Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Hasunga Awaasa Watumishi Wizara Ya Kilimo Kuwa Waadilifu

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Kilimo wameaswa kuwa waadilifu na kuzingatia ubora wa kazi wakati wanatoa huduma kwa wananchi.

Mwito huo umetolewa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) jana tarehe 30 Octoba 2019 wakati akizungumza na watumishi Jijini Dodoma alipotembelea ofisi za wizara hiyo eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mhe Hasunga amesema kuwa udilifu, nidhamu na weledi kwa watumishi wa umma ni kinga dhidi ya matumizi mabaya ya ofisi za umma na ni moja kati ya njia zinazowawezesha watumishi wa umma kuwa wachapakazi hodari.

“Kiwango cha juu cha Ubora wa kazi zetu na utendaji wa kazi unaozingatia weledi vitaweza tu kufikiwa kwa kuajiri watumishi wenye sifa stahiki, maadili, na bidii ya kuchapa kazi na wanaoweza kwenda sambamba na kasi kubwa ya mageuzi katika wizara ya kilimo,” Alisisitiza Mhe Hasunga

Alisema kuwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yam  mwaka 2015-2020.

Amewataka watumishi hao kusimama imara katika kufanya kazi na kutumia weledi wao kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kwamba uadilifu ndiyo silaha muhimu katika kufanya kazi ya Umma.

Amesema mtumishi atakayetumia vibaya rasilimali za serikali atahesabika adui namba moja wa Serikali na eneo analofanyia kazi huku akibainisha kuwa mtumishi wa aina hiyo kamwe hatohamishwa badala yake ataachishwa kazi.

Ziara ya waziri wa Kilimo kukutana na watumishi hao ilikuwa na lengo la kusalimiana na kusikiliza changamoto zinazowakabili katika utendaji kazi.

Jafo Atolea Ufafanuzi Malalamiko Yaliyowasilishwa Kwenye Zoezi La Uchukuaji Na Urejeshaji Wa Fomu

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo ametolea maelekezo malalamiko yaliyowasilishwa na wadau wa uchaguzi kuwa zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea nafasi za uongozi uzingatie Kanuni za uchaguzi na miongozo iliyotolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni Ofisini kwake Mtumba Jafo ameelekeza Wasimamizi/Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi, Vyama vya Siasa na wadau wengine woote kuhakikisha kila mmoja kwa nafasi yake anazingatia masharti na miongozo iliyotolewa kuhusiana na uchukuaji na urejeshaji wa fomu.

Amebainisha baadhi ya malalamiko yaliyowasilishwa toka kwa vyama vya siasa kuwa ni kutokuwepo vituoni kwa baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi, baadhi ya wasimamizi kutofungua kwa wakati vituo vya kuchukulia fomu, mihuri na masuala mengine ya Kikanuni.

“Malalamiko yaliyopokelewa yanaendelea kufanyiwa kazi, hata hivyo wadau na vyama vya siasa wanapaswa kuwasilisha malalamiko yao kwenye kamati za rufaa zilizopo katika maeneo ya uchaguzi,” alibainisha.


Akieleza maendeleo ya uchaguzi huo jana jijini hapa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo, alisema dosari zilizojitokeza ni chache kwenye baadhi ya mikoa.

Alisema katika Kata 3,959 ni kata 72 pekee ndizo amepokea malalamiko na kutaja maeneo machache kama vile Songwe, Lindi, Sengerema (Mwanza) na Moshi (Kilimanjaro).

Hata hivyo, Jafo alisema malalamiko kuhusu fomu zinazotolewa kwa wagombea kutogongwa muhuri, vyama vya siasa vinapaswa kufahamu kuwa, zitagongwa muhuri   pindi watakaporudisha au wakati wa uteuzi.

Kadhalika, alitoa msisitizo kwa wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi kuzingatia kanuni za uchaguzi kama zilivyowekwa.

Juzi, Waziri Jafo alitangaza wagombea kwenye uchaguzi huo kuanza kuchukua fomu kwenye ofisi za wasimamizi wa uchaguzi hadi Novemba nne mwaka huu.

Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti wa Mtaa, Kitongoji, Kijiji, Wajumbe wa Kamati ya  Mtaa, Waju,mbe wa Serikali ya Kijiji.

Uchaguzi huo ambao ni wa sita tangu kuanza mfumo wa vyama vya siasa nchini, unatarajiwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu ambapo wapigakura zaidi ya milioni 19 wanatarajiwa kushiriki

Waziri Mpina Atangaza Neema Kubwa Kwa Wafugaji

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Katavi
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kampeni ya kitaifa ya uogeshaji mifugo nchini na kutangaza neema kubwa kwa wafugaji ambapo sasa ng’ombe mmoja ataogeshwa kwa shilingi 50 badala ya sh 500 huku Mbuzi na Kondoo wakiogeshwa kwa sh 10 kila mmoja.

Uamuzi huu wa Serikali utawawezesha kuokoa shilingi bilioni 19 ambazo wafugaji wangezitumia kuogesha mifugo yao lakini ambapo sasa itatumika shilingi bilioni 2.16 tu huku Serikali ikiwapatia wafugaji ruzuku ya asilimia 90 ambapo kama wafugaji wangeendelea na bei hiyo ya miaka ya nyuma wangelazimika kutumia sh bilioni 21.6.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Kampeni ya uogeshaji mifugo awamu ya pili katika Josho la Kikonko wilayani Mlele na baadae mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Majimoto, Waziri Mpina alisema kupitia  mpango huo Serikali itasambaza dawa ya ruzuku lita 12, 546 kwenye majosho yanayofanya kazi 1,733 nchini kote.

Huku Mvua kubwa ikinyesha kwenye mkutano huo, Waziri Mpina alitumia zaidi ya saa moja kuhutubia huku akinyeshewa na mvua na kuwathibishia wananchi kuwa Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuleta mageuzi kwa vitendo hasa katika sekta ya mifugo.

Alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 25 kipengele  inaiagiza Serikali kuhakikisha mifugo yote inaogeshwa ili kuweze kuzuia magonjwa yote yanayoenezwa na kupe ambapo asilimia 72 ya vifo vya mifugo vinasababishwa na kupe.

Hivyo uogeshaji huo utawezesha mifugo kujikinga na maradhi na vifo ambapo Serikali itaogesha michonyo milioni 38 kwa Ng’ombe, michonyo milioni 18 ya Mbuzi, michovyo milioni 7 ya Kondoo, na michovyo 2500 ya Punda hivyo utaliwezesha taifa  kupata mifugo bora ambayo haina magonjwa.

Waziri Mpina alibainisha kuwa katika kipindi kifupi cha mwaka mmoja Serikali imekarabati majosho 400 na kwamba majosho yaliyobaki ambayo  hayajakarabatiwa ni 639 na kusisitiza kuwa yote yatakarabatiwa ili kuongeza kasi ya uogeshaji mifugo.

Waziri Mpina alisisitiza kuwa zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa hivyo uamuzi wa Serikali kuogesha mifugo pia umelenga kupambana na magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Hivyo juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono na watendaji wote wa Serikali, wafugaji wote ili kuboresha afya za mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo ikiwemo nyama, maziwa na ngozi sambamba na kuwakinga wananchi na maradhi yanayoweza kuambizwa kutoka kwenye mifugo.

Kufuatia uzinduzi huo, Waziri Mpina ameagiza kila kijiji nchini kiwe na josho kwenye  vijiji vyote zaidi ya 12,000 ili kila kijiji kiweze kuogesha mifugo na kusisitiza kuwa Serikali ya Rais Magufuli itakuja na mkakati wa kuhakikisha kila kijiji kinapata josho kama sehemu ya kuboresha afya za mifugo.

Pia ameziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha majosho yote yamekarabatiwa ndani ya mwezi mmoja na wizara itahakikisha inasambaza dawa kwenye majosho yote mabovu.

Aidha amesisitiza wanaokwenda kuogesha mifugo wafuate sheria za uogeshaji kuhakikisha mifugo inaogeshwa lakini kwa fedha ambayo Serikali imeitangaza ya sh 50 kwa kichwa na ng’ombe na sh 10 kwa kichwa cha mbuzi na zoezi hili litafanyika mfululizo kwa kipindi cha miezi 6 na kumuagiza  Mkurugenzi wa huduma za mifugo, Madaktari ya Mifugo wa Mikoa, na Wilaya kuhakikisha zoezi hilo linasimamiwa vizuri kuhakikisha wananchi hawatapeliwi

Pia Waziri Mpina ameweka wazi kuwa Serikali itatangaza bei elekezi ya chanjo ifikapo 15 Novemba mwaka huu na hakuna mtu mwingine atakayekwenda kuwaibia wafugaji tena na kwamba  chanjo ya homa ya mapafu ya ng’ombe itauzwa kwa sh 350 tofauti na siku za nyuma ambapo walichanja kwa sh 2000 kwa kichwa cha ng’ombe.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Komredi Juma Homera amemhakikishia Waziri Mpina kuwa Serikali ya mkoa huo inatasimamia maagizo yote na kwamba hakuna mfugaji atakayeonewa au kudhulumiwa na kwamba bei elekezi iliyotangazwa ya sh 50 kwa kichwa ngombe na 10 kwa mbuzi italeta neema kubwa kwa wafugaji.

Pia kuhusu malalamiko ya wafugaji kupigwa faini kubwa kuuawa kwa mifugo yao amemkabidhi nyaraka za malalamiko hayo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Katavi na kuwakamata watu wote waliotajwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Hezron Nonga amesema zoezi hilo la ugeshaji litafanyika nchi nzima na kuwataka wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao ili kuikinga na maradhi.

Jinsi Ya Kuandika CV Nzuri Ambayo Itamvutia Mwajiri na Kukufanya Upate KAZI Kirahisi

$
0
0
WATU wengi nchini wamekosa ajira  kwa sababu ya makosa wanayoyafanya wakati wa kuandika CV zao.

Kumbuka,  makampuni  karibia yote yanayotangaza nafasi za kazi hupokea wastani wa maombi 200-500 ya kazi kwa tangazo moja la kazi. 

Hivyo, CV yako lazima ikae vizuri ili kumshawishi mwajiri. Utaratibu wa kuomba kazi unaweza ukawa tofauti kati ya makampuni na mashirika, ila yote yatahitaji uwatumie CV.

CV ni nini?
CV ni maelezo ya ujumla kwa kiundani ya historia yako ya kazi na shule. Kawaida, inatumika kwenye maombi ya kazi ya nafasi za kati, za juu na za utafiti.

Mambo yafuatayo yatasaidia kuifanya CV yako iwe bora na hivyo, kukusaidia kupata interview za kazi.

👉Soma na kuelewa maelezo ya kazi
Una ujuzi gani? Mwajiri anatafuta mfanyakazi wa aina gani? Maswali haya ni muhimu kujua kama utaiweza hiyo kazi au la. Pia, ni vizuri kujua nini hasa ni muhimu kwa muajiri na kufanya maombi yako yaendane zaidi na mahitaji ya mwajiri.

Kwa mfano, kama kazi inaweka umuhimu kwenye ujuzi wa kutumia mitandao ya kijamii kwa matangazo, hakikisha CV yako ina kazi zote zilizohitaji matumizi ya mitandao ya kijamii.

👉Andika maneno muhimu yaliyotumika kwenye maelezo ya kazi, uyatumie kwenye CV
Usichukue sentensi nzima kutoka kwenye maelezo ya kazi na ukaitumia vile vile kwenye CV yako. Ila, tumia lugha na baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye CV.

👉Fanya utafiti juu ya kampuni iliyotangaza kazi
Pamoja na kuchambua maelezo ya kazi, ni muhimu kufanya utafiti juu ya kampuni yenyewe. Kama wana tovuti au wapo kwenye mitandao ya kijamii, jaribu kujua ni kazi gani na sekta ipi wanayohusika nayo. 

Pia, ikiwezekana jaribu kuwajua wafanyakazi/meneja wa kampuni hiyo. Hii itakusaidia kujua maadili na muelekeo wa kampuni. Hii itakusaidia kuweka maombi yako ya kazi yaendane na kampuni hiyo.

👉Orodhesha ujuzi wako wakufanya kazi
Hapa, usiweke kazi zote ulizozifanya maishani mwako ila, weka zile ambazo zilikuongezea ujuzi utakayo kusaidia kufanya kazi unayoomba.

==>Format/Staili inayotumika zaidi kwenye kuandika CV:
   1. Lengo la CV na ujuzi wako
    2.Ujuzi wako wa kazi
   3. Mafanikio maalum
   4. Elimu
   5. Ujuzi muhimu binafsi

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬
Angalizo:
  1.  Tumia maandishi ya kawaida ya Times New Roman
  2.  Tumia size 9 – 12 ya herufi
  3.   Hakikisha unatumia staili moja ya kuandaa CV kote
  4.   CV isiwe zaidi ya ukursasa 2
  5.   Usitumie sentensi ndefu
  6.  Hakikisha CV yako inasomeka kiurahisi na inawasilisha   mafanikio yako kwa uwazi.
  7.  Anza na kazi yako ya sasa hivi au ya hivi karibuni alafu rudi nyuma.
   ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 
   ==>.Hakikisha Yafuatayo:
1.Ukiwa unaandika jina la kampuni uliyo fanya kazi, andika jina la kampuni kikamilifu. 
2.Eleza kwa ufupi kampuni yao inahusika na nini. 
3.Tatu, weka muda uliyofanyakazi hapo (mwezi na mwaka).  
4.Baada ya hapo, orodhesha kazi na majukumu yako kwenye hiyo kampuni.
5.Usidanganye

👉Maandalizi ya Mwisho

1.Pitia kila kitu kwa mara ya mwisho
 -Print CV yako alafu ipitie. Hii huwa inasaidia kuona makosa yako.

2.Mpe Rafiki  yako apitie CV
-Muombe rafiki yako apitie CV yako. Macho manne ni bora zaidi ya mawili!

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Hatua ya kwanza kwenye kupata kazi unayotaka ni kutuma maombi. Tunatumaini kwamba maelezo yaliyoelezwa humu yatakusaidia kuandaa CV bora kwa ajili ya mwajiri.

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kuandika CV nzuri, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini.

AU 

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mkoani Mwanza

$
0
0
Jeshi La Polisi Mkoa Wa  Mwanza Kwa Kushirikiana Na Vyombo Vingine Vya Usalama Vikiwemo Vile Vya Uwanja Wa Ndege Wa Mwanza  Vilimkamata Raia Mmoja Wa India Kwa Tuhuma Za Kukutwa Na Madini Aina Ya Almasi Bila Kibali Na Kinyume Cha Sheria.

 Ufuatiliaji Wa Ukamataji Ulianza Tarehe 23/10/2019 Majira Ya 11;00 Hrs  Eneo La Uwanja Wa Ndege Jijini Mwanza. 

Raia Huyo Wa India Yogesh Sumatlal Shah Miaka 44, Mwenye Hati Ya Kusafiria Namba R9800410 Alikuwa Katika Hatua Za Mwisho Za Kusafiri Kutoka Mwanza Kuelekea Nairobi Kenya Kwa Kutumia Ndege Ya Precision Na Alikamatwa Katika Eneo La Upekuzi Akiwa Na Madini Ya Almasi Yenye Uzito Wa Grams 50 Yenye Thamani Ya Usd 282,898.07 Sawa Na Tshs 650,980,853.34/= 

Alikuwa Ameficha Madini Hayo Ndani Ya Mkono Wa Begi Lake. Upelelezi   Kuhusiana Na Tukio Hili Kwa Hatua Ya Awali Umekamilika Na Mtuhumiwa Leo Anafikishwa Mahakamani Kwa Makosa Matatu Ambayo Ni,

1) Kusafirisha Madini Bila Kibali

2) Kufanya Makosa Ya Kimtandao Na

3) Kutakatisha Fedha

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Litaendelea Kushirikiana Na Vyombo Vingine Vya Usalama Ili Kubana Na Kuziba Mianya Yote Inayotumiwa Na Wahalifu Kuiba Rasilimali Za Taifa Hili Na Kila Atakayekamatwa Hatua Kali Za Kisheria Zitachukuliwa . 

Aidha Wananchi Wanahakikishiwa Kuwa Kipindi Chote Cha mchakato  Wa Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Utakao Fanyika Tarehe 24 Mwezi Novemba Mwaka Huu Usalama Kwa Vyama Vyote Na Wananchi Kwa Ujumla Umeimarishwa. 

Watu Wajitokeze Kuchagua Viongozi Watakaowaletea Maendeleo.        

 Imetolewa Na;
Muliro J. Muliro- Acp
Kamanda Wa Polisi (M) Mwanza.
31october,2019.

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Linawashikilia Watuhumiwa Kumi [10] Kwa Tuhuma Mbalimbali.

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na Opresheni, Misako na Doria katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya ili kuhakikisha usalama wa raia na mali unakuwepo ikiwa ni pamoja na wananchi kuendelea na shughuli mbalimbali za kujitafutia kipato. Oktoba 30, 2019 Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya liliendesha Operesheni maalum katika maeneo mbalimbali na kupata mafanikio kama ifuatavyo:-

KUPATIKANA POMBE MOSHI @ GONGO.
Mnamo tarehe 30.10.2019 majira ya saa 10:00 asubuhi huko Kijiji cha Kibisi, Kata ya Kyimo, Tarafa ya Ukukwe, Wilaya ya Rungwe, Askari Polisi waliwakamata 1. AMBOKILE MWAISABILA [38], 2. ISAYA CHRISTOPHER [28] na 3. ZAINA KASIM [26] wote wakazi wa Kibisi wakiwa na Pombe Moshi @ Gongo ujazo wa lita kumi na mbili [12]. Watuhumiwa ni wauzaji na wanywaji wa Pombe hiyo.

KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI @ GONGO.
Mnamo tarehe 30.10.2019 majira ya saa 11:50 asubuhi huko katika Kitongoji na Kijiji cha Itete – Ndembo, Kata ya Kabula, Tarafa ya Busokelo, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya, Askari Polisi walimkamata TUNU KIJUMILE [21] mkazi wa Ndembo akiwa anauza pombe haramu [gongo] ujazo wa lita tatu [03] Mtuhumiwa ni muuzaji na mtumiaji wa gongo.

KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI @ GONGO.
Mnamo tarehe 30.10.2019 majira ya saa 14:30 mchana huko Igawa, Kata ya Lugelele, Tarafa ya Rujewa, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi wakiwa katika operesheni maalum walimkamata DAMIN MPINGA [71], mbena, mkulima, mkazi wa igawa akiwa na gongo ujazo wa lita 10 katika chupa 20 ];] mtuhumiwa ni muuzaji na mtumiaji wa pombe hiyo.

KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI @ GONGO.
Mnamo tarehe 30.10.2019 majira ya saa 14:30 mchana huko Kitongoji cha Matundasi "A" Kata ya Matundasi, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya.

Askari Polisi wakiwa katika operesheni maalum walimkamata MARIAM SIPO [42] mkazi wa Matundasi "A" akiwa na gongo ujazo wa lita tisa [9] kwenye madumu mawili madogo. Mtuhumiwa ni mpikaji, muuzaji na mtumiaji wa pombe hiyo.

KUPATIKANA NA BHANGI.
Mnamo tarehe 30.10.2019 majira ya saa 11:00 asubuhi huko Kijiji cha Kasumulu, Kata ya Ngana, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi wakiwa katika operesheni walimkamata ABRAHAMU NASON [27] mkazi wa Kasumulu akiwa na bhangi uzito wa kilogram 23 akiwa amehifadhi katika mifuko miwili [2] ya sandarusi na kuificha nyumbani kwake. Mtuhumiwa ni muuzaji na mtumiaji wa bhangi. Upelelezi unaendelea.

KUPATIKANA NA NYARA ZA SERIKALI.
Mnamo tarehe 30.10.2019 majira ya saa 12:30 mchana huko Kijiji na Kata ya Bitimanyanga, Tarafa ya Kipembawe, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi wakiwa katika operesheni kwa kushirikiana na askari wa wanyama pori [K.D.U – Iringa] waliwakamata watuhumiwa watatu ambao ni:-

1. ZEPHANIA FURAHISHA [65],
2. ALFRED MWANOGILE [42] na
3. ZAKAYO JACKSON [30] wote wakazi wa Bitimanyanga Wilayani Chunya wakiwa na vipande tisa vya nyama pori idhaniwayo kuwa nyama ya nyati. Watuhumiwa ni majangili.

Watuhumiwa wote watafikishwa Mahakamani mara tu upelelezi wa mashauri yao utakapokamilika.

Watu 70 wafariki Pakistan kufuatia moto kwenye treni

$
0
0
Watu wasiopungua 70 wameuwawa na dazeni kadhaa kujeruhiwa baada ya jiko la gesi kuripuka ndani ya treni iliyokuwa ikiwasafirisha waumini waliokuwa njiani kwenda kufanya ziara ya kidini nchini Pakistan.

Picha za televisheni zinaonyesha moto unaofuka ndani ya mabehewa matatu ya treni huku vilio vikisikia ndani ya treni hiyo katika eneo la vijijini la mkoa wa kati wa Punjab.

Baadhi ya abiria-wengi wao wakiwa waumini waliokuwa njiani kwenda katika ziara ya kidini katika mji wa mashariki wa Lahore, walikuwa wakipika chakula cha asubuhi pale majiko yao mawili ya gesi yaliporipuka-Ali Nawaz, afisa wa ngazi ya juu wa shirika la safari za reli la Pakistan ameliambia shirika la habari la Ufaransa AFP.

Wapakistan wengi wanabeba vyakula wanapokuwa katika safari ndefu lakini majiko ya gesi yamepigwa marufuku. Ali Nawaz anasema uchunguzi unafanywa kuhusu ajali hiyo.

Televisaheni za Pakistan zimeonyesha jinsi dazeni za watu walivyokusanyika njiani kuangalia jinsi moto unavyofuka ndani ya mabehewa  ambayo yaliachana na sehemu nyengine ya treni.

Waziri Mkuu Imran Khan ameamuru uchunguzi juu yakisa hicho kufanywa mara  moja
 
Vikosi vya  zimamoto vimefika haraka katika eneo hilo karibu na wilaya ya Rahim Yar Khan. Watumishi wa mashirika ya uokozi na wanajeshi pia wameonekana wakisaidia. Miili ya wahanga wa ajali hiyo iliyofunikwa shuka nyeupe imekuwa ikiondolewa.
 
-DW

Waziri Mkuu Majaliwa Atarajiwa Kuwa Mgeni Rasmi Wiki Ya Azaki.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika wiki ya asasi za Kiraia Tanzania  [AZAKI]itakayofanyika jijini Dodoma kuanzia Novemba 4-8,2019.
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma leo Oktoba 31,2019,Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Foundation for Civil Society  [FCS]BW.Francis Kimwanga amesema wiki ya asasi za kiraia nchini itakutanisha zaidi ya asasi za kiraia 500 kutoka nchi nzima Tanzania bara na visiwani Zanzibar.

Mkurugenzi mtendaji huyo wa  FCS]  amefafanua kuwa Wiki ya Asasi za Kiraia [AZAKI]itajumuiya Maonesho  ya kazi mbalimbali zinazofanywa na asasi hizo huku lengo likiwa ni kuimarisha ubia kati ya asasi za kiraia na wadau mbalimbali  katika kutimiza azma ya kuiletea Tanzania Maendeleo.
 
"Lengo la kongamano hilo nikuimarisha ubia kati ya asasi za kiraia na wadau mbalimbali katika juhudi za kutimiza azma ya kuileteaTanzanaia maendeleo," amesema .

Hata hivyo amesema "Kupitia  kongamano  hili asasi  za  kiraia  zitafanya majadilianao juu ya kazi  zao, kubadilishana uzoefu na kuona ni jinsi ambavyo zinaweza kushirikiana wenyewe kwa wenyewe na wananchi, serikali, bunge, wabia  wa  Maendeleo na sekta binafsi," amesema.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti  maalum mkoa  wa Dodoma  Fatma Taufiq ambaye  pia  ni  Mkurugenzi wa shirika  la  WOWAP  amesema wiki hiyo  ni  Wiki  ya kipekee  kwa  mwaka  huu washiriki  mbalimbali  wanatarajiwa kuwepo bila  kuwasahau viongozi  wakubwa kutoka serikalini huku pia akitoa rai kwa vyombo vya Habari kuhabarisha jamii umuhimu wa makundi maalum katika jamii.
 
“Asasi za kiraia zimekuwa na mchango mkubwa katika jamii,AZAKI inatekeleza Malengo 17 ya maendeleo endelevu hivyo nitoe rai kwa asasi ambazo zimekuwa zikienda kinyume na matakwa ya serikali na asasi sio adui zinashirikiana  na serikali .Pia nitoe rai kwa Vyombo vya Habari kuhabarisha umma juu ya Umuhimu wa Asasi hizi.amesema.

Hata hivyo  aliwataka  wananchi  wote kufika  katika viwanja  vya Jamhuri Novemba 4 Hadi 8 ili  kuweza  kuona  na  kujifunza  asasi  za  kiraia zinafanyaje  kazi zao n'a kuachana na  kusikiliza  habari  potofu kuwa  asasi za kiraia zinakula  hela na hazileti Maendeleo yoyote huo ni upotoshaji.

Msajili wa  asasi za kiraia kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,jinsia Wazee na Watoto,Charles Komba amesema asasi za kiraia zimekuwa chachu kubwa ya Maendeleo  na katika kuisaidia serikali.
 
“Asasi za kiraia ni Wadau wetu,ni wadau  wetu wakubwa   sana katika maendeleo ya kijamii,serikali haiwezi kufanya kwa kila jambo lakini sasi za kiraia zmekuwa mstari wa mbele kutusaidia.
 
Aidha,ameongeza kwa kusema ,Mpaka  mwaka 2017 serikali ilishasajili asasi za kiraia zaidi ya 10,000.

Mkurugenzi Mtendaji wa  Taasisi ya Haki,Rasilimali ,Mafuta ,Madini na gesi Rachel Chaganda amesema  taasisi hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kufanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na madini,Mafuta na gesi ambapo ni mchango mkubwa kwa serikali  Ya Tanzania.

Naye mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Ulemavu Tanzania[SHIVYAWATA] Ummy Nderiananga amesema katika wiki hiyo ya AZAKI,Kutakuwa na elimu pamoja na miradi mbalimbali  inayofanywa na watu wenye ulemavu huku afisa Uhusiano wa kituo cha sheria na Haki za Binadamu,Legal Human Rights   Centre[LHRC] Michael Malya akisema katika wiki hiyo kituo hicho kitajihusisha na utoaji wa huduma za kisheria.
 
Ikumbukwe kuwa FCS itatoa tuzo za Umahiri wa asasi za kiraia  ili kusheherekea na kutambua ufanisi na michango   za taasisi na watu binafisi  katika uchocheaji na uimarishaji wa sera ya maendeleo ya nchi.
 
Zaidi ya asasi za kiraia 15  zikishirikiana na FCS   Kuandaa wiki ya AZAKI ni LHRC,LSF,Save the children, Wajibu Institute,UN Women,Oxfam,Twaweza,Policy Forum,msichana Initiative,Hakirasilimali, UNA Tanzania, Acountability Tanzania,Sikika,TLS,SHIVYAWATA,na TANGO.
Kaulimbiu  wiki  ya asasi za Kiraia [AZAKI] Mwaka ,2019 ni ubia kwa Maendeleo ,Ushirikiano kama chachu ya Maendeleo.






Bashe:Serikali Imeamua Kuheshimu Na Kuweka Kipaumbele Sekta Ya Kilimo

$
0
0
Na.Faustine Galafoni,Dodoma.
NAIBU Waziri wa Kilimo,Husein Bashe amesema Serikali imeamua kuheshimu na kutoa kipaumbele mazao ya kilimo kama sekta zingine zinavyothaminiwa kwa kujenga miundo mbinu rafiki kwa mkulima hususani pembejeo bora.

Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa kwenye mkutano wa kitaifa wa wakulima wadogo Tanzania uliofanyika jijini Dodoma kujadili changamoto wanazokumbana nazo ulioandaliwa na Shirika la ANSAF.

Waziri Bashe amesema kuwa sekta ya kilimo imekuwa msaada katika kuinua uchumi wa nchi kutokana na kaya ,jamii kwa ujumla kutumia malighafi nyingi zinazotokana na kilimo mbali na changamoto zinazowakabili wakulima .

Amebainisha tarari serikali imeweka mikakati ya kuboresha miundo mbinu kwa wakulima wadogo katika suala zima la kuongeza maafisa ugani vijijini huku wakishirikana na maafsa watendaji kutembelea wakulima,pembejeo zilizo bora na bei rahisi,upatikanaji wa mbegu nzuri,sheria ya kulinda wakulima,kuwapatia Bima ya mazao ,pamoja na kuongea na taasisi za kifedha kupata mikopo yenye riba nafuu jambo ambalo litasaidia kuleta maendeleo.

"Kama Wizara itaendelea kutangaza  na kuhamasisha wakulima wadogo kuboresha miundo mbinu ili kuwe na kilimo chenye tija  kwani wamekuwa wachangiaji wazuri uchumi wa nchi na jamii imategemea chakula kutoka kwa wakulima wadogo"alisema Waziri Bashe.

Hata hivyo amepiga marufuku kwa viongozi wa Ushirika ambao sio wakulima kuongoza wakulima kutokana na malalamiko yanayotolewa ambapo wao kazi kubwa ni kujinufaisha badala ya kuwasaidia wakulima hao.
"Kuanzia leo kiongozi ambaye sio mkulima hapaswi kuongoza wakulima haiwezekani wewe sio dhehebu ya kiislamu halafu eti uwaongoze waislamu"amesema.

Mbali na hayo amesema wizara imeanzisha Dawati la masoko ambalo litashughulikia wakulima ambao ufanyiwa ukiritimba na TBS huku akisema kutakuwa na huduma bure ya mawasiliano ambayo itawala fursa wakulima kupiga simu kueleza changamoto zao na kutatuliwa hapo hapo.

Nae mwenyekiti kamati ya Bunge kilimo,mifugo na maji Mahamoud Mgimwa amesema wabunge wako tayari kuendelea kuwatetea wakulima ili serikali iweze kutatua changamoto zao lengo ni kufikia asilimia kumi .

Kwa upande wake  Mwenyekiti jukwaa la wakulima wadogo wanawake ,Janeth Nyamayahasi amesema wanakumbana na changamoto ya upungufu wa maafisa ugani vijijini kwenye sekta ya mifugo,kilimo na uvuvi na kwamba baadhi ya wataalamu hao hawatoi ushirikiano na mara utoa ushauri mbovu unaopelekea mazao yao kuharibika.

Mwanafunzi apoteza maisha baada ya kuchapwa viboko na mwalimu wake

$
0
0
Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 14 huko nchini Burundi amefariki baada ya kupigwa na mwalimu wake, baba wa mtoto huyo ameiathibitisha hilo.

Mtoto huyo, Chadia Nishimwe alipigwa viboko kwenye maeneo ya shingo na miguuni , kipigo ambacho kilimpelekea kutokwa damu puani na masikioni, alisema Jean-Marie Misago.

“Alikufa darasani mara baada ya kupigwa na mwalimu wake, na wakaenda kumtelekeza katika ofisi ya mwalimu mkuu,” Bwana Misago alisema.

Mkuu wa shule alijaribu kumuwahisha hospitalini mtoto huyo wakati mtoto ameshakufa tayari, aliongeza baba huyo.

Kwa mujibu wa BBC ilijaribu kutafuta taarifa zaidi katika sekta ya elimu bila mafanikio.

Mtoto huyo aliuwawa siku ya jumanne na kuzikwa siku hiyo hiyo .

Nchini Burundi, adhabu ya kuchapwa kwa mwanafunzi ni kinyume na sheria ingawa bado wanafunzi wanachapwa.

-BBC

Fahamu Zaidi Kuhusu Ugonjwa Wa Mshipa Wa Ngiri (Hernia/Hydrocele)

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya maumble ya kiume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0713785111

Rais Museveni aingilia kati maandamano ya wanafunzi wa Makerere....ayaagiza majeshi kuondoka chuo Hapo

$
0
0
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameagiza wanajeshi wanaozingira chuo kikuu cha Makerere kwa lengo la kutuliza maandamano waondoke mara moja chuoni hapo kwani hiyo sio kazi yao na badala yake jeshi la polisi lisimamie ulinzi chuoni hapo.

Wiki iliyopita, Wanafunzi 15 walikamatwa na Polisi kwa kuchochea vurugu na maandamano wakipinga ongezeko la asilimia 15 ya karo chuoni hapo.

Kwenye maandamano hayo wanafunzi hao walichoma vituo viwili vya Polisi mjini Kampala, Jambo lililopelekea Jeshi liingilie kati ili kutuliza ghasia hizo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema wiki hii na Afisa Habari wa Rais Museveni, Don Wanyama amesema kuwa Museveni ameagiza Wanajeshi waondoke chuoni hapo na jukumu hilo lichukuliwe na Jeshi polisi.

“Rais Museveni kasema wadau na viongozi wa chuo cha Makerere wakae chini kujadili matatizo yanayoendelea katika chuo hicho. Asubuhi hii amempigia Mkuu wa Chuo kamwambia wakae na wenzao wajadiliane. Pia ameagiza Wanajeshi waondoke chuoni hapo na kazi hiyo iwe chini ya Jeshi la Polisi la Uganda,”amesema Wanyama.

Mpaka sasa hatma ya ongezeko la ada chuoni hapo bado haijapatikana, Lakini hali ya usalama imeanza kurejea.

Ongezeko la 15% liliidhinishwa na baraza la vyuo vikuu nchini Uganda, Wanafunzi wanatakiwa kuanza kulipa ada yenye ongezeko hilo kwa miaka mitano ijayo baadaye kila mwanafunzi atatakiwa kulipa 75% zaidi.

Mo Dewj: "Niliwaambia walioniteka waniue"

$
0
0
Bilionea kijana Afrika na mmiliki wa mojawapo ya klabu maarufu ya soka Afrika mashariki Simba SC – Mohammed Dewji amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu sakata lake la kutekwa nyara mwaka jana na namna alivyotishiwa maisha yake nchini Tanzania.

Katika mahojiano maalum na ya kipekee na BBC Swahili, Mo ameeleza kuwa kwa kipindi kizima, alihisi kwamba kuna uwezekano mkubwa hatoweza kutoka salama na kuwa mwisho wake wa maisha unakaribia.

“Saa 24 za kwanza baada ya kutekwa zilikuwa kama mwezi. Imani ndio kitu kikubwa kilichonisaidia katika kipindi kizima.”

Katika kuikumbuka siku hiyo, Mo ameeleza: “Walinifunga macho, miguu na mikono kwa siku tisa. Tulikuwa hatuongei sana, walikuwa sio watu wa hapa.

“Walikuwa wakinitisha na kuniweka bastola kwenye kichwa na kuniambia wataniua.” ameeleza mfanyabiashara huyo.

“Kufunga mlango (wa gari) tu, kugeuka nimekuta watu wanne ambao wamevaa mask nyeupe – wamefunika uso, wakapiga bunduki juu mara mbili halafu wameniwekea bunduki.”

Anasema awali alidhani ni jaribio la kutaka kuibiwa gari, na hakuwa na budi kufuata maagizo alipoambiwa alale chini kwenye sakafu.

“Kwenye sekunde sitini hivi, hao watu wamekuja wamenibeba na kuniweka ndani ya gari.”

Anasema kilichofuata katika safari hiyo anayosema iliyokuwa ngumu, watekaji wake walimvua nguo kwa kuhofia huenda ana kifaa cha kutambua anakokwenda yaani tracker na kumfunga mikono na miguu na kwenye dakika 20 wakamfikisha katika nyumba.

“Niligundua kuwa lugha wanayotumia sio lugha ya Tanzania, ilikuwa ni geni.”

“Asubuhi walikuwa wananifungua mikono wananifunga mbele, lakini usiku ndio kulikuwa na mitihani walikuwa wananifunga nyuma. Na wakikufunga nyuma maanake huwezi kulala, lazima ulale kulia au kushoto.”

Mo anasema alikuwa akitoa ushirikiano kwa kila alichotakiwa kufanya. Kikubwa anasema alikuwa akimuomba Mungu atoke salama.

Siku ya tisa anasema “walinisukuma pale Gymkhana na nikasikia gari limeondoka.”

Kwa muda wote alipewa tu kipande cha khanga aliyotumia kujifinika mpaka siku walipomuachilia ndiyo aliyotumia pia kujifunika.

Mo Dewji alitekwa Oktoba 11 2018 na watu wasiojulikana alfajiri wakati alipokuwa akielekea mazoezini alipofika katika hoteli moja ya kifahari katika eneo la Oysterbay jijini Dar es Salaam kama ilivyo ada yake kila siku alfajiri kwa ajili ya kufanya mazoezi ya viungo.

Siku tisa baadaye, Dewji alirejea nyumbani salama.

-BBC

Mkurugenzi mstaafu wa kampuni ya Katani Limited, Salum Shamte na wenzake 2 Washitakiwa Kwa Makosa Ya Uhujumu Uchumi

$
0
0
Mkurugenzi mstaafu wa kampuni ya Katani Limited, Salum Shamte na wenzake 2 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga na kusomewa mashtaka matatu ya uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na kuisababishia Amcos hasara ya Sh1.1 bilioni.

Shamte amefikishwa mahakamani leo Alhamisi Oktoba 31, 2019 pamoja na wenzake,  Juma Shamte ambaye ni mkurugenzi wa sasa wa kampuni hiyo na mjumbe wa bodi ya Katani, Fatma Diwani.

Akisoma mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao mbele ya hakimu mkazi Desidery Kamugisha, wakili wa Serikali, Peter Maugo amesema kati ya Januari 2008 na Agosti 2018 katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Tanga na Mkoa wa Tanga, walikula njama kutekeleza mpango wa uhalifu.

Maugo aliyekuwa pamoja na wakili wa Takukuru, Barry Galinoma  na Winlucky Mangowi wa ofisi ya mwendesha mashtaka wa Serikali,  amesema shtaka la pili ni kusababisha hasara katika vyama vitano vya Amcos kiasi cha Sh1.14.bilioni  na shtaka la tatu ni utakatishaji fedha wa Sh1.14 bilioni.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo waliitakiwa kutojibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Mawakili wa Serikali wamesema upelelezi wa kesi hiyo iliyoahirishwa hadi Novemba 13, 2019 haujakamilika, washtakiwa kurudishwa rumande.

Picha ya Rais Magufuli yamponza Idris Sultan ....Makonda Amtaka Ajisalimishe Polisi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amemtaka mchekeshaji na muigizaji hapa nchini, Idris Sultan, kuripoti katika kituo chochote cha polisi, hii ni baada ya msanii huyo ku 'post' picha katika ukurasa wake wa Instagram, akiwa amehariri picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na kuweka sura yake.

Makonda ametoa agizo hilo leo Oktoba 30, 2019, kupitia ukurasa wake wa Instagramu.

"Naona mipaka ya kazi yako huijui, nenda sasa hivi kituo chochote cha Polisi, uwaambie Makonda kaniambie nije utakuta ujumbe wako" ameandika Makonda.

Idris aliweka picha hizo ikiwa ni siku moja tu imepita tangu Rais Magufuli, atimize umri wa miaka 60, ambapo msanii huyo aliandika kuwa.

 "Kwa siku moja tukabadilishana kazi ili a-enjoy birthday yake kwa amani".

Tanzania Kuanzisha Kituo Cha Kimataifa Cha Usuluhishi Wa Migogoro Ya Kibiashara

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Abidjan,Ivory Coast.
Tanzania na Taasisi ya ushauri wa kisheria ya Afrika (ALSF) iliyoko chini ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) zimekubaliana kuandaa mkakati maalum kwa ajili ya kutoa mafunzo maalum na ya haraka ya msaada wa kisheria kwa Ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu wa serikali (DPP) hususani katika kusimamia mashauri katika mahakama na mabaraza ya usuluhishi ya Tanzania na ya Kimataifa katika maeneo ya madini, biashara na usuluhishi na makampuni ya Kimataifa pamoja na mafuta na gesi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo mara baada ya majadiliano na Afisa Mtendaji Mkuu na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ya ushauri wa kisheria ya Afrika (ALSF) Bwana Stephen Karangizi mazungumzo yaliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) Abidjan Nchini Ivory Coast.

Prof. Kabudi amesema kuwa lengo la majadiliano hayo ni kuisaidia Tanzania kuweka mikakati kuimarisha sekta ya Sheria ikiwa ni pamoja na kuiongezea uwezo ofisi ya mwanasheria mkuu wa Tanzania hasa baada ya mabadiliko makubwa yaliyofanywa ya muundo mpya wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali ili kuiwezesha kutoa ushauri wa kina na wa kitaalam kwa serikali lakini pia kusimamia mashauri katika mahakama na mabaraza ya usuluhishi ya Tanzania na ya Kimataifa.

Ameongeza kuwa maombi ya Tanzania kwa taasisi hiyo kwa ajili ya kuisaidia ofisi ya mwanasheria na wakili mkuu wa serikali yamekamilika na kinachosubiriwa hivi sasa ni kuwasilisha maombi hayo kwa kikao cha bodi ili utekelezaji uanze.

Ameongeza kuwa eneo jingine ambalo Tanzania inahitaji msaada kutoka kwa  Tanzania na Taasisi ya ushauri wa kisheria ya Afrika (ALSF) iliyoko chini ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ni kuhusu kuisaidia Tanzania katika hatua iliyoichukua ya kutunga sheria mpya ya usuluhishi wa migogoro ya kimataifa nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na kuanzisha kituo kipya cha kusimamia usuluhishi wa migogoro.

Katika eneo hilo Taasisi ya ushauri wa kisheria ya Afrika (ALSF) iliyoko chini ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) itatoa wataalamu kusaidia Tanzania kupitia  miswaada ambayo imeandaliwa na serikali pia kuandaa andiko la namna kituo hicho kitawekwa Tanzania na kukidhi matakwa ya kimataifa.

Kwa uoande wake Afisa Mtendaji Mkuu na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ya ushauri wa kisheria ya Afrika Bw Stephen Karangizi amesema wamepokea ombi hilo na kwamba wanasubiri maamuzi ya kikao cha bodi ili kuweza kuanda program maalum kwa ajili ya kuimarisha na kuendeleza ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.

Ameongeza kuwa nchi nyingi za Kiafrika zimeshindwa katika usuluhishi wa migogoro hususani ya kibiashara,madini,mafuta na gesi na maeneo mengine na kuongeza kuwa suala hilo linapaswa kuwekewa mkakati maalum na kutekelezwa kwa haraka ili kuepuka makosa yaliyokwisha kufanywa katika siku zilizopita.

Taasisi hiyo ya ushauri wa kisheria ya Afrika (ALSF) iliyo chini ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ilianzishwa kutokana na ombi la Mawaziri wa fedha kutoka Afrika kwa lengo la kuzisaidia Nchi za Afrika kujijengea uwezo katika masuala ya kisheria hususani katika  madini,mafuta na gesi pamoja na madeni ili kuziwezesha nchi za Kiafrika kuwa na uwanda sawa wa majadiliano katika ngazi za Kimataifa kuhusu masuala ya kisheria yanahusu biashara na makampuni ya Kimataifa.

Jiji La Dodoma Latozwa Faini Kutokana Na Uchafu Wa Machinjio

$
0
0
Na Lulu Mussa
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) hii leo imefunga machinjio ndogo ya Msalato kwa muda usiojulikana na kupiga faini kwa kosa la kukithiri kwa uchafu wa mazingira na miundombinu chakavu.
 
Hatua hiyo imefikiwa mara baada ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kufanya ziara ya kushtukiza katika eneo hilo na kujionea Mazingira yasiyoridhisha kwa usalama wa afya za binadamu. 
 
Katika ziara hiyo, wabunge wamejionea mazingira yasiyoridhisha na kuhatarisha afya za watumiaji wa nyama inayochinjwa machinjioni hapo ikiwa ni pamoja na kurundikana kwa samadi, kukithiri kwa harufu kali na kukosekana kwa maji safi.
 
Bw. Gratius Mwesiga, Afisa Mifugo wa Jiji la Dodoma ameieleza Kamati hiyo kuwa ukarabati katika eneo hilo umeanza na unaendelea kwa awamu, ikiwa ni pamoja na ukarabati wa mifumo ya maji taka.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mussa Sima amesema lazima hatua kali za kisheria zichukuliwe kwa manufaa ya afya za walaji. "Sisi watu wa Mazingira afya za binadamu ni kipaumbele namba moja, hali hii haikubaliki" Sima alisisitiza. 
 
Waziri Sima amemuagiza Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Nchini (NEMC) Dkt. Samwel Gwamaka kufanya tathmini ya haraka na kina na kuhakikisha kuwa machinjio yanazingatia taratibu zilizopo katika Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004.
 
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bunge Viwanda, Biashara na Mazingira Kanali Mstaafu Masoud Ali amesema hali ya usafi katika machinjio hiyo haidhirishi na kuwataka NEMC kuchukua hatua. "NEMC msingechukua hatua, sisi Kamati tungechukua, haiwezekani hali hii haikubaliki" Alisisitiza Mhe. Masoud Ali.
 
Wakati huo huo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC amelitoza faini Jiji la Dodoma ya kiasi cha Shilingi Milioni tano (5) kwa mujibu wa kifungu namba 194 cha sheria ya usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kutakiwa kuilipa ndani ya wiki mbili.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa November 1

Idris Sultan Aachiwa kwa Dhamana.....Kuripoti tena Polisi Leo

$
0
0
Msanii  Idris Sultan aliyehojiwa na polisi  jana Alhamisi Oktoba 31, 2019 kwa saa tano na kupekuliwa nyumbani kwake ameachiwa kwa dhamana usiku wa kuamkia leo.

Baada ya kuhojiwa, mchekeshaji huyo ambaye jana alitakiwa kuripoti polisi na mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alikwenda na polisi nyumbani kwake.
 
Wakili wake, Benedict Ishabakaki amesema licha ya kwamba Msanii huyo ameachiwa kwa dhamana usiku, atatakiwa kuripoti tena Kituo cha Polisi leo saa mbili asubuhi ili Polisi waendelee na upelelezi wao.

Idris alitakiwa kwenda polisi baada ya kuweka picha yenye sura yake huku akiwa ameketi katika kiti chenye nembo ya Taifa.

Pia, Idris aliweka picha nyingine inayoonyesha sura ya Rais Magufuli akiwa amesimama huku amevaa suruali yenye mikanda inayoshikizwa mabegani

Twitter yapiga marufuku matangazo ya kisiasa

$
0
0
Jukwaa la mtandao wa kijamii Twitter limetangaza kwamba halitatangaza tena matangazo yenye muelekeo wa kisiasa.

Kiongozi mkuu ( CEO) wa Twitter, Jack Dorsey amearifu kwamba shirika hilo halitatoa tena matangazo yenye muelekeo wa kisiasa.

Dorsey amearifu kwamba uamuzi huo mpya utaanza kutumika mwishoni mwa mwezi Novemba.

Washindani wa mtandao wa kijamii wa Facebook hivi karibuni walifutilia mbali mpango wa kupiga marufuku matangazo ya siasa ya kibiashara.

Taarifa ya marufuku hiyo imeibua mgawanyiko katika kambi za kisiasa nchini Marekani zinapojiandaa katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Brad Parscale,meneja wa kampeni ya Raisi Donald Trump, kugombea muhula wa pili, amesema marufuku hiyo ni jaribio jingine la kumnyamazisha Trump
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images