==>Wewe ni kijana wa kitanzania ?
==>Unataka kuongeza kipato chako ?
Kama jibu lako ni NDIO basi hii ni HABARI NJEMA SANA KWAKO. Taasisi ya NEEMA INSTITUTE OF N.G.O MANAGEMENT kupitia MRADI WA UANZISHAJI, UENDESHAJI NA USIMAMIZI WA BIASHARA NDOGONDOGO inatangaza nafasi za kushiriki katika SEMINA YA UJASIRIAMALI. Somo litakalo fundishwa ni
UTENGENEZAJI WA PIPI ZA KIHINDI.
Pipi za Kihindi ni bidhaa inayo pendwa sana na watoto wa shule ya msingi na hata sekondari.
Washiriki katika Semina hii, watapewa nafasi za biashara katika shule mbalimbali za msingi zilizopo jijini Dar Es Salaam.
ADA YA KUSHIRIKI KATIKA SEMINA HII NI SHILINGI ELFU HAMSINI TU (Tshs.50,000/=)
Fomu za kujiunga katika semina hii, zinapatikana ofisini kwetu kwa gharama ya Shilingi ELFU KUMI NA TANO TU( Tshs.15,000/=).
Tunapatikana UBUNGO Dar Es Salaam, jirani na Shule Ya Msingi Ubungo National Housing nyuma ya jengo la Ubungo Plaza.
Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 30 JANUARY 2016 saa nane kamili mchana.
Semina itafanyika kwa siku tano, kuanzia tarehe 01 Februari 2016 hadi tarehe 05 February 2016.
FAIDA ZA KUSHIRIKI KWENYE SEMINA KUHUSU MAFUNZO YA UTENGENEZAJI WA PIPI ZA KIHINDI.
Taasisi ya Neema Institute Of N.G.O Management yenye ofisi zake jijini Dar Es Salaam, katika eneo la Ubungo imeandaa SEMINA KUHUSU UTENGENEZAJI WA PIPI ZA KIHINDI ambayo itafanyika kwa muda wa siku tano, kuanzia tarehe 01 FEBRUARY 2016 hadi tarehe 05 FEBRUARI 2016.
Lengo la semina hii ni kuwasaidia wajasiriamali wadogo wadogo na wale wa kati, kupata ujuzi utakao wasaidia kuongeza vipato vyao.
Zifuatazo ni faida za kushiriki katika semina hii:
1.Mafunzo yanafundishwa kwa njia ya nadharia na vitendo ( Theory and Practical )kila siku kwa siku zote tano za mafunzo . Katika siku zote tano utakazo hudhuria mafunzo haya, utapata kujifunza kwa vitendo jinsi ya kutengeneza pipi za kihindi. Lengo letu ni kuhakikisha kila anaye shiriki katika semina hii, anatoka akiwa amewiva katika suala zima la utengenezaji wa pipi.
2. NI BIDHAA YENYE SOKO LA UHAKIKA :
Pipi za kihindi ni pipi zinazo tengenezwa kwa kutumia malighafi iitwayo sukari guru pamoja na viambatano (ingredients ) vingine . Pipi hizi ni bidhaa inayo pendwa sana na watoto wanao soma katika shule za msingi na sekondari . Kwa muda mrefu sasa, wahindi wanajulikana dunia nzima kwa kuwa na umahiri mkubwa wa kutengeneza vitu vitamu tamu pamoja na vyakula vizuri kwa ujumla. Hivyo basi suala la pipi za kihindi.
Utafiti wetu umetuwezesha kugundua, kwa biashara ya kuuza pipi za kihindi mashuleni, unaweza kuingiza faida ya kati ya shilingi Elfu Thelathini ( Tshs.30,000/=) hadi Shilingi Elfu Themanini (Tshs.80,000/=) kwa siku, kutegemeana na kiwango cha uzalishaji wako.
Na kama utapata nafasi katika shule zaidi ya moja, kipato chako kitakuwa kikubwa maradufu.
3.UHAKIKA WA KUPATA NAFASI YA BIASHARA KWENYE SOKO LA UHAKIKA .
Baada ya kuhitimu mafunzo, kila mshiriki, atapewa nafasi ya biashara katika shule ya msingi yenye idadi kubwa ya wanafunzi iliyopo jijini Dar Es Salaam na hivyo kumuwezesha kutengeneza kipato cha uhakika, kupitia biashara ya pipi za kihindi. Sisi kama Taasisi tunazo nafasi zaidi ya mia ( 100 ) katika shule mbalimbali za msingi zilizopo jijini Dar Es Salaam zenye idadi ya wanafunzi kati ya mia nne (400) hadi elfu moja (1000).
Nafasi hizi za biashara tutazitoa kwa watakao hitimu mafunzo yetu.
Nafasi hii utaipata baada ya kumaliza mafunzo. Mafunzo yanaanza Jumatatu na kuisha Ijumaa. Siku hiyo hiyo ya Ijumaa unapewa details za shule utakayo enda kufanyia biashara yako, Jumamosi na Jumapili, unazitumia kufanya maandalizi ya kutengeneza pipi zako, na Jumatatu unaanza kuingiza pesa kupitia shughuli ya kuuza pipi kwenye shule ambayo tutakuwa tumekupangia.
( FURSA YA KUPATA NAFASI YA BIASHARA INAWAHUSU WALIOPO DAR ES SALAAM TU )
4.MTAJI MDOGO WA BIASHARA : Mradi wa kutengeneza na kuuza pipi za kihindi mashuleni, hauhitaji kiasi kikubwa cha fedha za mtaji. Hata kwa wajasiriamali ambao ndio kwanza wanaanza ujasiriamali na hawana uwezo mkubwa wa kifedha wanaweza kumudu.
5.UTAPATA FURSA YA KUUNGANISHWA NA WAJASIRIAMALI WENZAKO NA KUUNDA TAASISI ISIYO KUWA YA KISERIKALI.
Washiriki wa mafunzo haya, wataunganishwa pamoja na kuunda Taasisi isiyo kuwa ya kiserikali ( N.G.O ), ambapo wata saidiwa kuanzisha VICOBA pamoja na kufundishwa utengenezaji wa bidhaa nyinginezo zinazo pendwa sana na watoto mashuleni kama vile Ubuyu wa Zanzibar nakadhalika.
6.SEMINA INATOLEWA KWA MUDA AMBAO HAUWEZI KUHARIBU RATIBA YAKO.
Kutakuwa na madarasa ya asubuhi pamoja na madarasa ya jioni. Madarasa ya asubuhi yanaanza saa nne hadi saa sita. Na madarasa ya jioni yanaanza saa kumi hadi saa kumi na mbili Hivyo basi kama wewe ni muajiriwa na hauna nafasi muda wa asubuhi, unaweza kupata fursa ya kushiriki katika semina hii wakati wa jioni kuanzia saa kumi hadi saa kumi na mbili.
7.UNAWEZA KUJIFUNZA KUTENGENEZA PIPI ZA KIHINDI NA UKAAJIRI VIJANA WENGI WA KAZI NA KUTENGENEZA FEDHA MARADUFU.
Unaweza kujifunza kutengeneza pipi hizi, halafu ukatafuta nafasi ya biashara kwenye shule mbalimbali za msingi na kuwaweka vijana wa kazi. Ukipata nafasi katika shule nyingi, maana yake hata kipato chako kitaongezeka mara dufu.
Hizo ni baadhi ya faida za kushiriki katika mafunzo haya.
KWA WALIOPO NJE YA MKOA WA DAR ES SALAAM.
Kwa waliopo nje ya mkoa wa Dar Es Salaam, mafunzo haya yatatolewa kwa njia ya Posta. Utapatiwa DVD na VITABU vinavyo elezea STEP by STEP kuhusu namna ya KUTENGENEZA PIPI ZA KIHINDI.
JINSI YA KUJIUNGA NA MAFUNZO HAYA KWA WAOMBAJI KUTOKA NJE YA DAR ES SALAAM.
Kama upo nje ya mkoa wa Dar Es Salaam, na unataka kushiriki katika mafunzo haya, tuandikie barua pepe ya maombi ya kushiriki katika mafunzo haya. Barua pepe yetu ni : neemainstitute@gmail.com
Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 30 JANUARY 2016.
EWE MZAZI ! EWE MLEZI ! UNA NGOJA NINI ?
MLETE KIJANA WAKO APATE MAFUNZO YATAKAYO MSAIDIA KUINGIZA KIPATO CHAKE.
EWE KIJANA! ZAMA ZA KUAJIRIWA ZIMEPITWA NA WAKATI. USISUBIRI KUAJIRIWA. NJOO UPATE UJUZI UTAKAO KUSAIDIA KUINGIZA KIPATO KIZURI