SERIKALI imekanusha uvumi uliozagaa katika mitandao ya jamii wiki hii kuwa wanyama aina ya twiga wanatoroshwa kutoka pori tengefu la Loliondo na kupelekwa nje ya nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara Maliasili na Utalii, Dkt. Adelhelm Meru ameziita habari hizo kuwa za uongo, uzushi na uchochezi.
Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Dkt. Meru alisema jambo hilo si la kweli
Serikali Yakanusha Twiga Kutoroshwa kwa Ndege
↧
↧
Lowassa Kuzindua Kampeni ya ‘ TOROKA UJE ’ Leo
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kushirikiana na UKAWA
leo wanatarajia kuzindua kampeni nyingine iliyopewa jina la ‘Toroka
Uje’ katika viwanja vya Tanganyika Pekazi Kawe jijini Dar es salaam.
Habari za ndani zinaeleza kuwa kampeni hiyo inatarajiwa kuwa ya aina
yake katika dakika za mwisho kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba
25, 2015.
Uzinduzi huo ulipangwa
↧
NEC yatoa Uhuru kwa Waandishi siku ya Uchaguzi
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) itaruhusu waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kufika kwenye vituo vya kupigia kura na kufanya mahojiano na wapiga kura pamoja na wasimamizi wa uchaguzi kuhusu zoezi la kupiga kura litakavyokuwa likiendelea.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima wakati wa mafunzo ya siku mbili ya waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya
↧
Polisi Yathibitisha Mgombea Ubunge wa ACT-Wazalendo Kutekwa
Jeshi la Polisi mkoani Simiyu limethibitisha kutekwa kwa mgombea ubunge Jimbo la Bariadi, kupitia chama cha ACT Wazalendo Masunga Ng’hozo na watu wasiojulikana.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Gemini Mushy amesema kuwa tangu kutoweka kwa mgombea huyo, simu yake imekuwa ikitumika kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kwa wazazi wake.
Amesema
↧
NEC: Kalamu Yoyote inaruhusiwa Kupigia Kura
Ili kuondoa shaka miongoni mwa wananchi kutokana na tetesi zinazosambazwa juu ya ubora wa kalamu za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kila mtu anaruhusiwa kuja na kalamu yake kupigia kura Oktoba 25, mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa leo na NEC wakati ilipofanya mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari nchini ikiwa ni siku ya tatu ya
↧
↧
MAFURIKO: Picha 40 za Mikutano yote ya Lowassa Leo Jijini Dar es Salaam
Mgombe Urais wa CHADEMA Mhe. Edward Lowassa akiwa na Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo Saed Kubenea
Msafara wa Mgombea Urais wa CHADEMA akiwa maeneo wa Ubungo akiendelea na kampeni.. Jijini Dar es Salaam.
Wakazi wa Mwembeyanga, Temeke waliojitokeza kumsikiliza Mgombea Urais wa CHADEMA Mhe. Edward Lowassa.
Mgombe Urais wa UKAWA, Mhe. Edward Lowassa akiwasili katika viwanja vya
↧
Ndege ya JWTZ yaanguka, marubani wapotea
NDEGE ya mafunzo ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), imepata ajali ikiwa na marubani wawili katika eneo la Silversands, Visiwa vya Bundya, katika Mwambao wa Bahari ya Hindi Kaskazini Mashariki mwa Jiji la Dar es Salaam.
Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya Jeshi, Upanga, ilisema marubani hao wanaendelea kutafutwa baada ya kuzama
↧
Vijana sita wa JKT Bulombora, Kigoma Wafariki dunia Baada ya gari la Jeshi kushindwa Kupanda mlima na Kupasuka tairi
VIJANA sita waliokuwa katika mafunzo ya kijeshi ya kujitolea katika kikosi cha 821 JKT Bulombora mkoani Kigoma wamefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa vibaya kutokana na ajali ya gari iliyotokea jana jioni
Mganga Mfawidhi wa hospital ya mkoa wa Kigoma Dkt. Fadhil Kibaya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
"Ni kweli jana majira ya saa moja jioni tumepokea miili minne ya vijana wa
↧
Lowassa Ataja Vipaumbe vyake 13 Ndani ya Siku 100.
Mgombea urais wa Chadema na Ukawa, Edward Lowassa ametaja mambo 13 atakayoyafanya ndani ya siku 100 iwapo atachaguliwa kuwa Rais, huku akisema “atawakata kilimilimi” wanaombeza kuwa hawezi kuondoa umaskini wa wananchi.
Lowassa alikuwa akihitimisha mikutano minne aliyofanya kwenye wilaya tatu za Jiji la Dar es Salaam jana kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe.
Wakati Lowassa akieleza
↧
↧
Polisi Wakanusha Karatasi za Kura Zilizompa Alama Ya VEMA Magufuli Kukamatwa Masasi.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limekanusha taarifa zinazodaiwa kuandikwa katika mtandao mmoja wa kijamii, zikidai kukamatwa kwa baadhi ya watu katika kituo cha polisi wilaya ya Masasi mkoani hapa wakiwa na masanduku na fomu za kupigia kura zipatazo 2000 zikiwa tayari zimetumika.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe, alisema
↧
Picha 11 za MAFURIKO Ya Edward Lowassa mbele ya Wananchi wa Babati na Mto wa Mbu Oct 2.
Mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia
mwamvuli wa UKAWA Edward Lowassa October 2 2015 alisimama mbele ya
Wananchi wa Jimbo la Babati Mjini katika Mkutano wa hadhara wa Kampeni
uliofanyika kwenye Uwanja wa Kwaraha, Babati Manyara.
Edward
Lowassa akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Monduli kwa Chadema kupitia
mwamvuli wa UKAWA, Julius Karanga,
↧
Basil Mramba na Daniel Yona Wapunguziwa Kifungo Cha Mwaka Mmoja Kati Ya Mitatu Waliyokuwa Wamehukumiwa Hapo Awali
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana Oktoba 2, 2015, ilitoa hukumu ya rufaa dhidi ya mawaziri wastaafu,Basil Mramba na Daniel Yona ambapo Jaji Projest Rugazia, alikubaliana na hoja kwamba kwa mujibu wa mashtaka hayo yaliyowatia hatiani kwa matumizi mabaya ya Ofisi na kwa mujibu wa kifungo cha 35 cha adhabu PC ambacho Mahakama ilikitumia walipaswa kupewa adhabu ya kutumikia kifungo cha
↧
Mgombea Ubunge CCM Aanguka Jukwaani Akiruka Kichurachura........Alitaka Kunogesha Mtindo wa CCM wa Push Up za Magufuli
Mgombea ubunge wa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Tunduru Kaskazini,Mhandisi Ramo Makani alianguka jukwaani wakati akijaribu kuruka kichura chura.
Tukio hilo lilitokea katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za mgombea huyo, uliofanyika kwenye viwanja vya baraza la Idd mjini hapa.
Inasadikiwa kuwa alikusudia kunogesha staili ya
↧
↧
Magufuli Atinga Mkoani Singida....Aahidi Kuwajali Wananchi wa Kipato Cha Chini
Mgombea
wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia kwenye mkutano
wa kampeni za CCM ambapo aliwaambia wananchi waliojitokeza kwa wingi
kwenye uwanja wa Mnadani, Ikungi kumsikiliza kuwa serikali atakoyoiunda
itaondoa kero ndogo ndogo kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo
wadogo.
Mgombea
wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati
wa
↧
Rais Kikwete azindua mfumo wa BRELA wa kusajili biashara kwa njia ya mtandao.
Rais Jakaya Kikwete, jana amezindua mfumo wa usajili wa kampuni kwa njia ya mtandao utakao ondoa urasimu, rushwa na usumbufu kwa wananchi wanaotaka huduma hiyo. Awali watu walilazimika kusafiri hadi Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela).
Kabla ya kuzinduliwa kwa mfumo huo, Ikulu jijini Dar es Salaam, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Brela, Frank Kanyusi, alisema kazi ya mtandao huo ni
↧
Lowassa Amtosa Binti wa Sokoine ....Amtaka Ahamie UKAWA au Amsamehe
Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa jana amefanya kampeni kwa mara ya kwanza katika jimbo la Monduli na kumnadi mgombea ubunge wa Chadema, Julius Kalanga huku akieleza kuwa atazungumza na mgombea ubunge wa CCM, Namelock Sokoine kuona kama atakubali kupanda basi la Chadema chini ya Ukawa.
Lowassa aliwaeleza wananchi wa Mto wa Mbu katika uwanja wa Barafu kuwa atakutana na
↧
Magufuli azidi kuchanja mbuga, Awaomba Wana CHADEMA Mkoani Singida Waichague CCM
Magufuli akiwasalimia wanachadema wa Manyoni na kuwataka wampigie kura yeye na mbunge wake Daniel Mutuka.
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) John Magufuli, jana alimwaga sera katika Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma na kuingia Mkoa wa Singida ambapo alifanya mikutano kwenye vijiji miji ya Chikuyu, Kilimatinde, Manyoni, Itigi, na kumalizia na Itigi iliyopo Jimbo la Singida
↧
↧
Mwenyekiti wa Tume Ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva Amshangaa MBOWE Kwa Kuhamasisha Vijana Kubaki Vituoni Kulinda Kura
MWENYEKITI wa Tume ya Taifa Uchaguzi nchini Jaji Mstaafu Damian Lubuva, ameeleza kushangazwa na kauli zinazotolewa na baadhi ya vyama vya siasa wakiwahamasisha wafuasi wao hasa kundi la vijana kubaki vituoni ili kulinda kura.
Kauli hiyo ya Lubuva ambayo aliitoa Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari inaonekana kumjibu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (
↧
Picha 3: Wananchi wa Kisiwani Pemba Wakimsubiri LOWASSA Kwa Hamu. ......Lowassa Yupo Tanzania Visiwani Kuomba Kura
Mke wa mgombea urais wa CHADEMA, mama Regina Lowassa katika mikutano ya
kampeni, kisiwani Pemba leo.
Mgombea urais wa UKAWA kupitia CHADEMA,
Edward Ngoyayi Lowassa leo ameanza kampeni zake Tanzania visiwani.
↧
MauzaUZA: Mwanamke Akutwa Ndani Ya Nyumba Ya Mtu Akiwa Na Tunguri, Hirizi na Madawa...
Mwanamke mmoja mtu mzima, ambaye jina lake halikufahamika mara moja
amekutwa akiwa ndani ya nyumba ya mtu pasipo kueleweka namna
alivyoingia, kwani milango yote ilikuwa imefungwa kwa ndani.
Tukio
hilo lilijiri hivi karibuni majira saa 2 asubuhi maeneo ya Majengo,
wilayani Misungwi, mkoani Mwanza na kujaza watu wengi.
Shuhuda
wa tukio hilo amesema kuwa walisikia kelele za mtu
↧