Akijibu alisema, mkoa umejiwekea utaratibu wa kufanya ukarabati wa hospitali ya mkoa kupitia fedha za uchangiaji gharama za matibabu.

Hadi sasa zimetumika Sh 14,700,000 kwa ajili ya ukarabati wa mfumo wa maji, jengo la wagonjwa wa nje pamoja na jengo la madaktari waliopo mafunzoni na kuongeza kuwa mkakati uliowekwa ni kuimarisha makusanyo ya mapato ili kujenga uwezo wa kuihudumia hospitali hiyo.

Kuhusu suala la watumishi, alisema hospitali hiyo imepata kibali cha kuajiri watumishi wapya 79 katika mwaka 2015/17 na watumishi 65 wamepangwa kuajiriwa katika mwaka ujao wa fedha ili kukabiliana na upungufu uliopo.

Waziri Mpango: Tutaendelea Kukopa ili Tuendelee

$
0
0
WAKATI deni la Taifa likifikia zaidi ya Sh trilioni 35, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango amesema Tanzania ina mahitaji makubwa ya maendeleo yanayoilazimu kuendelea kukopa, kwa kuzingatia vigezo vya kimataifa vya uhimilivu wa deni.

Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara hiyo ya Sh trilioni 9.5, Dk Mpango alisema kwa kuwa lazima taifa likope ili kuleta maendeleo, ni lazima taifa liwe na madeni.

“Nchi yetu ina mahitaji makubwa ya maendeleo hivyo lazima tukope na ukikopa, unaingia katika madeni,” alisema na kufafanua mambo ya msingi yanayozingatiwa na Serikali wakati wa kukopa.

Jambo la kwanza wanalozingatia kwa mujibu wa Dk Mpango ni masharti ya mkopo, yanayojumuisha riba ambapo wanaangalia riba hiyo ni kiasi gani; muda wa kuanza kulipa baada ya kuchukua mkopo (grace period) na utaratibu wa malipo.

Suala la pili la msingi kwa mujibu wa Dk Mpango, ni mahali fedha hizo za mkopo zinakopelekwa ambapo alifafanua kuwa ukopaji wa Serikali hauna tofauti na ukopaji wa mtu binafsi, ambaye akielemewa anakaribisha matatizo.

Dk Mpango alisema Tanzania inakopa kwa ajili ya kutengeneza miundombinu, akatoa mfano wa ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya Kinyerezi na ujenzi wa barabara nchi nzima, ambao mafanikio yake yasingefikiwa bila mikopo.

Uhimilivu wa deni 
Pamoja na kuendelea kukopa na deni kuwa kubwa, Dk Mpango alisema Serikali hufanya tathimini ya kimataifa kuhusu uhimilivu wa deni kila mwaka ili kujiridhisha na mpaka sasa pamoja na deni hilo kuonekana kubwa kimataifa, Tanzania ina fursa ya kuendelea kukopa zaidi.

Tofauti na inavyoelezwa kila mara na wanasiasa ambao wamekuwa wakichukua deni la taifa na kugawanya kwa idadi ya watu, ili kupata fedha zinazodaiwa kwa kila Mtanzania ikiwemo mtoto aliyezaliwa leo, Dk Mpango alitoa vigezo ambavyo ni vya kimataifa kupima uhimilivu wa deni.

Vigezo hivyo vinavyotumiwa kimataifa kupima uhimilivu wa deni, ni tofauti na kigezo cha kugawanya deni kwa idadi ya watu ambacho ni cha kisiasa na hakitumiki popote duniani isipokuwa kwa wanasiasa wa Tanzania.

Kigezo cha kwanza cha kimataifa cha upimaji wa uhimilivu wa deni kwa mujibu wa Dk Mpango, ni uwiano kati ya deni la taifa na pato la taifa, ambapo kimataifa deni halipaswi kuzidi asilimia 50 ya pato la taifa na kwa Tanzania, deni lipo asilimia 19 tu ya pato hilo.

Kigezo cha pili kinachotumika kupima uhimilivu wa deni la taifa ni deni la taifa kwa uwiano wa mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi. Kimataifa, deni la taifa halitakiwi kuzidi asilimia 200 ya mauzo ya nje na kwa Tanzania, deni la taifa ni sawa na asilimia 97 tu ya mauzo ya huduma na bidhaa nje ya nchi.

Kigezo cha tatu kinachotumiwa kimataifa kupima uhimilivu wa deni la taifa kwa mujibu wa Dk Mpango, ni uwiano wa deni la taifa na mapato ya ndani. Kwa sasa kimataifa deni la taifa linatakiwa lisizidi asilimia 300 ya mapato ya ndani na kwa Tanzania, deni hilo la taifa ni asilimia 145.3 tu ya mapato ya ndani.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images