Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiswahili chapendekezwa kutumika Ukanda wa Maziwa Makuu

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Brazzaville,
Katika jitihada za kukuza lugha ya Kiswahili barani Afrika, Tanzania imeziomba nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu kuanza kutumia lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi na lugha ya kazi
 
Wito huo umetolewa katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu, uliofanyika mjini Brazzaville leo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro  
 
"Tumewaomba wenzetu wa maziwa makuu wakubali lugha ya Kiswahili kutumika kama lugha rasmi na lugha ya kazi katika nchi zote za maziwa makuu. Pia nchi sita ambazo zipo hapa na hazijaridhia mabadiliko ya mkataba wa Afrika kuruhusu Kiswahili kutumika kama lugha rasmi katika Afrika (AU) nchi hizo zimetuhakikishia kuwa zitaridhia mabadiliko hayo ili kuhakikisha kuwa Kiswahili kinaanza kutumika kama lugha rasmi ya kazi," Alisema Dkt. Ndumbaro
 
Kwa mujibu wa Waziri Ndumbaro, matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ukanda huo ni fursa ambayo italeta umoja wa kitaifa, na katika ukanda wa maziwa makuu lakini pia umuhimu wa Kiswahili kwamba ni lugha pekee ambayo haina uhusiano na ukoloni barani afrika. 
 
"Tunatumaini kwamba tutazipata sahihi za nchi sita na tukisha zipata tutabakiwa na sahihi ya nchi moja tu ili Kiswahili kiwe rasmi lugha ya kazi katika mikutano itakayo kuwa inafanyika barani Afrika," aliongeza Dkt. Ndumbaro 
 
Nchi sita ambazo hazijaridhia mabadiliko ya mkataba wa Afrika kuhakikisha kuwa Kiswahili kinatumika kama lugha rasmi ya kazi ni pamoja na Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sudani, Uganda na Zambia. 
 
Kwa sasa hivi ni lugha rasmi lakini siyo lugha ya kazi kwa hiyo tumekwenda vizuri kwenye Kiswahili tunaamini ni fursa nzuri ya kuanza kukuza lugha ya Kiswahili katika bara la Afrika
 
Wakati huo huo, Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa, katika mkutano huo nchi wanachama waliweza kuongelea agenda kuu za nchi wananchama wa ukanda wa maziwa makuu ambazo ni Amani, Utulivu na Usalama hususani katika eneo la mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
 
Sanjari na hilo, nchi nyingi zimeusifu uongozi wa Rais wa DRC, Felix Tshisekedi kuwa tangu alipoingia madarakani amejitahidhi kuhakikisha kuwa kuna kuwa na amnai ndani ya DRC pamoja na majirani zake. Pia Uganda, Rwanda pamoja na Angola zimesifiwa kufanikisha kusaini makubalianao ya kuleta amanai kati ya Uganda na Rwanda.
 
Akiongea awali wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje Mgeni rasmi ambae alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kongo, Bwn. Clement Mouamba alisema kuwa mkutano wa leo, umelenga kuisaidia nchi ya DRC katika changamoto inazopitia hasa katika ukanda wa mashariki.
 
"Nawapongeza sana kwa kazi ambayo mmekuwa mkiifanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha kuwa ugonjwa wa ebola unatokomezwa, kwani naamini kuwa umoja wetu tunaweza," alisema Mouamba.
 
Aliongeza kwa kuzitaka nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu kuendelea kulinda amanai na umoja walionao ili kuweza kuendelea na shughuli mbalimbali za maendeleo kwani bila amani ni vigumu sana kwa umoja huo kuendelea.
 
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianao wa Jamhuri ya Kongo, ambae pia alikuwa mwenyekiti wa mkutano huo Mhe. Jean Claude Gakosso aliwasisitiza mawaziri wa nchi wanachama kuwa amani na umoja katika ukanda huo ni nguzo muhimu sana na hivyo waendelee kuishika amani hiyo.
 
Pia aligusia ugonjwa wa ebola na kuwataka nchi wanachama kutokata tama ya kupambana na ugonjwa huo licha ya changamoto zinazojitokeza. 
 
"Juhudi mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ya DRC hadi sasa kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) pamoja na wadau wengine katika kupambana na ugonjwa huo ni kutoa chanjo ya kinga ya ugonjwa huo na elimu kwa wananchi wa maeneo yaliyoathirika na ugionjwa huo" alisema Waziri Gakosso.
 
Mkutano wa leo ulitanguliwa na mikutano miwili ambayo ilianza tarehe 11 hadi 14 Oktoba 2019, jijini Brazzaville ambapo pamoja na mambo mengine ilijadiliwa suala la ugonjwa wa ebola na hali ya amani katika maeneo yenye mlipuko wa ugonjwa huo.
 
Nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu ni pamoja na Angola, Burundi, Jamhuri ya Kati, Demokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kongo, Kenya, Rwanda, Sudan, Sudani Kusini, Tanzania, Uganda na Zambia.
 
Mwezi Augusti, 2019 Umoja wa Maendeleo ya Nchi za Ukanda wa Kusini mwa Africa (SADC) ulifanyika Tanzania Jijini Dar es Salaam nchi wananchama waliridhia na kuipitisha kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya Umoja huo baada ya Kiingereza, Kireno na Kifaransa.
Mwisho……

Waziri wa Fedha Dr Mpango: Benki Ya Dunia Iwekeze Fedha Kwenye Miradi Ya Kimkakati Ya Serikali

$
0
0
Na Eva Valerian na Ramadhani Kissimba, Washington Dc
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) ameiomba Benki ya Dunia-WB iwatume wataalam wake nchini Tanzania ili waainishe miradi mikubwa ya kimkakati inayotakiwa kutekelezwa kati ya Sekta Binafsi na Umma (PPP) badala ya taasisi hiyo ya Fedha Duniani kutaka Serikali itekeleze miradi midogo isiyo na tija kubwa kwa Taifa

Dkt. Mpango ametoa ushauri huo Mjini Washington DC nchini Marekani baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Afrika Bw. Hafez Ghanem ambapo aliwasilisha miradi mbalimbali ambayo Serikali inatekekeleza na ambayo ameiomba Benki hiyo isaidie rasilimali fedha.

‘’Nisingependa kuona Taasisi kubwa ya Kifedha kama Benki ya Dunia inakimbilia kufadhili utekelezaji wa vimiradi vidogo vya kujenga hostel au hotel za nyota tano; Kwa sasa nchi yetu inahitaji kujikita zaidi katika miradi mikubwa  ambayo itawaletea maendeleo ya haraka wananchi wetu’’ alisisitiza Mhe.Mpango.

Mhe. Mpango aliendelea kusisitiza kuwa kwa sasa Tanzania inatekeleza miradi mikubwa na inayohitaji fedha nyingi kuikamilisha, hivyo ni vyema Benki hiyo ikajielekeza katika kusaidia utekelezaji wa miradi hiyo.

Dkt. Mpango alianisha miradi kama ya Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), Ujenzi wa Bwawa la kuzalisha Umeme la Julius Nyerere katika Mto Rufiji mkoani Pwani, Mradi wa Ujenzi wa Reli kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay, Mchuchuma na Liganga ambako kuna rasilimali kubwa ya Madini ya Chuma na Makaa ya Mawe.

Aidha Dkt. Mpango alisema katika kutekeleza vyema miradi ya PPP Serikali imejikita katika mambo mawili moja ni kuwa na programu ya kujenga uwezo kwa maana ya wataalamu wa kuitambua hiyo miradi lakini pia, kuwa na uwezo wa kufanya uchambuzi wa kina ili kujenga uwezo wa majadiliano na Sekta Binafsi katika utekelezaji wa miradi hiyo.

‘’Nimewahimiza kwamba; kama kweli tunataka kutekeleza kwa ufanisi mpango wa ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi (PPP) ni lazima tutekeleze miradi mikubwa, na kwa kuanzia, wangekuja kuanza kutekeleza ule mradi wa kujenga reli ya kutoka Mtwara kwenda Mbaba-Bay, Mchuchuma hadi Liganga’’ alisema Mhe.Mpango.

Aliongeza kuwa ukamilishaji wa ujenzi wa reli hiyo utasaidia kuchochea kwa kasi maendeleo ya nchi  kutokana na rasilimali zilizopo katika maeneo inapopita reli hii.

Dkt. Mpango alimshukuru Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Bw. Hafez Ghanem kwa kukubali maombi mengi kutoka Tanzania ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

MWISHO

Announcement For Australia Awards Scholarships Short Courses) For 2020/2021

$
0
0
Applications are invited qualified officials from Public & Private Institutions to apply for the above-mentioned training opportunities in Australia.

Applications are now open for the following Tenable Training Programs:-

Mode of Application:
• Application forms and other relevant documents can also be found on the relevant COUNTRY PAGE


• All applications should be submitted electronically as per instructions onthe Website


Closing dates for applications:
i. Short Course Awards: 17th January, 2020.
N.B: - Applications from people with disability are strongly encouraged.
- Applications from women are strongly encouraged.


Kwa taarifa zaidi, <<Bonyeza hapa>>

Kiboko Ya Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
WET 3 POWER ni dawa bora ya vidonge asilia hutibu tatizo la nguvu za kiume na huanza kufanya kazi baada ya (dk 30 )  1. Huongeza nguvu za kiume mara dufu 
(2) Huimarisha misuli   pia  hii Itakufanya ufurahie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) bila kuchoka na kurefusha  kwa saizi uipendayo

Pia ninadawa yakutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma , kutokupata choo vizuri, ngiri na busha bila kupasuliwa . 

DARU MIX; ni dawa bora ya mitishamba yenye uwezo mkubwa wa kutibu ugonjwa wa KISUKARI kwa muda mfupi ( 1) hutibu ugonjwa wa kisukari haraka sana.
(2) Inaponya ugonjwa wa KISUKARI  kwa mtu aliyeugua kwa muda mrefu.
(3) Hurekebisha kongosho katika utoaji wa ute mchungu katika kuzalisha insulini na sukari kuwa normal (4-5-6) dozi yake ni ya siku 14 tu na mgonjwa kupona kabisa.

FIKA KATIKA OFISI YETU ILIYOPO MBAGALA ZAKHEM WASILIANA NA DR OMARY KWA SIMU NAMBA  0656551093 / Whatsapp namba 0689213043  

KWA WALIOKO MBALI HUDUMA HII INAKUFIKIA HAPO HAPO ULIPO TZ NA NJE YANCHI

Waziri wa Fedha Dkt. Mpango Aitaka Benki Ya Dunia Kusaidia Sekta Ya Kilimo Nchini Tanzania

$
0
0
Na Ramadhani Kissimba na Eva Valerian, Washington Dc
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango (Mb) ameitaka Benki ya Dunia kujikita zaidi katika kusaidia sekta ya kilimo nchini Tanzania ili kuweza kuwainua kiuchumi wakulima hasa wale wa kati na wadogo.

Dkt.Mpango aliyasema hayo wakati wa kikao cha majadiliano na timu nzima ya Benki ya Dunia ambayo inafanya kazi nchini Tanzania na wengine kutoka Makao Makuu ya Benki hiyo nchini Marekani.

Mhe.Mpango alisema katika mkutano huo  walipitia kwa pamoja utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea hivi sasa  inayofadhiliwa na Benki ya Dunia,  lakini pia walipitia na kujadili miradi ambayo inaanza kufikiriwa kwa ajili ya utekelezaji kwa mwaka utakaofuata.

‘’Moja ya vitu vilivyonifurahisha mwaka jana kwenye mjadala niliwaaomba sana kwamba hatuwezi kuendelea kuitaka Benki ya Dunia isaidie kwenye miradi mingine tu ni lazima nguvu kubwa ielekezwe pia kwenye miradi ya kilimo ambayo kwa sasa  msaada wa Benki ya Dunia katika miradi hiyo ni kidogo sana’’ alisema Dkt.Mpango.

Aidha Dkt.Mpango alielezea dhamira ya Tanzania kushirikiana na Benki ya Dunia ili kuanzisha programu itakayohakikisha kuwa tija inapatikana kwenye sekta nzima ya kilimo na mifugo, lakini pia kuweza kuyafikia masoko kwa mazao yanayozalishwa nchini, hasa yale yenye thamani kubwa duniani.

 Dkt. Mpango amefafanua kuwa Benki ya Dunia imeridhishwa na kasi ya mabdiliko inayofanyika katika sekta ya kilimo kwa maana ya uzalishaji kuongezeka, lakini vile vile  wakulima wa kati wamezidi kuongezeka.

Aidha, kuongezeka kwa maeneo ya kilimo imewafurahisha wataalamu wa Benki hiyo, ikiwa ni pamoja na  kuongezeka kwa aina ya mazao yanayolimwa   hasa yale yenye thamani kubwa ambayo yanalimwa  kwa kasi kubwa sana kuliko ilivyokuwa awali.

Pia Dkt. Mpango alisisitiza kuwa, Benki ya Dunia imeshafanya utafiti wao wa kutosha ambao umeonesha kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo kwa maana ya uzalishaji kuongezeka.

Mhe. Mpango aliishukuru Benki ya Dunia kwa kukubali tena kuleta timu ya wataalamu nchini Tanzania ambayo itakaa na sekta nzima ya kilimo na ufugaji ili kuona ni namna gani hasa Benki ya Dunia itasaidia kuinua sekta hiyo, na  kuwasaidia wakulima hasa katika matumizi ya nguvu kazi kwa upande mmoja na kuwaongezea kipato kwa upande mwingine.

Mwisho

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Waziri wa Fedha Dkt. Mpango Aitaka Benki Ya Dunia Kusaidia Sekta Ya Kilimo Nchini Tanzania

$
0
0
Na Ramadhani Kissimba na Eva Valerian, Washington Dc
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango (Mb) ameitaka Benki ya Dunia kujikita zaidi katika kusaidia sekta ya kilimo nchini Tanzania ili kuweza kuwainua kiuchumi wakulima hasa wale wa kati na wadogo.

Dkt.Mpango aliyasema hayo wakati wa kikao cha majadiliano na timu nzima ya Benki ya Dunia ambayo inafanya kazi nchini Tanzania na wengine kutoka Makao Makuu ya Benki hiyo nchini Marekani.

Mhe.Mpango alisema katika mkutano huo  walipitia kwa pamoja utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea hivi sasa  inayofadhiliwa na Benki ya Dunia,  lakini pia walipitia na kujadili miradi ambayo inaanza kufikiriwa kwa ajili ya utekelezaji kwa mwaka utakaofuata.

‘’Moja ya vitu vilivyonifurahisha mwaka jana kwenye mjadala niliwaaomba sana kwamba hatuwezi kuendelea kuitaka Benki ya Dunia isaidie kwenye miradi mingine tu ni lazima nguvu kubwa ielekezwe pia kwenye miradi ya kilimo ambayo kwa sasa  msaada wa Benki ya Dunia katika miradi hiyo ni kidogo sana’’ alisema Dkt.Mpango.

Aidha Dkt.Mpango alielezea dhamira ya Tanzania kushirikiana na Benki ya Dunia ili kuanzisha programu itakayohakikisha kuwa tija inapatikana kwenye sekta nzima ya kilimo na mifugo, lakini pia kuweza kuyafikia masoko kwa mazao yanayozalishwa nchini, hasa yale yenye thamani kubwa duniani.

 Dkt. Mpango amefafanua kuwa Benki ya Dunia imeridhishwa na kasi ya mabdiliko inayofanyika katika sekta ya kilimo kwa maana ya uzalishaji kuongezeka, lakini vile vile  wakulima wa kati wamezidi kuongezeka.

Aidha, kuongezeka kwa maeneo ya kilimo imewafurahisha wataalamu wa Benki hiyo, ikiwa ni pamoja na  kuongezeka kwa aina ya mazao yanayolimwa   hasa yale yenye thamani kubwa ambayo yanalimwa  kwa kasi kubwa sana kuliko ilivyokuwa awali.

Pia Dkt. Mpango alisisitiza kuwa, Benki ya Dunia imeshafanya utafiti wao wa kutosha ambao umeonesha kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo kwa maana ya uzalishaji kuongezeka.

Mhe. Mpango aliishukuru Benki ya Dunia kwa kukubali tena kuleta timu ya wataalamu nchini Tanzania ambayo itakaa na sekta nzima ya kilimo na ufugaji ili kuona ni namna gani hasa Benki ya Dunia itasaidia kuinua sekta hiyo, na  kuwasaidia wakulima hasa katika matumizi ya nguvu kazi kwa upande mmoja na kuwaongezea kipato kwa upande mwingine.

Mwisho

Waombaji 30,675 Bodi ya Mikopo wapata mkopo elimu ya juu awamu ya kwanza.

$
0
0
Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (Heslb) imetangaza orodha ya kwanza ya majina ya  wanafunzi 30,675 wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo kwa ajili ya mwaka wa masomo wa 2019/2020 yenye thamani ya Sh113.5 bilioni.

Kati ya idadi hiyo, wanaume ni 19,632 sawa na asilimia 64 ya waliopata mikopo awamu ya kwanza.

kurugenzi Mtendaji wa Heslb, Abdul-Razak Badru amesema orodha iliyotolewa leo ni ya kwanza lakini mchakato wa kuwapangia wanafunzi mikopo utaendelea kulingana na uhitaji na uchambuzi wa taarifa za wanafunzi wanaodahiliwa vyuoni.

Katika mwaka wa fedha wa 2019/2020, Serikali imetenga Sh450 bilioni kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu, ikiwa imeongezeka kutoka Sh427 bilioni zilizotengwa mwaka uliopita.

Badru amesema Sh125 bilioni tayari zimetolewa na Serikali ili kugharimia mkopo kwa awamu ya kwanza, ambapo Sh116 bilioni zimetengwa kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka kwanza ambao wataanza masomo hivi karibuni.

Hata hivyo, amesema awamu ya pili ya waliopata mikopo itatangazwa wiki ijayo kabla ya Oktoba 25, baada ya kukamilisha uchambuzi wa maombi ya mikopo kwa wanafunzi waliochelewa kukamilisha taratibu za udahili vyuoni na maombi ya mkopo mtandaoni.

Wanafunzi waliopata mikopo wanatakiwa kuingia katika akaunti zao walizotumia kuomba mikopo hiyo.


Tembelea <<HAPA >> Kwa taarifa zaidi


Waombaji 30,675 Bodi ya Mikopo wapata mkopo elimu ya juu awamu ya kwanza.

$
0
0
Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (Heslb) imetangaza orodha ya kwanza ya majina ya  wanafunzi 30,675 wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo kwa ajili ya mwaka wa masomo wa 2019/2020 yenye thamani ya Sh113.5 bilioni.

Kati ya idadi hiyo, wanaume ni 19,632 sawa na asilimia 64 ya waliopata mikopo awamu ya kwanza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Heslb, Abdul-Razak Badru amesema orodha iliyotolewa leo ni ya kwanza lakini mchakato wa kuwapangia wanafunzi mikopo utaendelea kulingana na uhitaji na uchambuzi wa taarifa za wanafunzi wanaodahiliwa vyuoni.

Katika mwaka wa fedha wa 2019/2020, Serikali imetenga Sh450 bilioni kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu, ikiwa imeongezeka kutoka Sh427 bilioni zilizotengwa mwaka uliopita.

Badru amesema Sh125 bilioni tayari zimetolewa na Serikali ili kugharimia mkopo kwa awamu ya kwanza, ambapo Sh116 bilioni zimetengwa kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka kwanza ambao wataanza masomo hivi karibuni.

Hata hivyo, amesema awamu ya pili ya waliopata mikopo itatangazwa wiki ijayo kabla ya Oktoba 25, baada ya kukamilisha uchambuzi wa maombi ya mikopo kwa wanafunzi waliochelewa kukamilisha taratibu za udahili vyuoni na maombi ya mkopo mtandaoni.

Wanafunzi waliopata mikopo wanatakiwa kuingia katika akaunti zao walizotumia kuomba mikopo hiyo.

Tembelea <<HAPA >> Kwa taarifa zaidi

Tembelea Ivigo Herbal Clinic: Kituo Cha Tiba Asili Na Tiba Mbadala Kwa Magonjwa Ya Binadamu

$
0
0
IVIGO HERBAL CLINIC ni Kituo cha Tiba Asili na Tiba Mbadala kwa Magonjwa ya Binadamu ikiwemo Kisukari, presha, Nguvu za Kiume, Vidonda vya Tumbo, Tambazi, MATATIZO ya Uzazi, BAWASIRI, Muwasho sehemu za siri, Miguu kuvimba, UVIMBE Tumboni, Tezi Dume, SHINGO ya KIZAZI kwa Akinamama ,Meno bila  kung'oa, Maumivu ya Mgongo na kiuno , Kuborsha Maumbile ya Kiume pamoja na MATATIZO Mbalimabali ya Kimaisha.

Kwa Huduma zetu Tembelea Vituo vyetu ulichokaribu nacho. MBEYA tupo barabara ya ISANGA kabla hujafika Darajani simu 0744687649, Mbarali KITUO KIPO IGAWA STAND YA BARABARA KUU YA KWENDA MBEYA SIMU 0767007704, DODOMA KITUO KIPO CHANG'OMBE STAND simu  0746906010 na Makao Makuu NJOMBE simu 0767944041.Nyote Mnakaribishwa IVIGO HERBAL CLINIC kwa Tiba  Bora

Waziri Mkuu Aagiza Wakurugenzi Wawili Waripoti Dar Kesho Asubuhi

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama na Mkurugenzi wa Umwagiliaji wa Kanda ya Kusini, wafike ofisini kwake Dar es Salaam kesho asubuhi na taarifa kuhusu skimu wa umwagiliaji wa Narunyu.

Ametoa agizo hilo leo mchana (Alhamisi, Oktoba 17, 2019) wakati alipoenda kukagua skimu hiyo ambayo imekuwa ikilalamikiwa tangu 2017. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama ni Bw. Warioba Gunze na Mkurugenzi wa Umwagiliaji wa Kanda ya Kusini, ni Mhandisi Mndeme.

Amechukua uamuzi huo baada ya kufika eneo la mradi na kupokea malalamiko ya wanajumuiya ya umwagiliaji kutoka kwa Mwenyekiti wao, Bw. Bakari Awadhi juu ya kusuasua kwa mradi huo lakini alipotaka apate maelezo ya wataalamu hakuna hata mmoja ambaye alikuwepo.

"Nilitaraji niwakute hapa Mkurugenzi wa Halmashauri, Afisa Umwagiliaji wa Wilaya na Mkurugenzi wa Umwagiliaji wa Kanda. Nimeagiza wanikute uwanja wa ndege Lindi au Dar es Salaam na kesho asubuhi waje ofisini kwangu wanipe taarifa kamili ya mradi huu. Nataka nijue fedha zilizobakia zaidi ya sh. milioni 240 ziko wapi."

"Walipaswa niwakute hapa wananisubiri kwa sababu nilitoa taarifa tangu jana kwamba nitapita hapa. Nimepata taarifa kwamba wamesafiri kutoka Mtwara na leo asubuhi walikuwepo Lindi mjini. Waje ofisini kesho, wakishindwa, nitachukua maamuzi mengine," amesema.

Akielezea umuhimu wa mradi huo wakati akizungumza na baadhi ya wanaushirika waliokuwepo, Waziri Mkuu amesema ni wa muhimu kwa sababu unatiririsha maji wakati wote. "Huu ni mradi wa kuringia. Mradi huu unatiririsha maji wakati huu wa kiangazi, tena mengi tu."

Amesema kutokana na umuhimu wa mradi huo, hivi sasa wangekuwa wanazalisha mazao ya kila aina. "Hapa ni mahali pa kuzalisha mazao mengi, leo unalima mahindi, ukivuna unapanda matikiti, ukitoa unapanda nyanya. Sasa nitapasimamia mwenyewe," amesisitiza.

Amewataka wanaushirika wanaounda jumuiya ya umwagiliaji wahakikishe kila mmoja anatambua eneo lake na mara kazi ikianza wawe tayari kuanza kilimo. "Huu mradi una manufaa kwa watu wa Ruo, Mahumbika hadi Mnazi Mmoja. Lazima tuung'ang'anie kwa sababu kuna idadi kubwa ya wakulima wanaoutegemea. Huu mradi lazima tuuvalie njuga."

Waziri Mkuu alipofika uwanja wa ndege wa Lindi, maafisa hao walikuwa hawajafika kwa sababu simu zao hazikupatikana, na akaagiza waje Dar es Salaam kesho asubuhi.

Mapema, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Bw. Shaibu Ndemanga alimweleza Waziri Mkuu kwamba katika mafaili aliyoyapitia ofisini kwake alibaini kwamba mradi huo ulitengewa sh. milioni 788 ambapo mkandarasi wa kwanza Chest Investments Company alilipwa sh. milioni 121 lakini akashindwa kazi.

"Mkandarasi wa pili ambaye ni D & L naye alilipwa zaidi ya shilingi milioni 400 naye pia akashindwa kazi ya kuondoka tope. Kwenye ripoti, inaonesha zilibakia sh. milioni 249," alisema.

Naye Mwenyekiti wa wanajumuiya ya umwagiliaji ya Narunyu, Bw. Bakari Awadhi alisema skimu hiyo yenye ukubwa hekta 1,200 imekuwa ikijaa maji na kufunika mitaro na hatimaye kujaa mchanga.

Alimwomba Waziri Mkuu awasaidie kuifufua skimu hiyo kwa sababu inawanufaisha wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Taarifa Kwa Umma Kutoka Ofisi Ya Bunge

Waziri Mkuu Akagua Ofisi Za Halmashauri Mtama

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua ofisi za muda za Halmashauri ya Mtama na kusema ameridhika na maandalizi aliyoyakuta.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Alhamisi, Oktoba 17, 2019) wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa Halmashauri hiyo pamoja na wazee wa kijiji cha Mtama kwenye ukumbi wa mikutano jirani na ofisi ya mbunge wa jimbo la Mtama.

"Nimeridhika na jitihada zenu za kuja kuandaa ofisi na kufanya usafi ili kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais. Lakini pia nimefarijika na uamuzi wenu wa kujitolea eneo la ekari 100 la kujenga Halmashauri yenu," amesema.

Amewataka watumishi hao wahamasishe ujenzi wa nyumba bora na kuhimiza usafi kwenye makazi ya watu ili mji wao uendane na hadhi ya makao makuu ya wilaya.

Hamasisheni ujenzi wa nyumba bora ili pawe na nyumba zenye muonekano wa Halmashauri mpya. Lakini Bwana Afya simamia usafi kuanzia stendi kule.

Halmashauri sasa pimeni viwanja. Pato la ndani la Halmashauri yenu mtalipata kwa kupima viwanja sababu vinauzika. Lazimapawe na mpangilio wa makazi, majengo kadhaa na maeneo ya biashara," amesisitiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amemwagiza Katibu Tawala wa Wilaya ya Lindi, Bw. Thomas Safari asimamie vizuri fedha za wilaya hiyo ili baadhi ya watumishi wasifuje fedha za Halmashauri.

"Hakikisha watu hawatumii fursa hii kufuja fedha za Halmashauri. Hamisha fenicha watu waanze kazi hapa. Tunahamisha Halmashauri kuja hapa, watumishi msilale Lindi, bali mlale Mtama."

Naye Mbunge wa Mtama, Bw. Nape Nnauye alimweleza Waziri Mkuu kwamba tangu Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli atoe agizo la kuhamishia makao makuu ya Halmashauri ya Mtama hapo Mtama,  wamekuwa na vikao mbalimbali na wamefanikiwa kupata ekari 100 ambazo wananchi wamejitolea bure.

"Tumekuwa na vikao mbalimbali na jioni tutakuwa na kikao na wazee wa hapa ili kuwajulisha mchakato mzima. Kesho tutakuwa na mkutano mkubwa na wananchi. Lengo letu ni kuhakikisha tunapunguza gharama kwa kiasi kikubwa," alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Wastaafu Wakabidhi Mapendekezo Ya Kuboresha Zaidi Sekta Ya Mifugo Nchini

$
0
0
Na. Edward Kondela
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amepokea mapendekezo ya wataalamu wa mifugo wastaafu na wadau wa sekta ya binafsi yaliyotolewa ili kuboresha zaidi sekta ya mifugo nchini.

Akizungumza wakati akimkabidhi Katibu Mkuu Prof. Gabriel mapendekezo hayo katika ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo jijini Dar Es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati Teule ya wajumbe sita Dkt. Jonas Melewas, amemwambia katibu mkuu huyo kuwa mapendekezo yaliyotolewa ni Sita na kamati anayoingoza ambayo yanatokana na maazimio 14 yaliyotolewa kwenye kikao kilichofanyika Tarehe 7 Mwezi Oktoba 2019.

Dkt. Melewas ametaja mapendekezo hayo sita kuwa ni: Kusimamia tozo mbalimbali ikiwemo ya zao la ngozi na kuimarisha usimamizi wa Sheria na Kanuni kwa kuboresha mifumo ya ukaguzi ya uendeshaji, uzalishaji na biashara katika sekta ya mifugo.

Aidha Dkt. Melewas amefafanua pendekezo la tatu ni matumizi sahihi ya dawa za uogeshaji kudhibiti kupe na magonjwa yaambukizwayo na kupe kuzuia usugu na hasara kwa wafugaji.

Amebainisha mapendekezo mengine ni udhibiti wa magonjwa ya mifugo, kuongeza uzalishaji na tija katika ufugaji mbari za mifugo, mifumo ya ufugaji, uvunaji, biashara na masoko.

Akipokea mapendekezo hayo Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amesema wizara itatumia taratibu mbalimbali kuhakikisha mapendekezo yaliyotolewa na wastaafu hao na wadau wa sekta binafsi yanafanyiwa kazi na kwamba wizara pia inafanya kila jitihada kuhakikisha afya ya watanzania inaimarika kwa kutumia mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa kutoka kwenye mifugo isiyo na magonjwa.

Prof. Gabriel amefafanua kuwa Asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na mifugo hivyo wizara itahakikisha inadhibiti magonjwa ya mifugo pamoja na kuhakikisha inasimamia vyema soko la mifugo nje ya nchi.

Mwisho.

Mifuko Ya Uwezeshaji Kiuchumi Yatakiwa Kuwawezesha Wananchi Mitaji Waanzishe Viwanda

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswaga ametoa wito kwa Mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kuangalia jinsi ya kuwezesha wananchi wengi zaidi kupata mitaji ya kuanzisha viwanda, ili uchumi wa nchi ukue na kupunguza changamoto zinazokabili jamii.

Kiswaga ameyasema wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika uzinduzi wa Maonesho ya tatu ya  mifuko/programu za uwezeshaji na vikundi vya kifedha  vya kijamii, uliofanyika Oktoba 16, 2019  katika Uwanja wa Halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

“Sote tunafahamu kwamba Tanzania inalenga kufikia uchumi wa katika ifikapo mwaka 2025 na viwanda ni nyenzo itakayowezesha nchi kufika huko; viwanda vina mchango mkubwa sana katika kukuza uchumi wa nchi  kwa kuwa vinanufaisha jamii kwa kutoa ajira, kulipa kodi, kununua malighafi kutoka kwa wakulima na mengine mengi,” alisema Kiswaga.

Aidha, Kiswaga alitoa wito kwa wananchi wa mikoa ya kanda ya ziwa na maeneo mbalimbali nchini kufika katika maonesho haya kupata maelezo kutoka kwa wawakilishi wa mifuko /programu za uwezeshaji za Serikali, kuonesha bidhaa, kunua bidhaa za wajasiriamali na kupata uelewa wa masuala ya uwezeshaji wananchi.

Naye Afisa Maendeleo ya Biashara wa Taasisi ya kusaidia sekta binafsi na Kilimo,  (PASS) Kanda ya Ziwa, Faustine Mungo amesema wameandaa mpango mkakati wa miaka mitano ambapo wanatarajia kutoa ajira 700,000 ambao unatarajia kuzifikia familia zaidi ya 200,000.

Kaimu Mkurugenzi wa Uwezeshaji na Ushiriki wa Watanzania katika Uwekezaji, Bi.Esther Mmbaga kutoka Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi(NEEC), amesema malengo ya maonesho haya ni pamoja na kukuza uelewa wa wananchi  kuhusu uwepo, majukumu na vigezo katika kutoa huduma za mikopo na programu za uwezeshaji.

Bi. Mmbaga ameongeza kuwa malengo mengine ni kuhamasisha wananchi ili waweze kunufaika na fursa zilizopo katika mifuko na programu za uwezeshaji na kuhamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza katika miradi yenye tija.

Maonesho ya tatu ya  mifuko/programu za uwezeshaji na vikundi vya kifedha  vya kijamii, yenye Kauli Mbiu “Mitaji ni Chachu ya Kujenga Uchumi wa Viwanda”ambayo yanaendelea katika uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi yanatarajiwa kufungwa rasmi Oktoba 20, 2019 .

MWISHO

Rais Magufuli Ambana Mkurugenzi Nachingwea....Ataja Sababu za Kutumia magari ziara yake mkoani Lindi

$
0
0
Rais  Magufuli amewabana Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea (DC) Rukia Muwango na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bakari B Bakari baada ya wananchi kulalamikia ucheleweshwaji wa miradi ya maendeleo.

Tukio hilo limetokea leo Jumatano Oktoba 16, 2019 wakati Rais akihutubia wananchi katika wilaya ya Nachingwea ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika mkoa wa Lindi.

Baada ya hotuba za viongozi mbalimbali, Rais alimuomba Mwenyekiti wa CCM, Mzee Hashim Mkanjauka aeleze matatizo yote yanayowakabili wakazi wa Nachingwea.

Mkanjauka alianza kuelezea miradi ya maendeleo iliyokwama hali iliyowafanya wananchi waibuke kwa shangwe na hivyo kumfanya Rais atake kujua Zaidi kero hizo.

“Viongozi wetu siyo wakweli, miradi wilaya ya Nachingwea vijijini haitekelezeki, stendi ya wajasiriamali hakuna, soko halina kitu mkandarasi waliyempa hajamaliza, redio imenunuliwa na kufungwa kwa fedha za wananchi zaidi ya Sh100 milioni lakini haifanyi kazi. Maji yamekuja na mwenge yameondoka na mwenge Nachingwea ni wilaya kongwe,” amesema Mzee Mkanjauka.

Baada ya maelezo hayo Rais alimuita Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo akimtaka atoe majibu ya kwanini miradi hiyo inasuasua na mingine imesimama kabisa.

“Sh200 milioni ilijenga sehemu ya kupumzikia wasafiri , mabanda 12 ya biashara sisi tulikuta imefungwa tuliwekeza kwa kuweka mabanda kwa mapato ya ndani ya Sh81 milioni, kujenga mabanda 26 kumalizia choo na kuanza kwa kuwa ni kubwa maeneo tuliyotenga kwa ajili ya wajasiriamali itabidi tuyapimie wameshapimiwa na wanaohitaji miundombinu ni mama lishe.”

Majibu hayo yalizalisha maswali zaidi kwamba ni kiasi gani hasa kilichotumika kwa upande wa soko pekee, Mkurugenzi huyo alijibu kuwa ni Sh71 milioni.

Baadaye Rais aliamua kushuka katika gari na kutembea mita kadhaa eneo la soko ili kujiridhisha kama kweli ujenzi unaendana na thamani ya fedha inayotajwa.

Baada ya kufika katika soko hilo na kuona hali halisi, alitaka kujua Sh71 milioni namna zilivyotumika lakini Mkurugenzi alionekana kujikanyaga namna alivyokuwa anajibu.

“Nawashukuru ndugu zangu wa Nachingwea kwa kuwa wakweli, ukweli humweka mtu huru, Tsh milioni 71 zimetumika kwa ajili ya ukarabati wa soko lakini mambo yanasuasua. Hayo mengine niachieni mimi nitafanya maamuzi.

“Tunahitaji watendaji wakali, huyu mkurugenzi wenu ameniuzi sana, anasema alikua anafanya kazi Marekani, sijui alikua anaokota makopo?

“Nafahamu shida mnayopitia barabara, ndiyo maana nimekuja na usafiri wa gari, ningeweza kuja na ‘helikopta’ lakini nimeamua kutumia barabara ili niyapate maumivu mnayoyapitia. Nataka niwahakikishie kuwa hii barabara ya kilometa 45 ya Nachingwea tutaijenga katika kiwango cha lami.

“Hii barabara tutaijenga kwa kiwango cha lami, kutoka Nachingwea – Ruangwa na Nanganga – Masasi, tumezoea kuona barabara za lami ni za mkoa kwa mkoa lakini sasa tunaanza kuunganisha hadi wilaya. Mliojenga pembezoni mwa barabara mjiandae kuhama bila fidia

Majina Ya Wanafunzi Waliopata Mkopo 2019/20 awamu ya kwanza. ....Tazama HAPA

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha ya awamu ya kwanza yenye wanafunzi 30,675 wa Mwaka wa Kwanza kwa mwaka wa masomo 2019/2020 waliofanikiwa kupata mikopo yenye thamani ya TZS 113.5 bilioni.

Katika mwaka huu wa masomo, Serikali imetenga TZS 450 bilioni zinazolenga kuwanufaisha jumla ya wanafunzi 128,285. Kati yao, zaidi ya wanafunzi 45,000 ni wa mwaka wa kwanza na wengine 83,285 ni wenye mikopo wanaoendelea na masomo. Mwaka 2018/2019, fedha zilizotengwa na kutolewa zilikua TZS 427.5 bilioni na ziliwanufaisha jumla ya wanafunzi 123,283 wakiwemo 41,285 wa mwaka wa kwanza.

Akizungumza na wanahabari leo (Alhamisi, Oktoba 17, 2019) na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru, amesema katika orodha hiyo, wanaume ni 19,632 (64%) na wanawake ni 11,043 (36%).

Badru amefafanua kuwa waombaji mikopo wafunfue akaunti zao binafsi (SIPA – Student’s Individual Permanent Account) walizofungua kuomba mkopo kupitia mfumo wa HESLB (olas.heslb.go.tz) ili kupata taarifa za mikopo. 


==>>KUONA ORODHA YA MAJINA AWAMU YA KWANZA, BOFYA HAPA.
 

Makundi Maalum – Yatima, Wenye ulemavu n.k
Kuhusu makundi maalum yenye uhitaji, Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema katika orodha ya awamu ya kwanza yenye wanafunzi 30,675, wapo wanafunzi 6,142 ambao ni yatima au wamepoteza mzazi mmoja, wenye ulemavu 280 na wengine 277 wanaotoka katika kaya zinazofadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

“Katika makundi maalum pia tuna wanafunzi 1,890, sawa na asilimia 6 ya wanafunzi 30,675 wa awamu ya kwanza ambao walisoma shule binafsi lakini kutokana na hali duni ya uchumi, walifadhiliwa na walithibitisha kwa kuweka nyaraka sahihi,” amesema Badru.
 

Kutangazwa orodha ya awamu ya pili
Kuhusu awamu ya pili, Badru amesema HESLB kabla ya Oktoba 25 ya wiki ijayo baada ya kukamilishwa kwa uchambuzi wa maombi ya mikopo kutoka kwa wanafunzi waliochelewa kukamilisha taratibu za udahili au kuchelewa kurekebisha maombi yao ya mkopo mtandaoni.



==>>KUONA ORODHA YA MAJINA AWAMU YA KWANZA, BOFYA HAPA.
 
 Wito kwa wanafunzi
Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Uchambuzi na Upangaji Mikopo wa HESLB Dr. Veronica Nyahende amewataka wanafunzi ambao taarifa zao hazijakamilika, kukamilisha ili wenye sifa wapangiwe mkopo.

“Kuna kama wanafunzi 1,000 ambao maombi yao hayajakamilika, watumie muda huu hadi tarehe 19 kukamilisha ili wenye sifa nao tuwapangie mkopo,” amesema.


👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
==>>KUONA ORODHA YA MAJINA  AWAMU YA KWANZA, BOFYA HAPA.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa October 18

Mfanyabiashara Salum Shamte Atiwa Mbaroni Kwa Ubadhirifu wa Bilioni 54

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martin Shigela ameliamuru Jeshi la Polisi mkoani humo, kumshikilia Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Bw. Salum Shamte, kufuatia madai ya Kampuni yake ya Katani LTD kufanya ubadhirifu wa fedha za wakulima wa Mkonge, NSSF pamoja na serikali.

Wengine waliokamatwa ni Juma Shamte ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa sasa wa Katani Limited, Fadhili Malima (mkurugenzi wa fedha), Theodora Mtejeta (ofisa uhusiano) na mjumbe wa bodi, Fatma Diwani.

Kukamatwa vigogo hao ni agizo la Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella kwa Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Edward Bukombe na Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa, Christopher Mariba.

Shigela alitoa agizo hilo baada ya kupokea ripoti ya mkaguzi wa ndani wa serikali aliyoitoa katika mkutano wa wadau wa mkonge uliofanyika jijini Tanga, ambapo ripoti hiyo ilionyesha kuwa Kampuni hiyo ina upotevu wa zaidi ya Sh. bilioni 54.

Awali akiwasilisha ripoti ya ukaguzi huo, Mkaguzi wa Ndani Mwaandamizi Wizara ya fedha na Mipango, Idrisa Ally, alieleza kuwa ukaguzi huo ulianza Januari 22, hadi Februaru 22 mwaka huu ambpo ulihusisha  mwaka 2008 hadi 2018.

Ally alieleza kuwa kazi ya ukaguzi huo ulilenga kuangalia miamala ya Shirika la wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakulima na fedha za Sacos ya wakulima hao sambamba na kuangalia mikataba  iliyoingiwa na pande zote tatu.

Alieleza kuwa katika ukaguzi huo, zaidi ya Sh. bilioni 54 hazikufahamika zilipo ama matumizi yake yakiwamo madeni ya wakulima, makato ya wanachama wa NSSF, mkopo na kutolipwa kwa kodi ya serikali kwa mujibu wa taratibu.

Mkaguzi huyo alieleza yaliyojitokeza katika ukaguzi huo ni pamoja na madeni ya wakulima Sh. bilioni 29.8 ambazo hata hivyo alieleza hazikuonyeshwa kwenye taarifa za kampuni hiyo kiasi cha Sh. bilioni 1.7 za makato waliyokatwa wakulima huku Sacos ya wakulima ikiidai kampuni hiyo Sh. milioni  5.55.

Hata hivyo, ripoti ya mkaguzi huyo ilionyesha fedha zinazodaiwa na kampuni hiyo kwa wakulima ni zaidi ya Sh. bilioni 2.8.

Baada ya ripoti hiyo kuwasilishwa kwenye mkutsano huo na Mkuu wa Mkoa kutoa nafasi kwa pande zote kujieleza ndipo Mmiliki wa kampuni ya Katan Ltd, Salum Shamte alisimama na kukanusha ripoti iliyowasilishwa hiyo akidai haina usahihi zaidi, na kwamba hawakushirikishwa katika kuiandaa.

Shamte alieleza kuwa wao kama walezi wa wakulima tangu mwaka 1999 walikuwa wakiendesha kilimo cha mkataba wa kibiashara baina yao,bodi ya mkonge na wakulima.

Watanzania Waishio Na Vvu Waaswa Kuendelea Kutumia Dawa Za Kufubaza Virusi

$
0
0
NA.MWANDISHI WETU
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu na Uwekezaji, Dorothy Mwaluko amewaasa Watanzania wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kuendelea kutumia dawa za kufubaza virusi hivyo ili waweze kuishi maisha yenye afya na amani wakati wote.

Ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wanachama wa Baraza la Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI katika Konga ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Mkoani alipowatembelea kukagua utekelezaji wa majukumu ikiwa ni pamoja na namna konga hiyo inavyoendesha shughuli za uzalishaji Wilayani hapo Oktoba 17, 2017 Mkoani Morogoro.

“Kipekee ninawapongeza kwa ujasiri wenu wa kujitokeza na kuonesha ulimwengu kuwa janga hili lipo na ni letu sote, kwani naamini hakuna mtu ambaye halijamgusa kwa namna moja au nyingine hivyo niwaombe mjitahidi kuendelea kutumia dawa hizi za kufubaza makali ya virusi ili kuendelea kuimarika zaidi,”alisema Mwaluko.

Aliwasisitiza kuendelea kuwa mabalozi wazuri kwa wengine ambao hawajatambua hali zao na wale waliotambua hali zao kuendelea kufubaza virusi na kutoacha kutumia  dawa hizo kwa kuzingatia umuhimu wake.

“Napenda kuwahamasisha msiache wala kuchoka kutumia dawa hizi kwa kuzingatia umuhimu wake katika kuhakikisha zinawapa nafuu na kuondoa magonjwa nyemelezi kuendelea kuwa na afya njema na kushiriki katika shughuli za kimaendeleo na kufanya dunia mahali salama pa kuishi,”alisisitiza Mwaluko.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utafiti na Tathimini kutoka Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwela aklieleza kuwa, hali ya kiwango cha maambukizi Mapya ni asilimia 4.7 Kitaifa na maambukizi hayo ni mengi kwa wanawake kuliko wanaume hivyo Serikali itaendeelea kuhudumia kundi hili kwa kuhakikisha lilapewa dawa hizo kwa kadri itakiwavyo.

“Serikali imejipanga kuhakikisha kundi la WAVIU wote wanahudumiwa na kupatiwa mahitaji yao muhimu ikiwemo upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya virusi (ARV) hivyo na kuhakikisha kundi kubwa la wanawake ambao ndiyo wanaoathiriwa zaidi linafikiwa kadiri iwezekanavyo na hii itaendeelea kusaidia kundi hilo kupunguza hatari ya kuingia katika maambukizi mapya,”alieleza Dkt.Kamwela.

Aliongezea kuwa takwimu zinaonesha hali ya maambukizi mapya kwa kila mwaka ni watu 72000 ambapo kundi la vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 24 linaongoza kwa asilimia 40 na kueleza kundi la wanawake wanachangia asilimia 80 ya maambukizi hayo.

“Serikali imetoa kipaumbele kuwa mwitikio wa masuala ya UKIMWI umelenga kundi la vijana ili kupunguza maambukizi mapya yanayolikumba kundi hilo,”alifafanua Dkt.Kamwela.

Aliongezea kuwa wananchi wasipotambua hali zao mapema wanasababisha kuanza tiba kwa kuchelewa na hivyo kulazimika kuanza dawa wakati wa hatari na kuwalazimu kuwa na juhudi za ziada katika kutumia dawa ili kutokomeza maambukizi mapya na kufubaza virusi vya UKIMWI.

Aidha Mwenyekiti wa Baraza la Watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi wa Konga hiyo Halida Ally alieleza kuwa hali ya utoro wa dawa imechangia kuongezeka kwa maambukizi mapya ambapo walifanikiwa kuhamasisha watu 30,712 kupima hali zao ambapo jumla ya watu 2,038 walikutwa na maambukizi kati yao wanawake ni 1,327  na wanaume ni 711.

Alisema hali ya utoro wa dawa ni changamoto katika kuhudumia kundi hilo inayochangiwa na uwepo wa sababu mbalimbali ambapo katika kundi la WAVIU 2,038 wanaotumia dawa za kufubaza virusi ni 1,707 kati yao wanawake ni 1,034 na wanaume ni 673 katika kundi hilo watoro wa dawa ni 996 kati yao wanaume ni 335 na wanawake ni 673 hali ambayo inachangia kuongezeka kwa maambukizi mapya na kuongeza ukubwa wa janga hilo katika Halmashauri yao.

Naye mmoja ya wanachama wa konga hiyo Betina Januari aliipongeza Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika mapambano dhidi ya Ukimwi na kuahidi uendelea kutoa ushirikiano katika jitihada za kuwawekea mazingira wezeshi na kufikia malengo ya sufuri tatu ifikapo 2030.

KONGA Kilombero ni Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (VVU) ngazi ya Wilaya. KONGA ya Kilombero imeundwa mwaka 2013 ikiwa na vikundi 14 vyenye jumla ya wanachama 354 ambapo wanawake ni 237 na wanaume 117.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images