Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim
Lipumba, Jumapili atachukua fomu ya kugombea urais ndani ya chama hicho
na atawaeleza Watanzania sababu ya kuwania nafasi hiyo.
Akizungumza jana, Mkurugenzi wa Mipango na
Uchaguzi wa chama hicho, Shaweji Mketo alisema, Profesa Lipumba ndiye
mgombea pekee wa urais aliyetangaza nia ya kuwania nafasi hiyo.
Alisema muda wa
Urais 2015: Profesa Lipumba Kuchukua Fomu ya Urais Jumapili ya Wiki hii.......Tukio hilo Litarushwa Moja Kwa Moja na Runinga Kadhaa
↧
↧
Urais 2015: Benard Membe Anusurika Kufa Baada ya Ndege yake Kutaka Kugongana "Uso kwa Uso" na Ndege Nyingine
Mio za kuwania kumrithi Rais Jakaya Kikwete miongoni mwa makada wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimezidi kushika kasi, safari hii Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, akinusurika
kifo baada ya ndege aliyokuwa akisafiria kuwapo katika hatari ya
kugongwa na ndege nyingine angani alipokuwa akielekea Zanzibar.
Waziri Membe akiwa na ujumbe wake wa watu nane
↧
Urais 2015: Kambi Ya Lowassa Yazidi Kutanuka........Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Atangaza Rasmi Kumuunga Mkono Edward Lowassa
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Steven Masele,
ametangaza kumuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa katika
harakati zake za kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Masele aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini kabla ya Baraza
la Mawaziri kuvunjwa, jana aliibukia katika mkutano wa kutafuta
wadhamini wa Lowassa uliofanyika mjini
↧
Urais 2015: Pinda achukua fomu, apanga kukuza uchumi
Waziri Mkuu , Mizengo Pinda akiwa ameshika fomu ya kuwania uteuzi wa CCM ili awe mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu ujao kwenye ofisi kuu ya CCM mjini Dodoma Juni 12, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitia saini kitabu baada ya kuwasili kuwasili kwenye Ofisi Kuu ya CCM mjini Dodoma kuchukuwa fomu za kuwania uteuzi wa CCM ili awe mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu ujao.
↧
Lowassa Azidi Kuvunja Rekodi.......Msafara Wake Waingia Tabora Kwa Kishindo, Apata Wadhamini 9516
Waziri
Mkuu wa Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM waliofika
kumdhani pamoja na wananchi wa Mji wa Tabora, kwenye viwanja vya ofisi
za CCM Tabora Mjini, leo Juni 12, 2015.
Waziri
Mkuu wa Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa
akiwapungia mkono maelfu ya wana CCM waliofika kumdhamini pamoja na
wananchi wengine, kwenye viwanja vya ofisi za CCM Tabora
↧
↧
Kortini kwa Kumpa Mwanafunzi Mimba
MKAZI wa Mpiji Magoe Hamis Mohameid (21), amefikishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni Dar es Salaam akikabiliwa na tuhuma za kumbaka mwanafunzi (14)Jina limehifadhiwa na kumpa mimba.
Akisomewa mashtaka mawili mbele ya Hakimu Flora Mtarania, Wakili wa Serikali Grace Lwila, alidai kuwa tukio hilo lilitokea kati ya Aprili na Mei24 mwaka huu maeneo ya huko Mpiji
↧
Sita wafa katika ajali, 45 wajeruhiwa Singida
WATU sita wamekufa na wengine 45 kujeruhiwa katika ajali mbili tofauti za barabarani zilizotokea juzi na jana mkoani Singida.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka alisema mjini
hapa jana kuwa ajali ya kwanza ilitokea Juni 11 mwaka huu saa 1.30 usiku
eneo la Manga nje kidogo ya mji huu kwenye Barabara Kuu ya Singida –
Mwanza.
Alisema ajali hiyo ililihusisha
↧
Atuhumiwa Kuiba Mtoto.
MAMA wa mtoto aliyeibwa kabla hajatimiza mwezi tangu azaliwe, Fatuma Bakari ameieleza Mahakama ya Wilaya ya Ilala jinsi mtoto huyo alivyoibwa na mshtakiwa Neema Patrick.
Shahidi huyo na mwingine walitoa ushahidi wao jana mbele ya Hakimu Adelf Shachore kwa kuongozwa na Wakili wa Serikali, Anunciata Leopold.
Awali mashahidi hao walikuwa watano ambao walifika mahakani kwa ajili ya
↧
Orodha kamili ya washindi wa Kilimanjaro Music Awards 2015........Ali Kiba Kashinda Tuzo 5, Diamond 2
Hii ni orodha kamili ya washindi wa tuzo za muziki Tanzania Kilimanjaro
Music Awards 2015 zilizofanyika 13 June 2015 Mlinani City jijini Dar es
salaam.
1. KIKUNDI BORA CHA MWAKA - BONGO FLEVA - YAMOTO BAND
2. KIKUNDI BORA CHA MWAKA TAARAB - JAHAZI MODERN TAARAB
3. BENDI BORA YA MWAKA - FM ACADEMIA
4. MSANII BORA CHIPUKIZI - BARAKA DA PRINCE
5. WIMBO BORA
↧
↧
Mafuriko Ya Lowassa Yatua Kigoma......Azoa Wadhamini 11,250
Umati
wa WanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Kigoma, ukiwa umefurika kwenye
Uwanja wa Ofisi Kuu ya CCM Mkoa wa Kigoma, kuja kumuona Mh. Edward
Lowassa (anaeonekana kule mbele) wakati alipofika kuomba udhamini wa
wanachama wa CCM, ili aweze kupata ridhaa ya Chama kuwania Urais wa
Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
Mh. Lowassa alipata udhaminiwa na
↧
Shule yafungwa kwa hofu ya simba mla watu
SHULE ya Msingi Saadani Chumvi iliyopo Kata ya Mkange wilayani
Bagamoyo mkoani Pwani, imefungwa baada ya wazazi kuwa na hofu baada ya
watu wawili na mbuzi 70 kuliwa na Simba kutoka kwenye Hifadhi ya Taifa
ya Saadani.
Shule hiyo ambayo iko jirani na hifadhi hiyo ilifungwa mwishoni mwa
mwaka jana kutokana na matukio hayo hali ambayo ilisababisha wazazi
kuogopa watoto wao kudhuriwa
↧
Lowassa Kumzuia Serukamba Kugombea Ubunge
WAZIRI Mkuu mstaafu Edward Lowassa amesema huenda akamzuia Mbunge wa
Jimbo la Kigoma, Peter Serukamba kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu wa
Oktoba mwaka huu ili amsaidie jukumu muhimu kwenye safari yake ya
matumaini.
Akizungumza wakati wa kuomba udhamini kutoka kwa wanachama wa CCM
mkoa Kigoma katika ofisi kuu ya CCM mkoa, Lowassa alisema Serukamba ni
mmoja wa wanakamati katika
↧
Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo Kujulikana Agosti 10
MGOMBEA wa Urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu kupitia chama cha ACT-Wazalendo, anatarajia kujulikana Agosti 10 mwaka huu.
Atakayebahatika kupeperusha bendera ya ACT-Wazalendo pia atawajibika
kuwa tayari kutangaza mali binafsi na vyanzo vyake kwa kutokana na
utaratibu ulioainishwa katika sehemu ya sita ya nyongeza ya kwanza ya
Katiba ya Chama hicho.
Hayo yalisemwa jana mjini
↧
↧
Yamoto Band kutimkia kwa GodFather
Kundi la muziki wa bongo flava nchini, Yamoto Band wanatarajia kukwea
pipa kwenda Afrika Kusini kwa ajili yakufanya video ya wimbo wao ‘Cheza
kwa Madoido’ na muongozaji mahili barani Afrika, Godfather.
Yamoto Band ambao usiku wa kuamkia jana walitwaa tuzo ya Kili katika
kipengele cha ‘Kikundi bora cha muziki (Bongo Flava) wameamua kwenda
Afrika Kusini kufanya video ikiwa ni hatua
↧
Dk Asha-Rose Migiro Ajitosa Kuwania Urais Kupitia CCM......Samuel Sitta Kurudisha Fomu ya Urais Leo
WAZIRI wa Sheria na Katiba, Dk Asha-Rose Migiro leo anatarajia
kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuwania nafasi ya urais
kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Aidha, taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii, kuwa Waziri wa
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein kuwa atachukua
fomu si za kweli kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya CCM.
↧
Urais 2015: Wanachama CUF waitikisa Dar, Prof. Lipumba Achukua Fomu ya Urais........Aweka Hadharani Vipaumbele Vyake
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba jana
alianzisha mchakato wa kuwania urais kupitia muungano wa kambi ya
upinzani nchini unaofahamika kama Ukawa, huku akisema yeye ndiye mtu
pekee anayefaa kupeperusha bendera ya vyama vya upinzani.
Akitangaza azma yake ya kuwania urais baada ya kuchukua fomu jijini
Dar es Salaam, alisema kutokana na kubobea katika
↧
Rais Obama Kupelekewa ‘kifimbo’ cha Nyerere
RAIS wa Marekani, Barack Obama anatarajiwa kuwa kiongozi wa tatu
duniani kuanza kubeba kifimbo kama kile cha Mwalimu Nyerere ambacho
tayari kimechongwa kwa ajili yake na msanii yule yule aliyetengeneza
fimbo ya Baba wa Taifa.
Kiongozi wa pili kukabidhiwa ‘kifimbo cha uongozi,’ kama kile cha
Nyerere alikuwa ni Rais Jakaya Kikwete aliyepewa rasmi fimbo yake
mwishoni mwa wiki mjini
↧
↧
Lowassa Aendelea Kupata Maelfu ya Wadhamini Mikoa ya Katavi na Rukwa.
Waziri mkuu wa zamani Mh. Edward Lowasa ameendelea na ziara yake ya kutafuta wadhamini katika mikoa ya Katavi na Rukwa na kupata maefu ya wadhamini na amewataka waananchi waliojiandikisha kutunza vizuri shahada zao kwani ndio tiketi ya kuwawezesha kufikia ndoto zao za kuchagua kiongozi wanayemtaka.
Mh. Lowasa baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mpanda na kupata mapokezi
↧
Faiza Ally Awaacha Watu hoi Tuzo za Kill 2015
Mwanadada faiza ally amezua gumzo kwenye fainali tuzo za
Kilimanjaro music Award zilizofanyika usiku wa kuamkia jana katika ukumbi wa
Mlimani City jijini Dar es salaam.
Mwanadada huyo alitinga kwenye Red kapeti tuzo za kili akiwa
na vazi linao onesha baadhi ya sehemu za makalio zikiwa wazi kama
ambavyo anao onekana katika picha hapo chini suala lililozua minong’ono
kwa baadhi
↧
Tanzia: Mufti Issa Bin Shaaban Simba( Kiongozi Mkuu wa Waislamu nchini Tanzania) Afariki Dunia
Kiongozi Mkuu wa Waislamu nchini
Tanzania, Mufti Issa Bin Shaaban Simba amefariki dunia leo asubuhi akiwa
Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa.
Marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari pamoja na shinikizo la damu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN
↧
More Pages to Explore .....