Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya CCM, January Makamba ameonesha
kutokubaliana kwake na ripoti za kinachojili kwenye mikutano ya mgombea
urais wa Chadema, Edward Lowassa na kueleza kuwa Magazeti hutumiwa kupiga
kampeni.
Makamba ameeleza hayo kupitia mtandao wa Twitter baada ya
mtu mmoja anaetumia jina la ‘Gachanja Muigai’, kumueleza kuwa kutokana
na kile wananachokisoma, inaonekana
January Makamba Adai Magazeti Yanampendelea LOWASSA Kwa Kumpigia Kampeni
↧
↧
Sheria ya Mtandao Yamtia Mbaroni Mtayarishaji wa Vipindi Mkoani Dodoma
Mtayarishaji wa vipindi, Sospiter Jonas amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Dodoma Mjini akishtakiwa kwa matumizi mabaya ya mtandao.
Sospiter alisomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Mussa mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo Emmanuel Bwile.
Mshtakiwa huyo anadaiwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook ujumbe kuwa “Pinda utakuwa muhubiri wa injili tu.”
Mussa
↧
Maduka ya Uchumi Supermarket yafungwa Tanzania na Uganda
Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Julius Kipng'etich, amesema Bodi imeamua kufunga vitengo vya kikanda ili kuimarisha shughuli zake nchini Kenya baada ya kupata hasara katika maduka yake ya Uganda na Tanzania
↧
Familia ya Nyerere katika ibada ya kumbukumbu ya kifo cha Mwalimu jana Oktoba 14
Mama Maria Nyerere, mjane wa baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere, jana aliungana na Wananchi wa kijiji cha Butiama katika
misa takatifu ya kumbukumbu ya miaka 16 baada ya kifo cha muasisi wa
Taifa la Tanzania, ambapo viongozi wa dini waliongoza misa iliyofanyika
katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Butiama huku suala la amani kuelekea
uchaguzi mkuu likihubiriwa.
↧
Mwapachu asema Nyerere angekuwapo angejitoa CCM
Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho, Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa.
Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho
↧
↧
Lowassa: Mliobaki CCM Nifuateni Chadema.
Mgombea wa urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kuungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa, amewataka viongozi na makada wengine waliobaki ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoroka na kujiunga na Chadema kwani hivi sasa ni wakati wa mabadiliko.
Lowassa alitoa kauli hiyo jana katika mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa
↧
Rais Kikwete Arusha Makombora UKAWA......Awaonya Wanaopanga Kulinda Kura Vituoni
RAIS Jakaya Kikwete, jana ametumia kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, akiwataka Watanzania kuchagua viongozi katika uchaguzi wa mwaka huu watakaodumisha amani.
Alitumia kumbukumbu hiyo kuwapiga vijembe baadhi ya wanasiasa wanaotaka kuchaguliwa kwa kutumia rushwa, misingi ya udini na ukabila ndani ya vyama vyao.
Akihutubia wakati wa kumbukumbu
↧
Mbowe Amjibu Rais Kikwete Kuhusu Idadi ya Wapiga Kura na Zuio la Wananchi Kulinda Kura Vituoni
Mwenyekiti wa Chadema, mh Freeman Mbowe amemtaka Rais Kikwete kutovuruga amani ya nchi na badala yake amemtaka aondoke madarakani na kuiacha nchi ikiwa salama.
Mbowe alitoa kauli hiyo jana jioni katika mkutano wa kampeni uliofanyika Mbogwe, wilayani Geita.
Alisema Rais Kikwete anatakiwa aondoke madarakani salama kama walivyofanya marais wenzake wastaafu.
“Rais Kikwete
↧
Magufuli Afichua Ushauri Aliopewa na Marehemu Dr. Kigoda Kabla ya Mauti Kumkuta
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli, jana aliwaongoza
wanachama wa chama hicho kuupokea mwili wa Dtk. Abdallah Kigoda
aliyepoteza maisha nchini India, ambapo alieleza kuwa alimpa ushauri
katika kipindi kifupi kabla Mungu hajamchukua.
Akiongea na waandishi wa habari, Magufuli alieleza kuwa Marehemu Kigoda
alimshauri masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na jinsi ya
↧
↧
Balozi Mwapachu arudisha Rasmi kadi ya CCM...... atangaza kujiunga UKAWA
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kada wa CCM, Balozi Juma Mwapachu leo amerudisha kadi ya uanachama katika ofisi za CCM Kata ya Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Amesema anajiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kwamba baada ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 atatangaza chama anachojiunga miongoni mwa Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na NLD vinavyounda umoja huo.
↧
Mahakama yamwamuru Gwajima kuthibitisha kama kweli anaumwa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemwamuru Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima awasilishe Mahakamani hapo vyeti vinavyoonesha kuwa ni mgonjwa.
Amri hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha baada ya Gwajima kushindwa kufika mahakamani kwa ajili ya usikilizwaji wa kesi inayomkabili.
Gwajima anakabiliwa na kesi ya kutumia lugha chafu dhidi ya
↧
Sad News: Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA, Dr. Makaidi Afariki Dunia
Mwenyekiti wa NLD, ambaye ni mwenyekiti mwenza wa vyama vya upinzani vinavyounda Ukawa, Dkt. Emmanuel Makaidi amefariki leo majira mchana katika hospitali ya Nangao mkoani Lindi.
Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Dkt. Makaidi ambaye alikuwa mgombea ubunge katika jimbo la Masasi alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.
Dkt. Makaidi ni mgombea ubunge wa tano kufariki katika
↧
Kiwanja Kinauzwa Kigamboni Mwongozo.....Wahi Fasta!!!
Kiwanja kinauzwa Kigamboni mwongozo Karibu na Dege village na Nyumba za NHC chenye ukubwa wa mita za mraba 4,000.
Kiwanja kipo katika barabara za Mtaa kwenye umbali wa 18KM toka Ferry na mita 800 toka barabara ya lami.Kinafaa kwa ujenzi wa warehouse (Godown),Saiti ya vifaa vya ujenzi na Nyumba za makazi.
HAKIJAPIMWA ila nakala za kisheria na za serikali za mtaa zipo.
Bei inaanzia
↧
↧
Lowassa Atikisa Sengerema....Tazama Picha za Mafuriko Yake
Mhe. Edward Ngoyai Lowassa akiongea na wananchi wa Sengerema katika viwanja vya Mnadani Alhamisi 15/10/2015
↧
Marekebisho Ya Ratiba ya Kampeni za Wagombea Urais 2015
Kuna Marekebisho ya Ratiba ya Kampeni za Wagombea Urais ambayo yamefanywa na NEC.
>>
↧
Update Kuhusu Helikopta ya CCM Iliyoanguka Mbugani Ikiwa na Mbunge Deo Filikunjombe
Usiku wa kuamkia leo October 16 2015 majukwaa ya siasa Tanzania yametawaliwa na ajali ya Helikopta ambayo imeanguka na kulipuka kwenye mbuga ya Wanyama ya Selous ambapo Waziri wa maliasili na utalii Lazaro Nyalandu alithibitisha kwamba mmoja wa waliokuwemo ndani ni Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM).
Kupitia ukurasa wake wa Twitter,Nyalandu aliandika;
"Tumetuma vikosi vya
↧
Magufuli Akiri Mafisadi Yako Ndani ya CCM.......Ameahidi Akiingia Ikulu Atawashughulikia Bila Woga. Pia kasema Mawaziri Wote Atawasainisha Mikataba
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema mafisadi wamo hadi ndani ya chama chake na ndiyo maana baada ya kuteuliwa kuwa mgombea urais wengi wao wameanza kuweweseka kutokana na hofu kubwa waliyo nayo dhidi yake.
Akizungumza kwa nyakati tofauti katika mikutano ya kampeni ya chama chake mjini Kisarawe, Pwani na baadaye Ukonga, jijini Dar es Salaam jana, Magufuli
↧
↧
UKAWA : Daftari la Wapigakura Limejaa VITUKO.....Majengo, Wachina na Namba za Pikipiki Zimeandikishwa Kama Wapiga Kura
WAKATI Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ikiwa ndio kwanza imelikabidhi Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi, ili kufanyiwa uhakiki, uchunguzi umeonesha daftari hilo ni chafu na haliaminiki.
Siri hii inafichuka siku tisa tu kabla ya Oktoba 25 ambapo Watanzania wapatao milioni 22 wanatarajiwa kujitokeza vituoni kupiga kura ya kuchagua Rais wa Jamhuri
↧
LOWASSA Atoa Onyo Kwa Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi.....Asema NEC Isipokuwa Makini Itavuruga Amani ya Nchi. Mbowe Katoa Mwongozo Kwa Wapiga Kura
Mgomea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, ameionya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kwamba kama haitakuwa makini, inaweza kuvuruga uchaguzi mkuu.
Lowassa ambaye anaungwa mkono na vyama vinne vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alitoa tahadhari hiyo alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni katika viwanja vya Sabasaba, mjini Magu jana.
↧
Baadhi Ya 'Vituko' Vilivyopo Ndani ya Daftari la Wapiga Kura.....Picha Zimepigwa jana Wakati UKAWA Wakiongea na Waandishi wa Habari
Huyu Kaandikishwa kwa jina la GGGHUH GGJGJHGHG GGHGGGHG
Mwangalie vizuri mzungu na majina yake. Picha ya pembeni kulia ni kitu cheusi na siyo sura ya mtu
Angalia Jina na hiyo picha. Kwa kuiangalia sidhani kama ni picha ya binadamu
Tazama majina na picha
Hizi picha mbili za kulia sio za binadamu. Moja ni kama ya
↧
More Pages to Explore .....