Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu October 21


Rais Magufuli Afichua Siri ya Ukamataji Vigogo Waliopiga Bilioni 1.2 za Korosho

0
0
Rais John Magufuli amesema Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inawashikilia viongozi wa vyama vya ushirika 92 mkoani Mtwara kwa tuhuma za kuwadhulumu wakulima wa korosho Sh. bilioni 1.2.

Amesema fedha hizo ni malipo ya korosho katika msimu wa mwaka 2016 hadi 2017, amewaahidi wakulima hao watalipwa fedha zao.

Aliyasema hayo jana, Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati akiwaapisha viongozi aliowateua mwishoni mwa wiki.

“Juzi nilikuwa Mtwara, Brigedia Jenerali Mbungo (Kaimu Mkuu Takukuru) anafahamu tulikuta malalamiko sana ya baadhi ya watu waliodhulumiwa malipo yao ya korosho kuanzia mwaka 2016 hadi 2017,” alisema na kuongeza:

“Na vilikuwa ni vyama vya ushirika 10, baada ya kumwagiza Brigedia Jenerali, akakuta ni vyama vya ushirika 32 ambavyo vilikuwa vinawadhulumu watu. Tulidhani walikuwa wamedhulumu Sh. milioni 80 tukakuta wamezdhulumiwa zaidi ya Sh. bilioni 1.2.”

Rais Magufuli alisema Takukuru imeweza kuwashika viongozi wa Amcos 92 na mpaka juzi walipokuwa wanampatia taarifa (Rais Magufuli) zilikuwa zimerudishwa Sh. milioni 255, na kwamba zilizobakia zinaendelea kurudishwa.

Waziri Mhagama Azitaka Halmashuri Kuhakiki Taasisi Ndogo Za Fedha Kubaini Taasisi Zinazowaibia Wananchi

0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu , Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu Jenista  Mhagama , ameziagiza  halmashauri zote nchini kufanya uhikiki wa kina wa taasisi ndogo za kifedha zinazotoa mikopo  kwa wananchi na vikundi, ili kuzibaini  taasisi zinazowaibia Watanzania badala ya kuwanufaisha kiuchumi..

Waziri Mhagama ametoa agizo hilo, katika kilele cha Maonesho ya tatu ya Mifuko/ Programu za Uwezeshaji na Vikundi vya Kifedha vya Kijamii, yaliyofanyika Kitaifa katika  Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Oktoba 20, 2019.

“Ninajua baadhi ya taasisi ndogo za fedha badala ya kuwasaidia  wanachama zimekuwa ziifanya kazi ya kuiba fedha za wanachama  na kuwafanya wanachama warudi nyuma badala kusonga mbele, agizo hili Baraza la Taifa la Uwezesheshaji wananchi Kiuchumi mlifuatilie kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI,” alisema Mhagama.

Katika hatua nyingine ameitaka mifuko/programu za uwezeshaji wanachi kiuchumi kutoa mikopo kwa riba nafuu tofauti na taasisi nyingine za kifedha, ambapo amebainisha kuwa takribani wajasiriamali 1,237,984 wamenufaika na mikopo ya mifuko hiyo na hadi kufikia Juni 2019 jumla shilingi bilioni 388.4 zimetolewa.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga ametoa wito kwa Taasisi za kifedha kuhakikisha zinajibu changamoto za wananchi huku akiwataka wananchi (wajasiriamali) walioshiriki maonesho haya kutumia vema fursa walizoziona katika mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ili wakuze uchumi wao

Baadhi ya wanufaika wa mikopo wilaya ya Bariadi na Busega mkoani Simiyu na Chato Mkoani Geita  wamezishukuru Taasisi za kifedha zilizowakopesha mitaji jambo ambalo limewasaidia kuimarsisha shughui zao za kiuchumi wanazofanya ikiwa ni pamoja na kilimo na ufugaji.

“Naishukuru Benki ya AZANIA na wadhamini wangu Taasisi ya PASS kwa kuniwezesha kupata mkopo wa shilingi milioni 20, kuanzia sasa nitalima kisasa na nitaenda kuongeza miundombinu ya maji kwenye shamba langu maana nilikuwa nalima ekari 10 kwa kumwagilia badala ya ekari 30 nilizo nazo,” alisema Elisha Malugu kutoka wilayani Busega.

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi(NEEC) Dkt. Festus Limbu amesema NEEC inaendelea kufuatilia agizo la Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa alilolitoa Juni 2019 la kila mkoa kuwa na kituo cha uwezeshaji wananchi kiuchumi, lengo likiwa kuvifanya vituo hivyo kuwa kitovu cha uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi. Beng’ Issa amesema Maonesho haya yameshirikisha Taasisi 45, wajasiriamali zaidi ya 200 kutoka mikoa ya Simiyu, Mbeya, Pwani, Mwanza, Tabora, Kagera , Mara, Singida na Dar es Salaam na kutoka nchi jirani za Burundi na Kenya.

Maonesho ya tatu ya Mifuko/ Programu za Uwezeshaji na Vikundi vya Kifedha vya Kijamii chini ya Kauli Mbiu, “Mitaji ni Chachu ya Kujenga Uchumi wa Viwanda” yametanguliwa na maonesho ya kwanza yaliyofanyika Mbeya mwaka 2017, ambapo ya pili yalifanyika mwaka 2018  jijini Dodoma.

Tanzania Kunufaikana Mikopo Ya Kuendeleza Miradi Ya Miundombinu Kutoka Benki Ya ‘Asianinfrastructure Investment’.

0
0
Na Eva Valerian na Ramadhani Kissimba, Washington DC
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango(Mb) amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa ‘Asian Infrustructure Investment Bank’ Bw. Danny Alexander jijini Washington DC. 

Katika mazungumzo na Benki hiyo wamekubaliana kusaidia katika miardi endelevu ya Miundombinu kama Barabara na Reli.

Mazungumzo hayo ambayo pia yalihudhuriwa na Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Mhe.Mohammed Abdiwawa, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga na Naibu Gavana wa Benki Kuu, Dkt.Yamungu Kayandabila yalikuwa na lengo la kuangalia fursa ambazo Tanzania inaweza kunufaika kutoka katika Benki hiyo.

Punguzo la bei ya Viwanja: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

0
0

Kwa Mapinga vipo viwanja vya 15/20 bei tsh 3 milion, 20/20 kwa tsh 4 milion, 25/25 kwa tsh 7 milion, sqm 2000 kwa tsh 25 milion, sqm 2400 kwa tsh 30 milion.


Viwanja hivi viko umbali wa km 3 kutoka main road (Dar to Bagamoyo Road)

Kwa Bunju vipo viwanja vya sqm 1000 kwa tsh 30 milion na sqm 1750 kwa tsh 51 milion.

Biashara hii haina dalali/udalali na Ukipata ujumbe huu, mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.


Mpigie mhusika kwa 0758603077 au whatsap 0757489709

TPDC -Kuunganisha Gesi Asilia Katika Nyumba 400 Mwaka Huu

0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
SHIRIKA la Maendeleo ya Petrol Tanzania (TPDC) linatarajia kuunganisha nyumba 400 kupitia mradi wa kuunganisha gesi asilia majumbani ,ambapo kati ya nyumba hizo nyumba125 zitakuwa mkoa wa Mtwara na nyingine  mkoa wa Dar es Salaam.
 
Aidha mpaka sasa viwanda 45 vinafanya uzalishaji kwa kutumia gesi inayosambazwa na TPDC na miongoni mwa viwanda hivyo ni DANGOTE kilichopo mkoani Mtwara na Goodwill kilichopo Mkiu wilayani Mkuranga ,mkoani Pwani.
 
Mtaalamu mwandamizi wa masuala ya Petroli(Geologist)kutoka TPDC Simon Zablon,alisema hayo katika  maonyesho ya bidhaa za viwandani yanayoendelea kufanyika kwenye viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani Mjini Kibaha.
 
Alisema, nyumba hizo zinatarajiwa kukamilishwa mwishoni mwa mwaka huu.
 
Zabron alisema,katika upande wa  viwanda ambavyo vitanufaika na mradi huo ni kiwanda cha Lodhia, NAF na Cokacola .
 
“TPDC tupo tayari kutoa huduma ya gesi  kwa urahisi kwenye viwanda vyote vilivyopo katika Mikoa ya Mtwara na Dar es Salaam na ambavyo miundombinu ya bomba la gesi imepita”
 
Katika hatua nyingine, alifafanua magari yanayotumia gesi hadi sasa yamefikia 200, na  kwamba magari yanayounganishwa na huduma hiyo ni yale yaliyokuwa kwenye mfumo wa kutumia petroli.
 
Alisema, awali mradi wa kuunganisha gesi kwenye magari ulianza miaka saba iliyopita lakini ulikuwa unasuasua kutokana  muamko kwenye vituo vya mafuta kuwa mdogo .
 
Zabron alielezea pia kumetokana na kituo kimoja kilichokuwa Ubungo jijini Dar es salam pekee kutoa huduma hiyo tofauti na hali ilivyo sasa.

Serikali ya Tanzania na Barrick waunda Kampuni Mpya ya Kusimamia Madini inayochukua nafasi ya Kampuni ya Acacia.

0
0
Jitihada za Rais John Magufuli za kuhakikisha rasilimali za Tanzania zinalindwa, zimeanza kuzaa matunda baada ya serikali na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kuingia ubia na kuanzisha kampuni mpya ya Twiga Mining Co. Ltd inayochukua nafasi ya Kampuni ya Acacia.

Kampuni ya Twiga iliyosajiliwa nchini na makao yake makuu yatakuwa Mwanza, Serikali ya Tanzania itamiliki asilimia 16 na Barrick Gold Corporation itakuwa na asilimia 84.

Sasa ndio itakayosimamia migodi mitatu iliyokuwa inasimamiwa na Acacia ambayo ni Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara na itaendesha shughuli zake zote nchini.

Hatua hiyo, imekuja baada ya Kampuni ya Barrick kuizika rasmi Acacia na kufunga ofisi zake zilizokuwepo jijini London, na kufuta kesi na madeni yote ambayo kampuni hiyo ya Acacia iliyafungua dhidi ya serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi alisema hatua hiyo imeingiza Tanzania katika historia mpya ya ukombozi wa kiuchumi.

Alisema kuanzishwa kwa kampuni hiyo mpya sasa kumefuta migogoro yeyote iliyokuwepo baina ya serikali na Acacia ambayo hisa zake za asilimia 63.9 zote zilinunuliwa na hivyo kumilikiwa na Barrick Gold Corporation.

Alieleza kuwa pamoja na kufuta migogoro hiyo, pia wamekubaliana kuwa Barrick itailipa Tanzania kiasi cha dola za Marekani milioni 300 kwa ajili malipo ya kodi zote zilizokuwa haijalipwa na migogoro mingine.

Announcement For Australia Awards Scholarships Short Courses) For 2020/2021

0
0
Applications are invited qualified officials from Public & Private Institutions to apply for the above-mentioned training opportunities in Australia.

Applications are now open for the following Tenable Training Programs:-

Mode of Application:
• Application forms and other relevant documents can also be found on the relevant COUNTRY PAGE


• All applications should be submitted electronically as per instructions onthe Website


Closing dates for applications:
i. Short Course Awards: 17th January, 2020.
N.B: - Applications from people with disability are strongly encouraged.
- Applications from women are strongly encouraged.


Kwa taarifa zaidi, <<Bonyeza hapa>>

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Mbowe na Vigogo wengine CHADEMA

0
0
Viongozi 9 wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wanatarajia kuanza kujitetea kwa siku tatu mfululizo kuanzia November 4, 5 na 8, 2019 katika kesi ya uchochezi inayowakabili Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Hatua ya viongozi hao wanaokabiliwa na Kesi ya jinai namba 112 ya 2018 inatokana na uamuzi mdogo uliotolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo katika uamuzi huo Viongozi wa CHADEMA wamewakilishwa na Wakili, Jeremiah Mtobesya na Hekima Mwasipu, huku upande wa Serikali ukiwakilishwa na Wakili Faraja Nchimbi, Wankyo Simon na Salim Msemo.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Simba amesema wiki tatu zilizoombwa na upande wa utetezi ni nyingi  hivyo amewapatia wiki mbili ili waweze kuwaanda washtakiwa waanze kujitetea kabla ya mashahidi wao na kusema mashahidi katika kesi hiyo mbali na washtakiwa ni wengi na wanafikia 200, hivyo upande wa utetezi wanahitaji kupewa muda wa maandalizi.

Pia Hakimu Simba amesema kuhusu kielelezo namba 5 ambacho ni video ya maandamano kilichoombwa na upande wa utetezi ili Wataalamu wao wakichunguze kwa sababu wana wasiwasi kimehaririwa, watakitumia kupitia vifaa vya mahakama kama vilivyotumiwa na upande wa mashtaka.

Upelelezi kesi ya anayedaiwa kumuua mkewe kwa Kumchoma Moto Wakamilika

0
0
Hatimaye upelelezi wa kesi inayomkabili mfanyabiashara Khamis Said anayedaiwa kumuua na kisha kumchoma na moto wa magunia mawili ya mkaa mke wake, Naomi Marijani, na kisha mabaki ya mwili huo kwenda kuyafukia shambani kwake Mkuranga, umekamilika.

Wakili  wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai hayo leo Jumatatu Oktoba 21, 2019 mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kuwa shauri lilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi umekamilika.

Simon amedai jalada la shauri hilo lipo kwenye hatua ya uchapaji kwa ajili ya maandalizi ili lipelekwe Mahakama Kuu ya Tanzania hivyo ameiomba mahakama hiyo ihairishe kesi hiyo.
 
Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mkuu wa Mahakama hiyo, Salumu Ally, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 4, 2019.

Mshtakiwa huyo anadiwa kutenda kosa hilo Mei 15, 2019, nyumbani kwake maeneo ya Gezaulole Kigamboni.

Tanzania Yateuliwa Kuwa Mwenyeji Wa Mkutano Wa Mawaziri Sekta Za Mazingira, Maliasili Na Utalii SADC

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo amefungua mkutano wa Mawaziri wa Sekta za Mazingira, Maliasili na Utalii wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Arusha kaskazini mwa nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki, amesema kuwa, mkutano huo utajadili mwenendo wa hali ya mazingira, mabadiliko ya hali ya hewa na hali ya utalii na misitu katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Aidha amesema kuwa, mkutano huo utajadili utekelezaji wa mikakati ya hifadhi na usimamizi wa mazingira na kupitia mikakati na miongozo juu ya masuala hayo katika kutekeleza majukumu ya kila nchi ndani ya jumuiya hiyo ya SADC.

Wakati huo huo, Tanzania imekabidhiwa Uenyekiti wa Shirikisho la Mashauriano ya Kisheria la Asia na Afrika (Asian-African Legal Consultative Organization (AALCO) 58th Annual Session).

Mkutano huo umefunguliwa na mikutano ya Wataalamu wa Sekta ya Wanyamapori na mkutano wa Makatibu Wakuu wa Sekta za Mazingira, Maliasili na Utalii ulioanza leo Oktoba 21 hadi 24, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Mapema mwezi Agosti mwaka huu, nchi ya Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa 39 wa nchi wanachama wa Jumuiya ya maendelea ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Rais John Pombe Magufuli alikabidhiwa na kupokea rasmi jukumu la uenyekiti wa jumuiya hiyo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzindakaya Mkoani Rukwa ajisalimisha polisi kwa kubaka Wanafunzi Wawili na Kuwatia Mimba

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Rukwa kuhakikisha Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzindakaya iliyopo kata ya Kaengesa, Wilayani Sumbawanga Dastan Mlelwa anafikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo baada ya kuwabaka na kuwatia mimba wanafunzi wawili wa kidato cha pili na cha tatu katika shule hiyo.

Amesema kuwa anataarifa kuwa mwalimu huyo tayari amekwishajisalimisha katika mikono ya polisi na hivyo kumtaka kamanda wa polisi mkoa, Kamanda wa TAKUKURU mkoa pamoja na Mkuu wa Usalama wa mkoa kufuatilia jambo hilo ili mwalimu huyo asitoke kwenye mikono ya polisi bali apelekwe mahakamani.

“Hili jambo hatutalifumbia macho, Mkuu wa shule kuwatafuta wanafunzi kimapenzi na mpaka kuwatia mimba, yeye kama mzazi na mwalimu haikubaliki hata kidogo, huu ni ubakaji kwasababu wale wanafunzi wa kidato cha pili na cha tatu hawana umri wa miaka 18 ni chini ya hapo, ni ubakaji,” Alisisitiza.

Katika kusisitiza suala hilo pia ameitaka kamati hiyo kufuatilia kesi ya Mwalimu wa Shule ya Sekondari Mpui iliyoopo Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga aliyembaka na kumpa mimba mwanafunzi wa kidato cha pili na baadaye mwanafunzi huyo kuhamishwa katika shule ya Sekondari Mazwi iliyopo Manispaa ya Sumbawanga. 

Katika hatua nyingine Mh. Wangabo amewaagiza wajumbe hao wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa kufuatilia kesi ya wizi wa mifugo inayomhusisha Afisa mifugo wa mji mdogo wa laela, wilayani Sumbawanga Emanuel Tluwey baada ya kukamatwa akiwa anachinja ng’ombe wa wizi kesi ambayo ilifikishwa polisi na kuonya kuwa kesi hiyo isifinyangwe finyangwe ili mwizi huyo  asichukuliwe hatua.

“Lakini kuna Mazingira tata huenda kesi ikafinyangwa finyangwa na mwizi huyu asichukuliwe hatua, sasa narudisha kwa timu hii hapa, TAKUKURU yuko pale, jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama fuatilieni suala hili kule Laela huyu mwizi wa mifugo lazima achukuliwe hatua ya kisheria afikishwe mahakamani haraka iwezekanavyo,” Alisema.
 
Mh. Wangabo ameyasema hayo wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika kikao maalum kilichowajumuisha wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na watumishi wa seksheni ya Elimu na watumishi wa seksheni ya uchumi na uzalishaji inayojumuisha watumishi wa  mifugo katika Mkoa.

Mh. Wangabo amesema kuwa nia ya kuyafanya hayo ni kupiga vita uhalifu ndani ya mkoa pamoja na ubakaji wa wanafunzi na kuonya kuwa itafika wakati kutakuwa na kura za maoni mashuleni kwa wanafunzi ili kumbaini anayewashawishi wanafunzi hao kujiingiza katika suala la mapenzi katika umri mdogo.

IMETOLEWA NA
OFISI YA MKUU WA MKOA WA RUKWA

Wanafunzi wavalishwa maboksi Kichwani ili Kuzuia Wasiangaliziane

0
0
Chuo cha The Bhagat Pre-University College, kilichopo nchini India kimeomba msamaha kufuatia kitendo cha kuwavalisha maboksi, Wanafunzi ili kuzuia kupiga chabo wakati wa majaribio ya zoezi hilo.

Taarifa za chuo hicho kufanya tukio hilo, zilisambaa baada ya kupostiwa katika mtandao wa kijamii wa Facebook na mmoja wa wafanyakazi katika chuo hicho ambazo zilionesha wanafunzi wamevaa maboksi, huku sehemu ya mbele la maboksi hayo yapo wazi.

Msamamizi mkuu wa chuo hicho, MB Satish, amesema walitumia njia hiyo kukabiliana na udanganyifu wa kupiga chabo kwa wanafunzi na walifanya hivyo kama jaribio la muda tu kisha waliwatoa maboksi hayo kichwani.

"Hakuna mwanafunzi aliyelazimishwa kuvalia boksi kichwani. Kama unavyoona katika picha hizi kuna baadhi ya wanafunzi ambao hawajazivalia, Waliokuwa wamevalia pia baadhi yao walivua baada ya dakika 15, wengine baada ya dakika 20 na hata sisi wenyewe tuliwambia wazivue baada ya saa moja" amesema MB Satish

"Kati ya wanafunzi 72 ni 56 ndiyo walivaa maboksi kama sehemu ya majaribio, walisema wanajisikia vizuri na jaribio hilo na chuo hakijamsumbua mwanafunzi yeyote kuhusu suala la kuvaa maboksi hayo" ameongeza.

Mamlaka ya usimamizi wa shule nchini India iliamuru chuo hicho kutoa ufafanuzi wa maelezo na kuomba  msamaha juu jaribio hilo.

Mahakama yataka kesi ya aliyekuwa Mhasibu Mkuu Takukuru itendewe haki

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema haki itendeke katika kesi ya kumiliki mali ya zaidi ya Sh3.6 bilioni kinyume na kipato halali inayomkabili aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru),Godfrey GugaI na wenzake wawili kwa kuwa washtakiwa hao hawana dhamana.
 
Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba  ameeleza hayo leo Oktoba 21, 2019 wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kuendelea na ushahidi lakini upande wa mashtaka kupitia wakili wa Serikali Silivia Mitanto kudai kuwa kesi hiyo ilikuja kwa  ajili ya kuendelea na ushahidi lakini mawakili wanaosimamia kesi hiyo hawapo wapo mahakama ya mafisadi.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Simba alisema hajafurahi kuona kesi hiyo inaahirishwa kwani lazima waitendee haki  kwa sababu mashtaka yanayowakabili washtakiwa hayana dhamana.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 28 mwaka huu kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.

Nafasi 500 za Kazi Zilizotangazwa Mwezi Huu.....Tazama Hapa

0
0
Hapa nimekuwekea mkusanyiko wa Nafasi mbalimbali za Kazi Zilizotangazwa Wiki Iliyopita na Wiki Hii. Usisahau kushare na rafiki yako anayetafuta kazi
  1. Nafasi 61 za Kazi Shirika la Hifadhi ya Taifa TANAPA | Elimu ni Kuanzia Cheti/Diploma/Degree | Mwisho Tarehe 30 Mwezi Huu 
  2. Jobs at UNICEF | Individual Consultant -Evaluation of the Zanzibar Social Protection Policy  
  3. Project Finance Assistant Job at Sightsavers Singida, Tanzania
  4. Project Assistant Job at Sightsavers Singida, Tanzania 
  5. Compliance Manager at IntraHealth International Mwanza, TZ 
  6. Research and Innovation Hub Coordinator Job at International Rescue CommitteeDar es Salaam, TZ 
  7. Electrical Manager Job at Radar Recruitment Tanzania 
  8. Job Opportunity at VodacomTanzania, Network Director 
  9. Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL) Team Lead – Tanzania PS3+ 
  10. Job Opportunity at Abt Associates, Communications Team Lead 
  11. Jobs in Tanzania 2019 : New Job Opportunities at Mom Easy Company Limited | Sales Officers (15 Post) 
  12. Job Opportunity at Bariadi District Council | Mtendaji wa Kijiji Daraja la III 
  13. Jobs in Tanzania 2019: New Job Vacancies at Oxfam Tanzania| Donor Contracts Coordinator (INT5881) 
  14. Jobs in Tanzania 2019: New Job Vacancies at Oxfam Tanzania| Warehouse Officer (INT5995) 
  15. Technical Manager Job at Mbeya Water Supply and sanitation Authority 
  16. Job Opportunity at PCI Tanzania ,Documentation Specialist 
  17. Job Opportunity at Pact Tanzania,Gender and Youth Officer 
  18. Job Opportunity at Pact Tanzania, Technical Services Coordinator-Case Management 
  19. Job Opportunity at Pact Tanzania, Technical Services Coordinator-Bi-Directional Referrals and Linkages 
  20. Job Opportunity at Pact Tanzania, Logistic Assistant/Driver 
  21. Field Assistant Grade Ii Job at Tropical Pesticides Research Institute TPRI 
  22. Job Opportunity at UONGOZI Institute, Research And Policy Department (Intern) 
  23. Job Opportunity at UONGOZI Institute, Finance And Administration Department (Intern)

==Kwa nafasi zingine za Kazi zaidi ya 5000, <<INGIA HAPA>.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya October 22

Halmashauri Ya Wilaya Ya Msalala kinara ukusanyaji wa mapato ya ndani

0
0
HALMASHAURI ya Wilaya ya Msalala imekuwa ya kwanza Kitaifa katika ukusanyaji wa mapato kwa kukusanya asilimia hamsini na mbili (52%)  ya makisio ya mapato ya ndani kwa kipindi cha robo ya kwanza ya  mwaka wa fedha 2019/20 huku Halmashauri ya Kyerwa ikiwa ya mwisho kwa kukusanya asilimi tatu tu ya makisio yake.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo alipokuwa akitoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri kwa kipindi cha Julai – Septemba, 2019

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imefanikiwa kukusanya mara mbili ya malengo  ya robo ya kwanza ambapo kila halmashauri inatakiwa kukusanya si chini ya asilimia 25 ya makisio ili kukamilisha asilimia 100 kwa robo nne za mwaka wa fedha.

Waziri Jafo alieleza kuwa Bajeti iliyoidhinishwa ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2019/20 ni shilingi Bilioni 765.48; Katika kipindi cha robo ya kwanza (Julai hadi Septemba, 2019) Halmashauri zimekusanya jumla ya shilingi bilioni 166.24 sawa na asilimia 22 ya makisio ya mwaka.

Alifafanua kuwa “Katika kipindi hiki Halmashauri zilipaswa kukusanya asilimia 25 ya makisio yake ya mwaka lakini halmashauri hamsini na nne tu (54) ndio zilizofanya vizuri kwa kukusanya zaidi ya asilimia 25 ya bajeti zao na halmashauri 121 hazikuweza kufikisha asilimia 25 ya mapato yake”.

Aidha, Mhe. Jafo alisema kuwa katika kuzipima Halmashauri zote kwa pamoja Halmashauri ya Jiji la Dododma imekusanya mapato mengi zaidi kuliko Halmashauri zote kwa kukusanya shilingi Bilioni 13.10 na Halmashauri ya Buhigwe imekuwa ya mwisho kwa kukusanya shilingi Milioni 35.15.

Pia Mhe Jafo aliongeza kuwa katika ngazi ya Mikoa, Mkoa wa Rukwa umeongoza kwa kukusanya wastani wa asilimia thethini na moja (31) ya makisio ya Halmashauri za Mkoa huo huku Mkoa wa Mwisho ukiwa ni Mtwara ambao Halmashauri zake zimekusanya wastani wa asilimi kumi na tatu (13) ya makisio yake.

Alisema Katika kipengele hicho cha Mikoa kwa kuzingatia wingi wa mapato Mkoa ambao unaongoza kwa kukusanya mapato ya ndani kwa wingi ni Mkoa wa Dar es salaam ambao umekusanya shilingi Bilioni 39.53 na Mkoa wa Mwisho katika wingi wa ukusanyaji wa mapato ni Mkoa wa Kigoma ambao umekusanya shilingi bilioni 2.12.

Akisoma mchanganuo wa ukusanyaji wa mapato kwa kuzingatia aina ya Halmashauri na vigezo mbalimbali Mhe. Jafo amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam imeongoza kundi la Halmashauri za Majiji kwa kukusanya mapato kwa asilimia 38 ya makisio yake ya mwaka huku halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwa ya mwisho katika kundi hili kwa kukusanya kwa asilimia kumi na nane (18%) ya makisio yake ya mwaka.

Mhe. Jafo alitaja Halmashauri za Majiji zilizokusanya mapato ya ndani kwa kigezo cha wingi (Ghafi) kuwa Jiji la Dodoma limeongoza kwa kukusanya shilingi bilioni 13.098 na Halmashauri ya Jiji la Mbeya imekuwa ya mwisho katika kundi hili kwa kukusanya shilingi bilioni 2.74 tu.

Halkadhalika Jafo alitaja Manispaa iliyoongoza kundi la Halmashauri za Manispaa kwa kigezo cha asilimia kuwa ni Manispaa ya Sumbawanga ambayo imekusanya kwa asilimia arobaini na mbili (42) na Manispaa ya mwisho katika kigezo hiki ni Manispaa ya Kigoma ambayo imekusanya kwa asilimia tisa tu ya makisio yake kwa mwaka.

“Katika kigezo cha wingi wa mapato kundi hili linaongozwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ambayo imekusanya shilingi bilioni 13.05 huku Manispaa ya Kigoma ikiwa ya mwisho tena kwa kukusanya kiasi kidogo cha fedha cha shilingi milioni 235.11 alisema Jafo”.

Akifafanua kipengele cha Halmashauri za Miji Jafo alisema kuwa Mji wa Tunduma umeongoza kwa kukusanya kwa asilimia thethini na tisa (39%) na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekua ya mwisho kwa kukusanya asilimia nne (4%) ya makisio ya mapato yake ya ndani kwa mwaka.

Mhe. Jafo alisema kuwa Halmashauri ya Mji wa Geita imeendelea kuongoza kwa wingi wa mapato katika Halmashauri za Miji kwa kukusanya shilingi bilioni 2.34 na Halmashauri ya mwisho ni Mji wa Nanyamba ambayo imeksuanya shilingi milioni 74.72.

Wakati huo huo Jafo alizataja Halmashauri za Wilaya zilizofanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato kiasilimia kuwa ni Halmashauri ya Msalala ambayo imekusanya kwa asilimia hamisni na mbili (52%) na Halmashauri ya Kyerwa imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia tatu (3%) ya makisio ya mapato ya ndani kwa mwaka.

Upande wa wingi wa mapato Mhe. Jafo alitaja Halmashauri ya Wilaya iliyoongoza katika kundi hili kuwa ni Halmashauri ya Chalinze ambayo imekusanya shilingi bilioni 2.05 na ya mwisho ni Halmashauri ya Buhigwe iliyokusanya shilingi milioni thethini na tano (35) tu.

Jafo alisema kuwa katika matumizi ya mapato ya vyanzo vya ndani katika taarifa hii ya robo ya kwanza haionyeshi picha halisi ya uchangiaji wa mapato hayo katika shughuli za maendeleo kwenye sekta ya Elimu, Afya na Maji.

“Uchambuzi kamili wa uchangiaji wa kila halmashauri katika miradi ya maendeleo utafanyika katika robo ya pili na mwisho wa mwaka wa fedha 2019/20 lakini kila Halmashauri ifanye jitihada kuhakikisha inachangia mapato ya ndani kulingana na asilimia inayopaswa kuchangiwa kwa mujibu wa bajeti zake” Alifafanua Jafo.

Aidha, Mhe. Jafo alieleza kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba,2019 Halmashauri zilitumia shilingi Bilioni 40.88 kati ya shilingi bilioni 340.68 zilizokasimiwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo swan a asilimia 12.

Mhe. Jafo alikumbushia matumizi sahihi ya mifumo ya kielektroniki ya ukusanyaji wa mapato na mashine za kukusanyia mapato (PoSs) na mifumo ya Kielektroniki ya kutolea taarifa.

Alimalizia  kuwataka viongozi kuweka mikakati madhubuti ya kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo vipya vinavyobuniwa na Halmashauri zao.

(mwisho)

Waziri Dkt. Mwakyembe Aipongeza Taifa Stars

Waziri Jafo Awataka Wakurugenzi Wasiotimiza Ukusanyaji Mapato Kujitathimini.

0
0
Na.Faustine Galafoni.Dodoma.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa ma Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh.Selemani Jafo amewataka wakurugenzi wasiotimiza lengo la ukusanyaji mapato katika Halmashauri zao kujitathimini.

Waziri Jafo ameyasema hayo    Oktoba 21,2019 Jijini Dodoma  wakati akitoa taarifa ya mapato ya vyanzo vya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha Mwezi Julai hadi Septemba mwaka 2019. .

Waziri Jafo amesema kuwa katika kuzipima Halmashauri zote kwa pamoja katika kipindi hiki imeonyesha kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeongoza kwa ukusanyaji mapato kuliko Halmashauri zote kwa kukusanya Shilingi Bilioni 13.10,huku Mapato ya ndani kimkoa kwa kuzingatia wingi wa mapato Mkoa wa Dar es Salaam umeongoza kwa kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 39.53

Pia Waziri Jafo amesema licha ya Serikali kuagiza ukusanyaji wa mapato kufanyika kwa njia ya kielektroniki lakini bado kuna Changamoto kwani kuna baadhi ya maeneo wanakusanya fedha na hawazipeleki benki hivyo kuwaagiza wakuu wa mikoa kusimamia suala hilo.

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma imekuwa ya mwisho katika pato ghafi kwa kukusanya Milion 35 kwa kipindi cha miezi mitatu na hivyo kumtaka Mkurugenzi wa halmashauri hiyo pamoja wengine ambao hawajafanya vizuri kujitathimini huku uchambuzi ukionesha kuwa katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2019/20,Jumla ya Halmashauri 54 kati ya Halmashauri 185 zimefanya vizuri kwa kukusanya mapato ya ndani kwa zaidi ya asilimia 25 ya makisio ya mwaka wa Fedha 2019/20.

Askofu Ezekiel Yona wa kanisa la Morovian Jimbo la Magharibi apiga Marufuku kwa Makasisi wa kanisa hilo kutumia mafuta chumvi na maji katika maombi

0
0
NA SALVATORY NTANDU
Makasisi na Mashemasi  wa kanisa la morovian jimbo la Magharibi wametakiwa kutojihusisha na vitendo vya  udanganyifu vinavyofanywa na baadhi ya Watoa maombi ambao wamekuwa wakitumia chumvi na maji pamoja na mafuta kuwahadaa waumini wanao hitaji maombi badala yake wafuate maelekezo ya Yesu kristo aliyokuwa akiyatumia katika maombi.

Kauli hiyo imetolewa jana na Askofu wa kanisa la Morovian Ezekiel Yona wa Jimbo la Magharibi katika hafla maalum ya kuliweka wakifu wa jengo jipya la kanisa la moroviani la kahama mjini pamoja na kuwa kuwasimika mashemas 17.

Askofu Yona amewataka Makasisi hao kuepuka maombezi yanayokwenda kinyume na taratibu mungu na badala yake wafuate taratibu na miongozo ya kanisa hilo ambayo ni mafundisho ya kristo ili kuendelea kutangaza habari njema kwa watu wote.

“ Kinachonitatanisha ni kitu kimmoja sasa hivi wapo baadhi ya  watoa huduma za maombi wanaowanywesha mafuta waumini wao na kisha wanaanguka chini na baadae wanawaombea na kuamka,vitendo hivi msivifanye na havikubaliki katika kanisa la Mungu”alisema Askofu Yona.

Katika hatua nyingine Askofu Yona amewataka Makasisi hao kuendelea kuliombea Taifa ili amani iendelee kudumu sambamba na kumwombea Rais John Pombe Magufuli ili aendelee kuwatetea wanyonge sanjari na kurudisha nidhamu serikalini kwa kusimamia rasilimali za nchi.
  
Nao baadhi ya Makasisi wapya waliopewa daraja hilo, Emanuel Sangosango kutoka Kanisa la Morovian kituo cha (SAUTI)Mwanza na Yona Mbogo wa kanisa la Morovian kituo Singida wameahidi kuwa waaminifu katika utoaji wa huduma kwa waumini wao pamoja na kujiepusha na maombi yasiyofuata mafundisho ya Mungu.

Wamesema wapo baadhi ya Wachungaji ambao wanatumia vitu kama vile mafuta, chumvi na maji kuwahadaa waumini wao ili kupona magonjwa mbalimbali waliyonayo jambo ambalo sio la kweli na kutoa rai kwa waumini kuepuka maombi ya namna hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images