Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ofisa TAKUKURU Auawa Kinyama.....Acharangwa Mapanga, Wauaji Watoweka

0
0
OFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) mkoani Dodoma, Emmanuel Meta (37) ameuawa kufuatia kupigwa na kukatwa mapanga  cha watu ambao mpaka sasa hawajafahamika. Hata hivyo Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo. Tukio hilo lilitokea Januari 20, mwaka huu majira ya saa 6:15 usiku katika eneo la Area C manispaa ya Dodoma.

Makusanyo ya Halmashauri Nchini Yaongezeka kwa 800% Baada ya Kuanza Kutumia Mfumo wa Kielektroniki Kukusanya Mapato

0
0
Makusanyo ya mapato katika halmashauri nchini, yameongezeka kufikia asilimia 800 hadi 900 baada ya kuanza kutumika kwa mfumo wa kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki katika halmashauri 164. Hayo yalibainishwa jana na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma Jaffo alisema

Benard Membe Amkosoa Rais Magufuli.....Asema Hajapunguza Baraza la Mawaziri, Apingana na Sera yake ya Kufuta Safari Nje ya Nchi

0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali iliyopita, Bernard Membe ameungana na waziri mwenzake wa zamani, Dk Makongoro Mahanga kukosoa sera ya kubana matumizi ya Rais John Magufuli ya kudhibiti safari za nje na kuteua baraza dogo la mawaziri. Kama ilivyokuwa kwa Dk Mahanga, waziri huyo aliyedumu kwa miaka tisa kwenye Wizara ya Mambo ya Nje amesema kiuhalisia, Rais

Kampuni Ya UDA Yaikana Familia Ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

0
0
Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena ameeleza kusikitishwa na taarifa zisizo za kweli zinazoihusisha familia ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete na umiliki wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na kusisitiza kuwa yeye ndiye mmiliki halali. Kisena alidai kwa muda mrefu watu wenye nia mbaya dhidi yake, wamekuwa wakihoji umiliki wa shirika hilo licha ya kuonyesha

UKAWA wasusia Kamati za Bunge Na Kugomea Uchaguzi......... Zitto Kabwe awaponda wao na Serikali, Awafananisha na 'Manyumbu'.

0
0
Wakati vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge vikitarajiwa kuanza leo kwa uteuzi wa wajumbe, wabunge wa upinzani tayari wameanza kwa kumtikisa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai, baada ya kususia uchaguzi wa wenyeviti wa kamati hizo. Dalili za mgawanyiko kwenye kamati hizo zilianza kuonekana juzi, baada ya wabunge hao wa Kambi ya Upinzani kufanya kikao na kuweka msimamo wa

Picha: Rais Magufuli Atua Jijini Arusha Kwa Kishindo......Aahidi Kuendelea Kutumbua Majipu Hadi Yaishe

0
0
RAIS John Magufuli ametoa mwito kwa Watanzania kumuombea ili aendelee kuwashughulikia wote wanaofanya ubadhirifu wa fedha za umma kupitia kampeni yake ya kutumbua majipu. “Nataka niwahakikishieni kuwa nitaendelea kutumbua majipu yote mpaka yaishe, na naomba mniombee ili kazi hii ya kutumbua majipu ifanyike kwa mafanikio,” alisema Dk Magufuli. Alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa

Picha Za Rais Magufuli Akiwa Ndani Ya Sare Za Jeshi Wakati Akisalimiana na Wananchi wa Jiji la Arusha

0
0
Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt Magufuli akiwasikiliza wananchi kwa makini alipopita maeneno ya Sanawali kuwasalimia wakati akielekea Wilayani Monduli. Rais Magufuli akiwa amevalia sare za kijeshi amesimamishwa na kuwasalimu wananchi katika maeneo ya Sanawali, Tekniko, Ngarenalo, Mbauda, Majengo Na Kisongo Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli

Rais Magufuli Asema Hataki Kusikia Malalamiko ya Wananchi juu ya Suala la Njaa......Ikitokea Akasikia, Mkuu wa Mkoa Atafukuzwa Kazi

0
0
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amesema kuanzaia sasa hataki kusikia malalamiko ya wananchi juu ya suala la njaa na ikitokea akasikia vilio hivyo vikiendelea mkuu wa mkoa husika atachukuliwa hatua ikiwemo ya kufukuzwa kazi.   Mh. Magufuli ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani Arusha ameyasema hayo alipokuwa njiani kutoka jijini Arusha kwenda wilaya Monduli

Breaking News: Baraza la Mitihani ( NECTA ) Latangaza Matokeo ya Darasa la Nne....... Bofya Hapa Kuyaona

0
0
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), limetangaza matokeo ya mitihani ya kujipima ya darasa la nne huku matokeo hayo yakionyesha wanafunzi wengi wamefeli katika somo la Kiingereza kwa asilimia 65.67 katika mitihani hiyo iliyofanyika mwishoni 2015. Akitangaza matokeo hayo leo Jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt. Charles Msonde amesema juhudi za makusudi zinahitajika

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Atangaza Rasmi Tarehe ya Kurudiwa kwa Uchaguzi Mkuu

0
0
TUME ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imetangaza kwamba uchaguzi wa marudio utafanyika Machi 20 mwaka huu na kuwataka wagombea wote walioshiriki katika uchaguzi uliofutwa wa Oktoba 25 mwaka jana, kujiandaa kushiriki uchaguzi huo. Mwenyekiti wa Zec, Jecha Salim Jecha ametoa tamko hilo leo na kuongeza kuwa uchaguzi huo, utahusu nafasi ya Rais wa Zanzibar, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Januari 23

Rais Magufuli Afunga Zoezi la Onesha Uwezo Medani Chuo cha Kijeshi Monduli Mkoani Arusha....Atoa Ajira Za Papo Kwa Papo Kwa Waliofanikisha

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunga “Zoezi la Onesha Uwezo Medani” lililoandaliwa na kutekelezwa na Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu ambalo ni sehemu ya Jeshi la wananchi Tanzania katika eneo la Lang’arurusu nje kidogo ya Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani Arusha. Akizungumza na Askari na Maafisa wa Jeshi la wananchi Tanzania kabla ya kufunga zoezi

Simbachawene Aapa Kuweka Historia Mpya .....Asema Ndani Ya Miaka Miwili Hakuna Mwanafunzi Atakaye Kaa Chini Kwa Kukosa Dawati

0
0
Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene amesema atahakikisha shule zote hapa nchini zinakuwa na madawati yanayofanana. Alisema hayo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari kuzungumzia changamoto za elimu bila malipo iliyoanza kutolewa Januari mwaka huu. “Katika historia ninayotaka kuandika ni kuhakikisha hakuna

Sarakasi Zaanza Tena Umeya Dar es Salaam

0
0
HALMASHAURI ya jiji la Dar es Salaam imeahirisha uchaguzi wa meya wa Jiji uliokuwa ufanyike leo, mpaka hapo tarehe itakapotangazwa baadaye. Mkuu wa Kitengo cha Itifaki na Uhusiano na Umma wa Jiji, Gaston Makwembe alisema uchaguzi huo uliokuwa ufanyike leo saa nne asubuhi katika ukumbi wa Mmikutano wa Karimjee, umeahirishwa. Alisema tarehe ya uchaguzi huo itapangwa baadaye na taarifa

Ahukumiwa Miaka Mitano Jela Kwa Kuiba Mbuzi Mmoja

0
0
MKAZI wa kitongoji cha Ilembo katika mji mdogo wa Vwawa wilayani Mbozi mkoani Mbeya, Patrick Moses (19) amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitano jela baada ya kukutwa na hatia ya wizi wa mbuzi mmoja mwenye thamani ya Sh 85,000. Hukumu hiyo imetolewa juzi na Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini, wilayani Mbozi ambapo Hakimu wa Mahakama hiyo, Lazima Mwaijage alisema ametoa hukumu hiyo kwa

Nape Nnauye: Kasi Ya Rais Magufuli Itaviua Vyama Vya Upinzani Hapa Nchini

0
0
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amesema kasi ya utendaji kazi ya Rais John Magufuli inaweza kuua uwepo wa vyama vya upinzani nchini. Hata hivyo alisema kuwa hangependa upinzani ufe kwa vile hiyo pia itakuwa imeua demokrasia nchini na kudai kuwa lengo la kuanzisha vyama vya siasa haikuwa kuviua bali ni kuviona vikiendelea kuwepo. Kauli hiyo

Amiri Jeshi Mkuu Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Atunuku Kamisheni Kwa Maafisa Wapya 205 Wa Jeshi La Wananchi

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Januari, 2016 ametunuku kamisheni kwa Maafisa wapya 205 wa jeshi la wananchi kundi la 57/15 katika Chuo cha mafunzo ya kijeshi (TMA) Monduli Mkoani Arusha.

Maafisa hao wapya wametunukiwa cheo cha Luteni Usu, ambapo kati yao 16 ni maafisa wanawake, na 189 ni maafisa wanaume.

Aidha, miongoni mwa maafisa wapya 205 waliotunukiwa kamisheni, maafisa 10 wametoka majeshi rafiki kutoka nchi za Uganda, Kenya na Burundi.

Akiwa katika uwanja wa paredi wa chuo hicho Rais Magufuli amepokea heshima zote za kijeshi ikiwemo kupigiwa wimbo wa Taifa na kukagua gwaride rasmi lililojumuisha maafisa hao wapya.

Baada ya kutunukiwa kamisheni, Maafisa wapya wa jeshi wamekula kiapo na wametoa heshima kwa gwaride lililopita mbele ya Rais kwa mwendo wa pole na mwendo wa haraka.

Viongozi wengine waliokuwepo katika tukio hilo ni pamoja na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange, Maafisa wa ngazi za juu jeshini na Maafisa wastaafu, viongozi wa mkoa na wilaya na wakufunzi kutoka nje ya nchi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kutoa kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la wananchi tangu achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Oktoba Mwaka jana.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Arusha.
23 Januari, 2016.

Watu wawili Wafariki Dunia na Wengine 36 Wajeruhiwa katika Ajali ya Basi la BM Morogoro.

0
0


Watu wawili wamefariki dunia na wengine 36 kujeruhiwa, kati yao wanne vibaya baàda ya basi walilokuwa wakisafiria kutokea jijini Dar es Salaam kuelekea Morogoro, mali ya kampuni ya BM kuligonga ubavuni lori lililokuwa likija mbele yake na kuangukia kwenye bonde pembeni ya barabara na kupinduka mara nne, katika eneo la Lubungo Mikese, barabara  kuu ya Morogoro-Dar es Salaam.


Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo akizungumzia ajali hiyo, amesema chanzo ni mwendo kasi na imetokea majira ya saa 3:30 usiku wa kuamkia leo  ikihuhusisha basi la mwisho kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Morogoro, mali ya kampuni ya BM, baada ya dereva wake kufika Lubungo eneo lenye kona na mteremko mkali, na akiwa mwendo kasi, kukutana mbele na lori likiwa na tela, likitokea uelekeo wa Morogoro kuelekea Dar es Salaam, likiwa linamalizia kupita lori jingine lililokuwa limeegesha barabarani baàda ya kuharibika, ambapo dereva wa basi aligonga tela la lori hilo lililokuwa kwenye mwendo na kukosa uelekeo na kupindukia bondeni na kusababisha vifo na majeruhi hao. 


CUF Wakutana Kujadili Kurudiwa Uchaguzi Zanzibar

0
0

CHAMA cha Wananchi CUF kimeitisha vikao vya juu vya kitaifa vya Chama ili kujadili marudio ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliotangazwa kurudiwa Machi 20, 2016 na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Katika taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa CUF, Ismail Jussa, imesema kuwa vikao hivyo vitafanyika Januari 27 na 28 mwaka huu, na ndivyo vitakavyotoa msimamo rasmi wa CUF.

Ifuatayo ni taarifa kamili ya Jussa.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kufuatia tangazo jengine la kihuni lisilozingatia Katiba wala Sheria la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kutangaza tarehe 20 Machi, 2016 kwamba ni siku ya kile anachokiita uchaguzi wa marudio Zanzibar, Chama Cha Wananchi (CUF) kimeitisha vikao vya juu vya kitaifa vya Chama ili kujadili suala hilo na kutoa msimamo rasmi wa Chama.

Kamati ya Utendaji ya Taifa itakutana Jumatano, tarehe 27 Januari, 2016 na kufuatiwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa litakalokutana Alhamis, tarehe 28 Januari, 2016. Vikao hivyo vitafanyika Ofisi Kuu ya Chama, mjini Dar es Salaam.

Chama kinatoa wito na kuwanasihi Wazanzibari wote waliochoshwa na utawala wa kibabe na wa kidikteta wa CCM na ambao walikikataa chama hicho kwa kishindo tarehe 25 Oktoba, 2015 kuendelea kutunza amani na kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu na kusubiri maamuzi ya chama chao wanachokiamini.

HAKI SAWA KWA WOTE
ISMAIL JUSSA
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI NA MAWASILIANO

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili Ya Leo Januari 24

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images