Mashabiki wa Diamond Platnumz hawajaipenda picha yake inayomuonesha akionesha kidole cha kati aka ‘the middle finger’.
“Is this the right finger that you are talkin about @roma2030
…?” ameandika kwenye picha ya Instagram aliyopiga na rapper Roma
Mkatoliki
Hata hivyo picha hiyo imevuta hisia za mashabiki wenye hasira
waliomwangushia mvua ya madongo kwenye Instagram ambapo ana followers
Diamond apewa mvua ya matusi baada ya "kuwatia dole" mashabiki wake....
↧
↧
Mwanamke ajilipua kwa petroli baada ya mumuwe kuoa mke wa pili huko Geita.
<!-- adsense -->
MWANAMKE mmoja ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nyankumbu, Kata ya
Kalangalala mkoani Geita amenusurika kifo baada ya kujimwagia mwilini
mafuta ya petroli kisha kujilipua baada ya mumewe kuoa mke wa pili.
Imeelezwa
kuwa mwanamke huyo, Anastazia Kubezya (28) Agosti 8 mwaka huu aliamua
kujimiminia petroli mwili mzima kabla ya kuchukua kiberiti na kujilipua,
hali
↧
Mh. Wenje atiwa mbaroni kwa kuongoza maandano ya CHADEMA jijini mwanza
↧
Serikali yakanusha kuwa Mama Salma Kikwete si Mnyarwanda na wala Kikwete si shemeji yao
Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO
Assah Mwambene leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara hiyo amekanusha taarifa
zilizoandikwa kwenye mtandao wa News for Rwanda na wanyarwanda kuwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni shemeji wa aliyekuwa
Rais wa Rwanda Juvenal
↧
Basi la Turu lachomwa moto na wanakijiji....Abiria 60 wamenusurika
Abiria
wapatao 60 waliokuwa wanasafiri na basi la Turu linalofanya safari zake
kati ya mkoa wa Singida na Haidom mkoani Manyara, wamelazimishwa
kuteremka toka ndani ya basi hilo na wananchi zaidi ya mia mbili ( 200 )
wa vijiji vitatu, na kisha kulichoma moto basi hilo.
Taarifa
toka eneo la tukio zinasema wananchi hao ni wa vijiji vya Singa,
Idabagadu na Nkungi mkoani Singida, ambao baada
↧
↧
Kilichomfanya mbuge Wenje atiwe mbaroni ni Uchochezi
SIKU moja baada ya Jeshi la Polisi mkoani hapa kulazimika
kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wananchi na wafuasi wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), waliokuwa wakiandamana kutoka
Uwanja wa Furahisha kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, mbunge wa Nyamagana
jijini Mwanza, Ezekiel Wenje (CHADEMA), amekamatwa akituhumiwa kutenda
makosa mawili.
Wenje alishikiliwa jana
↧
Godbless Lema augua ghafla, kesi yake yaahirishwa
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha jana imeshindwa kuanza
kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini,
Godbless Lema, dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, kutokana
na mbunge huyo kuwa mgonjwa.
Wakili wa Lema, Method Kimomogoro, aliieleza mahakama hiyo mbele
ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, anayesikiliza shauri hilo kuwa Lema
anaumwa na alikuwa amelazwa
↧
DIAMOND PLATNUMZ ATAJWA SAKATA LA UNGA, AHUSISWA NA MTANDAO WA MASOGANGE
KWA mara ya kwanza tangu lilipoibuka sakata la watu maarufu kujihusisha
ama na utumiaji au usafirishaji wa dawa za kulevya, jina la mwanamuziki
anayeaminika kuwa na ukwasi mkubwa kwa sasa hapa nchini, Nasseeb
Abdulmaliki, maarufu zaidi kwa jina la Diamond, limeanza kutajwa kuwa ni
miongoni mwa vigogo wa ‘unga.’Tayari mjadala mkubwa wa chini
chini umeibuka kwa watu mbalimbali wakiwemo
↧
MAMBO 100 USIYOYAJUA KUHUSU CHOKOCHOKO ZA RWANDA KWA TANZANIA.....
Historia ya Rwanda ni ndefu iliyojaa misukosuko ya
kisiasa, kupinduana, vita na mauaji ya wenyewe kwa wenye
yaliyosababishwa na ubaguzi wa kikabila.
Rwanda imekuwa ikipita katika vipindi vigumu na
vya hatari. Vipindi hivi hufuatana na mauaji ya raia wa nchi hiyo, sio
tu kutokana na sababu za ukabila bali pia uongozi mbaya wa kisiasa.
↧
↧
HII NDO KAULI YA DIAMOND BAADA YA KUHUSISHWA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA
Msanii Wa Muziki wa Bongofleva mwenye
jina kubwa Town na mwenye Mkwanja mkubwa hapa nchini Nasseeb Abdulmaliki“Diamond” amejitokeza na kukanusha kuwa hahusiki na biashara ya madawa
ya kulevya.
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na
taarifa za Diamond kujihusisha na biashara hiyo hasa kutokana na ukaribu
wake na wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya wenye maskani yao
nchini Afrika
↧
RAIS KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA MAKATIBU WAKUU NA MANAIBU WAKE....
Imeandikwa na Na Magreth Kinabo na Eleuteri Mangi — RAIS
Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya uongozi katika ngazi za juu za
utendaji wa Serikalini kwenye nafasi za Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu
Wakuu katika Wizara mbalimbali, ambapo wapo waliohamishwa,
wataopangiwa kazi nyingine na yumo anayestaafu.Kauli hiyo
ilitolewa leo jioni na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue wakati
↧
MFANYABIASHARA ALIYEJIREKODI AKIMLAWITI MFANYAKAZI WA DUKANI AKAMATWA
JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro limemkamata mfanyabiashara
mashuhuri wa mjini Moshi, Totolii Kimath anayedaiwa kurekodi mkanda wa
video ukimwonyesha akimlawiti mfanyakazi wake wa dukani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, aliliambia
Tanzania Daima kuwa kijana huyo ambaye anamiliki maduka ya kuuza na
kutengeneza CD katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini
↧
VIDEO TATU ZA MFANYABIASHARA WA MOSHI AKIMLAWITI MFANYAKAZI WA DUKANI....
<!-- adsense -->
JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro limemkamata mfanyabiashara mashuhuri wa mjini Moshi, Totolii Kimath anayedaiwa kurekodi mkanda wa video ukimwonyesha akimlawiti mfanyakazi wake wa dukani.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz amedai kuwa kijana huyo ambaye anamiliki maduka ya kuuza na kutengeneza CD katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini Moshi, alikamatwa
↧
↧
RWANDA NA UGANDA WAJITOA BANDARI YA DAR ES SALAAM
Chama cha Wasafirishaji wa Mafuta
Tanzania (Tatoa), kimesema Rwanda na Uganda zitajitoa kutumia Bandari ya
Dar es Salaam kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu.
Katibu Mtendaji wa Tatoa, Zacharia
Hanspope aliwaambia waandishi wa habari jana baada ya kukutana na Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi hizo zinajitoa kutokana na
matatizo mbalimbali ambayo kwa muda mrefu zimekuwa
↧
POLISI FEKI 7 WANASWA TENA....
SIKU chache baada ya kukamatwa kwa askari feki wa usalama barabarani, Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imewakamata watuhumiwa saba wa ujambazi, wakiwa na sare za Polisi, huku mwingine akijifanya ofisa Usalama wa Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaa, Suleiman Kova alisema watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na sare
↧
WATUMISHI WA ZAHANATI WATUHUMIWA KUFANYA MAPENZI NA WAGONJWA....
WATUMISHI wawili katika zahanati ya Mwanhala wilayani Nzega, wamekumbwa na kashfa ya kufanya mapenzi na wagonjwa hospitalini.
Kutokana na kashfa hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Bitun Msangi, ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa watumishi hao.
Agizo la mkuu huyo limetolewa hivi karibuni, baada ya Diwani wa kata ya Utwigu, Sawaka Shita kuwalalamikia
↧
MKE AFUMANIWA AKIMSALITI MUMEWE CHOONI....
Mwanaume aliyetambulika kwa jina moja la Juma, mkazi wa Tegeta
A, Dar amejikuta akikamuliwa faini ya Sh. laki tano kufuatia kufumwa
ugoni na mke wa mtu.
Katika tukio hilo lililojiri
Kimara-King’ong’o, Dar, Jumapili iliyopita, Juma alifumaniwa na mke wa
mwanaume aitwaye Swai aliyetajwa kwa jina moja la Cesilia, mkazi wa
maeneo hayo.
Ilidaiwa kuwa Cesilia alimwachia mumewe mtoto na
↧
↧
TUNDAMAN AFANIKIWA KUWATOROKA POLISI AKIWA NUSU UCHI....KISA NI DENI LA LAKI NANE
Msanii Tundaman amejikuta
akiambulia aibu ya mwaka baada ya kujitosa nusu uchi mtaani
akiwakwepa askari polisi ambao walivamia kwake leo asubuhi kwa
lengo la kumkamata....
Chanzo cha Tunda man kusakwa na polisi ni deni la sh. laki
nane ambazo alikopa mwanzoni mwa mwaka huu kwa mwanadada mmoja (
jina kapuni)....
Taarifa zinadai kwamba, baada
↧
MKUU WA FFU - ARUSHA NA POLISI WENGINE WATATU WAFUKUZWA KAZI
Imeandikwa na Lydia
Churi — Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewavua
madaraka Maafisa wanne wa Jeshi la Polisi nchini na kumsimamisha kazi
mmoja ambaye atafunguliwa mashtaka ya kijeshi kutokana na kukiuka
maadili na taratibu za jeshi hilo.Akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri Nchimbi amesema hatua hiyo ni
katika kuendeleza vita ya
↧
WATU SABA WANUSURIKA KWA AJALI YA NDEGE ILIYOTUA ZIWA MANYARA
Ndege ndogo ya shirika la
Tanzanair iliyokuwa ikitokea mjini Bukoba mkoani Kagera kwenda Dar ss
Salaam imelazimika kutua kwa dharura katika ziwa Manyara baada ya injini
yake moja kuzimika ghafla ikiwa angani.
Ndege hiyo ilikuwa na abiria
sita na rubani mmoja ambapo wote wamejeruhiwa na kukimbizwa katika
Hospitali ya Seliani mjini Arusha kwa matibabu.
Chanzo: ITV
<!-- adsense -->
↧
More Pages to Explore .....