Bunge maalumu la Katiba limepitisha rasimu ya katiba iliyopendekezwa. Hatua hiyo imefikiwa baada ya kura za ndio zilizopigwa na wajumbe kufikia kiwango kinachostahili.
Ili
katiba hiyo iliyopendekezwa ipite ilitakiwa kuungwa mkono na kura za
ndio theluthi mbili( 2/3) kutoka Tanzania bara na theluthi mbili (2/3) za ndio
kutoka Zanzibar.
Jumla ya wajumbe wote wa bunge hilo la
Rasimu ya Katiba inayopendekezwa yapitishwa kwa Kishindo
↧
↧
Juzi Wema Sepetu alitimiza miaka 26.....Leo Diamond Platunumz katimiza miaka 25......Happy Birthaday Diamond
Leo, Octoba 2, Staa wa muziki wa Bongo Flava Nasibu
Abdul 'Diamond Platunumz' anasherehekea siku yake ya kuzaliwa akiwa
anatimiza umri wa miaka 25.
Mpenzi wake, Wema Sepetu ambaye wengi wanasubiri kusikia atasema nini
au atatoa zawadi gani kwa Diamond ambaye alimpa gari aina ya Nissan
Murano, ameandika machache kwenye Instagram na kueleza kuwa anajipanga
kuandika ujumbe mzuri zaidi.
↧
Mume na Mke Wazichapa Hadharani......Wavuana Nguo na kutoana Manundu kisa Pombe!
Njemba mmoja aliyefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma Mtata,
wakazi wa mtaa Mrefu, Kigogo-Luhanga jijini Dar wamenaswa wakiangusha
bonge la timbwili barabarani na kusababisha umati wa watu kujikusanya
eneo hilo kujionea ‘sinema’ ya bure.
Tukio hilo lililofananishwa na muvi ya kivita lilitokea usiku wa
Jumanne iliyopita ambapo chanzo kimedaiwa kuwa ni mwanamke huyo
↧
Mgao wa Umeme kubaki histori Tanzania 2015
Hatua hiyo itafikiwa kutokana na mtambo unaojengwa katika kituo
kingine cha umeme kilichopo Tabata kinyerezi kuongezeka na kitakuwa
na uwezo wa kuzalisha umeme mega watts 150.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na
Madini Eliakimu Maswi amesema hadi sasa wana jumla ya vituo kumi
ambavyo vinazalisha umeme.
Naye Mkuu wa Mkoa Said Mecky
↧
Shibuda Anena...."Heri kuwa msaliti kuliko mhaini".....Ampongeza Rais Kikwete kwa usikuvu, Awapiga vijembe CHADEMA
MJUMBE wa Bunge Maalumu, John Shibuda, amesema ni heri kuwa msaliti kuliko kuwa mhaini kwa maslahi mapana ya Watanzania.
Shibuda ambaye alipewa nafasi kuzungumza baada ya Katiba Inayopendekezwa kupatikana, alisema anatoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), lakini amepinga kuwa sehemu ya kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Alisema anajua ataitwa msaliti, jambo
↧
↧
Pinda atamani kura kabla ya Uchaguzi Mkuu
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amesema ana shauku kuona Katiba Inayopendekezwa, inapigiwa kura na Watanzania na kuwa Katiba kabla hata ya Uchaguzi Mkuu wa mwakani, kwa kuwa ikiachiwa kuna watu wanaweza kuleta vurugu.
Alisema kazi iliyobakia ni kupeleka Katiba hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.
“Mimi naamini hata
↧
Wanajeshi, polisi watwangana risasi huko Tarime.......JWTZ 2 wajeruhiwa, Polisi 7 nao Hoi hospitalini
Watu 12 wamejeruhiwa wakati wa mashambulizi ya kurushiana risasi
baina ya askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) Kikosi 128 KJ cha Nyandoto
na Polisi wa Kituo cha Stendi wilayani Tarime mkoani Mara.
Hatua hiyo imekuja wakati wanajeshi hao walipokuwa
wakijaribu kumchukua askari mwenzao aliyekamatwa na Polisi wa Kikosi
cha Usalama Barabarani kwa kuendesha pikipiki bila kuwa na kofia ngumu
↧
Batuli: Sijavunja Uchumba wa Rose Ndauka
MSANII wa filamu Bongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’
ameshangazwa na madai kuwa, anahusika kuvunjika kwa uchumba wa msanii
mwenzake Rose Ndauka na kueleza kuwa hayo ni maneno ya watu wasiomtakia
mema.
Akizungumza na mwandishi wetu kuhusu madai hayo, Batuli
alisema hajawahi kuwa na uhusiano wowote na bwana wa Rose (Malick) na
kwamba ukaribu wao ni wa kikazi tu.
“Jamani siwezi
↧
Picha za Birthday Party ya Diamond Platinumz, zawadi ya Gari Aliyopewa na Video akibadilishana MATE na Wema Sepetu ziko hapa
Diamond Platinumz jana usiku alisherehekea siku yake ya kuzaliwa akitimiza umri wa miaka 25.
Sherehe
hiyo ilifana ambapo mama yake mzani na mpenzi wake Wema Sepetu pamoja
na ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria waliinogesha sherehe hiyo
iliyomalizika majira ya saa kumi alfajiri.
Pamoja na zawadi nyingine, Menejiment ya Diamond ilimpa zawadi ya gari jipya aina ya BMW X6.
↧
↧
Polisi Aliyemfungia Mwanafunzi Gesti na kufanya naye Mapenzi huko Moshi ashitakiwa kijeshi
Na Girdon Kalulunga
Taarifa kutoka mjini Moshi mkoani Kilimanjaro,
zinaarifu kuwa jeshi la polisi nchini limemkamata na kumfikisha katika
mahakama ya kijeshi askari wake Pc.Godlisen anayetuhumiwa kumtumikisha
katika vitendo vya ngono mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya
sekondari Okaoni iliyopo wilaya ya Moshi.
Habari zinasema kuwa, askari huyo ambaye Septemba 21 mwaka huu
↧
Davido, Diamond na Cassper Nyovest, kutumbuiza kwenye uzinduzi wa Big Brother, Jumapili hii
Davido, Diamond na rapper anayetamba kwa sasa Afrika Kusini Cassper
Nyovest wametangazwa kutumbuiza kwenye ufunguzi wa shindano la Big
Brother Afrika, Jumapili hii.
Ufunguzi huo utarushwa live kuanzia saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Cassper Nyovest anajulikana kwa ngoma zake kama “Gusheshe” na “Doc
Shebeleza” na amewahi kushare jukwaa na wasanii mbalimbali
↧
Wanafunzi wakithiri picha za ngono kwenye simu
BARAZA la Ushauri la Watumiaji Huduma za Mawasiliano Mkoa wa Iringa (TCRA-CCC) limewahadharisha vijana na matumizi yasiofaa ya huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia simu za mkononi.
“Picha za ngono na utafutaji wa wapenzi wapya ni sehemu ya huduma katika simu za mkononi zinazowavutia vijana wengi wakiwemo wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo,” alisema Mwenyekiti wa baraza
↧
Lulu Michael Afunguka kuhusu ukaribu wake na Martin Kadinda
Binti Mrembo ndani ya Bongo
Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefafanua ukaribu wake na Martin
Kadinda kwa kudai ni rafiki yake wa karibu na hakuna cha ziada.
Akizungumza na mwandishi wetu, Lulu
alisema yeye na Kadinda ni marafiki wa kweli na amekuwa akiyafurahia maisha
yao kwa kushauriana masuala mbalimbali ya kimaisha tofauti na wengine
wanavyojiongeza.
“Kadinda ni mtu
↧
↧
Ajiua kwa moto kisa Wivu wa Mapenzi
MKAZI mmoja wa kijiji cha Malolwa wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Ndikile Sunguli (38) amejichoma ndani ya nyumba hadi kufa baada ya kumjeruhi mke wake katika ugomvi unaoaminika ni wa mapenzi.
Tukio hilo la kutisha lilitokea Septemba 29, 2014 majira ya saa tano usiku katika kijiji cha Mlolwa.
Imeelezwa kuwa Sunguli alirudi kutoka matembezini akiwa amelewa huku akipiga makelele,
↧
CCM Mbeya wafagilia mafanikio ya Bunge Maalumu
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Mbeya mjini kimepongeza bunge maalumu kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuchakata maoni ya wananchi na hatimaye kupatikana Katiba inayopendekezwa.
Kupitia kwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa wa CCM kutoka Mbeya Mjini (MNEC), Charles Mwakipesile chama hicho kilitoa pongezi za dhati jana katika kikao maalumu na waandishi wa habari.
Mwakipesile alisema kupatikana kwa
↧
Kesi ya Ephrahim Kibonde wa Clouds Fm na Gadner Habash dhidi ya Askari wa Usalama barabarani yaahirishwa hadi Novemba 5
KESI ya kutumia lugha ya matusi na kutotii amri ya askari wa usalama barabarani, inayowakabili watangazaji wawili, Ephrahim Kibonde wa Kituo cha Habari cha Clouds Media Group na Gadner Habash wa Times Fm, imeahirishwa hadi Novemba 5 na 12 mwaka huu itakapoanza kusikilizwa.
Watangazaji hao waliiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni kuahirisha kesi hiyo kutokana na wakili wao kupata
↧
Rais Kikwete awacharukia Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanaosubiri taarifa ziletwe ofisini.....Asema atakayeshindwa kusimamia ujenzi wa maabara aachie ngazi
Rais Jakaya Kikwete amewakemea wakuu wa mikoa na wilaya wanaokaa
ofisini wakisubiri kuletewa taarifa bila kujua kinachoendelea katika
maeneo yao.
Amesema viongozi wa aina hiyo hawafai kuwapo kwenye nafasi hizo.
Aidha, aliwataka kukamilisha agizo lake la kujenga maabara katika
halmashauri zao na kuwa Desemba 9, mwaka huu atakagua shule zote.
Alitoa agizo hilo mjini Dodoma wakati
↧
↧
Uzuri wamponza, wenye wivu wamharibu sura
WASICHANA ndugu wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 16 na 18 wamemshambulia kwa visu binti mwenye miaka 15, kwa lengo la kumkomesha kwa sababu anasifiwa kuwa mzuri.
Katika tukio hilo la aina yake, ndugu hao walimvizia msichana huyo, Julia Alvarez(15), njiani wakati anakwenda nyumbani mjini Juan Domingo Peron kwenye jimbo la Formosa Kaskazini mwa Argentina.
Kwa mujibu wa kauli za
↧
CCM Moshi yaandaa mapokezi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kilimanjaro, kimepanga kufanya mapokezi
ya wajumbe waliokuwa katika Bunge la Katiba wakiwawakilisha wananchi wa
mkoa wa Kilimanjaro.
Mapokezi hayo, yanatarajiwa kuanzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (KIA), na kuelekea ofisi za CCM mkoa, na kufuatiwa na
mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya stendi kuu ya
mabasi mjini
↧
Video Inatisha: Muingereza mwingine akatwa kichwa na Wanamgambo wa Kiislamu ( ISIS )
Kundi la wanamgambo wa kiislamu la
Islamic state limetoa mkanda wa video unaoonyesha mateka Alan Henning
raia wa Uingereza akikatwa kichwa.
Henning mwenye umri wa miaka 47
ambaye ni dereva wa texi kutoka kaskazini mwa Uingereza alitekwa nyara
mwezi Disemba mwaka uliopita alipokuwa akilifanyia kazi shirika moja la
kutoa huduma za misaada kwa wakimbizi nchini Syria.
Kundi la
↧
More Pages to Explore .....