Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Idris Sultan Aripoti Tena Polisi

$
0
0
Msanii wa vichekesho, Idris Sultan leo Ijumaa Novemba 1, 2019 saa 2 asubuhi ameripoti Kituo cha Polisi ‘Central’ jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya masharti ya dhamana aliyopatiwa jana October 31, 2019.

Idriss alitakiwa kwenda polisi baada ya kuweka picha yenye sura yake huku akiwa ameketi katika kiti chenye nembo ya Taifa na kuambiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuripoti kituo chochote cha Polisi.

Ahukumiwa Kifungo Cha Maisha Jela Kwa Kumbaka na Kumpa Mimba Mtoto wake wa Kumzaa

$
0
0
Mahakama ya  Wilaya ya  Mpanda  Mkoani  Katavi  imemuhukumu  Lazaro  Charles (35)  Mkazi    wa Mtaa wa  Mji   Mwema katika  Manispaa ya   Mpanda Mkoa wa  Katavi kutumikia jela kifungo cha maisha baada ya kupatikana na hatia ya kumpa mimba mtoto wake wa kumzaa  mwenye (14) ambaye ni, mwanafunzi wa  darasa la  saba shule ya msingi  Majengo Manispaa ya  Mpanda.

Hukumu  hiyo iliyovuta hisia za wakazi  wengi  wa  Manispaa ya Mpanda, ilitolewa na Hakimu Mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Gosper Luoga baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa Mahakamani na upande wa mashtaka.

Awali katika kesi hiyo Mwanasheria wa Serikali Gregory  Muhangwa aliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo kwa nyakati tofauti hapo Januari 1 mwaka 2017 na April 29, 2019.

Mshtakiwa huyo alikuwa akitenda kosa hilo huko nyumbani kwake wakati mke wake ambaye ni mama  mzazi wa mtoto huyo alipokuwa amesafiri ndipo alipokuwa akiingia kwenye chumba alichokuwa akilala mtoto wake huyo na kumbaka kwa nguvu.

Mwendesha mashtaka huyo alieleza kuwa baada ya kuwa anambaka  alikuwa akimwekea majani kwenye sehemu zake za siri kama dawa ya kienyeji  ya  kumwondolea maumivu.

Hakimu Luoga amemtaka mshtakiwa kama atakuwa na sababu yoyote ile ya msingi ambayo inaweza kuifanya mahakama iweze kushawishika ili kumpunguzia adhabu basi inatoa nafasi kujijitetea.

Lazaro Charles ameiomba mahakama  impatie nakala ya hukumu ya mwenendo wa kesi hiyo tu kwani hana utetezi wowote ule.

Baada ya ombi hilo la mshtakiwa mwanasheria wa Serikali Gregory Muhangwa aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa wazazi wengine wenye tabia kama hiyo.

Hakimu Luoga baada ya kusikiliza pande hizo mbili alisoma hukumu na kuiambia Mahakama kuwa mshtakiwa amepatikana na kosa la kifungu cha sheria Namba 158 (1) (a ) SURA YA 16 ya marejeo 2002, hivyo Mahakama inamuhukumu kutumikia kifungo cha maisha jela kuanzia leo Novemba 1, 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro asimamia Zoezi la wanafunzi Watoro kuchapwa viboko mbele ya wazazi wao

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro jana Alhamisi  alisimamia zoezi la  kucharazwa viboko wanafunzi 3 ambao ni watoro sugu katika Shule ya Msingi Ligoma iliyoko wilayani humo ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kupambana na utoro sugu, nidhamu za wanafunzi na mimba za utotoni Tunduru.

Mkuu huyo wa wilaya  alimtaka mwalimu Mkuu wa shule hiyo kuwachapa viboko vinne wanafunzi hao na kuagiza  wapewe adhabu nyingine zisizohusiana na viboko, ikiwa ni pamoja na kuchimba visiki.

Baada ya viboko hivyo, aliwauliza wanafunzi hao lini wataanza kwenda shule na mmoja alijibu kuwa ataripoti Jumatatu,hata hivyo, mkuu huyo wa Wilaya alisema wote wanapaswa kuripoti leo.

Kundi la IS latangaza kiongozi mpya Atakayemrithi Abu Bakr al-Baghdadi

$
0
0
Kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS limemtangaza kiongozi wake mpya baada ya kuthibitisha kifo cha kiongozi wake Abu Bakr al-Baghdadi katika shambulizi lililofanywa na Marekani nchini Syria. 

Taarifa iliyotolewa kwenye chombo cha habari cha IS, al-Furqan imeeleza kuwa nafasi ya al-Baghdadi itazibwa na Abu Ibrahim al-Hashimi al-Qurayshi. 

Kundi la IS halikutoa taarifa zaidi kuhusu al-Qurayshi. Kiongozi huyo mpya anatambuliwa kama msomi, shujaa mashuhuri na kiongozi wa kivita ambaye amepambana na majeshi ya Marekani na ana ufahamu kuhusu vita hivyo. 

Taarifa hiyo pia imethibitisha kifo cha Abu Hassan al-Muhajir, msaidizi wa karibu wa al-Baghdadi ambaye alikuwa pia msemaji wa IS tangu mwaka 2016.

 Vifo hivyo ni pigo kubwa kwa kundi la Dola la Kiislamu karibu miezi saba tangu lilipofurumushwa kutoka kwenye ngome yake ya mwisho nchini Syria.

Serikali Yawatoa Hofu Wananchi Wa Handeni Mkoani Tanga

$
0
0
Serikali imewahakikishia wakazi wa Handeni, Mkoani Tanga uendelevu wa huduma ya maji licha ya kuharibika kwa miundombinu ya maji kulikosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga ametoa kauli hiyo hapo juzi wilayani hapa wakati wa ziara yake iliyolenga kukagua athari ya mvua kwenye miundombinu ya maji sambamba na kupata ufumbuzi wa haraka kufuatia hali ya mvua zilizonyesha kwa takribani wiki mbili mfululizo.

Mara baada ya kujionea hali halisi, Mhandisi Sanga aliwatoa hofu wananchi wa Handeni ambapo aliwataka kuwa watulivu na aliahidi kuwa Serikali itahakikisha huduma ya maji inarejea haraka iwezekanavyo.

"Ninawasihi wananchi kufanya subira na kuwa watulivu na kuzingatia maelekezo ya Serikali," alisisitiza Naibu Katibu Mkuu Sanga.

Mhandisi Sanga alibainisha kuwa zoezi la tathmini ya athari ya mvua hizo kwenye miundombinu ya maji wanaloendelea nalo halitochukua zaidi ya siku tatu kama ilivyoagizwa na Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa.

"Waziri wa Maji ametuagiza kuharakisha kukamilisha zoezi hili, nasi tutahakikisha linafanyika kwa kasi ikiwa ni pamoja na kutazama njia mbadala ili wananchi wapate huduma ya maji kwa haraka," alisema Mhandisi Sanga.

Aliongeza kuwa Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli haipo tayari kuona wananchi wake wanataabika na kwamba hatua madhubuti na za haraka zinachukuliwa ili kuhakikisha wananchi wanapata maji.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela akielezea kwa ujumla athari za mvua hizo kwenye Mkoa wa Tanga, alisema kuwa zimeleta madhara kwenye miundombinu ya barabara na madaraja na kusababisha huduma ya usafiri katika maeneo mbalimbali kuathirika.

“Tulichokibaini katika mvua hizi zilizonyesha ni kuwa zimeharibu mabwawa ya maji na kusababisha maji yaliyotoka katika mabwawa hayo kuathiri miundondombinu mbalimbali ikiwemo ya maji na barabara,” alieleza Shigela.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe akielezea athari za mvua hizo alisema ni pamoja na kuharibika kwa mabwawa 11 ya maji yanayotumiwa na wakazi wa Handeni na maeneo jirani na kati ya hayo yapo mabwawa makubwa matano ambayo aliyataja kuwa ni Kwenkambara, Mandera, Suwa, Msomera na Mkomba.

Aidha, Gondwe alipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna inavyotekeleza majukumu yake kwa wakati na kwa hatua mbalimbali za haraka zinazoendelea kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kurejesha mawasiliano ya miundombinu ya barabara na maji iliyoathirika.

Sambamba na hilo, Gondwe alimpongeza Mhandisi Sanga na timu ya wataalam aliyoambatana nayo kutoka Wizara ya Maji na taasisi zake kwa kufika Wilayani hapa mapema ili kufanya tathmini ya uharibifu wa miundombinu ya mabwawa ya maji ili kupata ufumbuzi.

“Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Handeni tunatoa shukrani nyingi sana kwa Mheshimiwa Rais kwa kutujali na kuwatuma watendaji wa Serikali kufika hapa Handeni ili kutatua matatizo yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha,” alisema Gondwe.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA), Mhandisi Clement Kivegalo ambaye ameambatana na Naibu Katibu Mkuu Sanga alisema kuwa wanaendelea na tathmini ila kwa mabwawa yaliyopasuka wamebaini yalijengwa chini ya kiwango na pia hayakuwa yakitunzwa inavyostahili na hivyo kupelekea kuharibika wakati mvua hizo zilizonyesha.

Kijana Aliyemtishia Mwenzake Kwa Bastola Yamkuta Mazito....IGP Amtaka Ajisalimishe Polisi

$
0
0
Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amemtaka kijana aliyemtishia mwenzake bastola kuripoti polisi baada ya kuonekana akifanya kitendo hicho katika picha za video zinazosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii nchini.

Mbali na kuripoti, Sirro amesema anatakiwa kusalimisha silaha yake.

Ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Utatu inayolenga kukomesha rushwa barabarani.

Sirro amesema ameagiza kukamatwa kwa kijana huyo lakini amekuwa akipiga chenga,  amemtaka akajisalimishe mwenyewe kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani.

Raia Magufuli aagiza Wizara ya Fedha kutoa shilingi Bilioni 40 kulipa madeni ya korosho yaliyobaki.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza Wizara ya Fedha na Mipango kutoa shilingi Bilioni 40 kwa ajili ya kumalizia madeni yote ya wakulima wa korosho yaliyobaki baada ya Serikali kununua korosho za wakulima katika msimu wa mwaka 2018/19.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo Ikulu Jijini DSM alipokutana na viongozi wa Wizara, Mikoa, Wilaya na Taasisi za Serikali ambazo zinahusika katika uzalishaji na mauzo ya zao la Korosho.

Mkutano huo umehudhuriwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa.

Pamoja na kuagiza Wizara ya Fedha na Mipango itoe fedha hizo kesho tarehe 02 Novemba, 2019 Rais Magufuli amewaagiza viongozi wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha fedha hizo zinawafikia wakulima na sio vinginevyo, na pia kuhakikisha wanalipwa wakulima wanaostahili kupata malipo hayo.

Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa kwake na utendaji kazi wa Wizara ya Kilimo na viongozi wa Mikoa na Wilaya ambao katika maeneo yao kumetokea wizi mkubwa wa fedha za wakulima kupitia vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) hali iliyosababisha wakulima wengi kuishi maisha duni.

Rais Magufuli amesema amesikitishwa kuona viongozi wa Wizara, Mikoa na Wilaya hawajachukua hatua madhubuti dhidi ya watu wanaowaibia wakulima mpaka alipoamua kumtuma Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Brig. Jenerali John Mbungo ambaye kwa muda mfupi amebaini kuwepo wizi wa shilingi Bilioni 1.23 na tayari amefanikisha kurejeshwa kwa shilingi Bilioni 375 katika Mkoa wa Lindi pekee.

Amewataka viongozi wa Wizara ya Kilimo, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kubadilika na kuhakikisha haki za wakulima zinalindwa ipasavyo kwa kurejesha fedha zilizoibwa na kuzuia mianya yote ya wizi.

“Nataka mfanye kazi, hakuna mtu wa kuwanyanyasa, nendeni mkashughulikie kero za wakulima, mna vyombo vya ulinzi na usalama nendeni mkavisimamie, kinyume na hapo nitakuona hutoshi kwenye nafasi hiyo” Rais Magufuli.

Polisi waua majambazi 4 Kagera

$
0
0
Watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, wamefariki Dunia wakati wakijibizana risasi na Jeshi la Polisi katika eneo la Pori la Ngazi Saba, lililoko wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

Kwa mujibu wa Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Liberatus Sabas, amesema tukio hilo limetokea wakati Polisi wakiwa katika Doria yao ya kawaida, ambapo waliona kundi la watu wakitokea katika pori hilo na kuwaamuru kujisalimisha.

Kamanda Sabas amesema badala ya kutii amri, watu hao waliwarushia Polisi risasi na polisi walipojibu walifanikiwa kuwapiga risasi na kupelekea vifo hivyo.

Kamishna huyo amesema kuwa Polisi kwa sasa wanaendesha operesheni maalum katika Mikoa ya Geita, Kigoma na Kagera, kufuatia mikoa hiyo kuwa na matukio mengi ya unyang’anyi wa kutumia silaha.

Waziri Mkuu Aagiza Mkurugenzi Mtwara Achukuliwe Hatua....Ni Baada Ya Kumtoza Mwekezaji Sh. Milioni 31 Za Kuendesha Vikao

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mtu yoyote anayekwaza wawekezaji nchini atachukuliwa hatua kali, hivyo amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwaamchukulie hatua Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtwara, Bw. Maisha Selemani Mtipa baada ya kumtaka mwekezaji alipe sh. milioni 31.6 kwa ajili ya gharama za vikao ili aweze kupatiwa eneo.

Ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Novemba 01, 2019), wakati akifungua Kongamano la Uwekezaji na Maonesho ya Biashara mkoa wa Mtwara lililofanyika kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Mtwara. “Yoyote anayekwaza uwekezaji nchini kwa kuwasumbua wawekezaji tutamshughulikia kabla ya kuwasumbua wawekezaji.”

Amesema Bw. Mtipa amemwandikia barua mwekezaji wa kampuni ya MBR Internation Company Limited akimtaka alipe sh. milioni 31.6 kwa ajili y a kulipa kamati mbalimbali zikiwemo sh. milioni 1.95 kwa kamati ya Menejimenti ya Halmashauri.

Waziri Mkuu amesema “fedha nyingine sh. milioni 2.27 kwa kamati ya kugawa ardhi ya wilaya, sh. milioni 4.43 kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango sh. milioni 5.14 na sh milioni 17.79 Baraza la madiwani ili wagawane tu, huu ni utaratibu wa wapi? huku ni kufukuza na kukwaza wawekezaji.”

Waziri Mkuu amesema Serikali imeshaondoa tozo zaidi ya 150 zilizokuwa zinakwaza wawekezaji kupata uwekezaji katika maeneo mbalimbali nchini, hivyo haitaki kusikia mahali popote panawekwa tozo zenye kuwakwaza wawekezaji. Amesema hatua zitakazochukuliwa kwa Bw. Mtipa ziwe fundisho kwa halmashauri zote nchini.

Mapema, Waziri Mkuu alizungumzia uuzwaji wa korosho na kuagiza kwamba mfumo uliotumika katika mnada wa kwanza wa uuzwaji wa zao la korosho uliofanyika jana (Alhamisi, Oktoba 31, 2019) ndio unaopaswa kuendelea, hivyo ameagiza wahusika wausimamie vizuri ili usiingie dosari.

Alisema Serikali ilibaini changamoto katika uuzwaji wa mazao mengine ya pamba na kahawa ya uwepo wa watu ambao wananunua mazao nje ya mfumo kama kangomba, hivyo ni muhimu wakadhibitiwa ili fedha zote ziende kwa wakulima.

Pia Waziri Mkuu aliagiza maandalizi yawe yanakwenda pamoja na msimu kama suala la magunia wasiachiwe watu wa ushirika pekee bali Wakuu wa Mikoa na Wilaya nao washiriki katika kutatua tatizo hilo ili minada ifanyike kikamilifu.

Pia chama kikuu cha ushirika pamoja na vyama vya msingi wazuie kuwepo kwa makato ya hovyo ambayo yalishaondolewa na Serikali ili kuhakikisha mkulima haumizwi kwa kupunguzwa kwa malipo yake.

Amewataka viongozi hao wasimamie mtiririko wa fedha kutoka kwa wafanyabiashara kwenda kwa mkulima na wahakikishe zinaingizwa katika akaunti za wakulima. Pia sheria ya ununuzi isimamiwe baada ya mnunuzi kupewa zabuni anatakiwa alipe ndani ya siku nne. “Sheria hii itaondoa watu wa kati na kumwezesha mkulima kulipwa fedha zake kwa wakati.”

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa amesema amesema wanunuzi wote wametakiwa wahakikishe wakulima wanalipwa kwa wakati. “Bei ya chini katika mnada wa korosho uliofanyika Mtwara ilikuwa sh. 2,409 na bei ya juu ilikuwa 2,559 na hali inaonesha uhitaji wa korosho duniani ni mkubwa kutokana na ubora wake.”

Amesema chama cha ushirika cha TANECU waliingiza sokoni tani 13,000 huku mahitaji yakiwa ni tani 40,000 na chama cha ushirika cha MAMCU walipelela sokoni tani 7,000 na mahitaji yalikuwa tani 22,000 hivyo wafanyabiashara wengi jana walikosa korosho.

Akizungumziakuhusu kilimo cha zao la korosho, Waziri Mkuu ametoa rai kwa viongozi wa mkoa wa Mtwara kuwa wasibweteke kwani mikoa mingine nayo imeanza kulima korosho, hivyo waweke mikakati mizuri ili zao la korosho liendelee kuwa zao kuu la biashara kwa mkoa.

Amesema Serikali kwa upande wake, itaendelea kuweka mazingira rafiki na miundombinu wezeshi kwa ajili ya kuvutia wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza mkoani Mtwara.

“Tusisahau kuwaMkoa wa Mtwara ni korosho na korosho ndiyo mkoa. Hili linadhihirishwa na usemi wa wenyeji kuwa korosho ni dhahabu ya kijani. Mtwara ndiyo mzalishaji mkubwa wa korosho Tanzania, huzalisha zaidi ya asilimia 65 ya korosho zote nchini.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwaasa wawekezaji wote kwamba waondoe hofu kuhusu kuwekeza Mtwara kwa sababu mkoa wa Mtwara wa sasa ni tofauti na Mtwara ile waliyokuwa wanaisikia zamani, uchumi wake unakuwa.

Waziri Mkuu amesema ushiriki wao kwenye kongamano hilo unaonesha utayari walionao katika kuiunga mkono Serikali kwa lengo la kuwaletea maendeleo na kujenga Tanzania ya Uchumi wa Viwanda ambayo wote wanaitamani.

Kongamano hili na mengine yaliyofanyika kwenye mikoa mbalimbali ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu alilolitoa wakati anafungua Kongamano la tatu la uwezeshaji wananchi kiuchumi jijini Dodoma Juni 18, 2018, ambapo aliagiza mikoa yote kuandaa Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa.

“Niendelee kusisitiza tena kwa mikoa ambayo bado haijatekeleza agizo hili la kuandaa Mwongozo wa Uwekezaji ifanye hivyo mapema.”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema licha ya Serikali kuwekeza kwa kiwango kikubwa kwenye miradi ya kijamii katika Mkoa wa Mtwara, pia imewekeza kwenye miradi mikubwa ya kimkakati ambayo inachochea kukua kwa uchumi kwa haraka.

Waziri Mkuu ameitaja miradi hiyo ni pamoja na upanuzi wa uwanja wa ndege na bandari ya Mtwara; ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mtwara hadi Nanyumbu mpakani na Msumbiji; ufufuaji na ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho.

Miradi mingine ni ujenzi wa reli kutoka Mtwara hadi Songea kwa ajili ya kusafirisha makaa ya mawe kutoka Mchuchuma na chuma kutoka Liganga na kuongeza uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia na vyanzo vingine.

Ufunguzi huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi - Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Angellah Kairuki, Waziri wa Kilimo Josephat Hasunga, Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa,Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme na watendaji wengine wa Serikali.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa 18 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika, Nordic

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na Nordic (Norway, Denmark, Finland, Sweden na Iceland) unaotarajiwa kufanyika tarehe 08 Novemba 2019 kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 


Akiongea na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe alisema kuwa mkutano huu utafunguliwa rasmi na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ambapo hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huu mkubwa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000.  


Kwa mujibu wa Dkt. Mnyepe, mkutano huu utajumuisha jumla ya mawaziri 34 wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Nordic pamoja na washiriki wengine ambao idadi yao inatarajiwa kufikia 250. Mawaziri watakaokuja kutoka nchi za Nordic ni wa nchi za Sweden, Norway, Denmark, Finland na Iceland. Kutoka nchi za Afrika watakuja Mawaziri wa Algeria, Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Burundi, Comoros na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC). 


Nyingine ni pamoja na Misri, Ethiopia, Ghana, Kenya, Lesotho, Mali, Malawi, Morocco, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Niger, Rwanda, Senegal, Somalia, Afrika Kusini, Tunisia, Uganda, Zambia, Zimbabwe na sisi wenyeji Tanzania. Aidha, mkutano huo utajumuisha Mawaziri, Mabalozi wa nchi shiriki za Afrika katika nchi za Nordic, Mabalozi wa nchi za Nordic hapa nchini pamoja na watendaji wa Serikali. Kauli mbiu ya mkutano huu ni: "Ushirikiano kwa Maendeleo Endelevu" 


"Mkutano huu unafanyika hapa Tanzania kutokana na ushirikiano kati ya Tanzania na nchi za Nordic ni wa kihistoria na wa kipekee. Ushirikiano huu ulianza hata kabla ya uhuru wa Tanganyika ambapo Wamisionari kutoka nchi hizo walikuja kufanya kazi hapa nchini kwenye sekta za afya na elimu. Katika sekta ya elimu, nchi hizo zilianzisha Kituo cha Kilimo cha Uyole na Kituo cha Elimu cha Kibaha kupitia Mradi wa Nordic-Tanganyika Project. Ushirikiano wa karibu kati ya Tanzania na nchi za Nordic ulichangiwa kwa kiwango kikubwa na falsafa zilizokuwa zinafanana kuhusu maendeleo ya watu, ukombozi wa Afrika, urafiki miongoni mwa viongozi wetu na nafasi ya kimkakati ya Tanzania katika Bara la Afrika," alisema Dkt. Mnyepe 


Katibu Mkuu aliongeza kuwa, "katika nchi za Afrika, Tanzania inapokea misaada mingi kutoka nchi za Nordic kuliko nchi nyingine yoyote. Kwa mfano kwa miaka mitano ya kuanzia mwaka 2013 hadi 2018, Tanzania imepokea takribani Shilingi za Kitanzania bilioni 900 kutoka nchi za Nordic. Nchi hizo zimekuwa zikisaidia sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo: elimu; afya; miundombinu; nishati; TEHAMA; utafiti; ukusanyaji wa kodi; bajeti; misitu; usawa wa jinsia; utunzaji wa mazingira; na ukuzaji wa sekta ya biashara,". 

"Kufuatia ushirikiano huu wa kihistoria kati ya Tanzania na nchi za Nordic, nchi hizo ziliiomba Serikali ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa mwaka huu kutokana na mahusiano na mazuri yaliyopo na hatua za kasi za kimaendeleo zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Kutokana na urafiki na historia hiyo hiyo Serikali ya Tanzania ilikubali kuwa mwenyeji wa mkutano wa mkutano huo na utafunguliwa na Mheshimiwa Rais. Kauli mbiu ya mkutano wa mwaka huu ni, Ushirikiano kwa Maendeleo Endelevu," aliongeza Katibu Mkuu  


Aidha, mkutano huu, utajadili fursa za uwekezaji, biashara, amani na usalama na masuala mengine mtambuka, kama vile athari za mabadiliko ya tabianchi. Katika mkutano huu, tutazungumzia pia mahusiano baina yetu na nchi moja moja hususan ubia wa kimaendeleo. Kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Tano, wenzetu wa Afrika na Nordic watapenda pia kusikia uzoefu na mafanikio ya Tanzania kwenye sekta za afya, elimu, nishati, miundombinu, kilimo, utalii, ukusanyaji wa kodi, mafanikio ya vita dhidi ya rushwa, ujangili, madawa ya kulevya na maeneo mengine.  


Kwa upande wake Balozi wa Norway nchini Tanzania, Balozi Elisabeth Jacobsen alisema kuwa mkutano huu utatoa pia fursa ya mazungumzo ya uwili (bilateral meetings) kati ya nchi za Nordic na nchi za Afrika. 

"Ni imani yangu kuwa kupitia mkutano huu tutaweza kujadilili mambo mbalimbali ikiwemo hatua za kimaendeleo zilizofikiwa katika sekta mbalimbali hususan afya, huduma za kijamii, elimu na mazingira kibiashara na uwekezaji kwani Tanzania imekuwa na mahusiano mazuri na nchi mbalimbali duniani zikiwemo za Nordic," alisema Balozi Elisabeth.   

Nae Balozi wa Sweden nchini, Balozi Anders Sjoberg alisema kuwa mkutano wa kwanza ulifanyika nchini Sweden mwaka 2001 ambapo baada ya hapo mikutano kama hii ilikuwa inafanyika kwa kupokezana kutoka Bara la Afrika na nchi za Nordic.  

"Kwanza kabisa niipongeza Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huu wa Mawaziri wa Mambo ya Nje, ni fursa kutumia mkutano huu kujadili masuala ya kibiashara, uwekezaji, amani na usalama kwa maslahi ya nchi za Afrika na Nordic," alisema Balozi Sjoberg. 
 

Mkuchika: Kila Mtanzania Ana Jukumu La Kupambana Na Rushwa

$
0
0
Na. Mwandishi Wetu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utwala Bora, Kapteni, George Mkuchika amewataka wananchi kuiunga mkono Serikali katika kupambana na Rushwa ili kupunguza ajali za barabarani pamoja na kuwezesha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Akizungumza katika uzinduzi wa Kampeni ya kuzuai rushwa barabarani Waziri Mkuchika amasema kuwa katika kampeni hiyo ijulikanayo kama “Utatu inayohusisha Taasisi ya kuzuia na Kupambana  na Rushwa Takukuru, Jeshi la Polisi na Wananchi inawezekana na itasaidia katika kutoa taarifa za rushwa zishughulikiwe kwa haraka ili kupunguza ajali barabarani.

“ Nyote mtakubaliana na mimi kuwa jukumu la kupambana na rushwa lilikasimiwa kwa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru, ili kukabiliana na vitendo vya Rushwa vinavypatikana katika maeneo yetu,kila mmoja wetu anapaswa kubeba jukumu la kupambana kama kampeni hii inavyoeleza”, alisema Waziri Mkuchika.

Alisema kuwa mara nyingi vitendo vya rushwa vinafanyika pale ambapo watu wanafanya kazi, wanafanya biashara, wanapata huduma na kwenye makazi kwa hiyo inawezekana kwa kila mtu kuchukua jukumu la kuzuia rushwa kwa sababu inatokea kwenye maeneo ambayo wananchi wanahusika,wanaisikia na kuona vitendo hivyo katika mazingira tofauti.

Waziri Mkuchika alieleza kuwa iwapo kila mtanzania atachukua dhamira ya dhati ya kuiunga mkono Serikali katika mapambano hayo, ajali za barabarani zitapungua, kwani mpaka sasa takwimu za mwaka 2018/2019 zinaonesha kuwa ajali za barabara zimepungua kwa kushirikisha wadau, Polisi na Taasisi ya kupambana na rushwa Takukuru.

Aidha Waziri Mkuchika amezindua Mfumo wa kitekenolojia unaoitwaTakukuru App unaopatikana kwenye simu ambao utatumika kuripoti vitendo vya Rushwa katika maeneo mbalimbali nchini.

“Mfumo huu ni mzuri kwani unamuwezesha mwananchi kukusanya taarifa na matukio ya vitendo vya rushwa kwa kutumia simu ya Mkononi na kuwasilisha kwa takukuru au jeshi la Polisi  ambapo zitafanyiwa kazi na mtuhumiwa kufikishwa sehemu husika”, Alisema Waziri Mkuchika.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro amesema kuwa Serikali inatakeleza jukumu kubwa la kuleta usawa wa haki kwa wananchi nchini kwa kupambana na rushwa ikiwemo ufisadi ili kuleta maendeleo kwa wananchi, kwa hiyo Jeshi la Polisi linaunga mkono jukumu hilo ambalo linafanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.

“ Mchakato wa kampeni hii ni sehemu ya matakwa ya kihistoria na kitaasisi katika jitihada za kupambana na rushwa nchini iliyoanzishwa chini ya sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa kifungu namba 11 ya mwaka 20007, sheria hii ilitungwa baada ya kufutwa kwa sheria ya kuzuia rushwa ya Takukuru sura 329 ambayo ilifanyiwa marejeo mwaka 2002, kwa hiyo katika kutekeleza majuku haya kampeni hii ambayo mchakato wake ulianza Novemba, 2017 leo inazinduliwa itasaidia sana kupunguza ajali barabarani”, Alisema IGP. Sirro.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi November 2

Wabadhilifu, Wezi wa Dawa za Serikali Wapewa ONYO Tena

$
0
0
Na. Atley Kuni- TAMISEMI
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dkt. Dorothy Gwajima, ameapa kwamba moto dhidi ya wabadhilifu wa dawa aliouwasha katika zoezi la ufuatiliaji hautazimika wala kupoa, huku akiwaomba wananchi kutoa ushirikiano wa karibu kwa kuwafichua watu/mtu yeyote atakayebainika kuhujumu jitihada za serikali.

Gwajima ametoa kauli hiyo ikiwa ni mara ya pili kurudia wito huo mbele ya Makatibu Tawala wa Mikoa, wataalamu Wafamasia kutoka mikoa 13 na wadau wa maendeleo Global Supply chain, waliokutana mjini Dodoma kwenye ukumbi wa Mikutano wa OR-TAMISEMI katika kikao kazi cha tathmini ya mbinu mpya ya kuimarisha takwimu za bidhaa za afya.

Akizungumza katika kikao hicho Gwajima amesema, vita hiyo wataweza kuishinda kwa kuunganisha nguvu na wananchi kutoka maeneo yote nchini.

“Niwaombe wanachi kuwa mstari wa mbele kufichua wale wote mtakaowabaini wanahujumu suala la dawa kwani vita hiyo siyo ya mtu mmoja mmoja wala serikali peke yake bali ni ya jamii nzima” alisema Gwajima na kuongeza kuwa, “wapo watu wanaotambua nani ni adui wao katika vita hivi ndiyo maana jana nimeona kwenye Jamiiforum wakinipa pole na kunipongeza, lakini nasema lazima tutembee na wananchi katika hili.” alisisitiza kiongozi huyo.

Gwajima alisema inashangaza unafika kwenye kituo ambacho kina wafamasia wasiopungua sita (6) lakini unakuta kitabu cha kupokelea dawa (ledger) hakijahuishwa kwa zaidi ya miezi 5, hii ni hali ya hatari sana, suala hilo halivumiki na wala hawezi kukubaliana nalo.

“Viongozi wangu Makatibu Tawala, mnaelewa tunatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015-2020, hivyo fuatilieni hili hadi kwenye stoo za kutunzia dawa lakini pia ombeni taarifa na ingieni kwenye mikutano yao muone kile wanachokijadili maana humo hakuna zuio lolote kwa kuwa taarifa zinazojadiliwa humo sio siri za mgonjwa, sasa wasije wakajifichia kwenye mwamvuli wa taarifa za kitabibu kwa kuwahadaa eti siri za Mgonjwa?” Alihoji na alikemea  

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Global Supply Chain Tukay Mavere aliwataka wachumi, watawala wa fedha pamoja na watumiaji wa mfumo wa eLMIS kukaa pamoja na kuja na mbinu mbadala za kudhibiti hali ya dawa na upatikanaji wake na kutoa mrejesho wa kile ambacho serikali imewekeza.

“Lengo la mfumo huu tunataka tuwe tunachukua jambo, tunalichakata na kisha tunalitolea majibu kwa wakati sio kungoja muda uende, aidha hii inakuwa ni zoezi endelevu katika utendaji wa siku kwa siku kama mfumo ulivyo, hivyo tumeitana ili tuwe na uwelewa wa pamoja juu ya hili tunalokusudia kulifanikisha” alisema Mavere.

Kwa upande wao washiriki wa warsha hiyo wameipongeza serikali na wadau kuja na mfumo huo, kwani ni matumaini yao utakuwa suluhu ya yale wanayofanyia kazi kila siku.

“Kama Naibu Katibu Mkuu alivyosema, mfumo huu utasaidia kuondoa ziada ya dawa inayosababisha upotevu wa pesa kutokana na kuchina kwa Bidhaa zilizoingizwa bila takwimu sahihi, vema sasa kila mmoja wetu akitoka hapa awe mstari wa mbele katika kuutumia mfumo kwenye utendaji wake.” alisema, Msalika Makungu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora.

Katika kikao hicho cha siku mbili pamoja na mambo mengine yatakayojitokeza, wataalam watajifunza kupata takwimu sahihi kwa ajili ya kufanyia maoteo kwa kuwa mfumo unaanzia chini kwenye huduma kwenda juu, hivyo itakuwa ni fursa ya kuwajengea uwezo timu za uratibu wa afya za Mikoa na Wilaya, kupata taarifa sahihi na kufanya ugawaji wa dawa kulingana na mahitaji na kuondokana na tatizo la dawa kwenye maeneo yenye dawa nyingi.

Mambo mengine ni kufanya bajeti kulingana na rasilimali zilizopo lakini pia kuwezesha kufanya usimamizi kwa njia ya mtandao Online Supervision.

Katika kikao hicho, Wataalamu hao walikumbushwa juu ya viapo vyao kwa kuongozwa na kiapo mbele ya Naibu Katibu Mkuu huku wakiwa wamenyoosha mikono juu na kuapa kwamba, watakuwa chachu ya mapambano dhidi ya ubadhilifu wa dawa na endapo wakishindwa basi wawe tayari kuachia nyadhifa zao hata kwa kutuma ujumbe wa maandishi kwenye mtandao wa kundi sogozi (WhatsApp) kuhusu  kuachia madaraka waliyonayo.

Ofisi Ya Makamu Wa Rais Kwa Kushirikiana Na Wizara Ya Viwanda Na Biashara Yakutana Na Wazalishaji, Wasambazaji Na Wauzaji Wa Mifuko Mbadala Wa Plastiki.

$
0
0
Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara imeandaa kikao kilichowakutanisha Wazalishaji, Wauzaji na Wasambazaji wa mifuko mbadala wa plastiki. 

Kikao hiko kimefanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Kmbarage Nyerere (JNICC) jijini Dar Es Salaama Lengo la Kikao hiko ni kusikiliza hoja na changamoto mbalimbali kutoka kwa Wazalishaji, Wauzaji na Wasambazaji wa mifuko hiyo, na hivyo basi kuwezesha Serikali kuzipatia changamoto hizo uvumbuzi.

Akiongea katika Kikao hiko Mgeni Rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Viwanda kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Leo Lyayuka alisema kuwa zoezi zima la upigaji marufuku mifuko ya plastiki limefanikiwa kwa kiasi kikubwa na lilifanyika kwa weledi hali iliyopelekea kutokua na malalamiko yoyote kutoka kwa wananchi.

“Kwenye mafanikio yoyote hapakosi changamoto, vivohivyo, kwenye zoezi hili, ingawa tumepata mafanikio makubwa lakini kuna changamoto ambazo zimejitokeza na kama zisipotafutiwa ufumbuzi wa haraka zitaharibu na kurudisha nyuma mafanikio makubwa yaliyopatikana. Kwahiyo kikao chetu kitajikita katika kuzibaini changamoto zote na kupendekeza mapendekezo namna ya kutatua”.Alisema Bwana Lyayuka.

Naye Mkurugenzi Msaidizi toka Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Kemilembe Mutasa alisema kuwa Kikao hiko kina lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa katazo la mifuko ya plastiki, kuibua changamoto za utekelezaji na namna ya kukabiliana na changamoto husika hususani katika masuala yafuatayo:- Viwango vya ubora vinavyotakiwa vya mifuko mbadala wa plastiki, Hali ya uzalishaji na usambazaji wa mifuko mbadala wa plastiki, Uzalishaji na upatikanaji wa malighafi kwa ajili ya mifuko mbadala wa plastiki, Viwango vya ubora wa mifuko mbadala na Changamoto zinazojitokeza katika uzalishaji wa mifuko mbadala wa plastiki.

Ofisi ya Makamu wa Rais imekua ikiandaa vikao kama hivyo mara nyingi ili kuweza kupata maoni na changamoto juu ya uzalishaji, usambazaji na biashara ya mifuko mbadala wa plastiki kwa pamoja.

Waziri Kigwangalla Aaigiza Maboresho Ya Huduma Mlima Kilimanjaro.

$
0
0
Na. Aron Msigwa – WMU, ARUSHA.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) lifanye maboresho ya miundombinu ya huduma za dharula na uokoaji ndani ya hifadhi ya mlima Kilimanjaro ili kuogeza usalama wa watalii wanaokweda 2kupanda mlima huo.

Pia, amelitaka shirika hilo liedelee kuboresha miudombinu ya malazi katika hifadhi hiyo ili iweze kuendana na mahitaji ya sasa ya wapanda mlima na kuangalia uwezekano wa kutafuta wawekezaji watakaojenga hoteli za kisasa kwa lengo la kuvutia watalii wengi zaidi.

Dkt.Kigwangalla ametoa maagizo hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya TANAPA na Wakuu wa Kanda wa Shirika hilo jijiini Arusha.

Amesema hatua hiyo imekuja kufuatia changamoto mbalimbali alizokutana nazo wakati akipada mlima Kilimanjaro Septemba, 28 mwaka huu, akiwa ameambatana na kundi la Wasanii na wadau mbalimbali kutoka taasisi za umma na binafsi.

Dkt. Kigwangalla ameieleza Menejimenti hiyo kuwa katika zoezi lake la kupanda mlima Kilimanjaro kuna changamoto alizibaini zikiwemo za kukosekana kwa miudombinu ya kutosha ya huduma za uokoaji na malazi ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi kwa haraka ili kuongeza ufanisi na idadi ya watalii wanaopanda mlima huo.

Kufuatia hali hiyo ameiagiza TANAPA ianze kuboresha huduma za dharula na uokoaji pia ijenge vituo vya kutolea tiba na huduma ya kwanza mlimani vitakavyokuwa na wataalam wa kuhudumia watalii wanaopata matatizo wakiwa mlimani pia kuboresha huduma za malazi katika baadhi njia za mlima huo.

Dkt.Kigwangalla amesema changamoto hizo zikitatuliwa kwa haraka zitauwezesha mlima huo kupata idadi kubwa ya watalii kuliko ilivyo sasa na kuiogezea serikali mapato.

Kuhusu uboreshaji wa huduma za uokoaji (Rescue services) kwa watalii wanaopanda mlima Kilimanjaro ameiagiza TANAPA ifanye utaratibu wa kuazisha huduma ya viberege maalum (Zip line) vitakavyokua vinatumika kushusha wapada mlima watakaokua wakipata matatizo ya kiafya kwa haraka hata wakati wa hali mbaya ya hewa.

“Suala la matumizi ya “Zip line” mliongezee nguvu ya kulitekeleza, hii itakua njia rahisi ya uokoaji na itawajengea ujasiri wapada mlima waelewe kwamba hata kama watapata shida yoyote ya kiafya wakati wa kupanda mlima wanajua wana uhakika wa usalama wa maisha yao hata pale ambapo hali ya hewa ni mbaya na helikopta haiwezi kutua mlimani” Amesisitiza Dkt. Kigwangalla.

Amesema uwepo wa huduma hiyo ya kisasa ya kushusha watalii wanaopata chagamoto za kiafya itawezesha watalii kupata huduma mlimani kupitia vituo vya kutolea huduma ya kwanza vitakavyojegwa mlimani ambavyo vitakua na wataalam wenye mafumzo watakaokuwa na jukumu la kutoa huduma muda wote.

Kuhusu uboreshaji wa huduma ya malazi mlimani Dkt. Kigwangalla ameonesha kuridhishwa na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na TANAPA kuboresha miundombinu ya malazi mlimani na kuitaka iangalie uwezekano wa  kuhamasisha wawekezaji wakubwa kwenye ujenzi wa hoteli za kisasa. 

Amesema uwepo wa hoteli hizo pamoja na mambo mengine utaongeza siku za watalii kukaa mlimani akitoa mfano wa hoteli nzuri na za kisasa zilizojengwa katika milima ya Alaps ambazo zinatembelewa na watu maarufu kutoka maeneo mbalimbali duniani.

Kufuatia maagizo hayo, Kamishna wa uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Dkt. Allan Kijazi amesema kuwa TANAPA inaendelea kufanya maboresho kwenye maeneo ya kulala wageni ili yaweze kwenda na wakati pia yawe na uwezo wa kupokea wageni wengi pia kuishirikisha sekta binafsi katika utoaji wa huduma mlimani.

Amesema kazi ya kuainisha maeneo kwa ajili ya ujenzi wa hoteli za kisasa inaendelea na kwa kuanzia maeneo manne yamekwishaainishwa kwa ajili ya uwekezaji na kuongeza kuwa baadhi ya wawekezaji wamekwishajitokeza na kuonesha nia ya kujenga hoteli za kisasa katika mlima huo.

Kuhusu uboreshaji wa huduma za ukoaji mlimani amesema kwa sasa kuna maeneo yana miundombinu ya barabara zinazowezwsha magari ya kubebea wagonjwa kufika katika baadhi ya maeneo na kutoa huduma ya uokoaji.

 Pia amesema wamekua wakitumia helikopta kutoa huduma za uokoaji licha ya huduma hiyo kushindwa kufanyika kazi wakati wa hali mbaya ya hewa na hivyo kulazimika kutumia machela za matairi zinazoendeshwa na watu kuhudumia watalii wanaopata matatizo ya kiafya.

Aidha, Dkt. Kijazi amesema TANAPA inaendelea kufanya maboresho ya huduma za dharula na uokoaji na itawasilisha kwake taarifa ya utekelezaji itakayoainisha mpango wa ujenzi wa njia za kisasa zitakazotumia viberenge maalum vya uokoaji vitakavyokua vikipita kwenye waya (Zip line) ili kazi ya ujenzi wa njia hizo ianze mara moja.

Aliyemtishia Mwenzake Kumuua kwa Bastola Akamatwa

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kinondoni, Mussa Taibu amesema wamemkamata Shabani Hamis Said ambaye anadaiwa kumtishia kwa Bastola dereva wa lori Venance John maeneo ya Mabwe Pande, saa 3 asubuhi, October 30, 2019.

Amesema baada ya lori la mchanga  alilokuwa anaendesha Venance kukwama bila kupata msaada wa haraka, akatokea mshtakiwa Shabani Hamis akiwa anaendesha gari lake aina ya Subaru na kumtaka dereva huyo ampishe ili apite na  akamjibu hawezi kumpisha kwa sababu amekwama katika mchanga.

Baadae wananchi wakatokea na kumpa msaada wa kumkwamua na kuondoka lakini alipofika mbele mshtakiwa alimzuia dereva huyo wa lori na kuanza kumtupia maneno kisha wakaanza kujibizana na kufikia hatua ya mshitakiwa kuamua kutoa Bastola na kutishia kumuua Venance.

Mchunguzi Mkuu TAKUKURU Amwandikia Barua DPP Kukiri Makosa Yake

$
0
0
Mchunguzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Cosmas Batanyika (44) anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwamo kushawishi rushwa ya zaidi ya Sh. milioni 300, kupokea na kutakatisha Dola za Marekani 20,000 amedai mahakamani amemwandikia barua Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ya kukiri makosa yake.

Batanyika alitoa madai hayo jana kesi yake ilipopangwa kwa ajili ya kutajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi, Kevini Mhina, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Wakili wa Serikali, Glory Mwenda, alidai kuwa kesi hiyo imepangwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika.

Hata hivyo, mshtakiwa alidai kuwa amemwandikia barua DPP na kwenye makubaliano anasubiri majibu ndugu zake wanafuatilia.

Hakimu Mhina alisema kesi hiyo itatajwa tena Novemba 15, mwaka huu na mshtakiwa ataendelea kukaa mahabusu

Maswali 15 Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kwenye Usaili ( Interviews ) na Namna ya Kuyajibu

$
0
0
Usail wa ajira (interviews) husababisha hofu na msongo wa mawazo kwa vijana wengi kabla au baada ya kutoka chumba cha usaili.

Tatizo hilo hutokana na hofu inayojenga wakati wa kujibu maswali unayoulizwa  na watu ambao wamekuzunguka wakati wa kufanyiwa usaili.

Njia moja ya kuzuia hii kutokea ni kufuatilia mfumo wa kujibu maswali.

Ifuatayo ni orodha yetu ya maswali 15 yanayoulizwa mara kwa mara kwenye interviews( Usaili) na namna ya kuyajibu;

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

1.Jitambulishe(Wewe ni Nani?)
Mara nyingi hili ni swali ambalo mtahiniwa huulizwa mara tu aingiapo kwenye chumba cha usaili. Kwa bahati mbaya watahiniwa wengi hudhani kuwa waajiri hutamani kujua majina yao. Hapana, majina yako wanayafahamu na pengine hata taarifa za ziada. Katika swali hili waajiri uhitaji kujua sifa zako zihusianazo na ajira zitakazo dhihirisha kuwa wewe ni mtu sahihi.

Mfano mtu anaweza kujibu hivi, “Jina langu ni Mti Mkavu, ni Mhitimu wa Shahada ya Masoko ya Chuo Kikuu Dodoma. Ni mtu makini, mbunifu, mchapa kazi na ninayependa watu. Pamoja na hayo ninao ujuzi usio na shaka kwenye masuala ya mawasiliano. Uwezo wangu unadhihirishwa na mrejesho ambao huwa na upata kwa kila mtu ninaye fanya naye kazi”.

Katika swali hili ni muhimu kujua kuwa halihitaji wewe kuzungumzia mambo yasiyo husiana na kazi na ajira. Kwenu mpo wa ngapi,jina la mama yako, mkoa unaotoka, kabila, kazi ya baba au mama yako havihitajiki katika taarifa unazotakiwa. 


2.Kwanini upewe ajira kwetu? | au unaweza ukaulizwa Kwa nini unahisi wewe ni mtu sahihi kwa kazi hii na siyo mwingine?

Kumbuka kuwa usaili wa kazi unahusisha ushindani hivyo swali hili linataka uoneshe utofauti ulionao. Katika kujibu swali hili zingatia mahitaji ya kazi husika kujenga hoja kwani hata kama una utofauti wa aina gani kama hautasaidia katika kufikia  malengo ya taasisi bado itakuwa ni kazi bure.

Mfano, “ Siyo kwamba mimi ni mchapakazi na mbobezi katika uhasibu pekee lakini pia ni mtu ambaye ninaweza kufanya shughuli zangu bila kusimamiwa. Mimi ni mtu wa matokeo hivyo kwa kila ambacho hufanya hulenga kutimiza malengo kwa wakati na kufikia viwango stahiki. 


"Ubora wangu unathibitishwa na tuzo kadhaa nilizowahi kupata ikiwemo mfanyakazi bora wa mwezi mara nne nilipokuwa nikifanya kazi na na Magogo Media. Hii inathibitisha kuwa mkinipa fursa hii hamtakuwa mnajaribu bali mtakuwa mnafanya maamuzi sahihi”.

3.Unajua nini kuhusu sisi?
Siku zote maandalizi ya usaili yanaenda sambamba na kutafuta taarifa sahihi za taasisi husika. Hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa taarifa unazotoa hapa ni sahihi na muhimu katika kudhirisha kuwa ulishafanya utafiti wa kutosha kuhusu taasisi husika.

Mfano, “ Benki yenu ilianzishwa mwaka 1987 ina maono ya kuwa benki bora kuliko zote nchini kwa kutoa huduma za kifedha zinazo aminika na kufikia maeneo mengi nchini. Kwa sasa benki yenu ina matawi 700 na ATMs 500 huku ikiwa na mpango wa kufungua matawi mengine Kigoma hivi karibuni. 


Endapo mtanipa fursa ya kufanya kazi na nyinyi nitahakikisha natumia vyema uwezo wangu katika masuala ya masoko ili kuongeza wateja na kuhaikisha huduma bora mnayotoa inafahamika kwa watu wengi.”

4. Ni vitu gani unavyojivunia?
Katika swali hili waajiri huhitaji kujua mambo kadhaa ambayo unayaona kama mtaji mkubwa katika utendaji kazi. Ni vyema kukumbuka kuwa mambo utakayo yataja hapa ni yale yenye umuhimu katika kuongeza ufanisi au ubora katika kazi husika kwani kila kazi inamahitaji yake ya tofauti na kazi nyingine.

Kwa mfano, “mambo makuu mawili ninayojivunia ni ujuzi na uwezo katika huduma kwa wateja na kujisimamia katika majukumu yangu. Kila ninapowahudumia wateja huwa napokea mrejesho chanya juu ya namna wanavyoridhishwa na huduma yangu hivyo kutamani kuhudumiwa nami tena.


Hii hunifanya nijione kuwa mtu muhimu sana katika taasisi yoyote ninayofanya nayo kazi. Pia, uwezo wangu katika kufanya shughuli bila kusimamiwa au chini ya usimamizi mdogo unanifanya niwe mtu wa kuaminiwa na kutegemewa katika kufanya shughuli zangu.Haya ni baadhi ya mambo mengi yanayonifanya mimi kuwa mtu wa tofauti. Nina amini hamtaacha fursa ya kufanya kazi nami”
 

5.Udhaifu wako ni upi?
Hili ni moja ya maswali ambayo watainiwa wengi huyachukia na kuyaona kama yana lengo la kuwatafutia sababu za kuwanyima kazi. Wengine kwa lengo la kuonesha ukamilifu huthubu kusema kuwa hawana udhaifu wowote-usithubutu kusema hivyo. Kila mtu ana udhaifu wake kwani hakuna aliye mkamilifu.

Suala la msingi ni kujua namna ya kujibu suali hili. Mambo ya kuzingatia ni pamoja na kuchagua udhaifu ambao hauta athiri utendaji wako na pili hakikisha udhaifu huo unahusiana na ujuzi na sio tabia. 


Ujuzi ni rahisi kuutafuata lakini kubadilisha tabia ni ngumu zaidi hivyo usiseme kuwa wewe ni mvivu,mdokozi, na mengineyo ya kitabia. Na unapotaja udhaifu wowote kumbuka kuonesha jitihada ambazo umeshazifanya ili kudhibiti udhaifu huo.

Kwa mfano, kwa kazi ya uhasibu mtu anaweza sema, “Udhaifu nilio nao ni masuala ya ‘graphic designing’ niligundua hili nilipohitaji kuandaa tangazo kwa ajili ya ofisi niliyokuwa nikifanya nayo kazi. Hata hivyo, nimeanza kujifunza mwenyewe kupitia mtandao wa internet na naona napata mabadiliko chanya kila leo”.

Kwa jibu hili ni dhahiri kabisa graphic designing siyo mahitaji muhimu ya kazi ya uhasibu hivyo haita athiti utendaji wa kazi.


6. Kwa nini uliacha kazi yako ya mwanzo?
Hapa unahitajikua makini sana, kumbuka na epuka kuzungumza vibaya kuhusu muajiri yeyote kabla au sasa au uwezo wa muajiri. 


Hapa unaweza ukawajibu tu kwamba;" Kwa sababu ya kuboresha na kuongeza ujuzi, pia natafuta fursa bora zaidi."

7.Unatarajia kupata nini kutokana na kufanya kazi hapa? au unaweza ukaulizwa | Baada ya miaka mitatu wewe mwenyewe utakua wapi?
Ongelea unachotumaini kutimiza ila kuwa mkweli. Pia usiongee kwa ujumla. Chagua kitu maalum ambalo ni muhimu kwa kampuni alafu ilenge. Ila, uwe wazi kwa kusema itachukua muda kujifunza zaidi kuhusu kampuni ili kufanikiwa zaidi.

Kwa mfano; “Nikiwa mwalimu wa kiingereza, lengo langu ni kuongeza asilimia ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa taifa kuwa 85% ya darasa yangu. Najua itachukua muda kujua vizuri changamoto za wanafunzi ila, naamini nitafanikiwa”


Ni vizuri kusema kwamba unatumaini kuona uwajibikaji zaidi  katika kampuni hiyo na kuongeza thamani katika kampuni kwa mchango wako. 

8.Kwanini umekaa muda mrefu bila kupata ajira?

Wajibu kwamba; "Nilikuwa najiendeleza katika taaluma yangu "


9. Eleza namna unavyoweza kujisimamia mwenyewe
Wajibu kwamba: Nitakuwa nafanya kazi niliyopewa nikishirkiana na wasimamizi wangu na viongozi juu ya namna ya kumaliza kazi kabla ya muda uliopangwa.


10. Kitu gani kinakukera miongoni mwa wafanyakazi wenzako?

Wajibu kwamba; "Naamini katika kufanya kazi kwa pamoja. Hata kama nikikerwa na kitu chochote, huwa najaribu kuepuka isipokuwa kama ni kitu cha binafsi."

11.Unategemea kufanya kazi kwa muda gani kama ukipewa ajira?

Wajibu:Kwa muda mrefu kama nitaendelea kuongeza kitu katika taaluma yangu.

12:Je, mwenyewe unajiona kufanikiwa?

Wajibu: Ndio, ukiachana na uwezo wa taaluma yangu, nadhani nimepata watu sahihi wa kufanya nao kazi.

13. Uwezo wako ni upi katika kazi?
Wajibu: Mimi huwa naelewa na kufundishika kwa haraka na ni mchapakazi wa kweli.

14,Unapenda nafasi au cheo gani katika timu unayofanya nayo kazi?
Wajibu: Haijalishi hadi nitakapojifunza kitu kipya kwa kila mradi au kazi.

15.Je, unaswali lolote kwetu? 

Mwishoni wa interview, ni kawaida kwa mwajiri kuuliza kama una maswali kwao. Ukipewa nafasi hii, usiulizie mshaara na faida zingine. Badala yake, uliza:
  1.     Maadili ya kampuni
  2.     Aina ya uongozi
  3.     Wafanyakazi wenzako
  4.     Chochote ambacho hukuelewa kuhusu kazi hiyo.
  5.     Watakupa jibu baada ya muda gani?
==>>USIFANYE HAYA MAKOSA KATIKA SWALI HILO:
- Je, kuna fursa ya kukua / kupandishwa ngazi?
- Nitapata siku ngapi za likizo?

- waajiliwa wanafaidika vipi na kampuni hii. 

==>Tiba bora ya msongo wa interview ni kujiandaa
Ingawa interview inaweza ikakupa misongo mingi, ukijiandaa vizuri Utashangazwa na mafanikio yako.

Interview ni nafasi yako ya mwisho kumvutia mwajiri, na vidokezo vilivyoelezwa hapo juu vitakusaidia na hilo.

Kumbuka, hamna haja ya kuwa na wasiwasi ukiwa umejiandaa. 


Nakutakia Mafanikio mema kwenye Interview
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kujibu vizuri maswali ya Interview, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini. 


Hilo ni Jukwaa Maalumu la Ajira zote za Serikali, Makampuni Binafsi n.k. Kuna Nafasi za Kazi zaidi ya 7000 kwa ajili yako.

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
http://ajirazote.com/jobs


▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Bonyeza <<HAPA>> ujiunge na Group letu la Telegram ili upate makala mbalimbali kama hizi pamoja na matangazo ya Ajira, Scholarships

Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Usafirishaji

$
0
0
NA; MWANDISHI WETU
Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuendelea kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya usafirishaji hapa nchini ili iweze kuongeza mchango wake katika kukuza uchumi.

Akizungumza Novemba 1, 2019 Jijini Dodoma wakati wa mkutano wa pamoja kati ya Vyama vya Madereva na Vyama vya Wamiliki wa Vyombo vya Usafirishaji, Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kujenga mazingira wezeshi kati ya wadau wote wa sekta ya usafirishaji hapa nchini wakiwemo madereva na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji.

“Moja ya maazimio ya mkutano wetu wa leo ni kuwataka wamiliki wa vyombo vya usafiri ambao hawajatoa mikata ya ajira kwa madereva wao waanze kutoa mikataba ya ajira iliyoboreshwa suala hilo lianze kutekelezwa mara moja kwa kuwa ni takwa la kisheria na sio jambo la hiari” Alisisitiza Mhagama

Kutolewa kwa mikataba hiyo ni matokeo ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya pande hizo mwaka 2017 yakitaka kuwepo kwa mikataba ya ajira iliyoboreshwa kwa madereva wote itakayoleta ustawi wa maslahi ya pande hizo na Taifa kwa ujumla.

Alifafanua kuwa mkutano huo umefanikisha kufikiwa kwa maazimio ya pamoja kati ya Serikali, wamiliki na madereva kupitia viongozi wa makundi hayo ili kuchochea ustawi wa sekta hiyo na kuondoa hali ya malalamiko na mapungufu yaliyobainika katika ukaguzi uliofanyika mwezi Julai na Agosti 2019 kwa lengo la kuona namna sheria za kazi  zinavyozingatiwa.

Azimio jingine ni kuendelea kutoa elimu kwa makundi hayo kupitia vyama vya wamiliki na madereva ili kupunguza au kuondoa changamoto zilizopo hasa zilizoibuliwa katika ukaguzi uliofanyika hivi karibuni.

Aidha, Waziri Mhagama ameviagiza vyama vya wamiliki wa vyombo vya usafirishaji kuhakikisha wanaruhusu wafanyakazi kuanzisha matawi ya vyama vya wafanyakazi kwa Makapuni ambayo hayajafanya hivyo bado.

“Vyama vya wafanyakazi vinasaidia sana kuleta tija na ufanisi katika maeneo ya kazi maana wafanyakazi hutumia vyombo hivyo kushauriana namna bora ya kutatua changamoto zinazowakabili,” alisema Mhagama

Katika hatua nyingine Waziri Mhagama aliwataka madereva na wamiliki wa vyombo hivyo kuendelea kuzingatia sheria na kuthamini utu na heshima pande zote mbili, Serikali itachukua hatua kwa yeyote atakayekiuka misingi hiyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri mkuu Kazi, Vijna na Ajira Mhe. Antony Mavunde amesema kuwa maazimio yaliyofikiwa katika mkutano huo yatasaidia kutatua changamoto zilizoibuliwa na madereva na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji.

Mkutano wa wadau wa sekta ya usafirishaji umefanyika Jijini Dodoma ukishirikisha Wizara zinazohusika na masuala ya uckuzi na Ujenzi.

=MWISHO=

Kampuni ya Nyanza Yapigwa Marufuku Dar

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda ametaka umakini katika utoaji wa tenda za ujenzi wa miradi mbalimbali ili kuepuka dosari.

Makonda ameayasema hayo leo, Jumamosi, Novemba 2, 2019, wakati akiwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya kimkakati inayoendelea katika wilaya za Ilala na Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Aidha, Makonda ametoa agizo kuwa Kampuni ya Nyanza inayosimamia mradi wa ujenzi wa Daraja la Mto Kivule isipewe tenda yoyote baada ya kukamilisha mradi huo, kutokana na kushindwa kukamilisha baadhi ya miradi ambayo wamewahi kupewa. Hata hivyo, Mkandarasi huyo tayari, ameanza ujenzi wa mradi huo baada ya kusikia RC Makonda anakwenda huko.

“Huyu mkandarasi huu uwe mradi wake wa mwisho katika Jiji la Dar es Salaam. Kama mnakumbuka hata Temeke aliwahi kufanya uzembe wa namna hii, vifaa hana vya kutosha kazi yenyewe haieleweki, tunataka Makandarasi wenye kasi kutekeleza miradi ya maendeleo,” amesem Makonda.

Amesema baadhi ya Makandarasi wanapewa tenda na kuishia kulipa madeni yanayowakabili kutokana na fedha wanazoingiziwa kukatwa na kusababisha miradi kutokamilika kwa wakati.

“Mnapotoa hizi tenda mjiridhishe wengine ndio kama hawa ambao hadi leo kazi hazionekani,  pia msiwape kazi kwa rushwa mtashindwa kusimamia miradi hii muhimu kwa wananchi,” amesema Makonda


Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, alitoa agizo la kuwekwa rumande kwa mkandarasi huyo kutokana na kusuasua kwa ujenzi huo.

Kwa upande mwingine, Mkandarasi anayejenga Machinjio ya Kisasa ya Vingunguti, Elisante Ulomi amesema, mradi wa machinjio ukikamilika utaongeza pato la Taifa kwa kuwa kila kitu kitakachoptoakana na zao la mifugo kitauzwa kwa mfano pembe, damu, ngozi, kwato na nyama ambapo Serikali itakusanya mapato na wananchi watafanya biashara kirahisi katika mazingira rafiki.

Katika hatua nyingine Makonda amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kutokana na kasi ya utekelezaji wa mradi wa Machinjio ya kisasa katika eneo la Vingunguti jijini Dar es Salaam.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images