Jumla ya wanafunzi 503,914 kati ya 518,034 waliofaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kwa kupata alama A, B na C, wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika shule za sekondari za Serikali katika awamu ya kwanza. Idadi hiyo ni sawa na asilimia 97.3 ya wanafunzi waliofaulu na wenye sifa ya kujiunga na kidato cha kwanza.
Hata hivyo, wanafunzi 12,847 kati ya hao waliofaulu kutoka
Wanafunzi 503,914 Wachaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza
↧
↧
CAG Akaidi Agizo la Rais Magufuli....... Aenda Nairobi, Kenya Kwa Fedha za Serikali Bila Kibali Cha Ikulu
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Juma Assad, amekiuka agizo la Rais Dk. John Magufuli, baada kusafiri nje ya nchi bila kibali cha Ikulu.
Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania, CAG aliondoka nchini Jumamosi (Desemba 12, 2015) kwenda jijini Nairobi, Kenya na kurejea nchini Jumanne wiki hii.
Taarifa hizo, zimesema CAG alikwenda kutoa mhadhara katika Chuo
↧
Makonda Aibua Ufisadi wa Bilioni 5.7 Kinondoni
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (pichani) ameamuru kusitishwa mara moja malipo yanayofanywa kwa makandarasi waliojenga barabara tano za ndani ya wilaya hiyo.
Amefanya hivyo kwa maelezo kuwa watendaji wa Manispaa hiyo, wameshirikiana na makandarasi hao kuiibia serikali Sh bilioni 5.7. Fedha hizo ni ongezeko ambalo makandarasi hao, wanatakiwa kulipwa baada ya kujenga barabara hizo
↧
Ziara ya Lowassa Nchi Nzima 'Yaota Mbawa' Ghafla......CHADEMA Watoa Ufafanuzi
Siku moja baada ya kuahirishwa ziara ya aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, chama hicho kimesema hakilitambui zuio la kufanya maandamano na mikutano ya kisiasa lililowahi kutolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu mwezi uliopita.
Kauli ya Chadema ilitolewa jana na Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini
↧
Viongozi wa Chadema na CCM Watwangana Ngumi Kwenye Uteuzi Wa Meya
Zogo kubwa liliibuka katika kikao cha kuwachagua Meya na Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma jana. Zogo hilo lilisababisha viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuzichapa kavukavu.
Hali hiyo ilitokea wakati wa kuapisha madiwani 56 na kufanya uchaguzi katika Viwanja vya Ukumbi wa Manispaa hiyo mjini Dodoma, ilisababishwa na lugha za vijembe na
↧
↧
Dkt. Kingwangalla atumbua MAJIPU ya watumishi wachelewaji wa Wizara ya Afya
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla amefanya ukaguzi wa kushtukiza katika ofisi za wizara hiyo kwa kusimama getini kuzuia wafanya kazi wote wa wizara ambao walikuwa wamefika ofisini baada ya saa 1:30 asubuhi muda ambao ndiyo mwisho wa wafanyakazi kuingia ofisini.
Awali Dkt. Kingwangalla alifika ofisini saa 1:05 asubuhi huku
↧
Rais Magufuli Aongoza Kikao cha Kwanza Cha Baraza La Mawaziri Ikulu Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam Alhamisi tarehe 18, 2015. Kulia kwake ni Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na kushoto kwake ni Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa.
Kikao hicho ni cha kwanza kufanyika tangu Rais Magufuli atangaze Baraza la Mawaziri la Serikali ya Awamu ya Tano
↧
Basi la New Force Lapata Ajali na Kuua Watu 12 Iringa
Watu 12 wamefariki dunia papo hapo baada ya lori la mbao lililokuwa likitokea njombe kwenda jijini Dar es Salaam kupasuka tairi na kugongana na basi la abiria la new force lililokuwa linatokea jijini Dar es Salaam kuelekea tunduma hii leo katika eneo la kitonga wilaya ya kilolo mkoani iringa.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa iringa, kamishina msaidizi wa polisi Ramadhani Mungi
↧
Marekani Kupitia Shirika la MCC Yainyima Mabilioni Ya Pesa Tanzania Kutokana na Mzozo wa Uchaguzi Zanzibar
Tamko kutoka kwa Balozi Mark B. Childress kuhusu uamuzi wa Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia kuahirisha kupigia kura mkataba wake na Tanzania
*********
Tarehe 16 Disemba, Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) haikuichagua Tanzania kwa mkataba wa pili. Bodi iliahirisha kupigia kura mkataba wa pili, ikisubiri kutatuliwa kwa masuala ya kiutawala.
Bodi inaweza kuangalia
↧
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi yaa Disemba 19
↧
Waziri wa Mambo ya Nje Dk Mahiga Kuzungumza Na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Kuhusu Hali Ya Usalama Nchini Burundi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga atafanya ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Arusha kuanzia leo Jumamosi tarehe 19 Desemba 2015.
Atakapokuwa mkoani Arusha, Balozi Mahiga atafanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dkt. Richard Sezibera. Mazungumzo yao yatahusu namna ya kutatua
↧
Kasi ya Rais Magufuli Yabaini Vyeti FEKI 219.......Waziri Ataka Hatua Kali za Kisheria Zichukuliwe Dhidi Yao
Kasi ya Mawaziri wa Rais John Pombe Magufuli kufanya ziara za kushtukiza na kutoa maagizo kwa watendaji imeanza kufumua uozo baada ya jana kubainika kuwa watumishi 219 kati ya 704 wa serikali wameajiriwa kwa vyeti vya kughushi.
Sakata hilo liliibuliwa baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki kutembelea Idara,vitengo vya
↧
Kauli Ya Mwenyekiti Freeman Mbowe Kuhusu Uamuzi Wa Bodi Ya MCC Kuzuia Msaada Wake Wa Trilioni 1 Kwa Serikali Ya Tanzania
Muda mfupi baada ya Bodi ya MCC kutoa taarifa inayoonesha Tanzania haitapata msaada kutoka shirika hilo kama ilivyotarajiwa kwa ajili ya mwaka 2016, Mwenyekiti wa Chama (T), Freema Mbowe ametoa kauli nzito juu ya suala hilo akisema kuwa kuchelewa kupatikana kwa fedha za MCC si tu kunachafua jina la nchi na hadhi yake katika medani za kimataifa, bali kutaathiri kwa kiasi kikubwa miradi yote
↧
↧
Profesa Muhongo Kafuta Likizo Zote Za Wafanyakazi wa Tanesco.......Kawaagiza Pia Washushe Bei ya Umeme
Bei ya umeme inatarajia kushuka wakati wowote kuanzia sasa baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (pichani )kuliagiza Shirika la Umeme (Tanesco), kushusha gharama za nishati hiyo.
Katika hatua nyingine, Waziri huyo amefuta likizo za wafanyakazi wa shirika hilo ili washughulikie tatizo la umeme nchini huku akisisitiza kuwa hataki kusikia kukatika katika kwa umeme.
↧
Watumishi 10 Tanesco Wasimamishwa Kazi Kwa Upotevu wa Milioni 100
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme (Tanesco), Felchesmi Mramba, amewasimamisha kazi maofisa 10 wakiwamo wahasibu waandamizi na mafundi kwa kusababisha upotevu wa mapato zaidi ya Sh.milioni 100.
Hasara hiyo ilitokea katika mfumo wa mita kupitia minara ya simu za mkononi na faini Sh. milioni 198.1 za wateja waliobainika kuiba umeme kwa kuchakachua mita zao.
Hata hivyo, shirika hilo
↧
TCRA Yatoa miezi Sita hadi June 16, 2016 kuzifunga simu zote feki Tanzania.....Hakiki Simu Yako Mapema
UTANGULIZI:Vifaa vya mawasiliano vya mkononi – hususan simu za kiganjani na vifaa vya mawasiliano vya kiganjani (tablets) – vina namba maalum inayovitambulisha. Namba hiyo inajulikana kama IMEI ambacho ni kifupi cha International Mobile Equipment Identity.Kifungu cha 84 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) ya 2010 kinataka kuwepo kwa mfumo wa rajisi ya namba za
↧
Wanyarwanda Wengi Waunga Mkono Mabadiliko ya Katiba Kumruhusu Paul Kagame Kuendelea Kutawala
Wanyarwanda wameunga mkono kwa wingi marekebisho ya katiba ambayo yatamruhusu Rais Paul Kagame kuendelea kuongoza, matokeo ya awali ya kura ya maoni yanaonyesha.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inasema 98% ya wapiga kura wameunga mkono marekebisho hayo ya katiba ambayo yatamruhusu Bw Kagame kuwania kwa muhula mwingine mwaka 2017, baada yake kumaliza muhula wa pili.
Tume hiyo imesema wilaya
↧
↧
Basi la Hood na Best Line Yagongana Jijini Mbeya Asubuhi Hii
Magari matatu yamepata ajali mkoani Mbeya asubuhi ya leo iliyohusisha mabasi ya Hood ya Mbeya na Arusha na basi la Best linalofanya safari zake Mbeya na Mwanza pamoja na lori eneo la Inyala Mbeya
Katika ajali hiyo mtu mmoja amejeruhiwa vibaya na wengine kupata majeraha madogo madogo.
Kamanda wa polis Mkoani mbeya ACP AHMED MSANGI amedhibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
↧
Taasisi 1,200 Duniani Zampa Tuzo ya Amani Edward Lowassa
Taasisi 1,200 duniani zitampa aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa Tuzo ya Amani kutokana na utulivu aliouonyesha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu.
Akizungumza kutoka Bukavu, DR Congo, mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga alisema Lowassa amechaguliwa jana mjini Bukavu na wajumbe 1,400 wa mkutano huo.
↧
Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi Ajali ya Basi la New Force Iringa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza kufuatia ajali ya basi la kampuni ya New Force kugongana na lori, na kusababisha vifo vya watu 12, na wengine 15 kulazwa Hospitali.
Ajali hiyo imetokea tarehe 18 Desemba, 2015 Majira ya saa nane mchana katika Kijiji cha Mahenge, Wilaya ya Kilolo Mkoani
↧
More Pages to Explore .....