Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Scholarships for Tanzanian Students| Ufadhili wa Kusoma Nje ya Nchi (Unalipiwa Kila Kitu) | Deadline ni Mwakani

0
0
📚 FURSA ZA UFADHILI  WA KUSOMA NJE YA NCHI

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

    🎓Tanzanian Scholarships

Kama wewe ni Mtanzania mwenye Ndoto ya Kusoma nje ya Nchi lakini hukuwa na uwezo, basi hii ni Nafasi yako. Kuna Nafasi Nyingi sana za Ufadhili zimetangazwa (Scholarships)


 Zote Hizo ni Full Funded( Unalipiwa kila Kitu) Japo kuna zingine utachangia kidogo 

_______________________ 

Bado hujachelewa, Deadline ni kuanzia Mwezi huu wa  kumi na moja  hadi Mwakani-2020
._______________________ 


1.Global Scholars Program- Clark University USA 

2.Hong Kong PhD Fellowship Scheme for International Students

3.Clarendon Fund Scholarships, University of Oxford, UK

4.Holland Scholarship for Non EEA International Students

5.Justus & Louise van Effen Excellence Scholarships in Netherlands

6.Oxford Pershing Square Graduate Scholarships in UK

7.Emile-Boutmy Scholarship in France for Non EU Students

8.Karen McKellin International Leader of Tomorrow Award, University of British Columbia

9.Weidenfeld-Hoffman Scholarships and Leadership Program

10.Radboud Scholarship Programme | Netherlands

Bofya hapo chini kujua zaidi
👇👇👇👇👇👇👇👇


http://ajirazote.com/scholarship/

Fahamu Zaidi Kuhusu Ugonjwa Wa Mshipa Wa Ngiri (Hernia/Hydrocele)

0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya maumble ya kiume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0713785111

Hiki Ndo Kikosi cha Yanga Kitakachowavaa Waarabu Misri Leo

0
0
Kikosi cha Yanga  kitakachoanza leo dhidi ya Pyramids FC ya Misri kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho utakaopigwa majira ya saa 3:00 Usiku.

Matokeo| Full Time- Simba Yapeleka Kilio Mbeya City

0
0
Klabu ya Soka ya Simba SC imeiadhibu bila huruma Mbeya City baada ya kuifunga goli 4 kwa sifuri kwenye mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam huku Medie Kagere akiendeleza moto wake wa kufunga

Mabao ya Simba yamefungwa na Medie Kagere dakika ya 8 kwa mkwaju wa penati huku mabao mengine yakifungwa na Clatous Chama dakika ya 43, Shiboub dakika ya 78 na Deo Kanda dakika ya 87.

Matokeo ya mechi zote leo (Jumapili November 3 ) ligi kuu Tanzania bara

Yanga Yateua Wakurugenzi Wapya Watatu

Bodi ya Mikopo HESLB Yatoa Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliopata Mkopo Awamu ya Tatu 2019/2020

0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa orodha ya tatu ya  majina ya wanafunzi waliopata mkopo  yenye jumla ya wanafunzi 4785 wa mwaka wa kwanza wa masomo 2019/2020.

Wanafunzi hao wamepata mikopo yenye thamani ya Sh14.3 bilioni na hivyo kufanya idadi  ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo kufikia 46,838. yenye thamani ya sh162.86.

Taarifa iliyotolewa  Jumapili Novemba 3, 2019 na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru imeeleza kuwa wanafunzi waliopata mikopo katika awamu ya tatu wanaweza kupata taarifa zao kupitia akaunti walizotumia kuomba mkopo

Kuhusu taratibu za malipo kwa wanafunzi, amesema fedha za wanafunzi waliopata mikopo zimeshapelekwa vyuoni na vyuo vimeelekezwa kuhakikisha fedha zinawafikia wanafunzi walengwa mara wanapofika na kukamilisha taratibu za usajili.

Ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga Sh450 bilioni kwa ajili ya wanafunzi 128,285. Kati yao, wanafunzi 83,285 ni wenye mikopo wanaoendelea na masomo ya mwaka wa pili, tatu na kuendelea.


==>>KUONA ORODHA YA MAJINA AWAMU YA TATU, BOFYA HAPA.

Mamia ya Wasafiri wamekwama baada ya Bomba la Gesi Kupasuka Kilwa,Lindi

0
0
Mamia ya Wasafiri wamekwama kwa saa zaidi ya 3 karibu na eneo la kati ya Songas na Banduka, Wilaya ya Kilwa Lindi baada ya bomba la gesi kwenye mitambo ya umeme kudaiwa kupasuka, Polisi wamezuia magari na vyombo vingine vya moto kupita eneo hilo ili kuepusha madhara.

Gesi hiyo inavuja kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) hivyo kuwashawishi walinzi wa kituo jirani cha kupokea gesi kutoka Madimba Mtwara na Songosongo kilicho chini ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kusaidia kuimarisha ulinzi.

“Ni kweli kuna hitilafu kidogo. Wataalamu wetu wanashughulikia hali hiyo ila hakuna moto wala madhara yoyote kwa binadamu,” amesema Nigel Whittaker mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Songas.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu November 4

Diamond Platnumz Amjibu Ali Kiba

0
0
Diamond Platnumz amezungumzia kilichoandikwa na msanii mwenzake, Ali Kiba katika mtandao wake wa  kijamii wa Instagram saa chache baada ya  kumualika kushiriki tamasha la Wasafi litakalofanyika Novemba 9, 2019.

Akizungumza jana Ijumaa Novemba Mosi, 2019 katika televisheni ya Wasafi ,Diamond alisema hakujua Ali Kiba alilenga nini, akibainisha kuwa hawezi kuwa na chuki naye.


“Alikiba ni kaka yangu, amenizidi umri na alianza muziki kabla yangu. Sijui aliandika vile akimaanisha nini, yeye na mimi ni miongoni mwa tunaoiletea sifa nchi kupitia muziki, upinzani wetu ni kwenye muziki tu, simchukii na nina imani naye pia hanichukii.

“Mimi nimetokea maisha ya chini sana ila Mwenyezi Mungu amenibariki ndio maana niliwashika mkono watu wengine ikiwemo Harmonize, tamanio la WASAFI ni kuona vijana tunapeana support na kumuunga mkono kwenye vitu ambavyo anavifanya.

“Mtu anavyofanikiwa na kuanza kushika mkono vijana wengine ni jambo zuri, furaha yangu ni kuona vijana wengi wa Tanzania wenye talent wanafanikiwa, pengine na mimi nisingemshika mkono, watu wasingeona kipaji chake.

”Nimefanya kazi nyingi za Kushikiana na wasanii, nina collabo nyingi ndani hadi natamani nizitaje, nina ngoma inakuja na Swaelee, kuna nyingine nimefanya na Steff London.

“Wasafi Festival itaanza mapema na kutakuwa na mashindano ya kuimba, Mshindi atapata Tsh. Millioni 10 na nafasi ya kusainiwa WCB Wasafi, kutakuwa na mashindano ya Dancers ambapo washindi pia watapata zawadi ya Tsh. Million 10 na nafasi ya kufanya kazi na wasanii wa WCB.

“Juzi tu hapa nilishinda Tuzo ya Mtumbuizaji bora Siku ya Festival nitatumbuiza kweli na hapa Nipo na Mh. Makonda Siwezi kumuangusha kwenye mkoa wake,” amesema Diamond.

Lugola: Siku za mtu anayejiita Kigogo kwenye mitandao ya kijamii zinahesabika

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, amesema kuwa hivi karibuni Jeshi la Polisi litamtia nguvuni mtu anayejiita kigogo kupitia ukurasa wa Twitter.

Ametoa kauli hiyo leo Novemba 2, 2019 katika mkutano na wanahabari wakati akitoa tathimini ya hali ya usalama hapa nchini kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo amesema kuwa muda si mrefu polisi watamtia nguvuni mtu huyo.

"Kalenda inazo tarehe, utahesabu mwezi mfupi na mrefu, nataka niwaambie kwa kifupi siku za huyo Kigogo zinahesabika na hana siku nyingi", amesema Waziri Lugola.

Aidha katika hatua nyingine, Waziri Lugola ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa na utulivu na amani na kutoa onyo kwa yeyote atakayekuwa na mpango wa kuvuruga uchaguzi ama kampeni basi atatumbukizwa kwenye gari lenye maji ya kuwashawasha.

''Niwaonye wanasiasa, siasa za majitaka na lugha ya matusi zinazoudhi wengine, Jeshi la Polisi limejipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kuwashusha kwenye majukwaa ili wasiendelee kumwaga sumu inayohatarisha amani kwa wananchi", amesema.

"Ole wake yule mwenye mpango wa kuvuruga kampeni au uchaguzi tutamshughulikia, tuna magari ya washawasha, wakorofi na watakaoleta fujo watawashwawashwa kweli, hatutawamwagia tu bali wakorofi kabisa tutawatumbukiza na kuwakogesha kwenye hayo maji yanayowashawasha'', ameongeza Kangi Lugola.

Waarabu wa Misri Waibana Mbavu Yanga....Yatolewa Rasmi Kombe la Shirikisho

0
0
Kikosi cha Yanga jana kimeshindwa kufurukuta mbele ya wapinzani wake Pyramids kwenye mchezo wa marudio wa Kombe la Shirikisho uliochezwa nchini Misri.

Yanga SC waliingia katika uwanja wa 30 June kurudiana na Pyramids wakiwa nyuma kwa magoli 2-1, magoli ambayo yalifungwa katika mchezo wa kwanza jijini Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, hivyo walitakiwa kuifunga Pyramids FC mabao 2-0 ili kupenya mbele hatua ya makundi

Kufunga magoli mawili bila kuruhusu kufungwa haikuwa kitu rahisi kwa Yanga, hivyo walijikuta  wakimaliza mchezo huo kwa kupoteza kwa kufungwa kwa magoli 3-0 .


Magoli ya Pyramids FC yalifungwa na Traory dakika ya 27, Farouk 79 na El Said dakika za nyongeza.

Matokeo hayo yanaitoa Yanga kwenye michuano ya kimataifa ambapo Pyramids inafuzu hatua ya makundi kwa juma ya mabao 5-1.

Kwa maana hiyo Tanzania sasa msimu wa 2019/20 haina muwakilishi yoyote wa kimataifa katima michuano hiyo. 

Beki wa Simba SC Shomari Kapombe atangaza kustaafu kuichezea timu ya Taifa | Taifa Stars

0
0
Beki wa Club ya Simba SC Shomari Kapombe ameamua kutangaza rasmi kuwa ameandika barua ya kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, licha ya kuwa umri wake bado unaruhusu kuendelea kuitumikia Taifa Stars.

Kapombe ametangaza kufikia hivyo baada ya kutathmini afya yake, kwani anadai Taifa Stars inahitaji wachezaji watakao kuwa fiti kwa asilimia 100 na upande wake haoni kama anaweza kujitoa kwa asilimia 100 kwa sababu amekuwa akikumbwa na majeraha, hivyo kaomba aendelee kuitumikia timu yake ya Simba SC ambayo haina mashindano mengi zaidi ya Ligi.

Scholarships for Tanzanian Students| Ufadhili wa Kusoma Nje ya Nchi (Unalipiwa Kila Kitu) | Deadline ni Mwakani

0
0
📚 FURSA ZA UFADHILI  WA KUSOMA NJE YA NCHI

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

    🎓Tanzanian Scholarships

Kama wewe ni Mtanzania mwenye Ndoto ya Kusoma nje ya Nchi lakini hukuwa na uwezo, basi hii ni Nafasi yako. Kuna Nafasi Nyingi sana za Ufadhili zimetangazwa (Scholarships)


 Zote Hizo ni Full Funded( Unalipiwa kila Kitu) Japo kuna zingine utachangia kidogo 

_______________________ 

Bado hujachelewa, Deadline ni kuanzia Mwezi huu wa  kumi na moja  hadi Mwakani-2020
._______________________ 


1.Global Scholars Program- Clark University USA 

2.Hong Kong PhD Fellowship Scheme for International Students

3.Clarendon Fund Scholarships, University of Oxford, UK

4.Holland Scholarship for Non EEA International Students

5.Justus & Louise van Effen Excellence Scholarships in Netherlands

6.Oxford Pershing Square Graduate Scholarships in UK

7.Emile-Boutmy Scholarship in France for Non EU Students

8.Karen McKellin International Leader of Tomorrow Award, University of British Columbia

9.Weidenfeld-Hoffman Scholarships and Leadership Program

10.Radboud Scholarship Programme | Netherlands

Bofya hapo chini kujua zaidi
👇👇👇👇👇👇👇👇


http://ajirazote.com/scholarship/

NACTE Yatangaza Awamu Ya Nne Ya Udahili Katika Ngazi Ya Astashahada Na Stashahada Kwenye Vyuo Na Taasisi Mbali Mbali Kwa Mwaka Wa Masomo 2019/2020

0
0
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linautangazia umma kwamba limefungua dirisha la udahili kwa AWAMU YA NNE na ya mwisho, kwenye Vyuo na Taasisi zinazotoa programu za Astashahada na Stashahada hapa nchini, zinazotambuliwa na Baraza kuanzia tarehe  1 Novemba, 2019  hadi tarehe 10 Novemba, 2019 ambapo dirisha hilo litafungwa.

Hatua hiyo imekuja kufuatia maombi yaliyowasilishwa na Vyuo na Taasisi mbalimbali kutaka nafasi zilizo wazi ziweze kujazwa. Kwa kuzingatia hilo, Baraza linatoa wito kwa wahitimu wa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita na wale wote walio na nia na sifa za kujiunga na programu mbalimbali kutumia fursa hii kutuma maombi ya udahili kwenye Taasisi na Vyuo ambavyo bado vinapokea maombi ya udahili katika ngazi ya Astashahada na Stashahada.

Aidha, Vyuo na Tasisisi zitakazohusika kwenye awamu hii, zinaarifiwa kwamba mfumo utakuwa wazi kupokea majina ya wanaodahiliwa ili kufanyiwa uhakiki hadi hiyo tarehe 10 Novemba, 2019. 

Vyuo na Taasisi zinazotaka kubadilisha taarifa za wanafunzi waliowasilishwa na kuonekana kuwa na mapungufu yaliyopelekea kukosa sifa, nazo zinashauriwa kufanya hivyo ndani ya kipindi hicho kuanzia leo tarehe 01 hadi 10 Novemba, 2019.

Ikumbukwe, kwamba uhakiki wa majina yote yatakayowasilishwa utafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 15 Novemba, 2019, na  matokeo ya uhakiki yatatolewa tarehe 17 Novemba, 2019.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)

Shirika la Reli Tanzania (TRC) Lakanusha Taarifa Zilizochapishwa Na Gazeti La Tanzania Mpya

Taarifa Kwa Umma Kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania - TPDC | Uvujaji Wa Gesi Katika Kituo Cha Songas - Somangafungu

LIVE toka IKULU | Rais Magufuli Anamwapisha CAG Mpya Pamoja na Viongozi Wengine Aliowateua Jana

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 04 Novemba, 2019 anawapisha viongozi mbalimbali aliowateua jana. Tazama tukio zima hapo chini.

Tigo yatangaza kuungana rasmi na Zantel

0
0
Kampuni ya Mawasiliano ya MIC Tanzania Public Limited Company (Tigo), leo imetangaza rasmi kuungana na kampuni ya Zanzibar Telecom Public Limited Company (Zantel) baada ya kukamilika kwa taratibu zote za kisheria na kiumiliki ambapo lengo kuu ni kukuza na kuboresha huduma za mawasiliano nchini.

Pamoja na kupata vibali kutoka mamlaka zinazohusika, mchakato wa kuhamisha hisa na umiliki kamili kutoka Zantel kwenda Tigo sasa umekwisha kamilika. Kufuatia kukamilika kwa zoezi hili sasa makampuni haya yataunganisha shughuli zake za kiutendaji Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.

Akizungumza kuhusu muungano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari alisema hatua hiyo ina manufaa makubwa kwa Taifa; “Ninaamini kuwa kuunganishwa kwa kampuni hizi - Tigo na Zantel kutajenga huduma jumuishi kwa watanzania wote siku za usoni. Wateja wote wa Tigo na Zantel wataweza kufurahia huduma bora kutoka kwenye soko imara litakalosaidia kuchochea ubunifu kwenye sekta ya mawasiliano,” alisema Karikari.

Muunganiko wa makampuni haya mawili utasaidia katika kuimarisha utoaji wa huduma kwa wateja wa Tigo na Zantel waliopo kote Tanzania Bara na Visiwani. Aidha, muungano huu utawezesha kupanua wigo wa huduma zetu pamoja na kuongeza ubora wa upatikanaji wa mawasiliano katika maeneo ya mijini na vijijini. Vile vile muungano huu utasaidia katika usambazaji wa huduma za mawasiliano kwa makampuni na taasisi mbalimbali nchini na pia kupanua huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi.

Tunategemea mafanikio chanya kutokana na muunganiko wa makampuni haya mawili wenye lengo la kuchangia kwenye maendeleo ya Taifa.

Zoezi la kuunganisha taratibu za kiutendaji wa makampuni haya mawili zinatazamiwa kuanza hivi punde. Aidha, wateja wa Tigo na Zantel wataendelea kupata huduma bila usumbufu wowote kutoka mtandao husika kwani namba na laini za wateja hazitabadilika.


                                   Mwisho

Taarifa Kwa Umma Toka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)

0
0
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unatoa wito kwa umma kuchukua tahadhari na matumizi ya moto kwenye maeneo yanayokaribiana na misitu. Tunawaomba wananchi wote wakiwemo wavunaji, warina asali, wawindaji, wafugaji na hususani wakulima kuepuka matumizi ya moto katika kuandaa mashamba kwani wamekuwa ni chanzo kikuu cha moto unaoingia kwenye misitu hasa kunapokuwa na upepo mkali.

Tunapenda kuuarifu umma kuwa kwa siku za hivi karibuni kumekuwepo na ongezeko la matukio ya moto katika mikoa ya Iringa na Njombe iliyopelekea kuunguza mashamba ya miti ya watu binafsi na yale ya serikali hususani shamba la miti la Sao Hill lililopo katika wilaya ya Mufindi. Moto huo umeunguza sehemu tofauti za msitu huo na kusababisha hasara kufuatia kuungua miti ya umri tofauti.

TFS inapenda kutoa pole kwa wadau waliounguliwa vifaa vyao vya uvunaji pamoja na mazao yaliyovunwa wakati mashine ya kuangushia miti (chainsaw) ilipolipuka ghafla katika moja ya tukio lililopelekea kusambaa kwa moto. 

Aidha, tunatoa shukrani nyingi sana kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama (W) Mufindi, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), JKT Mafinga, Jeshi la zimamoto, Jeshi la Akiba, wavunaji wa shamba la Sao Hill, vikosi vya moto vya shamba, watumishi wa TFS na wananchi wote wa maeneo jirani kwa ushirikiano wao wa hali na mali katika kupambana na moto. 

Katika hatua hiyo ninawakumbusha tena kwa mara nyingine waandaaji wa mashamba kuhakikisha kuwa wanapata vibali vya matumizi ya moto kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Namba 14 ya mwaka 2002 kama sehemu ya kukabiliana na changamoto hii.

Tunatoa wito kwa wananchi wote kuepuka shughuli zozote ambazo zinaweza kupelekea au kusababisha moto kwenye misitu ya asili au ya kupanda kwani moto ni adui namba moja wa misitu yetu.


Imetolewa na
Prof Dos Santos Silayo
KAMISHNA MHIFADHI - TFS
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images