Mbunge wa Muleba Kusini Prof Anna Tibaijuka amesema kuwa hausiki na aina
yoyote ya ufisadi wa fedha zilizokuwa katika akaunti ya Tageta Escrow.
Akiongea
na wajumbe wa chama hicho wilayani Muleba Mbunge wa jimbo la Muleba
kusini Profesa Anna Tibaijuka wakati akiendelea kuwatoa wasiwasi
wananchi wake juu ya sakata la Tegeta Escrow amesema kwamba anaendelea
kusimamia shughuli za
Sihusiki katika ufisadi wa Escrow - Prof Tibaijuka
↧
↧
Msama azungumzia "kuachana" na Rose Muhando, Akanusha Rose Muhando kutumia Madawa ya Kulevya
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, Alex Msama, ametamka kuwa yeye si Meneja wa malkia wa nyimbo za injili nchini, Rose Muhando akisema amekuwa akishirikiana naye katika mazingira ya kawaida kama ilivyo kwa waimbaji wengine.
Kwa mujibu wa taarifa ya Msama kwa vyombo vya habari juzi, yeye akiwa mlezi wa waimbaji wote wa muziki wa Injili, amekuwa akishirikana
↧
Waliokuwa wanaelekea kwa Lowasa 'kula mwaka mpya' warudia njiani
Baadhi ya wafuasi wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa wamerudia njiani baada ya kupata taarifa za kutokuwapo kwa sherehe ya kupokea mwaka mpya ambayo hufanyika kila mwaka nyumbani kwake Monduli ikijumuisha mamia ya watu kutoka ndani na nje ya nchi.
Lowassa amekuwa akifanya sherehe hiyo kwa zaidi ya miaka mitano lakini mwaka huu hakufanya kutokana na kutumia adhabu ya CCM.
Msaidizi
↧
Sheikh Ponda Anyimwa Dhamana
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Mkoa wa Morogoro imemnyima dhamana Katibu
wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa katika
kesi yake ya jinai namba 128 ya mwaka 2013 leo.
Kesi hiyo imesikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Marry Moyo ambaye
amesema amepokea hati ya kumfutia dhamana Sheikh Ponda kutoka kwa
Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kwa mamlaka aliyonayo hivyo
↧
Rais Kikwete amteua Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Rais Jakaya Kikwete amemteua George Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu
wa Serikali, akichukua nafasi iliyoachwa na Jaji Frederick Werema
aliyejiuzulu Desemba 16 kutokana na kuhusishwa na kashfa ya Akaunti ya
Tegeta Escrow.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Ikulu uteuzi huo ulianza rasmi Ijumaa, Januari 2, 2015
na anatarajiwa kuapishwa leo.
Kabla ya uteuzi wake,
↧
↧
Maajabu ya Shinyanga: Ndugu waamua kumzika marehemu na kuku tumboni
Katika hali isiyokua ya kawaida mwili wa Benadetha Steven mwenye
miaka 35 aliyefariki dunia juzi umefanyiwa matambiko ya kimila baada ya
kupasuliwa na wembe ukiwa kaburini na kuingizwa kuku ndani ya tumbo lake
ikiwa ni ishara ya kuondoa mkosi.
Tukio hilo lilitokea juzi katika mtaa wa Mapinduzi, Shinyanga wakati
waombolezaji wakiwa hatua ya mwisho ya kumzika marehemu lakini gafla
↧
Ikulu Yasema: Rais hajadharau Bunge
KURUGENZI ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, imesema Rais Jakaya Kikwete hajadhalilisha Bunge ama wabunge.
Pia, imesema uteuzi uliofanywa na Rais wa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Profesa Mighanda Manyahi haukulenga kumdhalilisha yeyote na kwamba umetokana na mamlaka aliyonayo kisheria.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, jijini Dar
↧
Panya Road 510 Wakamatwa Dar.....Wamo Viongozi Watatu wa Mtandao Mzima
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam linawashikilia vijana 510
wa kikundi cha uhalifu linachojiita panya Road wakiwemo viongozi watatu
wa kikundi hicho.
Hatua hiyo imekuja kutokana na Oparesheni iliyofanywa na jeshi hilo kufuatia
uhalifu, hofu na taharuki waliyosababisha siku ya Ijumaa katika maeneo
mbalimbali jijini Dar es salaam.
Akizungumzia Oparesheni hiyo
↧
Wastara: sifaidiki na kazi za Sajuki
Msanii wa filamu Wastara Juma, ambaye ni mjane wa aliyekuwa staa wa
filamu mahiri nchini, Marehemu Sajuki Juma Kilowoko, ameweka wazi kuwa
baada ya kufariki kwa mumewe, hakuna manufaa yoyote ambayo yanaendelea
kupatikana katika filamu.
Wastara
ameongezea kusema kuwa hakuna mafanikio ambayo yanaendelea kupatikana
ama yanatarajiwa kupatikana kwake na familia kutokana na mfumo wa
↧
↧
Kafulila: Wanaotetea 'wezi' wa Escrow wanajisumbua
Mbunge wa Kigoma kusini, David Kafulila, amesema wale wanaojaribu kumkingia
kifua Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo pamoja na
watuhumiwa wengine ili wasiwajibishwe wanajisumbua.
Kafulila
amesema Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alipewa
muda wa zaidi ya saa moja kujitetea bungeni lakini akashindwa
kuwashawishi wabunge kuwa hakuhusika na wizi wa
↧
Mwanasheria Mku MPYA Wa Serikali Aaapishwa.......Aahidi Kushughulikia Usiri katika Mikataba
Mwanasheria mkuu wa serikali George Masaju amewataka watanzania kujenga
imani na serikali yao juu ya masuala mbalimbali ikiwemo ya mikataba hasa
inayogusa maslahi ya taifa.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete
Ikulu jijini Dar es Salaam hafla iliyohudhuriwa pia na makamu wa Rais Dk
Mohamed Gharib Bilal, waziri mkuu Mizengo Pinda, jaji
↧
Mwanamke Ajifungua mapacha walioungana, Musoma
Mwanamke mmoja mkazi wa kata ya Buhare katika manispaa ya Musoma
mkoani Mara Bi Helena Paulo mwenye umri wa miaka 20 amejifungua watoto
wawili mapacha ambao wameungana katika eneo la kifua hadi
tumboni.
Tukio hilo limevuta mamia ya wananchi ambao wamefika katika
hospitali ya rufaa mkoa wa mara mjini musoma kwa lengo la
kutaka kushuhudia tukio hilo.
↧
Binti Achomekwa Chupa Sehemu za siri na Kujeruhiwa vibaya kwa Kipigo jijini Mwanza akituhumiwa Kutoka kimapenzi na mume wa mtu
MKAZI wa Kitangiri jijini hapa, Biera Edwin (22) amelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure akipatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake kwa tuhuma za kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mume wa mtu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola hakupatikana kuzungumzia tukio hilo, lakini Biera mwenyewe alisema kabla ya kufanyiwa kitendo hicho
↧
↧
Aua, ajiua, aacha ujumbe wa kurasa nne
Mfanyabiashara wa mbao Manispaa ya Songea, Emmanuel Moshi (40),
mkazi wa Marangu, mkoani Kilimanjaro amemuua mfanyabiashara mwenzake
aliyetambuliwa kwa jina la Didas Alphonce (64), mkazi wa Kilema
Kilimanjaro kwa kumpasua kichwa kwa shoka, kisha yeye mwenyewe
kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani katika stoo ya nyumba waliyokuwa
wakiishi.
Inadaiwa kuwa Moshi alichukua uamuzi huo
↧
Ewura Yashusha Bei za Mafuta.....Ni kuanzia kesho January 7 2015
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (Ewura), Felix
Ngamlagosi (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari
ofisini kwake Dar es Salaam leo, kuhusu mwenendo wa bei za mafuta nchini
na katika soko la Dunia. Kulia ni Mkurugenzi wa Petroli, Godwin Samwel.
Mkurugenzi wa Petroli, Godwin Samwel (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
Ofisa
↧
Mabomu ya Machozi yatumika Kuzima Vurugu zilizojitokeza jijini Dar wakati wa zoezi la kuwaapisha Wenyeviti wa Mitaa
Polisi Jijini Dar es Salaam wamelazimika kufyatua risasi hewani na
kufyatua mabomu ya machozi kufuatia kuibuka kwa vurugu katika hoteli ya
Land Mark Ubungo ambapo shughuli ya uapishaji wa wenyeviti wa serikali
Mitaa zilikuwa zinafanyika.
Vurugu
hizo, zinadaiwa kuibuliwa na wafuasi wa vyama vya upinzani kwa madai
kuwa Mwenyekiti mmoja wa Chama tawala CCM aliyetaka Kuapishwa
↧
Kamati ya Miss TZ waililia wizara
Kamati ya Miss Tanzania imesema kuwa imeiandikia barua Wizara ya Habari
Tamaduni na Michezo kuomba kikao cha pamoja kati yao na BASATA ili
kutafuta usuluhishi wa hatua ya Baraza hilo kuyafungia mashindano hayo
kwa miaka miwili.
Akiongea na eNewz, afisa Habari wa kamati ya Miss Tanzania, Bwana Hidan Rico amesema kuwa wameiomba Wizara kama Msimamizi Mkuu wa BASATA, vilevile wakiwa
↧
↧
Mkuu wa mkoa wa Mwanza atoa siku tano kwa wanakijiji kwimba kuhakikisha wanampata mtoto Albino Aliyetekwa tangu Disemba 27, 2014
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo ametoa muda wa siku tano kwa
wakazi wa kijiji cha Ndami na jeshi la jadi Sungusungu wilayani kwimba,
kuhakikisha wanampata mtoto mwenye ulemavu wa ngozi – Alibinism, Pendo
Emanuel akiwa hai au amekufa ikiwa ni pamoja na wahusika wa tukio hilo
kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola.
Agizo hili la mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo,
↧
Viongozi wa Siasa Wamtaka Rais Kikwete Afanye Maamuzi juu ya Waziri wa Nishati na Madini.
Viongozi wa vyama vya siasa nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete
kutekeleza ahadi yake aliyoahidi wakati wa mkutano na wazee wa Dar es
Salaam ya kufanya maamuzi ya kumwajibisha waziri wa nishati na madini
ambaye alimweka kiporo na kudai kuwa atatoa maamuzi ndani ya siku mbili
lakini hadi leo amekaa kimya.
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Prof Iibrahim Lipumba amesema
suala la
↧
CCM Shinyanga yalaani UVCCM kufunga ofisi.
KAMATI ya siasa ya halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) wilaya ya
Shinyanga Mjini mkoani humo, imelaani kitendo cha jumuiya ya umoja wa
vijana wa chama hicho, kufanya maandamano na kufunga ofisi za CCM,
wilaya hiyo.
Mwenyekiti
wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini kanali Mstaafu Tajiri Maulidi ametoa
kauli hiyo wakati akitoa tamko la chama, baada ya kamati ya siasa ya
halmshauri
↧
More Pages to Explore .....