Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mabweni ya Shule ya sekondari Idodi Jimboni kwa Lukuvi Yateketea kwa Moto TENA

$
0
0
BWENI la wanafunzi wa shule ya sekondari ya Idodi iliyoko Jimbo la Isimani Wilaya ya Iringa Vijijini Mkoani Iringa, limeteketea kwa moto na kusababisha hasara ya mamilioni ya shilingi, ikiwa ni miaka sita tu tangu bweni hilo liungue na kusababisha hasara kubwa na vifo vya wanafunzi 13.   Agosti 25, 2009 bweni la shule hiyo, liliwaka moto na kusababisha vifo vya wanafunzi wa kike 13, ambao

Mtuhumiwa sakata la Escrow kizimbani leo

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo inatarajia kumsomea maelezo ya awali Mkurugenzi wa Sheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rugonzibwa Mujunangoma anayekabiliwa na kesi ya kupokea Sh milioni 323.4 ambazo ni sehemu ya fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow.   Mujunangoma anatarajiwa kupanda kizimbani na kusomewa maelezo ya awali mbele ya Hakimu Mkazi

Uchaguzi Mkuu 2015: Polisi yaapa Kukabiliana na Vurugu za Aina Yoyote.....“Tutawakomesha Waleta Vurugu”

$
0
0
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limeahidi kuwa limejipanga vizuri, kukabiliana na vurugu na matukio ya kihuni kuelekea uchaguzi mkuu, utakaofanyika Oktoba mwaka huu.   Hayo yalisemwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Mihayo Msikhela alipozungumza na mwandishi ofisini kwake mjini hapa jana.   “Hatutakuwa na msalie Mtume kwa mtu yeyote atakayejihusisha na uvunjifu wa amani na kufanya mambo ya

Baba Amuunguza Mdomo Mwanae kisa Kadokoa Maharage

$
0
0
Vitendo vya kikatili na unyanyasaji wa Wanawake na watoto vinaendelea kushika kasi licha ya Serikali na mashirika mbalimbali ya haki za Binadamu kupiga vita vitendo hivyo kwa nguvu . Hali hiyo imejitokeza katika kijiji cha Kasaka, Kata ya Nyaruyoba Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma baada ya Baba mzazi aliyefahamika kwa jina la Sindotuma Nyamubi, kumchoma moto na kumuunguza vibaya sehemu za

Shinyanga Yaendelea Kulia na Ukosefu wa Maji.....Hizi ni Picha za Wakazi wake wakiteseka kutafuta Maji

$
0
0
WAKAZI wa manispaa ya Shinyanga na viunga vyake, wameendelea kuteseka kwa kukosa maji safi na salama kwa mfululizo wa siku nne sasa, baada ya mitambo ya kusukuma maji kutoka chanzo cha ziwa Victoria (Ihelele), na kusambaza maji hayo katika miji ya Kahama na Shinynga kupata hitilafu kwenye mfumo wa umeme.   Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamezitupia lawama mamlaka za

Matokeo ya Kidato cha Nnne ( Form four ) Kutangazwa Jumapili ya Wiki Hii

$
0
0
Matokeo ya mitihani ya kidato cha nne nchini ya mwaka 2014, yanatarajiwa kutangazwa na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Jumapili wiki hii. Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde (pichani), alitoa ahadi hiyo kama zawadi kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mpwapwa mkoani Dodoma, kufuatia ajali ya moto iliyotokea Januari  20, mwaka huu na kuteketeza mali zote zilizokuwa kwenye bweni

CHADEMA: Hatutakubali Kura Zetu ziibiwe tena.....Mbowe Azindua Mafunzo ya vijana 200 wa Red Brigade na Wacheza Kareti

$
0
0
Chama  Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kimejipanga kuhakikisha katika uchaguzi Mkuu hawaibiwi kura. Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa chama hicho, Freemon Mbowe  wakati akizindua mafunzo ya Kikosi cha Ulinzi na Usalama cha chama hicho (Red Brigade), kwa vijana 200 wa  Kanda ya Kati pamoja na Kikosi maalum cha Karate. “Katika  uchaguzi huu hatutaki  kulalamika

Mtoto wa Miaka 6 Abakwa na Kunyongwa Porini

$
0
0
MKAZI wa Kijiji cha Mayaka, Kata ya Minyughe, Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida, Samaha Mtawa (6) amekufa baada kubakwa na kunyongwa wakati akichuma matunda porini.   Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi, Thobias Sedoyeka, mwili wa mtoto huyo ulionekana Februari 7 mwaka huu saa 12 asubuhi umbali wa mita 150 kutoka nyumbani kwao.   "Uchunguzi wa awali

Hizi ni picha zinazoonyesha Jengo la ghorofa tatu la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lilipo Dar likiungua Moto.

$
0
0
Moto Mkubwa umezuka mapema leo kwenye moja ya nyumba za Jengo la ghorofa tatu la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lililopo Mtaa wa Moscow na Libya eneo la Posta Jijini Dar es Salaam na kuteketeza  mali kadhaa.    Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika rasmi.Jeshi la Polisi liliwahi kufika eneo la tukio kuhakikisha amani na utulivu vinakuwepo huku magari ya zimamoto nayo yakiendelea

Sauda Mwilima Ayaanika Maziwa Yake

$
0
0
Mtangazaji wa kituo kimoja cha runinga nchini, Sauda Mwilima ‘Mwarabu wa Kigoma’ juzikati alionekana akiwa ameachia nido zake ukumbini. Tukio hilo lilitokea katika Ukumbi wa Escape One, jijini Dar ambapo Sauda alikuwa ameambatana na mumewe, Kauli Juma huku sehemu ya kifua chake ikiacha nido zake wazi kutokana na nguo aliyokuwa ameivaa.   “Jamani hivi siku hizi imekuwa ni fasheni watu

Picha za Ommy Dimpoz na Wema Sepetu wakiwa kimahaba Kitandani zilipigwa Usiku wa Manane.....Dimpoz adai hakuwa na fahamu.

$
0
0
Zile picha za mahaba zilizosambaa kwenye mitandao zikimuonyesha Staa wa Bongo Fleva,Ommy Dimpoz na Wema Sepetu wakiwa kitandani zimezidi kuzua utata baada ya Ommy kusema hakujua alipigwa saa ngapi kwani hakuwa na fahamu bali aulizwe Wema. Ommy akizungumza katika  kipindi  cha  Uheard na Soudy Brown amesema kuwa hana maelezo zaidi ya kuzungumza zaidi ya kusema kuwa hajui ni muda upi

Suti ya Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mh Steven Wassira Yageuka GUMZO Baada ya Kukosewa Kufungwa Vifungo

$
0
0
Suti  ya  Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mh Steven Wassira  imegeuka  gumzo  mtandaoni baada  ya  kukosewa  kufungwa  vifungo  vyake..... Wassira  alionekana  ndani  ya  vazi  hilo wakati  wa   Sherehe za Utume zilizoandaliwa na kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) na kujumuisha nchi zingine 11 za Afrika Mashariki na Kati.   Sherehe  hizo  zilizofanyika  juzi uwanja wa taifa 

Uagizaji Mafuta kwa Pamoja Kuokoa Mabilioni

$
0
0
Tanzania inatarajia kuokoa mabilioni ya fedha kutokana na kuanza kutekeleza mfumo wa uagizaji mafuta kwa pamoja na kwa kiasi kikubwa. Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage alipofungua programu ya mafunzo maalumu ya wajasiriamali wanaoagiza nishati ya mafuta, yaliyoandaliwa na First National Bank (FNB).   Mafunzo hayo yanahusu namna

Kesi ya Sheikh Ponda Kusikilizwa tena Februari 16

$
0
0
Kesi inayomkabili kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini Shehe Ponda Issa Ponda jana imeahirishwa  hadi  Februari 16, mwaka huu kwa mashahidi wa upande wa mashitaka kuendelea kutoa ushahidi  mahakamani. Tayari mashahidi saba wa upande huo wameshatoa ushahidi wao mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mkoa wa Morogoro, akiwemo aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Faustine

Afisa Mtendaji Atandikwa Makofi Hadharani

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendegu **  OFISA Mtendaji wa kijiji cha Lumesule, Kata ya Lumesule, wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara, Swalehe Daimu, anadaiwa kupigwa na mkazi wa kijiji hicho, kwa madai ya kumkamata dada yake na kumtoza faini ya Sh 5,000 kwa kushindwa kushiriki shughuli za ujenzi wa maabara.   Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendegu, kijijini hapo jana,

Tanzania Yasikitishwa na Uamuzi wa Kenya wa kuzuia magari ya kitalii ya Tanzania

$
0
0
Serikali imeelezea kusikitishwa na uamuzi wa Kenya wa kuzuia magari ya kitalii ya Tanzania kwenda kuchukua na kushusha watalii wanaotumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, kwa kusema kuwa hatua hiyo haijengi wala kuendana na dhamira njema ya mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe alisema jana kuwa,  dhamira ya

Washitakiwa wa Kesi ya Dk Sengondo Mvungi waomba Kusikilizwa

$
0
0
Washitakiwa wa kesi ya mauaji ya mjumbe wa Tume ya Taifa ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi wameiomba Mahakama iwape haki ya kuwasikiliza. Waliwasilisha ombi hilo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema wakati kesi hiyo ilipotajwa na Wakili wa Serikali, Leonard Challo kudai upelelezi bado haujakamilika.   Mshitakiwa Longishu Losingo

Mwalimu Apandishwa Kizimbani kwa Kupora Mume wa Mtu

$
0
0
MWALIMU wa Shule ya Msingi Manga katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Mary Majilanga amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Utemini, mjini Singida kujibu shitaka la kukamatwa ugoni .   Katika kesi hiyo ya madai namba 8 ya mwaka huu, mshitakiwa Mary anatakiwa kulipa Sh milioni 8 za ugoni kwa kuishi kama mume na mke na mwalimu mstaafu, Julius Magandi ambaye imeelezwa ni mume

Simanzi Yatawala Wakati wa Mazishi wa Ndugu Sita wa Familia Moja Walioteketea kwa Moto Dar

$
0
0
Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal jana aliwaongoza mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, kuzika miili ya watu sita wa familia moja waliokufa katika ajali ya moto wakiwa nyumbani kwao Kipunguni, Manispaa ya Ilala usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita. Katika maziko hayo yaliyofanyika makaburi ya Airwing yaliyopo Ukonga Banana, ibada ya maziko iliongozwa na Askofu Msaidizi wa Kanisa

Babu Amlawiti Mjukuu Wake wa Kike.....Amhonga sh.2000 ili Asitoe Siri

$
0
0
POLISI wilayani Masasi mkoani Mtwara inamshikilia mkazi wa kijiji cha Maili Sita kata ya Mtandi, Daudi Pilipili (44) kwa tuhuma za kumlawiti mjukuu wake wa kike mwenye umri wa 13.   Mkuu wa Polisi wilaya ya Masasi, Azaria Makubi alisema inadaiwa alitenda kosa hilo juzi saa 9:00 katika kijiji cha Maili Sita huku bibi wa mtoto akiwa amekwenda nyumbani kwa mwalimu wa shule anakosoma mjukuu
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images