Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde amebaini kuwepo kwa wafanyakazi wa kigeni, walioletwa na kampuni za simu za mkononi kufanya kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania ikiwemo kufunga meza na viti vya kukalia.
Aidha, amebaini kuwepo kwa baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya simu ya Halotel, raia wa Vietnam, ambao wanaishi nchini bila
Kampuni Za Simu Zatozwa Faini Kwa Kuwapa AJIRA Raia Wa Kigeni Kinyume Cha Taratibu
↧
↧
Waziri Mkuu Atembelea Kambi za Wakimbizi Kigoma.....Awaonya Kutobeba Silaha Wanapoingia Nchini, Ataka walionazo wazisalimishe
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaasa raia wanaokimbia nchi zao na kupata hifadhi Tanzania kutobeba silaha wanapoingia nchini kuja kuishi kwenye kambi za wakimbizi.
Ametoa onyo hilo jana wakati akizungumza na mamia ya wakimbizi wanaoishi kwenye kambi za Nyarugusu na Nduta zilizoko wilayani Kasulu na Kibondo, mkoani Kigoma waliofika kumsikiliza kwenye mikutano ya hadhara iliyofanyika kwenye
↧
Lukuvu Aagiza Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kufanya kazi hadi Usiku, Abaini Urasimu Mkubwa Wizarani
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaagiza watumishi wa wizara hiyo katika kitengo cha huduma kwa wateja, kufanya kazi hadi usiku ili kuhakikisha wanawahudumia kwa muda wananchi wengi wanaofika katika kitengo hicho na kuondoka bila kupata huduma stahiki.
Waziri Lukuvi alitoa maagizo hayo jana alipofanya ziara katika kitengo hicho na kubaini kuwepo urasimu
↧
Polisi Ahukumiwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kubaka na Kumlawiti Mtoto
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, imemhukumu askari polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, G 9762 PC Daniel (24) kutumikia kifungo cha maisha jela, baada ya kupatikana na makosa ya kubaka na kumlawiti mtoto wa miaka 13.
Mbali na kifungo hicho, mtuhumiwa huyo ameamriwa kulipa fidia ya Sh milioni 2 ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo.
Hukumu hiyo
↧
TCRA Yazipiga Faini ya Milioni 25 Kampuni Za Simu ( Tigo,Halotel,Zantel na Airtel ) Kwa Kushindwa Kuwalinda Wateja Wake Kiteknolojia
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
HATUA ZA KISHERIA NA KIUDHIBITI KWA MAKAMPUNI YA SIMU YALIYOSHINDWA KULINDA WATEJA WAKE KITEKNOLOJIA NA KISHERIA KUHAKIKISHA USALAMA WA MAWASILIANO YAO
1. Katika shughuili zake za udhibiti wa huduma za mawasiliano nchini, Mamlaka ya Mawasilaino Tanzania imepokea malalamiko kutoka kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano dhidi ya kuwepo mazingira yasiyo
↧
↧
DART Yaonya Madereva Wazembe
Zikiwa zimesalia siku chache kabla ya mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) kuanza jijini Dar es Salaam, baadhi ya madereva wasio makini wameanza kuharibu miundombinu ya mradi huo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa jiji hilo.Uharibifu wa hivi karibuni kabisa kutokea unahusu basi lenye usajili T430 (YUTONG) ikiendeshwa na Abuu Nassar mali ya Kampuni ya Fashion Tourism Investment Limited
↧
Mbwana Samatta amtembelea Waziri Nape Ofisini Kwake.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta leo amekutana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Mh. Nape Nnauye kwenye ofisi ya Waziri huyo kwa ajili ya kumuaga kwa niaba ya serikali kabla ya kuelekea nchini Nigeria kuhudhuria sherehe za ugawaji wa tuzo za wachezaji bora wa Afrika.
Samatta amesema anatambua umuhimu wa mchango wa serikali katika kuchangia mafanikio
↧
Waziri Mkuu Aibua Ufisadi Kigoma......Atoa siku Mbili Kwa Katibu Tawala wa Mkoa Kukamilisha Uchunguzi ,Ataka Apewe Taarifa ya Maandishi Januari Mosi, 2016
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
ametoa siku mbili kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Eng. John
Ndunguru kukamilisha uchunguzi wake na kumpatia taarifa ya maandishi juu
ya tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma unaohusisha uuzwaji wa jengo la
KIGODECO na viwanja 12 vya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambao unadaiwa
kukiuka taratibu.
Ametoa agizo hilo leo mchana
(Jumatano, Desemba 30, 2015)
↧
Waziri Simbachawene Aagiza Afisa Biashara wa Halmashauri ya Dodoma Na Kaimu Wake Wasimamishwe Kazi Mara Moja!
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. George Simbachawene amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kuwasimamisha kazi mara moja Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa ya Dodoma Bw. Elias N. Kamara na Bibi Donatila D. Vedasto (Afisa Biashara) kuanzia leo tarehe 30/12/2015 kwa kosa la kusababisha urasimu katika utoaji wa leseni za biashara.
Kutokana na hali hiyo Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi
↧
↧
Nyumba 100 zawekwa X Jangwani, vurugu zatawala
Zoezi la uwekaji alama nyekundu katika zaidi ya nyumba 100 zinazotakiwa kubomolewa kwenye bonde la Mto Msimbazi, Jangwani limemalizika chini ya ulinzi mkali wa polisi baada ya vurugu za wananchi kuigomea serikali katika zoezi hilo.
Zoezi hilo lililoanza jana majira ya saa nne asubuhi likiongozwa na Mwanasheria wa NEMC, Machare Heche lilisababisha vurugu zilizotokana na wananchi kukataa
↧
Sasa ni Profesa Joyce Ndalichako na siyo "Dokta" tena
WIZARA ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, imefafanua
kuwa sifa ya kitaaluma ya waziri wa wizara hiyo ni Profesa Joyce
Ndalichako; na siyo Dk Joyce Ndalichako.
Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam juzi na Kitengo cha Mawasiliano
Serikalini cha wizara hiyo, ilisema tangu alipoteuliwa kushika wadhifa
huo wiki iliyopita, kwa bahati mbaya sifa ya kitaaluma ya waziri
↧
Rais mstaafu Kikwete, Waziri Lwenge wakagua mitambo ya maji Wami, Chalinze
Rais
mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete (katikati), akizungumza na
Waziri wa Maji, Gerson Lwenge wakielekea kukagua mitambo ya kusafisha na
kusafirisha maji Wami, katika Halmashauri ya Mji wa Chalinze, mkoani
Pwani, Desemba 30, 2015.
Rais Jakaya Kikwete na Lwenge wakiangalia mitambo ya kusafisha maji
Wakiwa katika picha ya pamoja
Rais
mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya
↧
Waziri Wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu Atembelea MSD...... Aahidi Kuwa Balozi Wao Na Kuwatatulia Changamoto Zinazowakabili Ikiwepo Deni Wanaloidai Serikali
Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu jana alitembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD) na kuahidi kuwa balozi wa kuhakikisha deni la serikali linalipwa ili kuiwezesha MSD kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Waziri huyo alieleza hayo baada ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu kueleza kuwa ukosefu wa fedha na deni la serikali ni
↧
↧
NAPE: 60% ya Muziki utakaochezwa katika vyombo vya habari lazima uwe wa nyumbani
Wakati baadhi ya wasanii na wadau mbalimbali wa burudani nchini wakiendelea kuwa na hofu juu ya mfumo mpya unaovitaka vituo vya redio na runinga kuwalipa wasanii mirahaba inayotokana na kucheza kazi zao, serikali imesema imeunda sheria ambayo itavifanya vishindwe kuepuka kucheza nyimbo za wasanii wa ndani.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa filamu ya ‘Home Coming’ Mlimani City jijini Dar es
↧
71 Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Uhalifu
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limesema limewakamata watu 71, silaha nne na dawa za kulevya katika oparesheni ya mwishoni mwa mwaka.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi Kanda hiyo, Suleiman Kova alisema Desemba 24 mwaka huu, maeneo ya Ubungo Kibo, Kinondoni, Polisi walipata taarifa kutoka kwa mwananchi ambapo walifanikiwa kumkamata
↧
Serikali Kupeleka Sh. 18.77 Bilioni kila Mwezi shule za Sekondari na Msingi, kugharamia Elimu
SERIKALI imepanga kupeleka Sh. 18.77 bilioni kila mwezi katika shule za sekondari na msingi kwa ajili ya kugharamia elimu ili kutekeleza dhana ya elimu bure kuanzia Januari, 2016.
Taarifa hiyo ilitolewa Mjini Dodoma jana na Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa elimu bure
↧
Kesi ya wafanyakazi wa TRA kusikilizwa Januari 13 Mwakani
UPELELEZI wa kesi ya uhujumu uchumi ulioisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 12.7 inayomkabili aliyekuwa Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Tiagi Masamaki na wenzake, haujakamilika.
Wakili wa Serikali, Diana Lukondo alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati kesi hiyo ilipotajwa. Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Huruma Shaidi aliahirisha
↧
↧
Watu 8 Wafikishwa Mahakamani kwa Tuhuma za Kuua Ng'ombe 151
WATU wanne wamefikishwa mahakamani kwa mashtaka ya kuua ng’ombe 151 wenye thamni ya Sh milioni 60.4, mali ya mfugaji, Shabani Kidaini.
Watu hao, wote wakazi wa Turiani wilayani Mvomero mkoa wa Morogoro, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa huo.
Waliopandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka hayo na wakili wa Serikali, Teodora Mlelwa, mbele ya hakimu Agripina Kimaze,
↧
Rais Magufuli Atangaza Makatibu Wakuu na Manaibu Wapya wa Wizara Mbalimbali[Orodha Hii Hapa]
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa makatibu wakuu na manaibu Katibu wakuu
katika Wizara mbalimbali.
Walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
Katibu
Mkuu Kiongozi
Balozi - Ombeni
Sefue
Katibu
Mkuu Ikulu
Peter Ilomo
Ofisi
ya Rais, Utumishi na Utawala Bora
Dkt. Laurian
Ndumbaro
Ofisi
ya Rais, Tawala za Mikoa na
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Tarehe 31 Disemba
↧
More Pages to Explore .....