Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Waziri Hasunga Aviagiza Vyama Vya Ushirika Kushiriki Katika Ununuzi Wa Mbolea Kwa Pamoja (BPS)

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Katavi
Kutokana na kuwepo kwa mfumo wa ununzi wa mbolea kwa pamoja (BPS) serikali imeviagiza Vyama vya ushirika vya msingi (AMCOs) na vyama vikuu (FCU) kuanza kushiriki kwenye ununzi wa mbolea kwa pamoja (BPS) ili kuhakikisha upatikanaji wa mbolea kwa bei nafuu na kwa wakati.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ametoa agizo hilo wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya mbolea Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika leo tarehe 13 Octoba 2019 katika viwanja vya shule ya msingi Kashaulili Wilayani Mpanda mkoani Katavi.

Amesema kuwa ili kuongeza matumizi ya mbolea nchini, Wizara ya kilimo kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakati na kwa bei nafuu ikiwemo mfumo wa unuzi wa mbolea kwa pamoja (BPS).

Pia, imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo kutoa elimu kwa njia tofauti kwa lengo la kuongeza uelewa wa umuhimu na kuongeza matumizi ya mbolea nchini hivyo ili tija na uzalishaji viongezeke vyama vya ushirika havina budi kushiriki kwenye ununuzi wa mbolea ili kuwarahisishia wanachama wao ambao ni wakulima kupata mbolea kwa wakati na kwa bei nafuu.

Mhe Hasunga ametoa mwito kwa wafanyabiashara wa mbolea kuuza mbolea kwa bei elekezi iliyopangwa na serikali na wazingatia bei hizo kwa mbolea za kupandia (DAP) na kukuzia (UREA) ambazo zinaingizwa nchini kwa mfumo wa Uingizaji wa Mbolea kwa Pamoja yaani Bulk Procurement System BPS.

“Kama mnavyofahamu, Serikali imeendelea kuratibu utoaji wa mikopo yenye riba nafuu kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo (Tanzania Agriculture Development Bank-TADB), Benki ya Uwekezaji (Tanzania Investment Bank TIB) na Mfuko wa Pembejeo wa Taifa. Hivyo, nitoe wito kwa wakulima wote wa Mkoa wa Katavi na Mikoa mingine kujiunga katika ushirika ili kuweze kutumia fursa zinazotolewa na taasisi hizi ili kujiletea maendeleo” Alikaririwa Mhe Hasunga

Waziri Hasunga amesema kuwa ili kuwa na matumizi sahihi ya mbolea, ufahamu juu afya ya udongo ni muhimu; hivyo, ameiagiza Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kutoa taarifa ya afya ya udongo kwa wakulima na wadau wengine ili matumizi ya mbolea yaendane na mahitaji ya zao na udongo husika.

Niwakumbusha wafanyabiashara wakubwa kuwa mbolea zinahitajika zaidi mikoani; hivyo ni wakati muafaka wa kuanza kusambaza mbolea mikoani haraka iwezekanavyo. Pia ni wakati sahihi wa kufungua matawi ya mauzo na maghala mikoani badala ya mbolea nyingi kurundikana kwenye maghala yaliyoko Dar es salaam ambako mahitaji yake ni madogo.

Ameongeza kwa kusema kuwa ili mbolea iweze kuwafikia wakulima kwa wakati, amelitaka shirika la reli Tanzania (TRC) kutoa kipaumbele katika usafirishaji wa mbolea kwa mikoa ya Tabora, kigoma na Katavi huku akiitaka Mamlaka ya udhibiti wa mbolea (TFRA) kuhakikisha inasimamia ubora wa mbolea kuanzia bandarini inapoingia hadi kwa muuzaji anayemuuzia mkulima.

Kauli mbiu ya maadhimisho haya ni ‘matumizi sahihi ya mbolea kwa uhakika wa chakula na uchumi wa viwanda’. Ambapo lengo la maadhimisho ya siku ya mbolea duniani nchini Tanzania ni kupata wigo mpana zaidi kwa Wadau kuelezea masuala mbalimbali katika tasnia ya mbolea.

Masuala hayo ni pamoja na mafaniko ya tasnia ya mbolea nchini, kuwahabarisha wadau wa mbolea hususani wakulima na wafanyabiashara wa mbolea mifumo mbalimbali ya upatikanaji na usambazaji wa mbolea; pia kutoa elimu kuhusu sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia tasnia ya mbolea.

Siku ya mbolea duniani ilianza kuadhimishwa kwa mara ya kwanza tarehe 13 Oktoba, 2016 huko nchini Uingereza. Siku hii ilianzishwa mahsusi kwa lengo la kuhamasisha Wadau wa tasnia ya mbolea duniani kote kutambua jukumu kubwa walilonalo la kuhakikisha kuwa wakulima wanatumia mbolea bora na sahihi ili kuleta mapinduzi ya kijani kwa uhakika wa chakula.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera amesema kuwa tayari serikali imetangaza bei elekezi ya mbolea hivyo wafanyabiashara watakaokiuka na kuanza kuuza kwa bei zaidi ya hiyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Amesema kuwa serikali inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli imedhamiria kuwanufaisha wakulima kwenye sekta ya kilimo hivyo kukiuka maelekezo ya serikali kwa wafanyabiashara wa mbolea hawana tofauti na wahujumu uchumi.

Akizungumzia kuhusu uzalishaji wa mazao ya chakula amesema kuwa mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo utahamasisha wakulima kulima mazao mengi kwa tija ili kuongeza uzalishaji utakaoimarisha usalama wa chakula nchini.

Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt Steven Ngailo amesema kuwa mbolea kwa ajili ya kukuzia na kupandia tayari imewasili nchini hivyo wakulima wana fursa mahususi kabisa ya kujitokeza na kuendeleza sekta ya kilimo katika kuongeza uzalishaji wa chakula kwa ajili ya biashara.

Ameitaja kuwa siku ya mbolea Duniani ni kumbukizi ya maadhimisho ya uvumbuzi wa mbolea aina ya Amonia uliofanywa na Bwana Fritz Haber mwaka 1908. Uvumbuzi huo ulichochea mapinduzi ya kijani katika karne ya 20 yaliyowezesha kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao kutokana na matumizi ya mbolea yaliyosaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa janga la njaa na kuleta uhakika wa chakula katika nchi nyingi duniani.

MWISHO

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano October 16

Asilimilia 68 Wajiandikisha Kupiga Kura Uchaguzi Serikali za Mitaa

$
0
0
Watanzania 15,543,604 sawa na asilimia 68 wameshajiandikisha kwenye daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali unaotarajiwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu.

Aidha, Mkoa wa Pwani umeongoza kwa kundikisha watu 473,639 sawa na asilimia 80, mkoa wa Dar es Salaam uliondikisha watu 2,064,820 sawa na asilimia 77 na Tanga ulioandikisha watu 823,194 sawa na asilimia 76.

Mikoa mingine ni Mtwara watu 530,523, Lindi watu 353,649 sawa na asilimia 75 na Iringa watu 381,134 sawa na asilimia 74.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, wakati akielezea tathimini ya uandikishaji ulioanza Octoba 8 hadi 14.

"Tamisemi imejiwekea malengo ya kuandikisha wapiga kura watapatao milioni 22.916 wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu, baada ya hamasa iliyofanywa na wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya watendaji idadi ya waliojiandikisha imefika watu milioni 15.543 sawa na asilimia 68 ya lengo," Jafo amesema

Aidha, amesema mikoa ambayo ipo chini kiuandikishaji hadi juzi ni Kilimanjaro ambayo imeandikisha watu 446,954 sawa na asilimia 48, Kigoma watu 555,856 sawa na asilimia 53 na Arusha watu 551,614 sawa na asilimia 59.

Amesema pia zipo Halmashauri sita ambazo zimefanya vizuri zaidi kwa kuandikisha zaidi ya asilimia 95 na kuendelea ambazo ni Mpanda, Mlele, Kibiti, Ngorongoro, Songwe na Mbozi.

Jafo amezitaja pia Halmashauri ambazo zimeandikisha chini ya asilimia 50 ambazo Manispaa za Moshi kwa asilimia 31, Jiji la Arusha kwa asilimia 32, Msimbo asilimia 41, Kigoma asilimia 43, Jiji la Mbeya asilimia 46 na Musoma asilimia 49.

Malawi Yakanusha Kuwa Na Mgonjwa Wa Ebola

$
0
0
Malawi imekanusha ripoti zilizoenea kwamba mtu mmoja amegunduliwa kuwa na Ebola kwenye eneo la Karonga linalopakana na Tanzania.

Hofu hiyo ilitokea Jumapili wakati wafanyakazi wa afya kwenye eneo hilo waligundua mwanamume mwenye umri wa miaka 37 kuwa na dalili za Ebola.

Afisa wa afya katika eneo hilo,  Louis Tukula amesema mtu huyo alikuwa na maambukizi ya bakteria na si Ebola.

Amesema eneo hilo limekuwa katika hali ya tahadhari tokea ugonjwa wa Ebola uripotiwe katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mbaroni Kwa Kujiandikisha Mara 2 Kwenye Daftari La Wapiga Kura

$
0
0
Mkazi wa Kasanga Manispaa ya Morogoro, Ngeze Mwagilo (29) anatuhumiwa kujiandikisha mara mbili katika Daftari la Wapiga Kura kwenye vituo viwili tofauti ndani ya Manispaa ya Morogoro

Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Wilbroad Mutafungwa amesema mtu huyo alikamatwa baada ya Polisi kupata taarifa na kumfuatilia Mtuhumiwa wakati wa shughuli ya uandikishaji

Amesema, mtuhumiwa huyo anadaiwa kujiandikisha katika Kituo cha Kasanga Kata ya Mindu na baadaye kwenda kujiandikisha katika Kituo cha Kiwanja cha Ndege Kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro

Aidha, Kamanda Mutafungwa amebainisha kuwa Mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na atafikishwa Mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika ili sheria ichukue mkondo wake

Mvua Yasababisha Vifo vya Watu 13 Morogoro Wakiwemo wanafunzi 9

$
0
0
Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini zimesababisha vifo vya watu 13 Mkoani Morogoro huku kati yao watoto wakiwa ni tisa (miaka 11 hadi 15)

Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Wilbroad Mutafungwa amesema tukio la kwanza ni la watoto watano waliofariki baada ya kuzama Mto Mvuha uliopo kata Kibogwa

Watoto hao ni Neema Rajabu (10), Latifa Khalid (9), Munila Khalid (11), Omary Khalid (14) pamoja na Zanisha Adam (9) ambaye mwili wake bado haujapatikana na shughuli ya kumtafuta inaendelea.

Mutafungwa alibainisha kuwa Said Rajabu (11) mwanafunzi wa darasa la tatu aliyekuwa na wenzie waliokufa alinusurika na kujeruhiwa baada ya kuona maji yakizidi, alikimbia na baadaye alianguka na anaendelea na matibabu katika zahanati ya Kibogwa.

Wengine waliokufa ni wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Kibwaya Tarafa ya Mkuyuni, Rajabu Issa (11) na Shabani Msimbe (15), baada ya kutumbukia kwenye dimbwi la maji walipokuwa wakiogelea.

Wanafunzi wengine wawili waliokufa maji ni Karim Athuman (13) na Hussein Hassan (14) wa Shule ya Msingi Ulundo waliozidiwa na maji wakiwa wanaogelea mto Ngerengere.

Uturuki yakataa pendekezo la Marekani kuhusu kusimamisha vita....Yasema Haigopi Vikwazo

$
0
0
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amekataa wito wa Marekani wa kusitisha mapigano kaskazini mwa Syria, akisema kuwa Uturuki itaendelea na mashambulizi yake.

Ameeleza hayo wakati ambao Naibu Rais wa Marekani ,Mike Pence na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo wakiwa wanajiandaa kuja kufanya makubaliano.

Siku ya jumanne, Urusi ilitoa angalizo kuwa haitaruhusu mapigano kutokea tena baina ya majeshi ya Uturuki na Syria.

Uturuki imesema kuwa lengo la kuendelea na mapigano hayo ni kutaka kuwaondoa wanajeshi wa kikurdi katika mipaka.

Uturuki inaaminika kuwa wanamgambo wa kikurdi 'Kurdish-led Syrian Democratic Forces (SDF)' ni asasi ya kigaidi .

Vikosi vya Uturuki pia vimebuni kile ambacho serikali yao inataja kuwa "eneo salama" la kuwapa makazi wakimbizi milioni mbili wa Syria ambao wamepewa hifadhi katika nchi hiyo.

Halmashauri Ya Lindi Vijijini Kuwa Halmashauri Ya Mtama

$
0
0
Rais Magufuli ameagiza Halmashauri ya Lindi Vijijini kuitwa Halmashauri ya Mtama na Makao Mkuu ya Halmashauri hiyo yahamishiwe Mtama kutoka Mjini

Amesema, ndani ya siku 15, Viongozi wa Halmashauri hiyo watoke Mjini na kuhamia Mtama na hiyo ndio italeta maendeleo kwani kama ni giza ndio watashughulikia umeme haraka

“Najua kulikuwa na mabishano, wapo wanaotaka Makao Makuu yaende Subi, wapo waliotaka yaende Mchinga, wapo waliotaka yaende Rondo, kila mmoja anataka la kwake

“Kwa kuwa mimi ndio Rais, na mimi napasua katikati kwa kufuata haki, nimetoa maagizo, Manispaa ya Lindi itachukua eneo lake iliyokuwa nalo mpaka Mnazi Mmoja hadi Mingoyo na kuongezewa eneo la Mchinga.”-Rais Magufuli

Yaliyojiri wakati wa ziara ya Rais Magufuli alipotoka Lindi Mjini kwenda Ruangwa.

Waziri Wa Madini Ashiriki Kujadili Changamoto Za Barabara Mkoani Geita

$
0
0
Na Tito Mselem Geita,
Waziri wa Madini Doto Biteko ameshiriki katika Kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika Oktoba 15,2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mkuu wa Mkoa wa Geita ili kujadili changamoto za barabara mkoani hamo. 

Kikao hicho kiliudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama cha Mapindizi wakiwemo Wabunge wa Majimbo ya Mkoa wa Geita akiwemo Mbunge wa Bukombe ambaye pia ni Waziri wa Madini Doto Biteko, Mbunge wa Chato ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, Mbunge wa Geita Mjini ambaye pia Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Costantine Kanyasu, Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma, Mbunge wa Mbogwe Augustino Masele, Mbunge wa Busanda Lolesia Bukwimba, Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema Pendo Peneza.

Vingozi wengine walioshiriki ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mjini Josephat Maganga, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Mkumba, Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe. Martha Mkupasi, Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Hamim Gwiyama, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa Geita Alhaji Said Kalidushi pamoja na Wakuu wa Idara mbalimbali.

Aidha Waziri Biteko amewapongeza viongozi wa TANROADS na TARURA kwa kazi nzuri wayoifanya katika Mkoa wa Geita kwa kuhakikisha kuwa barabara zinatengenezwa kwa kiwango kizuri na kumalizika kwa wakati.

Hata hivyo, Waziri Biteko amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel kwa usimamizi na ufuatiliaji mzuri katika kuhakisha barabara za Mkoa wa Geita zinakamilika kwa muda uliopangwa na zinakuwa kwenye viwango vinavyotakiwa.

Imeelezwa kuwa Mji wa Geita ni kati ya miji inayokua kwa kasi sana sambamba na ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi, hivyo kuwepo na msongamano mkubwa wa vyombo vya usafiri na watembea kwa miguu barabarani.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesema katika awamu hii ya tano Rais Dkt. John Pombe Magufuli alitupa ahadi ya ujenza wa barabara na ametekeleza ujenzi wa barabara ya Ushirombo mpaka Lusahunga kilometa 110 kwa gharama ya shilingi bilioni 114.557, Uwanja wa Ndege wa Chato kilometa 3.5 kwa gharama ya Shilingi Billioni 39.15. 

Aidha, Mhandisi Gabriel amesema kwamba, kazi ambazo zimekamilika ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Runzewe  mpaka Bwanga kilometa 45 kwa gharama ya shilingi bilioni 43.357 na barabara ya Bwanga mpaka Biharamuro kilometa 65.0 miradi yote hii inatekelezwa kwa fedha za serikali.

Katika hatua nyingine Mhandisi Gabriel ameeleza kwamba katika Mkoa wa Geita TANROADS inasimamia miradi ya usanifu wa kina katika barabara za Geita mpaka Kahama yenye kilometa 139.557 kwa gharama ya shilingi bilioni 440 inatelekezwa na mkandarasi ENV Engeneering, kazi imekamilika.

“TANROADS inasimamia pia usanifu  katika barabara ya Nyamirembe mpaka Katoke yenye urefu wa kilometa 50 kwa gharama ya shilingi bilioni 861.046 na Mhandisi Consult ambapo kazi hiyo imekamilika,” Gabriel amesema Mhandisi Gabriel.

Katika hatua nyingine Mhandisi Gabriel ametoa rai kwa wananchi kutunza miundombinu ya barabara kwa kutopitisha mifugo na kunyofoa alama za barabarani pamoja na kutovamia hifadhi za barabara.

Katika bajaeti ya mwaka 2018/2019 TARURA Mkoa wa Geita  unatarajiwa kutumia kiasi cha shilingi 6,844,393,140.37 kutoka mfuko wa barabara (Road fund) kwa ajili ya matengenezo ya barabara na shilingi 1,612,500,000.00 kwa ajili ya kazi za maendeleo, fedha hizo ni kutoka OR-TAMISEMI.

Hadi kufikia Tarehe 03/01/2019 jumla ya shilingi 2,249,253, 616.84 sawa na asilimia 32.86 zimepokelewa kwa ajili matengenezo ya barabara na jumla  ya shilingi  612,654,524.43 sawa na asilimia 37.99 zimepokelewa kwa ajili ya miradi maendeleo ya barabara za mkoani Geita.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Rais Magufuli atamani Msanii Harmonize Akagombee Ubunge Tandahimba

$
0
0
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika ziara yake mkoani Lindi, Wilaya ya Ruangwa jana Oktoba 15, 2019 alisema anatamani msanii Rajabu Abduli maarufu kama Harmonize kugombea Ubunge Jimbo la Tandahimba.

Akitoa shukrani na pongezi kwa watu waliotoa burudani katika mkutano huo, Rais Magufuli alisema “Lakumalizia nawapongeza sana waimbaji hawa wakina baba, lakini nampongeza sana Harmonize sijui anatoka jimbo gani?


“Anatoka jimbo gani huyu? Tandahimba? Mbunge wa kule ni nani?. Aaa ningetamani kweli Harmonize akagombee kule akawe mbunge wa Tandahimba” alisema

JPM Anamuenzi Nyerere Kwa Vitendo-RC Mtaka

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema serikali ya awamu ya tano chini ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe inamuenzi Hayati Baba wa Taifa, Mwl Julius Kambarage Nyerere kwa vitendo hususani katika kuendeleza kazi nzuri alizozifanya.

Mtaka ameyasema hayo Oktoba 14, 2019 katika Kongamano la Kitaifa la Kumbukizi ya Miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere lililofanyika Oktoba 14, 2019 Mjini Bariadi, likiwashirikisha viongozi wa Serikali, wananchi na baadhi ya viongozi wa CCM Mkoa wa Simiyu, UVCCM Simiyu, UVCCM kutoka mikoa mbalimbali nchini na ngazi ya Taifa(makao makuu).

“Mwalimu amepewa heshima ya kuenziwa ninyi  kizazi hiki mnashuhudia kwa macho, wapo watu wanasimuliwa tu kuwa ile barabara inaitwa ‘Nyerere road’, lakini hamkuwepo; leo mnajua kwamba hifadhi fulani inaitwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere, mnasikia Mradi mkubwa wa kufua umeme wa maji wa  J.K. Nyerere,  Mhe.Rais amemheshimisha Mwalimu kwa vitendo,” alisema Mtaka

“Mwalimu aliamini katika Watanzania kufanya shughuli za kiuchumi  ikiwemo kilimo,  ufugaji na uvuvi  na akataka waongeze thamani katika shughuli hizo; ndiyo maana Mhe Rais ameanza kufufua viwanda vya nguo, viwanda vya korosho, viwanda vya kahawa na mengine aliyoyaacha Mwalimu, “ aliongeza Mtaka.

Aidha, Mtaka amemzungumzia Mwalimu Nyerere kuwa alikuwa kiongozi wa karne mwenye utu, maono na msimamo ambaye alijua wapi anapotoka na anapotakiwa kwenda kama kiongozi na aliyewaheshimisha Watanzania.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito kwa Vijana wa UVCCM  kuwaeleza ukweli na kuwashauri viongozi vijana ndani ya Serikali kufanya kazi zao kwa kuzingatia misingi ya uongozi na kuepukana na tabia ya kuweka urasimu wa kufikika na watu , ili viongozi hao watekeleze vema wajibu wao wa kuwatumikia wananchi na kumsaidia Mhe. Rais Magufuli katika majukumu aliyowapa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Enock Yakobo amewataka vijana kumuenzi Hayati  Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere kwa kufanya kazi kwa bidii, ili wajiletee maendeleo kwa kuwa Mwalimu aliamini kuwa kazi ni kipimo cha uhai.

Naye Kaimu Katibu Idara ya Mahusiano ya Kimataifa na Vyuo Vikuu, Bi Asha Feruz amesema kwa kuwa vijana wengi wamezaliwa wakati Hayati Baba wa Taifa,Mwl. Julius K. Nyerere akiwa amefariki ni vema vijana hao wakasoma  vitabu, ili wajue historia ya mwalimu na waasisi wengine wa Taifa la Tanzania.

Mmoja wa Wajukuu wa Mwalimu Nyerere Chifu Edward Magige amesema pamoja na Watanzania kuendelea kukumbuka na kuenzi mambo mazuri yaliyofanywa na Hayati Mwalimu Nyerere ni vema pia wakaukumbuka mchango wa Mama Maria Nyerere katika kazi zilizofanywa na mwalimu.

Mbunge wa Jimbo la Itilima Mhe. Njalu Silanga ametoa wito kwa Vijana hapa nchini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura, ili waweze kuitumia vema haki yao kuchagua viongozi bora ikiwa ni namna mojawapo ya kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuchagua viongozi watakaosimamia misingi ya uongozi aliyoiweka.

MWISHO

Familia Yakaa Chini ya Ardhi kwa Miaka 9 Ikisubiri Mwisho wa Dunia

$
0
0
Familia moja iliyoishi katika chumba cha chini ya ardhi kwa miaka tisa "ikisubiri mwisho wa dunia" imepatikana na polisi nchini Uholanzi

Mwanamume wa miaka 58, na watoto wake sita walio na umri kati ya miaka 16 hadi 25 - walikuwa wakiishi katika shamba lao katika mkoa wa kaskazini wa Drenthe.

Walipatikana baada ya kijana wake mkubwa kuenda kununua pombe katika baa moja karibu na kijiji cha Ruinerwold, na kumfahamisha mhudumu wa baa hiyo kwamba anataka usaidizi,Kituo cha Televisheni cha RTV kiliripoti.

Waliomuona kijana huyo wanasema alionekana kana kwamba amechanganyikiwa.

Familia yake imekuwa ikiishi kwa kujitenga ikisubiri mwisho wadunia, RTV iliripoti.

"Aliagiza chupa tano za bia na kunywa zote. Baada ya hapo nilisema nae kidogo ndipo alipofichua kuwa ametoroka na kwamba anaomba usaidizi... tukapiga simu polisi," mmiliki wa baa hiyo Chris Westerbeek alikifahamisha kituo cha RTV.

Aliongeza kuwa: "Alikuwa na nywele ndefu, ndevu chafu,nguo zilizochakaa na alionekana kana kwamba amechanganyikiwa. Alisema hajawahi kwenda shule na kwamba hajawahi kunyolewa nywele kwa miaka tisa ."
 
"Alisema ana ndugu na dada zake ambao wanaishi katika shamba hilo. "

Maafisa walitembelea makaazi hayo ya vijijini ili kufanya upekuzi zaidi. Waligundua ngazi iliokuwa nyuma ya kabati katika sebule ya nyumba hiyo ambayo inaelekea chumba cha chini ya ardhi ambako familia hiyo ilikuwa ikiishi.

Polisi imethibitisha mjini Drenthe  kuwa mwanamume huyo wa miaka 58 amekamatwa na kuongeza anafanyiwa uchunguzi-baada ya kukataa kushirikiana nao. 

-BBC

Kiswahili chapendekezwa kutumika Ukanda wa Maziwa Makuu

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Brazzaville,
Katika jitihada za kukuza lugha ya Kiswahili barani Afrika, Tanzania imeziomba nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu kuanza kutumia lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi na lugha ya kazi
 
Wito huo umetolewa katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu, uliofanyika mjini Brazzaville leo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro  
 
"Tumewaomba wenzetu wa maziwa makuu wakubali lugha ya Kiswahili kutumika kama lugha rasmi na lugha ya kazi katika nchi zote za maziwa makuu. Pia nchi sita ambazo zipo hapa na hazijaridhia mabadiliko ya mkataba wa Afrika kuruhusu Kiswahili kutumika kama lugha rasmi katika Afrika (AU) nchi hizo zimetuhakikishia kuwa zitaridhia mabadiliko hayo ili kuhakikisha kuwa Kiswahili kinaanza kutumika kama lugha rasmi ya kazi," Alisema Dkt. Ndumbaro
 
Kwa mujibu wa Waziri Ndumbaro, matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ukanda huo ni fursa ambayo italeta umoja wa kitaifa, na katika ukanda wa maziwa makuu lakini pia umuhimu wa Kiswahili kwamba ni lugha pekee ambayo haina uhusiano na ukoloni barani afrika. 
 
"Tunatumaini kwamba tutazipata sahihi za nchi sita na tukisha zipata tutabakiwa na sahihi ya nchi moja tu ili Kiswahili kiwe rasmi lugha ya kazi katika mikutano itakayo kuwa inafanyika barani Afrika," aliongeza Dkt. Ndumbaro 
 
Nchi sita ambazo hazijaridhia mabadiliko ya mkataba wa Afrika kuhakikisha kuwa Kiswahili kinatumika kama lugha rasmi ya kazi ni pamoja na Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sudani, Uganda na Zambia. 
 
Kwa sasa hivi ni lugha rasmi lakini siyo lugha ya kazi kwa hiyo tumekwenda vizuri kwenye Kiswahili tunaamini ni fursa nzuri ya kuanza kukuza lugha ya Kiswahili katika bara la Afrika
 
Wakati huo huo, Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa, katika mkutano huo nchi wanachama waliweza kuongelea agenda kuu za nchi wananchama wa ukanda wa maziwa makuu ambazo ni Amani, Utulivu na Usalama hususani katika eneo la mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
 
Sanjari na hilo, nchi nyingi zimeusifu uongozi wa Rais wa DRC, Felix Tshisekedi kuwa tangu alipoingia madarakani amejitahidhi kuhakikisha kuwa kuna kuwa na amnai ndani ya DRC pamoja na majirani zake. Pia Uganda, Rwanda pamoja na Angola zimesifiwa kufanikisha kusaini makubalianao ya kuleta amanai kati ya Uganda na Rwanda.
 
Akiongea awali wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje Mgeni rasmi ambae alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kongo, Bwn. Clement Mouamba alisema kuwa mkutano wa leo, umelenga kuisaidia nchi ya DRC katika changamoto inazopitia hasa katika ukanda wa mashariki.
 
"Nawapongeza sana kwa kazi ambayo mmekuwa mkiifanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha kuwa ugonjwa wa ebola unatokomezwa, kwani naamini kuwa umoja wetu tunaweza," alisema Mouamba.
 
Aliongeza kwa kuzitaka nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu kuendelea kulinda amanai na umoja walionao ili kuweza kuendelea na shughuli mbalimbali za maendeleo kwani bila amani ni vigumu sana kwa umoja huo kuendelea.
 
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianao wa Jamhuri ya Kongo, ambae pia alikuwa mwenyekiti wa mkutano huo Mhe. Jean Claude Gakosso aliwasisitiza mawaziri wa nchi wanachama kuwa amani na umoja katika ukanda huo ni nguzo muhimu sana na hivyo waendelee kuishika amani hiyo.
 
Pia aligusia ugonjwa wa ebola na kuwataka nchi wanachama kutokata tama ya kupambana na ugonjwa huo licha ya changamoto zinazojitokeza. 
 
"Juhudi mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ya DRC hadi sasa kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) pamoja na wadau wengine katika kupambana na ugonjwa huo ni kutoa chanjo ya kinga ya ugonjwa huo na elimu kwa wananchi wa maeneo yaliyoathirika na ugionjwa huo" alisema Waziri Gakosso.
 
Mkutano wa leo ulitanguliwa na mikutano miwili ambayo ilianza tarehe 11 hadi 14 Oktoba 2019, jijini Brazzaville ambapo pamoja na mambo mengine ilijadiliwa suala la ugonjwa wa ebola na hali ya amani katika maeneo yenye mlipuko wa ugonjwa huo.
 
Nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu ni pamoja na Angola, Burundi, Jamhuri ya Kati, Demokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kongo, Kenya, Rwanda, Sudan, Sudani Kusini, Tanzania, Uganda na Zambia.
 
Mwezi Augusti, 2019 Umoja wa Maendeleo ya Nchi za Ukanda wa Kusini mwa Africa (SADC) ulifanyika Tanzania Jijini Dar es Salaam nchi wananchama waliridhia na kuipitisha kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne ya Umoja huo baada ya Kiingereza, Kireno na Kifaransa.
Mwisho……

Nafasi Za Kazi 8 Toka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

$
0
0
Nafasi Za Kazi  12  Toka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM)  kimetangaza nafasi 8 za Kazi. Mwisho wa kutuma Maombi ni Tarehe 31 mwezi huu wa 10,2019

👉Artisan IV (1 post)

👉Laboratory Scientist III

👉 Laboratory Engineer III 

👉Artist-In-Residence ll

👉Laboratory Technician

👉Workshop Instructor II

👉 Technician III 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

==>>Pia zipo nafasi mbalimbali za kazi UBER TANZANIA, VODACOM, AIRTEL, JUMIA, NOKIA TANZANIA,UMOJA WA MATAIFA

Bonyeza hapo chini kujua zaidi

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Waziri wa Fedha Dkt. Mpango Aitaka Benki Ya Dunia Kusaidia Sekta Ya Kilimo Nchini Tanzania

$
0
0
Na Ramadhani Kissimba na Eva Valerian, Washington Dc
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango (Mb) ameitaka Benki ya Dunia kujikita zaidi katika kusaidia sekta ya kilimo nchini Tanzania ili kuweza kuwainua kiuchumi wakulima hasa wale wa kati na wadogo.

Dkt.Mpango aliyasema hayo wakati wa kikao cha majadiliano na timu nzima ya Benki ya Dunia ambayo inafanya kazi nchini Tanzania na wengine kutoka Makao Makuu ya Benki hiyo nchini Marekani.

Mhe.Mpango alisema katika mkutano huo  walipitia kwa pamoja utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea hivi sasa  inayofadhiliwa na Benki ya Dunia,  lakini pia walipitia na kujadili miradi ambayo inaanza kufikiriwa kwa ajili ya utekelezaji kwa mwaka utakaofuata.

‘’Moja ya vitu vilivyonifurahisha mwaka jana kwenye mjadala niliwaaomba sana kwamba hatuwezi kuendelea kuitaka Benki ya Dunia isaidie kwenye miradi mingine tu ni lazima nguvu kubwa ielekezwe pia kwenye miradi ya kilimo ambayo kwa sasa  msaada wa Benki ya Dunia katika miradi hiyo ni kidogo sana’’ alisema Dkt.Mpango.

Aidha Dkt.Mpango alielezea dhamira ya Tanzania kushirikiana na Benki ya Dunia ili kuanzisha programu itakayohakikisha kuwa tija inapatikana kwenye sekta nzima ya kilimo na mifugo, lakini pia kuweza kuyafikia masoko kwa mazao yanayozalishwa nchini, hasa yale yenye thamani kubwa duniani.

 Dkt. Mpango amefafanua kuwa Benki ya Dunia imeridhishwa na kasi ya mabdiliko inayofanyika katika sekta ya kilimo kwa maana ya uzalishaji kuongezeka, lakini vile vile  wakulima wa kati wamezidi kuongezeka.

Aidha, kuongezeka kwa maeneo ya kilimo imewafurahisha wataalamu wa Benki hiyo, ikiwa ni pamoja na  kuongezeka kwa aina ya mazao yanayolimwa   hasa yale yenye thamani kubwa ambayo yanalimwa  kwa kasi kubwa sana kuliko ilivyokuwa awali.

Pia Dkt. Mpango alisisitiza kuwa, Benki ya Dunia imeshafanya utafiti wao wa kutosha ambao umeonesha kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo kwa maana ya uzalishaji kuongezeka.

Mhe. Mpango aliishukuru Benki ya Dunia kwa kukubali tena kuleta timu ya wataalamu nchini Tanzania ambayo itakaa na sekta nzima ya kilimo na ufugaji ili kuona ni namna gani hasa Benki ya Dunia itasaidia kuinua sekta hiyo, na  kuwasaidia wakulima hasa katika matumizi ya nguvu kazi kwa upande mmoja na kuwaongezea kipato kwa upande mwingine.

Mwisho

Tigo yazindua promosheni ya Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo Mkoani Dodoma

$
0
0
Kampuni inayolenga kuleta mageuzi ya kidigitali katika maisha ya watanzania, Tigo, leo imetangaza promosheni kabambe ijulikanayo kama Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo jijini Dodoma.Promosheni hiyo inaenda sambamba na msimu wa Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako ambayo ilizinduliwa jijini Mwanza na itamalizika jijini Dar es Salaam.

Wateja wa Tigo wanaoshiriki katika promosheni ya Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo kwa mara ya kwanza wana nafasi ya kushinda hadi Sh1 milioni kila wiki huku mshindi wa jumla ataweza kujinyakulia gari mpya aina ya Renault Kwid yenye thamani ya Sh23 milioni.

Washindi wa promosheni hiyo hutangazwa kila wiki na ili kushiriki kwenye promosheni hiyo, wateja wanatakiwa kujisajili kwa kutuma neno MUZIKI kwenda 15571 au kwakutembelea tovuti www.tigomusic.co.tz nakuchagua neno ‘Trivia’.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini, Lilian Mwalongo alisema “Shindano hili ni sehemu ya mkakati wa Tigo wa kujumuika na kuungana na wateja wetu kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa wateja wa aina zote hapa nchini.”

Aidha, Mwalongo aliwajulisha wateja wa Tigo watakaoshiriki katika tamasha la Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako jijini Dodoma kwamba wanaweza kulipia tiketi kwa njia ya Tigo Pesa kwa Sh5,000/= au pesa taslimu kwa Sh7,000.

 “Kama kampuni inayolenga kuchochea matumizi ya digitali, tumejizatiti kutoa huduma zenye kukidhi mahitaji ya wateja kila siku.Ili kununua tiketi kupitia Tigo Pesa mteja anatakiwa kufuata hatua za kawaida za kutuma pesa na kutuma Sh 8,000/= kwenda namba 0678 888 888 na watapokea ujumbe wa kuthibitisha malipo ya tiketi,” alisema.

Pia, aliwahimiza wateja wa Tigo walioko Dodoma kusajili upya namba zao za simu kwa kutumia mfumo wa alama za vidole hasa wakati wa msimu huu wa Tigo Fiesta kabla ya mwezi Desemba.

Zoezi la kusajili namba za simu kwa mfumo wa alama za vidole linalenga kudhibiti matumizi mabaya ya huduma za mawasilaino na pia kuwawezesha wateja kutambulika ili kupata hudma zenye usalama zaidi ikiwamo huduma za kifedha pamoja na malipo ya huduma kama maji, umeme pamoja na televisheni.

Mwisho.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Ofisi Ya Bunge

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images