Ripoti kutoka Vatican inasema ’Kanisa inabidi iwaruhusu na kuwakaribisha wapenzi ambao wapo kwenye mahusiano ya jinsia moja’.
Akizungumza na waandishi wa habari, katika mkutano uliofanyika Oct 13 ambao ulifanyika Jumatatu ili kutoa ripoti hiyo, Kadinali ‘Luis Antonio Tagle wa Philippines alisema ‘Wakatoliki wanafuatilia sana maswala ya umaskini, vita na uhamiaji na kuacha swala la watu
Tamko la Kanisa Katoliki kuhusu Wapenzi wenye mahusiano ya jinsia moja
↧
↧
Kumbukumbu ya Miaka 15 tangu kifo cha Mwalimu Nyerere
Watanzania leo tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka 15 tangu kufariki
kwa muasisi na Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere.
Mwalimu Nyerere alifariki dunia Oktoba 14, 1999 akiwa nchini
Uingereza alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa ya damu.
Akizindua rasmi maadhimisho ya kumbukumbu hizo jana, Mbunge wa Bunge
la Afrika Mashariki, Kate Kamba
↧
Big Brother Africa: Video Ya Mshiriki wa kike wa Tanzania ( Laveda) Akioga bafuni iko hapa
Hii ni video ya Mshiriki wa Tanzania ( Laved) akiwa na washiriki wenzake wakioga bafuni ndani ya jumba la big brother Africa.
Laveda ni miongoni mwa washiriki nane walioko kikaangoni wiki hii. Kura yako inahitajika kumnusuru asitolewe.
Unataka kumuona akiwa bafuni akioga? >
Ingia hapo juu kushuhudia video mbalimbali za
↧
Rais Kikwete augusia UJANA Urais 2015....." Katiba hairuhusu kijana chini ya miaka 35 kugombea Urais"
Wakati mbio za kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu 2015 zikianza
kushika kasi nchini, Rais Jakaya Kikwete amewataka vijana kumchagua mtu
anayefanana na kijana kurithi nafasi yake.
Kauli hiyo ya Rais Kikwete imekuja huku kukiwa na
makada kadhaa ndani ya chama chake ambao wametangaza nia ya kuwania
nafasi hiyo huku baadhi wakifungiwa kwa kuanza kampeni mapema na wengine
wakiendelea na
↧
Watakaoshindwa kutekeleza agizo la JK wapewe tiketi ya kwaheri
Zimesalia siku chache kabla ya kuingia mwezi mwingine wa
Novemba. Ni mwezi mchungu kwa watendaji wa wilaya kupitia halmashauri
mbalimbali waliopewa hadi mwezi huo kuhakikisha wanajenga maabara za
masomo ya sayansi.
Rais Jakaya Kikwete aliagiza kujengwa maabara za
shule katika maeneo yao na kuwataka kuhakikisha kuwa miundombinu hiyo
inakamilika mapema.
Akiwa katika mikutano ya
↧
↧
Rose Ndauka: Sitaki Kuwa na mwanaume tena
Siku chache baada ya uchumba wake kuvunjika, msanii
wa filamu Bongo, Rose Ndauka amefunguka na kusema kuwa kwa sasa haitaji
tena mwanaume kwani anajikita zaidi katika kufanya kazi.
Akizungumza na mwandishi wetu, Rose alisema katika maisha yake
ya uchumba alijifunza mambo mengi na anamshukuru Mungu amempa zawadi ya
mtoto hivyo anafanya kazi kwa bidii ili aweze kumlea mwanaye vizuri.
↧
Aunt Ezekiel naye Azungumzia Sakata la kutoka kimapenzi na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu
Staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel, amesema hakuna
ukweli wowote wa yeye kutanua na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro
Nyalandu nchini Marekani, kwani alikutana naye ukumbini, akiwa amealikwa
na blog iitwayo Vijimambo ambayo hutangaza utalii wa Tanzania nchini
humo kila mwaka.
Alisema wakati wa safari yake hakuelewa lolote kuhusu Waziri Nyalandu
na anashangazwa na yanayozungumzwa
↧
Chadema wapinga mchakato wa upigaji kura ya maoni bila Daftari la Kudumu la Wapigakura kuboreshwa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kitapinga kwa nguvu
zote mchakato wa upigaji kura ya maoni kuamua kuikubali au kuikataa
katiba inayopendekezwa, kuendeshwa bila Daftari la Kudumu la Wapigakura
kuboreshwa kwanza.
Kadhalika, chama hicho kimelalamikia baadhi ya kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa kwa madai kwamba, zina upungufu.
Msimamo huo wa Chadema ulitangazwa
↧
Ndugu wadaiwa kuua baba yao wakigombea mahari
POLISI mkoani Katavi inawashikilia ndugu wawili wakituhumiwa kumuua baba yao mzazi, Sado Shija (45) kwa kumcharanga kwa mapanga, wakigombea mahari iliyotolewa kwa dada yao alipokuwa akiolewa.
Imeelezwa kuwa wanandugu hao, Shinje Italam (25) na Shile Italam (20) walikuwa na ugomvi na baba yao huyo, wakigombea ng’ombe 20 zikiwa ni mahari iliyotolewa wakati alipoolewa dada yao.
↧
↧
CCM Yaanza Vikao Vizito mjini Dodoma
SIKU chache baada ya kumalizika kwa Bunge Maalumu la Katiba, macho na masikio ya wakazi wa mkoani hapa yanatarajiwa kuhamia katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) itakayofanya vikao vyake mjini hapa mwishoni mwa wiki.
Wakazi wa Dodoma walishuhudia Katiba Inayopendekezwa ikikabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar,
↧
Big Brother Africa: Mshiriki wa Kike wa Botswana AJILEGEZA Kwa jembe letu la Kiume ( Idris) linaloiwakilisha Tanzania
Siku washiriki wa BBA Hotshots wanatambulishwa, mwakilishi wa
Tanzania, Idris Sultan alimwambia mtangazaji IK kuwa cheche zake zipo
kwenye masuala ya wanawake. Huenda sasa shughuli imeanza.
Baada ya binti mrembo wa Botswana( Goitse) kumzingua mshikaji ( Idris ) aliyekuwa ametupa jiwe kumtaka awe mpenzi wake, hatimaye Idris jana alimnasa binti huyo na kula naye dinner
↧
Waliokufa Lori la Petroli wafikia Watano.....Polisi Aliyejaribu kuzuia aambulia kipigo
Idadi ya watu waliokufa kutokana na ajali ya moto wa lori lililopinduka na kisha kulipuka baada ya watu kulivamia kwa lengo la kujipatia mafuta, imeongezeka na kufikia watano kutoka vitatu vya awali.
Hayo yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.
Alisema katika ajali hiyo iliyotokea juzi usiku eneo la Mbagala, watu 16 walijeruhiwa baada ya
↧
Polisi yazungumzia Wimbi la Utekaji watoto Dar
Wakati hofu juu ya usalama wa watoto katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam ikizidi kutanda miongoni mwa wazazi na walezi, Polisi imekanusha kuwapo kwa matukio ya utekaji nyara watoto wanaosoma shule za msingi na kufanyiwa unyama ukiwamo ulawiti, kuuawa na hata kuchunwa ngozi.
Kwa wiki kadhaa sasa, hofu juu ya matukio ya aina hiyo yalichangiwa kwa kiasi kikubwa na taarifa za
↧
↧
Kombani Anusuru Ajira za DC, DEC Maabara za "Kikwete"
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani ametoa msaada muhimu wa Sh milioni 40 na bati 300 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara katika shule 12 za sekondari zilizopo katika jimbo la Ulanga Mashariki wilayani humo, mkoani Morogoro.
Mbali na msaada huo pia amesaidia vifaa mbalimbali ikiwamo sare, viatu na vyakula vyenye thamani ya Sh
↧
Mkuu wa Wilaya Akaangwa kwenye tume ya maadili
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, Anna Mwalende ameanika mbele ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma ushahidi wake dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Mrisho Gamba na kueleza namna alivyodhalilishwa na kunyanyaswa pamoja na viongozi wengine.
Mwalende ambaye ni shahidi wa tatu katika shauri linalomkabili Gamba, alidai amefanya kazi serikalini kwa miaka 24 katika
↧
Mvuvi Ajeruhiwa na Kiboko, Wawili waponea Chupuchupu
Shukurani Kando (34) ambaye ni mvuvi na mkazi kitongoji cha Kalumo kijiji cha Nambubi, Kata ya Kisorya amejeruhiwa kwa kung’atwa na kiboko na wengine wawili kunusurika wakati wakivua katika Ziwa Victoria wilayani Bunda, Mkoa wa Mara.
Kwa mujibu wa diwani wa kata hiyo, Misana Jigwila tukio hilo ni la juzi saa 1:00 asubuhi ambapo alisema kiboko huyo alitokea ghafla wakati wavuvi hao
↧
Wakimbizi 162,156 wa Burundi Wapewa Uraia wa Tanzania
Rais Jakaya Kikwete ametoa hati za uraia wa Tanzania kwa wakimbizi 162,156 kutoka nchi jirani ya Burundi na ambao wameishi nchini kwa miaka 42, tangu mwaka 1972.
Alitoa hati hizo juzi mjini Tabora, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo.
Kikwete alitoa hati hizo kwa wakimbizi 19 kwa niaba ya wenzao katika shughuli iliyohudhuriwa
↧
↧
Madai Mazito: Mchungaji atorosha mke wa mtu
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema anayedaiwa kutoroshwa na mchungaji huyo.
**********
Mchungaji anayejiita nabii na mtume, raia wa Jamhuri
ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyetajwa kwa jina moja la Emmanuel
amejikuta ndani ya majanga kufuatia madai mazito kwamba amemtorosha mke
wa mtu ambaye ni mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa
kasi,
↧
Mama Kanumba akanusha kutoka kimapenzi na kijana mdogo ambaye amemzidi umri (serengeti boy)
Mama wa marehemu, Steven Kanumba, Flora Mtegoa
amekanusha vilivyo taarifa zilizozagaa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na
kijana mdogo ambaye amemzidi umri (serengeti boy).
Mama Kanumba ambaye pia amefuata nyayo za mwanaye kwa kujiingiza
katika uigizaji, alifunguka hayo alipokuwa akizungumza na mwanahabari
wetu mambo mbalimbali yahusuyo maisha yake binafsi na sanaa kwa jumla.
↧
Wawekezaji wa gesi na mafuta wamiminika Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema taasisi mbalimbali za kimataifa zinazojishughulisha na masuala ya mafuta na gesi zimeanza kujitokeza kuomba fursa ya kuwekeza katika sekta hiyo.
Maombi hayo yamekuja kutokana na suala la mafuta na gesi kuondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano katika mchakato uliomalizika hivi karibuni wa Katiba Inayopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba.
↧
More Pages to Explore .....