WENYEVITI wa Kamati za Kudumu za Bunge, waliopendekezwa kuwajibishwa na Bunge hilo katika sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow, wamejiuzulu nyadhifa zao.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Spika Anne Makinda aliwaambia waandishi wa habari katika Ofisi ndogo ya Bunge, waliotaka kujua hatima ya wenyeviti hao, kuwa hawapo tena katika nafasi zao baada ya kujiuzulu.
“Wenyeviti hao kwa
Sakata la Escrow: Chenge, Ngeleja Waachia Ngazi Bungeni.......Spika wa Bunge Asema kilichobaki ni kamati kuchagua Viongozi Wapya
↧
↧
Kinana apiga MARUFUKU ziara za mikoani za Mwigulu Nchemba kwa madai kuwa zina harufu mbaya ya Kampeni za Urais
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania Bara), Mwigulu Nchemba amekubali kuitikia wito wa kusitisha ziara zake za kichama katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini, kama alivyoagizwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana.
Katika barua yake ya Januari 18, mwaka huu, Kinana alimwagiza Mwigulu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi mkoani Singida,
↧
Picha Pamoja na habari kwa Kina kuhusiana na Majambazi yaliyovamia kituo cha Polisi Ikwiriri na Kuua Askari Wawili na kupora Bunduki
Askari wawili wa Jeshi la Polisi katika Kituo cha Ikwiriri wilayani Rufiji mkoani Pwani, wameuawa baada ya kushambuliwa kwa silaha na majambazi, waliovamia kituo hicho na kuiba silaha baada ya kufanikisha mauaji.
Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi liko katika msako mkali, huku Mkuu wa jeshi hilo, IGP, Ernest Mangu akitangaza donge nono la Sh milioni 20 kwa watakaofanikisha kukamatwa
↧
Mafuriko yaikumba Mtwara, nyumba 200 zazingirwa na maji, RC atoa saa 24 yaondolewe
Zaidi ya nyumba 200 zimezingirwa na maji katika Manispaa
ya Mtwara Mikindani kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha
hasara kubwa ambayo thamani yake bado haijajulikana.
Kufuatia hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima
Dendegu ametoa saa 24 kwa wataalam kuhakikisha wanayaondoa maji ndani
ya makazi ya watu.
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wilaman Ndile amemwambia
mkuu
↧
Zaidi ya wanafunzi 600,000 wahofu kutopiga kura uchaguzi mkuu ujao.
Zaidi ya wanafunzi laki sita wa vyuo vikuu, vyuo vya kati na kidato cha
nne nchini huwenda wasishiriki kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu ujao
kutokana na ratiba ya wizara ya elimu kuhusu mihula ya kufunga na
kufungua vyuo nchini kukinzana ya NEC.
Ratiba
ya mihula ya kufunga na kufungua vyuo ambayo imetolewa na Wizara ya
Elimu mwaka huu, imeibua hofu kwa wasomi wa vyuo mbalimbali
↧
↧
Wanafunzi wakosa Makazi baada ya Mabweni kuungua moto
Wanafunzi 64 wa kike wanaosoma kidato cha tano na cha sita katika shule
ya sekondari ya Mpwapwa iliyopo mkoani Dodoma wamehifadhiwa katika
mabweni ya chuo cha ualimu Mpwapwa kufuatia bweni lao kuteketea kwa moto
juzi.
Akithibitisha
kutokea kwa moto huo mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Christopher Kangoye
alisema kuwa wamelazimika kuwahamishia wasichana hao katika mabweni ya
chuo cha
↧
Wema Sepetu Hajampeleka Diamond Mahakamani Kwa Deni La Milion 10 – Martin Kadinda
Meneja wa Wema Sepetu, Martin Kadinda amekanusha taarifa zilizoandikwa
kwenye vyombo mbalimbali vya habari nchini likiwemo gazeti la Mtanzania
kuwa amempeleka Diamond polisi kwa kile kinachosemwa ni kumtapeli
shilingi milioni 10.
Martin amesema kuwa Wema na Diamond hawadaiani chochote na kwamba habari hizo ni za uongo.
“Unajua tatizo ni kwamba hatujajua source ni nani. Kwa
↧
Watafiti wabaini mtindo wa Mwanamke kuwa juu ya mwanaume wakati wa tendo la ndoa ni hatari kwa wanaume!
Wanasayansi nchini Brazil wamefanya utafiti ili kubaini ni mtindo upi katika ufanyaji tendo la ndoa ulio hatari zaidi kwa mwanaume.
Kwa mujibu wa utafiti huo, mtindo ambao mwanamke anakuwa juu ya mwanaume ndio hatari zaidi na huwa na risk kubwa zaidi ya kusababisha hata kuvunjika kwa uume.
Wanasayansi hao wanasema:
Pindi mwanamke anapokuwa juu, mara zote hucontrol movement na uzito
↧
HakiElimu Waponda Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) katika Elimu
Shirika
la haki Elimu nchini Tanzania limetoa tathmini ya mpango wa matokeo
makubwa sasa BRN katika sekta ya elimu kwa kipindi cha mwaka mmoja
uliopita inayoonesha kwamba hali ya utekelezaji wa mpango huo si ya
kuridhisha.
Kaimu mkurugenzi wa shirika hilo Bw. Godfrey Boniventura amesema kuwa
pamoja na serikali kutambua kuwa sekta ya elimu hapa nchini ina
changamoto nyingi na
↧
↧
Diamond Platnumz ameingia tena kwenye Top 10 ya Trace TV ya Ufaransa
Post hii ni maalumu kwajili yako mpendwa msomaji kama ulikuwa na hamu
ya kufahamu video za Afrika zinazofanya vizuri duniani na iliyofanikiwa
kuchukua nafasi kwenye countdown za nchi kubwa.
Kituo
cha TV cha kimataifa cha Trace Urban cha Ufaransa, Jan 21
kilitoa list ya top 10 ya nyimbo kali za Afrika ikiwemo ya Diamond
Platnumz iitwayo Nitampata Wapi.
Hii ni list ya
↧
Vurugu zaibuka tena wakati wa zoezi la Kumwapisha Rasmi Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani kupitia CHADEMA
Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala, Hella Mlimanazi (kushoto), akiwaapisha
Wenyeviti wateule wa serikali za Mitaa wa Migombani na Minazi Mirefu
katika Kata ya Segerea jijini Dar es Salaam, Japheth Kembo (Chadema) na
Ubaya Chuma (CCM), katika zoezi la kuwaapisha rasmi baada ya mgogoro wa
muda mrefu, lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala, Hella Mlimanazi
↧
Mwanamke auawa kwa Mapanga Musoma
Matukio ya mauaji ya kikatili dhidi ya wanawake katika wilaya ya Butiama yameanza kurejea upya baada ya mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Maneke katika halmashauri ya Musoma mkoani Mara kuuawa kinyama kwa kukatwa mapanga tukio ambalo limehusishwa na imani za kishirikina.Kamanda wa polisi mkoa wa Mara kamishna msaidizi wa jeshi
↧
Panya waharibu ekari 880 za mashamba
PANYA wamevamia na kuharibu ekari 880 za mashamba ya mahindi na mbaazi katika kata ya Rondo mkoani Lindi. Ofisa Kilimo wa kata hiyo, Yahaya Nampate alisema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Kamati Ndogo ya Bunge inayoshughulikia kilimo, maji na mifugo.
Kamati hiyo ilikwenda kufanya ukaguzi wa chanzo cha maji cha Rondo na kuambiwa kwamba panya wanahatarisha usalama wa
↧
↧
CCM yarejesha amani Sudan Kusini....Makundi hasimu yaafikiana, Yatia Saini mkataba wa Amani jijini Arusha
Baada ya miezi mitano ya mazungumzo ya kurejesha amani Sudan Kusini yaliyoratibiwa na chama tawala, CCM, hatimaye Rais wa nchi hiyo, Salva Kiir na hasimu wake, Riek Machar wamesaini makubaliano ya kusitisha mapigano, yaliyoibuka tangu mwaka 2011.
Kutokana na machafuko hayo, zaidi ya raia 20,000 wa Sudan Kusini, wamepoteza maisha huku wengine zaidi ya milioni moja wakikosa makazi.
↧
Kamati ya Zitto Kabwe Yamvaa Mbunge wa Kibaha
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeiagiza Bodi ya Korosho Tanzania, kuandika barua inayoeleza hatua walizochukua katika kurudisha nyumba iliyouzwa kwa Mbunge wa Kibaha Mjini, Silvestry Koka (CCM).
Akitoa agizo hilo, Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe alisema kamati yake haijaridhishwa na namna nyumba hiyo ilivyouzwa.
Zitto aliitaka Bodi hiyo kuhakikisha inapeleka barua yenye
↧
Watu Wawili wauawa kikatili Sumbawanga
WATU wawili wakazi wa wilaya ya Mlele mkoani Katavi wameuawa kikatili ambapo mmoja amecharangwa kwa mapanga na mwili wake kukatwa vipande vipande kisha kuzikwa shambani kwake na mwingine kuchinjwa na watu wanaodaiwa kuwa wa familia yake.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kusema aliyekatwa vipande ni Minza Mwanalushinga (26)
↧
Wagombea Udiwani Watakiwa Kupima Virusi Vya Ukimwi Kabla ya Kuchua Fomu za Kugombea
MADIWANI wa Halmashauri ya Nsimbo wilayani Mlele katika mkoa wa Katavi wameshauriwa kupima afya zao ili kubaini kama wana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) kabla ya kuchukua fomu za kugombea nafasi ya udiwani katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika mwaka huu.
Diwani wa kata ya Kapalala, Reward Sichone alitoa ushauri huo katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo baada
↧
↧
Kiuno cha Demu wa Diamond Chamchengua Ommy Dimpoz
Umbile la mwanadada aliyefahamika kwa jina moja la Avril kutoka Kenya
ambaye aliwahi kudaiwa kutoka kimapenzi na Mwanamuziki Nasibu Abdul
‘Diamond’, hivi karibuni lilionesha kumchengua msanii wa Bongo Fleva,
Omari Faraji ‘Ommy Dimpoz’ baada ya kutupia picha inayomuonesha
akikitolea macho kiwowowo cha demu huyo.
Ommy alifanya hivyo kupitia ukurasa wake wa Instragram baada kuiweka
↧
ACT Walia kiongozi wao kuuawa......Ni yule aliyechinjwa Kinyama na kupikwa kwenye Sufuria kama Nyama ya kuku
CHAMA cha ACT-Tanzania kimelitaka Jeshi la Polisi nchini kuwasaka na
kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na tukio la mauaji
ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Masigo wilayani Mlele mkoani
Katavi, Christian Kahongo.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa
ACT-Tanzania, Samson Mwigamba, ilieleza kuwa chama hicho kinalaani
mauaji hayo
↧
Dr. Mwakyembe Aibua Mshituko.....Wasomi Wahoji Sababu za Kumwondoa Wizara ya Uchukuzi na Kumuweka Sitta
Wasomi na wananchi kadhaa jana walizungumzia mabadiliko ya
Baraza la Mawaziri yaliyofanywa na Rais Jakaya Kikwete, wengi wakihoji
sababu za kumhamisha Dk Harrison Mwakyembe kutoka Wizara ya Uchukuzi
kwenda Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Rais
alifanya mabadiliko kwenye baraza hilo baada ya mawaziri wawili kuanguka
kutokana na kashfa ya uchotwaji takriban Sh306 bilioni
↧
More Pages to Explore .....