Baadhi ya watendaji wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), pamoja na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), ni miongoni mwa watendaji wa taasisi nne ambao wametajwa katika utafiti kuwa wamekithiri kwa kupokea rushwa.
Takukuru na TRA zimetajwa kuwa na kadhia hiyo katika ripoti ya Taasisi ya Afro Barometer iliyofanywa kwa kushirikiana na Taasisi ya Kupunguza Umasikini (Repoa).
Polisi Yaongoza kwa Rushwa.....TRA, Mahakama na TAKUKURU Nao Wamo
↧
↧
Lowassa Ageuka Mbogo......Asema hana Haja ya Kutumia Pesa Kumnadi Mtu, Apangua tuhuma za Kuwahonga Milioni 10 Makada wa CCM
WAZIRI Mkuu wa Zamani Edward Lowassa, amekanusha taarifa
zilizochapishwa na gazeti moja la kila wiki iliyosema “Lowassa apanga
safu”, akisema hana haja ya kufanya hivyo wala kutumia fedha kumnadi
mgombea yeyote.
Taarifa iliyotolewa na ofisi yake ilisema habari hiyo ilijengwa na
taswira ya uongo kwamba kuna mpango wa kupanga nani atagombea ubunge
katika Jimbo la Monduli baada ya
↧
Familia, polisi, kanisa wamtenga askari aliyejiua kwa risasi mdomoni.....Mama mzazi asema kujiua ni ishara ya mkosi katika familia
Polisi aliyejiua kwa kujipiga risasi mdomoni, Aloyce Mafuru
(24), amezikwa katika makaburi ya Mugumu, Wilaya ya Serengeti, Mkoa wa
Mara bila huduma za kidini na kijeshi.
Askari huyo aliyekuwa dereva wa Kamanda wa Polisi
Wilaya ya Manyoni, Alute Makita alijiua Februari 2 nyumbani kwake na
kuacha ujumbe kuwa polisi wasiangike kufanya uchunguzi kwani huo ni
uamuzi wake binafsi.
↧
Diamond Akanusha Kupewa Milioni 500 na Lowassa ili Ampigie Kampeni....Asema taarifa hizo zinalengo la Kumchafua Lowassa
Meneja wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’, Babu
Tale, amesema hawajawahi kupewa kiasi cha fedha Sh mil 500 na Waziri
Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, ili wampigie kampeni za urais kupitia
Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na Mpekuzi, Babu Tale alisema watakuwa wehu
kukataa fedha nyingi kiasi hicho wakati wenyewe wanafanya muziki ili
kupata fedha, lakini
↧
Penzi la Wema Sepetu na Ommy Dimpoz Lawekwa Hadharani.......Wapiga Picha wakiwa bafuni Usiku
Hatimaye zile tetesi kwamba mwigizaji Wema Sepetu na
msanii wa muziki Ommy Dimpoz wanatoka kimapenzi zimekuwa kweli kwa zaidi ya asilimia 200....
Tetesi hizo zimethibitishwa na picha waliyopiga jana
usiku wakiwa bafuni huku Wema akiwa amevaa taulo tu na Ommy Dimpoz akionekana kwa mbali kama ananawa mikono.
Picha hii iliamsha watu kibao usiku wa jana hasa wale Team Wema, kwani
↧
↧
Alichokijibu Mbunge James Mbatia kuhusu ishu ya kusema kuwa Mrema ana UKIMWI
Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP) alitoa hoja binafsi Bungeni kwamba Mbunge James Mbatia amekuwa akipita Jimbo la Vunjo na kuwaambia wapigakura wasimchague Mrema kwa sababu ana UKIMWI.
“Napenda kusema kuwa mimi ni mbunge halali wa Vunjo na Mbatia hatapata jimbo hilo na ninatangaza kuwa nitagombea tena na hafi mtu hapa“– Alisema Mrema wakati akimalizia kuwasilisha hoja yake hiyo.
↧
Amanda Poshy: Msinipangie Wavazi ,nikivaa nguo fupi ni Mimi na kama Najiuza Niacheni Maana nauza Papu*chi yangu ....Sijaazima ya Mtu
Mwigizaji wa filamu, Amamnda Poshi amewatolea uvivu wanaomponda kwa kuvaa nguo fupi huko Instagram.
Amanda amewataka mashabiki wake kuachana na maisha yake binafsi kwa madai kuwa kama maisha yake yanategemea kujiuza kingono basi wamwache maana anayoiuza ni Papu**chi yake mwenyewe na hajaazima kwa mtu.
Huu ni ujumbe wake alioundika:
“Instagrameee
↧
Bunge Laahirishwa hadi March 17, 2015.....Serikali Yaahidi Kuwashughulikia wanaosababisha Migogoro ya Ardhi
Mkutano wa 18 wa Bunge la Jamhuri ya muungano umemalizika leo kwa bunge kujadili na kupitisha maazimio ya jinsi ya kumaliza migogoro ya ardhi nchini.
Katika maazimio hayo yaliyopokelewa na serikali , serikali imeziagiza mamlaka husika kuwachukulia hatua watendaji wote waliopewa dhamana za uongozi ambao wanasababisha migogoro ya Ardhi, Wakulima na Wafugaji kuendelea na kuifanya kama miradi
↧
Albino Vijijini HATARINI Kupata Saratani ya Ngozi
Watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) wanaoishi vijijini, wana hatari ya kupata magonjwa ya saratani ya ngozi, kutokana na kutokuwa na elimu ya afya bora na utunzaji wa ngozi.
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu wa Ngozi mkoani Dodoma, Ludovick Kowo, katika warsha ya mafunzo ya afya bora na utunzaji wa ngozi kwa albino wilayani Kongwa.
Alisema kutokana na ukosefu
↧
↧
Tume ya Utumishi wa Walimu Kuanza kazi mwezi wa Saba
Serikali imesema Tume ya Utumishi wa Walimu itaanza kazi Julai mwaka huu na kuhudumia walimu katika masuala mbalimbali huku muundo wa utumishi wa tume hiyo umehusisha ngazi za chini na juu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema serikali imekubali kuanzisha tume hiyo ya kuhudumia walimu nchini ili kuepuka walimu kuhudumiwa na wizara mbalimbali
↧
Mikoa 6 TAABANI Katika Ujenzi wa Maabara
Mikoa sita 'imevurunda' katika ujenzi wa maabara katika shule za sekondari baada ya kushindwa kufikia malengo. Ni mikoa mitatu pekee ndiyo imefanya vizuri kwa kuvuka nusu ya malengo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alitaja mikoa ambayo haikufika hata robo ya malengo kuwa ni Mtwara (asilimia 21), Lindi (asilimia 20), Tabora (asilimia 17), Dodoma (asilimia 12), Rukwa (asilimia 11) na Kigoma (
↧
Alikiba kuhusu collabo na Diamond: Nikiwa na wimbo unaomfaa ntamshirikisha
Alikiba amedai anaweza kumshirikisha Diamond kama tu akipata wimbo unaomfaa msanii huyo.
“Ngoja nikwambie ukweli, sidhani kama ninaweza kuja kufanya kolabo na
Diamond, ila nikipata wimbo ambao nadhani kwamba anastahili kuwapo,
kiukweli nitamshirikisha lakini kama hastahili haitawezekana,” Alikiba
aliliambia gazeti moja la kila siku.
Kwa upande mwingine akijibu swali la kama ana
↧
Mwasiti: Napromise March nitamuweka boyfriend wangu kwenye mtandao
Baada ya maswali kuwa mengi kuhusu uhusiano baina ya mtangazaji wa
EATV/EA Radio, Sam Misago na mwimbaji Mwasiti Almasi, wawili hao
wameamua kuzikanusha kwa pamoja taarifa hizo kupitia kipindi cha Friday
Night Live cha EATV jana Feb 6.
Tarehe 6 Feb. ilikuwa ni birthday ya Sam Misago, na katika
kuisheherekea aliwakaribisha studio za EATV wasanii Mwasiti, Damian Soul
na Makomando
↧
↧
Dereva Bodaboda Atuhumiwa Kulawiti Mwanafunzi wa Chekechea Kibaha
Dereva bodaboda Ismail Lucas (16), mkazi wa Kwa Mathias wilayani Kibaha mkoani Pwani, anatuhumiwa kumlawiti mtoto ambaye ni mwanafunzi wa Chekechea.
Mama wa mtoto huyo (jina limehifadhiwa) alisema kuwa kutokana na tukio hilo, mwanawe (jina limehifadhiwa) alijeruhiwa vibaya.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea saa 3:00 asubuhi eneo la Tanita wakati mtoto huyo alipokuwa akitokea dukani
↧
Wajawazito Wajifungua kwa VIBATARI Miaka Mitano-Masasi
Wajawazito wakazi wa kata za Sululu na Matawale katika Halmashauri ya Mji wa Masasi mkoani Mtwara, wamekuwa wanajifungua kwa kutumia vibatari muda wa usiku zaidi ya miaka mitano sasa.
Diwani wa Kata ya Sululu, Peter Mrope alisema hayo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi.
Alisema kuwa hali ya zahanati sio nzuri na zaidi ya miaka mitano wakazi wake na kata ya jirani
↧
Mama mzazi wa Nay wa Mitego anahisi mwanae ni freemason na hataki kupokea fedha yake
Mama mzazi wa Nay wa Mitego anahisi mwanae ni mfuasi wa jamii ya siri ya freemason na ameanza kusita kupokea fedha kutoka kwake.
Kwa mujibu wa mama yake, mafanikio ya haraka ya Nay yakiwemo kujenga
nyumba ya kifahari, kumiliki magari kadhaa na maisha yake ya kimilionea,
vimemfanya aamini maneno yanayosemwa na watu au kuandikwa kwenye
magazeti ya udaku kuwa mwanae amepata utajiri huo kwa
↧
Muswada wa Mahakama ya Kadhi kujadiliwa Bunge Lijalo
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameeleza sababu za Bunge kushindwa kujadili miswada kadhaa, ikiwemo uliohusu Marekebisho ya Sheria ya Kiislamu, inayotambua Mahakama ya Kadhi.
Akihitimisha shughuli za mkutano wa 18 wa Bunge jana, Pinda alisema muswada huo umesogezwa mbele, ili Kamati ya Bunge ipate nafasi na muda wa kupitia na kutoa ushauri kwa Bunge.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya
↧
↧
Wema Sepetu: Kwasasa Nimetulia, Nataka Kuolewa!
Wema Sepetu amechoka uhusiano wa boyfriend na girlfriend. Muigizaji hiyo wa filamu amesema anataka kuolewa.
Wema alisema hayo jana kwenye reality show yake, In My Shoes baada ya
meneja wake Martin Kadinda kumuuliza kwanini hana ‘kiki’ kwa sasa.
Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 alisema kuna vitu vingi anataka kuvifanya ikiwemo kuwa na hamu ya kutulia na kuwa mke wa mtu.
Hata
↧
Moto Wateketeza Babu, Bibi,Watoto na Wajukuu Dar es Salaam
Watu sita wa familia moja akiwamo Kapteni mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), wamekufa papo hapo baada ya kuteketezwa kwa moto jijini Dar es Salaam.
Janga hilo la moto limetokea jana saa 10:30 alfajiri katika eneo la Kipunguni A, Ukonga Banana, wilayani Ilala.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki alisema kuwa moto huo ulizuka ghafla katika nyumba inayomilikiwa na
↧
Matokeo ya Kidato cha Nne ( FORM FOUR) Yakamilika
Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limesema usahihishaji wa
mitihani ya kidato cha nne uliofanyika Novemba mwaka jana, umekamilika.
Katibu
mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema
kuwa “usahihishaji umekamilika na baraza lipo katika uchambuzi wa
kuyapanga na tutakapokamilisha tutayatangaza”.
Alipoulizwa
ni lini hasa matokeo hayo yatatangazwa, Dk Msonde alisema: “Tumemaliza
↧
More Pages to Explore .....