KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, imeitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kufanya ukokotoaji upya wa bei ya mafuta ili kumsaidia mlaji wa mwisho wa bidhaa hiyo kunufaika na punguzo la bei ya mafuta duniani.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kamati hiyo, Mbunge wa Tandahimba, Juma Njwayo (CCM) kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati hiyo
EWURA yatakiwa kufanya upya ukokotoaji na kupunguza bei ya mafuta ili kumnusuru mwananchi wa kawaida
↧
↧
JWTZ yaapa kupambana na majambazi wanao pora silaha za askari
Jeshi la wananchi nchini (JWTZ) kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama nchini limeahidi kukabiliana na makundi ya watu wanaodaiwa kuwa majambazi sugu ambao wanapora silaha za askari huku wengine wakiuawa hatua ambayo imeanza kutishia usalama wa nchi.
Akizungumza jijini Tanga kufuatia hivi karibuni makundi hayo kupora silaha na kisha kuua askari huko Rufiji mkoani Pwani na
↧
"Tupige kura ya NDIYO Katiba inayopendekezwa"- Rais Kikwete
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete amewataka watanzania wote kujitokeza na kuipigia Kura ya Ndiyo Katiba Inayopendekezwa muda utakapofika.
Dkt Kikwete ameyasema hayo katika sherehe za maadhimisho ya miaka 38 ya chama hicho zilizofanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea, ambapo amesema kuwa Katiba
↧
Prof. Lipumba Awataka Wananchi Kutowachukia Polisi
Chama cha Wananchi CUF kimewataka wananchi kutowachukia polisi kufuatia
kitendo cha kutotenda haki kwa raia ikiwemo kuwabambikizia kesi
mbalimbali na kuwashushia vipigo bila sababu zozote.
Hayo
yalisemwa na mwenyekiti wa taifa wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mapema jana jijini Dar es
Salaam.
Hata hivyo Profesa Lipumba amesema
↧
Rais ajaye Asipotoka CCM Nchi Itayumba - Kikwete
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Kikwete amewaagiza viongozi
wa chama hicho kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinashinda katika
uchaguzi ujao unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Dkt
Kikwete ametoa agizo hilo katika uwanja wa Majimaji mjini Songea ambapo
zimefanyika sherehe za maadhimisho ya miaka 38 ya chama hicho.
Akimnukuu mwalimu Nyerere, amesema kuwa Rais
↧
↧
Mbowe Asimikwa UTEMI wa Kabila la Wasukuma.....Asisitiza msimamo wa CHADEMA Kutoshiriki Kupiga Kura Ya Maoni Katiba Mpya
Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kimesisitiza msimamo wake
wa kutoshiriki kwenye mchakato wa kupiga kura ya maoni ya katiba mpya
inayopendekezwa na badala yake kimewataka wanachama wake na watanzania
kwa ujumla kuelekeza nguvu kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu
unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu.
Kikisisitiza msimamo huo uliotolewa hivi karibuni na
↧
Hoteli Zafungwa Arusha kwa Kukosa Watalii
Baadhi ya hoteli za kitalii mjini Arusha zimefungwa, huku mishahara ya wafanyakazi ikipunguzwa kwa asilimia 25, kutokana na kukosa watalii.
Akizungumza wakati wa tafrija ya kuukaribisha mwaka mpya 2015, zilizoandaliwa na Chama cha Mawakala wa Watalii Nchini (TATO), Mwenyekiti wa chama hicho, Willy Chambulo alisema hali ya biashara kwa miezi hii mbaya na kusababisha kufungwa kwa baadhi ya
↧
Watanzania Wahimizwa Kula Mayai ya Kwale
Watanzania wamehimizwa kutumia mayai ya ndege aina ya kwale na nyama yake kwa kuwa ni chakula bora chenye virutubisho mbalimbali.
Ushauri huo ulitolewa na mfugaji wa kwale ambaye ni mkazi wa Tegeta, Dar es Salaam, Susan Magibo alipokuwa akizungumza na Mpekuzi.
Magibo alisema ndege hao hivi sasa ni gumzo hapa nchini, kwani inasadikiwa kuwa ni dawa ya magonjwa mbalimbali kama pumu,
↧
Wabunge Waomba Wanaume Wafungwe Kizazi
Wabunge wametaka kuwepo na udhibiti wa ongezeko la watu nchini kwa kutaka wanaume wadhitibiwe katika uzazi, kama ilivyo kwa wanawake huku wengine wakitaka serikali kuboresha rasilimali bila kudhibiti uzazi.
Miongoni mwa waliotaka wanaume wafungwe kizazi kama inavyofanyika kwa wanawake ni Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki, Celina Kombani ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
↧
↧
RUSHWA: Magufuli Awafukuza Kazi Wafanyakazi 400 wa Mizani, Asema huo ni mwanzo tu
Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli amevitaka vyombo vya dola kuingilia kati suala la rushwa kwenye vituo vya mizani za kupimia uzito wa magari yanayosafirisha mizigo, akisema rushwa hiyo imekithiri.
Magufuli alitoa agizo hilo alipotembelea na kukagua kituo cha mizani cha Mpemba wilayani Momba, ambapo alipita kituoni hapo kwa kushtukiza, alipokuwa katika ziara yake ya kukagua barabara
↧
Mahakama ya Kadhi, Ripoti ya Msola Kutikisa Bunge
Bunge linaendelea na mkutano wake wa 18, ambao kamati mbalimbali zitaendelea kuwasilisha taarifa kwa ajili ya majadiliano.
Licha ya kamati za kisekta na zisizo za kisekta, kabla ya Bunge kuahirishwa wiki hii, pia Kamati Teule iliyoundwa kuchunguza na kuchambua Sera mbalimbali zinazohusu masuala ya ardhi, kilimo, mifugo, maji na uwekezaji kubaini kasoro zilizomo katika matumizi ya ardhi,
↧
Wanafunzi wajawazito kuendelea na masomo wakijifungua
Serikali imeruhusu wanafunzi wa shule za msingi na sekondari waliopata ujauzito kuendelea na masomo wanapojifungua.
Mratibu wa Masuala ya Jinsia wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Chimpaye Marango, wakati wa mjadala wa sababu za kuongezeka kwa idadi ya watoto ya mabinti wanaokosa elimu baada ya kupata mimba.
Mjadala huo ulioitishwa na asasi ya kiraia ya uchambuzi wa sera ya
↧
Polisi achomoka lindo na bunduki kwenda Kuua Raia
Jeshi la Polisi Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe, limeingia katika kashfa baada ya askari wake kutuhumiwa kumuua raia.
Raia huyo ambaye ni mkazi wa mtaa wa Mdonga, fundi wa magari, Januari Mtitu (20), inadaiwa kuwa aliuawa kwa risasi na askari mwenye namba G 6352, Abduel Nyuki.
Tukio hilo lilitokea Januari 23, mwaka huu, saa 7:00 usiku, na mtuhumiwa anafanya kazi katika Kituo cha Polisi
↧
↧
Mahabusu Afia Kituo cha Polisi Ubungo- Urafiki baada ya Kujitundika na Kunyinyonga
Mahabusu
mmoja Shabani Ramadhani (28), amekutwa amejinyonga katika choo cha
Kituo cha Polisi Ubungo- Urafiki, jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo lilitokea jana baada ya mahabusu huyo kufikishwa katika kituo hicho juzi akituhumiwa kufanya tukio la unyang’anyi.
Kaimu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Augustino Senga, alithibitisha
kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa marehemu
↧
Je, unasumbuliwa na tatizo la nguvu za kiume?? Unataka kuimarisha mishipa yako ili uweze kwenda Raundi mbili na kuendelea??....Bofya hapa ukutane na JIKO
Neema
Herbalist & Nutritional Foods Clinic ni wauzaji wa dawa
mbalimbali za asili.
Tunapenda kuwatangazia wateja wetu kuwa
tunayo dawa nzuri ya asili inatibu na kuponyesha kabisa tatizo
la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume.
Dawa hii iitwayo
JIKO ni ya asili kabisa (PURE HERBAL) na inaponyesha na
kumaliza kabisa tatizo la nguvu za kiume
↧
Kanngi Lugola ( CCM ) Awasha moto bungeni.....Awataka wananchi Wasiichague CCM
MBUNGE wa
Mwibara, Kangi Lugola (CCM), amewasha moto bungeni akifunguka kuwa
atawaambia wananchi wake wasiipigie kura CCM pamoja na yeye mwenyewe
kama maji hayatapatikana jimboni mwake wakati akichangia katika
majiadiliano ya hoja za kamati bungeni leo.
Pia Lugola
amehoji kwa nini nguvu zinazotumika kuwapiga watu kama akina Profesa
Lipumba zisitumike kupambana na wawekezaji
↧
Francis Cheka Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela
Bondia maarufu nchini wa ngumi za kulipwa Francis Cheka amehukumiwa kifungo cha miaka 3 jela na kutakiwa kulipa fidia ya shilingi millioni 1 kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi meneja wa baa yake iliyopo huko Morogoro
Meneja huyo ajulikanaye kwa jina la Bahati inaelezwa alienda kudai fedha zake alizokuwa hajalipwa na bondia huyo wakati akifanya kazi ya umeneja katika baa yake hiyo ndipo
↧
↧
Zitto Kabwe Amtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu AJIUZULU Ifikapo leo jioni
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amemtaka Waziri wa Maliasili
na Utalii, Lazaro Nyalandu ifikapo leo jioni awe ametoa tangazo katika
gazeti la serikali ili kuruhusu tozo mpya za mahoteli kwenye hifadhi la
sivyo ajiuzulu cheo chake.
Zitto ameyasema hayo leo wakati akichangia kwenye majadiliano ya hoja za kamati bungeni.
Zitto amesema kuwa serikali inapoteza shilingi bilioni
↧
Mahakama kuandika hukumu kwa Kiswahili
WIZARA ya Katiba na Sheria imesema iko haja ya hukumu zinazotolewa katika Mahakama nchini, ziandikwe katika Kiswahili kuwezesha haki kutendeka na ionekane imetendeka.
Naibu Waziri, Ummy Mwalimu alisema hayo jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Mwidau (CUF) aliyeshauri serikali kuangalia uwezekano wa hukumu kutolewa kwa lugha hiyo.
“Ni kweli kwamba kuna haja
↧
"Mabilioni" ya Kikwete bado hayajarejeshwa
FEDHA zilizotolewa na serikali kwa ajili ya kuwezesha wananchi kiuchumi maarufu kama mabilioni ya Kikwete, imeelezwa sehemu hazikutumika huku nyingine zilizokopwa hadi sasa hazijarejeshwa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uwekezaji na Uwezeshaji, Christopher Chiza alitoa taarifa hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Maryam Salumu Msabaha (Chadema).
↧
More Pages to Explore .....