Diamond Platnumz alipata A kwenye somo la kucheza na
akili ya mashabiki wake. Siku za hivi karibuni staa huyo amekuwa
akitease mashairi ya kile kinachoonekana kama wimbo wake ujao. Na sasa
amewapa mashabiki wake kitu kingine.. picha inayoonekana kuwa ni video
yake mpya.
Hicho ndicho kitu pekee ambacho staa huyo huwa hatua 100 mbele zaidi
ya wasanii wengi katika kazi zake. Kupitia
Diamond aonjesha picha ya video mpya na model mrembo wa kizungu!
↧
↧
Tanzania yaingia kwenye kashfa mpya, ni mpango wa kuwahamisha wamasai 40,000 ili kuwapa Waarabu eneo la kuwindia
Ikiwa bado Tanzania
inakabiliwa na skendo ya pembe za ndovu zinazodaiwa kuondoka na ndege ya
rais wa China alizuru nchini, kashfa nyingine kubwa imezuka!
Tanzania inashutumiwa kurejesha mpango wa kuwahamisha wamasai 40,000
katika eneo waliloishi kwa miaka na miaka, ili kuipa eneo hilo familia
ya kifalme ya Dubai kwaajili ya kuwinda wanyama.
Mwaka jana serikali ilidai kuahirisha
↧
Hospitali Za Serikali Majanga Matupu.....Muhimbili Vifo Nje Nje!
Hakufai. Pengine ni neno linaloweza kuwakilisha uhalisi wa hali
ilivyo katika baadhi ya hospitali kadhaa za Serikali nchini, ambako
mamia ya wagonjwa wanateseka kutokana na uhaba wa dawa, vitendanishi na
vifaa tiba ambao umeendelea kuzikumba.
Wengi wa
wagonjwa waliohojiwa wanalalamikia kushindwa kumudu gharama za dawa
ambazo wanapaswa kuzinunua kwenye maduka wakisema hali hiyo
↧
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP Ernest Mangu Aongeza Askari Kiteto Kuimarisha Ulinzi
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akimsikiliza Diwani wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto
Bw.Athuman Kidawa wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo
kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha
kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea kwa vifo.kushoto ni Afisa
tarafa wa Matui Bw.Eliakimu Ndelekwa.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
↧
Sijatangaza Kugombea Au Kutogombea Urais- Dkt. Shein
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed
Shein amesema hajatangaza kugombea au kutogombea Uraisi kwa Awamu
nyingine visiwani humo na wanaomtangazia kuwa hagombei tena waache
kudanganya.
Dkt.
Shein ametoa kauli hiyo Visiwani humo wakati akizungumza na viongozi
na wanachama wa CCM, ikiwa ni miongoni mwa mikakakati ya kuimarisha
chama ambapo amesema
↧
↧
Mwanamke Afanyiwa Ukatili wa Kutisha Jijini Arusha
Mwanamke
mmoja mkazi wa kijiji cha Olkokola Wilayani Arumeru Mkoani Arusha
amefanyiwa ukatili wa kutisha kwa kukatwakatwa na Panga kichwani na
kuondolewa kiganja cha Mkono, sikio na sehemu nyingine za mwili wake
Mwanamke huyo anayefahamika kwa jina la Paulina Joseph amefanyiwa
ukatili huo na mtu anayedaiwa kuwa ni shemeji yake kwa madai ya
kuingilia ndoa yake.
Tukio hilo
↧
Soko la Vinyago Arusha lateketea kwa moto
Soko la vinyago lililoko karibu na ofisi ya CCM wilaya ya Arusha limeteketea kwa moto usiku wa kuamkia tarehe 18 Novemba 2014 na kusababisha hasara ya mabilioni ya fedha.
Wananchi na wafanyabiashara ambao vibanda na mali zao zote zimeteketea wamesema walianza kupata taarifa za moto huo usiku wa kati ya saa tatu na saa Nne na
↧
Tarehe ya kujiandikisha kwa ajili ya chaguzi za Serikali za Mitaa
Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za
Mikoa na Serikali Mitaa Bwana Kharist Michael Luanda amesema wananchi
wanapaswa kujiandikisha katika daftari maalum la kupigia kura kwa ajili
ya kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuanzia tarehe 23/11/2014 hadi tarehe 29/11/2014.
Mkurugenzi huyo alisema kuwa wananchi wanaotaka kugombea nafasi
mbalimbali za
↧
Wema Sepetu Aanika Kisa Cha Kuachana na Diamond
MISS Tanzania 2006/07
ambaye ni staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful
Onyinye’, amevunja ukimya kwa kuamua kuanika kisa cha yeye kummwaga
aliyekuwa mwandani wake, nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond
Platnumz’.
Akizungumza na Amani katika mahojiano maalum jijini Dar, juzikati,
Wema alianza kwa kufunguka kwamba, kuna watu wamekuwa wakizungumzia ishu
ya yeye
↧
↧
Miss Sinza 2001, Husna Maulid Akumbwa na Skendo ya Picha Za Utupu
Miss Sinza 2001 na aliyekuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2011, Husna
Maulid ameonesha kuwa ni sikio la kufa baada ya kupiga picha za utupu
kwa mara nyingine.
Picha hizo zilizotapakaa kwenye mitandao
mbalimbali zimewashangaza watu ambapo Husna anaonekana akiwa kama
alivyozaliwa huku akiwa katika mapozi tofauti hali inayoonesha kwamba
alikuwa akipigwa picha hizo na mpenzi wake.
↧
Udini vyuo vikuu : Serikali yapiga marufuku wanafunzi kufanya mitihani siku ya Ijumaa na Jumamosi .....Wizara yatoa waraka maalumu
Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, imezuia uongozi
wa vyuo vikuu nchini kuwalazimisha wanafunzi kuingia darasani au kufanya
mitihani kwa siku zao za ibada.
Ingawa hazikutajwa, siku maalum za ibada zilizozoeleka kwa madhehebu mengi ni Ijumaa, Jumamosi na Jumapili.
Agizo la Serikali limetolewa na C.P. Mgimba kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
↧
Polisi aliyeua mwanafunzi wa Chuo Kikuu jijini Mbeya ahukumiwa kifo
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mbeya imemhukumu kunyongwa hadi kufa polisi wa
upelelezi, Maduhu, F 5842, aliyekuwa akikabiliwa na shitaka la mauaji ya
mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU), Daniel Mwakyusa.
Aidha,
mahakama hiyo imewaachia huru washitakiwa wengine wawili wa kesi hiyo,
polisi wa upelelezi, Shaaban, F 7769, na polisi wa kike mpelelezi,
Neema, F 6545, baada ya
↧
Mfanyabiashara Afariki Dunia Akifanya Mapenzi Ndani Ya Gari Lake Huko Kagera
Polisi mkoani Kagera inachunguza kifo cha mmiliki wa ukumbi wa klabu ya
usiku ya Linas Night, Leonard Mtensa (50) ambaye inadaiwa alifariki
dunia wakati akifanya mapenzi kwenye gari lake.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe alisema Mtensa,
ambaye alikuwa na mpenzi wake kwenye gari maeneo ya Buyekera, alifariki
dunia kabla ya kufikishwa kituo cha afya cha ELCT Ndolage.
↧
↧
Vijana, wanawake waongoza kwa maambukizi ya UKIMWI
Tume
ya kudhibiti ukimwi nchini Tanzania TACAIDS imelitaja kundi la Wanawake
na Vijana wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 25 kuwa ndio makundi
makubwa yanayoongoza kwa kuwa na virusi vya ugonjwa hatari wa ukimwi
hapa nchini.
Mwenyekiti
wa TACAIDS Dkt. Fatma Mrisho amesema hayo jana jijini Dar es salaam
wakati alipokuwa akizungumzia maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani
Desemba
↧
Taarifa ya Haraka kwa Vyombo vya Habari Kuhusu Mpango wa Serikali Kuwahamisha Wamasai 40,000 kumpisha Mwarabu afanye kazi ya Uwindaji
Sisi Viongozi wa Mila, Kisiasa, Wawakilishi wa Wanawake tumesikitishwa sana na Taarifa ya uongo aliyoitoa Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu juu ya ukweli wa Mgogoro wa Loliondo. Ifuatayo ni ufafanuzi wa hali halisi kinyume na Waziri alivyodanganya Dunia kupitia BBC tarehe 19/11/2014 na Gazeti la leo la Mwananchi
Kwamba eneo la Loliondo halina Wamaasai 40,000
↧
Rais Kikwete atolewa nyuzi.....Afya yake inaimarika na Anaendelea Vizuri
Rais
Jakaya M. Kikwete akitoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo
Baltimore Maryland baada ya kutolewa nyuzi katika mshono baada ya
kufanyiwa upasuaji wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena
hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na
ushauri. Kulia kwake ni Daktari wa Rais, Profesa Mohamed Janabi
Rais Kikwete akiwa amepumzika kwenye hoteli
↧
Serikali kuja na adhabu mbadala kwa makosa madogo ili kupunguza msongamano Magerezani
Serikali
ya Tanzania imesema ipo kwenye mchakato wa kuandaa adhabu mbadala kwa
wahalifu wa makosa madogo madogo ili kupunguza msongamano magerezani
ambao kwa sasa unapelekea hali mbaya katika Magereza hayo.
Akijibu swali bungeni mjini Dodoma jana kwa niaba ya Waziri wa Mambo
ya Ndani ya nchi, Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Utumishi Bi. Celina
Kombani amesema hali ya msongamano kwa
↧
↧
Kaimu Rais Atimuliwa Zambia
Aliyekuwa rais wa mpito nchi ya Zambia, Guys Scott.
Chama tawala nchini Zambia (PF) kimemtimua kaimu rais wa nchi hiyo Guys Scott kutoka chamani kwa kuvunja utaratibu wa katiba.
Taarifa
hii ni kwa mujibu wa msemaji wa chama hicho. ''Amekuwa akiwaajiri na
kuwafuta watu kazi ovyo na pia bila ya kushauriana na kamati kuu ya
chama,'' amesema Malozo Sichone.
Bwana Scott, ambaye
↧
Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono Alishwa SUMU
Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono amelishwa sumu wakati
akiwa kwenye safari ya kikazi jijini London nchini Uingereza, imeelezwa.
Kwa
mujibu wa tovuti ya The Citizen, Mkono ambaye pia ni mwanasheria
maarufu, aliugua ghafla alipokuwa jijini humo.
Madaktari wake walisema
kuwa alikuwa amelishwa sumu iliyokuwa imekusudiwa kuharibu figo zake
ndani ya saa 72.
“Ilikuwa siku
↧
Sita wafariki kwa kupigwa na radi Songea
Watu
Sita wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa wilayani Songea
mkoani Ruvuma baada ya kupigwa na radi kufuati mvua kubwa iliyonyesha
usiku wa kuamkia leo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela amesema kuwa
maafa hayo yalitokea majira ya saa mbili usiku wakati watu hao wakila
chakula cha usiku kwenye mgahawa wa chuo cha kilimo na mifugo cha Liti
Madaba
↧
More Pages to Explore .....