MVUTANO mpya unatarajiwa kuibuka katika ugawaji wa majimbo mapya kati ya
vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na Chama Cha
Mapinduzi (CCM).
Hatua hiyo inatokana na uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
kutangaza ugawaji wa majimbo ya uchaguzi huku mapya yakitarajiwa
kuongezeka.
Mchakato huo wa kugawa majimbo ya uchaguzi unatarajiwa kuanza leo kwa
kutoa tangazo
Majimbo Ya Uchaguzi Kupangwa Upya......Idadi Ya Wabunge Mwakani Kuongezeka, UKAWA Wapata Kibarua Kipya
↧
↧
Mwigulu Nchemba apewa ‘Upako’ wa Urais
Askofu Mkuu wa Kanisa la General Mission Center Limited (GMCL)
la jijini hapa, Nabii David Mpanji juzi alimkabidhi mafuta ya upako,
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba kwa ajili ya kung’arisha nyota
yake katika harakati zake za kuwania urais.
Nabii Mpanji alisema mafuta hayo yanaashiria
ufalme na utawala na kusisitiza kwamba kitendo hicho ni kudhihirisha
kuwa Nchemba, ambaye
↧
Kauli ya Shilole na Mchumba Wake Juu ya Picha CHAFU za Shilole Akiwa Stejini
Haya ndiyo maelezo ya wawili hao kuhusiana na picha za mwanadada
shilole zikimuonyesha wazi sehemu ya kifua chake wakati akiwa stejini
anatumbuiza huko nchini Ubelgiji.
"Show ni movement na uwezi mkataza mtu kupiga picha ukiwa kwa
stage'na kuna nguo za show na nguo za kutoka out kikawaida'ukiruka ruka
sana sidiria ni rahisi kuchomoka akina dada mnafaham na mtu yupo stejini
anakua
↧
Bunge La Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka 2015/2016 Laanza Mjini Dodoma Leo
Mkutano wa 20 na wa mwisho wa Bunge la 10 ambalo litapitisha Bajeti
Kuu ya Serikali kwa mwaka 2015/16 tayari umeanza mjini Dodoma asubuhi
hii.
Wabunge watachangia bajeti za wizara na Bajeti Kuu ya Serikali ndani
ya siku 44 ikilinganishwa na siku 56 zilizotumika kupitisha bajeti ya
mwaka 2014/15 na miaka ya nyuma na bunge hilo litamalizika Juni 27.
Badala ya Bunge kuanza saa 3.00
↧
Kundi La Vijana Marafiki Wa Lowassa Wafika Kilele Cha Mlima Kilimanjaro
Kundi la marafiki wa Lowasa kutoka kanda ya Kaskazini wakiwa katika kituo
cha Kibo, wakiwa katika maandalizi ya kuanza kwenda kwenye kilele cha
Mlima Kilimanjaro.
Sehemu ya juu ya mlima Kilimanjaro ikiwa imefunikwa kwa theruji.
Kundi la Marafiki wa Lowasa wakiwa katika kituo cha Stella, kikiwa ni kituo cha mwisho kuelekea kilele cha Uhuru.
Safari ya kurudi
↧
↧
Mkurugenzi Mkuu Vodacom aliyejiuzulu Aula Qatar ......Mitandao Yahusisha Kujiuzulu Kwake na Kashfa ya Upotevu wa Bilioni 700 za Kitanzania
Aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa Vodacom aliyejiuzulu hivi
karibuni Rene Meza amepata shavu katika kampuni nyingine ya
mawasiliano nchini Qatar ijulikayo kama Ooredoo Mynmar kuwa Mwenyekiti
mtendaji wa tawi la Mynmar.
Aidha, taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na kampuni hiyo
imesema kwamba Rene Meza atachukua nafasi ya Ross Cormack ambaye anatarajiwa kuachia
↧
Afande Selle: Picha niliyopigwa nikiwa na boxer haitonikosesha ubunge wa Morogoro Mjini
Seleman Msindi aka Afande Selle anawania kuwa mbunge mtarajiwa wa
jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi cha chama cha ACT Tanzania, na
haogopi maneno ya ‘haters’ wanaotaka kukiwekea mchanga kitumbua chake
kwa mambo yaliyopita.
Bila shaka unakumbuka ile picha ambayo Afande alipigwa akiwa amevua nguo na kubakia na boxer tu jukwaani wakati akitumbuiza!
Mfalme huyo wa Rhymes anaamini
↧
Serikali Yapewa Mbinu Kujikimu Katika Bajeti
WAKATI Tanzania ikiwa imeshindwa kutekeleza Malengo ya Milenia wadau wa uchumi wametoa mbinu za kujikimu katika bajeti badala ya kutegemea nchi wahisani.
Malengo manane ya Milenia ni pamoja na suala la kuondoa umasikini na njaa, elimu ya msingi kwa wote, usawa wa jinsia, kuzuia vifo vya watoto, afya ya uzazi, kupambana na Ukimwi, malaria na magonjwa mengineyo.
Akizungumza katika
↧
Upinzani Burundi Wawaonya Marais EAC
WAKATI marais wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wakitarajiwa kukutana Dar es Salaam leo kujadili mzozo wa Burundi, wapinzani wa Rais Pierre Nkurunziza, wameapa kwa kusema kuwa ni lazima kiongozi huyo ang’atuke madarakani.
Pamoja na hali hiyo pia wameonya kuwa silaha zinazozagaa kwa wanamgambo nchini humo zikusanywe kwa vile ni hatari hata kwa usalama wa nchi
↧
↧
Rais Kikwete Amteua Diwani Athumani kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya Jinai(DCI) .......Valentino Mlowola Kateuliwa Kuongoza Idara ya Intelijensia ya Jinai
RAIS Jakaya Kikwete amemteua Kamishna wa Polisi (CP) Diwani Athumani Msuya kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI),.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, kabla ya uteuzi huo, Diwani alikuwa Kaimu Kamishna wa Kamisheni ya Intelijensia ya Jinai.
“CP Diwani anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Robert Manumba ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria,”
↧
Rais kikwete Atembelea Maeneo Yaliokumbwa na mafuriko-Dar
RAIS Jakaya Kikwete jana alitembelea maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam ambayo yameathirika na mafuriko kutokana na mvua inayoendelea kunyesha.
Ziara hiyo ilianzia katika daraja linalotenganisha Mbagala Kuu na Mtoni Kijichi katika Wilaya ya Temeke na kumalizia katika Daraja la Jangwani katika Wilaya ya Ilala.
Rais Kikwete baada ya kuona daraja linalotenganisha Mbagala Kuu na
↧
Mashabiki Wachukizwa na Picha Hizi za Aunt Ezekiel
Staa wa bongo movies, Aunt Ezekiel amepondwa na baadhi ya mashabiki
wake kwa kupiga picha hizi akionyesha tumbo lake ukizingatia yeye ni
mjamzito.
Picha hizi zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii na
wengi wameonyesha kuchukizwa na tabia iliyozuka ya mastaa wa Bongo
kufanya hivi kwa kuwaiga mastaa wa nchi za ughaibuni.
Wewe, unamaoni gani juu ya hizi
↧
Wolper: Anayetoka na Nay wa Mitego Ameshajulikana..Nay Akuwahi Kuwa Mpenzi Wangu
Staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper, amewaweka njia panda mashabiki
wake kwa kauli yake kwamba msichana aliyekwenye uhusiano wa kimapenzi na
msanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’
ameshafahamika, tofauti na alivyokuwa akihisiwa yeye.
“Watu hawana dogo, ukiwa karibu na mtu basi utaambiwa mpenzi wako, Nay
hakuwahi kuwa mpenzi wangu kwa kuwa ni zaidi ya rafiki
↧
↧
‘Friends of Lowassa’ kuchangia damu Muhimbili
MAKAMU Mwenyekiti wa marafiki wa Waziri Mkuu wa zamani ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Angel George, amesema mipango imekamilika ya kwenda kuchangia damu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
George alitoa taarifa hiyo jana jijini hapa, baada ya kusoma taarifa kwenye vyombo vya habari ikieleza kwamba, Hospitali ya Taifa Muhimbili inakabiliwa na
↧
Serukamba Awasha "MOTO" Bungeni Kuhusu Sakata la Escrow na Opareshi Tokomeza.......Ashangazwa Na Kitendo Cha Ikulu Kuwasafisha Baadhi Ya Watuhumiwa
MBUNGE wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba (CCM), ametonesha vidonda vya ufisadi baada ya kuzungumzia ripoti ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue iliyowasafisha baadhi ya watendaji serikalini waliohusika katika kashfa ya Escrow.
Serukamba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, alishangazwa na taarifa hiyo kuwasafisha baadhi ya watu waliohusishwa katika kashfa hiyo na
↧
Waziri wa Ulinzi Auawa Kwa bunduki ya Kutungulia Ndege aina ya ZPU-4 Akituhumiwa KUSINZIA Kwenye Mkutano wa Rais
Hyon Yong-Chol aliyeuawa kwa kusinzia wakati wa hafla ya kijeshi.
WAZIRI wa Ulinzi wa Korea ya Kaskazini, Hyon Yong-Chol, ameuawa kwa
kupigwa na bunduki ya kutungulia ndege aina ya ZPU-4 kwa kusinzia kwenye
hafla ya kijeshi. Waziri huyo aliuawa kutokana na amri ya kiongozi wa
nchi hiyo, Kim Jong-Un.
Bunduki ya kutungulia ndege aina ya ZPU-4 iliyotumika kumuua Hyon.
↧
Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania
Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare
ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza
amepinduliwa madarakani.
Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua
hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya
tatu ya urais wa Nkurunziza.
Jenerali
huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema
↧
↧
Marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki WALAANI Jaribio la Mapinduzi Burundi......Aliyetangaza Mapinduzi Asema Kiburi Chake Kimemponza
WAKUU wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC),
wamelaani jaribio la mapinduzi ya kumng’oa Rais Pierre Nkurunziza wa
Burundi na kutaka Katiba ya nchi hiyo ifuatwe ili kudumisha amani na
utulivu nchini humo.
Aidha, wameagiza mamlaka husika nchini Burundi kutangaza kusimamisha
kwa muda uchaguzi mkuu uliokuwa ufanyike Juni 26 mwaka huu ili kurejesha
hali ya amani katika
↧
Hatma ya Rais Nkurunziza Bado Haijulikani.....Baraza la Usalama la UN Laitishwa kwa Dharura, Marekani Yasema Bado Inamtambua Nkurunzinza kama Rais
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kufanya mkutano wa
dharura hii leo kuijadili Burundi baada ya jenerali mwandamizi wa jeshi
nchini humo kutangaza kumpindua Rais Pierre Nkurunzinza kutoka
madarakani.
Ufaransa ndiyo imeitisha kikao hicho cha dharura ambacho kitafanyika hii
leo punde tu baada ya wanachama wa baraza hilo la usalama la Umoja wa
Mataifa kuijadili Iraq.
↧
Vijembe Vya Kisiasa Vyatawala Bungeni......Lusinde Asema Dr Slaa Hafai Kuwa Rais Maana Ikulu Sio Wodi Ya Wagonjwa
VIJEMBE vya kisiasa jana vilichukua sehemu kubwa ya mjadala wa Bajeti
ya Ofisi ya Waziri Mkuu unaoendelea, ambapo mvutano mkubwa ulikuwa kati
ya Serikali na vyama vya upinzani nani amechoka.
Akizungumza bungeni kwa vijembe, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde
(CCM), alisema hoja ya kambi rasmi ya upinzani kuwa Serikali imechoka,
inawezekana ni kweli ila haikuwekwa vizuri.
↧