Polisi mkoani Iringa wanawashikilia watu watatu wakiwamo madereva
wawili wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa tuhuma
za kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi alisema tukio hilo
lilitokea jana saa 11 alfajiri katika kituo cha ukaguzi cha Igumbilo
mkoani hapa na baada ya ukaguzi polisi walibaini magunia mawili
Madereva wa Kampuni ya Mwananchi Wakamatwa na Mirungi
↧
↧
Mahakama yachomwa Moto,nyaraka zote zateketea
Mahakama ya Mwanzo ya Riagoro wilayani Rorya mkoani Mara, imeteketezwa kwa moto na watu wasiojulikana huku nyaraka muhimu zilizokuwamo ndani yake zikiteketea zote.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Lazaro Mambosasa, alisema wanalifanyia uchunguzi tukio hilo na inaonyesha haikutokana na hitilafu ya umeme kutokana na kutokuwa na nishati hiyo.
Kamanda Mambosasa alisema
↧
Malalamiko ya wizi wa vifaa vya magari bandarini, Serikali imetoa tamko.
Imekuwa kawaida watu wengi kulalamikia vitendo vya wizi wa vifaa
mbalimbali katika magari eneo la bandari ya Dar es Salaam hali
iliyopelekea Serikali kutoa tamko rasmi juu ya mkakati unaoandaliwa
ili kukomesha wizi huo.
Akizungumzia mkakati huo Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles John Tizeba amesema;-
“..Wizi
huu umepungua kwa kiasi kikubwa sana na kwa sababu tumehakikisha
↧
Polisi yawatawanya wafuasi wa Mbowe kwa Mabomu
Wafuasi wa (Chadema) wilayani Mpanda jana jioni walilazimika
kutafuta vichochoro vya kukimbilia baada ya polisi kusambaratisha kwa
mabomu ya machozi, maandamano ya kumsindikiza Mwenyekiti wa chama hicho,
Freeman Mbowe baada ya mkutano.
Patashika hiyo
ilitokea baada ya mkutano wa Mbowe kumalizika na wafuasi wake kutaka
kumsindikiza hotelini, jambo ambalo polisi hawakulikubali.
↧
Mtoto Aliyefaulu Darasa la saba Nusura Atolewe Kafara
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limemtia mbaroni mganga mmoja
wa jadi anayedaiwa kuteka watoto kwa njia za kishirikina kwa ajili ya
kutolewa kafara.
Mbali na mganga huyo, pia wamemtia
mbaroni mwanamke mmoja, anayedaiwa kusuka mipango ya kutekwa nyara kwa
watoto na kuwahifadhi kwa mganga huyo.
Mganga huyo
ambaye anadaiwa ni mwenyeji wa mkoani Mbeya, alikutwa na mtoto wa kike
↧
↧
Kinana na Dr. Slaa kesho watashiriki katika Mjadala wa Rais wa Tanzania anayetakiwa 2015
Makatibu wakuu wa CCM, Abulrahman Kinana na Dk Willibrod Slaa wa
Chadema kesho watashiriki katika mjadala wa rais wa Tanzania
anayetakiwa kupitia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Mjadala
huo utakaofanyika Dar es Salaam, umeandaliwa na Asasi ya Twaweza ikiwa
ni sehemu ya uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa maoni ya wananchi juu ya
mwelekeo wa rais wanayemtaka kupitia uchaguzi wa mwaka 2015.
↧
Chid Benz Atinga Tena Mahakamani......Kesi Yake Yaahirishwa hadi Disemba 1
Rapper Rashid Abdallah Makwiro aka Chid Benz ambaye yupo nje kwa
dhamana kufuatia kukamatwa na dawa za kulevya uwanja wa ndege Dar es
salaam leo Nov 11 2014 alikwenda tena kwenye Mahakama ya hakimu mkazi
Kisutu Dar es Salaam.
Taarifa kutoka mahakamani hapo zinaarifu kwa, upande wa Jamhuri umeomba kesi ya msanii huyo iahirishwe mpaka December 1 2014 kwa kuwa upelelezi bado
↧
TCRA Yawataka Wamiliki wa Blogs Kuzitumia Vizuri Wakati wa Uchaguzi
Wamiliki wa Blogs nchini wametakiwa kuzitumia vyema blog zao katika
kuripoti habari na matukio mbalimbali wakati wa uchaguzi wa serikali za
mitaa, wabunge na urais.
Hayo yamesemwa na Mkurugezi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA), Profesa John Nkoma jana alipokuwa akizungumza na wamiliki wa
Blogs katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Profesa Nkoma
↧
Menina: Sijatoa Mimba ya Diamond
Mwanamuziki Hot Sexy hapa Bongo, Meninah
Atick ameifungukia ishu ya kuchoropoa mimba ya msanii Nasibu Abdul
‘Diamond’ na kusema hajawahi kubeba mimba ya staa huyo na wala katika
maisha yake hajawahi kufanya kitendo hicho.
“Jamani mimi ni mdogo, kwanza kwa nini watu
wanapenda kunibebesha vitu vikubwa, mimi sijawahi kubeba wala
kuchoropoa mimba katika maisha yangu,” alisema msichana
↧
↧
Mahututi aliyekimbiwa na Mwanamke GUEST HOUSE Afariki
Mtu mmoja amefariki dunia katika hospitali ya rufaa ya Mbeya baada ya kukutwa hali mahututi katika nyumba ya kufikia wageni.
Mtu huyo aliyetambuliwa kwa jina la Kassim Rashid (55) mkazi wa Ghana,
Mbeya alifariki dunia wakati akitibiwa katika hospitali hiyo ya rufaa
tarehe 10 Novemba 2014 mwendo wa saa kumi alasiri.
Taarifa ya Polisi kutoka mkoa wa Mbeya imesema kuwa awali majira ya
↧
Sitti Mtemvu: Siwezi kuwazuia watu kuongea, Ridhiwani amtia moyo
Aliyekuwa Miss Tanzania 2014 hadi Jumamosi iliyopita, Sitti Mtemvu ametoa kauli yake mpya ikiwa ni siku chache baada ya kutangaza
kujivua taji hilo.
Sitti ambaye taji la alilovua amepewa Lilian Kamazima kupitia twitter aliandika:
Siwezi kuwazuia watu kuongea lakini naweza kujizuia kuzungumza
— Sitii Abbas (@SitiiAbbasMtevu) November 10, 2014
Naye Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete
↧
Baada ya Wema na Penny kumaliza tofauti zao sasa waanza kushirikiana kwenye kazi
Baada ya staa wa filamu Wema Sepetu na mtangazaji wa radio VJ Penny
weekend iliyopita kumaliza tofauti zao zilizowatenganisha kwa muda
mrefu, hatimaye sasa wameanza kuwa karibu.
Kupatanishwa kwao kulikofanywa na rafiki yao Junaithar aliyewaalika
kwenye dinner ya birthday yake usiku wa Jumamosi, haukuishia hapo bali
sasa wamerudisha ukaribu kiasi cha kuanza kutembeleana.
Kupitia
↧
Dj Tass wa Magic Fm apata shavu la kutumbuiza kwenye Big Brother Africa Hotshots Ijumaa hii
DJ Tass wa kituo cha radio cha Magic Fm pamoja na kipindi cha
Wakilisha cha Maisha Magic-DSTV amepata shavu la kwenda kutumbuiza
kwenye jumba la Big Brother Africa Hotshots Ijumaa hii.
Tass amesema kuwa ataondoka Dar es salaam Ijumaa hii kuelekea Johannesburg, Afrika Kusini.
Kupitia Instagram pia ameshare taarifa hiyo kwa kuandika, “Official Dj for BBA Hotshots 2014 representing
↧
↧
"Panya road" Wafunga Mitaa Minne Dar es Salaam
Ilikuwa hekaheka iliyosababisha shughuli katika mitaa minne ya
Tabata, Dar es Salaam kusimama kwa saa nne baada ya kundi la vijana
wenye nondo, mawe na visu kushambulia watu, kupora na kuharibu mali
kutokana na kile kilichodaiwa kuwa ni kulipiza kisasi.
Kundi hilo la vijana zaidi ya 30 ambalo mmoja wao
ameuawa linalofananishwa na lile la Panya Road ambalo hivi karibuni
lilisumbua
↧
Waumini Wamfungia Ofisi Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania,
Alinikisa Cheyo amezuiwa na waumini wa kanisa hilo kuingia katika ofisi
yake iliyopo Jakaranda, Mbeya kwa saa 18.
Cheyo,
ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini
Magharibi, alifungiwa mlango na waumini wa kanisa hilo Usharika wa
Jakaranda kumzuia asiingie mpaka atakapoitisha mkutano na kumrudisha
Mchungaji
↧
Mabweni na Madarasa ya Shule ya Filbert Bayi iliyopo mjini Kibaha Yateketea kwa Moto
Wanafunzi 70 wa Shule ya Msingi Filbert Bayi iliyopo mjini
Kibaha, mkoani Pwani, wamenusurika kuteketea kwa moto baada ya mabweni
mawili ya shule hiyo kushika moto na kuungua kabisa.
Moto
huo unaodhaniwa ulitokana na hitilafu ya umeme, ulizuka ghafla shuleni
hapo kuanzia katika bweni namba nne la wasichana, ambalo ni moja ya
mabweni ya wanafunzi hao kuanzia saa 8 za usiku wa kuamkia
↧
Sakata la Wizi wa Dola za Marekani Milioni 200 Katika akaunti ya Tegeta Escrow Lachukua Sura Mpya Bungeni
RIPOTI ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhusu kuchotwa kunakodaiwa isivyo halali kwa fedha katika Akaunti ya Escrow, sasa haitajadiliwa bungeni.
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma jana alipokuwa akijibu Mwongozo wa wabunge kuhusu kujadiliwa kwa ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Takukuru kuhusu sakata
↧
↧
Maelfu Ya Wananchi Wamtakia Afya Njema Rais Kikwete.....Jana Aliondolewa Bandeji, Hali yake inazidi Kuimarika
HALI ya afya ya Rais Jakaya Kikwete imeendelea kuimarika kwa kasi na jana alizungumza kwa simu na uongozi wa juu wa Tanzania kwa mara ya kwanza tangu afanyiwe upasuaji wa tezi dume Jumamosi iliyopita.
Alizungumza na Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, lakini pia alikuwa anawasiliana na mamia kwa mamia ya
↧
Mtoto aliyepotea auawa kikatili, maiti yaokotwa ndani ya Pagala
Mtoto Nuru Mohamedi (7) ameuawa kikatili na kisha mwili wake
kutelekezwa kwenye nyumba ambayo haijakamilika ujenzi iliyo Majohe
Kichangani jijini Dar.
Tukio hilo, ambalo limezua hofu
na huzuni kwa wakazi wa mtaa huo, lilibainika jana baada ya kupatikana
kwa maiti ya mtoto huyo ambaye kabla ya mauti kumkuta alikuwa amepotea
katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 6.
↧
AJALI MBAYA: Watu Kadhaa Wapoteza Maisha leo Asubuhi baada ya basi kupinduka Kahama
Watu
kadhaa wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa asubuhi hii kwenye
ajali ya basi la Wibonela lililokuwa likitoka Kahama kwenda Dar
lililopinduka eneo la kona ya Phantom, Kahama.
Chanzo cha
ajali hiyo ni mwendo kasi uliopelekea dereva wa basi kushindwa kulimudu
lilipofika kwenye kona ya Phantom na kupelekea kuingia mtaroni na
kupinduka.
Idadi kamili ya
↧
More Pages to Explore .....