Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Bashe: Serikali Italinda Soko La Ndani La Pamba

$
0
0
Na Bashiri Salum, Wizara ya Kilimo
Serikali imesema inatakutana na wadau wa zao la pamba nchini mapema mwanzoni mwezi Novemba mwaka huu ili kujadili changamoto zilizopo za ukosefu wa soko la uhakika na upatikanaji wa viwanda vya kuchakata zao hilo.

Hayo yamesemwa jana (11.10.2019) na Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe wakati alipotembelea kiwanda cha Twenty One Century cha mjini Morogoro kukagua uzalishaji wa bidhaa za pamba.

Akiwa katika kiwanda hicho Naibu Waziri Bashe alibaini changamoto ya kiwanda kuzalisha bidhaa za pamba tani 24,000 kwa mwaka ambazo hazilingani na uzalishaji uliopo nchini.

“Kiwanda cha Twenty one Century ambacho ndicho chenye uzalishaji mkubwa kati ya viwanda vyote vya nguo hapa nchini lakini kinatumia tani elfu 24 tu za pamba kwa mwaka.” alisema Bashe .

Alibainisha kuwa wakulima mwaka huu wanategemea kuzalisha zaidi ya tani 700,000 tofauti na mwaka jana zilizalishwa takribani tani 400,000 hivyo kunahitajika viwanda vingi zaidi ili mkulima apate soko la uhakika.

Bashe amesema mkakati wa serikali ni kuona viwanda saba (ginnery) za Lugulu,Sola, KACU, Mbogwe, Chato, na Manawa zilizopo katika ukanda unaolima zao la pamba kwa wingi vinafufuliwa haraka.

Mkutano ujao wa wadau utawakutanisha Wawekezaji wa viwanda vya pamba ,Wachakataji wa pamba (Ginnery), Wizara ya Fedha, Wizara ya Viwanda na Biashara na Viongozi wa Vyama vya Ushirika ili kujadili changamoto zinazoikabili sekta ya pamba nchini.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Bashe amepokea malalamiko ya wawekezaji wa viwanda vya pamba kuhusu uwepo wa kanga na vitenge vinavyoingizwa nchini vikiwa na ubora hafifu toka nje , hali inayochangia kushusha bei ya bidhaa zinazotengenezwa Tanzania.

Naibu Waziri huyo ameahidi kufanyia kazi malalamiko haya ili kulinda soko la ndani na kuwezesha lengo la Serikali ya Awamu ya Tano kuimarisha uchumi wa viwanda linafanikiwa kwani malighafi ya viwanda inapatikana kwa wingi toka kwa wakulima.

Waziri wa Kilimo Amtaka Mkandarasi Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Maghala Na Vihenge Vya Kisasa Kanda Ya Sumbawanga

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Katavi
Waziri wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa maghala na vihenge vya kisasa kanda ya Sumbawanga kuongeza kasi ili kukamilisha haraka mradi huo kwa mujibu wa makubaliano.

Alisema kuwa kampuni iliyoteuliwa baada ya kushinda zabuni kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo ni UNIA ARAJ REALICZJE ya nchini Poland ambayo ilimteua mkandarasi msaidizi mzawa anayejulikana kwa jina la ELERAI CONSTRUTION CO. LTD wa Arusha, hivyo napaswa kuongeza kasi ya ujenzi kutokana na kasi iliyopo kwa sasa kutoridhisha.

Waziri Hasunga ameyasema hayo juzi tarehe 10 Octoba 2019 mara baada ya kutembelea ujenzi wa mradi huo kwenye Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi utakaowanufaisha wakulima wa mazao ya nafaka kwani serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) pamoja na Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko (CPB) itakuwa na uwezo wa kununua mazao mengi kwa wakulima na kuyahifadhi kwa muda mrefu.

Alisema kuwa kampuni hiyo inayojenga vihenge vya kisasa na miundombinu mingine ikiwemo maghala katika eneo la Kanondo Manispaa ya sumbawanga mkoani Rukwa na Mpanda Mkoani Katavi bado haijamfurahisha kutokana na kasi ndogo ya ujenzi wa mradi.

Mhe Hasunga amesema kuwa serikali imekusudia kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka nchini ili kuwanufaisha wakulima punde wanapovuna mazao yao hususani nafaka kwani kufanya hivyo wakulima wataongeza uzalishaji na tija kwenye mazao na kuliongezea Taifa pato kubwa.

Alisema kuwa vihenge hivyo vitakuwa na uwezo wa kuhifadhi jumla ya Tani 20,000 za nafaka huku ujenzi wa miundombinu mingine ukiendelea kama jingo la Ofisi ya utawala, Ghala la kawaida la ujazo wa Tani 5000 za nafaka, na Mzani mkubwa wa daraja (Electronic weighbridge).

Mradi huo utakuwa na gharama ya Dola za kimarekani 6,019,399 ambazo ni takribani shilingi za Kitanzania Bilioni 14 kwa mradi wa eneo la Kanondo Sumbawanga na vilevile Dola za Kimarekani 6,180,857 sawa na fedha za kitanzania Shilingi Bilioni 14.2

Mhe Hasunga ametilia nyundo kuwa serikali haitaongeza muda kwa mkandarasi endapo atashindwa kukamilisha mradi huo kwa wakati uliopangwa.

Muda wa mradi kuanza hadi kukamilika ni jumla ya miezi 18 (Mwaka mmoja na nusu), Kwa upande wa Mpanda mkoani Rukwa mradi umeanza tarehe 14 Januari 2019 na umepangwa kukamilika tarehe 14 Julai 2020 wakati upande wa Kanondo mkoani Katavi mradi huo umeanza tarehe 8 Septemba 2019 na unatarajiwa kukamilika tarehe 8 Machi 2021.

Punde mradi huu utakapokamilika mkoa wa Rukwa utakuwa na Maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) yenye uwezo wa kuhifadhi nafaka za Tani 58,500 wakati mkoa wa Katavi utakuwa na uwezo wa kuhifadhi Tani 28,000 ikihusisha pia maghala ya zamani.

MWISHO

Waziri Mkuu Azindua Mradi Wa Kitalu Nyumba Kwa Vijana Kwa Nchi Nzima

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya tano imeamua kupambana na ukosefu wa ajira kwa vijana kwa kuanzisha programu za kuongeza na kurasimisha ujuzi.

“Mwelekeo wa Serikali hivi sasa ni kuendeleza viwanda na viwanda hivi vinahitaji malighafi kutokana na mazao. Tumeamua kuongeza malighafi kupitia kilimo, lengo ni kuwafanya vijana waweze kuajiriwa kwenye sekta hii kubwa ya uzalishaji,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Alhamisi, Oktoba 10, 2019) wakati akizindua mradi wa kitaifa wa mafunzo ya ujenzi na kilimo cha kisasa kwa kutumia teknolojia ya kitalunyumba (greenhouse) kwenye viwanja vya maonesho vya Ngongo, mjini Lindi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya vijana kitaifa kwa mwaka 2019.

“Nataka vijana muondokane na dhana ya kwamba kuwa na ajira ni lazima uwe umekaa mezani na umeshika kalamu. Ajira ni kazi yoyote ya halali inayompatia mtu kipato iwe ni biashara ndogondogo, mamalishe au bodaboda.”

Akifafanua kuhusu teknolojia ya kitalunyumba, Waziri Mkuu alisema: “Programu hii inasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu. Serikali inayoongozwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imeweka msisitizo kwenye kilimo lakini tunaangalia na aina ya kilimo tulichonacho.”

“Maeneo mengi nchini hayana mvua za kutosha. Kwa hiyo tumeanzisha kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone na siyo kwa kuchimba mifereji. Kitalunyumba kinahitaji nafasi chini ya robo eka, na humo ndani kuna matuta manne tu. Kwa kutumia tenki la maji, unatumia maji kidogo sana kwa kila mche, kwa sbabu yanatoka kwa matone,” alisema.

Alisema mtu yeyote mwenye eneo la kutosha anaezaa kutumia teknolojia ya kitalunyumba wakiwemo wafanyakazi ili wapate mazao ya kujiongezea mapato. “Unaweza kulima mahindi ukala mwaka mzima, unaweza kulima vitunguu au mboga za majani ukauza na siyo nyanya peke yake, hawa wamepanda nyanya kwa sababu ni mfano tu,” alisisitiza.

Akitaja faida zake, Waziri Mkuu alisema mche wa kwenye kitalunyumba unadumu kwa muda mrefu, haupati magonjwa na unazaa kwa wingi. “Mche mmoja unaweza kuzalisha kilo 30 na ndani ya kitalunyumba kimoja kuna miche 580. Nimeambiwa nyanya tisa tu, zinajaa kilo moja. Hii ni fursa ambayo kila mmoja anaweza kulima akiwa nyumbani kwake,” aliongeza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo, Waziri wa Nchi OWM - Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Bi. Jenista Mhagama alisema Serikali ilifanya utafiti na kubaini kwamba asilimia 56 ya nguvukazi nchini ni vijana lakini wanakabiliwa na changamoto ya kukosa ajira.

“Katika utafiti mwingine wa Serikali, tulibaini kuwa kundi kubwa la vijana linaajiri na kuajiriwa lakini pia vijana hawa wanakosa ujuzi unaotambulika rasmi ndiyo tukaja na mkakati wa Taifa wa uwezeshaji wa vijana kwa kuboresha mazingira na kuwapa stadi na ujuzi mbalimbali unaohitajika katika soko la ajira. Stadi na ujuzi huu utawawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.”

Alisema mradi wa kitalunyumba ni mradi wa kiprogramu ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu na umelenga kuwapa vijana stadi za kilimo ili waweze kujiajiri au kuajiri wenzao. “Ofisi yako kupitia programu hii inatekeleza mradi wa kilimo cha kisasa kupitia teknolojia ya kitalu nyumba (greenhose) kwa vijana.”

“Mradi wa kitalunyumba ni ujuzi kwenye shamba wa kuwasaidia vijana kulima mazao ambayo yatawasaidia vijana kupata masoko, yatawasaidia wajiajiri ama kuajiri wenzao na kuongeza pato la Taifa,” alisema.

Alisema uzinduzi uliofanywa katika viwanja vya Ngongo unawakilisha vitalunyumba vyote nchini chini ya mradi utakaohusisha vijana 18,000 ambapo kila Halmashauri ina vijana 100 wanaoshiriki kwenye mradi huo ambao watanufaika na mafunzo ya kilimo cha kisasa.

Alisema hadi Septemba 2019, jumla ya vijana 8,700 kutoka katika Halmashauri 83 za mikoa 12 wamepatiwa mafunzo ya ujenzi na kilimo ndani ya kitalunyumba. Mikoa hiyo ni Mwanza, Iringa, Ruvuma, Shinyanga, Geita, Mbeya, Lindi, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Kagera na Simiyu. Alisema maandalizi ya kutoa mafunzo kwa vijana kutoka katika Halmashauri 102 zilizobaki za mikoa 14 yamekamilika, na yataanza kutolewa kabla ya Novemba, 2019.

Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu imetoa zabuni za kuendesha mafunzo hayo kwa kampuni zinazomilikiwa na vijana wa Kitanzania wenye taaluma za kilimo ambao ni wahitimu wa elimu ya juu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA). Kampuni zilizopewa kazi ya kufundisha vijana wenzao ni Sokoine University Graduates Corporation (SUGECO), Royal Agriculture Ltd na Holly Green Agriculture  Group Ltd.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Waziri Mkuu Azindua Mradi Wa Kitalu Nyumba Kwa Vijana Kwa Nchi Nzima

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya tano imeamua kupambana na ukosefu wa ajira kwa vijana kwa kuanzisha programu za kuongeza na kurasimisha ujuzi.

“Mwelekeo wa Serikali hivi sasa ni kuendeleza viwanda na viwanda hivi vinahitaji malighafi kutokana na mazao. Tumeamua kuongeza malighafi kupitia kilimo, lengo ni kuwafanya vijana waweze kuajiriwa kwenye sekta hii kubwa ya uzalishaji,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Alhamisi, Oktoba 10, 2019) wakati akizindua mradi wa kitaifa wa mafunzo ya ujenzi na kilimo cha kisasa kwa kutumia teknolojia ya kitalunyumba (greenhouse) kwenye viwanja vya maonesho vya Ngongo, mjini Lindi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya vijana kitaifa kwa mwaka 2019.

“Nataka vijana muondokane na dhana ya kwamba kuwa na ajira ni lazima uwe umekaa mezani na umeshika kalamu. Ajira ni kazi yoyote ya halali inayompatia mtu kipato iwe ni biashara ndogondogo, mamalishe au bodaboda.”

Akifafanua kuhusu teknolojia ya kitalunyumba, Waziri Mkuu alisema: “Programu hii inasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu. Serikali inayoongozwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imeweka msisitizo kwenye kilimo lakini tunaangalia na aina ya kilimo tulichonacho.”

“Maeneo mengi nchini hayana mvua za kutosha. Kwa hiyo tumeanzisha kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone na siyo kwa kuchimba mifereji. Kitalunyumba kinahitaji nafasi chini ya robo eka, na humo ndani kuna matuta manne tu. Kwa kutumia tenki la maji, unatumia maji kidogo sana kwa kila mche, kwa sbabu yanatoka kwa matone,” alisema.

Alisema mtu yeyote mwenye eneo la kutosha anaezaa kutumia teknolojia ya kitalunyumba wakiwemo wafanyakazi ili wapate mazao ya kujiongezea mapato. “Unaweza kulima mahindi ukala mwaka mzima, unaweza kulima vitunguu au mboga za majani ukauza na siyo nyanya peke yake, hawa wamepanda nyanya kwa sababu ni mfano tu,” alisisitiza.

Akitaja faida zake, Waziri Mkuu alisema mche wa kwenye kitalunyumba unadumu kwa muda mrefu, haupati magonjwa na unazaa kwa wingi. “Mche mmoja unaweza kuzalisha kilo 30 na ndani ya kitalunyumba kimoja kuna miche 580. Nimeambiwa nyanya tisa tu, zinajaa kilo moja. Hii ni fursa ambayo kila mmoja anaweza kulima akiwa nyumbani kwake,” aliongeza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo, Waziri wa Nchi OWM - Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Bi. Jenista Mhagama alisema Serikali ilifanya utafiti na kubaini kwamba asilimia 56 ya nguvukazi nchini ni vijana lakini wanakabiliwa na changamoto ya kukosa ajira.

“Katika utafiti mwingine wa Serikali, tulibaini kuwa kundi kubwa la vijana linaajiri na kuajiriwa lakini pia vijana hawa wanakosa ujuzi unaotambulika rasmi ndiyo tukaja na mkakati wa Taifa wa uwezeshaji wa vijana kwa kuboresha mazingira na kuwapa stadi na ujuzi mbalimbali unaohitajika katika soko la ajira. Stadi na ujuzi huu utawawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.”

Alisema mradi wa kitalunyumba ni mradi wa kiprogramu ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu na umelenga kuwapa vijana stadi za kilimo ili waweze kujiajiri au kuajiri wenzao. “Ofisi yako kupitia programu hii inatekeleza mradi wa kilimo cha kisasa kupitia teknolojia ya kitalu nyumba (greenhose) kwa vijana.”

“Mradi wa kitalunyumba ni ujuzi kwenye shamba wa kuwasaidia vijana kulima mazao ambayo yatawasaidia vijana kupata masoko, yatawasaidia wajiajiri ama kuajiri wenzao na kuongeza pato la Taifa,” alisema.

Alisema uzinduzi uliofanywa katika viwanja vya Ngongo unawakilisha vitalunyumba vyote nchini chini ya mradi utakaohusisha vijana 18,000 ambapo kila Halmashauri ina vijana 100 wanaoshiriki kwenye mradi huo ambao watanufaika na mafunzo ya kilimo cha kisasa.

Alisema hadi Septemba 2019, jumla ya vijana 8,700 kutoka katika Halmashauri 83 za mikoa 12 wamepatiwa mafunzo ya ujenzi na kilimo ndani ya kitalunyumba. Mikoa hiyo ni Mwanza, Iringa, Ruvuma, Shinyanga, Geita, Mbeya, Lindi, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Kagera na Simiyu. Alisema maandalizi ya kutoa mafunzo kwa vijana kutoka katika Halmashauri 102 zilizobaki za mikoa 14 yamekamilika, na yataanza kutolewa kabla ya Novemba, 2019.

Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu imetoa zabuni za kuendesha mafunzo hayo kwa kampuni zinazomilikiwa na vijana wa Kitanzania wenye taaluma za kilimo ambao ni wahitimu wa elimu ya juu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA). Kampuni zilizopewa kazi ya kufundisha vijana wenzao ni Sokoine University Graduates Corporation (SUGECO), Royal Agriculture Ltd na Holly Green Agriculture  Group Ltd.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili October 13

Ujerumani, Ufaransa, Uholanzi Zasitisha Mauzo ya Silaha kwa Uturuki Baada ya Kuivamia Kijeshi Syria

$
0
0
Ujerumani haitaidhinisha tena mauzo ya silaha  ambazo zinaweza kutumika katika mashambulizi ya kijeshi ya Uturuki kaskazini mwa Syria, waziri wa mambo ya kigeni Heiko Maas ameliambia gazeti la Bild am Sonntag.

"Kutokana  na mashambulizi  ya  kijeshi  ya  Uturuki kaskazini mashariki  mwa Syria , serikali  ya shirikisho haitatoa  tena vibali vipya  kwa  ajili  ya  vifaa  vya  kijeshi  ambavyo vinaweza  kutumika na  Uturuki nchini  Syria," Maas  amesema.

Maas  aliongeza kwamba  serikali  ya  Ujerumani  tayari imeweka vizuwizi katika  mauzo ya  nje ya  silaha  zake  kwa  Uturuki katika mwaka  2016 kutokana  na  mashambulizi  ya  nchi  hiyo katika  jimbo la  Afrin.

Washirika  wa  mataifa  ya  magharibi wamekosoa operesheni  ya Uturuki ndani  ya  Syria, ambayo  ilianza siku  ya  Jumatano , ikisema inatishia  mzozo  mkubwa  wa  kibinadamu pamoja  na  kufufua  kundi la itikadi  kali la  Kiislamu  linalojiita  Dola  la  Kiislamu  katika  eneo hilo.

Siku  ya  Jumamosi , wizara ya  mambo  ya  nje  na  ulinzi mjini  Paris zilisema  kuwa  Ufaransa  inasitisha  mauzo  yake  ya  silaha  kwa Uturuki  kutokana  na  mashambulizi  ya  Uturuki kaskazini  mwa Syria.

Serikali  mjini  Paris imeamua  kusitisha  mipango  yote ya  mauzo ya  silaha  kwa  Uturuki  ambayo  inaweza  kutumiwa  katika mashambulizi, wizara  hizo zilisema  katika  taarifa  ya  pamoja.

Siku  ya  Ijumaa , Uholanzi ilisema  imesitisha  kwa  muda mauzo yake  ya  silaha  kwa  Uturuki, na  Sweden  ikasema itatafuta kuungwa  mkono kwa  ajili  ya  kuwekewa  vikwazo  vya  Silaha Uturuki  na  mataifa  yote  ya  Umoja  wa  Ulaya katika  mkutano  wa mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Umoja  huo wiki  ijayo.

-DW

Naibu Waziri Wa Madini Alitembelea Eneo Lenye Mgogoro Wa Wachimbaji Wadogo

$
0
0
Serikali imeingilia kati mgogoro uliodumu kwa muda mrefu katika eneo la wachimbaji wadogo lililopo katika Mlima wa Sakenke kata ya Misigiri Wilaya ya Iranga Mkoani Singida.
 
Mgogoro huo uliodumu kwa takribani miaka 3 ni kati ya mchimbaji mdogo aliyekuwa afisa usalama  wa taifa mstaafu John Lutebeka, na Nabii Elia wote wanagombea eneo hilo ambalo Lutebeka anamiliki ardhi ya juu na Elia ameliombea Leseni ya Uchimbaji Madini.
 
Akizungumza kwenye eneo linalogombewa, Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, amewataka Lutebeka, Nabii Elia na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Chone Malembo wafike ofisini kwake Jijini Dodoma siku ya Jumatano Oktoba 16 mwaka huu kwa ajili ya kutatua mgogoro huo na kila mmoja aje na vielelezo vinavyomruhusu kuchimba madini katika eneo hilo.
 
Aidha, Nyongo amewataka Maafisa Madini kote Nchini kutoa elimu kwa wachimbaji juu ya sheria za madini ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima maana kuna haki ya umiliki wa ardhi ya juu na kuna haki ya umiliki wa ardhi ya chini kwa maana ya leseni ya uchimbaji hawa wote wana haki sawa wanaweza wakakaa wakazungumza  wakachimba pamoja.
 
Wakati huo huo Naibu Waziri Nyongo, amemtaka Nabii Elia aachane na uchimbaji wa madini karibu na nguzo za umeme anatakiwa awe mita 100 kutoka kwenye nguzo za umeme, vinginevyo atachukuliwa hatua.
 
Pia nyongo amewapongeza wachimbaji wa madini wa Mkoa wa Singida kwa ulipaji mzuri wa kodi na amesema rasilimali ya madini ni ya Watanzania wote, hatuko tayari kumuoneo mtu wala hatakubari mtu achimbe amdhulumu mwingine.
 
“Kwenye uchimbaji kuna kelele nyingi, kuna wengine wanamiliki leseni nyingi hata kuzihudumia hawawezi, mpaka sasa tumefuta leseni elfu 13 hivyo wale wanaojua wasitumie ujuaji wao kuwadhuru wengine tutampa haki mwenye haki yake,” alisema Nyongo.
 
Awali Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Malembo, alisema kwa nyakati tofauti, ofisi yake imesuluhisha  mgogoro huo, lakini Lutebeka huwa haridhiki na maamuzi tunayofikia ikabidi tuligawe eneo hilo leye hekari 7.2 na kumpa Lutebeka hekari 4 lakini bado hakuridhika.
 
Akizungumza kwa  masikitiko, Mkuu wa Wilaya ya Iramba Huhahuka amesema anasikitika kuingizwa kwenye mgogoro huo ambapo Afisa Usalama wa Taifa Mstaafu Lutebeka amekuwa akimtuhumu kuwa anawadhamini hao wanaotaka kuchimba eneo hilo.
 
Kwa mujibu wa Afisa Madini Mkazi wa Singida, Malembo amesema, kati ya Julai na Oktoba 11 mwaka huu, wamekusanya mapato ya zaidi ya shilingi 1.3 bilioni, Mapato hayo ni sawa na asilimia 271.94 ya lengo  kwa awamu ya kwanza la kukusanya shilingi 500,000,000, na asilimia 90.65 ya lengo la mwaka la kukusanya shilingi 1,500, 000,000/=.

Waziri Mhagama Ahimiza Vijana Kutumia Michezo Kuimarisha Mshikamano

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewamiza vijana nchini kutumia michezo ili kuimarisha amani, upendo na mshikamano.

Waziri Mhagama alitoa kauli hiyo wakati wa Bonanza la michezo kwa vijana lililofanyika katika shule ya Sekondari Lindi ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha wiki ya vijana nchini kuelekea kilele cha mbio za mwenge wa uhuru kwa mwaka 2019 na Kumbukizi ya Miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza hilo ambalo vijana walikusanyika kwa lengo la kushiriki katika michezo mbalimbali, Mheshimiwa Mhagama alieleza kuwa michezo imekuwa ikitumika kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha ushirikiano na kuwajengea vijana ari ya uzalendo.

“Kupitia michezo mnayofursa kama vijana kuendelea kuenzi falsafa za waasisi wa taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mzee Abeid Amani Karume ambao walikuwa wazalendo kwa taifa lao na waliimarisha muungano kwa maslahi ya watanzania wote,” alisema Mhagama

“Ni matumaini yangu kuwa kupitia michezo hii mtaendela kujikumbusha falsafa za waasisi hao kupitia michezo hii tunayoifungua leo kwa kuwa itatoa hamasa kwa vijana kupenda nchi yao na itajenga ari ya kuendeleza kuimarisha mshikamano kupitia michezo,” alisema Mhagama

Aliongeza kuwa michezo hiyo iliyowakutaisha vijana ikatumike kama sehemu ya kuwa na amani, uvumilivu na mshikamano.

“Vijana mnatakiwa kujenga taifa kwa vitendo vinavyodumisha amani, upendo na mshikamano kama ambavyo Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere alivyotujengea taifa lenye umoja,” alieleza Mhagama

Aidha Waziri Mhagama aliendelea kuwasihi vijana kutambua wajibu wao katika jamii na kuifanya michezo kuwa ni miongoni mwa mambo muhimu wanayopaswa kuyaendeleza katika kutekeleza mipango waliyonayo.

Pamoja na hayo alirejea ujumbe wa Mwenge wa uhuru mwaka huu ambao pia umesisitiza ushiriki wa wananchi katika uchaguzi wa Serikali za Mtaa. Aliwaomba vijana kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika uchaguzi ili waweze kupata viongozi bora kwa maendeleo ya taifa.

Waziri Mhagama alitumia fursa hiyo pia kuwapongeza wadau mbalimbali na vijana walioshiriki bonanza hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi alisema kuwa Bonanza hilo la michezo limejumuisha vijana kutoka sehemu mbalimbali ikiwa ni njia moja wapo ya kuwaendeleza vijana ili waweze kuimarika kiafya na kiakili.

MWISHO

Wilaya Ya Bukoba Mkoani Kagera Yafanikiwa Kwa Asilimia 82.4 Katika Zoezi la Uandikisha Wa daftari la mpiga kura Mkoani Humo

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Genelari Marco Elisha Gaguti ameendelea kuwasisitiza wananchi mkoani kagera kujitokeza  na kujiandikisha kwa wingi kwenye daftari la mpiga kura ndani ya siku mbili ambazo zimesalia kufikia tarehe 14 mwezi wa 9 mwaka huu ambapo itakuwa ni mwisho wa zoezi hilo.
 
Akizungumza na wananchi wa kata Kemondo katika mkutano wa hadhara, mkuu wa mkoa wa Kagera amebainisha tofauti iliyopo kati ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na zoezi la kujiandikisha katika daftari la mpiga kura ambapo amesema zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura lililohusisha pia uboreshaji wa taarifa mbalimbali za wananchi kuwa vitambulisho hivyo vilivyotolewa ni kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa madiwa,wabunge na Rais.
 
Brigedia Gaguti amesema kuwa zoezi linaloendelea kwasasa ni kwaajili ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa na vijiji,  hivyo amewataka wananchi ambao bado hawajajiandikisha kutumia vyema siku hizi mbili kujitokeza  nakujiandikisha katika vituo vilivyopo katika maeneo yao.
 
Sanjari na hayo Brigedia Gaguti ametoa pongezi kwa wananchi na viongozi wa halmashauri ya wilaya Bukoba kwa ushirikiano nakusema kuwa kwataarifa za awali zinazohusu uandikishaji wa wapiga kura zilizotolewa tarehe 11 mwezi huu wilaya ya Bukoba imefanikiwa  kwa asilimia 82.4 ambacho ni kiwango kikubwa ukilinganisha na wilaya za Karagwe,Kyerwa,Misenyi,Mleba,Ngara,Biharamulo pamoja na manisipaa ya Bukoba.
 
Hata hivyo mkuu wa mkoa amesema viongozi wa ngazi za mitaa na vijiji  ndio  viongozi muhimu na  watakaotumika kuleta maendeleo kutokana na ukaribu wao kwa wananchi katika kufikia uchumi wakati na wa viwanda kama ilivyo azima ya nchi.

Jinsi Ya Kuandika CV Nzuri Ambayo Itamvutia Mwajiri na Kukufanya Upate KAZI Kirahisi

$
0
0
WATU Wengi nchini wamekosa ajira na makampuni hupokea wastani wa maombi 200 ya kazi kwa tangazo moja la kazi. 

Hivyo, CV yako lazima ikae vizuri ili kumshawishi mwajiri. Utaratibu wa kuomba kazi inaweza ikawa tofauti kati ya makampuni na mashirika, ila yote yatahitaji uwatumie CV.

CV ni nini?
CV ni maelezo ya ujumla kwa kiundani ya historia yako ya kazi na shule. Kawaida, inatumika kwenye maombi ya kazi ya nafasi za kati, za juu na za utafiti.

Mambo yafuatayo yatasaidia kuifanya CV yako iwe bora na hivyo, kukusaidia kupata interview za kazi.

👉Soma na kuelewa maelezo ya kazi
Una ujuzi gani? Mwajiri anatafuta mfanyakazi wa aina gani? Maswali haya ni muhimu kujua kama utaiweza hiyo kazi au la. Pia, ni vizuri kujua nini hasa ni muhimu kwa muajiri na kufanya maombi yako yaendane zaidi na mahitaji ya mwajiri.

Kwa mfano, kama kazi inaweka umuhimu kwenye ujuzi wa kutumia mitandao ya kijamii kwa matangazo, hakikisha CV yako ina kazi zote zilizohitaji matumizi ya mitandao ya kijamii.

👉Andika maneno muhimu yaliyotumika kwenye maelezo ya kazi, uzitumie kwenye CV
Usichukue sentensi nzima kutoka kwenye maelezo ya kazi na ukaitumia vile vile kwenye CV yako. Ila, tumia lugha na baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye CV.

👉Fanya utafiti juu ya kampuni iliyotangaza kazi
Pamoja na kuchambua maelezo ya kazi, ni muhimu kufanya utafiti juu ya kampuni yenyewe. Kama wana tovuti au wapo kwenye mitandao ya kijamii, jaribu kujua ni kazi gani na sekta ipi wanayohusika nayo. 

Pia, ikiwezekana jaribu kuwajua wafanyakazi/meneja wa kampuni hiyo. Hii itakusaidia kujua maadili na muelekeo wa kampuni. Hii itakusaidia kuweka maombi yako ya kazi yaendane na kampuni hiyo.

👉Orodhesha ujuzi wako wakufanya kazi
Hapa, usiweke kazi zote ulizozifanya maishani mwako ila, weka zile ambazo zilikuongezea ujuzi utakayo kusaidia kufanya kazi unayoomba.

==>Format/Staili inayotumika zaidi kwenye kuandika CV:
   1. Lengo la CV na ujuzi wako
    2.Ujuzi wako wa kazi
   3. Mafanikio maalum
   4. Elimu
   5. Ujuzi muhimu binafsi

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬
Angalizo:
  1.  Tumia maandishi ya kawaida ya Times New Roman
  2.  Tumia size 9 – 12 ya herufi
  3.   Hakikisha unatumia staili moja ya kuandaa CV kote
  4.   CV isiwe zaidi ya ukursasa 2
  5.   Usitumie sentensi ndefu
  6.  Hakikisha CV yako inasomeka kiurahisi na inawasilisha   mafanikio yako kwa uwazi.
  7.  Anza na kazi yako ya sasa hivi au ya hivi karibuni alafu rudi nyuma.
   ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 
   ==>.Hakikisha Yafuatayo:
1.Ukiwa unaandika jina la kampuni uliyo fanya kazi, andika jina la kampuni kikamilifu. 
2.Eleza kwa ufupi kampuni yao inahusika na nini. Tatu, weka muda uliyofanyakazi hapo (mwezi na mwaka).  
3.Baada ya hapo, orodhesha kazi na majukumu lako kwenye hilo kampuni.
4.Usidanganye

👉Maandalizi ya Mwisho

1.Pitia kila kitu kwa mara ya mwisho
 -Print CV yako alafu ipitie. Hii huwa inasaidia kuona makosea yako.

2.Mpe Rafiki  yako apitie CV
-Muombe rafiki yako apitie CV yako. Macho manne ni bora zaidi ya mawili!

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

Hatua ya kwanza kwenye kupata kazi unayotaka ni kutuma maombi. Tunatumaini kwamba maelezo yaliyoelezwa humu yatakusaidia kuandaa CV bora kwa ajili ya mwajiri.

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kuandika CV safi, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini.

AU 

PICHA: Kangi Lugola Ajiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amejiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, katika Kituo cha Senta, Kijiji cha Nyamitwebili, Jimbo la Mwibara, Wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, leo Oktoba 13, 2019.

Wakurugenzi Wa Halmashauri Wana Wajibu Wa Kusimamia Utendaji Sekta Ya Ardhi

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM MWANZA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Wakurugenzi wa halmashauri nchini kuelewa kuwa pamoja na watumishi wa sekta ya ardhi kuhamishiwa Wizara ya Ardhi lakini bado wana jukumu la kusimamia utendaji wa sekta hiyo.

Dkt Mabula alitoa kauli hiyo jana alipofanya ziara katika halmashauri ya jiji la Mwanza pamoja na Manispaa ya Ilemela akiwa katika ziara ya kukagua utendaji wa sekta ya ardhi katika Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Mwanza, Simiyu, Mara na Geita.

Alisema, tangu watumishi wa sekta ya ardhi walivyohamishiwa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakurugenzi wengi wa halmashauri wameona kama wamejivua kusimamia utendaji wa watumishi wa sekta hiyo jambo alilolieleza kuwa siyo sahihi kwa kuwa mamlaka ya upangaji Majiji, Miji na Manispaa unabaki kwa halmashauri.

‘’kazi pekee inayosimamiwa na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa watumishi wa sekta ya ardhi ni katika masuala ya nidhamu na ajira ambapo katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi anawajibika’’ alisema Dkt Mabula.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema katika kuboresha sekta ya ardhi nchini huduma za sekta hiyo sasa zimesogezwa katika mikoa badala ya kutegemea ofisi za Kanda alizozieleza kuwa ziko mbali kwa baadhi ya mikoa jambo linalowafanya wananchi kushindwa kupata huduma kwa urahisi.

Katika kufanikisha hilo Dkt Mabula aliwataka Wakuu wa mikoa kuharakisha uanzishwaji ofisi za mikoa kwa kutenga ofisi ili wananchi waweze kupata huduma za ardhi bila usumbufu ambapo alitolea mfano wa mikoa ya Tanga, Ruvuma, Mtwara na Simiyu kuwa tayari ishatenga ofisi kwa ajili ya mikoa yake.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Ziwa Makwasa Biswalo alisema mkakati wa ofisi yake kwa mwaka huu ni kuhakikisha uanzishaji ofisi za mikoa usaidie kupunguza changamoto za sekta ya ardhi katika mikoa mbalimbali.

Akiwa katika ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Dkt Mabula lielezwa na Mkuu wa Idara ya Mipango Miji na Ardhi katika halmashauri hiyo Shukurani  Kyando kuwa, halmashauri hiyo imekuwa na mafanikio makubwa katika utoaji hati, urasimishaji na upimaji maeneo  mbalimbali ingawa imekuwa na changamoto kubwa ya utapeli unaofanywa na madali kwa kuuza kiwanja kimoja kwa mtu zaidi ya mmoja.

Hata hivyo, alisema katika kukabiliana na utapeli huo tayari wamewakama matapeli saba na baadhi yao tayari wamefikishwa katika vyombo vya sheria huku mmoja akikabidhiwa kwa Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa (Takukuru) na kuwataka wananchi wanaotaka kununua viwanja kuhakikisha wanajiridhisha katika ofisi za ardhi ama ofisi za ardhi za kanda ili kuepuka kutapelewa.

Uteuzi wa Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Maji


Nafasi Za Kazi 12 Toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

$
0
0
Nafasi Za Kazi  12  Toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  imetangaza nafasi 12 za Kazi. Mwisho wa kutuma Maombi ni Tarehe 25 mwezi huu wa 10,2019

👉 ICT Officers (System Developers)- Nafasi 10

👉 Assistant Lecturer-Nafasi 1

👉 Rating II-Nafasi 1
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

==>>Pia zipo nafasi mbalimbali za kazi UBER TANZANIA, VODACOM, AIRTEL, JUMIA, NOKIA TANZANIA

Bonyeza hapo chini kujua zaidi

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Jamii Yaaswa Kushiriki Kuzuia na Kupunguza Athari za Maafa

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
Jamii imeaswa kushiriki kikamilifu katika kuzuia na kupunguza athari za maafa pale yanapotokea katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
 
Aklizunmgumza leo Oktoba 13, 2019 Jijini Dodoma wakati wa maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Upunguzaji wa Athari za Maafa Duniani ambapo alikuwa mgeni rasmi, Katibu mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko amesema suala hilo linahitaji ushirikiano wa jamii nzima.
 
“Tumekutana leo hapa tukishirikiana na wenzetu Duniani kote kukumbushana mbinu na mikakati ya kupambana na maafa ikiwemo kuweka mikakati ya kupunguza maafa yanapotokea katika maeneo yetu”Alisisistiza Bi Mwaluko
 
Akifafanua amesema kuwa, Wanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) wanaosomea Shahada ya udhibiti wa maafa katika mazingira washiriki kikamilifu katika kutoa elimu kuhusu maafa katika shule za Sekondari na msingi zilizopo hapa Dodoma  kupitia chama cha udhibiti wa maafa katika chuo hicho.
 
Aliongeza kuwa wanafunzi hao wanatakiwa kuwa chachu katika kutoa elimu kuhusu maafa ili kupanua wigo wa elimu na kuagiza chama hicho kuhakikisha kuwa kinawasilisha mpango wake wa utoaji elimu katika Ofisi yake.
 
Aidha, Bi Mwaluko ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kujiandikisha ili waweze kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa na kuchagua viongozi watakaosaidia katika kuleta maendeleo kwa kusimamia kikamilifu rasilimali zinazotolewa na Serikali kwa maslahi ya wananchi.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, Ofisi ya Waziri mkuu, Kanali Jimmy Said amesema kuwa Sera ya Maafa inaelekeza kikamilifu majukumu ya kamati za maafa katika ngazi zote ili kurahisisha mawasiliano na kuimarisha utendaji .
 
Aliongeza kuwa kila mwananchi anapaswa kutimiza wajibu wake katika eneo lake ili kupunguza athari za maafa pale yanapotokea.
 
Siku ya maafa huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 13, ya kila mwaka ili kuwaleta pamoja wadau kujadili na kuweka mikakati ya pamoja katika kupambana na maafa.


Serikali Kuzipatia Ruzuku Kaya Zote Maskini Nchini Baada Ya Kuridhishwa Na Maendeleo Wanufaika Wa Tasaf

$
0
0
Na James K. Mwanamyoto-Nyasa
Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imeahidi kuzinufaisha kaya zote maskini nchini baada ya kuridhishwa na namna wananchi katika vijiji vilivyonufaika na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini walivyoboresha maisha yao na kujikwamua katika lindi la umaskini liliokuwa likiwakabili.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati akizungumza na wanufaika na wananchi wa kijiji cha Nangombo wilayani Nyasa akiwa katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Mpango huo wilayani humo.

Mhe. Mkuchika amefafanua kuwa, iwapo wanufaika wasingetumia ruzuku vizuri kuboresha maisha, Serikali isingesita kusimamisha utekelezaji wa Mpango huu wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

“Hongereni wanufaika wa TASAF kijiji cha Nangombo na maeneo mengine kwa kutumia ruzuku kuboresha maisha yenu, kujenga nyumba bora, kununua vifaa vya shule kwa ajili ya watoto na kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi,” Mhe. Mkuchika amepongeza.

Mhe. Mkuchika ameongeza kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano imeridhika na mafanikio yaliyopatikana, hivyo itaendeleza vita dhidi ya umaskini, lengo likiwa ni kuboresha maisha ya kaya zote maskini nchini.

Akiwasilisha taarifa ya kijiji cha Nangombo kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini, Afisa Mtendaji wa kijiji hicho, Bw. Joseph P. Ngogi amesema watoto 66 wa shule wananufaika na ruzuku inayotolewa hivyo imeongeza mahudhurio shuleni na kliniki kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, aidha kaya 65 zimeboresha makazi yao kwa kujenga ama kukarabati na kuezeka kwa bati.

Mmoja wa wanufaika wa Mpango wa TASAF kijiji cha Nangombo, Bi. Mariana Mkwaila amesema ruzuku anayoipata imemuwezesha kuwanunulia watoto wake sare za shule, viatu na madaftari ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba kubwa ambayo anatarajia kuizeka kwa bati hivi karibuni.

Naye, Bi. Elizabeth Damian amesema, alikuwa akiishi maisha ya kimaskini kwenye nyumba ya nyasi kabla ya kuingizwa kwenye Mpango, lakini baada ya kuanza kupokea ruzuku ameweza kufuga kuku, mbuzi na kufyatua tofali zilizomuwezesha kujenga nyumba iliyoezekwa kwa bati.

Mhe. Mkuchika amehitimisha ziara yake ya kikazi mkoani Ruvuma kwa kuitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma na kukagua utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wilayani humo.

Hazina Saccos Kuwekeza Mradi Wa Bilioni 52 Dodoma

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
CHAMA cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina Saccos kimeazimia kujenga kitega uchumi cha kisasa kwa gharamaya  Shilingi bilioni 52 kupitia mradi wa Njedengwa katika Jiji la Dodoma ili kukuza uchumi wa mkoa wa Dodoma na Taifa kwa kupitia kodi.

Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi wa chama hicho cha Ushirika Bw. Aliko Mwaiteleke  wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka  uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Hazina,  na kuongeza kuwa mradi huo upo katika hatua za mwisho za utekelezaji wake.

Mwaiteleke alisema mpaka sasa upembuzi yakinifu wa mradi huo utakaojengwa kwa njia ya ubia kati ya Hazina Saccos na mwekezaji kwenye neo lenye ukubwa wa ekari 22  kupitia utaratibu wa Jenga, Endesha na Hamisha (Build, Operate and Transfer - BOT) ambapo mwekezaji atagharamia ujenzi wote na kuendesha kwa muda ambao utakubaliwa ndani ya mkataba.

Alisema mradi huo unasimamiwa na Kamati ya watu Saba wakiongozwa na Profesa Esta Eshengoma kutoka Chuo Kiuu Cha Dar es Salaam na wajumbe wake kutoka Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru),  Bodi ya Manunuzi ya Umma (PSPTB), Kituo Cha Uwekezaji (TIC), na Chuo Kikuu cha Ardhi ambao kwa sasa wanafanya kazi ya kusaka mwekezaji ili kufanikisha mradi huo.

Bw. Mwaiteleke alifafanua kuwa Mradi wa Njedengwa upo mbioni kuanza  na unategemewa kuwa chachu ya maendeleo ya chama hicho kwa kukiingizia kipato kutokana na shughuli zitakazokuwa zikifanyika kupitia mradi huo.

Alifafanua kuwa  mradi huo utahusisha ujenzi wa hoteli ya kisasa, kumbi za  mikutano, majengo ya Ofisi,  Viwanja vya Michezo na bwawa maalum la kuogelea.

Aidha alisema Chama hicho cha Hazina Saccos ambacho kina wanachama 5,600 kina mtaji mtaji wenye thamani ya shilingi bilioni 10 ikiwa ni fedha taslimu na mali wanazozimiliki ikiwemo ardhi ambazo zimekuwa na manufaa makubwa kwa wanachama..

"Mwaka jana pekee kupitia akiba na mikopo  tulipata faida ya shilingi milioni 64 na kila mwanachama alipewa gawio la asilimia 20 kulingana na hisa zake"alisema Mwaiteleke.

Alisema faida nyingine waliyopata kupitia Hazina Saccoss ni kununua viwanja 150 katika maeneo mbali mbali ya mkoa wa Dar es Salaam na Pwani na kuwakopesha wanachama wao kwa bei nafuu ambapo wanalipa kidogo kidogo kwa miezi 60.

"Pia Dodoma tumenunua viwanja 897 katika maeneo ya Ihumwa Ngaloni, Iyumbu  (maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambavyo tumevigawa kwa wananchi na viwanja vya Nzuguni tutaanza kuvigawa baada ya taratibu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kukamilika ili kuwawezesha wanachama wetu waliohamia Dodoma kupata maeneo ya kujenga makazi yao” alisema Bw. Mwaiteleke

Naye Meneja wa Hazina Saccos Bw. Festo Mwaipaja, alisema Saccoss hiyo sio ya wafanyakazi wa Wizara ya Fedha peke yake bali watumishi wote wa serikali wanaruhusiwa kujiunga na chama hicho isipokua vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo ni jeshi, Polisi, na Usalama wa  Taifa.

Alisema kwa mtumishi wa umma kujiunga na chama hicho cha ushirika mbali na kuwa muajiriwa pia atapaswa kulipa kingilio cha shilingi 20,000 na kununua hisa kuanzia 20 ambazo kila hisa moja ni shilingi 10,000 na kufanya thamani ya hisa zote kuwa shilingi 200,000.

Aidha alisema kuna mchango wa shilingi 20,000 kila mwezi na kuwataka watumishi wa umma kutoka taasisi na idara zote za serikali kuchangamkia fursa ya kujiunga na ushirika huo ili kujiinua kiuchumi

Kuhusu viwanja, Bw. Mwaipaja alieleza kuwa Chama hicho kimetumia zaidi ya shilingi bilioni 4 kununua viwanja katika Jiji la Dodoma na kuchangia eneo hilo kuwa na mzunguko mkubwa wa fedha kwa wenyeji na kwamba hayo ni mafanikio yanayoihusu jamii.

Akifungua Mkutano Mkuu huo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Mary Maganga, ameipongeza Hazina Saccos kwa kuwapatia viwanja wanachama wake na kuwataka wanachama waliopata fursa ya kupata viwanja hivyo waviendeleze haraka ili kuodokana na changamoto ya malazi kwa kuwa baadhi walipata viwanja hivyo tangu mwaka uliopita, 2018.

Aidha, ameipata kongole Hazina Saccos kwa hatua waliyofikia ya kutafuta mwekezaji katika mradi wa Njedengwa ambao utaongeza mapato ya Ushirika na kuwataka viongozi na wanachama kuhakikisha wanazingatia taratibu Sheria na Kanuni ili kufanikisha mradi huo muhimu.

Mwisho

Waziri Lugola Aagiza Polisi Kuwakamata Wanaowapotosha Wananchi Uandikishaji Uchaguzi Serikali Za Mitaa

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA, Mwibara
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameliagiza Jeshi la Polisi Nchini, kuwakamata na kuwafunguliwa mashataka watu ambao wanawapotosha wananchi kutokujitokeza kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Lugola amesema watu hao wanawarubuni wananchi kwa njia za mitandao ya kijamii, kuwafuata majumbani kwao, wakiwapotosha kususia uchaguzi huo, pamoja na kuwadanganya kuwa walishajiandikisha kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, hivyo watatumia vitambulisho hivyo hivyo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 24, 2019.

Akizungumza na wananchi Jimboni kwake Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, mara baada ya kujiandikisha katika kituo cha Sokoni, Kata ya Kibara, alisema taarifa hizo amepewa na viongozi wa Serikali ya Kijiji pamoja na vyanzo mbalimbali, kuwa kuna kundi la wananchi wanapita mitaani kuwapotosha wananchi na pia kuwatisha wasifike vituoni kujiandikisha wakiwa na lengo la kuvuruga uchaguzi.

“Wananchi Kibara, wacha niwaambie, Serikali ya awamu ya tano si ya kuchezewa, watu hao ni wapotoshaji na lengo lao wanataka kuvuruga uchaguzi ambao ni muhimu kwa maendeleo ya wananchi, sasa naagiza polisi kuwasaka na kuwakamata watu hao, ili wawe mfano,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, Wizara yake inalinda amani katika uchaguzi huo, hivyo haiwezi kukaa kimya kuwaacha wapotoshaji hao wakiendelea kuharibu na kutamba mitaa jambo ambalo Serikali haiwezi ikawaacha.

Pia aliwataka wananchi wajitokeze kwa wingi katika vituo mbalimbali nchini kujiandikisha ili waweze kuwachagua viongozi wao na kuiletea maendeleo nchi.

“Leo mmejitokeza wengi, nawapongeza, nafikiri wengi wenu mmekuja labda baada ya kuniona mimi mbunge wenu nimefika, lakini bado siku hazijaasha, waambieni wananchi wajitokeze kuja kujiandikisha leo, pamoja na Kesho, viongozi msichoke, fanyeni kazi kwa nguvu zote, kwa maendeleo ya jimbo let una nchi kwa ujumla,” alisema Lugola.

Alisema kupitia uchaguzi huo, viongozi wa vijiji na mitaa watasaidia Wizara yake baada ya kuwapata viongozi hao ambao pia wataunda Kamati ya ulinzi na usalama ya Kijiji na usalama wa eneo husika unaimarishwa zaidi kutokana na uwepo wa viongozi hao.

Aidha, Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibara B, Laurent Mafwili Mnyaga, alikiri kuwepo kwa tatizo hilo kijijini kwake, lakini agizo alilolitoa Waziri Lugola litasaidia wananchi kujitokeza kwa wingi na pia litawasaidia viongozi wa Kijiji chake kuwahamasisha wananchi waende kujiandikisha kwa wingi zaidi, kwasababu wapotoshaji hao wanawajua na Serikali ya Kijiji hicho watahakikisha wanawapeleka polisi.

“Nimefurahi sana kumuona Mbunge wetu kufika Mwibara na kutuhamasisha zaidi, lakini alilolisema ni sahihi kabisa, baadhi ya wananchi wamepotoshwa wasije kujiandikisha, wakidanganywa kuwa kadi za zamani zitatumika kapigia kura uchaguzi wa Serikali za Mitaa jambo ambalo si sahihi,” alisema Mafwili.

Aliongeza kuwa, licha ya kukabiliwa na changamoto ya wananchi kupotoshwa, kutishwa na watu mitaani wenye nia ovu na serikali, lakini Mwenyekiti huyo alisema utoaji wa elimu kuhusu uandikishaji haukua na nguvu kiasi kilichosababisha wananchi kutokujitokeza kwa wingi.

Waziri Lugola tayari amejiandikisha katika Kijiji hicho na kupongezwa na wananchi hao, ambao wengi wao walijitokeza baada ya kumuona Mbunge wao kujitokeza katika kituo hicho.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images