Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Polisi Yaahirisha Kumhoji Maalim Seif Sharif Hamad

$
0
0
Jeshi la Polisi Zanzibar limeahirisha kumhoji Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad kwa sababu zilizoelezwa kuwa nje ya uwezo wake.

Katika barua yake kwa Maalim Seif iliyosainiwa na DCP Salum Msangi kwa niaba ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, haikutaja ni lini mahojiano hayo yatafanyika lakini imesema, “Tutakujulisha mapema siku ya mahojiano itakayofuata mara baada ya kukamilisha taratibu”.

Barua hiyo ya Mei 26 imenukuu barua ya awali ya Mei 22, 2016 iliyomuita mwanasiasa  huyo makao makuu ya polisi Zanzibar kwa mahojiano kuhusu, “masuala mbalimbali yanayohusu ulinzi na usalama wa visiwa hivi.”

Kutokana na hatua hiyo, Maalim Seif aliyetarajiwa kuwasili jana saa 3 asubuhi Zanzibar kutoka Dar es Salaam kwa ajili ya kuhojiwa aliahirisha safari hiyo na kuwasili Saa 10  jioni kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya kichama kuanzia leo katika wilaya  saba za Unguja.

Mkuu wa Mkoa Afumaniwa Akifanya Mapenzi na Mwanae

$
0
0

Mkuu wa zamani wa Mkoa wa Kaskazini Pemba na mshauri wa Rais wa Zanzibar kisiwani humo, Dadi Faki Dadi amekamatwa akituhumiwa kufanya mapenzi na mtoto wake wa kambo.

Dadi alikamatwa juzi akidaiwa kukutwa na mtoto huyo wa mkewe wa ndoa mwenye umri wa miaka 21 katika nyumba ya kulala wageni inayoitwa Executive, jirani na makao makuu ya Uhamiaji Zanzibar katika eneo la Kilimani chini na Maisara, mjini Unguja.

Mwanasiasa huyo alijikuta akipigwa pingu na polisi akiwa kifua wazi mbele ya mkewe na wanafamilia na kisha kupelekwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Mwembemadema.

Picha za video zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, zilimwonyesha Dadi akikabiliwa na mashambulizi makali ya maneno kutoka kwa watu waliomkamata, akiwamo mkewe.

“Mwacheni avae nguo kwanza, mpeleke bwana, twende bwana..." ni baadhi ya maneno yanayosikika katika video iliyorekodiwa wakati wa kumtia mbaroni.

Taarifa zilizopatikana miongoni mwa wanafamilia ya kiongozi huyo, zilidai kwamba alikamatwa baada ya kumtilia shaka binti huyo kutokana na mienendo yake ya hivi karibuni na kuamua kumfuatilia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam alithibitisha kumshikilia Dadi kwa muda kabla ya kumwachia kwa dhamana.

“Kijamii alitenda kosa, lakini sisi tunaendelea kufanya uchunguzi, iwapo tutabaini ametenda kosa la kisheria na anaweza kuwa mashtaka tutamkamata ili kumpeleka katika vyombo vya sheria,” alisema Mkadam.

Mmoja wa wanafamilia ambaye aliomba jina lake lisitajwe alisema:“Mwizi siku zake ni arobaini, tulimtega na hatimaye tumemnasa sasa tuone mwisho wake utakuwa nini na kipi kitajiri baadaye.”

Mazito Yaibuka Mauaji ya Dada yake Bilionea Msuya .........Yadaiwa Binti wa Kazi Alitoweka Mchana, Usiku Dada Akachinjwa

$
0
0
Siku moja baada ya kifo cha dada wa bilionea Erasto Msuya, Aneth imebainika kuwa msaidizi wa ndani aliondoka saa sita mchana kwa kuacha funguo nyumba ya jirani.

Akizungumza nyumbani kwa dada wa marehemu, Mbezi Juu, mama mdogo wa marehemu Lilian Benjamin alisema msaidizi huyo alimpigia simu bosi wake mchana na kumwambia anaondoka na hataendelea na kazi.

Alisema marehemu alilazimika kuomba ruhusa mapema kazini ili arudi nyumbani kwake Kibada lakini ilimlazimu kukaa nje ya nyumba kwa saa mbili baada ya kufika saa tisa alasiri na kukuta mlango umefungwa.

Mama huyo alisema baada ya kusubiri kwa muda aliwauliza majirani wakamweleza kuwa walipelekewa funguo na mwanafunzi wasiyemfahamu akadai kuwa alipewa na dada mmoja aliyemuelekeza aipeleke nyumba hiyo.

Haifahamiki mpaka sasa mahali alipo mfanyakazi huyo anayedaiwa kuwa mwenyeji wa Arusha.

Dada mkubwa wa marehemu, Happy Msuya alisema marehemu aliwaeleza mambo hayo baada ya kupigiwa simu na msichana huyo wa kazi.

Dada mwingine wa marehemu ambaye ni wa nne kuzaliwa kati ya watoto saba wa Elisaria Msuya, Ester, alisema wauaji hao hawakuwa na nia ya kuiba, bali ni kuua kwa sababu hawakuchukua kitu chochote zaidi ya televisheni ambayo nayo waliitupa mbali na nyumbani.

Ester alisema mara ya mwisho kuonana na marehemu ilikuwa Mei saba walipokutana benki na mazungumzo yao yalihusu hali ngumu ya maisha. Alisema hakuwahi kumwambia kama ana ugomvi na mtu kwa sababu alikuwa mpole na msiri.

Akielezea tukio hilo alisema inaonekana kulikuwa na purukushani kubwa chumbani kwa sababu besela la kitanda lilikuwa limevunjika na neti ilikuwa imetoka, huku nyaraka zikiwa zimepekuliwa na kusambazwa karibu kila kona ya chumba.

“Walikuja kuua, kuna kitu walikuwa wanatafuta katika nyaraka pia, ooh... Aneth umekufa kinyama, umechinjwa kama mnyama,” Ester alishindwa kuendelea na kuanza kulia na baadaye kidogo alisema wauaji walimkata marehemu koromeo lakini hawakutenganisha kichwa na kiwiliwili.

Simulizi ya mtoto 
Mtoto wa marehemu mwenye umri wa miaka minne ambaye alikuwa akiishi na mama yake alisema: “Walikuja watu watano weusi usoni, wakanifanya na kitu shii usoni, nikalala kwenye kiti mbu wameniuma hadi niliposikia gari la shule likiita pipii, nikaamka na nikamuamsha mama anivalishe nguo za shule lakini akakataa kuamka, ”alisema mtoto huyo na kuongeza.

“Nikavaa mwenyewe nguo za shule na nikamwambia mama nitaendaje shule huku sijafanya “Home work” lakini mama hakujibu, mbu walining’ata pale kwenye kochi nilipolala, nikatoka nje nikakuta gari limeshaondoka, nikaenda kwa mama Salum,” alisema.

Alisema alienda huko akale kwa sababu njaa ilikuwa inamuuma hakula jana yake baada ya ‘wageni’ hao kuja na yeye kulala.

Alieleza kuwa alipowaambia mama yake hamjibu amelala tu alirudi na dada ambaye amemsahau jina kutoka hapo kwa mama Salum ambaye alipofika nyumbani kwao na alipomuona mama yake alianza kupiga kelele.

Ester alisema mwili wa marehemu utasafirishwa Jumatatu ijayo kuelekea kijijini kwao Kairo, Simanjiro mkoani Manyara.

Mtu wa karibu na familia ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema mbali ya kaka yao Erasto kuuawa kwa risasi, dada yao Ester akiwa na mumewe katika Baa ya Hongera, Dar es Salaam alipigwa risasi na kunusurika kufa.

CCM Zanzibar Yawataka Viongozi Wake Kupambana Na Upotoshaji.

$
0
0

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewaagiza  viongozi wake kuzisoma vizuri Katiba ya CCM, Kanuni za maadili na Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984, ili wawe na uwezo wa kujibu hoja za baadhi ya watu wanaosambaza fitna na uzushi wa kukichafua chama hicho.

Kimesema kiongozi yeyote mwenye uwezo na uelewa mzuri juu ya miongozo hiyo hawezi kuyumbishwa na kauli na maneno ya mitaani badala yake atakuwa na msimamo imara wa kusimamia maslahi ya chama kupitia vikao halali.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai wakati akizungumza na viongozi mbali mbali wa Chama kuanzia ngazi za matawi hadi wilaya huko katika Wilaya ya Amani Kichama, Unguja.

Aliwasihi viongozi hao kutumia vikao halali vinavyokubalika kikanuni kujadili changamoto na kasoro zinazojitokeza ndani ya chama kwa lengo la kuepuka maneno ya mitaani yanayoweza kusababisha migogoro isiyokuwa ya lazima ndani ya CCM.

Alisema baada ya chama hicho kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa Marudio uliofanyika Machi 20 mwaka huu kwa asilimia 91, kilichobaki kwa sasa ni viongozi na wanachama kushirikiana vizuri na Rais, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani kusimamia vizuri Ilani ya Uchaguzi ya Chama hicho yam waka 2015/2020.

 “ Sisi viongozi tukiendelea kuwa wamoja na wenye kushirikiana kwa lengo la kusimamia maslahi ya CCM kwa vitendo basi, naamini kwamba chama chetu nacho kitaendelea kuwa imara na kushinda kwa kila uchaguzi.

"Pia tujue kwamba ushindi wa uchaguzi mkuu wa marudio ndio mwanzo wa kujipanga kimikakati kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020, kwani hakuna muda tena wa kusubiri ni lazima tuwe karibu zaidi na wanachama wetu ambao ndiyo wapiga kura wetu.”, alisisitiza Vuai huku akiwasihi vuiongozi hao kusoma alama za nyakati kwa kutathimini changamoto na kasoro zilizotokea katika uchaguzi mkuu uliopita ili zisizokee tena katika uchaguzi ujao.

Naibu Katibu Mkuu huyo, aliendelea kufafanua kwamba CCM ni chama chenye asili ya amani na utulivu na kinachoamini kwamba umoja na msikamano ndiyo fursa ya kuifikisha katika kilele cha Zanzibar na maendeleo endelevu ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Akizungumzia suala la ajira, Vuai aliwashauri vijana kutokata tamaa kwani CCM inaendelea kuikumbusha serikali kutafuta njia mbadala za kuhakikisha vijana wenye sifa, vipaji,uwezo na maarifa ya ujuzi mbali mbali wa chama hicho wananufaika na matunda ya ajira kutoka serikalini ama sekta binafsi.

Aidha Naibu Katibu Mkuu huyo, alilaani vikali kitendo cha Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad katika ziara yake ya Pemba cha kuwakataza wananchi hasa wafuasi wake wasilipe kodi na kuwapandikiza mbegu za chuki zinazolenga kuingiza nchi katika migogoro inayoweza kuathiri uchumi wa nchi.

Alisema kitendo hicho hakikubaliki kwani kinavunja sheria za nchi na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kwa makusudi jambo linalotakiwa kuchukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya dola kabla nchi haijangia katika machafuko.

“Sio kwamba serikali inamuogopa Maalim Seif bali inafanya kila jambo kwa kufuata sheria na Katiba ya nchi, lakini pia ni lazima tukumbuke kwamba hakuna mtu aliyekuwa juu ya sheria.”, alisema Vuai na kuwasihi wananchi hasa wafuasi wa CCM wasiwe na jazba na watulie huku wakisubiri mamlaka husika zichukue hatua kwa watu wanaovunja sheria za nchi.

Naye Katibu wa CCM Wilaya ya Amani Kichama, Abdallah Mwinyi alimuahidi Naibu Katibu Mkuu huyo kuyafanyia kazi mambo yote yaliyotolewa kama nasaha na ushauri kwa lengo la kuongeza ufanisi wa kiutendaji ndani ya chama hicho.

Nao baadhi ya viongozi wa ngazi mbali mbali  waliohudhuria kikao hicho, wameelezea kuridhishwa kwao na mikakati mizuri iliyopo ndani ya chama itakayosaidia kufanikisha ushindi wa dola katika uchaguzi mkuu 2020.

Pamoja na hayo wameahidi kuendelea kuwa wamoja katika kulinda maslahi ya CCM kwani ndiyo chama pekee kinachojali na kuthamini utu wa wananchi kupitia kauli njema za kuhimiza amani na utulivu wa nchi.

Wimbo wa 'Panya' Wakiponza Kitua cha EATV, Chapigwa Faini ya Milioni 3 na TCRA

$
0
0

Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), imevitoza faini vituo vya East Africa Television na Entertaiment FM (E- FM) baada ya kukiuka kanuni za utangazaji.

Akisoma nakala ya hukumu hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA, Joseph Mapunda alisema baada ya kupitia maelezo ya utetezi kutoka kwa viongozi wa vituo hivyo, kamati hiyo imeamua kuitoza EATV faini ya Sh3 milioni na Sh4 milioni kwa E-Fm.

“Pamoja na adhabu hiyo tumetoa onyo kali kwa kukiuka kanuni ya maudhui, lakini pia endapo kosa hili litajirudia tunaahidi kutoa adhabu kali zaidi,” alisema.

Katika maelezo ya awali ya hukumu hiyo, Mapunda alisema adhabu ya EATV imetolewa baada ya kituo hicho kupitia kipindi chake cha muziki mnene kurusha video ya wimbo wa Panya wa kundi la muziki la Bracket kutoka nchini Nigeria uliomshirikisha msanii Techno.

“Baadhi ya mavazi yaliyotumika katika wimbo huo hayaendani na maadili ya Kitanzania. Na kwa upande wa E-FM wameadhibiwa baada ya kurusha kipindi cha Ubaoni kilichotoa simulizi ya msichana mchawi aliyekiri kuua,”alisema Mapunda.

Baada ya kupokea nakala ya hukumu hiyo, Mkurugenzi wa EATV, Regina Mengi alisema hawana tatizo na adhabu hiyo na kwamba, atalifikisha suala hilo kwa uongozi wa kampuni yao.

“Bado siwezi kujibu lolote, uamuzi wa kuikubali au kukata rufaa itategemea na uamuzi wa bodi,” alisema.

Mkurugenzi wa E-FM, Scolastica Mazula alisema ameridhishwa na hukumu iliyotolewa, hivyo haoni kama kuna sababu ya kukata rufaa.

Mamlaka hiyo imevitaka vyombo vyote vya utangazaji nchini kuzingatia maadili na taratibu za sheria zinapofanya kazi ili kuepuka kuleta athari katika jamii.

Wabunge Waibana serikali Matukio ya Mauaji Mwanza

$
0
0

WAKATI matukio ya mauaji ya kikatili yakiendelea kuripotiwa kwenye maeneo mbalimbali nchini, Bunge limeitaka serikali kukomesha kadhia hiyo mara moja ili kuepusha maafa zaidi kwa watu wasio na hatia.

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, alitoa tamko hilo bungeni mjini Dodoma juzi wakati akitoa mwongozo kwa Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Amina Mollel.
 
Mbunge huyo alisimama na kuomba Mwongozo wa Spika akiitaka serikali itoe kauli kuhusu kuwapo kwa matukio ya mauaji hayo.
 
"Mheshimiwa Naibu Spika, nasimama kwa Kanuni ya 68(7), lakini vilevile nakuu kupitia Ibara ya 14 ya Katiba ya Tanzania ambayo inasema kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria," Amina alisema.
 
"Kumekuwapo na matukio yanayotokea katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, hasa mikoa ya Manyara na Mara. Na hata jana (Jumatano) kulifanyika mauaji ya familia moja, baba na mama wamekatwakatwa mapanga na cha kusikitisha zaidi, huyo mama alikuwa ni mjamzito.
 
"Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kauli ya serikali kwa mwongozo wako wewe ili basi tupate kauli ya serikali kwa sababu mauaji haya yamekuwa yakitokea kwa watu wasiokuwa na hatia.
 
"Ni lini na nini wajibu wa serikali katika kuhakikisha kwamba raia wote wa Tanzania wanaishi kwa amani na utulivu?" Alihoji.
 
Akitoa mwongozo wake kuhusu suala hilo, Dk. Ackson alisema: "Kwanza nianze kwa kusikitika sana kwa niaba yenu waheshimiwa wabunge, haya mauaji yamekuwa yakiendelea kila wakati, lakini tutakumbuka waheshimiwa wiki hii, nadhani Jumatatu au Jumanne tulisikia kauli ya serikali kwamba wanafanya nini lakini sasa mauaji haya yametokea tena jana kwa mujibu wa ripoti ya Mheshimiwa Amina Mollel."
 
"Lakini nikumbushe tu masikitiko yetu makubwa kwamba mauaji haya yanaendelea. Tunaiomba serikali, tafadhali ifuatilie kwa karibu ili mauaji yakomeshwe, lakini cha kukumbushana waheshimiwa wabunge, jambo kama hili haliombewi mwongozo,” alisema na kuongeza: “ Jambo kama hili linaletwa kwa kutumia kanuni nyingine ambayo siyo kanuni ya kuomba Mwongozo wa Spika kwa sababu Mwongozo wa Spika unaombwa kwa jambo lililotokea bungeni mapema," alisema
 
Mei 19, ikiwa ni siku moja baada ya kutokea kwa mauaji msikitini jijini Mwanza, Waziri wa Nchi, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama, alisema vyombo vya ulinzi na usalama vitafuatilia kwa kina chanzo cha matukio hayo nchini.

Watumishi Wavaa Vimini, vipedo, t-shirt, Jeans Kufyekwa Mshahara

$
0
0
HALMASHAURI ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga, imepiga marufuku watumishi wote wa halmashauri hiyo kuvaa mavazi ambayo hayana maadili katika sehemu za kazi na kwamba atakayebainika atarudishwa nyumbani na kukatwa mshahara wa siku husika.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga, Adriano Jungu wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Bomani wilayani Muheza juzi.
 
Alisema lazima mtumishi ahakikishe staha ya mavazi aliyovaa kabla hajaingia kazini katika ofisi yake na kwamba mtumishi atakayekiuka kuvaa mavazi ambayo hayaendani na maadili sehemu ya kazi atachukuliwa hatua za kinidhamu.
 
Akieleza zaidi, Jungu alisema kuwa mavazi ambayo hayaruhusiwi kwa watumishi ndani ya halmashauri yake ni pamoja na fulana, suruali za jeans, vimini, vitop, Pedo, yeboyebo, kaptula (pensi) na kandambili kwa sababu kuvaa vyote hivyo ni kinyume cha maadili ya utumishi.
 
Alisema kuwa mtumishi yeyote katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza kabla ya kuingia kazini lazima aangalie mavazi aliyovaa na kwamba sheria iko katika waraka wa utumishi wa umma namba 3 wa mwaka 2007 na lazima watumishi waheshimu waraka huo.
 
Jungu alisema mtumishi yeyote katika halmashauri ya Wilaya ya Muheza ambaye atakiuka sheria hiyo kwa kuvaa nguo za kihuni wakati wa kuingia kazini basi atarudishwa nyumbani na atakatwa mshahara wake wa siku hiyo.
 
Alisema kuwa lazima watumishi waheshimu sehemu ya kazi kwa kuvaa nguo za heshima ikiwamo wanawake na wanaume kwa kuwa ofisi hizo wanaingia watu wenye heshima ikiwamo wazee sasa haiwezekani mtumishi mwanamke anaingia ofisini na kimini kinachofika katika magoti na hivyo mapaja yake yanaonekana sasa anamtamanisha nani.
 
Jungu alisema kuwa kwa wanaume nao lazima wawe na nidhamu ya kuvaa mavazi ya heshima na siyo kuvaa mavazi ya jeanz mlegezo na flana zinazowabana ni marufuku kabisa katika halmashauri ya Muheza.
 
Alisema ataanza kupita kila ofisi Jumatatu Mei 30 asubuhi kwa ajili ya kuwakagua mavazi yao watumishi hao wakiwamo wanawake na wanaume ili kukomesha tabia kama hiyo ambayo ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma hapa Tanzania.
 
Jungu alitoa onyo kwa kupiga marufuku watumishi kufika kazini wakiwa wamelewa na mtumishi akibanika amefanya hivyo na ushaidi upo atampeleka hospitali kupimwa na akibainika atamtumbua jipu hadharani kwani serikali ya awamu ya tano ni ya  hapa kazi tu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 29


Makamu Mkuu wa Shule Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kumlawiti Mwanafunzi Wake

$
0
0

MAKAMU Mkuu wa Shule ya Sekondari Usevya katika Halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele , Makonda Ng’oka “Membele” (34) amefikishwa katika Mahakama ya mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake.

Mshtakiwa huyo alifikishwa juzi mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Chiganga Tengwa ambapo alikana shitaka lake na yupo nje baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyomtaka kulipa kiasi cha Sh 3,000,000 mahakamani.

Mwendesha Mashtaka, Wakili wa Serikali, Gregory Mhangwa alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo katika shule ya sekondari Usevya kati ya Novemba 2015 na Aprili 2016.

Alieleza mahakamani hapo kwamba katika kipindi hicho mshtakiwa alimuingilia mwanafunzi wake huyo kinyume cha maumbile. Hakimu Tengwa aliahirisha shauri hilo hadi Juni 26 , mwaka huu litakapotajwa tena.

Inadaiwa kuwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Makamu Mkuu huyo wa shule hiyo kunafuatia wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano katika shule hiyo kumkataa na kutishia kuandamana kupinga vitendo vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.

Kufuatia msimamo wa wanafunzi hao iliwalazimu Ofisa Elimu mkoa wa Katavi, Everest Hunji na Mkurugenzi Mtendaji Halmashari ya Mpimbwe wilayani Mlele, Evaristo Kiwale kufika shuleni hapo Jumatatu jioni na kuzungumza na wanafunzi hao.

Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo amekuwa akiwalawiti baadhi yao ikiwa ni adhabu mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni hapo. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mpimbwe, Kiwale alisema vitendo vya ushoga havikubaliki na kwamba tayari hatua stahiki zimeshachukuliwa za kumpeleka katika vyombo vya kisheria. 

“Msitaharuki mnapomuona mwalimu huyo mitaani msidhani hajachukuliwa hatua yoyote ile,” alisisitiza.

Mahakama Yataifisha Ng’ombe 1,312 Kwa Kosa la kuchunga ndani ya Hifadhi ya Wanyamapori

$
0
0
MAHAKAMA ya mkoa wa Katavi imetaifisha ng’ombe 1,312 walioingizwa na kuchunga ndani ya hifadhi ya wanyamapori ya Rukwa huku washtakiwa watatu wakinusurika kutumikia vifungo vya miaka miwili jela baada ya kulipa faini kati ya Sh 500,000 na 700,000.

Katika shauri la kwanza mfugaji, Shigera Mayunga (22) amenusurika kifungo cha miaka miwili jela baada ya kulipa faini ya Sh 700,000 katika Mahakama ya mkoa wa Katavi huku ikimwachia kwa masharti mdogo wake, mwenye umri wa miaka 12 .

Washtakiwa hao wawili walitiwa hatiani na mahakama hiyo kwa makosa ya kuingiza ng’ombe 532 na kuchungia ndani ya hifadhi ya wanyamapori ya Rukwa. 

Hakimu Odira Amworo akitoa hukumu hiyo pia aliamuru kutaifishwa kwa ngo’mbe wote 532 na kusema kuwa amelazimika kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wafugaji wengine wenye tabia kama hiyo.

Awali Mwendesha Mashtaka, wakili wa serikali Achiles Mulisa alisema washtakiwa hao wawili walitenda makosa hayo Machi , 2016 ambapo kwa pamoja waliingiza mifugo yao na kuchunga ndani ya hifadhi ya wanyamapori ya Rukwa kinyume cha sheria .

Katika shauri la pili wafugaji wawili, Ngusa Keleja “Mtungi” na Charles Mtokambali (40) wamenusurika kutumikia kifungo cha miaka miwili jela baada ya kila mmoja wao kulipa faini ya Sh 500,000 kwa kuingiza ng’ombe 780 na kuchunga ndani ya hifadhi ya wanyamapori ya Rukwa .

Akitoa hukumu hiyo , Hakimu Amworo pia aliamuru kutaifishwa kwa ng’ombe wote 780 na kuwa amelazimika kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wafugaji wengine wenye tabia kama hiyo.

Awali Mwendesha Mashtaka, Wakili wa Serikali , Mulisa alisema washtakiwa hao wawili walitenda makosa hayo Machi 25, 2016 ambapo kwa pamoja waliingiza mifugo yao na kuchunga ndani ya hifadhi ya wanyamapori ya Rukwa kinyume cha Sheria.

Maalim Seif Atikisa Zanzibar..... Mabomu Yarindima Kuwatawanya Wafuasi Wake

$
0
0
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad jana aliitikisa Zanzibar pale alipoanza ziara yake ya siku sita katika Wilaya ya Kaskazini A na kusababisha polisi kuwatawanya wafuasi wake kwa mabomu na risasi huku baadhi wakijeruhiwa.

Wakati wa ziara hiyo, shughuli za biashara zilisimama kwa muda ili kupisha ziara ya Maalim Seif na mamia ya wananchi wake kwa waume walimpokea na kumfuata kila alipoelekea.

Ulinzi uliimarishwa katika maeneo yote ya Mkoa wa Kaskazini Unguja, wakati wote wa ziara hiyo na vikosi vya ulinzi na usalama vilionekana vikipiga doria kila mahali.

Akiwa Kinyasini, Jimbo la Chaani ambako alifanya kikao cha ndani, wakazi wa eneo la Kivunge kwa mamia walianza kujikusanya katika maeneo ambako Maalim Seif alitarajiwa kutembelea huku wakijipanga barabarani kumsubiri kiongozi huyo. Hata hivyo, askari wenye silaha waliwatawanya.

Katika kuwatawanya, polisi walitumia mabomu ya machozi na risasi hali iliyosababisha kizaazaa kwa takriban dakika 30 katika eneo la Kivunge kabla ya kurudi hali ya kawaida.

Baada ya hapo baadhi ya askari waliokuwa na silaha waliwazuia waandishi kusogelea eneo hilo wala kuwapiga picha majeruhi.

Mkazi wa Kivunge ambaye alidai ni miongoni mwa watu waliopatwa na mkasa huo, Omari Makame (32) alisema, “Sisi tumejipanga kwa heshima zote kumsubiri kiongozi wetu kipenzi cha Wazanzibari, tukiimba kwa furaha lakini ghafla tumepata kipigo na mabomu ya machozi, nini hiki kama siyo chuki na choyo kibaya.”

Mkazi mwingine, Haji Omar (27) alisema hata baada ya kuwajeruhi wenzao, polisi wali wakatalia kuwapa fomu za kwenda kupata matibabu na hata walipopelekwa hospitali ya Kivunge, polisi walifika na kuwachukua kwa nguvu.

“Wamekataa ushauri wa madaktari wa hapa kwamba wawapeleke Hospitali ya Rufaa ya Mnazi mmoja, lakini wamewachukua kwa nguvu wamekwenda nao Kituo cha Polisi Mkokotoni,” alisema Omar.

Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, Salum Msangi alikiri kuwapo kwa tukio hilo akibainisha kuwa yote hayo yanatokea kwa sababu kuna watu hawataki kufuata sheria, lakini akasema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Hassina Tawfik ndiye mwenye nafasi ya kufafanua zaidi.

Juhudi za kumpata Tawfik hazikufanikiwa ikielezwa na baadhi ya watendaji wa ofisi yake kuwa bosi wao hapatikani na hawakuwa na mawasiliano na yeye.

Mkurugenzi wa Haki za Binaadamu wa CUF, Pavu Juma Abdalla alifika katika Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja na kushuhudia majeruhi hao wakiwa mikononi mwa polisi.

Waliojeruhiwa ni Makame Abdalla Makame (28), mkazi wa Kivunge Bondeni na Shaame Juma Haji (45) mkazi wa Tumbatu Chwaka.

“Tunapigwa kwa sababu ya umma kuonyesha mapenzi kwa Maalim Seif, wangelikuja watu wa vyama vingine wasingelipigwa lakini ipo siku hawa jamaa wataheshimu haki zetu,” alisema mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Haji akisema baadhi ya majeruhi ni ndugu zake.

Mkurugenzi wa Habari wa CUF, Salim Bimani ambaye alifika hospitali kuwaona majeruhi alisema:“Wenye mabomu na risasi wamewahujumu watu bure kwa sababu za chuki lakini yote hayo yana mwisho.”. 

Bimani alisema Chama chake kinalaani kwa nguvu zote uonevu na hujuma hizo walizo tendewa wananchi wasiokuwa na hatia.

“Tunatumia pia kumbukumbu za hujuma hizi za leo kuongeza ushahidi wa kesi yetu tutakaouwasilisha ICC,” alisema Bimani.

Ziara yenyewe 
Maalim Seif alianza ziara hiyo ya kwanza Unguja tangu kumalizika kwa uchaguzi wa marudio aliosusa kushiriki katika eneo la Kinyasini, Chaani na kupokewa na mamia ya wafuasi wake ambao walikuwa wakiimba “rais! rais! rais!

Aliambatana na viongozi na watendaji wa CUF, akiwamo Naibu Katibu Mkuu, Nassor Ahmed Mazrui; Bimani; Pavu Abdalla na Mkurugenzi wa Mipango na Chaguzi, Omar Ali Shehe.

Aliondoka Kinyansini kuelekea Gamba, Mkwajuni ambako mamia ya wananchi waliokuwa wakimshangilia walijipanga barabarani na walionekana kuongezeka kadri alivyoelekea Kaskazini na kukaribia Jimbo la Mkwajuni.

Baadaye Maalim Seif aliwahutubia wajumbe wa kamati mbalimbali za wilaya na majimbo akieleza kile alichosema ni mwelekeo wa kisiasa wa chama chake, Zanzibar na Tanzania kwa jumla.

Alisema dunia ilishuhudia ukiukwaji mkubwa wa haki na demokrasia visiwani humo, akidai kwamba pamoja na maonyo ya jamii mbalimbali za kitaifa na kimataifa, watawala waliamua kupora uamuzi wa mamlaka halali ya wananchi kupitia masanduku ya kura ya Oktoba 25, 2015.

“Angalieni watu hawa walivyokosa aibu, umma uliwakataa, mataifa yaliwakataa hata kuwanyima misaada lakini bado hawakuonyesha dalili za kujali kutokana na dhulma waliyotenda.

“Nasema hali hii haitupeleki pema sisi na Taifa kwa ujumla maana iliyoporwa ni haki ya umma na haiwezekani kuisamehe dhambi hii, hivyo mwishowe si mwema na dhuluma haiwezi kudumu kwa muda mrefu asilani, sasa kusema hivyo kuna ubaya gani?”

Hata hivyo, Mwangalizi Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU – EOM) kwa Tanzania, Judith Sargentini amesema atawasilisha ripoti kamili na mapendekezo ya umoja huo, kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana Alhamisi ijayo.

Maalim Seif aliwataka wananchi wote, kama walivyoikataa CCM kabla ya uchaguzi, wakati na baada ya kupiga kura Oktoba mwaka jana, kuunga mkono juhudi na mikakati ya CUF, ili kuhakikisha haki inapatikana, uamuzi wao unaheshimiwa, kwa masilahi ya nchi na Taifa kwa jumla.

Viongozi wa chama hicho Wilaya ya Kaskazini A, walimhakikishia Maalim Seif; “sisi tuko tayari kwa lolote, na naona siyo sisi pekee, kwa sasa kila mtu anaisoma namba, tutakuwa bega kwa bega mpaka haki yetu ipatikane,” alisema Makame Bakari, mmoja wa makatibu wa CUF.

Polisi Dar wahaha Kuwasaka Wauaji wa Dada wa Bilionea Msuya

$
0
0
Ikiwa bado kuna sintofahamu ya chanzo cha mauaji ya dada yake bilionea Erasto Msuya, Anneth, Polisi wamesema hawajabaini sababu za awali za kifo hicho na wanaendelea na msako wa waliohusika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto alisema hadi jana wauaji walikuwa hawajakamatwa, licha ya juhudi za upelelezi zinazoendelea.

Tukio la Anneth Msuya aliyeuawa Alhamisi usiku kwa kuchinjwa nyumbani kwake Kibada, Kigamboni jijini Dar es Salaam, limekuwa ni mwendelezo wa matukio mengine ya uhalifu kwa familia yao yaliyowahi kutokea baada ya kifo cha kaka yake, Msuya.

Miongoni mwa wanaotafutwa na Polisi ni mfanyakazi wa ndani aliyeondoka nyumbani kwa Anneth mchana kabla ya kutokea mauaji hayo, kwa madai kuwa hawezi kuendelea na kazi na kuacha ufunguo kwa jirani.

Bilionea Msuya aliuawa Agosti 2012 kwa kupigwa risasi, tukio lililofanyika mkoani Kilimanjaro.

Ikiwa ni miaka minne tangu kifo hicho, kingine kinatokea kwenye familia hiyo.

Dada wa Anneth, Ester, anayeishi Mbezi Makonde jijini Dar es Salaam, alisema juzi kuwa mazishi ya mdogo wake yatafanyika mkoani Kilimanjaro Mei 30.

Bado watu wengi wanajiuliza kuhusu mfululizo wa matukio katika familia ya Msuya, huku wakishangaa sababu za binti huyo kuuawa kama kaka yake.

“Ni kweli kifo hupangwa na Mungu, lakini siyo kwa kifo hiki. Kwa nini wanauawa?” alihoji Juma Majuto, mmoja wa waombolezaji wa msiba huo uliopo Mbezi Makonde.

Mtoto Wa Miaka 4 Afariki Dunia Baada Ya Kuungua Kwa Moto Ndani Ya Nyumba Yao Jijini Mwanza

$
0
0
MTOTO Vestina Masolwa (4) wa kitongoji cha Nyamungu– Mwabagole katika kata ya Mwangalangha tarafa ya Ndugu wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, amefariki dunia baada ya kuteketea kwa moto jikoni wakati nyumba yao ikiteketea kwa moto.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 9 alasiri katika kitongoji hicho, baada ya mama wa marehemu, Grace Wilson (30), kupika chakula na kisha kwenda shambani nje kidogo na nyumba hiyo akiwa amemuacha mtoto huyo jikoni.
 
Kwa mujibu ya taarifa ya Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema baada ya mama huyo kwenda shambani na kumuacha mtoto wake (marehemu), alianza kuchezea moto uliosababisha nyumba yao kuungua.
 
“Wakati mama wa marehemu akiwa anaendelea na shughuli zake shambani, aliona nyumba yake ikiungua moto na kuamua kukimbia kurudi nyumbani na kukuta nyumba ikiteketea na kusababisha mtoto Masolwa kufariki dunia papo hapo."
 
Kamanda Msangi alisema mwili wa marehemu tayari ulifanyiwa uchunguzi na daktari kisha kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi, lakini chanzo cha tukio hilo likidaiwa ni uzembe wa wazazi kushindwa kuwa waangalifu kwa mtoto huyo na kusababisha kifo na nyumba kuungua.
 
Hata hivyo, alitoa wito kwa wazazi wawe makini na waangalifu wakati wote na watoto ili kuwaepusha na ajali zinazoweza kuepukika, huku pia akiwataka kuhakikisha kabla hawajaondoka kwenda kwenye shughuli zao za kila siku, wanawaacha watoto wao kwenye mazingira salama.

JWTZ Washusha Abiria Kwenye Magari yao na Bodaboda ili Washiriki Zoezi la Usafi

$
0
0

KATIKA hali isiyo ya kawaida, askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) Mkoani Mtwara jana walisimamisha vyombo vya usafiri barabarani asubuhi na kushusha abiria waliokuwemo, ili washiriki kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kufanya usafi.

Mwandishi alishuhudia abiria wakishushwa katika magari, pikipiki katika maeneo mbalimbali ya mji wa Mtwara na kutakiwa kushiriki zoezi la usafi.
 
Ufanyaji usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi umekosa mwamko mjini Mtwara tangu kuzinduliwa na Rais Desemba 9, mwaka jana.
 
Bila kujali itikadi za vyama wala cheo cha mtu, JWTZ waliwataka wananchi kupaki vyombo vya usafiri na kufanya usafi ili kukabiliana na milipuko ya magonjwa.
 
Baadhi ya wananchi walioshiriki usafi huo, walipongeza jitihada za JWTZ katika kutilia mkazo zoezi la usafi mkoani humo.
 
Zoezi hilo la usafi liliongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Halima Dendego ambaye alisema litakuwa endelevu mkoni hapo.

Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye Akerwa na Ving'ang'anizi wa Madaraka

$
0
0
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye amezitaka nchi za Afrika kuhakikisha zinakubali kubadilishana madaraka pale chama kimoja kinaposhindwa kuongoza ili kuepusha nchi kuingia kwenye machafuko.

Aidha, Sumaye alisema ni vyema wataalam wakaongoza nchi kwa kubuni mbinu mbalimbali za kujikwamua kiuchumi.
 
Sumaye aliyasema hayo jana Jijini hapa wakati akizungumza kwenye kongamano la Nafasi ya Wasomi na Wafanyabiashara Katika Kujenga na Kukuza Uchumi wa Nchi, lililoshorikisha viongozi wa vyama, wafanyabiashara na wasomi wa kada mbalimbali wa Arusha.
 
Sumaye alisema uongozi ni kubadilishana nafasi na katika nchi za Ulaya kwa mfano, chama kikishindwa kutawala kinakubali lakini kwa nchi za Afrika kuna uroho wa madaraka au ubinafsi.
 
"Tunataka kuwajengea uwezo wasomi wetu kwa kujiamini na kujipatia fursa za kujikwamua kiuchumi," alisema Sumaye ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 mfululizo kati ya 1995-2005, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi.

"Ubinafsi tuache, tukishindwa uchaguzi achia ngazi.Mimi niliyasema haya nikiwa CCM na leo hii nipo Chadema nasema unapoang'angania madaraka, aidha unaogopa ukiachia utasababisha machafuko au ubinafsi."
 
Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Dk. Vincent Mashinji akifungua kongamano hilo, alisema chama chake kinataka kutengeneza mabepari wa kitanzania ambao watajiongeza wenyewe katika kujiinua kiuchumi.
 
Alisema Arusha ni mji wa kitalii hivyo ni vyema wafanyabiashara wakatumia fursa zilizopo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi, na inawezekana Jiji hilo kuwa na fursa nyingine za kibiashara badala ya kutegemea madini ya Tanzanite pekee.

Wanafunzi 7,000 Watimuliwa UDOM

$
0
0
Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kimewasimamisha masomo zaidi ya wanafunzi 7,000 wa kozi maalumu ya ualimu wa sayansi kwa ngazi ya stashahada na kuwataka waondoke chuoni hapo mara moja.

Jana, lilitolewa tangazo chuoni hapo likiwataka wanafunzi hao kuondoka kati ya jana hadi leo saa 12 jioni. Tangazo hilo lilieleza kuwa kutokana na matatizo yaliyopo katika ufundishaji wa stashahada hiyo, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imeamua wanafunzi hao kurejea majumbani na wataelezwa mustakabali wao “mapema iwezekanavyo”.

Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Idrisa Kikula alipotakiwa kufafanua suala hilo, alisema kwa ufupi kuwa suala hilo lipo lakini akaelekeza apigiwe simu Ofisa Uhusiano wa chuo hicho, Beatrice Baltazal kwa maelezo zaidi.

Baltazal alipotafutwa alisema kusimamishwa kwa wanafunzi hao kulitokana na agizo la Serikali na wametakiwa kulitekeleza.

Kuhusu lini na nini hatima ya wanafunzi hao, alisema bado hawajui hadi hapo watakapoelekezwa vinginevyo.

Hata hivyo, kulikuwa na malalamiko kwa wanafunzi hao juu ya namna walivyopewa taarifa za kusimamishwa masomo yao kwa ghafla na kutakiwa kuondoka.

Kozi ya stashahada ya ualimu wa sayansi, ilianzishwa maalumu kwa agizo la Rais Jakaya Kikwete kwa lengo la kuziba pengo la walimu wa sayansi na ilikuwa inatolewa UDOM pekee.

Waliokuwa na sifa za kujiunga na kupewa mikopo ni wanafunzi waliomaliza kidato cha nne na kufaulu vizuri masomo ya sayansi. 

Wanafunzi hao waliokuwa wamekopeshwa na Serikali wamesimamishwa siku mbili baada ya wenzao zaidi ya 480 wa Chuo Kikuu cha St. Joseph kusimamishwa baada ya kubainika hawakuwa na sifa za kudahiliwa. 

Serikali yatangaza kuisafisha Sekta ya Elimu na Watumishi wa umma wenye vyeti bandia.

$
0
0
Serikali imetangaza rasmi kuanza kwa kampeni ya kuwashughulikia na kuwaondoa katika utumishi wa umma watumishi wote walioajiriwa katika  sekta hiyo  wakitumia vyeti bandia .

Aidha, imewataka watumishi hao waanze kujitathmini na kuanza kujiondoa wenyewe kabla ya kufikiwa na mabadiliko makubwa ya kusafisha sekta ya elimu na utumishi wa umma yanayokuja nchini.

Kauli hiyo imetolewa Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi Prof.Joyce Ndalichako wakati wa majumuisho ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imejipanga kufanya mabadiliko makubwa katika Sekta ya Elimu nchini ili kuhakikisha kuwa Elimu inayotolewa katika shule, vyuo na taasisi mbalimbali inazalisha wahitimu wenye sifa na ubora kwa maslahi ya Taifa .

Amesema katika kulitimiza hilo Serikali itawachukulia hatua kali za kinidhamu na kisheria watendaji wote walioshiriki na wale wanaoendelea kushiriki kwa namna moja au nyingine kukwamisha maendeleo ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na wale waliohusika katika udahili wa wanafunzi wasio na sifa katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph Songea.

"Serikali ya awamu ya tano imedhamilia kwa dhati kabisa kuboresha kiwango cha elimu yetu kwa kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wa elimu, naomba niwahakikishie kwamba pale panapohitajika kufanyika mabadiliko tutayafanya bila woga" Amesisitiza.

Amesema katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali za elimu hapa nchini, serikali imejipanga kubadilisha mfumo wa elimu ambao umekuwa ukilalamikiwa kwa muda mrefu na kwamba mabadiliko hayo yatafanyika kwa kuwashirikisha wadau wote wa sekta hiyo.

" Tunapotaka kufanya mabadiliko kwenye mfumo wetu wa elimu tumekubali kwamba tuna changamoto,  katika changamoto hizi lazima tuwe na mahali pa kuanzia hivyo tunapochukua hatua tunaomba Watanzania mtuunge mkono" Amesisitiza Prof.Ndalichako.

Prof.Ndalichako Amesema lengo la Serikali kupitia Wizara yake ni kuhakikisha sekta ya elimu inaboreshwa hapa nchini kwa kuendelea kutoa wahitimu bora wanaokidhi vigezo na viwango katika soko la ajira.

Amesisitiza kuwa mkakati wa Serikali ni kuanza kuwafuatilia wahitimu wote wasio na viwango ambao wako katika maeneo mbalimbali ya ajira huku akisisitiza kwamba elimu ya Tanzania ni sawa na kiwanda kinahitaji malighafi nzuri ili kitoe bidhaa bora.

Ameeleza kuwa Serikali imejipanga kikamilifu kuvikagua vyuo vyote vinavyotoa elimu ya juu kuona kama vinakidhi sifa na vigezo vya kiutendaji ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wale wote wanaowadanganya wananchi  na kuwapotezea muda vijana wanaowadahili bila kuzingatia sifa.

"Wizara yangu tunaendelea kufanya mawasiliano na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili tuchukue hatua kwa wote walioichezea sekta hii muhimu, tulichofanya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph kinaendelea kwa vyuo vingine"

Kuhusu ujenzi wa maabara amesema kuwa Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 12 kwa ajili ya kununulia vifaa vya maabara kwa shule zote 1536 ambazo zimekamilisha ujenzi wa majengo ya maabara kote nchini.

Katika hatua nyingine amesema kuwa Serikali katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 itafanya ukaguzi wa vyuo vyote vya Maendeleo ya Jamii kote nchini ili majengo ya vyuo hivyo yaweze  kutumika kuanzishia vyuo vya Ufundi Stadi VETA katika wilaya na mikoa ili kuwapatia stadi za kazi vijana waweze kujitegemea kwa kujiajiri wenyewe.

Kwa upande wao baadhi ya Wabunge waliopata nafasi ya kuchangia wakati wa Kupitisha Bajeti ya wizara hiyo wameiomba Serikali kuweka mkazo katika usimamizi wa Sekta ya Elimu nchini ili shule, Taasisi na vyuo vya Tanzania vitoe wahitimu wenye ubora kwa maslahi ya Taifa.

Aidha, wameiomba Serikali kupitia Bajeti hiyo itenge fedha za kutosha kwa ajili ya kuimarisha shughuli za ukaguzi wa shule, kuboresha maslahi na kulipa madai ya walimu pamoja na kuziimarisha Mamlaka za Udhibiti wa Elimu ili ziweze kutimiza majukumu yao ipasavyo.

Muhongo Aitumbua Kampuni Iliyoingiza Mafuta FEKI Nchini

$
0
0
SERIKALI imemsimamisha msambazaji wa mafuta Kampuni ya Sahara Energy Resourses Limited ya Nigeria aliyeingiza mafuta ya ndege (JET A1) yaliyochafuka na kumtaka kusafisha matangi pamoja na mabomba ya mafuta ya kampuni zilizopokea mafuta hayo.

Aidha, imeelezwa pamoja na kutokea kwa tatizo hilo la kuchafuka kwa mafuta hayo nchi haitaingia katika ukosefu wa nishati hiyo muhimu kwa kuwa kuna akiba ya kutosha kwa siku 14 na tayari kampuni ya Puma imeagiza mafuta ambayo yataingia nchini Juni 7, mwaka huu. 

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alitoa kauli hiyo jana wakati alipotembea kampuni za mafuta zilizopokea mafuta yaliyochafuka kwa kuchanganyika na petroli jijini Dar es Salaam ili kubaini ukweli wa uhaba wa mafuta ya ndege.

Profesa Muhongo aliiagiza kampuni hiyo ya Sahara Energy Resources Limited ya Nigeria kuhakikisha inasafisha matangi pamoja na mabomba ya mafuta kuanzia leo na kama haitatekeleza hilo itakuwa ni mwisho kufanya kazi nchini. 

“Msafishe haya matenki pamoja na mabomba yote kwa gharama zenu. Haya ni maagizo sisi hatuwezi kuendelea kusubiri, hamuwezi mkasababisha nchi ikawa na uhaba wa mafuta kwa majadiliano yenu ambayo hayana mwisho.

“Usafishaji unatakiwa kuanza kesho, kama hautafanyika kuanzia hiyo kesho, basi Sahara isahau kufanya biashara katika nchi hii. Na sio hilo tu hata tenda (zabuni) alizokuwa amepata nazo tutazifuta,” alisema Profesa Muhongo. 

Alisema kuwa kampuni hiyo haitakiwi kupewa zabuni nyingine hadi hapo uchunguzi utakapokamilika wa kubaini ukweli wa mafuta hayo kuchafuka kwa kuchanganyika na petroli.

Profesa Muhongo alisema hatua walizochukua ya kwanza ni kumsimamisha kujihusisha na zabuni yoyote itakayotangazwa kuanzia sasa lakini pia kutakiwa kusafisha matangi na mabomba hayo. 

Aliongeza kuwa hii ni mara ya pili kwa kampuni hiyo mafuta yake kuwa na tatizo kwani mara ya kwanza mafuta yake yalibainika kuwa machafu akarudishwa nayo.

Awali mwakilishi wa kampuni hiyo ambaye yuko hapa nchini alisema, hawana sehemu ya kuhifadhi mafuta hayo ambayo yamechafuka hivyo wanasubiri meli yao irudi ili waweze kuyaondoa mafuta. 

Hata hivyo, kampuni ya kuhifadhi mafuta nchini ya Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER) ilimhakikishia Profesa Muhongo kuwa wana nafasi ya kuhifadhi mafuta yote yaliyochafuka, hatua ambayo waziri huyo aliiagiza kampuni hiyo kuhifadhi mafuta hayo katika matangi ya TIPER badala ya kusubiri meli.

“Hilo linatuchelewesha TIPER wameshakubali wana nafasi ya kuhifadhi hayo mafuta, kwa hiyo yahifadhi hapa ili msafishe hayo matenki, ili mafuta yatakayokuja yakute matenki ni masafi,” alisema. 

Aidha, alisisitiza kuwa taifa haliwezi kuingia kwenye uhaba wa mafuta ya ndege na yapo ya kutosha siku 14 kwani kampuni ya Puma tayari imeshaomba mafuta kutoka katika kampuni za Total na SP ya Rwanda.

Pia meli ya Puma itaingia nchini Juni 7 na meli nyingine itaingia Juni 13. 

Awali akizungumzia hali hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, Michael Mjinja alisema, meli hiyo iliingia nchini Mei 5, mwaka huu na mafuta hayo yalithibitishwa kuwa na ubora na Shirika la Viwango nchini (TBS). 

Alisema baada ya mafuta hayo kushushwa ilibainika kuwa yamechafuliwa hatua iliyowafanya kumuagiza aliyeleta mafuta hayo kuyaondoa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Felix Ngamlagosi alisema, kwa sasa kuna mafuta ya kutosha kwa siku 14 lakini kuna hatua nyingine zinazochukuliwa ili kuhakikisha hakuna uhaba wa mafuta utakaotokea.

 “Hayo yaliyochanganyika kuna hatua zinazochukuliwa ikiwa ni pamoja na kuchukua sampuli za pamoja na sisi ni wasimamizi ili kuhakikisha zinapelekwa maabara na kujua kitu gani kilitokea,” alisema.

Profesa Muhongo alizitembelea kampuni hizo ambazo ni Puma Energy, Gapco Tanzania Ltd, Oilcom, ORXY Energies na TIPER. Meneja wa Huduma za Usafiri wa Anga wa Oilcom, Haruna Magota alimwambia Waziri Muhongo kuwa, mafuta waliyopokea yalikuwa ni lita milioni 8.8 na wao walikuwa na lita milioni 2.6, ambapo mafuta hayo yote yameharibika.

Alisema ukosefu wa mafuta hayo umekuwa ni tatizo kwa wateja wao ambao ni mashirika ya ndege kwani jumla ya lita milioni 10.8 yote yamechafuka. 

Aidha aliongeza kuwa wakaguzi wa meli walishawahi kutoa onyo kwa kampuni hiyo kuwa meli zake hazina viwango vinavyotakiwa vya kubeba nishati hiyo. 

Aidha kampuni za kuagiza mafuta nchini zilitaka kampuni ya Sahara Energy Resources Ltd ya nchini Nigeria kuweka hadharani uthibitisho wa kuhujumiwa kuhusiana na kashfa ya uingizaji mafuta ya ndege machafu hapa nchini inayolikabili shirika hilo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta ya Petroli nchini (TAOMAC) iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari jijini Dar es Salaam juzi, waagizaji hao waliitaka kampuni hiyo kutaja jina la kampuni au mhusika yeyote anayeaminika kuihujumu kampuni hiyo kama ambavyo imenukuliwa na vyombo vya habari nchini ikijitetea kupinga kashfa hiyo.

“Tunawaomba wenzetu hawa wahakikishe wanakabidhi jina la kampuni au mtu yeyote wanayemshuku kuwa anahusika na kashfa inayowakabili kwa Jeshi la Polisi au chombo chochote cha usalama nchini vinginevyo sisi tutaamini kuwa utetezi wao ni uwongo na unalenga kutafuta njia ya kutokea,’’ alisema Mkurugenzi Mtendaji wa TAOMAC, Salum Bisarara kupitia taarifa hiyo.

Sakata la kuingizwa kwa mafuta machafu ya ndege aina ya Jet A1 na hofu ya kukosekana kwa mafuta hayo nchini liliibuliwa na Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017, alisema mafuta hayo yatakosekana kutokana na kampuni moja ya kigeni iliyopewa zabuni kuagiza mafuta hayo, kuingiza mafuta ambayo hayawezi kutumiwa na ndege.

Katibu Mkuu Mambo Ya Ndani Ya Nchi Afanya Ziara NIDA........, Atoa Habari Njema Kwa Watumishi 597 Walioachishwa Kazi

$
0
0
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira amesema fedha za kuwalipa watumishi 597 waliositishiwa mikataba yao katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) zipo na watalipwa hivi karibuni.

Rwegasira alisema kiasi cha shilingi bilioni 2.3 zimetengwa kwa ajili ya malipo ya Watumishi hao waliaochishwa kazi Machi 7, 2016 ambapo wanaidai Mamlaka mishahara ya miezi mitatu nyuma, malimbikizo ya fedha katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na makato ya fedha za Bima ya Afya.

Akuzungumza na watumishi wa Makao Makuu ya NIDA pamoja na Maafisa Wasajili wa Vitambulisho vya Taifa, jijini Dar es Salaam jana, Rwegasira aliwataka watumishi hao waliositishiwa mikataba yao, wasipotoshwe na mtu yeyote kuhusu kutokulipwa haki zao kwani wapo katika hatua ya mwisho ya kukamilisha taratibu ndogo ndogo kabla ya kuanza kuwalipa.

“Naomba muwaambie waondoe wasiwasi wowote, waache maneno, watulie kwani Serikali ipo makini na fedha tunazo na tutaanza kuwalipa mara tumalizapo taratibu ndogo ndogo zilizobaki.” Alisema Rwegasira.

Aidha, Rwegasira aliwataka watumishi wa Mamlaka hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha ifikapo Desemba 31 mwaka huu Watanzania Milioni 23 wanatakiwa watambuliwe na kupata namba kabla ya kuanza kupewa Vitambulisho vya Taifa.

Hata hivyo, watumishi hao walimuakikishia Katibu Mkuu huyo, kuwa kazi hiyo ya utambuzi itakamilika kama ilivyopangwa na itafanyika kwa umakini mkubwa kama inavyotarajiwa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa NIDA, Dk. Modestus Kipilimba alimshukuru Katibu Mkuu huyo kwa kuwatembelea na kuwatia hamasa katika kukamilisha kazi pamoja na kufikisha lengo lao la kukamilisha utambuzi ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

“Tunakuahidi Katibu Mkuu kuwa tutatimiza lengo letu na tunakuakikishia tutafanya kazi kadiri ya uwezo wetu tukiongozwa na kauli mbiu ya ‘hapa kazi tu’", alisema Dk. Kipilimba.

Katibu Mkuu Rwegasira alifanya ziara hiyo kwa lengo la kujifunza zaidi shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka, hata hivyo alipata muda wa kuzungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo kuhusu masuala mbalimbali ya kiutendaji. 
Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Ansigar Chilemba akitoa maelezo jinsi taarifa za muombaji wa Kitambulisho cha Taifa zinavyohakikiwa, kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia). Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dk. Modestus Kipilimba. Rwegasira alifanya ziara ya kikazi katika ofisi za Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam jana.
Afisa Usajili Kitengo cha Ubora wa Kadi, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Jemima Mulokozi (kushoto) akimuonyesha vitambulisho vilivyokamilika vikiwa na ubora unaohitajika, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati). Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dk. Modestus Kipilimba. Rwegasira alifanya ziara ya kikazi katika ofisi za Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam jana.

Basi Jingine la Mwendo kasi Lapata ajali Eneo la Magomeni Usalama

$
0
0
Basi jingine la mwendo kasi limepata ajali mabaya eneo la Magomeni Usalama. Ni baada ya gari dogo kukatisha kwenye barabara ya magari ya mwendo kasi.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images