Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TBS Yawataka Wazalisha Nondo Kuanza Kuweka Lebo ( TBS steel bar ID & labelling )


Gavana Azindua Mwongozo Wa Kwanza Wa Kitaifa Wa Elimu Na Ulinzi Kwa Mtumiaji Wa Huduma Za Fedha (N-FEF).

$
0
0

Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwa kushirikiana na Mfuko wa Kuendeleza Huduma za Kifedha Tanzania (FSDT), imezindua Mwongozo wa taifa wenye lengo la kuongeza uelewa kuhusu elimu ya mambo ya fedha kwa wananchi.

Uelimishwaji wa wananchi kuhusu mambo ya fedha utatekelezwa kupitia “Mwongozo wa kwanza wa kitaifa wa elimu na ulinzi kwa mtumiaji wa huduma za fedha” (N-FEF).

Gavana Prof. Beno Ndulu ameuzindua rasmi mwongozo huu ambao utajikita katika kutatua changamoto zilizobainishwa katika utafiti uliopima uelewa wa mambo ya fedha kwa watu wazima nchini Tanzania. Utafiti huu unaitwa “Uwezo wa Kifedha Tanzania” wa mwaka 2014.

Utafiti huo umebainisha kuwa watanzania wengi hawana elimu na ujuzi mahususi wa masuala ya mambo ya fedha kwa ujumla, hivyo kuwanyima fursa ya kutumia huduma za kifedha kwa faida yao.

Katika utafiti huo imeonyeshwa kuwa upatikanaji wa huduma za fedha umekuwa na changamoto katika maeneo mengi huku zile zitolewazo kwa njia ya mitandao bado hazikidhi matarajio ingawa zinawafikia wateja wengi kwa sasa.

Sambamba na hilo kumekuwa na uhaba wa nyenzo na miundombinu ya kuhifadhi na kufikisha taarifa za fedha kwa watumiaji wa huduma hizo kwa kuzingatia namna sahihi ya kutoa taarifa, kuwaelimisha na kuwalinda.

Kutokana na utafiti wa “Uwezo wa Kifedha Tanzania” wa mwaka 2014 wananchi kutoka makundi mbalimbali katika jamii hawana ujuzi wa hesabu za kawaida ambao ndiyo msingi mkuu katika nadharia ya masuala yahusuyo mambo ya fedha.

Elimu msingi katika masuala ya fedha umekuwa kikwazo kwa waliowengi hasa katika uandaaji wa bajeti, kutunza kumbukumbu ya matumizi, kupanga fedha kwa matumizi yasiyotegemewa ama ya ziada na muhimu zaidi kutunza kiasi kwa ajili ya matumizi ya uzeeni (baada ya kustaafu).

Inaonekana kuwa upatikanaji wa taarifa za masuala ya fedha hutegemea zaidi vyombo vya habari kama redio, televisheni na magazeti lakini vyombo hivi kwa sehemu kubwa, hufikisha zaidi taarifa za biashara na masoko kuliko ambavyo vinaelimisha jamii kuhusu matumizi na upangaji wa mapato yao.

“Haya ndiyo masuala mahususi ambayo mwongozo huu wa taifa kuhusu elimu ya huduma za fedha unalenga kushughulika nayo,” alisema Prof Ndulu.

Pamoja na kuwepo ongezeko la upatikanaji wa huduma za kifedha, mpaka asilimia 58 mwaka 2013 kutoka kiwango cha asilimia 17 mwaka 2009, miongoni mwa watu wazima nchini, bado mwongozo huu ni muhimu ili kuleta mfumo imara wa sekta ya fedha na Zaidi sana ili kuleta ustawi wa maisha ya watanzania kwa ujumla.

Prof. Ndulu anasema kutatua changamoto za kielimu kwa ujumla na hususan elimu ya huduma za fedha italiwezesha taifa kuwa katika mwelekeo mzuri wa kukabiliana na umasikini na kufikia malengo ya kukuza uchumi.

“Tunapaswa kujiuliza: ni kwa namna gani wananchi hasa wale masikini na wasiokuwa na elimu za kifedha za wanapambana kuendeleza biashara zao katika mazingira ya soko huria na lenye ushindani kila uchwao” alisisitiza Prof. Ndulu.

Hivyo, mwongozo huu utahakikisha watanzania wapata elimu sahihi na ya uhakika ya huduma za kifedha pamoja na njia anazoweza nazo kujilinda katika ushindani huu.

Vilevile mwongozo huu umeundwa ili kutatua changamoto za kifedha zinazohusiana na maamuzi miongoni mwa watumiaji wa huduma hizi na kuwa jumuishi na wenye tija kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Mwongozo wa taifa kuhusu elimu ya huduma za fedha umeandaliwa kwa kujumisha washikadau kutoka Tanzania bara na Zanzibar.

Unabainisha changamoto zinazohusuana na uwezo wa kifedha ambazo zinahitaji kutatuliwa kwa uwepo wa elimu ya fedha. Pia, unatoa taratibu wakufanikisha utekelezaji wa elimu ya fedha, na mwongozo wa kitaifa wa kuratibu elimu ya fedha nchini.

Lengo la mwongozo wa elimu ya huduma za fedha ni kuwa na wananchi na kaya zenye uwezo kifedha nchini.

Waziri Mkuu Majaliwa Awatembelea Waathirika Wa Mafuriko Iringa, Apokea Misaada Ya Maafa Ya Sh. Milioni 86/-

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea misaada mbalimbali yenye thamani ya sh. milioni 85.88/- kwa ajili ya wananchi walioathirika na mafuriko kwenye vijiji vya kata ya Mlenge, tarafa ya Pawaga,  wilaya ya Iringa vijijini mkoa wa Iringa. 

Misaada hiyo imetolewa na wadau mbalimbali kutokana na mafuriko ambayo yalibomoa nyumba 82 katika kitongoji cha Kilala, kijiji cha Kisanga na kuwaacha wananchi wake bila makazi. 
 
Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kasanga ambako alikwenda kukagua athari za mafuriko  na kuwapa pole wananchi hao jana mchana (Jumatatu, Februari 22, 2016), Waziri Mkuu aliwashukuru wadau wote waliojitolea kuwachangia watu waliopata maafa kutokana na mafuriko hayo.
 
Wadau waliotoa misaada hiyo ni Benki ya NMB mabati 500, mifuko ya saruji 500, kilo 820 za maharage, kilo 750 za unga wa mahindi na lita 250 za mafuta ya kupikia vyote vikiwa na thamani ya sh. milioni 20/-. Wengine ni Mfuko wa Pensheni wa PPF uliotoa mabati 200 na mifuko ya saruji 200  vyenye thamani ya sh. milioni 6.6/-.
 
Wengine ni Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) waliotoa mabati 200 na mifuko ya saruji 160 vyenye thamani ya sh. milioni 4.5/-; Kiwanda cha kusindika nyanya cha RedGold kimetoa mifuko ya saruji 100 na mabati 50 vyenye thamani ya sh. Milioni 3/-; mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya CHADEMA, Bi. Susan Chogisasa na wenzake wametoa mabati 150, mifuko 23 ya saruji, kilo 100 za  maharage, kilo 50 za chumvi na nguo mbalimbali vyote vikiwa na thamani ya sh. milioni 1.3/-.

Madiwani wa Iringa Vijijini walitoa sh. 380,000/-, Wabunge wa Viti Maalum kupitia CCM walitoa vifaa vya sh. Milioni 1.7/-; ofisi ya CCM Mkoa wametoa vifaa vya sh. milioni 6.1/-, Kamanda wa UVCCM Mkoa wa Iringa,  Bw. Salim Abri aliipatia Halmashauri ya Wilaya ya Iringa sh. milioni 5/- ili wanunue vyakula vya waliopatwa na maafa.
 
Naye Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni mbunge wa Isimani, Bw. William Lukuvi alitoa fedha taslim sh. milioni  20/- kati ya hizo sh. milioni  15 zikiwa ni zake na milioni 5/- ni za Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Bw. George Simbachawene.  Pia alikabidhi seti 251 za mashuka zenye thamani ya sh. milioni 4/- zikiwa ni mchango kutoka Benki ya CRDB.

Waziri Lukuvi ambaye alishatoa mabati 250, aliahidi kuongeza mabati mengine 250 (yote yana thamani ya sh. milioni 8), pia alikabidhi sh. milioni 1.5/- kwa diwani wa Mlenge ili ziwasaidie kukodi gari la kukarabati barabara yao ambayo imeharibika sana kutokana na mafuriko hayo. 
 
Mapema, akitoa taarifa ya maafa kwa Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Amina Masenza alisema jumla ya kaya 82 zilikosa makazi kutokana na mvua zilizonyesha Februari 12 na kusababisha mafuriko. Kabla ya hapo, kaya nyingine 75 zenye wakazi 377ziliathirika kutokana na mvua zilizoanza Februari 3, mwaka huu. 
 
Alisema miundombinu ya barabara na ya maji safi iliharibiwa vibaya na kusababisha hasara ya zaidi ya sh, milioni 250/-. Pia wakazi hao walikumbwa na ugonjwa wa kipindupindu kutokana na mto Mapogoro kufurika na kusomba baadhi ya vyoo vya wakazi hao. 
 
“Tangu Februari mosi, wamekwishapokea wagonjwa wa kipindupinda 351 lakini walioko wodini hivi sasa ni wagonjwa 25 tu,“ alisema Mkuu huyo wa mkoa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, FEBRUARI 22, 2016.
Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa akiwapa pole wanawake na watoto wakati alipotembelea makazi ya dharura  waliyojengewa na serikali katika kijiji cha Kasanga  wanapohifadhiwa waathirika wa mafuriko yaliyozikumba tarafa za Pawaga na Idodi , Iringa Februari 22, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akipokea taarifa ya msaada  kutoka kwa meneja uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mangele katika mkutano wa kuwapa pole wananchi wa tarafa za Pawaga na Idodi uliohutubiwa na Waziri Mkuu katika Kijiji cha Kasanga, Iringa Februari 22, 2016. Mfuko huo umetoa mabati 200 na saruji mifuko 200 vyote vikiwa na thamani ya sh. 6,600,000/=.
Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa akiwapa pole kinamama na watoto wakati alipotembelea makazi ya dharura  waliyojengewa na serikali katika kijiji cha Kasanga  wanapohifadhiwa waathirika wa mafuriko yaliyozikumba tarafa za Pawaga na Idodi , Iringa Februari 22, 2016.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya Februari 23

Wizara Ya Fedha Yasema Makusanyo Ya Fedha Kwa Mwezi Yamefika Trilioni 1.79........Mchanguo Wote Wa Matumizi wa Pesa Uko Hapa

$
0
0
SERIKALI imeendelea kupaa katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya hadi Sh trilioni 1.79, ambazo imezipeleka katika huduma za jamii, ikiwamo elimu, maji, miundombinu na miradi ya maendeleo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile alisema hayo jana wakati akitoa taarifa ya hali ya mapato kwa kipindi cha Februari mwaka huu. 

Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata alisema makusanyo yameongeza kutoka Sh trilioni 1.2 Desemba hadi Sh trilioni 1.79 Januari.

Kabla ya Oktoba mwaka jana, makusanyo hayo hayakuzidi Sh bilioni 900 kwa mwezi.

Dk Likwelile alitaja maeneo ambayo fedha hizo zimeelekezwa ni kwa Mamlaka ya Elimu (TEA) iliyopewa Sh bilioni 23.078; Sh bilioni 18.7 zinatekeleza utoaji wa elimu bure kwa wanafunzi wa shule za awali, msingi hadi kidato cha nne kwa ajili ya ada, chakula na ruzuku.

Aidha, Sh bilioni 13 zimeelekezwa kwenye mikopo ya elimu ya juu na Sh bilioni moja zitatumika kujengea uwezo walimu walio masomoni na wakufunzi wao. 

Pia Sh bilioni mbili zimeelekezwa kupanua udahili katika mkoa wa Dar es Salaam kama Rais John Magufuli alivyoahidi katika mkutano wake na wazee wa mkoa huo.

Dk Likwelile alitaja maeneo mengine yaliyonufaika na fedha hizo na shilingi kwenye mabano ni Mpango wa Maji Vijijini (bilioni 17.1), maendeleo ya ujenzi wa barabara (bilioni 58.8), miradi ya umeme vijijini (bilioni 20.2), reli (bilioni 2.034) Serikali za Mitaa (bilioni 4.5), na Mahakama zimepatiwa Sh bilioni 12.3.

Aidha, Dk Likwelile alisema ili kuwajengea uwezo walimu walio masomoni na wakufunzi wao, Wizara imetoa Sh bilioni 1.65 kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.

Kati ya fedha hizo, wakufunzi wamepatiwa Sh milioni 431.6, walimu walio masomoni wametengewa Sh milioni 249.2 kwa ajili ya vifaa vya kufundishia, posho na nauli.

Alisema kuwa fedha nyingine kati ya hizo, kiasi cha Sh bilioni 573.7 zimetolewa kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa umma na ulipaji wa deni la taifa kwa mwezi huu zimetolewa Sh bilioni 842.1 na mifuko ya hifadhi za jamii Sh bilioni 81.13.

Aidha kiasi kilichotolewa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ni Sh bilioni 166.2 huku Chuo kipya cha Sayansi ya Tiba kilicho katika hatua ya ujenzi cha Mloganzila huko Kibamba, nje ya Jiji la Dar es Salaam, kimepatiwa Sh bilioni 18 .
Kaimu kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Alfayo Kidata akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Tarishi Kibenga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata akifafanua kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam jinsi Mamlaka hiyo ilivyofanikiwa kukusanya mapato kutoka trilioni 1.2 kwa mwezi Disemba mpaka trilioni 1 na bilioni 79 kwa mwezi Januari

Serikali Yapanga Bei Elekezi Kwa Hospitali Binafsi Ili Kupunguza Mzigo wa Gharama

$
0
0

SERIKALI imesema itatoa bei elekezi katika sekta ya afya hivi karibuni baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kubariki bei hizo kuanza kutumika kwa lengo la kuwapunguzia mzigo wa gharama wananchi.

Bei elekezi kwa vituo vya afya zimeshasainiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na baadhi ya vituo vya afya vimeshaanza kutumia bei hiyo.

Aidha, serikali imepanga kuweka utaratibu wa wagonjwa kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ikiwa ni hatua ya kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali hiyo.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Hamis Kigwangalla wakati akizungumza na waaandishi wa habari baada ya kuzindua Matokeo ya Utafiti wa Kutathimini utoaji wa huduma za afya nchini kwa mwaka 2014/2015.

“Bei elekezi ziko mbioni kutoka na baadhi ya vituo wameshaanza kuzitumia kwa sababu zimeshasainiwa na Waziri, sasa hivi tunasubiri Baraka za Waziri Mkuu akiziridhia tutazitangaza rasmi,” alisema Dk Kigwangalla.

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania Afikishwa Mahakamani Kwa Matumizi Mabaya Ya Ofisi

$
0
0

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) Mkoa wa Dar es Salaam, Lawrence Mwalumwelo na wenzake wawili wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka ya matumizi mabaya ya madaraka.

Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Sophia Nyanda akishirikiana na Veronica Chimwanda mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage aliwataja washtakiwa wengine kuwa ni Ofisa Tawala, Modester Fumbuka na Ofisa Manunuzi, Radecunda Massawe, wafanyakazi wa TPC.

Chimwanda alidai kuwa kati ya Agosti Mosi na Oktoba 31, 2010 washtakiwa hao walitumia vibaya madaraka yao kwa kuipa mkataba wa kutafuta vibarua kampuni ya Technical Merchantile Service bila kupata kibali kutoka bodi ya zabuni.

Vilevile ilidaiwa kuwa Septemba 26 ,2011 washtakiwa hao walitumia vibaya madaraka yao kwa kuiongezea kampuni hiyo mkataba wa kutafuta vibarua kutoka Septemba 30 hadi Desemba 31, 2011 bila ya kuishirikisha bodi hiyo.

Ilidaiwa kuwa Januari Mosi, 2012 washtakiwa hao waliiongezea tena kampuni hiyo mkataba wa kutafuta vibarua kutoka Januari Mosi, 2012 hadi Machi 30, 2014 bila ya kuishirikisha bodi hiyo. Washtakiwa hao walikana mashtaka.

Washtakiwa hao waliachiwa baada ya kutumiza masharti ya dhamana na kesi hiyo kuahirishwa hadi Machi 17.

CCM Watuma Salamu za Pongezi Kwa Yoweri Museveni Kwa Ushindi wa Kiti cha Urais Uganda

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimepongeza Chama cha National Resistance Movement (NRM) cha nchini Uganda kwa ushindi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Februari 18.

Kutokana na ushindi huo  CCM inampongeza Rais mteule, Yoweri Museveni ambaye ndiye mwenyekiti wa NRM.

Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma wa CCM, Daniel Chongolo imeeleza kuwa wamefuatilia kwa ukaribu mchakato wa uchaguzi huo na walikuwa na imani kwamba NRM itaibuka mshindi dhidi ya waliokuwa wagombea wengine saba wa urais. 
===== 


Mwanamkakati wa Maalim Seif Aswekwa Ndani Na Jeshi La Polisi Zanzibar

$
0
0
Mwanamkakati  wa aliyekuwa mgombea urais wa Zanzibar, Mohamed Sultan Mugheiry, maarufu kwa jina la Eddy Riyami, amewekwa ndani na Jeshi la Polisi mjini Unguja kwa tuhuma za kumtukana Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

Eddy Riyami ambaye ni mmoja wa wana mkakati wa timu ya ushindi wa aliyekuwa mgombea urais wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alikutwa na mkasa huo jana baada ya kuitwa polisi kutoa maelezo kutokana na tuhuma zinazomkabili.

Riyami ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar, alikwenda Polisi Makao Makuu kuitikia wito wa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, SSP Simon Pasua, huku akiandamana na Mwanasheria wa CUF, Masoud Faki Masoud.

Mwanasheria huyo jana alisema Riyami anatuhumiwa kwa kosa la matumizi mabaya ya kimtandao.

Alisema licha ya kuzikana tuhuma hizo, lakini Jeshi la Polisi bado lilimshikilia kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Ni kweli ameshikiliwa na polisi kwa ajili ya kupitisha uchunguzi na yupo Polisi Madema, eti Eddy kaambiwa kamtukana Dr. Shein kwenye ‘audio’ ambayo hata si sauti yake, lakini dhamana ipo wazi na tutamchukulia dhamana,” alisema Masoud.

Akizungumzia kukamatwa kwa Riyami, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai, Salum Msangi, alithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Kitu ninachoweza kuthibitisha ni kuwa tunamshikilia Riyami kwa ajili ya kupitisha uchunguzi,” alisema Naibu Kamishna Msangi.
 
Februari 15, mwaka huu Ofisi ya Mkurunzi na Makosa ya Jinai, ilimwandikia Riyami barua ya wito na kumtaka kufika ofisi ya upelelezi iliyopo Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

Riyami alitii wito huo ambapo wiki iliyopita alikwenda lakini mmoja wa maofisa wa Jeshi la Polisi aliyemwandikia barua alikuwa nje ya Zanzibar kwa shughuli za kikazi na kumtaka kwenda jana jumatatu

Riyami si mwanachama wa CUF, lakini mara kadhaa amekuwa akitumiwa na chama hicho kwa ajili ya mikakati mbalimbali pamoja na ushauri.

Lipumba Amtaka Rais Magufuli Atangaze Mshahara Na Marupurupu Yake

$
0
0

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amemtaka Rais John Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake, kwa kuwa amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge.

Profesa Lipumba amelieleza gazeti la Mwananchi kuwa Rais Magufuli amejipambanua kuwa kiongozi anayeguswa na matatizo ya wanyonge, hapendi makuu, anahimiza ukusanyaji wa mapato ya Serikali na matumizi mazuri ya fedha za umma, lakini watanzania hawajui mshahara wake ni kiasi gani

Profesa huyo aliyejikita katika masuala ya uchumi, alirejea mijadala mbalimbali iliyowahi kuibuliwa kuhusu mshahara wa Rais, ikiwamo ule uliyowahi kuibuliwa mwaka 2013 na Zitto Kabwe, wakati huo akiwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema kuwa Rais analipwa Sh32 milioni kwa mwezi.

Pia alirejea taarifa iliyochapishwa na Mwananchi, Julai 27, 2015, iliyoandikwa kutoka katika mtandao wa African Review kuwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete ni wa nne miongoni mwa marais wa Afrika kwa kupata mshahara mkubwa wa dola za Marekani 192,000 kwa mwaka sawa na dola 16,000 kwa mwezi, ambayo ni sawa na Sh32 milioni kwa mwezi. Hadi jana jioni, dola moja ya Marekani ilikuwa sawa na Sh2,187.

“Taarifa ya Ikulu ilikanusha vikali habari zilizochapishwa na Mwananchi. Ikulu ilieleza kuwa habari hizo siyo za kweli. Hata hivyo, haikueleza mshahara wa Rais na marupurupu yake ni kiasi gani?

Pia, katika mjadala wa mshahara wa Rais, Naibu Spika wa Bunge lililopita ambaye ndiye Spika wa sasa, Job Ndugai alinukuliwa akieleza kuwa mshahara wa mtu ni siri yake.

Waziri wa Nchi Katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma wa wakati huo, Celina Kombani (kwa sasa ni marehemu) alisema kuwa ni kosa kutangaza mshahara wa Rais.

“…Kwa hivi sasa Rais Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake na kama mapato yake ni Sh32 milioni kwa mwezi, basi ajitolee alau nusu ya mapato hayo kuchangia elimu na afya ya wanyonge. Hatua hii itaimarisha taswira inayojengeka barani Afrika kuwa yeye ni Rais wa wanyonge,” amesema  Lipumba.

Wakati akizungumza na wazee wa Dar es Salaam wiki iliyopita, Rais Magufuli aliwataka mawaziri, naibu mawaziri na makatibu wakuu wachangie Sh1 milioni katika mishahara yao kuchangia elimu.

Pia Rais alieleza kuwa yeye mwenyewe, makamu wake na waziri mkuu watachangia Sh6 milioni kila mmoja, ili zifike Sh100 milioni kusaidia changamoto za elimu bure Mkoa wa Dar es Salaam.

Kutokana na tangazo hilo, Profesa Lipumba alisema, “Ikiwa Sh6 milioni zitakatwa katika mshahara wake wa mwezi mmoja ni wazi mshahara wake na ule wa makamu wake na waziri mkuu ni zaidi ya Sh6 milioni kwa mwezi.

“Mishahara na marupurupu ya viongozi wa Tanzania hayako wazi. Watanzania hawajui kila mwezi Rais, Makamu wa Rais na viongozi wakuu wa Serikali wanalipwa kiasi gani? Malipo ya wabunge pia hayako wazi?” alihoji.

Profesa Lipumba ambaye amewahi kuwa msaidizi wa Rais katika masuala ya uchumi kati ya mwaka 1991 na 1993, alisema kwa kuwa Rais Magufuli amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge, anawajibika kuwaeleza Watanzania mshahara na marupurupu yake.

“Ikiwa mshahara ni mkubwa sana achukue hatua za kuupunguza kama alivyofanya Mwalimu Nyerere mwaka 1965.”

Hata hivyo, alisema kifungu cha Katiba cha 43 (2) kinaeleza kuwa mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais havitapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba.

Profesa Lipumba alisema Rais Magufuli akitaka kupunguza mshahara wake itabidi kwanza abadilishe kifungu hicho cha Katiba.

“Anaweza kujitolea mchango wa kudumu utakaokatwa kutoka kwenye mshahara wake kusaidia sekta ya afya au elimu,”alisema.

Profesa Lipumba ambaye ni mshauri wa Benki ya Dunia (WB) na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika masuala ya uchumi, alisema ili kuimarisha utawala bora ni muhimu uongozi ulio madarakani utumie mamlaka waliopewa kwa manufaa ya Taifa.

“Mishahara na marupurupu ya viongozi yawe wazi na yaamuliwe na kupangwa na taasisi iliyo huru. Kuweka utaratibu ulio wazi wa kuamua mishahara na marupurupu ya viongozi wa umma wakiwamo Rais na makamu wake, mawaziri, wabunge, majaji, makatibu wakuu na viongozi wengine,”alisema.

Alisema ni muhimu katika ujenzi wa utawala bora, uwajibikaji na uwazi wa viongozi wa umma kwa wananchi wanao waongoza.

“ Inasemekana mshahara wa mbunge katika Bunge lililopita ulikuwa Sh3.4 milioni kila mwezi.Pia mbunge alilipwa Sh8.2 milioni, nyingine kama posho ya jimbo, gharama za ofisi, mafuta, malipo ya wasaidizi wake na dereva.

“Vile Vile, mbunge anapohudhuria kikao cha Bunge alilipwa posho ya Sh80,000 za kujikimu, Sh50,000 za mafuta ya gari na Sh200,00 za kuhudhuria kikao cha Bunge, jumla ni Sh330,000 kwa siku.

“Posho ya siku moja ya mbunge ni zaidi ya mara mbili ya kima cha chini cha mshahara wa Serikali kwa mwezi mzima ambacho ni Sh150,000. Mishahara inakatwa kodi, marupurupu hayakatwi kodi,”alisema.

Magufuli Atinga GHAFLA Kivukoni na Magari yenye Namba za Kawaida

$
0
0

Rais John Magufuli ameendelea kufanya ziara za kushtukiza, baada ya kutembelea ofisi za Kivukoni Dar es Salaam kimyakimya juzi jioni kuangalia mwenendo wa utoaji huduma za vivuko.

Mashuhuda waliokuwepo eneo hilo Jumapili jioni wakati Rais anafanya ziara hiyo, walieleza mtindo alioingia nao Dk Magufuli ulikuwa ni wa kawaida na vigumu kwa mwananchi wa kawaida kung’amu uwapo wa Rais.

Mfanyabiashara wa eneo hilo, Sharif Mkamba alisema Rais Magufuli aliingia saa 11 jioni akiwa na msafara wa magari matatu ya kawaida yaliyokuwa na namba za kiraia.

“Hakukuwa na king’ora chochote kama tulivyozoea bali ulikuwa ni msafara wa kimya kimya. Aliingia moja kwa moja kwenye zile ofisi na alitumia kati ya dakika 10 hadi 15 kabla ya kutoka,” alisema Mkamba.

Said Likoko alisema kuwa baada ya kugundua kati ya magari matatu alikuwepo Rais, walisogea kufuatilia kwa kina kwa kuwa haijazoeleka na walitegemea huenda baadhi ya watumishi wangewajibishwa.

“Aliteremka na kumuuliza aliyemkusudia na taarifa tulizozipata jana zinadai hakumkuta huyo bosi, sijui ni meneja au ofisa sisi hatujui,” alisema Likoko ambaye hujishughulisha pia na biashara ndogondogo eneo la kivukoni.

Likoko alisema pamoja na kwamba aliingia kimya kimya, Rais Magufuli hakusita kuwasalimia wasafiri waliokuwa wakisubiri kivuko wakati alipofanya ziara hiyo.

Alieleza kuwa kama wananchi walifurahishwa na hatua hiyo ya Rais, kwa kuwa watendaji wengi hawafanyi kazi siku za wikiendi licha ya huduma zake kufanyika siku zote.

Tangu jana asubuhi kumekuwa na video inayosambaa ikimuonyesha Rais Magufuli akiwa Kivukoni akitembea kwa miguu ndani ya eneo hilo huku akishangiliwa na wasafiri waliokuwa wakingoja kivuko.

Hata hivyo, jitihada za kutafuta mamlaka husika kueleza kwa undani malengo ya ziara hiyo ziligonga mwamba baada ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue kutopokea simu.

Ofisa habari wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) Theresia Mwami, alitaka utafutwe uongozi wa juu kueleza yaliyojiri kwenye ziara hiyo kwa kuwa yeye yupo likizo.

Rais Mugabe Atimiza miaka 92.....Wasaidizi wake Wasema Atawania Tena Urais Mwaka 2018

$
0
0

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametimiza umri wa miaka 92 huku chama chake kikisema atawania tena urais 2018.

Mnadhimu wake mkuu alisema kiongozi huyo ambaye ameongoza nchi tangu mwaka 1980, bado ana uwezo kamili wa kuongoza Serikali licha ya tetesi kwamba hawezi kuongoza kutokana na umri.

Akizungumza na gazeti la Serikali Sunday Mail, Katibu Mkuu wa Rais Misheck Sibanda alisema tetesi hizo si za kweli na hazina msingi kwani Mugabe ana ratiba ya wiki nzima kutekeleza kazi za Serikali na chama.

Rais Mugabe ambaye aliapa kuongoza nchi hadi atakapokufa, alishinda kipindi kingine cha urais cha miaka mitano kwenye uchaguzi wa mwaka 2013 uliofanyika chini ya katiba mpya inayoweka ukomo wa kuongoza kwa vipindi viwili tu vya miaka mitano.

Chama chake tayari kimetangaza kumpitisha Mugabe kama mgombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2018.

Mugabe amekua kiongozi wa Zimbabwe tangu 1980. Ni mwenyekiti wa chama tawala cha Zanu. 1980 alikuwa waziri mkuu na 1987 Rais wa Zimbabwe.

Utawala wa Mugabe umeitwa wa kidikteta tangu mwaka 2002 kutokana na  kudharau haki za binadamu nchi Zimbabwe.

Uingereza Yammwagia Sifa Rais Magufuli Kwa Kasi Yake Ya Kukusanya Mapato na Kupambana Na Wala Rushwa

$
0
0

Nchi ya Uingereza imempongeza Rais John Magufuli kwa utendaji wa serikali yake hususani katika kupambana na ubadhirifu wa mali za umma na ufisadi, kwa siku chache alizokaa madarakani.

Sifa hizo za Uingereza zimewasilishwa jana Ikulu jijini Dar es Salaam na Balozi wa nchi hiyo,, Balozi Dianna Melrose.

Balozi Melrose alieleza kuwa nchi yake imeridhishwa na juhudu za Rais Magufuli katika kulinda fedha za umma na kuahidi kushirikiana naye hususan katika kuimarisha idara ya Mahakama na Intelijensia nchini.

“Tunadhani ameonesha msimamo mkali dhidi ya rushwa na ufisadi, na miongoni mwa mambo ambayo tumezungumza ni namna ya kufanya kazi pamoja katika kupambana na rushwa. Tuna mazungumzo katika kuimarisha mifumo ya kiintelijensia na mahakama,” alisema Balozi Melrose.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alikutana na rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete Ikulu lakini mazumgumzo kati yao hayakuwekwa wazi.

TRA Yatoa Tamko ya Kuhusu Matumizi ya EFD Kwenye vituo vya Mafuta.

$
0
0

TANGAZO KWA UMMA
MATUMIZI YA MASHINE ZA EFD KATIKA VITUO VYOTE VYA MAFUTA NCHINI:

Kufuatia Tangazo kwa Umma lilitolewa kwenye vyombo vya Habari na kuchapishwa kwenye Magazeti, Uongozi wa Chama cha Wamiliki na Waendeshaji wa Vituo vya Mafuta Nchini (TAPSOA) ulikutana na Kaimu Kamishna Mkuu na kufanya majadiliano ya msingi kuhusu matumizi ya EFD na kufunga Mashine za EFD Maalum katika vituo vya mafuta kwa ajili ya kutolea risiti za mauzo. Makubaliano ya pamoja kutokana na majadiliano ni kwamba, agizo la Kaimu Kamishna Mkuu liendelee kutekelezwa katika utaratibu ufuatao;
  1.  Wamiliki wote wenye vituo vya mafuta walio katika kundi la Makampuni makubwa wanaoagiza mafuta na kutumia Mawakala kusambaza/kuuza mafuta kwa wateja (CODO) wakamilishe kufunga Mashine za EFD katika vituo vyao vyote Nchini kama ilivyokubalika katika kikao hicho (yaani kufikia tarehe 15 Machi 2016).
  2.  Wamiliki wote wenye vituo vya mafuta walio katika kundi la Makampuni wanaoagiza mafuta na kusambaza/ kuuza mafuta kwa wateja wao wenyewe (COCO) walioanza na wanaofunga Mashine za EFD kwenye pampu za vituo vyao waendelee kufanya hivyo wakati Mamlaka ya Mapato kwa kushirikiana na Wasambazaji na Uongozi wa TAPSOA wakiendelea kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazojitokeza za kiufundi na gharama ya Mashine za EFD kwa ajili ya pampu husika.
  3. Wamiliki/Waendeshaji wote wenye vituo vya mafuta walio katika kundi la Makampuni ya watu binafsi wanaonunua mafuta kutoka kwa Makampuni mama na kusambaza/kuuza kwa wateja moja kwa moja (DODO) ambao hawajafunga Mashine za EFD kwenye pampu waendelee kutumia Mashine za EFD za kawaida (ETR) wakati changamoto za kiufundi, mtandao na bei za Mashine za EFD zikishughulikiwa.
Mamlaka ya Mapato kwa kushirikiana na uongozi wa TAPSOA kwa pamoja tutaendelea kuhimiza Matumizi ya Mashine za EFD katika vituo vya mafuta vyote Nchini.

Ni vyema kila Mfanyabiashara akatambua wajibu wake na kujenga utamaduni wa kutekeleza matakwa ya sheria kwa hiari bila kushurutishwa.

Pamoja Tunajenga Taifa Letu
KAIMU KAMISHNA MKUU

Waziri Kitwanga Aagiza Mabadiliko Makubwa Idara Ya Uhamiaji

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga ameagiza yafanywe mabadiliko makubwa katika Vitengo mbalimbali vya Idara ya Uhamiaji ili kuboresha huduma na kuimarisha uadilifu katika Vitengo hivyo.
 
Mheshimiwa Kitwanga ametoa maagizo hayo leo wakati alipofanya kikao na Viongozi wa Idara ya Uhamiaji ambapo pia kilihudhuriwa na Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakiwemo Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara.  Kikao hicho kilifanyika katika Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Katika kikao hicho, Mheshimiwa Kitwanga ameagiza watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji walioko Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, wahamishwe na kupelekwa maeneo mengine nchini, wakiwemo wale wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
 
Wengine watakaohamishwa ni kutoka Kitengo cha Pasipoti, Uhasibu, Hati za Ukaazi na Kitengo cha Upelelezi, vyote vya Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.

Aidha ameagiza pia kuwa Wakuu wote wa Vitengo vya Upelelezi vya wilaya zilizopo jijini Dar es Salaam, na pia wale wa Vituo vya Tunduma, Mtukula, Holili na Kasumulo, wahamishiwe maeneo mengine, na pia watumishi wote waliokaa kwa zaidi ya miaka mitatu katika Vituo hivyo.

Amesema hatua hii inayochukuliwa sasa  ni mwanzo tu wa mabadiliko makubwa yatakayofanywa katika Idara ya Uhamiaji ili kuboresha huduma zinazotolewa na Idara hii ambayo ni moja ya Idara muhimu za Serikali.
 
Amesema katika kuisafisha Idara hii, uangalifu mkubwa utachukuliwa ili kuhakikisha kuwa hakuna mtumishi anayeonewa wala kupendelewa, lakini lengo kubwa ni kuvunja mtandao wa wapokea rushwa na wale wasiowajibika.

Amesema kufuatana na utafiti uliofanywa hivi karibuni umeonyesha kuwa matatizo ya rushwa katika Idara ya Uhamiaji yanashika nafasi ya kwanza kwa kuwa na asilimia 30, asilimia 20 ni uongozi mbovu na asilimia 20 ni matumizi mabaya ya madaraka. Asilimia 15 inahusisha vitendea kazi wa mifumo hafifu ya kufanya kazi, asilimia 10 huduma mbovu na asilimia 5 ukabila na upendeleo.

Amewataka Viongozi na watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya kazi na waepuke vitendo vya kupokea rushwa na kusaidia wahamiaji haramu na wauza madawa ya kulevya.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
23 Februari, 2016

Makala : Fahamu Kuhusu Ndumba Za Kichawi Na Jinsi Ya Kujikinga Nazo.

$
0
0
FAHAMU  KUHUSU  NDUMBA  ZA KICHAWI NA  JINSI  YA  KUJIKINGA  NAZO.

Mwandishi : Dokta. Mungwa  Kabili….0744 000 473

Nimekuwa  nikipokea  barua  pepe  kutoka  kwa  watu  mbalimbali, wakitaka  kujua  masuala  mbalimbali  kuhusu  ulozi, uchawi  na  jinsi  ya  kujikinga  dhidi  ya  uchawi  na  ulozi.

Kwa  kuwa  muda  na  nafasi  haviniruhusu  kumjibu  kila  mmoja  kwa  wakati  wake,  nitayajibu  maswali  yote  hapa  bloguni.

SWALI :   NIMESIKIA  KUWA  WACHAWI  HUWA  HAWAFI  UPESI.JE  KUNA  UKWELI  WOWOTE  KATIKA  HILO ?  NA  KAMA  NI  UKWELI, JE  NI  KITU  GANI HUWAPA  UWEZO  WA  KUISHI  MAISHA  MAREFU ?

DOKTA.  MUNGWA  KABILI  ANAJIBU :
Ni  kweli  kabisa  wachawi  wengi  huwa  hawafi  upesi  na  zipo  sababu  kuu  mbili  zinazo  wafanya  wachawi  waishi  muda  mrefu :

1.Kwanza  : NDUMBA  ZA  KINGA: Wachawi  wa  nchi  hutumia  ndumba  za  kinga, ndumba  hizo  husaidia  kuwakinga  dhidi  ya  shari  za  wanadamu   na  majini  wabaya na  hivyo kuwafanya  waishi  siko zote  walizo  pangiwa na  Mwenyezi  Mungu. Ikitokea  mchawi mwenye  kinga  hizo, amefariki  dunia, basi   anakuwa amefariki  kwa mkono  wa  Mungu mwenyewe  na  si mwanadamu. Watu  wengi  hufa  kwa mikono ya  wanadamu  waovu  na shari za  mapepo  wabaya.  Nitataja  ndumba  mbili  zenye nguvu  zinazo  tumiwa  na  wachawi.

i.  Kuna  ndumba   moja  ya  kichawi, ambayo  kwa  lugha  za  kisukuma  na  kinyamwezi  hujulikana  kama  LUFAKALE.

Ndumba hii  ya  kichawi   akichanjiwa  mtu  humkinga  dhidi  ya  shari za  wanadamu  na  mapepo  wabaya. Humfanya  aishi  kwa  kadri  Mungu  alivyop  mkadiria. Humkinga  na kumuepusha  na  shari  kama  ajali (hususani ajali za  kichawi ), kufa  kwa  kurogwa  nakadhalika.

Ndumba  hii  ina  nguvu  sana  kiasi  kwamba, mtu  aliye  chanjiwa , inapofika  siku yake  ya  kufa  roho yake  huchukua  muda  mrefu  sana  kuacha  mwili  wake. Inaweza  kumchukua mwaka  mmoja  hadi  miaka  kumi. Mtu  anakuwa anonyesha  dalili zote  za  kufa, au anakuwa  ameisha  kufa  kabisa, lakini  anakuwa  bado  anaongea.  Nikipata  nafasi  siku zijazo nitaelezea  kwa  kina  kuhusu   ndumba  hii.

ii. Ndumba  ya  pili, inatokana  na  mti  unaitwa  Msonihya . Huu ndio  mti mkuu  wa  wachawi. Mtu  huu  una  nguvu  sana  za  kichawi.  Mti  huu  hutumika kutengeneza  hirizi  ambayo  huvaliwa  mkononi  kama  bangili  au  kuwekwa nyumbani. Hakuna  pepo, jinni wala  kitu  chochote  kile  kibaya  kinaweza  kumdhuru mtu aliye  pewa  hirizi  hii.

Simba , nyoka  wa  kawaida  pamoja  na  samba  & nyoka  wa  kichawi au  mnyama  yoyote  yule  hawezi  kumdhuru.

2. NDUMBA  ZA  KUWAWEZESHA  KUONA  MAMBO  YATAKAYO  TOKEA   MBELENI.

Wachawi wa  nchi  wanazo  ndumba  zenye  uwezo  wa  kuwasaidia  kujua  mambo  yatakayo  tokea   mbeleni, hivyo basi  kama  kuna  hatari  yoyote  ile  inaenda  kutokea  kesho yake kama  vile  ajali  au  shari  yoyote  ile nakadhalika, wao  wanakuwa  wameshajua  siku  moja  kabla  na  hivyo  wanakuwa  na  nafasi ya  kuchukua  tahadhari mapema.

JINSI  WANAVYO  FANYA  ILI  KUWA  NA  UWEZO  WA  KUONA  MAMBO  YATAKAYO  TOKEA.

Zipo  njia  mbalimbali  wanazo  tumia, ili  kupata  uwezo  wa  kuona  mambo  yatakayo  tokea  mbeleni, lakini  kati  ya  njia  hizo  njia  ifuatayo  ni  maarufu sana  miongoni mwa  wachawi na  walozi.

i. Wanachukua  ubongo  wa  fisi

ii.  Wanachukua  ubongo  wa  kunguru

iii. Wanachukua  ubongo  wa  ndege  anaitwa  Mbesi. Ndege huyu  hupatikana  mtoni  na  chakula  chake  kikuu  ni  mizoga ya  ndege, wadudu, samaki na  wanyama. Katika ulimwengu  wa wachawi, ndege  huyu  hujulikana  kama  mtaalamu  wa  kugundua  mahali  ilipo mizogo  iliyo  kufa.

Kwa  mfano   tuchukulie  mkoa wote  wa  Dar  Es  Salaam  ni  pori,  huyu  ndege  yupo  mbagala halafu  maeneo  ya  msasani  kuna  ndege,samaki,wadudu  au mnyama  amekufa, basi  usiku wa  siku  hiyo  ndege  huyu  ataota  mahali  ulipo mzoga  huo, na  kesho  yake  atapaa  moja  kwa  moja hadi  sehemu  ulipo mzoga  huo  na  kuufanya  kuwa  kitoweo  chake.

Vitu  vyote  hivyo  hapo  juu  hukaushwa  na  kusagwa  kwa  pamoja  na  kisha  kuchanganywa  na  ndumba  tatu  za  kichawi  ambazo  sitazitaja hapa kwa  sababu  maalumu.

Baada  ya  hapo,  mchawi  husika  atachanjiwa  ndumba  hizo  kichwani pamoja  na  kwenye  zote  nne  za  mwili.

Basi, mchawi  huyo  anakuwa  na  uwezo  wa  kuona  ndotoni  kila  kitu  kitakacho  tokea kesho  yake  na  kuendelea.

SWALI NAMBA  MBILI :  NASIKIA  WATU  WANAZUNGUMZA  KUHUSU  DUDUMIZI. JE  DUDUMIZI  NI  NINI  NA ANATUMIKAJE  KATIKA  UCHAWI

DR. MUNGWA  KABILI  ANAJIBU ;
Dudumizi  ni ndege  anaye  patikana  porini. Katika  ukanda  wa  Pwani, ndege  hawa  wanapatikana  kwa wingi  sana  katika  mapori ya  Bagamoyo   mkoa wa  Pwani,  Kisarawe  vijijini  ( Hususani  katika vijiji  vya  Mwaneromango, Nzenga  na  Msanga ) pamoja  na  wilaya  ya  Pangani  mkoani  Tanga.

Ndege hawa  wana  macho mekundu, mkia  mrefu pamoja  na  kucha  ndefu  sana.

Dudumizi  hula wadudu, mijusi, nyoka, mayai,makinda, matunda, mizoga  na wanyama  wadogo pia.

Dudumizi  wengi  wana  mabawa yenye  rangi  ya  kahawia  nyekundu  na  kichwa  cheusi.  Lakini  pia  wapo Dudumizi  wenye  mkia  wa  rangi  ya  shaba, Dudumizi  weusi,Dudumizi wenye  koo  lenye  rangi nyeusi, Dudumizi  wenye  kichwa  chenye  rangi  ya  buluu, pamoja  na  Dudumizi wenye  nyushi nyeupe.

MAAJABU  YA  DUDUMIZI.
Dudumizi  ni ndege  mwenye maajabu mengi  sana, kwa  muwa  muda  hauturuhusu, leo nitataja  mawili  tu.

AJABU  LA  KWANZA :  Ana  uwezo  wa  kujifungua  kamba  mwenyewe. Kwa  mfano, ukienda  kwenye  kiota  cha  Dudumizi, halafu  ukawafunga  makinda  wa  Dudumizi kamba  kisha ukafunga  na  kwenye  mti. Kesho  yake  asubuhi  unakuta ile  kamba  imejifungua  yenyewe . Ukimnchukua  Dudumizi ukampeleka  nyumbani  kwako, ukamuweka  kwenye  banda, halafu ukamfunga  kamba  akiwa  bandani, ukafunga  banda halafu kamba  hiyo  ukaenda  kuifunga  kwenye  mti  au  kitu  chochote  kile, kesho  yake  unakuta Dudumizi  amefungua  hiyo kamba na  kuondoka, hata  kama  kamba  hiyo  itakuwa  kubwa  na  nzito  kwa  kiasi  gani.


AJABU  LA  PILI : Kwa  kawaida  Dudumizi  hutaga  mayai  kati  ya  mawili  hadi  matano. Dume  la  Dudumizi  ambalo  huwa  dogo  kwa  umbo  kuliko  jike, ndio  linalo  hatamia  mayai na  kutunza  makinda.

JINSI  WACHAWI  WANAVYO  MTUMIA  NDEGE  DUDUMIZI.

Katika  ulimwengu wa  wachawi, Dudumizi  ana  matumizi  mengi sana kichawi. Leo  nitataja  mawili tu  kwa  sababu  ya  muda.

1.Kamba  iliyo  tumika  kuwafunga  Dudumizi na  ikajifungua  yenyewe, ikichanganya  na  ndumba  za  kichawi  pmaoja na  vizimba  vyake, hutumika  kuwafungua  kichawi, watu  walio katika  vifungo  mbalimbali  vya kichawi  kama  vile  vifungo  katika biashara, vifungo  katika  mapenzi na  ndoa, vifungo  katika  rizki , vifungo  vya  mizimu,  nakadhalika.

2. Dudumizi  hutumika, kutengeneza  ndumba maalumu kwa  wale  wanawake  wanao penda  kuwa inamisha  waume  zao.

SWALI  NAMBA  TATU: JE  NI KWELI  KUWA  WACHAWI  WANA UWEZO WA KUMTIA  MTU  MIKOSI NA  KUFUNGA  RIZIKI  YAKE?

DOKTA.MUNGWA  KABILI  ANAJIBU ;
Ni kweli  kabisa,wachawi  wana  uwezo  wa  kumtia  mtu  mikosi . Zipo  njia  mbalimbali  wanazo  tumia  wachawi  katika  kuwatia  watu  mikosi, ila kutokana  na  ufinyu  wa  nafasi, nitaelezea  moja  hapa ;

Katika  njia  hii, wachawi  wakitaka  kumtia  mtu  mikosi, hufanya  mambo  yafuatayo :

i. Wanachukua  hela  ambayo  haitumiki

ii.  Mavi  ya  mbwa  mweusi ambayo  ameyanya  usiku

iii.Mkaa  ulio kwisha  tumika, ambao  umetumika  mahali  ambapo  watu  hawalali  kama vile  kilioni  au  kwenye  bara  na migawaha  inayo  kesha lakini  mara  nyingi, huchukua  mkaa  wa  kilioni.

iv. Mavi  ya  ndege  anaitwa  Mumbi. Huyu ndege  aitwae  Mumbi  anapatikana  porini. Anafanana  sana  na  bata  na  ana  puyanga  la rangi  nyekundu.

v.Shahidi la  kaburini  pamoja  na  ndumba  zingine  za  kichawi

vi.Kitu  chochote  cha  mtu  aliye  kusudiwa  kutiwa mikosi  kama  vile  picha  yake, mchanga  alipokanyagia, mate, kucha, au chochote  kile.

Baada  ya  hapo, mchawi  huyo  atakwenda  kaburini  usiku  wa  manane  na  kuvizika  vitu  vyote  nilivyo  vieleza  hapo  juu, huku  akisema  maneno  ya  kichawi ambayo  siwezi  kuyataja hapa. Basi  mtu  aliye  kusudiwa  na  uchawi  huu, kama  hana  kinga, ata andamwa  na  mikosi mikubwa  na  mizito  katika  maisha  yake  yote.

SWALI NAMBA  NNE  :  DOKTA, NINAPENDA  KUJUA  NINI  KINGA  DHIDI  YA  UCHAWI? NIFANYE  NINI  ILI  UCHAWI  USINIDHURU ?

DOKTA  MUNGWA  KABILI  ANAJIBU:
Kama  wewe  ni  Muislamu, uwe  mtu wa  swala  sana, kufanya  duwa na  visomo ( Ruqiya)  na  kutoa  Dhaka na swadaka  kwa  mola  wako, na  kama  wewe  ni  Mkristo, basi  uwe mtu  wa kusali  sana, kufunga  na  kuomba  bila  kusahau  kutoa  sadaka  na  fungu  la  kumi  kwa  Mungu  wako.

Lakini  kama  unajijua, hauwezi  kufanya  mambo  niliyo  yataja  hapo  juu, basi  unatakiwa  kupata  kinga  ya  mwili  wako.

Zipo  kinga  nyingi zenye  nguvu dhidi  ya  uchawi  na  ulozi. Zipo  Kinga, mchawi  akikutupia  uchawi  unamrudia  mwenyewe ana  kufa  papo hapo  au  anapooza  kwanza kwa muda mrefu  kisha  anakufa pia zipo kinga ambazo  mchawi ,  akitaka  kukutupia  uchawi, anashindwa  kukuona  katika rada zake  za  kichawi.

Hii  ni  kinga  muhimu  sana na haiishii  kukukinga  mwili wako  pekee.Inakinga nyumba, biashara, kiti  cha  ofisi  nakadhalika.

KINGA  HII  HUJULIKANA, KAMA  KINGA  YA  KUFICHA  KIVULI  CHAKO.

Inaitwa  Kinga  ya  Kuficha  kivuli, kwa  sababu  wachawi  wanapo taka  kumloga  mtu, huchukua  na  hushambulia  kivuli  chake. ( HAPA  SIZUNGUMZII  KIVULI  CHA  JUANI, NAZUNGUMZIA  KIVULI  CHAKO  CHA  KIROHO, YAANI  NAFSI YAKO )

Bila  kuona  kivuli  chako, wachawi  hawawezi  kukuloga.

Kinga  hii  hukupa  uwezo  wa  kutokuonekana  kwenye  rada  za  wachawi. Kwao  unakuwa  ni  sawa  na  mtu  aliye  kufa tu, kwa sababu  mtu  aliye  kufa kivuli  chake  hakionekani  na  pia hawezi  kurogwa  na  uchawi  wa  aina  yoyote  ile.

JINSI  YA  KUFICHA  KIVULI  CHAKO  KISIONEKANE  NA  WACHAWI.

i.  Chukua  nywele  za  saluni
ii. Chukua  mzizi  wa  mti  ulio  katisha  njia
iii. Chukua  tawi  la  mti  unaitwa  Ututukanga. Huu  mti  wa  Ututukanga  unapatikana  porini na  huwa  linaonekana  shina  lake  na  matawi  yake  tu, lakini  mzizi  wake huwa  hauonekani.

iv. Unachukua  mti   unaitwa  Msonihya

v.  Unasaga  pamoja  na  mti  unaitwa  mwavi.

vi. Baada  ya  hapo  unachukua  kuku  mweusi, unamfunga  kwenye kitambaa  cheusi  bila  kumchinja, unachukua  chungu  cheusi, unamuunguza  mpaka  anakuwa  mkaa, halafu  unamsaga  pamoja  na  miti  iliyo  tajwa  hapo  juu, unachanganya  na  mafuta  ya  simba.

vii. Unachukua  buja ama  dulya  la  ugali  wa  kilioni

viii. Kamba  ya  kitanda  alicho  lalia  maiti, au kama  maiti  ipo  kwenye  nyumba  ya  nyasi, unachomoa  nyasi  wakati  maiti  imo  ndani.

ix.  Unachimba  mzizi  wa  mti  unaitwa  mputika  bila  kivuli chako  kugusa mti..

x. Unaunguza  vyote  kwa  pamoja  ukiwa  na  kaniki  nyeusi  bila  kuvaa  nguo  yoyote  usiku wa  manane

xi. Unaipika  njia  panda pamoja na  mafuta  ya  mti  mmoja  wa  porini  ambao  jina  lake  linahifadhiwa  hapa.

Baada  ya  hapo, mtu  atachanjiwa  na  kuongeshwa pamoja  na  kufanyiwa  tambiko  maalumu.

Basi wachawi  watakuwa  wakijaribu  kutaka  kukutupia  uchawi, wanakuwa  hawakauoni  kwenye  rada  zao za  kichawi

SWALI NAMBA  TANO :  HABARI  YAKO DOKTA. NASUMBULIWA  SANA  NA  WIZI NYUMBANI  KWANGU. JE  IPO  NDUMBA YA  KUMKAMATA  MWIZI ?

DOKTA  MUNGWA  KABILI  ANAJIBU :
Zipo  ndumba  nyingi  za  kuwakamata  wizi. Leo  nitataja  ndumba  rahisi  kabisa  ya  kumkata  mwizi. Ukifanya  ndumba  hii, basi  mwizi  atajileta  mwenyewe  na  kuomba  msamaha.

i. Unachukua  kinyonga akiwa mzima

ii. Unaponda  majani ya  kisamvu

iii.Unachukua  na  changarawe  za  njiani  ambazo, hutembea  mvua  ikinyesha.

iv.                Huyo  kinyonga  unamuweka  kwenye  hayo majani  ya  kisamvu pamoja  na  hizo  changarawe, unafunga  kwenye  kitambaa  cheusi  halafu  unafunga  jikoni, kwenye sehemu  inayo  toka  moshi. Utamuacha  hapo  kwa muda  wa  siku  saba.

Baada  ya  siku  sita, unamtoa  hapo kwenye  moshi, unasaga  ukiwa  umefumba  macho  halafu  unaenda  kuvifunga  kwenye  mti  kwa  muda  wa  siku  saba. Kabla  siku  saba hazijaisha, mwizi  wako  atarudi  mwenyewe. Na  kama  mwizi  yumo  humo  humo  ndani, atajisalimisha  mwenyewe  mara  moja.

Hii  dawa  moja  tu, lakini  zipo  nyingine  nyingi.

SWALI NAMBA  SITA : DOKTA   NASIKIA  WACHAWI  WANA  UWEZO  WA  KUTUMIA  UCHAWI  KUMSHIKA  MWANAUME  KIMAPENZI . JE  NI  KWELI? NA  WANAFANYAJE  FANYAJE ?

DOKTA. MUNGWA  KABILI  ANAJIBU.
Katika masuala  ambayo  uchawi una  ishi na  kutawala  basi  ni  suala  la  mapenzi.

Asilimia  kubwa  ya  watu  wanao  enda  kwa  waganga, huenda  huko  kwa  sababu  ya  mapenzi  au  kwa  sababu  ya  mambo  yanayo  sababishwa  na  mapenzi.

Uchawi  wa  mapenzi  upo  wa  aina  nyingi  sana. Nikisema  nianze  kutaja na  kuelezea  kwa  kila  aina  ya  uchawi  na  ulozi  katika  mapenzi  hapa, sitamaliza  kwa  sababu  upo uchawi  wa  aina  nyingi  sana.

Nitataja na  kuelezea kwa  ufupi  sana, aina  chache  za  uchawi  katika  mapenzi, halafu  nitaelezea  aina  moja  ya  uchawi  wa  mapenzi  ambao  ni uchawi  hatari  na  wenye nguvu  sana.

KUMSHIKA  MWANAUME  KATIKA MAPENZI ;  Kumshika  mwanaume  katika mapenzi, wachawi  huchukua  njiwa  wawili  jike dume  walio zaliwa  kiota  kimoja pamoja  na  kiota  chawe, kisha  njiwa  hao huchinjwa , hupasuluwa  na  mioyo  yao  hunyofolewa, huchemshwa  kwenye  mafuta  ya  mti  mmoja  unapatikana  porini, halafu husagwa  hadi  kuwa  unga  unga. Baada  ya  hapo huchukua  njugu  mawe  nyeusi  moja, huchanganya  na  mti  unaitwa  mlama, pamoja  na  miti  mingine  mitatu  ya  porini, kisha   husagwa  pamoja  na ile  mizoga  ya  njiwa.

Vyote  hivi  kwa  pamoja, huchanganywa  na  vizimba  vitatu  vya  ndumba  za  kichawi, halafu  mwanaume  huwekewa  kwenye  chakula, basi mwanaume huyo atakuwa  hasemi chochote  kwa  mwanamke  huyo.Mwanamke atakuwa  mama  ake  atakuwa  baba  ake. Ni uchawi  mbaya  sana huu.

KUMFANYA  MWANAUME  ASIENDE  NJE  YA  NDOA :
Kumfanya  mwanaume  asiende  nje  ya  ndoa, wachawi  huchukua kamba  ya  mbuzi, moyo  wa  kondoo, mti unaitwa  INAMA  NIKUCHUME (  Mti  huu  unapatikana  Kigoma tu, na  watu  wa  kigoma  ndio  huuita  jina  hilo), mti  unaitwa Inyazya  kisha  vinasagwa  kwa  pamoja  halafu  vinachanganywa  na  nta ya  nyuki, kisha  wanatafuta  kucha, au nywele, au ndevu, au uzi wa nguo yake yoyote, halafu vinakaangwa  kwa  chumvi  ya  mawe  pamoja  na  vizimba  vya  zote  \nilizo zitaja  hapo juu, kisha vinafungwa  kwenye kitambaa chekundu, halafu  vinafukiwa  mlangoni  au  kwenye  mti  wowote. Basi mwanaume  huyu hawezi kwenda  nje  ya  ndoa  yake.

MWANAUME AKUONE  WEWE TU KILA ANAPOKUWA  NA  MWANAMKE MWINGINE : Wachawi  hutchukua   maji ambayo  mwanamke  ametumia  kunawa  uso wake kisha huchanganya  na  ndumba  13  za  kichawi  pamoja  na  vizimba  vyake kisha  kutengeneza  ndumba  itakayo  mfanya  mume  wa  mwanamke  huyo kuwa  anaumuona mke  wake  wakati  wote na pia  kuwa   anaona kama  anatokewa  na  mke  wake  kila  anapo  kuwa na  michepuko.

KUMFANYA  MUME  AKUPE  MSHAHARA  WAKE  WOTE  AU PESA  ZAKE ZOTE  KILA  AKIZIPATA: Uchawi  huu  umewalostisha  wanaume  wengi  sana. Hapa mchawi  anacho chukua  manii  za  mwanaume aliye  mkusudia, ana changanya  pamoja  na  baadhi  ya  vitu  alivyo pewa  na  mwanaume  huyo, halafu  vinaenda  kutengenezwa kichawi kwa  kutumia  ndumba  za  kichawi, basi mwanaume  huyo  atakuwa  kila  akipata  mshahara wake  anapeleka  zote  kwa  mwanamke  huyo. Asipojistukia  mapema, anaweza  uza  kila  kilicho  chake.

KUMVUTA  MPENZI :  Ipo miti  mitatu  inapatikana  porini, miti  hutumika  kumuita  kichawi  mwanamke  au  mwanaume  aliye  kusudiwa.

KUMTEGA  DAWA ZA  MAPENZI  MWANAMKE  AU  MWANAUME.
Chaurembo  kaenda  kwa  wachawi, na  kuwaomba  wampe  msaada  wa  kichawi  ili  aweze kumteka  kimapenzi Ndugu., Maridadi.

Wachawi  watamchukua  Chaurembo, watampa  ndumba  za  aina  tatu. Ndumba  ya  kwanza, atachanjiwa, kichwani  na katika  pembe  zote  za  mwili wake. Ndumba  ya  pili  atatumia kunywa, na  ndumba  ya  tatu  atatumia  kuoga  na  kuchoma.

Sikui  tatu  baada  ya kuanza  kutumia  ndumba  hizo, Chaurembo  atamuota  Maridadi anapita  katika  sehemu  ambayo  Chaurembo  anaifahamu.  Chaurembo atatakiwa  kuikariri  ndumba hiyo.

Kesho  yake, saa  saba  mchana, Chaurembo atatkiwa  kwenda  hadi  mahali  alipo  muona  Maridadi akiwa  anapita,akifika  katika  eneo  hilo, atatakiwa  kumwaga  dawa  aliyo pewa.

Maridadi  lazima  atapita  katika  eneo hilo, na  akipita  tu, basi  anakuwa  amenasa  kwenye  penzi la  Chaurembo.

Maridadi  atamtafuta  Chaurembo  kwa  udi  na  uvumba na  atafanya  kila  kitu  anacho kitaka  Chaurembo.

Huu  ni  uchawi  mbaya sana  na  hutumika  hata  katika  mambo  yasiyo  ya  mapenzi.

SIKU NYINGINE  NITAELEZEA  KWA  UREFU  SANA  KUHUSU  UCHAWI  MBALIMBALI  UNAO  TUMIKA  KATIKA  MAPENZI.

SWALI NAMBA  SABA : JE NI KWELI  WACHAWI WANA  UWEZO  WA  KUWAACHANISHA  WAPENZI  KWA  KUTUMIA  UCHAWI.
 
DOKTA  MUNGWA  KABILI  ANAJIBU :
Ni kweli kabisa, wachawi  wana  uwezo wa  kuwaachanisha  wapenzi. Mke na  mume  walio  ona  kwa  sherehe  ya  mamilioni  wanaweza  kuachana  ndani  ya  wiki  moja.

Zipo njia  nyingi sana  wanazo  tumia, ila  leo  nitaitaja  moja:

i.Wanachukua  mti  unaitwa  mpuga mbu.

ii. Mkia  wa  ndege  wa  porini  anaitwa  katyente

iii. Picha  ya  mke na mume  walio  kusudiwa pamoja  na  majina  yao.

iv. Wanachanganya  na  vizimba  vyake.

v. Vitu vyote  hivyo  vinasagwa  kwa  pamoja, kisha  vinakaangwa  kwa  kutumia  chumvi  ya  mawe, halafu vinaen da  kuchomwa  jalalani.

Hata  kama  wanapendana  vipi,wote  wataachana.

Ndumba  hii  ndio  inayo  tumika  pia  kushusha  thamani  ya  cheti  cha  mtu. Hata  kama  amesoma  vipi, hawezi  kupata  kazi  kama  akifanyiwa  uchawi  huu.

Kwa  leo  naomba  niishie  hapo, kesho  nitaendelea  tena  na  makala  haya.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA. MUNGWA KABILI, MTALAAMU  ALIYE  BOBEA  KATIKA  MASUALA  YA  ULIMWENGU USIO ONEKANA. ANAPATIKANA  JIJINI  DAR  ES  SALAAM, KWA  SIMU NAMBA 0744 000 473.


KWA  HABARI ZAIDI  KUHUSU  ULIMWENGU USIO ONEKANA, TEMBELEA  KILA  SIKU ;

Mkazi Wa Mafinga Aporwa Sh.milioni 12 Dar.

$
0
0

MKAZI wa Mafinga,  David Isack ( 32) alivamiwa na majambazi na kuporwa sh.milioni 12 ambazo alikuwa akipeleka katika Benki ya  DTB, ambapo alivamiwa na  watu  watano wanatuhumiwa kuwa ni majambazi wakiwa na usafiri wa pikipiki  mbili aina ya boxer.

Akizungumza na waandishi wa habari ijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro amesema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 12 mwaka huu katika eneo la Uwanja Ndege , katika kurupushani za kutaka kuchukua fedha hizo walitokea askari na kuwazingira na kisha kuanza kukimbia na kuweza kudondosha bunduki aina ya SMG pamoja na risasi 24 ambazo zilitakiwa kutumika katika tukio hilo.

Amesema askari walipowakamata wananchi walikusanyika katika tukio hilo na kuanza kuwapiga watu wanaodaiwa kuwa majambazi mpaka kupoteza maisha kutokana kushambuliwa huko na wengine watatu waliweza kukimbia na kiasi hicho cha fedha.

Kamishna Sirro amesema Isac alikuwa akitokea benki ya NMB na kwenda kupeleka fedha hizo katika benki ya DTB iliyopo Quality Plaza.

Katika operesheni nyingine imefanikiwa kukamata bastola moja ambayo ilipatikana  Februari 19 mwaka huu maeneo ya Kiwalani Kwa Gude kutokana na polisi kupata taarifa juu ya watu kujificha katika kichaka kwa ajili ya kufanya uhalifu  na baada ya kugundua polisi wapo eneo hilo walikimbia na kuacha silaha hiyo na jeshi la polisi linafanyia kazi mmiliki wa silaha.

Hata hivyo Jedhi la Polisi Kanda Maalumu linawashikilia watu wane wanaodaiwa kuwa ni majambazi sugu waliowakamata eneo la  Buguruni kwa Mnyamani ambao ni Mohamed Hassan maarufu kwa jina Kidali (21)Mkazi wa Vingunguti Speco,Hamis Alli (20) Mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani, Adam Salum (23) Mkazi wa Buguruni  kwa Madenge, Bakari Hamis (19) Mkazi wa Buguruni.

Aidha amesema katika taarifa usalama Barabarani wameweza kukusanya zaidi ya Sh. Bilioni moja  iliyotokana na makosa ya magari kuanzia Januari 02 hadi Februari 22 mwaka huu.

CUF Watoa Tamko Zito Kuhusiana Na Kukamatwa Kwa Mwanamkakati wa Maalim Seif

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wiki iliopita, mnamo tarehe 16 Februari, 2016, aliyekuwa mjumbe wa Timu ya Kampeni ya Chama Cha Wananchi (CUF), Ndugu Mohamed Ahmed Sultan Al-Mugheiry (maarufu kwa jina la Eddy Riyami), alipokea barua ya wito kutoka kwa Jeshi la Polisi Zanzibar ikimtaka kufika Makao Makuu ya Polisi, Ziwani, Zanzibar siku inayofuata, yaani tarehe 17 Februari, 2016, saa 2 asubuhi kwa kile kilichoelezwa kwamba “kuna mambo muhimu yanayomhusu” ambayo walitaka kuzungumza naye.

Bila ya kukosa, Eddy Riyami aliitikia wito huo na kufika Makao Makuu ya Polisi, Zanzibar na kuonana na SSP Simon S. Pasua wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CID). 

Hata hivyo, hakuhojiwa na badala yake alipewa simu na kutakiwa azungumze na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Bw. Salum Msangi ambaye alimwambia arudi tena Jumatatu, tarehe 22 Februari, 2016.

Eddy Riyami, akiwa raia mwema, alirudi tena jana kama alivyoagizwa. Alipofika hapo alihojiwa na Polisi na baadaye mwanasheria aliyefuatana naye akatakiwa kutafuta wadhamini wawili watakaomdhamini hadi atakapoitwa tena. 

Wakati mwanasheria wake aliporudi na wadhamini, akaelezwa kwamba Polisi imebadili uamuzi wake na imeamua kumuweka ndani hadi leo, tarehe 23 Februari, 2016. 

Mwanasheria na familia yake wakatakiwa kwenda tena Makao Makuu ya Polisi hiyo leo, saa 3 asubuhi. Walipofika leo asubuhi, wakaambiwa kwamba DCI kaacha maagizo kuwa suala la Eddy Riyami liachwe kwanza na wao warudi tena saa 6 mchana.

Hadi tunapotoa taarifa hii, hakujapatikana maelezo yoyote ya msingi juu ya kinachoendelea na wala Eddy Riyami hajafikishwa Mahakamani kusomewa mashtaka yoyote.

La ajabu zaidi, ni kwamba hata mke wake alipofika kituo cha polisi cha Madema anakoshikiliwa kwa ajili ya kwenda kumuona, hakuruhusiwa kumuona. 

Kutokana na mwenendo huu, Chama Cha Wananchi (CUF) kinalichukulia suala hili kwamba ni mwendelezo wa vitendo vya unyanyasaji wa kisiasa dhidi ya wapinzani wa CCM, vitendo ambavyo tunaamini vinafanywa kwa shinikizo la wanasiasa.

Itakumbukwa kwamba kwa muda mrefu tokea wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015 tumekuwa tukitoa tahadhari za kuwepo mipango ya kuwakamata viongozi wa CUF na wanaharakati wengine ili kufanikisha malengo ya kisiasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tuna kila sababu ya kuamini kwamba hatua ya kumkamata Eddy Riyami na kumuweka ndani bila ya kumfikisha Mahkamani ni utekelezaji wa mipango hiyo. La si hivyo, ikiwa Eddy Riyami ametenda kosa basi angelishafikishwa Mahkamani ndani ya muda wa saa 24 tokea kukamatwa kama sheria inavyotaka.

Chama Cha Wananchi (CUF) kinalitaka Jeshi la Polisi kuacha kutumiwa na kutumika kisiasa kufanikisha malengo ya kisiasa ya CCM. 

Tunashangazwa kwamba siku zote wanaoitwa kuhojiwa, kukamatwa na kuwekwa ndani ni wanasiasa wa vyama vya upinzani na wanaharakati wengine lakini hatujawahi kushuhudia viongozi wa CCM kuitwa kuhojiwa, kukamatwa na kuwekwa ndani.

CUF imetoa taarifa kadhaa kwa Jeshi la Polisi zinazohusu matamshi na vitendo vya viongozi wa CCM vyenye mwelekeo wa uhalifu lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Hizo ni dalili za waziwazi za Polisi kutumiwa na kukubali kutumika kisiasa.

Tunalitaka Jeshi la Polisi iwapo kweli lina kesi dhidi ya Eddy Riyami basi limfikishe Mahkamani haraka ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake.

Na iwapo hawana kesi, basi wamwachie huru mara moja. Umefika wakati wa Jeshi la Polisi kufanya kazi zake kitaalamu kama sheria na kanuni zao zinavyoagiza badala ya kuwatumikia wanasiasa wa CCM.

HAKI SAWA KWA WOTE
HAMAD MASOUD HAMAD
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI NA MAWASILIANO NA UMMA – CUF
23 Februari 2016

Rais Dr. Magufuli Ahakikishiwa Kuwa Hali Ya Burundi Ni Shwari.

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mheshimiwa Pierre Nkurunziza amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa hali ya Burundi ni shwari na kwamba tangu jana (Februari 22, 2016) nchi hiyo imepokea ugeni mkubwa wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Ban Ki-moon na inatarajia kupokea marais watano kutoka nchi za Umoja wa Afrika tarehe 25 Februari, 2016.

Ujumbe wa Rais Nkurunziza umewasilishwa na Mjumbe maalum ambaye pia ni Waziri wa Afrika Mashariki wa Burundi, Mheshimiwa Leontina Nzeyimana leo tarehe 23 Februari, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam, alipokutana na Rais Magufuli na kufanya nae Mazungumzo.

Pamoja na kumpa taarifa kuwa Burundi inaendelea vizuri, Mheshimiwa Nzeyimana pia amemueleza Rais Magufuli kuwa Burundi ipo tayari kupokea nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka kwa Rwanda, ikiwa ni kwa mujibu wa Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaoelekeza kuwa  nchi inayofuata kutoa Katibu Mkuu baada ya Katibu Mkuu wa sasa kumaliza muda wake, ni Burundi.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Mabalozi watatu wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.

Balozi wa Uholanzi hapa nchini Mheshimiwa Jaap Frederiks, amewasilisha salamu za Mfalme wa Uholanzi Mtukufu Willem-Alexander ambaye amempongeza Rais Magufuli kwa juhudi kubwa alizoonesha katika mwanzo wa utawala wake, katika kusimamia Uadilifu serikalini na katika biashara na pia kuisaidia Mahakama. Amesema Uholanzi inaamini kuwa maeneo hayo ndio yamekuwa yakileta vikwazo vya maendeleo, biashara na uwekezaji.

Balozi Jaap Frederiks amemhakikishia Rais Magufuli kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maendeleo kama ilivyofanya katika miaka 45 iliyopita, huku akitaja baadhi ya maeneo ya ushirikiano kuwa ni Kilimo na Nishati.

Balozi wa India hapa nchini Mheshimiwa Sandeep Arya, amewasilisha salamu za Waziri Mkuu wa India Mheshimiwa Narendra Modi, ambaye pamoja na kuitaja Tanzania kuwa lango muhimu katika mpango wake wa ushirikiano na Afrika, amemhakikishia kuwa India itaendeleza uhusiano wake na Tanzania hususani katika biashara na uwekezaji ikiwemo kuunga mkono mpango wa ujenzi wa viwanda Tanzania.

Nae Balozi wa Zambia hapa nchini Mheshimiwa Judith Kangoma Kapijimpanga ameelezea matumaini makubwa ya kuendelezwa kwa ushirikiano na mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Zambia na amemuomba Rais Magufuli aimarishe maeneo kadhaa ya kiushirikiano yakiwemo Reli ya TAZARA, Bomba la Mafuta la TAZAMA na taratibu za usafirishaji wa Mizigo katika bandari ya Dar es salaam na Mpaka wa Tanzania na Zambia.

Kwa upande wake Rais Magufuli amewahakikishia mabalozi hawa kuwa serikali yake ya awamu ya tano itaendeleza na kuimarisha zaidi mahusiano kati ya Tanzania na nchi hizo na kwamba atafurahi kuona mahusiano na ushirikiano huo unaleta manufaa kwa wananchi.

Baadhi ya maeneo ambayo amezialika nchi hizo kuongeza ushirikiano na Tanzania ni katika ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kisasa yaani "Standard Gauge" kuwekeza katika viwanda vya kusindika mazao na kuzalisha bidhaa mbalimbali, Elimu na Afya.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Jaji Mkuu wa Mahakama hapa nchini, Mheshimiwa Mohamed Chande Othman, Ikulu Jijini Dar es salaam.

Imetolewa;
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
23 Februari, 2016

Jengo la posta Dodoma lateketea kwa moto

$
0
0

JENGO Posta lililopo katika eneo la sabasaba katika Manispaa ya Dodoma  jana limeteketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa

Akizungumzia kutekeleza kwa jengo hilo Meneja wa Posta Mkoa wa Dodoma, Magreth Mlyomi alisema mpaka sasa kuna hasara kubwa kutokana na kutekeleza jengo hilo sambamba na vifaa vyote vya ofisi.

Mlyomi alisema licha ya kuwa hakuna mfanyakazi hata mmoja aliyepoteza maisha katika jengo hilo lakini mpaka sasa kuna vitendea kazi vingi vya ofisi pamoja na mizigo ya wateja imeteketea.

“Kuna mizigo mingi pamoja na vifaa vya kazi vyote vimeteketezwa na moto na kwa taarifa nilizopata kulikuwa na mizigo ya watu, inaonesha kuwa chanzo cha moto ni umeme,” alieleza Meneja huyo.

Akizungumzia kuhusu masuala ya miundombinu ya maeneo husika alisema ni mibovu na kutokana na changamoto hiyo suala hilo lipo katika mamlaka husika ya manispaa.

Kwa upande wake katibu wa wafanyabiashara katika soko la Sabasaba katika Manispaa ya Dodoma, Gergod Lugusi alisema jana saa nne asubuhi kulitokea moto mkali ambao uliunguza jengo hilo.

Alisema chanzo cha moto huo inasemakana kuwa ni tatizo la umeme na uongozi ulilazimika kutoa taarifa katika kikosi cha zima moto na bila kuchelewa walifika kwa wakati.

Hata hivyo alisema licha ya kufika kwa wakati katika tukio bado kikosi hicho kilikutana na kikwazo kwa kutokana na miundombinu kuwa mibovu na migumu kupitika.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images