Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Nape aagiza mkataba wa StarTimes na TBC Upitiwe Upya

$
0
0

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ameitaka Bodi mpya ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia upya mkataba wa StarTimes na shirika hilo.

Amesema kumekuwa na maneno kuhusu mkataba huo, hivyo bodi inapaswa kubainisha vifungu vya sheria ambavyo vitahitaji kufanyiwa marekebisho.

Akizungumza katika uzinduzi wa bodi mpya chini ya Mwenyekiti wake, Balozi Herbert Mrango, Nape alisema mapitio hayo yanaweza kufanyika ndani ya mwezi mmoja, kubaini mapungufu yaliyopo.

“Bodi hii inapokea majukumu yaliyoachwa na bodi iliyopita. Majukumu hayo ni pamoja na kupitia upya mkataba wa StarTimes na TBC kwani mkataba uliopo utaisha na utatakiwa kuwa na mkataba mpya,’’ alisema Nape.

Pia aliitaka bodi hiyo kuhakikisha kwamba baada ya miaka minne, TBC inajiendesha yenyewe kiuchumi kwa kuzingatia uwekezaji katika viwanja vyao.

Alisisitiza kuwa ni vyema bodi hiyo ikaangalia upya muundo wa shirika hilo na kwamba wawashirikishe wafanyakazi ili wajue nafasi zao.

Waziri Mkuu Akutana Na Mabalozi Wa Nchi Tatu

$
0
0

WAZIRI MKUU Kasim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi watatu kutoka nchi za Uturuki, Ireland na Uswisi pamoja na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa hapa nchini.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na mabalozi hao jana (Jumanne, Februari 23, 2016), ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu aliwashukuru mabalozi hao kwa kuja kujitambulisha rasmi na kwa pongezi walizokuja kumpatia na kuahidi ushirikiano zaidi pamoja na nchi hizo.

Mapema jana, Waziri Mkuu alikutana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa hapa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez ambaye alimweleza jinsi UNDP imekuwa ikisaidia programu za kukabiliana na maafa (resilience), ukuaji wa uchumi, utawala bora na masuala ya jinsia.

Alisisitiza haja ya Tanzania kuendeleza kampeni ya kupambana na ujangili na kusisitiza kuwa Umoja huo una nia ya kusaidia utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano.

Naye Balozi wa Uturuki, Bibi Yesemin Eralp alimweleza Waziri Mku nia ya nchi kuleta wawekezaji katika nyanja za kilimo, nishati, afya na ujenzi na kusisitiza kuwa kuna haja ya kufungua ubalozi wa Tanzania nchini kwao ili kuimarisha uhusiano uliopo.

“Tunao uwezo wa kifedha na tunao uwezo wa kitaalamu na kiteknolojia. Tukifungua viwanda hapa nchini, tunaweza kuongeza ajira kwa Watanzania,” alisema.

Naye Balozi wa Ireland nchini, Bibi Fionnuala Gilsenan alimweleza Waziri Mkuu jinsi ambavyo nchi yake imekuwa ikisaidia sekta za kilimo kupitia mpango wa ASDP, bajeti ya Serikali na suala la lishe na urutubishaji wa vyakula (food nutrition and fortification).

“Tulianza na suala la kilimo na bajeti ya Serikali. Hivi sasa tunataka kusaidia kwenye uelimishaji juu ya haki za wanawake, masuala ya uzazi wa mpango, pamoja na kupambana na ndoa za utotoni,” alisema.

“Tumeamua kupigia kelele suala la lishe na urutubishaji wa vyakula kwa sababu lishe duni imechangia kwa kiasi kikubwa udumavu wa watoto wengi. Tulipoanza tatizo hili lilikuwa limeenea kwa asilimia 46 kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano lakini sasa limepungua na kufikia asilimia 36 hadi 38,” aliongeza.

Alimuomba Waziri Mkuu Majaliwa alishikie bango suala hilo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kote nchini kwani mtoto akishadumaa kimakuzi hata akili yake pia inadumaa na tatizo lake haliwezi kurekebishwa kwa tiba yoyote ile.

Naye Balozi wa Uswisi nchini, Bibi Florence Mattli alimweleza Waziri Mkuu nia ya nchi yake kudumisha ushirikiano na Tanzania ambao umedumu kwa miaka 50 ili kukuza viwango vya uchumi na kuleta maendeleo kwa Watanzania.

Alimweleza Waziri Mkuu jinsi nchi yake imekuwa ikisaidia kundeleza nyanja za kupambana na rushwa kupitia TAKUKURU na kampeni ya kusaidia kujenga uelewa wa wananchi kupitia vyombo vya habari nchini.

Mkurugenzi wa Halmashauri Ya Kondoa Matatani Kwa Upotevu Wa Milioni 180

$
0
0

SELEMAN Jafo, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, amebaini upotevu wa Sh 180 milioni katika halmashauri ya wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.
 
Kutokana na kubainika kwa upotevu wa fedha hizo Jafo alitoa saa 48 kwa Hussein Issa ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, kuhakikisha anapeleka maelezo ya kina katika Ofisi ya TAMISEMI juu ya kuibiwa kwa fedha hizo ambazo ni za walipakodi watanzania.

Agizo hilo la Jafo lilitokana ziara ya kikazi iliyofanywa na naibu waziri huyo sambamba na kufanyika kwa kikao cha ndani katika Halmashauri hiyo.

Alisema, Serikali ya Awamu ya Tano haitavumilia kiongozi yoyote ambaye atafanya ubadhilifu kwa fedha ya Umma au jambo lolote ambalo linaonekana kuwepo na alufu ya ufisadi.

Alisema nchi imekuwa ikiendeshwa kimazoea na watu kujilimbikizia mali bila kuwa na hofu ya kuhojiwa jambo ambalo liliwafanya watumishi wa Umma kuwa na kiburi na kufanya kile wanachofikiria.

“Nchi imekuwa ikiendeshwa kimazoea sana watu wanakula hela bila utaratibu na wanafunika funika tu mambo huku wakiwafanya watu kama vipofu, hili haitavumiliwa hata kidogo lazima hatua stahiki zichukuliwe,” alisema.

Jafo alisema, anataka maelezo ya kina juu ya wizi wa fedha hizo na ndani ya masaa hayo 48 anataka awe amepata taarifa pale ofisini kwake.

Sambamba na hilo, aliagiza watu nane wanaotuhumiwa kuhusika na wizi wa fedha hizo wasimamishwe kazi na kukaa pembeni kupisha uchunguzi.

Aidha, aliwaagiza maofisa utumishi na wakuu wa idara kuwajibika na kutekeleza majukumu yao kikamilifu na kuachana na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea.

Naibu wiziri huyo alieleza kuwa kumekuwepo na malalamiko mengi juu ya watendaji we ngazi ya chini ambao wamekuwa wakionewa na kutopatiwa haki zao kama inavyostahili.

Alisema, watumishi hao wanalalamika kutolipwa malimbikizo yao mbalimbali kama fedha za likizo na kutopandishwa vyeo kwa wakati.

Kampuni Ya Kichina Matatani Kwa Kutengeneza Vibao Vya Namba Za Magari Kinyume Cha Sheria

$
0
0

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanya msako wa kushtukiza katika kampuni ya Tanzania China Trade and Tourism Development Ltd iliyoko Barabara ya Nyerere Dar es salaam baada ya kupata taarifa kutoka kwa msamaria mwema na kukamata vifaa pamoja na malighafi za kutengeneza na kutoa vibao vya namba za pikipiki kinyume na sheria.

Katika msako huo uliofanyika tarehe 19 Februari 2016 katika kampuni hiyo, Maofisa wa TRA waliweza kukamata na kutaifisha vibao vyenye namba za pikipiki 2,500 na vibao 5,600 ambavyo havikuwa na namba. Pia maofisa wa TRA walikamata malighafi za rangi ya vibao katoni tatu, pamoja na mashine ya kupaka vibao rangi yenye uzito wa kilo 155.

Mashine nyingine iliyokamatwa katika msako huo ni ya kutengeneza namba za magari yenye uzito wa kilo 902 ambayo imezuiwa isihamishwe kutoka katika kampuni hiyo pamoja na kompyuta mpakato ambayo imepelekwa katika maabara ya uchunguzi TRA kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Taarifa za kuwepo kwa utengenezaji wa vibao vya magari kinyume na taratibu na sheria zilitolewa na msamaria mwema ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni husika Donglinh Guo, Meneja wa Kiwanda Yong Qing Cheng na Meneja wa ghala Peng Zhan walikamatwa baada ya kutokea fujo wakati wa msako na kufikishwa katika kituo cha Polisi Changombe.

Kampuni ya Tanzania China Trade and Tourism Development LTd ndio waingizaji pekee wa pikipiki za Falcon tangu mwaka 2008 ambapo inatuhumiwa kutoa vibao vya namba za pikipiki kwa wateja wake kwa shilingi 5,000 kinyume na sheria.Uchunguzi wa thamani ya kodi iliyopotea bado unaendelea.
 
Vibao vya magari na pikipiki hutolewa na kampuni ambazo zinatambuliwa na TRA baada ya kupewa idhini. Kampuni hizo ni Masasi Sign, Auto Zone, Sign Industry, Kiboko, Budda Auto works, Parkinson Ltd na Next Telecom.

Ili kujiridhisha kuwa kadi za pikipiki zinazotolewa kwa wateja wa kampuni hiyo ni halali, TRA ilifanya uchunguzi na kugundua kuwa kadi hizo zinatolewa kihalali.

TRA inawatahadharisha wananchi kufuata taratibu na sheria ili kuepuka usumbufu unaoweza kutokea endapo watagundulika kujihusisha na vitendo ambavyo ni kinyume na sheria.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Akana Kutoa Amri ya Kufuta Matokeo ya Uchaguzi Zanzibar

$
0
0

MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete amesema hajahusika kufutwa kwa uchaguzi Zanzibar kwa kumpigia simu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha.

Aliyasema hayo juzi mjini Kibaha wakati wa uzinduzi wa jengo la Ofisi ya Chama ya Kibaha Mjini mkoani Pwani na kusema maneno hayo ni ya uongo, hayana ukweli wowote na watu hawapaswi kutoa shutuma hizo juu yake.

Rais huyo wa Awamu ya Nne alisema maneno hayo hayana kichwa wala miguu wala hajawahi kumpigia simu Jecha kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya kufutwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kwani tume hiyo inajitegemea.

“Wasitoe lawama zisizohusika, wapuuzeni sikuwahi kufanya hivyo hata kwa Damian Lubuva wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania hivyo nashangaa watu wanavyosema kuwa nimehusika kufutwa uchaguzi huo,” alisema Kikwete.

“Tume ya Zanzibar ni tume huru na inajitegemea kwani ina mambo yake hata Dk Ali Mohamed Shein (Rais wa Zanzibar) hana uwezo wa kuingilia na kuahirisha uchaguzi huo, watu hao wasipake watu matope wasio husika kwani kila mtu ana nafasi yake,” alifafanua Kikwete.

Alisema kikubwa kinachotakiwa ni kuwaombea Wazanzibari wafanye uchaguzi wao mkuu wa marudio kwa amani na utulivu ili wapate viongozi wao wa kuiongoza Zanzibar na wawaombee wagombea wa CCM washinde.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Mwinshehe Mlao alisema Mbunge wa Kibaha Mjini, Silvestry Koka ameonesha njia ya kiongozi kutumia fursa kuboresha mazingira ya utendaji kazi Awali, Koka ambaye ndiye aliyejenga ofisi hiyo yenye thamani ya Sh milioni 100, alisema aliamua kujitolea kujenga ofisi hiyo kwa lengo la kukisaidia chama kiendeshe shughuli zake.

Koka alisema aliamua kujenga kama kumbukumbu kwa wanaKibaha ili iwe kielelezo cha uongozi wake kama mbunge wa Jimbo hilo kwa ajili ya kufanya shughuli za chama badala ya kufanyia sehemu zisizo na hadhi yao.

Kurasa za Mbele na Nyuma Za Magazeti ya Uingereza ya Leo February 24, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya Februari 24

Baba Amchoma Mwanawe vidole kisa Mboga Ya Sh. 500

$
0
0

MKAZI wa kitongoji cha Kazima – Kichangani Kata ya Kawajense, Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Emmanuel Joseph (31) amemfanyia unyama mtoto wake wa kumzaa, George Emmanuel (4) kwa kuvichoma kwa moto vidole vyake vya mkono wa kushoto, akimtuhumu kukomba mboga yote ya majani aina ya ‘chainizi’ yenye thamani ya Sh 500.

Inasemekana baba huyo amekuwa akiishi na watoto wake watatu baada ya kuachana na mkewe wa ndoa, Semsni Jahala (28) Machi mwaka jana.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Rashid Mohamed amethitibisha amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema lilitokea juzi saa 12 jioni katika kitongoji cha Kazima– Kichangani.

Akisimulia mkasa huo, Kaimu Kamanda Mohamed alisema mtuhumiwa huyo amekamatwa kwa mahojiano na anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wa awali wa shauri lake kukamilika.

“Jioni hiyo ya tukio saa kumi na moja jioni mtuhumiwa huyo (Emmanuel) alipika chakula cha jioni, ugali na mboga za majani maarufu chainizi kisha akakihifadhi chakula hicho jikoni na kuondoka … aliporudi nyumbani saa kumi na mbili jioni ili kuandaa chakula cha jioni ndipo alipobaini mtoto wake (George) amekomba mboga yote ya majani. 

"Alikasirishwa na kitendo hicho na kusababisha kumpiga kisha kumchoma moto vidole vyake vitatu vya mkono wa kushoto na kumsababishia maumivu makali,” alieleza Kaimu Kamanda.

Kwa mujibu wa mashuhuda kutoka eneo hilo la tukio, mtoto huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ambako amelazwa kwa matibabu.

Akizungumzia tukio hilo, Ofisa Ustawi wa Jamii wa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda, Oscar Mkenda alisema mke aliamua kuachana na mumewe huyo baada ya kuchoshwa na ukatili na unyanyasaji aliokuwa akifanyiwa, ikiwemo kupigwa mara kwa mara bila sababu yoyote.

“Mtoto George alikomba mboga hizo zote za majani baada ya kushinda na njaa mchana kutwa kwani hata kifungua kinywa hakupa asubuhi… hivyo baada ya baba yake kubaini mtoto wake George amekomba mboga zote, ndipo alipochochea moto na kuukandamiza mkono wake wa kushoto na kuunguza vibaya vidole vyake vitatu,” alieleza Mkenda.

Ezekiel Maige Atajwa Ufisadi Ngorongoro

$
0
0

Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii katika serikali ya awamu ya nne, Ezekiel Maige, jana alitajwa katika kesi inayomkabili aliyekuwa Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Bernard Murunya  ambaye ameshitakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi.
Katika kesi hiyo, Maige anadaiwa kulipiwa nauli ya safari ya nje na mamlaka hiyo kwa idhini ya Murunya, ambaye sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki. 
Shahidi wa kwanza katika kesi hiyo, Sezari Semfukwe, alidai kuwa Murunya na aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Mamlaka hiyo, Shad Kiambile, waliidhinisha malipo ya dola 66,890. Alidai kuwa fedha hizo zilikuwa kwa ajili ya safari ya Maige na msaidizi wake aliyetajwa kwa jina la E. Muyungi na Murunya mwenyewe.
Semfukwe, ambaye ni Kaimu Mhasibu Mkuu wa mamlaka hiyo, alidai kuwa Murunya na Kiambile, ndio walioidhinisha madokezo kwa ajili ya malipo hayo. 
Akiongozwa na Wakili wa Serikali Hamidu Sembano, akisaidiana na Rehema Mteta, mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha, Patricia Kisinda, Semfukwe alidai kuwa utaratibu wa maombi ya safari, unatokana na maelekezo ya mkuu wa idara na kujaza fomu inayoonyesha anakwenda wapi na kwa muda gani.
Sambamba na hilo, alidai kuwa aina zingine za safari zinahusisha watu wa nje ambao, si waajiriwa wa NCAA kwa dokezo la mkuu wa idara au shirika.
Alidai kuwa alitoa hundi ya malipo namba 309/0238 ya Septemba 9/2011, ambayo ilikuwa na dokezo la safari kutoka kwa Murunya kwenda kwa Mkuu wa Kitengo cha Fedha. Pia  alitoa hundi ya malipo nyingine iliyokuwa ikionyesha imelipwa dola zaMarekani  66,890 kwa kampuni ya Wakala wa Usafirishaji ya Cosmas.
Aliendelea kudai kuwa hundi za malipo namba 310/0379 ya Oktoba 29, 2011 na ankara namba 5609 ya Septemba 7,  2011 zililipwa kwa Antelope Tours & Traveling kwa ajili ya tiketi za Murunya, Muyungi na Maige kwa malipo ya dola za Marekani 66,890 (zaidi ya Sh. milioni 133).
Shahidi hiyo alidai kuwa kumbukumbu ya kitabu cha malipo ya hundi inaonyesha hundi namba 002758 na 002755 za Septemba 9,  2011 zililipwa kwa kampuni ya Cosmas Travelling Agent na zilitiwa saini na Kiambile na Murunya.
Hata hivyo, wakati shahidi huyo akitoa vielelezo hivyo mahakamani hapo ili vitumike kama ushahidi, malumbano ya kisheria yaliibuka baina ya mawakili wa pande zote.
Malumbano hayo yaliibuka baada ya upande wa washtakiwa, ukiongozwa na wakili Amani Mirambo, kutaka kujua ni vielelezo vingapi au vya aina gani ambavyo upande wa mashtaka unavileta.
Hatua hiyo ilisababisha malumbano ya kisheria hivyo kumfanya hakimu kuahirisha kesi kwa dakika 10. Baada ya muda huo, alirejea mahakamani baada ya dakika hizo na kuwahoji.
Baada ya kuhoji pande zote mbili, kutokana na malumbano ya kisheria, Hakimu alikatizwa na Wakili wa Serikali Hamidu Simbano, aliyemwomba  kuahirisha kesi hiyo na kutaja tarehe nyingine ya  washtakiwa kusomewa maelezo yao ya awali.
Awali, Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Rehema Mteta, aliwasomea maelezo ya awali juu ya tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka yaliyosababisha mamlaka hiyo kupoteza dola 66,890 (Sh. 133,780,000).
Mteta aliwataja washitakiwa, mbali na Murunya na Kiambile, kuwa ni Meneja Utalii wa mamlaka hiyo, Veronica Funguo na Salha Issa ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Cosmas Travelling Agent.

NECTA Yasitisha Kugawa vyeti kwa Wahitimu wa Kidato cha Sita 2015 ......Vilivyogawiwa Vyatakiwa Kurudishwa Haraka

$
0
0

Baraza la Taifa la Mitihani (Necta), limeagiza kusitishwa kwa ugawaji wa vyeti vya kidato cha sita kwa wanafunzi waliohitimu mwaka 2015, huku vile vilivyokwisha gawanywa kwa watahiniwa hao vikitakiwa kurejeshwa kwenye chombo hicho.

Hali hiyo imeibua utata mkubwa, huku baadhi ya wadau wakiwamo maofisa elimu, wakihisi hatua hiyo ya Necta huenda inalenga kuvibadili vyeti hivyo kutoka kwenye mfumo wa wastani wa alama (GPA), kwenda kwenye ule wa jumla (division).

Ofisa Elimu Mkoa wa Dodoma, Juma Kaponda, alipoulizwa  kama amepokea agizo hilo, alithibitisha kuwa shule zote za mkoa huo zenye kidato cha tano na sita zimepewa taarifa ya kutakiwa kurudisha vyeti hivyo Necta.

Alisema sababu ya kuvirudisha vyeti hivyo anadhani ni kufanya mabadiliko kutoka GPA na kurudi kwenye divisheni.

Ofisa Elimu Mkoa wa Arusha, Nestory Mloka, alisema amepata barua ya maelekezo hayo kutoka Necta ikimuelekeza kuwataka maofisa elimu wilaya wawasiliane na wakuu wa shule za kidato cha tano na sita wasigawe vyeti vya wanafunzi waliohitimu mwaka 2015.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya St. Matthew iliyoko Kongowe, Mkuranga mkoani Pwani, Abraham Shafuri, naye alikiri kuwapo kwa agizo la Necta la kusimamisha utoaji wa vyeti hivyo kwa wahusika.

Alisema aliambiwa na maofisa wa Necta kuwa vyeti hivyo vinatakiwa kurejeshwa kwenye baraza hilo na kwamba sababu zilizotolewa ni kuwa kuna marekebisho kidogo yanapaswa kufanyika.

“Nilichoambiwa ni kwamba shule karibu zote za Dar es Salaam zimesharejesha vyeti hivyo na kwamba kwa sisi wa mkoa wa Pwani, maofisa hao watapita kuvichukua lakini hatujui ni lini watakuja,” alisema Shafuri.

Hata hivyo, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk, Charles Msonde, alipoulizwa   alikanusha vikali madai hayo, akisema vyeti hivyo havitabadilishwa kutoka kwenye mfumo wake bali vimesitishwa kugawanywa ili baraza lijiridhishe na baadhi ya vitu.

“Vyeti hivi baraza limevigawa hivi karibuni na lilichofanya sasa limezuia kwanza shule zisigawe mpaka litakapotoa maelekezo mengine, msingi huo wa kuzuia uko kwenye hoja ya kuhakikisha tu kwamba linajiridhisha kwenye takwimu zake kama zimekaa sawasawa katika vyeti vilivyokwenda kila shule.

“Baadhi ya vyeti kwenye mkoa wa Dar es Salaam vipo Necta, lakini kwenye mikoa mingine yote viko shuleni,” alisema Dk Msonde na kuongeza;
 
“Kama mkuu wa shule alikuwa amegawa vyeti viwili, vitatu kabla havijarejeshwa baraza ni suala jingine, lakini kiujumla kinachofanywa na baraza hapa ni kuhakiki cheti hiki, kama vimekaa kama utaratibu wetu ulivyo.”

Alisema suala la kubadilisha kutoka kwenye GPA kwenda kwenye divisheni halipo na kwamba matokeo yaliyotangazwa kwa utaratibu wa GPA vyeti vyake vitaendelea kuwa katika mfumo wa GPA na matokeo yaliyotangazwa kwenye utaratibu wa divisheni vyeti vyake vitabaki kuwa kwenye divisheni.

Alisema kwa wale ambao tayari wako nje ya nchi, hakuna atakayeathirika na kama baraza likihitaji cheti chake litafanya utaratibu wa kukipata.

Kikwete Kuwatumbua MAJIPU Wanachama Wasaliti wa CCM Waliokihujumu Chama Wakati wa Uchaguzi Mkuu

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Jakaya Kikwete amesema kuwa chama chake kitawachambua na kuwaadhibu wote ambao walikisaliti katika Uchaguzi Mkuu uliopita, kuanzia ngazi za matawi, kata, wilaya, mkoa hadi Taifa.

Dk. Kikwete ametoa kauli hiyo Jumatatu ya wiki hii mjini Kibaha alipohudhuria sherehe za uzinduzi wa ofisi mpya ya chama hicho mjini humo.

“Baada ya mchakato wa Dodoma wapo ambao walisusa kabisa na wakawa wanajificha. Unakuta hahudhurii mikutano yetu ya kampeni, lakini ya wenzetu upinzani unamkuta na akiulizwa anasema eti alialikwa,” alisema na kusisitiza kuwa wanachama kama hao ni wasaliti na uanachama wao una mashaka.

Kikwete alisema mchakato wa kuwaadhibu wanachama wasaliti utafanyika wakati wowote baada ya kuyapitia majina ya wote wanaotuhumiwa kukihujumu chama.

“Tayari tuna majina ya watu ambayo yanadhaniwa walikihujumu chama. Tutayapembua katika vikao mbalimbali halali kuanzia ngazi za matawi, kata, wilaya, mkoa na Taifa na tutaamua kwa haki wakati wa kuwaadhibu,” alisema.

Aliwataka wanachama hao kufanya tathmini na kutambua waliokisaliti chama lakini alionya vikao vya kuwabaini vitende haki bila kumuonea mtu akisema yapo baadhi ya majina yanatajwa kuwa ni wasaliti kutokana na migogoro binafsi baina yao.

Ray C Alia na Ugumu wa Maisha.....Aeleza mtindo anaotumia kupanda daladala Ili Kukwepa Aibu

$
0
0

Ray C ameweka wazi kuwa yuko taabani kiuchumi, hali inayompelekea kukosa hata pesa ya usafiri wa kwenda hospitali kupata dozi ya tiba ya maradhi yanayomkabili kutokana na kuathirika na matumizi ya dawa za kulevya.

Akiongea na Planet Bongo ya EATV hivi karibuni, Ray C alieleza kilio chake akidai kuwa sio tu kwamba amekosa pesa ya kuendelea kusapoti muziki wake baada ya aliyeahidi kumsaidia kumkimbia, bali inamlazimu kupanda daladala akiwa ndani ya vazi la ‘ninja’ kutokana na kushindwa gharama za usafiri.

“Jamani kiukweli haya maisha ya wasanii nyie acheni tu, yaani inabidi tumuombe tu mungu, mtu akikuona msanii kwenye daladala nani atanunua albamu yako, nani atakuja kwenye show yako, lakini mama ananiambia vaa ninja mwanangu nenda kapate tiba.  Kwa sababu kila siku kukodi taxi ni gharama sana, kutoa elfu 25,000 kutoka Bunju mpaka hospitali kila siku ni nyingi sana," alieleza.

“Sometimes namwambia mama inabidi tutoke mapema saa 11 hivi nivae ninja twende kwanza kanisani then naweza nikachukua hata bajaji kwenda hospitali. Haya ni maisha sio kitu cha kucheka ni lazima nifanye hivyo ili niweze kumaliza dozi,” aliongeza.

Ray C alieleza kusikitishwa na namna ambavyo baadhi ya magazeti yanamuandika na kumchafulia jina kwa kile alichodai ni habari za kutungwa kuwa amerudia dawa za kulevya, badala ya kuandika habari njema zinazomhusu.

Mwimbaji huyo ambaye album yake imekwama studio, aliwaomba wadau na wananchi kwa ujumla kumsaidia hata kwa kumchangia kiasi kidogokidogo cha fedha ili aweze kumudu gharama za maisha na hata kurejea jukwaani.

Taarifa ya Uteuzi wa MKurugenzi MKuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)

$
0
0

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amemteua Hamza Said Johari kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA).
 
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa na Katibu Mkuu (Uchukuzi), Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leornald Chamurinho ambapo imeeleza kuwa uteuzi huo unaanza Februari 22 mwaka huu.
 
Kabla ya uteuzi huo, Johari alikuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Walaji wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA – Consumer Consultative Council).
 
Mkurugenzi Mkuu huyo mteule amejaza nafasi iliyokuwa ikikaimiwa na Redemptus Bugomola.

Chuo Kikuu cha St. Joseph Tawi La Arusha chafungwa kwa muda Usiojulikana

$
0
0

Uongozi  wa  Chuo  Kikuu  cha St. Joseph tawi  la  Arusha  umekifunga chuo  hicho  kwa  muda  usiojulikana  baada  ya  wanafunzi  kufanya  vurugu  chuoni  hapo.

Inaelezwa  kuwa, wanafunzi  wa  chuo  hicho  wamekuwa  katika  hali  ya  wasiwasi  wakihofia  chuo  chao  kufungwa  na  serikali  kama  kilivyofungwa  St. Joseph  tawi  la Songea 

Wanafunzi  wote  wameamriwa  kuondoka chuoni  na  wametakiwa  kusoma magazeti  au  kutembelea tovuti  ya  chuo  hicho  ili  kujua  hatima  yao.


Mtoto wa Miaka Mitatu Abakwa Na Kunyongwa Hadi Kufa

$
0
0

Mtoto mwenye umri wa miaka 3 na miezi 4 Mariam Deogratius mwanafunzi wa shule ya awali ya Makoko iliyopo katika Manispaa ya Mji wa Musoma mkoani Mara, amebakwa kisha kunyongwa hadi kufa na mtu asiyejulikana Usiku wa kuamkia leo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara kamishna msaidizi Philllip Kalang amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa Jeshi la Polisi linafanya Msako kuhakikisha Mhalifu anapatikana.

Mwakyembe: Katiba Mpya sio Kipaumbele cha Rais Magufuli....Wanaofikiri Tutaanza Na Rasimu Ya Warioba Wanapoteza Muda

$
0
0

Dr. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria amewataka Watanzania wanaoulizia hatima ya mchakato wa katiba mpya kutambua kuwa suala hilo si sehemu ya vipaumbele vya Dk. John Magufuli.

Mwakyembe amesema hayo jana usiku katika mahojiano maalum aliyofanya na Marin Hassan, mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), juu ya utendaji wa wizara yake katika siku 100 za serikali ya awamu ya tano.

Waziri huyo alisema kuwa katiba mpya haina umuhimu mkubwa katika maisha ya kila siku ya watu na wala sio kipaumbele cha rais Magufuli kwani ni kiporo tu alichoachiwa na serikali ya awamu ya nne na atakifanyia kazi wakati atakapoona inafaa.

“Watu wanadhani katiba mpya ndiyo kila kitu, wanaona katiba ni muhimu kuliko kulipia watoto waende shule, wanafikiri katiba mpya ikishapitishwa tu basi kesho yake wataletewa mkate na chai kitandani jambo ambalo sio kweli,” amesema Dk. Mwakyembe.

Aliongeza kuwa: “Kwa sasa rais bado anafanyia kazi vipaumbele vyake kwanza ikiwemo kusimamia elimu bure, kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato ya serikali na kusimamia uwajibikaji wa watumishi wa umma na hivyo kelele za katiba mpya hazina msingi.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mwakyembe alisema Watanzania ambao bado wana ndoto kuwa mchakato wa katiba mpya unaweza kuanzia katika hatua ya kujadiliwa kwa rasimu ya katiba ya Jaji Joseph Warioba kuachana na wazo hilo kwani limepitwa na wakati.

Alisisitiza kuwa katiba iliyopendekezwa na kupitishwa na wajumbe wengi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni halali kwani ilipatikana kwa mujibu wa sheria na taratibu licha ya kususiwa na wajumbe wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Ukawa unaoundwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), National League for Demokracy (NLD) na NCCR Mageuzi.

“Rais alishasema alipohutubia bunge, kwamba kuna kiporo nimeachiwa, sasa mimi nashangaa hawa watu! tena wengine wana shahada za sheria, wanaongea nini? Hatua ya rasimu ya Warioba ilishapitwa na wakati na tayari tunayo katiba pendekezwa,” aling’aka.

Mwakyembe alihitimisha kwamba utakapofika wakati wa kulifanyia kazi suala la katiba mpya, serikali ya awamu ya tano itaendelea na hatua ya kura ya maoni ya katiba pendekezwa na sio vinginevyo.

Rais Magufuli Azungumza Na Katibu Mtendaji Wa Afrika Mashariki.....Wameongea Nini? Bofya Hapa

$
0
0

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Richard Sezibera Ikulu Jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine Rais Magufuli amepokea taarifa ya maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika tarehe 02 Machi, 2016 Katika Jiji la Arusha, Nchini Tanzania.

Rais Magufuli ndiye Mwenyekiti wa sasa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inayojumuisha nchi tano wanachama ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo hayo Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo Dkt. Richard Sezibera, amesema maandalizi kuhusiana na mkutano huo yanakwenda vizuri.

Amesema pamoja na mambo mengine mkutano huo, utajadili masuala kadhaa yakiwemo mpango wa kuanzisha viwanda vya magari ndani ya Jumuiya ili kupunguza uingizaji wa magari kutoka nje ya nchi na Marais kuzindua pasi ya kusafiria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kuhusu hali ya Jumuiya, Dkt. Sezibera amesema inaendelea vizuri na ametaja baadhi ya mambo ambayo yamefanyika kuwa ni kutiwa saini kwa mkataba wa umoja wa forodha, makubaliano ya soko la pamoja na makubaliano ya sarafu moja.

Mengine ni kuwepo kwa mazungumzo kuhusu uimarishaji wa miundombinu kama vile reli na umeme ndani ya Jumuiya, na mazungumzo kuhusu umoja wa kisiasa.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Dkt. Augustine Mahiga, amesema Tanzania ikiwa ni mwenyeji wa kikao hicho ipo tayari kupokea ugeni na kwamba pamoja na kufanyika kwa kikao hicho, marais wa Tanzania na Kenya watafungua barabara inayounganisha Tanzania na Kenya katika Mpaka wa Holili na kutakuwa na shughuli ya kuweka jiwe la msingi katika kituo cha pamoja cha mpakani kwa ajili ya kuwezesha upitaji wa mizigo na watu yaani "One Stop Boarder Post"

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es salaam.
24 Februari, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Dkt. Richard Sezibera, Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Ikulu jijini Dar es Salaam Februari 24,2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Dkt. Richard Sezibera, Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Ikulu jijini Dar es Salaam Februari 24,2015 baada ya mazungumzo 

Bodi ya Mikopo Ya Wanafunzi Yatoa Utaratibu wa Kuwasilisha Malalamiko.

$
0
0

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa  utaratibu wa kushughulikia  malalamiko ya wanafunzi wanaopata mikopo katika taasisi za elimu ya juu nchini.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano Omega Ngole alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko ya wanafunzi wa elimu ya juu nchini.

“Utaratibu huu ulioboreshwa, ni msisitizo na maelekezo ya Serikali ya mwezi Agosti 2011 kupitia iliyokuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambayo ilielekeza Taasisi zote za Elimu ya Juu nchini zinazopata mikopo kutoka Bodi ya Mikopo kuanzisha Madawati ya Mikopo ili kuongeza ufanisi katika utoaji mikopo”,Alisema Ngole.

Ameongeza kuwa, dawati hilo linatakiwa kusimamiwa na mtumishi teule wa chuo husika mwenye sifa na uhusiano mzuri na jamii na linapaswa kuwa chini ya Makamu Mkuu wa chuo husika anayeshughulikia taaluma.

Meneja Ngole amesisitiza kuwa kwa sasa vyuo vyote vina Maofisa Mikopo ambao wanawajibika kutafuta suluhisho la suala linalowasilishwa na kulitolea majibu.

Akifafanua hatua zinazotakiwa kufuatwa na Maofisa hao katika kutafuta suluhisho la malalamiko ya wanafunzi amesema kuwa, baada ya malalamiko kufika kwa Ofisa Mikopo yanatakiwa yapate suluhisho ndani ya siku mbili tangu kuwasilishwa kwake,ikiwa hatakua na ufumbuzi atatakiwa kuwasiliana na uongozi  wa juu wa chuo husika.

Endapo uongozi  wa juu wa chuo hautokuwa na ufumbuzi, malalamiko hayo yatatakiwa kupelekwa kwenye Ofisi za Kanda ambazo zinapatikana katika Mikoa ya Mwanza, Dodoma, Arusha na Zanzibar au ofisi za makao ya makuu ya Bodi  zilizoko jijini Dar es Salaam.

Bodi ya Mikopo ilianzishwa kwa sheria ya Bunge namba 9 ya mwaka 2004 na kuanza rasmi mwezi Julai 2005 kwa majukumu ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji waliodahiliwa katika Taasisi za Elimu ya Juu pamoja kukusanya marejesho ya mikopo yote iliyotolewa tangu mwaka 1994.

Rais Magufuli Amtumia Salamu Za Pongezi Rais Yoweri Museveni Kwa Kushinda Urais Uganda

$
0
0
The President of the United Republic of Tanzania, H.E Dr. John Pombe Joseph Magufuli has sent congratulatory message to the President of the Republic of Uganda, H.E Yoweri Kaguta Museveni following his re-election as the President at the election held on February 18th 2016. The message reads as follows:

H.E. Yoweri Kaguta Museveni,

President-Elect of the Republic of Uganda,

KAMPALA.

Your Excellency and Dear Brother,
It gives me great pleasure, on behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, to extend to Your Excellency our heartfelt congratulations on your re-election as the President of the Republic of Uganda. Your re-election at the helm of your country is a true reflection of the confidence that the people of Uganda have in you as well as a testimony of their trust in your exemplary leadership.

I also take this opportunity to congratulate your party, National Resistance Movement for its outstanding victory in the General Elections. As you are well aware, both my party, Chama Cha Mapinduzi (CCM) and the Government of the United Republic of Tanzania have enjoyed brotherly relations with the Ugandan people throughout the years.

While congratulating you on your well deserved re-election, I wish to reaffirm my readiness and determination to continue working with you in further strengthening our relations for the benefit of our two countries and peoples.

Please accept, Your Excellency and Dear Brother, the assurances of my highest consideration.

Issued by the Ministry of Foreign Affairs, East Africa, Regional and International Cooperation

February 24, 2016.

Mwanafunzi Wa Kidato Cha Tatu Ajinyonga

$
0
0

Mwanafunzi wa Kidato cha Tatu katika Shule ya Sekondari Nyanungu Tarafa ya Ingwe wilayani Tarime mkoani Mara, Charles Chacha (19), amekutwa amejinyonga chumbani kwake kwa kutumia kamba ya katani.

Diwani wa kata hiyo ya Nyanungu, Mang’enyi Ryoba amesema Chacha alijinyonga Februari 23, mwaka huu usiku, baada ya yeye na wenzake wawili wa kike kupewa barua shuleni siku hiyo ya adhabu ya kutodhudhuria shuleni kwa siku 14.

"Sababu ya kupewa barua hiyo ya adhabu haijafahamika. Tunafutilia kujua tatizo la wanafunzi hao lilikuwa ni nini.Tulitoa taarifa kituo cha Polisi Kegonga na Nyamwaga ambao walifika na kuuchukua mwili wa marehemu huyo,” alisema Diwani Mang’enyi.

Kamanda wa Polisi Tarime/ Rorya, Gemini Mushi alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kueleza kuwa chanzo kinachunguzwa.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images