Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali ya Tanzania yasifika kwa kuwa na uongozi unaozingatia Sheria na Utawala Bora.

0
0
Serikali ya Tanzania yasifika kwa kuwa na uongozi unaozingatia Sheria na Utawala Bora.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angella Kairuki alipokuwa akifungua Mkutano wa siku mbili  wa Kimataifa kuhusu Utawala wa Sheria na Utawala bora.
 
Lengo la mkutano huo ilikuwa ni  kujadili masuala ya Afrika katika kukuza utawala wa sheria katika utekelezaji wa agenda ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030 na agenda ya Umoja wa Afrika ya 2063.

“Mkutano huu wa kistoria nchini Tanzania utasaidia kuleta mageuzi katika Taasisi zinazosimamia masuala ya Sera na Sheria ambayo yatachochea maendeleo mazuri katika nchi za Afrika”, alisema Waziri Kairuki.

Akiendelea kuzungumza Waziri Kairuki alisema uwepo wa Marais wastaafu kama Mhe.Benjamin Mkapa na Dkt. Jakaya Kikwete, katika mkutano huo ni ushahidi tosha wakuwepo na mafanikio ya utawala wa sheria na utawala bora nchini Tanzania.

Kwa upande wa Rais Mstaafu Mhe.Benjamin Mkapa, amesema ili Bara la Afrika liendelee Kiuchumi ni lazima watu wake wapate elimu ya uraia ili waweze kushiriki zaidi katika masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo yao pamoja na kuwepo na uongozi utakaoleta mabadiliko “transformative leadership”.

Naye, Waziri wa Haki Sudani ya Kusini Mhe. Pwanauwilla Unango amesema pamoja na kuwa Bara la Afrika lina matatizo mengi kama vita, njaa, magonjwa na ndoa za utotoni, dunia isiitazame Afrika kwa mtazamo huo pekee, bali inahitaji msaada kutoka Jumuiya za Kimataifa.

Mkutano huo wenye kauli mbiu “Kufikia agenda ya 2030 na agenda ya 2063:Utawala wa Sheria kwa Maendeleo Endelevu ya Afrika”, (Achieving the 2030 agenda and agenda 2063:The rule of law as a driver of Africa’s suistainable development) , umeandaliwa na  Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Sheria (IDLO) la nchini Italia, kwa Ushirikiano wa Serikali ya Tanzania  umehusisha wadau mbalimbali wakiwemo Mawaziri, kutoka nchi mbalimbali za Afrika, Mabalozi kutoka ndani na nje ya Afrika pamoja na wawakilishi wa Mashirika ya kutetea Haki za Binadamu.

Watuhumiwa 6 wa makosa tofauti yakiwemo ya kubaka na kusambaza picha chafu za ngono wanyimwa dhamana, warudishwa rumande.

0
0
Washtakiwa sita wanaokabiliwa na makosa tofauti yakiwemo ya kubaka, kulawiti na kusambaza picha chafu na za ngono wameendelea kusota rumande kwa kukosa dhamana, baada ya mvutano mkali wa mawakili wa upande wa mashtaka na upande wa washtakiwa kuibuka mahakamani hapo, na hakimu anayesikilisha shauri la dhamana kuahirisha shauri hadi Juni 15 mwaka huu kutoa uamuzi juu ya dhamana.

Miongoni mwa washtakiwa hao, wawili,Iddi Adam Mabena (21) mkazi wa Njombe na Zuberi Thabit (30) mkazi wa Mbarali Mbeya wanaokabiliwa na shtaka la kumbaka na kumlawiti binti mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa Wami Dakawa,wilayani Mvomero wanalodaiwa kutenda Aprili 27 mwaka huu majira ya usiku katika nyumba ya kulala wageni ya titii iliyopo wami dakawa wilayani mvomero,shauri lao linalosikilizwa faragha limeahirishwa tena mbele ya Hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya mkoa wa Morogoro Mary Moyo.

Upande wa mashtaka katika shauri hilo linalosikilizwa faragha kwa mujibu wa sheria, umewakilishwa na waendesha mashtaka Gloria Rwakibalila,Edgar Bantulaki,Calistus Kapinga na Mohamed Mkali na limepangwa kufikishwa tena mahakamani hapo Juni 15 mwaka huu kwaajili ya kuanza usikilizwaji wa awali baada ya upelelezi kukamilika.

Uamuzi wa dhamana itolewe ama isitolewe umeshindwa kufikia muafaka baada ya mvutano wa kisheria wa mawakili wa utetezi na wa Jamhuri, katika shtaka la kusambaza picha chafu na za ngono kwa njia ya mtandao kinyume na sheria ya makosa ya mtandao no 14 ya mwaka 2015, linalosikizwa mbele ya hakimu Ivan Msaki,wa Mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa Morogoro,dhidi ya washtakiwa sita,iddi Mabena na Zuberi Thabit,wanaotetewa na wakili Mohamed mkali,na Rajab Salehe,Ramadhani Ally Makunja, Muhsin Ngai na John Peter Thabiti maarufu kama paroko, wakazi wa wami dakawa wilayani Mvomero wanaotetewa na wakili Ignas Punge.

Upande wa mashtaka umeendelea kutetea uamuzi wake wa kuwasilisha kiapo cha kupinga dhamana kwa vile shauri hilo limevuta hisia ya watu, usalama wao utakuwa mashakani wawapo uraiani hasa ikizingatiwa wanadaiwa kudhalilisha utu wa mwanamke na kutoharibu upelelezi kwa vile bado haujakamilika,na kwamba taarifa za kiintelijensia zimebainisha wakiachiwa huru wanaweza wakadhuriwa na jamii.

Hata hivyo upande wa utetezi uliowasilisha hati kupinga kiapo hicho umedai dhamana ni haki ya mshtakiwa,hakuna raia aliyewasilisha kiapo kuhusu hasira kali alizonazo dhidi ya washtakiwa isipokuwa labda ni hisia za mkuu wa upelelezi wa mkoa.

Hakimu Ivan Msaki ameahirisha shauri hilo hadi Juni 15 mwaka huu ambapo uamuzi wa washtakiwa kupewa dhamana au kunyimwa dhamana utajulikana.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya June 2

Sheria ya Mahakama ya Mafisadi Yatinga Rasmi Bungeni

0
0

Serikali imewasilisha miswada miwili ya marekebisho ya sheria mbalimbali ya mwaka 2016 ikiwamo ya kuanzishwa kwa Mahakama Maalumu ya Rushwa.

Watakaokutwa na hatia ya makosa ya rushwa au uhujumu uchumi, watafungwa kifungo kisichopungua miaka 20 na kisichozidi miaka 30.

Kuanzishwa kwa mahakama hiyo ni kutimiza ilani ya CCM na ahadi ya Rais John Magufuli kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana kuwa ataianzisha ili kushughulika na mafisadi pamoja na wahujumu uchumi.

Kwa mujibu wa muswada huo, mahakama hiyo inaanzishwa katika marekebisho ya Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 yatakayo fanyika katika Kifungu cha 3. 

“Lengo la marekebisho hayo ni kuanzisha Divisheni ya Mahakama Kuu ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi itakayokuwa na mamlaka ya kusikiliza na kuamua mashauri yanayohusiana na makosa ya rushwa na uhujumu uchumi, ambayo itakuwa na mamlaka ya kusikiliza mashauri yenye thamani isiyopungua Sh1 bilioni,” unaeleza muswada huo uliowasilishwa kwa mara ya kwanza bungeni jana.

Mbali na makosa hayo, pia mahakama hiyo itashughulika na makosa ya uhujumu uchumi bila kujali thamani yake.

Katika sheria hiyo, yatafanyika marekebisho mengine yanayohusu muundo, mamlaka na utekelezaji wa mahakama inayopendekezwa.

Pia masuala ya kuzuia ufilisi, mamlaka ya Jaji Mkuu kutengeneza kanuni na makosa ya rushwa na uhujumu uchumi, ni mambo yaliyozingatiwa katika marekebisho hayo.

Muswada huo umeeleza kuwa masharti yaliyomo kwenye Sheria ya Usalama wa Mashahidi, Sura ya 446 yanapendekezwa kutumika katika masuala yanayohusiana na usalama wa mashahidi kwa kukifanyia marekebisho kifungu cha 53.

Masuala mengine yanayopendekezwa yanahusu utaratibu wa kuwafikisha watuhumiwa mahakamani, utoaji wa dhamana na adhabu, pamoja na utaratibu wa kukata rufaa.

“Taratibu nyingine za uendeshaji na utekelezaji wa masharti ya sheria hii itakuwa kama itakavyofafanuliwa katika kanuni zitakazoandaliwa na Jaji Mkuu,” umeeleza mswada huo.

Kikwete: Nchi za Afrika Haziwezi Kukwepa Misaada ya Wazungu

0
0
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema nchi za Afrika haziwezi kukwepa misaada kutoka nchi za Ulaya kwa kuwa misaada hiyo ni jukumu lao la kihistoria.

Kikwete alisema hayo jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku mbili unaojadili malengo mapya 17 ya Umoja wa Mataifa yanayohusu ‘Maendeleo Endelevu kwa mwaka 2030’.

Mkutano huo umejikita kujadili lengo namba 16 linalohimiza haki, amani na jamii shirikishi, hasa katika masuala ya utawala wa sheria kama chachu ya maendeleo endelevu.

Kikwete alisema jukumu hilo linapaswa kuendelezwa kwa kuwa maendeleo ya nchi za Ulaya yalitokana na rasilimali walizozitoa Afrika kipindi cha ukoloni.

Alisema nchi za Afrika zina rasilimali za kutosha hivyo, ili zifanye kazi bado kunahitajika uwekezaji ambao utaweza kuinua viwanda na kukuza uchumi wa nchi za Afrika, kwani bila hivyo itachukua muda mrefu kufika mbali kiuchumi.

Hata hivyo, alisema nchi za Afrika lazima zijiwekee utaratibu wa namna ya kupokea misaada hiyo, lakini lengo liwe ni kunufaisha wazawa na kwa kufuata sheria za nchi husika na zile za kimataifa.

“Misaada tunayoizungumzia siyo lazima iwe fedha, bali tunahitaji wawekeze zaidi kwetu kwa mikataba ya kisheria inayolinda wazawa, kwa mfano Tanzania tuna rasilimali za kutosha kama gesi, madini na vinginevyo, lakini hivi vyote vinahitaji kuibuliwa na kutayarishwa. Lazima tuwape nafasi ili kufanikisha lakini kwa sheria zitakazowalinda Watanzania,” alisema Kikwete.

Kauli hiyo ya Kikwete imekuja wakati Rais wa Awamu ya Tano, John Magufuli amekwisha kuweka msimamo katika hotuba zake kadhaa akitaka Tanzania ijitegemee kwa asilimia kubwa badala ya kutegemea misaada ya nje.

Wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya kwanza ya juu (flyover) katika makutano ya Barabara za Mandela na Nyerere eneo la Tazara, Rais Magufuli aliita misaada ya wahisani ‘mkate wa masimango’ na kusema kuliko kula mkate huo ni bora kushindia muhogo.

Ingawa hakufafanua wala kuzungumza kwa undani juu ya kauli hiyo, lakini aliitoa ikiwa zimepita siku chache tangu Shirika la Maendeleo la Milenia (MCC) la Mareka ni kusitisha msaada wa Dola za Marekani milioni 472.8 karibu Sh1 trilioni kwa madai kuwa Tanzania ilikiuka misingi ya kidemokrasia kwa kurudia uchaguzi wa Zanzibar na kushindwa kusimamia She ria ya Makosa ya Mtandao.

Pia, Rais Magufuli Machi 29, akiwa katika kijiji cha Mlimani, Wilaya ya Chato mkoani Geita alisema jukumu kubwa lililo mbele ya Watanzania kwa sasa ni kushikamana na kujisimamia katika maendeleo ili kila mmoja ahakikishe anaongeza uzalishaji na utendaji kazi mahali pake pa kazi.

“Kwa hiyo ni lazima tujisimamie sisi wenyewe, na tukijisimama sisi wenyewe kwa kila mmoja kuwajibika mahali alipo, kama ni mfanyakazi afanye kazi kwelikweli, kama ni mkulima afanye ukulima wake kwelikweli, kama ni mfanyabiashara afanye biashara kwelikweli, kama ni mfugaji afuge kwelikweli, kama ni mvuvi avue kwelikweli, Tanzania hii tutavuka,” alisema.

Mkutano huo ulioandaliwa na Taasisi ya Kimataifa ya Maendeleo ya Sheria (IDLO) yenye makao makuu yake nchini Italia, ambayo kwa Tanzania mlezi wake ni Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mkapa alisema katika nchi yeyote ili kupata maendeleo ni lazima kuwe na Katiba ya wananchi ambayo haitalenga kundi moja.

“Awali nchi nyingi za Afrika hazikuwa na Katiba ya wananchi, bali kulikuwa na Katiba ya chama ambayo kwa sasa ni nchi za kidikteta pekee zimebaki na mfumo huo, kwa sasa tulilenga kuweka sera, mikakati thabiti ili tuweze kutekeleza malengo mapya ya dunia chini ya dira mpya ya Umoja wa mataifa ya maendeleo ya dunia,” alisema Mkapa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki alisema kama ilivyo ajenda ya nchi za Afrika, nchi haiwezi kuwa na utawala wa sheria kama hakuna upatikanaji mzuri wa sheria.

“Lazima uweke mifumo mizuri ya kutatua migogoro pia, utoaji wa vibali bila kutoa rushwa, hata katika uwekezaji utakapokuwa huna sheria nzuri inayolinda upande huo ni vigumu wawekezaji kuwepo,” alisema Kairuki.

Mkurugenzi Mkuu wa IDLO, Irene Khan alisema mkutano huo umejikita katika kujadili haki, amani na jamii shirikishi.

“Lengo ni kuwa na dira mpya ya maendeleo ya dunia inayolenga kutokomeza umaskini, kulinda mazingira, kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kushirikisha makundi yote kwenye jamii katika masuala ya maendeleo,” alisema Khan.

Serikali kukosa mabilioni ya msaada toka USAID

0
0

Serikali itakosa mchango wa dawa zenye thamani ya Dola 375 milioni za Marekani (Sh787 bilioni), ambazo zimekuwa zikichangwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID).

USAID ilitoa mchango huo chini ya mradi wa kutunza na kugawanya dawa hasa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi (ARV) kwa kipindi cha miaka 10 nchini.

Mradi huo ambao pia umeisaidia Serikali kujenga maghala ya kuhifadhia dawa umefikia mwisho.

Hata hivyo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto, Dk Mpoki Ulisubisya alisema licha ya mradi huo kufikia ukomo na kuwa na msaada, wizara imejipanga kuhakikisha kuna uhakika wa upatikanaji wa dawa nchini.

Dk Ulisubisya alisema hata bajeti ya mwaka 2016/17 ya Wizara ya Afya imetoa kipaumbele kwenye dawa.

“Tunataka kuhakikisha Watanzania wanafikiwa na huduma ya dawa kote nchini,” alisema.

Dk Ulisubisya alisema kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita, USAID ilitekeleza mradi huo na wananchi zaidi ya 8,000 wamefikiwa na kupata huduma ya dawa.

Alisema wakati mradi huo unaanza watu waliokuwa wanatapa dawa hasa za ARV walikuwa wachache.

Dk Ulisubisya alisema shirika hilo pia lilisaidia kuweka mfumo wa kisasa wa kielektroniki wa kufuatilia matumizi na mahali dawa zinapopatikana.

Kaimu Mkurugenzi Afya wa USAID nchini, Janeane Dauis alisema mradi huo umekuwa na mafanikio nchini.

Dauis alisema shirika hilo litaendeleza ushirikiano wake na Serikali ya Tanzania ili kuweka msukumo zaidi wa kuboresha sekta ya afya nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu alisema mbali na kupata msaada wa kujengewa maghala na USAID, wako kwenye mkakati wa kujenga maghala yao ya kuhifadhi dawa.

Bwanakunu alisema shirika hilo lilitoa Dola 14.2 milioni za Marekani (Sh29.8 bilioni) kwa ajili ya ujenzi wa maghala.

Mkurugenzi huyo alisema MSD inatarajia kujenga maghala yake.Alitaja maeneo wanayotarajia kujenga maghala hayo kuwa ni Dar es Salaam eneo la Buguruni, Mtwara na Moshi.

Pia, alisema MSD inaendelea kupanua wigo wake katika mikoa mbalimbali ukiwamo Iringa.

Jambazi auawa Mwanza akirushiana risasi na polisi

0
0
POLISI mkoani Mwanza imemuua jambazi baada ya mtu huyo akiwa na wenzake wawili kurushiana risasi na polisi waliokuwa doria baada ya kushindwa kutii amri ya kusimama walipotakiwa kufanya hivyo na polisi.

Akizungumza ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema mauaji hayo yalitokea Mei 31, mwaka huu saa 4.10 usiku katika Mtaa wa Ilemela katikati ya barabara inayopita kati ya eneo zilipo ofisini za Radio Free Afrika (RFA) na Kiwanda cha Samaki cha Mwanza.

Alisema polisi waliokuwa doria katika eneo hilo waliwatilia mashaka watu watatu waliokutana nao usiku huo wakiwa wamebeba sanduku na walipoamriwa kusimama, hawakutii.

“Hawakutii, badala yake watu wale waliongeza mwendo, huku mmoja wao akitoa mfuko uliokuwa na kitu, kumbe ilikuwa ni bunduki na kuanza kurushiana risasi na polisi,” alieleza Kamanda Msangi.

Alisema mtu huyo alifyatua risasi kati ya tatu hadi nne kwa polisi, lakini hazikuleta madhara kwa walinzi hao wa usalama wa raia waliomuua kujibu mapigo kwa kumpiga risasi na kumuua papo hapo huku wenzake wawili wakikimbia na kuelekea kusikojulikana.

Alisema baada ya tukio hilo, polisi walimkuta jambazi huyo akiwa na silaha aina ya SMG iliyochakaa na namba zake zikiwa zimefutika ikiwa na magazini yenye risasi 16. Alisema upelelezi kwa ajili ya tukio hilo unaendelea.

Kamanda Msangi alisema silaha iliyokamatwa hutumika kwenye majeshi na kuwa mwananchi wa kawaida haruhusiwi kutumia silaha ya aina hiyo. 

“Tutapeleka silaha hii kwa wataalamu kwa ajili ya kuitambua maana bunduki ya aina hii hatuna kwenye majeshi yetu,” alisema na kuongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa ajili ya utambuzi.

Dr. Shein Aahidi Kutumbua Majipu ndani ya CCM

0
0
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amewataka wanaCCM kufanya kazi kwa ajili ya kuimarisha chama na kuahidi kuyatumbua majipu hadi katika chama.

Dk Shein alisema kwa upande wa serikali kazi ya kuunda serikali inaendelea na kuwataka watendaji walioteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali kufanya kazi kwa maslahi ya taifa na wananchi wake.

Alisema mtendaji atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake katika sehemu za kazi ni bora akajiondoa kabisa hata kabla ya kusubiri kuondolewa. 

Kwa upande wa CCM, aliwataka watendaji kusimamia majukumu yao bila ya kusubiri kusimamiwa kwa ajili ya kuimarisha chama, kwani kazi hiyo ni ya kujitolea na waliopewa dhamana hizo wanatakiwa kulifahamu hilo na kujituma kwa kujenga chama imara.

“Wapo watendaji katika chama hawatekelezi na kusimamia majukumu yao vizuri na kama ndiyo majipu yenyewe basi tutayaondoa,” alisema.

Afikishwa Mahakamani kwa Tuhuma za Kumuua Mkewe Baada ya Kumkuta Akifanya Mapenzi na Mwanaume Mwingine

0
0
Mkazi wa Kijiji cha Ussonge, Kata ya Nyandekwa, Mkungu Kodoli (50) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora akikabiliwa na mashtaka ya kumuua mkewe.

Akimsomea mashtaka jana mbele ya Hakimu Mfawidhi, Ajali Milanzi, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Frank Matiku alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Mei 26, mwaka huu saa 4.30 usiku nyumbani kwake.

Matiku alidai kuwa mshtakiwa alimpiga mkewe, Nsungurwa Dotto (46) kwa fimbo kichwani na kusababisha kifo chake.

Alidai chanzo cha mauaji hayo ni baada ya mshtakiwa kumfumania mkewe akifanya mapenzi na mwanaume mwingine.

Mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Mshtakiwa hakutakiwa kujibu kitu chochote kwa sababu Mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria kusikiliza kesi za mauaji hadi atapofikishwa Mahakama Kuu baada ya upelelezi kukamilika.

Matiku alidai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na Hakimu Milanzi kuiahirisha hadi Juni 14, itakapotajwa tena.

Serikali Yazidiwa Mzigo wa Vijana Wanaotakiwa Kujiunga JKT ......Waziri Asema ni Vigumu Kuwachukua Vijana Wote Kutokana na Uhaba wa Fedha

0
0

VIJANA wenye sifa za kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kwa mujibu wa sheria wamekuwa wengi kiasi cha kuifanya Serikali kushindwa kuwachukua wote, Bunge limeelezwa.

Hivyo, kutokana na sababu hiyo, Serikali imeamua kuongeza idadi ya kambi za mafunzo ili wachukuliwe wote. Hayo yalisemwa bungeni jana mjini hapa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Munira Mustafa Khatib (CCM) aliyetaka kufahamu ni kwa nini Serikali isianzishe mpango maalumu wa kuwapeleka JKT vijana wanaomaliza kidato cha nne.

Akijibu swali hilo, Waziri Mwinyi alisema, “Uwezo wa JKT kwa sasa kuchukua vijana wa kujitolea ni kati ya vijana 5,000 hadi 7,000 kwa mwaka kutokana na bajeti inayotolewa. 

Alisema, utaratibu wa sasa wa vijana kujiunga na JKT ni ule wa kujitolea kwa vijana wenye elimu ya kuanzia shule ya msingi hadi vyuo vikuu na ule wa mujibu wa sheria unaowahusu waliomaliza kidato cha sita.

“Kuwachukua vijana wote wanaomaliza kidato cha nne kama anavyoshauri mbunge hautowezekana kutokana na uwezo mdogo kifedha,” alisema. 

Hata hivyo, alisema ushauri huo ni mzuri na serikali itafanya maandalizi ya kambi nyingi zaidi na kutenga bajeti kubwa zaidi kwa ajili ya uendeshaji kwa kadri uwezo wa kifedha utakavyoruhusu.

Walioandaa Mgomo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kuadhibiwa

0
0
Wakati Rais John Magufuli akitarajia kuwasili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo, wanafunzi walioandamana wakishinikiza malipo yao ya fedha za kujikimu juzi, huenda wakakumbwa na hatua za kinidhamu.

Wanafunzi hao huenda wakaadhibiwa kwa kosa la kukikuka sheria ndogo ya chuo kwa kuandaa mkusanyiko pasipo kibali cha menejimenti.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma), Florens Luoga alisema jana kuwa, mamlaka za nidhamu chuoni hapo zinaendelea na uchunguzi kubaini nani aliyehusika katika tukio hilo.

“Taratibu na sheria ndogo za chuo haziruhusu mtu kuandaa mkusanyiko ambao haujaidhinishwa na menejimenti. Taratibu hizo lazima ziheshimiwe ili ziendelee kuwa imara. Hivyo tunasubiri ripoti ya waliohusika,” alisema Luoga.

Juzi, wakati wa maandamano ya wanafunzi hao walikuwa wakipaza sauti iliyotolewa na Rais Magufuli wakati wa kampeni za kuwania wadhifa huo akisema:

“Serikali yangu haitarajii kuona mwanafunzi akifukuzwa chuo kwa kosa la kugoma kisa mkopo, bali ikitokea mgomo, watawajibisha maofisa wa Bodi ya Mikopo kwa kuchelewesha fedha.”

Taarifa zilizopatikana jana zilieleza kuwa fedha za wanafunzi hao zimeshawekwa kwenye akaunti zao, juzi jioni.

Rais wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo, Erasmi Leon alisema licha ya wanafunzi hao kukiuka utaratibu, haoni sababu za kuwachukulia hatua kwani hawakusababisha madhara wala uharibifu wowote.

“Endapo kamati ya nidhamu itaamua kufanya hivyo ni vyema wakafanya suala hilo kimantiki na kibinadamu na endapo usimamizi wa sheria ukifuata zaidi unaweza ukasababisha kuibuka kwa mambo mengine tofauti,” alisema Leon.

Alisema wanaendelea kuwasihi wanafunzi kuhakikisha suala hilo halijitokezi tena kwani linaitia doa Serikali yake, uongozi wa chuo na Taifa kwa jumla.

Wanafunzi hao waligoma kuanzia Jumatatu usiku na mgomo wao kuisha juzi, baada ya kupewa fedha zao ambazo zilichelewa kwa madai ya uhakiki wanafunzi hewa unaondelea.

Wabunge 7 wa Upinzani Waliosimamishwa Kuhudhuria Vikao vya Bunge Waongezewa Adhabu

0
0
Wabunge saba wa upinzani waliosimamishwa bungeni, watakumbana na kibano kingine cha kukatwa mshahara na posho kwa kipindi chote cha kutumikia adhabu.

Wabunge hao ambao Jumatatu walisimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa muda tofauti kwa madai ya kukiuka kanuni ni Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Halima Mdee (Kawe), Ester Bulaya (Bunda Mjini), John Heche (Tarime Vijijini) na Godbless Lema (Arusha Mjini).

Adhabu hiyo ilitolewa  kama azimio la Bunge baada ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kupendekeza wabunge hao waadhibiwe kutokana na kuomba mwongozo wa kiti cha Spika kwa jambo ambalo tayari lilishatolewa uamuzi.

Habari zilizopatikana bungeni zilieleza kuwa wabunge hao watakumbana na Kanuni ya Bunge ya 75, ambayo inahusika na masharti ya mbunge aliyesimamishwa kazi.

Naibu Katibu wa Bunge (Shughuli za Bunge), John Joel alithibitisha kuwa utekelezwaji wa kanuni hiyo utafuatwa kwa wabunge wote ambao wamefukuzwa.

Akizungumzia hatua hiyo, Heche alisema hadi sasa hajapata barua ya kusimamishwa Bunge, hivyo hata kama watakata posho au mshahara haimsumbui kwa kuwa hawezi kusikitikia kitu hicho wakati haki inaminywa.

Zitto alisema hajasikia taarifa hizo za kukatwa mshahara kwa kuwa hajapewa barua inayoeleza mambo hayo wala ya kusimamishwa Bunge.

Wapinzani Wawasilisha Hoja ya Kumwondoa Madarakani Naibu Spika, Dr Tulia Ackson

0
0
Wabunge wa upinzani wamewasilisha kwa Spika wa Bunge hoja ya kumwondoa madarakani Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kwa kutokuwa na imani naye.

Hatua hiyo imefikiwa na wabunge hao kufuatia kutoridhishwa na mwenendo wa uongozi wa Dk Tulia anapokalia kiti cha Spika.

Tangu Jumanne wiki hii, wabunge hao wamekuwa wakisusa vikao vinavyoongozwa na kiongozi huyo kwa madai anaminya demokrasia.

Walifikia uamuzi huo baada ya Dk Tulia kuzuia kujadiliwa hoja ya kufukuzwa kwa wanafunzi zaidi ya 7,000 wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) iliyowasilishwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na kukatisha mjadala wa bajeti ya maji.

Kitendo hicho kiliwafanya wabunge wote wa upinzani kupingana na maamuzi ya Dk Tulia, jambo lililosababisha watolewe bungeni.

Kutokana na hali hiyo wabunge hao kupitia Mbunge wa Simanjiro, James Ole Millya akisindikizwa na Mbunge wa Kibamba, John Myika wa Chadema na Mbunge wa Konde wa CUF, Khatibu Said Haji waliwasilisha hoja hiyo kwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah baada ya Spika, Job Ndugai kutokuwapo bungeni.

Hoja hiyo iliwasilishwa kwa mujibu wa Kanuni ya 138 (1)ambayo inaeleza utaratibu wa jinsi ya kumwondoa Naibu Spika.

Kanuni hiyo inasema, “Utaratibu wa kumwondoa Naibu Spika madarakani chini ya Ibara ya 85(4)(c) ya Katiba utakuwa kama ule wa kumwondoa Spika, isipokuwa tu taarifa ya kusudio la kumwondoa Naibu Spika madarakani inayoeleza sababu kamili za kuleta hoja hiyo, itapelekwa kwa Spika ambaye ataiwasilisha kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kuijadili.”

Fasili ya pili ya Kanuni hiyo inasema: “Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaridhika kuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Naibu Spika zinazohusu uvunjaji wa Katiba, Sheria au Kanuni zinazoongoza Shughuli za Bunge, basi Kamati hiyo itaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe bungeni ili iamuliwe.”

Kwa mujibu wa Ibara ya 85(4)(c), Naibu Spika atakoma kuwa Naibu Spika na ataacha kiti cha Naibu Spika endapo ataondolewa kwenye madaraka ya Naibu Spika kwa azimio la Bunge.

Akizungumzia uwasilishwaji wa hoja hiyo, Millya alisema taarifa zaidi watatoa leo kuhusu msimamo wao huo.

Dk Tulia aliwataka wabunge wenye malalamiko juu ya utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za Bunge kukata rufaa kwa kufuata Kanuni za Bunge.

Alisema kanuni ndogo ya 5(2) inasema Spika atawajibika kutilia nguvu kanuni zote za Bunge na 5(3) inasema Spika anaweza kumtaka mbunge yeyote anayekiuka kanuni hizi kujirekebisha mara moja.

Alisema kwa hiyo mbunge yoyote asiyeridhika, kanuni za Bunge zinamruhusu kukata rufaa na zinamweleza nini cha kufanya.

JWTZ Yajitosa Mauaji Ya Watu 8 Tanga.......Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange Atangaza Msako usiku na Mchana

0
0

SERIKALI imetuma kikosi maalumu cha ulinzi, kikiongozwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya kuwasaka watu wanaodaiwa kuwa majambazi ambao wanaendesha mauaji ya kinyama mkoani Tanga.

Uamuzi huo umechukuliwa baada ya watu wanane kuuawa kinyama kwa kuchinjwa juzi usiku katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Manispaa ya Tanga.

Habari za uhakika ambazo tulizipata jana, zinasema tayari vikosi hivyo vimeanza operesheni kali katika mapango ya Amboni ambayo yanadaiwa kuwa maficho ya watu hao.

Akitoa salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya marehemu wanne kati ya wanane waliozikwa Kibatini jana, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange, alisema vyombo vya dola vitahakikisha watu wote waliohusika katika mauaji hayo wanatiwa mbaroni.

“Ndugu zangu nawapeni pole kutokana na kuondokewa na wapendwa wetu… naomba kuwahakikisha sisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola tutahakikisha tunawatia nguvuni watu wote waliohusika na mauaji haya,” alisema Jenerali Mwamunyange.

Alisema tukio la mauaji hayo ni la kusikitisha mno kutokana na Tanzania kusifika kuwa nchi ya amani duniani.

“Tanzania inasifika kuwa na amani duniani kote, lazima hatua za kiusalama zichukuliwe haraka ili kunusuru amani yetu isichezewe.

“Ni tukio la ajabu ambalo limegusa watu wengi wasio na hatia, tutasaidiana na wenzetu kuhakikisha wahalifu hawa wanapatikana,” alisema Jenerali Mwamunyange.

Naye Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Masauni Hamad Masauni, alisema Serikali inaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo ili kuwakamata wahusika ndani ya kipindi kifupi.

Aliwahakikisha wananchi kuwa ulinzi unaimarishwa na kwamba matukio hayo hayatajirudia tena.

“Vyombo vya ulinzi vitafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha tunawatia nguvuni haraka watu waliohusika na mauaji hayo,” alisema Masauni.

Aliwaomba ndugu na jamaa ambao wamefiwa na ndugu zao kuwa na subira wakati Serikali inaendelea kuchukua hatua.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu alisema wataendelea kuimarisha ulinzi na usalama maeneo yote.

Katika hatua nyingine, wakazi wa mitaa mitatu ya Mleni Kati, Mleni Mashariki na Kibatini katika Kata ya Mzizima, Manispaa ya Tanga, wameanza kukimbia makazi yao kwa kuhofia usalama wao baada ya mauaji hayo.

Mauaji hayo yalitokea juzi usiku ambapo watu wanaoaminika kuwa majambazi walivamia nyumba tatu katika eneo hilo, wakiwa wamelala usiku, kisha kuwateka na kuwapeleka msituni kabla ya kuwachinja.

Wakazi hao wanaounda zaidi ya kaya 30, walisema wameamua kuyakimbia makazi yao kwa kutokuwa na imani ya usalama wao katika eneo hilo, baada ya wale wanaoitwa majamabzi kuvamia makazi yao kwa mara ya pili kwa staili ya kutisha.

Kabla ya tukio hilo la juzi, watu wasiofahamika walivamia makazi yao na kuchinja kuku 40, mbuzi wanne na ng’ombe mmoja na kukimbilia mapango ya Amboni na hawajawahi kukamatwa.

Mwandishi wetu  jana  alishuhudia wanawake na watoto wakiwa na mizigo mithili ya wakimbizi wakiondoka katika eneo hilo huku wanaume wakibaki kwa ajili ya kuzika ndugu, jamaa na marafiki zao waliouawa katika tukio hilo.

Mmoja wa wananchi hao, Juma Issa, alisema wamelazimika kuwahamisha wanawake na watoto kwa kuhofia wanaweza kuvamiwa tena kwa mara ya pili.

Nae Lucas Muhina alisema kuwa anashindwa kuhama katika eneo hilo kutokana na kuwa na mifugo, hivyo anashindwa kujua mahali salama pa kuihifadhi.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kibatini, Shabani Mwamini, alithibitisha baadhi ya wananchi wa mitaa mitatu kuhama katika eneo hilo.

“Nyumba nyingi zimebaki na wanaume pekee yake kwani wanawake na watoto wote wamehama kwa sasa,” alisema.

Wakati huohuo, maiti nne kati ya nane zimezikwa jana huku nyingine nne zikisafirishwa nje ya mkoa huo.

Mwamini aliwataja waliozikwa kuwa ni Issa Husein, Mkola Husein, Issa Hamis na Salim Adam.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella alisema kuwa vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.

Simulizi ya Mauaji
Mtoto wa marehemu Mkola Hussein anayeitwa Salimu Mkola (16) alisababisha vilio na simanzi kwa waombolezaji baada ya kusimulia namna watu hao walivyomchukua baba yake na kwenda kumchinja mbele ya nyumba yake.

Akisimulia tukio hilo huku akibubujikwa machozi, mtoto huyo alisema watu hao walifika nyumbani kwao wakagonga mlango saa sita usiku na kumuamrisha baba yao atoke na fedha.

“Nilipoona hivyo nilijaribu kupiga kelele kuomba msaada kwa majirani, lakini mmoja wa wauaji aliingia ndani na kunitoa nje ya nyumba yetu, huku akiniuliza wakati wale vijana saba
wanachukuliwa na polisi mimi nilikuwa wapi.

“Waliendelea kuniuliza kama nina habari ninayoijua, huku wakiwa wameshika mapanga na bunduki, ndipo waliponiambia wapo kwa ajili ya kutetea dini yetu.
 
“Baadaye waliniruhusu niingie ndani na kulala, lakini niliendelea kusikia vishindo vya kipigo na watu wakikoroma ambayo ilikuwa ni ishara ya kuwa baba yangu alikuwa anakata roho pamoja na watu wengine,” alisema.
 
Mtoto mkubwa wa marehemu, Abuu Mkola, alisema vijana saba ambao sasa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi awali walionekana katika Kitongoji cha Kibatini wakiwa wanakimbia kusikojulikana.

Alisema baada ya hali hiyo baba yake ambaye ni marehemu, Mkola Hussein akishirikiana na wananchi wa mtaa huo walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ambao walikuja na kuwakamata vijana hao lakini mmoja wao alifanikiwa kukimbia.
 
Abuu alisema kuwa katika tukio la juzi, wauaji hao wakati wanamchukua baba yake walisema wanawahitaji vijana wao saba waliokamatwa na polisi, lakini aliposema hajui ndipo walimuunganisha na watu wengine kwa ajili ya kumchinja.

Bunge Lataka Taarifa
Ofisi ya Bunge imeiagiza Serikali kutoa taarifa rasmi kuhusu mauaji yanayoendelea nchini ili kuwatoa hofu wananchi waliopo katika maeneo mbalimbali.

Akitoa maagizo hayo, Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson alisema Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni anapaswa kuzungumza na Kamati za Ulinzi na Usalama katika maeneo yote ambayo yametokea mauaji ili aweze kutoa taarifa ndani ya Bunge.

“Waziri atuletee taarifa kwa sababu Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) yupo hapa na waziri anayehusika na mambo ya Bunge yupo, naomba watuletee taarifa kwa sababu mauaji yamekuwa yakitokea mara nyingi na tumekuwa tukiwasihi Serikali ituletee taarifa na si mtakuwa mnazitafuta,” alisema Dk. Tulia.

Baada ya maelezo hayo Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM) alisimama na kuomba mwongozo chini ya kanuni 68 (7).

“Mheshimiwa Naibu Spika pamoja na haya uliyoyatolea maelezo juu ya mauaji yanayotokea katika nchi yetu, nimelazimika kuomba mwongozo huu kwa sababu matukio yaliyoanza kujitokeza katika maeneo mbalimbali na maeneo mengine mambo haya tuliwahi kuyauliza Serikali na kuahidi watayatolea ufafanuzi.

“Sasa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani  amekwenda kuangalia na atazungumzia jambo hilo wakati mambo haya wabunge tulishaiomba Serikali itoe ufafanuzi ni jinsi gani inajipanga kukabiliana nayo,” alisema Lugola.

Alisema kitendo cha Serikali kusema Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi amekwenda kushughulikia jambo hilo wakati huo huo mambo ambayo yametokea Mwanza na maeneo mengine yalishaombewa ufafanuzi lakini hakuna majibu si kizuri.

Jinsi Ya Kutengeneza Tiba-lishe Ya Kutibu Na Kuponyesha Kabisa Tatizo La Vidonda Vya Tumbo.

0
0

Vidonda  vya  tumbo  ni  tatizo  linalo  watesa,  mamilioni  ya  watu  duniani.  Hata  hivyo, kama  wewe  ni  mhanga  wa  tatizo  la  vidonda  vya  tumbo, unaweza  kupona  tatizo  lako  kwa  kutumia   lishe  ( Tiba-Lishe )  Asilia.

Asali
Tiba lishe  asilia  ya  kutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la  vidonda  vya  tumbo, inaandaliwa  kama  ifuatavyo :

MAHITAJI.
i.Maziwa  fresh   nusu   lita.
ii.Mayai  manne  ya  kuku  wa  kienyeji
iii.Asali mbichi  ya  nyuki  wadogo  nusu  lita. ( Igawanye  katika  robo lita )
iv.Kijiko  kimoja  kikubwa  cha  unga  wa  makaratusi
v.Kijiko  kimoja  kikubwa  cha  unga  wa  Habat   Sodah.
vi. Ufuta  robo  kilo
vii. Dawa  asilia  ya  Mkatavido.

MATAYARISHO :
A. Chukua  maziwa  fresh  kiasi  cha  nusu  lita  na  uyachemshe, kisha  yaipue  halafu  yaache  hadi  yapoe.  Yakisha  poa, tia  ndani  yake  viini  vinne  vya  mayai ya  kuku  wa  kienyeji.  Halafu  ongeza  robo lita  ya  asali  mbichi  ya  nyuki  wadogo, kisha  weka  kijiko  kimoja  kikubwa  cha  unga  wa  makaratusi, pamoja  na  kijiko  kimoja  kikubwa  cha  unga  wa  Habbat   Sodah. Koroga  mchanganyiko  wako  na  uuhifadhi  kwenye   chombo  kisafi.

MATUMIZI : Tumia  kula  vijiko  viwili  vikubwa, mara  tatu  kwa  siku  kwa muda  wa  siku  saba.

B : MATAYARISHO.
Chukua  ufuta  robo  kilo, utwange  kisha  uchanganye  kwenye   robo lita  ya asali  mbichi  ya  nyuki  wadogo, weka  kwenye  chupa  ya  plastiki, tikisa  na  uache  mchanganyiko  wako  kwa  muda  wa  lisaa  limoja.

MATUMIZI :  Tumia  kula   vijiko  viwili vikubwa, mara  mbili  kwa  siku  kwa  muda   wa  siku  kumi.

C : MATAYARISHO.
Chukua  vijiko  viwili  vya  dawa  ya  MKATAVIDO, kisha  changanya  kwenye  glasi  yenye  maziwa  ya  moto  ambayo  ujazo  wake  ni  milimita  mia  mbili  na  hamsini. Ukimaliza  hapo  koroga  kisha   iache  kwa  muda  wa  dakika  tatu.

MATUMIZI : Tumia  kunywa  mara  mbili  kwa  siku, asubuhi  na  jioni  kwa  siku  thelathini.

JINSI  YA  KUPATA  DAWA  YA  MKATAVIDO :  Kwa  mahitaji  yako  ya  dawa  ya  MKATAVIDO    pamoja  na  dawa  zote  zilizo  orodheshwa  hapo  juu,  fika  katika  ofisi  za  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC, duka  la  kuuza  dawa  mbalimbali  za  asili  lililopo  jijini  Dar  Es  Salaam, katika  eneo  la  UBUNGO  jirani  na  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING, nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.
 
Kwa  wateja  wa  jijini  Dar  Es  Salaan, wasio   na  nafasi  ya  kufika  ofisini  Ubungo, watapelekewa  dawa  mahali  walipo, kwa  wateja  waliopo   mikoani  na  nchi  jirani, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabasi, kwa  wateja  waliopo   Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  Boti, kwa  DIASPORA, watatumiwa  dawa  kwa   njia  ya  POSTA  au  DHL.
 
KWA  MAWASILIANO   YA  SIMU, PIGA  SIMU NAMBA  0766  53  83  84.
 
Na  Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu,  tembelea  kila  siku :


Maalim Seif Aitisha Mgomo Baridi Unguja

0
0
SIKU moja tu baada ya kuhojiwa na Polisi kwa saa tatu visiwani hapa, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, amesema njia pekee ya kumwondoa Rais Dk. Ali Mohamed Shein madarakani, ni kuendeleza mgomo baridi.

Maalim Seif alisema hayo jana alipozungumza na wafuasi wa chama hicho, Kilimahewa Wilaya ya Mjini Unguja, katika ziara zake za kuimarisha CUF katika kila wilaya za Zanzibar.

Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Salum Msangi, aliwaambia waandishi wa habari juzi kuwa jeshi lake lilimhoji Maalim Seif kwa saa tatu.

Ingawa Msangi hakusema walimhoji katika masuala gani, Wakili wa Maalim Seif, Awadh Ali Said, alisema juzi kuwa mteja wake aliwekwa kati na maafisa 12 wa polisi, ambao walitaka kujua pamoja na mambo mengine, ni kwa nini hawakatazi wafuasi wake kumwita Rais.

Akizungumza jana, Maalim Seif alisema mataifa ya nje hayawezi kumwondoa Dk. Shein madarani lakini kama wananchi na wafuasi wa CUF wataungana kufanya mgomo baridi, haitafika miezi mitatu kabla hajaachia madarakara.

“Wala msidhani kwamba atakuja Mmarekani kumwondoa Dk. Sheni," alisema Maalim Seif na kuongeza kuwa: "Hii ni nchi, taifa lingine haliwezi kuingilia."

Katibu mkuu huyo alisema anachoweza kufanya Mmarekani ni kuzuia misaada na wameshalianza hilo.

"Sasa hawa wezetu mataifa ya nje wanatubeba na anayebebwa hujikaza. Tukikaza uzi huyu bwana miezi mitatu hafiki kwa sababu hana fedha, ataweza vipi kuiongoza Serikali wakati baadhi ya mataifa yameshazuia misaada yao?" alihoji.

CUF imegoma kuitambua serikali ya Dk. Shein kwa madai kuwa uchaguzi mkuu wa marudio wa Machi 20, mwaka huu, uliomwingiza madarakani ni batili.

CUF inadai kutambuliwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana, ambao ilielekea kushinda na ambao matokeo yake yalifutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanizbar (ZEC), Jecha Salum Jecha, kwa madai ya kuwapo kwa kasoro nyingi.

ZEC ilifuta matokeo hayo licha ya waangalizi wa ndani na wa kimataifa, wakiwemo kutoka Jumuiya ya Madola, Jumuiya ya Ulaya (EU) na Marekani kuutangaza kuwa huru na haki.

Akizungumza katika kikao hicho jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui, alisema Maalim Seif ndiye mkombozi wa Wazanzibari kama alivyokuwa Nelson Mandela wa Afrika Kusini.

Alisema wana imani kuwa Maalim Seif ndiye Rais wa Zanzibar na wataendelea kumwita Rais na hakuna wa kuwazuia kwa sababu yeye ndiye aliyeshinda katika uchaguzi wa Oktoba 25.

Alisema kitendo cha wafuasi wa CUF kuwatenga wafuasi wa CCM na viongozi wa Serikali walioko madarakani ni halali na kuwataka wafuasi hao kuendelea na mgomo huo.

“Hakuna cha kuogopa, endeleeni kuwagomea," alisema Mazrui na kuwataka wasiende katika shughuli zao, mazishi na wanaouza maduka wasiwauzie bidhaa mpaka haki yao irejee.

Update: Wabunge Wote Wa Upinzani Watoka Nje Asubuhi Hii Kupinga Naibu Spika Kuendesha Vikao vya Bunge

0
0

Wabunge wote wa vyama vya upinzani leo tena  wametoka nje kupinga Naibu Spika wa Bunge  Dk. Tulia Ackson kuendesha vikao vya Bunge na kumwachia Bunge yeye na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Taarifa kutoka Bungeni zinaeleza kuwa, wabunge wote wa upinzani wametoka nje kususia kikao cha Bunge ikiwa ni kutekeleza azimio lao la kutokuwa na imani na Dk Tulia.

Baada tu ya kusomwa dua ya kufungua Bunge, wabunge hao wametoka nje  majira ya saa 3:00 asubuhi na kumwacha Dk. Tulia akiwa na wabunge wa CCM pekee.

Kambi  upinzani  ilianza utaratibu huo juzi kwa kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge baada ya Dk. Ackson kuingia ukumbini.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, juzi alisema wataendelea kutoshiriki vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika hadi pale "haki itakapopatikana."

Rais Magufuli Azungumzia Sakata la Wanafunzi Waliotimuliwa UDOM.......Ashangaa Fedha za Mikopo kupelekwa kwa ‘Vilaza’

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma walioondolewa chuoni hivi karibuni hawakuwa na sifa za kujiunga na masomo chuoni hapo.

Akizungumza leo katika uzinduzi wa Maktaba mpya ya Kisasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Magufuli amewataka watanzania kuweka siasa kando nakuzungumzia masuala ya msingi, huku akiwashangaa wanasiasa waliojitokeza kuwatetea wanafunzi hao.

“Nimeshukuru wale vijana wameondoka. Wanasiasa haohao, ‘eti ooh.. hao vijana wamekosa pa kulala.. it’s nonsense’. Taifa letu tuliweke mbele kwanza. Siasa zije nyuma,” alisema.

Alisema kuwa baadhi ya wanafunzi ambao walibainika kuwa na elimu ya kidato cha nne waliofeli masomo yao na kuruhusiwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu ni watoto wa viongozi.

“Ukimchukua mtoto wa form four ukampeleka pale, hata kama atafanikiwa kupata degree… itakuwa ya ajabu. Na baadhi ya watoto waliopelekwa pale ni watoto wa viongozi. Watoto wa Maskini wenye qualification wamekosa nafasi za kwenda Chuo Kikuu. Watoto wa watu fulani fulani wanapelekwa wakati walifeli. It can’t be,” Dk. Magufuli alisisitiza.

Rais Magufuli aliongeza kuwa Serikali yake haitaruhusu fedha zinazopaswa kutumika kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kupelekwa kwa ‘vilaza’ huku waliofaulu wakikosa mikopo ya elimu ya juu.

Dk. Magufuli ameahidi kuwa Serikali yake itahakikisha wanafunzi waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza na la pili (division 1 &2) wanajengewa mazingira mazuri ya kuendelea na masomo.

“Waliofeli watafute vyuo vyenye size yao,” alisisitiza.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya June 3

Mama Janeth Magufuli amshukuru TB Joshua kwa kuuunga mkono jitahada zake za kusaidia wazee.

0
0
Mke wa Rais, Janeth Magufuli amewaomba viongozi kusimamia na kuhakikisha misaada yote inayotolewa kwa ajili ya wazee na watu wenye mahitaji maalumu inawafikia walengwa.

Pia, alimsifu mhubiri wa Nigeria, TB Joshua kwa kujitoa katika kuwasaidia wazee na watu wasiojiweza nchini huku akiitaka jamii iige mfano huo.

Mama Magufuli alisema hayo alipokuwa akitoa misaada katika Kituo cha Kaseka cha Wazee na Walemavu wa Ukoma kilichopo wilayani hapa Mkoa wa Mtwara.

“Niombe viongozi waliopo hapa kuhakikisha walengwa wanafaidika na misaada wanayopata, tayari nimepata malalamiko mengi kutoka kwa Wasukuma wenzangu kule Mwanza, yanavunja moyo.

‘‘Naomba watu wasiuze wala kuiba ni dhambi kubwa ukichukua chakula cha mtu mwenye mahitaji na asiyejiweza hiyo laana itakufuatilia kwa sababu ni sadaka ishaombewa,” alisema.

Mama Magufuli kwa kushirikiana na Mke wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa walikabidhi misaada mbalimbali ikiwamo vyakula, nguo, saruji, vitanda na magodoro ambavyo vimetolewa na TB Joshua, kampuni ya Super Doll, Dangote na viongozi wanawake wa Mkoa wa Mtwara.

“Niombe wizara, taasisi, Serikali na mashirika ya ndani na nje kuiga mfano wa TB Joshua kwani hakuangalia utaifa wala dini, uwapo wetu hapa unaonyesha ni namna gani nchi na mila zetu za Kitanzania zinavyothamini na kuheshimu wazee na watu wenye mahitaji maaalumu,” alisema Mama Magufuli.

Mwenyekiti wa wazee hao, Cosmas Mbego aliwashukuru waliotoa misaada hiyo akisema wanashangazwa kwani hawakuwahi kutembelewa na wake wa viongozi waliopita.

“Lakini niseme ukweli maji huwa hatupati. Mlipokuja ninyi yanatoka lakini mtakapoondoka watayafunga,” alisema Mbego 

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego aliwahakikishia wazee hao kuwa tatizo la maji limeondoka na watakapoondoka yataendelea kutoka.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images