Marekani imeiweka njiapanda Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, baada ya Bodi ya shirika lake la Changamoto za Milenia (MCC) kuamua kukutana kesho kujadili masuala kadhaa ya utoaji wa misaada kwa nchi zinazoendelea huku angalizo lake kwa serikali ya Tanzania kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar likiwa bado halijapatiwa ufumbuzi.
Kwa mujibu wa ratiba ya MCC, kikao chao cha Bodi kitakutana
Marekani Yamuweka Rais Magufuli Njiapanda......MCC inakutana Kesho Huku Suala La Zanzibar Likiwa Bado Ni Kitendawili
↧
↧
Wanne Wakataa Uwaziri wa Magufuli Wakihofia Kushindwa Kuendana na Kasi Yake
WABUNGE wanne wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wametajwa kukataa uteuzi wa nafasi ya uwaziri ili kujaza nafasi za wizara nne zilizokuwa wazi.
Hatua hiyo imetokana na kile kilichoelezwa kuwa ni hofu ya wabunge hao kushindwa kwenda na kasi ya Rais Dk. John Magufuli, ambaye aliwaapisha mawaziri wapya Desemba 12, mwaka huu.
Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania, wabunge wamedai kuwa kasi ya Rais
↧
Saed Kubenea Apandishwa Mahakama Ya Kisutu na Kusomewa Shitaka La Kutoa Lugha Chafu Dhidi Ya Makonda
Mbunge wa jimbo Ubungo kupitia Chadema, Saed Kubenea amepandishwa kizimbani kortini Kisutu, jijini Dar es Salaam leo na kusomewa shtaka la kutoa lugha chafu dhidi ya Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.
Hata hivyo, Kubenea amekana kufanya kitendo hicho na kesi yake kuahirishwa hadi Desema 29, mwaka huu huku uchunguzi ukiendelea.
↧
Mgombea wa CCM apinga Matokeo ya Godbless Lema......Alitupia Lawama Jeshi la Polisi Kwa Kuwatisha Wapiga Kura kwa Silaha za Kivita
Aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya CCM, Philemon Mollel amepinga matokeo ya uchaguzi huo yaliyompa ushindi wa kishindo, Godbless Lema wa Chadema.
Akiongea na waandishi wa habari baada ya msimamizi wa uchaguzi huo kutangaza matokeo, Mollel alidai kuwa kulikuwa na udanganyifu mkubwa ambao unafanya matokeo hayo kutokuwa halali.
Alisema kuwa wakati zoezi la
↧
TAFFA Yaibua Mapya Ya Utoroshaji Wa Kontena Bandarini
CHAMA cha Mawakala wa Forodha nchini (TAFFA) kimesema kuwa wizi wa kontena bandari ya Dar es Salaam na kusababisha serikali kukosa mapato ni tatizo la muda mrefu ambalo ni limekuwa likisababishwa na watumishi wa bandari.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Rais wa TAFFA, Steven Ngatunga alisema tatizo lilojitokeza ya uondoshaji wa kontena 329 katika bandari
↧
↧
Uturuki Kuisaidia Tanzania Kufanikisha Mpango wa Elimu Bure
Serikali ya Uturuki imeahidi kuisaidia Serikali ya Tanzania kufanikisha mpango wa utoaji wa elimu bure kwa wanafunzi utakaoanza January mwakani.
Hayo yalizungumzwa jana na Balozi wa Uturuki nchini Bi Yasemin Eralp alipokuwa akizungumza na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson Mwansasu alipomtembelea ofisini kwake.
Balozi yasemin Eralp aliainisha
↧
Simbachawene Aagiza Taka Zilizokusanywa Wakati Wa Uhuru Disemba 9 Zizolewe Kabla Ya Disemba 20
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurungenzi wote wa halmashari nchini kuhakikisha wanazoa taka zote zilizokusanywa wakati wa siku ya uhuru kabla ya tarehe 20 mwezi huu.
Kauli hiyo aliitoa wakati alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa kikao cha kumkaribisha katika
↧
Washitakiwa Watatu wa TRA Wanaohusika na Utoroshaji Makontena Wapewa Dhamana.......Yupo Masamaki na Wenzake Wawili
Mahakama kuu ya Tanzania imeridhia dhamana kwa washitakiwa watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA wanaokabiliwa na mashitaka ya kutoa makontena 329 bandarini bila kulipiwa kodi na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 12.7.
Maamuzi hayo ya mahakama kuu ya Tanzania yametokana na ombi lililowakilishwa mahakamani hapo na washtakiwa watatu wakiongozwa aliyekuwa Kamishina wa
↧
Mbowe Azungumzia Kasi ya Rais Magufuli.....Adai Kuwa Mpinzani Haimaanishi Upinge Kila Kitu
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amezungumzia kasi aliyoanza nayo rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli pamoja na baraza lake la mawaziri.
Akizungumza jana na mwandishi wa habari wa Azam TV, Mbowe alisema kuwa rais Magufuli ameanza vizuri kiutendaji na kwamba ameanza kuzifanyia kazi hoja zilizokuwa zikihubiriwa na Chadema ndani na nje ya Bunge.
“Hoja ya kubana
↧
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Disemba 16
↧
Chama cha Wahasibu Tanzania (TAA) Chaahidi Kupambana Na Wahasibu Wala Rushwa, Wezi na Mafisadi
CHAMA cha Wahasibu Tanzania (TAA) kimetishia kuwaondoa wahasibu waliokuwepo kwenye daftari la chama hiko endapo watakiuka taratibu na maadili ya kazi kulingana na matakwa ya chama hicho ikiwemo ya rushwa, wizi na ufisadi.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa chama hicho, Fred Msemwa katika mazungumzo yake na wanahabari wakati akitoa pongezi na kuunga mkono kwa
↧
Mapigano ya Wafugaji na Wakulima Morogoro: Serikali Yabomoa Mabanda ya Wafugaji Na Kupiga Mnada Ng'ombe Zao
WAFUGAJI waliovamia maeneo ya wakulima katika kijiji cha Dihinda wilayani Mvomero mkoani Mogorogo na kusababisha mapigano yaliyoua mkulima na ng’ombe 71, wamekimbia kijijini hapo na kutokomea kusikojulikana.
Akizungumzia hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Wilaya ya Mvomero, Mkuu wa Wilaya hiyo, Betty Mkwasa alisema ulinzi bado umeimarishwa eneo hilo, na kwamba wafugaji
↧
Mchungaji na Mkewe Watiwa Mbaroni kwa Kumfungia Ndani Mtoto Wao Mlemavu kwa Miaka 12
POLISI mkoani Singida inamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Itaja na mkewe kwa tuhuma za kumfungia ndani ya chumba mtoto wao mlemavu wa viungo kwa miaka 12 bila kutoka nje.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni David Mtipa (59) ambaye ni Mchungaji wa Kanisa hilo na mkewe Mariam Philipo (45) wote wakazi wa kijiji cha Itaja katika
↧
↧
Lowassa kuzunguka nchi nzima kuanzia kesho
Aliyekuwa mgombea urais wa Chadema akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa ataanza ziara ya kuzunguka nchi nzima kuwashukuru Watanzania kwa kumpigia kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 na kesho atakuwa Tanga.
Katika ziara hiyo, Lowassa ataambatana na viongozi waandamizi wa Chadema na Ukawa kuwashukuru wananchi kwa namna walivyounga mkono
↧
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu Afanya Ziara ya Kushtukiza Hospitali ya Muhimbili Leo na Kukuta Mashine za CT Scan na MRI Zimeharibika Tena
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Ummy Mwalimu amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo na kukuta mashine za CT Scan na MRI hazifanyi kazi.
Katika ziara hiyo aliyoifanya asubuhi ya leo, alikutana na mzee wa miaka 90 ambaye alikuwa akisubiri huduma hiyo tangu jana.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Wa Hospitali hiyo, Lawrence Museru, mashine
↧
Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru......Wanne Wafutwa Kazi Kwa Kukaidi Agizo la Kusafiri Nje ya Nchi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dkt. Edward Hoseah kutokana na kutorishwa na namna taasisi hiyo ilivyokua ikitekeleza wajibu wake katika kukabiliana na rushwa hususani kwenye upotevu wa mapato ya serikali katika bandari ya Dar es salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi
↧
Tanzania na Japan zasaini mkataba wa shilingi bilioni 210 za umeme
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini mkataba na Serikali
ya Japani kiasi cha shilingi bilioni 210/= kwa ajili ya maendeleo ya
mradi wa njia ya kusafirishia umeme kati ya Tanzania na Kenya ambao
utasaidia upatikanaji wa umeme wa kutosha.Mkataba huo wa
masharti nafuu ulisaininiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na
Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile
↧
↧
Kauli ya ACT-Wazalendo kuhusu yanayoendelea Burundi
CHAMA CHA ACT-WAZALENDO KINAITAKA TANZANIA NA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KUKOMESHA MAUAJI NCHINI BURUNDI
1. Chama cha ACT-Wazalendo kinasikitishwa sana na maujai
yanayoendelea nchini Burundi na hasa Mji Mkuu wa nchi hiyo Bujumbura.
Hali hii ya mauaji imesababishwa kwa kiasi kikubwa na uamuzi wa Rais wa
sasa wa nchi hiyo Ndugu Piere Nkurunzinza kuendelea kugombea na hatimaye
kuchaguliwa
↧
Walimu Wakuu Wote Ambao Wanawafunzi Wao Wataingia Darasa La Tatu Wakiwa Hawajui Kusoma na Kuandika WATAFUKUZWA Kazi
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Mhandisi Stella
Manyanya (wa pili kulia) akikata utepe na Makamu wa Rais wa Kampuni ya
Total, Jean-Christian Bergeron (wa tatu kulia) wakati wa hafla ya
kukabidhi madawati 1000 yaliyotolewa kama msaada na Total kwa ajili ya
Shule 10 za mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.(Picha na Francis Dande)
***
SERIKALI imesema itawafukuza kazi walimu
↧
Waziri Mkuu wa Japan Atuma Salamu Za Pongezi Kwa Rais Magufuli
Waziri Mkuu wa Japan Mheshimiwa Shinzo Abe amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa awamu ya tano wa Tanzania na kumuahidi kuwa Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi, maendeleo na ushirikiano wa kimataifa.
Akiwasilisha ujumbe maalum wa maandishi kutoka kwa Mheshimiwa Abe, Mjumbe Maalum
↧