Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Yanga Yateua Wakurugenzi Wapya Watatu


Diamond Platnumz Amjibu Ali Kiba

$
0
0
Diamond Platnumz amezungumzia kilichoandikwa na msanii mwenzake, Ali Kiba katika mtandao wake wa  kijamii wa Instagram saa chache baada ya  kumualika kushiriki tamasha la Wasafi litakalofanyika Novemba 9, 2019.

Akizungumza jana Ijumaa Novemba Mosi, 2019 katika televisheni ya Wasafi ,Diamond alisema hakujua Ali Kiba alilenga nini, akibainisha kuwa hawezi kuwa na chuki naye.


“Alikiba ni kaka yangu, amenizidi umri na alianza muziki kabla yangu. Sijui aliandika vile akimaanisha nini, yeye na mimi ni miongoni mwa tunaoiletea sifa nchi kupitia muziki, upinzani wetu ni kwenye muziki tu, simchukii na nina imani naye pia hanichukii.

“Mimi nimetokea maisha ya chini sana ila Mwenyezi Mungu amenibariki ndio maana niliwashika mkono watu wengine ikiwemo Harmonize, tamanio la WASAFI ni kuona vijana tunapeana support na kumuunga mkono kwenye vitu ambavyo anavifanya.

“Mtu anavyofanikiwa na kuanza kushika mkono vijana wengine ni jambo zuri, furaha yangu ni kuona vijana wengi wa Tanzania wenye talent wanafanikiwa, pengine na mimi nisingemshika mkono, watu wasingeona kipaji chake.

”Nimefanya kazi nyingi za Kushikiana na wasanii, nina collabo nyingi ndani hadi natamani nizitaje, nina ngoma inakuja na Swaelee, kuna nyingine nimefanya na Steff London.

“Wasafi Festival itaanza mapema na kutakuwa na mashindano ya kuimba, Mshindi atapata Tsh. Millioni 10 na nafasi ya kusainiwa WCB Wasafi, kutakuwa na mashindano ya Dancers ambapo washindi pia watapata zawadi ya Tsh. Million 10 na nafasi ya kufanya kazi na wasanii wa WCB.

“Juzi tu hapa nilishinda Tuzo ya Mtumbuizaji bora Siku ya Festival nitatumbuiza kweli na hapa Nipo na Mh. Makonda Siwezi kumuangusha kwenye mkoa wake,” amesema Diamond.

Lugola: Siku za mtu anayejiita Kigogo kwenye mitandao ya kijamii zinahesabika

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, amesema kuwa hivi karibuni Jeshi la Polisi litamtia nguvuni mtu anayejiita kigogo kupitia ukurasa wa Twitter.

Ametoa kauli hiyo leo Novemba 2, 2019 katika mkutano na wanahabari wakati akitoa tathimini ya hali ya usalama hapa nchini kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo amesema kuwa muda si mrefu polisi watamtia nguvuni mtu huyo.

"Kalenda inazo tarehe, utahesabu mwezi mfupi na mrefu, nataka niwaambie kwa kifupi siku za huyo Kigogo zinahesabika na hana siku nyingi", amesema Waziri Lugola.

Aidha katika hatua nyingine, Waziri Lugola ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa na utulivu na amani na kutoa onyo kwa yeyote atakayekuwa na mpango wa kuvuruga uchaguzi ama kampeni basi atatumbukizwa kwenye gari lenye maji ya kuwashawasha.

''Niwaonye wanasiasa, siasa za majitaka na lugha ya matusi zinazoudhi wengine, Jeshi la Polisi limejipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kuwashusha kwenye majukwaa ili wasiendelee kumwaga sumu inayohatarisha amani kwa wananchi", amesema.

"Ole wake yule mwenye mpango wa kuvuruga kampeni au uchaguzi tutamshughulikia, tuna magari ya washawasha, wakorofi na watakaoleta fujo watawashwawashwa kweli, hatutawamwagia tu bali wakorofi kabisa tutawatumbukiza na kuwakogesha kwenye hayo maji yanayowashawasha'', ameongeza Kangi Lugola.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili November 3

Mabadiliko Halmashauri ya Mji wa Ifakara na Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro.

Yaliyojiri Katika Utatuzi Wa Mgogoro Wa Ardhi Kati Ya Kiwanda Cha Saruji Cha Mbeya Na Kijiji Cha Nanyala Mkoani Songwe Novemba 2, 2019

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliagiza Wizara za Ardhi, Madini, Tamisemi na Viwanda zishughulikie mgogoro wa Ardhi baina ya Kijiji cha Nanyala na kiwanda cha Saruji cha Mbeya.

Mgogoro unahusisha ekari 2315 ambapo ekari 1475 zipo Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe na ekari 840 ziko wilaya ya Mbeya.

Leo tumekuja kama alivyoagizwa kujionea hali halisi ikiwa lengo letu ni kuumaliza mgogoro huo na tutafuata sheria taratibu na kanuni zote katika kutatua mgogoro huu.

Kufikia Jumatatu Kiwanda cha Saruji kiondoe kesi tatu zilizoko mahakamani baina ya kiwanda na wana kijiji cha Nanyala kama alivyo agiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, hii si hiyari, haiwezekani Mkuu wa Nchi anaagiza jambo halafu kuna mtu anajivuta kutekeleza.

Utoaji wa leseni za madini katika eneo lenye mgogoro usitishwe, Kijiji cha Nanyala, Wilaya za Mbozi na Mbeya zisitishe utoaji wa hati za kimila katika eneo lenye mgogoro.

Wakulima na wafugaji ambao wanalima na kufuga katika eneo hilo, mgogoro huu hauna maslahi nao hivyo wasizuiliwe kuendelea na shughuli za kilimo na ufugaji.

Wachimbaji wadogo wadogo wa chokaa wanaofanya shughuli zao kwa msimu katika eneo lenye mgogoro wasizuiliwe waendelee kufanya kazi zao.

Naibu Waziri Madini Stanslaus Nyongo

Wataalamu waangalie namna ya kubalidisha Sheria ya Service Levy ili halmashauri za Mbeya na Mbozi waweze kufaidika kwa pamoja na sio halmashauri moja kufaidika huku nyingine ikipunjwa.

Kiwanda cha Saruji cha Mbeya kama wanataka kutunza eneo kwa ajili ya matumizi ya baadaye waangalie namna bora inayotambulika kisheria na sio kukwepa gharama kwa kutofuata taratibu na sheria.

Naibu Waziri OR TAMISEMI Josephat Kandenge

Halmashauri ambayo haikupata service levy na ilistahili kupata ilipwe kwakuwa tusirekebishe ya mbele bila kuangalia stahiki zilizopita za Halmashauri hizi.

Naibu Waziri Viwanda na Biashara Mhandisi Stella Manyanya

Wizara ya Viwanda na Biashara ingependa kuona mgogoro huu unaisha kwakuwa kiwanda cha Saruji na vingine vilivyopo katika eneo hilo vina mchango katika maendeleo ya taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila

Migogoro inapoendelea sana lazima kuna upande unakuwa hauna uelewa hivyo wataalamu watusaidie katika hilo pia tusiingie sana katika mgogoro wa mapato kuwa yaende kwa nani isipokuwa tujielekeze kuumaliza mgogoro huo.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela

Mkoa wa Songwe tunaomba kesi zifutwe ili wananchi waendelee kufanya shughuli zao kwa uhuru.

Mkoa wa Songwe tunataka wawekezaji na tunawakaribisha waje kwakuwa sisi tuna mali ghafi za kutosha ila tu wajue kuwa lazima sheria na taratibu zifuatwe.

Milioni 600 Kujenga Upya Kituo Cha Afya Lukole Kilichoachwa na Wakimbizi Mkoani Kagera.

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi,Kagera.
Zaidi  ya  sh milioni 600 Za kitanzania  zimetengwa na Halmashauli  ya  wilaya ya Ngara  ili kujenga upya kituo cha afya Lukole kilichokuwa kimejengwa kwa tope na kilichokuwa  kikiwahudumia wakimbizi waliokuwa wakiishi katika kambi hiyo.
 
Hatua hiyo imefikiwa baada ya  wakimbizi  kutoka nchi jirani za Burundi na Rwanda  waliokuwa wakiishi  kambini hapo kuondoka na kituo cha afya  kuendelea kuwahudumia wananchi wanaoishi jirani na kambi hiyo.
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauli ya Ngara  Aidan Bahama   amesema kwa bahati mbaya kituo  hicho kilijengwa  kwa tope na kupelekea  baadhi ya majengo  Kuwa na hali mbaya na kuwa katika  hatari ya kuanguka.
 
Kadhalika Aidan ambaye ni Mkurugenzi wa halmashauri hiyo na amemshukuru  mh rais John Pombe Magufuli kwa kutoa pesa ambapo baada ya ujenzi huo kituo hicho kitakuwa ni moja ya vituo bora wilayani Ngara.
 
Nao baadhi ya wananchi na wafanyakazi katika kituo hicho cha Afya Ambao ni Bw Joseph Hezzron,bw James Charles,Bi Noral Charles Mihayo  wameipongeza hatua hiyo ya serikali nakusema kuwa nijitihada za kujali huduma za wananchi.
 
Mkurugenzi huyo amebainisha kuwa Jumla ya majengo sita yatajengwa katika kituo hicho ikiwa ni pamoja na jengo la wagonjwa wa nje,jengo la upasuaji,maabara,jengo la kuhifadia maiti na nyumba moja ya mtumishi.

Viongozi wa vyama vya Ushirika watakiwa kutotumia fedha za wanachama bila idhini ya Mkutano mkuu wa Chama.

$
0
0
SALVATORY NTANDU
Viongozi wa Chama cha  Ushirika wa  akiba na mikopo SHIRIKISHO SACCOS LIMITED wilayani  Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kutotumia fedha za wanachama kinyume na makisio yalioridhiwa  na mkutano mkuu na badala yake ili kuondoa migogoro isiyokuwa na tija.

Hayo yamebainishwa na Daniel Kimatha na Prisca Agustino kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa SHIRIKISHO SACOSS LIMITED uliofanyika Mjini kahama ambao ulikuwa na lengo la kutathimini hoja mbalimbali zinazokikabili chama hicho kwa mwaka 2019 na kuangalia namana bora ya kuzipatia ufumbuzi.

Wamesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongzo katika shirikisho hilo kutumia fedha kinyume na makisio yaliyoridhiwa na mkutano mkuu wa mwaka na kusababisha kuibuka kwa malalamiko kutoka kwa wanachama wao na badala yake wanapaswa kuwashirikisha kabla ya kufanya matumizi.

“katika mwaka huu wa 2019 viongozi wetu wametumia shilingi laki mmoja kinyume na makisio yalioridhiwa na mkutano mkuu suala hili halikubaliki walipaswa kutushirikisha,alisema Kimatha.

Akijibu hoja hizo Mwenyekiti wa {SHIRIKISHO SACCOS LIMITED} Tito  Greyson Okuku amekiri kujitokeza kwa suala hilo na kusema kuwa walitumia fedha za faida walizopata kutokana na rida walizokusanya  na kuomba radhi wanachama hao na kuahidi kuwa suala hilo halitajitokeza tena.

Kwa upande Dronick Kamugisha ni afisa Ushirika wa Halamshauri ya Mji wa Kahama amesema kutokana na kasoro mbalilimbali zilizojitokwza katika chama hicho wao kama Halamshauri wamejipanga kutoa elimu ili wananchama waelewe dhima ya Ushirika na namna bora ya Uendeshaji.

Naye Mkaguzi wa vyamba vya Ushirika mkoa wa Shinyanga Rodrick Kilemile  amesema ofisi yake imebaini vyama vingi vya ushirika hawana wataalamu wa mahesabu hali ambayo imekuwa ikiwapa shida katika uandaaji wa taarifa za mwaka na kusababisha kuwepo kwa migororo.

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia Ashauri Muda wa Kuchukua Fomu Serikali za Mitaa Uongezwe

$
0
0
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia amemtaka Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo kuongeza muda kuchukua fomu za uchaguzi wa Serikali za mitaa kutokana na kasoro mbalimbali zilizojitokeza.

Wagombea wa vyama mbalimbali vya siasa walianza kuchukua na kurejesha fomu kuwania uwenyekiti wa kijiji, mtaa, kitongoji na ujumbe wa kamati ya mtaa kuanzia Oktoba 29, 2019. Shughuli hiyo inayofanyika kwa siku saba itakamilika Novemba 4, 2019.

Akizungumza mjini Dodoma jana Jumamosi Novemba 2, 2019 Mbatia alisema baadhi ya maeneo ofisi zilifunguliwa siku mbili tu, baada ya hapo zilifungwa jambo lililowakosesha  nafasi wagombea wengine kuchukua fomu.

Amesema Serikali imetoa muda wa siku saba kwa ajili ya wagombea kuchukua na kurudisha fomu lakini baadhi ya vituo vinafungwa kabla ya muda.

Amesema malalamiko ni mengi kila kona, na kumtaka Jafo kuongeza muda ili wenye nia ya kugombea kujitokeza kwa wingi.

BREAKING:Rais Magufuli Amteua Charlse Kichele Kuwa CAG Mpya Kuchukua Nafasi ya Profesa Mussa Assad

$
0
0
Rais Magufuli amemteua Charles Kichere kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuanzia leo  akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Mussa Assad ambaye muda wakeu unaisha kesho.

Viongozi wengine walioteuliwa ni Majaji 12 wa Mahakama Kuu, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait ( Mwandisi Aisha Amuru ), Kamishna wa Kazi (Kanari Francis Leonard Mbindi ) na Katibu Tawala mkoa wa Njombe (Katalina Tengia Levekati )

Viongozi wote walioteuliwa leo na mheshimiwa Rais Magufuli wataapisha kesho asubuhi saa tatu na nusu viwanja vya Ikulu.

Waziri Kigwangalla Kuogoza Kampeni Ya Kutangaza Vivutio Vya Utalii.

$
0
0
Na.Aron Msigwa – WMU
Waziri wa Malisili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema  ataongoza kampeni ya kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika ukanda wa kusini na ukanda wa Kaskazini magharibi kwenye hifadhi mpya za Taifa zilizotangazwa hivi karibuni.

Amesema kampeni hiyo itawahusisha wasanii na watu maarufu wenye ushawishi katika jamii na inalenga kuhamasisha utalii wa ndani na kutangaza vivutio vya utalii vilivyo katika hifadhi za Taifa za Ruaha,Mikumi, Nyerere na Burigi – Chato.

Dkt.Kigwangalla ameyasema hayo alipokuwa akizugumza na Menejimenti ya Shirika la hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) na wakuu wa Kanda wa shirika hilo jijini Arusha.

Amesema hatua hiyo ya kuwatumia wasanii na watu maarufu wenye ushawishi katika jamii inalenga kuogeza hamasa kwa watanzania wavijue na kuvitembelea vivutio vya utalii vilivyopo katika hifadhi hizo hivyo kuogeza idadi ya watalii wa ndani.

Dkt.Kigwangalla amesema wasanii hao na watu maarufu wana wafuasi wengi wanaofuatilia kazi zao na matukio wanayofanya katika jamii kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii hivyo ni vyema wakatumika kutangaza utalii katika maeneo hayo.

Amesema hatua kazi hii ya kuhamasisha utalii wa ndani ni vyema wadau na watumishi walio kweye sekta husika wakawa wa kwanza kuvijua vivutio vya utalii vilivyopo katika maeneo mbalimbali ili iwe rahisi kuvielezea na kuvitagaza.

“Tukitaka kutagaza soko la utalii wa ndani lazima sisi wenyewe tuanze kwanza kuyajua maeneo ya vivutio tuliyonayo ili iwe rahisi kuwafikia watu wengine, tuna marafiki zetu ndani na nje ya Tanzania inakua rahisi kwetu kuwaalika na kuwakaribisha kwenye vivutio hivyo kwa kuwa sisi wenyewe tunavijua” Amesisitiza Dkt.Kigwangalla.

Amesema mkakati wa sasa ni wa kusambaza uelewa kuhusu vivutio vilivyopo ndani ya nchi ili kuwahamasisha watanzania wengi zaidi kutembelea vivutio hivyo akibainisha kwamba mkakati huo utakuwa na matokeo ya haraka na gharama nafuu ya kuhamasisha utalii wa ndani katika maeneo mengine ya nchi tofauti na ilivyo sasa ambapo watu wengi wanayafahamu maeneo machache na hasa yaliyo mikoa ya Kaskazini.

“Nilipoamua kuutangaza mlima Kilimanjaro na mimi mwenyewe kushiriki kupanda mlima kila mtu alishuhudia nini kilichotokea, kila mtu alikua akiuzungumzia mlima na hii inaongeza umaarufu wa mlima ndani ya nchi huu ni mkakati tunaotakiwa kuutumia katika maeneo mengine” Amesema.

Dkt. Kigwangalla ameiagiza TANAPA iendelee kukusanya takwimu za makundi mbalimbali ya watalii wa ndani wanafanya utalii katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo watazania wanaoshiriki mbio za marathon.

Katika hatua nyingine Waziri wa Maliasili na Utalii ameiagiza TANAPA kuifanyia kazi na kuikamilisha miradi ya ujenzi wa magati na ununuzi wa vivuko na Boti zitakazokuwa zikitumika kusafirisha watalii katika ukanda wa Pwani wa Bahari ya Hindi kwenye eneo la Hifadhi ya Taifa ya Saadani.

Amesema gati hizo zitajengwa Dar es salaam, Saadani, Pangani, Pangani na Tanga ili kuwezesha boti hizo kusimama katika maeneo hayo yenye vivutio vya utalii na kushusha watalii wanaotaka kutembelea maeneo hayo.

“Hili ni eneo muhimu sana kwetu na rahisi kuuza huduma zetu za utalii wa ndani ya maji kutokana na uwepo wa visiwa na idadi ya watu wanaokwenda kuvitembelea, Ni lazima tujipange kuzitumia fursa hizi kwa kuwa na boti nzuri zitakazowawezesha watu kufanya utalii, mikutano, harusi na sherehe mbalimbali ndai ya maji na hii itakua ni Biashara kubwa kwetu na njia moja nzuri ya kulitumia vizuri eneo la bahari tulilo nalo” Amesisitiza Dkt. Kigwangalla.

Amesema ili kuitangaza hifadhi ya Taifa ya Saadani ni lazima kuiunganisha na utalii wa fukwe ili kuwavutia watalii wengi zaidi na kuongeza kuwa hifadhi hiyo kutokana na maeneo mazuri yaliyopo,sehemu za kulala na ukaribu wake na Bagamoyo na Dar es salaam.

Dkt. Kigwangalla amefafanua kuwa uanzishaji safari za boti za siku kutokea Dar es Salaam kwenda Bagamoyo na kurudi Dar es salaam utawawezesha watalii kwenda kati katika maeneo hayo kwa haraka na ni rahisi kuuza huduma hiyo kwa wageni watakaokuwa wanakwenda kufanya utalii mwisho wa wiki na kuiwezesha Serikali kupata faida ya kiuchumi kutokana na uwepo wa huduma hizo.

Nafasi 200 za Kazi Zilizotangazwa , Tazama Hapa | Deadline Mwezi Huu

$
0
0
Hapa nimekuwekea mkusanyiko wa Nafasi mbalimbali za Kazi Zilizotangazwa Wiki Iliyopita na Wiki Hii. Usisahau kushare na rafiki yako anayetafuta kazi
  1.  Job Opportunity​ at CRDB Bank | Senior Specialist; Financial Literacy
  2. Job Vacancy at CRDB Bank | Manager; Strategic Partnership
  3. New Government Job | Senior Corporate Communications Officer II at UCSAF
  4. Job Vacancy at Precision Air | Reservation & Ticketing Sales Agent
  5. Job Vacancy at Precision Air | Sales Manager Northern & Lake Zone
  6.  Job Vacancy at Standard Chartered Bank | Credit Analyst, Global Subsidiaries
  7. New Job Opportunity | Sales Capability Manager – Serengeti Breweries Limited
  8. New Job Opportunity | Marketing Manager, Spirits – Serengeti Breweries Limited 
  9. Nafasi 61 za Kazi Shirika la Hifadhi ya Taifa TANAPA | Elimu ni Kuanzia Cheti/Diploma/Degree | Mwisho Tarehe 30 Mwezi Huu 
  10. Jobs at UNICEF | Individual Consultant -Evaluation of the Zanzibar Social Protection Policy  
  11. Project Finance Assistant Job at Sightsavers Singida, Tanzania
  12. Project Assistant Job at Sightsavers Singida, Tanzania 
  13. Compliance Manager at IntraHealth International Mwanza, TZ 
  14. Research and Innovation Hub Coordinator Job at International Rescue CommitteeDar es Salaam, TZ 
  15. Electrical Manager Job at Radar Recruitment Tanzania 
  16. Job Opportunity at VodacomTanzania, Network Director 
  17. Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL) Team Lead – Tanzania PS3+ 
  18. Job Opportunity at Abt Associates, Communications Team Lead 
  19. Jobs in Tanzania 2019 : New Job Opportunities at Mom Easy Company Limited | Sales Officers (15 Post) 
  20. Job Opportunity at Bariadi District Council | Mtendaji wa Kijiji Daraja la III 
  21. Jobs in Tanzania 2019: New Job Vacancies at Oxfam Tanzania| Donor Contracts Coordinator (INT5881) 
  22. Jobs in Tanzania 2019: New Job Vacancies at Oxfam Tanzania| Warehouse Officer (INT5995) 
  23. Technical Manager Job at Mbeya Water Supply and sanitation Authority 
  24. Job Opportunity at PCI Tanzania ,Documentation Specialist 
  25. Job Opportunity at Pact Tanzania,Gender and Youth Officer 
  26. Job Opportunity at Pact Tanzania, Technical Services Coordinator-Case Management 
  27. Job Opportunity at Pact Tanzania, Technical Services Coordinator-Bi-Directional Referrals and Linkages 
  28. Job Opportunity at Pact Tanzania, Logistic Assistant/Driver 
  29. Field Assistant Grade Ii Job at Tropical Pesticides Research Institute TPRI 
  30. Job Opportunity at UONGOZI Institute, Research And Policy Department (Intern) 
  31. Job Opportunity at UONGOZI Institute, Finance And Administration Department (Intern)

==Kwa nafasi zingine za Kazi zaidi ya 5000, <<INGIA HAPA>.

Mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka 2019 Kuanza Kesho

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles  Msonde amesema jumla watahiniwa 485,866 wamesajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka 2019 kati yao wa shule ni 433, 052 na 52, 814 wa kujitegemea.

Dk Msonde ameeleza hayo leo Jumapili Novemba 3, 2019 wakati akizungumza kuhusu kuanza kwa mitihani hiyo kesho  katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema kati ya watahiniwa 433,052 waliosajiliwa wanaume ni 206,420 sawa na asilimia 47.67 na wanawake 226,632 sawa na asilimia 52.33 huku wanafunzi wenye mahitaji maalumu wakiwa 842.

Dk Msonde amesema maandalizi kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa mitihani, vijitabu vya kujibia na nyaraka zote za muhimu zinazohusu mchakato huo katika mikoa ya yote ya Tanzania Bara na Visiwani.

Wanawake wa jamii ya kibarbeig Babati kunufaika na utalii

$
0
0
Wanawake jamii ya Kibarbeig wilayani Babati, mkoa wa Manyara wanatarajiwa kuanza kunufaika zaidi na Utalii baada ya kuanzishwa vituo vya kuvutia watalii katika maeneo yao.

Afisa Maendeleo ya jamii ya Taasisi ya Chemchem association, Walter Palangyo amesema,Taasisi hiyo iliyowekeza shughuli za Utalii,katika hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Burunge, kupitia hoteli za Kitalii za Chemchem imejipanga kuboresha maisha ya jamii hiyo ili inufaike zaidi na Utalii.

Ofisa Utamaduni wa wilaya ya Babati, Beatrice Maliseli  akizungumza katika uzinduzi wa kituo hicho Leo Jumapili Novemba 3, 2019, aliwataka wanawake wa jamii hiyo kukitumia  vizuri kujiongezea kipato.

Amesema sasa watalii wataweza kuwatembelea na kununua vifaa vyao , kuona ngoma na tamaduni zao na hivyo kujiongezea fedha kwa ajili ya maisha yao.

Maliseli aliwataka wanawake na vijana wa jamii hiyo,kuongeza ubunifu wa vifaa vyao na kuanza kujifunza lugha za kigeni ili waweze kuwasiliana vizuri na watalii.

Jafo Atoa ONYO Kwa Wanasiasa Uchaguzi Serikali Za Mitaa

$
0
0
Waziri wa Tamisemi Suleiman Jafo amewataka wanasiasa kuacha kutoa kauli za  upotoshaji ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu.

“Niwaombe wana siasa kuacha kutoa kauli tata lengo ni moja kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu. Pia nivisihi vyama visicheze rafu huko maana kuna malalamiko mengine yanakuja upinzani kwa upinzani wanahujumiana,”-Jafo

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Novemba 3, 2019, Jafo amesema uchukuaji wa fomu umekwenda vizuri katika maeneo mengi na zilipotokea dosari aliagiza hatua zichukuliwe kwa haraka.

Kuhusu uwezekano wa kuongeza muda wa kuchukua na kurudisha fomu Jafo amesema hakuna mpango huo hivyo wagombea wote wakamilishe zoezi hilo ndani ya muda.

Haji Manara: Simba ni Klabu Bingwa ya taifa hili

$
0
0
Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, amefunguka mambo kadhaa kuhusiana na kikosi cha timu hiyo kuelekea mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbeya City leo;

 
Nyie ni Klabu Bingwa ya taifa hili,nyie ni timu bora kupita zote Afrika Mashariki na ya kati kwa sasa! Nyie ni Wachezaji mnaoishi comfortable kuliko wachezaji wengine wowote ktk ukanda huu wa Afrika!!

Na nyie ndio Timu maarufu kupita zote ktk Zone hii, na mmetajwa na CAF ni klabu ya kumi na Sita bora Afrika nzima!!


Nadhan mtakuwa mmeelewa Wanasimba wanahitaji nn jioni ya leo hapa Uhuru Stadium,hususan baada ya kupoteza Kwenye last game!!


No Excuse today zaidi ya ushindi, hamtaeleweka na mm mtaninifanya niiasi insta kwa muda bila sababu!!! Nipo huku Cairo nikiamini Mtatenda kitakachotendwa hapa ilipoishi Mitume mingi. 

Ratiba ya Michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo

Yanga Kuvaana Tena Leo na Pyramids FC

$
0
0
Wawakilishi wa Tanzania, Yanga SC, Leo Jumapili wapo dimba la Ugenini nchini Misri kukipiga na Pyramids FC katika mechi ya marudiano kufuzu hatua ya makundi kombe la Shirikisho Barani Africa.

Ikumbukwe kwamba katika mchezo wa kwanza uliopigwa kwenye dimba la CCM Kirumba, jijini Mwanza klabu ya Pyramids FC iliibuka na ushindi wa bao 2-1.

Mechi hiyo inatarajia kuanza saa tatu kamili ( 3:00) usiku.

Apps 20 Hatari Unazoshauriwa Kuziondoa Kwenye Simu Yako Haraka

$
0
0
Watumiaji wa Android wamepewa orodha ya apps za kuziondoa kwenye simu zao kwa sababu za kiusalama wa data na kuondoa matangazo yanayotokea sehemu zisizohusika kwenye simu zao.

Ushauri huo umetolewa na watafiti kutoka ESET ambao wamegundua app 42 kwenye soko la Google Play Store ambazo zimekuwa zinakuja na mfumo wa kimatangazo usio rasmi – adware. Mfumo huo una sababisha betri ya simu kuisha haraka, utumiaji wa data – intaneti na ata kuchukua taarifa zako binafsi kwenye simu.

Baada ya utafiti wa ESET kuweka wazi Google waliondoa apps hizo kwenye soko lao la Apps, ila inakuitaji wewe kuziondoa mwenyewe. Pia kuzifahamu ni muhimu kwa watu ambao wanatumia masoko mengine ya apps nje ya soko la Google Play Store. Apps hizo zimepakuliwa zaidi ya mara milioni 8.

Apps hizo zinauwezo wa kuonesha matangazo ata kama simu imefungwa (locked) kitu ambacho huwa kinapigwa na Google, kwani kufanya hivyo kuna sababisha utumiaji mkubwa wa betri na nje ya makubaliano yao na watengenezaji wa apps.

Apps hizo ni: Smart Gallery, SaveInsta, Mini lite for Facebook, Free Radio FM Online, Free Video Downloader, Free social video downloader, File Downloader, Water Drink Reminder, Smart Notes for You, DU Recorder, Tank classic, Heroes Jump, Solucionario, Ringtone Maker, Video downloader, Ringtone Maker Pro, Basketball Perfect Shot, HikeTop+, MP4 video downloader, Flat Music Player, Free Top Video Downloader.

Pitia orodha vizuri  hapo chini na kama kuna app bado unaitumia unashauriwa kuiondoa.

==>>Apps za kuziondoa  <<Hapa>>

Ufadhili wa Kusoma Nje ya Nchi | Scholarships for Tanzanian Students

$
0
0
📚 FURSA ZA UFADHILI  WA KUSOMA NJE YA NCHI

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

    🎓Tanzanian Scholarships

Kama wewe ni Mtanzania mwenye Ndoto ya Kusoma nje ya Nchi lakini hukuwa na uwezo, basi hii ni Nafasi yako. Kuna Nafasi Nyingi sana za Ufadhili zimetangazwa (Scholarships)

*📌 PHD
*📌 MASTERS
*📌 UNDERGRADUATE

 

ZIKO WAPI😳😳
✈(1)Zipo za Hong Kong
🛩(2) Marekani
✈(3)Uingereza
🛫(4)Canada

 Zote Hizo ni Full Funded( Unalipiwa kila Kitu) Japo kuna zingine utachangia kidogo
. _______________________
Bado hujachelewa, Deadline ni kuanzia Mwezi huu wa kumi mwishoni hadi Mwakani-2020
._______________________ 

Bofya hapo chini kujua zaidi
👇👇👇👇👇👇👇👇


http://ajirazote.com/scholarship/
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images