Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Asema Rais Magufuli Hana Mamlaka Kikatiba Ya Kuingilia Mambo Ya Zanzibar

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju amesema Rais John Magufuli hana mamlaka ya kikatiba ya kuingilia masuala ya Zanzibar ukiwamo uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20.

Hii ni kauli ya pili kutolewa ndani ya wiki moja ikieleza hali hiyo, baada ya ile ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Luvuba aliyoitoa wiki iliyopita baada ya kufanya mazungumzo na Rais Magufuli, Ikulu, Dar es Salaam.

Akizungumza bungeni juzi, Masaju alisema: “Katiba ya Zanzibar si ya Muungano, masuala ya ulinzi na usalama ndiyo ya Muungano na ndiyo sababu ulinzi umeimarishwa visiwani humo kuhakikisha nchi hiyo inakuwa salama."

Alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati akifafanua mambo mbalimbali yaliyozungumzwa na wabunge wakati wa mjadala wa mwongozo wa mpango wa Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha wa 2016/17 na Mapendekezo ya Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa mwaka 2016/17.

Tangu kuibuka kwa mgogoro Zanzibar watu wa kada mbalimbali wamekuwa wakisema mwarobaini wa mgogoro huo kwa kutumia jitihada za ndani, ufanywe na Rais Magufuli baada ya jitihada za viongozi wa kisiasa visiwani kukwama.

Mgogoro huo, ambao umekuwa kawaida kuibuka kila baada ya Uchaguzi Mkuu, uliibuka baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salum Jecha kufuta matokeo Oktoba 28 na baadaye kuuitisha upya, kitendo ambacho CUF inakipinga.

Tangu wakati huo, Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, Rais wa Zanzibar, Dk Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Idd na marais wa zamani wa Zanzibar, Dk Salmin Amour, Ali Hassan Mwinyi na Amani Karume wamekuwa kwenye mazungumzo ambayo hayakuzaa muafaka.

“Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua uwepo wa Serikali mbili. Hizi Serikali uwepo wake ni Katiba ya Muungano na Katiba ya Zanzibar. Ukisoma Ibara ya nne ya Katiba si tu kwamba inaweka mgawanyo wa madaraka katika mihimili mitatu ya Dola, bali inaweka mgawanyo wa madaraka kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar.”

Ibara ya 4 ya Katiba inasema (1) Shughuli zote za Mamlaka ya nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji, vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki na pia vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma.

(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki vitakuwa ni Idara ya Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Idara ya Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni Bunge na Baraza la Wawakilishi.

(3) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za umma katika Jamhuri ya Muungano, na kwa ajili ya mgawanyo wa madaraka juu ya shughuli hizo baina ya vyombo vilivyotajwa katika ibara hii, kutakuwa na mambo ya Muungano kama alivyoorodheshwa katika nyongeza ya Kwanza iliyoko mwishoni mwa Katiba hii, na pia kutakuwa na mambo yasiyo ya Muungano ambayo ni mambo mengine yote yasiyo ya Muungano.

(4) Kila chombo kilichotajwa katika ibara hii kitaundwa na kutekeleza majukumu yake kwa kufuata masharti mengine yaliyomo katika Katiba hii.

Masaju alisema Katiba ya Zanzibar ndio inayozaa ZEC.

“Kile ambacho baadhi ya wabunge wamekisema hapa ni kama kuitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingilia mamlaka ya Zanzibar na tafsiri yake ni kama unataka kuleta hoja ya kujenga Serikali moja,” alisema.

Alisema kufanya hivyo ni kuvunja Katiba ya Muungano na ya Zanzibar na Serikali haiwezi kufanya hivyo.

Lowassa Afunguka........Asema Kuitwa FISADI Kulimfanya Ajioondoe CMM Na Kuhamia Chadema

$
0
0

Aliyekuwa mgombea urais wa Chadema chini ya mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa amesema kusakamwa kwa maneno ya kejeli, vijembe na vitisho, kuitwa gamba na fisadi ndani ya CCM ndiko kulikomfanya kukihama chama hicho na kwenda upinzani.

Lowassa aliyekuwa na nguvu ya ushawishi ndani na nje ya CCM, alihamia Chadema baada ya jina lake kukatwa katika mchakato wa kumsaka Rais wa Tanzania, katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana.

Akizungumza katika mahojiano maalumu ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Lowassa alisema licha ya kuitumikia CCM kwa zaidi ya miaka 30 tangu mwaka 1977, chama hicho kiliamua kutumia watu kumsakama kwa kila aina ya maneno jambo lililomfanya achoke na kuamua kuondoka.

“Nakifahamu Chama cha Mapinduzi, nakiheshimu kwani ndicho kilichonilea, lakini, kwa hali tuliyokuwa tumefikia, inafika mahali unasema imetosha,” alisema Lowassa.

Alitaja sababu nyingine iliyomfanya kuihama CCM kuwa ni kutaka mabadiliko na aliamini mabadiliko ya kweli yatapatikana nje ya chama hicho tawala na akisema hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alisema mabadiliko yatatafutwa hata nje ya CCM.

Alisema kwa namna yoyote, kamwe hana mpango na hawezi kurudi CCM na akasema jukumu lililopo mbele yake kwa sasa ni kuijenga Chadema ambayo yeye ni Mjumbe wa Kamati Kuu.

“Sina mpango na wala siwezi kurejea CCM, mimi ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, na jukumu lililoko mbele yangu ni kukijenga na kukiimarisha chama changu hiki kiwe imara tangu katika ngazi ya matawi,” alisema na kuongeza kuwa kazi iliyoko mbele yake sasa ni kukiimarisha chama hicho na wamejipanga kuzunguka nchi nzima kufanya kazi hiyo pamoja na kuwashukuru nwananchi kwa imani waliyoionyesha kwake na chama chake.

Lowassa alidai kuwa kama si kura kuchakachuliwa, alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kwa sababu wananchi walishaichoka CCM na wakawa wanataka mabadiliko.

Alisema kazi nyingine kubwa waliyonayo sasa ni kuhakikisha Katiba Mpya inapatikana na Tume ya Uchaguzi inaundwa upya kwani iliyopo si huru hata kidogo.

Alisema kama isingekuwa busara na ukomavu waliouonyesha Ukawa, basi hata hali ya siasa Tanzania Bara isingelikuwa shwari kama ilivyo sasa.

“Mara baada ya matokeo ya uchaguzi, niliwashauri vijana watulie, wasifanye fujo, nashukuru walinisikiliza.”

Alisema katika uchaguzi huo yeye na Ukawa walishinda kwa kishindo isipokuwa matokeo yalivurugwa makusudi ili CCM iendelee kubaki madarakani.

“Nilishinda na Ukawa ilishinda, kilichotokea kura zilichakachuliwa kwa kiasi kikubwa… wao wanajua, Watanzania wanajua na kila mtu anajua, tulishinda kwa kura nyingi sana na tulipokonywa ushindi wetu,” alisema.

Vijana wa Chadema kukamatwa 
Alisema miongoni mwa mambo yanayomuumiza na ambayo hatayasahau katika uchaguzi huo ni kitendo cha polisi kwa maagizo ya watendaji wa Serikali kuwakamata vijana waliokuwa wanakusanya matokeo na kuwadhalilisha ikiwa ni pamoja na kuwaweka mahabusu.

Alidai kuwa kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuvuruga kituo chao walichokuwa wakijumuisha matokeo na kuacha kile cha CCM kilikuwa kibaya na kilichoonyesha wazi kuwa hawakuwa tayari kukubali kuona wakishindwa.

Alisema: “Ni aibu kubwa kwa Serikali kuwaumiza na kuwaweka ndani vijana wadogo wasiokuwa na hatia eti kwa sababu tu walikuwa wakiunga mkono mabadiliko."

 Uhuru wa NEC 
Lowassa alisema miongoni mwa mambo yanayozorotesha chaguzi nchini ni NEC ambayo alisema siyo huru na badala yake ni chombo kinachotumika na watawala.

Alisema chombo hicho hakitendi haki na kwamba ingekuwa mamlaka yake baada ya uchaguzi kwisha angekiondoa madarakani.

Alisema wakati umefika kwa Watanzania kuungana kudai Katiba Mpya na tume huru ya uchaguzi kwa maelezo kuwa bila Katiba mpya na tume huru kamwe hakuwezi kufanyika uchaguzi ulio huru na wa haki.

Demokrasia bungeni 
Akizungumzia mwenendo wa Bunge, alisema linakwenda vizuri lakini ni mapema kulizungumzia kwa sasa.

“Katika Bunge hili wameingia vijana madhubuti bungeni, lakini hatua ya Serikali kuzuia Televisheni ya Taifa (TBC) kurusha matangazo ya Bunge moja kwa moja, hiyo ni dalili ya kuminya demokrasia.”

Alisema ni aibu kubwa kwa Serikali kutumia polisi kuingia ndani ya Bunge badala ya kujenga hoja na akasema hali hiyo ikiachwa ikaendelea italitia aibu Taifa.

Alisema moja ya mambo yaliyohimizwa na ambayo Watanzania waliachiwa na Mwalimu Julius Nyerere ni utaratibu wa kujenga hoja na kutumia nguvu ya kushinda na akaongeza kuwa kitendo cha polisi kuingia na kupiga wabunge ni kuminya na kudidimiza demokrasia.

“Tanzania tunasifika duniani kote kwa kuheshimu na kufuata demokrasia, lakini Serikali imeamua kutumia polisi kuminya demokrasia, hii ni aibu kubwa kwa Taifa… Watanzania tukiacha demokrasia ikaminywa tutalitia aibu Taifa,” alisema.

Shukrani kwa Watanzania 
Lowassa anasema licha ya kupokonywa ushindi, anajivunia mafanikio makubwa aliyoyapata kutoka kwa Watanzania walio wengi ambao walimuamini na kumuunga mkono.

“Watanzania waliniunga mkono kwa wingi sana, hali ile ilinipa faraja kubwa…nilifarijika pia nilipowaomba watulie wakanielewa na kutulia… nawashukuru sana Watanzania walionielewa na kutulia,” alisema.

Alitoa wito kwa Watanzania kuilinda amani ya nchi huku akisema anasubiri Rais Magufuli kutimiza siku 100 ndipo atoe tathmini yake kuhusu utawala wake.

“Marais wanapimwa kwa siku 100, nasubiri siku hizo, nitasema.”

Hali ya kisiasa Zanzibar 
Akizungumzia hali ya kisiasa ya Zanzibar na uamuzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), kutangaza kurejewa uchaguzi upya, Lowassa alisema suala hilo ni zito na gumu na linahitaji maombi maalumu na umakini wa hali ya juu katika kulitatua.

Alitoa wito kwa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM na Rais Magufuli kulishughulikia suala hilo mapema kabla ya Machi 20.

“Wasikubali tufike pabaya. Bado naamini tunaweza kulimaliza kwenye meza,” alisema na kuongeza:

 “Nawasihi sana viongozi hawa wasilipuuze hili suala, jambo hili likiendelea litaleta shida kubwa kwa nchi yetu, magaidi wanaweza kulitumia na kuleta madhara makubwa, wasisubiri kufika pabaya, waanze kulishughulikia sasa.”

Alitoa wito pia kwa wanaoshughulikia suala hilo kuvishirikisha na vyama vingine badala ya kulifanya kuwa ni suala la CCM na CUF pekee.

Alisema ni imani yake kuwa Watanzania ni wamoja na hakuna mtu wa kuwagawa kwa namna yoyote na kuwa wasikubali uchaguzi huo wa marudio kuwa sababu ya kuivuruga amani ya nchi

Waasi Wa Burundi Wakimbilia Nchini Kushawishi Watanzania Wajiunge Na Vikundi Vya Waasi

$
0
0

BAADHI ya askari waasi wa Burundi, wamebainika kukimbilia nchini na kuanza kushawishi vijana wajisajili ili wajiunge na vikundi vya waasi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema hayo jana alipokuwa akifunga Mkutano wa Pili wa Bunge mjini Dodoma jana na kuwataka wakimbizi na wananchi, kushirikiana na vyombo vya usalama, kutoa taarifa za uhalifu.

“Kutokana na ujio wa wimbi kubwa la wakimbizi kutoka Burundi, kumejitokeza matukio ya uhalifu wa kutumia silaha za moto ndani na nje ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu.“ 

"Aidha, kutokana na upekuzi na ukaguzi kwa wakimbizi unaofanywa kwa pamoja na vyombo vya dola sanjari na taarifa za ki-intelijensia, imebainika kuwepo kwa askari waasi waliokimbia pamoja na raia wa kawaida, ambao wanajaribu kuwashawishi vijana kujisajili ili kujiunga na vikundi vya waasi,” alisema Majaliwa.

Pamoja na changamoto hiyo, ambapo kambi za wakimbizi zilizoko mikoa ya Kigoma, Katavi, Tabora na Tanga zinahifadhi wakimbizi wapatao 218,895 kutoka mataifa ya Burundi (156,377), Congo-DRC (62,176), Somalia (150) na mataifa mchanganyiko (192) ikiwemo Rwanda, Uganda, Sudan Kusini na Ethiopia, hali usalama katika nchi kwa ujumla ni shwari.

Akizungumzia kuimarisha maadili na utendaji serikalini, Majaliwa alisema Serikali imedhamiria kurejesha nidhamu na maadili ya watendaji wa Serikali na watumishi wa umma katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.

“Katika kuhakikisha watumishi wa umma na Watanzania wote wanafanya kazi, Mheshimiwa Dk John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuja na kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu.

 “Tafsiri ya falsafa hii ni kuwataka Watanzania wote katika nafasi mbalimbali walizopo, kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vya uzembe, urasimu na kutenda kazi kwa mazoea,” alisema.

Alimtaka kila mwananchi, kuwa na nidhamu ya kazi na kuhakikisha anafikia malengo yaliyowekwa na kuwakumbusha watumishi wa umma kuwa, wamepewa dhamana ya kuwahudumia wananchi kwa niaba ya Serikali.

Kwa kuzingatia wajibu huo, amewataka watumishi hao kuhakikisha wanawahudumia wananchi kwa haki, weledi, uadilifu na kwa taaluma zao na kuhakikisha kuwa wanatatua kero za wananchi.

Waziri Mkuu alisema wanatambua kuwa wapo watumishi wanaotekeleza vyema majukumu yao, lakini pia wapo watumishi ambao hawazingatii maadili ya kazi zao na pia wanafanya kazi kwa uzembe.

“Serikali haitaacha kuchukua hatua za nidhamu kwa watumishi wote wasiozingatia kikamilifu sheria, kanuni na taratibu katika utumishi wa Umma. 

"Aidha, kwa kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Rais, viongozi na watumishi wote wa umma lazima tufanye kazi kwa kuzingatia weledi na kujiamini. Kila mtu anapaswa kujitathmini kama dhamana aliyopewa anaitendea haki,” alisema.

Kuhusu dhana ya kutumbua majipu, Majaliwa alisema Rais ametumia dhana hiyo kusimamia uwajibikaji, hasa kwa wale wenye dalili ya kukosa maadili ya utumishi wa umma.

“Tafsiri ya dhana hii ya “Kutumbua jipu” inalenga katika kuwarejesha watumishi wa umma na walioko serikalini katika mstari mzuri wa utendaji. Nitoe mwito kwa waheshimiwa wabunge wote kama tulivyo na kwa umoja wetu tumuunge mkono Mheshimiwa Rais katika vita hii kubwa ya ‘Kutumbua Majipu’. 

“Tukiwa pamoja na kwa kushirikiana tutaweza kuibadilisha nchi yetu kuwa nchi ya maadili na yenye sifa ya juu katika utendaji wa utumishi wa umma,” alisema.

Kuhusu elimu, Majaliwa alisema tangu Rais Magufuli atoe maelezo ya utekelezaji wa elimu msingi bila malipo, kumekuwa na umuhimu wa kutoa elimu na ufafanuzi zaidi juu ya utekelezaji wa agizo la elimu bila malipo kwa Watanzania kuanzia darasa la awali hadi kidato cha nne katika shule za umma.

Alisema katika mpango huo, Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa mwanafunzi atasoma kuanzia darasa la awali hadi kidato cha nne bila ya wazazi na walezi kulipa ada ya shule, gharama za mitihani na michango mbalimbali.

“Hata hivyo, yapo majukumu ambayo yataendelea kutekelezwa na wazazi na walezi ambayo ni pamoja na kununua sare za shule na michezo, madaftari, kalamu na chakula kwa wanafunzi wa shule za kutwa. 

“Maeneo mengine ni kulipia nauli ya kwenda na kurudi shule, na mahitaji mengine kama kununua godoro, shuka na vifaa vya usafi binafsi. Mzazi au mlezi ana wajibu wa kugharamia matibabu ya mtoto wake,” amesema.

Kuhusu elimu ya juu, amesema hadi kufikia mwishoni mwa Januari 2016, Serikali ilikuwa imetoa mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 207.9 kwa wanafunzi 122,786 wa elimu ya juu, wakiwemo wanafunzi wa mwaka wa kwanza 53,850 ambao ni asilimia 98.9 ya wanafunzi 55,254 walioomba mikopo hiyo.

Kuhusu uendeshaji wa Bunge, Majaliwa alisema uzoefu alioupata katika muda mfupi aliokaa pamoja na wabunge Dodoma, amegundua kuwa kuna wabunge mahiri waliobobea katika nyanja mbalimbali.

Alisema amebaini wapo wasomi wa ngazi zote, wazee kwa vijana ambao wana uzoefu na utaalamu mkubwa na kuongeza kuwa wakitumia utaalamu na uwezo mkubwa walionao katika kuijenga nchi, nchi itapiga hatua.

Aliwataka wabunge watangulize uzalendo katika kila jambo wafanyalo kwa manufaa ya Taifa na watu wake, ili nchi ifike mahali ambapo kwa elimu, busara na hekima na kwa kuacha ushabiki wa kisiasa, watazame mbele katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Mbowe Amtosa Zitto Kabwe Baraza La Mawaziri

$
0
0

Kambi rasmi ya upinzani bungeni, imetangaza baraza lake la mawaziri kivuli ambalo Chama cha ACT Wazalendo, chenye mbunge mmoja, Kabwe Zitto, ndicho hakikuingizwa kwenye baraza hilo. Kiongozi wa kambi hiyo, Freeman Mbowe alitangaza jana bungeni baraza hilo.

Chadema chenye wabunge wengi katika kambi hiyo, kina mawaziri vivuli wengi ikilinganishwa na vyama vingine na wakati huo huo, kina wizara nyingi ambazo kinaongoza peke yake kwa maana ya kuwa na mawaziri na naibu mawaziri vivuli.

Mbowe alisema idadi ya wizara alizotangaza inafanana na ya wizara za Serikali ya Awamu ya Tano ambazo zipo 19.


Mbali na kutangazwa kwa majina hayo ,Bunge lilifanya uchaguzi wa wajumbe wa kuliwakilisha kwenye taasisi mbalimbali za kibunge.

Wajumbe hao ni wa Tume ya Utumishi wa Bunge, Bunge la Afrika (PAP), Jukwaa la Wabunge wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-PF), Kamati ya Utendaji wa Bunge la Jumuiya ya Madola (CPA) na Umoja wa Wabunge Duniani (IPU).

 Akitangaza wabunge walioshinda katika uchaguzi huo, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema idadi ya wajumbe waliorudisha fomu za kuwania nafasi hizo ilikuwa inalingana na idadi ya nafasi zilizokuwa zikiwaniwa, hivyo kuwafanya wote kupita bila kupigiwa kura.

1.Tume ya Utumishi wa Bunge Kangi Lugola, Fakharia Shomar Khamis, Mary Chatanda, Mussa Azzan Zungu, Salim Hassan Turky, Magdalena Sakaya na Peter Msigwa.

2.Bunge la Afrika Mboni Mhita, Asha Abdullah Juma, Dk Faustine Ndugulile, Stephen Masele na David Silinde.

3.Jukwaa la Wabunge wa SADC Jamal Kassim Ali, Esther Mmasi, Selemani Zedi na Ally Abdallah Saleh.

4.Kamati ya Utendaji ya Bunge la Jumuiya ya Madola Amina Mollel, Maria Kangoye, Zainab Vullu, Khamis Mtumwa Ali, Salum Rehani, Japhet Hasunga, Josephat Kandege, Dk Raphael Chegeni, Jitu Soni, Immaculate Semesi, Juma Hamad Omar na Tundu Lissu.

5.Umoja wa Mabunge Duniani Dk Pudenciana Kikwembe, Juma Othman Hija, Mohamed Mchengwerwa, Peter Serukamba na Susan Lyimo. 

Mwenyekiti Wa CCM, Jakaya Kikwete Aomba Wazee Wamuunge Mkono Rais Magufuli

$
0
0

MWENYEKITI  CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete, amewaomba wazee kote nchini, kumuunga mkono Rais John Magufuli katika uongozi wake ili kumpa moyo wa  kuwatumikia Watanzania.

Amesema kipindi ambacho Dk Magufuli ameingia madarakani hadi sasa ni muda mfupi, hivyo si vema kuanza kudodosa na kulaumu panapopwaya, badala yake Wazee na watanzania kwa jumla wazidi kumuunga mkono ili kumtia moyo wa kutekeleza  yote aliyokusudia kuyafanya kwa manufaa ya taifa.

Kikwete alitoa ombi hilo alipokuwa akizungumza katika mkutano na wazee wa Mkoa wa Singida, ambapo alisema kuwa kuongoza bila ushauri wa wazee nchi inaweza kuyumba.

“Kuongoza nchi bila wazee mambo hayaendi vizuri na  ukikosa mzee kwenye jahazi wapiga makasia vijana wanaweza kuanza kuzozana na chombo kwenda mrama, lakini wakiwepo wazee watawaongoza vizuri  na chombo/ nchi kwenda  salama”. Alisema Kikwete huku akishangiliwa na wazee.

Alisisitiza kwamba ukitaka nchi itulie kamata wazee, lakini ukiongoza nchi kwa kutumia vijana  pekee nchi inaweza kuyumba, na itafika mahali mtakosa mahali pa kushika. 

Alisema kuwa hata yeye kwa mara ya kwanza .alipokwenda kuomba ubunge jimboni kwake Bagamoyo, Pwani aliunda kamati ya wazee ambayo ilimsaidia sana.

Wazee ni sehemu ya matumaini ya chama na Serikali, panapokuwepo  wazee hapaharibiki jambo.

 “Nawashukuru sana wazee endeleeni kukijenga chama na kuiunga mkono Serikali inayoongozwa sasa na Dk John Magufuli.” Alisisitiza Kikwete na kuongeza kuwa,

“Hata kwenye chama chetu tumeunda Baraza la Washauri la Wazee wasitaafu ambapo wengi walipinga. Hata hao wazee tuliowataka waunde baadhi yao walipinga, lakini mwisho walikubali kwa masharti kwamba wawe wanaitwa panapotokea jambo kubwa litakalohitaji ushauri wao.”
 
Alisema mmoja wa viongozi aliyekuwa msitari wa mbele kuunda baraza hilo alikuwa Rais msitaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ambaye alitoa ushauri wa kuitwa kutoa ushauri panapotokea jambo kubwa na kwamba hata wakitoa ushauri, viongozi waliopo madarakani wawe hiari kuukubali au kuukataa.
 
Aliwataka wazee kuendelea kuiunga mkono serikali ya sasa ambayo kwa hivi sasa imetimiza muda mfupi wa miezi mitatu ambaye ni sawa na mtoto mdogo anayekua.

Alisema kuwa Jambo kubwa ni kuwaunga mkono, kuliko kuwalaumu ama sivyo watavunjika moyo, ndani ya miaka mitano itakuwa hasara. ...."Watieni moyo ili wajiamini wahudumie vizuri zaidi ili nchi isonge mbele kimaendeleo."
 
Kikwete alisisitiza kuwa hata yeye akitakiwa kwenda kutoa ushauri atakwenda  na akiwa na jambo la kushauri atakwenda pia, lakini aliwaasa kuwa  si kila jambo wazee watake kwenda kutoa ushauri, itachelewesha mambo mengi.

Picha Za Maadhimisho Ya Miaka 39 Ya CCM Kitaifa Mkoani Singida

$
0
0
Msafara wa Mh. Rais John Pombe Magufuli ukiwasili kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida tayari kwa kuhudhuria sherehe hizo.

Mh.Rais Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Singida Mh. Dk. Parseko Kone
Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Rais Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasili uwanjani hapo katikati ni Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan.
Rais Dk. John Pombe Magufuli akiwapungia mikono wana CCM na wananchi wakati alipowasili kwenye uwanja huo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akipokelewa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili kwenye maadhimisho ya miaka 39 ya CCM yanayofanyika kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mh. Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo mara baada ya kuwasili uwanjani hapo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akizungumza na Mh. Rais John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais Mh.Mama Samia Hassan Suluhu, Kushoto ni Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Move waliohudhuria katika maadhimisho hayo kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.

Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete Asema CCM Ilisikitishwa Sana na Uamuzi wa ZEC Kufuta Uchaguzi Zanzibar

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza rasmi kuachia kiti hicho kabla ya mwezi Februari mwakani, huku akisema CCM imesikitishwa na uamuzi wa ZEC kufuta uchaguzi wa Zanzibar.

Dkt Kikwete ambaye pia ni Rais wa awamu ya nne wa serikali ya Jamhuri ya Tanzania, ametoa tamko hilo leo katika sherehe za miaka 39 ya chama hicho zilizofanyika katika uwanja wa Namfua mjini Singida, ambapo yeye ndiye aliyekuwa mgeni Rasmi.

Katika hotuba yake, Dkt Kikwete amewaeleza wana CCM waliofurika kiwanjani hapo kuwa hizo ndizo zitakuwa sherehe zake za mwisho kwake kuhudhuria huku akiwa mwenyekiti, kwa kuwa katika sherehe zijazo mwenyekiti wa chama hicho atakuwa ni Rais John Magufuli.

"Hii ni mara yangu ya mwisho kuhudhuria sherehe hizi kama mwenyekiti wenu, Katika sherehe za mwakani, mwenyekiti wenu atakuwa ni Rais John Magufuli"

Chama hicho kinataraji kufanya maadhimisho yake ya miaka 40 ya kuzaliwa kwake mwezi Februari mwaka 2017 mwaka ambao pia ni wa uchaguzi mkuu wa chama hicho kwa mujibu wa katiba yao.

Kuhusu Uchaguzi mkuu wa Zanzibar, Kikwete amesema wao kama CCM hawakupenda uchaguzi huo urudiwe kwa kuwa walikuwa wana uhakika wa ushindi, na tayari walikuwa wanajiandaa kusherehekea ushindi mnono, lakini wanalazimika kukubaliana na maamuzi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa kuwa hawana namna nyingine.

“Tulikuwa tumejiandaa kushangilia, lakini Tume wakasema kuwa uchaguzi unafutwa kwa kuwa kulikuwa na dosari kubwa, tukasikitika sana lakini kwa kuwa tume wameamua, tukashauriana na wenzetu wa Zanzibar, tukaona ni bora kukubali kurudia uchaguzi huo, lakini hatukupenda”

Amewataka wana CCM wote visiwani Zanzibar kujiandaa na uchaguzi siku ya Machi 20, mwaka huu na kwamba wahakikishe wanatunza shahada zao kwa ajili ya kuchagua wagombea wa CCM.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete ametumia nafasi hiyo kuelezea mafanikio ya chama hicho katika kuwaletea watanzania maendeleo ambapo amesema katika miaka yake 39, chama hicho kimefanikisha mengi ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara.

Pia amezungumzia mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo licha ya kukiri kuwa chama hicho kilikuwa kwenye wakati mgumu, amesema bado kiko imara, na kitaendelea kuwa imara.

Amesema licha ya baadhi ya watu kukitabiria kifo chama hicho, watanzania bado wameendelea kukiamini na kukipa ushindi wa kishindo huku akitolea mfano ushindi ambao chama hicho kimeupata katika ngazi ya urais, udiwani, na ubunge mwaka 2015.

“Katika ubunge sisi tumepata asilimia 73 ya viti vyote vya ubunge wa majimbo, na hata katika udiwani tumeshinda asilimia zaidi ya 73 katika kata zote, nashangaa kuna watu wanadai kwamba eti CCM haipendwi, yaani hata hesabu zinawashinda..” Amesema Kikwete.

Akizungumzia utendaji kazi wa serikali ya awamu ya tano, Dkt Kikwete amempongeza Rais Magufuli kwa kufanya yale aliyotumwa katika Ilani ya CCM na kuahidi kumpa ushirikiano ili ayafanikishe yote yaliyomo katika ilani hiyo.

Amewakosoa watu wanaodai kuwa Magufuli hatekelezi Ilani ya CCM bali ya vyama vingine na kusisitiza kuwa kila jambo linalofanywa na serikali hiyo limo ndano ya ilani ya CCM.

Kikwete ametolea mfano suala la kuanzishwa kwa mahakama maalum ya kushughulikia rushwa na wahujumu uchumi na kusema kuwa suala hilo limo ndani ya ilani ya CCM, na wala sio jambo la kuzuka.

Amesema wanaodai Magufuli anatekeleza sera zao wameishiwa na hawana la kuzungumza tena.

"Watani zetu wanasema anatekeleza mambo yao, wamekosa ya kusema wanasubiri akija bungeni watoke, watu wazima hovyooo"

Pia amewataka wanachama wa CCM kuchagua viongozi bora na watakaoweza kukijenga upya chama hicho katika uchaguzi wa chama hicho utakaofanyika mwakani , huku akiwataka wajiandae kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

“Mwisho wa uchaguzi mmoja ni mwanzo wa uchaguzi ujao, tumemaliza wa mwaka 2015 tuanze kujiandaa na uchaguzi wa 2020”

Sherehe za Miaka 39 ya CCM: Rais Magufuli Atuma Salamu Kwa Watendaji Wavivu Serikalini.

$
0
0

Rais John Magufuli amewataka watendaji wote wa serikali kuhakikisha kuwa wanatekeleza ipasavyo matakwa ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndicho kinachoongoza nchi kwa sasa.

Magufuli ametoa agizo hilo leo kwenye sherehe za miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi zilizofanyika katika uwanja wa Namfua mjini Singida.

Rais Magufuli ambaye alikuwa ni miongoni viongozi wakuu wa serikali waliohudhuria sherehe hizo akiambatana na makamu wake Samiah Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema yeye na serikali yake wamejipanga kutekeleza kikamilifu ilani ya CCM na kwamba hawezi kukiangusha chama hicho.

Akitoa salam zake katika sherehe hizo, Magufuli ametumia muda usiozidi dakika 10 kueleza mambo ambayo tayari serikali yake imeanza kuyafanya na ambayo itaendelea kuyafanya ikiwa ni pamoja na "kutumbua majipu" kwa ustawi wa maisha ya watanzania wote bila kujali vyama vyao.

Ametumia nafasi hiyo kuwaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya pamoja na watendaji wote serikalini kufanya kazi kwa nguvu, uadilifu na uzalendo ili kuwaletea watanzania maendeleo, na kwamba atakayeona hawezi atamuweka pembeni ili wengine wafanye kazi.

“Nawaeleza watendaji wote serikalini kuwa atakayeshindwa kufanya kazi, nitamueleza kwa upole sana maana mimi ni mtu mpole, nitamuambia akae pembeni apishe wengine”

Rais Magufuli pia ameupongeza uongozi wa CCM mkoa wa Singida kwa kuchangia madawati 1000 kwa shule za Singida na kuwaagiza wakuu wote wa mikoa na wilaya kuhakikisha wanafunzi hawakai chini.

“Mh mwenyekiti inasikitisha sana kuona sisi tunajifungia kwenye maofisi makubwa yenye viyoyozi, na maviti ya kuzunguka lakini tukitoka tu nje tunakuta wanafunzi wamekaa chini kwenye mavumbi, sasa nawaagiza wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa hakikisheni wanafunzi hawakai chini”

Rais Magufuli pia ametumia nafasi hiyo kukishukuru Chama cha Mapinduzi kufanikisha yeye kuwa Rais kwa kuwa bila chama hicho yeye asingekuwa Rais.

“Nataka watanzania wote wajue kuwa bila CCM mimi nisingekuwa Rais wao, kwa hiyo huwezi kunitenganisha mimi na CCM, ndiyo maana leo nimekuja nimevaa kijani yangu hapa”

Pia amesema haoni kama kuna chama kingine chochote kitakachokuja kutawala Tanzania zaidi ya CCM

"Nataka ifikie hatua watanzanie wote wasiwaze wala kuota vyama vingine, tutafanya yale ambayo wao wanataka kuyafanya, ... Hakuna mtawala anayetaka kutawaliwa, tena kwa bahati mbaya atawaliwe na vyama vya hovyohovyo, CCM itaendelea kutawala"

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili Ya Februari 7

Polisi Watatu Wafa Ajalini Msafara wa Rais Magufuli

$
0
0
Askari polisi watatu wamefariki dunia na wengine wawili wamejeruhiwa baada ya gari lao lililokuwa kwenye msafara wa Rais John Magufuli kutoka Singida kwenda Dodoma, kupasuka tairi na kupinduka.

Rais Magufuli alikuwa mjini Singida alikokuwa amekwenda kushiriki maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.

Hiyo ni mara ya pili kwa askari kufariki wakiwa kwenye msafara wa Dk Magufuli baada ya aliyekuwa akiongoza msafara wake wakati wa kampeni kugongana na dereva bodaboda katika eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam.

Askari huyo alikuwa kwenye pikipiki maalumu iliyokuwa ikiongoza msafara wakati Dk Magufuli akitoka katika Hospitali ya Lugalo kuaga mwili wa aliyekuwa mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP Thobias Sedoyeka alisema ajali hiyo ilitokea saa 9.40 alasiri, katika Kijiji cha Isuna, Wilaya ya Ikungi mkoani humo baada ya moja ya matairi ya gari hilo kupasuka na dereva kushindwa kulimudu.

Aliwataja waliofariki kuwa ni Mkaguzi Mwajelo, Sajenti Elias Mrope na Sajenti Gerard.

Waliojeruhiwa ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Singida (RCO), Peter Majira (50
na PC Charles Simon (34) ambao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni.

Gari hilo lililopata ajali ni lile lililokuwa limetangulia ili kufagia barabara kabla ya msafara wa Rais, likiongozwa na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani cha mkoa huo.

Sedoyeka alisema miili ya askari hao imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha hospitali ya mkoa huo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni, Kitundu Jacks alisema hali za majeruhi waliofikishwa kwenye hospitali hiyo zinaendelea vizuri.

“Mrope ndiye aliyeletwa akiwa kwenye hali mbaya, alikuwa amevunjika mbavu na mkono na akafa mara tu baada ya kufikishwa hospitalini hapa. Majeruhi wengine wamepata michubuko na wanaendelea vizuri,” alisema. 

Rais Magufuli Aomboleza Vifo Vya Askari Waliofariki Dunia Singida

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Ernest Mangu kufuatia vifo vya askari watatu waliopoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea jana tarehe 06 Februari, 2016 katika kijiji cha Isuna, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Askari waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Inspekta Miraji Mwegelo, Sajenti Elias Mrope na Sajenti Gerald Ntondo.

Katika salamu hizo Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa na vifo vya askari hao, ambao wamekutwa na mauti wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kikazi.

"Kupitia kwako Mkuu wa Jeshi la Polisi natoa pole nyingi kwa familia za Askari waliopoteza maisha, Ndugu, Jamaa na Marafiki pamoja na askari wote wa Jeshi la Polisi Tanzania ambao wameguswa kwa namna ya pekee na msiba huu" Amesema Rais Magufuli.

Ameongeza kuwa anaungana na wote walioguswa na vifo hivyo katika kipindi hiki kigumu, na amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi, Amina.

Rais Magufuli pia amewatumia salamu za pole Askari walioumia katika ajali hiyo, akiwemo Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani katika Mkoa wa Singida Mrakibu wa Polisi Peter Magira na kuwaombea wapone haraka ili waweze kuendelea na majukumu yao ya kila siku.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
07 Februari, 2016

Makamishna Wawili Kati Ya Sita Wa Tume Ya Uchaguzi Zanzibar Wamepinga Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar

$
0
0

Wakati wadau mbalimbali wa masuala ya kisiasa wakipinga kile kinachoendelea Zanzibar, nao makamishna wawili wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Nassor Khamis Mohamed na Ayoub Hamad wameibuka na kupinga uchaguzi huo wa marudio.

Wakizungumza na wandishi wa habari mjini Dar es salaam leo, makamishna hao wamesema kuwa sababu kubwa ya kupinga kufanyika kwa uchaguzi huo ni kutokana na kuvurugwa kwa katiba ya zanzibar tangu tukio la kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa oktoba 25, mwaka jana.

Makamishna hao wa ZEC, wakizungumza kwa hisia na kujiamini, wamesema kuwa mwenyekiti wa tume hiyo, Jecha Salim Jeche hakuwa na mamlaka ya kisheria kufuta uchaguzi huo bila kuwashirikisha makamishna wa tume hiyo.

Tayari, Jecha ametangaza kuwa uchaguzi wa marudio utafanyika siku ya Jumapili, Machi 20, mwaka huu. Lakini wajumbe hao wa ZEC, kwa pamoja wamesema wanapinga kufanyika kwa uchaguzi huo kutokana na ukiukwaji wa katiba:

“Tunapinga marudio ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi wa Machi. Uchaguzi huo si halali kulingana na matukio yaliyotokea tangu kufanyika kwa uchaguzi halali wa Oktoba 25, mwaka jana,” walisema makamishna hao wanaowakilisha CUF ndani ya ZEC.

Wamesema kuwa sababu nyingine inayowafanya kupinga uchaguzi wa marudio ni kutokana na kukamilika kwa uchaguzi wa mwaka jana ambapo uchaguzi huo ulikuwa umekamilika na baadhi ya washindi wa viti vya uwakilishi na udiwani walishakabidhiwa vyeti vyao.

Wamesema kurudiwa kwa uchaguzi huo ambao unatarajiwa kutumia zaidi ya shilingi billion saba hadi kukamilika kwake ni matumizi mabaya ya fedha za wananchi, kwani uchaguzi Zanzibar ulishafanyika na kinachoendelea ni mbinu za kuubatilisha.

Wamesema kuwa tukio la kufutwa kwa uchaguzi huo lilitanguliwa na matukio kadhaa ambayo yalionyesha wazi kuwa kuna kikundi cha watu ambacho kinamshauri Jecha, na sio maamuzi ya tume yote nzima.

“Tarehe 26 october mwaka jana CCM walileta barua ya malalamiko na kumtaka mwenyekiti na tume kufuta uchaguzi huo wakati tayari tulishaanza kutoa vyeti kwa washindi.

“Baada ya hapo mwenyekiti aliitisha kikao cha tume na tuliamua kwa pamoja kuwa maombi ya CCM hayakuwa na mashiko hivyo mchakato uliendelea.” amesema Nassor Khamis mmoja wa makamishna wa tume hiyo.

Amesema kwamba baada ya maamuzi hayo ya tume, ndipo siku iliyofuata Jecha (Mwenyekiti wa Tume), hakufika katika ujumuishaji wa matokeo kwa siku nzima na baadaye walisikia tu kuwa ametangaza kufuta uchaguzi bila kuwashirikisha wajumbe wengine wa tume.

Nassor amesema: “Baada ya hapo ndipo ofisi yetu ilianza kuzungukwa na wanajeshi na kuamuriwa tusifanye lolote huku Jaji wa mahakama kuu ya Zanzibar, naye akiwa amekamatwa na kupelekwa polisi.”

Wajumbe hao, wamesema kwa matukio kama hayo wanaamini kuwa tume hiyo imeacha kufanya kazi zake kisheria na sasa inafanya kazi kisiasa, jambo ambalo linampotezea sifa mwenyekiti wake kuendelea kuiongoza tume hiyo.

Aidha, wamesema kuwa hali iliyopo ndani ya tume kwa sasa sio hali ya kawaidia kuweza kusimamia uchaguzi wa haki kutokana na wajumbe wake kupingana hovyo hovyo:

“Wajumbe wamekuwa wakipingana kwa kila hoja inayoletwa…jambo ambalo linafanya uchaguzi wa marudio kutiliwa mashaka na wajumbe wengi wa tume hiyo,” amesema wajumbe hao.

Makamishna hao wamesema kuwa wametoa wito kwa wajumbe wengine wa ZEC, kuacha kufuata mkumbo na kuamua kusimamia sheria inavyosema, ili kuwapatia wazanzibar haki yao ya kikatiba..

Waziri Simbachawene Apongeza Uchaguzi wa Meya Dar es Salaam Kuahirishwa

$
0
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, imetumia busara kuahirisha uchaguzi wa Meya uliopangwa kufanyika leo.

Juzi halmashauri hiyo, iliahirisha uchaguzi huo, ikiwa ni mara ya pili baada ya kubaini nyongeza ya wajumbe 14 katika orodha iliyowasilishwa kwa wakurugenzi wa Manispaa za Kinondoni na Ilala.

Kasoro hizo zilijitokeza katika kikao cha viongozi wa halmashauri hiyo kilichongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Sarah Yohana na kuhudhuriwa na viongozi wa CCM, Chadema na CUF kujadili ajenda mbili.

Ajenda hizo ni taratibu za kuendesha uchaguzi wa Meya na kupitia orodha ya wajumbe wanaostahili kushiriki.

Kutokana na hali hiyo, ilimlazimu Yohana kuwaagiza wakurugenzi wa manispaa za Kinondoni na Ilala kuyafanyia uhakiki majina hayo wakishirikiana na viongozi wa vyama ili kuyapeleka halmashauri kesho kutwa.

Simbachawene alisema jana kuwa halmashauri na viongozi wa vyama hivyo walitafakari maelezo aliyoyatoa awali kabla kufikia hatua ya uchaguzi huo.

“Sijapata taarifa za kuahirishwa ndiyo kwanza nasikia kwako, lakini kama sababu ndiyo uliyoniambia basi wamefanya jambo jema. Kwa sababu uchaguzi huu una mvutano hivyo ni lazima mambo yaende kwa makubaliano.

“Pia ni hatua nzuri, itakayoleta maelewano baina yao ili kupata haki sawa kwa wajumbe watakaostahili kupiga kura. Tamisemi kazi yetu ni kueleza sheria inasemaje,” Simbachawene.

Hivi karibuni, Simbachawene aliahirisha uchaguzi huo, kisha kutoa sababu kuwa ni kuandaa mfumo wa upatikanaji wa wajumbe kutoka manispaa tatu kwa kuwa ule wa chama kimoja haukuwa na shida kama ilivyo sasa.

Katibu wa Chadema, Kanda ya Dar es Salaam, Henry Kilewo alisema kukwama kwa uchaguzi huo kunatokana na viongozi kutosikiliza mawazo ya upinzani.

 “Januari 27, nilimwandikia barua Simbachawene ya kutaka atupatie utaratibu wa uchaguzi huu utakavyokuwa, lakini hadi leo (jana), hakunijibu ndiyo maana matatizo kama haya yanatokea,” alisema.

Mkurugenzi Mtendaji Mbeya Afikishwa Mahakamani Kwa Ufisadi Wa Milioni 4

$
0
0

Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), imewafikisha mahakamani watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya akiwamo Mkurugenzi mtendaji, Upendo Sanga kwa madai ya kuhujumu uchumi.

Awali, Sanga alifika mahakamani hapo kusikiliza hukumu ya kesi yake iliyofunguliwa na Takukuru mwaka 2014.

 Baada ya hakimu kumwaachia huru, Takukuru walimzunguka na kumkamata tena na maofisa wake ambao walipandishwa tena kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Sarah Martin aliwasomea mashtaka washtakiwa hao, Mweka Hazina, Hafidhi Mgagi, Mhasibu Gershom Bwire na Sanga.

Sarah alidai kuwa washtakiwa hao walimdanganya mwajiri wao na kujipatia fedha kwa kutumia nyaraka za kughushi na kuisababishia Serikali hasara ya Sh4 milioni.

Mwendesha mashitaka huyo alidai kuwa Sanga na Mgagi kati ya Novemba 23 hadi 28, 2012 waliidhinisha malipo ya Sh4 milioni kwa Gershom Bwire kutengeneza vitabu 150 vya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).

Alidai kuwa katika shtaka la pili mshtakiwa wa tatu, Bwire Novemba 23 na 28, 2012 alijipatia fedha isivyo halali, mali ya mwajiri.

Mwendesha mashtaka alidai kuwa washtakiwa hao wameitia hasara halmashauri kwa kujipatia Sh4 milioni.

 Washtakiwa walikana mashtaka na kuachiwa kwa dhamana. Hakimu wa mahakama hiyo, Rashid Chaungu aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 17.

Wajane Wawili Wauawa Kwa Kukatwa Mapanga Wakidaiwa Kusambaza Kipindupindu Mkoani Mbeya

$
0
0

Wajane wawili wa Kitongoji cha Bulinda wilayani Kyela wameuawa kwa mapanga wakidaiwa kusambaza ugonjwa wa kipindupindu baada ya kufiwa na waume zao katika eneo hilo.

Waliouawa ni Geneli Kapwela (65) na Rahabu Bungulu (70) waliokuwa wakiishi peke yao.

Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Mbeya  Ahmed  Msangi  alisema  jana kuwa  wajane  hao  waliuawa  juzi  baada  ya  kipindupindu  kuhusishwa  na  imani za kishirikina.

Takwimu  za  mauaji toka polisi zinaonyesha  karibu watu wawili wanauawa  mkoani  Mbeya  kwa  imani  za  kishirikina

Mkuu Wa Mkoa Wa Kilimanjaro Amos Makalla Akagua Mpaka Wa Tanzania Na Kenya Na Kuteketeza lita 140 za Gongo

$
0
0

Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Kilimanjaro imeteketeza lita 140 za gongo, mapipa 40 na mitambo sita ya kutengeneza pombe hiyo haramu vyenye thamani ya Sh10 milioni.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Amos Makala, alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Rombo 

Alisema  mitambo hiyo  ya  gongo  iliteketezwa  katika  kijiji  cha Kikelelwa  Tarakea  wilayani  humo.

Makala  alisema  pombe  hiyo  imekuwa  ikileta  madhara  kwa  wananchi  hasa  vijana  ambao  wamekuwa  wakishindwa  kufanya  shughuli  za  maendeleo  kutokana  na  kunywa  muda  wa  kazi

 Alisema  wilaya  hiyo  inaongoza  kwa  kutengeneza  pombe  za  kenyeji  zaidi  ya 50  kwa  kutumia  kemikali  hatarishi.
  
"Gongo inaathari kubwa kutokana na utengenezaji wake, nimeambiwa wanaweka maji ya betri na kinyesi cha binadamu,” alisema Makala.

Alisema pombe hiyo inatajwa kuharibu nguvu za kiume na kupoteza nguvu kazi kubwa kwa Taifa hali inayosababisha kazi za wanaume kufanywa na wanawake.

Awali, kamati hiyo ya ulinzi na usalama ilikagua mipaka ya Kenya na Tanzania kuanzia Holili hadi Tarakea.

Mkuu wa Wilaya ya Rombo Lembris Kipuyo, alisema anapambana kukomesha unywaji wa pombe saa za kazi na utengenezaji wa pombe hizo.

Alisema wataendelea kukamata mitambo pamoja  na  malighafi  za  kutengeneza  pombe hizo
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amos Makalla na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na usalama Mkoa wakikagua mpaka wa Tanzania na Kenya

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Ashiriki Ibada Ya Kumsimika Askofu Mkuu Wa Pili Wa Eagt, Dkt Mwakipesile, Apanga Kukutana Na Viongozi Wa Dini

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ataitisha kikao cha viongozi wa dini zote hivi karibuni ili wapange na kuainisha ni mambo gani ambayo wanaweza kutoa ushauri kwa Serikali na kupata njia bora ya kuwahudumia Watanzania.

Alitoa ahadi hiyo jana mchana (Jumapili, Februari 7, 2016) wakati akizungumza na mamia ya waumini walioshiriki ibada ya kumsimika Askofu Mkuu wa Pili wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Askofu Dk. Brown Abel Mwakipesile iliyofanyika kwenye kanisa la EAGT la Mlimwa West nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Waziri Mkuu Majaliwa ambaye alihudhuria ibada hiyo kwa niaba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli alisema: “Hivi karibuni nitaitisha kikao cha viongozi wa dini zote kitakachojumuisha Maaskofu Wakuu, Masheikh na baadhi ya wachungaji ili tukae na kubaini ni nini kifanyike ili kuisadia Serikali namna nzuri ya kuboresha maisha ya Watanzania.”

Akijibu risala iliyosomwa na Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Dk. Leonard Mwizarubi, Waziri Mkuu alisema Serikali imeanza kufanya mapitio ambayo yatawawezesha Watanzania kupata huduma kwa urahisi.

“Katibu Mkuu pamoja na Baba Askofu Mkuu wamegusia suala la upandaji wa gharama za vifaa vya ujenzi pamoja na suala la makazi bora. Mwezi ujao tunaanza vikao vya Bunge vya kupitia bajeti ya Serikali, tutaliangalia hili kwa kumshirikisha Waziri wa Fedha… tutafanya mapitio katika hili ili mwananchi wa kawaida aweze kumudu maisha,” alisema huku akishangiliwa na waumini hao.

Aliwaomba viongozi wa kanisa hilo pamoja na waumini wake waendelee kuiombea nchi pamoja na viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano kwani kazi ya kutumbua majipu waliyoianzisha ina mitihani mikubwa.

“Kutokana na maombi yenu kwa viongozi wakuu wa kitaifa nina imani Taifa hili litafika tunakotaka liende. Endeleeni kutuombea kwa sababu kazi ya kutumbua majipu ina mitihani mikubwa. Lakini pia napenda niwahakikishie kuwa Serikali hii itatumbua majipu hayo kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa. Hakuna mtu ambaye ataonewa,” alisisitiza Waziri Mkuu.

Kuhusu mgogoro wa kiwanja cha kanisa hilo kilichopo eneo la Ipagala, Waziri Mkuu aliahidi kulishughulikia suala lao Jumatatu( leo ) asubuhi kabla hajaondoka kurejea Dar es Salaam. 

“Kesho ( leo) asubuhi nitamuita Mkurugenzi Mkuu wa CDA na kumtaka anipe taarifa sahihi kuhusu mgogoro huu. Najua suala hili liko mahakamani, lakini naamini Mkurugenzi anaweza kuwa kiungo kizuri kati ya wananchi waliojenga eneo hili pamoja na kanisa ambao mnamiliki kiwanja husika”.

“Kama atapata eneo jingine na kupima viwanja, kisha akawapatia hawa wananchi anaweza kuwa amesaidia kuondoa mgogoro huu. Wananchi walienda mahakamani huku wakijua eneo lenu limewekewa uzio, sasa wanagoma kutoka kwa sababu hawana mahali pa kwenda,” aliongeza.

Mapema, akitoa hotuba yake, Askofu Mkuu Dk. Mwakipesile alisema kanisa litaendelea kuiombea Serikali ya awamu ya tano ili nchi idumu katika amani na utulivu.

Aligusia eneo la kanisa lililopo kiwanja na 34, kitalu ‘E’, Ipagala East, Dodoma, ambalo ujenzi wa shule yake umesimama kutokana na mgogoro baina yao na wananchi waliovamia eneo lao kwa kujenga nyumba za kuishi licha ya kuwa eneo hilo lilikwishawekewa uzio.

“Kama kanisa tumeshindwa kukamilisha ujenzi wa shule kwa sababu wananchi hao walifungua kesi mahakamani kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa. Tunaomba uamuzi wa kesi hii uharakishwe,” alisema huku akishangiliwa.

Alisema kanisa hilo lina majengo 4,670 nchini kote na viwanja 420 ambavyo ni vya kujenga makanisa na vituo vya kutoa huduma mbalimbali za kijamii.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Dk. Mwizarubi alisema katika risala yake kwamba wanaiomba Serikali ifikirie kushusha bei ya vifaa vya ujenzi ili wananchi waweze kuwa na nyumba bora za kuishi.

“Maisha bora maana yake ni kuwa na nyumba bora. Tunaiomba Serikali yako ipunguze bei ya vifaa vya ujenzi ili Watanzania waweze kuwa na makazi bora,” alisema huku akishangiliwa.

Serikali Yawalipa Makandarasi Bilioni 400.....Yawataka Waliosimamisha Kazi Warudi 'Site' Haraka

$
0
0

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amewataka Makandarasi waliosimamisha kazi za ujenzi wa barabara nchini kuendelea na ujenzi baada ya Serikali kuanza kuwalipa madai yao.

Akizungumzamara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani yenye urefu wa kilomita 48.6 Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro, Prof. Mbarawa alisema tayari Serikali imeshalipa makandarasi mbalimbali nchini shilingi bilioni 400 na itaendelea kufanya hivyo ili kumaliza madeni yao kwa haraka.

“Hakikisheni mnarejea kazini na kuwapa mikataba ya ajira wafanyakazi wenu katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa ili ujenzi wa barabara na madaraja ukamilike kwa mujibu wa mkataba na hivyo kuondoa usumbufu kwa watumiaji wa barabara hii”, alisema Prof Mbarawa.
 
Profesa Mbarawa amemhakikishia mkandarasi China Civil Engineering Construction Corporation anayejenga barabara ya Magole-Turiani kuwa tayari serikali imeshamlipa zaidi ya kiasi cha dola za kimarekani zaidi ya laki 735 na Shilingi za kitanzania zaidi ya Milioni 795 hivyo ni wakati wa kukamilisha ujenzi huo hususan sehemu za madaraja kabla ya mvua za masika kuaanza.

Akizungumza katika ukaguzi huo Mbunge wa Mvomero Mhe. Sadick Murad ameiomba Serikali kumalizia daraja la Diwale lenye urefu wa mita 75 ili liweze kupitika.

Katika hatua nyingine Waziri Prof. Mbarawa alikagua karakana ya ujenzi wa vichwa vya treni mjini Morogoro na kumtaka mkandarasi anayekarabati vichwa hivyo kufanya kazi hiyo kwa haraka na kutoa kazi nyingine kwa watanzania ili kuwajengea uwezo wa kazi hizo.
 
Amewataka wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Kufanya kazi kwa ubunifu, uadilifu na uwazi ili kufufua hadhi ya Shirika hilo ambalo ni muhimu kwa uchumi wa nchi hii.

Alisema takribani asilimia 96 ya mizigo inayoshushwa katika Bandari ya Dar es salaam husafirishwa kwa njia ya barabara hivyo ni jukumu la TRL kuhakikisha inapata mizigo ya kutosha ya kusafirisha ili kupunguza mizigo hiyo kusafirishwa na barabara lakini kufufua uchumi wa TRL na taifa kwa ujumla.

“Fanyeni kazi kwa bidii, uwazi na kwa kushirikiana ili kujenga Shirika la Reli la kisasa lenye uwezo wa kujitegemea acheni vitendo vya hujuma na migomo vinavyoweza kudhoofisha shirika hili”, alisisitiza Prof. Mbarawa.

Naye Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani alikemea vitendo vya wizi wa mafuta na kuhujumu Reli vinavyofanywa na watumishi wasio waaminifu na kuwataka kuwa wazalendo kwa nchi yao ili kuchochea kasi ya maendeleo.

Profesa Mbarawa alikuwa kwenye ziara ya kukagua utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano ambapo alipata fursa ya kukagua ujenzi wa mizani ya kisasa ya Mikese na kituo cha mtandao wa mawasiliano ya simu vijijini ya Halotel unaosambazwa katika taasisi za Serikali ikiwemo Hospitali, Polisi, Mahakama na Shule hapa nchini.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Februari 8

Jaji Damian Lubuva Amtaka ' Lowassa' Aache Kuupotosha Umma

$
0
0

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji Damian Lubuva amewataka wanasiasa walioshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu waache kujitangaza kuwa walishinda, akisema wanapotosha wananchi.

Kauli hiyo ya Jaji Lubuva imekuja siku chache baada ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa kudai kuwa kama si matokeo kuchakachuliwa, alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kwa sababu wananchi walishaichoka CCM na wakawa wanataka mabadiliko.

Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalum na waandishi wa habari ofisini kwake, akisema yeye na Ukawa walishinda kwa kishindo isipokuwa matokeo yalivurugwa makusudi ili CCM iendelee kubaki madarakani.

Jana, akiwa kwenye mkutano wa tathmini kati ya NEC na asasi za kiraia kuhusu utoaji elimu kwa mpigakura uliofanyika Dodoma, Jaji Lubuva alisema uchaguzi umeshapita na kilichobaki sasa ni kufanya kazi tu.

Bila ya kutaja jina la mwanasiasa huyo, Jaji Lubuva alisema kama kuna mtu alishindwa katika uchaguzi uliopita, ajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020.

“Hata wananchi wanawashangaa kwa kuwa wao ndio walioamua ni nani anafaa kuwaongoza,” alisema Jaji Lubuva.

Alisema kuwa NEC ilikuwa inapokea matokeo ya uchaguzi kutoka majimboni na kuyasoma kama yalivyotumwa na katika hilo hakuna wakala hata mmoja wa chama ambaye aliyapinga matokeo hayo.

“Sasa nashangaa kuna baadhi ya wagombea wanaotaka Tume ifukuzwe kazi eti tu kwa sababu wao hawakushinda. Naomba ifahamike kwamba katika kila uchaguzi duniani kuna kushinda na kushindwa.

"Sasa kama kila atakayeshindwa atataka tume ifukuzwe kazi hapatakuwa na tume ya uchaguzi kwa sababu kila atakayekuwa anashindwa atakuwa anataka tume ifukuzwe kazi,” alisema Jaji Lubuva.

Chadema, ambayo iliungana na vyama vitatu kuunda Ukawa, iliitaka NEC kusitisha utangazaji matokeo ikidai kuwa kilichokuwa kikitangazwa ni tofauti na takwimu walizokusanya kutoka majimboni. Lakini NEC ikaendelea kutangaza.

Baadaye, Chadema ililalamika ikidai kituo chao cha kukusanya na kujumlisha matokeo kilivamiwa na polisi na kompyuta kuchukuliwa na hivyo kuvuruga ufuatiliaji wao wa matokeo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa huduma kutoka NEC, Emmanuel Kavishe alisema kuwa Tume inafanya kazi kwa mujibu wa sheria na Katiba na kwamba hata siku moja haijawahi kumpendelea au kumuonea mtu yeyote.

Katika uchaguzi wa urais, John Magufuli alipata kura milioni 8.8 huku Lowassa akipata milioni 6.07.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images