Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Ampa Maagizo Mazito CAG Mpya....." Usijifanye Muhimili, Kaliheshimu Bunge"

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Charles Kichere, leo Novemba 4 Ikulu Jijini Dar es Salaam na kumpa maagizo katika kazi yake mpya.

Moja ya maagizo aliyompa ni kuhakikisha anasuka upya uongozi ndani ya taasisi hiyo ili kuhakikisha kuwa inafanya kazi kulingana na sheria na maagizo  ya mihimili inayoongoza nchi.

Maagizo mengine aliyopewa ni, "CAG nenda kafanye kazi huko, usije ukajifanya na wewe ni muhimili mwingine, mihimili ni mitatu na umeshaiona hapa. Nafasi yako ni Mkaguzi Mkuu wa Serikali, kafanye kazi zako vizuri bila ya kuonea watu.


 “Unapopewa kazi na mihimili mingine kama Bunge au Mahakama kaitekeleze usibishane nao wewe ni mtumishi. Kasimamie hiyo ofisi kuna baadhi ya watendaji wako wanapokwenda kukagua kwenye balozi wanaomba fedha, sasa nenda kawachambue.” Amesema Rais Magufuli.

Aidha, amesema Rais ana mamlaka ya kumtoa CAG kulingana na Katiba na Sheria akieleza kuwa upo uwezekano wa mtumishi wa nafasi hiyo kutolewa muda wowote hata chini ya miaka mitano.

"Unaweza kumaliza miaka yako mitano au ukaishia mmoja. katika maisha ya duniani huwezi ukapewa mamlaka ya kuteua halafu usiwe na mamlaka ya kutengua, sikutishi lakini wewe nenda kafanye kazi zako"

Kuhusu suala la rushwa, Rais Magufuli amesema, "lakini pia kasimamie hiyo ofisi kuna baadhi ya watendaji wako wanapotumwa kwenda kukagua kwenye balozi wanalipwa pesa hapa na wakifika huko nako wanaomba pesa, ofisi ya CAG sio safi kama mnavyofikiri".

Kijana Aliyemtishia Mwenzake Kwa Bastola Afikishwa Mahakamani

$
0
0
Kijana Shaban Hamisi amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni akikabiliwa na kosa la kumtishia silaha  Dereva wa lori la mchanga Venance John ikiwa ni siku chache baada ya kusambaa mitandaoni video ya tukio.

Amesomewa mashtaka yake na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mkunde Mshanga mbele ya Hakimu Mfawidhi, Frenk Moshi, ambapo inadaiwa tukio hilo amelitenda Oktoba 30, 2019 maeneo ya Mbezi Mabwepande.

Inadaiwa alikutwa na Pistol aina ya Berreta yenye namba za usajili 102969 ambapo kwa makusudi alimtishia Venance John huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria, baada ya kusomewa shtaka alikana ambapo pia upande wa mashitaka umesema hauna pingamizi na dhamana.

Baada ya kueleza hayo, Hamisi ambae pia ni Mume wa Mtangazaji Zamaradi Mketema ameachiwa kwa dhamana ya Wadhamini wawili wenye barua na vitambulisho vya Taifa na wamesaini Bondi ya Sh.Mil 2 kwa kila mmoja, kesi imeahirishwa hadi November 13, 2019, mshitakiwa yupo nje kwa dhamana.

Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Usafirishaji:waziri Mhagamawaziri Mkuu Azitaka Azaki Zihimize Ulipaji Kodi ...Ataka Fedha Wanazopata Zitumike Kujenga Miradi Mikubwa

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Asasi za Kiraia ziendelee kuelimisha umma juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

“Nitoe rai kwenu wana AZAKI, muendelee kuielimisha jamii kuhusu umuhimu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla ili Serikali iweze kujenga miradi mikubwa ya kijamii,” amesema.

Ametoa wito huo leo jioni (Jumatatu, Novemba 4, 2019) wakati akizungumza na mamia ya wananchi na washiriki wa Maonesho ya Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) nchini yaliyoanza leo kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Maonesho hayo yatafikia kilele chake Ijumaa, Novemba 8, mwaka huu.

Amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa mashirika yasiyo ya Kiserikali katika kusukuma gurudumu la maendeleo nchini kama vile kuwajengea uwezo viongozi wa Serikali za Mitaa wakiwemo Madiwani, viongozi wa vijiji na mitaa ili watambue majukumu yao.

“Niwatoe hofu tu kwamba Serikali inatambua mchango wenu wa kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo; kujiongezea kipato na kupata ujuzi; utoaji wa huduma za kijamii hususan elimu, afya, upatikanaji wa maji, huduma za kisheria na huduma za mikopo midogo.

“Pia tunatambua mchango wa AZAKI wa kuleta teknolojia mpya na rahisi kwa wananchi pale mnapoona kuna uhitaji. Pia mnaisaidia Serikali kupinga mila potofu na kandamizi hasa kwa makundi yenye mahitaji maalum,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuzitaka AZAKI nchini zizingatie sheria iliyofanyiwa marekebisho ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24/2002 na kanuni zake, ambayo ilipitishwa na Bunge kupitia Sheria Na. 3/2019 na kusisitiza kwamba marekebisho hayo yalilenga kuboresha sekta hiyo.

“Nipende kuwahakikishia wana-AZAKI kuwa marekebisho hayo yalilenga kuboresha sekta ya NGOs na siyo kuyabana mashirika yasiyo ya Kiserikali kama ambavyo imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu. Marekebisho hayo yalizingatia misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977,” amesema.

Kuhusu mapato ya AZAKI, Waziri Mkuu amesema fedha wanazopata zinaweza kufanya miradi mikubwa ambayo itawanufaisha wananchi na akawasihi wazitumie kwenye ujenzi wa miradi mikubwa inayoonekana badala ya kuendesha semina na warsha.

“Tunajua fedha mnazopata zinaweza kusaidia kwenye miradi hii. Kwa mfano, kuanzia Januari hadi Septemba, mwaka huu, tulifanya mapitio ya ufadhili wa fedha mnazopata. Na katika upekuzi uliofanyika kwenye taasisi 92, ilibainika kwamba zilipokea jumla ya sh. bilioni 261.059 ambazo zimeingia kwenye AZAKI hizi.”

“Vilevile, mwaka 2016 hadi 2017, tuliangalia mapato ya NGOs 51, tukagundua kuwa katika kipindi cha miaka miwili, zimepokea jumla ya shilingi trilioni 2.5. Kama fedha hizi zote zingeratibiwa vizuri kwa kupunguza matumizi yasiyo na umuhimu ni lazima tungefika mbali. Tutumie vizuri fedha hizi za ufadhili kwa miradi inayoonekana,” amesisitiza.

Akizungumzia kuhusu ajira kwa vijana, Waziri Mkuu amesema vijana ni kundi lenye umuhimu mkubwa katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo licha ya kuwa wanakabiliwa na uhaba wa ajira.

Amesema Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, inaonesha asilimia 35 ya Watanzania wote ni vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35. Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa nguvukazi ya Taifa wa mwaka 2014, vijana wamebainika kuwa ndio kundi kubwa la nguvukazi ya Taifa ambao ni asilimia 56 ya nguvukazi yote nchini.

“Kila mwaka, kumekuwa na ongezeko la vijana wanaoingia kwenye soko la ajira. Kwa mfano, taarifa ya hali ya ajira ya Shirika la Kazi Duniani (ILO) kwa mwaka 2019 inaonesha kuwa asilimia 11.8 ya nguvukazi ya vijana duniani ambao ni takriban vijana million 59.1 hawana kazi,” amesema.

Mapema, Waziri wa Nchi (OR-TAMISEMI), Bw. Suleiman Jafo alizishukuru asasi zote za kiraia ambazo zinafanya kazi Tanzania kwa sababu zinawahudumia wananchi kwa karibu zaidi. “Ninazishukuru NGOs zote kwa kusaidia kutoa elimu kwa wananchi. GTunazishukuru kwa kazi kubwa mnayoifanya Tanzania nzima kwa kushirikiana na Ofsi ya Rais TAMISEMI,”

Akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu alisema mwaka huu, wizara yake imesajili mashirika yasiyo ya Kiserikali 617 ikilinganishwa na mashirika 385 yaliyosajiliwa mwaka 2017.

“Kati ya hayo mashirika 617, mashirika 44 ni ya ngazi ya kimataifa; 551 ni ngazi ya kitaifa, saba ni katika ngazi ya mikoa na mashirika 15 ni katika ngazi ya wilaya. Hadi kufikia Oktoba, 30, 2019, tumeshasajili mashirika 19,318” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Azitaka Azaki Zihimize Ulipaji Kodi ...Ataka Fedha Wanazopata Zitumike Kujenga Miradi Mikubwa

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Asasi za Kiraia ziendelee kuelimisha umma juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

“Nitoe rai kwenu wana AZAKI, muendelee kuielimisha jamii kuhusu umuhimu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla ili Serikali iweze kujenga miradi mikubwa ya kijamii,” amesema.

Ametoa wito huo leo jioni (Jumatatu, Novemba 4, 2019) wakati akizungumza na mamia ya wananchi na washiriki wa Maonesho ya Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) nchini yaliyoanza leo kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Maonesho hayo yatafikia kilele chake Ijumaa, Novemba 8, mwaka huu.

Amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa mashirika yasiyo ya Kiserikali katika kusukuma gurudumu la maendeleo nchini kama vile kuwajengea uwezo viongozi wa Serikali za Mitaa wakiwemo Madiwani, viongozi wa vijiji na mitaa ili watambue majukumu yao.

“Niwatoe hofu tu kwamba Serikali inatambua mchango wenu wa kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo; kujiongezea kipato na kupata ujuzi; utoaji wa huduma za kijamii hususan elimu, afya, upatikanaji wa maji, huduma za kisheria na huduma za mikopo midogo.

“Pia tunatambua mchango wa AZAKI wa kuleta teknolojia mpya na rahisi kwa wananchi pale mnapoona kuna uhitaji. Pia mnaisaidia Serikali kupinga mila potofu na kandamizi hasa kwa makundi yenye mahitaji maalum,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuzitaka AZAKI nchini zizingatie sheria iliyofanyiwa marekebisho ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24/2002 na kanuni zake, ambayo ilipitishwa na Bunge kupitia Sheria Na. 3/2019 na kusisitiza kwamba marekebisho hayo yalilenga kuboresha sekta hiyo.

“Nipende kuwahakikishia wana-AZAKI kuwa marekebisho hayo yalilenga kuboresha sekta ya NGOs na siyo kuyabana mashirika yasiyo ya Kiserikali kama ambavyo imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu. Marekebisho hayo yalizingatia misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977,” amesema.

Kuhusu mapato ya AZAKI, Waziri Mkuu amesema fedha wanazopata zinaweza kufanya miradi mikubwa ambayo itawanufaisha wananchi na akawasihi wazitumie kwenye ujenzi wa miradi mikubwa inayoonekana badala ya kuendesha semina na warsha.

“Tunajua fedha mnazopata zinaweza kusaidia kwenye miradi hii. Kwa mfano, kuanzia Januari hadi Septemba, mwaka huu, tulifanya mapitio ya ufadhili wa fedha mnazopata. Na katika upekuzi uliofanyika kwenye taasisi 92, ilibainika kwamba zilipokea jumla ya sh. bilioni 261.059 ambazo zimeingia kwenye AZAKI hizi.”

“Vilevile, mwaka 2016 hadi 2017, tuliangalia mapato ya NGOs 51, tukagundua kuwa katika kipindi cha miaka miwili, zimepokea jumla ya shilingi trilioni 2.5. Kama fedha hizi zote zingeratibiwa vizuri kwa kupunguza matumizi yasiyo na umuhimu ni lazima tungefika mbali. Tutumie vizuri fedha hizi za ufadhili kwa miradi inayoonekana,” amesisitiza.

Akizungumzia kuhusu ajira kwa vijana, Waziri Mkuu amesema vijana ni kundi lenye umuhimu mkubwa katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo licha ya kuwa wanakabiliwa na uhaba wa ajira.

Amesema Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, inaonesha asilimia 35 ya Watanzania wote ni vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35. Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa nguvukazi ya Taifa wa mwaka 2014, vijana wamebainika kuwa ndio kundi kubwa la nguvukazi ya Taifa ambao ni asilimia 56 ya nguvukazi yote nchini.

“Kila mwaka, kumekuwa na ongezeko la vijana wanaoingia kwenye soko la ajira. Kwa mfano, taarifa ya hali ya ajira ya Shirika la Kazi Duniani (ILO) kwa mwaka 2019 inaonesha kuwa asilimia 11.8 ya nguvukazi ya vijana duniani ambao ni takriban vijana million 59.1 hawana kazi,” amesema.

Mapema, Waziri wa Nchi (OR-TAMISEMI), Bw. Suleiman Jafo alizishukuru asasi zote za kiraia ambazo zinafanya kazi Tanzania kwa sababu zinawahudumia wananchi kwa karibu zaidi. “Ninazishukuru NGOs zote kwa kusaidia kutoa elimu kwa wananchi. GTunazishukuru kwa kazi kubwa mnayoifanya Tanzania nzima kwa kushirikiana na Ofsi ya Rais TAMISEMI,”

Akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu alisema mwaka huu, wizara yake imesajili mashirika yasiyo ya Kiserikali 617 ikilinganishwa na mashirika 385 yaliyosajiliwa mwaka 2017.

“Kati ya hayo mashirika 617, mashirika 44 ni ya ngazi ya kimataifa; 551 ni ngazi ya kitaifa, saba ni katika ngazi ya mikoa na mashirika 15 ni katika ngazi ya wilaya. Hadi kufikia Oktoba, 30, 2019, tumeshasajili mashirika 19,318” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kuanza Kwa Mkutano Wa Kumi Na Saba Wa Bunge

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne November 05

Shehena Ya Mifuko Isiyokidhi Viwango Yakamatwa

$
0
0
Ofisi ya Makamu wa Rais inaendelea kusimamia marufuku ya katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki kwa kushirikiana na Kikosi kazi cha Kitaifa. 

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la uzalishaji, utengezaji na uingizaji na usambazaji wa mifuko isiyokidhi viwango vilivyowekwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Kikosi kazi cha Kitaifa cha kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki pamoja na Kamati za Mikoa na Wilaya wanaendesha oparesheni maalumu nchi nzima kwa lengo la kusaka mifuko isiyokidhi viwango.

Tarehe 30/10/2019 NEMC ilikamata marobota 21 katika Wilaya ya Misenyi, Mkoani Kagera na marobota 7 Mkoani Arusha ambayo yanashikiliwa katika kituo cha polisi cha Arusha. Upelelezi wa mashauri haya bado unaendelea.

Tarehe 4/11/2019 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi kwa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mwanza wamekamata shehena ya mifuko isiyokidhi viwango gunia 8 yenye thamani ya Shilingi 10,000,000/-  Mifuko hiyo iliingia kupitia bandari bubu ya Bwiru jijini Mwanza ikitokea nchi jirani. Watuhumiwa watafikishwa mahakamani na mifuko hiyo itateketezwa kwa mujibu wa sheria kama itakavyoelekezwa na NEMC.

Ofisi ya Makamu wa Rais, inatoa wito kwa wafanyabiashara wote wanaojihusisha na uingizaji, usambazaji na uuzaji wa mifuko mbadala kuhakikisha wanazingatia matakwa ya Sheria. Aidha, wafanyabiashara wanasisitizwa kuacha kuzalisha, kuingiza nchini, kuuza na kusambaza mifuko isiyokidhi viwango. Hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote wanaokiuka agizo hilo.

Waziri wa Kilimo: Tumejipanga Kudhibiti Sumukuvu

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Arusha
Hivi karibuni, Serikali ya Tanzania ilipata fedha za kutekeleza mradi wa kuzuia kuenea kwa sumukuvu hapa nchini (TANIPAC). Mradi huo unalenga kupunguza kutokea kwa madhara ya sumukuvu katika mfumo wa chakula kupitia udhibiti husishi kwenye mnyororo wa thamani wa mazao ya mahindi na karanga, hivyo kuboresha uhakika na usalama wa chakula na hatimae kuimarisha afya na lishe ya jamii yetu na kuimarisha biashara kati ya Tanzania na nchi zinazotuzunguka.

Mradi huo unatekelezwa kwa kuzingatia mkakati Madhubuti kwa kushughulikia masuala yote yanayohusu sumukuvu hapa nchini. Mkakati huo unazingatia udhibiti wa sumukuvu katika hatua za uzalishaji, uvunaji, udhibiti wa kibilojia, teknolojia baada ya kuvuna na njia za ukaushaji, uhifadhi, kujenga uwezo wa kitaasisi, uratibu na kutoa elimu ya kuhamasisha wadau muhimu. Ushiriki wa sekta binafsi ni muhimu katika uhaulishaji wa teknolojia pamoja na kuhakikisha mradi unakuwa endelevu.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo leo tarehe 4 Novemba 2019 wakati akifungua Mkutano wa kwanza wa Afrika wa kudhibiti Sumkuvu (Alfasafe) kwenye vyakula uliofanyika katika Hoteli ya Mount Meru Jijini Arusha.

Mhe Hasunga amesema kuwa Ushirikiano wa kiutafiti, kati ya sekta binafsi na watunga sera, ni muhimu katika kufanikisha mageuzi ya kilimo.

Waziri Hasunga amesema kuwa Tangu kuibuka kwa tatizo la sumukuvu mwaka 2016, Tanzania imechukua hatua mbalimbali za kupunguza kusambaa kwa sumukuvu hapa nchini. Kwa kutambua changamoto za kukabili sumukuvu, ambapo kunahitajika kutumia njia mbalimbali kuanzia kwenye hatua za uzalishaji, uvunaji, uhifadhi, usindikaji na kuhusisha sekta za Umma na Binafsi katika kupunguza upotevu wa chakula na kuongeza upatikanaji wa chakula salama na lishe bora.

Amesema, Tanzania imeanzisha Kamati  Jumuishi ya Uendeshaji inayohusisha sekta na taaluma kutoka taasisi mbalimbali chini ya Uenyekiti wa Wizara ya Kilimo ambayo ina mamlaka ya kusimamia masuala yote yanayohusu sumukuvu.

Kadhalika, amewahakikishia washiriki hao kuwa kinga ya sumukuvu - Alfasafe TZ01;  imeshasajiliwa kwa matumizi hapa nchini Tanzania.  "Aidha, nimefarijika kuwa kazi hii inafanywa na Kampuni Binafsi ambayo imewekeza katika uzalishaji, na usambazaji wa bidhaa hii ambayo itaokoa Maisha ya watu hapa nchini" Alisisitiza

"Napenda kuwahakikishia utayari wa Wizara yangu katika kuyatumia maazimio mtakayokubaliana katika mkutano huu. Aidha, Serikali ya Tanzania, inatilia maanani na inaunga mkono hatua zinazochukuliwa katika kuhimiza biashara ya chakula salama, usalama wa chakula na lishe" Alisema Mhe Hasunga

Tanzania kwa sasa inatekeleza Awamu ya Pili Programu ya Uendelezaji wa Sekta ya Kilimo (ASDP II) yenye lengo la kuleta mageuzi ya sekta ya kilimo kuwa na kilimo chenye tija na kibiashara, pamoja na kukuza uchumi wa wakulima wadogo na kuboresha maisha, uhakika wa chakula na lishe bora.

Uhakika wa chakula na lishe ni muhimili ambao ni muhimu wa ASDP II Katika kufikia malengo hayo, uwekezaji katika utafiti wa kilimo ni muhimu katika kuleta matokeo kwa wakulima na wadua wengine katika mnyororo wa thamani.

Waziri Hasunga amesema kuwa kutokana na takwimu za Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) za mwaka 2017, Tanzania inaongoza katika uzalishaji wa mahindi na karanga katika ukanda wa nchi za Afrika Mashariki, kwa kuzalisha tani milioni 6 na tani milioni moja mtawalia.

Amesema, Pamoja na mafanikio hayo, Serikali inatambua kuwa, ingawa mazao hayo ni muhimu kwa chakula cha kila siku, lakini yanakabiliwa na ukubwa wa tatizo la sumukuvu ambalo linahatarisha usalama wa chakula na kuwa kikwazo cha biashara ya mazao hayo kwa nchi jirani na Tanzania.

Mkutano huu ambao umewaweka pamoja watafiti, wafanyabiashara, watunga sera na wadau wa maendeleo, ambao unalenga kupanga mikakati ya kuongeza kasi ya matumizi ya kinga ya sumukuvu (Alfasafe), na kukabili sumukuvu barani Afrika, unadhihirisha mabadiliko chanya ya kimtazamo tunayoyahitaji.

Iran yatangaza hatua mpya za kukiuka mkataba wa silaha za nyuklia

$
0
0
Iran imetangaza leo hatua zake mpya za kukiuka makubaliano makubwa ya silaha za nyuklia yaliyosainiwa mwaka 2015 kati ya mataifa yenye nguvu kubwa duniani. 

Iran imesema kwa sasa inatumia nyenzo ambayo ina kasi ya mara 50 zaidi ya ile iliyokubaliwa na mkataba huo. 

Tangazo hilo limetolewa wakati Iran ikianzisha maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 40, tangu Marekani ilipoukamata ubalozi wake mnamo mwaka 1979, mzozo uliodumu kwa siku 444. 

Mkuu wa shirika la kitaifa la nishati ya Atomiki nchini Iran Ali Akbar Salehi amesema kwa kuanza kutumia nyenzo hizo za kasi kubwa, Iran itapunguza muda wa mwaka mmoja ambao wataalam walisema Iran itauhitaji ili kuwa na vifaa vyote vya kutengeneza silaha za nyuklia endapo itaamua kufanya hivyo. 

Iran ilishakiuka makubaliano hayo kuhusu urutubishaji madini ya urani kama hatua ya kuushinikiza Umoja wa Ulaya kupata mkataba mpya, mwaka mmoja tangu Marekani ilipojiondoa katika mkataba huo.

-DW

LIVE: Kutoka Bungeni Dodoma Kwenye Kipindi Cha Maswali Na Majibu

$
0
0
LIVE:  Kutoka Bungeni Dodoma Kwenye Kipindi Cha Maswali Na Majibu

PICHA: CAG Mpya Akabidhiwa Ofisi Rasmi

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mpya Charles Kichere, aliyeapishwa jana Novemba 04, amekabadhiwa ofisi na Mtangulizi wake Prof. Mussa Assad leo Novemba 05, katika makao makuu ya ofisi hiyo yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mpya Charles Kichere, aliyeapishwa jana Novemba 04, akikabidhiwa Rasmi ofisi na Prof. Mussa Assad aliyemaliza muda wake leo Novemba 05, 2019 katika makao makuu ya ofisi hiyo yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Msimamo Wa Ligi Kuu Tanzania Bara Ulivyo Kwa Sasa

Ofisi Yavunjwa, Nyaraka mbalimbali zikiwemo fomu za uchaguzi Zaibiwa

$
0
0
Mnamo tarehe 31.10.2019 majira ya saa 19:50 usiku huko Kijiji cha Pashungu, Kata ya Itawa, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya. JACKSON MATONYA [28] Afisa mtendaji wa Kijiji cha Pashungu, mkazi wa Pashungu aligundua kuvunjwa ofisi ya Kijiji cha Pashungu na kuibiwa nyaraka mbalimbali kama ifuatavyo;

1. Fomu za wagombea wenyeviti wa vijiji na vitongoji.
2. Fomu za wajumbe wa kundi maalum la wanawake zilizojazwa 21 za
wagombea wa chadema 7 za wagombea wa ccm.
3. Fomu 24 za wenyeviti wa vijiji na vitongoji ambazo hazijajazwa.
4. Fomu 46 za kundi maalum la wanawake ambazo hazijajazwa.
5. Mhuri wa msimamizi msaidizi wa uchaguzi.
6. Faili moja la mihtasari ya malipo ya walengwa wa TASAF.
7. Faili la mihtasari ya vikao vya Halmashauri ya Kijiji na mikutano ya hadhara.
 
Kutokana na tukio hilo, jumla ya watuhumiwa nane [08] wamekamatwa ambao ni:-
1. MWAWA POSTA [40] katibu wa CHADEMA Kata ya Itawa
2. ENOCK JECK MWASILE [25]
3. ALEX JECK MWASILE [21]
4. AMONI SIFUKU MWASILE [40]
5. ALUWA JOHN NGELEKA [37]
6. BAHATI SIFUKU YANJILWA [45]
7. MOSKO ALLAN MWASELE [32]
8. CHARLES MANGENI MWASILE [31] wote wakazi wa Kijiji cha Pashungu.

Video Mpya | Kayumba Ft Linah - UMENIWEZA

$
0
0
Video Mpya | Kayumba Ft Linah - UMENIWEZA

Video Mpya | Walter Chilambo - God Of Mercy

$
0
0
Video Mpya | Walter Chilambo - God Of Mercy

Video Mpya | Harmonize - UNO

Kimataifa | Marekani kujiondoa rasmi makubaliano ya tabia nchi ya Paris

$
0
0
Marekani imeanza rasmi mchakato wa kujitoa kutoka katika makubaliano ya Paris ya mazingira, kulingana na waziri wake wa mambo ya kigeni Mike Pompeo.

Rais wa  Marekani Donald Trump  alikuwa  mpinzani  mkubwa  wa makubaliano  hayo  wakati  alipokuwa  anawania  kiti  cha  urais, na utawala  wake  umekuwa  ukifanya  kila  unaloliweza kubadilisha sheria  za  mazingira, ukisema zinazuwia  biashara  na  kutoa  kwa nchi  nyingine  nguvu  ya  ushindani.

Pompeo alielezea  kuhusu kile  alichokiita "mzigo usio wa  haki wa kiuchumi uliowekwa  kwa  wafanyakazi wa  Marekani, biashara, na walipa  kodi, kwa  ahadi za Marekani  zilizotolewa  chini  ya makubaliano  hayo," wakati  akitangaza  kujitoa  huko. Amesema ,"mfano bora  na  wenye  uhalisia" utapendekezwa  na  Marekani kupinga  makubaliano  hayo  ya  dunia.

Makubaliano  ya  mwaka  2015 yalitiwa  saini  na  karibu  nchi  zote, na  kuuweka  utawala  wa  Trump  dhidi  ya  karibu  washirika  wake wote  pamoja  na  washindani  wake  wakuu  kuhusiana  na  suala  la mabadiliko  ya  tabia  nchi. Trump  binafsi  ni  mtu  mwenye  shaka na  mabadiliko  ya  tabia  nchi.

Utawala  wa  Trump rasmi uliuarifu  Umoja  wa  mataifa  hatua  yake hiyo  ya  kujitoa  siku ya Jumatatu, ukianza  mchakato  wa  mwaka mmoja  ambao  utakamilika  siku  moja  baada  ya  uchaguzi  wa  rais wa  Marekani  mwaka  2020.

Msemaji  wa  Umoja  wa  mataifa  alilithibitishia shirika  la  habari  la Ujerumani dpa kuwa  taasisi  hiyo  ya  dunia  imepokea  barua ya Marekani.

Credit:DW

Rais Xi Jinping wa China Aimwagia Sifa Tanzania....Korosho, Madini ya Tanzanite Yamvutia Zaidi

$
0
0
Maonesho ya pili ya kimataifa ya bidhaa zinazoagizwa China yamefunguliwa leo mjini Shanghai, China. Rais Xi Jinping wa China amehutubia ufunguzi huo.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu ya "zama mpya, kunufaika kwa pamoja na mustakabali wa pamoja" yameshirikisha zaidi ya makampuni 3,000 kutoka nchi na sehemu 150 za mabara matano duniani.

Katika hafla hiyo viongozi wa Mataifa 64 walihudhuria akiwemo Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Mawaziri Wakuu wa Jamaica; Serbia na Greece huku ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa. ‪

Aidha baada ya kufungua maonesho hayo Rais wa China ametembelea Mabanda ya nchi (5) yakiwemo mabanda ya Ufaransa; Ugiriki; Serbia; Jamaica na Tanzania.

Katika ziara ya kutembelea Banda la Tanzania Rais Xi Jinping alifuatana na Waziri Mkuu wa Jamaica; Greece na Serbia na kupokelewa na Waziri Bashungwa.
 
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki, alitoa maelezo juu ya bidhaa mbalimbali za kilimo na madini zinazopatikana nchini Tanzania na vivutio vya utalii. Aidha, Balozi Kairuki aliwasilisha salaam za Rais wa Tanzania Dk. John Magufuli kwa Rais wa China.

Kwa upande wake Rais wa China ameipongeza Tanzania kwa kushiriki katika maonesho ya pili ya Kimataifa ya Bidhaa za Nje na ametuma salaam za pongezi kwa Rais Magufuli kwa kuimarisha mahusiano ya kiuchumi kati ya Tanzania na China.

Rais Xi alivutiwa zaidi na bidhaa ya korosho za Tanzania na madini ya Tanzanite ambapo alitaka kufahamu zaidi juu ya upatikanaji wa bidhaa hizo katika soko la China.

Michezo | Kocha Mkuu wa Yanga SC, Mwinyi Zahera Atimuliwa

$
0
0
Uongozi wa Klabu ya Yanga leo Jumanne Novemba 5,umetangaza rasmi kumfuta kazi Kocha Mkuu wa timu hiyo Mwinyi Zahera pamoja na benchi lake lote la ufundi hadi walinzi wa timu hiyo

Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Yanga Mshindo Msolla ambapo amesema Boniface Mkwasa atakaimu kama Kocha Mkuu wa muda.

Prof. Mussa Assad Aahidi Kumpa Ushirikiano CAG Mpya.....Ataja Kazi Yake Mpya Atakayoifanya Kwa Sasa

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali aliyemaliza muda wake, Prof. Mussa Assad ameahidi kumpa ushiarikiano wowote atakaouhitaji CAG mpya, Charles Kichere kwani wao wanafahamiana kwa kipindi kirefu tangu akiwa anafundisha katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne Novemba 5, alipokuwa akimkabidhi Kichere ofisi ambapo amesema kuwa akihitaji kitu kutoka kwake au kutokana na ujuzi wake binafsi atakuwa tayari kumsaidia.

“Kichere nimefahamiana naye kwa muda mrefu sana sio mtu mgeni kwangu hivyo ninachoahidi ni kwamba akihitaji chochote kile kutoka kwangu binafsi au kutokana na ujuzi wangu wa miaka mitano nitampa, siku yoyote akipiga simu nitakuwepo kwaajili yake.

“Kichwani kwangu mimi ni mtu ambaye ninapenda nipande bamia nilisimamie liote liingie jikoni nile kwahiyo kwasababu hiyo katika miezi miwili iliyopita nilianza kuwekeza katika kilimo hivyo ni nachokifikiria sasa hivi nikae shambani kwangu na kupumzika kule lakini wakinihitaji watu wa mjini watanipigia simu nitakuja kufanya kazi zangu,” amesema Prof. Assad.

Katika hatua nyingine, Profesa Assad  amemshauri  CAG Kichere kuwa ni vyema akawajengea uwezo watumishi waliopo kuliko kuwafanyia mabadiliko kwa haraka kwa sababu hatua hiyo inaweza kuharibu utendaji wa taasisi.

“Taasisi haitakiwi kufanyiwa mabadiliko ya haraka muhimu ni kuwajengea uwezo waliopo, kinyume na hapo unaweza kuharibu taswira.

“Huwa naamini changes  zinaweza kutokea ila zitokee katika namna ambayo zimepangwa vizuri, si mwaminifu katika mfumo wa kutoa watu wote na kuweka new team usually lazima kutakuwa na mkanganyiko and can be very expensive kwa institutions kama hizi ambazo mtu anajifunza kwa miaka mingi.

“Kufikia level ya DAG lazima amefanya kazi na amekaa kwenye ofisi miaka 10 hadi 15, kwa hiyo experience yake ni muhimu kuihamishia kwa mtu mwingine, ukifanya immediate changes unaweza kupoteza ile instution memory,” amesema Profesa Assad
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images