Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wadakwa Wakisafirisha kilo 500 za Mirungi kwa Kutumia Gari Dogo

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Mara linawashikilia wakazi wawili wa Mtaa wa Nyegezi, Wilaya ya Nyamagana, Mkoa wa Mwanza kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ramadhani Ng’anzi alisema jana kuwa watuhumiwa hao walikamatwa Mei 17, saa nane mchana katika Kijiji cha Mulyaza wilayani Butiama wakiwa na kilo 500 za dawa hizo zimehifadhiwa kwenye vifurushi 15 yenye uzito wa zaidi ya nusu tani.

Alisema watuhumiwa hao walikuwa wakisafirisha dawa hizo kwa kutumia gari aina ya Toyota Carina lililokuwa likiendeshwa na mmoja wao wakitokea Sirari, Wilaya ya Tarime wakielekea Mwanza.

Hata hivyo, aliwaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kusaidia kuwakamata watu wanaokiuka sheria na taratibu za nchi.

Baadhi ya wakazi wa mjini hapa walisema udhibiti wa dawa za kulevya ni jukumu la kila Mtanzania kwa sababu madhara yake husababisha athari katika jamii inayozunguka eneo husika.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aapa Kukomesha Lumbesa

$
0
0

WAZIRI Mkuu, Kasim Majaliwa, ametoa onyo kwa wafanyabiashara wanaodhulumu wakulima kwa kununua mazao kwa kuyafunga kwenye magunia bila kuzingatia vipimo sahihi maarufu kama lumbesa, na kutaka viongozi kuanzia ngazi ya vijiji mpaka mikoa kusimamia.

Alisema serikali itapambana na wafanyabiashara wanaoendelea kulazimisha kufungasha mazao katika magunia bila kuzingatia vipimo sahihi hivyo kuwapunja na kuikosesha serikali mapato.

Akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Saumu Sakala (CUF) katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Majaliwa alikiri kuwa serikali ilishazuia matumizi ya kipimo cha lumbesa na kuahidi kwamba awamu hii, itakomesha dhuluma hiyo.

Awali mbunge huyo alitaka kauli ya serikali dhidi ya vitendo hivyo kuendelea ingawa kupitia viongozi mbalimbali wa serikali, vilishapigwa marufuku.

Waziri Mkuu alitoa mwito tena kwa wakuu wa wilaya, halmashauri zao, maofisa biashara katika halmashauri hizo kuhakikisha unyonyaji huo unakomeshwa.

“Jambo hili wala siwaachii wakuu wa wilaya peke yao bali nawaagiza hata wakuu wa mikoa kupitia kamati zao za ulinzi na usalama kuhakikisha agizo hili linatekelezwa, swali hili la mbunge linaashiria mambo haya bado yanafanyika,” alisema.

Pia aliwaagiza watendaji wa vijiji na kata, kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanaouza mazao kwenye maeneo yao, hawauzi mazao kwa kipimo cha lumbesa.

Katika hatua nyingine, Majaliwa alisema tayari maelekezo yametolewa kwa Wakala wa Vipimo, kuhakikisha biashara yote ya mazao ya kilimo nchini yanauzwa kwa vipimo vya kilogramu na siyo kwa kufungashwa lumbesa.

Alisema ingawa kuna vijiji visivyokuwa na mizani, hali hiyo siyo kigezo cha kuhalalisha lumbesa, badala yake alisema magunia yote nchini yametengenezwa kwa vipimo hivyo mazao yanapojazwa gunia lazima lifungashwe kwa kushonwa kwa uzi au kamba.

TGNP Yalia na Udhalilishaji Wanawake

$
0
0

KUTOKANA na matukio ya udhalilishaji dhidi ya wanawake kuongezeka kwa kasi nchini, taasisi zinazotetea haki za wanawake na watoto, zimevitaka vyombo vya dola kuamka na kuchukua hatua za haraka zitakazosaidia kukomesha matukio hayo

Akizungumza jana na waandishi wa habari Dar es Salaam Lilian Liundi, Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia (TGNP), akiwa na wanaharakati wengine alisema kuwa, tangu Januari hadi kufikia Aprili mwaka huu matukio ya udhalilishaji na unyanyasaji dhidi ya wanawake yamekuwa yakizidi kushika kasi.

“Tuko hapa kwa pamoja tukilaani vikali ukatili dhidi ya wanawake unaoendelea kukithiri nchini, mfano kuna tukio lilitokea hivi karibuni katika mji mdogo wa Dakawa wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro ambapo binti wa miaka 21 alikuwa akibakwa na picha za video dhidi ya tukio hilo kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii,

“Si hilo tu bali taarifa tulizozikusanya juu ya matukio ya ukatili wa kijinsia tangu mwaka huu uanze ni mengi katika kila kona ya Tanzania, tunaona Aprili mwaka huu Yunis Peter mkazi wa Dar, alichomwa na kitu chenye ncha kali katika nyumba ya kulala wageni, Rehema Lubinza mkazi wa Mlele, aliuwawa kikatili kwa kukatwa na mapanga na mumewe kisha mwili wake kufungiwa ndani, si hivyo bali tukio la muuguzi wa Zahanati ya Kagu Geita, bi Elizabeth Msango, ambaye aliuwawa na watu wasiojulikanayapo matukio mengi ambayo ni unyanyasaji unaonekana kabisa”alisema.

Akizungumzia kuhusu udhalilishaji uliofanywa Mvomero, Gladness Munuo, Mratibu wa dawati la usuluhishi kutoka chama cha Wahariri Wanawake Tanzania, (TAMWA), alisema tukio hilo ni kinyume na sheria ya kanuni ya adhabu sura 16(Kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 ambayo imeainisha makosa ya kujamiana).

Alisema pamoja na sheria za ndani, serikali ya Tanzania imeridhia mikataba na matamko mengi kuhusu haki za wanawake na usawa wa kijinsia ikiwamo mkataba wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake(CEDAW), pamoja na mkataba wa haki za watoto (CRC), sambamba na tamko la kimataifa la haki za binadamu (UDHR,19),ambalo linatambua haki za wanawake na watoto.

Theodosia Nshala, Mkurugenzi wa kituo cha msaada wa sheria kwa wanawake (WLAC), alisema kama kituo tayari wameshapokea kesi kumi na mbili lakini licha ya kufanya jitihada za kuzishughulikia bado wahusika ama waathirika wamekuwa wakikata tamaa kutokana na kesi hizo kuchukua muda mrefu ambapo kesi moja ambayo ina ushahidi uliojitosheleza inaweza kuchukua hata miaka mitatu mpaka mitano .

Grace Mwangamila, Mwanasheria kutoka Kituo cha Sheria na haki za binadamu(LHRC), alisema kupitia tafiti zao matukio ya udhalilishaji dhidi ya wanawake yameoneka kuwa mengi huku kwa upande wa watoto udhalilishaji na unyanyasaji umebainika ukifanyika ndani ya familia.

Tume ya Maendeleo ya Ushirika yakusudia Kuvifuta Vyama 1,862 Vilivyokiuka Matakwa ya Sheria

$
0
0
TUME ya Maendeleo ya Ushirika inakusudia kuvifuta vyama 1,862 vya ushirika nchini, kutokana na kukiuka matakwa ya sheria ya vyama hivyo na kushindwa kutimiza masharti ya usajili wake.

Miongoni mwa vinavyofutwa ni Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo (Saccos) cha Madiwani wa Manispaa ya Kinondoni, Saccos ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Madiwani Saccos ya Kagera na cha Madiwani wa Mpwapwa na vingine vya ushirika.

Akizungumza na wanahabari juu ya kusudio hilo, Kaimu Mrajisi wa vyama hivyo na Mtendaji Mkuu wa Tume hiyo, Dk Audax Rutabanzibwa alisema hatua watakazochukua baada ya kufuta vyama hivyo ni kuendelea kuwafuatilia waliosajili vyama hivyo na warajisi wasaidizi ili kubaini ukweli wa uanzishwaji wake.

Alisema kuna uwezekano waliosajili walishirikiana na warajisi wasaidizi ili kuanzisha vyama hewa kwa lengo la kujipatia fedha.

Alitaja vyama vitakavyofutwa kulingana na maeneo, kwa upande wa Arusha kuwa ni 83, Dar es Salaam 91, Dodoma 50, Geita 16, Iringa 74, Kagera 240, Katavi 19, Kigoma 38, Manyara 73, Mara 203, Morogoro 278, Mtwara 52, Njombe 18, Pwani 324, Rukwa 14, Ruvuma 14, Shinyanga 89, Simiyu 93, Singida 15, Tanga 77 na Lindi kimoja.

Aliongeza kuwa kutokana na sababu hizo, vyama vinavyokusudiwa kufutwa ni 1,862 na vitafutwa baada ya siku 90 kuanzia Mei 13, mwaka huu.
Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Audax Peter Rutabanzibwa akiwaeleza waandishi wa habari (Hawapo pichani) Kuhusu makusudio ya Tume hiyo kuvifuta vyama 1862 katika daftari la vyama vya Ushirika vyama ambavyo vimekiuka matakwa ya sheria ya vyama vya ushirika No.6 ya mwaka 2013. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa.

Mkuu wa Mkoa na Waziri Kitwanga Watofautiana Kuhusu Kuwepo Kwa Tawi la Magaidi wa Al Shabaab na Islamic State (IS) jijini Tanga

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Charles Kitwanga na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela wametofautiana juu ya taarifa za kuwapo kwa tawi la kundi la kigaidi la Islamic State (IS) jijini Tanga

Juzi, Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC Swahili) lilitangaza uwepo wa watu waliojitambulisha kuwa wawakilishi wa kundi hilo wanaoendesha operesheni kwa nchi za Afrika Mashariki.

Shirika hilo lilieleza kuwa kundi hilo limetuma ujumbe na kujitambulisha kwa kutumia video ya dakika moja waliyoituma kwenye mtandao wa Twitter na kuzungumza na Waziri Kitwanga ambaye alithibitisha kuwa na taarifa hizo.

“Tumezisikia na tumechukua hatua. Askari wetu wanafanya operesheni,” alikaririwa Waziri Kitwanga.

Hata hivyo, jana Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela aliwaambia waandishi wa habari, kuwa mauaji na matukio ya ujambazi wa kutumia silaha yaliyotokea mfululizo katika maeneo mbalimbali jijini hapa siku za karibuni hayahusiani na ugaidi.

Alifafanua kuwa wahalifu waliopo huko wamegundulika kuwa wahamiaji haramu kutoka Ethiopia, ambao wanaingia nchini kwa kutumia vichochoro vilivyoko kwenye mapori ya mpaka wa Kenya na Tanzania, wakielekea nchi jirani. Wamekuwa wakiingia nchini kupitia baadhi ya maeneo ya wilaya ya Mkinga.
 
Wahalifu hao hutumia mapango hayo, kujificha kwa muda wakati wakisubiri kuendelea na safari yao kuelekea nchi za Kusini mwa Afrika. 

“Napenda kuwajulisha wakazi wa Tanga na taifa kwa ujumla kwamba hapa mkoani hatuna vita dhidi ya kundi lolote la ugaidi wala kikosi cha Al-Shabaab, isipokuwa kuna operesheni maalumu ya kikosi kazi chetu cha ulinzi na usalama, kinachopambana na mambo makuu matatu; kubwa ni matukio ya uhalifu unaofanywa na wahamiaji haramu,” alisema Mkuu wa Mkoa.
 
Alisema kamati ya ulinzi na usalama mkoa, baada ya kutafakari mwenendo wa kiusalama kutokana na matukio ya uhalifu wa hapa na pale, imeunda kikosi kazi kukomesha vitendo hivyo, vinavyofanya mkoa kutumiwa kama uchochoro.
 
Shigela ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, aliyataja mambo yanayoshughulikiwa na kikosi kazi hicho ni kudhibiti uingizaji wa dawa za kulevya, magendo ya bidhaa zisizoruhusiwa au kuingizwa bila kufuata utaratibu pamoja na wahamiaji haramu.
 
“Wahamiaji haramu ndilo jambo hatarishi sana hapa kwa sasa, kwa sababu hao watu wakishaingia nchini kwa njia za panya na kufanikiwa kujificha, basi wanaposikia njaa hulazimika kujitokeza mitaani kutafuta chakula kwa kuvamia maduka, kama walivyofanya katika duka kuu la Central Bakery mwishoni mwa mwezi uliopita”, alisema.
 
Akizungumzia wakazi wa Kata ya Amboni yaliko mapango na mapori husika, aliwataka kuchukua tahadhari, hasa wale wanaofanya shughuli za kilimo jirani, kwa kuacha kuwenda kwa muda maeneo hayo, hasa kipindi hiki ambacho kikosi kazi kinaendeleza operesheni.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya May 20

Rais Magufuli Atoa Salamu za Pole kwa Wakazi wa Jiji la Mwanza Kufuatia Mauaji ya Watu Watatu Msikitini

$
0
0

Rais John Magufuli ametoa salamu za pole kwa wakazi wa mkoa wa Mwanza, kutokana na mauaji ya watu watatu, waliouawa kwa kukatwa mapanga wakiwa msikitini.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam jana, ilisema Rais Magufuli amesema yupo pamoja na wakazi wa mkoa huo wa Mwanza katika kipindi hiki cha majonzi, kuomboleza watu hao na pia alisema anawaombea wale waliojeruhiwa wapone.

Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Ndani imesema imesikitishwa na mauaji ya watu hao watatu, waliouawa msikitini katika wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

Kauli hiyo ya Serikali, ilitolewa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Masauni Yussuf Masauni.

Masauni alisema kuwa Serikali inawapa pole wakazi wa Mwanza, viongozi wa mkoa na wilaya ya Nyamagana na mbunge wa jimbo hilo, Stanslaus Mabula.

Wizara ya Nishati Yatengewa Tril.1.22/- Katika Bajeti ya Mwaka wa fedha 2016/17

$
0
0
WIZARA ya Nishati na Madini imetengewa Sh trilioni 1.22 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/17 huku fedha za miradi ya maendeleo zikiwa ni asilimia 94 ya fedha hizo.

Pia katika kuongeza kiwango kikubwa cha uzalishaji wa nishati, kuongeza mchango wake katika Pato la Taifa, asilimia 98 ya Bajeti ya Maendeleo imetengwa kwa ajili ya sekta ya nishati.

Aidha, serikali imeongeza bajeti ya maendeleo ya fedha za ndani kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kufikia Sh bilioni 534.4, huku wateja wa umeme wa REA na Tanesco wakifikia 220,128. Mbali na hayo, kiwango cha upatikanaji wa huduma ya umeme kimeongezeka kufikia asilimia 40.

Hayo yalisemwa bungeni jana mjini Dodoma na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2016/17.

Profesa Muhongo alisema bajeti ya wizara kwa mwaka 2016/17 ni Sh trilioni 1,22,583,517,000, na kati ya fedha hizo, Sh 1,056,354,669,000 ni fedha za miradi ya maendeleo sawa na asilimia 94.

“Kwa kuzingatia Ibara ya 43(a) ya Ilani ya CCM ya mwaka 2015-2020 inayoelekeza serikali kuongeza kiwango kikubwa cha uzalishaji wa nishati ili kuongeza mchango wake kwenye Pato la Taifa, asilimia 98 ya Bajeti ya Maendeleo imetengwa kwa ajili ya sekta ya nishati,” alisema Profesa Muhongo.

Alisema katika mwaka wa fedha 2015/16, waliidhinishiwa na Bunge Sh bilioni 642.12, na kati ya fedha hizo, Sh bilioni 502.30 sawa na asilimia 78 ya bajeti yote zilikuwa ni bajeti ya maendeleo.

“Hata hivyo, Bajeti hiyo iliongezeka kutoka shilingi bilioni 642.12 hadi shilingi bilioni 762.12. lengo la ongezeko ni kutekeleza miradi mikubwa ya kufua umeme ukiwemo Mradi wa Kinyerezi II – MW 240 ili kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini,” alisema Profesa Muhongo.

Megawati zaongezeka
Akizungumzia sekta ndogo ya umeme, alisema uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme nchini umeongezeka kutoka megawati 1,226.24 Aprili, 2015 hadi kufikia megawati 1,461.69 Aprili, 2016 sawa na ongezeko la asilimia 19.

“Ongezeko hilo limechangiwa na mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia baada ya kukamilika kwa bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka Mtwara na Lindi hadi Dar es Salaam,”alisema.

Aidha, alisema mahitaji ya juu ya umeme yameongezeka kutoka megawati 988.27 Desemba, 2015 hadi kufikia megawati 1,026.02 Machi, 2016 sawa na ongezeko la asilimia nne. 

Kuhusu upatikanaji wa umeme nchini, alisema kiwango cha huduma ya upatikanaji wa umeme kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka.

“Watanzania waliofikiwa na huduma hiyo wameongezeka kutoka asilimia 36 mwezi Machi, 2015 hadi kufikia takribani asilimia 40 mwezi Aprili, 2016. 

“Ongezeko hilo limetokana na juhudi za serikali za kusambaza umeme nchini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),” alisema Profesa Muhongo.

Alisema kuanzia Julai, 2015 hadi Aprili, 2016 idadi ya wateja waliounganishwa na umeme wa REA pamoja na Tanesco ni 220,128 sawa na asilimia 88 ya lengo la kuunganisha wateja 250,000 ifikapo Juni mwaka huu. 

Umeme bila MCC 
“Katika kuongeza wigo wa upatikanaji wa umeme vijijini, serikali imeongeza Bajeti ya Maendeleo ya fedha za ndani kwa REA kutoka shilingi bilioni 357.12 kwa mwaka 2015/16 hadi shilingi bilioni 534.4 kwa mwaka 2016/17. Tumeongeza asilimia 50 na hakuna fedha za MCC (Shirika la Changamoto za Milenia) hapa,” alisema Muhongo.

"Ongezeko hilo ni kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya Mwaka 2015 – 2020. Aidha, fedha za nje zilizotengwa kwa ajili ya mradi huo ni shilingi bilioni 53.21 sawa na asilimia tisa na hivyo kufanya jumla ya bajeti yote ya REA kwa mwaka 2016/17 kuwa shilingi bilioni 537.61.”

Mitambo kuongezwa 
Akizungumzia miradi ya kuzalisha na kusafirisha umeme, alisema serikali itatekeleza miradi mingi ambayo baadhi itakamilika katika mwaka wa fedha 2019/2020.

Alisema katika juhudi za kuongeza uzalishaji umeme, serikali imepanga kuongeza mitambo mingine ya kuzalisha umeme ya Kinyerezi – I Extension wa megawati 185.

Alitaja mingine ni Kinyerezi II megawati 240, huku akitaja miradi iliyo katika hatua za mwisho za maandalizi ya miradi ambayo ni Kinyerezi III (megawati –MW 300), Rusumo Falls MW 80), Malagarasi MW 45 na Kanoko MW 87.

Kuhusu miradi ya usafirishaji umeme, alisema ujenzi wa mradi wa Iringa hadi Shinyanga wa kilovolti 400 umefikia wastani wa asilimia 89, ambao gharama zake ni Sh bilioni 387.5 na utakamilika Septemba mwaka huu.

Alisema serikali inaendelea kutekeleza miradi ya ujenzi wa njia za kusafirisha umeme zenye uwezo mkubwa hususan kilovolti 400. 

Miradi ambayo utekelezaji wake unatarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2019/20 aliitaja kuwa ni Singida – Arusha – Namanga kv 400, Bulyahulu – Geita kv 220, Geita – Nyakanazi kv 220, North East Grid kv 400 na Somanga – Kinyerezi kv 400.

Aidha, alisema mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 kutoka Somanga Fungu hadi Kinyerezi, Tanesco imeshakamilisha ulipaji wa fidia kwa wananchi wanaopisha mradi huu. 

“Hadi kufikia mwezi Aprili, 2016 shilingi bilioni 26.06 tayari zimelipwa na Tanesco kwa watu 947 katika wilaya za Ilala na Temeke,” alieleza.

Katika kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini, mwaka 2014 Tanesco ilianzisha Kampuni Tanzu ya Tanzania Concrete Poles Manufacturing Company Limited (TCPCO), kwa ajili ya kujenga viwanda vya kutengeneza nguzo za zege nchini.

“Baada ya kukamilisha maandalizi ya ujenzi wa viwanda hivyo, TCPCO inatarajia kuanza uzalishaji wa nguzo za zege mwaka 2016/17,” alisema.

Kuhusu punguzo la viwango vya bei za umeme, Profesa Muhongo aliliarifu Bunge kuhusu punguzo hilo lililoanza Aprili mosi, mwaka huu.

Alisema serikali imepunguza bei ya umeme kwa kati ya asilimia 1.5 na 2.4, na pia imeondoa tozo ya kuwasilisha maombi ya kuunganishiwa umeme ya Sh 5,000 na tozo ya huduma ya mwezi ya Sh 5,520 kwa wateja wa umeme wa Daraja la TI na DI, ambao wengi wao ni wa majumbani.

“Hatua hii itawasaidia watumiaji wadogo wa umeme mijini na vijijini kumudu gharama hizo, hivyo kuboresha shughuli za kijamii na kiuchumi,” alisema Profesa Muhongo aliyerejea katika wizara hiyo baada ya kuwahi kuiongoza katika Serikali ya Awamu ya Nne.

Kuhusu gesi asilia, alisema kukamilika kwa ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Mtwara kupitia Lindi hadi Dar es Salaam kumeongeza mchango wa uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia kufikia asilimia 49.

Aidha, alisema uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia umewezesha gharama za uzalishaji umeme nchini kupungua kutoka wastani wa Sh 262 hadi 229 kwa uniti moja ya umeme.

Profesa Muhongo alisema bomba hilo lenye urefu wa kilometa 542 ni pamoja na mitambo ya kusafisha gesi asilia katika maeneo ya Madimba (Mtwara) na Songo Songo (Lindi). Mradi huo ulizinduliwa rasmi Oktoba, 2015 na Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete.

Akizungumzia shughuli za utafutaji gesi asilia, alisema Kampuni ya Dodsal imekamilisha tathmini ya kiasi cha gesi asilia kilichogunduliwa katika kisima cha Mambakofi – I kwenye Kitalu cha Ruvu Mkoa wa Pwani. Alisema tathmini hiyo inaonesha uwepo wa gesi asilia kiasi cha futi za ujazo trilioni (TFC) 2.17.

“Hivyo kufanya gesi asilia iliyogunduliwa nchini hadi Mei, 2016 kufikia TCF 57.25 ikilinganishwa na TCF 55.08 zilizokuwepo mwezi Aprili, 2015. Kati ya kiasi hicho, TCF 47.13 zipo kwenye kina kirefu baharini na TCF 10.12 zipo nchi kavu,” alisema.

Akizungumzia usambazaji wa gesi asilia jijini Dar es Salaam, alisema lengo la mradi huo ni kujenga mtandao wa kusambaza gesi asilia kwa njia ya mabomba na iliyoshindiliwa (CNG).

Sakata la Escrow na IPTL Laibuka Upya Bungeni

$
0
0
Kambi ya upinzani imeliibua upya  bungeni sakata la Escrow, Richmond na umiliki wa kampuni ya IPTL, huku ikihoji sababu za Rais John Magufuli kutoheshimu maazimio ya Bunge ya kumwajibisha Sospeter Muhongo, badala yake kumteua tena kuwa Waziri wa Nishati na Madini.

Hoja hizo ziliibuliwa na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika wakati akiwasilisha maoni ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2015/16 na makadirio ya matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka 2016/17.

Muhongo alikuwa akiiongoza wizara hiyo wakati kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh300 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kuhifadhi fedha za malipo umeme kusubiri kumalizika kwa mzozo wa kimkataba baina ya kampuni ya IPTL, inayozalisha umeme  na Shirika la Umeme (Tanesco).

Bunge lilimuona Profesa Muhongo kuwa alishindwa kuwajibika na kusababisha Serikali kupoteza mapato.

Profesa Muhongo alilazimika kujiuzulu wadhifa huo saa chache kabla ya Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kutangaza baraza jipya.

Hata hivyo, Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma lilimsafisha na kashfa hiyo iliyohusisha malipo yaliyofanywa kwa mawaziri, majaji, wabunge na watumishi waandamizi wa umma.

Jana, Mnyika, ambaye ni mbunge wa Kibamba (Chadema), alirejea maazimio ya Bunge la Kumi akisema lilishafanya maamuzi kuhusiana na mikataba ambayo Serikali inaingia na kampuni mbalimbali, hasa kwenye sekta ya nishati na madini.

“Katika maazimio ya Bunge kuhusiana na fedha, ufisadi uliofanyika katika akaunti ya Tegeta Escrow na umiliki wa IPTL yanayohusu sekta ya nishati na madini, bado hayajatekelezwa kwa ukamilifu wake,” alisema Mnyika.

 Akinukuu Azimio Namba 2, Mnyika alisema liliagiza kwamba Serikali iangalie uwezekano wa kununua mitambo ya kufua umeme ya IPTL na kuimilikisha kwa Tanesco kwa lengo la kuokoa fedha inazolipa kwa kampuni hiyo binafsi.

Alisema kambi hiyo inasikitika kuona kwamba mbali ya Serikali kushindwa kununua, bado inaendelea kulipia gharama za uwekezaji na hivyo kuendelea kukiukwa kwa azimio hilo.

Akizungumzia azimio la saba linalohusu kuwajibishwa kwa mawaziri na watendaji wakuu wa wizara na bodi ya Tanesco, Mnyika alisema Profesa Muhongo naye aliwajibishwa kwa uteuzi wake kutenguliwa, lakini Rais Magufuli amemteua tena kuongoza wizara hiyo.

“Rais bila ya kujali nini Bunge lilishaazimia katika kikao ambacho na yeye alikuwa sehemu ya azimio hilo, akamteua Muhongo kuendelea kuiongoza wizara hii. Kambi ya upinzani inaliona jambo hili kama ni dharau sana kwa Bunge na ni fedheha binafsi kwake,” alisema.

Alisema kambi ya upinzani imelazimika kunukuu maazimio hayo kutokana na ukweli kwamba Serikali imeshindwa kabisa kutekeleza maazimio ya Bunge na badala yake mikataba hiyo inaendelea kutekelezwa kama ilivyoingiwa.

“Mfano mzuri ni Tanesco kuendelea kuilipa IPTL fedha za capacity charge mpaka sasa. Jambo hili linazidi kuliondolea shirika hilo la umeme uwezo wa kuwahudumia wateja wake kwa kuwa haliwezi kuwekeza zaidi katika miundombinu ya kusambaza umeme kutokana na kutokuwa na fedha za kutosha,” alisema.

Jinsi Kitambi Kinavyopatikana na Jinsi Kinavyoondolewa na Dawa ya Mkataa Kitambi

$
0
0

Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na  wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.
JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili wa binadamu.

 Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.

Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:

i.Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi

ii.Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k

SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili  wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

VYAKULA  VINAVYO  CHANGIA KULETA  KITAMBI

Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :
i.Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya  kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa  mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.

ii.Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.

iii. Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa( added  sugar ), kama  vile  soda  na  keki.

iv. Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nakadhalika

v. Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama  vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  kadhalika.

Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo  kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.

vi. Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo(  physical  exercises  )  kwa  muda  mrefu.

JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).

Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.

BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.

Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.

Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.

MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA  KUPATWA  NA  KITAMBI
Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula  pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa  tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na  kitambi.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka  watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :

1. Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio  zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha  aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu  anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :

Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda  moja.  Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.

Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.

Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.

Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima  atapatwa  na  kitambi.

2. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi

3. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  

4.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa ( added  sugar  ).

5.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.

6.Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.

7.Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo  ( physical  exercises  ).

Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa  mbaya  zaidi. 

NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe  kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena “

Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili  wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.

Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya  mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta( fats  )  yasihotika  yaliyomo ndani  ya  mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.

Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa  hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.

NJIA  ZA  KUONDOA  KITAMBI.
Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya  mwili  na  viungo.

Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

DAWA   ASILIA  YA  KUONDOA  KIAMBI  NA  MAFUTA  MWILINI.
Hii  ni  njia  ya  uhakika  kabisa  ya  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

 Unaweza  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  DAWA  ASILIA   IITWAYO YA  MKATAA  KITAMBI.

 Dawa   hii  ni  ya asili  kabisa
“  Pure  Herbal “, ambayo  haijachanganywa  na  kemikali  yoyote, haina  side  effect kwa  mtumiaji  na  inaondoa  kabisa  tatizo  la  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

JINSI  DAWA  YA  MKATAA  KITAMBI  INAVYO  FANYA  KAZI.
1.Huyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

2.Husaidia  kupunguza  hamu  ya  chakula.

3.Inazuia  kutengenezwa  kwa  seli  za  mafuta  ( fat cells  ) katika  mwili  wa  mwanadamu. Unapokula  chakula  chenye  mafuta  mengi, dawa  hii asilia  hupambana  kuyafanya  mafuta  hayo  yasitengeneze  seli  za  mafuta  mwilini  mwako. Hali  hii  huuepusha  mwili  wako  kuhifadhi  mafuta   yasiyo  hitajika  mwilini.

4. Husaidia  kupunguza  uzito wa mwili  kwa  haraka  sana  endapo  itatumika  pamoja  na  diet  ya  kabechi.

UFANISI  WA  DAWA.
Ufanisi  wa  dawa  hii  ni  wa  asilimia  mia  moja. Dozi  ya  dawa  hii  hutumika  kwa  muda  wa  siki  ishirini  na  moja.

MATOKEO  YA  DAWA:
Dawa  hii  huondoa  kabisa  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

BEI  YA  DAWA :
Dawa  hii  inaoatikana  kwa  kiasi  cha  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU  (Tshs. 50,000/=)

MAHALI  TUNAPO  PATIKANA.
Tunapatikana  jijini  DAR  ES  SALAAM, katika  eneo  la  UBUNGO  karibu  na  SHULE  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

KWA  WATEJA  WASIO  WEZA  KUFIKA  OFISINI  KWETU.
Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu  Tabata, tunao  utaratibu  wa  kuwafikishia  dawa  mahali  popote  walipo  ndani  ya  jiji  la  Dar  Es  salaam.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  DAR  ES  SALAAM.
Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  Dar  Es  salaam, tunawatumia  dawa  kwa  njia  ya  MABASI.

Kwa  wateja  wa  ZANZIBAR  tunawatumia  dawa  kwa njia  ya  boti.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  NCHI:
Kwa  wateja  wa  nje  ya  nchi, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA : 0766  53 83 84

TUTEMBELEE:

Kessy Amvaa John Mnyika......Asema Hapaswi Kumfananisha Profesa Muhongo na Edward Lowassa

$
0
0
Jina la aliyekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya Chadema akiungwa mkono na vyama vya upinzani vilivyounda Ukawa, jana liliingia tena katika Bunge la Kumi na Moja na kuzua mvutano.

Lowassa alitajwa na Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy (CCM), wakati akijibu hoja za Mbunge wa Kibamba, John Mnyika aliyekuwa akihoji na kuonesha kushangazwa na uteuzi wa Profesa Sospeter Muhongo kuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati alijiuzulu bungeni hapo baada ya kuelemewa na kashfa ya akaunti ya ‘Tegeta Escrow’.

Akijibu hoja hizo, Keissy ambaye siku zote ni mbunge mwenye hoja machachari alimvaa Mnyika  na kuhoji mbona wao ( UKAWA) walimchukua  Lowassa na kumfanya  kuwa mgombea wao wa Urais  wakati alijiuzulu uwaziri Mkuu kwa kashfa ya Richmond.

“Mnabeza  uteuzi wa Muhongo wakati Lowassa alivyojiuzulu hapa hapa bungeni mlimchukua mkamtembeza nchi nzima. Leo angekua Rais mgesema nini?" Alihoji Keissy .

Mnyika alikuwa alisoma hatuba ya kambi ya upinzani kwa Wizara ya Nishati na Madini ambayo ilikuwa ikiponda uteuzi wa Profesa Muhongo

Kigogo wa CCM Ataka Maalim Seif Sharif Hamad Akamatwe

$
0
0
Kigogo wa CCM aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Sukwa Said Sukwa amevishauri vyombo vya dola visiwani Zanzibar kumchukuliwa hatua haraka Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kwa kauli yake aliyoihusisha na kosa la uhaini.

Sukwa aliitaja kauli ya Maalim Seif aliyoitoa alipokuwa akihutubia katika mkutano wa hadhara kisiwani Pemba kuwa Dk. Ali Mohamed Shein hatamaliza kipindi chake cha urais mwaka 2020 na kwamba ni dikteta.

Sukwa amesema kuwa kauli hiyo ya Maalim Seif haipaswi kupuuzwa hata kidogo kwakuwa kauli kama hizo ni zaidi ya sumu.

“Sivilazimishi vyombo vya dola kufanya ninavyotaka, lakini tunashauri tu visipuuze ushauri wetu kwa sababu ulimi wa mtu unaweza kuwa sumu hatari kuliko matendo yake,” Sukwa aliliambia gazeti la Raia Tanzania.

Maalim Seif amekuwa akifanya mikutano kuwataka wananchi kumuunga mkono kuikataa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Shein, akieleza kuwa uchaguzi wa marudio haukuwa wa haki.

Serikali Yajibu Hoja za Kivuko cha MV Dar es Salaam na Uuzwaji wa Nyumba Zake

$
0
0
Serikali imejibu hoja za upinzani kuhusu uuzwaji wa nyumba za Serikali na kutetea ununuzi wa kivuko cha MV Dar es Salaam ambacho kilitakiwa kufanya safari zake kati ya Dar na Bagamoyo.

Hoja hizo ziliibuliwa katika hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, James Mbatia akitaka kutekelezwa kwa azimio la Bunge la urejeshwaji wa nyumba hizo serikalini lililotolewa Aprili 2008.

Pia, ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ilibainisha upungufu katika kivuko cha MV Dar es Salaam ambao ni kutolipiwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), kutokuwa na kasi kadri ya mkataba na kutokuwapo hati ya makabidhiano.

Hoja hizo za upinzani zilijibiwa juzi jioni na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ambaye alisema hakuna taratibu zozote zilizokiukwa wakati wa ununuzi wa kivuko hicho ambacho kwa zaidi ya mwaka hakijaanza kazi.

Alisema wizara ilipata taarifa ya CAG ambayo ilibainisha upungufu kadhaa ikiwa ni pamoja na kivuko hicho kununuliwa kwa Dola za Marekani 4.9 milioni (Sh7.9 bilioni) bila kulipiwa VAT, lakini akasisitiza kwamba hakukuwa na ukiukwaji wowote wa taratibu za ununuzi.

“Ni kweli kivuko kina mapungufu ikiwamo kasi ndogo, lakini hakuna ukiukwaji wowote wa taratibu wakati wa ununuzi. Temesa ilitangaza zabuni na baada ya maombi kupitiwa, kampuni ya MS Jones Gram Hansen ilishinda zabuni hiyo kwa kuwa na bei nafuu,” alisema Profesa Mbarawa.

Alisema baada ya kivuko kuletwa nchini Desemba 2014, kilifanyiwa majaribio na kubainika kwamba hakikuwa na kasi ya kuridhisha. Alisema makubaliano yalikuwa ni kujenga kivuko chenye kasi ya nots20, lakini hicho kilikuwa na kasi ya nots 15.7.

Kutokana na hali hiyo, alisema Serikali ilimtaka mkandarasi kurekebisha kasoro hiyo kwa gharama zake na kuwa ameshawasilisha andiko juu ya namna atakavyoifanya kazi hiyo.

“Mpaka sasa mzabuni huyo hajalipwa asilimia 10 ya malipo yaliyokubaliwa mpaka pale atakapokamilisha kazi hiyo. Kwa hiyo, taratibu zote zilifanyika kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Kuhusu nyumba, Profesa Mbarawa alisema Serikali iliidhinisha mpango huo Aprili 24, 2008 baada ya kupata ridhaa ya Bunge ilipopeleka suala hilo kujadiliwa.

“Suala la uuzwaji wa nyumba za Serikali, pia taratibu zilifuatwa. Serikali ilileta mpango huo bungeni na kupata ridhaa ya wabunge wote. Kwa hiyo, niwaambie tu wabunge kwamba suala hili lilipata baraka zao,” alisema waziri huyo.

Uuzwaji wa nyumba za Serikali na ununuzi wa kivuko cha Mv Dar es Salaam vilifanyika wakati Rais John Magufuli akiwa waziri wa ujenzi kwa nyakati tofauti.

Kambi ya upinzani imekuwa ikisisitiza kwamba kuna ukiukwaji wa sheria uliofanyika wakati wa uuzaji wa nyumba na ununuzi wa kivuko hicho. Hata hivyo, Serikali imeshikilia msimamo wake kwamba sheria zilifuatwa.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Gardner Amjibu Lady Jay Dee, Agoma kuomba Radhi

$
0
0
Hatimaye mtangazaji wa Clouds Fm, Gardner G. Habash amemjibu aliyekuwa mkewe, Lady Jay Dee, aliyemtaka aombe radhi ndani ya siku saba kwa kauli aliyoitoa iliyodaiwa kuwa imelenga kumdhalilisha. Katika majibu yake amekana madai hayo.

Siku chache zilizopita, Gardner alionekana katika kipande cha Video akisherehesha tukio la kumsaka mrimbwende wa chuo cha Tanzania Institute of Accountancy (TIA) jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa “yule binti sina tatizo naye, nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi…”, kisha wimbo wa ‘Ndindindi’ wa Jay Dee ukachezwa na DJ.

Kama ilivyokuwa kwa Lady Jay Dee aliyetoa siku saba za kuombwa radhi kupitia kwa mwanasheria wake Amani Tenga, Gardner amejibu kupitia mwanasheria wake Stephen Axwesso.

Katika barua yake kwa mwanasheria wa Lady Jay Dee, mwanasheria huyo wa Gardner amekiri kuwa ni kweli mteja wake alizungumza maneno hayo alipokuwa katika shughuli iliyotajwa, lakini alidai kuwa hakuna sehemu aliyomtaja mkewe huyo wa zamani.

Alisema kuwa madai ya upande wa Lady Jay Dee hayana mashiko na alimshauri mwanasheria huyo kupitia upya sheria inayozungumzia wanandoa waliotalakiana ili aweze kumshauri vizuri mteja wake kuhusu suala hilo.

Nakala ya barua hiyo pia imetumwa Clouds Media Group na kwa Rais wa Wanafunzi wa Chuo cha TIA.


Tanzia: Askari wa Usalama Barabarani, Ally Kinyogoli Auawa kwa Kupigwa Risasi

$
0
0
Watu wasiojulikana wakiwa na pikipiki aina ya Boxer,usiku wakuamkia leo wamemuuwa kwa kumpiga risasi kadhaa katika sehemu mbalimbali za mwili wake Askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani, Ally Kinyogoli nyumbani kwake Mwandege, Mkuranga mkoani Pwani.

Baada ya kumuua, watu hao walitokomea kusikojulikana bila kuchukua kitu chochote

Kinyogoli alijizolea umaarufu katika kipindi cha redio One kila siku asubuhi alipokua akitoa taarifa za hali za barabarani zikiwemo njia zenye foleni kwa wakazi wa jijini.
 

Diamond Atajwa Kuwania Tuzo za BET 2016

$
0
0
Diamond Platinumz anaendelea kupaa katika ulimwengu wa muziki kimataifa ambapo mwaka huu pia nyota yake imeng’aa kwenye tuzo kubwa za Black Entertainment Television (BET 2016).
 
Mwimbaji huyo ametajwa kuwania kipengele cha Best International Act: Africa akichuana na wasanii wengine nguli Afrika ambao ni pamoja na AKA kutoka Afrika Kusini, Cassper Nyovest wa Afrika Kusini Black Cofee wa Afrika Kusini, Yemi Alade wa Nigeria, Wizkid wa Nigeria, Mzvee wa Ghana na Serge Beynaud wa Ivory Coast.

Tuzo hizo zitafanyika Juni mwaka huu nchini Marekani ambapo Diamond pia ametajwa kati ya watakaotumbuiza.

Mwanafunzi Mbaroni Kwa Kumtukana Rais Wa Zanzibar Dkt.shein Pamoja Na Mkuu Wa Majeshi Mwamunyage.

$
0
0
Jeshi la polisi mkoani Arusha linamshikilia mwanafunzi wa Mwaka wa tatu wa chuo cha maendeleo ya jamii Tengeru aliyejulikana kwa jina la Harold Mmbando (23) mkazi wa Arusha kwa kosa la kutoa taarifa za uchochezi dhidi ya Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Mkuu wa majeshi Davis Mwamunyange pamoja na kusambaza ujumbe wa maneno makali juu ya viongozi hao.

Akiongelea tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo alisema kuwa tukio hilo lilitokea May 17 mwaka huu majira ya saa 09:00 asubuhi .

Alisema kuwa mwanafunzi huyo alitoa taarifa za uchochezi kuhusu mkuu wa majeshi ambapo alimtaka mkuu huyo wa majeshi kupindua nchi na kusema kuwa haiwezekani viongozi wote wawe nje ya nchi huku akuna kiongozi aliyepewa mamlaka ya kukikaimu kiti.

Mtuhumiwa huyo aliandika maneno haya,Mwamunyange pindua nchi haiwezekani wote wawe nje halafu hakuna aliyepewa mamlaka ya kukalia kile kiti,hayo ndio maneno aliyoyasema mtumiwa huyo“alisema Mkumbo.

Aidha aliongeza kuwa mbali na maneno hayo pia mtumiwa huyo alisambaza ujumbe mwingine wenye maneno yafuatayo,Dr Shein akiuawa kama Karume sitashangaa wala kustuka naomba mungu mauaji ya kisiasa yaliyotokea Zanzibar yawe kwa viongozi wa kisasa hasa watawala na sio wananchi wa kawaida hayo ndio maneno aliyoyaandika mtuhumiwa huyo kupitia mitandao ya kijamii kama facebook."

Mkumbo alisema kuwa mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani pindi tu upelelezi utakapo kamilika,huku akitoa rai kwa watu wote wanaotumia mitandao ya kijamii kutumia mitandao hiyo ya kijamii pasipo kukiuka sheria na taratiu za kisheria .

Alitumia muda huo pia kutoa onyo kali kwa yoyote atakaye bainika anatumia mitandao vibaya na kusema kuwa atachukuliwa hatua kali za kisheria dhidi yake.
 
Wakati hayo yakiendelea mshtakiwa wa kesi ya kumtukana Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli Isaac Emily (40), mkazi wa Olasiti jiji hapa inatarajiwa kuanza kusikilizwa mfululizo kuanzia Juni 5 mwaka huu katika mahakama ya hakiku mkazi Arusha.

CUF Yataka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aombe Radhi

$
0
0

Chama cha Wananchi(CUF) kimemtaka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa awaombe radhi watanzania kwa kuwadhalilisha kuwa hawapendi kufanya kazi, badala yake  wanashinda kuangalia Bunge, hali ambayo imeisababisha lisirushwe moja kwa moja.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF Taifa, Twaha Taslima amesema Waziri Mkuu alitoa tuhuma hizo kwa wananchi akiwa nchini Marekani hivi karibuni,wakati  siyo kweli kwamba watanzania wanakesha kuangalia bunge tangu  linapoanza hadi linakwisha bila kufanya kazi.

Hivi karibuni Waziri Majaliwa akizungumza na watanzania waishio Uingereza alisema sababu ya bunge kutorushwa moja kwa moja ni kutekeleza kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’

“Kama ni hivyo basi maisha ya watanzania wengine yangekwama hivyo Serikali ya awamu ya tano kazi yake kubwa sasa ni kutaka kuwarudisha watanzania kwenye woga wa kutoiwajibisha Serikali kwa kisingizio cha hapa kazi tu slogani hii ni ya kuua demokrasia,” amesema Taslima.

Taslima ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu hali ya demokrasia nchini na mwelekeo wa CUF baada ya Uchaguzi.

Amesema kuna madhara mengi katika kukandamiza demokrasia, ikiwamo wananchi kujenga chuki na Serikali, hivyo kushindwa kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za maendeleo.

Taslima ametumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi waliowezesha chama hicho kuongeza idadi ya wabunge kutoka 34 mwaka 2010 hadi 42 katika uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana.

Amesema CUF baada ya kumaliza shughuli za uchaguzi inajipanga kufanya ziara nchi nzima, lakini pia inajiandaa na uchaguzi wa kuziba mapengo ya uongozi ngazi mbalimbali kuanzia kwenye matawi hadi taifa.

“ Kwa sababu tofauti baadhi ya nafasi za uongozi badi zipo wazi  hivyo  ndani ya kuipindi cha miezi miwili ijayo tunatarajia kujaza nafasi hizo, wakati ile ya Mwenyekiti wa taifa ambaye alijiuzulu itajazwa Agosti chama kitakapoitisha mkutano mkuu wa taifa,” amesema.

Akizungumzia kuhusu ushirikiano ulivyo baina ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Taslima alisema umoja huo ulishinikizwa na wananchi walioichoka CCM, hivyo walihitaji vyama hivyo viunganishe nguvu ili kushika dola.

“Lakini ni wazi kwamba sheria hairuhusu kuungana hivyo UKAWA tupo nje ya sheria lakini hatujavunja sheria, sasa tunafikiria kuanza kufanya mchakato wa kujijenga ndani ya misingi ya sheria kwa chaguzi zijazo,”
amesema Taslima.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa CUF, Sheweji Mketo amesema ushindi wa majimbo 10 walioupata unatokana na tathimini ambayo waliifanya mara baada ya uchaguzi wa mwaka 2010.

“Baada ya uchaguzi ule kupita tulifanya CUF tulifanya tathimini ambapo tulibaini kwamba kuna majimbo 54 ambayo CCM licha ya wananchi kuichoka, lakini ilishinda kwa sababu kulikuwa na wagombea wengi wa vyama vya upinzani hali iliyosababisha kushindwa suluhisho lilikuwa ni kuungana,” amesema .

Breaking News: Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Waziri Wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga Baada Ya Kuingia Bungeni Akiwa Amelewa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Charles Kitwanga kuanzia leo tarehe 20 Mei, 2016.

Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kufuatia kitendo cha Mheshimiwa Charles Kitwanga kuingia bungeni na kujibu swali linaloihusu wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akiwa amelewa.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam

20 Mei, 2016
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images